Simulizi ya Kijasusi: Kiguu Na Njia

Nakukubalii[emoji109][emoji91][emoji91]
Leo ndio nimemaliza kusoma riwaya hii bora kabisa ya kusisimua lazima nikiri riwaya hii kuna maeneo imenitoa machozi sehemu nyingine imenifanya nicheke peke yangu kama chizi na kuna maeneo yamenifikirisha sana

Mkuu mimi shida yangu kubwa ni kupata hichi kitabu kinapatikana wapi na bei yake ni tshs ngapi?

Mwisho kabisa nitoe pongezi zangu za dhati kwako kwa kutuletea riwaya hii humu jamvini pia hongera kwa mtunzi kwa kazi hii iliotukuka

Hakika riwaya hii imejaa mafunzo makubwa elimu iliojaa humu hata kama mtu atakuwa hajafika maeneo yaliotajwa atakuwa amejifunza kitu maana kwa 99% ni ukweli mtu
 
Nashukuru sana mkuu..
Asante pia kwa kusoma riwaa hii kali..

Vitabu vipo maduka mengi tu nchini hada yale makubwa. Lakini Heko publishers ndo wasambazaji wa hivi vitabu.

Unaweza mtafuta huyu dada ndiye anayeviuza. Kiguu na njia ni 15,000/= vitabu vingine utavipata kwa 7000-10,000
0763 044 459 au 0712 504 985
 
Naomba nikili wazi ,hii kwangu ni riwaya bora kuwahi kuisoma humu Jf .imenitembeza kila pembe ya nchi..Hakika nimeburudika na kuhuzunika pia[emoji174]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…