Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #21
SEHEMU YA 17
Hivyo, mara tu nilipopata mshahara wangu wa mwezi huo, ambao uliongezwa mara dufu, nilitoweka.”
Nilicheka sana. Kwangu ilikuwa habari ya kusisimua sana. Ilinisisimuazaidikumsikiababu,kwamarayakwanza,akisimulia tukio lililomuhusu kwa kirefu kiasi hicho. Mara nyingi yeye alikuwa mtu wa simulizi na kujibu maswali kwa mkatomkato. Nilikuwa na kila sababu ya kumhurumia babu. Kwa upande mwingine, maelezo yake yalizidi kunithibitishia jambo moja kubwa; umuhimu wa elimu. Lakini mara nikakumbuka kuwa babu alikuwa hajafikia au kugusia kiini cha maelezo hayo. Sababu ya kulala kwangu kwake na kuchinjwa kwa jogoo wake bora kuliko wote; kwa kila hali kulihusiana na
majonzi aliyokuwa nayo babu. Nikamkumbusha hilo.
“Nakumbuka vizuri sana,” Babu aliniambia. “Lakini,” aliongeza. “Kama nilivyosema awali unahitaji kuwa na kifua. Taarifa nitakayokupa huenda ikakutisha au kukuogofya. Lakini unatakiwa kupokea kama mwanamume na kuichukulia kwa upande wa pili kama msukumo wa ufunguo mpya wa maisha yako.”
Niliona kama babu anazidi kunichanganya. Nikamtumbulia macho ya mshangao na kumtegea sikio kwa makini.
“Inabidi uondoke kijijini hapa mara moja,” babu
aliniambia ghafla.
Kati ya yote niliyotarajia, hilo la kuondoka halikuwemo katika mawazo yangu, “Nani? Mimi!”
Babu akakubali. “Kwa nini?” “Wanataka kukuua.”
Sikuyaamini masikio yangu, “Wanataka kuniua mimi, watu gani hao?”
“Wanakijiji. Wakazi wa eneo hili.”
Bado sikumwelewa babu. Nilihisi huo ulikuwa utani wake mwingine, pengine kwa nia ya kupima ujabari wangu. Ili kumthibitishia hivyo niliangua kicheko na kumwambia taratibu, “Babu acha utani huo. Unanichulia kifo.”
Lakini macho ya babu yalikuwa hayana utani wala mzaha wa aina yoyote alipoongeza, “Wanataka kukutoa kafara. Lazima uondoke haraka iwezekanavyo.”
* * *
Kwa takribanimiakamitatuiliyopita eneo letulilikumbwa na ukame. Mazao yaliyopatikana yalikuwa machache sana. Mimea mingi ilinyauka, hata baadhi ya vyanzo vya maji vilianza kukauka. Mbaya zaidi ni pale ilipoonekana wazi kuwa mwaka huo pia hakukuwa na dalili ya mvua.
Zaidi ya tatizo hilo la ukame lilikuwepo tatizo jingine kubwa zaidi, tatizo la ugonjwa wa malale. Eneo kubwa la mapori na misitu iliyovizunguka vijiji vyetu ilikuwa na mbung’o wengi sana ambao walidaiwa kusababisha malale. Mbung’o hao walianza hata kuvamia mifugo iliyokuwemo zizini na hivyo kusababisha maradhi ya usingizi na hatimaye vifo vya ng’ombe wengi. Wala haikuwa mifugo pekee. Zaidi ya watu wanane kijijini hapo walikuwa wamekwishakufa kwa malale huku wengine wasiopungua ishirini, wakiugua ugonjwa huo ambao haukusikia dawa.
Kwa mujibu wa babu, Mwami, wasaidizi wake na wazee wenye busara kijijini hapo waliketi vikao vingi kujadili namna ya kupambana na matatizo hayo bila mafanikio. Hali
Hivyo, mara tu nilipopata mshahara wangu wa mwezi huo, ambao uliongezwa mara dufu, nilitoweka.”
Nilicheka sana. Kwangu ilikuwa habari ya kusisimua sana. Ilinisisimuazaidikumsikiababu,kwamarayakwanza,akisimulia tukio lililomuhusu kwa kirefu kiasi hicho. Mara nyingi yeye alikuwa mtu wa simulizi na kujibu maswali kwa mkatomkato. Nilikuwa na kila sababu ya kumhurumia babu. Kwa upande mwingine, maelezo yake yalizidi kunithibitishia jambo moja kubwa; umuhimu wa elimu. Lakini mara nikakumbuka kuwa babu alikuwa hajafikia au kugusia kiini cha maelezo hayo. Sababu ya kulala kwangu kwake na kuchinjwa kwa jogoo wake bora kuliko wote; kwa kila hali kulihusiana na
majonzi aliyokuwa nayo babu. Nikamkumbusha hilo.
“Nakumbuka vizuri sana,” Babu aliniambia. “Lakini,” aliongeza. “Kama nilivyosema awali unahitaji kuwa na kifua. Taarifa nitakayokupa huenda ikakutisha au kukuogofya. Lakini unatakiwa kupokea kama mwanamume na kuichukulia kwa upande wa pili kama msukumo wa ufunguo mpya wa maisha yako.”
Niliona kama babu anazidi kunichanganya. Nikamtumbulia macho ya mshangao na kumtegea sikio kwa makini.
“Inabidi uondoke kijijini hapa mara moja,” babu
aliniambia ghafla.
Kati ya yote niliyotarajia, hilo la kuondoka halikuwemo katika mawazo yangu, “Nani? Mimi!”
Babu akakubali. “Kwa nini?” “Wanataka kukuua.”
Sikuyaamini masikio yangu, “Wanataka kuniua mimi, watu gani hao?”
“Wanakijiji. Wakazi wa eneo hili.”
Bado sikumwelewa babu. Nilihisi huo ulikuwa utani wake mwingine, pengine kwa nia ya kupima ujabari wangu. Ili kumthibitishia hivyo niliangua kicheko na kumwambia taratibu, “Babu acha utani huo. Unanichulia kifo.”
Lakini macho ya babu yalikuwa hayana utani wala mzaha wa aina yoyote alipoongeza, “Wanataka kukutoa kafara. Lazima uondoke haraka iwezekanavyo.”
* * *
Kwa takribanimiakamitatuiliyopita eneo letulilikumbwa na ukame. Mazao yaliyopatikana yalikuwa machache sana. Mimea mingi ilinyauka, hata baadhi ya vyanzo vya maji vilianza kukauka. Mbaya zaidi ni pale ilipoonekana wazi kuwa mwaka huo pia hakukuwa na dalili ya mvua.
Zaidi ya tatizo hilo la ukame lilikuwepo tatizo jingine kubwa zaidi, tatizo la ugonjwa wa malale. Eneo kubwa la mapori na misitu iliyovizunguka vijiji vyetu ilikuwa na mbung’o wengi sana ambao walidaiwa kusababisha malale. Mbung’o hao walianza hata kuvamia mifugo iliyokuwemo zizini na hivyo kusababisha maradhi ya usingizi na hatimaye vifo vya ng’ombe wengi. Wala haikuwa mifugo pekee. Zaidi ya watu wanane kijijini hapo walikuwa wamekwishakufa kwa malale huku wengine wasiopungua ishirini, wakiugua ugonjwa huo ambao haukusikia dawa.
Kwa mujibu wa babu, Mwami, wasaidizi wake na wazee wenye busara kijijini hapo waliketi vikao vingi kujadili namna ya kupambana na matatizo hayo bila mafanikio. Hali