Simulizi ya kichawi: Makaburi ya wasio na hatia (The Graves of The Innocents)

Simulizi ya kichawi: Makaburi ya wasio na hatia (The Graves of The Innocents)

Uzi wa simulizi nikadhani nimeingia uzi wa jukwaa la sports. Mleta mada kakuomba odds mkuu?
Nisamehe mkuu. Ni kweli nimeona huu mcharuko wangu,
Nilikuwa nasoma simulizi kisha nikahamia kuwawekea code wa wazee wa sports. Kumbe nilipo tupia sio upande wake.
 
Mjomba Santos06 miiba miguuni imesababisha madhara makubwa mwilini nini?
Tumia hata ujasusi wa kichawi maana sasa wewe ni mchawi kuendeleza episode hapa jukwaani.
 
Hakuna ch
Mtoa post kaliwa nyama na wachawi baada ya kumkanya asitoe siri zao nae akakaidi[emoji16][emoji2957].
Mwenye ile story inayoishia episode ya 66 apokee kijiti ila ajitathmini kwanza kama ana uwezo wa kuzuia wachawi wasimle nyama au kumfanya msukule wao
Hakuna cha kuliwa nyama na wachawi wala nini, anakotegemea kukopi stori nao wamesitisha.
 
Sehemu ya 54

ILIPOISHIA:

Ni kweli nilikuwa na marafiki wengi wanaonipenda kule nyumbani Chunya lakini sikuwa tayari hata kidogo kuona mtu yeyote asiye na hatia anapatwa na matatizo kwa sababu yangu. Nilijikuta nikijilaumu sana kwa upumbavu wangu wa kutaka kwenda kujionea mwenyewe kilichotokea kule Mlandizi.

“Tunasubiri jibu lako,” baba alinizindua kutoka kwenye lindi la mawazo.

SASA ENDELEA…

“Lakini baba…”

“Lakini nini? Hakuna mjadala, kinachotakiwa hapa ni utekelezaji tu,” alisema baba na kunitishia kwamba endapo sitatoa majibu, kwa kuwa yeye anawafahamu marafiki zangu, atapendekeza jina lolote.

Kwa mara nyingine nilikuwa nimeingia kwenye mtego hatari wa kutaka kupoteza maisha ya mtu asiye na hatia kwa sababu ya uzembe wangu. Nilijisikia vibaya sana, nikashindwa kuzuia machozi yasiulowanishe uso wangu.

“Hata sisi mwanzo tulikuwa kama wewe, utazoea tu,” alisema baba yake Rahma. Sikujua ni nini hasa kilichotokea kwenye akili za baba na baba yake Rahma mpaka wachukulie kitendo cha kukatisha maisha ya mtu asiye na hatia kuwa cha kawaida kiasi kile.

Baada ya kulumbana kwa muda mrefu, baadaye niliamua kusalimu amri, nikamtaja rafiki yangu kipenzi, Sadoki. Kilichosababisha nikamchagua Sadoki, ni kwa sababu dakika za mwisho, urafiki wetu ulikuwa umeingia dosari baada ya siku moja kumkuta akishirikiana na watu wengine kumteta baba yangu kwamba alikuwa mchawi.

Kwa kipindi hicho, nilikuwa bado sijajua ukweli kwamba baba ni mchawi au mganga kwa sababu mara zote nilizokuwa namuuliza alikuwa akisema kwamba yeye ni mganga na wala si kweli kwamba anajihusisha na mambo ya kishirikina kwa hiyo yeyote niliyemsikia akizungumza mabaya ya baba, alikuwa akigeuka na kuwa adui yangu.

Siku nyingi zilikuwa zimepita tangu siku tulipotaka ‘kuzichapa’ maana baada ya kumkuta akimsema vibaya baba, nilimjia juu sana, kama isingekuwa watu wazima waliokuwa jirani nasi, huenda tungepigana na kuumizana sana.

Hata hivyo, tukio hilo moja halikuharibu ukweli kwamba tulikuwa marafiki wakubwa kwa sababu nakumbuka mara kwa mara alikuwa akija kwetu, na mimi nilikuwa nikienda kwao. Kwa kifupi ni kwamba ukiachilia mbali hiyo dosari ndogo iliyotokea, tulikuwa tumeshibana kisawasawa.

Baada ya kumtaja jina, sikuweza kuendelea kukaa mle chumbani, nilitoka na kwenda bafuni huku nikichechemea, nikajifungia na kuanza kulia kwa uchungu, baba na baba yake Rahma wakabaki chumbani kwangu wakiendelea kujadiliana mambo yao. Nililia mpaka macho yakawa mekundu kabisa, nilimuonea huruma Sadoki, nilimuonea huruma mama yake na wadogo zake.

Walikuwa wakimtegemea kwa sababu baba yao alifariki wakiwa bado wadogo kwa hiyo baada tu ya kumaliza shule ya msingi, Sadoki alikuwa akienda kufanya vibarua kwenye machimbo ya dhahabu na fedha kidogo alizokuwa akizipata ndizo zilizokuwa zikiihudumia familia yao.

Nikiwa bado naendelea kulia kule bafuni, baba alikuja kunigongea, ikabidi ninawe uso harakaharaka, nikatoka huku uso wangu nikiwa nimeuinamisha. Tulirudi chumbani kisha akaanza kunipa maelekezo kwamba usiku wa siku hiyo tunatakiwa kusafiri kuelekea Chunya.

“Tukifika, inabidi twende mpaka nyumbani kwa huyo rafiki yako, kuna dawa utaitega mlangoni, asubuhi akiwa anatoka anatakiwa airuke, akishairuka tu kazi itakuwa imekwisha.

“Sasa tutaendaje Chunya na kufanya hivyo unavyosema kabla hakujapambazuka?” niliuliza kwa sababu kama ni mabasi, muda huo tusingeweza kupata la kwenda Mbeya na hata kama lingepatikana, tusingewahi kama baba alivyokuwa anasema.

“Hutakiwi kuhoji sana, sikiliza kwa makini ninachokueleza,” baba alinikatisha, akaendelea kunipa maelezo ya namna ya kukamilisha zoezi hilo ambayo kwangu yalikuwa yakiingilia sikio la kushoto na kutokea la kulia.

Sikuona sababu yoyote ya kumuadhibu Sadoki kwa makosa ambayo nilikuwa nimeyafanya mwenyewe, nikajikuta nikijihisi hatia kubwa mno ndani ya moyo wangu. Basi tuliendelea kuzungumza pale, kisha baba akaniambia nijiandae kwa safari.

Walitoka na kuniacha nimejilaza kitandani, machozi yakaanza kunitoka tena na kwa sababu nilikuwa nimejilaza kwa kutazama juu, yalikuwa yakichuruzika kupitia kona za macho yangu mpaka kichwani na kupotelea kwenye shuka lililokuwa limetandikwa pale kitandani.

“Hivi ndiyo nimeshakuwa mchawi?” nilijiuliza swali kama mwendawazimu. Ni mimi ndiye niliyekuwa na shauku kubwa ya kuwa na nguvu zile za ajabu lakini sijui ni kutoelewa au ni kitu gani, ndani ya muda mfupi tu nilishaanza kuhisi kwamba pengine nimebeba mzigo mzito ambao sina uwezo nao. Zile kauli za baba akinikebehi kwamba bado nina akili za kitoto zikawa zinajirudia ndani ya kichwa changu.

Niliendelea kutafakari kwa kina na baadaye usingizi mzito ulinipitia, nikiwa usingizini nilianza kuota ndoto za ajabuajabu na kusababisha niwe nashtuka mara kwa mara. Baadaye ndoto hizo zisizoeleweka zilikoma, nikalala mpaka majira ya saa mbili za usiku nilipokuja kuzinduliwa na sauti ya baba aliyekuwa akiniita, nikakurupuka na kuamka.

“Umeshajiandaa?”

“Ndiyo,” nilimjibu huku nikijifikicha macho na kujinyoosha. Ukweli ni kwamba sikuwa nimejiandaa chochote.

“Haya nifuate.”

“Lakini bado sijala.”

“Utaenda kula mbele ya safari,” alisema baba huku akinihimiza nisimame. Nilishuka kitandani, miguu ikawa inauma sana hasa kwenye nyayo kutokana na majeraha ya ile miiba niliyotolewa na Rahma. Ilibidi nijikaze kisabuni kwa sababu ni mambo ambayo nilijitakia.

Tulitoka mpaka nje bila kuonekana na mtu yeyote, tukamkuta baba yake Rahma amesimama mlangoni, akionesha kwamba alikuwa akitusubiri. Alinipa kofia kubwa na kuniambia niivae, sikumuelewa kwa sababu gani amefanya vile. Tulitoka, mimi nikiwa katikati na kwenda hadi pale kwenye maegesho ya Bajaj, tukaingia kwenye mojawapo na baba yake Rahma akampa maelekezo dereva kwamba atupeleke Mwenge.

Sikuwa napajua Mwenge zaidi ya kupasikia tu, ni hapo ndipo nilipoelewa kwa nini baba yake Rahma alinipa ile kofia kwa sababu japokuwa nilikuwa nimeivaa, na kuziba sehemu kubwa ya uso wake, wale madereva Bajaj walikuwa wakinitazama kama wanaotaka kuhakikisha kama ni mimi kweli au laah!

Sikuwajali zaidi ya kuwadharau kwa sababu sasa nilikuwa na uwezo wa kumfanya mtu yeyote ninavyotaka mimi. Bajaj ilianza kukata mitaa na baada ya muda, tuliingia kwenye barabara ya lami iliyokuwa na magari mengi.

Safari ikaendelea mpaka tulipofika mahali kwenye mataa yenye mwanga mkali ambayo licha ya kwamba ilikuwa ni usiku, yalikuwa yakiangaza sehemu yote, watu wakiendelea na shughuli zao utafikiri ni mchana.

Tulishuka kwenye Bajaj huku nikishangaa huku na kule, moyoni nikawa najisemea ‘mjini kuzuri sana’. Tukaanza kuvuka barabara mbili pana ambazo katikati zimetenganishwa na bustani ya maua.

Kiukweli kama ningekuwa peke yangu, nisingeweza kuvuka kwa sababu kulikuwa na magari mengi mno, nikawa naung’ang’ania mkono wa baba Rahma maana baba naye alionesha kuwa na mchecheto.

Tulivuka salama mpaka upande wa pili ambako tulipanda magari mengine yanayoelekea Kunduchi. Kila kitu kilikuwa kigeni kwangu, safari ikaanza mpaka tulipofika Kunduchi, tukashuka kwenye gari na kuanza kutembea kwa miguu. Sikuwa najua tunaelekea wapi, baada ya muda tukatokezea kwenye makaburi yaliyokuwa karibu na bahari.

“Haya ni makaburi ya Wagiriki, ni ya zamani sana na hapa ndiyo hutumika kama njia ya kuingia na kutoka kwenda sehemu yoyote,” baba yake Rahma alinielekeza kwa sauti ya upole, tukaingia mpaka katikati kabisa ya makaburi hayo, mahali palipokuwa na mti mkubwa wa mbuyu.

“Tunaenda Chunya, hutakiwi kwenda kinyume na maelekezo tunayokupa, ukifanya uzembe tu, kitakachokutokea ni juu yako,” alisema baba kwa sauti ya msisitizo, nikawa natingisha kichwa kukubaliana naye. Tulikaa chini na kuweka kama duara hivi, tukashikana mikono kisha nikaambiwa nifumbe macho.

Je, nini kitafuatia?
 
Sehemu ya 55



ILIPOISHIA:

Ni kweli nilikuwa na marafiki wengi wanaonipenda kule nyumbani Chunya lakini sikuwa tayari hata kidogo kuona mtu yeyote asiye na hatia anapatwa na matatizo kwa sababu yangu. Nilijikuta nikijilaumu sana kwa upumbavu wangu wa kutaka kwenda kujionea mwenyewe kilichotokea kule Mlandizi.

“Tunasubiri jibu lako,” baba alinizindua kutoka kwenye lindi la mawazo.

SASA ENDELEA…

“Lakini baba…”

“Lakini nini? Hakuna mjadala, kinachotakiwa hapa ni utekelezaji tu,” alisema baba na kunitishia kwamba endapo sitatoa majibu, kwa kuwa yeye anawafahamu marafiki zangu, atapendekeza jina lolote.

Kwa mara nyingine nilikuwa nimeingia kwenye mtego hatari wa kutaka kupoteza maisha ya mtu asiye na hatia kwa sababu ya uzembe wangu. Nilijisikia vibaya sana, nikashindwa kuzuia machozi yasiulowanishe uso wangu.

“Hata sisi mwanzo tulikuwa kama wewe, utazoea tu,” alisema baba yake Rahma. Sikujua ni nini hasa kilichotokea kwenye akili za baba na baba yake Rahma mpaka wachukulie kitendo cha kukatisha maisha ya mtu asiye na hatia kuwa cha kawaida kiasi kile.

Baada ya kulumbana kwa muda mrefu, baadaye niliamua kusalimu amri, nikamtaja rafiki yangu kipenzi, Sadoki. Kilichosababisha nikamchagua Sadoki, ni kwa sababu dakika za mwisho, urafiki wetu ulikuwa umeingia dosari baada ya siku moja kumkuta akishirikiana na watu wengine kumteta baba yangu kwamba alikuwa mchawi.

Kwa kipindi hicho, nilikuwa bado sijajua ukweli kwamba baba ni mchawi au mganga kwa sababu mara zote nilizokuwa namuuliza alikuwa akisema kwamba yeye ni mganga na wala si kweli kwamba anajihusisha na mambo ya kishirikina kwa hiyo yeyote niliyemsikia akizungumza mabaya ya baba, alikuwa akigeuka na kuwa adui yangu.

Siku nyingi zilikuwa zimepita tangu siku tulipotaka ‘kuzichapa’ maana baada ya kumkuta akimsema vibaya baba, nilimjia juu sana, kama isingekuwa watu wazima waliokuwa jirani nasi, huenda tungepigana na kuumizana sana.

Hata hivyo, tukio hilo moja halikuharibu ukweli kwamba tulikuwa marafiki wakubwa kwa sababu nakumbuka mara kwa mara alikuwa akija kwetu, na mimi nilikuwa nikienda kwao. Kwa kifupi ni kwamba ukiachilia mbali hiyo dosari ndogo iliyotokea, tulikuwa tumeshibana kisawasawa.

Baada ya kumtaja jina, sikuweza kuendelea kukaa mle chumbani, nilitoka na kwenda bafuni huku nikichechemea, nikajifungia na kuanza kulia kwa uchungu, baba na baba yake Rahma wakabaki chumbani kwangu wakiendelea kujadiliana mambo yao. Nililia mpaka macho yakawa mekundu kabisa, nilimuonea huruma Sadoki, nilimuonea huruma mama yake na wadogo zake.

Walikuwa wakimtegemea kwa sababu baba yao alifariki wakiwa bado wadogo kwa hiyo baada tu ya kumaliza shule ya msingi, Sadoki alikuwa akienda kufanya vibarua kwenye machimbo ya dhahabu na fedha kidogo alizokuwa akizipata ndizo zilizokuwa zikiihudumia familia yao.

Nikiwa bado naendelea kulia kule bafuni, baba alikuja kunigongea, ikabidi ninawe uso harakaharaka, nikatoka huku uso wangu nikiwa nimeuinamisha. Tulirudi chumbani kisha akaanza kunipa maelekezo kwamba usiku wa siku hiyo tunatakiwa kusafiri kuelekea Chunya.

“Tukifika, inabidi twende mpaka nyumbani kwa huyo rafiki yako, kuna dawa utaitega mlangoni, asubuhi akiwa anatoka anatakiwa airuke, akishairuka tu kazi itakuwa imekwisha.

“Sasa tutaendaje Chunya na kufanya hivyo unavyosema kabla hakujapambazuka?” niliuliza kwa sababu kama ni mabasi, muda huo tusingeweza kupata la kwenda Mbeya na hata kama lingepatikana, tusingewahi kama baba alivyokuwa anasema.

“Hutakiwi kuhoji sana, sikiliza kwa makini ninachokueleza,” baba alinikatisha, akaendelea kunipa maelezo ya namna ya kukamilisha zoezi hilo ambayo kwangu yalikuwa yakiingilia sikio la kushoto na kutokea la kulia.

Sikuona sababu yoyote ya kumuadhibu Sadoki kwa makosa ambayo nilikuwa nimeyafanya mwenyewe, nikajikuta nikijihisi hatia kubwa mno ndani ya moyo wangu. Basi tuliendelea kuzungumza pale, kisha baba akaniambia nijiandae kwa safari.

Walitoka na kuniacha nimejilaza kitandani, machozi yakaanza kunitoka tena na kwa sababu nilikuwa nimejilaza kwa kutazama juu, yalikuwa yakichuruzika kupitia kona za macho yangu mpaka kichwani na kupotelea kwenye shuka lililokuwa limetandikwa pale kitandani.

“Hivi ndiyo nimeshakuwa mchawi?” nilijiuliza swali kama mwendawazimu. Ni mimi ndiye niliyekuwa na shauku kubwa ya kuwa na nguvu zile za ajabu lakini sijui ni kutoelewa au ni kitu gani, ndani ya muda mfupi tu nilishaanza kuhisi kwamba pengine nimebeba mzigo mzito ambao sina uwezo nao. Zile kauli za baba akinikebehi kwamba bado nina akili za kitoto zikawa zinajirudia ndani ya kichwa changu.

Niliendelea kutafakari kwa kina na baadaye usingizi mzito ulinipitia, nikiwa usingizini nilianza kuota ndoto za ajabuajabu na kusababisha niwe nashtuka mara kwa mara. Baadaye ndoto hizo zisizoeleweka zilikoma, nikalala mpaka majira ya saa mbili za usiku nilipokuja kuzinduliwa na sauti ya baba aliyekuwa akiniita, nikakurupuka na kuamka.

“Umeshajiandaa?”

“Ndiyo,” nilimjibu huku nikijifikicha macho na kujinyoosha. Ukweli ni kwamba sikuwa nimejiandaa chochote.

“Haya nifuate.”

“Lakini bado sijala.”

“Utaenda kula mbele ya safari,” alisema baba huku akinihimiza nisimame. Nilishuka kitandani, miguu ikawa inauma sana hasa kwenye nyayo kutokana na majeraha ya ile miiba niliyotolewa na Rahma. Ilibidi nijikaze kisabuni kwa sababu ni mambo ambayo nilijitakia.

Tulitoka mpaka nje bila kuonekana na mtu yeyote, tukamkuta baba yake Rahma amesimama mlangoni, akionesha kwamba alikuwa akitusubiri. Alinipa kofia kubwa na kuniambia niivae, sikumuelewa kwa sababu gani amefanya vile. Tulitoka, mimi nikiwa katikati na kwenda hadi pale kwenye maegesho ya Bajaj, tukaingia kwenye mojawapo na baba yake Rahma akampa maelekezo dereva kwamba atupeleke Mwenge.

Sikuwa napajua Mwenge zaidi ya kupasikia tu, ni hapo ndipo nilipoelewa kwa nini baba yake Rahma alinipa ile kofia kwa sababu japokuwa nilikuwa nimeivaa, na kuziba sehemu kubwa ya uso wake, wale madereva Bajaj walikuwa wakinitazama kama wanaotaka kuhakikisha kama ni mimi kweli au laah!

Sikuwajali zaidi ya kuwadharau kwa sababu sasa nilikuwa na uwezo wa kumfanya mtu yeyote ninavyotaka mimi. Bajaj ilianza kukata mitaa na baada ya muda, tuliingia kwenye barabara ya lami iliyokuwa na magari mengi.

Safari ikaendelea mpaka tulipofika mahali kwenye mataa yenye mwanga mkali ambayo licha ya kwamba ilikuwa ni usiku, yalikuwa yakiangaza sehemu yote, watu wakiendelea na shughuli zao utafikiri ni mchana.

Tulishuka kwenye Bajaj huku nikishangaa huku na kule, moyoni nikawa najisemea ‘mjini kuzuri sana’. Tukaanza kuvuka barabara mbili pana ambazo katikati zimetenganishwa na bustani ya maua.

Kiukweli kama ningekuwa peke yangu, nisingeweza kuvuka kwa sababu kulikuwa na magari mengi mno, nikawa naung’ang’ania mkono wa baba Rahma maana baba naye alionesha kuwa na mchecheto.

Tulivuka salama mpaka upande wa pili ambako tulipanda magari mengine yanayoelekea Kunduchi. Kila kitu kilikuwa kigeni kwangu, safari ikaanza mpaka tulipofika Kunduchi, tukashuka kwenye gari na kuanza kutembea kwa miguu. Sikuwa najua tunaelekea wapi, baada ya muda tukatokezea kwenye makaburi yaliyokuwa karibu na bahari.

“Haya ni makaburi ya Wagiriki, ni ya zamani sana na hapa ndiyo hutumika kama njia ya kuingia na kutoka kwenda sehemu yoyote,” baba yake Rahma alinielekeza kwa sauti ya upole, tukaingia mpaka katikati kabisa ya makaburi hayo, mahali palipokuwa na mti mkubwa wa mbuyu.

“Tunaenda Chunya, hutakiwi kwenda kinyume na maelekezo tunayokupa, ukifanya uzembe tu, kitakachokutokea ni juu yako,” alisema baba kwa sauti ya msisitizo, nikawa natingisha kichwa kukubaliana naye. Tulikaa chini na kuweka kama duara hivi, tukashikana mikono kisha nikaambiwa nifumbe macho.

Je, nini kitafuatia?
 
Sehemu ya 56


Tunaenda Chunya, hutakiwi kwenda kinyume na maelekezo tunayokupa, ukifanya uzembe tu, kitakachokutokea ni juu yako,” alisema baba kwa sauti ya msisitizo, nikawa natingisha kichwa kukubaliana naye. Tulikaa chini na kuweka kama duara hivi, tukashikana mikono kisha nikaambiwa nifumbe macho.

SASA ENDELEA…

Kweli nilifumba macho, baba na baba yake Rahma wakawa wanazungumza maneno fulani ambayo sikuwa nayaelewa kwa kuyarudiarudia, kisha nikaanza kusikia kama upepo mkali ukianza kuvuma kwa nguvu, sikuelewa tena kilichoendelea mpaka niliposikia baba akinitingisha kwa nguvu.

“Tumeshafika! Fumbua macho,” alisema baba, nikafumbua macho na kujikuta nikiwa kwenye mazingira tofauti kabisa. Sikuelewa tumetumia muda gani maana ninachofahamu mimi kuna umbali mrefu sana kutoka Mbeya mpaka Dar es Salaam, ni safari ya kutoka alfajiri na mapema na kufika usiku.

“Unashangaa nini tumeshafika!” baba alisema huku akinivuta mkono maana kiukweli nilikuwa nimepigwa na butwaa, nikishangaa huku na kule, nikijaribu kukumbuka kama eneo lile nalifahamu.

“Mungu wangu!” nilijisemea moyoni baada ya kugundua kwamba tulikuwa kwenye shule ya msingi niliyosoma pale Chunya, chini ya mti mkubwa uliokuwa nyuma ya shule ambao kwa kipindi kirefu nilikuwa nikisikia watu wakisema kwamba una majini.

“Tumefikaje huku?” niliuliza nikiwa bado nashangaashangaa nikiwa siamini. Yaani nifumbe macho nikiwa kwenye makaburi ya Wagiriki, Kunduchi jijini Dar halafu ninapofumbua macho muda mfupi baadaye, usiku huohuo nijikute nipo Chunya, ilikuwa ni zaidi ya maajabu.

“Huu si muda wa maswali,” baba aliniambia huku akinitaka niongeze mwendo, tukawa tunatembea kuelekea upande wa Magharibi mwa shule, kulipokuwa na njia ya kuingilia na kutokea shuleni hapo.

Baba alikuwa mbele, mimi katikati na nyuma alikuwepo baba yake Rahma, tukawa tunatembea na baadaye tukafika kwenye eneo la uwanja wa shule. Japokuwa ilikuwa ni usiku, uwanja ulionesha kuwa na pilikapilika nyingi sana, watu wengi walikuwa wamekusanyika na kuweka makundi matatu, kundi la kwanza lilikuwa upande wa goli la kwanza, wengine walikuwa katikati ya uwanja na wengine kwenye goli jingine.

Ilionesha kama kuna shughuli fulani zinaendelea ingawa zilionesha kwamba si za kawaida kwa sababu watu wengine walikuwa watupu, wengine walikuwa wakicheza ngoma za kienyeji na wengine walikuwa wamekaa chini.

“Hutakiwi kugeuka nyuma, ni mwiko,” baba aliniambia wakati tukiendelea kuchanja mbuga, tukawa tunapita kwenye njia ambayo wakati nasoma, ndiyo niliyokuwa nikiitumia kwenda na kurudi shule.

Tulipita kwenye vichaka kadhaa na baadaye tukatokezea kwenye nyumba za nyasi zilizokuwa pembezoni mwa kijiji, tukasimama ambapo baba aliniambia kwa sababu mimi ndiye ninayefahamu nyumbani kwa huyo rafiki yangu, Sadoki ambaye ndiye niliyemchagua kumtoa kafara, nitangulie mbele.

Akarudia kunisisitiza kwamba sitakiwi kugeuka nyuma wala kuzungumza hovyo, kazi yangu ni moja tu, kuongoza njia. Nilitii nilichoambiwa huku nikitetemeka sana. Mara kwa mara taswira ya Sadoki ilikuwa ikinijia ndani ya kichwa changu, nikawa najisikia uchungu mno ndani ya roho yangu hasa kutokana na ukweli kwamba yeye ndiye aliyekuwa tegemeo la familia yao.

Niliongoza njia na kwa sababu vichochoro vyote vya Chunya nilikuwa navijua kwa sababu hapo ndipo nilipozaliwa na kukulia, sikupata tabu. Baada ya kutembea kwa dakika kadhaa, hatimaye tuliwasili kwenye nyumba chakavu ya akina Sadoki. Nikaonesha kwa ishara kwamba tayari tumeshafika, baba akanivuka na kutangulia mbele.

Kwa muda wote huo, baba yake Rahma alikuwa kimya kabisa, baba akaanza kutoa maelekezo kwamba tunatakiwa kuizunguka nyumba hiyo mara saba, kutokea upande wa kulia kwenda kushoto. Nilichojifunza, mambo mengi yanayofanywa na watu wa jamii hizi, huwa yanakwenda kinyume na utaratibu wa kawaida, tukaanza kufanya vile baba alivyosema.

Tulikuwa tukipiga hatua fupifupi huku baba na baba Rahma wakiimba nyimbo fulani za kutisha ambazo hata sikuwa nazielewa, tukazunguka mpaka ilipofika raundi ya saba, tukamalizia pale kwenye kona ya nyuma tulipoanzia kuzunguka.

Baba alipiga mguu wa kushoto chini, mara ukuta ukawa kama umefunguka, akatangulia yeye kuingia kinyumenyume, akapotelea ndani.

Tukabaki mimi na baba Rahma, akaniambia na mimi nipige mguu wa kushoto chini kwa nguvu, nikafanya hivyo, ule uwazi ukatokea tena, akanielekeza kuingia kinyumenyume, nikafanya hivyo na kujikuta nipo ndani, pembeni ya baba ambaye alikuwa amesimama akitusubiri.

Mara baba yake Rahma naye akaingia kwa mtindo uleule. Wasichokijua wengi ni kwamba watu wabaya wanapoamua kuingia ndani ya nyumba yako, huwa hawatumii mlango kwa hiyo hata ufunge milango kwa makufuli makubwa, ujenge fensi hata yenye umeme na uweke walinzi wenye silaha nzito, huwezi kuwazuia watu wenye nguvu za giza kuingia ndani kwako.

Maisha waliyokuwa wakiishi akina Sadoki yalikuwa ya chini sana maana hata sebuleni kwao hakukuwa na kitu chochote cha maana zaidi ya viti vya mbao na meza ndogo, na vyombo vya jikoni. Japokuwa nyumba yote ilikuwa giza, cha ajabu ni kwamba nilikuwa na uwezo wa kuona kila kitu, mpaka kijiko.

Tulianza kutafuta chumba anacholala Sadoki na kwa sababu nilishawahi kuwa naingia mpaka chumbani kwake, niliwaongoza, tukaenda mpaka kwenye chumba chake na kumkuta Sadoki akiwa amelala na mdogo wake wa kiume juu ya kitanda cha kamba.

Kwa wale waliowahi kuishi vijijini watakuwa wananielewa vizuri ninapozungumzia kitanda cha kamba. Maskini! Sadoki alikuwa akikoroma pamoja na mdogo wake, wakiwa hawaelewi chochote kinachoendelea.

Baba alinielekeza kukizunguka kitanda hicho na kusimama upande ambao kichwa cha Sadoki kilikuwepo, nikafanya hivyo, baba akasimama upande wa miguuni na baba yake Rahma akasimama pale katikati.

Moyo ulikuwa ukiniuma sana na sikuelewa natakiwa kufanya nini, nikawa nasubiri maelekezo tu, huku moyo wangu ukijihisi kuwa na hatia kubwa mno. Sadoki hakuwa amefanya kosa lolote baya kustahili adhabu kali kiasi kile maana kama ni kupishana maneno, kilikuwa ni kitu cha kawaida kabisa kwa marafiki walioshibana.

Baba alinielekeza kuinamisha kichwa kumuelekea Sadoki pale kitandani, nao wakafanya hivyohivyo kisha baba akaanzisha wimbo ambao mimi sikuwa naujua, baba yake Rahma akawa anaitikia. Niliogopa sana kwa sababu walikuwa wakiimba kwa sauti ya juu ambayo ingeweza kuwaamsha watu waliokuwa ndani ya nyumba hiyo.

Baada ya kuimba mara kadhaa, baba alitoa kichupa kidogo kilichokuwa na ungaunga mweusi ndani, akakitingisha kwa nguvu kisha akampa baba Rahma ili anipe mimi, kikanifikia ambapo alinipa maelekezo kwa ishara kwamba nikitingishe kwa nguvu kisha nichukue ungaunga kidogo na kumpaka Sadoki kwenye paji la uso wake.

Nilifanya kama nilivyoelekezwa, nikampaka kwenye paji la uso kwa kuchora ishara kama ya msalaba hivi, kisha baba akanipa maelekezo kwamba natakiwa kugeuka na kumpa mgongo Sadoki, nikageuka, na wao wakageuka kisha baba akapiga makofi akiashiria tugeuke tena.

Tulipogeuka, nilishtuka sana kumuona Sadoki akiwa amekaa kweye kitanda chake lakini akiwa amefumba macho. Baba akanielekeza kwamba nimshike mkono, kweli nikafanya hivyo, nikamshika, akasimama kisha baba akanionesha ishara kwamba nimuangalie kwa makini anachokifanya.

Alisogea kwenye pembe moja ya chumba na kupiga mguu chini kwa nguvu, ukuta ukafunguka ambapo alitoka nje kinyumenyume, huku nikitetemeka na mimi nikasogea kwenye ile kona huku nikiwa nimemshika Sadoki mikono yake yote miwili. Japokuwa alikuwa amesimama, bado alikuwa amefumba macho.

Nikapiga mguu chini kwa nguvu na kugeuka, nikawa nataka kutoka lakini nilishangaa mwili wangu ukiwa mzito kama ninayevutwa na kitu kurudi ndani. Sijui nini kilitokea kwani nilishtukia baba Rahma ameyeyuka, nikabaki mimi na Sadoki, nikapiga tena mguu kwa nguvu na kutaka kutoka lakini safari hii, ukuta haukufunguka kabisa, kijasho chembamba kikaanza kunitoka.

Nikiwa bado nashangaa nikiwa sijui nini cha kufanya, Sadoki alifumbua macho, tukawa tunatazama ana kwa ana. Ni kama fahamu zake zilikuwa zimemrejea kwani alishtuka sana kuniona ndani ya chumba chake, akageuka huku na kule huku akijaribu kujitoa kwenye mikono yangu kwa hofu kubwa.

“Togoo! Umeingiaje humu?” aliniuliza kwa sauti ya juu, nikasikia mlango wa chumba cha pili ukifunguliwa kuashiria kwamba kuna mtu alikuwa amesikia na sasa anatoka.

“Nimekwisha!” nilijisema huku nikigeuka huku na kule, sikumuona baba wala baba yale Rahma, Sadoki akanibadilikia na kunishika kwa nguvu ii nisipate nafasi ya kukimbia.

Je, nini kitafuatia?
 
Sehemu ya 57



ILIPOISHIA:

Ni kama fahamu zake zilikuwa zimemrejea kwani alishtuka sana kuniona ndani ya chumba chake, akageuka huku na kule huku akijaribu kujitoa kwenye mikono yangu kwa hofu kubwa.

“Togoo! Umeingiaje humu?” aliniuliza kwa sauti ya juu, nikasikia mlango wa chumba cha pili ukifunguliwa kuashiria kwamba kuna mtu alikuwa amesikia na sasa anatoka.

SASA ENDELEA…

“Nimekwisha!” nilijisema huku nikigeuka huku na kule, sikumuona baba wala baba yale Rahma, Sadoki akanibadilikia na kunishika kwa nguvu ii nisipate nafasi ya kukimbia.

Akili za haraka, zilinituma kutumia nguvu zangu kujiokoa na kwa kuwa nilikuwa na ile kinga yangu ya hirizi mkononi, nilipiga mguu wa kushoto chini huku nikiwa nimevibana vidole gumba na vile vya mwisho. Hii ni mbinu niliyofundishwa ya kutaka kupotea kwenye macho ya watu, yaani unakuwepo sehemu hiyohiyo lakini huonekani.

Nilipofanya hivyo, nilishtukia nikiwa mwepesi kama upepo, Sadoki akabaki ameduwaa kwani japokuwa alikuwa amenishika, alishtukia nikiyeyuka mikononi mwake, giza nene likatanda chumba kizima.

Mara mlango ulianza kugongwa kwa nguvu, Sadoki akaenda kuufungua maana alikuwa amefunga kwa komeo kwa ndani, mama yake Sadoki akaingia mbiombio akiwa ameshika kibatari.

“Una nini Sadoki?”

“Mama! Nimemuona Togo kwa macho yangu, hata sijui ameingiaje humu ndani wakati milango ilikuwa imefungwa.”

“Togo huyu rafiki yako? Wewe utakuwa unaota, Togo ataingiaje humu wakati milango yote imefungwa? Halafu mbona watu wenyewe hawapo hapa kijijini na hakuna anayejua walikohamia?” mama yake Sadoki alisema huku akionesha kumshangaa mwanaye.

“Kweli mama, nimemuona kwa macho yangu!”

“Kwanza umemuonaje wakati hukuwa umewasha kibatari? Acha kutushtua wenzako kwa sababu ya ndoto zako,” alisema mama yake Sadoki huku akimulika huku na kule kwa kibatari. Japokuwa nilikuwa mlemle ndani, hakuna aliyeniona, mwanamke huyo akawa anamtuliza mwanaye na kumwambia kwa kuwa wanalindwa na Mungu hakuna jambo lolote baya linaloweza kuwapata.

Japokuwa mama yake Sadoki aliamini kwamba mwanaye alikuwa ndotoni, mwenyewe aliendelea kushikilia msimamo wake na alipoona mama yake hamuamini, aliamua kunyamaza lakini mara kwa mara alikuwa akigeuka huku na kule, akionesha kuwa na hofu kubwa ndani ya moyo wake.

“Haya sogea huku tusali,” alisema mama yake Sadoki, akamshika mwanaye mikono, wote wakafumba macho. Kabla hata hawajaanza kusali, nilishtukia nikivutwa kwa nguvu kuelekea nje, kutazama vizuri kumbe walikuwa ni baba na baba yake Rahma, tukadondokea kwenye majani pembeni ya nyumba ya akina Sadoki, wote wakiwa wanahema kwa nguvu.

“Mpumbavu sana wewe,” alisema baba huku akinizabua kibao kwa nguvu, nikashangaa kwa nini ananipiga kwa sababu sikuwa nimefanya kosa lolote.

“Kwa nini hukumgeuza kinyumenyume kama wewe?” alisema baba kwa ukali, ni hapo ndipo nilipolitambua kosa langu. Wakati nikitoka na Sadoki, mimi ndiye niliyetanguliza mgongo lakini yeye alikuwa ameelekea nilipo mimi kwa sababu nilikuwa nimemshika mikono nikimvuta, hakutanguliza mgongo.

“Lakini hukuniambia hivyo baba,” nilisema huku nikiugulia maumivu makali ya kibao cha baba. Muda huo tayari walishaanza kusali, wakawa wanakemea na kutaja jina la Mungu kwa nguvu.

Ukweli ambao wengi hawaujui, ambao hata mimi mwenyewe nilikuwa siujui, hakuna sumu mbaya kwa jamii ya watu wa nguvu za giza, kama mtu anayesali na kumuamini Mungu kwa moyo wake wote, bila kujali ni wa dini gani.

Hapa nazungumzia wale watu ambao kweli wanafuatisha amri za Mungu, yaani kama ni Mkristo, awe anafuatisha yale yote aliyoagizwa na dini yake na kama ni Muislam vivyo hivyo.

Watu wa namna hii, huwa hawagusiki kabisa maana hata pale baba aliniambia kama wasingetumia nguvu za ziada kuingia na kunivuta kwa nguvu, maombi ya Sadoki na mama yake yangenidhuru vibaya sana na hata wao hawajui nini kingenipata.

Ila kitu ambacho nilikuja kujifunza baadaye, ambacho ningependa watu wengine wajue, kinga waliyonayo watu wanaomuamini Mungu, haiwahusu wale wanaosali kinafiki, kwamba ukifika kwenye nyumba za ibada unajifanya wewe ni mwema sana lakini kumbe ni mwizi, mwongo, mwasherati au unashinda kwa waganga wa kienyeji.

Ilibidi tuondoke haraka pale nyumbani kwa akina Sadoki kwa sababu sasa palikuwa hapakaliki tena kutokana na maombi yaliyokuwa yanaendelea ndani, njia nzima baba akawa ananilaumu kwa uzembe nilioufanya. Kwa bahati nzuri baba Rahma alinitetea kwamba ni kwa sababu sikuwa najua.

Kiukweli lawama za baba zilikuwa ni uonevu wa hali ya juu, maelezo aliyokuwa ananipa, alikuwa ananielekeza vitu nusunusu, sasa kwa mfano hapo kwa akina Sadoki, mimi ningejuaje kama natakiwa kumgeuza Sadoki pia atoke kinyumenyume huku nikiwa nimemshikilia bila kupewa maelekezo?

“Sisi tunakusaidia wewe mwenyewe kwa sababu ya upumbavu ulioufanya, kwani sisi ndiyo tulikutuma uende kwenye msiba ambao wewe mwenyewe ndiye uliyeusababisha? Utajuana mwenyewe na Mkuu, we fanya masihara utaona mwisho wake,” alisema baba.

Tayari tulishakaribia pale kwenye uwanja wa shule ya msingi niliyosoma ambapo ndipo tulipofikia.

“Sasa mzee mwenzangu, tukiendelea kufanya mambo kwa hasira, kweli tutampoteza huyu kijana, hapa kinachotakiwa ni kuhakikisha tunamaliza kwanza suala la Mkuu na Togo na kama unavyoona huku ndiyo tayari tumeshakwama na muda unayoyoma,” alisema baba yake Rahma.

Mwanzo nilikuwa nalichukulia suala hilo kama jepesi lakini kwa jinsi mazungumzo hayo yalivyokuwa, niligundua kwamba kweli nipo kwenye hatari kubwa kwa sababu ya makosa niliyokuwa nimeyafanya bila kujua.

“Hivi si kuna yule mtu aliyepoteza maisha kwenye ile ajali ya bodaboda aliyoisababisha huyu mwendawazimu?” baba aliuliza. Baba yake Rahma akamjibu kwa kutingisha kichwa, nikiwa na shauku kubwa ya kutaka kusikia baba atasema nini.

“Taarifa zinaonesha kwamba amezikwa jioni ya leo, ila sijui amezikwa wapi, kama tukifanikiwa kujua, tunaweza kumtumia kama mbadala wa Sadoki ili tulimalize hili tatizo la huyu mwendawazimu,” alisema baba huku akiendelea kunishutumu.

Sikuelewa anamaanisha nini na hata kama tungelijua kaburi lake tungefanya nini.

“Twendeni Mlandizi, tutajua hukohuko tukifika, si unalikumbuka eneo la ajali?” baba aliniuliza, nikatingisha kichwa kwa sababu ilikuwa ni palepale kwenye nyumba iliyokuwa na msiba ndipo hiyo ajali nyingine ilipotokea. Yaani baba alivyokuwa akizungumza, utafikiri kutoka Chunya mpaka Mlandizi ni karibu sana.

Kukukumbusha tu, hapa aliyekuwa anazungumziwa aliyekuwa ni yule dereva wa bodaboda ambaye wakati nikiwa nakimbia kuokoa maisha yangu baada ya wale wazee kunishtukia pale kwenye msiba, nilimgonga wakati nikivuta barabara, yeye akiwa kwenye bodaboda iliyokuwa kwenye kasi kubwa. Pale alipodondoka hakuweza hata kuomba maji, alipoteza maisha palepale na sikuwa najua mpaka nilipokuja kuambiwa na akina baba ambao hata sijui wao walijuaje.

Basi tulienda mpaka pale chini ya ule mti, tukakuta kuna watu wengine wengi wakiwa wanafanya mambo ambayo hata sikuyaelewa lakini yalionesha kuhusiana na nguvu za giza.

Tukakaa na kuweka duara kama tulivyofanya kule Kunduchi wakati tukitaka kuondoka, nikaambiwa nifumbe macho na nisifumbue mpaka nitakapoambiwa, lakini baba akanisisitiza kwamba natakiwa kuwa nalifikiria eneo lile ajali ilipotokea.

Kweli nilifanya hivyo, wao wakafanya tena mambo yao kama kule Kunduchi na muda mfupi baadaye, upepo mkali ulianza kuvuma, sikuelewa tena kilichoendelea mpaka nilipokuja kuzinduliwa na baba aliyekuwa akinitingisha kwa nguvu.

Yaani kilichokuwa kinatokea, inakuwa kama nimepitiwa na usingizi mzito wa ghafla, kisha nikizinduliwa najikuta nipo kwenye mazingira mengine tofauti kabisa. Nilishtukia nikiwa nimelala pembeni ya barabara ya lami, baba aliponiamsha, nikawa nashangaashangaa, nikageuka huku na kule kama ninayejaribu kuvuta kumbukumbu.

Sikuyaamini macho yangu kugundua kwamba tulikuwa Mlandizi, tena jirani kabisa na pale ile ajali ilipotokea. Nilipotazama upande wa pili wa barabara, niliwaona watu wengi wakiwa wamekaa na kuuzunguka moto, pale kwenye ile nyumba iliyokuwa na msiba wa kwanza wa yule mtoto, moyo ukashtuka sana nikikumbuka kilichotokea.

“Mbona umeshtuka,” baba aliniuliza.

Je, nini kitafuatia?
 
Duh,
Wewe mchawi we.
Sodoki ataeneza kijiji kizima uchawi wako.
Natamani udakwe kwenye tukio aisee!
 
Back
Top Bottom