Simulizi ya Kijasusi: Kiguu Na Njia

Simulizi ya Kijasusi: Kiguu Na Njia

Nakukubalii[emoji109][emoji91][emoji91]
Leo ndio nimemaliza kusoma riwaya hii bora kabisa ya kusisimua lazima nikiri riwaya hii kuna maeneo imenitoa machozi sehemu nyingine imenifanya nicheke peke yangu kama chizi na kuna maeneo yamenifikirisha sana

Mkuu mimi shida yangu kubwa ni kupata hichi kitabu kinapatikana wapi na bei yake ni tshs ngapi?

Mwisho kabisa nitoe pongezi zangu za dhati kwako kwa kutuletea riwaya hii humu jamvini pia hongera kwa mtunzi kwa kazi hii iliotukuka

Hakika riwaya hii imejaa mafunzo makubwa elimu iliojaa humu hata kama mtu atakuwa hajafika maeneo yaliotajwa atakuwa amejifunza kitu maana kwa 99% ni ukweli mtu
 
Leo ndio nimemaliza kusoma riwaya hii bora kabisa ya kusisimua lazima nikiri riwaya hii kuna maeneo imenitoa machozi sehemu nyingine imenifanya nicheke peke yangu kama chizi na kuna maeneo yamenifikirisha sana

Mkuu mimi shida yangu kubwa ni kupata hichi kitabu kinapatikana wapi na bei yake ni tshs ngapi?

Mwisho kabisa nitoe pongezi zangu za dhati kwako kwa kutuletea riwaya hii humu jamvini pia hongera kwa mtunzi kwa kazi hii iliotukuka

Hakika riwaya hii imejaa mafunzo makubwa elimu iliojaa humu hata kama mtu atakuwa hajafika maeneo yaliotajwa atakuwa amejifunza kitu maana kwa 99% ni ukweli mtu
Nashukuru sana mkuu..
Asante pia kwa kusoma riwaa hii kali..

Vitabu vipo maduka mengi tu nchini hada yale makubwa. Lakini Heko publishers ndo wasambazaji wa hivi vitabu.

Unaweza mtafuta huyu dada ndiye anayeviuza. Kiguu na njia ni 15,000/= vitabu vingine utavipata kwa 7000-10,000
0763 044 459 au 0712 504 985
 
SEHEMU YA MWISHO





Alivaa nguo zake zile alizozipenda, kaptula na shati nyeupe. Ziling’ara kama nilivyoziacha! Miguuni alitilia buti zake ambazo nazo ziling’ara kwa kiwi, ingawa zilianza kuchoka. Alikuwa peke yake katikati ya pori, isipokuwa kwa mifugo mingi ya mbuzi, kuku na bata. Watu wa pwani wangeweza kuapa kuwa ni jini jeupe linalokaa peke yake msituni. Babu alikuwa ametusikia toka mbali. Hivyo, alimfunga mbuzi yule harakaharaka na kusimama akitukodolea macho. Alipotuona alitukimbilia na kunidaka juujuu. Angeweza kunibeba… angeweza kunitia mweleka…. Babu alikuwa na nguvu zake. Ilikuwa kama ni binadamu pekee aliyebishana na uzee. Binadamu ambaye hakukubali kusalimu amri kwa kifo.







Pamoja na baba tulikuwa na vijana wengine wawili ambao nilielekezwa kuwa ni ndugu zangu. Vijana hao walipewa amri ya kumkamata beberu mkubwa kuliko wote na kumchinja. Akachunwa. Moto ukawashwa. Muda mfupi baadaye, tulikuwa tukimla mbuzi yule, wa kuchoma. Babu, akiwa na meno yake yote alitafuna mguu mzima wakati wengine tukishika shika hapa na pale.

Baadaye babu aliwataka baba na wale wenzetu wengine kuondoka kwa maelezo kuwa alikuwa na mengi ya kuzungumza na mjuu wake faragha. Usiri wangu na babu halikuwa jambo geni kwa baba, toka utoto wangu. Hivyo, hakutia ubishi, walichukua nyama ya kula nyumbani wakaondoka zao kwa ahadi ya kunifuata kesho.

Nikapata wasaa wa kuchomoa zile elfu hamsini nilizobakiza na kumkabidhi babu. “Zawadi pekee niliyoweza kukuletea ni hii,” nilisema kwa masikitiko.

Babu hakuzipokea. Badala yake alicheka kabla ya kusema, “Sidhani kama nazihitaji. Za nini? Kaa nazo, zitakufaa wewe zaidi. Naamini bado unasafari nyingine ndefu, yenye mafanikio makubwa zaidi. Halafu, bado tuna mengi ya kuzungumza, mimi na wewe.”



“Bila shaka. Niliitikia.

“Miaka mingapi vile toka tumetengana?” Babu aliniuliza. “Mingi sana. Ni aibu kuitaja.” Nilimjibu.

“Aibu ya nini? Mwanaume anayeonea aibu masaibu yake hafai. Kwa nini ufanye jambo ambalo utalijutia maishani mwako?”

Nilijua darasa la babu limeanza. Sikuwa tayari kwa darasa lolote wala somo lolote kabla ya kumtaka radhi. Hivyo nikajikongoja na kumwambia, “Babu ningeomba nianze kwa kukutaka radhi.”







“Radhi ya nini?” “Hirizi.” “Ilifanyaje?” “Ilipotea!”

Nilitarajia babu abadilike, akasirike. Lakini kwa mshangao nilimwona akiachia tabasamu jembamba. “Nisubiri kidogo,” alisema akiinuka na kuingia ndani, aliporejea alikuwa na hirizi mkononi.

“Hirizi hii siyo?”

Niliitazama kwa makini. Nisingeweza kuisahau. Ilikuwa



ileile!





Sikuyaamini macho yangu. Nikamkodolea babu macho



ya mshangao.

“Hii ndiyo inayokusumbua?” babu aliongeza baada ya kicheko kingine. “Usiwe na wasiwasi. Ilipotea ikatafuta njia, ikarudi nyumbani kukusubiri.”

Bado sikuweza kuelewa. Hirizi hiyo ilipotea porini katika purukushani za kuikimbiza isianguke mikononi mwa padri. Yule kimbelembele, Byabato, alinihakikishia kuwa aliiokota tena na kumrudishia padri Backhove ambaye aliichoma, ikakataa kuungua. Kwamba baadaye ilitupwa baharini. “Ilifikaje kwako?” nikamuuliza.

“Ni hadithi ndefu. Ili kuifanya fupi pengine nikuambie tu kuwa ililetwa.”

“Na nani?” nilizidi kumbana babu. “Na mizimu ya babu zetu.”

Bado nilikuwa sijamwelewa. Nikamwambia hivyo. “Mizimu ina njia nyingi ya kuwalinda wahanga wake,”

alifafanua. “Chochote kilichokutokea hadi hirizi hii kutengana nawe wahanga walikuwa wakiona. Ama kwa kujigeuza ndege,







ama kwa kuwatuma ndege, hirizi hii ililetwa hadi katika mikono yangu.”

Babu alipoona kuwa bado sijaridhika na ufafanuzi huo aliamua kuwa wazi zaidi. Alisema kuwa jioni moja alikuwa akiwinda katika mwambao wa mto Malagalasi. Mara akaona kundi kubwa la ndege aina ya hondohondo wakitua hatua chache toka alipokuwa. “Walikuwa wengi. Kama elfu moja hivi. Waliponiona waliruka kunikimbia. Lakini mwenzao mmoja hakuweza kuruka. Alikuwa akipigapiga mabawa kwa nia ya kupaa lakini hakuweza. Nikamsogelea kuona kapatwa na nini. Nikabaini kuwa shingo yake ilikabwa na kamba nyeusi ambayo ilinasa kwenye kichaka cha mti. Nilipomshika ili kumkwamua ile kamba nilishangaa kuona kuwa ilikuwa hirizi ile niliyokupa. Nikaitoa na kumwacha ndege ambaye alipaa kuwaendea wenzake waliokuwa wakihangaika angani kumsubiri.”

Ilikuwa habari ya ajabu kwangu. Hirizi yangu, iliyopotea zaidi ya miaka thelathini iliyopita imerejea mikononi mwangu. Niliipokea, nikaipapasa. Ilikuwa ileile, kwa rangi na uzito. Kwamba imerudi mikononi mwangu halikuwa jambo la ajabu sana, ni namna iliyoifanya irudi ambayo kichwa changu hakikuweza kupokea.

Falsafa nyingi zilipita kichwani mwangu. Kama kweli ilitupwa ziwani bila shaka ingeweza kuoza. Kama hilo halikutokea ni wazi kuwa ilimezwa na samaki ambaye huenda alivuliwa na kuliwa. Kama ilikuwa hivyo hirizi itakuwa ilitupwa kama sehemu ya uchafu wa matumbo ya samaki wanayotayarishwa kwa ajili ya minofu kusafirishwa Ulaya na “mapanki” kuvamiwa na akina baba na mama ntilie. Inawezekana kuwa katika jitihada za kujitafutia chochote ndege yule alijikuta ameivaa hirizi ile na kuisafirisha bila







kujua? Kama ni kweli kwa nini ailete hadi miguuni mwa babu? Katika pitiapitia yangu vitabuni nilikuwa nimesoma mahala tabia za ndege. Moja ya tabia zao za ajabu ni ile ya kuhama au kusafiri safari za mbali kila ifikapo msimu fulani. Mara nyingi ndege hao wanaweza kusafiri safari za mbali toka Marekani au Ulaya hadi Afrika. Inaaminika kuwa wengi uhama katika vipindi vya hali fulani ya hewa na kurudi hali inapotengemaa. Inaaminika pia huko ambako huenda ndiko ambako ndege huzaliana na kurejea likiwa kundi kubwa zaidi. Inawezekana kabisa kuwa hondohondo aliyebeba hirizi yangu alikuwa katika msafara huo. Anaweza kuwa alikuwa akitoka

zake Ulaya au nchi za Kiarabu na kuelekea Afrika Kusini!

Babau alikuwa kama anayeyasoma mawazo yangu. Alikohoa kidogo kabla ya kusema, “Naona na wewe tayari umeambukizwa yale maradhi yenu.”

“Maradhi gani?

“Maradhi ya kisomi. Naona unavyoona shida kuamini kuwa mizimu ya babu wa babu zako imekurejeshea hirizi hii! shauri lako. La msingi ni kwamba hirizi yako imerejea na tangu leo utaivaa tena. safari hii milango yote uliyoshindwa kuifunguwa itafunguka,” alisema akinivisha hirizi hiyo na kisha kunitemea mate kichwani na kifuani.

“Kuna jambo la pili.” Alisema akiinuka tena na kurudi ndani. Aliporejea alikuwa na bahasha tatu mkononi. Alinikadhi. Ilikuwa barua. Juu ziliandikwa jina lake na anuani ya kiji chake. Ilielekea barua hizo zilitoka nje ya nchi, kwani stempu zote zilikuwa na picha ya malkia au wafalme wazungu, muhuri ukiosomeka waziwazi “Stockholm-sweden”. Tarehe kwenye mihuri hiyo zilionyesha kuwa zilitumwa zaidi ya miaka kumi na mitano iliyopita!







“Barua!” Niliropoka.

“Ndiyo,” babu alijibu “Mbona hazijafunguliwa? Ni za zamani sana,” nilisaili.

Babu naye akaonyesha mshangao wake kwangu, “Mjukuu wangu, zinalekea kuwa ni barua muhimu sana. Unadhani ningeweza kumpelekea mtu yeyote asome siri zangu na kuanza kunitangaza? Nilikuwa nakusubiri, nilijua ungerudi salama.”

“Ni wewe peke yako utakayekuwa wa kwanza kuelewa chochote kilichoandikwa humo.”

“Zilifikaje hapa?” Niliuliza nikianza kufungua moja

niliyoiona ya zamani zaidi.

“Zililetwa. DC alileta kwa mkono wakemwenyewe.

Alinishawishi kufungua lakini nilikataa katakata.”

Baada ya maelezo hayo babu alikunjua kiti chake cha uvivu, kilichotengenezwa kwa ngozi ya nyati na kujilaza kimya kwa namna ya kunipa wasaa wa kusoma barua hizo kwa tuo. Barua ya kwanza ilikua ndefu kidogo. Ilianza kwa salamu za siku nyingi, ikaendelea kwa taarifa ya kuipongeza kazi yake alipokuwa nchini humo, “Tumetengeneza filamu mbili za ile michezo uliyoshiriki kuicheza. Filamu hizo zimependwa sana Ulaya nzima zinanunuliwa kama peremende. Taarifa tuliyoichapisha hapa chini ni malipo yako ya mrabaha hadi sasa. Tunaomba ufanye kila uwezalo kuwasiliana nasi ili

upokee malipo yako,” ilieleza barua hiyo.

Sehemu ya pili ya barua hiyo ilikuwa na mahesabu ya idadi ya mikanda iliyouzwa na televisheni zilizonunua hakimiliki na hakishiriki. Kwa hesabu za harakaharaka asilimia ya babu ilionyesha kama dola 227,000. Sikuyaamini macho yangu. Nikainua macho kumtazama. Alikuwa amesinzia, tabasamu likiwa mdomoni.







Nikafungua barua ya pili. Hii iliandikwa mwaka mmoja baadaye. Ilisisitiza, umuhimu wa babu kwenda haraka au kumtuma mrithi wake yeyote anayeaminika. Iliongeza kuwa iwapo kuna tatizo lolote la vitambulisho mwakilishi huyo alichotakiwa ni kwenda na ile hirizi ambayo ilikuwa haibanduki shingoni mwake. “Benki yetu tayari imearifiwa juu ya hilo. Usiwe na wasiwasi,” iliongeza barua hiyo.

Barua ya tatu iliambatanishwa na hundi. Hesabu zilizoandikwa juu ya hundi hiyo zilinitatanisha dola 812,000! Barua ilisisitiza fedha hizo kuchukuliwa. Ikiongeza kuwa benki yao tayari imefungua matawi nchini katika miji ya Dar es Salaam na Mwanza, haikuwepo haja ya kusafiri hadi Ulaya tena.

Mara nikaanza kupata njozi za mchana. Nilijiona nikiandika kitabu, ambacho kiliyahusu maisha yangu mwenyewe. Niliyaumba na kuyaumbua matukio, mikasa na visa vyote vilivyonikumba toka katika safari zangu kuu mbili safari ya kimaisha iliyonifikisha kila pembe ya nchi na ile ya kimaumbile ambayo ilinitoa utotoni na kuniingiza ukubwani. Nilihisi hata jina la kitabu likinijia akilini; Kiguu na Njia.

Zikanijia njozi nyingine. Katika njozi hizi nilijiona nikiwalekeza watu wa masuala ya filamu wapi pa kuelekeza kamera zao, katika filamu niliyokua nikiitengeneza. Niliwataka ihusishe maeneo yote muhimu ya nchi yetu, mbuga za wanyama, maziwa na mito yote ambayo haikupata kutangazwa vizuri. Kwa njozi niliona mikanda ya filamu hiyo ikigombewa na kuwafanya watazamaji waone hazina kubwa iliyosahauliwa ambayo walijaliwa na Muumba.

Nikaona jinsi nilivyokuwa nikiishi na mke wangu Nashifa kwa furaha. Watoto wetu wawili wenye afya njema







wakicheka na kufurahi…

Halafu nikamkumbuka mwenye fedha zake, ambazo zingeniwezesha kufanikisha ndoto hiyo. Nikageuka.

“Babu!” niliita tena nikimtazama.

Alikuwa bado amelala vilevile kwenye kiti chake cha uvivu. Tabasamu lake lilikuwa bado limesahauliwa palepale usoni kama mtu aliyekuwa katika dimbwi la starehe. Niliinuka na kumshika bega. Nikamtikisa taratibu, baadaye kwa nguvu kidogo, “Babu… babu… babu…!

Kimya! Kimya!

Nikashtuka. Alikuwa kama hapumui! Nikamshika kifua kusikiliza mapigo ya moyo. Hayakuwepo. Hata mwili wake tayari ulikuwa umepoa. Ndio kwanza nikabaini kuwa babu hatukuwa naye tena duniani! Tabasamu lake lililobakia palepale kama ishara ya ushindi kwa jambo zito lililokuwa likimsumbua kwa muda mrefu.

Nilitetemeka mwili mzima. Nguvu zikaniishia, furaha, faraja na matumaini makubwa niliyoyapata mara baada ya kuisoma barua yake, ikatumbukia nyongo.

MWISHO






BURE SERIES
Naomba nikili wazi ,hii kwangu ni riwaya bora kuwahi kuisoma humu Jf .imenitembeza kila pembe ya nchi..Hakika nimeburudika na kuhuzunika pia[emoji174]
 
Back
Top Bottom