Simulizi ya Kijasusi: C.O.D.EX.

Simulizi ya Kijasusi: C.O.D.EX.

110.
Upande wa Agent Darling na Jeff mambo pia yalikuwa mazuri, walimaliza kambi zote jangwani pamoja na ndege zilizotumwa kwenda kupambana nao. Walipohakikisha hawafauatiliwi tena, walirudi kambini kwao, "hongereni sana" Jeff aliongea kuwapongeza majenedari wake. "huu ndio kwanza mwanzo kwa hiyo tusudhani tumeshinda" aliendelea kuongea na alipomaliza kila mtu alitawanyika na kuelekea sehemu yake ya kupumzika.
"inavyoonekana hutaki kutoa ushirikiano kwa njia ya amani" Alex aliongea baada yule kijana kuleta ubishi. "basi hakuna shida" alitoa sindao ndogo yenye dawa kiasi na kumchoma, "hii ni sindano ya ganzi" aliongea baada kumchoma na kusubiri dakika kadhaa. Wakati huo mpaka raisi alikuwa akishuhudia mateso anayotoa Alex. Alifungua pochi maalum na kutoa sindano ndefu jma sentimita tani na kuanza kumchom chini ya kucha kwenye vidole vya mkono. Aliingiza urefu wote hadi mwisho mpaka alipohakikisha amevichoma vidle vyote kumi.

"saa hivi huhisi kitu lakini niamimi hiyo ganzi ikiisha utajuta kwanini hukutoa ushrikiano mapema" Alex aliongea na kukaa tena kwenye kiti akisuiri ganzi iishe. Baada kama dakika sita jamaa alianza kukunja uso, na kwa mbali macho yake yalianza kurowa maji. "muda umefika, sasa nambie kambi yenu kuu iko wapi?" Alex aliongea, lakin bado jamaa alikuwa mbishi. Alex alianza kuchomoa sindano ya kidole kimoja na kuirudisha kama vile anachokonoa kitu.
Jamaa alipiga sana kelele, "yaani nimekwambia hata ikibidi nikukaushe damu niupate ukweli basi nitafabya hivo kwa maana huu ni mwanzo tu" Alex aliongea kwa hasira huku akiedelea kufanya kazi yake. "nitasema tafadhali usifanye tena hivo" maumivu yalipozidi jamaa aliamua kutoa ushirikiano, "mambo si hayo sasa, ungekubali mapema tusingefika hapa" Alex aliongea na kukaa kwenye kiti. Basi jamaa hakuwa na jinsi aliongea kila kitu bila kuficha hata kidogo, "tafadhali naomba unichome tena ganzi ili nipunguze maumivu" aliomba baada kumaliza kuongea.
"usijali yatakwisha sasa hivi" alijibiwa lakini si na Alex bali ilikuwa nisauti ya raisi, alisogea mpaka alipo Alex na kuchomoa bastola ndogo. Alimuekea kichwani na kumpasua kichwa, "tunajitahidi kuleta amani nyinyi mnaleta upumbavu, eti mapinduzi" aliongea raisi baada kumchapa risasi. Wote walipigwa na bumbuwazi na wasiamini kitendo alichokifanya raisi, "muheshimiwa bado kitu kimoja" Alex aliongea na kuunganisha computer yake na rubinga kubwa iliokuwepo hapo ukumbini.
"Jeff mambo yameendaje" Alex aliongea baada kioo cha runinga kuonesha picha ya Jeff akiwa na majemedari wake. "umekwenda vizuri sana na hakuna hata kambi moja iliosalia jangwani" alijibu, "safi sana, sasa tunaelekea hatua ya mwisho. Zimebaki kambi kadhaa pamoja na kambi yao kubwa" Alex alimueleza Jeff kila kitu na wakakubaliana wakutane sehemu karibu na kambi hizo ambazo ziko porini. Baada ya maongezi ya dakika kadhaa alimpisha raisi nae aongea kijana Jeff ambae cheo chake ni zaidi ya kamanda..
**************************************************
Katika ndege mia zilizotoka ilirudi moja tu, ilipotua tu alishuka rubani wa ndege hiyo na kukimbilia ofisini kwa general David. "mkuu tupo matatani" aliongea baada kuingia katika ofiso hiyo, "kivipi" aliuliza kamanda Willy ambae alikuwa akiongea na general wakati rubani huyo ameigia ofisini. "ndege zote zimeripuliwa, mimi nimeokoka ki bahati bahati tu. Pia sijawahi kuona ndege zenye uwezo kama tulizokutana nazo huko, na mbaya zaidi kambia zetu za jangwani na baharini zimeripuliwa zote na sidhani kama kuna mtu aliepona. Na kama wapo basi sijui hata kama mia wanafika" alieleza kijana huyo.
"hii kasheshe nyingine" kamanda Willy aliongea huku akitikisa kichwa, "hizi ni alama za majanga" aliongea General David. "master mind wa mchezo huu ni Alex, na ili kujihakikishia ushindi lazima tumuue" aliendelea kuongea. "kamanda Willy tuma ujumbe kwa wakuu wote tukutane leo hii kabla jua halijazama", kamanda Willy aliinuka na kuondoka. "hivi kwanini ulizaliwa we mwanaharamu Alex, ah lakini kosa ni langu kudhani utanifaa" alijisemea mwenyewe general
"majemedari wote tusikilizane, leo hii ndio itaamua hatma ya nchi yetu. Tuwaonyeshe wale wanaidhani wanaweza kuchwza na amani yetu. Vita ya leo ni ua ama uawa lakini mpaka kieleweke" hayo yalikuwa ni maneno General Griffin kwa vijana wake. "tumekusoma mkuu" walijibu kwa pamoja, "Alex utaendelea na kikosi hicho kidogo, na kazi yako ni kutufngula njia tu. Mimi nitakuja na kikosi kikubwa halafu tutaongana katika mapambano" General aliongea na Alex alitikisa kichwa kukubali. "mimi je" ilikuwa sauti ya raisi, "mkuu usalama wako ni muhimu" alijibu General Griffin.
"Muheshimwa raisi tutahitaji msaada wako" Alex aliongea na kumsogelea kisha akamnong'oneza kitu sikioni. Raisi alitabasamu na kuashiria amemuelewa, "basi hakuna shida wacha mimi niondoke niwaache muendelee na majukumu mengine" Raisi aliongea na kusimama kisha akaondoka. Waliendelea kupanda mipango yao kwa makini sana, walifanya hivo kuhakikisha hatoki mtu hata mmoja kati ya waasi.
 
111

Mipango ilipokamilika Alex aliondoka na kikosi chake, walikuwa wamejipanga kisawa sawa. kila mtu alibeba ile silaha ambayo aliamini ni rafiki yake mkubwa. Walipanda ndege na safari ikaanza, kila mtu kwenye ndege alisali anavyojua yeye. "baada ya vita hii,kutakuwa na mambo mazuri sana" aliongea Alex huku akicheka na kuwafanya wenzake wote kumuangalia kwa sintofahamu.
Ndege ilifika karibu na eneo la waasi kushuka usawa wa bahari, Alex na kikosi chake waliruka na kuingia kwenye maji. Waliogelea mpaka nchi kavu, "tutasubiri kikosi cha Jeff na Darling kifike" aliongea Alex na kila mmoja akatafuta kicha cha kujificha. Nusu saa baadae waliibuka watu kadhaa kutoka maji, walianza kutembea taratibu mpka juu kabisa kwenye mchanga. Mmoja wao aliweka silha chini na kuinyanyua mara tatu, Alex alitoka na kikosi chake. "nimefurahi kukuona tena Allen jr" Alex aliongea baada kumuona Christine, "Jeff nashkuru kwa kufika" aliongea tena na kumpa mkono Jeff ambae aliupokea kwa tabasamu.
"tunaanzia wapi?" aliuliza Jeff, "tusubiri kama dakika kumi hivi" tutapata pa kuanzia. Alex aliongea na wote wakatoa ishara ya kuelewa. Walianza kuongea utasema hawako hatarini, baada ya dakika kumi zilipita ndege kadhaa zinazojulikana kwa jina la DRONE au ndege isio na rubani. Zilianza kushambulia kambi ndogo ndogo zote ambazo zimezunguka kambi kubwa. "natumai tushapata pakuanzia" Alex aliongea na kushika mtutu wake vizuri.
Kazi ilianza huku wakijitahidi kuwaondoa wale walibahatika kupona mavamizi ya ndege zile zisizo na rubani. Walipohakikisha wamesafisha njia, Alex alitoa radio na kuongea "miba yote imeendoka", "rodger" alijibiwa upande wa pili. Vilianza kutoka vifaru kwenye maji pamoja na jambizi amabzp zilishusha magari na vifa vingine vya kivita. Walifika mpaka walipo kina Alex na Jeff, "kazi nzuri kijana" aliongea general Griffin. Waliingia kwenye gari na safari ikaanza, sasa walikuwa wamebakiwa na kambi kubwa tu..
"mkuu kitumbua kimeingia mchanga" Kamanda Willy alirpoti, wakati huo kulikuwa na kikao kinaendelea. "inavyoonekana Alex amekucheza akili mkuu" aliendelea kuongea Willy, "kivipi" aliuliza General David. "alijua akishambulia kambi ndogo ungeita wakuu wote ili kujadili mstakbali wa dhamira yenu na inaonekana amelenga ndipo" alifafanua Kamanda Willy. "ndio yuko sahihi kabisa" walisikia sauti, "msishtuke sana, kwasababu hivi punde tu tutakutana. Na nasikitika sana kukwambia General David, kosa lako kubwa ulolifanya ni kucheza na familia yangu. Kosa hilo litakugharimu vile inavyostahiki" aliongea Aex kwa sauti nzito na kukata mawasiliano.
"mkuu tumevamiwa" aliingia mwanajeshi mwengine na kuongea, sasa wale wote waiokuwepo katika kikao hicho walianza kuhisi tumbo la kuharisha. "sasa tnafanyaje" aliuliza mzee mmoja alieonekana muoga kidogo. "hapa hakuna la kufanya tumezungukwa na mjeshi ya serekali, mimi niliwaambia tufanye mapema mukaniona mjinga" aliongea General David. "sasa kila mtu hapa atatoka kwa nguvu zake" aliendelea kuongea na alipomaliza aliinuka na kuondoka.
Huko nje moto ulikuwa si wa kitoto, mkali Alex na Jeff na vikosi vyao walikuwa wakitembeza dozi. "Scarlet achana nae huyo kashakufa" Adrian alimwambia Scarlet baada kumuona akimuamsha mwenzake mmoja ambae amepigwa risasi. Mpambano ulizidi kuwa mkali, maana hiyo kambi haikuwa na wanajeshi kidogo. Wakati mpambano unaendelea Scarlet alizembea kidogo na kuna mtu alikuwa kashamlenga mlenga, ghafla General Griffin alipita mbele yake na kukinga kifua. Risasi iliopigwa kwa lengo la kumuua Scarlet ilipenya kifuani mwa General na kuanguka chini. Alipotaka kuongea nae alimpa ishara aendelee kupambanaa.

Huko ufukweni ziliibuka nyambizi nyinngine zikiongozwa na raisi mwenyewe, mambo sasa yalizidi kunoga maana waasi hawakutegemea kama jeshi kubwa kama vile lingekwenda kupambana nao. Jeshi hilo lilokuwa chini ya raisi liliekea uwanjani na kuendeleza mapigano, general David alifanikiwa kufika mpaka kwenye helicopter. "tuondoke haraka" aliongea na hapo aliongezeka mwanajeshi mmoja kwa ajili ya ulinzi na helicopter ikaondoka. Ilipofika kwenye ufukwe ilianza kushuka, "mbona unaishusha hapa" aliuliza.
 
112.


"ulidhani unaweza kututoroka" sauti ya Alex ilisikika kutoka mbele, "general mzima unaacha wanajeshi wako wanakufa wewe unakimbia" sauti ya kike ilisikika pembeni yake na ilikuwa ni ya Agent Darling.
Helicopter ilikanyaga fukwe na papo hapo ikazungukwa na wanajeshi, "wekeni silaha chini" ilikuwa sauti ya raisi. "mheshimiwa raisi mkuu wa waasi huyu hapa" Alex aliongea huku akimshusha general David kwa nguvu. "kazi nzuri kijana" raisi alimpongeza, "Agent Darling nahisi mimi nikuachie wewe huyo mpuuzi, mfanye unavotaka na hakuna atakae kuuliza" Raisi aliongea na kurudi nyuma. Masikini General David alichokutana nacho nahisi atamsimulia Allen huko kwa alipokwenda. Agent Darling alipohakikisha General David hajiwezi tena, alimchapa risasi ya kichwa na kummaliza kabisa.
Vita hiyo ilikwisha na waasi wote waliokamatwa waliuliwa huko huko, lakini hali ya general Griffin ilikuwa mbaya mno. Aliwaita Scarlet na Adrian na kuongea nao kitu kidogo, baada ya hapo raisi alifika "mheshimiwa nasikitika sitokuwepo karibu yako tena na kukusaidia katika kufanikisha malengo yako" aliongea japo kwa tabu kidog. "siku zote utakuwa karibu yangu, najivunia kuwa na General kama wewe katika nchi yangu" aliongea raisi na kumshika General mkono. "una ombi lolote la mwisho kabla hujasafiri safari ya milele" raisi alimuuliza.
"ndio mkuu, naomba Alex aongoze kikosi cha THE PIRATES. Ana mbinu nyingi sana za kivita na uwezo wa kipekee, atasaidia katika kiwango kikubwa sana katika kuimarisha ulinzi wa nchi yetu" aliongea General na kukohoa damu. "kwa mamlaka niliokuwa nayo kama raisi wa nchi hii, Bwana Alex Jr umepandishwa cheo na kuwa General wa nchii hii. Kuanzia sasa utakuwa mkuu wa kikosi cha The Pirates" raisi alimuapisha Alex mbele ya General Griffin ambae alikata roho huku ametabasamu.
Maiti yake ilibebwa a safari ya kurudi ufukweni ikaanza, lakini kabla hajaingia kwenye nyambizi Alex alimnongoneza kitu raisi nae akaonesha kama kukumbuka kitu. "Adrian, Ariella, Jeff na Christine nomba musogee hapa" alitoa amri rais, nao walisogea lakini walikuwa hawajui kitu gani kinaendelea. Ghafla kwenye nyambizi alishuka mchungaji akiwa amembatana na watu kadhaa. Walifungishwa ndoa hapo hapo katika uwanja wa vita, "Alex asante na naomba unisamehe" aliongea Christine na kumkumbatia. "usijali mdogo wangu, Allen alinambia nikulinde mpaka pale utakapopata wa kukulinda mwengine" Alex alimjibu huku akicheka.
Waliigia kwenye nyambizi na safari ya kurudi ikaanza, siku hiyo iliwekwa katika kumbukmbu za nchi hiyo kama siku ya mashujaa. Mazishi yalikamilika huko Adrian na Scarlet wakianza maisha yao nje ya jeshi, Jeff na Christine walielekea Qatar kwa ajili ya kuwasalimu ndugu wa Christine. Alex alirudi katika kambi ya the pirates kwa lengo la kukikuza kikosi hicho na kuwa hatari kuliko wanajeshi wa Project CODE X. Amani ilirejea nchini na hofu ilipotea, na kila mwaka waliadhimisha siku ya mashuja katika nchi hiyo.
.
UZALENDO NI NGAO PEKEE YA KUIKOMBOA NCHI KUTOKA KATIKA MAJANGA, JIVUNIE KUWA RAIA WA NCHI YAKO MAANA KUWEPO KWA NCHI NDIO KUNATAFSIRI UTAIFA WAKO.
IN GOD WE TRUST

MWISHO.


imeletwa kwenu NA BURE SERIES
 
FRANK MASAI = C.O.D.EX 4 (A Missing Soldier).jpg


Simulizi : C.O.D.EX. 4
Mwandishi: FRANK MASAI
Imeletwa kwenu na: BURE SERIES

SEHEMU YA 113


“Tulikuwa ni watu kama watu wengine. Tuliwapenda wazazi wetu kama watoto wengine. Tuliishi na kufurahi kama watu wengine. Na tukapata malezi bora kama watoto wengine. Lakini mambo yalikuja kubadilika baada ya kuingia mikononi mwa Wanasayansi. Watu ambao hawajali uwepo wa nyama miili mwetu na mzunguko wa damu katika mishipa ya damu. Wakapandikiza kemikali zao kwenye damu zetu, wakatengeneza miili yao kwa kutumia nyama zetu. Na hatimaye tukaitwa wanajeshi. Na tena wanajeshi wenye uwezo wa kipekee duniani. Maisha ni kama upepo, ukiamua kubadilika, hubadilika bila kuambiwa ubadilike. Maisha yetu yakabadilikia hapo, na sasa tukaitwa wanajeshi hatari.”

NEW YORK, MAREKANI.

Kulikuwa ndani ya jengo kubwa na lenye mwanga mkali kila mahali. Watu mbalimbali walioenekana ndani ya mavazi ya kitabibu huku wamekamata Ipad za gharama ambazo walionekana wakizichezea chezea na wakati huohuo wakiangalia miili ya watu iliyokuwepo ndani ya majokofu yenye matirio ya kioo na ndani yake kulikuwa na maji yaliyojaa. Binadamu waliokuwepo humo, waliingiziwa mipira midomoni na puani na walibandikwa vitu fulani vifuani mwao kwa ajili ya kupima mapigo yao ya moyo.

“We called them, New Generation Soldiers, Sir (Tunawaita Wanajeshi wa Kizazi Kipya, Mkuu)” Aliongea bwana mmoja ambaye alikuwa nje ya maabara ile lakini aliweza kuona kila kinachoendelea kupitia kioo kikubwa kilichokuwa ndani ya jengo lile.

“Are you sure about your generation? (Unahakika na kizazi chako)” Bwana mmoja mwenye suti na mwenye asili ya Kimarekani, alimuuliza yule tabibu aliyekuwa kasimama pembeni yake akijinadi juu ya wale wanajeshi waliokuwa ndani ya majokofu zaidi ya hamsini.

“Yes Prime Minister. These are the best soldiers we ever created before. They can fight for so long without tired. (Ndio Waziri Mkuu. Hawa ni wanajeshi bora kuliko tuliyowahi kuwatengeneza hapo kabla. Wanaweza kupigana kwa muda mrefu bila kuchoka)” Akajibu yule tabibu ambaye alivaa kitambulisho kilichoonesha sura yake, jina na cheo chake. Bwana mmoja aliyekuwa na asili ya Kimarekani, na ilionekana kuwa kaongozana na Waziri Mkuu, aliangalia kitambulisho hicho kabla hajaongea.

“Tutegemee nini katika wanajeshi wako Dokta Ice Mujo.” Akauliza yule bwana aliyeongozana na Waziri Mkuu kwa lugha ya Kiingereza.

“Maajabu ya dunia. Wanajeshi watano pekee, wanaweza kuingamiza Urusi yote ndani ya saa moja. Tumewapachika uwezo wa kipekee na silaha nzito wanazo vichwani mwao.” Alijibu Dokta Ice.

“Silaha gani hiyo Dokta?” Akauliza tena bwana aliyeongozana na Waziri Mkuu.

“Nyuklia bombs. Kila mwanajeshi hapo, kabla hajaenda mapambanoni, tunampandikiza chip ndogo ambayo inaweza kuruhusu mabomu ya nyuklia yalipuke mahali ambapo yatapandikizwa. Kati ya wanajeshi watano tunaoweza kuwatuma, wawili ni lazima wawe na mabomu ya Nyuklia. Hawa ndio wanauwezo wa kipekee.” Alijibu Daktari.

“Wanauwezo gani?” Akauliza Waziri Mkuu.

“Angalia hii.” Akamsogezea Ipad. Kisha akabonyeza sehemu ya video na hapo wakaanza kuonekana wanajeshi wakifanyiwa majaribio. Picha ambayo iliwafanya wale mabwana waliokuja pale kushangaa, ni mlipuko mkubwa uliotoka kwenye mwili wa mwanajeshi mmoja, halafu baada ya mlipuko huo, yule mwanajeshi alitoka ndani ya moto akiwa anawaka lakini akitembea bila wasiwasi… Baadae moto huo unazima, na mwanajeshi anaoekana hana makovu yoyote ya moto licha ya nguo zake zote kuungua.

“Hatari sana hii.” Aliongea waziri mkuu huku katabasamu.

“Hiyo ndio C.O.D.EX improved chemical.” Daktari alijigamba kwa mbwembwe.

“Kwa hiyo ni ile C.O.D.EX ya wale wanajeshi wengine?” Aliuliza bwana yule aliyeongozana na Waziri Mkuu.

“Ndio Waziri wangu wa Ulinzi.” Kwa tabasamu pana alijibu Dokta Ice.

“C.O.D.EX ni nini?” Akauliza Waziri Mkuu.

“Ni kifupisho cha maneno haya, CINDREX OLTIVIASO DECA ENDROLINE X. Ni chemikali zilizobuniwa miaka kumi nyuma na walitengenezwa wanajeshi kadhaa ambao walisumbua sana CIA na FBI. Baada ya kujua kemikali hizi, CIA waliweza kuharibu maabara yote ya kutengenezea wanajeshi hawa. Sasa hivi ndio tumepewa kibali cha kutengeneza silaha kupitia kemikali hizi.” Alijibu Daktari.

“Kuna tofauti gani kati ya wanajeshi hawa na wale wa miaka kumi iliyopita? Hawawezi kuleta madhara kama yale?” Aliuliza Waziri wa Ulinzi.

“Hapana. Hawawezi fanya hivyo. Tatizo kubwa la wale waliyopita, hawakuwatoa kumbukumbu wale waliowatengeneza, hivyo ilikuwa rahisi kwa zile kemikali kurudisha kumbukumbu baada ya kuanza kuisha. Hilo likaleta tatizo kwa baadhi ya wanajeshi ambao kumbukumbu ziliwarudia.” Akajibiwa.

“Okay. Kwa hiyo hawa hawana kumbukumbu?” Akauliza tena Waziri wa Ulinzi.

“Ndio. Kabla hatujawaingizia C.O.D.EX, tulihakikisha kwanza tunafuta kumbukumbu zao zote za maisha yaliyopita. Tuna uhakika tumefanikiwa katika hilo.” Alijibiwa na daktari.

Waziri wa Ulinzi akaangaliana na Waziri Mkuu kisha kwa ishara fulani walipeana kuonesha kuwa wamekubaliana na ile kazi ya C.O.D.EX.

“Sawa Dokta. Ila kwanza ni lazima tufanye majaribio na silaha zako.” Waziri wa Ulinzi aliongea na kumpa nafasi dokta naye aongeze jambo kama analo.

“Mmepanga wapi kufanya majaribio yenu?” Akauliza Dokta.

“Iraq na Iran.” Akajibiwa na dokta akaonesha kukubaliana na majibu hayo.

“Ila kuna jambo moja ambalo tumelipandikiza kwenye miili yao.” Akakumbusha daktari.

“Lipi hilo?” Akaulizwa.

“Hawana huruma hata kidogo. Kitendo cha huruma kwao kimepita kushoto. Kwa hiyo hayo majaribio, tujaribu kuyafanya mbali na raia.” Akaongea dokta.

“Hamna shida.” Akajibiwa na Waziri wa Ulinzi kwa kifupi.

Baada ya maongezi hayo marefu, wale viongozi wa serikali ya Marekani, walianza kuondoka eneo lile huku nyuma wakifuatiwa na walinzi wao muhimu kabisa.

****

BAADA YA WIKI MBILI.

Vyombo vya habari duniani vilikuwa vinatangaza kuhusu Iran kuvamiwa na mitambo yake ya nyuklia kuharibiwa vibaya na wakati huo mateka wa Iraq walisemekana kuwa wamekombolewa na wanajeshi wa jeshi la Marekani lakini hawatambuliki ni wapi walipo. Habari zilikuwa zimezagaa na kuzusha maswali kadhaa kwenye vichwa vya habari na watu wote kwa ujumla.

Vyombo vya habari viliuliza kuhusu wanajeshi hao na Waziri Wa Ulinzi alithibitisha uwepo wa wanajeshi hao na kuahidi kuwa, Marekani itakuwa na nguvu kubwa kuliko nchi yoyote duniani.

Wakati hayo yanaendelea, daktari mkuu wa ile maabara alikuwa anatazama na kusikiliza vyombo vya habari kila kukicha. Jambo ambalo hakuwaambia wale viongozi, ni uwezo wa wale wanajeshi kuchukua matukio yote kwenye chipu iliyokuwa imepandikizwa vichwani mwao kwa ajili ya kuwatuma wafanye mambo fulani.

“Wajinga sana hawa. Niliwaambia wasifanye majaribio kwenye makazi ya raia wema. Matokeo yake wamewaua mateka wote. Washenzi sana. Natakiwa kufanya jambo moja muhimu sana kabla sijaondoka hapa.” Alijiwazia Dokta Ice na hapohapo akaifata kompyuta yake iliyokuwa katika ofisi ndogo kwenye chumba chake na kuanza kusoma mambo kadhaa kwenye mafaili yaliyokuwepo kwenye kompyuta hiyo.

Kesho yake ilikuwa Asubuhi ya Jumapili yenye bashasha nyingi sana. Dokta akiwa anajua wazi kabisa kuwa siku hiyo ni ya mapumziko kwake, alitoka ndani ya nyumba yake akiwa kakamata mkoba wenye makaratasi kadhaa, kisha akapanda gari lake la gharama na kuelekea zilipo ofisi zao.

Huko aliamrisha baadhi ya wafanyakazi waondoke kwa sababu alikuwa na kazi nyeti ya kufanya bila wao kuijua. Alipofanikiwa kuwatoa, akafungua jokofu moja ambalo lilikuwa tofauti na yale mengine. Lenyewe lilikuwa halioneshi na lilifanana na lile la kuhifadhia maiti. Alipolifungua, akaonekana muafrika mmoja aliyekuwa kafumba macho yake kama marehemu na mvuke ukimtoka kwa sababu ya kuganda kwa mwili wake.
 
114.
Ice Mujo, akabofya vitufe kadhaa kwenye lile jokofu nalo likaanza kuvia maji ambayo yalikuwa ya moto. Maji hayo yakayayusha barafu iliyopo mwilini mwa muafrika yule na kumfanya awe laini na mwenye hali ya umoto.

Akabofya tena vitufe kadhaa kwenye ipad yake. Vitu fulani vikatokea angani na kisha vikashuka hadi kwenye lile jokofu. Vikazama ndani ya maji na kumkamata yule bwana, kisha vikatoka naye na kumuweka kwenye lile jokofu lingine ambalo lilikuwa linauwezo wa kujazwa maji pamoja mitambo ya kumuwezesha binadamu kupumua.

Dokta Ice, akambandika vile vifaa vya mapigo ya moyo pamoja na mipira maalumu kwa ajili ya kupumulia. Alipomaliza, akafunga lile jokofu na kufungulia maji yaliyoanza kujaa ndani yake.

Akasogea kwenye kompyuta inayoonesha hali ya yule binadamu muafrika. Akaanza kuruhusu kemikali aina ya C.O.D.EX ianze kuingia mwilini mwa yule bwana. Kilikuwa ni kitendo cha dakika kumi pekee kukamilisha tendo lile na lilifanikiwa kwa sababu muafrika yule alianza kupumua akiwa ndani ya jokofu lile.

Kwa haraka, akabonyeza tena vitufe kwenye kompyuta na hapohapo maji yakaanza kupungua na baada ya kuisha yote, yule bwana alijikuta akisogezwa nyuma kwa kasi na kisogo chake kikagota nyuma ya kidirisha kidogo ambacho kilifunguka na hapohapo mwanga fulani mwekundu ukaanza kupitia sehem hiyo ya kisogoni. Kisogo cha yule bwana kikafunuliwa kidogo kwa kutumia ule mwanga ambao ulitumika kukata sehemu hiyo.

Kiasi kidogo cha ubongo kikatolewa, na baada ya hapo, Dokta Ice alifungua mkoba wake na kutoa Diskette na kuchomeka kwenye sehemu maalumu ya kwenye komyuta aliyokuwa anaitumia. Ikaanza kusoma harakahara na baadaye ikaandika ‘loading succefully, 100%’. Dokta akashusha pumzi na kisha akabofya kitufe cha Enter. Hapo kule kwenye kisogo cha yule bwana, ikapandikizwa chipu na kisha ile ngozi iliyotolewa kisogoni, ikapachikwa na kupitiwa na mwanga ule mwekundu. Pakarudi vilevile.

Yule muafrika akatoka kule alipobananishwa na kusogezwa katikati ya lile jokofu. Dokta akabonyeza tena vitufe kadhaa kwenye kompyuta yake, yule bwana akaanza kuzunguka taratibu kwenye lile jokofu kw a dakika zipazo kumi. Aliposimama, kompyuta ikaongea kwa sauti ya kike, ‘upgrade complete’. Kisha maji yakajazwa ndani ya jokofu na dokta akawa kamaliza kazi ambayo alipanga kuifanya jana yake.

Dakika ishirini mbele, akamtoa mtu yule kwenye jokofu na kumuingiza kwenye mashine nyingine iliyoanza kuupembua mwili wa muafrika yule hadi ikaridhika na kutamka maneno mengine ya kiingereza, ‘Scan Complete’.

Dokta Ice akatabasamu baada ya kufungua mashine ile na yule muafrika kusimama mwenyewe na kumtazama Dokta.

“Nipo tayari kukutumikia mkuu.” Aliongea bwana yule kwa Kiingereza na kumfanya Dokta kuzidi kutabasamu.





Yule mwafrika akatoka kule alipobananishwa na kusogezwa katikati ya lile jokofu. Dokta akabonyeza tena vitufe kadhaa kwenye kompyuta yake, yule bwana akaanza kuzunguka taratibu kwenye lile jokofu ka dakika zipazo kumi. Aliposimama, kompyuta ikaongea kwa sauti ya kike, ‘upgrade complete’. Kisha maji yakajazwa ndani ya jokofu na dokta akawa kamaliza kazi ambayo alipanga kuifanya jana yake.

Dakika ishirini mbele, akamtoa mtu yule kwenye jokofu na kumuingiza kwenye mashine nyingine iliyoanza kuupembua mwili wa mwafrika yule hadi ikaridhika na kutamka maneno mengine ya kiingereza, ‘Scan Complete’.

Dokta Ice akatabasamu baada ya kufungua mashine ile na yule mwafrika kusimama mwenyewe na kumtazama Dokta.

“Nipo tayari kukutumikia mkuu.” Aliongea bwana yule kwa Kiingereza na kumfanya Dokta kuzidi kutabasamu.

ENDELEA.

“Nakutuma Tanzania. Nenda kaishi huko, usirudi tena Marekani. Nenda katende yaliyomema kwa walio wema. Usithubutu kuangamiza kilicho chema. Na watakaojaribu kuangamiza kile kilichochema, basi ni ruhusa kwako kuwaangamiza au kuwapoteza.” Aliongea Daktari Ice huku kakamata mikono miwili ya yule mwanajeshi.

“Kwa nini Tanzania?” Akauliza yule mwanaume aliyeundwa na Ice.

“Ni kwa sababu ni sehemu salama kwako kuliko sehemu nyingine yoyote duniani.” Akajibu Daktari kwa Kiingereza.
 
115.
“Sawa. Nitafanya hivyo mkuu.” Akajibu yule bwana kwa heshima.

“Huko utatumia jina la Idris Iris,” Aliongea hayo huku anapekua mkoba aliokuja nao na kutoa passport kadhaa za bwana yule zikiwa na jina hilo alilolitaja. “Kuna nyumba ipo Arusha, ramani yake ipo humu.” Pia akamuonesha diskette ambayo alisema ndimo ramani ilimo. “Na hizi,” Akamuonesha mfuko fulani, yule mwanaume akauvuta. “Ni nguo zako.” Ilikuwa ni suti nyeusi na yule bwana alizivaa kwa haraka kwa sababu bado alikuwa hana kitu mwilini.

“Ahsante Mkuu.” Alishukuru Idris Iris baada ya kupendeza ndani ya suti ya gharama katika dunia ya leo.

“Wewe ni mwanajeshi. Hata kama utavaa vazi la namna gani. Kumbuka hilo Idris. Komboa waliokuwa wema na teketeza wabaya. Nakuamini sana, nimekutengeneza kwa uwezo wa kipekee, unauwezo mkubwa kuliko hawa wengine. Kaikomboe dunia dhidi ya waonevu.” Aliongea Daktari na hapohapo akaanza kupanga vitu vyake. Na kwa haraka, akaanza kutoka na Idris ndani ya maabara ile.

Alifanikiwa kufika nje na kukwea ndani ya gari lake akiwa na Idris lakini wakati anataka kufunguliwa geti ili atoke ndani ya jengo lile kubwa, alikutana na upinzani toka kwa walinzi wakitaka kumjua Idris ni nani, na kwa nini atoke mle ndani wakati hakuingia naye.

Dokta alipoona hali imekuwa tete, akakanyaga mafuta ya gari lake na kugonga geti huku akiwaacha wanajeshi waliokuwa wakilinda lango lile kufyatua risasi kadhaa nyuma yake. Lakini kwa bahati mbaya, risasi hizo ziliinshia kwenye kioo kisichoingiza risasi kwenye gari lile.

Kwa tukio hilo, haraka taarifa zikapelekwa makao makuu ya wanajeshi wale pamoja na CIA. Walipokuja ndani ya maabara, kweli walikuta kuna mwanajeshi mmoja aliyekuwa bado hajawekewa C.O.D.EX katoweka na ni wazi Dokta Ice ndiye alihusika kufanya hivyo.

“Ni lazima Dokta Ice atafutwe na haraka sana amlete yule mwanajeshi hapa kabla ya masaa ishirini na nne hayajapita.” Alibwata mkuu wa kitengo kile cha C.O.D.EX. “Tuma C.O.D.EX Soldier 0ne and Two. Aidha Dokta na mwanajeshi wake waangamizwe, au waletwe wakiwa hai.” Alitoa agizo haraka yule mkuu na bila kuchelewa, wanajeshi wawili toka kwenye jokofu lenye maji, walitolewa na kuvishwa magwanda ya kijeshi kabla ya kupewa silaha za kijeshi na misheni ambayo walipaswa kwenda kuifanya.

“Waleteni wakiwa wazima, hasa daktari, huyo mwanajeshi, mnaweza kummaliza tu.” Aliongea jamaa mmoja mwenye mamlaka juu ya ile maabara na C.O.D.EX kwa ujumla. “Mnaweza kwenda.” Baada ya maneno hayo, wale wanajeshi wawili ambao sura zao hazikuwa na tabasamu wala aina yoyote ya furaha, walitoka ndani ya maabara ile huku wanakimbia kama wachezaji wa mpira wanaopasha misuli yao joto kabla ya mechi.

Safari yao iliishia nje ya maabara ile kubwa na walikuta ndege maalumu ya kisayansi ikiwasubiria nje. Nao waliipanda kwa haraka na ndege hiyo ikachoma mafuta na kupaa kwa kasi toka ndani ya maabara ile.

Ikiwa ni saa tisa ya alasiri, kwenye nyumba ya Dokta Ice, wanajeshi wale wawili wanavamia nyumba hiyo kwa kuingilia madirishani. Ilikuwa ni kimuhemuhe kwa sababu waliingia kwa kupasua vioo kwa kutumia miguu yao ambapo kwa huku juu walikuwa wamekamata kamba iliyowawezesha kuning’inia na kuingia ndani ya jengo la Dr. Ice kwa mbwembwe hizo.

Wakatua ndani na macho yao yaliypokuwa yamevikwa mawani myeusi, yalianza kuangaza huku na huko. Japo ulikuwa ni muda wa alasiri, lakini ndani mle mlikuwa na giza linaloweza kumfanya yeyote asiweze kuona kirahisi.

“Scan the house.” Sauti ilisikika kwenye masikioni mwao kuwataka wale wanajeshi waweze kuitizama ile nyumba kwa kina zaidi. Wakashika kwenye mawani zao, nazo zikatoa mwanga wa kijani. Wakaanza kutazama huku na huko kuona kama kuna kiumbe chochote kitakachoonekana.

“Scanning Detected.” Mawani ya mmoja wa wanajeshi, ikaandika maandishi hayo ikimaanisha katika tafuta tafuta kwa kutumia teknolojia ile, iliewenza kung’amua kitu aina fulani ya binadamu au mnyama.

Miwani hizo ni kwa ajili ya kuwatambulisha kitu wanachokitafuta hasa ikiwa ni chenye damu, nyama, karatasi maalumu ambayo ni lazima wapewe taarifa zake ndipo waziseti hizo miwani kwa ajili ya msako.

Mwanajeshi mmoja anapewa taarifa kuwa miwani yake imeona kitu ambacho kinamaumbile sawa na wanachokitafuta.

“Easy soldier.” Ilisikika sauti ya aliyewatuma ikimwambia taratibu. Naye mwanajeshi akawa anaenda kama ananyatia kitu kilisikimbie angali alikwishaingia kwa fujo ndani ya nyumba ya Dokta Ice. Miwani yake ikazidi ikaonesha kuwa inakaribia hicho kitu, nayo mikono ya mwanajeshi yule ikajikaza kwenye bunduki hatari aliyoikamata. Alifika sehemu hiyo na kunyanyua meza kwa nguvu na kuitupa pembeni. Hapo paka fulani mwenye mabaka akatoka mbio. Si kiongoi wao wala wale wanajeshi ambao hakushusha pumzi kali waliyokuwa wameibana.
 
116.
“Shit.” Kiongozi aliyewatuma alitukana baada ya kuona sicho wanachokitafuta. Yule mwanajeshi akageuka nyuma tayari kwa kuendelea na msako ndani ya jumba lile lakini kwa mshtuko mkubwa, kitu toka juu ya dali kilidondoka na kumvaa mwanajeshi yule hadi bunduki yake ikadondokea mbali na yeye. Pale alipojaribu kuifata, kitu kile kilijirusha kwa sarakasi ya chinichini na kuipigia mbali bunduki ile.

Mwanajeshi mwingine alipokuja kutahamaki, alikuwa karibu na mtu mweusi ambaye alikwishaikamata vema bunduki yake na tayari kwa kuitoa mikononi mwake kwa sababu alikuwa anaing’ang’ania kwa nguvu huku akiivuta. Alikuwa ni Idris Iris, mwanajeshi mpya toka kwa Dokta Ice.

Mwanajeshi wa pili aliyekuwa kakamata vema bunduki yake akiwa hataki kabisa kuiachia, alijikuta akisukumwa hadi ukutani na kufanya ukuta huo utikisike kutokana na mtikisiko wa miili ile iliyokumbana. Wakati huo mwanajeshi wa kwanza aliyevamiwa toka juu ya dari, alikuwa anaenda kwa kasi nyuma yao na alipokaribia, alijikuta akisimamishwa mwendo wake kwa teke zito la kifuani ambalo lilimrusha hadi kwenye kochi mojawapo lililopo kwenye ile nyumba.

Macho ya Idris yakamuangalia mwanajeshi aliyekuwa anang’ang’ania bunduki, wote walikuwa hawana chembe ya huruma ndani yao. Ni Idris pekee ndiye aliyekuwa anaweza kupambana nao. Naye hakumchelewesha sana huyu ambaye shingoni alivaa cheni yake ya kijeshi yenye jina C.O.D.EX Soldier 1. Idris akamtwanga kichwa cha puani, Soldier One bado akawa hataki kuachia bunduki, na badala yake, alimgeuza haraka Idris na kumbamizia ukutani. Ile bunduki akaanza kuisogeza maeneo ya shingoni tayari kumkaba nayo hadi kumyonga kabisa.

Idris na Soldier One wakawa wanashindana nguvu, huyu anataka kumkaba, na huyu mwingine anazuia tendo hilo. Mwisho wake ulikuwa Idris kupiga mguu mmoja wa Soldier One kwa mguu wake wa kulia, nao mguu wa Soldier ukakubali kulegea. Ile bunduki ikamtoka Soldier na kubaki mikononi mwa Idris ambaye alimpiga teke zito la uso yule mwanajeshi aliyelega-lega hadi mawani yake ikadondokea pembeni.

Soldier One akamtazama Idris kwa macho ya kithirani, na Idris kuonesha yupo vema, akatupa bunduki ile pembeni na kukaa sawa kimapambano. Soldier One akasimama wima, naye Soldier Two toka kule alipodondokea, akajizoa zoa na kujiunga na mwenzake, naam, wakawa wanataka kumuonesha Idris kuwa wao si wa mchezo.

“Ngoja tujue yupi ni mwanajeshi imara.” Aliongea mkuu wa C.O.D.EX ambaye alikuwa akishuhudia mpambano ule moja kwa moja kupitia skrini kadhaa zilizokuwepo mle mjengoni ambazo ziliundwa na kuungwa kwenye kompyuta.

Idris akiwa tayari kwa mpambano ule, alianza kusogelewa na wale mabwana ambao walijaa miili yao kama wanyanyuao vitu vizito. Walipomfikia, walianza kumshambulia kwa mateke na ngumi kadhaa ambazo Idris kwa ustadi mkubwa alikuwa anazikwepa na nyingine kuzitolea nje. Alipoanza yeye kucheza zake, wale mabwana walijikuta katika hali mbaya ambayo kiukweli hawakutegemea kama kuna mwanajeshi anaweza kupigana kulikoni wao.

Idris aliruka angani na kisha miguu yake miwili ikaibana shingo ya mwanajeshi mmoja na mikono yake ikakaba shingo ya mwanajeshi mwingine. Idris akawa juu kwenye vichwa viwili. Akajipindua kwa nguvu na kuwafanya wale mabwana nao kupinduka naye na kisha wakajikuta wanabamiza vichwa vyao kwenye sakafu.

Ilikuwa ni vita vya kimyakimya. Hamna ambaye alikuwa analia kwa maumivu kwa sababu miili yao iliondolewa kabisa hali ya kuhisi maumivu. Ni damu pekee ndizo zilizoweza kuwatoka lakini hawakuthubutu hata kulia au kugugumia kwa maumivu.

Baada ya kubwaga chini, Idris alisimama na kupanda juu meza kubwa iliyopo mle ndani, na kisha kwa nguvu zake zote, alijirusha kama mwanamieleka na mwili wake kudondokea tumboni kwa Soldier Two ambaye naye alikaza meno yake kuonesha lile pigo limemuingia haswa.

Idris alipomuangalia Soldier One, alimuona akijivaa vaa taratibu ili asimame na hilo likawa kosa lake kwani Idris alimchota ngwara nzito na jamaa yule alirudi chini akidondokea kisogo na kabla hata hajajua la kufanya, soli ngumu ya kiatu cha Iris ilikita kwenye mdomo wake na kuzidi kumpoteza kabisa.

Akiwa kasimama katikati ya wanajeshi wale wawili. Alisikia mlio wa simu toka mle ndani. Kwa haraka akaanza kukimbia kuelekea dirishani na kupasua kioo kilichokuwa kimebakia baada ya kupasuliwa mara ya kwanza na wale C.O.D.EX soldiers. Akajitupa nje na hapo helikopta kubwa ilitokea angani lakini helkopta hiyo ilijikuta inapoteza muelekeo wa Idris baada ya mlipuko mkubwa kutokea kwenye nyumba ya Dokta Ice.

Akili zao zikawaza kuwapoteza wale wanajeshi wawili na kumsahau kabisa Idris ambaye alidandia pikipiki moja kubwa iliyokuwa nje ya geti la Dokta Ice. Akaingiza gia, na kuanza kutokomea toka eneo lile akiwaacha wale wababe wengine wakihaha ndani ya jumba la Dokta Ice.





Idris alipomuangalia Soldier One, alimuona akijivaa vaa taratibu ili asimame na hilo likawa kosa lake kwani Idris alimchota mtama mzito na jamaa yule alirudi chini akidondokea kisogo na kabla hata hajajua la kufanya, soli ngumu ya kiatu cha Iris ilikita kwenye mdomo wake na kuzidi kumpoteza kabisa.

Akiwa kasimama katikati ya wanajeshi wale wawili. Alisikia mlio wa simu toka mle ndani. Kwa haraka akaanza kukimbia kuelekea dirishani na kupasua kioo kilichokuwa kimebakia baada ya kupasuliwa mara ya kwanza na wale C.O.D.EX soldiers. Akajitupa nje na hapo helikopta kubwa ilitokea angani lakini helkopta hiyo ilijikuta inapoteza muelekeo wa Idris baada ya mlipuko mkubwa kutokea kwenye nyumba ya Dokta Ice.
 
117.
Akili zao zikawaza kuwapoteza wale wanajeshi wawili na kumsahau kabisa Idris ambaye alidandia pikipiki moja kubwa iliyokuwa nje ya geti la Dokta Ice. Akaingiza gia, na kuanza kutokomea toka eneo lile akiwaacha wale wababe wengine wakihaha ndani ya jumba la Dokta Ice.

ENDELEA.

Safari ya Idris iligotea kwenye hotel moja ya kifahari Jijini New York. Akaingia huko na kuchukua lift ambayo ilimpandisha hadi ghorofa ya juu kabisa na huko alikutana na Dokta Ice ambaye muda mwingi alikuwa kasimama kwenye dirisha la chumba alichopanga.

“Unajua ni sababu gani nimekuachia wewe huru?” Dokta Ice aliongea baada ya Iris kuingia na kusimama kiheshima nyuma ya Ice.

“Hapana Mkuu.” Akajibu kikakamavu kama wafanyavyo wanajeshi.

“Ni kwa sababu dunia haina usawa kabisa. Dunia hii inamambo ambayo ukiingia kiundani, haitendi vile tunavyotaka itende.” Akaanza kwa hasira kidogo Dokta Ice. “Wametengeneza….. Hapana, tumetengeneza wanajeshi, lakini wanajeshi hawa ni kama silaha. Hawana huruma hata kidogo. Kabla hatujaingia wazo la kuwawekea chipu za huruma, wamewachukua baadhi ya wanajeshi na kuwapeleka huko wanapopajua. Huko kuna baadhi ya mateka wakiwa watoto na wanawake wameuawa kikatili sana na hawa wanajeshi. Mwenye roho kama mimi, siwezi kuvumilia. Nimekutengeneza wewe ili kidogo wafahamu kuwa nyie si silaha za maangamizi bali pia ni wokovu kwa wasiojiweza.” Alitabanainisha Dokta Ice.

“Umeoa Mkuu?” Akauliza swali ambalo Dokta Ice hakulitegemea. Akamuangalia mwanajeshi wake kisha akatabasamu kwa masikitiko.

“Yeah! Nilioa na nilipata mtoto mmoja wa kike lakini niliwapoteza kwa ajali ya gari miaka kumi iliyopita. Toka hapo sikuwa na haja ya kuoa tena.

“Ilikuwaje ukawapoteza kwa ajali na wewe ukabaki?” Akauliza tena Idris Iris.

“Ni kama wewe navyotaka kufanya. Nilikuwa nawatorosha kwa sababu CIA walikuwa wananiwinda sana kwa ajili ya kutengeneza upya folmura ya C.O.D.EX. Sasa ili niepushe familia yagu kuingia matatizoni, nikataka kuwahamisha na kuwapeleka Afrika.” Alihadithia Dokta Ice.

“Afrika. Tanzania tena au wapi?” Akamuuliza swali lingine.

“Ndio. Nilitaka kuwapeleka Tanzania kwa sababu kule pana amani na wanaurafiki mkubwa na nchi zenye nguvu duniani hivyo kama Marekani wakiamua kuwapiga Watanzania, wajue watakuwa vitani na Cuba, China, Urusi na nchi zote za ujamaa.”

“Ajali ilikuwaje?” Akaendelea na maswali Iris.

“Mke wangu ndiye alikuwa dereva. Mimi nilimwambia akimbie na nikabaki nawazubaisha CIA kwa gari lingine. Walipogundua kuwa mke wangu anakimbilia uwanja wa ndege, ndipo wakatuma helikopta ambayo iliifutilia mbali familia yangu kwa kuizinga kwa taa zake na kisha kulipotezea muelekeo gari alilokuwa anaendesha mke wangu. Likaingia darajani na kupinduka huko. Likawaka moto na baadae kulipuka.”

“Mwanao alikuwa na miaka mingapi kipindi hicho?” Swali lingine toka kwa Idris. Dokta akamtazama kwa macho ya masikitiko kisha akamtaka mwanajeshi wake akae kwenye kitanda cha hotel ile.

“Alikuwa na miaka tisa pekee,” Dokta Ice akamjibu na kisha akaendelea. “ Hamna kitu kinachouma kama kumpoteza mtu au watu unaowapenda. Hadi leo inaniuma sana. Nilitaka kujivika roho ya kikatili na kulipa kisasi kwa watu ambao hawana hatia, lakini moyo umekataa kabisa baada ya kushuhudia mauaji ya kutisha ya kule Iraq kwa wale mateka.

“Samahani na pole kwa hilo mkuu. Lakini swali la mwisho, mkeo yeye alikuwa anafanya kazi gani?” Akaulizwa tena.

“Alikuwa ni daktari mwenzangu. Baada ya mimi ni yeye. Hata hii folmura ya C.O.D.EX ni mimi na yeye ndio tuliijenga lakini kulikuwa na kashikashi fulani ambazo zilinifanya nitake kumtorosha mke wangu. Hapo ndipo yakatokea yaliyotokea.” Akajibu swali kwa ufasaha kabisa Dokta Ice.

Macho ya Idris yakaonesha yanajambo la kutaka kuongea lakini hakutoa nafasi ya kuyatoa ambayo kayahisi toka moyoni mwake.

Japo Idris Iris alikuwa ni mwanajeshi wa kutengenezwa, lakini yeye aliumbwa kiufasaha sana na Dokta Ice. Yeye aliweza kuhisi yale ambayo kila binadamu anaweza kuyahisi. Lakini yeye hakuwa sana na binadamu kwa sababu alikuwa na kiruhusuji au activetor maalumu ya kulipua mabomu ya nyuklia. Mbali na hapo, yeye hakuwa sawa na wale wanajeshi wengine ambao wanaweza kuungua mavazi pekee. Yeye aliweza kuungua hadi kuisha kabisa mwili wake na kubaki vyuma fulani vilivyopandikizwa mwilini mwake kwa kemikali za C.O.D.EX ambazo ndizo zinamfanya aungue mwili mzima na baadae kemikali hizo, huanza kuujenga mwili wake kwa kutengeneza ngozi mpya. Tendo hilo huchukua dakika moja pekee.

“Unatakiwa kuondoka usiku huu Idris. Utashukia Dar es Salaam. Na hapo utakuta ndege maalumu kwa ajili yako, nayo itakupeleka hadi Arusha. Huko napo utakuta gari maalumu kwa ajili yako, nalo litakuchukua hadi kwako. Huko ishi kwa amani.” Aliongea Dokta Ice huku akikusanya baadhi ya vitu na kutumbukiza kwenye mkoba maalumu wa nguo.
 
View attachment 1751972

Simulizi : C.O.D.EX. 1
Mwandishi: FRANK MASAI
Imeletwa kwenu na: PSEUDEPIGRAPHAS

SEHEMU YA 113


“Tulikuwa ni watu kama watu wengine. Tuliwapenda wazazi wetu kama watoto wengine. Tuliishi na kufurahi kama watu wengine. Na tukapata malezi bora kama watoto wengine. Lakini mambo yalikuja kubadilika baada ya kuingia mikononi mwa Wanasayansi. Watu ambao hawajali uwepo wa nyama miili mwetu na mzunguko wa damu katika mishipa ya damu. Wakapandikiza kemikali zao kwenye damu zetu, wakatengeneza miili yao kwa kutumia nyama zetu. Na hatimaye tukaitwa wanajeshi. Na tena wanajeshi wenye uwezo wa kipekee duniani. Maisha ni kama upepo, ukiamua kubadilika, hubadilika bila kuambiwa ubadilike. Maisha yetu yakabadilikia hapo, na sasa tukaitwa wanajeshi hatari.”

NEW YORK, MAREKANI.

Kulikuwa ndani ya jengo kubwa na lenye mwanga mkali kila mahali. Watu mbalimbali walioenekana ndani ya mavazi ya kitabibu huku wamekamata Ipad za gharama ambazo walionekana wakizichezea chezea na wakati huohuo wakiangalia miili ya watu iliyokuwepo ndani ya majokofu yenye matirio ya kioo na ndani yake kulikuwa na maji yaliyojaa. Binadamu waliokuwepo humo, waliingiziwa mipira midomoni na puani na walibandikwa vitu fulani vifuani mwao kwa ajili ya kupima mapigo yao ya moyo.

“We called them, New Generation Soldiers, Sir (Tunawaita Wanajeshi wa Kizazi Kipya, Mkuu)” Aliongea bwana mmoja ambaye alikuwa nje ya maabara ile lakini aliweza kuona kila kinachoendelea kupitia kioo kikubwa kilichokuwa ndani ya jengo lile.

“Are you sure about your generation? (Unahakika na kizazi chako)” Bwana mmoja mwenye suti na mwenye asili ya Kimarekani, alimuuliza yule tabibu aliyekuwa kasimama pembeni yake akijinadi juu ya wale wanajeshi waliokuwa ndani ya majokofu zaidi ya hamsini.

“Yes Prime Minister. These are the best soldiers we ever created before. They can fight for so long without tired. (Ndio Waziri Mkuu. Hawa ni wanajeshi bora kuliko tuliyowahi kuwatengeneza hapo kabla. Wanaweza kupigana kwa muda mrefu bila kuchoka)” Akajibu yule tabibu ambaye alivaa kitambulisho kilichoonesha sura yake, jina na cheo chake. Bwana mmoja aliyekuwa na asili ya Kimarekani, na ilionekana kuwa kaongozana na Waziri Mkuu, aliangalia kitambulisho hicho kabla hajaongea.

“Tutegemee nini katika wanajeshi wako Dokta Ice Mujo.” Akauliza yule bwana aliyeongozana na Waziri Mkuu kwa lugha ya Kiingereza.

“Maajabu ya dunia. Wanajeshi watano pekee, wanaweza kuingamiza Urusi yote ndani ya saa moja. Tumewapachika uwezo wa kipekee na silaha nzito wanazo vichwani mwao.” Alijibu Dokta Ice.

“Silaha gani hiyo Dokta?” Akauliza tena bwana aliyeongozana na Waziri Mkuu.

“Nyuklia bombs. Kila mwanajeshi hapo, kabla hajaenda mapambanoni, tunampandikiza chip ndogo ambayo inaweza kuruhusu mabomu ya nyuklia yalipuke mahali ambapo yatapandikizwa. Kati ya wanajeshi watano tunaoweza kuwatuma, wawili ni lazima wawe na mabomu ya Nyuklia. Hawa ndio wanauwezo wa kipekee.” Alijibu Daktari.

“Wanauwezo gani?” Akauliza Waziri Mkuu.

“Angalia hii.” Akamsogezea Ipad. Kisha akabonyeza sehemu ya video na hapo wakaanza kuonekana wanajeshi wakifanyiwa majaribio. Picha ambayo iliwafanya wale mabwana waliokuja pale kushangaa, ni mlipuko mkubwa uliotoka kwenye mwili wa mwanajeshi mmoja, halafu baada ya mlipuko huo, yule mwanajeshi alitoka ndani ya moto akiwa anawaka lakini akitembea bila wasiwasi… Baadae moto huo unazima, na mwanajeshi anaoekana hana makovu yoyote ya moto licha ya nguo zake zote kuungua.

“Hatari sana hii.” Aliongea waziri mkuu huku katabasamu.

“Hiyo ndio C.O.D.EX improved chemical.” Daktari alijigamba kwa mbwembwe.

“Kwa hiyo ni ile C.O.D.EX ya wale wanajeshi wengine?” Aliuliza bwana yule aliyeongozana na Waziri Mkuu.

“Ndio Waziri wangu wa Ulinzi.” Kwa tabasamu pana alijibu Dokta Ice.

“C.O.D.EX ni nini?” Akauliza Waziri Mkuu.

“Ni kifupisho cha maneno haya, CINDREX OLTIVIASO DECA ENDROLINE X. Ni chemikali zilizobuniwa miaka kumi nyuma na walitengenezwa wanajeshi kadhaa ambao walisumbua sana CIA na FBI. Baada ya kujua kemikali hizi, CIA waliweza kuharibu maabara yote ya kutengenezea wanajeshi hawa. Sasa hivi ndio tumepewa kibali cha kutengeneza silaha kupitia kemikali hizi.” Alijibu Daktari.

“Kuna tofauti gani kati ya wanajeshi hawa na wale wa miaka kumi iliyopita? Hawawezi kuleta madhara kama yale?” Aliuliza Waziri wa Ulinzi.

“Hapana. Hawawezi fanya hivyo. Tatizo kubwa la wale waliyopita, hawakuwatoa kumbukumbu wale waliowatengeneza, hivyo ilikuwa rahisi kwa zile kemikali kurudisha kumbukumbu baada ya kuanza kuisha. Hilo likaleta tatizo kwa baadhi ya wanajeshi ambao kumbukumbu ziliwarudia.” Akajibiwa.

“Okay. Kwa hiyo hawa hawana kumbukumbu?” Akauliza tena Waziri wa Ulinzi.

“Ndio. Kabla hatujawaingizia C.O.D.EX, tulihakikisha kwanza tunafuta kumbukumbu zao zote za maisha yaliyopita. Tuna uhakika tumefanikiwa katika hilo.” Alijibiwa na daktari.

Waziri wa Ulinzi akaangaliana na Waziri Mkuu kisha kwa ishara fulani walipeana kuonesha kuwa wamekubaliana na ile kazi ya C.O.D.EX.

“Sawa Dokta. Ila kwanza ni lazima tufanye majaribio na silaha zako.” Waziri wa Ulinzi aliongea na kumpa nafasi dokta naye aongeze jambo kama analo.

“Mmepanga wapi kufanya majaribio yenu?” Akauliza Dokta.

“Iraq na Iran.” Akajibiwa na dokta akaonesha kukubaliana na majibu hayo.

“Ila kuna jambo moja ambalo tumelipandikiza kwenye miili yao.” Akakumbusha daktari.

“Lipi hilo?” Akaulizwa.

“Hawana huruma hata kidogo. Kitendo cha huruma kwao kimepita kushoto. Kwa hiyo hayo majaribio, tujaribu kuyafanya mbali na raia.” Akaongea dokta.

“Hamna shida.” Akajibiwa na Waziri wa Ulinzi kwa kifupi.

Baada ya maongezi hayo marefu, wale viongozi wa serikali ya Marekani, walianza kuondoka eneo lile huku nyuma wakifuatiwa na walinzi wao muhimu kabisa.

****

BAADA YA WIKI MBILI.

Vyombo vya habari duniani vilikuwa vinatangaza kuhusu Iran kuvamiwa na mitambo yake ya nyuklia kuharibiwa vibaya na wakati huo mateka wa Iraq walisemekana kuwa wamekombolewa na wanajeshi wa jeshi la Marekani lakini hawatambuliki ni wapi walipo. Habari zilikuwa zimezagaa na kuzusha maswali kadhaa kwenye vichwa vya habari na watu wote kwa ujumla.

Vyombo vya habari viliuliza kuhusu wanajeshi hao na Waziri Wa Ulinzi alithibitisha uwepo wa wanajeshi hao na kuahidi kuwa, Marekani itakuwa na nguvu kubwa kuliko nchi yoyote duniani.

Wakati hayo yanaendelea, daktari mkuu wa ile maabara alikuwa anatazama na kusikiliza vyombo vya habari kila kukicha. Jambo ambalo hakuwaambia wale viongozi, ni uwezo wa wale wanajeshi kuchukua matukio yote kwenye chipu iliyokuwa imepandikizwa vichwani mwao kwa ajili ya kuwatuma wafanye mambo fulani.

“Wajinga sana hawa. Niliwaambia wasifanye majaribio kwenye makazi ya raia wema. Matokeo yake wamewaua mateka wote. Washenzi sana. Natakiwa kufanya jambo moja muhimu sana kabla sijaondoka hapa.” Alijiwazia Dokta Ice na hapohapo akaifata kompyuta yake iliyokuwa katika ofisi ndogo kwenye chumba chake na kuanza kusoma mambo kadhaa kwenye mafaili yaliyokuwepo kwenye kompyuta hiyo.

Kesho yake ilikuwa Asubuhi ya Jumapili yenye bashasha nyingi sana. Dokta akiwa anajua wazi kabisa kuwa siku hiyo ni ya mapumziko kwake, alitoka ndani ya nyumba yake akiwa kakamata mkoba wenye makaratasi kadhaa, kisha akapanda gari lake la gharama na kuelekea zilipo ofisi zao.

Huko aliamrisha baadhi ya wafanyakazi waondoke kwa sababu alikuwa na kazi nyeti ya kufanya bila wao kuijua. Alipofanikiwa kuwatoa, akafungua jokofu moja ambalo lilikuwa tofauti na yale mengine. Lenyewe lilikuwa halioneshi na lilifanana na lile la kuhifadhia maiti. Alipolifungua, akaonekana muafrika mmoja aliyekuwa kafumba macho yake kama marehemu na mvuke ukimtoka kwa sababu ya kuganda kwa mwili wake.

Code X
 
Mwanzo kama sikuielewa lkn sasa nimeielewa barabaraa poti asante sana wanyumbani
 
118.
“Kwa nini mimi lakini?” Akauliza Idris.

“Ukifika sehemu yoyote, fungua kompyuta hii, kisha tazama mafaili pamoja na video kadhaa ambazo zipo humo. Sina muda wa kukuhadithi kila kitu kwa sasa. Muda si mrefu C.O.D.EX wanatuvamia hapa.” Alijibu Dokta Ice na kulazimika kuanza kumzoa zoa Idris ili waondoke mle ndani.

Bomu lililolipuka nyumbani kwa Dokta Ice, ni bomu ambalo lilitegwa na dokta huyu mwenyewe. Ni bomu la kawaida ambalo halikuwadhuru wale wanajeshi. Hivyo baada ya kuokolewa, wale wanajeshi walipewa mavazi mapya tayari kwa kurudi kuwasaka Ice na Iris.

****

Saa mbili usiku, gari moja la kifahari lilisimama kwenye jiji la maraha nchini Marekani. Jiji la Las Vegas. Lakini kwa bahati mbaya gari hilo halikuwa limekuja kushangaa raha za Las Vegas na badala yake, alishuka Idris na Ice na kisha kuchukua treni ya umeme ambayo iliwapeleka hadi uwanja wa ndege. Huko Idris aliagana na Dokta Ice ambaye baada ya kuhakikisha kuwa mwanajeshi wake amekwishakwea ndege, akarudi haraka kwenye treni inayorudi mjini ambapo alliacha gari lake.

Idris akiwa katulia ndani ya ndege kabla haijaanza kuondoka, alichungulia nje kwa mara ya mwisho kabla ya kuanza safari ya kuiaga Marekani.

“America, Land of Opportunities. Godbless America. (Amerika, nchi/ardhi ya bahati/nafasi. MUNGU ibariki Amerika)” Idris aliongea maneno hayo akimaanisha kuwa Marekani ni nchi ya bahati au nafasi. Yaani alimaanisha kuwa, yeyote atayeishi Marekani basi anauwezo mkubwa wa kutoka kimaisha. Kifupi, nchi ya Marekani kama ukijishughulisha, basi unauhakika wa kuishi kama mfalme. Hamna ambaye anajishughulisha Marekani kisha awe fukara. Idris alilitambua hilo.

Baada ya nusu saa, ndege ilikuwa angani na Idris aliamua kutoa kompyuta mpakato aliyokabidhiwa na Dokta Ice. Akaifungua na kisha alianza kusoma mafaili kadhaa yaliyomo humo lakini kwa bahati mbaya, hakuwa akielewa ni nini hasa yalikuwa yanamaanisha. Akaamua kufungua video zilizomo humo, huko ndipo alipotulia na kuanza kuumia moyo wake.

“Happy Birthday to you… Happy Birthday To You…. Happy Birthday Dear Best, Happy Birthday To You.” Wimbo huo ulikuwa unaimbwa na watu kadhaa huku mwanaume mmoja mwenye nywele nyingi akiwa kakamata keki akielekea ilipokuwa meza kubwa.

Wakati anaelekea huko kwenye meza, mchukua video ile alianza kuwachukua watu waliokuwa wamehudhuria kwenye sherehe ile ya siku ya kuzaliwa.

Mama mmoja mwenye asili ya weusi, alionekana mwenye furaha sana na mchukua video alikuwa anamchukua kwa makini zaidi kwani mama yule alienda mahali hadi alipokuwa amekaa mtahiniwa wa sherehe ile. Hapo Idris akashtuka baada ya kumuona mtoto aliyekuwa anasheherekea miaka yake mitano ya kuzaliwa.

Alikuwa ni mtoto mweusi kama mama yake. Na kilichomfanya ashtuke ni ule muonekano ambao ulionekana kama yeye. Japo yeye alikuwa mkubwa kulikoni yule kwenye video, lakini hakutilia shaka kabisa kuwa yule kafanana naye. Akabonyeza stop na video ile ikasimama.

“Huyu ni mimi, lakini anaitwa Best, na mimi ni Idris.” Akajiwazi na kwa haraka akafungua mafaili ambayo hapo mwanzo aliyafunga kwa sababu hakuyaelewa.

“Best Boucher. Kazaliwa tarehe….” Akaanza kusoma yale mafaili kwa makini zaidi.

Baba yake Dokta Boucher, alikutwa kajinyonga ndani ya chumba chake baada ya kumuua mkewe. Mtoto wao alikutwa kajificha kwenye zizi la farasi na jukumu la kulelewa alipewa Dokta Ice ambaye alikuwa rafiki mkubwa wa Dr. Boucher.

Best alipotimiza umri wa miaka kumi na saba. Alipotea katika mazingira ya kutatanisha na baadaye taarifa zilitoka kuwa amekutwa kwenye fukwe za Miami amefariki.

Ni kifo cha utata sana kwa sababu Dokta Ice hakuwa tayari kufanya mazishi hayo wala kutaka maiti ionekane. Na yeyote aliyethubutu kuhoji kuhusu mwili wa Best, alipewa kilema cha maisha na watu wasiojulikana.

Katika vifo vya Dokta Bouncher na Mkewe ambaye alikuwa ni Mwanasheria, iligundulika kuwa mke wa Bouncher hakuuawa na mumewe na wala mumewe hakujinyonga. Mwili ulivyopimwa, kulikutwa na sumu kali sana ambayo leo hii wanaiita C.O.D.EX. Kemikali hii kwa maiti huwafanya wazinduke na kuwa watu wenye nguvu sana, lakini kwa wale wazima huwapotezea uhai wao haraka sana kwa kuwatoa damu kwenye kila tundu linalopatikana kwenye miili yao.

Mtu aliyefanya uchunguzi huo alikutwa maiti ndani ya ofisi yake na taarifa hizi zilizuka miaka mitano mbele kwa mtoto wa yule aliyefanya uchunguzi kuziweka hadharani. Naye hakuchukua muda, akapigwa risasi siku moja wakati anatoka mahakamani kusimamia kesi ya mtuhumiwa fulani huko Marekani.

Vifo vya familia ya Boucher vilijaa utata pekee na kila aliyejaribu kuvifuatilia alikutwa anakilema cha maisha au mfu. Hata mawakili wakubwa duniani, walikwishakataa kuzungumzia kesi ya Bouncher.

Idris akaendelea kuyasoma maelezo muhimu ndani ya mafaili yale ya kwenye kompyuta. Aliporidhika, akarudi kwenye video zilizopo. Akafungua video nyingine iliyokuwepo mbele ya kioo cha kompyuta.

“Dokta Ice. Tunakaribia kupotezwa. Mimi na familia yangu tunapotezwa muda si mrefu. Naomba umtunze mwana wetu. Nakuomba Dokta. Ukumbuke pia ile formula mpya C.O.D.EX.” Video hiyo iliongea hayo na picha ya Boucher ilionekana akiwa na wasiwasi mwingi sana, kwani aliangalia huku na huko wakati anayaongea hayo. “Nimemficha mwanangu kwenye zizi la farasi, utamkuta huko. Mlee vema kama…..” Hakumaliza maneno yake Dokta Bouncher, mlango wa nyumba yake ukafunguliwa kwa kishindo cha bunduki.

Kwa haraka akakimbilia kwenye kabati moja lililomo mle ndani na kufungua kisha akatoa gobole, lakini alikuwa amekwisha chelewa sana. Mwanajeshi mmoja mkubwa wa mwili alikuwa nyuma yake, na Bouncher alipogeuka tu! Akakuta na kabali nzito na kunyanyuliwa juu huku akiliachia gobole lake na kuanza kutapatapa.

Hayo yote yaliendelea kuonekana kwenye video ambayo ilikuwa inacheza kwenye kompyuta mpakato ya Idris.





“Dokta Ice. Tunakaribia kupotezwa. Mimi na familia yangu tunapotezwa muda si mrefu. Naomba umtunze mwana wetu. Nakuomba Dokta. Ukumbuke pia ile formula mpya C.O.D.EX.” Video hiyo iliongea hayo na picha ya Boucher ilionekana akiwa na wasiwasi mwingi sana, kwani aliangalia huku na huko wakati anayaongea hayo. “Nimemficha mwanangu kwenye zizi la farasi, utamkuta huko. Mlee vema kama…..” Hakumaliza maneno yake Dokta Bouncher, mlango wa nyumba yake ukafunguliwa kwa kishindo cha bunduki.

Kwa haraka akakimbilia kwenye kabati moja lililomo mle ndani na kufungua kisha akatoa gobole, lakini alikuwa amekisha chelewa sana. Mwanajeshi mmoja mkubwa wa mwili alikuwa nyuma yake, na Bouncher alipogeuka tu! Akakuta na kabali nzito na kunyanyuliwa juu huku akiliachia gobole lake na kuanza kutapatapa.

Hayo yote yaliendelea kuonekana kwenye video ambayo ilikuwa inacheza kwenye kompyuta mpakato ya Idris.

ENJOY.

Dokta Bouncher aliendelea kutapatapa pale alipokuwepo hadi akatulia kabisa ndipo lile bwana lilipomuachia. Baada ya hapo, likaanza kuangaza huku na huko na ndipo macho yake yakaelekea kwenye kompyuta ambayo bado ilikuwa inaendelea kuchukua tukio zima lililokuwa linaendelea ndani ya nyumba ya Dokta Bouncher.
 
119.
Mwanajeshi yule alianza kwenda taratibu kwenye ile kompyuta na kisha akaanza kuikagua taratibu huku bado inaendelea kunakili kila kitu. Wakati anazidi kukagua, mara ukasikika mlio mkali wa bunduki na hapohapo yule mwanajeshi aliinama chini kwa maumivu na kitendo hicho cha kuinama, kikatoa nafasi kwa yule aliyefanya tendo lile kuonekana. Alikuwa Mama wa Best, Mke wa Dokta Bouncher akiwa kakamata gobole ambalo mumewe aliligwaya baada ya kupokea kabali nzito ya Mwanajeshi asiye na huruma. Mama yule akafyatua risasi nyingine na mwanajeshi yule alisikika akilia kwa uchungu zaidi.

“Mbwa wewe.” Mama yule aliongea kwa kithilani baada ya kufika chini alipolala yule mwanajeshi na maneno hayo yakafuata na mlio mkali mwingine wa bunduki. Kimya kikatanda.

Mama Best, mke wa Dokta Bouncher. Alijulikana kama Jesabel Amour. Ni raia wa Brazil. Kasomea sheria Marekani na baada ya hapo akaolewa na Dokta Ice ambaye alikutana na mwanamama huyu kwenye harakati za kuwakomboa waathirika wa tetemeko huko Haiti. Mmoja alikuwa Daktari wa Marekani, na mwingine alikuwa ni Mwanasheria aliyekuwa mafunzoni (field). Mapenzi yakawaka kuanzia hapo na siku hiyo, Jesabel, anapukutisha mwanajeshi aliyemuua mumewe.

Baada ya milipuko kadhaa na sauti ya mwanajeshi kupotea kwenye chumba kile, Mama Best, au Jesabel Amour. Anachukua kompyuta ile haraka na ikiwa vilevile bado inarekodi, anaiweka juu ya pambo moja ambalo lipo chumbani na lilikuwa limekamata taa zipatazo nne. Pambo hilo lilikuwa katikati ya dari, na alipoiweka kompyuta hiyo, ikakaa vizuri bila shida na kwa bahati nzuri, iliweza kumuelekea yule mwanajeshi ambaye alikuwa kapukutishwa na Jesabel. Alikuwa kafumuliwa kichwa vibaya sana na kifua chake kilikuwa kimelowana damu pekee. Ni wazi alikuwa kakiona cha moto toka kwa mwanamke jasiri wa Kibrazil.

Baada ya dakika kadhaa, sauti ya mwanamke ilisikika ikilia kwa nguvu nje ya chumba kile. Na baada ya muda kidogo, sauti hiyo ilisikika ndani ya chumba kilekile ambacho Dokta Bouncher na Mwanajeshi walikuwa maiti. Vishindo vya haraka vikasikika na mara watu wawili walionekana kuufuata mwili wa yule mwanajeshi na kuanza kuuchunguza.

Kwa hasira bwana mmoja alibwata na ghafla kwenye kitanda ambacho nacho kilikuwa kinaonekana kwenye ile kompyuta iliyokuwa inachukua tukio zima, Jesabel alirushwa na kudondokea hapo. Kisha yule bwana aliyebwata baada ya kuona mwanajeshi wake kauawa, akachomoa mkanda wa suruali kisha akaanza kumtandika mwanamke yule kwa hasira nyingi sana. Kilio kilikuwa kikubwa lakini hakukuwa na msaada wowote ule.

Damu zikawa zinamtoka mwanamama yule. Na yule bwana baada ya kuridhika na kipigo chake alichokitoa, alionekana akitoa ishara kule alipotekea kabla ya kwenda kumuona mwanajeshi wake.

Dakika moja mbele, yule bwana mwenye mkanda akatoka eneo lile, na hapohapo akatokea mwanajeshi mwingine mkubwa na huyu alikuwa anaasili ya weusi kwenye ngozi yake. Akasimama pembeni ya kitanda ambacho Jesabel alikuwa amelala. Yule mwanajeshi mweusi alijipekua nyuma ya mgongo na kisha akatoa panga moja refu kama yale wanayomiliki Yakuza (Kundi la Mafia la Japan). Mwanajeshi yule akiwa hana chembe ya huruma, alishusha panga lake kwenye shingo ya Jesabel na damu nyingi zikaruka na kuchafua mashuka ya kitanda chote. Mama yule alinyanyua miguu yake juu kabla hajaishusha na mwisho wake ukawa hivyo.

“Huyo Dokta mtoeni humu, kamtundikeni chumbani kwake.” Sauti ya yule bwana aliyemchapa Jesabel kwa mkanda, ilisikika na dakika hiyohiyo, mburuto ulisikika kabla ya yule mwanajeshi hajaja na kumchukua mwanajeshi wake na baadae kurudi tena na kuanza kusafisha damu za yule mwanajeshi Ili kupoteza ushahidi.

Video iliendelea kuonesha maiti ya Jesabel kwa dakika kama kumi. Na Idris aliendelea kuangalia sura ya mwanamke yule huku akiwa haamini kama kuna watu wakatili namna ile duniani.

Baada ya dakika hizo, ilisikika sauti ya mtu ikibishana na watu nje ya chumba hicho. Idris akashtuka na kuzidi kutega sikio lake.

“Nimesema sitaki mtu ndani ya chumba hichi. Nitafanya mlichoniambia lakini si kwa kupelekeshwa, hamtaki, na mimi niuweni tu.” Ilifoka sauti hiyo kwa lugha ya Kiingereza.

“Okay. Fanya unachoweza. Ila hakikisha hamna ushahidi.” Sauti ya bwana wa kuchapa kwa mkanda ikasikika.

Baada ya hapo, mtu akaingia kwenye chumba kile ambacho kilifanyika mauaji na sauti ya mlango kufungwa na baadae kusikika funguo nayo kufunga, vikasikika. Bado kompyuta iliendelea kuchukua matukio yote. Alikuwa kavaa suti nyeusi, na alipofika pembeni ya kitanda, alisimama kwa muda akiwa kainama jambo ambalo lilifanya ile kompyuta isiweze kuona uso wake vema.

“Jesabel dada yangu. Samahani sana dada yangu. Najua ulinipenda kama kaka yako, lakini nimeshindwa kukutetea dada yangu. Umeondoka na kaka yangu kipenzi. Hakika sitawasahau maishani mwangu. Ipo siku watakuja kulipa haya yote.” Maneno hayo aliyatoa yule bwana mwenye suti na yalikuwa yanasikika vema kwenye masikio ya Idris.

Sauti ile aliijua vema na alitamani sana mtu yule ainue uso wake aweze kumjua.

Bwana yule akafungua mkoba aliokuja nao na kutoa vitu fulani na kuvivaa mikononi. Kisha akachukua kitambaa na kuanza kufuta maeneo yote yaliyokuwa wazi. Kila kitambaa kilipokuwa kinalowa damu, alitumbukia kwenye kikopo kimoja ambacho kilikuwa na kimiminika kilichokuwa kinamwaga povu kila kitambaa kikiwekwa humo. Mwili wa Jesabel ukawa safi baadhi ya maeneo ambayo yalikuwa wazi kama miguuni, mapajani, mikononi na usoni.

Baada ya zoezi hilo, yule bwana alitoa vitu vingine kwenye mkoba na kuanza kuvipaka kwenye mwili wa Jesabel kwa uangalifu zaidi.

“Nadhani hizo ni alama za Bouncher. Na ndio maana yasemekana yeye ndiye aliyemuua mkewe. Lakini yawezekana hiyo aliyomfutia ni kemikali ya C.O.D.EX na ndio maana ukazuka utata mwingine baadaye.” Aliongea peke yake Idris huku akiwa na shahuku ya kutaka kujua ni nini kiliendelea.

Baada ya kupakapaka sehemu za mwili ambazo alizifuta, yule bwana aliyetumwa kufanya hivyo, akatoa kichupa kingine na kukiminya. Damu zikaruka maeneo yale aliyoyafuta. Akameza funda kubwa kukubaliana na kile alichokifanya.

Akasimama pembeni kuangalia kazi yake. Akaona ipo sawa. Akainama kuonesha kutoa heshima yake ya mwisho. Na baada ya hapo akageuka na kuanza kuangaza huku na huko na kwa bahati mbaya au nzuri, uso wake ukatizama juu ya pambo ambalo ile kompyuta iliwekwa na Jesabel.

“Dokta Ice?” Akajiuliza kwa mshangao mkubwa Idris Iris.

****
 
120.
Baada ya kutoka Jijini Vegas kumsindikiza Idris, Dokta Ice anaamua kurudi kwenye nyumba yake ya siri iliyopo Los Angeles. Alichukua siku moja tokea usiku aliomsindikiza Idris hadi usiku uliofuata, ndipo anafika Los Angeles kwa kutumia gari lake lililokuwa linauwezo mkubwa wa kusafiri kwa umbali mrefu bila kupoteza ubora wake.

Nyumba aliyokwenda, ni nyumba ambayo alikuwa anapenda sana kwenda kuvinjari na mkewe siku za mapumziko na sherehe mbalimbali. Aliweka mlinzi mmoja ambaye aliishi kwenye nyumba mojawapo ya nje lakini akiwa na mitambo kadhaa ya kuangalia watu wanaokuja na kutoka.

Dr. Ice anakwenda katika nyumba hiyo na kumkuta mlinzi wake akiwa katika uangalizi mzuri kabisa. Wanasalimiana na Dokta anaingia ndani kwake na kuanza kufanya uchunguzi mdogo hasa wa usafi. Anaona pako sawa, anawasha runinga iliyopo humo kabla hajachukua jukumu la kwenda kuweka mwili wake safi na kisha kurudi sebuleni ambapo anapata wasaha mwanana wa kupata chakula cha usiku.

Saa nane usiku akiwa kalala, anasikia kurupushani nje ya nyumba yake jambo linalomfanya ainuke na kwenda kuchungulia dirishani upande ule ambapo anasikia kurupushani hizo. Hapo anashuhudia mlinzi wake akivutiwa gizani akiwa kalegea na baadae wanajeshi wenye mavazi meusi na pua na midomo yao ikiwa imezibwa na maski, wanaonekana na mitutu yao ya bunduki ikiwa mbele.

Dokta Ice anawahi kwenye kabati lake na kuchukua maski ambayo kwa pembeni kulikuwa na vichupa viidogo vya gesi ya oksijeni. Anavaa haraka kabla hajasikia kioo cha dirisha lake kikivunjwa na bomu la machozi kudondokea ndani. Moshi wa hatari unaanza kutapakaa mle ndani.

Dokta Ice anaenda chumba kingine na kufungua kabati moja kubwa la nguo. Huko anapekua hadi nyuma ya nguo zilizopo na kushika kitasa ambacho anakiminya na kufunguka. Anaingiza kichwa chake na baada ya dakika kadhaa, anatoka na bunduki moja kubwa na boksi la risasi ambazo zilikuwa na kimiminika ndani yake.

“Pumbavu hawa, nimewaunda mwenyewe, hawanizuii kuwafanya lolote. Ngoja niwaoneshe.” Akaongea kwa hamasa Dokta Ice huku akiijaza bunduki yake zile risasi zenye kimiminika cha rangi ya kijani.

Baada ya tendo hilo, Dokta Ice, anaelekea sebuleni huku bado akiwa na maski yake na moshi ukizidi kutumwa toka kwa wale wanajeshi waliopo nje.

Anafungua mlango fulani ambao upo kwenye ‘silling board’ ya sebuleni, mlango ule unafunguka na ngazi moja inashuka ambayo Dokta Ice anaipanda na kuingia juu ya paa la nyumba yake. Anaelekea sehemu moja ambayo ilikuwa na dirisha dogo kiasi lakini lenye uwezo wa kuona eneo kubwa lililopo pale nje. Anashuhudia wale mabwana wakiwa wamejipanga kwa mstari na bunduki zao za mabomu ya machozi.

Anaikoki bunduki yake na kuipitisha kwenye dirisha lile dogo. Anachukua shabaha kwa kumlenga mmoja wa wanajeshi wale kwenye jicho. Anaachia risasi na inamkuta yule bwana kwenye jicho kama alivyodhamiria. Mwanajeshi anadondoka chini na kuanza kulia huku taratibu ngozi yake ikianza kuchubuka na nyama kuanza kumwagika ardhini. Ilikuwa ni picha ya kutisha pale wanajeshi wengine walipokuwa hawaamini kama mwenzao anakufa. Sekunde pekee zilitosha kumgeuza yule bwana majivu kwani kemikali za risasi zile zilikuwa harari sana.

“Nadhani mmeshuhudia kifo cha mwenzenu, nanyi mtakufa vivyo hivyo.” Dokta Ice aliongea na kuachia risasi nyingine ambayo ilimbabatiza mwanajeshi mwingine pembeni ya kichwa chake.







Anaikoki bunduki yake na kuipitisha kwenye dirisha lile dogo. Anachukua shabaha kwa kumlenga mmoja wa wanajeshi wale kwenye jicho. Anaachia risasi na inamkuta yule bwana kwenye jicho kama alivyodhamiria. Mwanajeshi anadondoka chini na kuanza kulia huku taratibu ngozi yake ikianza kuchubuka na nyama kuanza kumwagika ardhini. Ilikuwa ni picha ya kutisha pale wanajeshi wengine walipokuwa hawaamini kama mwenzao anakufa. Sekunde pekee zilitosha kumgeuza yule bwana majivu kwani kemikali za risasi zile zilikuwa harari sana.

“Nadhani mmeshuhudia kifo cha mwenzenu, nanyi mtakufa vivyo hivyo.” Dokta Ice aliongea na kuachia risasi nyingine ambayo ilimbabatiza mwanajeshi mwingine pembeni ya kichwa chake.

ENJOY.

Naye aliweza kufa kwa kifo sawasawa na cha yule mwenzake. Mwanajeshi aliyebakia akawa hana la kufanya zaidi ya kuangalia kule risasi zinapotoka. Kwa macho yake ambayo yalikuwa na kitu kama darubini, yalieweza kumuona Dokta Ice akibonyeza kifyatulio cha bunduki yake. Naye bila kupoteza muda, risasi ya kichwa pia iliingia kwenye paji lake la uso. Kifo kibaya kikashirikishwa kwenye maisha yake.

Kosa kubwa ambalo Dokta Ice alilifanya, ni kumuachia yule mwanajeshi amuangalie kwani baada ya kuonekana kwenye macho ya yule bwana, taarifa zilifika haraka makao makuu ya C.O.D.EX Soldiers na hapohapo kupitia satelaiti, walituma taarifa hizo kwa wale waliowaleta wale wanajeshi. Ndipo mwanajeshi mwingine aliweza kutuma mionzi mikali ya bunduki yake na kusambaratisha nyumba ya Dokta Ice. Wakati mwanajeshi yule amesimama tayari kwa kutuma mionzi yake ambayo ilikuwa ni hatari sana. Ni mionzi iliyotengezwa kwa madini ambayo yanapatikana chini ya bahari. Dokta Ice aliweza kumuona na alijua tayari yupo kwenye hatari. Hali hiyo ikimfanya Ice kutoka kule juu na kujitupa hadi chini na kulala ili mlipuko ule uliokusanyika na moto mkubwa usiweze kumfikia.

Baada ya kimya kidogo. Dokta Ice aliinua kichwa chake na kutaka kusimama lakini alishindwa kusimama kwa sababu ya kuhisi maumivu makali kwenye miguu yake. Tokea kule juu aliporuka hadi chini, ulikuwa umbali mrefu sana japo yeye mwenyewe aliona kawaida sana kwa sababu alikuwa anajitahidi kuokoa roho yake.

“Upo chini ya ulinzi.” Mwanajeshi mmoja aliongea huku kamuelekezea Dokta Ice bastola yake.

“Usimuue. Tunamuhitaji.” Sauti ilisikika kwenye masikio ya yule mwanajeshi na bila mchecheto, akarudisha bastola yake kiunoni na kumnyanyua Dokta Ice kwa nguvu na kuanza kwenda naye kwenye gari ambalo sasa lilibakiwa na dereva tu.

Akamsukumia Dokta Ice nyuma ya gari lile na kufunga mlango vema ili mtuhumiwa wao asitoroke wala kuleta shida njiani. Safari ya kuanza kurudi New York ikaanza.

****

“Dokta Ice, karibu tena New York.” Sauti ilisikika na bwana mmoja mwenye suti matata sana alioongea baada ya Dokta Ice kufumbua macho yake na kujikuta yupo kwenye kiti ndani ya ile maabara aliyokuwa anafanyia kazi.

“We’ ni mjinga Uzo. Ni mjinga sana. Unadhani unaweza kusimamisha nilichokiwaza?” Dokta Ice aliongea na wakati huo mtu aliyemuita Uzo, alikuwa anakagua jeshi lake lililokuwa kwenye jokofu. Alikuwa kakamata Ipad yake ya kufanyia kazi.

“Si hivyo Dokta Ice. Na wala siwezi kukukwamisha ulichoanza, ila….” Uzo aliongea kwa kejeli huku anaenda pale alipokuwa amekalishwa Dokta Ice. “Wapo ambao watafanya hivyo.” Akaongezea huku uso wake akiusogeza karibu kabisa na Dokta Ice.

“Unajidanganya. Mimi ndiye alpha na omega kwenye kutengeneza hiyo kemikali na kuifanya iwe bora zaidi. Nilioshirikiana nao, wote mliwaua. Bado mimi ni jiwe la pembeni.” Akaongea pia Dokta Ice.

“Una uhakika Ice?” Akauliza Uzo huku ametabasamu.

“Unauliza maembe Tanzania mwezi wa kumi mbili?” Naye akajibu kwa kejeli.

“Inaonekana unapajua sana Tanzania. Hamna kitu wale, tukiamua kuiangamiza ni dakika tano tu. Ila sipo huko, nilikuuliza kama unauhakika na kauli yako. Tatizo ni kwamba hujui unalolizungumza. Hamna alpha wala omega duniani. Labda Shetani na MUNGU. Napo vita yao ni lazima mmoja akubali kupigwa. Je ni nani? Shetani au MUNGU. Na wewe upo upande gani hadi sasa? Kwa MUNGU ama Shetani?” Akatulia kidogo huku bado macho ya Dokta Ice yakimtazama kwa uchu. “Hata hivyo sipo huko, nataka nikutambulishe kwa mrithi wako.” Baada ya maneno hayo, akaoneshea mkono kwenye mlango wa kuingilia ambao ulikuwa nyuma ya Dokta Ice. Nao mlango ukafunguliwa jambo lililofanya Dokta Ice kugeuka kuona anayeletwa.
 
Back
Top Bottom