SEHEMU YA 364.
Harufu iliofifia ya ‘Sanitizer’ ndani ya wodi hio ilifurahisha pua zao kwa kiasi fulani , huku ukimya pia ukitawala, Edna alikuwa akifikiria maneno aliongea Roma ya juu ya kunyofoa moyo wake na kumuonyesha jinsi anavyojisikia .
“Hakuna maneno mazuri Zaidi ya kuongea mpaka useme unataka kunyofoa moyo wako?”
“Unafikiri hata nikitumia maneno mzuri zaidi unaweza kunisikiliza na kunielewa , chukua maji na sukutua kidogo, ijapokuwa ndio umeamka lakini mwili wako uko sawa kwa sasa, lakini unapaswa kupumzika”Aliongea Roma huku akimkabidhi Edna maji kwenye chupa na aliipokea na kushuka kitandani.
“Roma siwezi kuendelea kukaa hapa , kuna mambo mengi napaswa kuyafanyia maamuzi , nitajiweka sawa na kurudi kazini”Aliongea na kumfanya Roma kupumua huku akiwa ameshika kiuno.
“Nilijua tu huwezi kunisikiliza”Aliongea huku Edna akiingia maliwatoni kujisafisha.
Roma alivyokuja hapo hospitali aliweka simu yake silence ili asipate usumbufu , hivyo ilibidi aitoe na kuangalia watu waliompigia , na alijiikuta akishangaa kwani kulikuwa na Missed call 11 za Nasra ,Tano za Monica , kumi na tatu za Dorisi , mbili za Diego na sita zikiwa ni za Amina.
Roma aliona aanze na Diego, lakini kabla hata hajaanza kupiga simu yake ilianza kuita na mpigaji alikuwa ni Nasra.
“Ooh! Hatimae umepokea simu , Roma Edna upo nae hospitalini , anaendeleaje , amepona , uko hospitali gani , nitakufa na mawazo mimi”
“Yuko sawa punguza wasiwasi , muda si mrefu nitamleta kazini , mbona umenipigia mara kibao ni kwa ajili ya hali ya Edna tu au kuna lingine?”
“Nipo kwenye wakati mgumu muda huu , waandishi wa habari wamejazana nje ya kampuni wakiuliza maswali na muda huu tena kuna mtu kavujisha habari Edna kapoteza fahamu na kupelekwa hospitalini , kila mfanyakazi anachanganyikiwa , Edna kama yuko sawa mrudishe kwenye kampuni ili kupoza hii hali , ikiendelea hivi Jumatatu tunaweza kufilisika”
“Naona bado hawajaridhika na matokeo na wanatusaka mpaka mwisho”Aliongea Roma , lakini simu haikujibiwa na ni makelele tu yaliosikika.
“Roma nitakupigia”Aliongea Nasra na kukata simu.
Roma baada ya kumaliza kuongea na Nasra alimpigia Diego ili kujua kile ambacho kinaendelea .
“Diego how is analysis and investigation that I made you do?”Aliuliza akimaanisha kwamba vipi kuhusu uchunguzi pamoja na majaribio aliompatia afanye.
“Your Majesty Pluto, I’m very sorry. Ernest Komwe background is slightly too complicated. I can’t compile anything of substance just yet. I need a bit more time. But as for the two things that you asked us to analyze, we’ve already gotten the result.”
“Mfalme Pluto , niwie radhi, Ernest Komwe ubini wake kidogo unaonekana kuwa na mkanganyiko , siwezi kuelezea chochote kwa sasa , nahitaji muda kidogo lakini kuhusu vitu viwili ulivyoniambia nivifanyie kazi nishapata majibu”
Roma alijikuta akishangaa kidogo mnara baada ya kusikia neno mkanganyiko kwenye maneno ya Diego, Roma anachojua ni kwamba Ernest Komwe alikuwa moja ya wafanyakazi wa Vexto, kampuni ya Yamakuza ndio ilimpendekeza Ernest Komwe kuja Tanzania kuwa CEO msaidizi swala ambalo lilikubaliwa na Edna.
“Diego kwanini taarifa yake ziwe za mkanganyiko , Ernest ni mfanyakazi wa kawaida tu ndani ya Vexto anashikilia cheo cha CEO msaidizi , kwanini taarifa zake ziwe ngumu kupatikana?”
“Mfalme Pluto hata mimi nilifikiria hivyo hivyo , lakini kwa namna tulivyoweza kutafuta taarifa tumegundua Ernest Komwe sio jina lake halisi na kabla ya kufanya kazi katika tawi la Vexto Kenya ashawahi kufanya kazi kwenye kampuni ya Yamakuza tawi la HongKong, CV yake pia inaonekana haipo sawa kabisa na taarifa zake nyingi zinaonekana kufanyiwa sana marekesbisho , ndio maana kuna mkanganyiko, Mfalme Pluto naomba unipe muda kidogo nifuatilie hili”Aliongea Diego
Roma hakutegemea swala la Ernest Komwe kuchukua muda kiasi hicho , kwani tokea jana Diego alikuwa akitafuta Habari za Ernest komwe , lakini hata hivyo aliona ampe muda Diego afanye kazi yake.
“Vipi kuhusu Ushahidi niliowaambia mkauchukue kwenye kampuni , majibu yakoje?”
“We’ve already gotten the results. There is poison in that coffee indeed. It is a substance similar to ‘tannin’ that can be found in tea leaves. When this kind of acid is combined with a certain extract from animal protein, for example a substance in the proteins of dogs, it will produce a type of carcinogen that destroys humans’ internal organs.”
“Tushapata majibu, ni kweli kwenye kahawa kulikuwa na sumu inayofanana sana na ‘Tannin’ ambayo inapatikana katika majani ya chai ambayo yana Acid ndani yake , Aina hio ya Acid ikiunganishwa na aina flani ya protini ambazo zinatoka kwa Wanyama , kwa mfano protini ya mbwa inadhalisha aina flani hivi ya chembechembe zinazosababisha ‘Cancer’ ambazo zikiingia kwenye mwili zinaharibu ogani za ndani”Aliongea halafu akaendelea.
“Pia tumegundua kikombe hakina tu hii ‘Tanin’ bali kina aina nyingine ya protini ambayo hatujafahamu ni ya mnyama gani , kwa lugha nyepesi mfalme Pluto ni kwamba kahawa hio ilikuwa ikdhamiria kumuua mnywaji”
“Pia mfalme Pluto sumu ya aina hii kwenye mwili inafanyakazi kwa muda mrefu sana na inatakiwa muhusika kuinywa karibia kila siku ili iweze kuleta madhara , kwa maana hio ninaweza kukadiria kwamba Madam Persephone alianza kuwekewa sumu hii kwenye kahawa wiki iliopita na kwa vyovyote muwekaji wa sumu atakuwa ni mtaalamu sana kwani aliweka kiasi kinachotakiwa na kinacholeta madhara kwa muda husika , ukijumlisha na namna tukio la kuvujinshwa kwa nyaraka lilivyotokea basi malengo yake ilikua ni leo”
Roma baada ya kusikiliza maelezo yote ya Diego , alijikuta ile hamu ambayo alikuwa ni kama ameisahau kwa muda ikianza kumtekenya , hamu ya kuona damu ya mtu ikimwagika, Roma alijiambia kama Edna alikuwa akinywa kahawa yenye sumu muda wote huo basi hawezi kumruhusu Monica kuendelea kuwa sekretari wa Edna kwa namna yoyote ile hata kama hahusiki.
Roma ile anakata simu , Edna alitoka maliwatoni , Edna baada ya kuona Roma alikuwa akiongea na simu ilibidi amuulize kama kuna kilichotokea.
“Vipi kuna dharula imetokea?”
“Kampuni inakuhitaji , waandishi wa Habari wanaonekana kujazana nje ya kampuni , tuondoke kama umemaliza”Aliongea Roma na Edna alitingisha kichwa na safari ya kurudi kazini ikaanza.
Roma wakati akiwa kwenye gari alijaribu kumpigia Amina ili kujua alikuwa na shida gani na ilionekana Amina alikuwa na wasiwasi tu ndio maana alipiga simu na Roma alijaribu kumtuliza.
“Ushajua nani kahusika na kuibiwa kwa nyaraka ndani ya ofisi ya Benadetha?”
“Muhusika anaonekana alijipanga kwa muda mrefu sana na anafanya mambo yake kwa umakini na muda wote anatuchora tu tunavyojihangaisha”
“Unamaanisha nini?”
“Hakuna kitu chochote kilichoibiwa kwenye ofisi ya Benadetha , bali aliiba sehemu nyingine , wakati huo huo akitufanya tuone ameiba ndani ya ofisi yake”Aliongea Roma na kumfanya Edna kushangaa.
“Tokea jana macho yetu yote yalikuwa kwenye sanduku la usalama ambalo lipo kwenye ofisi ya Benadetha na hio ni kwasababu kila mmoja anajua kulikuwa na kopi mbili tu na ni rahisi kuona kwamba wewe huwezi kunufaika kwa chochote kama nyaraka hizo utazivujisha , kwahio kila mmnoja wetu tukaamini upande mmoja tu , na hata tukafikiria labda kuna Camera ambazo zimefungwa ndani ya ofisi ya Benadetha pasipo kujua, hivyo ukiachana na kisanduku , akili zetu zilikuwa zikimtamfuta mtu ambaye anaweza kuingia ndani ya ofisi ya Benadetha na kuiba nyaraka hizo “Aliongea Roma
“Lakini si ndio ilivyo , kama sio kutoka kwenye ofisi ya Benadetha ni wapi , nina uhakika kabisa hazikuvuja kupitia ofisi yangu , ukiachana na Monica hakuna mtu mwingine ambaye anaweza kuingia kwenye ofisi yangu nikiwa sipo lakini pia sehemu yote karibu na sanduku hakuna aina yoyote ya Camera”
“Ngoja nimalize kukuelezea …. Ukweli hata mimi mwenywe niliingia kwenye mtego wa mwizi . alionekana kujipanga , na alionekana alikuwa akinifahamu mimi sana kabla hata hajaanza mpango wake au unaweza kusema amefanya vitu vingi kutuchanganya kabla ya tukio , muhusika alionekana kwanza siku kadhaa zilizopita alikuwa akitembelea sana ofisi ya Benadetha mara kwa mara bila hata ya kuwa na sababu za msingi na alihakikisha kila mtu anafahamu anatembelea ofisi ya Edna sio wafanyakazi tu hata kwa mimi mwenyewe”
“Mke wangu usiniambie haujamfahamu mtu mwenyewe ni nani mpaka hapo, nafikiri hata wewe pia umemshuku ndio alievujisha nyaraka na nadhani ndio maana hukuita polisi kufanya uchunguzi na ukaniacha mimi nifanye uchunguzi si ndio?”
“Unamzungumzia Ernest , maana ndio aliekuwa akitembelea ofisi ya Benadetha, pia alionekana kuwa na ukaribu nae mara nyingi na hili linajulikana kwa wafanyakazi wengi wa kampuni, ijapokuwa hata mimi nilikuwa nikimshuku lakini sikuweza kulitaja jina lake kwani hakuna ushihidi wowote kama amehusika”Aliongea
“Hakika hakuna ushahidi , hata nilivyoenda kuangalia rekodi za kamera na nikapiga mahesabu muda ambao angetumia kufungua sanduku na kuiba nyaraka havikuwa vikishabihiana kabisa , alichokuwa akikifanya ni kutufanya tufikirie wote nyaraka zimeibiwa kutoka ofisi ya Benadetha , wakati huo hakuwa na mpango wa kuiba kutoka kwenye ofisi yake”
“Kwahio unamaanisha kwamba yote aliokuwa akiyafanya ni mtego wa kutuchanganya , lakini hata hivyo amewezaje?”
“Hata mimi nilikuwa nikifiria vilevile , lakini nilichogundua sio binadamu alietusaliti bali ni mashine ya kutolea kopi ndani ya ofisi ya Monica”
“Mashine ya kutolea kopi! , unamaanisha kwamba Monica alitengeneza kopi nyingine? , hilo haliwezekani , nishakuambia nilisimamia mwenye kazi hio”
“Sikulaumu kwa kutolifahamu hili mapema , lakini sasa hivi mashine zote za photocopy zinakuja na ‘Internal Harddisk’ au ‘Solid state disk’(Kifaa kama memori ya simu), ukishamaliza kutoa kopi kuna taarifa zinahifadhiwa humo kama akiba, kwa mtaalamu wa komputa anchokifanya ni kutoa hio Hardisk na kisha kuchomeka kwenye tarakishi na baada ya hapo atatumia dakika kadhaa tu kupata taarifa zote , mambo kama haya yanatokea sana kwenye ulimwengu wa kijasusi watu kuiba taarifa kupitia mashine za kutolea kopi, ndio maana idara nyingi mashine nyingi zinazotumika hulindwa sana na wanabadilisha hizi hardisk kila baada ya muda au kuziharibu kabisa”
Edna alijikuta akipatwa na mshangao kupitia maneno ya Roma , hata hivyo ilikuwa sawa tu kwani mrembo huyo alisomea maswala ya biashara , hivyo yeye likija vifaa vya kieletroniki anachojua ni matumizi tu na sio vinavyofanya kazi.
“Lakini bado kuna swali moja , kama kweli ameiba kupitia ofisi ya Monica , ninachojua mimi chumba kinachohifadhia mashine kinafungwa mara baada ya Monica kutoka kazini”Aliongea Edna na Roma alitabasamu , aliona Edna hamfahamu vizuri sekretari wake.
“Mke wangu , kampuni yetu imejaaliwa warembo wengi , lakini katika wanawake wote warembo Ernest akaamua kutoka kimapenzi na Monica , amefanya hivyo ili kwanza Monica kuweza kumuamini”Aliongea Roma na kumfanya Edna kushangaa kwani Habari hio ilikuwa mpya kwake.
“Unamaanisha Monica na Ernest ni wapenzi?” Roma alitabasamu na kisha akamwangalia mke wake.
“Kwenye mashindano ya Kizazi nyota niliwaona wote wakiwa wameshikana kimahaba kwa Zaidi ya mara mbili , mara moja nilidhani labda walikutana njiani lakini walivyokuja kwenye fainali wakiwa pamoja ndio nilifahamu ni wapenzi , huwa nina tabia ya kuangalia watu wanaonizunguka kwa kila wanachofanya , hususani mahusiano ya mmoja na mwingine , hii inanisadia sana kwenye baadhi ya nyakati”
“Muwindaji kwenye ubota wako , eti inanisaidia kila wakati kwanini usiende moja kwa moja?”Aliongea Edna.
“Unamaanisha nini?”
SEHEMU YA 366.
Nasra alionekana kuulizia ni kipi afanye , kwani alikuwa akishindwa kufanya baadhi ya maamuzi kutokana na kwamba yalikuwa yakimtaka CEO mwenyewe na ndio maana akapiga simu , lakini Edna alimjibu kwamba yupo eneo la maegesho hivyo anapandisha juu na Nasra alionekana kupata ahueni.
“Roma unaruhusa yangu kumtoa Benadetha polisi , nataka arudi kazini anisaidie baadhi ya kazi zinazohusiana na idara yake”Aliongea Edna.
“Okey mke wangu, wewe kapambanie kampuni mengine niachie mimi lakini pia upunguze wasiwasi”Aliongea Roma.
“Wewe ndio wa kupunguza wasiwasi, kwani haitotokea siku nikashindwa kujihudumia kimatumizi kama nitafilisika , hivyo usiogope sana na kinachoendelea kwenye kampuni”Aliongea Edna na kisha alifungua mlango na kutoka na kumuacha Roma akimwangalia kwa nyuma na kujiambia kuna muda ni vizuri mwanamke kuweza kujitegemea , lakini muda mwingine mwanamke akijitegemea kwa kila kitu sio jambo zuri.
Roma wakati akigeuza gari alikuwa akiwaza baadhi ya mambo , kwa mfano aliwaza wanawake wake wote walikuwa wakiweza kujitegemea na hakuwahi hata kuwaza kutoa hata mia yake mfukoni kwa ajili ya kuwasaidia ijapokuwa sio kama hakuwa na uwezo wa kuwasaidia pesa, lakini kwa upande mwingine alijiona kuwa na bahati, ndio hata hivyo wanaume wengi hawapendi kuombwa pesa lakini wakati huo huo hawataki wanawake wakiwazidi wanaume kimapato ki ufupi sio mwanamke tu ambaye haeleweki bali hata wanaume muda mwingine hawaeleweki ni vile tu wanawake wanaongoza kwa kutokueleweka.
Dakika kadhaa tu alifika kituo husika cha magogoni , ambacho ndio sehemu ambayo Benadetha alikuwa amezuiliwa na kwakua hakupenda sana kudili na polisi ilibidi ampigie Mage simu na Mage alimuunganisha na polisi wa hapo atakaemuongoza.
Alivyotoka kwenye gari na kuingia kituoni aliweza kumuona Benadetha akiwa eneo la mapokezi na alionekana alikuwa akimsubiri kwnai alimpungia mkono huku akitoa tabasamu hafifu.
“Mr Roma unaweza kuondoka na Miss Benadetha asharuhusiwa tayari kwa maagizo ya Miss Edna”Aliongea moja ya polisi ambaye aliagizwa na Mage kumpa ushirikiano Roma na alishangaa kidogo , kwani aliamini kungekuwa kidogo na hatua za kufuata kabla ya kuondoka nae , lakini anakuta kila kitu kishakamilika.
Roma alimchukua Benadetha , hakupenda sana kukaa kituo cha polisi , alikuwa kama watanzania wengi wasiopenda kuonekana maeneo ya vituo vya polisi.
“Roma Boss Edna anaendeleaje , nasikia alipatwa na shida kiafya amepona?”Aliongea Benadetha akiwa ni mwenye wasiwasi na Roma alitabasamu.
Utofauti wa Benadetha na wafanyakazi wengine , pengine kama utamfananisha kati ya Nasra na Dorisi, Benadetha alikuwa ni mtu siriasi kwa kila anachokifanya na ukitaka umjue Benadetha tabia yake ni namna anavyoongea , hakuwa muongeaji sana lakini pia hakuwa mkimya sana ,alikuwa akipenda utani wakati mwingine lakini hata katika utani , maneno yake anakuwa ameyachuja sana , ni rahisi kusema kwamba alikuwa amebarikiwa na hekima kwani maneno yake yamejaa upole sana.
“Haumkasirikii boss wako kukulaza polisi mpaka muda huu, kwanin hata unajali afya yake?”Aliuliza Roma huku akimfungulia mlango wa gari kuingia na Benadetha alitabasamu kidogo.
“Siwezi kumkasirikia boss Edna, kwani amejaariwa roho nzuri , ijapokuwa amenileta kituoni jana lakini bado aliendelea kunijali”
“Umejuaje anakujali wakati amekulaza kituoni?”
“Wakati nakuja polisi nilikuwa na wasiwasi sana , lakini huwezi kuamini nimelala kama nipo hotelini tu licha ya kukosa uhuru , nililazwa kwenye chumba cha watuhumiwa VIP na jana Boss Edna alinipigia simu na kuniambia nivumilie walau usiku mmoja atafute muhusika, na mimi nilimuelewa anachomaanisha . nilipata chakula kizuri pia hata kuoga”Aliongea Benadetha na kumfanya Roma kushangaa kidogo , hakuamini ubabe wote ule wa mke wake wa siku ya jana , ulikuwa wa maigizo tu , kumbe alienda mbali mpaka kuhakikisha Maisha ya Benadetha kituoni sio magumu.
“Hata hivyo ni haki yako , tokea nifike kwenye kampuni , unaeonekana kuwa siriasi na kile unachokifanya mchango wako ni mkubwa na Edna anapaswa kukulinda kama mfanyakazi wake”Aliongea Roma na kuwasha gari na kulitoa mdogo mdogo , huku Benadetha akimwangalia usoni.
“Hongera pia kwa kuwa na mke mzuri kama Edna, ambaye ana kila kigezo”Aliongea Benadetha na kumfanya Roma kutabasamu.
“Hahaha.. Edna ni mwanamke mzuri ndio , lakini haimaanishi kama amekamilika kwa kila kitu , upendo wangu kwake unayafunika madhaifu yake yote na yeye hunivumilia”
“Hio sehemu ya mwisho ndio ninasisitizia”Aliongea Beenadetha.
“Ipi?”
“Kukuvumilia Roma”Aliongea Benadetha na kumfanya Roma kushangaa kidog.
“Wote tunajua unamichepuko mingi , Dorisi , Nasra, yule sekretarri wako , lakini Boss bado anakupenda hivyo hivyo, siamini ingekuwa mimi nipo kwenye nafasi yake ningejisikiaje”Aliongea Benadetha na kumfanya Roma na yeye kujiona mwenye hatia.
“Benadetha baba yako amenipigia?”Aliongea Roma na kumfanya Benadetha kushangaa .
“Amekupigia! , amepata wapi namba yako?”
“Nikuulize wewe , amenipiga mkwala huku akiniambia wewe ni mpenzi wangu kitu ambacho sio kweli”Aliongea Roma na kumfanya Benadetha kushangaa na kuona aibu kwa wakati mmoja.
“Baba sijui alikufahamu vipi , ila miezi miwili iliopita alivyokuja kututembelea hapa Dar alianza kuuliza kuhusu Habari zako , huku akiniambia ahakikishe unakuwa mkwe wake na alikuwa akiomba sana namba zako ila sikumpatia na nilimueleza sina mahusiano na umfanyakazi mwenzangu tu , lakini hakutaka kunikubalia , aliendelea kunisisitizia kwamba anahitaji akuite mkwe kila siku anavyonipigia simu”Aliognea Benadetha kwa sauti ndogo sana na kumfanya Roma kushangaa , lakini kwa Benadetha kuona aibu.
Roma alifikiria kwanza maneno ya Benadetha na kuona inawezekana Mzee Nguluma ni kweli anamfahamu yeye , ukizingatia kwamba alishawahi kujihusisha sana na maswala ya kibiasahara katika ulimwengu wa wahalifu , wakati akimsaidia Rose kudili na baba yake , hivyo aliamini huenda alimfahamu kupitia huko.
“Umesema baba yako anakuja kuwatembelea na kukupigia mara kwa mara?”
“Ndio baba aliachana na mama yangu wakati nikiwa kidato cha kwanza , ijapokuwa hawakuwahi kuoana kwa ndoa lakini walitambulika kama wanandoa , baba baada ya kuhamia Shinyanga ndipo mama alivyojua kuwa baba ana mwanamke mwingine huko Kahama na amezaa nae pia , ndio ugomvi ulipoanzia mpaka wakaachana , baba aliendelea kunilea kwa kutuma matumizi tu na mahitaji mengine”Aliongea Benadetha na sasa kumfanya Roma kuelewa , kwa jinsi Benadetha anvyoongea Roma aliona huenda hajui kama baba yake anajihusisha na madawa ya kulevya pamoja na kuwa na ushirikiano na makundi ya kigaidi huko Congo.
“Kwahio mama yako pia ameolewa hapa Dar?”
“Hajaolewa , mama licha ameachana na baba lakini bado anampenda na baba kila akija Dar analala nyumbani kwetu , lakini mama ukimuuliza atasema wameachana ,nikimuuliza kwanini analala kwetu kama wameachana anashindwa kujitetea”Aliongea Benadetha na kumfanya Roma kutabasamu.
“Unavyofanya kazi kwa juhudi nikajua una majukumu mengi kumbe baba yako anajiweza kiuchumi, au Benadetha kuna mwanaume unamlea nini?”Aliongea Roma kiutani na kumfanya Benadetha kucheka.
“Sina mwanaume mimi , kuweka juhudi kwa kila ninachokifanya ni kupigania ndoto zangu na sehemu pekee ambayo naona naweza kufanikisha ni kwenye kampuni ya Vexto”
“Unaamini vipi Vexto inaweza kuwa msaada mkubwa wa kutimiza ndoto zako?”
“Boss Edna amejipambanua mara nyigi sana juu ya ndoto zake za kuifanya kampuni ya Vexto kuwa kubwa kimataifa , ndoto zake haziwezi kutimia pasipo ya kuwa na msaada kutoka wetu , kampuni ya Vexto msingi wake kwanzia mwanzo ulijengwa na mwanamke na mpaka sasa kampuni inawafanyakazi asilimia themanini wote wakiwa ni wanawake , chochote kitakachokamilishwa na Vexto siwezi kukosekana ,ndoto yangu kubwa ni kuwa sehemu ya historia ya Vexto , kuwa sehemu ya wanawake waliofanikisa kampuni kuwa kubwa kimataifa”Aliongea Benadetha na Roma alitingisha kichwa kukubaliana nae.
Lakini wakati huo huo akimuona kweli Edna alikuwa kiongozi , kwani ukimwangalia Dorisi hana mpango wa kuondoka Vexto kabisa ,licha ya kwamba alikuwa na uwezo wa kufungua kampuni yake mwenyewe , ukimwangalia Nasra na yeye anaonyesha dalili ya kuendelea kudumu ndani ya kampuni ya Vexto kwa muda mrefu licha ya kwamba alikuwa na uwezo wa kuanzisha kampuni yake , kwa urahisi ni kusema kwamba Edna aliweza kuishinda mioyo ya wafanyakazi wake wote licha ya ukauzu wake.
Roma hakutaka sana kuingizia maswala ya mapenzi na Benadetha kabisa, alikuwa akijifahamu mwenyewe kwamba hakuna mwanamke ambaye alikuwa na uwezo wa kujizuia kwake kutokana na yeye mwenyewe alivyo.
Roma wakati akiwa chini ya mafunzo ya Master Chi kwenye jangwa la Gobi , alikuwa akikumbuka baadhi ya maneno ambayo alielezewa na Master wake na kubwa Zaidi ilikuw ni kumpa tahadhari Roma juu ya wanawake.
“Hii mbinu inahusina na namna ambavyo utaweza kuvuna nishati inayohusiana na Yang , kadri itakavyokuwa inatawala mwili wako ndio utakapokuwa unavutia Zaidi nishati ya Yin”Aliongea Master Chi huku kijana mdogo alievalia kitamaduni akiwa amekaa chini akifanya tahajudi kwa kuangalia jua linalozama upande wa magharibi”
“Master unamaanisha nini kusema nitavutia Zaidi Yin Energy?”
“Ijapokuwa Yang Energy inasimama kwenye maana ya vitu vingi lakini ukija katika ubinadamu inasimama kama nguvu ya kiume na Yin Energy inasimamam kama nishati inayozalishwa na mwanamke , siku zote nishati hizi mbili zinatofautiana lakini ni zenye kuvutana, ukikutana na mwanamke mwenye nishati Yin dhaifu na nishati yako ya Yang utammeza kihisia”Aliongea na kumfanya kijana kufumbua macho na kumwangalia Master wake kwa mshangao , lakini alijikuta akipigwa na kigongo cha mgongo.
“Sijakuambia ufumbue macho kabla ya giza , endelea kunyonya nguvu ya Yang inayozalishwa na jua linalozama “Aliongea kwa kufoka na kumfanya kijana mdogo kuendelea kufumba macho huku akiwa kama anasali .
Alichokuwa akijaribu kuelezewa ni kwamba kadri atakavyokuwa anazidi kunyonya nishati ya Yang na kadri itakavyojaa kwenye mwili wake, ndio itamfanya wanawake wenye nishati ndogo ya Yin kutomkataa kimapenzi katika maneno yake ya kumeza kihisia , hio ndio pointi yake.
Kila mtu anazaliwa na hii nishati ambayo wachina wameipa jina la Yang kwa upande wa wanaume , lakini pia Yin kwa upande wa mwanamke , nishati hizo kila mtu anazaliwa nazo lakini zinatofautiana mtu na mtu , wengine wanazaliwa zikiwa nyingi sana kwenye miili yao , kiasi kwamba aina ya watu hawa kwenye jamii unaweza kuwatambua kutokana na mvuto wao.
Lazima yupo mwanamke anaependwa sana kwenye jamii licha ya kuwa na tabia mbovu mbovu kwenye jamii yako , hio yote ni kutokana na kwamba amezaliwa na kiwango kikubwa sana cha hii nguvu asili ya Yin, hivyo akikutana na mwanaume ambaye ana nguvu hafifu za Yang ni lazima uingie kwenye mtego wake kwa namna yoyote ile na wewe mwanaume ambaye una nguvu chache za Yang huwezi kupindua.
Hivyo hivyo kwa wanaume kuna wale ambao wanazaliwa na nishati za Yang kwa kiwango kikubwa na hawa wanaume unaweza kuwatambua tu kwa jinsi walivyokuwa na mvuto kwenye mambo mengi , unaweza ukamkuta mwanaume yupo yupo tu , hana hela, hana mwonekano , hana kingine cha ziada kukushinda wewe unaejitahidi kujipuliza unyunyu na kuramba midomo, lakini likija swala la warembo anakuacha mbali na unaishia kusema tu huyu jamaa ana kamzizi kumbe siri ni nishati ya Yang.
Hao ndio watu waliozaliwa na hii nishati asili ya Yang , kwa maana kwamba mwanaume wa aina hio kila atakapokutana na mwanamke ambaye ana nguvu ndogo ya Yin basi mwanamke huyo atajishtukia tu yupo kitandani na kesho asubuhi unakuta analalamika amemsaliti mume wake au sababu zinginezo ambazo hazijui kwanini zimemfikisha kwenye kitanda cha mwanaume, lakini vile vile kwa mwanaume utakuta anajilaumu kuwa dhaifu mbele ya mwanamke Fulani na kujishutikia kufanya nae uzinzi yote hayo ni kuwa na nguvu dhaifu za Yang kwa mwanaume au Yin kwa mwanamke.
Sasa ili Maisha yako kuwa bora Zaidi aidha kwa mwanamke au kwa mwanaume ni kwa kuzinyonya hizi nguvu katika mazingira , kwani zipo kila mahali , japo inasemekeana sana Yang inapatikana kwa wingi kwenye jua linalochomoza na linalozama, utaweza kuipata kwa njia tofauti tofauti lakini sio kuota jua licha ya kwamba inasaidia wakati mwingine.
Ieleweke tunaposema Yang Au Ying ni nishati tu na haimaanishi siku zote imebeba upande wa mwanamke na mwanaume bali ni maneno hayo ndio yanayoashiria tu kwamba kuna aina hizo za nishati kwenye mazingira, kwa mfano ukija katika tafiti rasmi wanabailojia walienda mbali kwa kusema Yang And Yang ni sawa na kusema ‘Pheromones’?(hapa nenda google).
Hata hivyo ili uweze kupata mafanikio mazuri kwenye Maisha ni kuweza kubalansi hizi nguvu zote mbili hapo ndipo utaona zikikuletea faida.
Naam ilikuwa ni siku nyingine kabisa yaani jumapili , siku hii Edna alishindwa kabisa Kwenda kutembelea Watoto kutokana na kile kinachoendelea kwenye kampuni, ijapokuwa alirudi nyumbani lakini aliendelea kufanya kazi , upande wa Roma aliacha kwanza Kundi lake la the Eagles kuendelea na uchunguzi wao unaohusiana na taarifa za Ernest Komwe.
Macho ya kila mfanyakazi wa Vexto ilikuwa ni Jumatatu wakati soko la hisa litakapofunguliwa , kila mmoja alikuwa na wasiwasi na kile mabacho kitatokea, kwa upande wa Edna siku ya jumapili hakuwa na chakufanya, kwani bado hakukuwa na ushahidi wa moja kwa moja kusema nani kavujisha siri za kampuni , hivyo maamuzi namna ya kuokoa kampuni ilitakiwa kufanyika siku ya jumatatu, hali itakavyokuwa sokoni ndio atakavyoweza kufanya maamuzi , alishapokea simu za vitisho kutoka kwa wawekezaji wengi na washirika wa kibaisahra juu ya kuvunja mkataba na kampuni yake , lakini aliwahakikisha kwamba anafanya kila liwezekanalo kuirudisha kampuni kwenye ubora wake.
Ikiwa ni muda wa jioni kabla giza la saa moja halijafunika anga la jiji la Dar es salaam , Roma aliweza kupokea simu kutoka kwa Diego.
“Vipi umepata chochote?”
“Mfalme Pluto niseme kwamba hata mimi nimeshangazwa , taarifa zake zinachanganya sana tofauti na nilivyofikiria? Ijapokuwa taarifa tuliokuwa nayo haijathibitishika bado , lakini tumegundua kuna uwezekano madam Persephone na Ernest wakawa ndugu kwa upande wa Mama”Aliongea Diego na kumfanya Roma kushangaa kidogo.
“Unasema kweli?”
“Ndio mfalme Pluto , siwezi kukuelezea kila kitu , ila nitakutumia faili kwa njia ya Email usome”.
“Kama ni hivyo fanya haraka”Aliongea Roma na wakakamilisha maongezi na dakika hio hio faili liliweza kuingia kwenye simu yake kubwa kupitia email.
Roma alieketi kwenye masofa kwenye sebule ya juu , alijikuta uso wake ukibadilika badilika kadri alivyokuwa akisoma faili ambalo limetunwa na Diego , kuna muda alikuwa akishangaa , kuna muda alikuwa na wasiwasi na kuna muda alirudi kwenye mshangao , alitumia dakika kama kumi na moja tu kupitia faili lote na kwa hasira aliweka simu yake pembeni na kuendelea kuangalia runinga.
Ilikuwa ni siku nyingine kabisa , saa kumi kamili za asubuhi ndani ya kampuni ya Vexto Edna na wafanyakazi wengine walikuwa washafika kwa ajili ya kuanzisha mapambano ya kuokoa kampuni.
Soko lilikuwa lishafunguliwa masaa kadhaa yaliopita na kwa maelezo ya Nasra ni kwamba hali ilikuwa mbaya Zaidi kuliko livyotegemewa , kwani hisa zilikuwa zikishuka mno thamani na wawekezaji wengi walikuwa wakizutoa sokoni.
“Edna , if this goes on, within less than half an hour our stocks would plummet through the twenty-percent baseline!”
“Edna kama hali itaendelea hivi ndani ya nusu saa ijayo hisa zitashuka thamani kwa asilimia ishirini Zaidi”Aliongea Nasra wakiwa ndani ya chumba cha idara ya masoko wote wakiwa wamesimama wakikodolea macho tarakishi ambazo zinaonyesha namba namba tu , kama hujasomea uchumi kinachoonyeshwa hapo ndani utaona nyota nyota tu , lakini kwao kila kitu kilikuwa kikijieleza kwa lugha ya kiuchumi Zaidi.
Edna aliesimama , akiwa na uso wake wa kupendeza aliendelea kuangalia soko , huku akisoma kila namba inayoonekana kwenye skrini huku karamu yake ikiwa imegusa lipsi za mdomo , licha ya kwamba alionekana kuwa na wasiwasi , lakini alionekana alikuwa akifikiria.
Kulikuwa na wafanyakazi Zaidi ya saba ndani ya ofisi hio ambao wote walikuwa ndani ya ofisi moja na Edna , huku upande wa idara nyingine wafanyakazi walikuwa washafika kazini muda mrefu tu , tena kuna wengine hawakuondoka kabisa kurejea nyumbani hususani idara ya Finance ambayo ilikuwa ikisimamiwa na mwanamama aliefahamika kwa jina la Elizabeth Mlowe.
“Miss Eliza , pass a message to the financial management department. When our share price falls to fifteen percent, purchase two to five thousand units using separate accounts. Repeat the purchase every ten to fifteen minutes. Alternate these purchases via at least a hundred accounts.”
“Miss Eliza , toa maagizo wa idara ya udhibiti wa feza , hisa zetu zitakaposhuka thamani kufikia asilimia kumi na tano, zinunuliwe hisa kwa mafungu yenye thamani elfu tano kwa kutumia akaunti tofauti tofauti , warudie mchakato huo kila baada ya dakika kumi na tano , hayo mafungu ya manunuzi angalau yawe katika akaunti mia moja”Aliongea Edna , hapa kwa wale ambao wanaelimu ya uchumi watakuwa wameelewa.
Anachomaanisha ni kwamba kuwe na akaunti mia moja ambazo kila akaunti inatakiwa kununua hisa katika fungu la thamani ya dola elfu moja au milioni mbili za kitanzania na zoezi hilo lifanyike kila baada ya dakika kumi na tano katika akaunti angalau mia moja, anachojaribu kufanya Edna ni kujaribu kuzinununa hisa kwa kutumia hela ya kampuni ili zisizidi kuporomoka thamani.
“Madam unasema?”Aliongea Eliza kionyesha kutokuelewa.
“Vipi tena , unataka nirudie?”aliongea Edna.
“Boss Edna , the problem is if we do that, it wouldn’t do any good for our current situation. There are tons of investors getting rid of our shares in the hundreds of thousands. We would hardly be doing anything to help the downward trend.”
“Boss Edna , tatizo tukifanya hivyo , haileti maana kutokana na hali ilivyo , kuna wawekezaji wengi ambao wanaziuza hisa zetu kwa mamia maelfu , , tutashindwa kushindana na soko linaloshuka thamani”
“Ninachokuambia ni kufanya kama nilivyokuagiza na sija kuomba unitolee maelezo”Aliongea Edna
“Edna najua una wasiwasi lakini alichokisema mkuu wa idara ya usimamizi wa Feza ni sahihi , hakuna sababu ya kufanya hivyo”
Hapa usichanganyikiwe, Nasra ni mhasibu mkuu wa kampuni na Eliza yeye alikuwa akisimamia idara ya fedha , tofauti ilipo kati ya hawa wawili ni kwamba idara ya fedha yenyewe inahhusika na maswala ya mipango na uelekezwaji wa miamala yote ya kampuni , wakati huo ofisi ya mhasibu inahifadhi na kutoa ripoti zote zinazohusiana na hio miamala , kwa mfano mtu wa finance atafanya miamala yote ya kampuni kutoa hela benki na kuziingiza , wakati huo huo mhasibu yeye kazi yake itakuwa ni kutunza kumbukumbu ya ile miamala pamoja kuitolea ripoti na mengineyo, katika baadhi ya taasisi idara ya fedha na uhasibu zinaweza kuwa sehemu moja au ofisi moja katika idara moja , lakini baadhi ya taasisi nyingine ni idara mbili tofauti hio yote ni kurahisisha kazi,lakini pia naweza kusema kwamba mtu wa ‘Fedha’ anaweza kuwa na majukumu mengi Zaidi kuliko mtu wa ‘mhasibu kwasababu mhasibu yeye anadili na namba tu pamoja na kumbukumbu wakati huo mtu wa fedha anakuwa na vitu vingi vya kuzingatia katika idara yake kuanzia kufanya tafiti juu ya taarifa zinazoendana na mipango ya kampuni na mengineyo.
“Ninafanya hapa linalowezekana kuhakikisha tunaidhibiti hii hali wakati huo huo tukisubiria kile ambacho Mungu ametupangia kuweza kukipitia siku ya leo, Nasra ninataka uwasiliane na watendaji wakuu wa benki zote ili kuhakikisha fedha zetu zinapatikana kwa wakati na katika mfumo wa taslimu”Aliongea Edna.
“Okey boss lakini kwanini tusiingize kiasi cha pesa Kwenda Athena , huenda wakatusaidia katika hili?”Aliuliza Nasra.
“Hatuwezi kuwatemegea ‘Traders’ kwenye swala kama hili , unaona kabisa hata wawekezaji ambao walinunua hisa zetu sikiwa na thamani ya juu wanaziuza kwa thamani ndogo , hii ni kwasababu wanajua wakiendelea kubaki nazo watapata hasara Zaidi , hivyo hata Athena hawawezi kushindana na mitazamo ya watu wengi kwenye soko la hisa ,wataishia kupoeza hela ya kampuni tu, I will discuss with the others to modify the issues of acquisition and allocation. We can do this”
Nasra ilibidi akubaliane na Edna , kwani hakuwa na pendekezo lingine zuri Zaidi kudili na hali.
Katika vyombo vya Habari vingi vilikuwa vikioanisha kwamba hasara Zaidi itatokea ndani ya kampuni ya Vexto baada ya matawi yote kufungua siku hio ya jumatatu, kampuni pekee ambayo ilikuwa ikitegemewa kutoathirika sana ni kampuni ambayo inaongozwa na Roma , Vexto entartaiment, hio ni kwamba bado kuna makubwa Zaidi yaliokuwa yakitegemeewa kupitia kampuni hio kutokana na kipaji ambacho alikuwa nacho Sophia , wananchi wengi walikuwa wakiegemea wimbo wa kwanza atakaoachia Sophia kwa kupitia Vexto Media , hivyo raia walikuwa wakiamini mauzo yatakuwa juu, sasa kampini nyingine za mavazi , ujenzi , uchakataji wa mazao na mafuta ulionekan kwend akuathirika sana.
Washindani wa kampuni ya Vexto wakati Edna akihangaika kuikoa kampuni wao walikuwa kwenye mahoteli wakinywa mvinyo mwekundu kwa kujipongeza kwa kile kinachoendelea, kila mmoja alikuwa akiamini Vexto inakwenda kufa kifo cha mende.
Upande mwingine wakati hayo yakiendelea , upande wa Bagamoyo kwenye moja ya Jumba la kifahari kinachoendelea ni ni srori nyingine kabisa.