Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #101
SEHEMU YA 79
aliyofikia kwa kukosa pesa za kulipia.”
“Ndipo alipofikia hatua ya kufanya kile ambacho kamwe hakupenda kukifanya, kujikabidhi mikononi mwa wanaume ambao waliuchezea mwili wake kama mzoga kwa malipo hafifu ambayo yaliandamana na kashfa. Ulikuwa wakati mgumu kuliko nyakati zote alizowahi kupitia, kulazimika kumkumbatia mwanaume yeyote; mbaya kwa mzuri; anayetisha kwa anayechekesha; anayetesa kwa anayesimanga; anayependeka kwa asiyependeka. Yeyote, mradi ana chochote ambacho kingemwezesha kuishi. Wote waliomfikia ingawa aliwalaki kwa tabasamu, lakini moyoni aliwachukia zaidi ya sumu. Alijua ni mbwa mwitu katika ngozi ya kondoo, haja yao si zaidi ya kuburudisha nafsi zao zenye kiu isiyokatika. Na alimchukia zaidi yeyote ambaye alijitia kumpenda na kusisitiza ndoa. Mtu wa aina hiyo alimwona kama chui ambaye alitaka kuwa na zizi la mbuzi mwituni. Aliona kheri aendelee kuwa jamvi la wote badala ya kigoda cha mmoja wao.”
“Wakati ulipotimu alijifungua mtoto mzuri wa kiume. Usiku uleule ambao alimzaa akafanya kile ambacho wasichana wote waliopotoka hufanya mara wapatapo mtoto asiyehitajika. Alimnyonga na kuutumbukiza mzoga chooni.”
“Hakumtupa mtoto huyo kwa ajili ya upotovu kama wasichana wengine ili aendelee kuitwa msichana badala ya mama, la. Wala haikuwa kwa hofu ya kushindwa kumlea ipasavyo. Kilichomfanya amtupe hasa ilikuwa kule kuona kuwa kazaa kiumbe mwingine wa kiume, kiumbe mwingine ambaye angeendeleza kanuni ileile ya kuwafanya wanawake watwana au vyombo ambavyo vililetwa duniani kumstarehesha mwanaume. Yeye ambaye anahitaji kuiondoa kanuni hiyo, yeye ambaye ameteseka kwa ajili ya kanuni hiyo, vipi akubali kutunza kiumbe mwingine wa kiume? Ni hilo ambalo lilimshawishi kuangamiza damu yake mwenyewe.”
“Kitendo chake kilifahamika kwa jirani ambao waliiarifu polisi. Msichana huyo alikamatwa na kufikishwa mahakamani ambako alikiri kosa lake lakini hakuruhusiwa kueleza hoja zake. Akahukumiwa kifungo cha miaka mitatu na kazi ngumu. Huko gerezani aliteseka sana. Alipofunguliwa alirejea mtaani, katika vichochoro vilevile vya Buguruni, Magomeni, Kariakoo na kwingineko. Hali ikiwa ngumu kiuchumi, wanaume waliadimika mno. Ikawa vigumu kuwaona wakimfuata kama awali. Hivyo, akawajibika kuomba kazi ya kuuza pombe kwenye mabaa mengi, akikutana na watu wengi. Kati yao alifahamiana na majambazi, wafanya magendo na wagongaji, kama ambavyo alikutana na mahakimu, walimu na wakulima. Wote hao walimshirikisha katika harakati zao za maisha na siri zao bila ya kujijua. Ndipo akapata fursa ya kuwafahamu majambazi wengi na mienendo yao.”
“Ni wakati ambao alikuwa ameajiriwa West Bar alipokutana na mtu ambaye kamwe asingeweza kumsahau, mtu ambaye alikuwa kisa hasa cha kuanguka kwake kimaisha, adui yake mkubwa, Ukeke Maulana. Hasira zikampanda ghafla na njaa ya kulipiza kisasi kumteka hata akamwendea na kumshawishi mapenzi. Alipolaghaika badala ya kupokea mahaba aliyoyategemea alijikuta akipokea pigo la kisu, pigo lililomtoa duniani.”
***
Joram aliisikiliza hadithi hiyo kwa makini sana, macho yake yakimtazama Suzana hali mikono yake ikishughulikia sigara moja baada ya nyingine. Msichana huyo aliposita na kuvuta pumzi kwa nguvu, Joram alijirekebisha juu ya kiti na kunong’ona jambo ambalo halikumfikia Suzana.
“Msichana huyo ni mimi, Joram. Mimi hapa. Na hiyo ni hadithi ya kweli inayohusu maisha yangu.” Baadaye alisema kwa sauti ndogo, iliyotofautiana na ile aliyotumia kueleza habari nzima.
aliyofikia kwa kukosa pesa za kulipia.”
“Ndipo alipofikia hatua ya kufanya kile ambacho kamwe hakupenda kukifanya, kujikabidhi mikononi mwa wanaume ambao waliuchezea mwili wake kama mzoga kwa malipo hafifu ambayo yaliandamana na kashfa. Ulikuwa wakati mgumu kuliko nyakati zote alizowahi kupitia, kulazimika kumkumbatia mwanaume yeyote; mbaya kwa mzuri; anayetisha kwa anayechekesha; anayetesa kwa anayesimanga; anayependeka kwa asiyependeka. Yeyote, mradi ana chochote ambacho kingemwezesha kuishi. Wote waliomfikia ingawa aliwalaki kwa tabasamu, lakini moyoni aliwachukia zaidi ya sumu. Alijua ni mbwa mwitu katika ngozi ya kondoo, haja yao si zaidi ya kuburudisha nafsi zao zenye kiu isiyokatika. Na alimchukia zaidi yeyote ambaye alijitia kumpenda na kusisitiza ndoa. Mtu wa aina hiyo alimwona kama chui ambaye alitaka kuwa na zizi la mbuzi mwituni. Aliona kheri aendelee kuwa jamvi la wote badala ya kigoda cha mmoja wao.”
“Wakati ulipotimu alijifungua mtoto mzuri wa kiume. Usiku uleule ambao alimzaa akafanya kile ambacho wasichana wote waliopotoka hufanya mara wapatapo mtoto asiyehitajika. Alimnyonga na kuutumbukiza mzoga chooni.”
“Hakumtupa mtoto huyo kwa ajili ya upotovu kama wasichana wengine ili aendelee kuitwa msichana badala ya mama, la. Wala haikuwa kwa hofu ya kushindwa kumlea ipasavyo. Kilichomfanya amtupe hasa ilikuwa kule kuona kuwa kazaa kiumbe mwingine wa kiume, kiumbe mwingine ambaye angeendeleza kanuni ileile ya kuwafanya wanawake watwana au vyombo ambavyo vililetwa duniani kumstarehesha mwanaume. Yeye ambaye anahitaji kuiondoa kanuni hiyo, yeye ambaye ameteseka kwa ajili ya kanuni hiyo, vipi akubali kutunza kiumbe mwingine wa kiume? Ni hilo ambalo lilimshawishi kuangamiza damu yake mwenyewe.”
“Kitendo chake kilifahamika kwa jirani ambao waliiarifu polisi. Msichana huyo alikamatwa na kufikishwa mahakamani ambako alikiri kosa lake lakini hakuruhusiwa kueleza hoja zake. Akahukumiwa kifungo cha miaka mitatu na kazi ngumu. Huko gerezani aliteseka sana. Alipofunguliwa alirejea mtaani, katika vichochoro vilevile vya Buguruni, Magomeni, Kariakoo na kwingineko. Hali ikiwa ngumu kiuchumi, wanaume waliadimika mno. Ikawa vigumu kuwaona wakimfuata kama awali. Hivyo, akawajibika kuomba kazi ya kuuza pombe kwenye mabaa mengi, akikutana na watu wengi. Kati yao alifahamiana na majambazi, wafanya magendo na wagongaji, kama ambavyo alikutana na mahakimu, walimu na wakulima. Wote hao walimshirikisha katika harakati zao za maisha na siri zao bila ya kujijua. Ndipo akapata fursa ya kuwafahamu majambazi wengi na mienendo yao.”
“Ni wakati ambao alikuwa ameajiriwa West Bar alipokutana na mtu ambaye kamwe asingeweza kumsahau, mtu ambaye alikuwa kisa hasa cha kuanguka kwake kimaisha, adui yake mkubwa, Ukeke Maulana. Hasira zikampanda ghafla na njaa ya kulipiza kisasi kumteka hata akamwendea na kumshawishi mapenzi. Alipolaghaika badala ya kupokea mahaba aliyoyategemea alijikuta akipokea pigo la kisu, pigo lililomtoa duniani.”
***
Joram aliisikiliza hadithi hiyo kwa makini sana, macho yake yakimtazama Suzana hali mikono yake ikishughulikia sigara moja baada ya nyingine. Msichana huyo aliposita na kuvuta pumzi kwa nguvu, Joram alijirekebisha juu ya kiti na kunong’ona jambo ambalo halikumfikia Suzana.
“Msichana huyo ni mimi, Joram. Mimi hapa. Na hiyo ni hadithi ya kweli inayohusu maisha yangu.” Baadaye alisema kwa sauti ndogo, iliyotofautiana na ile aliyotumia kueleza habari nzima.