THE SPIRIT THINKER
JF-Expert Member
- Sep 9, 2019
- 419
- 652
Nipo Kagera leo umenionyesha historia ya kweli
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ngj niagize alkhasus yangu hapa na miogo mibichi kusubiri jukwaaSEHEMU YA 44 & 45
yake. Jambo hilo liliifanya serikali ya mkoloni imkamate na kumhukumu kunyongwa. Lakini hakuna aliyethubutu, kwani kabla ya hukumu hiyo kutekelezwa alifungwa katika kimojawapo cha visiwa vidogovidogo vilivyo baharini katika pwani ya Bahari ya Hindi, huko Dar es Salaam. Hata hivyo, ilielezwa kuwa Ng’wanamalundi huyo kila jioni alionekana katika vilabu vya pombe Dar es Salaam akiwa amevuka bahari kwa kutembea juu ya maji. Wakoloni wakalazimika kumwachia.
Sifa nyingine ya nchi ya Wasukuma ni zile hadithi kuwa kulikuwa na milima ya mawe, ama majini ama nchi kavu. Baadhi ya milima hiyo ilielezewa kuwa ilikuwa katika maumbile ya binadamu, ikiwa imesimama miaka nenda rudi kama inayosubiri mwujiza fulani utokee, ili ipate uhai na kuanza kutembea kama binadamu wengine.
Nchi hiyo pia ilikuwa ikisifiwa sana kwa ukubwa wa ardhi na wingi wa rutuba yake. Kilimo cha mazao ya chakula na yale ya biashara kama pamba na katani kilielezewa kuwa hakikupata kumtupa mtu. Kwa bahati mbaya, mimi sikupata kuwa mkulima wa haja. Wala sikuona kama ningeweza kuwa na ustahimilivu wa kulima leo kusubiri mavuno miezi au miaka kadhaa baadaye. Mimi nilikuwa mtu wa maji. Mtu wa kutupa nyavu na kuzitupa huku tayari zimejaa samaki! Hivyo, sababu kubwa iliyonipa msukumo wa kutamani kufika huko hasa lilikuwa ziwa. Jiografia yangu ilionyesha kuwa Wahaya na Wasukuma walichangia ziwa hili. Wakati Wahaya wakiwa Magharibi wakilitumia kwa shughuli zilezile.
Kwa kuzingatia hali yangu ya kutokuwa na kazi wala ujuzi wowote wa kuweza kupata ajira nyingine nililichukulia ziwa hili kuwa mkombozi wangu pekee. Nilitegemea ziwa
liniajiri, linilee, kwani taaluma ya uvuvi niliyoipata katika likizo zangu ilitosha kabisa kunipatia ajira hiyo.
Ni kwa mtazamo huo ndipo nilipojikuta nikijiunga na vikundi mbalimbali vya uvuvi kwa lengo la kujipatia fedha. Siku zote za uvuvi wangu nilifuata ziwa kuelekea upande wa kushoto kwangu badala ya upande wa kulia. Kama ningeelekea kushoto, ningelazimika kufika Uganda na baadaye Kenya, kabla ya kuingia Tarime, Musoma, Bunda hadi kufika Mwanza. Ingekuwa safari ndefu isiyo na sababu yoyote.
Mimi nilielekea kulia. Nilivua katika pwani na visiwa mbalimbali kama Bambire, Iroba, Rubondo na Nyamiende. Ilikuwa safari ndefu na ngumu sana. Takribani mwaka mzima uliishia njiani. Ama nilikwamishwa na ukosefu wa majahazi yanayoelekea huko nilikokuwa nikielekea, ama upepo mkali wa siku kadhaa ziwani ulifunga kabisa njia. Msimu wa masika ulioambatana na mvua kubwa za radi na mingurumo ya kutisha ni miongoni mwa sababu nyingine iliyonichelewesha njiani. Nililazimika kusubiri kwa zaidi ya miezi minne katika kijiji fulani huko Biharamulo.
Urefu huo wa safari ulikuwa na faida moja. Kwanza, ulinipa fursa ya kupata ukomavu na uvumilivu mkubwa katika pilikapilika za ziwani na nchi kavu. Ningeweza kuvumilia mvua ya siku mbili au tatu ikinipiga mwilini, niliweza kustahimili jua kali linalochoma kama mkaa wa moto. Niliweza pia kuipuuza njaa kwa muda mrefu. Zaidi, mwili wangu ulijenga uwezo mkubwa wa kuyashinda maradhi madogomadogo kama homa au tumbo bila haja ya kutumia dawa za madukani au mitishamba tele niliyopata kuelekezwa na babu.
Faida nyingine kubwa niliyoipata kutokana na urefu wa safari hiyo ilikuwa udugu. Nilikutana na watu mbalimbali,
nikashirikiana nao kwa hili na lile na kujikuta nimepata ndugu na marafiki tele, ambao kila nilipoondoka kuendelea na safari yangu walisikitika sana, lakini haikuwa kabla ya kunitakia kheri na baraka za safari.
Nilikosa raha kiasi pale tulipofika kisiwa cha Kome tukikaribia kabisa Mwanza. Rafiki zangu hao walishauri tubadili mwelekeo na kwenda kwanza Ukerewe. Tulifika Nansio. Tukafanya shughuli zetu za uvuvi hapa na pale, katika kijiji hiki na kile hadi tukajikuta tumeingia katika kisiwa kingine kidogo kiitwacho Ukara.
Ulipata kuona au kusikia juu ya mawe yanayocheza muziki? Kama hujapata hata kusikia mwenzio niliyaona kwa macho yangu katika kisiwa hicho cha Ukara. Kisiwa hicho kina mawe yaliyokaa kiajabu ajabu. Mtu anaweza kufikiria kuwa yalipangwa na binadamu, kwani baadhi yako juu ya mengine, yakiwa yamegusana kwa sehemu ndogo sana lakini hayadondoki si kwa mawimbi wala dhoruba la ziwani. Nilikuwa nikiyakodolea macho mara kwa mara mawe yale hadi mwenzangu mmoja aliposema, “Unashangaa kuyaona yalivyokaa, jee ukiyaona yanacheza?”
Nilidhani ni mzaha. Tulipobishana jamaa hawa walinipeleka katika kijiji cha Kome, ambako tulipata mwenyeji aliyetupelekeka eneo la Kululibha yalipo mawe haya ya ajabu. Mwenyeji wetu alitoa amri kwa lugha yake ya Kikara. Mara mawe hayo yakaanza kucheza kama watoto mapacha moja juu ya jingine. Hadi leo sijui ni kitu gani kinachotokea hadi mawe hayo yamtii binadamu.
Lakini huo si muujiza pekee wa Ukara. Pale kijijini kuna kisu chenye makali pande mbili. Unapotokea uhalifu wa aina yoyote watuhumiwa hupelekwa kwa mtaalamu na kuamriwa
ITAENDELEA
Asante mkuuSimulizi nzuri
tuko pamoja mkuuNipo Kagera leo umenionyesha historia ya kweli
Inafika mwisho mkuuHii hadithi ishawai kutumwa Umu ndani lakini muwasilishaji hakuimaliza tunaomba uimalize tafadhali [emoji120]
🔥 🔥 🔥[emoji106]
Tuendelee sasaNgj niagize alkhasus yangu hapa na miogo mibichi kusubiri jukwaa
Tuko pamoja arifSEHEMU YA 59 & 60
haikuwa imara kama awali.
“Popote,” nilimjibu kama awali.
Alitazama huko na huko kama anayetaka kuomba msaada. Kisha akasema, “Leo kuna treni mbili. Moja inakwenda Kigoma, itapita usiku. Nyingine inakwenda Mpanda, itaondoka hapa baada ya nusu saa.”
Nipe ya Mpanda.” Nilisema bila ya kufikiri sana.
“Shilingi tano, njia moja.”
“Nipe,” nilimjibu nikimlipa. Nikapokea tiketi na chenji zangu na kuzitia mfukoni. Nikaenda mgahawa mmoja uliokuwa karibu ambapo nilinunua wali kwa maharage, nikayashushia kwa chai ya rangi. King’ora cha abiria wa treni ya Mpanda kilipolia nilikuwa mmoja wa abiria wa kwanza kuiparamia.
* * *
Sikuhitaji kufikiri sana kabla ya kukata tiketi hiyo kwa sababu nyingi. Kwanza, nilikuwa na hisia kuwa Tabora haukuwa mji wangu wa bahati. Kuumbuliwa na mkuu wa shule kwa kiwango kile kulinitia doa na dosari kubwa iliyofanya nijisikie aibu isiyo na kifani. Mimi sio yatima. Nina baba na mama. Nina babu mwerevu kuliko mamia ya mababu ninaowajua. Kiu ya elimu haikuwa sababu nzuri ya kunifanya nikubali wazo la kipuuzi la kufanywa mtoto wa kambo wa Chifu Masanja.
Ni wazo hilo lililofanya nitupilie mbali wazo la kurejea Usukumani. Ningemwambia nini Chifu?
‘Nimebainika. Mtoto wako halisi yuko shuleni, kwa hiyo nitafutie hifadhi mpya!’ Aibu iliyoje. Ningemwambia nini mkewe na watumishi wa himaya yake ambao bila shaka wengi waliijua kinachoendelea?
Ndipo nilipowaza juu ya kurudi nyumbani. Nipande garimoshi hadi Kigoma, huko nitafute njia ya kufika Kasulu. Huenda tayari kulikuwa na malori ambayo yalibeba watu na mizigo kama sehemu nyingine za nchi.
Hata hivyo, hilo pia sikulitekeleza kwa sababu tele. Moja ilikuwa aibu. Mwanamume akitoka ametoka. Akirudi ana kitu cha kuonyesha kijijini. Ama vyeti vya kuhitimu masomo yako ama fedha au mtaji au kujenga nyumba bora zaidi. Mimi ningerudi na aibu tupu. Sikuwa tayari kufanya hivyo.
Sababu nyingine iliyonizuia kwenda nyumbani ni babu yangu. Ni kweli alinipenda sana na angefurahi sana kuniona. Lakini sikupenda kujitokeza mbele yake kichwa kitupu, mikono mitupu. Alitegemea nirudi na elimu. Alitegemea nirudi na mali. Kamwe asingefurahi kuona nikirudi mnyonge, kama kinda la ndege, linalotegemea mama akutafutie, akutafunie, umeze.
Lakini kuna sababu nyingine, kubwa zaidi, iliyonifanya nisijisikie kumtazama babu machoni. Hirizi yake. Hirizi hiyo ya familia, ambayo kwa mujibu wa maelekezo yake ilivaliwa na babu yake, baba yake na kisha yeye mwenyewe. Hirizi ambayo ilimpeleka Ughaibuni na kumrejeshha salama. Naam, hirizi ambayo aliivua na kunivisha mimi, badala ya baba, ili nipate kile ambacho aliamini kingeinua ukoo na familia yetu.
Hirizi ambayo niliipoteza kwa uzembe!
Haikuwa kweli kuwa chanzo cha migogoro yangu hii mipya, ikiwa pamoja na kukataliwa nafasi ya kusoma, kwa namna moja au nyingine ilihusiana na kupotea kwa hirizi ile? Mara kwa mara niliwaza.
* * *
Gari moshi liendalo mpanda hulazimika kueleka magharibi kwa kilometa kadhaa kabla ya kuchepuka kuelekea kusini. Kwangu mimi ilikuwa sawa na kuelekea nyumbani, Kigoma. Tuliiacha stesheni ya Tabora, tukatafuna reli hadi Usoke. Toka hapo tuliingia Urambo. Tuliacha Urambo na kufika Kaliua ambako tulianza safari ya kusini.
Kama ilivyokuwa safari ya kutoka Mwanza safari hii pia ilikuwa sawa na kusafiri katikati ya bustani ya Eden. Kila upande tulizungukwa na ama misitu minene iliyoashiria kila aina ya hazina, ama mapori ya kutisha yaliyoonya juu ya wingi wa mbolea katika ardhi yake.
Mara kwa mara tulipishana na wanyama ainaaina waliokuwa kando wakitushangaa, pamoja na ndege ainaaina walioruka hapa na pale juu ya miti, wakifaidi asali ya maua na wadudu wadogowadogo. Baadhi ya maeneo kulikuwa na mabwawa makubwa yaliyoshawishi kilimo cha mpunga au mito ambayo ilinikumbusha samaki wa ziwa Nyanza.
Toka Kaliua tuliingia Mfulu, baadaye Ugalla na hatimaye tukawasili Mpanda. Huo ulikuwa mwisho wa reli hii, lakini haikuwa mwisho wa safari yangu.
Pamoja na shahuku yangu kubwa ya kuondoka Tabora, ndoto yangu ya kuja Mpanda ilikuwa na malengo yake. Zilikuwepo fununu za hapa na pale kuwa maeneo mbalimbali ya huku yalikuwa dhahabu. Uchimbaji wa dhahabu hiyo sikuona kama kwa namna yoyote ile ungenishinda. Kuchimba udongo hadi ufikie mchanga maalumu kuchekecha mchanga huo hadi uone chembechembe za dhabahu na kuiokoteza, vipi kungenishinda?
Hilo lilikuwa wazo la kwanza. Wazo la pili, ambalo nilikuwa na hakika nalo zaidi ni uvuvi. Toka Mpanda hadi
Ikola au Kerema ambayo ni miji ya kandokando mwa ziwa Tanganyika haikuwa safari ndefu. Ningeweza kufika huko hata kwa miguu. Nilipanga, kama kazi ya kuchimba dhahabu ingeshindikana ningeelekea huko na kujiunga na uvuvi. Ndiyo, nasikia ziwa Tanganyika lina kina kirefu kuliko maziwa yote duniani. Kama kuna ukweli kwa hilo bila shaka samaki wake pia ni wengi zaidi na watamu zaidi. Ningekuwa mmoja kati ya walaji wake. Wala nisingeishia kula tu; samaki hao wangenipatia fedha za mtaji ili nirudipo kwetu nirudi kishujaa. Hivyo ndiyo ilikuwa ndoto yangu. Kwa bahati, nzuri au mbaya, haikwenda kama nilivyotarajia. Hali hiyo ilitokana na kukutana kwangu ana kwa ana na mtu ambaye sikutarajia kamwe kumwona tena katika maisha yangu, mtu ambaye sikupata hata kulifahamu jina lake. Alikuwa mmoja kati ya wale Wamanyema wawili waliofuatana na Mwarabu katika safari yetu ya miguu toka Buha hadi kwa Wahaya, miaka zaidi
ya mitano iliyopita.
Ni yeye aliyeniona kwanza, “We mtoto wewe! Kama nakufahamu vile?”
Nikageuka kumtazama. Mara moja nilimkumbuka, “Mmanyema! Unafanya nini huku?” niliuliza kwa mshangao.
“Wewe je? Umefikaje huku?” Sikujua nimweleze nini. “Babu yako hajambo?”
Sikuwa na jibu. Nikainamisha uso kwa aibu.
Nadhani Mmanyema alisoma kitu fulani katika uso wangu, kwani alinitazama kwa muda kabla hajanikaribisha chai kwa mihogo ambayo alikuwa akiila. Nikapokea kikombe cha chai ya maziwa na kipande cha muhogo. Njaa iliyoanza kuninyemelea ikakimbia mara moja.
ITAENDELEA