Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #121
110.
Upande wa Agent Darling na Jeff mambo pia yalikuwa mazuri, walimaliza kambi zote jangwani pamoja na ndege zilizotumwa kwenda kupambana nao. Walipohakikisha hawafauatiliwi tena, walirudi kambini kwao, "hongereni sana" Jeff aliongea kuwapongeza majenedari wake. "huu ndio kwanza mwanzo kwa hiyo tusudhani tumeshinda" aliendelea kuongea na alipomaliza kila mtu alitawanyika na kuelekea sehemu yake ya kupumzika.
"inavyoonekana hutaki kutoa ushirikiano kwa njia ya amani" Alex aliongea baada yule kijana kuleta ubishi. "basi hakuna shida" alitoa sindao ndogo yenye dawa kiasi na kumchoma, "hii ni sindano ya ganzi" aliongea baada kumchoma na kusubiri dakika kadhaa. Wakati huo mpaka raisi alikuwa akishuhudia mateso anayotoa Alex. Alifungua pochi maalum na kutoa sindano ndefu jma sentimita tani na kuanza kumchom chini ya kucha kwenye vidole vya mkono. Aliingiza urefu wote hadi mwisho mpaka alipohakikisha amevichoma vidle vyote kumi.
"saa hivi huhisi kitu lakini niamimi hiyo ganzi ikiisha utajuta kwanini hukutoa ushrikiano mapema" Alex aliongea na kukaa tena kwenye kiti akisuiri ganzi iishe. Baada kama dakika sita jamaa alianza kukunja uso, na kwa mbali macho yake yalianza kurowa maji. "muda umefika, sasa nambie kambi yenu kuu iko wapi?" Alex aliongea, lakin bado jamaa alikuwa mbishi. Alex alianza kuchomoa sindano ya kidole kimoja na kuirudisha kama vile anachokonoa kitu.
Jamaa alipiga sana kelele, "yaani nimekwambia hata ikibidi nikukaushe damu niupate ukweli basi nitafabya hivo kwa maana huu ni mwanzo tu" Alex aliongea kwa hasira huku akiedelea kufanya kazi yake. "nitasema tafadhali usifanye tena hivo" maumivu yalipozidi jamaa aliamua kutoa ushirikiano, "mambo si hayo sasa, ungekubali mapema tusingefika hapa" Alex aliongea na kukaa kwenye kiti. Basi jamaa hakuwa na jinsi aliongea kila kitu bila kuficha hata kidogo, "tafadhali naomba unichome tena ganzi ili nipunguze maumivu" aliomba baada kumaliza kuongea.
"usijali yatakwisha sasa hivi" alijibiwa lakini si na Alex bali ilikuwa nisauti ya raisi, alisogea mpaka alipo Alex na kuchomoa bastola ndogo. Alimuekea kichwani na kumpasua kichwa, "tunajitahidi kuleta amani nyinyi mnaleta upumbavu, eti mapinduzi" aliongea raisi baada kumchapa risasi. Wote walipigwa na bumbuwazi na wasiamini kitendo alichokifanya raisi, "muheshimiwa bado kitu kimoja" Alex aliongea na kuunganisha computer yake na rubinga kubwa iliokuwepo hapo ukumbini.
"Jeff mambo yameendaje" Alex aliongea baada kioo cha runinga kuonesha picha ya Jeff akiwa na majemedari wake. "umekwenda vizuri sana na hakuna hata kambi moja iliosalia jangwani" alijibu, "safi sana, sasa tunaelekea hatua ya mwisho. Zimebaki kambi kadhaa pamoja na kambi yao kubwa" Alex alimueleza Jeff kila kitu na wakakubaliana wakutane sehemu karibu na kambi hizo ambazo ziko porini. Baada ya maongezi ya dakika kadhaa alimpisha raisi nae aongea kijana Jeff ambae cheo chake ni zaidi ya kamanda..
**************************************************
Katika ndege mia zilizotoka ilirudi moja tu, ilipotua tu alishuka rubani wa ndege hiyo na kukimbilia ofisini kwa general David. "mkuu tupo matatani" aliongea baada kuingia katika ofiso hiyo, "kivipi" aliuliza kamanda Willy ambae alikuwa akiongea na general wakati rubani huyo ameigia ofisini. "ndege zote zimeripuliwa, mimi nimeokoka ki bahati bahati tu. Pia sijawahi kuona ndege zenye uwezo kama tulizokutana nazo huko, na mbaya zaidi kambia zetu za jangwani na baharini zimeripuliwa zote na sidhani kama kuna mtu aliepona. Na kama wapo basi sijui hata kama mia wanafika" alieleza kijana huyo.
"hii kasheshe nyingine" kamanda Willy aliongea huku akitikisa kichwa, "hizi ni alama za majanga" aliongea General David. "master mind wa mchezo huu ni Alex, na ili kujihakikishia ushindi lazima tumuue" aliendelea kuongea. "kamanda Willy tuma ujumbe kwa wakuu wote tukutane leo hii kabla jua halijazama", kamanda Willy aliinuka na kuondoka. "hivi kwanini ulizaliwa we mwanaharamu Alex, ah lakini kosa ni langu kudhani utanifaa" alijisemea mwenyewe general
"majemedari wote tusikilizane, leo hii ndio itaamua hatma ya nchi yetu. Tuwaonyeshe wale wanaidhani wanaweza kuchwza na amani yetu. Vita ya leo ni ua ama uawa lakini mpaka kieleweke" hayo yalikuwa ni maneno General Griffin kwa vijana wake. "tumekusoma mkuu" walijibu kwa pamoja, "Alex utaendelea na kikosi hicho kidogo, na kazi yako ni kutufngula njia tu. Mimi nitakuja na kikosi kikubwa halafu tutaongana katika mapambano" General aliongea na Alex alitikisa kichwa kukubali. "mimi je" ilikuwa sauti ya raisi, "mkuu usalama wako ni muhimu" alijibu General Griffin.
"Muheshimwa raisi tutahitaji msaada wako" Alex aliongea na kumsogelea kisha akamnong'oneza kitu sikioni. Raisi alitabasamu na kuashiria amemuelewa, "basi hakuna shida wacha mimi niondoke niwaache muendelee na majukumu mengine" Raisi aliongea na kusimama kisha akaondoka. Waliendelea kupanda mipango yao kwa makini sana, walifanya hivo kuhakikisha hatoki mtu hata mmoja kati ya waasi.
Upande wa Agent Darling na Jeff mambo pia yalikuwa mazuri, walimaliza kambi zote jangwani pamoja na ndege zilizotumwa kwenda kupambana nao. Walipohakikisha hawafauatiliwi tena, walirudi kambini kwao, "hongereni sana" Jeff aliongea kuwapongeza majenedari wake. "huu ndio kwanza mwanzo kwa hiyo tusudhani tumeshinda" aliendelea kuongea na alipomaliza kila mtu alitawanyika na kuelekea sehemu yake ya kupumzika.
"inavyoonekana hutaki kutoa ushirikiano kwa njia ya amani" Alex aliongea baada yule kijana kuleta ubishi. "basi hakuna shida" alitoa sindao ndogo yenye dawa kiasi na kumchoma, "hii ni sindano ya ganzi" aliongea baada kumchoma na kusubiri dakika kadhaa. Wakati huo mpaka raisi alikuwa akishuhudia mateso anayotoa Alex. Alifungua pochi maalum na kutoa sindano ndefu jma sentimita tani na kuanza kumchom chini ya kucha kwenye vidole vya mkono. Aliingiza urefu wote hadi mwisho mpaka alipohakikisha amevichoma vidle vyote kumi.
"saa hivi huhisi kitu lakini niamimi hiyo ganzi ikiisha utajuta kwanini hukutoa ushrikiano mapema" Alex aliongea na kukaa tena kwenye kiti akisuiri ganzi iishe. Baada kama dakika sita jamaa alianza kukunja uso, na kwa mbali macho yake yalianza kurowa maji. "muda umefika, sasa nambie kambi yenu kuu iko wapi?" Alex aliongea, lakin bado jamaa alikuwa mbishi. Alex alianza kuchomoa sindano ya kidole kimoja na kuirudisha kama vile anachokonoa kitu.
Jamaa alipiga sana kelele, "yaani nimekwambia hata ikibidi nikukaushe damu niupate ukweli basi nitafabya hivo kwa maana huu ni mwanzo tu" Alex aliongea kwa hasira huku akiedelea kufanya kazi yake. "nitasema tafadhali usifanye tena hivo" maumivu yalipozidi jamaa aliamua kutoa ushirikiano, "mambo si hayo sasa, ungekubali mapema tusingefika hapa" Alex aliongea na kukaa kwenye kiti. Basi jamaa hakuwa na jinsi aliongea kila kitu bila kuficha hata kidogo, "tafadhali naomba unichome tena ganzi ili nipunguze maumivu" aliomba baada kumaliza kuongea.
"usijali yatakwisha sasa hivi" alijibiwa lakini si na Alex bali ilikuwa nisauti ya raisi, alisogea mpaka alipo Alex na kuchomoa bastola ndogo. Alimuekea kichwani na kumpasua kichwa, "tunajitahidi kuleta amani nyinyi mnaleta upumbavu, eti mapinduzi" aliongea raisi baada kumchapa risasi. Wote walipigwa na bumbuwazi na wasiamini kitendo alichokifanya raisi, "muheshimiwa bado kitu kimoja" Alex aliongea na kuunganisha computer yake na rubinga kubwa iliokuwepo hapo ukumbini.
"Jeff mambo yameendaje" Alex aliongea baada kioo cha runinga kuonesha picha ya Jeff akiwa na majemedari wake. "umekwenda vizuri sana na hakuna hata kambi moja iliosalia jangwani" alijibu, "safi sana, sasa tunaelekea hatua ya mwisho. Zimebaki kambi kadhaa pamoja na kambi yao kubwa" Alex alimueleza Jeff kila kitu na wakakubaliana wakutane sehemu karibu na kambi hizo ambazo ziko porini. Baada ya maongezi ya dakika kadhaa alimpisha raisi nae aongea kijana Jeff ambae cheo chake ni zaidi ya kamanda..
**************************************************
Katika ndege mia zilizotoka ilirudi moja tu, ilipotua tu alishuka rubani wa ndege hiyo na kukimbilia ofisini kwa general David. "mkuu tupo matatani" aliongea baada kuingia katika ofiso hiyo, "kivipi" aliuliza kamanda Willy ambae alikuwa akiongea na general wakati rubani huyo ameigia ofisini. "ndege zote zimeripuliwa, mimi nimeokoka ki bahati bahati tu. Pia sijawahi kuona ndege zenye uwezo kama tulizokutana nazo huko, na mbaya zaidi kambia zetu za jangwani na baharini zimeripuliwa zote na sidhani kama kuna mtu aliepona. Na kama wapo basi sijui hata kama mia wanafika" alieleza kijana huyo.
"hii kasheshe nyingine" kamanda Willy aliongea huku akitikisa kichwa, "hizi ni alama za majanga" aliongea General David. "master mind wa mchezo huu ni Alex, na ili kujihakikishia ushindi lazima tumuue" aliendelea kuongea. "kamanda Willy tuma ujumbe kwa wakuu wote tukutane leo hii kabla jua halijazama", kamanda Willy aliinuka na kuondoka. "hivi kwanini ulizaliwa we mwanaharamu Alex, ah lakini kosa ni langu kudhani utanifaa" alijisemea mwenyewe general
"majemedari wote tusikilizane, leo hii ndio itaamua hatma ya nchi yetu. Tuwaonyeshe wale wanaidhani wanaweza kuchwza na amani yetu. Vita ya leo ni ua ama uawa lakini mpaka kieleweke" hayo yalikuwa ni maneno General Griffin kwa vijana wake. "tumekusoma mkuu" walijibu kwa pamoja, "Alex utaendelea na kikosi hicho kidogo, na kazi yako ni kutufngula njia tu. Mimi nitakuja na kikosi kikubwa halafu tutaongana katika mapambano" General aliongea na Alex alitikisa kichwa kukubali. "mimi je" ilikuwa sauti ya raisi, "mkuu usalama wako ni muhimu" alijibu General Griffin.
"Muheshimwa raisi tutahitaji msaada wako" Alex aliongea na kumsogelea kisha akamnong'oneza kitu sikioni. Raisi alitabasamu na kuashiria amemuelewa, "basi hakuna shida wacha mimi niondoke niwaache muendelee na majukumu mengine" Raisi aliongea na kusimama kisha akaondoka. Waliendelea kupanda mipango yao kwa makini sana, walifanya hivo kuhakikisha hatoki mtu hata mmoja kati ya waasi.