Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Hahahahahahaha, daaaah!!! Eti 440,aiseeee! Nawaonea wivu walio wasap!!
 
Kuna story moja matata sana ya kijasusi humu inaitwa vipepeo weusi! Tulifuatilia kwa miaka miwili tangu 2016 mpaka 2018 ikawa inaendelea mpaka 2020 ndo tukakata tamaa haijaisha mpaka leo! Hata hii tutavumilia tu! Nimechungulia tangu imeanza! Jamaa bado ana moyo wa kutupostia! Ukweli ni kwamba sisi wa free basic na vi itel vya batan tunateseka sana! Kaka singanojr tafadhal fumbua macho utuone kama wale wa wasap tu! Tunateseka mno
 
Kuna story moja matata sana ya kijasusi humu inaitwa vipepeo weusi! Tulifuatilia kwa miaka miwili tangu 2016 mpaka 2018 ikawa inaendelea mpaka 2020 ndo tukakata tamaa haijaisha mpaka leo! Hata hii tutavumilia tu! Nimechungulia tangu imeanza! Jamaa bado ana moyo wa kutupostia! Ukweli ni kwamba sisi wa free basic na vi itel vya batan tunateseka sana! Kaka singanojr tafadhal fumbua macho utuone kama wale wa wasap tu! Tunateseka mno
Bora tutulie tu akitaka ataweka, na cc tutasoma
 
SEHEMU YA 379.

Licha ya Roma kuwa katika hali ya msisimko , lakini alijikuta akiuhusudu uwezo wa Omari kugeuza maji kuwa siraha , Roma alikuwa akielewa katika ulimwengu wa majini kila kitu kinaweza kugeuzwa kimaajabu na kuwa siraha. Lakini licha ya kusikia juu ya habari hizo hakuwahi kushuhudia kwa macho, licha ya kwamba alikuwa amejifunza mbinu za kijini kupitia kwa Master Chi hakuwahi kufika ujinini kabisa na kushuhudia majini ya levo za juu wanavyotumia uwezo wao kimaajabu katika mapambano, hivyo ni rahisi kusema kwamba Roma alikuwa na shauku sana yeye mwenyewe ya kujua akifika levo za juu ni uwezo wa aina gani ambao aataweza kuwa nao.

Omari hakutaka kumchelewesha Roma kwani baada ya kutengeneza donge la maji ambalo lilikuwa likizunguka kwenye mikono yake palepale aliligeuza na kuwa kama kitenesi cha barafu.

“Hades chukua hio?”Aliongea Omari na kisha kama vile mwanamke akicheza mpira wa rede alurusha kitenesi kile cha barafu kuelekea kwa Roma , upande wa Roma wala hakuwa na wasiwasi , kwani alijiambia ni rahisi sana kukwepa barafu huo kutokana na spidi yake tena alidharau kwa kitendo cha Omari kumrushia siraha ya kitoto namna hio.

Lakini ni kama Omari alikuwa akitegemea Roma kukwepa kirahisi na siraha yake ilipomkaribia Roma kama nusu nchi , palepale Omari alifanya maajabu mengine na kupasua kile kitenesi cha barafu na kugeuka vipande vya barafu vikiwa na mwonekano kama wa glasi.

Roma mwenyewe alijikuta akipatwa na kiwewe kwani hakutegemea kama Omari anaweza kufanya jambo la aina hio , kugeuza barafu kuwa kama vipande vya glasi , na kwakuwa yeye mawazo yake mwanzoni yalikuwa ni kukwepa hivyo alishindwa kukwepa vipande vyote kwa haraka na viwili kati ya vingi vilimchoma kwenye mwili wake katika eneo la kifua na kwenye paja la mguu

Roma alijikuta akijisikia maumivu yasiokuwa ya kifani , kwani kilichomchoma sio vipande vya glasi bali ni barafu hivyo ule ubaridi wake ulimletea maumivu makali sana.

Omari baada ya kuona baadhi ya vipande vilimpata na kumchana kwenye mwili , palepale alitengeneza kitenesi kingine cha barafu na ile anakamilisha , Roma ashatoa vile vipande na mwili wake ulikuwa ukijiponyesha kwa haraka sana , hivyo maumivu yalikuwa makali sana mwanzoni , lakini kadri muda ulivyokuwa ukisogea yalikuwa yakipona kwa haraka sana, hata kutoyasikia tena.

Roma alivyoona Omari anarusha tena barafu lingine kuja kwake aliona akifanya uzembe vipande vile vitampata tena hivyo alitumia uwezo wake wa kuhama sehemu moja Kwenda nyingine na jaribio lake lilileta faida kwani Omrri alivyorusha barafu lile kuelekea kwake alipotea sehemu aliokuwa amesimama na kuja kuibuka nyuma yake na kudhamiria kumpiga teke la ubavuni , lakini Omari alionekana kuwa na hisia kali sana kwani ile Roma anamkaribia kwa ajili ya kumpiga alitumia spidi kujiondoa na teke la Roma likapita.

Sasa ukumbuke huu ni mpambano wa kutumia mbinu za kijini peke yake yaani kwa maana rahisi Roma hakutakiwa kubadilika kabisa kama mwili wake ulivyotengenezwa.

“Hades kabla ya kuja hapa Tanzania nimejifunza mbinu zote ulizotumia kupambana na maadui wengi , hvyo nimejiandaa vya kutosha kukwepa mapigo yako”Aiongea Omari.

“Naona umenileta baharini kwa ajili ya kutumia maji kama siraha , lakini hii ni mbinu ambayo imepitwa na wakati dakika moja iliopita”Aliongea na kumfanya Omari kutabasamu.

“Hades unaonekana kutokufahamu mambo mengi sana kuhusu uwezo wa kijini , lakini kutengeneza barafu sio lazima uwepo wa maji , ninaweza kukusanya mvuke angani na kutengeneza barafu vilevile”Aliongea na palepale alianza kuinua mikono yake juu akiwa kama anajiandaa kupiga mbu hewani na palepale mikono yake ilitengeneza mvuke kama wingu na alianza kulizungusha lile wingu kwa kasi sana kama vile analipoza na palepale mvuke ule uligeuka maji na hatimae barafu kama kitenesi kwa mara nyingine.

Roma alijikuta akishangaa na kumfanya Omari kutoa kicheko.

“Umewezaje?”Aliuliza Roma na Omari alitabasamu.

“Hades katika mbinu za kichawi kile ambacho unanuia kwenye akili yako ndio unatengeneza kama siraha , ijapokuwa nipo kwenye levo ya Nafsi haimaanishi mtu mwingine ambaye yupo kwenye levo kama yangu atakuwa na mbinu sawa za kimajaabu katika kupambana , kila mtu anapata siraha kutokana na namna anavyofikiria”Aliongea Omari na palepale alipotea akiwa ameshikilia barafu lake na kuja kuibuka nyuma ya Roma , lakini akapotea tena na akaaja kutokea mbele yake tena na Omari akapotea tena na kutokea upande wa kulia halafu akapotea tena , lakini sasa jambo ambalo limemshangaza Roma ni kwamba baada ya Omari kupotea walitokea Omari wanne kwa pamoja wanaofanana kila kitu , yaani katika maeneo yaleyale ambayo alisimama na kupotea kwa mara nne mfululizo na Omari wote wa nne walikuwa wameshikilia vitenesi vya barafu, sasa kwa binadamu wa kawaida asingeona , lakini Roma aliona kwani hakuwa wa kawaida.

“Hahaha … Hades upo ndani ya mtego wangu kwa levo yako ni ngumu kutoka” waliongea Omari wote na kumfanya Roma kushindwa kumjua Omari halisi ni yupi kati yao , mpaka hapo alijua hao wote watakuwa feki na mmoja wao atakuwa ndio Omari mwenyewe , lakini alishindwa kujua haraka sana ni yupi kati yao , alijiona akiwa yupo kwenye duara.

Roma aliona hapo akizembea atamruhusu Omari kumuadhibu na pigo lingine , jambo ambalo hakuwa akitaka litokee kabisa na palepale alifumba macho yake na kuanza kufikiria kwa kutumia hisia kwa hali ya spidi sana.

Upande wa Omari aliekuwa amejigawa kwa sura nne hakutaka kumruhusu Roma kupata muda mrefu wa kufikiria , hivyo alirusha mabarafu yale yaliokuwa kwenye mfumo wa vitenesi kwa pamoja kumlenga Roma aliesimama katikati.

“Arrrgh…!!!” Ulisikika mguno wa maumivu na haukuwa ni wa Roma bali ulikuwa ni wa Omari mwenyewe.

“Hahahaha…!!”Roma alijikuta akitoa cheko la furaha mara baada ya kutegua mtego wa Omari.

“Mbinu yako ni ya kijinga sana , nikiri sikuwa na uelewa wa kutambua mtego wako kwa haraka sana , lakini baada ya kuelewa kuwa sura zako zote nne ni feki nikafikiria ni kwa namna gani unaweza kuzidumisha zote kwa pamoja na kuonekana kuwa halisi nikajua tu kuna namna ambavyo unazitawala”Aliongea Roma baada ya kumpiga pigo la ngumi Omari.

Sasa ilikuwa hivi baada ya mabarafu kurushwa kuelekea upande alipokuwa amesimama , palepale aliweza kufikiria namna ambavyo Omari aliweza kutengeneza sura hizo feki Roma aliona abahatishe kwa kuamini kwamba sura zote nne ambazo zimemzunguka ni feki , hivyo aliamini Omari atakuwa amesimama sehemu ambayo ataweza kuziongoza sura zote hizo na kuonekana halisia na ndio maana yale mabarafu yalivyomkaribia mkaribia alitoka pale aliposimama kwa spidi kali sana kuelekea juu katika mstaari mnyoofu huku akidharimiria katika akili yake kwamba lazima Omari atakuwa juu yake na ni kweli ile anafika mita kadhaa tu aliweza kuhisi uwepo wake na kuachia ngumi ambayo ilimpata vyema Omari na hatimae sura zake zote nne zikapotea.

Kitu kingine ambacho kilimfurahisha Roma ni kwamba kitendo alichokifanya ni kama kimemuwezesha kuelewa maana halisi ya levo ya Mzunguko kamili( muunganiko wa Yin na Yang).

“Umewezaje kugundua nipo juu Hades?”Aliongea Omari ambaye alikuwa akijiandaa kuachia pigo lingine.

“Ni rahisi sana mbinu uliotumia inaeleweka hata kisayansi, umetumia ‘Centripetal Force’(nguvu kati) kuweza kutengeneza na kuzidumisha sura zote nne zinazofanana kwa kila kitu na wewe , umefanikiwa kufanya hivyo kwa kutumia levo zote mbili , ya mzunguko kamili pamoja na ya Nafsi”Aliongea Roma na kumfanya Omari kutabasamu.

“Naona umevuka mtego huu lakini pia umeweza kutoka levo ya Nusu Mzunguko Kwenda Mzunguko mwingine hongera sana, fumbo linalokuja huwezi kulielewa na itakuwa ni mwisho wako , kwani nina kwenda kutumia uwezo wangu wa juu Zaidi”Aliongea Omari.

Ni kweli kabisa maneno alioongea Roma ni sahihi , unachopaswa kuelewa katika maswala ya kuweza kung’amua mbinu za kijini ni kwa kufumbua fumbo kwa namna ya kufikiria(meditation) , sasa kwa mfano mbinu ya kimaajabu aliotengeneza Omari ilikuwa ya kawaida sana kama utaifikiria kisayansi kwa kutumia kanuni za kifizikia , ilikuwa ni kama ‘Centripetal Force’(Nguvu kati) , hii ni kwa mfano pale mtu anapounganisha kitu kwenye Kamba na kuanza kukizunganisha juu kwa kasi na kutengeneza duara , sasa ndio alichokifanya Omari , kwamba alitumia mbinu za kichawi kumzunguka Roma kwa mara nne na kisha akajitoa kabisa kwenye zile nafasi na akaenda kukaa upande wa juu na akatengeneza umbo feki ambalo linamwakilisha yeye mwenyewe , sasa kuna namna ya kufanya mtu kutokuona mzunguko , hicho ndio kilichotokea , hivyo kitendo cha Roma kutoka nje ya duara aliweza kufumbua fumbo la levo ya Mzunguko kamili mwanzoni Roma alielewa levo ya Mzunguko kamili ilikuwa ipo ndani ya duara , lakini baada ya kutoka nje ya mtego wa Omari aligundua levo ya mzunguko ni lazima uwe nje ya mzunguko kutengeneza balansi.

Omari mwenyewe alishangazwa na uwezo wa Roma kuelewa mambo kwa haraka sana, kilichomfanya mara ya kwanza kujiamini ni pale alipoweza kuona Roma alikuwa katika levo ya chini kuliko yeye , lakini mtego aliomuwekea umemfanya kutoka levo moja Kwenda nyingine , sasa jambo hilo lilikuwa la kushangaza kwani yeye mwenyewe alichukua miaka Zaidi ya miwili kutoka levo ya nusu mzunguko Kwenda mzunguko kamili , lakini Roma yeye imemchukua muda mfupi sana.

“Nipo tayari kuona uwezo wako wote”Aliongea Roma.

“Usijindanganye kama unaweza kujifunza kitu kutoka kwangu , ijapokuwa umeweza kufanikisha kupanda levo moja Kwenda nyingine, lakini levo ya nafsi huwezi kuielewa kirahisi na kuifikia”Aliongea na kumfanya Roma kufikiria kidogo huku akikumbuka baadhi ya meneno ambayo alikuwa akielekezwa na mastar wake wakati wa mafunzo.

“Master ni zipi kanuni kubwa ya nguvu hizi?”Aliuliza kijana mdogo huku akimwangalia mchina aliekuwa mbele yake .

“Mbinu ninayokufundisha ina kanuni nne ambazo unapaswa kuzizingatia siku zote nazo ni namna nguvu zinavyopingana , zinavyotegemeana, zinavyovutana na zinavyopitia mabadiliko , unatakiwa kuelewa msingi wa hii dunia kila kitu kina uhusiano na kitu kingine na ndio maana halisi ya uwiano”

“Master je naweza kujua namna ya uhusiano kati ya kitu na kitu?”Aliuliza na kumfanya Master kumwangalia.

“Kifo na uhai ni mfano wa uhusiano ninaozungumzia”Aliongea na kumfanya kijana mdogo kuelewa.

Sasa Roma hayo ni moja ya mafunzo ya Master Chhi aliokuwa akimuelekeza ndani ya jangwa la Gobi na aliamini kwa fumbo lolote ambalo Omari anaweza kumtengenezea atatumia misingi ya dunia kuweza kufumbua.

Roma wakati akiwaza , alijikuta akishangaa mara baada ya kumuona Omari akifanya kitendo ambacho hakuwa amekitegemea , Omari alishika jicho lake la kushoto na sio kushika kwa kuziba bali alishika kwa namna ya kulitoa.

“Unataka kufanya nini?”Aliuliza Roma kwa wasiwasi.

“Hahaha.. Hades kama utabahatika kushinda basi nitakueleza namna ambavyo niliishi Maisha yangu kwa kutumia jicho moja tu baada ya kupata ajali”Aliongea Omari.

“Unamaanisha jicho lako la kushoto sio la kibinadamu?”

“Hilo ni jibu Hades , uliniuliza kwanini nimeweza kufikia levo za juu haraka ikiwa mimi ni binadamu , jibu langu kwako ndio hili , kitendo cha kuwekewa jicho la kondoo kwenye jicho langu la kulia ilihali siwezi kutumia kuona ilikuwa motisha kubwa san ilionipelekea kujifunza mbinu za kimatibabu za kichina” Aliongea na palepale alilinyofoa jicho lote nje na kulitupia baharini a kumfanya kubakia na jicho moja tu , huku sehemu ambayo ambayo ametoa jicho lile kukibakia shimo.

Kitu kingine Zaidi kilichomshangaza Roma ni kwamba baada ya Omari kutoa jicho lake ni kama mwili wake ulijaa nguvu isiokuwa ya kawaida ambayo ilikuwa ikimzunguka.

Haya ni majaabu”Aliwaza Roma kwenye kichwa chake huku akimwangalia Omari ambaye anasambaza hewa iliojaa presha ya hali ya juu na kufanya mawimbi ya maji kuanza kuwa makubwa.

“Arrgh !!.. Arghhh , aargh”Roma alikuwa akilalamika kwa mapigo aliokuwa akipigwa na Omari , kilichokuwa kikimfanya Roma kihisi maumivu makali ni kitendo cha kuhisi mwili wake ni kama unachomwa na vijipini mithili ya sindano pande zote za mwili.

Jambo moja ambalo lilimsiadia ni kwasababu alikuwa akipona haraka na alijiambia kama angekuwa hana mafunzo ya nguvu za kijini za kimaandiko basi asingeweza kumudu mashambulizi ya Omari.

Omari mwenyewe alijikuta akishangaa kwa uwezo wa Roma kuhimili mvua ya sindano aliomtengenezea.

“Usishangae naweza kutokuwa levo za juu katika mbinu za kijini lakini mimi ni moja kati ya wachache walioweza kufanikisha kutumia nguvu ya kimaandiko ya urejesho isio na kikomo”

“Nimesikia sana kuhusu hio mbinu na ni ngumu sana kueleweka hata ndani ya jamii ya majini yenyewe lakini hata hivyo hainifanyi kushindwa hili pambano”Aliongea na palepale alitumia maji ya bahari kutengeneza upanga wa barafu, lilikuwa jambo la kimaajabu kweli na kumfanya Roma kutabasamu kifedhuli., Roma alikwepa sana kila pigo la Omari , lakini jambo moja ambalo lilimshinda kufanya ni kutengeneza maajabu ambayo yataweza kumshinda Omari kutokana na kwamba hakutaka kuvunja kanuni za pambano hilo , kwani ilikuwa ni sheria yeye kutumia mbinu za kijini tu kupambana.

Mpaka masaa mawili yanamalizika Omari alionekana kutengeneza kila aina ya maaajabu kutokana na levo yake , lakini kila linapomfikia Roma aliishia kulipangua au kuliacha limpige na kuruhusu nguvu ya kimaandiko kumponya kwa haraka.

“Hades nimeishiwa mbinu zangu zote za kijini na siwezi kushinda lakini pia siwezi kusema pambano hili ni droo kutokana na uwezo wako kuwa chini kuliko wa kwangu , hivyo kwa maksi nitasema umeshinda”Aliongea Omari na kumfanya Roma kutabasamu .

Ni kweli kabisa ijapokuwa Roma hakuweza kumpiga Omari kwa shambulizi lolote lakini kutokana na levo yake na alivyoweza kupangua kila pigo lililorushwa kwake inamfanya kuwa mshindi.

Roma mwenyewe hakuona kuna haja ya kuendelea kupambana , kwani kama wataendelea inaweza kuchukua muda mrefu na inaweza kumfanya kutumia uwezo wake nje ya wa kijini ili kumshinda Omari kuokoa muda , jambo ambalo hakutaka kufanya kwani angekuwa nje ya kanuni walizopanga kabla ya pambano, lakini jambo kubwa sana kwake usiku huo alipata kujifunza vitu vipya kupitia Omari.

*****

Adeline na Fanny haikueleweka walikuwa wamemuwekea nini Kizwe kwani licha ya kwamba alikuwa macho lakini mwili wake ni kama haufanyi kazi , ni kama vile mgonjwa ambaye amepalalaizi kipande cha chini, hivyo hata baada ya kukabidhiwa kwa wanaume waliokuwa mbele yake alishindwa kabisa kujitetea au kutumia mbinu yoyote kuwaepuka.

Hivyo kila kitu kilichokuwa kikiendelea kwenye mwili wake alikuwa akikiona wazi kabisa na alishindwa kuongea lolote kwani hata hivyo wanaume hao mafukara hawakuwa wakielewa lugha ya kingereza.

Upande wa wale wazungu mara baada ya kumkabidhi Kizwe kwa vijana kwa ajili ya kazi kuanza walipandisha juu kabisa darajani na kuanza kurekodi tukio zima linavyoendelea , hawakutaka kufanya moja kwa moja kwani waliamini wale mafukara wasingefanya kazi kwa ufanisi.

“Oya wadau kwenye Maisha yangu sijawahi kukutana na mwanamke mwenye Ngozi laini kama huyu , hii ni bahati ya mtende”Aliongea Tulo huku akijikakamua kushusha mzigo.

“Maliza fasta wewe fala acha sifa zako za kimama”Aliongea yule jamaa aliekuwa akiamshwa dakika kadhaa zilizopita , yeye zamu yake ilikuwa ni mtu wa tatu , yaani baada ya Tulo kumaliza.

Yaani kilchofanyika kilikuwa kitendo cha kikatili mno , kwani vijana wote walimbaka Kizwe kwa zamu mpaka kurizika na hawakujali sana baada ya hapo kitatokea nini , licha ya kwamba walikuwa mafukara ilikuwa ni rahisi kwao kuelewa mwanamke huyo alikuwa na matunzo ya hali ya juu kutokana Ngozi na yake jambo ambalo liliwafanya wafurahie mchezo.

Kizwe yote hayo wakati yanafanyika alishuhudia na kwakua hakuwa na uwezo wa kufanya chochote kutokana na mwili wake kuwa katika hali ya kupooza aliishia kutoa machozi tu , huku akimlaani Roma kwa kila laana anayoijua, aliamini yeye ndio kamleta hapo kwani mara ya mwisho alipozimia alikuwa kwenye jumba kule Bagamoyo na mtu pekee ambaye alikuwa na uwezo wa kumfanyia hivyo ni Roma.

Kzwe hakujua kama aliletwa hapo na wazungu , kwani baada ya kukabidhiwa kwa wabakaji hao waliondoka na hapo ndipo kizwe aliporejewa na fahamu licha ya mwili wake kukosa nguvu.

Wakati vijana wanamaliza shughuli kila mmoja kwa mizunguko mitatu mitatu wote walijikuta wakijichokea na kukinai na kuyasogelea maboksi yao na kumuacha Kizwe vilevile.

“Oya wadau , wale wazungu si walisema watatulipa?”Aliongea Tulo.

“Unatepeta sana mwamba kiakili , hakuna tena maswala ya mikwanja malipo tushayapata”Aliongea mwingine na kumfanya Tulo kuona kweli aliongea ujinga.

“Wazee Lekcha huyu hapa”Aliongea mwingine baada ya kumuona mwanaume aliebeba mfuko mkubwa akiingia hayo maeneo , mwanaume huyo walikuwa wakimuita kwa jina la Lekcha yaani Lecture au mkufunzi kwa kiswahiili , kilichowafanya kumuita mwanaume huyo ni kutokana na kwamba alikuwa akisifika mitaa yote hio ya uswahilini kwa uwezo wake mkubwa wa kuongea lugha ya kingereza , huku akijitapa siku zote kwamba amesoma sana kuliko Mtanzania yoyote na mama yake ni Malkia Elizabethi wa Uingereza na aliongea hayo yote wakati akiwa amelewa chakali sasa katika mazungumzo yake alikuwa akimalizia kwa kujiita yeye ni Lecture sasa waswahili wao wakambatiza namna yao ya kumita na kumpa jina la Lekcha

Lakini ilikuwa ngumu kwa wanajamii wote kumuelewa mwanaume huyo , ni kweli kwamba alikuwa akijua lugha ya kingereza , lakini kilichowashangaza wengi ni kwamba hakuwa na makazi na alikuwa ni fukara kama wengine na kazi yake kubwa ilikuwa ni kuokota chupa za maji au soda na Kwenda kuziuza.

Sasa siku zote bwana huyu hakuwahi kuitwa kwa jina lake halisi na watu wengi wanamfahamu kwa jina la Lekcha , yaani Lecture au Mkufunzi yote hio ni kutokana na kwamba alikuwa akiongea lugha ya kingereza sana , hususani wakati akiwa amelewa, huyu mwanaume watu wengi washawahi kumfatilia kutaka kujua ni wapi ametokea , lakini hakuna aliefanikiwa kujua ni wapi alitokea mpaka kuwa ndani ya maeneo hayo ya uswahilini ya jiji na kuwa kafara, hivyo watu waliamini huenda hakuwa na akili nzuri hivyo hata alipozaliwa amesahau , alikuwa mkubwa wa miaka kama arobaini hivi.

“Kuna nini kinaendelea hapa?”Aliuliza Lekcha mara baada ya kumuona mwanamke akiwa uchi pembeni ya hao vijana.

“Lekcha bwana mitikasi mingi ya nini , wakati kila kitu unaona , ni zamu yako na wewe kuukwea”Aliongea Tulo na kumfanya Lekcha kumsogelea yule mwanamke na mara baada tu ya kumuona vizuri kwa mwanga uliozalishwa na baadhi ya taa za nyumba za karibu alijikuta akisisimka mwili.

“Hahaha… Lekcha kumbe na wewe umo?” Walijikuta wale vijana wte wakicheka lakini Lekcha hakutaka kuwajali Zaidi ya kushusha suruali yake haraka haraka.

Upande mwingine barabarani mita kadhaa kutoka kwenye daraja hilo Adeline na Fanny walionekana kumaliza kazi yao ya kurekodi kila kitu.

“Fanny ijapokuwa Mfalme Pluto ana mbinu za kikatili likija swala la mateso , ila hii imezidi”Aliongea huku akikagua video iliokuwa ikionekana kwenye Camera.

“Nini tunakwenda kufanya baada ya hapa Adeline?”

“Mfalme Pluto amesema anataka kazi ya kisanaa Zaidi huu ni mwanzo tu , tunatakiwa kuendelea kufatilia”Aliongea na kumfanya Fanny kushangaa.

“Kinachofuata nini Adeline si kila kitu kishaisha tunazo hizi Vidio zinazo onyesha sura ya Kizwe kuna haja gani ya kuendelea Zaidi”

“Mfalme Pluto hajatuambia tuishie kwenye kurekodi tu , bali tuendelee kurekodi hatua zote atakazopitia ili kuifanya kazi kuwa ya kisanaa , kuhusu hizi tulizoweza kurekodi , nitamtumia asubuhi”Aliongea na Fanny alishindwa kupinga na kuondoa gari yao huku wakipanga kuendelea siku inayofuata.
 
SEHEMU YA 380

Saa kumi na moja kamili za asubuhi ndio muda ambao Roma aliweza kurudi nyumbani Roma mara baada ya mapambano yake na Omari kuisha yeye aliendelea kubakia ndani ya eneo hilohilo bila kuondoka , alikuwa akitafakari Zaidi kuhusu mbinu za kijini , alitamani sana kupanda levo za juu Zaidi ili kuwa na uwezo mkubwa wa kimapambano pasipo ya kupitia mabadiliko yoyote ya kimwili.

Roma alijiambia kama atataka kuwalinda watu wake wa karibu basi ni lazima ahakikishe anakuwa na uwezo mkubwa Zaidi wa kijini katika kupambana, alikuwa akimhofia Athena anaweza kufanya jambo la kuhatarisha usalama wa watu wake wa karibu halafu yeye kushindwa kuwalinda na ndio maana Roma akatumia muda uliobaki wa usiku huo kutafakari kwa kina mara baada ya kuachana na Omari.

Sasa Roma aliweza kubakia kwenye fukwe hio mpaka muda wa saa kumi na moja ndipo alipoweza kumaliza kile alichokuwa akikifanya na aliishia kutabasamu mwenyewe , ilionekana kuna vitu aliweza kuvigundua ndani ya masaa Zaidi ya matatu aliotumia kukaa hapo ufukweni akitafakari.

Sasa saa kumi na moja alikuwa ndio anaingiza gari, bado nyumba ilionekana kutulia mno , ikiashiria watu bado hawajaamka , alipaki gari yake na kisha alitoka na kutembea taratibu kuingia ndani ya nyumba , huku akiangalia shati lake ambalo lilikuwa na mchanga na pia likuwa limechanika kiasi sehemu ya kifuani, damu ambayo iliomtoka j mara baada ya kuchanwa na barafu iliweza kusafishwa na maji ya bahalini , hivyo Ushahidi pekee uliokuwa umebakia kwamba jana alikuwa akipambana na mtu ni kutoboka kwa shati pamoja na suruali eneo la kwenye paja.

“Edna usiniambie haujalala hapa usiku kucha?”Aliuliza Roma mara baada ya kumkuta Edna akiwa amekaa eneo la sebuleni akiwa mchomvu kweli na Edna mara baada ya kumuona Roma alisimama haraka haraka na kumsogelea, licha ya kutovaa kitu chochote miguuni alionekana kupendeza na vazi la kulalia..

Edna jana usiku wake mara baada ya kupewa ushauri na Blandina hakuweza kulala kabisa , alienda chumbani kwake lakini usingizi haukumjia na alichokifanya kwa wakati wote wa usiku ni kufikiria maneno yote alioelezwa , lakini wakati huo huo akisubiria muda ambao Roma angerudi ,hata ilivyofika saa kumi na moja kamili za asubuhi alishuka kukaa sebuleni , aliamini Roma angerudi muda huo.

Sasa Edna mara baada ya kumuona Roma karudi alijikuta akijawa na hisia mchanganuyiko , hisia za makasiriko, hisia za hatia , pamoja na hisia za furaha kwa Roma kurudi.

“Roma naomba usiwe na hasira tena… nakuomba”Aliongea Edna , ndio neno la kwanza lililomjia mara baada ya kumuona Roma.

Kwa jinsi Roma alivyoweza kumuona Edna , ni kama vile mwanamke huyo alidhania kama hatorudi nyumbani kabisa kwani alikuwa ni mwenye unyenyekevu wa hali ya juu, jambo ambalo Roma hakuwahi kuliona kwa Edna.

“Usiwe na wasiwasi tena , nimefanya kosa jana kutotoa taarifa kama nisingerudi kabisa , unapaswa kupumzika kampuni bado haijapoa na una mambo mengi ya kufanya”Aliongea Roma huku akitaka Kwenda juu kwa ajili ya kuoga kwani nguo zake zilikuwa zikitoa harufu ya maji ya bahari.

“Haujanipatia jibu bado, naomba uniambie kama hutoendelea kukasirika , jana nimefanya makosa na sikupaswa kuongea vile , naomba usiendelea kuwa na hasira na mimi”Aliendelea Edna kubembeleza na kumfanya Roma kutabasamu.

“Niko sawa na sikuwa na hasira hata jana sikutaka tu kuendelea kubakia nyumbani”

“Unadanganya Roma, kama haukuwa na hasira kwanini haukurudi nyumbani?”Aliuliza Edna na kumfanya Roma kushindwa kutoa maelezo ya kina , kwanza asingejibu kama jana yake alimsaidia Benadetha , lakini pia asingeweza kumueleza Edna kama alienda kupambana na mwanaume anaeitwa Omari , mwenye jicho moja la kibinadamu na jicho lingine la kijini.

“Roma naomba unisamehe , ninakuahidi kuanzia sasa nitakuelezea kila kitu , nitajitahidi kuwa mwema kwako kwa namna nitakavyoweza na nitakuwa nafikira kabla ya kuongea , naomba tusahau ya jana , kama unataka nipige magoti kwa ajili ya kuomba msahama nitafanya hivyo”aliongea Edna na kumfanya Roma kushangaa sana , hakuamini kama anaeongea ni Edna yule mke wake mwenyewe anaemfahamu kwa ukauzu , ambaye sio mwenye kujali, alijikuta akishindwa kuzuia tabasamu.

“Mbona unatabasamu sasa.. mimi nipo siriasi mwenzio”Aliongea Edna

“Nimetabasamu kwasababu siku zote nimekuwa wa kukuomba msamaha na leo siamini kama imekuwa kinyume chake”

“Nimekosea ndio maana ,siwezi kushupaza shingo kama baadhi ya wanawake wengine , kama nimekosea nitaomba msamaha”Aliongea na kumfanya Roma kukuna kwanza kichwa chake.

“Okey! Sasa tuache kuongea maswala ya kuombana misamaha , nishakuambia sikuwa na hasira , jana nilioneoka kwasababu hisia zangu hazikuwa sawa , ni kweli nilighafirika kwa madakika kadhaa , lakini baada ya pale hasira zangu ziliisha , siwezi kukasirika usiku mzima kwa jambo kama lile , nakujua vyema hivyo usiwe na wasiwasi , hisia sio mkopo wa benki au jicho kwa jicho kama lazima tulipane, wewe ni mke wangu na siwezi kukukasirikia muda wote”Aliongea Roma.

“Kwahio huna hasira tena , lakini kwanini haukurudi jana , nilidhania hautorudi tena”Aliongea Edna kwa namna ya upole.

“Jana kuna mambo yalitokea , naweza kusema usiku mzima umeisha kwa namna yake”

“Ooh..”Aliongea Edna na kisha alishindwa kuendelea Zaidi , ijapokuwa alitamani kujua ni wapi Roma alipokuwepo usiku mzima lakini alishindwa kuendelea kuuliza maswali na Roma alijikuta akipumua kwa ahueni maana asingeweza kuelezea kila kitu kilichotokea jana.

Kusameheana ni jambo la kawaida kwa wanandoa na walikuwa na safari ndefu mbele yao , hivyo Roma hakuona haja ya kumfanya Edna kuwa na wasiwasi juu yake , alihakikisha anamaliza wasiwasi wake wote kwa kumuweka sawa kwa namna ya kumfariji ili asiendelee kujiona ni mwenye hatia.

Roma wakati anaanza kupandisha ngazi , ni kama Edna alikumbuka kitu.

“Unaumwa njaa , jana ulikula? , ngoja nikakuandalie kifungua kinywa”Aliongea Edna na kumfanya Roma kugeuka na kumwangalia Edna , alishangaa Edna kuwa na mabadiliko yasiokuwa ya kawaida.

“Usijali , kwasasa ninataka nioge na nipumzike kidogo na tutapata kifungua kinywa watu wote wakishaamka , hata wewe unaonekana umechoka unapaswa Kupumzika kidogo kabla ya kwenda kazini”Aliongea Roma.

“Ooh.. sawa”Aliongea Edna na kumfanya Roma kuendelea na safari yake ya kupanda juu huku akiendela kujiuliza maswali , hakuamini kama kitendo cha jana kuondoka ndio kimemfanya kuwa hivyo , lakini kubwa Zaidi hakumzoea Edna kuwa mpole na mke mtiifu sana na tabia yake asubuhi hio ilimfanya mwenyewe kujisikia kidogo vibaya.

“Bora aendelee kuwa kauzu , sijamzoea hivi mimi?”Aliwaza Roma wakati akiingia bafuni kwenye chumba chake , ijapokuwa Roma na Edna walianza kulala pamoja , lakini Roma nguo zake za kubadilisha zilikuwa chumbani kwake , hivo pia hata baadi ya mahitaji yake mengi yalikuwa kwenye chumba chake.

Dakika kama kumi tu hivi kupita mara baada ya Roma kumaliza kuoga akiwa anajifuta maji na taulo mlango wake uligongwa.

“Roma naweza kuingia?” Sauti ya Edna ilisikika nje ya mlango.

“Ndio , kuna nini?”Aliongea Roma huku akijifunga taulo vizuri na Edna aliweza kuingia ndani

“Naomba unipatie nguo zako chafu nikazisafishe na mashine”Aliongea Edna kwa sauti ya unyenyekevu..

Kusema ukweli kwa jinsi Edna alivyokuwa akiongea , ni kama sio yeye vile na hata Roma alijikuta akimwangalia Edna kama kuna mahali amejiumiza labda na kumpelekea akili yake kidogo kutokaa sawa , maana kila alichokifanya ni kipya kwake na hajamzoea hivyo.

Sasa asichokijua Roma ni kwamba mwenzake alikuwa akijaribu kufanyia kazi ushauri wa Mama mkwe.

Kitendo cha Roma kutokumjibu Edna kilimfanya akose kujiamini na kujua ni kipi kingine anapaswa kuongea , mpaka hapo alikuwa akijitahidi lakini alikuwa akikosa pointi za kuendelea.

Edna alijikuta akikumbuka pia katika shule ya jana aliopewa na Mama mkwe aliambiwa kwamba si kila kitu lazima mume wake aanze kuna mengine anatakiwa kuyaanzisha yeye.

Roma alimwangalia Edna kwa mshangao huku Edna na yeye akimwangalia Roma pasipo ya kuongea.

“Mama aliniambia niwe naanzisha mimi , nikamkumbatie au , au nikambusu , mh ngoja nikakae kitandani nimuonyeshe kidogo mapaja na kujirembulisha”Edna alikuwa akiwaza kwa kujiuliza maswali kibao , alionekana kutoelewa vizuri shule ya jana.

Wakati Roma akiendelea kuwaza Edna yeye alijongea tarratibu na kisha akaenda kukaa kitandani na kjitahidi kukaa kihasara hasara kumvutia Roma na kuanza kujirembulisha , mara mguu aweke hivi mara aweke vile , upande wa Roma alishikwa na bumbuwazi huku wasiwasi ukimzidia , kwanza kabisa aliamini huenda Edna hayupo kwenye akili yake ya kawaida , kwani alikumbuka kabisa walikuwa washajadiliana kama ni kufanya mapenzi ni baada ya kufunga ndoa kwa mara ya pili sasa kitendo cha Edna kufanya jambo lisilokuwa la kawaida hakuzoea kabisa na vitendo vyake havikumfurahisha hata kidogo.

Wakati Roma akifikiria matendo ya Edna ambayo kiukweli hayakumtia mzuka , simu yake ilianza kuita na kumfanya Edna aliekuwa amekaa kitandani akitokwa na jasho la uso kuchukua baadhi ya nguo ambazo aliona ni chafu na kisha kukimbilia nje na kumfanya Roma atamani kucheka.
 
SEHEMU YA 381.

Licha ya Roma kuchekeshwa na matendo ya Edna , lakini moyo wake ulimhurumia hakuamini kama kuondoka kwake jana ndio kumemfanya Edna kuwa hivyo , alijihisi huenda jana alimuumiza kihisia nio maana akawa na mabadiliko ya aina hio.

Aliangalia simu kuona nani anapiga na aligundua ni Adeline wa The Eagles ndio aliekuwa akipiga.

“How is progress?”Aliuliza Roma akimaanisha vipi kuhusu maendeleao.

“Mfalme Pluto , jana nilikesha kuhakikisha kazi ulionipa inaenda kama ulivyosema nishakutumia faili la video kutumia barua pepe yako , kwa jinsi tulivyopatia kuchukua tukio kama itasambaa itaharibu kabisa taswira yake kama mke wa raisi , nataka kujua kama ninatakiwa kuendelea kirekodi?”Aliuliza Adeline kwa lugha ya kingereza.

“Haina haja ya kuendelea na hio kazi , kwasasa itakuwa juu yake mwenyewe kuweza kuishi na aibu au kujiua”Aliongea Roma na Adeline upande wa pili alipokea maagizo na kisha simu ikakatwa.

Roma baada ya simu kukatika , alifungua barua pepe yake kuangalia faili alilotumiwa kupitia simu na alijikuta akitabasamu kwa kile alichokuwa akiangalia kwani kwa namna ambavyo wahusika wote wa’ show’ walivyokuwa wakionekana ni kama Adeline alikuwa na mafunzo ya kutengeneza filamu.

Roma aliwaangalia wanaume wanne wote wakimnyandua Kizwe kwa zamu na kisha akaweza pia kushuhudia namna ambavyo mwingine wa mwisho anavyomalizia kazi , baada ya kuona ni kama alivyotaka aliwasiliana na Diego na kumpa maagizo kwamba aangalie namna ya kufikisha faili hilo kwa Mheshimiwa Jeremy wa Rwanda bila ya kufahamika.

Roma hakuwa na mpango wa kuiachia video hio kwenye vyombo vya Habari , alijua akifanya hivyo jambo hilo lisingekuwa na faida bali hasara kwani Kizwe ni mke wa raisi na tukio limetokea Tanzania , hivyo kama litakuwa mtandaoni dunia itainyooshea Tanzania vidole na ingeleta sana mvutano , hivyo alichotaka kufanya ni kuifikisha kwa muhusika mkuu ambaye ni raisi Jeremy mwenye mke, aliamini kama atafanya hivyo ni vigumu sana kwa Kizwe kurudi uraiani kwa kuwa na nguvu alizokuwa nazo mwanzo kwani heshima yake ameishusha kwa asilimia mia moja.

*******

Upande mwingine , wakati Roma akitoa maagizo Kwenda kwa Diego chini ya Daraja la reli , Kizwe sasa aliweza kushituka kutoka usingizini huku akikumbana na harufu kali ambayo kwenye Maisha yake hakuwahi kuinusa, akili yake ni kama ilikuwa na mawingu na alivyofungua vizuri macho ndio alijishangaa akiwa chini ya daraja tena akiwa amelala kwenye maboksi , lakini pia kitu kingine sehemu zake za viungo vya uzazi kuuma sana , hapo hapo akili zake zilimrudisha jana usiku yake , alianza kukumbuka tukio zima la yeye kubakwa na wanaume wanne, akishindwa kukumbuka kwamba sio wanne bali ni wa tano , kwani wa mwisho alikuja akiwa tayari ashapoteza fahamu kwa mara nyingine,

Akijikuta akibubujikwa na machozi , alijua mpaka hapo hakuwa na thamani tena kama mke wa raisi , na alifahamu kwa hakika kabisa lazima kila kitu kimerekodiwa na huenda kishamfikia mume wake huko nchinii Rwana au huenda pia muda huo taarifa zake za kubanduliwa zilikuwa zikisambaa mtandaoni , Kizwe alijikuta akikumbuka Watoto wake lakini pia alijikuta akikumbuka Maisha yake kama mke wa raisi.

“Huna haja ya kutoa machozi , kilichofanyika juu yako kishafanyika , machozi yako yanafaida gani tena?”Ilisikika sauti upande wa nyuma na kumfanya kizwe kugeuza macho , kilichomfanya kutotambua uwepo wa mtu , ni kutokana na eneo hilo kuwa na makelele ya watu na kilichosaidia tu ni kwamba ni watu wachache sana waliokuwa na uwezo wa kuona kinacheondelea chini ya daraja hilo.

Kizwe baada ya kumuangalia mwanaume aliekuwa mita kadhaa akiwa amekaa chini akifyonza machungwa asubuhi asubuhi pamoja na maembe kichafu alijikuta akitoa machozi na kisha kujiangalia mwili wake uliokuwa umesitiliwa na koti lililojaa vumbi.

“Hapana kwa aibu kama hii siwezi kuendelea kuishi , ni bora kujiua tu , Roma na Edna najua mmenifanyia haya , lakini kisasi changu nitakilipa hata kwenye kifo changu”Aliwaza kwenye kichwa chake na alionekana kabisa kukata tamaa , hakutaka kujihusisha kabisa na mwanaume fukara aliekuwa amekaa nyuma yake , uwepo wake tu kwanza ndio unazidi kumuongezea machungu ya kutaka kujiua.

Kizwe mara baada ya kuangalia upande wake wa kulia hatimae aliweza kuona chupa ya bia iliopasuka kidogo na alijiburuza pasipo kujali alikuwa uchi na kisha kuichukua ile chupa na kuigonga kwenye jiwe la Zege na ikapasuka vipande vipande.

“Unafanya nini wewe?”Aliongea yule mwanaume kwa Kiswahili, kitendo cha kushika chupa tu alijua lazima mwanamke huyo alikuwa akidhamiria kujiua, sasa mara baada ya kuona mwanamke yule hamsikilizi alibadilisha lugha na kuongea kwa kingereza.

Naam mwanaume mwenyewe alikuwa ni yule wa jana anaefahamika kwa jina la la Lekcha(Lecture) yaani mkufunzi wa chuo au mwalimu wa chuo, Lekcha ndio aliekuwa amekaa kando ya mwanamke Kizwe na hata koti ambalo alimfunika , lilionekana kuwa ni la kwake , ilionekana jana baada ya shughuli aliamua kumsitiri.

Sasa jambo moja ambalo jana ambalo halikuweza kuonekana kwa Lekcha ni kwamba mguu wake mmoja sio wa kawaida , yaani ulikuwa ni wa bandia na moja ndio ulikuwa wa kawaida.

Kizwe baada ya kusikia mwanaume yule kuongea ligha ya kingereza aligeuza shingo na kumwangalia kwa dakika kadhaa na kisha akarudia kwenye kile ambacho alikuwa akidhamiia kukifanya , kitendo cha kujiua kwa kutumia chupa, Lekcha alimsogelea kwa haraka na kisha akamponya ile chupa kwa kuipiga na kudondokea pembeni.

“Unataka kujiua ? kipi kinakupa sababu ya kujiua, ni kweli jana vijana waliufaidi mwili wako , lakini kwa ninavyokuona wewe ni mzee tayari , unafikiri una thamani gani mpaka ujiue kisa kuchezewa , ungekuwa msichana mdogo sawa , lakini wewe ni mzee”Aliongea Lekcha kwa lugha ya kingereza safi kabisa kilichonyooka, ilikuwa haki ya kuitwa mwalimu wa chuo.

“What did you just say?”Aliongea Kizwe kwa kupayuka , maneno ya Lekcha yalimgusa vilivyo , katika Maisha yake alikuwa akijichukulia wa thamani sana na ndio sababu ambayo ilikuwa ikimpa sababu ya kujiua , lakini kitendo cha kuambiwa ni mzee asie na thamani na hana haja ya kuwazia sana kuhusu kubakwa kilimgusa.

“Wewe mwanaume ni mbwa , chokoraa ,fukara wewe , unanijua mimi ni nani?”Aliuliza kwa hasira na kumfanya Lekcha kutojali sana maneno yake, na kurudi kwenye boksi lake na kuendela kula machungwa yake kichafu”

“Sijali wewe ni nani , umeniita mbwa, ndio mimi ni mbwa , tena mbwa dume na ndio maana usiku kucha tulikuwa pamoja, hivyo ni rahisi kusema wewe ni mbwa jike”Aliongea na kumpandisha Zaidi Kizwe hasira.

Kizwe alikuwa mwanajeshi, lakini muda huo ashasahau kama alikuwa mwanajeshi tena , ila alionyesha kukasirika tu , huenda alishindwa kuinuka na kumpiga huyo mwanaume kutokana na kuwa uchi.

“Unanitukuna , nakuuliza unanitukana wewe Mbwa , Bastard , nitakuua kabla sijajiua”

“Hey ! Shangazi ninachomaanisha ni wewe kuacha mawazo ya kijinga ya kujiua , hebu jaribu kufikiria , kama utajiua utakuwa umekufa bure , kuliwa na vijana kama sisi ni kitu gani cha kusababisha kutaka kujiua kwa umri wako , kwanini usiishi ukalipiza kisasi chako, huwezi kulipa kisasi ukiwa umekufa , lakini unaweza ukaishi na kulipa kisasi”

“Unanifundisha? Au unanipa ushauri?”Aliongea kwa hasira.

“Haha.. naitwa Lecture , jina linalonifanya kuwa mwalimu lakini ninachosema sio kukufundisha bali ni kukueleza ukweli , huwezi kujiua kwasababu wanaume kama sisi jana usiku tulikufaidi bwana usiku kucha “Aliongea na kumfanya Kizwe palepale kuchukua jiwe lililokuwa karibu yake na kumlenga Lekcha.Lakini Lekcha alionekana kuwa vyema , kwani alilikwepa.

“Hahaha.. wewe mwanamke unashangaza , pamoja na kuhudumia wanaume watano jana usiku , lakini unapata nguvu ya kunirushia mawe , huenda hata haujaonewa na ni kazi yako”Aliongea Lekcha.

Kwa jinsi Lekcha anavyoongea ni vigumu sana kuelewa kama kweli alikuwa kichaa kama watu wa mtaani walivyokuwa wakimuona , kwani kwanza alikuwa akitumia kingereza kilichonyooka kabisa na hakuwa akisita sita kwenye kuongea na sio hivyo tu alikuwa na lugha ya kukera , tena ile ya kimarekani iliojaa tamathali za matusi ya kukera lakini aliongea kwa namna flani ambayo ilikuwa ikimsahaulisha Kizwe mawazo yake ya kujiua.

“Unaonekana kuwa mtu mzima lakini maziwa yako hayajalala sana , sijui ni siri gani unaitumia lakini niseme umejua kujitunza , jana tulifaidi”Aliongea tena makusudi, lakini kauli yake ilimfanya Kizwe kujiangalia na kuona aibu na kutamani kutoa ukulele wa kilio.

“Chukua hizo nguo jisitiri ,, umenipatia huduma nzuri usiku wa jana ambayo sijawahi kuipata mahali popote , hivyo sikutaka kukukimbia kama wengine ,ndio maana nikaenda kuiba baadhi ya nguo za kike na kukuletea , naamini zitakutosha”Aliongea Lekcha huku akimrushia Kizwe dela , lilikuwa chakavu mno.

“Siwezi kuvaa nguo inayonuka”

“Basi endelea kubaki uchi , unafikiri utaweza kuondoka hapa ukiwa hivyo?”Aliongea na kumfanya Kizwe kuangalia Dela lililokuwa chini yake mita kadhaa na kisha akageuka na kumwangalia Lekcha na sasa alitakiwa kuchagua kama atavaa dela hilo inamaanisha safari yake ya kulipiza kisasi itaanza rasmi na kama hatovaa inamaana ameamua kujiua.

“Malizia kuvaa haraka upate kifungua kinywa , ukanisaidie angalau kuokota makopo huenda ikakusiadia nauli kurudi ulikotoka”Aliongea huku akimuonyesha maembe na machungwa alioweka chini.
 
SEHEMU YA 382.

RWANDA -KIGALI

Ni siku nyingine ndani ya Ikulu, Raisi Jeremy alionekana akiwa ameketi kwenye ofisi yake kama kawaida , lakini leo hii alionekana hakuwa sawa kabisa kimawazo kutokana na mwonekano wake.

Ukweli tokea siku ya jana hakuwa amelala kabisa mara baada ya kupata taarifa kutokuonekana kwa mke wake kutoka kwa walinzi waliokuwa wakimpatia ulinzi nchini Tanzania , alijaribu kuwasiliana na Raisi Senga ili kupata msaada wa haraka wa mke wake kutafutwa , lakini mpaka inafikia siku nyingine muda wa asubuhi hio hakukuwa na taarifa.

Upande wa mtoto wake Desmond alisharudishwa Rwanda na Linda na Raisi Jeremy alimpa onyo Desmond kutomsogelea Edna kabisa , jambo ambalo lilimfanya Desmond kumkasirikia baba yake sana , aliona ni kama baba yake anamfanya kutokuwa na hadhi ya kutoka na Edna kimapenzi , hivyo hakutaka kumuelewa baba yake bila sababu ya msingi.

“Baba kama hakuna sababu ya msingi, basi huwezi kunizua kumpenda Edna na kumfanya mpenzi wangu”Aliongea Desmond lakini alijikuta akipokea kibao kutoka kwa Raisi Jeremy kilichomyumbisha.

Desmond hakuamini kama baba yake ndio aliempiga , tokea amefikia utu uzima huo hakuwahi kupigwa na baba yake kabisa na alikuwa ni mtu mzima anejua jema na baya hivyo baba yake kitendo cha kumpiga kilimkasirisha.

“Desmond hurusiwi kumsogelea Edna na sio kumsogelea tu, hata kumgusa hauruhusiwi , ikitokea umemgusa mimi na wewe hatutoelewana’Aliongea Raisi Jeremy.

“Baba kwanini unamtetea Edna kiasi cha kuniadhibu… au baba unaniambia na wewe unamtaka Edna… haha…baba ni haki yako kabisa kufanya hivyo , yule mwanamke ana urembo wa usiokuwa wa kawaida na hata siku ile kwenye kikao nilikuona ukimwangalia sana”Aliongea Desmond kwa hasira mara baada ya kupigwa kibao na baba yake.

Lakini maneno yake kwa Jeremy yalikuwa ni kama matusi kwake , kwani ni yeye pekee aliekuwa akifahamu ukweli kwamba Desmond na Edna ni kitu na dada yake na mapenzi baina yao yamekatazwa , sio kidini tu lakini ni mtazamo wa dunia nzima , hakuna mtu ambaye anaweza kuruhusu ndugu kuwa na mahusiano ya kimapenzi.

“Desmond kuanzia sasa umezuiwa Kwenda Tanzania bila ruhusa yangu lakini pia huwezi kutoka nje ya hii nchi , unaweza kuondoka”Aliongea Jeremy huku akijitahidi kujizuia , alijua sehemu kubwa kwa kile kinachotokea alikuwa ndio chanzo , Desmond kumpenda Edna sio kosa lake , kwani hakuwa na uelewa kama wao ni ndugu yaani kaka na dada.

Sasa hio ilikuwa ni jana yake , wakati Kizwe akianza safari ya kuelekea Tanzania upande wa Desmond alikuwa akirudishwa Rwanda hivyo kwa maneno marahisi unaweza kusema kwamba hawakuweza kukutana nchini Tanzania.

Sasa jana yake jioni ndio Raisi Jeremy alipopata taarifa za kupotea kwa kizwe mke wake , ilikuwa ni taarifa ya kushangaza kwani walinzi wake hawakuwa kabisa na uelewa ameelekea wapi , Jeremy alikuwa akijua Kizwe alikuwa ndani ya Tanzania kwa ajili ya kumsaidia Edna katika kile kinachoendelea ndani ya kampunni na hata baada ya Edna kuweza kudhibiti hali na kuzidi kupaa Zaidi ki utajiri na kujichukulia sifa kedekede , alijikuta pia akijivunia kuwa na mtoto kama Edna na alitamani wangekuwa wanafahamiana kama baba na mwana na ampongeze moja kwa moja , lakini hilo halikuwa likiwezekana tena , kwani. Kuna makubaliano ya Edna kubakia kuwa mtoto wa familia ya Adebayo lakini ukiachana na hilo asingeweza kumuweka Edna hadharani kama mtoto wake , kwani kwake siasa ndio muhimu Zaidi kuliko mtoto , hivyo asingeweza kuharibu taswira yake kwa mtoto aliezaliwa nje ya ndoa.

Wakati akiendelea kuwa katika mawazo , asubuhi hio kwenye ofisi yake , simu yake iliita mara moja na kuipokea.

“Any News?” Kuna taarifa yoyote ?”Ilikuwa simu kutoka chumba cha mawasiliano ndani ya ikulu.

“Hapana Sir , lakini kuna mtu yupo kwenye mawasiliano na anazungumzia kuhusu Madam , ametoa maagizo uangalie barua pepe yako binafsi”Ilisikika sauti upande wa pili na kumfanya Raisi Jeremy kumwemwesa midomo yake , alishangaa kuhusu kuambiwa aangalie barua pepe yake binafsi, jambo ambalo mara nyingi halikuwa la kawaida.

Baada ya kuingia kwenye Email yake kwa kutumia taarifa , aliweza kweli kuona meseji moja ambayo imetumwa na mtu asiejulikana dakika mbili zilizopita , kwani sehemu ya jina na Email hakukuwa na chochote na kwa haraka haraka aliamini huenda akaunti yake imedukuliwa kwa namna moja ama nyingine , lakini hata hivyo kuna faili la video ambalo limetumwa pamoja na hio Email.

Mpaka hapo aliamini jambo ambalo linakusudiwa kutumwa kwake halikuwa la kawaida , kwani mara nyingi barua pepe zake hupokelewa na wafanyakazi wake na kisha hupitiwa na kama kuna ya muhimu ndio huletwa ofisini kwake , lakini mtu kumtumia kwa njia ya moja kwa moja aliamini kabisa kilichotumwa ni siri ambayo imekusudiwa kwake peke yake.

Jeremy baada ya kujituliza na kuangalia video hio , alijikuta akipagwa , hakuamini kama aliekuwa akionekana ni mke wake kweli au kuna janja imefanyika , lakini kadri alivyoangalia kila kitu kilionekana kuwa halisia.

“Kizwe , Mama Desmond , mke wangu , siamini…”Alijikuta akishindwa kuhema kabisa.

*******

Ndani ya jiji la Dar jua lilikwisha kuchomoza kabisa, upande wa familia ya Edna , nyumba ilimezwa na harufu nzuri ya vyakula kutoka jikoni , huku Blandina na Bi Wema vicheko vyao vikisikika kutoka jikoni.

Roma mara baada ya kutoa maagizo ya video kutumwa kwa Raisi Jeremy alitoka kwenye chumba chake na kushuka chini sebuleni kwa ajili ya kupata kifungua kinywa.

“Goodmorning Anko Roma?”Alisalimia Yezi akiwa amemkumbatia Roma kwa nyuma , wote wakiwa wanaelekea chini kwa ajili ya kifungua kinywa, Yezi alionekan tayarri ashajiandaa kwa ajili ya Kwenda chuo.

“Unaonekana kama mtoto , kumbe ni mdada mkubwa ulieanza chuo, Yezi unaonaje ukaniita baba nikawa na Watoto wawili wakike?”Aliongea Roma huku akimfinya kwenye shavu.

“Siwezi kuwa mtoto wako”Aliongea Yezi huku akinuna na kujitoa kwa Roma.

“Goodmorning dad” Ilisikika sauti nyuma yao na kumfanya Roma kugeuka , aliesalimia alikuwa ni Lanlan akiwa ameshikwa mkono na mlezi wake Qiang Xi..

Ilikuwa ni siku ya kwanza kwa Roma kuitwa baba na Lanlan tokea waanze kumlea , Roma aligeuka na kisha kumsogelea na kumpakata.

“Goodmorning Chubby Girl”Aliongea Roma na kumfanya Lanlan asipendezwe na jina la Chuby lakini alikubali kupakatwa hivyo hivyo, alionyesha kuanza kukubaliana na jina analoitwa na baba yake.

Moja ya sababu ya Roma kupenda kumuita Lanlan jina la Chubi ni kutokana na umbo lake la ukibonge , Lanlan hakuwa mtoto mwembaba , alikuwa na mwili wa kunenepa ndio maana.

Yezi alimwangalia Lanlan na baba yake na kujikuta akiona wivu , alimuonea Lanlan Wivu kutokana na kwamba yeye katika Maisha yake hakuwahi kubahatika kulelewa na wazazi , kwa upande wa Lanlan licha ya kwamba aliona alikuwa akilelewa , lakini Maisha yake yalikuwa ya tofati sana , Lanlan alikuwa akipendwa sana na mama yake hivyo ni kama Edna alikuwa mzazi kamili na kubwa Zaidi ni kwamba alikuwa akifanana nae.

Ni dakika kdhaa Roma akiwa ashaketi kwenye meza akiwa anampakulia Lanlan chakula , Edna alishuka kutoka juu akiwa amevalia mavazi yake akiwa amependeza , lakini mavazi yake hayakuwa yale ya kwendea kazini kama ilivyozoeleka , kwani mara nyingi angevaa suti , siku hio alikuwa amveaa gauni la maua maua ambalo lilimfanya kuonekana mrembo Zaidi , huku nywele zake akiwa amezirudisha nyuma na kuzibana na kibanio., huku mabega yake yakiwa wazi.

“Honey unaenda kazini ukiwa umevaa hivyo?”Aliuliza Roma akimwangalia Edna.

“Linaonekana vizuri?”Aliuliza Edna huku akiona aibu na kuvuta kiti na kukaa pembani ya Lanlan.

“Sister Edna unaniangusha , hutakiwi kuuliza swali la namna hio?”aliuongea Yezi na kumfanya Edna kumwangalia.

“Ningeulizaje?”

“Ungeuliza kama ishawahi kutokea siku ukawa haujapendeza na kuwa mrembo”Aliongea Yezi

“Ndio mke wangu Yezi hajakosea kabisa,”Aliongea Roma akikazia na kumfanya Edna kutabasamu na kumwangalia Yezi.

“Yezi unajua kupamba watu na maneno mazuri kwa njia isio ya moja kwa moja , chukua mayai ule ushibe ili ujiandae vizuri na mtihani”Aliongea. Edna huku akimsogezea sahani.

“Mambo ya chuo yanachosha kweli , natamani kumaliza tu japo ndio naanza”.

“Masomo ndio yalivyo , ila kama utakuwa na ndoto kubwa ya kukamilisha mbeleni utapata sababbu inayokusukuma kusoma na mambo yatakuwa rahisi , chuoni hujapata marafiki?”Aliuliza Edna.

“Marafiki ninao , ila wengi wao hatuendani kitabia , hivyo naishia kukata tamaa na kubakia kuwa mwenyewe”Aliongea.

“Kwa tabia yako ni kawaida kukosa marafiki, umekulia mazingira magumu na ukashinda changamoto zote si ajabu kuwa na mtazamo wa kiutu uzima”Aliongea Roma.

“Kwahio inabidi afanye nini?”Aliongea Edna.

“Kuna kipi cha kufanya Yezi ni mtu mzima tayari , hivyo maamuzi ni yake , kama anataka kuwa na marafiki asioendana nao basi inatakiwa aigize kuendana nao, ila kama anataka kuishi kama yeye basi ni bora kuvumilia na marafiki anaotaka watajitokeza, dunia ya sasa imebadilika hata mimi siwezi kuwa na rafiki ambaye muda wote anakuwa kama mzazi”Aliongea Roma huku akitabasamu kifedhuli.

“Anko Roma wewe ni mchokozi , kwahio mimi naonekana kama mzazi?”

“Sijamaanisha wewe ni mzazi , namaanisha una mtazamo wa kiutu uzima kitu ambacho wenzako wengi wanakosa , hivyo ukitaka marafiki unatakiwa kuwa na watu wazima wenzako”Aliongea Roma kurekebisha.

“Hubby unaonaje leo tukipumzika nyumbani?”Aliongea Edna huku akimwangalia Roma , sasa kauli yake kidogo tu imfanye Roma ateme chakula anachokula , kuitwa Hubby na Edna ni jambo ambalo halikuwa la kawaida kabisa.

“Edna unaendeleza mchezo wako ulionzisha asubuhi? Kama ndio mwendelzo naomba uache sijakuzoea hivyo”Aliongea Roma kwani matendo ya Edna hayakuwa ya kawaida tokea arudi asubuhhi hio., sasa alikuwa akikumbuka namna Edna alivyokuwa akijrembulisha asubuhi alivyoingia kwenye chumba chake.

Kauli ya Roma ilimnyong’onyesha Edna na kuonekana kama mtu aliekata tamaa, Roma alikuwa haelewi kama mwenzake alikuwa akijitahidi kuwa ‘Wife material’ na kumwambia wabaki nyumbani ilikuwa ni kutaka kupata muda wa kuwa pamoja.

“Sio mchezo , nilitaka tupumzike siku ya leo , umekuwa bize sana tokea juzi kunisindikiza kazini na kunirudisha, kama hutaki kubaki nyumbani basi sawa”Aliongea Edna kwa kuonyesha namna ya kulalamika huku Yezi akijitahidi kuwa bize na chakula chake , kwa upande wa Lanlan yeye kama kawaida akila hataki usumbufu wa kuongea ndio maana hakumzingatia sana mama na baba yake na kama ataoangea basi ni wakati wakuhitaji chakula cha nyongeza na kubwa Zaidi Kiswahili hajui , hivyo kushindwa kufuatisha maongezi.

“Unamaanisha hutaki Kwenda kazini leo?”

“Ndio kazi ngumu ishaisha na kilichobaki ni wafanyakazi wangu kufanyia kazi sehemu zilizobaki , lakini pia Richie yupo atanisaidia kwenye baadhi ya kazi muhimu”Aliongea.

Roma alishafahamu mahusiano ya Richie na Edna ni ya kikazi , lakini kubwa Zaidi waikuwa marafiki walivyokuwa chuoni , hivyo hakuwa na wasiwasi tena na ukaribu wao, kwani Richie alikuwa nchini kwa ajili ya kazi.

“Ooh ! Kwahi sababu ya kumleta Richie Tanzania sio kwa ajili ya kukusaidia tu kwenye kuunda mavazi , lakini pia kukusaidia katika baadhi ya mambo ya kampuni kama mbadala wa Ernest? Kama ni hivyo ni maamuzi mazuri kwani inaonekana unamuamini”Aliongea Roma.

“Hubby tusiongee mambo ya kazini muda huu , leo ni siku yetu ya mapumziko unaonaje tukiendelea kula?”Aliongea Edna akimkatisha Roma , lakini Edna kauli yake hakujua ni kwa kiasi gani iliwashitua Yezi na Roma , ongea yake ni kama sio yeye vile .

Baada ya maongezi yao ya madakika kadhaa kuisha , huku Roma akiendelea kujiuliza ni kipi kinaendelea , Blandina, Qiang na Bi Wema walijumuika mezani kuendelea kupata kifungua kinywa.

Kwasababu Edna hakuwa akienda kazini siku hio alimwambia Yezi yeye na Lanlan watamsindikiza hadi chuoni na Yezi alifurahi , kwani tokea aanze chuo usafiri wake mkubwa ulikuwa ni daladala au mwendo kasi na mara chache ndio angetumia Uber au Bolt.

Baada ya madakika kadhaa ya Lanlan , Edna naYezi kuondoka Roma alikaa sebuleni akiwa na mama yake.

“Roma unaonaje mabadiliko ya mke wako?”Aliuliza Blandina huku akitabasamu.

“Mama umemfanya nini Edna mpaka akawa hivi , siamini kama ni hatia tu ya kutotimiza majukumu yake kama mke ndio imembadilisha ndani ya usiku mmoja?”

“Siwezi kukusaidia sana maswala ya mke wako kwani sio muda wote nitaishi na nyie , nimejaribu kumuelezea tu Edna umuhimu wa ujana wake , lakini pia nilimuelezea umuhimu wa kuboresha uhusiano na mume , lakini pia nikamuelezea umuhimu wakua na vipaumbele”Aluongea Blandina kwa ufupi.

Upande mwingine wakati Edna akiwa anaendesha kuingia barabara ya Sam Nujoma Yezi aliekuwa amekaa siti ya mbele aliamua kuvunja ukimya.

“Sister Edna , unaonekana wa tofauti sana leo , umeamua kuuteka rasmi moyo wa Anko Roma?”

“Wewe bado mdogo sana , ukiwa mtu mzima utaelewa haya mambo”Aliongea Edna akijifanyisha kwamba yeye alikuwa gwiji wa mapenzi na Yezi hakuwa akijua vitu vingi.

“Mimi sio mtoto tena , ni mwanachuo tayari, Sister nina mbinu za kimauaji ambazo ninaweza kukufundisha, kwa uzoefu wangu niliothibitisha mbinu hizi zinamfanya mwanaume muda wote kukuwazia”Aliongea Yezi kwa kujiamini kwa lugha ya Kiswahili.

Lanlan yeye alikuwana Tablet yake viti vya nyuma akicheza gemu , mtoto huyu tokea aingizwe kwenye ulimwengu wa kucheza magemu alikuwa akiyapenda kweli, lakini mengi aliyaona mitego yake ni mirahisi sana , na kuivuka kwa haraka jambo ambalo linamfanya kujaribu magemu mengine magumu magumu.

“Una mbiniu gani wewe , kwanza hata mapenzi huyajui , acha kuongea ujinga na kazana na masomo”Aliongea Edna

“Sawa Sister nilitaka kukusaidia tu maana niliona mbinu zako ni za kitoto sana”Aliongea Yezi huku akijifanyisha kutulia.

“Unaamini mbinu zangu ni za kitoto?”

“Sister Edna hata mimi mwenyewe nilivyokuona leo nimejikuta nikikosa utulivu , mbinu zako haziibui hisia za mapenzi ila zinamfanya mtu kukosa utulivu, ila kwasababu hutaki , nikikuelezea ngoja nikae kimya”Aliongea Yezi.

“Nina mbinu zangu nyingi za kumteka mwanaume , kama ya asubuhi sio nzuri nitaanzisha nyingine , unaonaje ukajaribu kuongea za kwako angalau nione uwezo wako wa akili”Aliongea Edna huku akiweka usiriasi na Yezi alijikuta akishindwa kuvumilia na kutoa cheko.
 
SEHEMU YA 383.

Edna alijikuta akijisikia vibaya kidogo baada ya Yezi kucheka , alijionea huruma yeye mwenyewe na kujiambia kwanini ni yeye pekee ambaye hakuwa akijua namna ya kudili na mwanaume , ilihali alikuwana uzuri usiokuwa wa kawaida.

“Unacheka nini sasa , kama hutaki kuniambia basi”

“Sister Edna kwa ninavyomjua Anko Roma , ukweli ni mtu mrahisi sana unachotakiwa kufanya ni….”Aliongea na kumsogelea karibu kumuelezea na kumfanya Edna kushangaa kidogo.

“Hio mbinu itafanya kazi?”

“Ndio imnafanya kazi sana , tatizo muda wote uko bize na kazi hata muvi haungalii ungekuwa unajifunza baadhi ya vitu vingine nje na taaluma yako, jaribu angalau kuangalia hata tamthilia za kikorea”AliongeaYezi na kumfanya Edna kukunja uso.

Hakuwa sana mpenzi wa matamthilia wala muvi na mara nyingi alikuwa akiangalia Tv basi ni taarifa ya Habari , hakujua kama kwenye muvi kunaweza kumpatia ujuzi kama alioambiwa.

Upande wa Roma baada ya kukaa kwa muda na mama yake wakiongea kwa kucheka , Roma alikumbuka jambo ambalo hakuwa ameliweka sawa mpaka muda huo , jambo lenyewe lilikuwa ni juu ya mama yake na Nasra , aliona amuelezee mama yake swala lake ili aone kama anaweza kumsaidia.

“Mama unamkumbuka Nasra?”Aliuliza Roma na kumfanya Blandina kumwangalia mwanae.

“Kwanini nimsahau si yule uliempeleka kwao, namjua kwani ashawahi kuwa chini ya uangalizi wa kituo changu tokea akiwa mdogo, vipi mmeingia kwenye migogoro?”

“Hapana!, sio Nasra bali mama yake”

“Mama yake kafanya nini?”Aliuliza na Roma alimuelezea kwa ufupi juu ya Mama yake Nasra kukataa yeye kuendelea na mtoto wake na Blandina mara baada ya kuambiwa hivyo alishangaa na kuvuta pumzi kwa wakati mmoja.

“Mama yake hana makosa kabisa kukukataa, kila mzazi anapenda mtoto wake wa kike kuona anapata mume na sio kuwa mchepuko”Aliongea.

“Mama nahitaji hili swala liishe , kwani linamfanya Nasra kuwa na mawazo na mimi njia zangu zote zimegonga mwamba na sijui ni kipi ambacho kinamfanya mama yake kuwa na msimamo mkali wa kutotaka mimi kuendelea na mtoto wake”

“Kwahio unataka nifanye nini?”

“Ninachotaka ni wewe kunisaidia kuongea nae , huenda wewe kwasababu ni mama yangu akakuelewa isitoshe wanawake mnajua namna ya kupozana”

“Yaani wewe mtoto umekosa aibu , hivi unajua unachoniomba? Ninaanza vipi Kwenda kuongea na mama yake Nasra ilihali tayari namtambua Edna kama mkwe wangu? Vipi kuhusu Edna atanifikiriaje akifahamu?”Aliongea Blandina.

“Mama ninachokuomba ni msaada wako wa kunikingia kifua kwa Mama yake Nasra anaweza akakuamini wewe kuliko mimi”

“Jamani Roma , unaniweka kwenye wakati mgumu na mkwe wangu Edna”.

“Naelewa mama yangu , lakini Edna hatofahamu kwa sasa na hata akijua nitajitahidi kumuweka sawa na asikukasirikie”Aliongea Roma na kumfanya Mama yake kuvuta pumzi, Blandina licha ya kwamba hapendi kujiingiza kwenye mahusiano ya Roma , lakini kuombwa msaada na mtoto wake ambaye anajitahidi kujaza nafasi asizozikamilisha kama mama katika malezi ilikuwa ngumu kumkatalia kwa ombi lake.

Lakini wakati wakiwa kwenye maongezi Edna aliweza kurudi na kuwakatisha kwa kile walichokuwa wakiongea.

“Wife nikajua utachelewa kurudi kidogo?, Kwenye hio mifuko umenunua nini”

“Nilikuambia nampeleka Yezi tu chuo, ndio maana nimerudi , nataka niandae chakula cha mchana haya ni mahitaji”

“Una uhakika utaweza kutoa chakula kitamu?”

“Usiwe na wasiwasi nina kumbuka kila kitu alichonielekeza Najma”Aliongea Edna huku Lanlan akienda kukaa karibu na bibi yake.

Roma alijikuta akimkumbuka Najma , alijua Najma yupo Marekani kwa msaada wa mke wake , lakini hakuwahi kumuuliza ni makubaliano gani alikuwa ameyafanya mpaka akamsaidia kimasomo na matibabu ya kaka yake , lakini Roma hakutaka kumuuliza Edna na kumharibia mudi yake , ilihali alikuwa akijitahidi kuwa mke siku hio .

Ukweli Roma alikuwa pia akipanga kumuuliza Edna kuhusu ‘Deposit Box’ ndani ya benki ya Swiss In , lakini alishindwa kwani alikuwa akihofia huenda mama yake Edna aliweka taarifa ambayo itamfanya Edna kuwa katika mawazo, kwanza alihofia Edna atafahamu Seventeen ni pacha wake , kwani mpaka hapo Edna hakuwa na uelewa wowote kama amezaliwa na pacha mwenzie , lakini pia aliogopa Edna kuelewa kama mama yake alikufa kwasababu ya mwili wake kufanyiwa majaribio ya kisayansi ya kimiminika cha ufufuo.

“Roma acha kumkatisha tamaa mwenzako , huoni anajitahidi?”Aliongea Blandina akimuonya Roma na kweli Roma alitulia.

Mchana Edna aliweza kupika chakula kwa kusaidana na Qiang Xi na alijitahidi sana , iijapokuwa upishi wake haukuwa wa kiwangu cha juu kama wa Bi Wema na Mama mkwe , lakini alijitahidi

Blandina na Bi Wema wote wlaijikuta wakipatwa na ahueni mara baada ya kuonja chakula na kuona ni kitamu na Roma mwenyewe alijikuta akitabasamu na kumnyooshea mke wake dole gumba mara baada ya kuonja chakula kilichopikwa , Edna alijikuta akitabasamu kwa sifa alizopewa.

“Chuby msifie mama yako kakupikia chakula kitamu”Aliongea Roma na kumfanya Edna kumgeukia Lanlan.

“Mom you are the best”Aliongea Lanlan na kumfanya Qiang kucheka kutokana na mwonekano wake.

Baada ya chakula chakula cha mchana Edna alisaidiana na Qiang Xi na kusafischa vyombo , ijapokuwa Bi Wema alimtaka Edna akapumzike , lakini Edna alimwambia atafanya , yeye ndio akapumzike na Blandina alimkonyeza Bi Wema akubali na wote wakakaa kwenye TV wakimuacha Edna afanye kazi zake za nyumbani.

Edna mara baada ya kumaliza kuosha vyombo alikata kata matunda kwa kuyachanganya na mananasi pamoja na matikiti na kisha akamuwekea mama mkwe wake pamoja na Bi Wema na akachukua sahani iliobaki na kutoka nayo nje akimtafuta Roma.

Haikua kawaida kwa Roma kubakia nyumbani siku za katikati ya wiki , hivyo alikaa eneo la bustani sehemu ya mapumziko na kujilaza kivivu akiruhusu chakula kimengenywe vizuri.

“Hubby nimekuletea matunda”Aliongea Edna tena akijifanyisha Romantic

“Wife unaonaje ukinilisha?”Aliongea Roma na kumfanya Edna kumwangalia , ijapokuwa alikuwa akijitahidi kuwa mke bora , lakini aliona Roma anamchukulia kama mtumwa wake,ila alijiambia ngoja ajitahidi hilo lipite.

Nitajitahidi kuwa mke bora kwa siku kadhaa , Nikimteka kimapenzi hawezi kunionea tena kama hivi, mtu ana mikono anataka nimlishe”Aliwaza Edna na kisha akamsogelea Roma na kuchukua kipande na kumlisha mdomoni na Roma alitabasamu kwa kufumba macho bila wasiwasi.

“Ni tamu? ,hili nanasi naona kama halijakwiva vizuri?”

“Hata kama halijaiva ilimradi umenilisha wewe mke wangu kwangu litakuwa tamu”Aliongea Roma huku akiwa ameegamia kwenye kitanda cha kuegamia.

“Wewe ni muongo , kama sio tamu si uniambie”Aliongea Edna kwa kulalamika na Roma alitabasamu.

“Babe ni tamu kweli , endelea kunilisha na ukimaliza nitataka ulale juu ya kifua changu tupunge upepo pamoja”Aliongea huku akijiwazia kwenye akili yake , kama leo ndio siku ya kuhakikisha anachukua pointi zote kabla Edna hajarudi kwenye ukauzu wake.

Sasa Edna mara baada ya kuambiwa akimaliza kazi ya kumlisha anatakiwa kulala kifuani kwa Roma , moyo wake ulienda spidi spidi , alichokuwa akiongea Roma hakutaka kukubali kwani aliamini watu wanaweza kuwaona na mambo kama hayo yanatakiwa yakafanyikie chumbani.

Lakini Edna alijikuta akikumbuka mbinu aliopewa na Yezi asubuhi , alifikiria kidogo bila ya kuwa na uhakika kama ataweza kuitumia muda huo. , huku akiendelea na kazi ya kumlisha Roma.

Baada ya dakika kama tano ya kumaliza Roma alimwambia ni wakati wa kuja kulala nae kwenye kijitanda hicho kidogo cha mapumziko ambacho kinatosha mtu mmoja , ikimaanisha kwamba kama yeye ataongezeka basi itambidi kumlalia Roma kwa juu.

“Babe kama huwezi wewe sema siwezi au naweza”Aliongea Roma huku akicheka kidogo akimwangalia Edna aliekuwa akijiuliza maswali.

Edna alikuwa akisita sita , ukweli hakutaka kumkatalia Roma hususani wakati huo anaojitahidi kufanyia kazi ushauri wa mama mkwe , lakini upande mwingine hakuwa tayari kuonyesha mapenzi waziwazi.

Edna alijikuta aking’ata meno yake na kisha akaweka sahani pembeni na kuinama taratibu kama mtu anaelazimishwa.

“Mtu anaefanya mambo kwa hiari yake hawezi kuwa kama hivi , ni nini kinaendelea kwenye kichwa cha huyu mwanamke?”Aliwaza Roma huku akimwangalia Edna.

Lakini ghafla tu Edna alianza kutoa machozi ya kilio na kuchuchumaa chini na kumshangaza Roma.

“Hubby….. naomba tusifanyie hapa nje”Aliongea Edna kwa kulegeza kimaigizo sauti huku akifuta machozi kwa mkono kama mtoto mdogo, lakini wakati huo huo akitamani litokee shimo atumbukie.

Edna kusema hivyo sio kama hakumuelewa Roma , ila ndio mbinu alioambiwa na Yezi , yaani Yezi alimwambia Edna ajilize bila sababu na kujifanyisha kama mtoto asielewa chochote kuhusu mapenzi, ndio maana Edna akajifanyisha kutafsiri vibaya kauli ya Roma ya kumlalia kifuani na kuigiza kulia huku akitoa kisauti cha kimaigizo.

“Pff.. Hahahahaa” Roma alijikuta akishindwa kujizuia na kuangua kicheko , alijikuta akicheka mpaka machozi yakaanza kumtoka.

“Hahahaha.. Dah! , Edna utaniua ,unachekesha hahaha…” Edna alijikuta akishikwa na aibu kwa jinsi Roma alivyokuwa akimcheka , alijikuta akikasirika na kupiga piga miguu chini.

“Wewe!.. hakuna kuendelea kucheka , Roma acha kunicheka nakuambia”Aliongea kwa kulalamika na Roma alijikuta akijituliza maana siku hio alicheka sana na hakujua mara ya mwisho kutoa kicheko kama hicho ni lini, ila Edna alimchekesha sana kujifanyisha kama wale wadada wanaoigiza kwenye filamu za kikorea.

“Hii mbinu umejifunzia wapi , usiniambie siku hizi na wewe umeanza kuangalia filamu , ungeniita sasa kwa jina la ‘Oppaa’ “Aliongea Roma lakini kwa Edna alijikuta akijutia kwa kitendo chake , huku lawama zote akimpachika Yezi huko aliko.

“Sawa wewe ni cheke tu unavyotaka , nakuambia sirudii tena , nimejitahidi leo kwasababu nilikukosea jana”Aliongea Edna akijiapiza.

“Sio hivyo..”Aliongea Roma na palepale kwa spidi alimchukua Edna na kumkalisha kwenye mapaja yake kwenye kiti.

“Nisamehe sikutakiwa kucheka , umefanya hivyo ili kunifurahisha lakini nikashindwa kujizuia maana ulikuwa unafurahisha”Aliongea na kumfanya Edna kutulia kimya , huku akisikiliza upepo wa baharini ukiwapuliza.

“Ngoja nikukumbatie , mtu yoyote akitusogelea nitafahamu na kukuachia sawa?”Aliongea Roma na Edna alitingisha kichwa na Roma akamvutia kwake na kumkumbatia na kisha wakalala kwenye kiti pamoja cha kuegamia wakipigwa na upepo na kuonekana kimapenzi Zaidi.

Edna alijikuta akitulia tuli hakusogeza hata mguu , alikuwa akisubiria hatua inayofuata baada ya kukumbatiwa , lakini mwishowe Roma hakuonyesha kumfanyia chochote na kupata ahueni lakini pia kuonekana kutorishidhwa , mwenyewe alijishangaa kwani hakujua ni kipi kingine alitegemea mara baada ya kukumbatiwa.

Baada kama nusu saa tu kupita wakiwa wamelaliana Edna alijikuta akiinua uso wake na kumwangalia Roma , lakini alishangaa kwani Roma alikuwa usingizini na aliendelea kumwangalia kwa namna ya kushangaa uso.

“Unashangaa uhandsome wa mumeo?”aliongea Roma pasipo ya kufumbua macho na Edna hakujibu na Roma alifumbua macho na kutabasamu na kisha akanza kumgusa gusa nywele zake kwa namna ya kuzichezea.

“Edna kwenye Maisha yangu niliamini Maisha ya ndoa ni aina ya Maisha ambayo siku zote unakuwa na furaha na kucheka na mwenza wako , kutembea pamoja , Kwenda matembezini na kufanya vitu vingi kwa pamoja , kununuliana zawadi na mengineyo , lakini nilikuja kuamini Maisha ya ndoa vyote hivyo ni vya ziada na kikubwa Zaidi ni kuchangamkiana kama mke na mume kwa namna ya kupendana , iwe jua iwe mvua, iwe nyakati za huzuni au nyakati za furaha kikubwa ni kwamba unae mtu wa kumtegemea ambaye unaweza kumueleza shida zako na mkafarijiana nyakati zote na kuelewana , kama sasa nimeweza kupitiwa na usingizi huku mtu ninaempenda akiwa kwenye mikono yangu , tulichonacho kati yetu kinatosha sana , hivi inatosha kabisa”Aliongea Roma.

“Hivi tu mbona ni rahsi inatosha kweli?”Aliuliza Edna kwa upole.

“Mhmh! Kwangu mimi sitaki ufanye mambo mengi kwa ajili yangu , unafikiri sisi kutokufanya mapenzi ni hitajio langu kubwa kutoka kwako , umri wangu huu sio wa kijana anaeanza balehe au ambaye hajawahi kukutana na mwanamke kimwili , wewe unahisi muda wote nawaza kufanya mapenzi na mwanamke ?”

“Edna tokea mwanzo nilichokuwa nahitaji kutoka kwako ni kubadilika na sio kubadilika kwa kunijali mimi bali kujijali wewe mwenyewe , nahitaji kukuona ukiacha kufanya kazi kama hakuna kesho , kushirikisha watu wanaokupenda kwa kila kitu kinachokutia wasiwasi , sijali sana kama utakuwa ‘Romantic’ kama ulivyofanya leo au siku za mbeleni , siku nilivyokuoa si kwasababu ya mwili wako , ninachotaka kutoka kwako ni wewe kuwa naMaisha ya furaha, ukiwa na furaha sitoweza kuwa mwenye hatia na mimi pia nitakuwa ni mwenye furaha” Aliongea Roma kwa kirefu na kumfanya Edna kuanza kutoa machozi.

“Ijapokuwa nimefurahishwa na juhudi zako za kutaka kunifurahisha , lakini sitaki ufanye vitu ambavyo hujazoea , mapenzi hayako hivyo na mimi pia mumeo sio mgumu sana kufurahi”Aliongea Roma na kufanya moyo wa Roma kuwa wa moto.

“Wewe ni mgumu kufurahishwa, kama kweli hujali sana kufanya mapenzi kwanini una wanawake wengi?” Aliuliza Edna na kumfanya Roma kushindwa kutoa jibu , alijifanyisha kama hajasiki swali aliloulizwa.

“Mom , Dad..!Lanlan anataka kucheza gemu na hawezi kucheza peke yake”Ilisikika sauti ya Lanlan na kumfanya Edna kujitoa kwenye mwili wa Roma .
 
SEHEMU YA 384.

Kwenye watu ambao walikuwa na taarifa ya kupotea kwa Kizwe alikuwa ni Matilda pamoja na Gavana wa benki , Matilda ndie aliekuwa mwenyeji wa Kizwe tokea kufika kwake hapa nchini akishirikiana kwa karibu na Gavana na hata kikao cha Kizwe kuweza kukutana na wakuu wa benki wao ndio waliokiratibu.

Mwanzoni Matilda alijua kabisa Edna anakwenda kupoteza kampuni kwa yale ambayo yalikuwa yakiendelea kwenye kampuni na hata wakati wakuangalia soko la hisa pamoja na kufatilia maendeleo ya kampuni ya Vexto ,Kizwe alikuwa pamoja na Matilda ndani ya makao makuu ya kampuni ya JR.

Matilda hakutaka kabisa kuhusika moja kwa moja katika kudili na Edna , alikuwa akimsaidia Kizwe sana pamoja na Ernest katika mipango ya kumfilisi Edna , lakini alihakikisha anacheza karata zake nyuma ya pazia kwa namna ya kutoa msaada, kwanza kabisa hakuwa na knyongo sana na Edna kama ilivyokuwa kwa Kizwe pamoja na Ernest , yeye mapambano yake na Edna yalikuwa ni ya kibiashara Zaidi na hakukuwa na Zaidi ya hapo na Zaidi ni kwamba alichokuwa akitaka Matilda sio kampuni ya Edna bali ni kuwa na umiliki wa asilimia mia moja wa kampuni ya JR, alichokuwa nacho Matilda labda ni ule wivu tu wa mafanikio ya Edna akijilinganisha nae , lakini sio chuki a ya kulipiza kisasi.

Sasa Matilda alikuwa ni moja ya watu ndani ya Tanzania ambao hawakuamini kile alichokifanya Edna kuokoa kampuni na haikuwa kuokoa kampuni bali hakuamini Ernest kuingia kwenye mtego wa Edna kwa kuiba nyaraka feki , lakini kubwa Zaidi yeye mwenyewe alishindwa kuelewa imekuwaje mpaka Edna kafanikisha kushinda mradi wa Adani kwani hata kampuni yake ilikuwa imetoa ombi la kupewa zabuni ya ununuzi wa mradi huo na kuuendeleza.

Matilda alijikuta akimkubali Edna licha ya kwamba alikuwa akimuonea wivu , kitendo cha kuwaaminisha watu kama kampuni inafilisika halafu dakika za mwisho kupindua meza , kilikuwa ni cha kishujaa ambacho hata yeye mwenyewe aliamini kwamba hawezi kufanya licha ya kwamba walikuwa na nafasi sawa.

Sasa siku hio wakati wakishuhudia kupindua meza kwa Edna alikuwa pamoja na First Lady , yaani Kizwe na kitendo cha Edna kufanikiwa kilimkasirisha sana First Lady na hata mwanamama huyo alipochukua jukumu la kumfuata Ernest hakutaka kuingilia sana na kukaa pembeni , hakutaka kuiba ugomvi uliokuwa nao , ni kweli Edna alimchukulia kama adui lakini vita vyao havikuwa vya kupigana ana kwa ana bali vilikuwa ni kushidana mbinu kiakili na wakati huo alikuwa ameshinda na alipaswa kukubali kushindwa tofauti na First Lady.

Sasa ilipita siku nzima pasipo ya kusikia kitu chochote kutoka kwa Kizwe na kubwa Zaidi ambalo lilimfanya kuwa na wasiwasi ni kusikia kwamba Ernest katoka nje ya nchi akiwa na mwanamke wake , jambo hili lilimtia sana wasiwasi na kuamini huenda Roma alikuwa akihusika moja kwa moja , kwani alikuwa akielewa hakuwa mtu wa kawaida kabisa kwa kile alichokishuhudia kikitokea kwa baba yake.

Matilda siku hio alikuwa ndani ya ofisi yake akiendelea na majukumu lakini licha ya hivyo alikuwa na maswali mengi juu ya mahali alipo First Lady , kuna hisia zilikuwa zikimwambia ashakufa lakini pia kuna hisia zikimwambia hajakufa.

Baada ya kuona akili yake haikai sawa na vijana wake aliowapa taarifa hawampi majibu anayoyataka , alifanya maamuzi ya kuondoka ofisini akidhamiria Kwenda nyumbani kumsalimia baba yake , kwani ni takribani siku tatu hakuwa ameonana nae.

Baada ya kutoa baadhi ya maelekezo kwa msaidizi , ambaye ni mpenzi wake bwana Isaack , aliondoka hapo na kuelekea nyumbani.

Dakika chache tu alikuwa ashafika , Matilda licha ya kwamba jumba lao lilikuwa kubwa lakini hakuwa akiishi kwao na jumba lote alikuwa akiishi Queen na baba yake pamoja na wafanyakazi.

Matilda mara baada ya kuingia ndani aliulizia wafanyakazi kama baba yake yupo na aliambiwa yupo kwenye chumba chake cha kujisomea , aliulizia na uwepo wa Queen na aliambiwa pia yupo alikuwa amelala , Matida alishangaa kidogo kuambiwa Queen amelala.

Alipandisha juu mpaka kwenye chumba cha baba yake na aligonga mlango na kuruhusiwa kuingia na akamkuta Mzee Alex akiwa bize akisoma kitabu.

“Matilda mbona umekuja kuniona muda huu , ni kwema huko utokako?”Aliuliza Mzee Alex huku akvua miwani yake ya kujisomea kwa ukaribu na kumwangalia Matilda.

“Kwema tu baba?”

“Okey afadhali , haya niambie kilichokuleta niendelee kusoma”Aliongea na kumfanya Matilda kumwangalia baba yake ambaye alikuwa na mabadiliko makubwa.

“Honestly! Dady come on , unajua kilichonileta”Aliongea.

“Nitajuaje kama hujaniambia , umesema kampuni inaendelea vizuri na hakuna tatizo lipi lingine la manufaa , kama huna la kuniambia mimi nina chakukuelezea”Aliongea na kumfanya Matilda kuvuta pumzi.

“Firsl Lady is missing Dady!”Aliongea kimaanisha kwamba mke wa raisi amepotea.

“Una uhakika?”

“Ndio baba , naogopa isije kitu kibaya kumpata”

“Kwanini unahisi kitu kibaya kumpata , Yule ni mtu mzima na anajua anachokifanya na kama kuna kitu cha hatari alichokianzisha inamaanisha alikuwa akijua matokeo yapo ya aina mbili kufanikiwa au kushindwa , kwanini uwe na wasiwasi kwa mtu ambaye ametake ‘Risk’?”

“But Dady I am involved”Aliongea akimaanisha kwamba na yeye anahusika.

“Najua unahusika , lakini si nilikuambia kama usijihusihe moja kwa moja kwenye mipango yake , haukuufanyia kazi ushauri wangu?”

“Nimefanya hivyo baba lakini mpango umefeli Edna was too clever”Aliongea na kumfanya Mzee Alex kutabasamu.

“Sio kuwa na akili tu , Edna ni mtoto aliezaliwa kufanya biashara ni kipaji alichozaliwa nacho ia makosa kufanya vitu kushindana nae kwa njia zisizo sahihi kwani ataendelea kutuoana wapinzani dhaifu”Aliongea Mzee Alex na kumchanganya Matilda.

“Kwahio baba unashauri nini?”

“Kwasasa akili yako inatakiwa kuwazia namna ya kuifanya kampuni yetu kuwa kubwa na sio kumuwazia First Lady, wewe ni mtoto wangu na kama kuna namna yoyote utahusika kwa kile kitakachomtokea basi nitahakikisha hakuna kinachokupata”Aliongea na kumfanya Matilda kuwa na ahueni.

“Matilda ushawahi kusoma kitabu cha Ferrucio Lamborgin kinachohusiana na maisha yake ya kibiashara katika magari?”Aliuliza.

“Baba unajua mimi mvivu wa kusoma , sijui kama ashawahi kutoa kitabu?”Aliongea Matilda na kumfanya Mzee Alex kutabasamu.

“Kwa staili yako hio ya kutopenda kujifunza kusoma vitabu huwezi kumshinda Edna , una safari ndefu ya kufikia levo yake”

“Unanilaumu wakati wewe ndio uliosababisha , hakuwahi kutulea kwa ajili ya kuongoza kampuni , mimi ni tofauti na Edna”

“Najua na sio wakati wa lawama kwa sasa lakini hata hivyo nilifanya kwa ajili yenu, kwasasa nakupa kazi ya kusoma kitabu cha Lamborgin ukimaliza nitakueleza hatua inayofauatia namna ya kumshinda Edna kibiashara”Aliongea Mzee Alex na kumfanya Matilda kushangaa lakini aliishia kutingisha kichwa.

“Ukitoka hapa nataka ukae chini na mdogo wako Queen , kuna jambo kubwa limemtokea na nataka umsaidie”Aliongea na kumfanya Matila kushangaa , hakujua kama Queen alikuwa na matatizo.

“Ninaenda kumuona sasa hivi”Aliongea na kisha akanyanyuka na moja wa moja akaenda chumbsni kwa Queen na ile anaingia alijikuta akishangaa kwa hali aliokuwa nayo mdogo wake na aliishia kuita jina lake kwa mshangao.

******

Kizwe hakutaka kufa , ni kweli kwamba alikuwa amebakwa na wanaume Zaidi ya wanne , lakini kwa maneno ya Lekcha aliyaona yana ukweli wake, alijiambbia maadui zake wapo hai wanafurahia Maisha huku yeye akiwa hapo uchi wa mnyama hivyo hakustahili kufa , alijiapiza maumivu anayopitia ni lazima ayarudishe kwa Zaidi ya mara kumi.

Yale mawazo ya kuwa mke wa raisi hakuwa nayo tena na mpango wake mpya ni kuishi kwa ajili ya kisasi , aliamini hata mume wake kama taarifa zishamfikia asingemtaka tena na kumpa thamani aliokuwa akimpa mwanzo hivyo hata kurudi Rwanda sio wazo lake la kwanza kuwa nalo kwenye akili , alikuwa na watu wengi pia wakupigia ndani ya Tanzania kuwaomba msaada , lakini pia hakuwa tayari kufanya hivyo.

Lekcha alijikuta akutoa tabasamu mara baada ya kumuona Kizwe kuvaa dela alilomletea pamoja na nguo ya ndani mpya, licha ya kwamba dela lilichakaa sana lakini lilimpendeza na kumfanya kama mwanamke wa kawaida na sio kama mke wa raisi tena.

Lekcha alimpatia Kizwe machungwa , lakini mwanamke huyo alikataa , hakuzoea kula machungwa asubuhi asubuhi pamoja na maembe na Lekcha hakumlazimisha kufanya hivyo.

“Tunaendelea wapi?”Aliuliza Kizwe kwa kingereza na kumfanya Lekcha kutabasamu.

“Naona ushaanza kuwa na adabu”Aliongea Lekcha huku akichukua gunia lake.

“Nimekuuliza swali, sitaki uswahili”

“Okey! Kazi yangu kubwa ni kuokota makopo ya plastic na Kwenda kuuza nazunguka ndani ya wilaya yote hii ya Temeke kufanya kazi hio”Alielezea Lekcha na kumfanya Kizwe aangalie mguu mmoja wa Lekcha lakini alishindwa kuongea chochote ijapokuwa Lekcha alionekana kuwa fukara wa kutupwa , lakini alionekana kwa ukaribu kama mwanaume mwenye uso mzuri ni hivyo tu umekosa matunzo na alijiuliza Lekcha atakuwa na stori gani kwenye Maisha yake , kwani alionekana kubwa na busara.

Lekcha baada ya kutoa maelekezo ya kazi yake kwa kirefu kama vile mtu anaejivunia sana na kazi hio , alipomaliza alimwambia Kizwe amfuatishe kuna sehemu ampeleke akajisafishe na Kizwe alijikuta akijawa na tumaini kwa maelezo ya Lekcha na safari ya kutoka darajani ilianza rasmi.

Kizwe hakuamini kama ni yeye , kila alipokuwa akitembea hatua kadhaa alikuwa akijishutukia ni kama vile aliogopa watu kumtambua kutokana na namna wanavyomuangalia , lakini hio sio kweli kilichomfanya kuangaliwa sana ni kitendo cha kuwa na Lekcha , kwani jamaa huyo alikuwa maarufu na hakuwahi kuonekana na mwanamke.

Sasa kilichokuja kumuacha hoi Kizwe ni kwamba hakupelekwa kule alikoahidiwa bali Lekcha alikuwa bize kukusanya chupa kila anapopita na safari ilionekana kutofikia mwisho.

Walipita chocho zote za Tandika na wakasonga mbele huku Lekcha akiwa mbele na Kizwe akiwa nyuma na kila baada ya dakika kadha aalikuwa akigeuka nyuma na kumwangalia mwanamke huyo.

Kilichomsaidia Kizwe kuweza kutembea umbali mrefu ni mazoezi , aliokuwa akifanya kila siku ya kuweka mwili wake sawa, lakini licha ya hivyo kutokana na joto la jiji la Dar uvumilivu ulikuwa ukimshinda.

“Vumilia bado safari ndogo sana kufika sehemu niliokuwambia na tutapumzika”

“Nahisi njaa”Aliongea kwa kingereza na kumfanya Lekcha kufikiria kidogo na kisha akaangaza macho kulia na kushoto na aliweza kuona duka moja lilikuwa mbele yake upande wa kushoto.

“Nina hizi mia tatu tu zilizobakia nitakununulia mkate”Aliongea.

“Nahitaji maji kwanza”Aliongea na Lekcha hakumjali na kuendelea mbele na furushi lake la chupa na alivyofika dukani alinunua Donat za Azam mbili kwa hela aliokuwa nayo na kisha akampatia Kizwe akamwambia safari iliobaki ni kutafuta maji ya kunywa.

Watu waliokuwa wakimwangalia Kizwe kwa mshangao , unajua licha ya kwamba alikuwa mtu mzima lakini uzuri wake haukujificha alikuwa na sura nyororo na nywele ndefu ambazo zina matunzo licha ya kuchafuka kidogo , sasa wengi ya watu waliokuwa wakimfahamu Lekcha walijiuliza huyo mwanamke ni nani.

Kizwe hakujali watu waliokuwa wanamwangalia , kwanza alikuwa akikwepesha macho kila aliekuwa akimwangalia usoni.

“Usiwajali wanaokuangalia wananishangaa mimi kwa kuwa na mwanamke mzuri kama wewe”Aliongea Lekcha na kumfanya Kizwe kumshangaa.

“Nimechafuka namana hii, bado naonekana mzuri kwenye macho yako?”

“Unaongea nini wewe , licha ya kwamba umechafuka lakini uzuri wako haujifichi, wewe ni mzuri ndio”Aliongea Lekcha na kumfanya Kizwe kumshangaa na kisha akaendelea kumfuata kwa nyuma , hakuwa akielewa kwanini anamfuata mwanaume huyo muokota chupa , alijiambia labda ni kwasabau alikuwa amemuahidi kuna sehemu ataweza kupata maji ya kuoga.

Baada ya kufika sehemu moja kwenye kijiduka chenye friji nje , Lekcha alinunua kandoro na kisha akampatia Kizwe aliekuwa kwenye mshangao.

Lakini kwakuwa Kizwe ashawahi kuwa mwanajeshi hakuleta ubishi , alichukua kale kandoro na kisha alifyonza maji yote na nusu yaliobaki alisuuza mikono na kutoa ile donati kwenye mfuko na kula huku akitembea na kumfanya Lekcha kwa mara ya kwanza kutabasamu.

Baada ya kutembea Zaidi ya nusu saa nyingine hatimae walikuja kutokezea kwenye mtaa wa Chalambe, Rangi tatu, maeneo ya Kilamba , upande huo Lekcha alionekana kutofahamika sana kwani watu walipunguza kumkodolea macho.

Baada ya kutembea kwa madakika kadhaa , hatimae walikuja kusimama nje ya geti la rangi nyekundu eneo Bias Tanesco na kisha kugonga mlango na kufunguliwa na mwanamke alievaa juba.

“Lekcha ingia , ni Zaidi ya wiki sikukuona ukirudi?”

“Wanaume tuna mambo mengi ya kiutafutaji”Aliongea Lekcha lakini Mwajabu macho yake yalikuwa kwa Kizwe.

“Mwajabu huyu ni mgeni wangu”Aliongea.

“Oooh! Sawa , hongera”Aliongea Mwajabu huku akitabasamu na Lekcha hakujibu kitu Zaidi ya kumpa ishara Kizwe aingie.

Sasa ilionekana Lekcha alikuwa akiishi hayo maeneo na alikuwa amepanga kwenye nyumba hii ya Juma , kwani baada ya kufika , alienda moja kwa moja kwenye chumba ambacho Roma alikuwa akiishi na kumkaribisha Kizwe chini kwenye godoro.

Kizwe alijikuta akiangalia mazingira ya chumba hiko , alikuwamtu mzima na mwwenye uzoefu mwingi hivyo kwake mazingira kama hayo hakuwa mwenye kuyashangaa sana na alishawahi kuyaishi.

“Nilijua makazi yako ni kule kwenye daraja?”

“Kuna sababu ya mimi kuwa na makazi ya aina mbili, hapo nje kuna bomba la maji chukua ndoo hii ukachote na ukajisafishe nitatafuta namna ya wewe kupata chakula”Aliongea na Kizwe hakuleta ubishi.

Mwajabu alikuwa ni mke wa Juma ambaye aliolewa mara baada tu ya Juma kutoka hospitalini , alikuwa ni mwanadada ambaye anaheshimu dini sana na alimkuta Lekcha akiishi hapo nyumbani kwao akiwa kama mpangaji.

Lakini kwa maelezo ya mume wake Lekcha hakuwahi kuonekana na mwanamke , lakini pia kitu kinachoshangaza sana kuhusu Lekcha licha ya kwamba alikuwa amepanga hapo alikuwa akilala mara moja moja sana lakini pia hakuwahi kushinda hapo , hivyo Lekcha kwenye mtaa huo hakuwa maarufu kabisa kama mtaa wa kule darajani.

Kizwe hakumuonea aibu tena Lekcha alivua nguo zake zote mbele yake kitendo kilichomfanya Lekcha kukosa utulivu kutokana na umbo la mwanamama huyo ambaye amempita umri Lekcha alikuwa na miaka arobaini tu hivi ila Kizwe umri wake ulikuwa Zaidi ya arobaini.

Baada ya kujifunga na kipande cha shuka kilichokuwa juu ya godoro alitoka na Kwenda kujisafisha baada ya kuelekezwa bafu lilipo.

Baada ya Kizwe Kwenda kuoga ilibidi Lekcha kutoka na Kwenda kubisha hodi nyumbani kwa Mwajabu na aliomba kama kuna chakula chochote Mwajabu amsaidie huku Lekcha akielezea kuwa mwanamke aliekuwa naye yupo kwenye matatizo na aliamua kumsaidia.

Mwajabu hakuwa na Roho mbaya kulikuwa na mihogo aliopika hivyo aliipasha na kisha akampatia Lekcha pamoja na juisi ya kutengeneza.

Ukweli Maisha ya Juma hayakuwa mabaya sana , kulikuwa na mabadiliko makubwa tofauti na mwanzo na Juma ile kazi yake ya kubeba mizigo alishaasha na alikuwa akifanya kazi ya miamala yaani kazi ya uwakala. Na mtaji aliupata kupitia Edna , kwani licha ya kutoa hela ya matibabu Edna alitoa na hela ya ziada ambayo ingemsaidia Juma kwenye matumizi ya kawaida wakati dada yake akiwa masomoni.

Hivyo hela aliopata ndio akafanya maamuzi ya kufungua biashara lakini pia kiasi kidogo akaamua kulipia mahali na kumuona Mwajabu, hivyo Maisha hayakuwa mabaya sana na Juma alikuwa amejifunza kupitia tatizo lake na alimrejea Mungu na kuishi Maisha ya kutendea watu wema kama alivyotendewa yeye na tabia yake hio alimuelekeza na mke wake , kuhakikisha anatendea watu wema kwani ndio ibada na Mwajabu alionekana kumuelewa mume wake kwani hata yeye alikulia kwenye mazingira ya dini.

Lekcha alipatiwa vitu vyote muhimu na Mwajabu akaweza kumpatia Dela na vijisendo akimwambia Lekcha akampe yule mwanamke kubadilisha raba zake ambazo zimechafuka na Lekcha alishukuru.

Baada ya Kizwe kumaliza kuoga Lekcha alimuonyesha dela lingine ambalo amepewa na Mwajabu na Kizwe alitabasamu na kulipokea kwa furaha pamoja na vijisendo vya kuvaa miguuni.

Kizwe haikueleweka alikuwa akifikiria nini , lakini kadri alivyokuwa akimwangalia Lekcha ni kama kuna kitu ambacho sio cha kawaida alichoona kutoka kwake ni hisia ambazo kwa utu uzima huo aliwahi kuzipata miaka mingi nyuma wakati akiwa anakutana na mume wake raisi Jeremy.

“Mbona uniangalia , kaa chini ule chakula tukaendelee na kazi”Aliongea.

“Niambie kwanini uliamua kunisaidia nisijiue na sasa nipo hapa ukiendelea kunisaidia au unafahamu mimi ni nani?”Aliuliza Kizwe.



ITAENDELEA WIKI IJAYO ALHAMISI SEE YOU
NAMBA WATSAPP 0687151346
 
Kuna story moja matata sana ya kijasusi humu inaitwa vipepeo weusi! Tulifuatilia kwa miaka miwili tangu 2016 mpaka 2018 ikawa inaendelea mpaka 2020 ndo tukakata tamaa haijaisha mpaka leo! Hata hii tutavumilia tu! Nimechungulia tangu imeanza! Jamaa bado ana moyo wa kutupostia! Ukweli ni kwamba sisi wa free basic na vi itel vya batan tunateseka sana! Kaka singanojr tafadhal fumbua macho utuone kama wale wa wasap tu! Tunateseka mno
vipepeo weusi iliisha ikaenda Hadi part two.

nilipenda kile kipande jamaa alipojipeleka jera huko na nuimbo zao
 
SEHEMU YA 379.

Licha ya Roma kuwa katika hali ya msisimko , lakini alijikuta akiuhusudu uwezo wa Omari kugeuza maji kuwa siraha , Roma alikuwa akielewa katika ulimwengu wa majini kila kitu kinaweza kugeuzwa kimaajabu na kuwa siraha. Lakini licha ya kusikia juu ya habari hizo hakuwahi kushuhudia kwa macho, licha ya kwamba alikuwa amejifunza mbinu za kijini kupitia kwa Master Chi hakuwahi kufika ujinini kabisa na kushuhudia majini ya levo za juu wanavyotumia uwezo wao kimaajabu katika mapambano, hivyo ni rahisi kusema kwamba Roma alikuwa na shauku sana yeye mwenyewe ya kujua akifika levo za juu ni uwezo wa aina gani ambao aataweza kuwa nao.

Omari hakutaka kumchelewesha Roma kwani baada ya kutengeneza donge la maji ambalo lilikuwa likizunguka kwenye mikono yake palepale aliligeuza na kuwa kama kitenesi cha barafu.

“Hades chukua hio?”Aliongea Omari na kisha kama vile mwanamke akicheza mpira wa rede alurusha kitenesi kile cha barafu kuelekea kwa Roma , upande wa Roma wala hakuwa na wasiwasi , kwani alijiambia ni rahisi sana kukwepa barafu huo kutokana na spidi yake tena alidharau kwa kitendo cha Omari kumrushia siraha ya kitoto namna hio.

Lakini ni kama Omari alikuwa akitegemea Roma kukwepa kirahisi na siraha yake ilipomkaribia Roma kama nusu nchi , palepale Omari alifanya maajabu mengine na kupasua kile kitenesi cha barafu na kugeuka vipande vya barafu vikiwa na mwonekano kama wa glasi.

Roma mwenyewe alijikuta akipatwa na kiwewe kwani hakutegemea kama Omari anaweza kufanya jambo la aina hio , kugeuza barafu kuwa kama vipande vya glasi , na kwakuwa yeye mawazo yake mwanzoni yalikuwa ni kukwepa hivyo alishindwa kukwepa vipande vyote kwa haraka na viwili kati ya vingi vilimchoma kwenye mwili wake katika eneo la kifua na kwenye paja la mguu

Roma alijikuta akijisikia maumivu yasiokuwa ya kifani , kwani kilichomchoma sio vipande vya glasi bali ni barafu hivyo ule ubaridi wake ulimletea maumivu makali sana.

Omari baada ya kuona baadhi ya vipande vilimpata na kumchana kwenye mwili , palepale alitengeneza kitenesi kingine cha barafu na ile anakamilisha , Roma ashatoa vile vipande na mwili wake ulikuwa ukijiponyesha kwa haraka sana , hivyo maumivu yalikuwa makali sana mwanzoni , lakini kadri muda ulivyokuwa ukisogea yalikuwa yakipona kwa haraka sana, hata kutoyasikia tena.

Roma alivyoona Omari anarusha tena barafu lingine kuja kwake aliona akifanya uzembe vipande vile vitampata tena hivyo alitumia uwezo wake wa kuhama sehemu moja Kwenda nyingine na jaribio lake lilileta faida kwani Omrri alivyorusha barafu lile kuelekea kwake alipotea sehemu aliokuwa amesimama na kuja kuibuka nyuma yake na kudhamiria kumpiga teke la ubavuni , lakini Omari alionekana kuwa na hisia kali sana kwani ile Roma anamkaribia kwa ajili ya kumpiga alitumia spidi kujiondoa na teke la Roma likapita.

Sasa ukumbuke huu ni mpambano wa kutumia mbinu za kijini peke yake yaani kwa maana rahisi Roma hakutakiwa kubadilika kabisa kama mwili wake ulivyotengenezwa.

“Hades kabla ya kuja hapa Tanzania nimejifunza mbinu zote ulizotumia kupambana na maadui wengi , hvyo nimejiandaa vya kutosha kukwepa mapigo yako”Aiongea Omari.

“Naona umenileta baharini kwa ajili ya kutumia maji kama siraha , lakini hii ni mbinu ambayo imepitwa na wakati dakika moja iliopita”Aliongea na kumfanya Omari kutabasamu.

“Hades unaonekana kutokufahamu mambo mengi sana kuhusu uwezo wa kijini , lakini kutengeneza barafu sio lazima uwepo wa maji , ninaweza kukusanya mvuke angani na kutengeneza barafu vilevile”Aliongea na palepale alianza kuinua mikono yake juu akiwa kama anajiandaa kupiga mbu hewani na palepale mikono yake ilitengeneza mvuke kama wingu na alianza kulizungusha lile wingu kwa kasi sana kama vile analipoza na palepale mvuke ule uligeuka maji na hatimae barafu kama kitenesi kwa mara nyingine.

Roma alijikuta akishangaa na kumfanya Omari kutoa kicheko.

“Umewezaje?”Aliuliza Roma na Omari alitabasamu.

“Hades katika mbinu za kichawi kile ambacho unanuia kwenye akili yako ndio unatengeneza kama siraha , ijapokuwa nipo kwenye levo ya Nafsi haimaanishi mtu mwingine ambaye yupo kwenye levo kama yangu atakuwa na mbinu sawa za kimajaabu katika kupambana , kila mtu anapata siraha kutokana na namna anavyofikiria”Aliongea Omari na palepale alipotea akiwa ameshikilia barafu lake na kuja kuibuka nyuma ya Roma , lakini akapotea tena na akaaja kutokea mbele yake tena na Omari akapotea tena na kutokea upande wa kulia halafu akapotea tena , lakini sasa jambo ambalo limemshangaza Roma ni kwamba baada ya Omari kupotea walitokea Omari wanne kwa pamoja wanaofanana kila kitu , yaani katika maeneo yaleyale ambayo alisimama na kupotea kwa mara nne mfululizo na Omari wote wa nne walikuwa wameshikilia vitenesi vya barafu, sasa kwa binadamu wa kawaida asingeona , lakini Roma aliona kwani hakuwa wa kawaida.

“Hahaha … Hades upo ndani ya mtego wangu kwa levo yako ni ngumu kutoka” waliongea Omari wote na kumfanya Roma kushindwa kumjua Omari halisi ni yupi kati yao , mpaka hapo alijua hao wote watakuwa feki na mmoja wao atakuwa ndio Omari mwenyewe , lakini alishindwa kujua haraka sana ni yupi kati yao , alijiona akiwa yupo kwenye duara.

Roma aliona hapo akizembea atamruhusu Omari kumuadhibu na pigo lingine , jambo ambalo hakuwa akitaka litokee kabisa na palepale alifumba macho yake na kuanza kufikiria kwa kutumia hisia kwa hali ya spidi sana.

Upande wa Omari aliekuwa amejigawa kwa sura nne hakutaka kumruhusu Roma kupata muda mrefu wa kufikiria , hivyo alirusha mabarafu yale yaliokuwa kwenye mfumo wa vitenesi kwa pamoja kumlenga Roma aliesimama katikati.

“Arrrgh…!!!” Ulisikika mguno wa maumivu na haukuwa ni wa Roma bali ulikuwa ni wa Omari mwenyewe.

“Hahahaha…!!”Roma alijikuta akitoa cheko la furaha mara baada ya kutegua mtego wa Omari.

“Mbinu yako ni ya kijinga sana , nikiri sikuwa na uelewa wa kutambua mtego wako kwa haraka sana , lakini baada ya kuelewa kuwa sura zako zote nne ni feki nikafikiria ni kwa namna gani unaweza kuzidumisha zote kwa pamoja na kuonekana kuwa halisi nikajua tu kuna namna ambavyo unazitawala”Aliongea Roma baada ya kumpiga pigo la ngumi Omari.

Sasa ilikuwa hivi baada ya mabarafu kurushwa kuelekea upande alipokuwa amesimama , palepale aliweza kufikiria namna ambavyo Omari aliweza kutengeneza sura hizo feki Roma aliona abahatishe kwa kuamini kwamba sura zote nne ambazo zimemzunguka ni feki , hivyo aliamini Omari atakuwa amesimama sehemu ambayo ataweza kuziongoza sura zote hizo na kuonekana halisia na ndio maana yale mabarafu yalivyomkaribia mkaribia alitoka pale aliposimama kwa spidi kali sana kuelekea juu katika mstaari mnyoofu huku akidharimiria katika akili yake kwamba lazima Omari atakuwa juu yake na ni kweli ile anafika mita kadhaa tu aliweza kuhisi uwepo wake na kuachia ngumi ambayo ilimpata vyema Omari na hatimae sura zake zote nne zikapotea.

Kitu kingine ambacho kilimfurahisha Roma ni kwamba kitendo alichokifanya ni kama kimemuwezesha kuelewa maana halisi ya levo ya Mzunguko kamili( muunganiko wa Yin na Yang).

“Umewezaje kugundua nipo juu Hades?”Aliongea Omari ambaye alikuwa akijiandaa kuachia pigo lingine.

“Ni rahisi sana mbinu uliotumia inaeleweka hata kisayansi, umetumia ‘Centripetal Force’(nguvu kati) kuweza kutengeneza na kuzidumisha sura zote nne zinazofanana kwa kila kitu na wewe , umefanikiwa kufanya hivyo kwa kutumia levo zote mbili , ya mzunguko kamili pamoja na ya Nafsi”Aliongea Roma na kumfanya Omari kutabasamu.

“Naona umevuka mtego huu lakini pia umeweza kutoka levo ya Nusu Mzunguko Kwenda Mzunguko mwingine hongera sana, fumbo linalokuja huwezi kulielewa na itakuwa ni mwisho wako , kwani nina kwenda kutumia uwezo wangu wa juu Zaidi”Aliongea Omari.

Ni kweli kabisa maneno alioongea Roma ni sahihi , unachopaswa kuelewa katika maswala ya kuweza kung’amua mbinu za kijini ni kwa kufumbua fumbo kwa namna ya kufikiria(meditation) , sasa kwa mfano mbinu ya kimaajabu aliotengeneza Omari ilikuwa ya kawaida sana kama utaifikiria kisayansi kwa kutumia kanuni za kifizikia , ilikuwa ni kama ‘Centripetal Force’(Nguvu kati) , hii ni kwa mfano pale mtu anapounganisha kitu kwenye Kamba na kuanza kukizunganisha juu kwa kasi na kutengeneza duara , sasa ndio alichokifanya Omari , kwamba alitumia mbinu za kichawi kumzunguka Roma kwa mara nne na kisha akajitoa kabisa kwenye zile nafasi na akaenda kukaa upande wa juu na akatengeneza umbo feki ambalo linamwakilisha yeye mwenyewe , sasa kuna namna ya kufanya mtu kutokuona mzunguko , hicho ndio kilichotokea , hivyo kitendo cha Roma kutoka nje ya duara aliweza kufumbua fumbo la levo ya Mzunguko kamili mwanzoni Roma alielewa levo ya Mzunguko kamili ilikuwa ipo ndani ya duara , lakini baada ya kutoka nje ya mtego wa Omari aligundua levo ya mzunguko ni lazima uwe nje ya mzunguko kutengeneza balansi.

Omari mwenyewe alishangazwa na uwezo wa Roma kuelewa mambo kwa haraka sana, kilichomfanya mara ya kwanza kujiamini ni pale alipoweza kuona Roma alikuwa katika levo ya chini kuliko yeye , lakini mtego aliomuwekea umemfanya kutoka levo moja Kwenda nyingine , sasa jambo hilo lilikuwa la kushangaza kwani yeye mwenyewe alichukua miaka Zaidi ya miwili kutoka levo ya nusu mzunguko Kwenda mzunguko kamili , lakini Roma yeye imemchukua muda mfupi sana.

“Nipo tayari kuona uwezo wako wote”Aliongea Roma.

“Usijindanganye kama unaweza kujifunza kitu kutoka kwangu , ijapokuwa umeweza kufanikisha kupanda levo moja Kwenda nyingine, lakini levo ya nafsi huwezi kuielewa kirahisi na kuifikia”Aliongea na kumfanya Roma kufikiria kidogo huku akikumbuka baadhi ya meneno ambayo alikuwa akielekezwa na mastar wake wakati wa mafunzo.

“Master ni zipi kanuni kubwa ya nguvu hizi?”Aliuliza kijana mdogo huku akimwangalia mchina aliekuwa mbele yake .

“Mbinu ninayokufundisha ina kanuni nne ambazo unapaswa kuzizingatia siku zote nazo ni namna nguvu zinavyopingana , zinavyotegemeana, zinavyovutana na zinavyopitia mabadiliko , unatakiwa kuelewa msingi wa hii dunia kila kitu kina uhusiano na kitu kingine na ndio maana halisi ya uwiano”

“Master je naweza kujua namna ya uhusiano kati ya kitu na kitu?”Aliuliza na kumfanya Master kumwangalia.

“Kifo na uhai ni mfano wa uhusiano ninaozungumzia”Aliongea na kumfanya kijana mdogo kuelewa.

Sasa Roma hayo ni moja ya mafunzo ya Master Chhi aliokuwa akimuelekeza ndani ya jangwa la Gobi na aliamini kwa fumbo lolote ambalo Omari anaweza kumtengenezea atatumia misingi ya dunia kuweza kufumbua.

Roma wakati akiwaza , alijikuta akishangaa mara baada ya kumuona Omari akifanya kitendo ambacho hakuwa amekitegemea , Omari alishika jicho lake la kushoto na sio kushika kwa kuziba bali alishika kwa namna ya kulitoa.

“Unataka kufanya nini?”Aliuliza Roma kwa wasiwasi.

“Hahaha.. Hades kama utabahatika kushinda basi nitakueleza namna ambavyo niliishi Maisha yangu kwa kutumia jicho moja tu baada ya kupata ajali”Aliongea Omari.

“Unamaanisha jicho lako la kushoto sio la kibinadamu?”

“Hilo ni jibu Hades , uliniuliza kwanini nimeweza kufikia levo za juu haraka ikiwa mimi ni binadamu , jibu langu kwako ndio hili , kitendo cha kuwekewa jicho la kondoo kwenye jicho langu la kulia ilihali siwezi kutumia kuona ilikuwa motisha kubwa san ilionipelekea kujifunza mbinu za kimatibabu za kichina” Aliongea na palepale alilinyofoa jicho lote nje na kulitupia baharini a kumfanya kubakia na jicho moja tu , huku sehemu ambayo ambayo ametoa jicho lile kukibakia shimo.

Kitu kingine Zaidi kilichomshangaza Roma ni kwamba baada ya Omari kutoa jicho lake ni kama mwili wake ulijaa nguvu isiokuwa ya kawaida ambayo ilikuwa ikimzunguka.

Haya ni majaabu”Aliwaza Roma kwenye kichwa chake huku akimwangalia Omari ambaye anasambaza hewa iliojaa presha ya hali ya juu na kufanya mawimbi ya maji kuanza kuwa makubwa.

“Arrgh !!.. Arghhh , aargh”Roma alikuwa akilalamika kwa mapigo aliokuwa akipigwa na Omari , kilichokuwa kikimfanya Roma kihisi maumivu makali ni kitendo cha kuhisi mwili wake ni kama unachomwa na vijipini mithili ya sindano pande zote za mwili.

Jambo moja ambalo lilimsiadia ni kwasababu alikuwa akipona haraka na alijiambia kama angekuwa hana mafunzo ya nguvu za kijini za kimaandiko basi asingeweza kumudu mashambulizi ya Omari.

Omari mwenyewe alijikuta akishangaa kwa uwezo wa Roma kuhimili mvua ya sindano aliomtengenezea.

“Usishangae naweza kutokuwa levo za juu katika mbinu za kijini lakini mimi ni moja kati ya wachache walioweza kufanikisha kutumia nguvu ya kimaandiko ya urejesho isio na kikomo”

“Nimesikia sana kuhusu hio mbinu na ni ngumu sana kueleweka hata ndani ya jamii ya majini yenyewe lakini hata hivyo hainifanyi kushindwa hili pambano”Aliongea na palepale alitumia maji ya bahari kutengeneza upanga wa barafu, lilikuwa jambo la kimaajabu kweli na kumfanya Roma kutabasamu kifedhuli., Roma alikwepa sana kila pigo la Omari , lakini jambo moja ambalo lilimshinda kufanya ni kutengeneza maajabu ambayo yataweza kumshinda Omari kutokana na kwamba hakutaka kuvunja kanuni za pambano hilo , kwani ilikuwa ni sheria yeye kutumia mbinu za kijini tu kupambana.

Mpaka masaa mawili yanamalizika Omari alionekana kutengeneza kila aina ya maaajabu kutokana na levo yake , lakini kila linapomfikia Roma aliishia kulipangua au kuliacha limpige na kuruhusu nguvu ya kimaandiko kumponya kwa haraka.

“Hades nimeishiwa mbinu zangu zote za kijini na siwezi kushinda lakini pia siwezi kusema pambano hili ni droo kutokana na uwezo wako kuwa chini kuliko wa kwangu , hivyo kwa maksi nitasema umeshinda”Aliongea Omari na kumfanya Roma kutabasamu .

Ni kweli kabisa ijapokuwa Roma hakuweza kumpiga Omari kwa shambulizi lolote lakini kutokana na levo yake na alivyoweza kupangua kila pigo lililorushwa kwake inamfanya kuwa mshindi.

Roma mwenyewe hakuona kuna haja ya kuendelea kupambana , kwani kama wataendelea inaweza kuchukua muda mrefu na inaweza kumfanya kutumia uwezo wake nje ya wa kijini ili kumshinda Omari kuokoa muda , jambo ambalo hakutaka kufanya kwani angekuwa nje ya kanuni walizopanga kabla ya pambano, lakini jambo kubwa sana kwake usiku huo alipata kujifunza vitu vipya kupitia Omari.

*****

Adeline na Fanny haikueleweka walikuwa wamemuwekea nini Kizwe kwani licha ya kwamba alikuwa macho lakini mwili wake ni kama haufanyi kazi , ni kama vile mgonjwa ambaye amepalalaizi kipande cha chini, hivyo hata baada ya kukabidhiwa kwa wanaume waliokuwa mbele yake alishindwa kabisa kujitetea au kutumia mbinu yoyote kuwaepuka.

Hivyo kila kitu kilichokuwa kikiendelea kwenye mwili wake alikuwa akikiona wazi kabisa na alishindwa kuongea lolote kwani hata hivyo wanaume hao mafukara hawakuwa wakielewa lugha ya kingereza.

Upande wa wale wazungu mara baada ya kumkabidhi Kizwe kwa vijana kwa ajili ya kazi kuanza walipandisha juu kabisa darajani na kuanza kurekodi tukio zima linavyoendelea , hawakutaka kufanya moja kwa moja kwani waliamini wale mafukara wasingefanya kazi kwa ufanisi.

“Oya wadau kwenye Maisha yangu sijawahi kukutana na mwanamke mwenye Ngozi laini kama huyu , hii ni bahati ya mtende”Aliongea Tulo huku akijikakamua kushusha mzigo.

“Maliza fasta wewe fala acha sifa zako za kimama”Aliongea yule jamaa aliekuwa akiamshwa dakika kadhaa zilizopita , yeye zamu yake ilikuwa ni mtu wa tatu , yaani baada ya Tulo kumaliza.

Yaani kilchofanyika kilikuwa kitendo cha kikatili mno , kwani vijana wote walimbaka Kizwe kwa zamu mpaka kurizika na hawakujali sana baada ya hapo kitatokea nini , licha ya kwamba walikuwa mafukara ilikuwa ni rahisi kwao kuelewa mwanamke huyo alikuwa na matunzo ya hali ya juu kutokana Ngozi na yake jambo ambalo liliwafanya wafurahie mchezo.

Kizwe yote hayo wakati yanafanyika alishuhudia na kwakua hakuwa na uwezo wa kufanya chochote kutokana na mwili wake kuwa katika hali ya kupooza aliishia kutoa machozi tu , huku akimlaani Roma kwa kila laana anayoijua, aliamini yeye ndio kamleta hapo kwani mara ya mwisho alipozimia alikuwa kwenye jumba kule Bagamoyo na mtu pekee ambaye alikuwa na uwezo wa kumfanyia hivyo ni Roma.

Kzwe hakujua kama aliletwa hapo na wazungu , kwani baada ya kukabidhiwa kwa wabakaji hao waliondoka na hapo ndipo kizwe aliporejewa na fahamu licha ya mwili wake kukosa nguvu.

Wakati vijana wanamaliza shughuli kila mmoja kwa mizunguko mitatu mitatu wote walijikuta wakijichokea na kukinai na kuyasogelea maboksi yao na kumuacha Kizwe vilevile.

“Oya wadau , wale wazungu si walisema watatulipa?”Aliongea Tulo.

“Unatepeta sana mwamba kiakili , hakuna tena maswala ya mikwanja malipo tushayapata”Aliongea mwingine na kumfanya Tulo kuona kweli aliongea ujinga.

“Wazee Lekcha huyu hapa”Aliongea mwingine baada ya kumuona mwanaume aliebeba mfuko mkubwa akiingia hayo maeneo , mwanaume huyo walikuwa wakimuita kwa jina la Lekcha yaani Lecture au mkufunzi kwa kiswahiili , kilichowafanya kumuita mwanaume huyo ni kutokana na kwamba alikuwa akisifika mitaa yote hio ya uswahilini kwa uwezo wake mkubwa wa kuongea lugha ya kingereza , huku akijitapa siku zote kwamba amesoma sana kuliko Mtanzania yoyote na mama yake ni Malkia Elizabethi wa Uingereza na aliongea hayo yote wakati akiwa amelewa chakali sasa katika mazungumzo yake alikuwa akimalizia kwa kujiita yeye ni Lecture sasa waswahili wao wakambatiza namna yao ya kumita na kumpa jina la Lekcha

Lakini ilikuwa ngumu kwa wanajamii wote kumuelewa mwanaume huyo , ni kweli kwamba alikuwa akijua lugha ya kingereza , lakini kilichowashangaza wengi ni kwamba hakuwa na makazi na alikuwa ni fukara kama wengine na kazi yake kubwa ilikuwa ni kuokota chupa za maji au soda na Kwenda kuziuza.

Sasa siku zote bwana huyu hakuwahi kuitwa kwa jina lake halisi na watu wengi wanamfahamu kwa jina la Lekcha , yaani Lecture au Mkufunzi yote hio ni kutokana na kwamba alikuwa akiongea lugha ya kingereza sana , hususani wakati akiwa amelewa, huyu mwanaume watu wengi washawahi kumfatilia kutaka kujua ni wapi ametokea , lakini hakuna aliefanikiwa kujua ni wapi alitokea mpaka kuwa ndani ya maeneo hayo ya uswahilini ya jiji na kuwa kafara, hivyo watu waliamini huenda hakuwa na akili nzuri hivyo hata alipozaliwa amesahau , alikuwa mkubwa wa miaka kama arobaini hivi.

“Kuna nini kinaendelea hapa?”Aliuliza Lekcha mara baada ya kumuona mwanamke akiwa uchi pembeni ya hao vijana.

“Lekcha bwana mitikasi mingi ya nini , wakati kila kitu unaona , ni zamu yako na wewe kuukwea”Aliongea Tulo na kumfanya Lekcha kumsogelea yule mwanamke na mara baada tu ya kumuona vizuri kwa mwanga uliozalishwa na baadhi ya taa za nyumba za karibu alijikuta akisisimka mwili.

“Hahaha… Lekcha kumbe na wewe umo?” Walijikuta wale vijana wte wakicheka lakini Lekcha hakutaka kuwajali Zaidi ya kushusha suruali yake haraka haraka.

Upande mwingine barabarani mita kadhaa kutoka kwenye daraja hilo Adeline na Fanny walionekana kumaliza kazi yao ya kurekodi kila kitu.

“Fanny ijapokuwa Mfalme Pluto ana mbinu za kikatili likija swala la mateso , ila hii imezidi”Aliongea huku akikagua video iliokuwa ikionekana kwenye Camera.

“Nini tunakwenda kufanya baada ya hapa Adeline?”

“Mfalme Pluto amesema anataka kazi ya kisanaa Zaidi huu ni mwanzo tu , tunatakiwa kuendelea kufatilia”Aliongea na kumfanya Fanny kushangaa.

“Kinachofuata nini Adeline si kila kitu kishaisha tunazo hizi Vidio zinazo onyesha sura ya Kizwe kuna haja gani ya kuendelea Zaidi”

“Mfalme Pluto hajatuambia tuishie kwenye kurekodi tu , bali tuendelee kurekodi hatua zote atakazopitia ili kuifanya kazi kuwa ya kisanaa , kuhusu hizi tulizoweza kurekodi , nitamtumia asubuhi”Aliongea na Fanny alishindwa kupinga na kuondoa gari yao huku wakipanga kuendelea siku inayofuata.
Ohoooooo
 
Back
Top Bottom