Simulizi ya Kijasusi: C.O.D.EX.

Simulizi ya Kijasusi: C.O.D.EX.

88.
"mpendwa mwanangu Christina" iliskika sauti ya Allen James, "wakati utakapoupokea ujumbe huu uenda nikawa sipo tena duniani, nakuomba sikiliza kwa makini na uwatabue marafiki zako na maadui zako usije ukatumika kama nilivyotumika mimi" baada hapo sauti ya Allen ilikata na kuanza kusikika sauti nyingine "ndio baada Allen James kukamilisha kazi inabidi na yey afe, si mnaelwa kuwa kazi hii ni siri ya hali ya juu na hatakiwi mtu mwengien asiehusika afahamu, na kama Allen atashidwa kumuua Alex basi itabidi sisi tumuue yeye halafu kesi hii tunambambikizia Alex. Akirudi Christina na kufahamu kuwa babaake ameuwawa na Alex, nina uhakika hatopumzika mpaka atakapohakikisha Aex amekufa na baada ya hapo na yeye pia tunamuua ili kupoteza ushahidi kabisa. Mapinduzi hayawezi kuzuilika, na mtu na mwanae wote watatumika kama mbwa wa kuwindia"baada ya sauti hiyo kukata ilirudi tena sauti ya Allen "natumai utakuwa umefahamu nani mbaya wako na nani rafiki yako, atakae kuletea ujumbe ni Alex na ni mmoja kati ya watu ambao watakuwa msaada mkubwa kwako katika kukamilisha kazi ntakayokupa kama babaako. Nataka uwasambaratishe kama vumbi wale wote wanaotaka kuitndea nchi yetu mabaya, na kunitenda mimi babaako. Ni matumaini yangu kwamba utafanikisha zoezi hili kwa hali na mali, kama ikibidi ufe ili likamilike basi fanya hivo. Nakupenda sana mwanangu...mimi babaako Allen James" hapo ndio ulikuwa mwisho wa rikodi hiyo na katika kioo cha TV hio kutaoke maandishi mekundu yaliosemeka "THE END IS THE BEGINNING".

Christina alijikuta machozi yakimtoka bila mategemeo na kujisemea kwa sauti ya kinyonge "kwanini hukunipa mapema taarifa hii Alex", "Christina punguza jazba" aliongea Jeff. "najaribu ila nshindwa, kwakweli mtu niliokuwa nataka kumuua ndie mtu aliekuwa bega kwa bega na babangu katika mapambano, unafikiri ningemuua ningeenda kuiweka sura yangu siku ambayo ningekutana na babaangu" alianza kujilaumu sasa. "lakini jambo zuri ni kwamba hujamuua" aliongea Jeff akijaribu kumpa moyo. "una uhakika gani, mi sidhani kama atakuwa amepona baada majeraha yale niliompa" alizidi kujilaumu huku moyoni akijiapiza kulipiza kisasi hata kama itabidi damu yake imwagike. Jeff baada kusikia hivo, ikabidi anyamaze kwanza na kisha akainuka na kutoka na kutoka nje huku akimuacha Christina akiendelea kulia. "mbona umemuacha peke yake" aliuliza Talbot, "ndio inavotakiwa, kwa sasa anajaribu kukabiliana na uhalisia kwamba aliekuwa anamuwinda sie aliemuaa baba ake. Na tujiandae kwa mechi ngumu mbele kwasababu lazima atahitaji msaada wetu kukamilisha kazi yake" Jeff alijibu na kuelekea chumbani kwake kwa ajili ya kupumzika.

Christina aliendelea kulia huku akiwa mwekundu kwa hasira ambayo ilianza kukikitesa kichwa chake, mara kadhaa alipiga kelele na kuangusa vitu chini. Lakini hakuna mtu alieingia katika chumba chake, "hahaha....Christina wewe ni mjinga sana tena mjinga wa mwisho, hukuona muda wote kama Alex alikuwa kiajribu kukufikishia ujumbe". "hahaha... lakini amefanya uzembe mwenyewe kwa kutokupa ujumbe mapema", "General David mpumbavu mkubwa wee, utalipa huu unyama kwa damu yako mjinga mkubwa wewe. Ulidhani mimi ni babaangu, umekosea sana kucheza na baba angu kwani umesaini mkataba wa kifo na mimi...hahaha mshenzi wee". Alikuwa akiongea mwenyewe na kujijibu huku akicheka na baadhi ya wakati alikuwa analia, alionekana kama mtu aliechanganyikiwa tena si kidogo maana chumba kizima alikichafua chafua, alikuwa mevunja kila kitu kilichokuwemo katika chumba hicho kuanzia vitu viukubwa mpaka vidogo vidogo. "THE END IS THE BEGINNING....NDIO KWANZA SAFARI IMEANZA" alisema kwa nguvu huku machozi yakimtoka. "furahia siku zako za mwisho na kila anaehusika na wewe,nitauwa kuanzia sisimizi na kila kitu ambacho kimo katika himaya yako na yoyote atakaekaa mbele yangu na yeye pia atakufa...General David" alijisemea na kusimama kwenye kiti alichokuwa amekaa baada ya kushuka kitandani.

CODE X 3: THE REAL ME 2

***************************

"nimekwambia nenda nyumbani ukanyonye. leo ni siku mbya sana" Alex aliikumbuka sentensi aliomwambia Allen Jr kabla ya kumpa kichapo cha fisi mwizi. "natumai kwa sasa utakuwa ushaujua ukweli" alijisemea huku akijisifu kwa kufikisha ujumbe wa mwalimu wake Allen. Siku ile baada ya kumpiga mpaka kumzimisha, alitoa ile recorder alioambiwa kuwa ni kwa ajili ya Christina na kumtilia katika mfuko wa suruali yake kisha yeye akaondoka na kuendelea na pambano lake. "hivi kwanini hukuniacha nife tu maana tayari nilishapanga kwena kukutana na familia yangu mzima" Alex alimuuliza Scarlet aliekuwa pembeni bize akicheza game ya kivita. "unadhani kila mtu ambae anapata mikosi angetaka kufa, unadhani kungekuwa nawatu amabao wangekuwa tayari kupigania haki ya mtu" Scarlet alijibu na kuacha kucheza game, alionekana kukerwa na swali hilo la Alex. " ni bora ushukuru ulikuwa sehemu ambayo ulikuwa na marafiki na walikuwa wakikujali japo mlikuwa kambini" Scarlet aliongea huku akikaa mbele ya Alex na kumuangalia usoni. "mimi nimeishi maisha ya manyanyaso sana tokea nilipozaliwa" Scarlet aliendelea kuongea huku akionekana wazi kuumizwa na anachokiongea. "hebu nielezee maisha yako" Alex aliomba na kukaa mkao wa kula kusuburi binti huo aanze kumporomoshea mkasa wa maisha yake.

********************

Scarlet alianza kuelezea hadithi ya maisha yake "Jina langu halisi sio Scarlet kama wanavolifahamu wengi, ila jina langu ni Ariella Mark. Ni mtoto wa pekee katika familia yangu, na babaangu alinipa jina hilo kwa sababu mama angu alijifungua katika wakati mgumu sana wa maisha yao. Japo hali ilikuwa duni lakini niliweza kukuwa vizuri tu bila kusumbuliwa na magonjwa kama wengi walivyodhani. Ukweli wazazi wangu walinipenda sana, tena sana kupita maelezo. Nilipata kila kitu nilicholikitaka, taratibu maisha yalianza kunyooka na kuwa mazuri huku kubadilika huko kwa maisha kukiwachukiza ndugu wa karibu wa wazazi wangu. Nikiwa na miaka minne tulihama tulipokuwa tunakaa na kuhamia mjini kabisa ambako baba alikuwa amejenga nyumba mpya na ya kisasa kwa wakti huo. Nilianza shule japo nilikuwa nimechelewa lakini wazazi wangu hawakumsikliza mtu, nilianza shule ya awali na baada ya miaka mitatu niliingia darasa la kwanza. Wakati huo nilikuwa na miaka saba lakini kutokana na mwili wangu kuwa mdogo sana hakuna alieamini kuwa nina miaka hiyo. Lakini nashukuru Mungu kwa kunipa wazazi wenye hekima na busara kama wale, lakini kama tunavojua kuwa duniani tunapita hakuna kiumbe kitakachoishi milele. Basi hivyo ndivyo ilivokuwa kwa babaangu ambae nikiwa na kumi alpoteza ajali katika ajali ya ndege nikabaki na mama yangu tu.
 
89 - 90

Maisha yalizidi kusonga mbele huku ndugu zake baba wakizidi kuleta vita juu ya mali alioacha baba, na taratibu walianza kutupora. Na walipoona mama ameleta ubishi sana wa kuzikabodhi mali, Baba mkubwa alituma vijana wakaja kuchoma nyumba yetu moto. Moto huo ulianzishwa usiku wa manane, na ulitanda kwa kasi ya ajabu. Nilikuja kushtuka baada kuhisi maumivu makali usoni na kugundua kuwa chumba changu kina moshi mwingi sana. Na haukupita muda mama alifika chumbani na kunibeba huku nikilia kwa nguvu. Kwakweli siwezi kuyasahau maumivu nilioyapata usiku ule, na kwa sababu moti ulikuwa umeshaienea sana ilikuwa hakuna jinsi ya kutoka ndani ya nyumba hiyo. Mama alichokifanya alinitia kwenye friza, nikiwa humo ndani nilihisi friza hilo likisogea kwa nguvu huku nikisikia kelele za mama kutoka na maumivu anayoyapata baada moto huo kuanza kumuunguza. Aliendelea kulisukuma friza hilo lakini ghafla nilihisi kama likianguka na kweli kwasababu lilipiga chini kwa nguvu na kunifanya niumie. Baada hapo nilisikia mlipuko mkubwa sana, kutokana na baridi kuwa kali katika friza hilo nilipoteza fahamu. Nilikuja kushtuka niko hospitali, na swali la kwanza lilikuwa ni kumuulizia mamaangu lakini majibu niliokutana nayo yalikuwa ni ya kutisha sana. Huwezi amini ndani ya miezi minne baada kifo cha babaangu, nilimpoteza mamaangu tena kwa kifo cha mateso. Na taarifa nyingine mbaya ambao niliipokea baada kuamka ni kuwa upande wa kushoto wa uso wangu wote ulikuwa umeungua, na kutokana na umri wangu kuwa mdogo sana ilikuwa ni vigumu kufanyiwa plastic surgery. Nilikaa kwa sikukadha hospitali bila hata ndugu yangu mmoja kuja kunitembelea.

Baada wiki kupita huku kukiwa hakuna dalili ya mtu yoyote anaenifahamu kuja kuniona, daktari mkuu wa hospitali hiyo alichukuwa uamuazi wa kunipeleka katika kituo cha kulelea watoto yatima. Na kwasababu alikuwa hanijui jina na mimi sikutaka kumwambia mtu jina kutokana na kutonesha kidonda kibichi kwa sababu kila nnapolitaja jina hilo nawakumbuka wazazi na kuanza kumlaumu Mungu kwa kunitenda. Sasa sikutaka kumkosoa na kuingilia majukumu ya muumba wangu na hivyo ndivyo nilivyofundisha na wazazi wangu kuwa kila linalotokea basi limepangwa na Mungu litokee. Basi aliniandikisha kwa jina la Scarlette. Maisha mapya yalianza baada tu daktari huyo kuondoka, yule mama nilomkuta katika zamu siku niliofika alikuwa na roho nzuri. na alinieleza kuwa nijiandae kwa maisha magumu sana kutokana na tabia za watoto waliekuwepo katika kituo hicho na baadhi ya wasimamizi. Alinipelaka mpaka katiak chumba ambacho ndio nilitakiwa kulala na kunikabidhi kwa kiongozi wa chumba hicho. Yule msichana alikuwa anaitwa Harleen, alikua ni binti mwenye asili ya kihindi aliyechanganyika na muingereza. Yeye pia alikuwa na roho nzuri na alikuwa mchangamfu, alinipeleka mpaka kwenye kitanda ambacho kilikuwa pembeni ya kitanda chake. Alinikabdihi shuka kadhaa pamoja na nguo za kubadilisha, kwakweli nilimshkuru sana. Siku hiyo ilipita huku usiku kucha nikiwa macho bila kupata hata lepe la usingizi na usiku mzima nilikuwa nikilia huku nikijaumu kwa nini sikufa pamoja na mama ili tukaenda kuonana na baba tukiwa pamoja na kuungana tena kwa mara ya pili kama familia nzima. Hapo awali maisha katika kituo hicho yalikuwa magumu kutokana na kuwa mgen wa mazingira hayo, pia waschna wengine walinitenga kutokana na kovu langu usoni. Walinipa majina tofauti tofauti, wapo walioniita laana wakimaanisha kuwa nimelaaniwa. Kuna wengine waliniita jini, wengine waliniita mdudu. Yote kwa yote kila mtu aliniita alivojisikia, kwa kweli nilikuwa najiskia vibaya sana hasa nnapo kumbukua uzuri wangu ulioteketezwa na moto na kuuzika pamoja na jina langu.

Lakini kadiri siku zilivyokwenda nilizoea hali hiyo, baada wiki moja katika kituo hicho. Nilipelekwa shule kwa ajili ya kujiendeleza kimasomo. Nilifurahi sana na wakati huo huo nilikuwa na hofu, kwasababu ya sura yangu ambayo ilikuwa nyeusi upande mmoja na nyeupe uoande mwengine. Siku ya kwanza shuleni watu wengi walinicheka hasa wanaume, hakuna hata mwanafunzi mmoja aliekuwa akiniongelesha darasani. Wote walinitenga na wengine walikimbia mbio waliponiona, kuna baadhi waliziba pua wakati napita. Hali hizo zilinitesa sana lakini ningefanyaje na yote ni mipango ya muumba. Mwaka uliisha na hatimae tukafanya mitihani ya kuingia darasa la nne, nilipasi vizuri tu lakini sikuwa na furaha kabisa kwa sababu hakuna mtu alionekana kuthamini matokeo yangu. Baada likizo kuisha tulirudi shule kwa ajili ya mwaka mpaya wa masomo, niliamua kufanya mabadiliko kwa kuzichukulia changa moto zote zilizonikuta mwaka uliopita kama sehemu yangu ya maisha ya kila siku. Hivyo basi niliondoa wasiwasi kabisa na kuyavaa maisha yangu kwa sura ya kipekee, nilifanya hivo baada kugundua maana ya jina langu halisi kuwa ni SIMBA JIKE LA MIUNGU YA KIGIRIKI.



Niliamua kuwapuuzia wote wanaonikejeli na kuendelea na maisha yangu mweyewe mimi kama mimi bila kuendeshwa na woga uliokithiri. Hali hiyo ilipelekea hata hali yangu ya kimwili kutengemaa kutokana na kudhoofika na mawazo ya mwanzo kuhusu watu wanavonichukulia. "atakae nikimbia na akimbie, atakaeziba pua na azibe nnapo pita, mimi ni mimi na siwezi kubadilika hata kama ntacukia......

THIS IS THE REAL ME"



Hiyo ndio ilikuwa kauli mbiu yangu.

Basi jitihada zangu zote nilizielekeza kwenye masomo sasa, sikujali tena waliokuwa wakinikera. Japo nikuwa mzito kidogo darasani sikuwa tayari kukubali kufeli, hivyo niliongeza bidii mara dufu katika masomo. Siku moja nikiwa peke yangu nikipata chakula wakati wa mapumziko, nilisikia mtu akiniita. Nilipogeuka nikakutana na kijana mmoja mzuri sana, "samahani wewe ndio Scarlet" aliniuliza. Nikamjibu ndio, wakati huo upande ambao nilikuwa nimeungua na moto ulikuwa umefunikwa kwa nywele. Alitabasamu kidogo kisha akajitambulisha "mimi naitwa Adrian", pia alinambia kuwa yeye ni mwanafunzi mgeni pale shuleni hivyo wakati anaulizia sehemu akaelekezwa aje kwangu. Maskini hakujua kama aliambiwa aje pale ili anicheke kutokana na kovu langu kubwa usoni. "kwangu hukuambiwa uje nikuelekeze, umeambiwa uje kuniangalia usoni, nina kovu kubwa la moto" nilimwambia huku nikimkazia macho lakini cha kushangaza alikuwa kaitabasamu tu kisha akanijibu "unajua kuwa na kasoro si jambo la kujitenga na wengine, we huoni kama Mungu amekupendelea kukufanya hivo. Huoni kama kuna mantiki ya wewe kuwa hivyo labda ungekuwa kama wengine huwezi jua mangapi yangekuwa yamekufika mpaka sasa. Mimi naelewa ni kiasi gani upweke unanyonya na kumiza, muda wowote ukitaka mtu wa kuongea nae usisite kunitafuta rafiki yangu Scarlet" maneno alioongea yalikuwa na busara kubwa ndani yake hasa ukizingatia umri wake na darasa. Adrian ndio mwanaume wa kwanza kujenga nae urafiki, na kila wakati tuliokuwa tunaonana, nilikuwa nasahau kabisa karaha zangu.

Alikuwa mcheshi na muelwa, alifahamu wakati nilokuwa niko sawa na wakati ambao niliko sawa. Na alikuwepo nyakati zote nilizomuhitaji, ukaribu wangu kwake uliendelea kukuwa kadri siku zilivyokuwa zinasonga mbele. Tulimaliza elimu ya msingi na kuanz elimu ya sekondary na kwa bahati nzuri tulipata shule moja hivyo urafiki wetu uliendelea. Wakati tunaingia sekondary mimi nilikuwa na miaka kumi na sita na Adrian alikuwa na miaka kumi na saba, hapo nilianza kuhisi kitu tofauti kwangu lakini nilikipotezea. Urafiki wetu waliwakera sana wanawake wanaotaka sifa kutoka na wanaume tofauti hasa wa kitajiri kama Adrian. Nilianza kupokea vitisho kuwa niache kujipendekeza kwa Adrian. Ukweli maneno hayo yaliniumiza sana na kuamua kumuita Adrian na kumueleza lakini kabla sijamaliza kuongea Adrian alinivuta karibu na kunikumbatia kisha akanambia "mimi na wewe tumetoka mbali sana, hakuna mtu anaekujua vizuri zaidi yangu. Wewe ni rafiki wangu wa damu, wa kufa na kuzikana na wala yasikutishe maneno ya wajinga wewe wa puuze tu" maneno yake yalinipa faraja kubwa sana, ukiunganishe na mkubatio ndio kabisa. Basi maisha yaliendelea hivo hivo huku wenye wivu wakizidi kuumia, siku moja uongozi wa shule ukatangaza sherehe ndogo ya msimu wa joto. Ilikuwa ni sherehe ya kucheza maarufu kama "dancing ball", nikiwa sina hili wala lile Adrian alinifuata na kuniomba niwe mweza wake katika usiku wa sherehe. Nilikataa kwa kisngizio cha kutokujua kucheza lakini akanambia hilo si tatizo na kwa sababu kulikuwa na wiki nzima kabla ya sherehe basi angenufundisha kucheza. Nilijaribu kutoa sababu nyingi ili mradi tu nisiende kwenye sherehe lakini alinizidi ujanja na mwisho nikakubali, basi kunzia siku hiyo tulikuwa tunakutana sehemu na akawa ananifundisha kucheza mchezo aina ya blues. Nilishangaa kuona kwa jinsi nilivyokuwa mwepesi katika mchezi huo wakati darasani nilikuwa mzito sana kupita maelezo kuelewa. Siku moja kabla ya sherehe alikuja na box la wastani na kunikabidhi kisha akanambia natakiwa kilichokuwa humo wakati wa sherehe. Sikulifunua hapo tuliendelea kufanya mazoezi mpaka tukamaliza na kuondoka tukikubaliana nimsubiri nje ya kituo nnacho kaa siku ya pili kwa ajili ya kwenda huko kwenye hiyo sherehe. Nilirudi nyumbani na kukaa kitandani kisha nikalifungua box, macho yalinitoka kama mjusi aliebanwa na mlango baada kukuta gauni kubwa lenye rangi ya dhahabu, lilikuwa zuri kupita kiasi. Pia nilikuta kinyago cha dhahabu kikiwa kiana ujumbe juu "kama unaona aibu kutokana na sura yako, vaa hichi". Nilitabasamu kidogo na kulifunga box hilo kisha nikaliweka pembeni ya kitanda changu.
 
91 - 92
Siku ya pili jioni nilianza maandalizi na kwa msaada wa Harleen nilimaliza mapema, nilipotoka ndani kila mtu alitoa macho huku wakionesha kutoamini wanachokiona mbele yao. Kila mtu aliongea neno lake, yote kwa yote walinisifu kwa kuniambia "umependeza kama sio wewe vile rangi mbili usoni". Tulicheka wote kutokana na kuwa nilishazoea kuitwa majina kama hayo, na huo ulikuwa ni utani tu. Nilitoka mpaka nje ya kituo na wala sikukaa sana, nilishangaa kuona garo aina Rolls Royce nyeusi ikisamama mbele yangu. Mlango ulifunguka na Adrian akashuka, alikuja upande wa pili na kunifungulia mlango. Wakati naingia kwenye gari alininong'neza "umependeza sana", sikuwa na cha kusema zaidi ya kujichekesha tu kama mjinga. Safari ilianza huku kila mmoja akiwa kimya mpaka sehemu ya sherehe, baada ya kushuka nilimsikia akiongea na dereva wakem "Simon unaweza kwenda kujirusha au sio, nikikuhitaji nitakushtua", "sawa mkuu" yule dereva alijibu kwa furaha na kuondoka. Adrian alikuja nilipokuwa nimesimama na kunishika mkono kisha tukaanza kutembea kuingia ndani ya ukumbi, kila tuliepishana nae hakuacha kutushangaa na kutusifu. Kutokana na kinyang'o usoni hakuna alienitambua. Kinyang'o hicho kilikuwa kimeifunika sehemu yangu nlioungua yote, kiufupi kiliugawa uso wangu katika nusu mbili. Baada kuingia humo ndani nilishangaa kuona tunaelekea upande wa V.I.P, nilisita lakini Adrian aliminya kidogo. Tulifika kwenye meza moja iliopambwa vizuri sana na juu ilikuwa ilikuwa imeandikwa "THE GOLD PARTNERS" (marafiki wa dhahabu). Sherehe ilifunguliwa rasmi na ratiba ikawa inaendelea vizuri, Adrian aliniomba tukacheze na mimi nikakubali. Siku hiyo ilikuwa ni miongoni mwa siku nilizokuwa na furaha katika maisha yangu na pia ni miongoni mwa siku nilizopata huzuni kubwa pia. Tuliendelea kucheza kwa kuburudika na baada ya muda kidogo kukatangazwa mashindano ya kucheza wawili wawili. Adrian aliinua mkono na kunionyesha ishara na mimi niinue. Baada ya kupatikana washindani wa kutosha, mashindano yalianza na kuendelea mpaka mwisho. Mshindi alitangazwa kuwa ni "THE GOLD PARTNERS", ambao ni mimi na Adrian. Tulikabidhiwa tuzo na kurudi katika meza yetu kwa ajili ya kupata chakula.

Wakti tunaendelea kula nilianza kuhisi harufu flani hivi ambayo nilishwahi kuihis huko nyuma, moyo ulianza kwenda mbio huku kinyasho chembamba kikinitoka. Adrian alinishika mkono baada kugundua hilo, nilimuangalia na kumwambia kuwa nahisi harufu ya kitu kuungua. Na kweli kabla hata hajanijibu ghfla moto mkubwa ulirupuka na kila akaanza kukimbia upande wake. ukweli mimi na moto ni vitu viwili tafauti kabisha, nguvu ziliniishia na taswira ya uso wangu kuungua ikaanza kunirudia. "Scarlet tuondoke" nilisikia kwa mbali Adrian akinambia lakini hata hivo nilishindwa kinua hata kidole nikamjibu "wewe nenda tu mimi siwezi hata kuinuka hapa". Moto ulizidi kuwa mkali huku mimi na Adrian tukizidi kubishana juu ya swala zima la kuondoka. Adrian alipoona nmekuwa mbishi alininyanyua kwa nguvu na kunibeba kisha akaanza kukimbia, kwa muonekano wake sikutegemea kama angekuwa na nguvu kiasi kile.





Alifika mlangoni na kukuta moto umeshatanda, bila kusita alielekea uoande wenye dirisha na kulivunja kisha akanisukuma nje na yeye akafuata. Alipotua tu alitoa simu yake na kupiga "baba naomba helicopter yangu sasa hivi ije huku kwenye sherehe kuna mgonjwa amezidiwa" nilimsikia akiogea maneni hayo kwa masikio yangu, nilianza kuona kiza kinatanda machoni mwangu, na kabla sijafunga macho nilivua cheni yangu yenye kopa la dogo na kumkabidhi mkononi. Hakuijali aliitia mfukoni mwake na kwa mbali nikaanza kusikia mlio wa helicopter ila kabla haijafika nilipoteza fahamu kabisa. Sikujua nini kiliendelea, mawazo yagu ya mwisho kabla ya kufunga macho nilidhani kuwa ndio siku yangu yamwisho duniani..

Nilikuja kushtuka, na kitu cha kwanza macho alikutana na mwangaza mkali sana na baada kuangaza kulia na kshoyo nikagundua niko hospitali. Nilijivuta vuta ili nikae lakini nesi aliniwahi na kunirudisha kitandani na kunambia sijaruhusiwa kukaa. Baada ya dakika kumi alikuja daktari na kuchukua vipimo kisha akatoka na baada ya nusu saa alirudi tena na kuchukua kiti kisha akakaa pembeni na kuanza kuniuliza maswali. Mengi yalikuwa ni kunijaribu kama kumbukumbu zangu ziko sawa, na baada kurdhika na majibu alioyapata alinikabidhi bahasha nyekundu. Niliifungua ndani na kukuta kuna barua, niliitoa na kuanza kuisoma. "najivunia kuwa na rafiki kama wewe, umenitoa upweke ambao ulikuwa umejizika ndani ya moyo wangu. Kitu ambacho sikuwahi kukwambia ni kwamba mimi nilikuwa mpweke kama wewe baada ya kumpoteza mama yangu mzazi pamoja na pacha wangu wa kike Adriana na kaka zangu wengine wawili na dada mmoja. Lakini baada ya kukutana na wewe upweke huo wote ulinitoka na kujikuta nikiwa huru kabisa, nakushukuru kwa hilo. Pia asante kwa zawadi yako nzuri ulionipa lakini nasikitika kuwa kwa sasa hatutaweza kuonana tena mimi na wewe mpaka pale Mungu atakapo tukutanisha tena kwa mara ya pili lakini kaa ukijua nakupenda sana. Nilipanga nikwambie siku ile ya sherehe na niliweka pete ya uchumba katika chupa yenye kinywaji lakini mambo yakaenda bila kutegemea. Nakuahidi kuwa nitakuhifadhia penzi lako ikibidi hata nizikwe nalo lakini nitakutafuta kwa ajili ukurasa mpya wa maisha yetu. NAKUPENDA SANA ARIELLA......WAKO ADRIAN" barua ilishia hapo na bila kutegemea nikajikuta nanyong'ojea na macho yangu yalishindwa kuhimili hali hio na kuanza kutoa machozi. Nililia kwa muda mrefu lakini jibu nililolipata ni kuwa yote ilikuwa ni mipango ya Mungu na kama amepanga mimi na Adrian tuoanane tena basi hakuna atakaeweza kuzia na kama amepanga vingine basi hakuna atakaeweza kubadilisha..

Baada ya baada ya siku mbili niliruhusiwa na kurudi nyumbani, daktari alinipa dawa fulani hivi ya kuondoa kovu japo alinambia kuwa kovo hilo haliwezi kuondoka lote kutokana na kuwa limekwenda ndani sana ya sura yangu. Hivyo dawa ingesaidia kuondoa ule uvimbe na kuirudisha sura yangu kuwa laini huku ikiacha alama ya weusi wa kimtindo. Nilirudi katika kituo nlichokuwa nakaa na kuanza maisha upya huku nikiwa nimepata funzo kuwa "ukijiona uko mpweke basi jua kuna ambae ni mpweke zaidi kuliko wewe" maisha yaliendelea na baada ya mwaka mmoja alikuja mzee mmoja na mkewe kwa lengo la kutaka mtoto wa kulea. Hivyo tuliitwa wote na kuelezwa kuwa mmoja kati yetu amgepata bahati ya kupata wazazi siku hiyo, hivyo tusiache nafasi hiyo ipite bila kutoka. Baada ya nusu saa alianza kuingia mmoja katika chumba maalum ambcho walikuwepo wanafamilia hiyo. Zamu yangu ilifika na kuingia, nilisalimia kwanza kisha nikakaa kwenye kiti. Yule mzee aliniangalia kisha akatabasamu na kunambia kuwa alikuwa na maswali machache anataka kuniuliza. Nilitikisa kichwa kuashiria nimemuelewa, "unaitwa nani" ndio swali la kwanza kuniuliza. "jina langu ni Scarlette Mark Anderson" nilimjibu jina kamili. "hivi una ndoto ya kuwa nani na kwanini" likuwa swali lake la pili na la mwisho, "nataka kuwa mtu ambae ataitumikia jamii bila kujali rika wala kabila kwa sababu furaha yangu ni kuona watu wakiwa na furaha" nilijibu huku nikimuangalia usoni. Yule mzee alitabasamu na kumuangalia mkewe, yule mama alinigeukia na kuniuliza "usoni umefanya nini". Nilimueleza kila kitu na swali jingine aliloniuliza lilikuwa "hujisikii vibaya au aibu kutembea na njiani na sura kama hiyo". Kwa upande fulani nilihisi kama amenidhalilisha lakini sikutaka kuonesha wazi. "hapana sijiskii aibu kabisa tena nahisi faraja kutembea kama nilivo bila kuificha sura kwa sababu hivi ndivyo nilivo na hata kama nitiaficha siwezi kubadilika....THIS IS THE REAL ME" hivyo ndivyo nilivojibu na kumwanagalia mama yule usoni kwa mbali nikamuona akitabasamu na kumgeukia mumewe kisha akatingiha kichwa. Baada ya hapo waliniruhusu nitoke ili waendelee kuongea na wengine. Baada ya muda kidogo kupita wote tulikuwa vyumbani mwetu. Aliingia msimamizi wetu na kuniita, aliongoza njia na mimi nikafata nyuma mpaka katika chumba kingine. Huku nilimkuta yule mzee na mkewe wakiwa wanaongea, walipotuon waligeuka na kuniangalia huku wakitabasamu. "hongera Scarlette umepata wazazi wa kukulea sasa" aliongea yule msimamizi wetu. Nilifurahi sana japo sikuonesha wazi kiasi nimefurahi, basi taratibu zote zilifuatwa ikiwemo kubadilishwa jina la baba na kuitwa Scarlette G. Jackson ambalo ni jina la mzee huyo.

Niliwaaga wenzangu na kuwaahidi kuwa nikipata nafasi nitawatembelea, tuliondoka hapo kituoni na siku hiyo hiyo tulioanda ndege na kuja America. Tokea siku hiyo maisha yangu yalibadilika kabisa, wazazi hao walinipenda sana kama mtoto wao wa kuzaa. Nikiwa na miaka ishirini Baba alikuja akiwa na karatasi mkononi na kunikabidhi kisha akakaa pembeni kwenye kochi na kuongea "ulisema unataka kuitumikia jamii ili iwe na furaha, basi nafasi hiyo imetoka kujiunga na kitengo cha polisi" aliongea maneno hayo huku akitabasamu. Nilisogea pale alipo na kupiga magoti mbele yake na kwa mara ya kwanza sikumuangalia kama baba bali nilimwangalia katika cheo chake, combat aliokuwa ameivaa ilikuwa imechafuka na vyeo vya kutosha vilivomtanabahisha mbele ya wengine na kuitwa General Griffin Jackson. "hii ndio kazi niliokuwa naitaka ila nilikuwa nashindwa niaizie wapi" niliongea na kuinuka kwa nguvu kisha nikamkumbatia "najua unataka kulinda heshima ya familia yako basi usijali hapa heshima na thamani ya familia hii itadumishwa mpaka mwisho wa dunia" nilimnong'oneza hilo wakati nimemkubatia. kwakweli sikuwahi kuona sikua liofurahi mzee huyo kama siku hiyo tokea nianze kukaa nae. Mama alikuja na kumwambia taarifa hizo nae alionekana kufutahi sana, walianda kijisherehe kidogo kwa ajili yangu. Na baada ya hapo niliijazo fomu ya kujiunga na mafunzo ya polisi, baba aliipeleka inapostahiki.



Alirudi nyumbani na fomu nyingine na kunikabidhi na kunambia kuwa natakiwa niripoti kituo kikubwa siku ya pili.Basi siku ya pili ilifika mapema na baba alinikabidhi suti nzuri sana na kunambia nivae. Baada hapo tuliungana na mama sebleni tukapata chai ya asubuhi kisha mimi na baba tukatoka kuelekea kituo kikuu. Tulifika na baba akaniacha hapo kisha yeye akaelekea makao makuu ya jeshi ambako alikuwa ameitwa. Niliingia ndani na kukuta atu wengine washafika, kuna baadhi waliponiona walianza kucheka lakini wala sikuwajali kabisa. Niliwachukulia kama wapuuzi tu, baada muda kidogo alikuja mkuu wa kituo hicho na kuanza kutueleza mambo kadhaa. Baada ya hapo wanawake tulielekezwa katika chumba maalum kwaajili ya kuchukuliwa vipimo mbali vikiwemo vya magonjwa. Baada kumaliza mchakato huo tuliambiwa tufike katika kambi maalum kwa ajili ya mafunzo kuanza.

Basi nilirudi nyumbani nikiwa na furaha sana, nilimueleza mama kila kitu na alionekana mwenye kufurahi sana. Baada ya hapo kila mtu aliendelea na majukumu yake na jiobi ilipofika baba alirudi lakini alikuwa tofauti na alivyoondoka asubuhi. Alionekana mwenye huzuni sana, mama alijaribu kumdadisi lakini hakuongea kitu bali alimpatia karatasi. Mama nae baada ya kuisoma alianza kunyong'onyea, ilibidi niichukue na mimi niisome na hapo ndio nikagndua kwanini wote wamenyong'onyea. ilikuwa ni barua ilioandikwa na kusainiwa na raisi wa nchi hii ikimueleza baba kuwa amelitumikia taifa sana hivyo alitakiwa kustaafu na kupumzika ili awaachie wengine waendelee kupeperusha bendera.

.

Kitu hicho kilmuuma sana baba hata mama pia, basi nilimsogolea na kumwambia kuwa kila kitu kinachofanyika ni mipango ya Mungu. Labda kwa wakati ule alikuwa anatakiwa akae nyumbani aendeshe maisha ya kawaida ili alipe ule muda wote aliokuwa mbali na mama. Niliongea nae sana mpaka mwisho akaelewa na kuchangamka tena, mama aliandaa chakula cha usiku tukala na kila mtu akaelekea chumbani kwake kupumzika. Siku ya pili mapema baba aliamka na kupeleka barua ya kukubali kustaafu, alirudi nyumbani akiwa mchangamfu kama kawaida na kuungana na mimi pamoja na mama. Siku chache mbele iliandaliwa sherehe ya kuagwa na mheshimiwa raisi, na hapi alikabidhiwa medani ya dhahabu ya General bora katika kulitumikia taifa lake.
 
93 - 94
Siku ya kuripoti mafunzoni ilifika na mapema niliwasili katika kambi tulioambiwa, tulipewa maelekezo yote yaliokuwa yanatuhusu na baada hapo tukaanza mazoezi. Kwakweli yalikuwa mazoezi magumu sana kuliko nilivofikiria, ulifika wakati nilifikiria hata kutoroka lakini kila nilipokumbuka hadi niliompa baba nilipata ujasiri na kuendelea na mazoezi. Nilichunika chunika vya kutosha mpaka basi. Ila mwisho nilizoea maumivu na kuendelea na mazoezi bila shida yoyote ile. Muda wa mazoezi ulimaliza na tulikabidhiwa vyeti vyetu pamoja na nguo za kazi, siku hiyi ilikuwa ni ya furaha sana kwa kila mtu ambae alishieiki katika mazoezi yale magumu. Baada ya sherehe fupi tulipew ruhusa ya kurudi nyumbani huku tukisubiri kupangiwa vituo vya kufanyia kazi. Baba alionesha furaha ya hali ya juu sana, alinifanyia kasherehe kadogo hivi. "mwanangu jukumu ulilobeba sio dogo na sio kila mtu atakua na furaha na wewe, kwa hiyo ujiandae vilivo" maneno yalitoka kinywani mwa baba akinihusia. Nilitikisa kichwa kuashiria nimemuelewa, baada ya siku ya mbili nilipokea simu kuwa nimepangiwa kituo kikuu. Hiyo ilikuwa furaha nyingine kwa sababu sikupangiwa mbali na nnapo kaa. Siku ya pili niliwasili kituoni na kutambulishwa kituoni pamoja na kutambulishwa kwa mtu ambae nitakuwa nashirikiana nae. Alikuwa anaitwa Mike, alikuwa mtu mcheshi sana na alikuwa mchangamfu na mchapa kazi. Mike alikuwa mzoefu katika kazi hio, alikuwa na zaidi ya miaka mitatu. Mwanzo kila mtu alinisangaa kituoni kutokana na kovu langu usoni lakini kadiri siku zilivyokwenda walinizoea na kutokana na kujichanganya kwangu nao basi ilikuwa rahisi sana kupata marafiki wengi. Baada ya wiki moja nilipangiwa kazi ya kwanza nje ya kituo, na ilikuwa ni kuongoza msafara wa waziri mkuu katika eneo karibu na kituo chetu. Haikuwa kazi ngumu kabisa hasa ukizingatia ilikuwa ni kufunga njia tu wakati msafara unapita. Nilimaliza na kuripotu kituonim, Maisha kama askari wa kawaida yaliendelea kuwa mazuri huku kila siku sifa zangu zikizidi kutapakaa kutokana na uchangamfu wangu.

Siku moja nikiwa na Mike katika mgahawa mmoja hivi nikipata chai, ghafla tulisikia mlio wa risasi na bila kuchelewa tulitoka huku mikono ikiwa viunoni ambako kulikuwa na bastola zetu ndogo. Tulishuhudia gari moja likitupita kwa kasi huku mtu mmoja akiwa ametoa kichwa nje na kushambulia, tuliingia kwenye gari yetu na kuanza kuwafukuza. Ukweli Mike alikuwa dereva mzuri sana maana aliweza kumudu gari na kukwepa gari nyingi akiwa katika mwendo kasi. Nilitoa kichwa nje na kuipiga gari tuliokuwa tunaifukuza risasi katika tairi ya nyuma na kusababisha ipoteze muelekeo na kugonga nguzo pembeni. Walishuka watu watatu na kuanza kutushambulia, kwa bahati mbaya risasi moja ilimpata Mike begani. Sikuhitaji kufikiria mara mbili, niliteremka kwenye gari na kujificha pembeni kwenye mlango kisha nikatoa radio call na kuomba msaada. Wakati nasubiri msaada mashambulizi yalizidi kuwa makali kawa sababu wale majambazi walikuwa wanatumia silaha nzito sana. Wakati nikiendelea kushambuliana nao nilishutuka mlango ukifunguliwa na Mike akajiangusha chini kisha akanipa ishara niende nyuma kwenye buti. Nilifanya hivo bila kuchelewa, nilifika nyuma na kukuta buti limeshafunguliwa, nilikuta bastola aina ya shotgun na SMG. Nilibeba zote mbili na kurudi mbele ambako Mike alikuwa akiendelea kupambana nao. Nilimkabidhi SMG lakini akanambia nitumie mimi yeye akachukua shotgun. Hapo sasa moto ulizidi kuwa mkali maana sasa uwezo wa silaha ulikuwa unafanana. Baada ya dakika chache msaada ulifika na hapo tukafaikiwa kuwakamata, gari ya wagonjwa ilifika na Mike pamoja na raia kadhaa waliojeruhiwa katika pambano hilo waliwahishwa hospitali punde baada ya kupatiwa huduma ya kwanza. Niliporudi kituoni, mkuu wa kituo aliniita ndani moja kwa moja nikajua kuwa hizo ni lawama. Lakini haikuwa hivo, mkuu wa kituo alinisifu kutokana na ujasiri wangu hasa ukizingatia bado nilikuwa mgeni kati anga hizo. "karibu katika matatizo" mkuu wangu aliongea maneno hayo ambayo kwa haraka sikuweza kuifahamu maana yake, Baada ya hapo niliruhusiwa kurudi nyumbani kupumzika. Lakini nilipofika nyumbani nilimkuta mzee akiwa amevimba kwa hasira, nilipojaribu kumuuliza kuna tatizo gani hakunijibu kitu na kuinuka akaingia zake ndani. Hapo kichwa kilijaa mawazo, basi niliingia chumbani kwangu na kujifanyia usafi kisha nikatoka. Nilipofika ukumbini nilimkuta mzee akiwa anaangalia taarifa ya habari, nilimsalimia kisha nikakaa pembeni yake. "jemedari mzuri anazuia uhalifu na wakati huo huo ana hakikisha mtu asiehusika hapati jeraha lolote, na pia jemedari mzuri ni yule anaehakikisha mwenzake hajeruhiwi" alianza kuongea maneno hayo kisha akaniangalia na kunambia "umefanya vizuri lakini unatakia ujitahidi na kuhakikisha usalama wa raia". Baada kuongea maneno hayo alinikabidhi karatasi nyeupe ambayo haikuandikwa kitu, kisha akanipa ishara nisiongee kitu na niihifadhi ile karatasi..

Baada maongezi mafupi na baba chakula kilikuwa tayari, wote tulisogea mezani na kupata chakula cha usiku. Tulipomaliza niliaga na kuingia chumbani kwangu kulala, na kutokana na uchovo wa mchana, usingizi ulinizoa nilipogusa tu kitanda. Nilikuja kushtuka baada kuota ndoto mbaya sana, nilipoangalia saa nikagundua ilikuwa saa kum na moja usiku. Niliamka na kujiandaa, niliingia jikoni na kuandaa chai na vitafunuwa vya asubuhi. Nilipomaliza niliandika ujumbe na kuuacha mezani kisha nikatoka. Kitu cha kwanza nilichokifanya, nilielekea hospitali kwenda kumuangalia Mike ambae alikuwa anendelea na matibabu. Baada ya hapo nilielekea kituoni kwa ajili ya kuanza majukumu yangu ya kila siku. Kila mtu kituoni alikuwa akinisifu, na magazeti hayakuwa nyuma nayo. Kila gazeti liliandika linavojisikia "tunahitaji polisi kama huyu", "Waabudu matatizo kaeni pembei, simba jike kaingia mtaani". "mamilioni ya pesa yaoolewa". Hivyo ni baadhi ya vuchwa vya habari vya magazeti machache, niljifanya kama siyashughulikii lakini moyoni nilikuwa nnafuraha na kichwa kilikuwa kikubwa kama dunia kwa sifa. Niliendelea na majukumu yangu ya kila siku kama polisi, baada ya mwezi mmoja Mike alirudi kazini na kuendelea kama kawaida. Wakati huo jina langu lilikuwa lishasambaa na kila mtu alikuwa anataka kunijaribu na kila aliefanya hivo alikutana na kisiki. Baada ya Mike kurudi alianza kunipa mazoezi mengine ya kupigana, kila siku baada ya kazi tulikutana Gym na kuoata mazoezi kadhaa ya kujiweka powa. Maana alinambia kuwa niko hatarini sana kutokana na sifa zangu, mpaka majambazi sugu na wale wanasiasa watakuwa wananiwinda hivyo ni lazima niwe fiti, nisiwe nategemea silaha tu. Na pia alinishauri nihame nyumbani ili familia yangu iwe salama kutokana na mikono ya wabaya. Nililiwasilisha wazo hilo kwa mzee nae hakupinga alikubali na taratibu za kutafuta nyumba zikaanza, haukipita muda nilikuwa na kwangu. Kumbuka hapo nilikuwa na miaka ishirini tu na tayari nilishakutana na vikwazo vingi sana katika kazi yangu.Niliendelea na majukumu yangu huku nikiendelea kupokea mafunzo ya ngumi kutoka kwa Mike, ambae alionekana kama komando. Maana mazoezi aliyokuwa ananipa hayakuwa na tofauti na yale nliokuwa nayaona katika TV na movie mbalimbali wakifanya makomando. Miaka miwili ilipita huku nikiwa nimepandishwa cheo mara mbili, siku hiyo baada ya kumaliza mazoezi. Mike aliniita na kunambia kuwa anataka kuanambia kitu. Mapigo ya moyo yalianza kudunda na kihasho chembamba kikaanza kunitoka. "nimemaliza kazi niliopewa na General, natumai umeiva vya kutosha sasa" aliogea maneno hayo na kuniacha njia panda na kumuomba anielezee. Na hapo ndio akafunguka kuwa yeye ni Leutenant General Mike Kings, na alipewa kazi ya kuhakikisha kuwa naiva vya kutosha katika mafunzo ya kijeshi hasa kwenye mkono.







Na hapo akanitonya kitu kuwa kuwa polisi ni maandalizi ya kuelekea katika jeshi la nchi hiyo. Baada ya mazungumzo hayo aliniaga na kunambia kuwa tutakuja kuonana tena labda jeshini katika mafunzo maalum. Kisha akaondoka, nilikaa kitako kwanza huku nikijiambia mwenyewe kuwa naota na nikiamka kila kitu kitakuwa sawa. Lakini ukweli ulibaki kuwa ukweli tu, maana siku ya pili nilipofika kazini nikakabidhiwa msaidizi mwengine na nilipouliza kuhusu Mike nikaambiwa kuwa amehamishwa kituo. Hapo sasa nikaamini kuwa ndio ulikuwa mwisho wa kuonana na Mike.



Baada ya miezi sita tokea Mike nilipokea barua kuwa nimeitwa katika makao makuu ya jeshi, na bila kuchelewa nilielekea huko. Nilishanga kumkuta baba akiwa katika Gwanda zake za Kijenerali huku pembei akiwa amesimama Mike katika combat takatifu ya Lt. General. Baada ya robo saa waliingia watu wengine sita wakiwa wameongozana na vijana ambao walikuwa mapolisi kama mimi kisha tukaelekezwa katika chumba maalumu cha vikao. Hapo alisimama baba na kutoa salamu kisha akaanza kuonge "najua wengi mtajiuliza kwanini mumeitwa hapa, ila ukweli ni kuwa toke mwanzo nyinyi mlichaguliwa kujiunga na kikosi maalum cha kupambana wahalifu sugu. Natumai wote mumewahi kusikia kikosi kinachoitwa "THE PIRATES". Na wengi mlikuwa mnadhani ni stori lakini kikosi hichi kipo na ndio kinachopambana na wahalifu sugu hapa nchini na je ya nchi. Na sheria, ili ujiunge na kikosi hichi ni lazima uanze katika ngazi za askari wa kawaida. Hivyo basi hongereni na karibuni katika anga za majanga".

Kuna kitu sikukielewa na nlipotaka kuongea kitu, mzee alinipa ishara kuwa ninyamaze. Baada ya kikao kile kifupi cha utambulisho tulipelekwa katika chumba maalum na kupigwa picha kisha tukaruhusiwa turudi katika maeneo yetu ya kazi na kuambiwa kuwa hiyo ni siri na hakutakiwa mtu mwengine zaidi yetu kujua. Nilirudi kituoni kwangu nikiwa na maswali kadhaa lakini wa kuyajibu alikuwa ni mzee tu. Hivyo nilisubiria mpaka zamu yangu ilipokwisha na kuondoka kituoni lakini sikwenda nyumbani kwangu. Moja kwa moja nilielekea nyumbani kwa wazazi wangu na nilipofika tu baba alitabasamu na kunipa ishara nikae. Na kwa sababu mama alikuwa hayupo nikaona huo ndio mwanya pekee wa kumuuliza maswali yangu. Swali la kwanza lilikuwa ni ilikuwaje hasa akarudia gwanda wakati yeye alishastaafu. Nae akanijibu kuwa kustaafishwa kwake ilikuwa ni moja kati ya mipango ya raisi ili amkabidhi majukumu mengine ambayo yalikuwa ni siri. Akasema kuwa ile siku alipokwenda kukabidhi barua ya kukubali kustaafu, mheshimiwa raisi alimwambia kuwa hajastaafishwa bali alipewa majukumu mengine makubwa zaidi ya kuendesha kikosi maalum cha THE PIRATES.

. Yeye mwenyewe alishangaa baada kusikia jina hilo kwani alikuwa akidhani uwepo wa kikosi kile maalum ni maneno tu ya watu. Lakini mhshimiwa raisi alitaka baba akiongoze kikosi hicho ambacho alikuwa akikiongoza mwenyewe kwa muda mrefu, kutokana na majukumukuwa mengi aliamua kukibadhi kikosi hicho kwa mtu ambae ni mzalendo sana na hakuwa mwengine isipokuwa baba. Baada ya hapo ndio akapewa maelekezo yote yanayostahiki, baada kunieleza hivo kidogo roho yangu ilitulia. Basi tuliendelea na mazungumzo mengine mpaka mama aliporudi nikamsalimia na baada dakika kidogo niliaga na kuondoka. Nilirudi nyumbani nikiwa mwepesi kabisa baada ya maswali yangu yote kujibiwa, nilipumzika kwa amani kabisa usiku huo.

Siku iliofuata mapema niliamka na kufanya mazoezi kisha niakaoga na kupata kifungua kinywa, nilipomaliza kila kitu nilitoka na kuelekea kazini. Nilipofika niliambiwa nahitajika na bosi ofisini, na nilipoingia tu alinikabidhi karatasi ya uhamisho wangu. Nilijua tu mambo yashaiva, niliichukua karatasi ile na kurudi nayo ofisini kwangu. Niliifungua na kuanza kuiosoma mwisho iliandikwa "ukiupata ujumbe huu, mara moja fika makao makuu ya jeshi ukiwa na hii karatasi". Nilitoka ofisini kwangu mbio za ajabu na moja kwa moja hadi kwenye gari yangu na safari ikaanza. Nilikanyaga mafuta kisawa kwa mara ya kwanza sikuheshimu hata sheria za barabara. Baada ya dakika kumi nilifika makao makuu na kuwaonyesha ile karatasi wanajeshi waliokuwa getini. Walinipa maelekezo ni wapi natakiwa nifike, bila asante niliondoa gari na kuelekea sehemu ya megesho. Nilishuka na kuanza kukimbia, nilifika katika koridoo ambayo ndio nilipoelekzwa nikakuta karatasi imeandikwa "una sekunde sitini tu kufika juu kabisa ya jengo hili, ukichelewa helicopter ina kuacha" nilihisi kuchanganyikiwa hasa ukizingatia katika koridoo ile kulikua na watu wengi kweli. Nilianza kukimbia huku nikipigana vikumbo na watu wengine lakini wala sikujali, na nilipoona nazidi kuchelewa ilibidi nitumie mafunzo ya ziada ili kuwapita watu hao. Nilivua viatu huku nakimbia, hapo sasa nilianza kuwaruka kwa kukanyaga kuta za koridoo hio. Wengine niliwasukuma kwa nguvu na kuwatupa pembeni, niliongeza mwendo huku akili yangu ikiwa inafanya kazi kama computer. Nilifika juu ya jengo hilo lakini sikuikuta helicopter, nilianza kujilaumu lakini ghafla alitokea mtu kwa pembeni na kunipa ishara nimfate kisha yeye akaongoza njia. Tulifika katika chumba kimoja hivi na kuwakuta wengine wakiwa wananiangalia, mara walianza kupiga makofi. "umetumia sekunde hamsini na tatu" aliongea Mike huku akitbasamu. Baada ya nusu saa tulipewa mabegi na kuambiwa tuongozane na Mike mpaka juu kule, tulipofika tulikuta helicopter ikitusubiri. Tulipanda na safari ikaanza, tukiwa ndani ya chombo hicho tulipewa maziwa kuambiwa tujwe kwa sababu safari ni ndefu sana. Cha ajabu baada ya kunywa tu maziwa hayo macho yalianza kuwa mazito na mwisho wote tukapitia na usingizi mzito. Mimi nikuja kushtuka baada kuhisi hewa nzito, na nilipofungua macho nilishtuka baada kuona chombo tulichopanda kinawaka moto, niliwaangalia marubani wote walikuwa wakivuja damu. Nilianza kuwaamsha wenzangu wengine ambao kwa ujumla wetu tulikuwa saba, wote tulitoa nje ya chombo hicho. Baada kuridhika kuwa hakuna hata mmoja wetu alieumia sana, tulikaa kwanza huku kila mtu akitafakari kuwa ni jambo gani lililotokea. Kutokana na kiza tulishindwa kugundua tuko wapi, na ilibidi tulale hapo hapo. Siku ya pili mapema tuliamka na kila mtu alichukua begi lake alilopewa na kufungua, ndani ya mabegi hayo kulikuwa na combat pamoja na silaha nyepesi na vifaa vya mawasiliano.
 
95 - 96
Kila mtu alitoa nguo na kubadili kisha akachukua na vile vifaa maalum vya mawasiliano na kuweka sikioni. "jamani ndio tumepata ajali hivi, tunatakiwa tutafute njia ya kutokea" aliongea mwanaume mmoja kati yetu. Na wote tulikubaliana nae na pia tukakubaliana kuwa tutakaa pamoja hata litokee jambo gani. Kila mtu alijipanga vilivyo na wakati naendelea kukagua begi langu nikakuta ramani, niliitoa na kuitandika chini kisha kwa pamoja tukaanza kuiangalia kwa makini. Mschana mmoja alitoa kampas na kuweka juu ya ramani hio, wakati tunendele kukagua ramani hio tukaona alama ya fuvu. Tukakualiana kuwa tunaelekea hapo kweye hiyo alama, baada hapo tulisimama na safari ikaanza huku tukiwa tunapiga stori mbili tatu ili kupunguza safari. Baada ya masaa sita mfululizo ya kutembea tulifika pahali tukakuta makazi yaliokimbiwa na watu kabisa. Majumba ya eneo hilo yalikuwa yamevunjika na kubomoka, sehemu hiyo ilitawaliwa na vumbi na moshi. "jamani hapa tunatakiwa tuwe makini sana" niliongea huku nikitoa bastola yangu ndogo na kuishika vizuri mkononu. Na wengine wote waliniunga mkono nao wakatoa za kwao na tukaaanza kutembea taratibu kwa umakini wa hali ya juu kabisa. Tulitembea huku macho yetu yakiwa wazi na kuangaza pande zote, ghafla tulianza kusikia milio ya risasi. Ilibidi tujibanze pembeni na hapo sasa kila mtu akawa muoga kukaa mbele, ilibidi nijitolee kuwa kiti moto. Nilishika bastola yangu kisawa na kucungulia, kwa mbali nilimuona mtu akiwa amejibanza sehemu huku akiwa na bastola. Niliwageukia wenzangu na kuwaambia nilichokiona, baada kushauriana tukaaanza kukimbia ukuta baada ya ukuta. Cha ajabu yule mtu alikuwa hashambulii lakini tulipomkaribia zilirindima risasi kama mvua, ilibidi tugawanyike makundi mawili ili kumchanganya. Tukawa tunasogea taratibu, na alipowashambulia wenzangu kundi jingine. Nilichomoka sehemu nilio kwa kasi kubwa na kubirngitia kabla hata hajageuka nilipo nilifyetu risasi iliompata kifuani na kumfanya aanguke kama mzigo.

.

Tulimsogelea na kumuangalia, baada kuhakikishakuwa ameshakufa tayari. Nilirudisha bastola yangu ndogo kiunoni na kubeba ile AK47 aliokuwa anatumia adui yetu. Safari iliendelea kwa umakini wa hali ya juu huku mara kadhaa tukishambuliana na watu. Kadri muda ulivyokwenda walizidi kuwa wengi lakini tulifanikiwa kupita eneo hilo bila hata mmoja kupata majeraha makubwa zaidi ya michubuko tu. Baada ya kutoka eneo hilo tuliingia porini na kwa vile tulitembea muda mrefu bila kupumzika na hasa baada ya kupata ule mshikemshike tulijikuta tukiwa tumechoka sana na kuamua kupiga kambi ndani ya msitu huo ili siku ya pili. Tuligawana majukumu, wengine walitengeneza mahema na wengine tuliinia vichakani kutafuta kuni za kuwashia moto. Baada ya kazi zote kukamilika, tuligawana majukumu ya ulinzi usiku huo. Wawili walilinda na wengine walila, baada ya masaa matatu wale walikuwa wanalinda walikuja kuniamsha mimi na mwenzangu mmoja tukaendelee na zoezi lile wakati wao wanapumzika. Baada ya masaa matatu mengine tuliwaamsha wengine waendelee na kazi ya ulinzi lakini mimi sikurudi ndani kulala.



Niliendelea na wale wengine mpaka asubuhi, palikucha na kila mtu alijiandaa kuendelea na safari. Kwa kweli njaa ilikuwa inauma sana, siku nzima tulikuwa hatujala baada ya kunywa ya maziwa yaliotulaza. Wenzetu wawili walikuwa wameshaanza kulegea, lakini ilibidi wajikaze tu maana safari haikuwa ndefu tena. Baada ya masaa mawili tulifika katika geti kubwa. Tulishangaa kweli baada kwaona wale marubani ambao tuliamini walikuwa wamekufa katika ajali ya ndege wakiwa wanatusubiri getini. "hongereni kwa kumaliza mafunzo ya awali" waliongea wanajeshi hao na kutukabidhi kila mmoja wetu chupa ya maji. Baada ya hapo tuliingia ndani ya kambi hiyo kubwa na kupelekwa katika sehemu ya kula na kupata chakula. Kila mtu alikula kama chakula kinataka kukimbia, chezea njaa wewe.

Baada ya kumaliza kula tulipelekwa katika vyumba vyetu vya kupmzikia na kuambiwa tupumzike mpaka pale tutakapoitwa. Niliingia chumbani kwangu na kujilaza na viatu vyangu, na kutokana na uchovu wa hali ya juu usingizi ulinichukua gubigubi. Nilikuja kushtuka baada ya kusikia mlango ukigongwa kwa nguvu. Niliufungua na kukutana na Mike ambae alinipa ishara nimfuate, tulitembea kama dakika tano kisha tukaingia katika chumba maalum. Mike alwasha TV kubwa, macho yalinitoka baada kuona matukio yote tulioyafanya katika mafunzo ya awali. Kumbe tukio zima lilikuwa linarikodiwa, pia alinionyesha makosa tuliyatenda wakati wa kozi nzima. Baada ya kumaliza aliinuka na kunipa ishara niondoke.
Nilirudi chumbani kwangu na kuendelea kupumzika, huku nikiwaza kama nitaweza kumaliza kozi nyingine maana ni balaa. Jioni tuliitwa na kupata chakula cha jioni kisha tukapelekwa kwenye chumba kingine na tukaambiwa tusubri humo. Baada ya dakika mbili hivi aliingia mtu mmoja na kutukabidhi funguo za gari kila na kila mmoja wetu alipewa funguo ya kwake. Baada ya kukabidhiwa fungo hizo tuliambiwa turudi vyumbani mwetu ili kuchukua mabegi yetu na kisha tukutane katika uwanja wa maegesho ya gari. Tulifanya hivo na kufika eneo husika, tulipewa maelezo kuwa tunatakiwa tufike katika bandari fulani hivi. Na safari hio kwa kawaida ilichukua siku tatu lakini tuliambiwa tufike katika bandari hiyo ndani ya masaa arobaini na nane. Hapo nadhani utaelewa kuwa tulitakiwa tundeshe vipi, basi baada ya maelezo hayo tulipewa ruhusa na kila mmoja aliwkenda kwenye gari yenye namba iliofanana na namba ya funguo alipewa. Tuliwasha gari na safaro ikaanza, safaru hio ilianza karibu na kiza kungia, tuliendesha kwa umakini wa hali ya juu japo mwendo ulikuwa mkubwa sana. Safari hio iliendelea usiku kucha bila kupumzika, tayari mpaka asubuhi tulishatumia zaidi ya masaa kumi na mbili na tulikuwa hatujamega hata robo ya safari. Hapo mimi binafsi nikaona kuna dalili za kuchelewa. Kwa kupitia kifaa maalum cha mawasiliano niliwaambia wenzangu kuwa tumechelewa hivo tunatakiwa tuongeze mwendo zaidi. Mwanzo walinipinga kutokana na kuhofia kupata ajali, na nlipoona hawataki kukubaliana na mimi nikajisemea isiwe tabu kwa sababu kila atakula alichokivuna. Niliweka gia na kuamua kukanyaga mafuta kisawasawa, na gari nayo ilitii kwa kutimua vumbi la kutosha katika barabara hiyo ya vumbi. Nlikuwa makini sana huku mikono ikiwa metulia katika usukani, nilitembea kwa mwendo kasi huo kwa muda mrefu sana. Wenzangu nilikuwa nimewaacha umbali mkubwa sana, kuna wakati nilianza kuhisi uchovu na ikabidi nisimamishe gari. Nikatoa dumu moja la maji na kuanza kujimwagia ili niondoe uchovu kisha nikarudi kwenye gari na kuendelea na safari.

.
Tayari masaa ishirini na kadhaa yalishapotea na kiza kilianza kuingia tena, lakini gari ilikuwa na taa zenye mwanga za mkali sana. Hivyo haikuwa shida kutembea mwendo ule ule wa kibabe. Nilzidi kukanyaga mafuta huku nikiwa na lengo niimalize safari hiyo chini ya masaa arobaii na nane. Ghafla mvua kubwa ilianza kunyesha na kutoka na njia ile kuwa ya vumbi, ilipolowa iligeuka na kuwa tope. Ilibidi sasa nipunguze mwendo ili kuepuka kuteleza, mara kadhaa gari ilitaka kukwamba lakini asante kwa alietengeneza ile gari na kuiweka mashine yenye nguvu sana huku ikiwa inasukumwa na matairi yote manne. Nilitembea hivo kwa muda kidogo kabla kuamua kutembea tena kwa mwendo kasi japo ilikuwa hatari lakini bado nilikuwa nataka niweke rikodi mpya ya kutembea masaa machache zaidi. Ilkuwa hatari lakini sikujali kabisa, baada ya masaa kadhaaa mvua ilikata na cha ajabu zaidi baada mwendo wa dakika kama tano hivi nilikuta njia yenye vumbi kama ile mwanzo utadhani mvua haikunyesha kabisa. Niliangalia computer yangu ili kujua wenzangu nimewaacha kilometa ngapi, baada kuona kuwa nimewaacha kilometea zaidi ya kumi nilitabsamu na kuuendelea na safari kwa mwendo uleule. Niliangalia saa yangu na kugundua kuwa nilishatumia masaa thalathini, niliongeza mwendo tena na kufikia wakati nikamaliza kisahani chote. Mshale wa kuonyeshea spidi iliogonga mwisho kabisa, laiti kama gari ingepanda jiwe dogo tu basi leo ingekuwa stori nyingine kabisa. Baada ya mwendo wa masaa manne hatiamae niliikuta barabara ya lami na kwa mbali niliana kuona makazi ya watu japo walikuwa si wengi sana. Nilipunguza mwendo kwa sababu tayari nilishaingi mjini, lakini cha ajabu hakuna mtu alieshughulika kila mtu aliendelea na shughuli zake kama kawaida. NIliumaliza mji na kuanza tena kazi ya mwanzo, kwa sababu barabara ilikuwa ya lami sikupata shida sana kwenda kasi. Kwa mbali niliaza kuona bahari, nilipata matumaini kuwa huenda nikawa nishafika lakini wapi, nilitembea kwa masaa matano mpaka nipoaza kuona bandari na tayari nilishatumia masaa arobaini na na tatu na baada saa moja nilikuwa tayari nimeshafika sehemu tuliotakiwa kufika. Mtu aliekuja kunipokea hakuwa mwengine bali alikuwa ni baba, nilifurahi sana maana nilikuwa na siku kama mbili hvi sijamuona. Alinionyesha ishara ya dole gumba kama kunisifia na baada ya masaa manne waliingia wenzangu, wakati huo tayari mimi nilishaoga na kujipumzisha. Siku ya pili mapema tuliitwa na kuanza kukabdhiwa nafasi, mimi nilichaguliwa kuwa kiongozi na jina nililopewa likuwa ni RED BUTTERFLY (kipepeo mwekundu).
 
97 - 98
Kila mtu alifurahi kutokana na cheo alichopewa, baada ya hapo tuliruhusiwa kuzunguka ndani ya meli hiyo kubwa ilikouwa ikakata mawimbi kuelekea nisipopajua. Baada ya safari ndefu hatimae meli ilitia nanga katika kisiwa kimoja hivo, tulishuka na kuzama ndani ya msitu wa kisiwa hicho. Tulikuja kutokea mbele ya ukuta mkubwa sana ukiwa umechorwa alama ya fuvu. Wakati nikiendelea kushangaa ghafla ukuta huo ulianza kufunguka na kisha tukaingie ndani. "karibuni nyumbani" aliongea Lt general Mike, kwa kweli ukisikia watu wanamaficho basi haya yalikuwa balaa maana hiyo mitambo ilikuwa inalinda eneo hilo si mchezo kabisa. Tuliingia mpaka ndani na kupelekwa katika vyumba vyetu kisha tukaambiwa tukutane uwanjani baada ya nusu saa. Nilijilaza kitandani huku nikiwaza juu ya mazoezi yote niliopitia maana kama mtu ungekuwa na moyo laini basi kama sikuacha ungekuwa ushakufa maana acha kabisa. Muda ulipotoka nilivaa gwanda na kutoka nje, huko tulikutana na Mike akiwa kama msimamizi wetu. Kuanzia siku hiyo tulianza kufanya mazoezi yenyewe sasa, na yalikuwa magumu kupita maelezo. Kutegua viuongo katika mazoezi hayo ilikuwa ni jambo la kawaida sana, mazoezi hayo yaliendelea kwa muda wa mwaka mzima. Na baada ya safri ndefu hatimae mazoezi yaliisha na hapo sasa tukaapishwa rasmi kuwa PIRATES, ikiwa ni pamoja na kuchorwa tatu ya fuvu kwenye mkono wa kulia" Scarlette alipofika hapo alinyamaza na kumuangalia Alex usoni, alikuwa ameacha mdomo wazi huku akimshanga mwanamke huyo ambae kwa kumuona nje hivi utadhani ni mlaini sana kumbe ni moto wa kuotea mbali. "sasa ikawaje baada ya kumaliza mazoezi" Alex aliuliza huku akionekana kunogewa na simulizi ya maisha ya bidada Scarlette.
Scarlette alikaa sawa na kuendelea "baada ya kumaliza mazoezi hayo tulipewa ruhusa ya kurudi majumbani kwetu, huku tukiambiwa tutakapohitajika basi tutaambiwa. Nilifurahi sana kwa sababu ni muda mrefu sana sijamuona mama, tulikunja kunja na siku ya pili mapema tulipanda helicopter na kurudi majumbani. Lakini taarifa niliokutana nayo nyumbani ilikuwa si nzuri, mama alikua hospitali kalazwa baada kuzidiwa. Haraka niliacha vitu vyangu na kubadili nguo kisha nikachukua gari na kuelekea hospitali, aliponiona aliyabasamu na kuniita. Nilisogea na kukaa pembeni yake kisha akafunua shuka na aliokuwa amefunikwa na kunionesha tatoo ya fuvu mgongoni kwake. Macho yalinitoka baada kugundua kuwa hata mama pia alikuwa ni mmoja kati ya wanajeshi wa kikosi cha siri na pia kilichonichosha zaid ni pale aliponambia kuwa alikuwa akiniftilia kila siku katika mazoezi. Kwa maana nyingine na yeye alikuwepo katika sehemu zote nilizopita. Baada ya hapo ndio akanieleza kuwa hata baba pia alikuwa ni mmoja kati yao na huko ndipo walipokutana na pia huko ndio chanzo kikubwa cha wao kupoteza uwezo wa kuzaa baada kupigwa na mionzi mikali sana ya bomu. Tuliongea mengi sana na alionekana kuchangamka sana, muda wa kutizama wagonjwa uliisha.
.



Nilimuaga na kuondoka huku nikiahidi kurejea siku ya pili, nilirudi nyumbai kwangu na kujipumzisha kitandani na kutokana na kuwa ni muda mrefu sikupata kulala vizuri basi usingizi ulinichukua na kutokomea katika ulimwengu wa ndoto za kivita tu. Nilikuja kushtuka baada ya alarm ya saa kulia, nilishuka kitandani na kupasha mwili kidogo kisha nikaingia chooni na kujisafisha. Nilipata kifungua kinywa na baada ya hapo nilingia kwenye gari na kuelekea hospitali, lakini nilipofika katika kile chumba alichokuwa amelazwa sikumkuta. Wakati natoka nilikutana na baba ambae alionekana kuwa na majonzi huku akijikaza asitoe machozi. Nilimsogelea na kumshika mkono kisha nikamwambia anipeleke alipo mama. Na hapo ndio akaniambia tayari alishatangulia mbele za haki, nilijikaza sana nisilie lakini nilishindwa na kujikuta nikitoa machozi kwa kilio cha kimya kimya. Nilimuomba baba turudi nyumbani kwenda kuanda taratibu za mazishi, alikubali na tukarudi nyumbani. Lakini nilichogundua kua baba alikuwa akijizuia kulia, nilimshika mkono na kumwambia kulia sio ishara ya udhaifu. Ni kama nilifungua bomba la maji maana alianza kulia kama mtoto mdogo, lakini wala sikumnyamzisha nilimuacha aendelee kulia mpaka atakaporidhika. Baada masaa kadhaa alikuwa kashatulia na hapo tukapanga taratibu za mazishi na siku ya pili mapema tulimzika na kutokana na heshima yake mpaka raisi alihudhuria mazishi yake. Baada kumaliza kila mtu alitawanyika na kurudi nyumbai kwake, pale makabrini nilibaki mimi na baba tu.
.

Baada ya dakika chache tuliondoka na kurudi nyumbani, siku za mwanzo zilikuwa ni miongoni mwa siku ngumu sana kwa baba kutokana na mazoea na mapenzi aliyokuwa nayo juu ya mke wake. Lakini hakukuwa na jinsi kwani kazi ya Mungu haina makosa, kwani binaadamu wote safari yetu ndio hiyo moja. Baada ya mwezi kupita mzee alikaa sawa na kuendelea na majukumu yake kama kawaida. Siku hiyo tukiwa nyumbani ghafla ilituwa Helicopter na bila kuchelewa mzee alinipa ishara tuingie na safari ya kuelekea kambini ikaanza. Tulifika huko na kukaribishwa na barua maalum iliyotoka kwa mheshimiwa raisi. Mzee aliisoma kwa makini kisha akaichana na kuichoma moto, baada ya hapo alituambia baada ya nusu saa tukutane katika chumba cha mikutano. Kila mmoja wetu aliingia chumbani kwake na kuvaa combat ya kazi na baada nusu wote kwa pamoja tulifika katika chumba cha mikutano. Baba alisimama na kuanza kuongea "nimepokea ujumbe kutoka ngazi ya juu kabisa katika nchi hii, ujumbe huu umeandikwa kwa mikono ya raisi pamoja na kuweka saini yake. Kuna mtu mmoja ametekwa na watu wasiojulikana, lakini kupitia vyombo vya kiintelijensia wameweza kugundua alipopelekwa. Mtu huyo ni muhimu sana na tunatakiwa tumrudishe nyumbani na kama itashindikana basi auwawe ili kulinda siri aliokuwa nayo". Wote tulishangaa na mimi nilijiuliza ni kitu gani hasa alichokuwa amekificha mpaka raisi afanye maamuzi magumu kiasi kile. Chini ya uongozi wa Lt general Mike pamoja kikosi kichanga chetu tulipewa masaa sabini na mbili tuwe tumekamilisha kazi hiyo. Baada mzee kutoa amri hiyo, Lt general Mike alituomba tumfate mpaka katika chumba cha kupanga mikakati.
Tuliingia ndani ya chumba hicho na kukuta silaha kadhaa ambazo ndizo zingetumika katika kufanikisha kazi hiyo, tuliambiwa tukae kwenye viti kisha taa zilizimwa na kuwashwa projector kubwa. Lt genaral Mike aliinuka na kuanza kutueleza "hizo picha mnazo ziona katika runinga hii, zimepigwa muda si mrefu kwa kutumia ndege aina ya drone, picha hizo ni za kambi anashikiliwa huyo mlengwa wetu. Kambi hii ipo katikati ya msitu mmoja mkubwa sana, upande mmoja wa msitu huo kuna bahari na hiyo ndio njia tutakayoingilia katika kambi hiyo. Kutoka eneo la bahari mpaka ilipo kambi hiyo ni mwendo wa masa matano ya kukimbia bila kusimama. Na ijulikane kuwa tukiondoka hapa tuna masaa sabini na mbili tu mpaka kurudi hivyo umakini wa hali ya juu unatakiwa uzingatiwe katika kufanikisha kazi hii, tumeelewana", sote kwa pamoja tuliitika kuwa tumeelewa. Basi baada ya hapo tuliondoka na kuelekea sehemu ambayo kulikuwa ndege ikitusubiri. Tulipanda na safari ikaanza huku kila mmoja akionekana kuwa wababridi kutokana na kuwa hio ndio ilikuwa kazi yetu ya kwanza tena ilikuwa ni hatari sana. Tulikaa angani kwa muda wa masaa zaidi ya matano huku kila mmoja akiomba mungu wake kazi ile iende vizuri. na kumbuka tulikuwa kiloketa kadhaa kutoka kwenye kisiwa amabcho tulitakiwa kufika. Ndege ilishuka mpaka usawa wa bahari na hapo tukapewa ishara ya kuruka, haikuwa ngumu kwa sababu mazoezi kama hayo tulishafanya kipindi cha nyuma. Tulikuwa watu nane tu, na baada kuingia ndani ya maji ndipo kasheshe ikaanza tulitakiwa kuogelea mpaka nchi. Lt general Mike alikuwa sawa kupita maelezo, aliogelea kwa kasi ya ajabu huku sisi tukimfata kwa nyuma mpaka tukafika kisiwani. Tulitoka kwenye maji na kupumzika kwa nusu saa kabla ya kuendelea na safari, mapumziko yalipokwisha Lt general Mike alitupa amri ya kusimama na kuendelea na safari.
Safari ilikuwa ni mchakachaka tu huku kila mtu akiwa makini, tulitembea kwa muda wa masaa zaidi ya matatu mpaka tukawa tumebakiza kilometa nne mpaka kufika kweye kambi ile. Hapo ndio tukaambiwa tuweke kambi kwaajili ya kuendelea na operesheni siku ya pili. Mpaka wakati huo tulikuwa tumeshatumia masaa kama tisa hivi kati ya masaa sabini na mbili tuliopewa. Kila alifuahi sana aliposikia kupumzika, tuliweka vitu chini lakini wakati tunataka kutandika vitambaa maalum vya kulalia chini. Lt G Mike alituambia kuwa kulala ni juu ya miti na si chini, baada ya hapo kwa kasi ya ajabu alikimbia na kukanyaga mti kisha akashika tawi na kupotelea kwenye miti. Hatukuwa na budu kumuiga, tulipanda kila mtu na mti aliochagua. Kufika kwenye tawi kila mtu allitoa kamba yake na kujifunga vizuri kisha tukalala, nilikuja kushtuka baada kitu kunipiga kichwani na nilipoangalia chini nilimuona LTG Mike akiwa anawashtua wengine. Nilishuka kwenye mti na kunawa uso kisha LTG Mike akatowa karatasi yenye ramani na kuitandika chini kisha akaanza kutupangia majukumu. Sara pamoja Alfred wakapangiwa utunguaji(sniper). James, Kyle na mimi tukapangiwa kazi ya kuzama ndani ya kambi na kutoka na mlengwa. LTG Mike na wawili waliobaki ambao ni Lameck na Rosequeen walikuwa ni wakuwapoteza maadui zetu. Baada kila mtu kukabidhiwa majukumu yake tuliagana na kukubaliana tukutane ufukweni baada ya kazi hiyo kuisha. Kila kikundi kilishika njia yake na kutokomea upande wake, tuliwasiliana kupitia vifaa maalum vya mawasiliano. Mimi na wenzangu watatu tulisogea mpaka karibu na fensi kubwa ya kambai na kujificha. Kwa mbali tulishuhudia wale walinzi wanaokaa juu kama masniper, wakianguka mmoja baada ya mwengine mpka waote wanne wakaisha. Baada ya hapo tulimuona LTG Mike na kikosi chake wakiingia kambini na kuuwasha moto. Wakati huo huo na sisi tukapenya bila kuonekana katika kambi hiyo. .
Na kwa sababu tulikuwa tunajua hasa target wetu yuko wapi, hatukupata shida sana kumtafuta. Shida ilikuwa ni kukabiliana na wale wanajeshi wa kambi hio. Tulifanikiwa kufika ndani kabisa na kukumta target akiwa hoi, nilikimbia mbio mpaka alipo na kumfungua kamba kisha nikaampa maji yeye chemichal maalum yenye kuzalisha nguvu kwa wakati mfupi. Kisha nikamkabidhi bastola moja kisha safari ya kutoka ikaanza. Huku nje milio iliokuwa inasikika ilikuwa ni hatari tupu, risasi zilikuwa zinarindima si masihara. Tulifanikiwe kutoka nje ya kambi hiyo bila shida yoyote na kuanza safari ya kuelekea ufukwenu ambapo tulikubaliana tukutane. Huyo jamaa tuliomuokoa alikuwa balaa, alikuwa hapigi risasi zaidi ya moja kwa kila aliepita mbele yake. Alihakikisha hakosei, tulitembea kwa kasi bila kupumzika mpaka tulipohakikisha tumefika mbali na kambi. Tuliwasiliana na wengien ili kujua mambo yakoje upnde wao, na wao walitujibu kuwa wako njiani wanaelekea ufukweni. Baada ya kupokea taarifa hizo tulianztena safari huku tukiwa makini tusije kamatwa. Baada ya masaa mawili na kidogo hivi tulifika ufukweni na kujifcha sehemu. Nusu saa baadae wenzetu wengine waliingia na hapo sisi tuakatoka tulitoka na kuelekea walipo wenzetu. Yule jamaa tuliemuokoa alipofika tu alipiga salute na kumpa heshima LTG Mike, tulikaa hapo ufukweni kwa robo saa tu kisha zikapita ndege mbli za kivita na kuelekea kule kwenye kambi na hazikupita hata sekunde chache tuliskika milio ya mabomu. "mission accompilished", LTG Mike aliongea maneno hayo kisha akaongea na code maalumu na baada ya nusu saa ilitua ndege katika maji na safari ya kuelekea kambini ikaanza.
 
99 - 100



Tulipokewa kwa furaha kubwa sana, na nilishangaa pale nilipomuona raisi mwenyewe akiwa ni miongoni mwa watu walikuja kutupokea. Tulishuka kwenye ndege na kuelekea mpaka alipo raisi na kutoa heshima. Raisi alitabasamu na kutupongeza kwa kazi nzuri tulioifanya. Baada ya mapokezi hayo tulikea katika ukumbi wa vikao na raisi akaongea maneno mawili matatu hasa upande wa uaminifu. Na alituasa kuwa bora mtu afe kuliko kutoa siri ya nchi, baada kikao kifupi raisi aliondoka pamoja na yule jamaa tuliekwenda kumuokoa.

Kila mmoja wetu alitawanyika na kurudi chumbani kwake kwa ajili ya kupumzika maana shughuli tuliokwenda kuifanya haikuwa ndogo. Kutokana na uchovu niliokuwa nao usingizi mzito ulinichukuwa na kuanza kuota ndoto kuwa niko kule katika kituo cha kulelea watoto yatima. Katika ndoto hiyo alikuja mtu kunitembelea lakini hakuruhusiwa kuniona na kuondoka. Nilishtuka kutoka usingizini baada ya kuota ndoto hiyo ambayo sikujua maana yake hasa ni nini. Ah kwa sababu ilikuwa ni ndoto tu niligeuka upande wa pili na kuendelea kulala.
Niikuja kushtuka tena baada kusikia mlango wanu ukigongwa, nilikurupuka kitandani na kwenda kuufungua na kumkuta anae gonga ni baba. Aliingia ndani na kuketi kwenye kiti kidogo, tuliongea mambo mawili matatu kuhisiana na kazi ile. Baada ya maopngezi hayo nilimuuliza kama naweza kupata likizo fupi nataka niende nikatembee kule kwenye kituo cha kulelea watot yatima. Alinijibu kuwa inawezakana lakini nisikae sana maana ndio kwanza kazi ilikuwa imeanza.
Nilimshukuru na kuanza kupanga mipango ya safari, siku ya pili niliondoka kambini kwa ndege maalim na kupelekwa hadi kwenye kambi ya kawaida ya jeshi na hapo nikapewa ari ya kuelekea uwanja wa ndege. safari haikuwa kubwa sana nilifika uwanja wa ndege na kukata ticket tayari kwa safari. Muda wa safari uliwadia na kuodoka, safari yote sikupata usingizi hata kidogo kwani nilikuwa na shauku ya kutaka kufika tu. Baada ya masaa kadha kuwa angani hatimae ndege ilikanyaga ardhi na abiria wote tukashuka. Kwangu kufika huko tu ilikuwa ni furaha tosha na mtu hakuhitaji kuuliza kwani hata sura yangu pekee ilinekana kuwa na furaha sana.

Nilitoka nje ya uwanja na kupanda taxi na kumpa maelekezo nnapowenda, baada ya hapo safari ilianza huku njia nzima nikiwa nimetabasamu. Alinifikisha mpaka nje ya geti la kituo kile, nilimlipa na kushuka. Kwa mwendo wa taratibu nilijongea getini ambako nilikutana na mlinzi, nilimuomba kuingia ila alikataa kutokana na kile alichoamini kuwa siku hiyo haikuwa siku ya kuwatembelea mayatima.
nilijaribu kuongea nae lakini alikataa kata kata kunikubalia, nilimuelewa na kuamua kukaa pmbeni ya kituo hicho nikiwa natumaini labda huenda akatokea mtu ambae ananifahamu. Nilikaaa zaidi ya masaa mawili bila kutokea mtu yoyote, mwisho nilikata tamaa. Ila wakati nataka kuondoka nilimuona mwanamke kwa mbali akiwa anakuja maeneo ya getini. Nilipomuangalia kwa makini nikagundua kuwa alikuwa Harleen, bila kutaka nilijikuta namkimbilia na nilipomfikia nilimrukia na kumkumbatia. Lakini nilipomuacha niligundua kuwa amenikodolea macho.
Nilitabasamu kuzitoa nywele zangu upande wa uso ambao nilikuwa na kovu, hapo sasa nilimuona akianza kutabasamu na kunikumbatia tena kwa nguvu. Kwa pamoja tuliongozana na kuingia ndani, nilishangaa kukuta kumebadilika sana. Harleen alinambia kuwa yeye amekuwa matron wa kituo baada ya yule aliekuwepo mwanzo kufariki.
Tuliongea mambo mengi sana na hapo ndio nikagundua kuwa nilikuwa nimepitwa sana na maisha ya kawaida kutokana na muda mwingi kuwa kambini. Baada ya maongezi marefu alinionesha chumba ambacho ningelala, yeye alielekea jikoni kuanda chakula wakati mimi nikiingia ndani kwa ajili ya kuoga.
Baada ya saa na nusu alikuja kunigongea na kwenda kupata chakula, wakati tunakula alinambia kuwa Adrian alirudi kuja kunitembelea lakini nilikuwa nishaondoka. Hivyo aliacha barua kutokana na kuwa wakati huo nilikuwa sina hata simu. Tulipomaliza kula Harleen aliingia chumbani na kurudi na barua mkononi na kunikabidhi..
Niliifungua na kusioma mpaka mwisho kisha nikatabasamu na kuendelea na maongezi menine na Harleen pamoja na waschana wengine. Niliendelea kufurahia maisha hayo ya uraiani kwa siku tatu. Siku ya nne nilipokea simu inayo nitaka niripoti kambini kambini haraka iwezekanavyo. Bila kuchelewa niliwaaga wenyeji wangu na kuondoka kituoni hapo.
Nilichukua gari mpaka nje mji kidogo kisha nikashuka na hapo nikapiga simu maalum na kuongea code za sehemu niliopo. Nusu saa baadae ilifika chopa ya jeshi nikapanda na safari ikaanza, baada ya masaa kadhaa chopa ile ilitua kambini na bila kusubiria niliruka na kukimbilia kwenye ukumbi wa vikao kwa ajili ya kuripoti.
Baada ya kuripoti nilikabidhiwa bahasha ndogo na kuifungua, kama kiongozi wa kikosi changu niliifunua bahasha ile na kusoma maelezo. Baada ya kujiridhisha na maelezo yaliokuwemo humo niliaga na kuondoka kwenye ukumbi huo. Nilitoa kifaa maalum kama simu kilichoitwa Jet telecommunicator (J.T.C). Nilibonyeza mara kadhaa kisha nikatuma ujumbe kwa wenzengu wote.
Baada ya dakika tano wote tulikuwa katika chumba maalum, niliwaeleza kila kitu. Mission yetu ilikuwa ya kuokoa watoto ambao wanatekwa nchi mbali mbali na kuuzwa nchi nyingine. Baada ya maelezo hayo tulikubaliana tukutane baada ya nusu saa kwa ajili ya kuelekea eneo la tukio ili kukamilisha kazi hiyo muhimu sana.
Tulikutana tena na moja kwa moja tukaelekea kweny ndege na safari ikaanza, njia nzima tulikuwa tunaongea mambo ya kawaida kama watu ambao tunakwenda kwenye sherehe. Rubani alituambia tukae tayari kwa ajili ya kuruka maana uokozi huo ulikuwa unafanyika baharini katika meli kubwa ambayo ndio ilikuwa inasafirisha watoto hao.
Na kwa sababu ilikuwa ni usiku, maadui zetu hawakufanikiwa kutuona wakatu tunatoka katika ndge. Bahati nzuri sana sisi hatutumii maparashuti kwa misheni za baharini labda chombo kiwe kinatembea. Tulipiga mbizi kwenye maji na kuogelea mpaka ilipo meli hiyo, kwa umakini wa hali ya juu tulipanda minyororo ya nanga na kufanikiwa kuingia ndani bila kushtukiwa.
Niliwakabidhi wenzangu majukumu kisha tukatawanyika huku tukikubaliana tuifanye kazi hiyo kwa siri kubwa sana ili kuwapunguza maadui zetu. tulijigawa katika timu za watu wawili wawili isipokuwa mmoja wetu tu, yeye alikuwa ni sniper hivyo alitafuta sehemu ya juu kabisa katika meli hityo na kujitega huko.
Kwa umakini wa hali ya juu tulianza kazi huku tukiwasiliana kwa vifaa maalum, kazi ilikwenda kama yulivyoipanga huku maadui zetu wakiwa hawajui nini kinaendelea. Tuliendelea na kazi ya kuwapunguza taratibu mpakatuliporidika ndio tukaanza kuwashambulia bila siri tena. Moto uliowaka ulikuwa si mdogo maana hata hao tuliokuwa tunapamabana nao walikuwa wanajihami kwa silaha nzito sana.
Baada mpambano wa takriban saa nzima tulifanikiwa kuiteka meli na kuwakamata wote waliohusika. Baada ya hapo tulikwenda moja kwa moja katika vyumba ambavyo walikuwa wamefungiwa watoto hao. Kwa kweli machozi yalinitoka baada kukuta watoto wengi sana ambao kwa muda ule walitakiwa wawe nyumbani kwa wazazi wao lakini wamejikuta wakichukuliwa kwaajili ya biashara.
Tulipohakikisha tumeidhibiti vilivyo meli hiyo, nilipiga simu makao makuu na kutoa taarifa kuwa kazi imekamilika. Tulikaa mpaka asubuhi ambapo zilifika meli kadhaa za serekali ya eneo la bahari tuliopo. Tuliwakabidhi watoto hao na sisi tukasubiria ndege helicopta ambayo ilifika na safari ya kurudi kambini ikaanza.

Njia nzima kila mtu alikuwa akijisifi kwa jinsi alivyo wachakaza maadui zetu, basi zilikuwa ni stori za damu tu. Tulifika kambini na kupokielea kwa shangwe kubwa. Baada ya siku hiyo sasa ikawa ni vita kati yetu na wanaojifanya wapindishaji sheria. Japo kikosi kilikuwa ni siri lakini kilikuwa tishio kwa kila mtu ambae anajua kabisa ni mkiukaji wa sheria.
Baada muda wote tulipandishwa vyeo na kuwa makando sasa, na mpaka tunafikia cheo hicho kuuwa kwetu ilikuwa jambo dogo sana. Yaani akili zetu ailijenga mazingira ya kuwa haziwezi kutulia ikiwa utapita muda mrefu bila kuingia kazini. Na kila mtu alifurahia kazi hii, ni kwa kazi hii tumetembea nchi nyingi sana na kujifunza tamaduni za watu mbali mbali.
Siku moja niliitwa na wakuu wangu na kukabidhiwa bahasha, niliifungua na kuisoma na kujikuta nikishangaa. Maana mission hiyo nilitakiwa kuwa mpelelezi na nitakiwa kuifanya peke yangu pasi na wenzangu kujua chochote. Nilikubali na nilianza maandalizi ya kuondoka kambini hapo kwa kisingizio cha kuumwa. Na wenzangu wote waliniamini na kunisindikiza katika ndege kwa majonzi makubwa sana.
Ndege hiyo iliondoka kambini hapo na moja kwa moja kuelekea mjini New York, ndege ilituwa katika uwanja wa jeshi na baada ya hapo nikapelekwa hadi ikulu kwa raisi na kukabidhiwa mafaili maalum. Niliyapititia kwa umakini wa hali ya juu sana na baada kuridhika niliruyarudisha kisha nikapewa passport mpya pamoja na kila kilichohitajika kwaajili ya kazi hiyo muhimu sana.
Baada ya hapo nilielekea nyumbani kwa ajili ya maandalizi ya mwisho ya safari hiyo, kwa wakati huo jina lilikuwa ni Judith. Nilipohakikisha kila kitu kipo sawa, niliamua kungia chooni na kuanza kujibadilisha muonekano maana niliambiwa kuwa kuna watu wakubwa wa nchi yetu wanashirikiana na hao nnao kwenda kuwachunguza..
Nilipomaliza kila kitu nilitoka na kupanda kitandani kwa ajili ya kupumzika, siku ya pili mapema nilitoka nyumbani na kuelekea uwanja wa ndege bila mtu yoyote kujua. Hilo nilifanikiwa kwa kiasi kikubwa baada ya kuzipunguza nywele zangu na kuwa ndogo kiasi. Dakika kumi baadae nilikuwa uwanja wa ndege tayari, na wala sikupata shida yoyote ile kwa sababu taarifa zangu zote zilikuwa tayari zipo kwenye mitandao ya nchi.
Muda wa kupanda ndege ulifika na abiria wote tuliokuwa tunalekea Hongkong tulipanda ndege na safari ikaanza. Njia nzima nilikuwa nawaza jinsi ya kuweza kuingia katika himaya ya ninaekweda kumchunguza. Kwa sababu nilielewa kabisa ni kiasi gani mtu huyo ni hatari, nikiwa naendelea kuwaza njia mbadala ghafla usngizi ulinichukua. Nilikuja kushtuka baada mtikisiko mdogo uliosababishwa na magurudumu ya ndege hiyo wakati yanakanyaga uwanja barabara za uwanja wa ndege wa Hongkong.
Tukiongozana na abiria wengine, tulishuka ndege na kuelekea sehemu ya ukaguzi. Baada ya kumaliza taratibu zote tuliruhusiwa kutoka nje ya uwanja, huko nilikutwa mji ukiwa umechangamka kweli kweli. Nilichukua Taxi na kumpa kikaratasi kidogo kilichoandikwa jina la hoteli, yule dereva alitabasamu na safari ikaanza. Aliendesha kwa muda wa nusu saa kabla ya kusimama mbele ya hoteli kubwa, nilimlipa kiasi cha fedha anachotaka na kushuka.
Nilisimama hapo nje nikaiangalia hoteli hiyo kwa makini kisha kwa mwendo wa haraka nikaanza kutembea mpaka mapokezi. Nilikamilsha taratubu zote na kuchukua funguo ya chumba changu na kuondoka. Nilipofika chumbani nilijibwaga na kutoakana na uchovu wa safari nilipitiwa na usingizi mzito. Nilikuja kushtuka baada ya simu yangu kuita, niliipokea na kuongea kwa dakika kama tano hivi. Nilipokata uliingi ujumbe ukinieleza sehemu ambayo nitapata kila ninachokitk kukamilisha kazi hiyo.
Niliweka simu pembeni na kuingia bafuni kwa ajili ya usafi wa mwili, nilimaliza na kujianda vya kutosha niliangalia saa yangu ya mkononi ilionambia kuwa ni majira ya saa moja usiku. Nilitoka chumbani kwangu na kuelekea chini ambapo niliacha funguo mapokezi kama desturi ya hoteli hiyo. Baada y kuikbidhi nilitok nje kabisa na kuanza kuangaza huku na kule nikitafuta sehmu ya kuanzia kazi yangu.
Kutokana na kuwafahamu kwa sura watu ambao natakiwa kuwachunguza, sikutaka kujipa shida sana. Niliulizia Casino ambalo ndilo vibosile hao hukuta kwa ajili ya kupanga mipango yao, haikuwa shida sana kuweza kujua lilipo casino hilo hasa ukizingatia nilitumia uschana zaidi. Niliweza kufika katika casino hilo, kufanya utaratibu wa kuingia ndani
 
101.

Naam wala sikubahatisha niliwakuta wanne kati ya nane walikuwepo sehemu hio, lakini kwasababu nilikuwa natafuta njia ya kwa karibu ili nipate taarifa zao, basi sikuwa na haraka kabisa. Nilitembea mpaka counter na kuagiza kinywaji na kuanza kunywa taratibu. Ila kwa kweli hakuna kilevi kilichokuwa kinanipangua akili, huwa nalewa lakini kila nnalofanya nilikuwa nalielewa kabisa.
Niliendelea kupata mvinyo wa kirusi huku nikisindikizwa na muziki laini wa kiingerea, muda wote huo wakati naendelea kunywa nikuwa namuangalia mmoja wao na kumkonyeza. Ah kam ilivyokawaida yenu wanaume, mschana akikuangalia sana eti amekupenda. Basi jamaa alijikusanya taratibu na kusogea sehemu nilipo.
Alipofika tu kwanza alinilipia kinywaji na kunambia kama nataka kuongeza, basi tukaanza kuongea mawili matatu huku ukiendelea kupata maji ya dhahabu. Na nilichagua pombe kali makusudu kumuangalia kama anamoto au nguvu ya gesi tu. Tuliendelea kunywa pale mpaka nilipomuona jamaa ameanza kurembuwa, ndipo nikamwambia tuondoke. Nae alikubali bila kinyongo, tuliongozana huku tumeshikana viuno. Wenzake walipomuona anatoka walimpigia makofii kama kushangilia ushindi wake. Moja kwa moja mpaka katika hoteli ambyo haikua mbali na casino lile.
Tulichukua chumba hapo na nikaagiza mtungi mwengine wa Red wine uletwe chumbani. Tulipoingia chumbani hata hatujakaa sana mlango uligongwa na nilipofunga nilimkuta muhudumu akiwa na chupa nilioagiza. Nilimshukuru na kuingia ndani, hapo sasa tulianza mashindano ya kunywa. Siku hiyo ni miongoni mwa siku ambazo nimewahi kunywa pombe nyingi kweli, shindano liliendelea mpaka jamaa akanoki na kuangakia kitandani.
Baada kuhakikisha kuwa amelala fofofo, nilitoa kisindano chenye dawa kidogo na kumdunga shingoni. Dawa iliokuwemo katika sindano ile inamfanya ahisi anafanya mapenzi kumbe anaota. Hapo sasa nikaanza kazi yangu ya kupekuwa, nilianza simu yake na nikanyonyo kila taarifa nilioikuta. Niliendelea na kazi hio mpaka niliporidhika, nikamvua nguo zote na kumfunika shuka halafu namimi nikalala pembeni yake.
Asubuhi mapema niliwahi kuamka na kuagiza kifungua kinywa, kilipofika ndipo nikamuamsha yule jamaa. Basi alipofungua tu macho alianza kutabasamu na kunushukuru kwa penzi zito nililompatia usiku. Aliingia bafuni na kuoga, alipotoka tulikunywa chai na baadae tukatoka hotelini hapo na kila mtu akachukua mia zake huku jamaa akiniachia namba yake ya simu,
Nilirudi hoyeli niliofikia na nilipoingia tu chumbani nilifungua begi langu na kutoa Laptop na kuchomeka microchip ndogo ambayo ilikuwa na taarifa zote nilizochukua kutoka kwenye ile simu. Baada ya kuzikagua vizuri na kuridhika, niliingiza code maalum kwenye computer yangu na kuzituma.
.
Nilitoa simu yangu na kuingiza namba fulani hivi ambazo pia niliziingiza katik simu ya yule jamaa jana yake. Hapo nikawa nimeunganisha simu yangu na yake bila yeye kujua.
Baada ya hapo niliingia bafuni, nilipotoka nilika kitandani na kuanza kuwafatilia kinaga ubaga. Usiku wa siku hiyo nilitoka kivingine zaidi nikiwa nimevalia wigi jeupe lililonibadilisha kabisa. Nilikwenda mpaka sehemu niliombiwa nitakuta kila nnacho kitaka kwa ajili ya kazi yangu. Baada ya kuhakikisha nimechukua kila ninachotaka, nilifunga safari ya kuelekea sehemu moja hivi ambako siku walikuwa na kikao.
Kwa msaada wa simu yangu niliweza kufika eneo la tukio bila shida, nilitoa kinyago cha dhahabu na kukivaa. Kinyago hicho kiliniziba sehemu yenye kovu la moto, kwa kutumia mbinu ninazo jua mwenyewe nilifanikiwa kuingia katika ukumbi huo na kujificha sehemu. Nilitoa kifaa maalum kidogo kinachoitwa microcamera na kuanza kurikodi mkutano mzima.
Kila kitu kilikwenda kama nilivotaka mpaka kikao hicho kinaisha, kasheshe lilikuwa kwenye kutoka eneo hilo. Maana ulinzi uliongezeka nje ile mbaya utasema alikuwa anakuja raisi, na kwa bahati mbaya wakati natafuta njia ya kutokea ghafla mlinzi mmoja aliniona na kuanza kunifukuza. Sikutaka kupambana sehemu ile kwa maana wao walikuwa wengi kweli kweli.
Nilikimbia kadiri miguu yangu ilivyonibeba na nilipoangalia nyuma walikuwa wameshaingezeka. Nilifika sehemu na kujibanza kwanza ili nivute pumzi, nilitoa bastola yangu ndogo na kuifunga kiwambo cha kuzuia sauti. Taratibu na kwa umakini mkubwa sana nilianza kuwapunguza mmoja baada ya mwengine, na hapo sijisifii lakini kilichowakuta nahisi waliopona walikwenda kusimulia wenzao.





Baada ya kusafisha njia yangu, niliondoka eneo hilo na kurudi hotelini nilipofikia. Nilichomeka ile micro camera kweny computer na kuanza kuangalia tena kikao kile, halafu kama kawaida nikaingiza code maalum na kuituma video ile.
Kazi niliiendeleza kwa umakini wa hali ya juu huku nikijitahidi nisijulikane mapema, maana niliielewa hatari ya kazi hiyo. Siku moja nilikuwa katika mawindo yangu kama kawaida lakini kikao cha siku hiyo kilihudhuriwa na watu wengi sana na kutoka mataifa mbai mbali. Jambo kubwa lilikuwa linaongelewa hapo lilikuwa ni PROJECT CODE X, mwanzo sikulifahamu vizuri lakini baadae kijasho kilianza kunitoka baada kusikia wingi wa jeshi linalohusiana na project ile.
Niliendelea kusikiliza wakati huo nikirudi mkutano mzima bila kushtukiwa na yoyote, ila wakati natoka kuna mzee mmoja alikuwa na combat flani hivi ya kipekee. Kwa haraka niligundua kuwa gwanda ile ilikuwa na ya nchi hii. Tulipishana mlangoni lakini aliniangalia sana kisha akatabasamu na kuendelea na mia zake. .
Nilirudi hotelini na kuituma ile video pamoja na picha ambazo nilizipiga kwenye kikao kile,baada ya nusu saa uliingia ujumbe ukinataka nifanye haraka nirudi kambini. Nilituma ujumbe kutaka kujua kwanini nirudi muda huo wakati nilikuwa naelekea mwisho kabisa wa upelelezi wangu. Nilijibiwa kuwa kuna mtu hatari sana, anaitwa General David. Huyo akikuangalia tu anajua kama wewe ni mpelelezi, hapo sasa nikarudisha kumbukumbu zangu nyuma na kumkumbuka mtu alieniangalia kisha akatabasamu.
Nilituma tena ujumbe mwingine ili nitumiwe picha, na haikupita hata dakika iliingia picha ya General David. Hapo sasa nikaona hali ya hatari iko mbele yangu, bila kupoteza muda nilichukua Cd maalum na kuitia katika computer. Cd hiyo ilikuwa ni virus maalum ya kuharibu computer ili kufuta ushahidi wowote ule. Baada kuhakikisha data zote zimeliwa kweye computer hiyo, niliingia nayo chooni na kutia kwenye jakuzi lililojaa maji na kuiharibu kabisa.
Nilirudi chumbani na kuchukua bastola zang ndogo nne na kuziweka kiunoni, pia nilikusanya makaratasi yote na kuyachoma moto. Nilipohakikisha nimeteketeza ushahidi wote, nilitoka chumbani na kuelekea kwenye lift. Taratibu lift ilianza kushuka huku mikono yangu ikiwa nyumakaribu na bastola zangu. Iliposimama tu nilizishika vizuri kwa ajili ya usalama zaidi, lakini nashkuru kulikuwa salama kabisa.

ITAENDELEA
BURE SERIES
 
102.
Nilitoka katika lift na kuelekea mapokezi ambapo nilikabidhi funguo na kuaga kisha nikatoka nje ya hoteli hiyo kwa tahadhari kubwa sana. Nilikodi taxi na kutafuta sehemu ili kutafuta sehemu salama kwa ajili ya kupitisha usiku ili siku ya pili nifanye utaratibu wa kurudi kambini. Lakini wakati naingia kwenye taxi hiyo nilimuona mtu ambae nilimfananisha akiingia kwenye gari nyingine. Hivyo basi nikamwambia dereva wa taxi aifaute ile gari.
Aliifata mpaka nje ya bar moja hivi, nilishuka na kumlipa kisha taratibu nikaanza kusoge kwenye bar hiyo. Lakini nikakumbuka kuwa nguo nilizofaa zilikuwa ni za kazi zaidi. ilibidi niingie katika duka la nguo la nguo la karibu na kubadilisha kwanza halafu nikaelekea bar. Nilifika na kutafuta sehemu na kukaa, dakika kumi baadae uliingia wewe (Alex) na kuanza kuniletea fujo. Natumai kilichotokea pale una kikumbuka vuzuri" Scarlet aliongea maneno hayo na kumuangalia Alex usoni.
Alex alikisa kichwa kuashiria kuwa anakumbuka vizuri sana, "duh pole kwa mkasa yote iliyokukuta" Alex alijikuta akimpa pole huku akitabsamu. Wakati akiendelea kuongea aliingia mtu mmoja na kuwapa taarifa kuwa chakula kipo tayari. "nina njaa kweli" Alex aliongea na kusimama jambo ambalo lilimuwacha Scarlet mdomo wazi. "ongoza njia basai bibie" Alex aliongea tena baada kumuona Scarlet amekodoa macho.
Alisimama na taratibu wakaanza kutembea kuelekea sehemu ya kupata chakula, watu wote waliokuwepo huko walimkaribisha Alex kwa tabasamu. Walikaa kwenye meza na kuanza kupata kula, wakati wakiendelea kula General Griffin alimuuliza Alex "hivi Alex unafahamu nini kuhusu C.O.D.E X". "mnata kufahamu kuhusu CODE X, nipeni wiki moja tu nifanye mazoezi halafu nitawaonyesha hilo ni balaa gani" Alex alijibu huku akitabsamu na kumuangalia General ambae alikubaliana nae.
Siku zilikatika na hatiame wiki ikatimia, siku hiyo asubuhi mapema Alex alitoka akiwa amevaa nguo za mazoezi. "General, habari za asubuhi" Alex aliongea alipofika sehemu alipokuwa amesimama mtu huyo. "leo ndio umesema utanieleza kuhusu CODE X", "ndio lakini nitakueleza kwa vitendo kwa maana nikikueleza kwa maneno tutakesha hapa" alijibu Alex huku akinyoosha nyoosha viungo kisha akaendelea "Mimi napasha lakini naomba uandae vijana kumi ambao unaamini wana uwezo wa hali ya juu katika kupambana bila silha, uniandalie mtunguaji mmoja mkali sana na mtu mmoja ambae unaamini kwenye kucheza na silaha ni hatari sana"
General aliwaita wanajeshi wote katika kambi hiyo na kuchagua wale wakali zaid kuliko wote katika kupamabana bila silaha akiwemo Scarlet. Alichagua na wengine kama alivyotaka Alex, "vipi wako tayari" Alex aliuliza baada ya kumaliza mzunguko wa hamsini katika kiwanja hicho. "ndio" General alijibu na kuwapa amri vijana wake waingie uwanjani nao wakatii. Kwa kwel kila mu alikuwa na hamu ya kutaka kujua Alex anataka kuwaonyesha nini. Wapo waliosema anataka umaarufu na wengine walisema amechanganyikiwa.
Basi Alex alikaa katikati ya duara la watu kumi na kutabasamu kisha akajisemea "like old days". kipenga kilipulizwa na wote kumi kwa wakati mmoja walimvamia, Alex hakuwa na papara kabisa kwani alikuwa akijiamini vya kutosha. Taratibu alianza kupambana nao na kadiri muda ulivyokwenda ndio mpambano ulizidi kupamba moto. Alipigana nao kwa muda wa dakika kumi na tano tu na wote kumi walikuwa chini hoi bi taabani.

.
Baada ya mpambano huo alikwenda mpaka kwenye meza maalum ya maji na kuchukua chupa mbili za maji na kurudi nazo mpaka walipo wengine. Alimkabidhi mwanajeshi mmoja na kumwambia azipeleke umbali wa mita mia mbili kisha azifukie nusu. Baada alimuomba mtunguaji (sniper) aliechaguliwa, "umeziona zile chupa mbili, moja ni yako na moja ni yangu na unatakiwa upige sehemu ya kifuniko" Alex aliongea na kuchukua bastola aina ya Riffle huku yule kijana akichukua bastola maalum ya masniper.
Kila mmoja alitafuta sehemu yake na kulala chini, kumbuka bastola ya Alex haikuwa hata na darubini na kuvutia kitu na kukiona kwa ukaribu zaidi. Kipenga kilipulizwa na wote kwa pamoja wakafyetua risasi, "kijana hujapiga kifuniko, umepiga kwenye shingo ya chupa" Alex aliongea huku akiikabidhi bastola yake kwa mwanajeshi mwengine. Yule aliepeleka zile chupa alirudi huku akiwa haamini kabisa kilichotokea.
Alizikabidhi zote mbili kwa generel na hapo sasa wote walitoa macho, chupa iliopigwa na Alex ilikuwa umetawanyika sehemu ya kifunikio tu na ile nyingine ilikuwa imetawanyika katika shingo. Baada ya hapo Alex alimuomba mtu aliechaguliwa upande wa utmiaji silaha, Scarlet aliingia uwanjani akiwa na bastola maalum zenye risasi za mpira wenye rangi. Alex alichuku bastolo yenye vigololi maalum ambavo hata vikimpat mtu hawezi kuumia sana. Kwa pamoja waliingiwa uwanjani kwa ajili ya kuonyeshana nani ni mkali zaid.
Kama kawaida yake General lipuliza penga na mmpambano ukaanza, na mpaka unaisha nguo za Alex zilikuwa kama wa walivyoanza ila nguo za Scarlet zikuwa zimejaa madoa ya risasi. "natumai general utakuwa umpeta jibu lako"Alex aliongea baada kuikabidhi bastola yake. "kijana hivi wewe ni mtu au mashine" General aliuliza kwa sintofahamu. "hahaha, mimi ni mtu wa kawaida mbona" Alex alijibu. "hapana wewe huwezi kuwa mtu wa kawaida kwa mambo ulioyafanya hapa leo hakuna atakae amini kama wewe ni mtu wa kawaida" General alijibu huku akionekana kutoamini kilichoyokea muda mfupi ulipita.
"Sasa subiri niwaeleza maana ya CODE X" Alex aliongea na wote walisogea karibu kusikiliza kwa umakini wa hali ya juu. "kirefu cha CODE X ni CINDREX OLTIVIASO DECA ENDROLINE X, hii chemical maalumu imetengenezwa kwa ajili kuwafanya wanajeshi kuwa hatari zaid. Ni project ambayo ni hatari sana kuliko watu wengi wanavyoifikiria, na mtu wa kwanza ambae ilitumika kimikali hii na kufanikiwa alikuwa naitwa Alen James. Huyo ndie aliekuw hatari zaidi lakinu ameshafariki tayari, mtu wa kwa hatari ni mimi Alex Jr au Project 75".
 
103.
Alex alinyamaza kidogo na kuwaangalia kisha akaendelea "Mimi nina uwezo wa kupiga risasi mita mia mbili bila kutumia darubini, pia nina uwezo wa kukwepa risasi na natumai mumeona baada ya pamabano na Scarlet. Na katika ubora wangu nina uwezo wa kupambana na makomando zaidi ya kumi na tano, sasa jiulizeni kambi ya kawaida ya vibaka naifanyaje. Na kwa wakati huu siko peke yangu, kuna wanajeshi wengine wengi wanaandaliwa na kikundi kinachojulikana kama WANAMAPINDUZI. Na harakati zote zile za kusakwa ilikuwa ni kuhakikisha wananizuia siingilia kati katika kufanikisha hilo" Alex alimaliza kuwaeleza kwa ufupi kuhusiana na Project CODE X.
Alex aliwaangalia wote kwa umakini wa hali ya juu sanana kugundua wasiwasi waliokuwa nao. "Kijana asante kwa kutifmbua macho maana ni muda mrefu sasa tumadili na kikosi fulani xha watu ambao hatuwajui" general aliongea huku akimshika bega Alex. "chochote kwa taifa langu" Alex alijibu kisha akapia salute kama ishara ya heshim. Walirudi ndani na kila mtu akaelekea upande wake, general alielekea katika chumba cha mawasiliani kwa ajili ya kuzifikisha taarifa hizo kwa raisi.
"habari yako muheshimiwa" General aliongea baada kuunganishwa ikulu na rais, "nzuri tu, pole na majukumu" Raisi alijibu. "asante mkuu, kuna video nitakutumia naomba uiyangalie kwa makini kisha tujadii kitu mkuu"."ok, hakun shida", General akampa ishara mtalamu wa computer na hapo akaituma video ambayo ilirikodiwa wakati Alex anaonyesha uwezo wake. Raisi aliiangalia mpaka mwisho, "naam general unataka tujadili kitu" Raisi aliongea baada kumaliza kuangalia video hiyo.
"Mi nashauri huyu kijana tumuunge na kikosi hichi kwa sababu atakuwa ni msaada mkubwa sana kwetu", "wewe umeamuamini?". "ndio mkuu, huyu ni mzalendo na haina haja ya kumtilia mshaka kabisa", "basi hakuna shida juu ya hilo, andaa taratibu zote zinazohitajika kuapishwa kwa kijana huyo. Mimi kesho asubuhi nitakuwa hapo kwaajili ya kumkabidhi gwanda zake". Walimaliza kuongea na kuagana, General alitoka katika chumba hicho na kumuita mtu maalum wa kuchora tattoo na kuongozana nae mpaka katika ukumbi maalum. .
Aliamuru wanajeshi wote waitwe, haukupita muda mrefu wote walikuwa katika eneo hilo. "msishangae kwanini nimewaita wakati sio muda mkusanyiko, lakini ni hivi nimeongea na raisi muda si mrefu na kumtumia video ambayo ilirikodiwa wakati wa mazoezi ya Alex. Hivyo basi ametoa agizo kuwa Alex awe miongoni mwetu katika kulitumikia taifa" General aliongea na uwanja mzima ulilipuka kwa sauti za kushangilia.
Alex alipewa amri atoke mbele kwaajili ya kuchorwa tattoo la kikosi hicho, bila kupinga alivua fulana yake na kusogea. Mchoraji alianza kazi yake huku watu wakishuhudia tukio hilo, "ebwana unajua huyu ndugu habari nyingine". "huyu jamaa ana hatari kwakweli, sasa ikiwa huyu mmoja tu yuko hivi hao wengie sijui wakoje". "lakini si mbaya, tunae mmoja wao kati yetu hivyo tutajifunza kupitia yeye jinsi ya kukabiliana nao katika mpambano" hayo ni baadhi ya yaliokuwa yakiongelewa na baadhi ya wanajeshi wakati zoezi la uchoraji likiendelea.
**************
"may day, may day mimi ni rubani wa kikosi cha KING's SQUAD (K.S)" Alisikika kijana mmoja akiongea kupitia kifaa maalum, "rodger, tunaomba nambari yako tuhakikishe" upande wa pili ulimjibu. "Nambari yangu KS099" alijibu rubani huyo, "tueleze kuna nini". "nimefanikiwa kuupata mzigo lakini sidhani kama nitafika nao, kuna ndege nyingine nne za waasi zinani fukuza na mpaka muda huu tunaongea wenzangu wawili wameshatung....." kabla hajamaliza mawasilino yalikata na kila control tower ilivojaribu hakupatina.
Ripoti ya kutunguliwa ndege hiyo ilifikishwa kwa raisi, wakati huo alikuwa anajianda kuelekea katika kambi ya THE PIRATES kwaajili kumuapisha kijana Alex. Baada ya kupewa taarifa hiyo alitoa amri kuwa iandikwe haraka na apewe hiyo document aondokea nayo. Hazikupita hata dakika kumi ilikuwa imeshakamilika na raisi aliichukua na kuondoka nayo. Safari ilianza huku raisi akiwa na wasiwasi sana kutokana na tarofa muhimu alizokuwa nazo rubani aliepotea.
Baada ya masaa kadhaa hatimae ndege ilikanyaga uwanja wa PIRATES, raisi alishuka na kuelekea ndani. Haikuchukua muda mrefu kumuapisha kutokana na maandalizi yalikuwa yamekamilika. Baada shughuli hiyo fupi, Alex alikabidiwa gwanda zake rasmi na kupewa amri akazivae muda huo huo. Raisi alimwita General na kumkabidhi ile bahasha yenye ile document, kisha yeye akaaga na kuondoka. General aliifungua bahasha ile na kusoma kilichokuwemo ndani na aliporidhika alibofya kitufe fulani hivi ikaanza kusikika honi ya dharura.

Muda huo huo kikosi chote kikasanyika katika ukumbu wa vikao, Scarlet na timu yake akaambiwa ajiandae. Alex pia alijumuishwa katika kikosi hicho chenye jumla ya wati saba hivyo na yeye akawa mtu wa nane. Baada kukamilisha maandalizi walirudi katika ukumb huo na kupewa maelekezo "kuna rubani mmoja ametunguliwa na alikuwa amebeba taarifa muhimu sana, tunaamini ametunguliwa maeneo hayo" General aliongea na kuonyesha sehemu katika ramani.
Alex alishtuka kidogo baada general kuonesha hio sehemu, ni kama kwamba anaifahamu. "samahani general, hiyo kambi ni kambi ya watu gani?" aliuliza. "mpaka sasa hatujahakikisha ni kambi ya wtu lakini nahisi ni kambi ya ncho amabazo hatupatani nazo General alijibu kisha akauliza "kwani vipi". Alex alikaa kimya kwa muda kama mtu amabe alikua anajaribu kukumbuka kitu, alishtuka tena na hapo akijipa uhakika kuwa hajakosea. "hiyo ni kambi nambari ishirini ya jangwani, ni moja kati ya kambi kubwa sana Project CODE X" Alex alijibu kwa uhakika.
 
104.
Wote waliokuwepo pale walishtuka baada ya kusikia hivo, "basi vizuri kwasababu sasa tumeshaifahamu, basi hakuna shida" General alijibu na kuendelea kutoa maelezo. Kikosi cha Scarlet kiliingia katika chumba maalum cha kuchukua silaha na hapo ndipo alipozidi kuonyesha maajabu. "hivi katika kikosi hichi kuna sniper wangapi?" aliuliza Alex, "wawili tu" alijibu Scarlet. "ok, sasa inatakiwa kuwe na wanne" Alex aliongea na kuwafanya wote wamuangalie.
" Na wote hao wanatakiwa wakae masafa yenye umbali zaidi ya mita mia mbili, na bastola ziwe zile ambazo ni nzito sana" Alex aliongea na wote wakakubaliana nae. Walimaliza maandalizi na kuondoka kambini hapo kwa chopa maalum amabyo iliandaliwa kwa kazi hiyo tu.
"kijana unaleta jeuri sio" aliongea mtu mmoja kwa hasira sana, "narudia tena kwa mara ya mwisho, jina lako nani na ni nani aliekutmuma". "huna haki ya kujibiwa na mimi, mimi najibu wakubwa zangu tu" aliongea kijana huyo ambae alikuwa amerowa damu baada ya kuchezea kichapo kikali sana. "naona wewe hujafunzawa kwenu"aliogea tena kwa hasira yule mtu na kumtandika ngumi ya tumbo. "P102 (project 102) unaitwa na mkuu" aliingia kijana mwengine na kutoa taarifa.
P102 aliondoka na kuelekea ofisini kwa mkuu wake "umepata chochote kutoka kwa yule rubani?" aliuliza mkuu wake, "hapana anaonekana amekaza kweli kweli" P102 alijibu. "sawa muache apumzike kwanza utaendelea kumhoji baadae maana huyo mtu ni muhimu sana" aliongea mkuu huyo na kumpa ishara aondoke. P102 alifunga mguu na kuondoka huku akiwa mechukiwa kwa kitendo cha kuambiwa amuache.
.

Wakati huo tayari kikosi cha PIRATES killishakanyaga ardhi ya eneo la jangwa, walikuwa umbali wa kilometer kama nne hivi kutoka katika kambi hiyo. Taratibu walianza kusogea huku macho yao yakiwa wazi sana. Ilikuwa ni vigumu kujulikana kutokaana na kiza kilichokuwepo kwa wakati hu, wao waliweza kuona vizuri kutokan na kuvaa miwani maalum za kwenye kiza. Walitembea mchaka mchaka mpaka walipoikaribia kambi hiyo. Kama walivyokubaliana, masniper wanne walikaa umbali wa mita miatatu kutoka katika kambi hiyo huku kila mmoja akitafuta sehemu nzuri ya kufanya kazi yake.
Uzuri eneo hilo lilikuwa na vyuma chakavu vingi sana, na hiyo iliwapa urahisi masniper hao kwa kupata sehemu za juu kidogo. Alex akiongozana na Scarlet na wengine wawili waliendelea na safari huku wakikubaliana na wale wengine kuwa wasishambulie mpaka watakapopewa ishara. Walitembea mpaka karibu na kambi hiyo kabisa, hapo Alex alichukua begi dogo lenye mabomu aina ya C4 na kuondoka eneo hilo.
Kwa mbinu anazozijua yeye mwenyewe alizunguka kambi nzima na kutega mabomu hayo yalipokwisha na kurudi walipo wenzake. "sasa hapa mchezo unacheza hivi, nitakwenda kufunga kifaa maalum kwenye ile sehemu ya kuzalishia umeme. Umeme ukikata tu tutakuwa na nusu saa kabla ya kurudi na huo muda tunatakiwa tuwe tumeshamaliza kazi ikwezekana na kutokomea" Alex aliongea hivo na wote watatu walioko pale pamoja na wale wanne ambao ni masniper walikubaliana nae.
"Mimi nitakuwa nawasumbua huku nje Scarlet na wenzako mutaingia ndani kwaajili ya kumuokoa rubani, na kumbukeni risasi pigeni za vichwa tu" Alex alimaliza kuongea kuondoka. Moja kwa moja mpaka kwenye mtambo wa kuzalishia umeme na kuweka kile kifaa kinachojulikana kama Electromagnetic pulse (EMP). Kifaa hichi kinatoa mionzi ya sumaku na kupelekea kukatika kwa umeme. Bila kuchelewa alibonyeza kitufe katika rimoti yake na papo hapo umeme ukakata.
Kila mtu aliweka miwani yake sawa na kuanza kazi, Alex aliingia katika kambi hiyo bil kujifich ili wale wanajeshi wamfate yeye na Scarlet na kikosi chake waingie ndani. Na kweli mbinu hiyo ilifanya kazi, Alex alianza kupambana akisaidiwa na wale masniper wanne. Scarlet na wenzake wawili waliingia ndani ya kambi hiyo na kufanya kama walivyoelekezwa na Alex. Mpambano ulizidi kuwa mkali huku kila upande ukijitahidi kujilinda.
Scarlet na kikosi chake walifanikiwa kufika katika chumba ambacho alikuwepa rubani baada ya kukagua vyumba vingi sana. walimfungu kamba na kumuinuia, kisha wakampa vidonge maalum atafune kwa ajili ya kurudisha nguvu. Baada hapo Scarlet alitoa bastola moja na kumkabidhi "tunakwenda nyumbani" Scarlet aliongea huku akiwa ameshika kifaa sikioni "ok tokeeni upande wa kusini wa kambi" Alex alijibu wakati akiendelea kupambana na wale waliokuwa nje na kusahau kama wana mateka ndani.
Walifanya kama walivyopokea maelezo kutoka kwa Alex na kufanikiwa kutok nje ya kambi lakini kwa bahati mwenzao mmoja alipigwa risasi ya mgongo kabla ya aliempiga kutunguliwa na sniper. "wape mtoto" Scarlet aliongea na hapo Alex akatafuta upenyo na kutoroka. Alipotoka tu nje ya kambi hiyo alitoa rimoti ndogo na kuongea kabala ya kukibonyeza "ungizi mwema mtoto" na kukibonyeza.Ndani ya sekunde kadhaa kulikuwa na moto tu eneo hilo, kambi nzima iliangamizwa na kuwa majivu kama ya kuni. Na hiyo ndio kazi kubwa ya bomu aina ya C4, wenyewe wanaliit kumuta kunguni kwenye kitanda.
Walimbeba yule mwenzao aliepigwa risasi na kuelekea sehemu waliokubaliana wakutane baada ya kufanya tukio. "vipi kafanyaje tena huyo?" Alex aliuliza walipofika, "kapigwa risasi ya mgongo" Scarlet alijibu. Alex akampa ishara amlaze kifudi fudi kisha akato kisu kidogo pamoja na spirit. Alikimwagia kisu kile na kisha akaanza kazi ya kuitoa risasi hiyo mgongoni, alifanya hivo akielewa kuwa ingebakia kwa muda mrefu basi ingekuwa hatari zaidi.
"vipi rubani unajisikiaje" Alex aliuliza, "ah kawaida tu nimeshazoea mambo ya aina hii" alijibu rubani huyo. Kwa vile kulikuwa na kiza hawakufanikiwa kuonana vizuri na hawakutaka kuwasha kitu chochote kile ambacho kingewakamatisha kama ingekuwa wanatafutwa. Scarlet alitoa kifaa maalum na kuanza kuongea, alitoa code zote sehemu walipo na kisha akarudisha kifaa hichi na kukaa pembeni ya wenzake. "tunakuja kuchukuliwa saa ngapi?" aliuliza yule rubani, "baada ya masaa matatu watakuwa washafika" Scarlet alijibu.
"mh masaa matatu ni mengi sana kwa kweli" Alex alijibu huku akisimama, ni kama mtu aliehisi kitu. "samahani rubani, hivi ulikuwa ukifatana ndege ngapi" aliuliza Alex, "tulikuwa watatu" alijibu kijana huyo. "kuna kitu hakipo sawa hapa" Alex machale yalimcheza na kuanza kupiga hesabu anazozijua yeye mwenye kichwani mwake. "kwani vipi Alex" ilibidi Scarlet aulize, "kwa haraka ndege yake huyu haikutunguliwa na ndege ya maadui kama ilivyosema ripoti" Alex alijibu huku akiwa anawaza kitu.
 
105.
.
"hivi Scarlet wamekuuliza jina lako la kazi wakati unawapa maelezo ya sehemu tulipo" Alex aliuliza tena wakati huu alikuwa kashabadilika. "ha..p..ana, damn wanevamia mawasiliano yetu" Scarlet alijibu baada ya kushtuka. "hii sehemu sio salama kabisa" aliongea kijana mwengine, "inabidi tuondoke hapa haraka iwezekanavyo" aliongezea mwengine. Bila kupoteza muda walimbeba yule aliepigwa risasi na kuanza safari, "jamani mimi niacheni nitawachelewesha bure, hiyo taarifa aliokuwa nayo huyo rubani ni muhimu zaidi" aliongea kijana yule aliekuwa amepigwa risasi.
"marafiki hawaachani nyuma" Alex alijibu huku wakizidi kukaza mwendo, "subirini" Alex aliongea na kuwafanya wenzake wote wasimame. "kama hapa kuna kambi basi lazima kutakuwa na kambi nyingine ndogo ya kuwekea silaha za dharura ikiwa kambi kubwa itavamiwa" Alex aliongea kwa sauti ndogo kama mtu alikuwa anajisimulia kitu mwenyewe. "Alex unawaza nini, muda hakuna ni lazima tuondoke" Scarlet aliongea kwa hasira kidogo.
"hivi hatutafika, tutakamatwa tu" aliongea Alex na kuzidi kuwachanganya wengine. "hapa tutafute sehemu ya kujificha kwanza halafu tutapanga tunaondokaje maana hatuwezi kuwasiliana na makao makuu kwa muda huu" Alex aliongea huku akiangaza angaza sehemu tofauti. "Nifateni" aliongea na kuanza kuelekea mashariki mwa jangwa hilo. Walitembea kwa nusu saa na hatiamae walifikia sehemu zenye mawe makubwa sana. "sasa hapa ndio mtakapo jificha, ingieni kwenye hilo pango na msije mkajaribu kuwasiliana na mtu yoyote yule" Alex aliongea huku akionysha kidole sehemu kwenye uchochoro flani hivi.
"wewe huingii" alihoji Scarlet, "hapana mimi nakwenda kutafuta usafiri, kawaida huwa kuna kambi kubwa na kambi ndogo ya dharura na huko lazima nitakut gari japo moja" Alex aliongea akionekana kuwa na uhakika kabisa. "Nipeni masaa mawili kama sijarudi ondokeni eneo hili" Alex aliongea na wote wakatisa vichwa kuashiria kuwa wamemuelewa. Ilibidi wafanye vile alivyowaambia kwa sababu na yeye lishawahi kupitia katika kambi kama hiyo.
Alex alichukua bunduki ndogo ana kuondoka eneo hilo, alipofika mita kadhaa kutoka kwenye yale mawe alianza kukimbia. Alikimbia kwa nusu saa mpaka alipofika katika kambi ile aliyoiripuwa na kuanza kutafuta kitu. Alizunguka eneo hilo kwa dakika kadhaa kabla kusimama na kuangalia chini, kulikuwa na shimo flani hivi lilionekana ni lakutengeneza. Bila kupoteza muda alianza kushuka ndani ya shimo hilo huku akiwa bastola yake mkononi.
Alikuwa akishuka kwa umakini wa hali ya juu sana kutokana na kuwa alikuwa hajui kama kuko salama au laa ndani ya shimo hilo. Alifika mpaka chini na kuanza kuifata njia iliokuwa mbele yake, alitembea dakika kama kumi na tano hivi mpaka alipofika mwisho wa njia hio. Aliangaza huku na kule na kuona ngazi, alianza kupanda taratibu mpaka alipofika juu na kufungua mfuniko uliokuwa umefunika shimo hilo. Alitoka na kujibanza sehemu kwa ajili ya kulichunguza vizuri eneo alilotokea.
Baada kuridhika aliondoka sehemu aliojibanza na tarattibu alianza kuelekea katika mlango mkubwa ambao ulikuwa umeandikwa control room. Aliufungua taratibu n kuoenya pasi kujulikana na mtu yoyote aliekuwemo ndani ya chumba hicho. Hata hivyo kulikuw na watu watatu tu ndani ya chumba hicho ambao walikuwa wakijaribu kuwasiliana na makao makuu yao kwa ajili ya msaada.
"nimekwambi wawili kati yenu watangulie ili kufanya uchunguzi kama kuna aliepona kambini" ilisikika sauti ya mtu kwenye spika maalum. "mkuu ni vigumu sana kuenda huko kwa sababu hatujui wako wanagapi" alijibu mtu mmoja. "ni kikosi cha watu nane tu, hizo ni taarifa za uhakika nilizozipata kutoka kwa mpelelezi wangu aliekuwemo katika kambi ya THE PIRATES" alijibu. Alex alisikiliza kwa makini na simu ilipokatwa tu aliwavamia na kuwaua wote.
"zimebaki dakika kumi na tano tu, kama hajarudi tunaondoka" aliongea Scarlet, "hapana kama yatatimia masaa mawili hajarudi inabidi tuumpe nusu saa nyingine baada ya hapo kama hajarudi ndio tuondoke" alishauri yule rubani. Wakati wakiendelea kubishana ghafla waliona mwanga wa taa ukija upande wao. Kila mmoja alitoa bunduki yake na kujiweka sawa kwaajili ya chochote.
Gari ile ilisimama mbele ya mawe hayo na mtu akashuka kuelekea ndani, "taratibuni mimi ni Alex" Alex aliongea huku akiingia ndani katika mawe hayo. "tufanyeni haraka, tuondoke eneo hili maana kuna hatari kubwa inakuja mbele yetu" Alex aliongea na kugeuza. Alitoka nje na wengine wakafuata nyuma, waliingia kwenye gari na safari ikaanza. "tubaelekea wapi" Scarlet aliuliza, "kilometer kama hamsini hivi kutoka hapa kuna kambi nyingine na katika kambi hiyo kuna uwanja wa ndege na ndipo tunapoelekea" Alex alijibu huku akiongeza mwendo wa gari hiyo.
"sasa tukishafika tunaingiaje katika kambi hiyo bila kujulikana" aliuliza mwenzao mmoja, "musijali kila kiti nishapanga ninacho waomba kuwa mufate vile ntakavowaambia" Alex alijibu swali hilo huku akipunguza mwendo wa gari na kupunguza mwanga wa taa kwa sababu tayari walikuwa washakaribia kambini. Tartibu alisogea mpaka katika geti la kambi hiyo, Mlinzi alinyoosha mkono kusimamisha gari hiyo.
.

"Yametukuka mapinduzi" Alex aliongea huku akipiga ngumi kifuani mara tatu kisha akanyoosha mkono juu. Yule mwanajeshi nae akafanya vile vile "hawa ni wale wanajeshi tuliopewa taarifa tuwakamate" Alex aliongea na kumpiga Scarlet kibao. Jambo lilimuudhi Scarlet na kujikuta akifoka, "umeona wana hatari sana, huyo nyau nimemgusa kakasirika" aliendelea kuongea Alex. "vipi usafiri ulioandaliwa kuwabeba upo tayari?" aliuliza swali, "ndio nyoosha mpaka katika barabara nambari ishirini kuna ndege hapo inawasubiri" alijibu yule mlinzi bila kujua kuwa nachezwa akili.
Alex alimshukuru na kuondoka, muda wote Scarlet alikuwa amevimba kwa hasira lakini Alex hakumuuliza kitu wa kumsemesha. Walifika mpaka walipoelekezwa na kukuta ndege ikiwa inawasubiri. Alisimama nyuma ya ndege hiyo na kushukua kisha akawafokea washuke, nao walitii na kushuka. Alex aliwaongoza mpaka mlangoni na kutoa taarifa kwa wale wanajeshi waliokuwa wakisubiri. Wakawashika na kuwapandisha kwa nguvu huku wakiwapiga vibao na ngumi, Alex nae alifuata nyuma huku akitamani kucheka.
Walipoingia kwenye ndege yule mlinzi aligeuka na kukutana na ngumi nzito ya shingo ilimpeleka hadi chini na kukata mawasiliano. Alex aligeuka na kufunga mlango, baada ya hapo alielekea chumba cha marubani huku akiwa amembeba yule mwanajeshi aliempiga. Alibonyeza kitufe maalum na kumuelekeza yule mwanajeshi kwenye camera maalum. Mlango wa marubani ulifunguliwa na hapo aliingia ndani ndani ya chumba hicho kwa kasi ya juu sana na kuwachapa marubani wote wawili.
Alipohakikisha wote wapo chini, aliwaburuza mpaka nje ya chumba na kurudi walipo wenzake. Alimpa rubani ishara amfate nae aliinuka moja moja kwa moja mpaka katika kile chumba cha marubani. Alex alikaa upande mmoja na yule rubani akakaa upande mwengine, "ndugu zangu, makamanda wenzangu katika kuimarisha ulinzi tunawaomba mukae kwenye viti na mufunge mikana. Muda wowote kuanzia sasa tutaanza safari" Alex alionge kupitia kipaza sauti na wote walifanya hivo.
"ok, rubani hii ndio nafasi pekee ya kuokoka" Alex aliongea huku akibonyeza vitufe vidogo vidogo. Yule rubani nae hakuwa nyuma, alibonyeza vitufe vingine na mashine za ndege hiyo ziliamka na kuanza kufanya kazi yake. Taratibu ndege ilinza kutembea mpaka ilipofika kwenye njia inayotumika kwa ndege kupaa na kutua. Baada kukamilisha taratibu zote za awali walipata ruhusa kutoka kitengo kinachoongoza ndege (contrilling tower). Rubani alianza taratibu nyingine na taratibu ndge ilianza kushika kasi na hatimae iliacha ardhi.
 
106.
Wote kwa pamoja walifurahi kwa nguvu, ndege ilizidi kutokomea angani mpaka pale ilipofika umbali unaotakiwa na kukaa sawa. Baada kuhakikisha hakuna shida yoyote Alex alitoka katika chumba cha rubani na kuelekea walipo wengine. Kitu cha kwanza alichokutana nacho ni ngumi ya tumbo kutok kwa Scarlet "hiyo ni malipo ya kunipiga kibao" Scarlet aliongea huku akitabasamu. "sawa hakuna shida" Alex alijibu na kucheka kidogo.
Safari iliendelea huku wote wakiwa wamepitiwa na usingizi kutokana na uchovu kasoro Scarlet peke yake. Alivoona hakuna wa kuongea nae aliamua kwenda chumba cha rubani labda huenda akapata mawili matatu. "Vipi naona kimya huko" aliongea yule rubani, "ah wote wamelala" Scarlet alijibu huku akikaa kwenye kiti. "mbona umeshika huo mkufu mkononi" Scarlet aliuliza, "ah huu mkufu ndio unaonifanya niendelee kuishi hata kama nitakutana na balaa la aina gani" aliongea rubani.
"inavyoonekana una maana sana kwako", "ndio tena sana" alijibu yule rubani. Lakini Scarlet alipouangalia vizuri aligundua kuwa ulikuwa na kopa. "Adrian" Scarlet alijesemea kwa sauti ya chini huku akijikunyata, "umeita jina gani?" aliuliza rubani. "a..h hamna sijaita jina lolote" Scarlet alibabaika kifogo kabl kujibu swali hilo, "unajua nimesikia kama umetaja Adrian" aliongea yule rubani na wakati aligeuka ili amuone vizuri Scarlet. Alikuta akitoa macho huku kama akifikiria kitu, "haiwezekani nimemfananisha tu" aliongea yule rubani huku akigeuza uso wake mbele.
Alikaa kwa muda huku akionekana kuwaza mambo mengi sana,"litakalokuwa na liwe tu" alijisemea yule rubani kisha akabonyeza kitufe kilichoandikwa autopilot. Kitufe hicho huifanya ndege ijiongoze yenyewe, kisha alimgeukia Scarlet ambae muda wote alikuwa kimya na mwenye kujikunyata. "Ariella" aliita kwa sauti ya chini, Scarlet alishtuka baada kusikia jina hilo. "hivi ni kweli au naona miujiza tu" alizidi kuongea yule rubani na kupeleka mkono kwaajili ya kuziondoa nywele usoni mwa Scarlet.
"Ariella ni wewe kweli" aliongea huku akisimama na kutok kwenye kiti alichokuw amekaa, alifungua mkufu mkononi na kumkabidhi Scarlet. Yeye alisimama bila kumwambia kitu, Scarlet alifungua lile kopa na kukuta picha mbili, moja yake moja ya Adrian kipindi walichokuwa wadogo. Aliinuka kwa nguvu na kumrukia Adrian ambae alikuwa akitokwa na machozi ya furaha. walikumbatiana kwa nguvu huku wote wawili wakitokwa na machozi, "nilidhani sitokuona tena" aliongea Scarlet. "shhshh usiongee kitu tafadhali" Adrian alimnyamazisha.
**************************.
"mnasemaje nini wewe" alifoka general David baada ya kupoekea taarifa mbaya, "ndio mkuu, yule rubani mwenye taarifa ametoroshwa" alijibu aliekwenda kuripoti. "hilo sasa tatizo kwa kweli" aliongea General David na kuka kwenye kiti kama mtu aliotoka safari ndefu yenye kuchosha. Wakati wakiendelea kuongea, ghafla aliingia mwanajeshi mwengine huku akiwa na bahasha mkononi na kumkabidhi general. Alifungua na kuangalia kilicho ndani, alishtuka kidogo na kujikuta akiishiwa nguvu kabisa.
"sasa kazi yetu itazidi kuwa ngumu" aliongea na kutoa kitambaa cha kujifuta jasho, "kivipi mkuu" aliuliza kamanda Willy ambae ndie alieleta ile bahasha. "mtu ambae nilidhani ameshakufa yuko hai kumbe" alijibu, "ni nani kwani huyo". "Alex, Alex, Alex" aliongea General David huku akikuna kichwa, "na kama Alex hajafa maana yake Agent Darling atakuwa kashaujua ukweli, hili ni tatizo kubwa sana" alijoiongelesha mwenyewe General David. "Kamanda Willy sambaza ujumbe kwa wakuu wote wa kambi zote, waambie tukutane ndani ya masaa ishirini na nne" alitoa amri hiyo general David kisha aliinuka na kuondoka.
 
107.



Kamanda Willy aliondoka na kuelekea katika chumba cha mawasiliano, alifanya kama alivyoambiwa na General David. Masaa matano baadae watu walianza kufurika katika kambi hiyo, wengine walionekana kukerwa na wito huo kutokana na sura kujiknja sana. "ndugu zangu nashukuru kwa kuitika wito huu wa ghafla tu" General David alianza kuongea, "wacha nielekee moja kwa moja katika jambo ambalo nataka kusema. Mpaka jana mambo yalikuwa yanakwenda kama tulivyopnga lakini taarifa nilizozipokea leo ndizo zilizonifanya niwaite ili tujadili na kuona tutafanya nini. Natumai wote mtakuwa mnajua kuwa Alex alifariki" aliongea mpaka hapo na kuangalia umati utaitikaje..
"nilitegemea sura zenu ziwe hivyo, sasa naomba muelewe kuwa Alex yuko hai na ndie alietuvurugia mipango yetu. Ila kwa sasa hatuwezi kukabiliana nae kirahisi kwa sababu kuna kikosi kikubwa na hatari sana THE PIRATES kinashirikiana nae. Nimewaita hapa kutak maoni yenu tunafanya kitu ili kuondoa kizuizi hichi" alimaliza kuongea General na kuwaangalia wenzake.
"mimi naona bora tutume vijana wetu wakawaangamize huko huko kambini kwao" alisimama mzee mmoja na kuonge, "kuwashambulia kambini kwao itakuwa vigumu, mimi naona tucheze kamchezo fulani kitakachomtoa kambini halafu tunamalizana nae kiume zaidi" alisimama mtu mwengine na kutoa wazo lake. Hilo lilionekana kuungwa mkono na wengi, "hilo wazo ni zuri sana ila na mimi nina wazo langu" aliongea General David. "mimi nahisi ule mpango wa kufanya mapinduzi uanze tu" aliendelea kuongea na kutoa wazo lake.
"lakini bado maandalizi hayajakamilika mkuu, tutaanza vipi" aliongea mtu mmoja, "hakuna haja ya kuchelewesha kwa sababu maandalizi yote yamekamilika na hizo taarifa alizokuwa nazo yule rubani si muhimu sana. Mi nawaambia tukichelewa basi Alex atatukaa kooni, huyu kijana mimi namjua vizuri sana. Ni hatari kuliko yoyote yule ambae amepitia Project CODE X" alijibu General na kuwafafanulia vizuri. Ukimya ulipita kidogo huku kila mmoja akionyesha kuyatafakri maneno alioyasema general, "mi nahisi wazo la genera lina mashiko, kwanini tusubirie wakati maandalizi yote yalishakamilika" alisimama mwanaume mmoja lafudhi kirusi na kuongea.
Kuliibuka mzozo mkubwa na watu wakawanyika pande mbili, kuna wale waliokubaliana na general na wale waliopingana nae. Mzozo huo ulidumu kwa muda mrefu na mwisho wote walikubaliana na general katika wazo lake. Kikao hicho cha dharura kilimaliza huku viongozi wote wakikubaliana kukutana baada siku tatu kwa ajili ya mcahakato mzima wa kuanza mapinduzi, kila mtu alitwanyika na kurudi alipotoka.
**************************
"mkuu tumepata taarifa nzuri na mbaya kwa wakati mmoja" aliingia kijana mmoja ndani ya ofisi ya Jeff, "haya anza na mbaya halafu utafata nzuri" Jeff alimjibu huku akimuagalia Aget Darling ambae alikuwa akifanya mambo yake. "taarifa nzuri ni kwamba siku tatu kutoka leo kile kikundi cha wana mapinduzi kitaanza kufanya ushenzi wake, na taarifa nzuru ni kwamba ule muda wa kunyoosha viongo umefika" alimaliza kijana huyo aliejulikana kwa jila La Talbot.
"mwisho kabisa, General David unatoka kuja kujibu mashtaka yako" Agent Darling aliongea huku akianza kuvimba kwa hasira. "Ok, sasa anzeni maandalizi ili wao wakianza sisi tunamaliza" Jeff alijibu na Talbot akatoka. "mpenzi kwa hasira hizo General David atakuuwa" Jeff aliinuka huku akiongea na kumsogelea Agent Darling au Christine jina lake halisi na kumkumbatia kwa nyuma. Wakati huo tayari machozi yalisharowanisha mashavu yake.
Alex akiwa usingizini alishtuka ghafla na kuinuka, moja kwa moja hadi cumba cha rubani. Alipofungua mlango alipigwa na bumbuwazi baada ya kukuta wawili hao wakiwa wamekumbatiana. "samahanini kwa kuingilia kati starehe zenu" aliongea, "hapana tena bora ulivyokuja maana huyu bibie hataki kuniacha" alijibu Adrian na kujaribu kumtoa Scarlet KIfuani. "Ariella tafadhali punguza basi, najua ni muda mrefu lakini wacha tumalize ili kwanza halafu nitakuacha unikumbatie mpaka uridhike" Adrian aliongea kwa sauti ya chini lakini Alex alifanikiwa kusikia jina la Ariella. "Adrian" aliita Alex, "ndio mimi" Adrian alijibu.
.

"Ni hivi kwa sasa hatuwezi kuelekea kambini, si kwetu wala si kwako. Hii ni kwasababu katika kambi zote mbili kuna kunguni wamepandikizwa na waasi" aliongea Alex, "unasemaje?" Scarlet aliropokwa kwa nguvu. "natumai umenisikia bila shaka, kuna vikunguni vimepandikizwa na ile kambi kwa sasa sio siri tena kwasababu waasi wanajua ilipo na kila kinachofanyika humo" alijibu Alex na kufafanua. "Adrian sasa hivi tuko wapi" aliuliza Alex, Adrian alisoma rada "tunakaribia New York".
"hii ndege inabidi tuiangushe majini ili tusijulikane tulipo, Scarlet kawaambie wavae makamanda wavae parashute kabisa" Alex aliongea na Scarlet alitoka katika chumba hicho na kuelekea walipo wengine na kuwapa taarifa. Bila kuchelewa walianza kujiandaa, "Adrian igeuze ndege na uielekeze chini" Alex aliongea na kutoka chumbani humo. Adrian aliigeuza na ufanya kama alivyoelekezwa. Kisha alitoka humo nakwenda kuungana na wengine.
Walipohakikisha kila mtu amejiandaa, walifungua mlango wa nyuma wa ndege hiyo na wote wakaruka na kuiacha ndege ikielekea baharini na kulipuka. Alex akiwa kama kiongozi kwa sasa, aliongoza msafara huo unaoelea angani kuelekea mjini New York. Baada kama dakika ishirni hivi walifungua maparachute na kushuka nje ya mji kidogo. Walipohakikisha wote wakosalama, Alex aliwapa ishara wamfuate. Walitembea kwa nusu saa mpaka walipofika katika nyumba moja ambayo ilikuwa imejitenga sana na nyingine.
Alex alisogea mlangoni na kubonyeza sehemu, kilitoka kitu kama keyboard ndogo. alibonyeza bonyeza na mlango ukafunguka, "karibuni nyumbani" Alex aliongea na kuingia ndani huku nyuma akiafatiwa na makamanda wengine. "Alex hii nyumba ni ya nani?" aliuliza Scarlet, "ni ya mwalimu wangu Allen James" Alex alijibu na kukaa kwenye kochi. Kila mtu alionekana kuchoka kivyake vyake, baada muda kidogo kupita Alex aliinuka na kuelekea katika chumba chake. Alikaa kwa muda kabla ya kusikikia vitu vikivunjika. Wote walikimbilia chamba ambcho alikwenda Alex, walimkuta akimeshika picha mschana huku akilia kwa majonzi ya hali ya juu. "najua bado amani hujaipata lakini nakuahidi kuwa muda si mrefu utaipata" Alex aliongea huku akifuta machozi.
 
108.
Scarlet alipoona vile aliwaambia wenzake watoke na wamuache peke yake, afanye analotaka. Dakika ya saa kupita Alex alirudi ukumbini akiwa anatabasamu sana, "Scarlet wasialiana na general mwambie aondoke kambini hapafai tena" aliongea Alex na kumkabidhi simu maalum lakini kila Scarlet alipojaribu namba ya General haikupatikan kabisa. Alijaribu zaidi ya mara kumi lakini hali ilikuwa ndio ile ile. Alijikuta akiingiwa na baridi ghafla, wenzake walijaribu kumtuliza na kumwambia kuwa atakua salama. "labda amezima simu kwa sababu za kiusalama zaidi" aliongea Adrian.
"jamani leo pumzikeni maana kuanzia kesho kutakuwa na kazi kubwa sana ya kufanya" Alex aliongea na kuwaomba wamfuate, aliwaonyesha vyumba vya kulala na mwisho alibaki yeye, Scarlet na Adrian. "nyinyi chumba chenu kile pale, maana hueda baada ya leo msipate tena usiku wa kuwa pamoja" Alex aliongea na kuwafanya wote wacheke. Waliagana na kuelekea vyumbani mwao, huko chumbani kwa Scarlet na Adrian kulikuwa ni peponi kwa usiku huo.
Baada ya kuingia chumbani kwake Alex alitoa computer ndogo inayojulikana kama master computer. Aliichezea na kuingiza code anazojua yeye mwenyewe na akili yake kisha akatuma ujumbe "Allen Jr za siku nyingi" ndivyo ulivyosomeka ujumbe huo. "Christine kuna ujumbe wako huku" Martina alimuita Christine, macho yalimtoka baada kugundua kama ujumbe huo umetoka kwa Alex. Na hilo halikumpa tabu kutokana na kuwa ni Alex pekee ndie anaemuita Allen Jr. "unataka nini?" alijibu, "wakati huu ni wakati wa kueka tafauti zetu pembeni" Alex alijibu. "unamaanisha nini?" Christine alihoji.
"wewe unataka kulipa kisasi cha babaako na mimi nataka kulipa cha mwalimu wangu, sasa kwanini mimi na wew tuwe maadui?" alex alijibu na kuuliza swali. "sihitaji msaada wako" Christine alijibu kuonesha jeuri, "bado hujakua kumbe, au unaringa kwasababu uko na Jeff" alijibu pigo na kuwafanya wote washtuke. "musishituke sana na wala musihangaike kutafuta ni wapi ninapo waonea" Alex alijibu. "sasa ni hivi mimi najua ulipo nakupa nafasi ya mwisho, aidha tueke tafauti pembeni au tuendelee kuwa maadui" Alex alituma tena ujumbe.
"na kama nikikata kushirikiana na wewe" Christine alijibu, hapo hapo computer zao zilizima na zilipo waka tu ilionekana picha ya Alex akicheka. "naona kukuandikia kwa ujumbe hutaki kunielewa na natumai sasa tutaelewana vzuri" aliongea kisha akaendelea "ukikataa, hao wote waliouwa pembeni yako watakufa mmoja baada ya mwengine". "Christine hebu kaa pembeni kwanza" aliongea Jeff, "Alex tuongee kiume maana huyu mtoto wa kike anaonekana hajakua bado" Jeff aliongea jambo lilimkera sana Christine. .
"Mambo si hayo sasa, Allen Jr kaa pembeni kaka zako tuongee" aliongea Alex na kucheka kidogo. "Sasa ni hivi hawa jamaa wanakambi nyingi sana na ili kuwapunguza makali tuanze kuteketeza kambi moja moja mpaka zibakie chache ambazo tutaweza kuzimudu" Aliongea Alex. "kwa makadirio zinafika kambi ngapi" Jeff aliuliza, "mia moja na hamisini na kidogo hivi lakini hazifiki mia mbili" Alex alijibu. "hizo nyingi kweli" Jeff alijibu na kuendelea "sasa una mpango gani?" aliuliza, "hizo kambi zimegawanyika sehemu tatu, kuna za baharini, za msituni na za jangwani. Nyingi ziko jangwani na baharini na hizo ndio rahisi kuziangamiza" alifafanua Alex na kuendelea "kwa vile sisi tuko makundi mawili, inabidi tugawane kundi moja lichukue kamba za baharini na kundi la pili lichukue za jangwani. Tukizimaliza hizo tushirikiane kuzimalizia za msituni maana hizo ndio kambi kubwa kuliko zote".
"sawa hakuna shida mimi na timu yangu tutachukua za jangwani, kesho usiku tutahakikisha zimekweisha zote" Jeff aliongea na kutabasamu. "ok sis huku tutachukua za baharini, tukutane tena kesho usiku kwa ajili ya mipango mengine" Alex alimaliza kuongea na kukata mawasiliano. Sekunde chache tu baada ya kukata mawasiliano hayo, uliingia ujumbe kambini kwa Jeff. Ilikuwa ni ramani ya kambi za janngwani, "kwa nini unataka kushirikiana nae?" Christine alifoka. "tatizo lako wewe hutaki kuwa muelewa, unadhani pekeetu tungewezaje kupata taarifa zote hizi. Kuna baadhi ya wakati inabidi ukubali tu kama umeshindwa, na kuanzia sasa jina langu ni Ghost na sio Jeff" Jeff aliongea huku akikunja sura. Christine alitaka kumjibu lakini Talbot alimuwahi na kumziba mdomo kisha akamwambia "kumjibu ni wazo baya sana na utalijutia, ni bora unyamze tu maana ushamvuruga. Akibadilisha jina na kujiita Ghost ujue tayari yupo katika maandalizi ya kuuwa au kutoa dozi isio na kipimo maalum"
Christine alipoambiwa hivo alinyamaza kimya, Jeff alielekea chumbani kwake na kujichimbia. Alianza kupanga na kupangua mipango yake, mpaka muda huo alishaelewa kusudio la Alex. "kwanini yule mwanamke anakuwa kichwa ngumu" alijiuliza swali hilo, wakati akiendelea kuwaza mlango ulifunguliwa na alieingia alikuwa ni Christine. "Jeff nimekukwaza?"aliuliza, "hivi kwanini unaweka sana vinyongo, we hujaona maana ya Alex kukutafuta" aliongea Jeff au Ghost kama anavyojulikana na wakiuka sheria wengi.
"kinachoniuma ni babaangu kufa kwaajili ya mtu mwengine" Christine alitoa donge hilo moyoni, "wewe kwani leo unavyopambana na majambazi sugu, unapigania maisha ya familia yako au?" alifoka Jeff. "hapana napigania maisha ya watu wa nchi yangu" alijibu huku akiona aibu, "sasa babaako kufa kwa ajili ya mtu mwengine huoni kama alikuwa akitimiza wajibu wake" Jeff aliongea. "basi yaishe nimejifunza" ilibidi Christine akubali sasa, "sio kujifunza unatakiwa kuwa mwanajeshia aliekomaa, yaani pamoja na kuwa na cheo kikubwa kama cha THE ONE AND THE ONLY. Unashindwa na mtu mwenye cheo cha ukomando tu kweli mpenzi wangu" Jeff alionekana kukereka sana na tabisa alioinesha Christine mbele ya Alex na mbele ya kikosi chake chote.
 
109.
Ilibidi Christine atumie nguvu ya ziada kuomba msamaha, kwasababu alielewa ni kiasi gani amekidhalilisha cheo chake. Baada kuomba msamaha muda mrefu, Jeff alisamehe na kumona ikiwa atarudia tena basi atamvua cheo. Hilo lilikuwa onyo kali sana ambalo Christine tokea anze kulitumikia jeshi hakuwahi kupewa. Jeff alirudi ukumbini na kukiita kikosi chake chote "kesho kutakuwa na kazi ngumu sana ya kufanya, na kazi hiyo ndio itatupa muelekeo wa nchi zetu. Tukae tukijua kuwa tukiharibu basi tumeziumiza nchi zetu. Kufa vitani ni ushujaa kuliko kurudi nyumbani na mkia katikati ya mapaja eti tumeshindwa. Tunasimama pamoja hadi mwisho, hadi tujue mbivu na mbichi" Jeff alimaliza kuongea na kuweka mkono kati, ilifata mikono mingine juu na kwa pamoja wakasema "pamoja hadi mwisho".
Upande wa Alex huko nako mambo yalikuwa yameiva sana, "sisi tuko tisa na ndege zipo tano, sasa ni hivi kila ndege itakuwa na watu wawili kasoro moja. Hiyo moja ntakuwa pekeangu, kumbukeni kuwa kuifanikisha kazi hii ni muhimu sana hata kama itatugharimu maisha yetu" aliongea Alex na alionekana kuwa makini sana na anacho kiongea. "nifateni" aliwaambia na kuanza kuongoza njia, aliingia katika chumba chake na kufungua kabati ambako kulikuwa na mlango wa siri. Waliingia wote, mlango ulifungwa na lift ikaanza kushka chini. Kumbe ilie ni lifti, iliposimama na mlango kufuguka wote walipgwa na bumbuwazi baada kkutana na ndege za kipekee za kivita.
"sijawahi kuona ndege kama hizi zaidi ya kwenye filamu" aliogea Adrian, "basi leo utarusha kabisa" Alex alijibu na kutabasamu. walichagua wawili wawili na kila kikundi kikaelekea kwenye ndege moja, "kabla ya kuondoka, kila mtu aombe mungu wake kutokana na imani yake. Maana huenda tusionane tena baada ya leo" alimaliza kuongea Alex na kila mtu akasali anavojua yeye. Waliingia kwenye ndege zao, mlango mkubwa ulifunguka na kuonesha njia ndege kwa uzuri zaidi. Zilianza kutoka moja moja, Alex ndie aliekuwa wa mwisho. Zilifuatana kwa dakika tano kisha kila ndege ikashika njia yake, haikuwa shida kwa sababu ramani walikua nazo wote.Wakati huo huo upande wa kina Christine walitoka na ndege zao, na kuelekea katika kambi zilizokuwa jangwani.
***********************
.

"Mkuu kambi zetu zaidi ya hamsini zimesharipuliwa" aliingia kamanda Willy na kutoa taarifa ofisini kwa general David. "unasemaje wewe, mbona sikuelewi" aliuliza huku akisimama, "kambi zetu zaid ya hamsini zimesharipuliwa na hakuna hata mwanajeshi mmoja aliepona" alifafanua kamanda Willy. "zimeshambuliwa kwa kitu gani" aliuliza General, "ndege za kivita lakini hazijulikani ni za kikosi gani" alijibu kamanda Willy. "Alex" general David aliita kwa nguvu, "tuma ndege miamoja zikakabiliane nao kabla hawajatumalizia kambi zetu" General David alitoa amri hiyo iliotekelezwa punde tu baada kamanda Willy kuondoka.
Ndege mia moja za kikosi cha waasi ziliingia angani, wakati huo Alex na kikosi chake walikuwa wanakaibia kuzimaliza kambi za waasi zilizokuwepo baharini. "makamanda hakikisheni tunazimaliza kambi zote, zimebakia kumi tu. Halafu kwa kasi ya ajabu elekeeni upande wa kambi ya The pirates, msishuke piteni maana muda si mrefu tutapata marafiki kutoka kwa waasi" aliongea Alex kupitia kifaa maalum kilichowaunganisha kikosi chote. "umesomeka mkuu" walijibu kwa pamoja na kila mmoja akaendelea na kazi ya kuziteketeza kambi zilizosalia. Baada kuhakikisha zimekwisha walianza kugeuza na kuelekea upabde wa kambi ya the pirates.
"general Griffin unanisoma" Alex aliongea, "unasomeka over" General alijibu. "nakuletea tunakuletea sherehe upande wako" Aleo aliongea, "muziki uko tayari over". "rodger" Alex aliongea na kuanza kuongeza mwendo wa ndege yake. Wakati huo tayari ndege kadhaa za waasi ailikuwa nyuma yao zinawafukuza huku zikijaribu kuwashambulia. Lakini kutokana na teknolojia ya ndege wanazo endesha, mabomu ya ndege hizo yalijkuta yakipoteza muelekeo na kugongana yenyewe.
Kwa mbali Alex aliona ndege wenzake zikielekea kule aliposema, "hapo kwenye sehemu yenye vitufe, kuna kitufe kimoja kimeandikwa HS. Hiyo inamaanisha hypersonic speed, bonyezeni hicho kitufe na mufurahie mwendo kasi usio wa kawaida" aliongea kupitia kifaa maalum. "umesomeke" walijibu kwa pamoja na kila akabonyeza. Ndege hizo ziliongezeka kasi na kuanza kutoweka hasa katika upeo wa ndege za waasi. Masiki waasi bila kujua kama walikuwa wanaingizwa megoni, waliendelea kuwafukuza. Ndge za kina Alex zilipita juu ya kambi ya the pirates, na zilipoanza tu kupita za waasi, zilianza kutunguliwa na bunduki maalum zinazoitwa Anti-aircraft.
Ndege zote za waasi zilizokuwa zinawafukuza zilitunguliwa na bastola hizo, baada ya hapo Alex alitoa amri wageuze na kutua katika kambi yao hiyo ya the pirates. Dakika chache baada ndege zilitua lakini zilikuwa nne tu moja haikuwepo, walishuka wote ila kabla hawajafanya lolote Alex aliwaita "tufungeni macho ili tuwaombee wenzetu wawili waliopoteza maisha vitani". Walishtuka kidogo lakini walifunga macho na Adrian akaongoza sala. "karibuni nyumbani mashujaa" General Griffin alongea huku akija upande wao akiwa anaongozana na raisi.
Adrian alipomuona tu raisi alimsogelea na kutoa heshima kisha akatoa kisu kidogo na kujichana sehemu ya nyuma katika paja la kulia. Wote walimshangaa, alitoa kitu kilizunusha katika mfuko maalum. Aliufungua na kutoa chip ndogo, "muheshimiwa nawasilisha taarifa ulizoziagiza" aliongea Adrian na kumkabidhi raisi ile chip. "asante na pole kwa yaliokukuta" raisi aliongea na kutoa amri madaktari wamshughulikie Adrian. Waliingia ndani na kila akaelekea chumbani kwake kwa ajili kuoga na kupumzika.
Baada ya nusu saa wote waliitwa katika ukumbi maalum wa vikao, "Alex umekuja na ule mzigo" aliuliza general. "ndio mkuu" Alex alijibu, "mleteni huyo kunguni huku" General aliongea na hapo wakaingia wanajeshi wawili wakiwa na mtu mmoja aliefungwa pingu. "makamanda huyu ndie kunguni aliepandikizwa na waasi. "umemjuaje?" Scarlet aliuliza akionekana wazi kutokubaliana na aliloliongea Alex. "siku ile niliokuwa nikonyesha uwezo wangu, si nilisema achaguliwe sniper bora" Scarlet alikisa kichwa kuashiria anakumbuka. "huyu alijikosesha makusudi, kwa sababu aliogopa nitamgindua. Kwa hiyo baada ya kupiga kifuniko akapiga chini kidogo katika shingo ya ile chupa, sio hilo tu. mgongoni ana mchoro unaotukuza mapinduzi" Allex aliongea hivo na kuinuka.
Alisogea mpaka alipo yule muasi na kuwaambia wale waliomshika wamlaze chini, "someni hayo maneno kinyumenyume" aliwaamba wengine. Hapo kila mmoja alishangaa kuona maneno hayo yakisomeka "yametukuka mapinduzi", lakini katika hali ya kawaida huwezi yagundua kabisa. Baada hapo Alex alimsimamisha na kusogea nae kwenye meza, alimfungua pingu na kuwambia aeke mikoni kwenye meza. Aliifunga mikono hiyo na vyuma maalum vilivyokuwa katika meza hiyo na kuacha vodole vikiwa vimenyooka. "sasa ni hivi kijana, naomba unambie kambi yenu kubwa iko wapi na nakutahadharisha kama hutotoa ushurikiano basi nitahakikisha naukamua ukweli hata kama itabidi nikukaushe damu" Alex aliongea akionekana hatani hata kidogo.
 
Back
Top Bottom