Duh humu sisi nazani tutaimaliza hii story 2030..
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Duh humu sisi nazani tutaimaliza hii story 2030..
ukiambiwa alhamis we jua ni jumapili, hatunzi ahadi huyu jamaa....Alhamis
Sasa kama nikilipia nazipata zote mpaka hapo mlipoishia?
jamaa anajua ila ndo anatutesaaukiambiwa alhamis we jua ni jumapili, hatunzi ahadi huyu jamaa....
jamaa anajua ila ndo anatutesaaukiambiwa alhamis we jua ni jumapili, hatunzi ahadi huyu jamaa....
Bora tutulie tu akitaka ataweka, na cc tutasomaKuna story moja matata sana ya kijasusi humu inaitwa vipepeo weusi! Tulifuatilia kwa miaka miwili tangu 2016 mpaka 2018 ikawa inaendelea mpaka 2020 ndo tukakata tamaa haijaisha mpaka leo! Hata hii tutavumilia tu! Nimechungulia tangu imeanza! Jamaa bado ana moyo wa kutupostia! Ukweli ni kwamba sisi wa free basic na vi itel vya batan tunateseka sana! Kaka singanojr tafadhal fumbua macho utuone kama wale wa wasap tu! Tunateseka mno
Mtu chake mkuu! Acha tubembeleze! Hiki ndio kilevi chetu! Hatupigi mitungi wa mademu! Hatuvuti fegi wala njemu! Unadhani tunamwagilia moyo na nini? DaahBora tutulie tu akitaka ataweka, na cc tutasoma
vipepeo weusi iliisha ikaenda Hadi part two.Kuna story moja matata sana ya kijasusi humu inaitwa vipepeo weusi! Tulifuatilia kwa miaka miwili tangu 2016 mpaka 2018 ikawa inaendelea mpaka 2020 ndo tukakata tamaa haijaisha mpaka leo! Hata hii tutavumilia tu! Nimechungulia tangu imeanza! Jamaa bado ana moyo wa kutupostia! Ukweli ni kwamba sisi wa free basic na vi itel vya batan tunateseka sana! Kaka singanojr tafadhal fumbua macho utuone kama wale wa wasap tu! Tunateseka mno
OhooooooSEHEMU YA 379.
Licha ya Roma kuwa katika hali ya msisimko , lakini alijikuta akiuhusudu uwezo wa Omari kugeuza maji kuwa siraha , Roma alikuwa akielewa katika ulimwengu wa majini kila kitu kinaweza kugeuzwa kimaajabu na kuwa siraha. Lakini licha ya kusikia juu ya habari hizo hakuwahi kushuhudia kwa macho, licha ya kwamba alikuwa amejifunza mbinu za kijini kupitia kwa Master Chi hakuwahi kufika ujinini kabisa na kushuhudia majini ya levo za juu wanavyotumia uwezo wao kimaajabu katika mapambano, hivyo ni rahisi kusema kwamba Roma alikuwa na shauku sana yeye mwenyewe ya kujua akifika levo za juu ni uwezo wa aina gani ambao aataweza kuwa nao.
Omari hakutaka kumchelewesha Roma kwani baada ya kutengeneza donge la maji ambalo lilikuwa likizunguka kwenye mikono yake palepale aliligeuza na kuwa kama kitenesi cha barafu.
“Hades chukua hio?”Aliongea Omari na kisha kama vile mwanamke akicheza mpira wa rede alurusha kitenesi kile cha barafu kuelekea kwa Roma , upande wa Roma wala hakuwa na wasiwasi , kwani alijiambia ni rahisi sana kukwepa barafu huo kutokana na spidi yake tena alidharau kwa kitendo cha Omari kumrushia siraha ya kitoto namna hio.
Lakini ni kama Omari alikuwa akitegemea Roma kukwepa kirahisi na siraha yake ilipomkaribia Roma kama nusu nchi , palepale Omari alifanya maajabu mengine na kupasua kile kitenesi cha barafu na kugeuka vipande vya barafu vikiwa na mwonekano kama wa glasi.
Roma mwenyewe alijikuta akipatwa na kiwewe kwani hakutegemea kama Omari anaweza kufanya jambo la aina hio , kugeuza barafu kuwa kama vipande vya glasi , na kwakuwa yeye mawazo yake mwanzoni yalikuwa ni kukwepa hivyo alishindwa kukwepa vipande vyote kwa haraka na viwili kati ya vingi vilimchoma kwenye mwili wake katika eneo la kifua na kwenye paja la mguu
Roma alijikuta akijisikia maumivu yasiokuwa ya kifani , kwani kilichomchoma sio vipande vya glasi bali ni barafu hivyo ule ubaridi wake ulimletea maumivu makali sana.
Omari baada ya kuona baadhi ya vipande vilimpata na kumchana kwenye mwili , palepale alitengeneza kitenesi kingine cha barafu na ile anakamilisha , Roma ashatoa vile vipande na mwili wake ulikuwa ukijiponyesha kwa haraka sana , hivyo maumivu yalikuwa makali sana mwanzoni , lakini kadri muda ulivyokuwa ukisogea yalikuwa yakipona kwa haraka sana, hata kutoyasikia tena.
Roma alivyoona Omari anarusha tena barafu lingine kuja kwake aliona akifanya uzembe vipande vile vitampata tena hivyo alitumia uwezo wake wa kuhama sehemu moja Kwenda nyingine na jaribio lake lilileta faida kwani Omrri alivyorusha barafu lile kuelekea kwake alipotea sehemu aliokuwa amesimama na kuja kuibuka nyuma yake na kudhamiria kumpiga teke la ubavuni , lakini Omari alionekana kuwa na hisia kali sana kwani ile Roma anamkaribia kwa ajili ya kumpiga alitumia spidi kujiondoa na teke la Roma likapita.
Sasa ukumbuke huu ni mpambano wa kutumia mbinu za kijini peke yake yaani kwa maana rahisi Roma hakutakiwa kubadilika kabisa kama mwili wake ulivyotengenezwa.
“Hades kabla ya kuja hapa Tanzania nimejifunza mbinu zote ulizotumia kupambana na maadui wengi , hvyo nimejiandaa vya kutosha kukwepa mapigo yako”Aiongea Omari.
“Naona umenileta baharini kwa ajili ya kutumia maji kama siraha , lakini hii ni mbinu ambayo imepitwa na wakati dakika moja iliopita”Aliongea na kumfanya Omari kutabasamu.
“Hades unaonekana kutokufahamu mambo mengi sana kuhusu uwezo wa kijini , lakini kutengeneza barafu sio lazima uwepo wa maji , ninaweza kukusanya mvuke angani na kutengeneza barafu vilevile”Aliongea na palepale alianza kuinua mikono yake juu akiwa kama anajiandaa kupiga mbu hewani na palepale mikono yake ilitengeneza mvuke kama wingu na alianza kulizungusha lile wingu kwa kasi sana kama vile analipoza na palepale mvuke ule uligeuka maji na hatimae barafu kama kitenesi kwa mara nyingine.
Roma alijikuta akishangaa na kumfanya Omari kutoa kicheko.
“Umewezaje?”Aliuliza Roma na Omari alitabasamu.
“Hades katika mbinu za kichawi kile ambacho unanuia kwenye akili yako ndio unatengeneza kama siraha , ijapokuwa nipo kwenye levo ya Nafsi haimaanishi mtu mwingine ambaye yupo kwenye levo kama yangu atakuwa na mbinu sawa za kimajaabu katika kupambana , kila mtu anapata siraha kutokana na namna anavyofikiria”Aliongea Omari na palepale alipotea akiwa ameshikilia barafu lake na kuja kuibuka nyuma ya Roma , lakini akapotea tena na akaaja kutokea mbele yake tena na Omari akapotea tena na kutokea upande wa kulia halafu akapotea tena , lakini sasa jambo ambalo limemshangaza Roma ni kwamba baada ya Omari kupotea walitokea Omari wanne kwa pamoja wanaofanana kila kitu , yaani katika maeneo yaleyale ambayo alisimama na kupotea kwa mara nne mfululizo na Omari wote wa nne walikuwa wameshikilia vitenesi vya barafu, sasa kwa binadamu wa kawaida asingeona , lakini Roma aliona kwani hakuwa wa kawaida.
“Hahaha … Hades upo ndani ya mtego wangu kwa levo yako ni ngumu kutoka” waliongea Omari wote na kumfanya Roma kushindwa kumjua Omari halisi ni yupi kati yao , mpaka hapo alijua hao wote watakuwa feki na mmoja wao atakuwa ndio Omari mwenyewe , lakini alishindwa kujua haraka sana ni yupi kati yao , alijiona akiwa yupo kwenye duara.
Roma aliona hapo akizembea atamruhusu Omari kumuadhibu na pigo lingine , jambo ambalo hakuwa akitaka litokee kabisa na palepale alifumba macho yake na kuanza kufikiria kwa kutumia hisia kwa hali ya spidi sana.
Upande wa Omari aliekuwa amejigawa kwa sura nne hakutaka kumruhusu Roma kupata muda mrefu wa kufikiria , hivyo alirusha mabarafu yale yaliokuwa kwenye mfumo wa vitenesi kwa pamoja kumlenga Roma aliesimama katikati.
“Arrrgh…!!!” Ulisikika mguno wa maumivu na haukuwa ni wa Roma bali ulikuwa ni wa Omari mwenyewe.
“Hahahaha…!!”Roma alijikuta akitoa cheko la furaha mara baada ya kutegua mtego wa Omari.
“Mbinu yako ni ya kijinga sana , nikiri sikuwa na uelewa wa kutambua mtego wako kwa haraka sana , lakini baada ya kuelewa kuwa sura zako zote nne ni feki nikafikiria ni kwa namna gani unaweza kuzidumisha zote kwa pamoja na kuonekana kuwa halisi nikajua tu kuna namna ambavyo unazitawala”Aliongea Roma baada ya kumpiga pigo la ngumi Omari.
Sasa ilikuwa hivi baada ya mabarafu kurushwa kuelekea upande alipokuwa amesimama , palepale aliweza kufikiria namna ambavyo Omari aliweza kutengeneza sura hizo feki Roma aliona abahatishe kwa kuamini kwamba sura zote nne ambazo zimemzunguka ni feki , hivyo aliamini Omari atakuwa amesimama sehemu ambayo ataweza kuziongoza sura zote hizo na kuonekana halisia na ndio maana yale mabarafu yalivyomkaribia mkaribia alitoka pale aliposimama kwa spidi kali sana kuelekea juu katika mstaari mnyoofu huku akidharimiria katika akili yake kwamba lazima Omari atakuwa juu yake na ni kweli ile anafika mita kadhaa tu aliweza kuhisi uwepo wake na kuachia ngumi ambayo ilimpata vyema Omari na hatimae sura zake zote nne zikapotea.
Kitu kingine ambacho kilimfurahisha Roma ni kwamba kitendo alichokifanya ni kama kimemuwezesha kuelewa maana halisi ya levo ya Mzunguko kamili( muunganiko wa Yin na Yang).
“Umewezaje kugundua nipo juu Hades?”Aliongea Omari ambaye alikuwa akijiandaa kuachia pigo lingine.
“Ni rahisi sana mbinu uliotumia inaeleweka hata kisayansi, umetumia ‘Centripetal Force’(nguvu kati) kuweza kutengeneza na kuzidumisha sura zote nne zinazofanana kwa kila kitu na wewe , umefanikiwa kufanya hivyo kwa kutumia levo zote mbili , ya mzunguko kamili pamoja na ya Nafsi”Aliongea Roma na kumfanya Omari kutabasamu.
“Naona umevuka mtego huu lakini pia umeweza kutoka levo ya Nusu Mzunguko Kwenda Mzunguko mwingine hongera sana, fumbo linalokuja huwezi kulielewa na itakuwa ni mwisho wako , kwani nina kwenda kutumia uwezo wangu wa juu Zaidi”Aliongea Omari.
Ni kweli kabisa maneno alioongea Roma ni sahihi , unachopaswa kuelewa katika maswala ya kuweza kung’amua mbinu za kijini ni kwa kufumbua fumbo kwa namna ya kufikiria(meditation) , sasa kwa mfano mbinu ya kimaajabu aliotengeneza Omari ilikuwa ya kawaida sana kama utaifikiria kisayansi kwa kutumia kanuni za kifizikia , ilikuwa ni kama ‘Centripetal Force’(Nguvu kati) , hii ni kwa mfano pale mtu anapounganisha kitu kwenye Kamba na kuanza kukizunganisha juu kwa kasi na kutengeneza duara , sasa ndio alichokifanya Omari , kwamba alitumia mbinu za kichawi kumzunguka Roma kwa mara nne na kisha akajitoa kabisa kwenye zile nafasi na akaenda kukaa upande wa juu na akatengeneza umbo feki ambalo linamwakilisha yeye mwenyewe , sasa kuna namna ya kufanya mtu kutokuona mzunguko , hicho ndio kilichotokea , hivyo kitendo cha Roma kutoka nje ya duara aliweza kufumbua fumbo la levo ya Mzunguko kamili mwanzoni Roma alielewa levo ya Mzunguko kamili ilikuwa ipo ndani ya duara , lakini baada ya kutoka nje ya mtego wa Omari aligundua levo ya mzunguko ni lazima uwe nje ya mzunguko kutengeneza balansi.
Omari mwenyewe alishangazwa na uwezo wa Roma kuelewa mambo kwa haraka sana, kilichomfanya mara ya kwanza kujiamini ni pale alipoweza kuona Roma alikuwa katika levo ya chini kuliko yeye , lakini mtego aliomuwekea umemfanya kutoka levo moja Kwenda nyingine , sasa jambo hilo lilikuwa la kushangaza kwani yeye mwenyewe alichukua miaka Zaidi ya miwili kutoka levo ya nusu mzunguko Kwenda mzunguko kamili , lakini Roma yeye imemchukua muda mfupi sana.
“Nipo tayari kuona uwezo wako wote”Aliongea Roma.
“Usijindanganye kama unaweza kujifunza kitu kutoka kwangu , ijapokuwa umeweza kufanikisha kupanda levo moja Kwenda nyingine, lakini levo ya nafsi huwezi kuielewa kirahisi na kuifikia”Aliongea na kumfanya Roma kufikiria kidogo huku akikumbuka baadhi ya meneno ambayo alikuwa akielekezwa na mastar wake wakati wa mafunzo.
“Master ni zipi kanuni kubwa ya nguvu hizi?”Aliuliza kijana mdogo huku akimwangalia mchina aliekuwa mbele yake .
“Mbinu ninayokufundisha ina kanuni nne ambazo unapaswa kuzizingatia siku zote nazo ni namna nguvu zinavyopingana , zinavyotegemeana, zinavyovutana na zinavyopitia mabadiliko , unatakiwa kuelewa msingi wa hii dunia kila kitu kina uhusiano na kitu kingine na ndio maana halisi ya uwiano”
“Master je naweza kujua namna ya uhusiano kati ya kitu na kitu?”Aliuliza na kumfanya Master kumwangalia.
“Kifo na uhai ni mfano wa uhusiano ninaozungumzia”Aliongea na kumfanya kijana mdogo kuelewa.
Sasa Roma hayo ni moja ya mafunzo ya Master Chhi aliokuwa akimuelekeza ndani ya jangwa la Gobi na aliamini kwa fumbo lolote ambalo Omari anaweza kumtengenezea atatumia misingi ya dunia kuweza kufumbua.
Roma wakati akiwaza , alijikuta akishangaa mara baada ya kumuona Omari akifanya kitendo ambacho hakuwa amekitegemea , Omari alishika jicho lake la kushoto na sio kushika kwa kuziba bali alishika kwa namna ya kulitoa.
“Unataka kufanya nini?”Aliuliza Roma kwa wasiwasi.
“Hahaha.. Hades kama utabahatika kushinda basi nitakueleza namna ambavyo niliishi Maisha yangu kwa kutumia jicho moja tu baada ya kupata ajali”Aliongea Omari.
“Unamaanisha jicho lako la kushoto sio la kibinadamu?”
“Hilo ni jibu Hades , uliniuliza kwanini nimeweza kufikia levo za juu haraka ikiwa mimi ni binadamu , jibu langu kwako ndio hili , kitendo cha kuwekewa jicho la kondoo kwenye jicho langu la kulia ilihali siwezi kutumia kuona ilikuwa motisha kubwa san ilionipelekea kujifunza mbinu za kimatibabu za kichina” Aliongea na palepale alilinyofoa jicho lote nje na kulitupia baharini a kumfanya kubakia na jicho moja tu , huku sehemu ambayo ambayo ametoa jicho lile kukibakia shimo.
Kitu kingine Zaidi kilichomshangaza Roma ni kwamba baada ya Omari kutoa jicho lake ni kama mwili wake ulijaa nguvu isiokuwa ya kawaida ambayo ilikuwa ikimzunguka.
“Haya ni majaabu”Aliwaza Roma kwenye kichwa chake huku akimwangalia Omari ambaye anasambaza hewa iliojaa presha ya hali ya juu na kufanya mawimbi ya maji kuanza kuwa makubwa.
“Arrgh !!.. Arghhh , aargh”Roma alikuwa akilalamika kwa mapigo aliokuwa akipigwa na Omari , kilichokuwa kikimfanya Roma kihisi maumivu makali ni kitendo cha kuhisi mwili wake ni kama unachomwa na vijipini mithili ya sindano pande zote za mwili.
Jambo moja ambalo lilimsiadia ni kwasababu alikuwa akipona haraka na alijiambia kama angekuwa hana mafunzo ya nguvu za kijini za kimaandiko basi asingeweza kumudu mashambulizi ya Omari.
Omari mwenyewe alijikuta akishangaa kwa uwezo wa Roma kuhimili mvua ya sindano aliomtengenezea.
“Usishangae naweza kutokuwa levo za juu katika mbinu za kijini lakini mimi ni moja kati ya wachache walioweza kufanikisha kutumia nguvu ya kimaandiko ya urejesho isio na kikomo”
“Nimesikia sana kuhusu hio mbinu na ni ngumu sana kueleweka hata ndani ya jamii ya majini yenyewe lakini hata hivyo hainifanyi kushindwa hili pambano”Aliongea na palepale alitumia maji ya bahari kutengeneza upanga wa barafu, lilikuwa jambo la kimaajabu kweli na kumfanya Roma kutabasamu kifedhuli., Roma alikwepa sana kila pigo la Omari , lakini jambo moja ambalo lilimshinda kufanya ni kutengeneza maajabu ambayo yataweza kumshinda Omari kutokana na kwamba hakutaka kuvunja kanuni za pambano hilo , kwani ilikuwa ni sheria yeye kutumia mbinu za kijini tu kupambana.
Mpaka masaa mawili yanamalizika Omari alionekana kutengeneza kila aina ya maaajabu kutokana na levo yake , lakini kila linapomfikia Roma aliishia kulipangua au kuliacha limpige na kuruhusu nguvu ya kimaandiko kumponya kwa haraka.
“Hades nimeishiwa mbinu zangu zote za kijini na siwezi kushinda lakini pia siwezi kusema pambano hili ni droo kutokana na uwezo wako kuwa chini kuliko wa kwangu , hivyo kwa maksi nitasema umeshinda”Aliongea Omari na kumfanya Roma kutabasamu .
Ni kweli kabisa ijapokuwa Roma hakuweza kumpiga Omari kwa shambulizi lolote lakini kutokana na levo yake na alivyoweza kupangua kila pigo lililorushwa kwake inamfanya kuwa mshindi.
Roma mwenyewe hakuona kuna haja ya kuendelea kupambana , kwani kama wataendelea inaweza kuchukua muda mrefu na inaweza kumfanya kutumia uwezo wake nje ya wa kijini ili kumshinda Omari kuokoa muda , jambo ambalo hakutaka kufanya kwani angekuwa nje ya kanuni walizopanga kabla ya pambano, lakini jambo kubwa sana kwake usiku huo alipata kujifunza vitu vipya kupitia Omari.
*****
Adeline na Fanny haikueleweka walikuwa wamemuwekea nini Kizwe kwani licha ya kwamba alikuwa macho lakini mwili wake ni kama haufanyi kazi , ni kama vile mgonjwa ambaye amepalalaizi kipande cha chini, hivyo hata baada ya kukabidhiwa kwa wanaume waliokuwa mbele yake alishindwa kabisa kujitetea au kutumia mbinu yoyote kuwaepuka.
Hivyo kila kitu kilichokuwa kikiendelea kwenye mwili wake alikuwa akikiona wazi kabisa na alishindwa kuongea lolote kwani hata hivyo wanaume hao mafukara hawakuwa wakielewa lugha ya kingereza.
Upande wa wale wazungu mara baada ya kumkabidhi Kizwe kwa vijana kwa ajili ya kazi kuanza walipandisha juu kabisa darajani na kuanza kurekodi tukio zima linavyoendelea , hawakutaka kufanya moja kwa moja kwani waliamini wale mafukara wasingefanya kazi kwa ufanisi.
“Oya wadau kwenye Maisha yangu sijawahi kukutana na mwanamke mwenye Ngozi laini kama huyu , hii ni bahati ya mtende”Aliongea Tulo huku akijikakamua kushusha mzigo.
“Maliza fasta wewe fala acha sifa zako za kimama”Aliongea yule jamaa aliekuwa akiamshwa dakika kadhaa zilizopita , yeye zamu yake ilikuwa ni mtu wa tatu , yaani baada ya Tulo kumaliza.
Yaani kilchofanyika kilikuwa kitendo cha kikatili mno , kwani vijana wote walimbaka Kizwe kwa zamu mpaka kurizika na hawakujali sana baada ya hapo kitatokea nini , licha ya kwamba walikuwa mafukara ilikuwa ni rahisi kwao kuelewa mwanamke huyo alikuwa na matunzo ya hali ya juu kutokana Ngozi na yake jambo ambalo liliwafanya wafurahie mchezo.
Kizwe yote hayo wakati yanafanyika alishuhudia na kwakua hakuwa na uwezo wa kufanya chochote kutokana na mwili wake kuwa katika hali ya kupooza aliishia kutoa machozi tu , huku akimlaani Roma kwa kila laana anayoijua, aliamini yeye ndio kamleta hapo kwani mara ya mwisho alipozimia alikuwa kwenye jumba kule Bagamoyo na mtu pekee ambaye alikuwa na uwezo wa kumfanyia hivyo ni Roma.
Kzwe hakujua kama aliletwa hapo na wazungu , kwani baada ya kukabidhiwa kwa wabakaji hao waliondoka na hapo ndipo kizwe aliporejewa na fahamu licha ya mwili wake kukosa nguvu.
Wakati vijana wanamaliza shughuli kila mmoja kwa mizunguko mitatu mitatu wote walijikuta wakijichokea na kukinai na kuyasogelea maboksi yao na kumuacha Kizwe vilevile.
“Oya wadau , wale wazungu si walisema watatulipa?”Aliongea Tulo.
“Unatepeta sana mwamba kiakili , hakuna tena maswala ya mikwanja malipo tushayapata”Aliongea mwingine na kumfanya Tulo kuona kweli aliongea ujinga.
“Wazee Lekcha huyu hapa”Aliongea mwingine baada ya kumuona mwanaume aliebeba mfuko mkubwa akiingia hayo maeneo , mwanaume huyo walikuwa wakimuita kwa jina la Lekcha yaani Lecture au mkufunzi kwa kiswahiili , kilichowafanya kumuita mwanaume huyo ni kutokana na kwamba alikuwa akisifika mitaa yote hio ya uswahilini kwa uwezo wake mkubwa wa kuongea lugha ya kingereza , huku akijitapa siku zote kwamba amesoma sana kuliko Mtanzania yoyote na mama yake ni Malkia Elizabethi wa Uingereza na aliongea hayo yote wakati akiwa amelewa chakali sasa katika mazungumzo yake alikuwa akimalizia kwa kujiita yeye ni Lecture sasa waswahili wao wakambatiza namna yao ya kumita na kumpa jina la Lekcha
Lakini ilikuwa ngumu kwa wanajamii wote kumuelewa mwanaume huyo , ni kweli kwamba alikuwa akijua lugha ya kingereza , lakini kilichowashangaza wengi ni kwamba hakuwa na makazi na alikuwa ni fukara kama wengine na kazi yake kubwa ilikuwa ni kuokota chupa za maji au soda na Kwenda kuziuza.
Sasa siku zote bwana huyu hakuwahi kuitwa kwa jina lake halisi na watu wengi wanamfahamu kwa jina la Lekcha , yaani Lecture au Mkufunzi yote hio ni kutokana na kwamba alikuwa akiongea lugha ya kingereza sana , hususani wakati akiwa amelewa, huyu mwanaume watu wengi washawahi kumfatilia kutaka kujua ni wapi ametokea , lakini hakuna aliefanikiwa kujua ni wapi alitokea mpaka kuwa ndani ya maeneo hayo ya uswahilini ya jiji na kuwa kafara, hivyo watu waliamini huenda hakuwa na akili nzuri hivyo hata alipozaliwa amesahau , alikuwa mkubwa wa miaka kama arobaini hivi.
“Kuna nini kinaendelea hapa?”Aliuliza Lekcha mara baada ya kumuona mwanamke akiwa uchi pembeni ya hao vijana.
“Lekcha bwana mitikasi mingi ya nini , wakati kila kitu unaona , ni zamu yako na wewe kuukwea”Aliongea Tulo na kumfanya Lekcha kumsogelea yule mwanamke na mara baada tu ya kumuona vizuri kwa mwanga uliozalishwa na baadhi ya taa za nyumba za karibu alijikuta akisisimka mwili.
“Hahaha… Lekcha kumbe na wewe umo?” Walijikuta wale vijana wte wakicheka lakini Lekcha hakutaka kuwajali Zaidi ya kushusha suruali yake haraka haraka.
Upande mwingine barabarani mita kadhaa kutoka kwenye daraja hilo Adeline na Fanny walionekana kumaliza kazi yao ya kurekodi kila kitu.
“Fanny ijapokuwa Mfalme Pluto ana mbinu za kikatili likija swala la mateso , ila hii imezidi”Aliongea huku akikagua video iliokuwa ikionekana kwenye Camera.
“Nini tunakwenda kufanya baada ya hapa Adeline?”
“Mfalme Pluto amesema anataka kazi ya kisanaa Zaidi huu ni mwanzo tu , tunatakiwa kuendelea kufatilia”Aliongea na kumfanya Fanny kushangaa.
“Kinachofuata nini Adeline si kila kitu kishaisha tunazo hizi Vidio zinazo onyesha sura ya Kizwe kuna haja gani ya kuendelea Zaidi”
“Mfalme Pluto hajatuambia tuishie kwenye kurekodi tu , bali tuendelee kurekodi hatua zote atakazopitia ili kuifanya kazi kuwa ya kisanaa , kuhusu hizi tulizoweza kurekodi , nitamtumia asubuhi”Aliongea na Fanny alishindwa kupinga na kuondoa gari yao huku wakipanga kuendelea siku inayofuata.