Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #181
152.
“Pumbavu hawa. Sijui wanatengeneza majitu ya hivi ya nini,” Agent alijiuliza huku akiwa kaacha kumchungulia Idris. “Zile risasi zilitakiwa zimpige na kumtokea mgongoni. Ila zilibaki mwilini mwake. Sasa kumbe ni liroboti tu nalo hili.” Akamaliza na tusi.
Akachomoza uso wake tena na kuchungulia na alishuhudia macho ya Idris yatoa mwanga wa kijani ambao ulikuwa unapanda na kushuka toka kwenye chumba kile.
“Mbwa ananitafuta huyu,” Akaongea Unknowm ma kutizama saa yake. Ikawa ipo asilimia tisini na tano. Akachungulia tena lakini eneo lile, hakumuona Idris. Akarudisha kichwa ndani na hapohapo, akashangaa Idris ametokeza mbele yake na kumkaba shingoni na kisha kuanza kumnyanyua juu kwa kutumia mkono mmoja. Miguu ya Unknown ikawa inaelea, na huku juu akawa anajaribu kuindoa mkono wa Idris shingoni kwake lakini mwanaume hakumuachia.
Mkono mwingine wa Idris, ukachomoa panga refu na wakati huohuo, saa ya Agent Unknown ililia sauti ambayo iliashiria, nguvu za roboti wake, tayari zilirudi hadi asilimia mia. Agent akajitahidi kuupeleka mkono wake mwingine kwenye saa yake na kisha akaibonyeza saa ile kwenye kitufe kimoja kilichokuwepo pembeni.
Idris naye alikwisha dhamiria kummaliza kabisa Unknown. Aliuvuta mkono wake wenye panga kwa nyuma, tayari kwa kumshindilia kichwani panga lile Unknown.
Lakini kabla hajatimiza adhma hiyo. Mkono wa The Lens ulitokea na kuingia kwenye mkono wa Unknown na Agent hakufanya kosa hata kidogo. Alitumia mkono ule wa chuma kwa kumtwanga konde zito Idris. Konde hilo lilitua kwenye kidevu na kumfanya Idris amuachie Unknown huku kidonda kikubwa kikijitengeza kwenye kidevu.
Vile vifaa vya The Lens vikarudi na kujitengeneza tena na kuwa roboti kubwa sana. Unknown akafungulia viatu vyake, naye akapaa na kuingia mwilini mwa The Lens ambapo yeye alikaa kwenye kiti kimoja ambacho kilikuwa kifuani kwa roboti yule.
“Muda wangu sasa. Mmenionea sana.” Unknown aliongea kwa kisirani na kuubadilisha mwili wa The Lens kuwa kioo kwa asilimia kubwa sana.
Nyuma ya The Lens, alikuwepo mwanadada Merice ambaye alijichaji nguvu zake nyingi nakuzirusha kwenda kwa The Lens. Lakini hakujua sababu ya The Lens kujigeuza kuwa kioo. Mwili ule ulijengwa kwa kioo ili aukisi kila nguvu ya jua au moto kila utakapovamiwa. Na kosa kubwa alilofanya Merice, ni kurusha nguvu hizo za jua {nyuklia} kwenda kwa roboti yule ambapo nguvu zile zilidunda na kumrudia yeye mwenyewe na kumpiga vibaya sana kwa mlipuko uliyojitokeza.
Idris aliweza kushuhudia tukio like na kujikuta akikumbwa na maumivu yaliyochanganyika na hasira. Hali hiyo ilimfanya naye aanze kupigana bila huruma na wakati huo, kidevu chake kilikuwa kimejirudi baada ya kupokea konde zito la chuma toka kwa Unknown.
Idris akapotea pale alipo na ghafla akatokea mbele ya The Lens na kuanza kutumia kisu kuchimbua miguu ili kukata nyaya zilizoungwa kwenye mwili wa The Lens. Macho yake yawezayo kuona hadi ndani, yaliweza kugundua uwepo wa nyaya zinazomuendesha The Lens hivyo alianza kuchimbua mwili wa The Lens ili aziharibu.
The Lens alitupa teke lililompata Idris tumboni na kumrusha toka mahali alipo na kwenda kujibamiza kwenye ukuta na wakati huohuo, The Lens naye aliruka juu kidogo na kisha kutua mbele ya Idris tena na kumshindilia ngumi nyingine akiwa palepale chini. Idris alipotaka kupotea kama afanyavyo, alijikuta anaumia mwenyewe. Vile vioo vya The Lens viliakisi nguvu zake na kujikuta hawezi kupotea bali kubaki palepale na kupokea kipondo cha nguvu. Alipotaka kutengeneza nguvu za nyuklia, akakumbuka hali iliyomtokea Merice. Uoga ukamkumba. Angejilipua yeye mwenyewe, lakini aliona ni mapema sana hasa kwa sababu hajawamaliza maadui zake.
“Umeshindwa mwanajeshi. Sasa ni muda wa kufa.” The Lens alimwambia Idris.
“We’ ni nani?” Ikabidi Idris amuulize The Lens hasa kwa kile kichapo alichokipokea.
“The Lens.” Ilikuwa ni sauti nene iliyomjibu Idris.
“Hapana. Nataka kukujua wewe unayeendesha hii silaha.”
“Kwa kuwa upo katika wakati wako wa mwisho, naweza kukwambia,” Akajibiwa Idris na kujiweka tayari kumjua anayempa kashi kashi. “Naitwa The Last, kwetu Tanzania naitwa Wa….” Hakumaliza kauli yake, Idris akadakia.
“Wa Mwisho. Au Man’Sai. Baba Martina, mume wa Lisa.” Kauli hiyo ikamfanya The Lens kutulia kidogo na kisha Agent Unknown akachomoka toka mle ndani na kushuka hadi chini alipokuwepo Idris.
“Umenijuaje?”
“Nina urafiki na Watanzania. Nimeishi kule na nimeoa kule. Nina urafiki ambao si mkubwa sana na Agent Zero. Ndiye aliyenijenga na kufika hatua ya kupambana hivi.” Akajibu Idris.
“Agent Zero,” The Last alinong’ona. Idris akaitikia kuwa anajuana naye. “Ni mwanafunzi wangu yule.” Akaongeza The Last.
“Nafahamu na tulifika hadi FISSA, mimi na Merice na kuonana na uongozi wako. Kwa kifupi, wamekukumbuka sana.” Maneno hayo yakamfanya The Last apumue pumzi kubwa na kukumbuka mara ya mwisho alipotizama runinga. Alikumbuka kuwa Merice na Idris ndio walikuwa wamekamatwa na jeshi la Uzo.
“Sasa imekuwaje mkataka kutengenezwa tena humu?” Akauliza The Last.
“Hapana. Walitaka kutuua. Yaani damu yangu, watengenezwe wanajeshi wengine wenye roho mbaya kupitia mimi. Lakini mimi na Merice tulikwishapanga kuhusu hilo. Nilitaka na Merice awe kama mimi, na wa kutubadilisha alikuwa ni mama yake. Agent Zero alisoma njia karibu zote za kumbadilisha Merice, lakini mitambo ya kufanya hivyo, haikuwepo kule Tanzania. Ndipo akachukua jukumu la kumtumia barua pepe Mama wa Merice kumuonyesha njia ya kutengeneza wanajeshi wengine kama mimi. Hakujua ile barua kuwa imetoka kwetu. Naye akaongeza kazi ya kutuhitaji ili atufanyie huo ujinga. Hakujua kuwa ananipa nguvu zaidi.” Idris akaeleza kwa kifupi kilichotokea.
“Wajua nini. Hatuna muda sana wa kuongea. Nina watafuta wale wajinga wanamichezo nimalizane nao. Naomba nikawafanye kitoweo. Samahani sana kwa kilichotokea.” The Last aliongea na kuwasha viatu vyake tayari kupanda ndani ya The Lens.
“Namuhitaji Uzo pia. Anahusika na kifo cha wazazi wangu. Nahitaji alipe yote aliyoyafanya.” Idris alimwambia The Last.
“Unahitaji Lift?” Maneno hayo yalienda sambamba na The Lens kubadilisha vioo na kuwa ile Roketi. Idris akanyanyuka na kwenda kupanda nyuma ya The Last ambaye alikuwa ndiye dereva.
Roketi ikawashwa na kuanza kwenda kwenye lile dirisha ambapo The Lens alitupwa na mlipuko alioutoa Idris. “Hey. Unaweza kukaa na mwenzako huko nyuma?” Akaulizwa Merice ambaye alikuwa bado hajarudiwa na nguvu baada ya ule mlipuko uliyojirudi kwake.
Merice akamtazama Idris, akamuona asiye na wasiwasi.
“Id. Ni nani huyu?” Ikabidi naye aulize swali lilelile kama aliloulizwa The Last baada ya kichapo kikali kumuangukia.
“Ndiye The Last.” Akajibiwa kwa kifupi.
“Man’Sai?” Akauliza kwa mshangao wa haja.
“Hatuna muda dada. Tupande, tukamalize kazi.” The Last aliongea na Merice bila kuuliza tena, akapanda nyuma na kumkalia juu Idris. Roketi ile ikachomoka toka mle ndani na kuanza kwenda nje umbali kama kilomita mbili.
“Hatuhitaji tena huu ujinga. C.O.D.EX, ndio mwisho wake.” The Last aliongea huku anafungua vifuniko kwenye vifyatulio vya mabomu yaliyopo kwenye mabawa ya ile roketi. Akatuma bomu moja ambalo lilienda hadi kwenye ile maabara kuilipua vibaya sana.
Mlipuko ule ulifanya waliokuwepo chini pia washtuke hasa baada ya ghorofa lile kuwa kivutio kikubwa sana Jijini New York. Maabara ya C.O.D.EX ikawa imelipuliwa. The Last akaishusha roketi ile hadi chini, mbele ya jeshi jipya lililoitwa na Jenero, F.O.F. Roketi ikajibadilisha na kuwa The Lens huku Idris na Merice wakitokea na kusimama pembeni ya roboti yule.
“Naona sasa mmeunganika na kuwa kitu kimoja.” Aliongea Jenero huku akitoka nyuma ya jeshi aliloliita, na kusogea hadi mbele, akawa anaonekana vema. “Kuna C.O.D.EX na Roboti.” Akaongeza huku anawaonyeshea kidole Idris na Merice pamoja na The Lens. “Ninao pia, C.O.D.EX na Maroboti wangu hawa.” Muda huohuo, wale C.O.D.EX wanamichezo, wakajitokeza mbele na kuungana na Jenero huku wale aliowaita maroboti, nao wakianza kujitengeneza.
“Hao sio maroboti, ni Transformers.” The Lens alitoa sauti kurekebisha kauli ya Jenero baada ya watu wake kujibadilisha na kuwa maroboti makubwa, sawa na The Lens.
“Hapana. Transformers, wanatoka kwenye magari, ndege, helikopta, pikipiki na vyombo vingine vya usafiri. Ila hawa wangu, wanatoka kwenye nyama ya binadamu. Na wewe wako huyo…” Akamuangalia The Lens. “Huyo ni Iron Man.” Akamalizia kauli yake na kuanza kucheka. Alimfananisha The Lens na yule bwana wa kwenye filamu ya Iron Man.
“Hapana. Naitwa The Lens.” The Lens akabadilika na kuwa kioo, kisha mwanga mkali wa jua ukamtoka na kuurusha mbele ya wale wanajeshi wachezaji. Mlipuko mkubwa ukajitokeza huku wachezaji wale wakirushwa kushoto na kulia, pembeni na katikati kwa sababu ya mlipuko na wakati huohuo, wale maroboti wa Jenero, walimkinga Jenero ili asidhulike na mlipuko ule.
The Lens alichomoka ghafla na kufika hadi eneo ambapo F.O.F wanne walikuwa wamemkinga Jenero, na kisha kwa nguvu nyingi alizonazo, alitoa muale mwingine wa jua na kuwapiga wale maroboti, nao wakatupwa mbalimbali kama walivyotupwa wale wachezaji wa C.O.D.EX. Jenero akajikuta yupo wazi na uso wake unatazamana na The Last ambaye alishuka toka ndani ya The Lens.
“Umekosea njia Mzee. Na utajuta kwa nini umepita hii njia.” The Last alimwambia Jenero kwa sauti kavu na kumpiga ngumi nzito ya tumbo. Mzee yule alishika tumbo lake huku kainama na kumpa nafasi The Last ya kumfunua kwa kumpiga kwa goti lake sehemu ya kidevu. Damu zikamruka Jenero na wakati huo, maroboti yake yalinyanyuka na kutengeneza silaha mikononi mwao tayari kwa kumvamia The Last.
“Pumbavu hawa. Sijui wanatengeneza majitu ya hivi ya nini,” Agent alijiuliza huku akiwa kaacha kumchungulia Idris. “Zile risasi zilitakiwa zimpige na kumtokea mgongoni. Ila zilibaki mwilini mwake. Sasa kumbe ni liroboti tu nalo hili.” Akamaliza na tusi.
Akachomoza uso wake tena na kuchungulia na alishuhudia macho ya Idris yatoa mwanga wa kijani ambao ulikuwa unapanda na kushuka toka kwenye chumba kile.
“Mbwa ananitafuta huyu,” Akaongea Unknowm ma kutizama saa yake. Ikawa ipo asilimia tisini na tano. Akachungulia tena lakini eneo lile, hakumuona Idris. Akarudisha kichwa ndani na hapohapo, akashangaa Idris ametokeza mbele yake na kumkaba shingoni na kisha kuanza kumnyanyua juu kwa kutumia mkono mmoja. Miguu ya Unknown ikawa inaelea, na huku juu akawa anajaribu kuindoa mkono wa Idris shingoni kwake lakini mwanaume hakumuachia.
Mkono mwingine wa Idris, ukachomoa panga refu na wakati huohuo, saa ya Agent Unknown ililia sauti ambayo iliashiria, nguvu za roboti wake, tayari zilirudi hadi asilimia mia. Agent akajitahidi kuupeleka mkono wake mwingine kwenye saa yake na kisha akaibonyeza saa ile kwenye kitufe kimoja kilichokuwepo pembeni.
Idris naye alikwisha dhamiria kummaliza kabisa Unknown. Aliuvuta mkono wake wenye panga kwa nyuma, tayari kwa kumshindilia kichwani panga lile Unknown.
Lakini kabla hajatimiza adhma hiyo. Mkono wa The Lens ulitokea na kuingia kwenye mkono wa Unknown na Agent hakufanya kosa hata kidogo. Alitumia mkono ule wa chuma kwa kumtwanga konde zito Idris. Konde hilo lilitua kwenye kidevu na kumfanya Idris amuachie Unknown huku kidonda kikubwa kikijitengeza kwenye kidevu.
Vile vifaa vya The Lens vikarudi na kujitengeneza tena na kuwa roboti kubwa sana. Unknown akafungulia viatu vyake, naye akapaa na kuingia mwilini mwa The Lens ambapo yeye alikaa kwenye kiti kimoja ambacho kilikuwa kifuani kwa roboti yule.
“Muda wangu sasa. Mmenionea sana.” Unknown aliongea kwa kisirani na kuubadilisha mwili wa The Lens kuwa kioo kwa asilimia kubwa sana.
Nyuma ya The Lens, alikuwepo mwanadada Merice ambaye alijichaji nguvu zake nyingi nakuzirusha kwenda kwa The Lens. Lakini hakujua sababu ya The Lens kujigeuza kuwa kioo. Mwili ule ulijengwa kwa kioo ili aukisi kila nguvu ya jua au moto kila utakapovamiwa. Na kosa kubwa alilofanya Merice, ni kurusha nguvu hizo za jua {nyuklia} kwenda kwa roboti yule ambapo nguvu zile zilidunda na kumrudia yeye mwenyewe na kumpiga vibaya sana kwa mlipuko uliyojitokeza.
Idris aliweza kushuhudia tukio like na kujikuta akikumbwa na maumivu yaliyochanganyika na hasira. Hali hiyo ilimfanya naye aanze kupigana bila huruma na wakati huo, kidevu chake kilikuwa kimejirudi baada ya kupokea konde zito la chuma toka kwa Unknown.
Idris akapotea pale alipo na ghafla akatokea mbele ya The Lens na kuanza kutumia kisu kuchimbua miguu ili kukata nyaya zilizoungwa kwenye mwili wa The Lens. Macho yake yawezayo kuona hadi ndani, yaliweza kugundua uwepo wa nyaya zinazomuendesha The Lens hivyo alianza kuchimbua mwili wa The Lens ili aziharibu.
The Lens alitupa teke lililompata Idris tumboni na kumrusha toka mahali alipo na kwenda kujibamiza kwenye ukuta na wakati huohuo, The Lens naye aliruka juu kidogo na kisha kutua mbele ya Idris tena na kumshindilia ngumi nyingine akiwa palepale chini. Idris alipotaka kupotea kama afanyavyo, alijikuta anaumia mwenyewe. Vile vioo vya The Lens viliakisi nguvu zake na kujikuta hawezi kupotea bali kubaki palepale na kupokea kipondo cha nguvu. Alipotaka kutengeneza nguvu za nyuklia, akakumbuka hali iliyomtokea Merice. Uoga ukamkumba. Angejilipua yeye mwenyewe, lakini aliona ni mapema sana hasa kwa sababu hajawamaliza maadui zake.
“Umeshindwa mwanajeshi. Sasa ni muda wa kufa.” The Lens alimwambia Idris.
“We’ ni nani?” Ikabidi Idris amuulize The Lens hasa kwa kile kichapo alichokipokea.
“The Lens.” Ilikuwa ni sauti nene iliyomjibu Idris.
“Hapana. Nataka kukujua wewe unayeendesha hii silaha.”
“Kwa kuwa upo katika wakati wako wa mwisho, naweza kukwambia,” Akajibiwa Idris na kujiweka tayari kumjua anayempa kashi kashi. “Naitwa The Last, kwetu Tanzania naitwa Wa….” Hakumaliza kauli yake, Idris akadakia.
“Wa Mwisho. Au Man’Sai. Baba Martina, mume wa Lisa.” Kauli hiyo ikamfanya The Lens kutulia kidogo na kisha Agent Unknown akachomoka toka mle ndani na kushuka hadi chini alipokuwepo Idris.
“Umenijuaje?”
“Nina urafiki na Watanzania. Nimeishi kule na nimeoa kule. Nina urafiki ambao si mkubwa sana na Agent Zero. Ndiye aliyenijenga na kufika hatua ya kupambana hivi.” Akajibu Idris.
“Agent Zero,” The Last alinong’ona. Idris akaitikia kuwa anajuana naye. “Ni mwanafunzi wangu yule.” Akaongeza The Last.
“Nafahamu na tulifika hadi FISSA, mimi na Merice na kuonana na uongozi wako. Kwa kifupi, wamekukumbuka sana.” Maneno hayo yakamfanya The Last apumue pumzi kubwa na kukumbuka mara ya mwisho alipotizama runinga. Alikumbuka kuwa Merice na Idris ndio walikuwa wamekamatwa na jeshi la Uzo.
“Sasa imekuwaje mkataka kutengenezwa tena humu?” Akauliza The Last.
“Hapana. Walitaka kutuua. Yaani damu yangu, watengenezwe wanajeshi wengine wenye roho mbaya kupitia mimi. Lakini mimi na Merice tulikwishapanga kuhusu hilo. Nilitaka na Merice awe kama mimi, na wa kutubadilisha alikuwa ni mama yake. Agent Zero alisoma njia karibu zote za kumbadilisha Merice, lakini mitambo ya kufanya hivyo, haikuwepo kule Tanzania. Ndipo akachukua jukumu la kumtumia barua pepe Mama wa Merice kumuonyesha njia ya kutengeneza wanajeshi wengine kama mimi. Hakujua ile barua kuwa imetoka kwetu. Naye akaongeza kazi ya kutuhitaji ili atufanyie huo ujinga. Hakujua kuwa ananipa nguvu zaidi.” Idris akaeleza kwa kifupi kilichotokea.
“Wajua nini. Hatuna muda sana wa kuongea. Nina watafuta wale wajinga wanamichezo nimalizane nao. Naomba nikawafanye kitoweo. Samahani sana kwa kilichotokea.” The Last aliongea na kuwasha viatu vyake tayari kupanda ndani ya The Lens.
“Namuhitaji Uzo pia. Anahusika na kifo cha wazazi wangu. Nahitaji alipe yote aliyoyafanya.” Idris alimwambia The Last.
“Unahitaji Lift?” Maneno hayo yalienda sambamba na The Lens kubadilisha vioo na kuwa ile Roketi. Idris akanyanyuka na kwenda kupanda nyuma ya The Last ambaye alikuwa ndiye dereva.
Roketi ikawashwa na kuanza kwenda kwenye lile dirisha ambapo The Lens alitupwa na mlipuko alioutoa Idris. “Hey. Unaweza kukaa na mwenzako huko nyuma?” Akaulizwa Merice ambaye alikuwa bado hajarudiwa na nguvu baada ya ule mlipuko uliyojirudi kwake.
Merice akamtazama Idris, akamuona asiye na wasiwasi.
“Id. Ni nani huyu?” Ikabidi naye aulize swali lilelile kama aliloulizwa The Last baada ya kichapo kikali kumuangukia.
“Ndiye The Last.” Akajibiwa kwa kifupi.
“Man’Sai?” Akauliza kwa mshangao wa haja.
“Hatuna muda dada. Tupande, tukamalize kazi.” The Last aliongea na Merice bila kuuliza tena, akapanda nyuma na kumkalia juu Idris. Roketi ile ikachomoka toka mle ndani na kuanza kwenda nje umbali kama kilomita mbili.
“Hatuhitaji tena huu ujinga. C.O.D.EX, ndio mwisho wake.” The Last aliongea huku anafungua vifuniko kwenye vifyatulio vya mabomu yaliyopo kwenye mabawa ya ile roketi. Akatuma bomu moja ambalo lilienda hadi kwenye ile maabara kuilipua vibaya sana.
Mlipuko ule ulifanya waliokuwepo chini pia washtuke hasa baada ya ghorofa lile kuwa kivutio kikubwa sana Jijini New York. Maabara ya C.O.D.EX ikawa imelipuliwa. The Last akaishusha roketi ile hadi chini, mbele ya jeshi jipya lililoitwa na Jenero, F.O.F. Roketi ikajibadilisha na kuwa The Lens huku Idris na Merice wakitokea na kusimama pembeni ya roboti yule.
“Naona sasa mmeunganika na kuwa kitu kimoja.” Aliongea Jenero huku akitoka nyuma ya jeshi aliloliita, na kusogea hadi mbele, akawa anaonekana vema. “Kuna C.O.D.EX na Roboti.” Akaongeza huku anawaonyeshea kidole Idris na Merice pamoja na The Lens. “Ninao pia, C.O.D.EX na Maroboti wangu hawa.” Muda huohuo, wale C.O.D.EX wanamichezo, wakajitokeza mbele na kuungana na Jenero huku wale aliowaita maroboti, nao wakianza kujitengeneza.
“Hao sio maroboti, ni Transformers.” The Lens alitoa sauti kurekebisha kauli ya Jenero baada ya watu wake kujibadilisha na kuwa maroboti makubwa, sawa na The Lens.
“Hapana. Transformers, wanatoka kwenye magari, ndege, helikopta, pikipiki na vyombo vingine vya usafiri. Ila hawa wangu, wanatoka kwenye nyama ya binadamu. Na wewe wako huyo…” Akamuangalia The Lens. “Huyo ni Iron Man.” Akamalizia kauli yake na kuanza kucheka. Alimfananisha The Lens na yule bwana wa kwenye filamu ya Iron Man.
“Hapana. Naitwa The Lens.” The Lens akabadilika na kuwa kioo, kisha mwanga mkali wa jua ukamtoka na kuurusha mbele ya wale wanajeshi wachezaji. Mlipuko mkubwa ukajitokeza huku wachezaji wale wakirushwa kushoto na kulia, pembeni na katikati kwa sababu ya mlipuko na wakati huohuo, wale maroboti wa Jenero, walimkinga Jenero ili asidhulike na mlipuko ule.
The Lens alichomoka ghafla na kufika hadi eneo ambapo F.O.F wanne walikuwa wamemkinga Jenero, na kisha kwa nguvu nyingi alizonazo, alitoa muale mwingine wa jua na kuwapiga wale maroboti, nao wakatupwa mbalimbali kama walivyotupwa wale wachezaji wa C.O.D.EX. Jenero akajikuta yupo wazi na uso wake unatazamana na The Last ambaye alishuka toka ndani ya The Lens.
“Umekosea njia Mzee. Na utajuta kwa nini umepita hii njia.” The Last alimwambia Jenero kwa sauti kavu na kumpiga ngumi nzito ya tumbo. Mzee yule alishika tumbo lake huku kainama na kumpa nafasi The Last ya kumfunua kwa kumpiga kwa goti lake sehemu ya kidevu. Damu zikamruka Jenero na wakati huo, maroboti yake yalinyanyuka na kutengeneza silaha mikononi mwao tayari kwa kumvamia The Last.