Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

SEHEMU YA 464.

Roma mara baada ya kumwambia Diego kwamba atashughulikia kumuokoa mke wake , alisimamisha gari na kisha akaunganisha simu yake na GPS kwa kutumia Code maalumu , alifungua Aplication maalumu kwenye simu na kisha akaingiza herufi mfano wa Serial number na palepale simu ilianza kutafuta kwa kasi na ndani ya dakika kidoti cha rangi nyekundu kilionekana juu ya Ramani nje kidogo na jiji la Dar es salaam.

Namba alizoingiza kwenye simu zilikuwa za kifaa maalumu ambacho aliwapatia wanawake wake kubonyeza pale watakapokutana na Clone ya Yan Buwen , ni kama Panick Button lakini ambacho kinatoa mawimbi ambayo yanaweza kunaswa na mfumo wa GPS.

Roma baada ya kuona kifaa hicho kinafanya kazi alifikiahitimisho moja kwa moja mtekaji aliacha kiwe kinafanya kazi kwa ajili ya yeye kumtafuta.

Ali’zoom’ ramani kusoma jina la eneo ambalo kidoti chekundu kunaonyesha na jina lilisomeka Lugoba , ni sehemu ambayo haikuwa akiifahamu lakini alijua ipo ndani ya mkoa wa pwani na ni kilomita kadhaa kutoka Dar.

Hakutaka kujishauri mara mbili alishuka kwenye gati akaangalia kulia na kushoto na aliona hakuna mtu anaemwangalia na palepale alipotea .

Roma alikwenda kutokezea kwenye kichaka mita kadhaa kutoka barabara inayoelekea Tanga kutuokea Chalinze , sehemu alitokezea kulikuwa na sheli ambayo ilionyesha kutelekezwa lakini upande wa kulia kwake kulikuwa na boma la kanisa ambalo lilionyesha halitumiki.

Alitumia uwezo wake wa kijini kukagua enelo lote na kisha alitembea kufuata uelekeo wa kanisa.

Edna hakuwa amefungwa lakini alikuwa amejikunyata kwenye kona upande wa kushoto huku akionyesha kutetemeka kwa woga na hata sura ilimpauka, alitia huruma kwa mwonekano wake.

Upande wa kulia kwake eneo liliojengwa kama kimbweta alionekana mwanaume mweusi tii aliekuwa amenyoa kipara na kuvaa mavazi ambayo yalikuwa ni kama ya wale watu wanaosalia Budha , alikuwa na shanga nyingi amezivaa kwenye shingo na mwili wake ulionyesha kuwa ni wenye kushiba mazoezi.

Mkononi alionyesha kushikilia kitu kama Medali lakini ambacho kimefungwa na mkufu au Chain na kuandikwa kwa ligha isiokuwa ya kawaida.

Edna alikamatwa muda ambao alikuwa akitoka nyumbani akianza safari ya kuelekea kazini , alisimamishwa njiani kabla hajaingia ndani ya barabaa ya Bagamoyo na aliposimamisha gari alijikuta akipoteza fahamu bila hata ya kujielewa na alipokuja kushituka alikuwa ndani ya jumba hilo bovu ambalo aligundua lilikuwa ni kanisa.

Edna alijaribu kukimbia lakini miguu yake ni kama ilikuwa imefungwa kwani alishindwa kupiga hatua, ni kama alikuwa ameshikiliwa na kamba kutoka nyuma yake.

“Inaonyesha mpenzi wako hakujali kabisa , kwanini mpaka muda huu hajajitokeza tu bado”Aliongea yule mwanaume kwa lugha ya kingereza huku akionyesha sura ya kukosa uvumilivu, alikuwa na rafudhi ambayo Edna alishindwa kujua mtu huyo ni wa nchi gani au kabila lipi, alijua sio mtanzania kutokana na kushindwa kuzungumza kiswahili.

Edna alishindwa kujibu zaidi ya kuendelea kujikunyata kwenye kona huku akitamani Roma atokezee , hata hivyo kwa muonekano wa huyu mtu alionyesha kabisa alikuwa na uadui na Roma, maana hakuonekana mtu wa kawaida kabisa kwake.

Baada ya mwanaume yule kuona Edna haongei chochote alimsogelea na kuanza kumchunguza kwa kumwangalia vizuri na alijikuta akitabasamu kifedhuli na kilichonekana zaidi ni meno , alikuwa mweusi kuliko isivyokuwa kawaida ni kama amepakwa masinzi.

“Unaonekana kuwa mrembo sana , kwenye maisha yangu sijakutana na mwanamke Kiafrika mwenye muonekano kama wako , kama nisingekuwa na kitu kingine ninachohitaji nisingekuacha salama”Aliongea na kumfanya Edna kuzidi kutetemeka alijiambia akibakwa na huyu mwanaume atajiua kuliko kuishi na kumbukumbu ambayo hatoweza kuvumilia maisha yake yote, alishasahau kabisa hata Roma alimfanya bila ya ridhaa yake.

“Ineonyesha umechoka kuishi”Sauti nyuma yake ilisikika na kumfanya Edna kunyanyua macho haraka na kuangalia mbele na alijikuta akijawa na ahueni mara baada ya kumuona Roma.

Yule mwanaume mara baada ya kumwangalia Roma alianza kuongea mwenyewe kwa lugha ambayo haikueleweka ilikuwa ni ya kabila gani , lakini palepale kile kichuma mfano wa medali alichoshikilia kilianza kutoa mwanga mkali , ni kama vile kioo kinapolengeshwa na jua na kuakisi mwanga wake..

Muda ule ule yalionekana maputo kama ya kupuliza lakini haya yalikuwa ya kichawi yakijitengeneza hewani na kuanza kumsogelea Roma na palepale aliinua mkono na yale maputo ni kama yalipulizwa na upepo kwani yalimsogelea Roma kwa kasi , lakini kabla hata hayajamfikia Roma aliyabadilisha mwelekeo.

“BOOM!”

Yalipasuka yote lakini nguvu yake ilikuwa kama ya bomu kwani yalibomoa kipande cha dirisha kuruka nje.

Roma aliguna baada ya kuona maajabu hayo , alimkagua yule mwanaume na kugundua hakuwa binadamu wa kawaida, alikuwa ni jini kabisa ambalo limejitengenezea mwili, lilikuwa kwenye levo ya Nafsi kwa Roma alivyopima uwezo wake.

Roma mara baada ya kitedo kile cha maputo kupasuka alisogea kwa kasi kumsogelea yule Jini, lakini alipokaribia yule Jini mweusi aliinua mkono na kunyoosha kile kimedali na Roma alikumbana na nguvu ambayo ilikuwa kama upepo ambayo ilimrudisha nyuma kwa nguvu.

Roma alijikuta akishangaa mno kwa tukio lile , hakuamini anaweza kudhibitiwa na kifaa ambacho kilionekana kama kijichuma tu kwake.

Alijikuta akikumbuka baadhi ya maneno ya Zenzhei kuhusu uwepo wa Dhana katika miliki za kijini, aliamini huenda alichoshika yule mwanaume ndio moja wapo ya dhana hizo.

“Chukua hio”

Aliongea yule mwanaume na palepale macho ya Roma yaliweza kuona Rungu la kichawi ambalo lipo kama chuma likija kwa kasi huku likitoa msisimko wa kuwa na nguvu isiokuwa ya kawaida.

Roma hakutaka kuzembea aliita nguvu za kijini na kisha kutengeneza ngao na kuzuia lile Nyundo na alifanikiwa kwani baada ya nyundo ile kugongana na nguvu yake ya kijini lilirudishwa nyuma kwa spidi kurudi kwa alielituma lakini kabla halijamfikia yule jini mweusi palepale lilirudi tena kwa kasi kwenda kwa Roma kwa mara nyingine

“Hehe… ngoja uonje nini maana ya nguvu halisi Kivimbo , unafikiri nimekuja bila ya kujipanga”Aliongea huku akichekelea

Roma alikasirishwa na kauli yake , alimdharau adui yake kwa kuwa katika levo ya nafsi lakini aligundua kile alichoshikilia mkononi ndio siraha yake kubwa ambayo ni kama imeongeza uwezo wake kwa zaidi ya mara mbili.

Roma alijiambia kama kweli ujinini kuna vitu vyenye nguvu kubwa kama hivyo , basi kama atakutana na jini ambalo lipo kwenye levo sawa na yake na kumiliki dhana za namna hio huenda anaweza asifanikiwe kushinda.

Edna alikosa ujasiri wa kuangalia yale mapigano na alipofungua macho na kuona Roma hajapatwa na madhara yoyote alijikuta akiwa mwenye ahueni.

“Edna usiogope tena nipo hapa kwa ajili yako”Aliongea Roma mara baada ya kuweza kupita upande wa Edna .

“Jamani inaonyesha mnapendana sana hadi nawaonea wivu mimi”Aliongea yule mwanaume na Lipsi zake hazikuweza hata kuonekana zaidi ya meno , Roma alijiambia kama utakutana na mtu mweusi namna hii muda wa usiku basi kama huna ujasiri unaweza kukimbia nduki.

“Wewe ni nani?”Roma aliuliza.

“Jina langu halina umuhimu kwako , ambacho ni muhimu ni kile ninachotaka kutoka kwako”Aliongea .

“Unataka nini kutoka kwangu?”

“Andiko la Urejesho”Aliongea na kumfanya Roma kushangaa na palepale maswali yalibuuka na kujiuliza je huyu ndio yule aliekutana nae nchini China wakati alipoenda na Magdalena.

“Na kwanini nikupatie?”

“Tusema ni kama biashara, nitamuacha mkeo kuwa hai na mimi utanipatia ninachotaka”

“Unadhani unaweza ukanishinda, sijatumia hata robo ya uwezo wangu wote nitakupatia kifo ambacho hakitakuwa na maumivu kama utaniambia ninachotaka kujua kutoka kwako”

“Kama unapanga kuniua basi mkeo atatangulia kwanza”Aliongea.

“Unamaanisha nini?”Aliongea Roma na kumfanya Edna aliesimama kumsogelea Roma.

“Ushawahi kusikia laana ya kutupiwa ya kichawi inayohusiana na minyoo?”Aliuliza na kumfanya Roma kuanza kufikitia.

“Unamaanisha umemtpia mke wangu Laana?”Aliongea na kumfanya Edna kuchanganyikiwa baada ya kusikia kauli hio.

“Nimetumia mbinu yangu maalumu niliokuwa nayo kwa muda mrefu, ni laana ya minyoo ambayo akitupiwa binadamu na kuingia kwenye mwili wake inaweza kumuua kwa kutoboa moyo”Aliongea

Edna baada ya kusikia ndani ya mwili wake kuna minyoo alijikuta akihisi kichefu chefu muda ule ule.

“Tokea nimesafiri mpaka kufika hapa nilikuwa najua ungeniua kirahisi ndio maana nikawa mbele ya muda , nasikia unasifika kwa ukatili wa kutosamehe maadui zako hivyo ukinua na mkeo anatangulia”

Roma alimuwekea Edna mkono kwenye eneo la kifua kujaribu kumpima kama kuna nguvu ya ziada ndani ya mwili wake na kweli aliweza kuhisi vitu visivyokuwa vya kawaida vikitambaa ndani ya kifua, Roma alijikuta akijawa na wasiwasi mpaka Edna akaogopa kwani hajawahi kumuona Roma akiwa na wasiwasi wa namna hio.

“Niko sawa Roma , sio kama anavyoongea”

“Binti nadhani huelewi hata ninachoongea , unajihisi uko sawa kiafya, ni kwasababu sijawapa maelekezo watoto wangu kukutoboa ndani kwa ndani”

“Sijisikii chochote ndani ya mwili wangu, ninaweza vipi kukuamini kama unaongea ukweli?”Aliongea Edna huku awamu hii akiwa na hali ya kujiamini , ile hali dhoelefu ya kiburi cha kuzaliwa ilianza kujionyesha.

“Nadhani huelewi , nimesema ni laanna na sio sumu”Aliongea na kisha akatabasamu kifedhuli.

“Arrgh!!”

Edna alijikuta akitoa kilio cha maumivu huku akishikiria shingo yake , alijihisi ni kama vile anameza watoto wa nyoka kwenda tumboni , maumivu yake hayakuwa yakielezeka na alijikuta akitapika palepale na kilichoonekana sio chakula kutoka tumboni bali alitema damu.

“Ednaa!!”

Roma alijikuta akishistushwa na kitendo kile na kumshikilia haraka na kisha kumwingizia nguvu za kijini kutuliza maumivu.

“Umemfanyia nini?”Aliuliza Roma huku jicho lilikuwa jekundu mno.

“Punguza presha nimeruhusu minyoo itoboe kidogo ili kukuaminisha kwamba siongei utani”Aliongea

Roma alikuwa na hasira kiasi ambacho alitamani kumuua palepale , lakini alishindwa kufanya hivyo kwani usalama wa Edna ulikuwa ni kipaumbele.

“Roma .. naogopa .. sitaki kufa na kumuacha Lanlan”Aliongea Edna huku akianza kulia.

“Edna huwezi kufa , utaondoka hapa ukiwa salama”Aliongea Roma kwa kumfariji na palepale alijikuta akipata tumaini baada ya kufikiria kitu , alijiambia vipi kama atatumia uwezo wake wote kumwingizia Edna nguvu ya kimaandiko ndani ya mwili wake na kuua laana hio ya kutupiwa ya minyoo.

“Nakushauri usije ukatumia nguvu za kijini ukidhamiria kuwaua ,watapasuka ndani kwa ndani na mkeo atakufa kifo cha maumivu makali mno”Aliongea jini mwuesi.

Roma ilibidi amwingizie kiasi kidogo cha nguvu ya kijini kwenye mwili wake ili kumponyesha maumivu na ilisaidia kwani maumivu yalipotea lakini hakuacha kutoa kilio ,Edna kwenye maisha yake hakuwahi kuhisi maumivu ya aina hio , aliogopa kile kilichopo ndani ya mwili wake kwani alihisi kabisa vitu kama nyoka vikitembea tembea ndani ya mwili wake, Roma ilibidi amkumbatie huku akimuonea huruma.

“Kama nitakupatia unachotaka , je unanihakikishia utamwondolea hio Laana?”Aliuliza

“Hakika , Hao ni watoto wangu na nimewakuza kwa zaidi ya miaka kumi nitapata hasara kama nitawatumia kwa binadamu wa kawaida kama mkeo , lakini..”

“Lakini nini?”

“Sikuamini kabisa , ninachotaka uniruhusu kwanza nikufungie uwezo wako wa kijini kwanza ili kuhakikisha kwamba huwezi kunishambulia , nitakapona sio tishio kwangu na kupata ninachotaka basi nitamwoneolea mkeo laana yangu”Aliongea

“Kwahio unaniona mimi ni mjinga , kama nitakuruhusu ufungie uwezo wangu wa kijini utaniua kirahisi”

“Kwahio una chaguzi ipi nyingine , hapa tunazungumzia ni aidha ukubaliane na mimi nifungie uwezo wako wa kijini nichukue ninachotaka au mkeo afe ukiwa unamwangalia”.

Roma alijikuta akipandwa na hasira kwani hakujua huyu mwanaume anaenda kufanya nini kufungia uwezo wake wa kijini , aliogopa anaweza kuvuliwa nguvu zake zote za kijini na alijiambia hata kama anao uwezo wa kutumia kanuni za anga kama alivyofanya kwa Drogba na Mourihno kwa jini ambalo lipo kwenye Levo ya Nafsi asingeweza kufanikisha ndani ya muda.

“Roma usimsikilize anachotaka ni kukuua tu , anataka kunitumia mimi kama chambo kwasababu hana uwezo wa kukuzidi , Roma najua unao uwezo mkubwa hivyo unaweza kumua na kisha kuniokoa na mimi”Aliongea Edna kwa msisitizo huku akiwa amemshika mkono.

Roma alijikuta akimwangalia Edna kwa uchungu mwingi.

“Edna mke wangu nisamehe tu kwa leo nitakuangusha , lakini siwezi kukuangalia ukifa , nitampatia anachotaka”Aliongea Roma kwa huzuni huku akimfuta machozi kwa mkono wake wa kushotO





SEHEMU YA 465

Edna alikuwa kama haamini maneno ya Roma , hakuwa pia tayari kuona Roma anapoteza nguvu kwa ajili yake, ni kama aliogopa ataishi kwa kuwa na deni maisha yake yote.

“Kwahio unamaanisha utamuachia afanye kama anavyotaka?”

“Nina uhakika ninaweza kumuua kwa pigo moja tu , lakini siwezi kuhatarisha maisha yako , natamani nikusikilize lakini siwezi , sio kwa muda huu..”

“Wewe usifanye hivyo ..”

“Najua nimekuumiza mara kibao nadhani hiki ndio ninachostahili kama adhabu , kama sio mimi usingekuwa kwenye hali hii ya hatari hivyo siwezi kuruhusu ukipoteza maisha”Aliongea Roma na kumfanya Edna machozi kuanza kujitengeneza kwenye macho yake.

“Usifanye chochote cha hatari kama nitakufa naamini atakuacha hai, anachotaka ni nguvu zangu za kijini na nitampatia , ukishatoka hapa tumia simu yangu kupiga simu namba ya mwisho nilioipigia”Aliongea Roma na kisha alitoa simu yake na kumpatia Edna ambaye aliipokea kwa wasiwasi, baada ya kuipokea aliitupa chini.

“Sitaki simu yako , huwezi kuniambia unataka kufa halafu umeniumiza sana na kunikasirisha, ukifa kabla sijakusamehe nitakuchukia milele”

“Edna usifanye hivyo , nisikilize tafadhari ..”

“Mimi sitaki, unaruhusiwa kufa baada ya sisi kufunga ndoa , huwezi kuniahidi kitu halafu usitimize”Aliongea huku akianza kukasirika na kutoa machozi kwa wakati mmoja.

“Edna kaa pembeni na kaa kimya, nishafanya maamuzi tayari na ukinizuia nitakufosi ufanye ninavyotaka”Aliongea Roma kwa kumfokea na kumfanya Edna kumwangalia kwa wasiwasi akiwa haamini kama Roma kweli anataka kufanya kama alivyopanga.

“Hahaha.. nyie ndege wawili mpendanao , mshamaliza kuongea?”Aliuliza yule mwanaume .

“Fanya unachotaka”Aliongea Roma.

“Ndio ndio”Alijibu na palepale kisu mfano wa daga rangi ya silver kilionekana kwenye mikono yake , haikuwa Dagger ya kawaida bali ya kichawi ,ilikuwa ikitoa msisimko wa ajabu mno.

“Hii ni Dhana ya zama za kale inafahamika kwa jina la Dragoni Dagger , ni sehemu ya siraha nne za kijini ambazo zina uwezo wa kuzuia nguvu za kijini kwenye mwili wa mtu ambaye amefikia kwenye levo ya kuipita dhiki , ni kama sumu hivyo kama utajifanyisha mjanja kutaka kuutumia uwezo wako basi utakufa hapo hapo, najua Nguvu ya kimaandiko inaweza kuponyesha moyo wako hivyo..”Aliongea

“Kwahio unataka kunichoma kwenye moyo wangu?”Aliuliza Roma kwa mshangao.

“Ndio ninachomaanisha”

“Sasa nakupaje nguvu zangu za kimaandiko?”

“Ni rahisi sana”Aliongea na kisha akatoa kifaa flani kama kibuyu lakini kilichotengenezwa na malighafi ya Jade.

“Unachotakiwa kufanya ni kuruhusu nguvu zako zote za kijini kuingia kwenye hii dhana na mimi nitaweza kuthibitisha kama nguvu ya kimaandiko ni halisi ili usije ukanidanganya na baada ya hapo nitamwondolea mkeo laana”Aliongea

Roma alishangazwa na mwonekano wa kile kijifaa baada ya kukishika, ni moja wapo ya Dhana ambazo aliweza kusikia kutoka kwa Zenzhei na alijiambia hawezi kutegemea uwezo wake pasipo kuwa na moja ya wapo ya Dhana kama atahitaji kuwa na nguvu nyingi za kushinda hata majini kutoka Hongmeng.

Roma alishindwa pia kumjua mwanaume aliekuwa mbele yake ni miliki gani anatokea mpaka kumiliki Dhana za aina hio.

“Nitaingiza nguvu yote ya kimaandiko kwenye hii Dhana na nitakupatia kuithibitisha na utakapoweza kuona ni halisi basi nitatumia hio Daga kujichoma moyoni na utakaporidhika nimekuwa dhaifu utamuondolea mke wangu Laana”Aliongea Roma.

“Deal”Aliongea kwa shauku baada ya kuridhika na maelezo ya Roma .

Edna alijikuta ngozi yake ikiota vipele mara baada ya kusikia Roma angejichoma na Daga kwene eneo la moyo.

“Roma jamani acha kuwa mjinga, huoni anataka kukuua”Aliongea Edna kwa kufoka.

“Kimya! , ninafanya haya kwa ajili ya maisha yako hivyo usiingilie”Aliongea Roma na kumfanya Edna kujawa na hasira huku machozi yakitiririka kwenye macho yake.

Yule jini mweusi alionyesha kufurahishwa na maongezi hayo , mpaka hapo alijiambia anayakaribia mafanikio.

“Fanya haraka unipatie nguvu za kimaandiko , Minyoo yangu ninaweza kushindwa kuiongoza ikihisi njaa”Aliongea na kumfanya Roma kupandwa na hasira lakini hata hivyo hakuwa na namna kwa wakari huo zaidi ya kutiii shuruti kwani kwake Edna alikuwa muhimu.

Alifumba macho huku akiwa ameshikilia ile Dhana ya kibuyu na kulengesha mkono karibu na mdomo wa ile Dhana na palepale kulionekana mfano wa mvuke ukiingia ndani.

Baada ya dakika kumi za Roma kuwa makini kuhamisha nguvu zake za kimaandiko alifumbua macho na kisha alimrushia yule mtekaji kile kibuyu baada ya kuona amemaliza.

Baada mtekaji kuridhika ilikuwa nguvu halisi ya kimaandiko alimrushia Roma ile Daga.

“Hakikisha unafanya kama tulivyokubaliana”Aliongea Roma.

“Fanya hivyo haraka sina muda wa kupoteza”Aliongea na Roma alifumba macho na kisha alijidunga na ile Daga eleo la kifuani akilenga moyo na palepale damu ziliruka mara tatu .

Roma alishindwa kuvumilia maumivu na palepale alidondoka chini kwa kupiga magoti huku uso wake ukionyesha kupauka kwa haraka sana.

“Romaa...!!” Edna aliita akimkimbilia pale chini kwa wasiwasi.

Roma alikuwa akijihisi maumivu, ijapokuwa nguvu ya kimaandiko haikuwa imetoka yote hivyo kujaribu kumponyesha, lakini alihisi maumivu makali kwani spidi yake ilikuwa ya chini mno kupona.

Dakika kadhaa mbele mwili wake ulianza kupoteza nishati ya mbingu na Ardhi na kuendelea kuwa dhaifu.

Sasa hapa utofautishe vitu viwili, kuna nguvu ya kijini ya kimaandiko ambayo inamsaidia kupona lakini pia kuna nguvu ya kijini ya kinishati ya mbingu na Ardhi , ni kama ilivyo kwa Omari au kwa jini ambalo lipo mbele yake , ijapokuwa lilikuwa na nguvu ya Nishati ya mbingu na Ardhi lakini halikuwa linamiliki nguvu ya kimaandiko kutokana na kutumia njia fupi ya kujifunza mbinu za kijini.

Hivyo Daga ilikuwa ikimzuia Roma kutumia nguvu zake za nishati za mbingu na Ardhi ili bwana aliekuwa mbele yake aweze kumponyesha Edna kwa kumuondolea laana na baada ya hapo aweze pia kutoroka kwani Roma hatokuwa na uwezo wa kumdhibiti kwasababu angekuwa ni dhaifu sana kufanya hivyo.

Yule mtekaji mara baada ya kupokea kile kibuyu, alitoa kijisahani kama cha Plastiki lakini ambacho kilionyesha kutengenezwa pia na madini ya Jade na kisha aliruhusu zile nguvu ambazo zipo kwenye ile Dhana ya kibuyu kutoka na kuvamia kile kisahani na palepale maandishi yalianza kujitengeneza kwenye kile kisahani , yalikuwa ndio maandiko ambayo yanaitwa nguvu ya urejesho.

“Nitasoma kwanza haya maandishi na baada ya hapo ndio nitamuondolea mkeo laana”Aliongea akimwangalia Roma ambaye amepiga magoti huku akiugulia maumivu.

“Hakikisha unatimiza ahadi yako”

“Haupo kwenye nafasi ya kuniambia kipi nifanye , wewe ni binadamu wa kawaida ambaye hukupaswa kumiliki kitu muhimu kama hichi , tamaa zako za kutaka kumiliki visivyo vyako ndio zinakuua sasa”

Edna alipatwa na wasiwasi na kisha akashika ile daga

“Unataka kufanya nini?”Aliuliza Roma

“Utakufa Roma kama damu zitaendelea kukutoka, ninaitoa hii daga , anakudanganya tu hawezi kuniondolea laana”

“Edna nisikilize mimi usifanye hivyo”Aliongea Roma kivivu na kumfanya Edna kuanza kulia akiamini Roma anakwenda kufa.

Yule mwanaume mara baada ya kusoma maandishi na kuridhika alioneysha tabasamu.

“Nadhani tumefikia mwisho wa kubagain”

“Okey fanya haraka na mwondolee mke wangu hio laana”

“Sio mbaya nitafanya hivyo , uwezo wako naona umeshuka mpaka kufikia nusu mzunguko , ngoja tumalizane sasa”Aliongea.

Palepale alianza kuongea maneno yasioeleweka kwa spidi kubwa kwa zaidi ya dakika mbili na Edna alijihisi kutapika kwani kuna vitu ambavyo vilikuwa vikitoka tumboni kwa fujo namna ambayo hata yeye alishindwa kuelewa lakini ajabu hakuweza kuona chochote zaidi ya kuhisi mwepesi baada ya vitu kumtoka.

Roma alijikuta akivuta pumzi ya ahueni mara baada ya kuona Edna ashaondolewa ile laana ya minyoo.

Edna alijikaza na kisha akamshikilia Roma vizuri na kumsimamisha, Roma alikuwa dhaifu mno.

“Roma usije kufa kwenye mikono yangu sasa hivi tafadhari jikaze”Aliongea Edna kwa kubembeleza, hakuwa tena CEO wa kampuni kubwa bali muda huu alikuwa akifanana na mtoto ambaye anaomba hela kutoka kwa mzazi.

Alijikuta akianza kujutia kwa kosa lake la siku ya jana la kumfukuza kuondoka nyumbani, alijiambia huenda yote hayo yasingetokea

“Usijali mke wangu siwezi kufa, nitaweza kupona”Aliongea Roma akimfariji.

“Huwezi kujiponyesha , nimesema ninaweza kumuondolea mkeo minyoo lakini kuhusu wewe siwezi kukuacha hai”Aliongea yule mtekaji.

“Wewe muuaji?”Edna alijiktua akitetema kwa hasira mara baada ya kusikia ile kauli.

“Haha..Sijaahidi chochote mimi”Aliongea na kumfanya Roma kufumba macho yake na kisha alishikilia ile Daga na kuichomoa kwa nguvu na damu zilitoka kidogo tu na kuacha, lakini hata hivyo Roma alijaribu kuita nguvu za kijini lakini ilionyesha sumu ya ile Daga ilikuwa ikimzuia kufanya chochote.

“Huwezi kuepuka kifo siku ya leo”Aliongea huku akianza kuminya vidole vyake na palepale aliita nguvu za kijini na kunyoosha ile medali kuelekea aliposimama Roma na Edna, palepale lile Rungu la kichawi liliibuka tena hawani likimsogelea Roma kwa kasi.

BOOM!

Kabla lile Rungu halijamkaribia Roma mlipuko ulitokea kwenye mikono ya yule mtekaji na kilicholipuka hakikuwa kingine bali kile kibuyu Roma alichoingiza nguvu ya kimaandiko.

Ulikuwa ni mlipuko mkubwa ambao uliondoka na nusu ya mkono wa metakaji huku yeye mwenyewe akirushwa na kwenda kutua kwenye ukuta wa kanisa na kufanya uchafu uliokuwa juu kuanza kudondoka chini kwa mtikisiko.

Edna alijikuta akiziba mdomo wake kwa mshangao akiwa haamini kile ambacho alikuwa akiangalia.

Roma alitoa tabasamu la kifedhuli na kisha aliruhusu nguvu ya kijini na kisha akakusanya sumu ya Daga iliokuwa ndani ya mwili wake na kisha akaikausha yote mara moja na palepale mwili wake ulianza kujiponyesha kwa kasi mno.

Upande wa mtekaji alikuwa ametapakaa damu zake yeye mwenyewe akiwa chini akigulia maumivu , ashapoteza mkono lakini pia ilionyesha damu zilikuwa zikivilia ndani kwa ndani ya mwili baada ya kukohoa na kutema damu.

“Umenifanyia .. nini?”Alianza kuongea huku akijikaza na maumivu akiwa haamini kila kitu kimebadilika.

“Ni kama ulivyosema wewe , sijakuahidi chochote baada ya kuondoa laana kwenye mwili wa mke wangu, ushajua mimi ni mtu wa aina gani lakini ukatoka huko ulikotoka na kuja kunichokoza , unaonekana unakipenda kifo kuliko uhai na nitatimiza unachotaka”aliongea Roma huku akitembea kwa kumsogelea.

Edna macho yalimtoka hakuamini yule Roma dhaifu alikuwa sawa kama vile hakuna kilichomtokea.

“Hapana haiweizekani, uwezo wako ulikuwa upo kabisa kwenye nusu mzunguko” Aliongea kwa hamaki na Roma baada ya kumkaribia alikanyaga ule mkono uliokatika.

“Arrgh!”

Edna alijikuta akigeuka nyuma pasipo ya kupenda yeye mwenyewe, kilichokuwa mbele yake kilimuogopesha kuangalia,

“Haujui hata ni kwa namna gani nilivyoweza kugeuza maandishi kuwa nguvu lakini bado unahitaji nguvu zangu” Aliongea Roma huku akitabasamu kwa kejeli.

“Unamaanisha nini?”

“Nilichokupatia sio maandiko halisi bali nilikuwekea mtego kwa kutumia maandishi, upo levo ya chini mno kuelewa nilichokifanya ndio maana ukaamini kweli nilichokupatia ni kitu halisi , sio kweli bali nilikutengenezea bomu” Aliongea Roma na kumfanya yule mtekaji kuanza kukata tamaa , mpaka hapo alijua hana cha kufanya zaidi ya kusubiri kifo chake kwani keshazidiwa ujanja.

Alimdharau Roma kwa kuona kwamba walikuwa kwenye levo sawa na yeye ndio maana hakuchukua tahadhari na hilo ndio kosa lake , Roma akamdhibiti kwa kutumia mpango wake mwenyewe.

“Sasa ni muda wa kuniambie wewe ni nani , na nani kakutuma”Aliongea Roma.

“Niue tu”

Crack!

Roma aliongea kwa vitendo , alipindisha mguu wake kwa nguvu na kukatika palepale. Na kumfanya kupiga ukulele.

Roma aligeuka nyuma na aliona ni afadhali Edna hakuwa akiangalia kile alichokifanya maana alikuwa akidhamiria kufanya ukatili wa hali ya juu.

“Utaniambia au niendelee”

“Siwezi kukuambia chochote , hata hivyo ninakwenda kufa”

Roma alichukua ile daga iliotumika kumchoma kifuani na kisha alimchana mtekaji eneo la tumboni kama anafanya upasuaji na kufanya damu kutoka nyingi huku viungo vya ndani vikionekana ikiwemo Ini.

“Argg!”

“Uniambie usiniambie ni chaguo lako , ila nitahakikisha nakata kiungo kimoja kimoja kadri utakavyoshindwa kujibu swali langu , nakushauri ufanye maamuzi maana unaweza kuongea mwishoni na vivungo ukawa huna”Aliongea Roma na kumfanya Mtekaji kuanza kujawa na hofu mno.

Roma alipanga kukata maeneo ambayo yasingemfanya adui yake kupoteza maisha haraka kwani alikuwa akiijua vizuri anatomi ya mwili.

“Wewe ni pepo kichaa na huwezi kupona kwa sumu iliopo kwenye mwili wako”Mtekaji aliongea kwa hasira.

“Wrong answer “Aliongea Roma na kukata kwa mara nyingine, ile daga ilikuwa na makali mno kama wembe.

“”Nishafeli kwenye misheni yangu tayari, kama sitokufa kwa mikono yako nitakufa kwa mikono ya walionituma, hivyo kuna haja gani ya kukupatia majibu ili uridhike”Aliongea na palepale mwili wake ulianza kukakamaa na damu zilianza kumtoka mfululizo kwa kila tundu kama vile mgonjwa wa Ebola na ndani ya dakika chache tu mwili wake ulianza kuoza kwa spidi kubwa kiasi cha kusababisha harufu kali mno.

Roma alijikuta akishangazwa na jambo kama hilo , alijuwa mwanaume huyo alikuwa na uwezo wa kutawala minyoo ambayo inaweza kula moyo wake lakini hakuamini kama anaweza kujiua mwenyewe kwa kuozesha mwili wake aliona ni kama alishajiwekea mtego wa kujimaliza mambo yatakapoenda kombo.

Alijikuta akiwa na wasiwasi na kujjiuliza kaama mtu huyoa metumwa kwa ajili ya nguvu zake za kijini , je hao waliomtukma anaogopa wangeuuwa wana uwezo mkubwa kiasi gani.

Roma alijiktua akiwaza kwa muda mfupi huku moyo wake ukiwa mzito, alijiambia kwanzia muda huo ni kuwalazimisha wanawake wake kuanza mazoezi ya kujifunza mafunzo ya kijini kwa haraka , kwani kama maadui zake wangekuwa na nguvu kubwa asingeweza kuwalinda.

Aliangalia lile rungu la kijini likiwa bado lipo chini na ile medali pia ilikuwepo chini , aliinama na kuviokota vyote . Roma alishika ile Medali na kuanza kusoma maandishi yake, lakini lugha ilikuwa ngumu kuielewa hivyo aliachana nayo , alitumia kanuni za anga na kisha alificha kwenye Space storage

Baada ya kuhakikisha hajaacha kitu muhimu aligeuka na kumsogelea Edna ambaye bado alikuwa upande wa nyuma kabisa akiogopa kusogea mbele kwani hata harufu ilikuwa ikimfikia.

Alimwangalia Roma kwa wasiwasi, hata hivyo alishaanza kumzoea Roma kwani kwake kuua ni jambo la kawaida.

“Edna umepata mshituko mkubwa kwa yaliotokea siku ya leo , Vipi unajisikia vizuri sasa?”

“Maneno ambayo ulikuwa ukiongea, je kila kitu ulipanga..?”Aliuliza Edna.

“Unaweza kusema hivyo , nisingemwaminisha asingekuwacha hai ndio maana nilikuigizia hata wewe uamini natoa nguvu zangu kweli”Aliongea Roma.

“You bastard”Aliongea Edna kwa kufoka , hakuamini alikuwa amechezewa akili bila ya kujitambua na kulia vyote vile.









SEHEMU YA 466

Edna alijikuta akiinua mguu wake wa kulia na kisha kumpiga teke Roma kwa hasira.

“Umeufanya moyo wangu kuumia kwa kujua kabisa unakwenda kufa , kama ilikuwa mpango kwanini hukuniambia hata kwa ishara, ulikuwa ukifurahia mimi kulia mbele yako au ndio kinilipizia kisasi?”

“Sikuwa na chaguzi nilitakiwa kumfanya aniamini kwa namna yoyote ile , ilitakiwa aamini kweli ninakufa kwa kuona machozi yako, ningekutarifu angeshitukia mchezo”

“Vipi kama angekataa kuniondolea laana alioniwekea ya minyoo ungekubali kufa kwa ajili yangu?”Aliuliza Edna.

“Edna mke wangu nishakuambia kwamba kadri nitakavyokuwa naishi nitahakikisha na wewe unaishi vilevile”

“Kwahio ndio unachotaka, tuseme kwamba tungekufa wote hukoi kuzimu bado ningekuwa na deni kubwa kwako kwa kujua umekufa kwa ajili yangu. si ndio ilikuwa mpango wako?”

“Muone sasa , kuna haja gani ya kuanza kukumbuka yaliopita wakati muda huu tupo salama”Aliongea Roma.

“Kwako hili linaweza lisiwe la umuhimu ila kwangu ni muhimu sana , umetumia maisha yako kuokoa ya kwangu”

“Hukumbiki hata wewe ulinidanganya kwa kuniaminisha kampuni yako inafilisika?”

“IIe ni kwasababu..”Alikosa usemi

“Niliamini usingekasirika baada ya kuekuelezea baada ya matokeo”

“Upo sahihi baada ya siku ile kugundua ukweli sikuweza kuwa na kinyongo juu yako licha ya kwamba sikupenda njia yako , kwasababu nilikuwa nikielewa nia yako halisi , naamini hata wewe pia utaweza kunielewa kwa nilichokifanya”

“Vyovyote vile kikubwa uhai”Aliongea Edna

Roma alitaka kumkumbatia Edna kwa nyuma lakini alikumbuka bado walikuwa kwenye ugomvi na hawakuwa wamesameheana na alikuwa akijiuliza kama Edna ameshasamehe.

“Tunapaswa sasa kuriudi , Recho alikuwa na wasiwasi kweli , ni kheii ukampigia simu muda huu”Aliongea Roma na Edna alitingisha kichwa na kuokota simu ya Roma na kumpigia na baada ya hapo Roma alimvuta kwake na kumkumbatia kifuani.

“Nitafanya hivi kwa ustaarabu , fumba macho yako kwani unaweza kushindwa kuvumilia utakachoona”Aliongea Roma.

“Unamaanisha tunapaa kurudi mjini?”Aliongea Edna pasipo kuamini kama angepaa kwa mara yake ya kwanza.

“Unafikiri ni kwa usafiri upi tutaondoka nao hapa kurudi hii ndio njia pekee rahisi”

Edna alijikuta akifumba macho yake na ndani ya muda mfupi tu Roma aliweza kutua nje ya eneo la bustani kwenye nyumba yao.

“Unaweza kuangalia sasa tumefika”Aliongea Roma

Edna baada ya kufumbua macho yake alijikuta akishangaa mno , hakuamini kama ni kweli wapo nyumbani, ulikuwa ni uzoefu wa mara ya kwanza kuupata katika maisha yake.

Roma alinwangalia Edna ambaye alionyesha hali ya kushangaa kwa muda na Edna alivyogeuka kumwangalia Roma aliona alikuwa akimwangalia.

“Mbona kama unataka kuongea”

Roma alikuwa amefukuzwa nyumbani hivyo hakujua kama anapaswa kuingia ndani au aondoke na ndio maana alikuwa akisubiria maamuzi ya Edna.

“Ah… nishakufikisha nyumbani salama , nadhani napaswa kuondoka sasa”Aliongea Roma kimtego.

Edna alishindwa kuongea chochote zaidi ya kushikilia gauni lake la maua maua ambalo limechafuka kwa vumbi na damu.

Licha ya Edna kuishi na wazungu lakini mavazi yake muda wote yalikuwa yakivuka magoti, vazi pakee ambalo alikuwa akivaa kuonyesha umbo lake labda suruali, lakini alikuwa akiheshimu sana utu wake ,ni heshima ambayo wafanyakazi wake walimpendea lakini Edna yote hayo ni kutokana na malezi

Katika wanawake wa Roma ni Amina ambaye alikuwa akivaa kihasara hasara , ile hali ya kuishi Uingereza mpaka kutokijua kiswahili vizuri ilimjengea maisha ya kizungu.

Roma alitamani Edna aongee neno kwani alikuwa ashaanza kupiga hatua kuelekea getini, kwenye maisha yake hakuwahi kujihisi mdogo mbele ya mwanamke , hata kipindi alipokuwa na Seventeen alikuwa mbabe lakini kwa Edna maisha yake yalikuwa ya tofauti sana,

“Edna ndio naondoka hivyo kweli ujue”Aliongea Roma lakini Edna alimwangalia tu na alipogikia geti tu Edna aliongea na kumfanya Roma kusimama.

“Kwahio ndio unaondoka kweli?” Edna alivunja ukimya.

“Sitaki kukaa hapa huku nikiamini nitakukasirisha tena”

“Roma tangu lini ukawa mvivu wa kufikiria , wewe si umesema mwenyewe mara kibao unanipenda?, kama kweli unanipenda kwanini usingenibembeleza hata mara nne ile jana uliponikosea , Ulitakiwa kuniomba msamaha mara nyingi nyingi na kunibembeleza na ningejifanyisha kukusamehe , Roma wewe ni muongo sana hata hunipendi”Aliongea kwa hasira.

Jana hakudhamiria kumfukuza Roma ila alifanya vile ili Roma ahangaike kuomba msamaha, ilikuwa tabia ya wanawake kupendwa kubembelezwa pale wanapokosewa.

Roma mara baada ya Edna kuongea maneno yale alishangazwa na palepale alimsogelea na kumsukumia kwenye ukuta huku akimwangalia kwa ukaribu.

“Mimi sio muongo bali ni mwizi.. nimeiba moyo wako”Aliongea Roma na palepale alimkisi Edna mdomoni

Edna alishindwa kumzuia kufanya vile kwani viongo vyake ni kama vimepalalaizi , licha ya kuogopa Bi Wema angetoka na kuwaona lakini bado aliacha Roma afanye atakavyo.

“Ijapokuwa kuna mtu ameniambia sipaswi kumuambia mke wangu ‘I am sorry’ lakini naomba nikwambie ‘I am sorry’ kwa mambo mengi mabaya niliokufanyia , nakuahidi hakutatokea Rufi mwingine kwenye maisha yetu”

“Sitaki kusikia jina lake?”Aliongea Edna na kumfanya Roma kumuachia Edna baada ya kuhisi mlango wa kuingilia ndani unafunguliwa,

“Miss Edna usharudi”

“Ndio nimerudi Bi Wema”Aliongea Edna na palepale mlango ulifunguliwa na Bi Wema akatoka nje.

“Mr Roma nini kimetokea mbona nguo zenu zimejaa damu?”Aliuliza Bi Wema kwa mshangao.

“Bi Wema tulipata ajali ila tupo sawa , usiwe na wasiwasi”Aliongea Roma.

Bi Wema alijitahidi kutulia licha ya sababu ya Roma kumtia wasiwasi kwani damu zilikuwa nyingi mno ni kama wametoka buchani.

“Lakini kwa mwonekano huo mtakutana vipi na mgeni?”

“Kuna mgeni ? ni nani Bi Wema”Aliuliza Roma kwa mshangao.

“Kuna mdada amefika hapa amejitambulisha kwa jina la Rufi”Aliongea Bi Wema na kauli yake ilimpa Roma ubaridi wa moyo.

Alishindwa kuelewa Rufi alikuwa akimtafutia nini mpaka kuja tena nyumbani kwake , ndio kwanza alikuwa ameyajenga na mke wake lakini ana haribu kila kitu , alijiambia awamu hii hawezi kumsamehe.

Edna na yeye baada ya kusikia kauli hio alijikuta akikasirika na kumwangalia Roma , moja kwa moja alijua huenda Roma alikuwa hajamalizna na huyo mwanamke, kama ni hivyo kwanini apate ujasiri wa kuja mpaka nyumbani.

“Ondoka” Aliongea Edna kwa hasira na kisha akaingia ndani , Bi Wema alishindwa kuelewa hasira za ghafla za Edna zinatoka wapi , aliijua lazima kuna tatizo.

Roma hakuondoka alifuata ndani ili kujua Rufi kaja nyumbani kwake kufanya nini , hakuwa tayari kumuacha Edna kuongea nae peke yake.

Rufi alikuwa amekaa kiwasiwasi ndani ya jumba hili huku akizungusha macho , kulia na kushoto ilikuwa nyumba nzuri mno kwa macho yake.

Mbele yake kulikuwa na glasi ya juisi lakini alionyesha hakuigusa hata kidogo , baada ya kumuona Edna ameingia hapo ndani alisimama kwa wasiwasi na kumwangalia kwa mshangao kutokana na kuchafuka kwake.

Alishangaa zaidi alipomuona |Roma na yeye akiingia akiwa amechafuka na damu mwili mzima.

“Ondoka nyumbani kwangu”Aliongea Edna kwa kingereza na Rufi alijikuta akivuta pumzi alitegemea Edna kuwa hivyo.

Roma aliekuwa nyuma alishangazwa na kauli ya Edna na kujikuta akivuta pumzi na kuangalia juu kwenye ceilingboard, akitafakari namna ya kudhibiti hali hio pasipo kugombana zaidi na Edna.

“Mlikuwa mmeenda wapi , Boss Edna kwanini unoanekana kuchafuka hivyo na Roma kutapakaa damu?”

“Hayakusu, niimesema ondoka , hujanisikia”Aliendelea kuongea kwa hasira

“Hatuwezi kukaa chini na kuongea?, nipo hapa kwa ajili ya kuongea swala muhimu”

Edna ni kama hajamsikia, alimgeukia Bi wema ambaye hakuelewa mazungumzo kwani ligha iliokuwa ikitumika ni kingereza.

“Bi Wema mgeni wetu anaondoka, naomba umsindikize nje”Aliongea Edna na kumfanya Bi Wema kushangaa.

Mgeni aliekuwa mbele yake alimuona mpore sana na alitamani hata kufahamiana nae, lakini lugha ilikuwa tatizo

“Rufi nitakusindikiza kwenda, nje unaweza kuja wakati mwingine” Aliongea BiWema kwa ishara na Rufi alijikuta aking’ata lipsi zake kwa hasira na kumwangalia Roma kwa macho ya kuomba kuhurumiwa.

“Roma hata wewe unanifukuza?” Aliongea.

“Kwanini uniulize hivyo , nilikusaidia kuponyesha sumu iliokuwa kwenye mwili wako , nikakupatia pesa lakini bado umekuja kuharibu mahusiano yangu , unatakiwa kushukuru upo hai mpaka sasa”Aliongea Roma huku akionyesha chuki.

“Unamaanisha nini kumponyesha sumu?”Aliuliza Edna mara baada ya kusikia Roma anataja maswala ya sumu.

Roma alimwelezea kwa ufupi kile kilichotokea mpaka kumponyesha Rufi sumu ilipo kwenye mwili wake.

“Rufi kama hivyo ndio ilitokea unapaswa kushukuru badala ya kutaka kuharibu familia yangu ili kufanikisha matamanio yako”

“Upo sahihi , nimekuja hapa kwa ajili ya kuomba msahamaha”Aliongea na palepale alisogea mpaka katikati sehemu ya wazi na kupiga magoti mbele ya Edna, kitendo kile kilimshangaza hata Roma.

“Ni makosa yangu , akili zangu ziligubikwa na kisasi na kushindwa kufanya maamuzi yaliosahihi , Nilitaka kuharibu familia yako Edna kwa kutumia gistoria yangu na Roma , maisha yangu ya ukimbizi na kuyahofia maisha yangu ndio kilichonifanya nikafika mpaka hapa Tanzania , Boss Edna natamani kuendelea kuishi naomba uniokoe, bila ya wewe kunisaidia siwezi kwenda popote”Aliongea huku akianza kulia kama mtoto mdogo , ilionyesha alikuwa akijikaza muda wote.

Kitendo cha Rufi kulia kama mtoto kilimuumiza sana Bi Wema na alimkimbilia na kumwambia asipige magoti akae kwenye sofa lakini Rufi alikataa.

‘Nitaendelea kupiga magoti mpaka nisikie Edna amenisamehe” Aliongea

Roma alishangaa kwani ni mara ya kwanza kumuona Rufi akiwa na mwonekano wa aina hio , leo hii mwanamke huyu alionyesha kweli kuhitaji msamaha na mwonekano wake ndio uhalisia wake ambao hakuwahi kuona tokea walipokutana..

Edna alikuwa mwepesi wa kuguswa na wenye uhitaji hivyo licha ya kwamba alijua Rufi ndio chanzo cha migororo yake na Roma lakini kumuona analia alijikuta akimuonea huruma.

“Umesema akili zako ziligubikwa na roho ya kisasi , unamaanisha nini?”Aliuliza Edna.

“Nilikimbia kutoka kwenye nchi yangu niliozaliwa , familia yangu pamoja na wakwe zangu wananitafuta na wanapanga kunirudisha nyumbani”Aliongea na kumfanya Bi Wema kumwangalia Roma alihitaji kutafsiriwa na Roma alifanya hivyo.

“Kwanini?, kwanini umekimbia familia yako na wakwe zako , si ndio ndugu zako?”Aliuliza Bi Wema na Roma alitafsiri.

“Kwangu siwachukulii kama familia yangu , natamani ningekuwa na uwezo kuwararua rarua wote”

Aliongea huku akionyesha hasira waziwazi na Roma mabadiliko ya Rufi aliweza kuyatafsiri kama uhalisia na sio maigizo.

Alikuwa ashaanza kuelewa kwani ashaongea na Rufi kabla , hivyo kwa kuunganisha kauli zake alihisi ni kweli kuna kinacheendelea kwenye maisha ya huyu mwanamke.

“Inuka na ukae kwenye sofa”Aliongea Roma kwa kuamrisha

“Miss Edna Umenisamehe?”Aliuliza

“Kaa na unieleze kila kitu kuhusu wewe ni wapi unapotokea”Aliongea Roma lakini Rufi alitaka kwanza kusikia kauli kutoka kwa Edna.

Edna aliekuwa amesimama alimwangalia Roma na mwonekano usoelezeka .

“Fanya kama alivyosema ,nitakusamehe kama utaongea kila kitu”Aliongea Edna mara baada ya kuona Rufi ameshindwa kuamka akisubiria kali yake.

“Thank you..”Alijibu kwa kutabasamu na kisha alisimama na kukaa kwenye sofa na wote kwa pamoja waliketi ili kuweza kumsikiliza.

“Mngefanya hivi tokea mwanzo jamani kuliko kumfanya akalia, Edna kwanini usiende kwanza kubadili mavazi? , hata Mr Roma sio vizuri kuendelea kuw ana mavazi hayo yalichafuka”Aliongea Bi Wema akivuta pumzi ya ahueni baada ya kuona Rufi amekwisha kusamehewa.

“Babe twende tukaoge pamoja”Aliongea Roma akimshika Edna kiumo ni kama alikuwa akifanya makusudi mebele ya Rufi.

“Sawa twende”Edna na yeye alisoma mchezo na kuitika lakini alijitoa kwenye mikono ya Roma , bado alionyesha kama alikuwa na chuki , ijapokuwa alimsamehe Rufi lakini hakutaka kuendelea kumuona hapo ndani.

“Bi Wema muda umeenda sana ni bora tukapata chakula kabisa” Aliongea Edna na Bi Wema aliwaambia alikuwa katikati kuandaa chakula na Qiang Xi yupo barabarani akisubiria gari ya shule ili kumpokea Lanlan..

Edna alitamani kwenda kumpokea Lanlan mwenyewe lakini kutokana na maongezi, aliona kwanza wahitimishe kilichpo mbele yake, hata hivyo Qiang Xi alikuwa barabarani tayari.

Rufi aliwaangalia Roma na Edna wakipandisha ngazi kwenda juu na alimfanya Bi Wema kumwangalia na kisha alitabasamu na kuondoka kuelekea jikoni, alitamani kumshauri Rufi jambo lakini kwakuwa lugha ilikuwa kikwazo alishindwa kuongea lolote.

Baada ya nusu saa kupita Edna na Roma walimwita Rufi juu kwenye chumba cha kujisomea kwa ajili ya maongezi.

Edna alikaa kwa umakini kutaka kusikiliza stori ya Rufi, alijiambia sasa hivi atataka kujua kila kitu kinachomzunguka Roma kutokana na tukio la kukamatwa leo na mwanaume ambaye alikuwa jini.

“Tuambie kila kitu, usije ukapanga kudanganya tena kama unataka kweli msaada wetu” Aliongea Roma kwa tahadhari na Rufi alivuta pumzi nyingi na kuzishusha.

“Sina uhakika kama mshawahi kusikia kuhusu miliki za kijini?” Aliongea Rufi

********

KIGALI NATIONAL UNIVERSTY

Ni ndani ya chuo kikuu nchini Rwanda katika jiji la Kigali, leo hii ilikuwa tofauti kidogo na siku zote kutokana na uchache wa wanafunzi wanaotoka ndani ya chuo hicho na kuingia kwa ajili ya masomo na yote hio ni kutokana na wanafunzi kwenda likizo fupi, lakini licha ya hivyo bado kuna wanafunzi waliokuwepo ndani ya Campus ambao walikuwa wakiingia na wale ambao walikuwa wakitoka makundi makudi na kuna wale waliokuwa peke yao.

Katika geti la kuingilia chuoni hapo alionekana mwanadada aliekuwa amevalia vazi la kisasa kama gauni rangi nyekundu na nyeupe na kofia aina ya Hat pamoja na mkoba wa bei ghali , alikuwa amependeza haswa.

Alikuwa amevalia miwani ya jua huku miguuni akiwa amevalia viatu vya high heels, alitembea kwa madaha na kujiamini huku akiingia ndani ya chuo hicho na kwa muonekano wake ilionyesha kabisa hakuwa mgeni.

Baada ya kukata kwenye viunga vya chuo hicho alikuja kusimama kwenye jengo moja refu kwenda juu la ghorofa kama tano hivi ambalo lilikuwa na maandishi ya Jengo la Utawala kwa liugha mbili, moja ya Kifaransa na Kingereza.

Mwanamke yule aliingia ndani ya jengo hilo huki akipishana na baadhi ya watu kadhaa na ndani ya dakika chache aliingia ndani kabisa ya jengo hilo na kupandisha kwa ngazi na kuingia kwenye Floor namba tatu ambayo ilikuwa na ofisi za wakufunzi wa chuo hiki.

Alitembea akionyesha kujua kilichompeleka hapo na alikwenda kusimama kwenye idara ya Sayansi na kusimama nje na kisha akajiweka sawa na kugonga mlango.

Mwanaume aliekuwa na mwonekano wa kipekee alievalia suti alikunja sura mara baada ya kusikia mtu kugonga mlango , alikuwa na mengi aliokuwa akifikiria na kubwa zaidi alikuwa akisoma kitabu, na kwakuwa wanafunzi wengi wamefunga chuo hakuwa akitegemea mtu kuja kwenye ofisi yake hasa kwa muda kama huo ambao alihitaji utulivu.

Alijinyanyua kutoka kwenye meza iliokuwa imepangiliwa kwa vitabu vingi na kusogelea mlango na kuufungua , alijikuta akitoa mshangao mara baada ya kumuona mwanamke mrembo sana akiwa mbele yake , kilichomshangaza zaidi na kurudi nyuma kama kaona mzimu ni mara baada ya yule mwanamke kuvua ile miwani.

“You. you..!!”Aliongea kwa mshangao

“Why!, little Cripple , its me Am I that scary?”Aliongea akimwita yule mwanaume kilema huku akisema kama alikuwa akiogopesha.

“Mwanamke yule alitoa kofia aliokuwa amevalia na kuonyesha nywlee zake ndefu ambazo zimechanwa vyema kurudishwa nyuma, alikuwa na ngozi laini mno , unaweza kusema ni msichana wa miaka therathini.

Naam hakuwa mwingine mwanamke huyu bali alikuwa ni Kizwe, yule ambaye aliombolezwa kitaifa kwa kufa kwa tatizo la moyo.

Mwanaume aliekuwa mbele yake alikuwa ni Lekcha, ambaye alionyesha mshangao wa hali ya juu mno kama ameona mzimu.

Hakuamini mwanamke ambaye alimshuhudia kwa macbo yake akipoteza maisha ni huyu aliesimama mbele yake , ilikuwa ngumu sana kuamini kile alichokuwa akikishuhudia.

Huenda kama Lekcha hakuwa ameshuhudia mambo makubwa kwenye maisha yake , angepoteza fahamu hapo hapo , lakini hata hivyo kwa kumchunguza Kizwe aliona kuna jambo ambalo halipo sawa.

Kizwe alimpita Lekcha aliekuwa akishangaa shangaa na kuingia ndani kabisa na kisha akatupa mkoba wake kwenye sofa huku akianza kunyoosha mwili wake na kumgeukia Lekcha ambaye alikuwa akihema kwa shida na kuanza kucheka

“Lekcha , why are you still in a daze , Are you so excited to see me that you can’t talk?”

“Lekcha kwanini unashangaa shangaa , au ni mshituko wa kuniona ndio umekufanya kushindwa kuongea”

Lekcha alijikuta akimeza mate mengi na kuvuta pumzi nyingi na kisha kuzitoa huku macho yake yakimwangalia mwanamke aliekuwa mbele yake kwa tahadhari

“Kwanini … nilifikiria ulikufa?”Aliongea Lekcha kwa mshangao kidogo huku akishusha sauti yake na kujitahidi kujituliza ,

Kizwe alitabasamu na kisha alikunjua mikono yake akimpa ishara Lekcha kumkumbatia na Lekcha bila kujielewa anakumbatia mzimu alimsoogelea Kizwe na kisha wakakumbatiana.

“Naomba unisamehe kwa kukufanya kuwa na wasiwasi , ilikuwa kweli kidogo tu nipoteze maisha lakini Mungu alinionea huruma na kunifanya niendelee kuwa hai”Aliongea

“Kama ni hivyo wapi ulikuwa umeenda?, Nilikumisi sana na kukufikria kila wakati”Aliongea Lekcha.

“Nilikumisi pia mpenzi “Aliongea na kisha akambusu Lekcha kwenye shavu kimahaba.

“Nimefurahi mpaka sasa unaendelea kuishi , nilikuwa na wasiwasi yule shetani kakuua , Nimempata mtu wa kunisaidia kulipiza kisasi changu”Aliongea

“Kulipiza kisasi ?Nani?”Aliuliza Lekcha kwa mshangao lakini Kizwe hakumjibu.

‘”Hatujaonana kwa muda mrefu , huoni kama nimebadilika na kuzidi kuwa mrembo?”

Lekcha alimwangalia Kizwe kwa kumchunguza kwa mara nyingine huku hofu ikiwa imepungua na alijiktua akimeza fundo la mate maana Kizwe alikuwa mrembo mno , alikuwa kama mwanamke ambaye ndio kwanza anatimiza miaka therathini.

“Nimemisi sana.” Aliongea Lekcha huku akiweka tabasamu la kifedhuli.

“Acha haraka mara ya mwisho hukunikoleza vizuri”Aliongea Kizwe huku akiweka tabasamu la kimtego.

“Nitafanya vyema awamu hii” aliongea na palepale alimsogelea na kisha kuanza kubusiana mdomoni kwa dakika na Kizwe alimwangalia Lekcha kwa tabasamu.

“Najua wewe ndio mwanaume pekee ambaye ulitokea kunijali na kunipenda kwa madhaifu yangu , Nimeweza kuishi kwa sababu yako tu na sasa nimekupata nataka niwe wako milele”Aliongea Kizwe na kauli ile ilikuwa kama kichocheo kwa Lekcha kwani alimtupia Kizwe kwenye sofa na kuacha gauni lake liache wazi mapaja yake, alilipandisha juu zaidi na kisha akashusha nguo ya ndani kwa spidi na kisha akazama chumvini.

Dakika chache mbele ni migunio ya kimahaba pekee iliotawala ofisi nzima , Lekcha alionyesha kufanya kazi njema kabisa pasipo ya kujiuliza mwanamke aliekuwa mbele yake aliponaje katika tundu la kifo.
 
SEHEMU YA 465

Edna alikuwa kama haamini maneno ya Roma , hakuwa pia tayari kuona Roma anapoteza nguvu kwa ajili yake, ni kama aliogopa ataishi kwa kuwa na deni maisha yake yote.

“Kwahio unamaanisha utamuachia afanye kama anavyotaka?”

“Nina uhakika ninaweza kumuua kwa pigo moja tu , lakini siwezi kuhatarisha maisha yako , natamani nikusikilize lakini siwezi , sio kwa muda huu..”

“Wewe usifanye hivyo ..”

“Najua nimekuumiza mara kibao nadhani hiki ndio ninachostahili kama adhabu , kama sio mimi usingekuwa kwenye hali hii ya hatari hivyo siwezi kuruhusu ukipoteza maisha”Aliongea Roma na kumfanya Edna machozi kuanza kujitengeneza kwenye macho yake.

“Usifanye chochote cha hatari kama nitakufa naamini atakuacha hai, anachotaka ni nguvu zangu za kijini na nitampatia , ukishatoka hapa tumia simu yangu kupiga simu namba ya mwisho nilioipigia”Aliongea Roma na kisha alitoa simu yake na kumpatia Edna ambaye aliipokea kwa wasiwasi, baada ya kuipokea aliitupa chini.

“Sitaki simu yako , huwezi kuniambia unataka kufa halafu umeniumiza sana na kunikasirisha, ukifa kabla sijakusamehe nitakuchukia milele”

“Edna usifanye hivyo , nisikilize tafadhari ..”

“Mimi sitaki, unaruhusiwa kufa baada ya sisi kufunga ndoa , huwezi kuniahidi kitu halafu usitimize”Aliongea huku akianza kukasirika na kutoa machozi kwa wakati mmoja.

“Edna kaa pembeni na kaa kimya, nishafanya maamuzi tayari na ukinizuia nitakufosi ufanye ninavyotaka”Aliongea Roma kwa kumfokea na kumfanya Edna kumwangalia kwa wasiwasi akiwa haamini kama Roma kweli anataka kufanya kama alivyopanga.

“Hahaha.. nyie ndege wawili mpendanao , mshamaliza kuongea?”Aliuliza yule mwanaume .

“Fanya unachotaka”Aliongea Roma.

“Ndio ndio”Alijibu na palepale kisu mfano wa daga rangi ya silver kilionekana kwenye mikono yake , haikuwa Dagger ya kawaida bali ya kichawi ,ilikuwa ikitoa msisimko wa ajabu mno.

“Hii ni Dhana ya zama za kale inafahamika kwa jina la Dragoni Dagger , ni sehemu ya siraha nne za kijini ambazo zina uwezo wa kuzuia nguvu za kijini kwenye mwili wa mtu ambaye amefikia kwenye levo ya kuipita dhiki , ni kama sumu hivyo kama utajifanyisha mjanja kutaka kuutumia uwezo wako basi utakufa hapo hapo, najua Nguvu ya kimaandiko inaweza kuponyesha moyo wako hivyo..”Aliongea

“Kwahio unataka kunichoma kwenye moyo wangu?”Aliuliza Roma kwa mshangao.

“Ndio ninachomaanisha”

“Sasa nakupaje nguvu zangu za kimaandiko?”

“Ni rahisi sana”Aliongea na kisha akatoa kifaa flani kama kibuyu lakini kilichotengenezwa na malighafi ya Jade.

“Unachotakiwa kufanya ni kuruhusu nguvu zako zote za kijini kuingia kwenye hii dhana na mimi nitaweza kuthibitisha kama nguvu ya kimaandiko ni halisi ili usije ukanidanganya na baada ya hapo nitamwondolea mkeo laana”Aliongea

Roma alishangazwa na mwonekano wa kile kijifaa baada ya kukishika, ni moja wapo ya Dhana ambazo aliweza kusikia kutoka kwa Zenzhei na alijiambia hawezi kutegemea uwezo wake pasipo kuwa na moja ya wapo ya Dhana kama atahitaji kuwa na nguvu nyingi za kushinda hata majini kutoka Hongmeng.

Roma alishindwa pia kumjua mwanaume aliekuwa mbele yake ni miliki gani anatokea mpaka kumiliki Dhana za aina hio.

“Nitaingiza nguvu yote ya kimaandiko kwenye hii Dhana na nitakupatia kuithibitisha na utakapoweza kuona ni halisi basi nitatumia hio Daga kujichoma moyoni na utakaporidhika nimekuwa dhaifu utamuondolea mke wangu Laana”Aliongea Roma.

“Deal”Aliongea kwa shauku baada ya kuridhika na maelezo ya Roma .

Edna alijikuta ngozi yake ikiota vipele mara baada ya kusikia Roma angejichoma na Daga kwene eneo la moyo.

“Roma jamani acha kuwa mjinga, huoni anataka kukuua”Aliongea Edna kwa kufoka.

“Kimya! , ninafanya haya kwa ajili ya maisha yako hivyo usiingilie”Aliongea Roma na kumfanya Edna kujawa na hasira huku machozi yakitiririka kwenye macho yake.

Yule jini mweusi alionyesha kufurahishwa na maongezi hayo , mpaka hapo alijiambia anayakaribia mafanikio.

“Fanya haraka unipatie nguvu za kimaandiko , Minyoo yangu ninaweza kushindwa kuiongoza ikihisi njaa”Aliongea na kumfanya Roma kupandwa na hasira lakini hata hivyo hakuwa na namna kwa wakari huo zaidi ya kutiii shuruti kwani kwake Edna alikuwa muhimu.

Alifumba macho huku akiwa ameshikilia ile Dhana ya kibuyu na kulengesha mkono karibu na mdomo wa ile Dhana na palepale kulionekana mfano wa mvuke ukiingia ndani.

Baada ya dakika kumi za Roma kuwa makini kuhamisha nguvu zake za kimaandiko alifumbua macho na kisha alimrushia yule mtekaji kile kibuyu baada ya kuona amemaliza.

Baada mtekaji kuridhika ilikuwa nguvu halisi ya kimaandiko alimrushia Roma ile Daga.

“Hakikisha unafanya kama tulivyokubaliana”Aliongea Roma.

“Fanya hivyo haraka sina muda wa kupoteza”Aliongea na Roma alifumba macho na kisha alijidunga na ile Daga eleo la kifuani akilenga moyo na palepale damu ziliruka mara tatu .

Roma alishindwa kuvumilia maumivu na palepale alidondoka chini kwa kupiga magoti huku uso wake ukionyesha kupauka kwa haraka sana.

“Romaa...!!” Edna aliita akimkimbilia pale chini kwa wasiwasi.

Roma alikuwa akijihisi maumivu, ijapokuwa nguvu ya kimaandiko haikuwa imetoka yote hivyo kujaribu kumponyesha, lakini alihisi maumivu makali kwani spidi yake ilikuwa ya chini mno kupona.

Dakika kadhaa mbele mwili wake ulianza kupoteza nishati ya mbingu na Ardhi na kuendelea kuwa dhaifu.

Sasa hapa utofautishe vitu viwili, kuna nguvu ya kijini ya kimaandiko ambayo inamsaidia kupona lakini pia kuna nguvu ya kijini ya kinishati ya mbingu na Ardhi , ni kama ilivyo kwa Omari au kwa jini ambalo lipo mbele yake , ijapokuwa lilikuwa na nguvu ya Nishati ya mbingu na Ardhi lakini halikuwa linamiliki nguvu ya kimaandiko kutokana na kutumia njia fupi ya kujifunza mbinu za kijini.

Hivyo Daga ilikuwa ikimzuia Roma kutumia nguvu zake za nishati za mbingu na Ardhi ili bwana aliekuwa mbele yake aweze kumponyesha Edna kwa kumuondolea laana na baada ya hapo aweze pia kutoroka kwani Roma hatokuwa na uwezo wa kumdhibiti kwasababu angekuwa ni dhaifu sana kufanya hivyo.

Yule mtekaji mara baada ya kupokea kile kibuyu, alitoa kijisahani kama cha Plastiki lakini ambacho kilionyesha kutengenezwa pia na madini ya Jade na kisha aliruhusu zile nguvu ambazo zipo kwenye ile Dhana ya kibuyu kutoka na kuvamia kile kisahani na palepale maandishi yalianza kujitengeneza kwenye kile kisahani , yalikuwa ndio maandiko ambayo yanaitwa nguvu ya urejesho.

“Nitasoma kwanza haya maandishi na baada ya hapo ndio nitamuondolea mkeo laana”Aliongea akimwangalia Roma ambaye amepiga magoti huku akiugulia maumivu.

“Hakikisha unatimiza ahadi yako”

“Haupo kwenye nafasi ya kuniambia kipi nifanye , wewe ni binadamu wa kawaida ambaye hukupaswa kumiliki kitu muhimu kama hichi , tamaa zako za kutaka kumiliki visivyo vyako ndio zinakuua sasa”

Edna alipatwa na wasiwasi na kisha akashika ile daga

“Unataka kufanya nini?”Aliuliza Roma

“Utakufa Roma kama damu zitaendelea kukutoka, ninaitoa hii daga , anakudanganya tu hawezi kuniondolea laana”

“Edna nisikilize mimi usifanye hivyo”Aliongea Roma kivivu na kumfanya Edna kuanza kulia akiamini Roma anakwenda kufa.

Yule mwanaume mara baada ya kusoma maandishi na kuridhika alioneysha tabasamu.

“Nadhani tumefikia mwisho wa kubagain”

“Okey fanya haraka na mwondolee mke wangu hio laana”

“Sio mbaya nitafanya hivyo , uwezo wako naona umeshuka mpaka kufikia nusu mzunguko , ngoja tumalizane sasa”Aliongea.

Palepale alianza kuongea maneno yasioeleweka kwa spidi kubwa kwa zaidi ya dakika mbili na Edna alijihisi kutapika kwani kuna vitu ambavyo vilikuwa vikitoka tumboni kwa fujo namna ambayo hata yeye alishindwa kuelewa lakini ajabu hakuweza kuona chochote zaidi ya kuhisi mwepesi baada ya vitu kumtoka.

Roma alijikuta akivuta pumzi ya ahueni mara baada ya kuona Edna ashaondolewa ile laana ya minyoo.

Edna alijikaza na kisha akamshikilia Roma vizuri na kumsimamisha, Roma alikuwa dhaifu mno.

“Roma usije kufa kwenye mikono yangu sasa hivi tafadhari jikaze”Aliongea Edna kwa kubembeleza, hakuwa tena CEO wa kampuni kubwa bali muda huu alikuwa akifanana na mtoto ambaye anaomba hela kutoka kwa mzazi.

Alijikuta akianza kujutia kwa kosa lake la siku ya jana la kumfukuza kuondoka nyumbani, alijiambia huenda yote hayo yasingetokea

“Usijali mke wangu siwezi kufa, nitaweza kupona”Aliongea Roma akimfariji.

“Huwezi kujiponyesha , nimesema ninaweza kumuondolea mkeo minyoo lakini kuhusu wewe siwezi kukuacha hai”Aliongea yule mtekaji.

“Wewe muuaji?”Edna alijiktua akitetema kwa hasira mara baada ya kusikia ile kauli.

“Haha..Sijaahidi chochote mimi”Aliongea na kumfanya Roma kufumba macho yake na kisha alishikilia ile Daga na kuichomoa kwa nguvu na damu zilitoka kidogo tu na kuacha, lakini hata hivyo Roma alijaribu kuita nguvu za kijini lakini ilionyesha sumu ya ile Daga ilikuwa ikimzuia kufanya chochote.

“Huwezi kuepuka kifo siku ya leo”Aliongea huku akianza kuminya vidole vyake na palepale aliita nguvu za kijini na kunyoosha ile medali kuelekea aliposimama Roma na Edna, palepale lile Rungu la kichawi liliibuka tena hawani likimsogelea Roma kwa kasi.

BOOM!

Kabla lile Rungu halijamkaribia Roma mlipuko ulitokea kwenye mikono ya yule mtekaji na kilicholipuka hakikuwa kingine bali kile kibuyu Roma alichoingiza nguvu ya kimaandiko.

Ulikuwa ni mlipuko mkubwa ambao uliondoka na nusu ya mkono wa metakaji huku yeye mwenyewe akirushwa na kwenda kutua kwenye ukuta wa kanisa na kufanya uchafu uliokuwa juu kuanza kudondoka chini kwa mtikisiko.

Edna alijikuta akiziba mdomo wake kwa mshangao akiwa haamini kile ambacho alikuwa akiangalia.

Roma alitoa tabasamu la kifedhuli na kisha aliruhusu nguvu ya kijini na kisha akakusanya sumu ya Daga iliokuwa ndani ya mwili wake na kisha akaikausha yote mara moja na palepale mwili wake ulianza kujiponyesha kwa kasi mno.

Upande wa mtekaji alikuwa ametapakaa damu zake yeye mwenyewe akiwa chini akigulia maumivu , ashapoteza mkono lakini pia ilionyesha damu zilikuwa zikivilia ndani kwa ndani ya mwili baada ya kukohoa na kutema damu.

“Umenifanyia .. nini?”Alianza kuongea huku akijikaza na maumivu akiwa haamini kila kitu kimebadilika.

“Ni kama ulivyosema wewe , sijakuahidi chochote baada ya kuondoa laana kwenye mwili wa mke wangu, ushajua mimi ni mtu wa aina gani lakini ukatoka huko ulikotoka na kuja kunichokoza , unaonekana unakipenda kifo kuliko uhai na nitatimiza unachotaka”aliongea Roma huku akitembea kwa kumsogelea.

Edna macho yalimtoka hakuamini yule Roma dhaifu alikuwa sawa kama vile hakuna kilichomtokea.

“Hapana haiweizekani, uwezo wako ulikuwa upo kabisa kwenye nusu mzunguko” Aliongea kwa hamaki na Roma baada ya kumkaribia alikanyaga ule mkono uliokatika.

“Arrgh!”

Edna alijikuta akigeuka nyuma pasipo ya kupenda yeye mwenyewe, kilichokuwa mbele yake kilimuogopesha kuangalia,

“Haujui hata ni kwa namna gani nilivyoweza kugeuza maandishi kuwa nguvu lakini bado unahitaji nguvu zangu” Aliongea Roma huku akitabasamu kwa kejeli.

“Unamaanisha nini?”

“Nilichokupatia sio maandiko halisi bali nilikuwekea mtego kwa kutumia maandishi, upo levo ya chini mno kuelewa nilichokifanya ndio maana ukaamini kweli nilichokupatia ni kitu halisi , sio kweli bali nilikutengenezea bomu” Aliongea Roma na kumfanya yule mtekaji kuanza kukata tamaa , mpaka hapo alijua hana cha kufanya zaidi ya kusubiri kifo chake kwani keshazidiwa ujanja.

Alimdharau Roma kwa kuona kwamba walikuwa kwenye levo sawa na yeye ndio maana hakuchukua tahadhari na hilo ndio kosa lake , Roma akamdhibiti kwa kutumia mpango wake mwenyewe.

“Sasa ni muda wa kuniambie wewe ni nani , na nani kakutuma”Aliongea Roma.

“Niue tu”

Crack!

Roma aliongea kwa vitendo , alipindisha mguu wake kwa nguvu na kukatika palepale. Na kumfanya kupiga ukulele.

Roma aligeuka nyuma na aliona ni afadhali Edna hakuwa akiangalia kile alichokifanya maana alikuwa akidhamiria kufanya ukatili wa hali ya juu.

“Utaniambia au niendelee”

“Siwezi kukuambia chochote , hata hivyo ninakwenda kufa”

Roma alichukua ile daga iliotumika kumchoma kifuani na kisha alimchana mtekaji eneo la tumboni kama anafanya upasuaji na kufanya damu kutoka nyingi huku viungo vya ndani vikionekana ikiwemo Ini.

“Argg!”

“Uniambie usiniambie ni chaguo lako , ila nitahakikisha nakata kiungo kimoja kimoja kadri utakavyoshindwa kujibu swali langu , nakushauri ufanye maamuzi maana unaweza kuongea mwishoni na vivungo ukawa huna”Aliongea Roma na kumfanya Mtekaji kuanza kujawa na hofu mno.

Roma alipanga kukata maeneo ambayo yasingemfanya adui yake kupoteza maisha haraka kwani alikuwa akiijua vizuri anatomi ya mwili.

“Wewe ni pepo kichaa na huwezi kupona kwa sumu iliopo kwenye mwili wako”Mtekaji aliongea kwa hasira.

“Wrong answer “Aliongea Roma na kukata kwa mara nyingine, ile daga ilikuwa na makali mno kama wembe.

“”Nishafeli kwenye misheni yangu tayari, kama sitokufa kwa mikono yako nitakufa kwa mikono ya walionituma, hivyo kuna haja gani ya kukupatia majibu ili uridhike”Aliongea na palepale mwili wake ulianza kukakamaa na damu zilianza kumtoka mfululizo kwa kila tundu kama vile mgonjwa wa Ebola na ndani ya dakika chache tu mwili wake ulianza kuoza kwa spidi kubwa kiasi cha kusababisha harufu kali mno.

Roma alijikuta akishangazwa na jambo kama hilo , alijuwa mwanaume huyo alikuwa na uwezo wa kutawala minyoo ambayo inaweza kula moyo wake lakini hakuamini kama anaweza kujiua mwenyewe kwa kuozesha mwili wake aliona ni kama alishajiwekea mtego wa kujimaliza mambo yatakapoenda kombo.

Alijikuta akiwa na wasiwasi na kujjiuliza kaama mtu huyoa metumwa kwa ajili ya nguvu zake za kijini , je hao waliomtukma anaogopa wangeuuwa wana uwezo mkubwa kiasi gani.

Roma alijiktua akiwaza kwa muda mfupi huku moyo wake ukiwa mzito, alijiambia kwanzia muda huo ni kuwalazimisha wanawake wake kuanza mazoezi ya kujifunza mafunzo ya kijini kwa haraka , kwani kama maadui zake wangekuwa na nguvu kubwa asingeweza kuwalinda.

Aliangalia lile rungu la kijini likiwa bado lipo chini na ile medali pia ilikuwepo chini , aliinama na kuviokota vyote . Roma alishika ile Medali na kuanza kusoma maandishi yake, lakini lugha ilikuwa ngumu kuielewa hivyo aliachana nayo , alitumia kanuni za anga na kisha alificha kwenye Space storage

Baada ya kuhakikisha hajaacha kitu muhimu aligeuka na kumsogelea Edna ambaye bado alikuwa upande wa nyuma kabisa akiogopa kusogea mbele kwani hata harufu ilikuwa ikimfikia.

Alimwangalia Roma kwa wasiwasi, hata hivyo alishaanza kumzoea Roma kwani kwake kuua ni jambo la kawaida.

“Edna umepata mshituko mkubwa kwa yaliotokea siku ya leo , Vipi unajisikia vizuri sasa?”

“Maneno ambayo ulikuwa ukiongea, je kila kitu ulipanga..?”Aliuliza Edna.

“Unaweza kusema hivyo , nisingemwaminisha asingekuwacha hai ndio maana nilikuigizia hata wewe uamini natoa nguvu zangu kweli”Aliongea Roma.

“You bastard”Aliongea Edna kwa kufoka , hakuamini alikuwa amechezewa akili bila ya kujitambua na kulia vyote vile.









SEHEMU YA 466

Edna alijikuta akiinua mguu wake wa kulia na kisha kumpiga teke Roma kwa hasira.

“Umeufanya moyo wangu kuumia kwa kujua kabisa unakwenda kufa , kama ilikuwa mpango kwanini hukuniambia hata kwa ishara, ulikuwa ukifurahia mimi kulia mbele yako au ndio kinilipizia kisasi?”

“Sikuwa na chaguzi nilitakiwa kumfanya aniamini kwa namna yoyote ile , ilitakiwa aamini kweli ninakufa kwa kuona machozi yako, ningekutarifu angeshitukia mchezo”

“Vipi kama angekataa kuniondolea laana alioniwekea ya minyoo ungekubali kufa kwa ajili yangu?”Aliuliza Edna.

“Edna mke wangu nishakuambia kwamba kadri nitakavyokuwa naishi nitahakikisha na wewe unaishi vilevile”

“Kwahio ndio unachotaka, tuseme kwamba tungekufa wote hukoi kuzimu bado ningekuwa na deni kubwa kwako kwa kujua umekufa kwa ajili yangu. si ndio ilikuwa mpango wako?”

“Muone sasa , kuna haja gani ya kuanza kukumbuka yaliopita wakati muda huu tupo salama”Aliongea Roma.

“Kwako hili linaweza lisiwe la umuhimu ila kwangu ni muhimu sana , umetumia maisha yako kuokoa ya kwangu”

“Hukumbiki hata wewe ulinidanganya kwa kuniaminisha kampuni yako inafilisika?”

“IIe ni kwasababu..”Alikosa usemi

“Niliamini usingekasirika baada ya kuekuelezea baada ya matokeo”

“Upo sahihi baada ya siku ile kugundua ukweli sikuweza kuwa na kinyongo juu yako licha ya kwamba sikupenda njia yako , kwasababu nilikuwa nikielewa nia yako halisi , naamini hata wewe pia utaweza kunielewa kwa nilichokifanya”

“Vyovyote vile kikubwa uhai”Aliongea Edna

Roma alitaka kumkumbatia Edna kwa nyuma lakini alikumbuka bado walikuwa kwenye ugomvi na hawakuwa wamesameheana na alikuwa akijiuliza kama Edna ameshasamehe.

“Tunapaswa sasa kuriudi , Recho alikuwa na wasiwasi kweli , ni kheii ukampigia simu muda huu”Aliongea Roma na Edna alitingisha kichwa na kuokota simu ya Roma na kumpigia na baada ya hapo Roma alimvuta kwake na kumkumbatia kifuani.

“Nitafanya hivi kwa ustaarabu , fumba macho yako kwani unaweza kushindwa kuvumilia utakachoona”Aliongea Roma.

“Unamaanisha tunapaa kurudi mjini?”Aliongea Edna pasipo kuamini kama angepaa kwa mara yake ya kwanza.

“Unafikiri ni kwa usafiri upi tutaondoka nao hapa kurudi hii ndio njia pekee rahisi”

Edna alijikuta akifumba macho yake na ndani ya muda mfupi tu Roma aliweza kutua nje ya eneo la bustani kwenye nyumba yao.

“Unaweza kuangalia sasa tumefika”Aliongea Roma

Edna baada ya kufumbua macho yake alijikuta akishangaa mno , hakuamini kama ni kweli wapo nyumbani, ulikuwa ni uzoefu wa mara ya kwanza kuupata katika maisha yake.

Roma alinwangalia Edna ambaye alionyesha hali ya kushangaa kwa muda na Edna alivyogeuka kumwangalia Roma aliona alikuwa akimwangalia.

“Mbona kama unataka kuongea”

Roma alikuwa amefukuzwa nyumbani hivyo hakujua kama anapaswa kuingia ndani au aondoke na ndio maana alikuwa akisubiria maamuzi ya Edna.

“Ah… nishakufikisha nyumbani salama , nadhani napaswa kuondoka sasa”Aliongea Roma kimtego.

Edna alishindwa kuongea chochote zaidi ya kushikilia gauni lake la maua maua ambalo limechafuka kwa vumbi na damu.

Licha ya Edna kuishi na wazungu lakini mavazi yake muda wote yalikuwa yakivuka magoti, vazi pakee ambalo alikuwa akivaa kuonyesha umbo lake labda suruali, lakini alikuwa akiheshimu sana utu wake ,ni heshima ambayo wafanyakazi wake walimpendea lakini Edna yote hayo ni kutokana na malezi

Katika wanawake wa Roma ni Amina ambaye alikuwa akivaa kihasara hasara , ile hali ya kuishi Uingereza mpaka kutokijua kiswahili vizuri ilimjengea maisha ya kizungu.

Roma alitamani Edna aongee neno kwani alikuwa ashaanza kupiga hatua kuelekea getini, kwenye maisha yake hakuwahi kujihisi mdogo mbele ya mwanamke , hata kipindi alipokuwa na Seventeen alikuwa mbabe lakini kwa Edna maisha yake yalikuwa ya tofauti sana,

“Edna ndio naondoka hivyo kweli ujue”Aliongea Roma lakini Edna alimwangalia tu na alipogikia geti tu Edna aliongea na kumfanya Roma kusimama.

“Kwahio ndio unaondoka kweli?” Edna alivunja ukimya.

“Sitaki kukaa hapa huku nikiamini nitakukasirisha tena”

“Roma tangu lini ukawa mvivu wa kufikiria , wewe si umesema mwenyewe mara kibao unanipenda?, kama kweli unanipenda kwanini usingenibembeleza hata mara nne ile jana uliponikosea , Ulitakiwa kuniomba msamaha mara nyingi nyingi na kunibembeleza na ningejifanyisha kukusamehe , Roma wewe ni muongo sana hata hunipendi”Aliongea kwa hasira.

Jana hakudhamiria kumfukuza Roma ila alifanya vile ili Roma ahangaike kuomba msamaha, ilikuwa tabia ya wanawake kupendwa kubembelezwa pale wanapokosewa.

Roma mara baada ya Edna kuongea maneno yale alishangazwa na palepale alimsogelea na kumsukumia kwenye ukuta huku akimwangalia kwa ukaribu.

“Mimi sio muongo bali ni mwizi.. nimeiba moyo wako”Aliongea Roma na palepale alimkisi Edna mdomoni

Edna alishindwa kumzuia kufanya vile kwani viongo vyake ni kama vimepalalaizi , licha ya kuogopa Bi Wema angetoka na kuwaona lakini bado aliacha Roma afanye atakavyo.

“Ijapokuwa kuna mtu ameniambia sipaswi kumuambia mke wangu ‘I am sorry’ lakini naomba nikwambie ‘I am sorry’ kwa mambo mengi mabaya niliokufanyia , nakuahidi hakutatokea Rufi mwingine kwenye maisha yetu”

“Sitaki kusikia jina lake?”Aliongea Edna na kumfanya Roma kumuachia Edna baada ya kuhisi mlango wa kuingilia ndani unafunguliwa,

“Miss Edna usharudi”

“Ndio nimerudi Bi Wema”Aliongea Edna na palepale mlango ulifunguliwa na Bi Wema akatoka nje.

“Mr Roma nini kimetokea mbona nguo zenu zimejaa damu?”Aliuliza Bi Wema kwa mshangao.

“Bi Wema tulipata ajali ila tupo sawa , usiwe na wasiwasi”Aliongea Roma.

Bi Wema alijitahidi kutulia licha ya sababu ya Roma kumtia wasiwasi kwani damu zilikuwa nyingi mno ni kama wametoka buchani.

“Lakini kwa mwonekano huo mtakutana vipi na mgeni?”

“Kuna mgeni ? ni nani Bi Wema”Aliuliza Roma kwa mshangao.

“Kuna mdada amefika hapa amejitambulisha kwa jina la Rufi”Aliongea Bi Wema na kauli yake ilimpa Roma ubaridi wa moyo.

Alishindwa kuelewa Rufi alikuwa akimtafutia nini mpaka kuja tena nyumbani kwake , ndio kwanza alikuwa ameyajenga na mke wake lakini ana haribu kila kitu , alijiambia awamu hii hawezi kumsamehe.

Edna na yeye baada ya kusikia kauli hio alijikuta akikasirika na kumwangalia Roma , moja kwa moja alijua huenda Roma alikuwa hajamalizna na huyo mwanamke, kama ni hivyo kwanini apate ujasiri wa kuja mpaka nyumbani.

“Ondoka” Aliongea Edna kwa hasira na kisha akaingia ndani , Bi Wema alishindwa kuelewa hasira za ghafla za Edna zinatoka wapi , aliijua lazima kuna tatizo.

Roma hakuondoka alifuata ndani ili kujua Rufi kaja nyumbani kwake kufanya nini , hakuwa tayari kumuacha Edna kuongea nae peke yake.

Rufi alikuwa amekaa kiwasiwasi ndani ya jumba hili huku akizungusha macho , kulia na kushoto ilikuwa nyumba nzuri mno kwa macho yake.

Mbele yake kulikuwa na glasi ya juisi lakini alionyesha hakuigusa hata kidogo , baada ya kumuona Edna ameingia hapo ndani alisimama kwa wasiwasi na kumwangalia kwa mshangao kutokana na kuchafuka kwake.

Alishangaa zaidi alipomuona |Roma na yeye akiingia akiwa amechafuka na damu mwili mzima.

“Ondoka nyumbani kwangu”Aliongea Edna kwa kingereza na Rufi alijikuta akivuta pumzi alitegemea Edna kuwa hivyo.

Roma aliekuwa nyuma alishangazwa na kauli ya Edna na kujikuta akivuta pumzi na kuangalia juu kwenye ceilingboard, akitafakari namna ya kudhibiti hali hio pasipo kugombana zaidi na Edna.

“Mlikuwa mmeenda wapi , Boss Edna kwanini unoanekana kuchafuka hivyo na Roma kutapakaa damu?”

“Hayakusu, niimesema ondoka , hujanisikia”Aliendelea kuongea kwa hasira

“Hatuwezi kukaa chini na kuongea?, nipo hapa kwa ajili ya kuongea swala muhimu”

Edna ni kama hajamsikia, alimgeukia Bi wema ambaye hakuelewa mazungumzo kwani ligha iliokuwa ikitumika ni kingereza.

“Bi Wema mgeni wetu anaondoka, naomba umsindikize nje”Aliongea Edna na kumfanya Bi Wema kushangaa.

Mgeni aliekuwa mbele yake alimuona mpore sana na alitamani hata kufahamiana nae, lakini lugha ilikuwa tatizo

“Rufi nitakusindikiza kwenda, nje unaweza kuja wakati mwingine” Aliongea BiWema kwa ishara na Rufi alijikuta aking’ata lipsi zake kwa hasira na kumwangalia Roma kwa macho ya kuomba kuhurumiwa.

“Roma hata wewe unanifukuza?” Aliongea.

“Kwanini uniulize hivyo , nilikusaidia kuponyesha sumu iliokuwa kwenye mwili wako , nikakupatia pesa lakini bado umekuja kuharibu mahusiano yangu , unatakiwa kushukuru upo hai mpaka sasa”Aliongea Roma huku akionyesha chuki.

“Unamaanisha nini kumponyesha sumu?”Aliuliza Edna mara baada ya kusikia Roma anataja maswala ya sumu.

Roma alimwelezea kwa ufupi kile kilichotokea mpaka kumponyesha Rufi sumu ilipo kwenye mwili wake.

“Rufi kama hivyo ndio ilitokea unapaswa kushukuru badala ya kutaka kuharibu familia yangu ili kufanikisha matamanio yako”

“Upo sahihi , nimekuja hapa kwa ajili ya kuomba msahamaha”Aliongea na palepale alisogea mpaka katikati sehemu ya wazi na kupiga magoti mbele ya Edna, kitendo kile kilimshangaza hata Roma.

“Ni makosa yangu , akili zangu ziligubikwa na kisasi na kushindwa kufanya maamuzi yaliosahihi , Nilitaka kuharibu familia yako Edna kwa kutumia gistoria yangu na Roma , maisha yangu ya ukimbizi na kuyahofia maisha yangu ndio kilichonifanya nikafika mpaka hapa Tanzania , Boss Edna natamani kuendelea kuishi naomba uniokoe, bila ya wewe kunisaidia siwezi kwenda popote”Aliongea huku akianza kulia kama mtoto mdogo , ilionyesha alikuwa akijikaza muda wote.

Kitendo cha Rufi kulia kama mtoto kilimuumiza sana Bi Wema na alimkimbilia na kumwambia asipige magoti akae kwenye sofa lakini Rufi alikataa.

‘Nitaendelea kupiga magoti mpaka nisikie Edna amenisamehe” Aliongea

Roma alishangaa kwani ni mara ya kwanza kumuona Rufi akiwa na mwonekano wa aina hio , leo hii mwanamke huyu alionyesha kweli kuhitaji msamaha na mwonekano wake ndio uhalisia wake ambao hakuwahi kuona tokea walipokutana..

Edna alikuwa mwepesi wa kuguswa na wenye uhitaji hivyo licha ya kwamba alijua Rufi ndio chanzo cha migororo yake na Roma lakini kumuona analia alijikuta akimuonea huruma.

“Umesema akili zako ziligubikwa na roho ya kisasi , unamaanisha nini?”Aliuliza Edna.

“Nilikimbia kutoka kwenye nchi yangu niliozaliwa , familia yangu pamoja na wakwe zangu wananitafuta na wanapanga kunirudisha nyumbani”Aliongea na kumfanya Bi Wema kumwangalia Roma alihitaji kutafsiriwa na Roma alifanya hivyo.

“Kwanini?, kwanini umekimbia familia yako na wakwe zako , si ndio ndugu zako?”Aliuliza Bi Wema na Roma alitafsiri.

“Kwangu siwachukulii kama familia yangu , natamani ningekuwa na uwezo kuwararua rarua wote”

Aliongea huku akionyesha hasira waziwazi na Roma mabadiliko ya Rufi aliweza kuyatafsiri kama uhalisia na sio maigizo.

Alikuwa ashaanza kuelewa kwani ashaongea na Rufi kabla , hivyo kwa kuunganisha kauli zake alihisi ni kweli kuna kinacheendelea kwenye maisha ya huyu mwanamke.

“Inuka na ukae kwenye sofa”Aliongea Roma kwa kuamrisha

“Miss Edna Umenisamehe?”Aliuliza

“Kaa na unieleze kila kitu kuhusu wewe ni wapi unapotokea”Aliongea Roma lakini Rufi alitaka kwanza kusikia kauli kutoka kwa Edna.

Edna aliekuwa amesimama alimwangalia Roma na mwonekano usoelezeka .

“Fanya kama alivyosema ,nitakusamehe kama utaongea kila kitu”Aliongea Edna mara baada ya kuona Rufi ameshindwa kuamka akisubiria kali yake.

“Thank you..”Alijibu kwa kutabasamu na kisha alisimama na kukaa kwenye sofa na wote kwa pamoja waliketi ili kuweza kumsikiliza.

“Mngefanya hivi tokea mwanzo jamani kuliko kumfanya akalia, Edna kwanini usiende kwanza kubadili mavazi? , hata Mr Roma sio vizuri kuendelea kuw ana mavazi hayo yalichafuka”Aliongea Bi Wema akivuta pumzi ya ahueni baada ya kuona Rufi amekwisha kusamehewa.

“Babe twende tukaoge pamoja”Aliongea Roma akimshika Edna kiumo ni kama alikuwa akifanya makusudi mebele ya Rufi.

“Sawa twende”Edna na yeye alisoma mchezo na kuitika lakini alijitoa kwenye mikono ya Roma , bado alionyesha kama alikuwa na chuki , ijapokuwa alimsamehe Rufi lakini hakutaka kuendelea kumuona hapo ndani.

“Bi Wema muda umeenda sana ni bora tukapata chakula kabisa” Aliongea Edna na Bi Wema aliwaambia alikuwa katikati kuandaa chakula na Qiang Xi yupo barabarani akisubiria gari ya shule ili kumpokea Lanlan..

Edna alitamani kwenda kumpokea Lanlan mwenyewe lakini kutokana na maongezi, aliona kwanza wahitimishe kilichpo mbele yake, hata hivyo Qiang Xi alikuwa barabarani tayari.

Rufi aliwaangalia Roma na Edna wakipandisha ngazi kwenda juu na alimfanya Bi Wema kumwangalia na kisha alitabasamu na kuondoka kuelekea jikoni, alitamani kumshauri Rufi jambo lakini kwakuwa lugha ilikuwa kikwazo alishindwa kuongea lolote.

Baada ya nusu saa kupita Edna na Roma walimwita Rufi juu kwenye chumba cha kujisomea kwa ajili ya maongezi.

Edna alikaa kwa umakini kutaka kusikiliza stori ya Rufi, alijiambia sasa hivi atataka kujua kila kitu kinachomzunguka Roma kutokana na tukio la kukamatwa leo na mwanaume ambaye alikuwa jini.

“Tuambie kila kitu, usije ukapanga kudanganya tena kama unataka kweli msaada wetu” Aliongea Roma kwa tahadhari na Rufi alivuta pumzi nyingi na kuzishusha.

“Sina uhakika kama mshawahi kusikia kuhusu miliki za kijini?” Aliongea Rufi

********

KIGALI NATIONAL UNIVERSTY

Ni ndani ya chuo kikuu nchini Rwanda katika jiji la Kigali, leo hii ilikuwa tofauti kidogo na siku zote kutokana na uchache wa wanafunzi wanaotoka ndani ya chuo hicho na kuingia kwa ajili ya masomo na yote hio ni kutokana na wanafunzi kwenda likizo fupi, lakini licha ya hivyo bado kuna wanafunzi waliokuwepo ndani ya Campus ambao walikuwa wakiingia na wale ambao walikuwa wakitoka makundi makudi na kuna wale waliokuwa peke yao.

Katika geti la kuingilia chuoni hapo alionekana mwanadada aliekuwa amevalia vazi la kisasa kama gauni langi nyekundu na nyeupe na kofia aina ya Hat pamoja na mkoba wa bei ghali , alikuwa amependeza haswa.

Alikuwa amevalia miwani ya jua huku miguuni akiwa amevalia viatu vya high heels, alitembea kwa madaha na kujiamini huku akiingia ndani ya chuo hicho na kwa muonekano wake ilionyesha kabisa hakuwa mgeni.

Baada ya kukata kwenye viunga vya chuo hicho alikuja kusimama kwenye jengo moja refu kwenda juu la ghorofa kama tano hivi ambalo lilikuwa na maandishi ya Jengo la Utawala kwa liugha mbili, moja ya Kifaransa na Kingereza.

Mwanamke yule aliingia ndani ya jengo hilo huki akipishana na baadhi ya watu kadhaa na ndani ya dakika chache aliingia ndani kabisa ya jengo hilo na kupandisha kwa ngazi na kuingia kwenye Floor namba tatu ambayo ilikuwa na ofisi za wakufunzi wa chuo hiki.

Alitembea akionyesha kujua kilichompeleka hapo na alikwenda kusimama kwenye idara ya Sayansi na kusimama nje na kisha akajiweka sawa na kugonga mlango.

Mwanaume aliekuwa na mwonekano wa kipekee alievalia suti alikunja sura mara baada ya kusikia mtu kugonga mlango , alikuwa na mengi aliokuwa akifikiria na kubwa zaidi alikuwa akisoma kitabu, na kwakuwa wanafunzi wengi wamefunga chuo hakuwa akitegemea mtu kuja kwenye ofisi yake hasa kwa muda kama huo ambao alihitaji utulivu.

Alijinyanyua kutoka kwenye meza iliokuwa imepangiliwa kwa vitabu vingi na kusogelea mlango na kuufungua , alijikuta akitoa mshangao mara baada ya kumuona mwanamke mrembo sana akiwa mbele yake , kilichomshangaza zaidi na kurudi nyuma kama kaona mzimu ni mara baada ya yule mwanamke kuvua ile miwani.

“You. you..!!”Aliongea kwa mshangao

“Why!, little Cripple , its me Am I that scary?”Aliongea akimwita yule mwanaume kilema huku akisema kama alikuwa akiogopesha.

“Mwanamke yule alitoa kofia aliokuwa amevalia na kuonyesha nywlee zake ndefu ambazo zimechanwa vyema kurudishwa nyuma, alikuwa na ngozi laini mno , unaweza kusema ni msichana wa miaka therathini.

Naam hakuwa mwingine mwanamke huyu bali alikuwa ni Kizwe, yule ambaye aliombolezwa kitaifa kwa kufa kwa tatizo la moyo.

Mwanaume aliekuwa mbele yake alikuwa ni Lekcha, ambaye alionyesha mshangao wa hali ya juu mno kama ameona mzimu.

Hakuamini mwanamke ambaye alimshuhudia kwa macbo yake akipoteza maisha ni huyu aliesimama mbele yake , ilikuwa ngumu sana kuamini kile alichokuwa akikishuhudia.

Huenda kama Lekcha hakuwa ameshuhudia mambo makubwa kwenye maisha yake , angepoteza fahamu hapo hapo , lakini hata hivyo kwa kumchunguza Kizwe aliona kuna jambo ambalo halipo sawa.

Kizwe alimpita Lekcha aliekuwa akishangaa shangaa na kuingia ndani kabisa na kisha akatupa mkoba wake kwenye sofa huku akianza kunyoosha mwili wake na kumgeukia Lekcha ambaye alikuwa akihema kwa shida na kuanza kucheka

“Lekcha , why are you still in a daze , Are you so excited to see me that you can’t talk?”

“Lekcha kwanini unashangaa shangaa , au ni mshituko wa kuniona ndio umekufanya kushindwa kuongea”

Lekcha alijikuta akimeza mate mengi na kuvuta pumzi nyingi na kisha kuzitoa huku macho yake yakimwangalia mwanamke aliekuwa mbele yake kwa tahadhari

“Kwanini … nilifikiria ulikufa?”Aliongea Lekcha kwa mshangao kidogo huku akishusha sauti yake na kujitahidi kujituliza ,

Kizwe alitabasamu na kisha alikunjua mikono yake akimpa ishara Lekcha kumkumbatia na Lekcha bila kujielewa anakumbatia mzimu alimsoogelea Kizwe na kisha wakakumbatiana.

“Naomba unisamehe kwa kukufanya kuwa na wasiwasi , ilikuwa kweli kidogo tu nipoteze maisha lakini Mungu alinionea huruma na kunifanya niendelee kuwa hai”Aliongea

“Kama ni hivyo wapi ulikuwa umeenda?, Nilikumisi sana na kukufikria kila wakati”Aliongea Lekcha.

“Nilikumisi pia mpenzi “Aliongea na kisha akambusu Lekcha kwenye shavu kimahaba.

“Nimefurahi mpaka sasa unaendelea kuishi , nilikuwa na wasiwasi yule shetani kakuua , Nimempata mtu wa kunisaidia kulipiza kisasi changu”Aliongea

“Kulipiza kisasi ?Nani?”Aliuliza Lekcha kwa mshangao lakini Kizwe hakumjibu.

‘”Hatujaonana kwa muda mrefu , huoni kama nimebadilika na kuzidi kuwa mrembo?”

Lekcha alimwangalia Kizwe kwa kumchunguza kwa mara nyingine huku hofu ikiwa imepungua na alijiktua akimeza fundo la mate maana Kizwe alikuwa mrembo mno , alikuwa kama mwanamke ambaye ndio kwanza anatimiza miaka therathini.

“Nimemisi sana.” Aliongea Lekcha huku akiweka tabasamu la kifedhuli.

“Acha haraka mara ya mwisho hukunikoleza vizuri”Aliongea Kizwe huku akiweka tabasamu la kimtego.

“Nitafanya vyema awamu hii” aliongea na palepale alimsogelea na kisha kuanza kubusiana mdomoni kwa dakika na Kizwe alimwangalia Lekcha kwa tabasamu.

“Najua wewe ndio mwanaume pekee ambaye ulitokea kunijali na kunipenda kwa madhaifu yangu , Nimeweza kuishi kwa sababu yako tu na sasa nimekupata nataka niwe wako milele”Aliongea Kizwe na kauli ile ilikuwa kama kichocheo kwa Lekcha kwani alimtupia Kizwe kwenye sofa na kuacha gauni lake liache wazi mapaja yake, alilipandisha juu zaidi na kisha akashusha nguo ya ndani kwa spidi na kisha akazama chumvini.

Dakika chache mbele ni migunio ya kimahaba pekee iliotawala ofisi nzima , Lekcha alionyesha kufanya kazi njema kabisa pasipo ya kujiuliza mwanamke aliekuwa mbele yake aliponaje katika tundu la kifo

SEHEMU YA 467.

Roma alipatwa na mshangao baada ya kusikia miliki za kijini lakini hakuonyesha mshangao wake waziwazi , alitaka kumpa nafasi Rufi kuelezea kila kitu.

Upande mwingine Edna alionyesha kushangaa mara baada ya kusikia kuhusu miliki za kijini , hakuelewa Rufi alikuwa akitaka kumaanisha nini.

Kwa maelezo ya Rufi ni kwamba amezaliwa katika miliki ya kijini ifahamikayo kwa jina la Kekexil, anasema miliki ya Kekexil ni kama miliki ya Hongmeng ambayo ilikuwa ikipatikana ndani ya China.

Ni miliki ambayo ilikuwa pia ikiaminika kwa kuwa na nguvu kutokana na majini kuvuna nishati ya mbingu na ardhi , lakini pia ni miliki iliokuwa ikiisifika sana kwa matumizi ya dhana za kimababu.

Tukisema Dhana namaanisha vitu mfano wa pete za majini , bangiri za majini na vingine vingi vifananavyo na hivyo.

Anasema kutokana na kuzaliwa kwa kuchanganya damu , yaani ya binadamu wa kawaida na ya jini mwili wake ulikuwa tofauti na watu wa jamii ya majini yalioishi ndani ya miliki hizo.

Inapotokea Binadamu wa kawaida akapata ujauzito wa jini mtoto atakaezaliwa atakuwa na kiwango kikubwa cha nguvu ya Yin kuliko Yang(Yin Meridian) hivyo atashindwa kujifunza mbinu za kijini kutokana na kushindwa kubalansi hizo nguvu.

Katika ulimwengu wa roho tukisema Meridiani ni sehemu ambazo hazionekani katika mwili ambazo mara nyingi ndio zinafanya udhibiti wa mfumo wa uelekeo wa nishati ya mwili au nguvu, hizo ni sehemu ambazo kama mchawi akikuroga basi moja kwa moja atatumia hizi Meridian ni sawa sawa kabisa na Acupancture point, kwa mfano kama mchawi akaziba meridiani ambazo zipo tumboni basi magonjwa utakayohisi ni ya eneo hilo, sasa basi kila binadamu anazo spiritual energy ambazo zinadhibitiwa na hizo Meridiani.

Faida kubwa ya kuzaliwa na Yin Meridian ni kwamba mwili unakuwa mstahimilivu na aina ya sumu nyingi au magonjwa , yaani unaweza kupewa sumu lakini ukashindwa kufa na hiko ndio kilichokuwa kwa Rufi.

Baba yake aliemtaja kwa jina la Mozheng hakuwa akimpenda na ilisemekana alipewa misheni maalumu ya kuzaa na binadamu wa kawaida ili kupatikana kwa nusu jini ambaye atakuwa na Yin Meridian kwa ajili ya kumtumia kwenye majaribio ya madawa ambayo yatatumika kusaidia majini kuvuna nishati..

Hivyo maisha ya Rufi ndani ya miliki ya Kekexil yalikuwa magumu kwani hakuchukuliwa kama mtu wala jini bali alichukuliwa kama kifaa cha majaribio ya dawa.

Anasema tokea akiwa mdogo alikuwa akipewa dawa nyingi sana kwa ajili ya majaribio lakini hakuweza kufa kutokana na mwili wake ulivyo , dawa alizopewa zilikuwa sumu hivyo ilimfanya kuishi na maumivu makali sana katika mwili wake kwa karibia miaka ishirini yote mpaka alipokuja kukutana na Roma baada ya kutoroka ujinini.

Rufi anasema baada ya kutumika kwa miaka mingi kama chombo cha majaribio, Koo ya kijini kutoka China ifahamikayo kwa jina la Luo ilikuja kwenye miliki ya koo yao na kufanya mazungumzo ya kibiashara ya kubadilishana mbinu za kuvuna nishati ya mbingu na Ardhi , katika mazungumzo yaliofanyika Mozheng ambaye alikuwa ndio mtoto wa mkuu wa miliki ya Kekexil ilibidi amtoe Rufi kama mabadilishano.

Yaani kwa maneno marahisi jamii ya Luo kutoka China walimtaka binadamu aliezaliwa na nusu jini nusu binadamu ambaye angekuwa na Yin Meridian kwa ajili ya kwenda kufanyia majaribio wakati huo huo Luo wakitoa baadhi ya mbinu zao mahili za kujifunza uchawi wa kijijni.

Hivyo Rufi alitolewa kwenda jamii ya Luo kwa njia ya ndoa na kuwa wakwe rasmi wa jamii ya kijini ya Luo.

“Kwahio ndio maana ukawa na sumu nyingi mwilini nilipokutana?”Aliuliza Roma na Rufi alitingisha kichwa kukubali

“Sumu ulioitoa nilikuwa nayo kwa miaka ishirini , sikuamini kama ulifanikisha kuitoa kirahisi”

“Miaka ishirini?”Roma alijikuta akishangaa mno.

“Nashindwa kuelewa kwanini mzazi akamfanyia mtoto wake ukatili wa namna hio”Aliongea Edna kwa huzuni maana simulizi ilimgusa vilivyo.

“Boss Edna huwezi amini, lakini kwenye miliki za kijini utajiri na nguvu ndio vinavyotawala na mzazi hashindwi kumtoa kafara mtoto kwa ajili ya kupata uwezo mkubwa wa nguvu kila fursa inapojitkeza”Aliongea Rufi.

“Kwahio uliweza kutoka vipi mpaka tukakutana Loss Angeles?”Aliuliza Roma na swali lake ni kama lilimkumbusha Rufi mbali na kumfanya aanze kutoa machozi na ilibidi kwanza wampe nafasi kutulia.

“Mwezi mmoja mara baada makubaliano ya kibiashara kukamilika na mimi kwenda katika miliki za kijini za China ndipo nilipotorishwa”Aliongea Rufi na kuwafanya kumwangalia kwa umakini.

“Ulitoroshwa?”

“Kama nilivyosema sikuwa na mama zaidi ya kuwa na baba ambaye hakuwa akinipenda , katika makuzi yangu yote nililelewa na mlezi ambaye alikuwa pia ni jini na ndio huyo aliejitolea maisha yake kunitorosha miezi kadhaa tu mara baada ya kuingia katika miliki za China”

Kwa maelezo ya Rufi ni kwamba alikuwa na mlezi ambaye alimlea kutoka utotoni na mlezi alikuwa kama mzazi kwa Rufi na ndio mtu pekee ambaye alikuwa akimpenda na kumjali , lakini licha ya hivyo hakuwa na namna ya kumsaidia Rufi pale mwili wake ulipokuwa ukitumiaka kama majaribio ya dawa , sababu kubwa iliompa ugumu mlezi kutokumsaidia Rufi ni kutokana na kwamba hakuwa akijua namna ya kumtoa Rufi kwenda kwenye ulimwengu wa kawaida kupitia miliki yao ya kijini na njia pekee ya ‘shortcut’ ambayo alikuwa akiifahamu ya kutoka katika miliki ya kijini ni kupitia China katika jamii ya Hongmeng au Luo.

Hivyo pendekezo la kuozeshwa kwa ukoo wa Luo huku kukiwa na ajenda ya siri ya Rufi kwenda kutumika tena kama chombo cha kujaribishia madawa , mlezi wake ndipo alipoona hio ni nafasi adhimu sana ya kumtorosha Rufi.

Na mpango wa kwanza aliofanya ni kuhakikisha anaambatana na Riufi kwenda miliki ya Luo kama ndugu pekee wa Rufi atakaemsaidia na kupitia huko atatafuta mbinu ya kumtorosha na hiko ndio kilichotokea.

Sasa kwa maelezo ya Rufi hakuelewa mlezi wake alifanikisha vipi, ila alisema alipotoroshwa na kuletwa kwenye ulimwengu wa kawaida alipatiwa kila kitu kuanzia hela na vidhibiri vya kusafiria pamoja na kumwambia aende nchi yoyote mbali na bara la Asia akaanze maisha upya.

Rufi hakutaka kutengana na mlezi wake , lakini mlezi alimwambia kwamba yeye lazima arudi ujinini ili kuweza kuwasubirisha majini wasimpate mpaka atakapo toka nje ya bara la Asia , akiamini kwamba kuna mkataba wa The Gods Treaty ambao ungemlinda Rufi kwani majini yasingetoka kwenda bara lingine kufanya fujo na hiko ndio kilichotokea, Kwahio kwa maneno marahisi mlezi alijitoa kafara kwa ajili ya Rufi.

Rufi anasema alitumia mwaka mmoja tu kujifunza lugha na maisha ya kawaida katika ulimwengu wa kawaida na kutokana na kuzaliwa nusu binadamu nusu jini uwezo wake wa akili ulikuwa mkubwa sana.

Hivyo maisha yake ndani ya jiji la New York hayakuwa magumu kwani alijifunza udukuzi lakini wakati huo huo alijifunza namna ya kutapeli watu.

“Vipi ulisema mzazi wako ni mwafrika katoka Afrika ya mashariki , ulijuaje au ulikuwa unaongea uongo?”Aliuliza Edna.

“Nilichosema ni kweli , Mlezi wangu aliniambia nimetokea Afrika ya mashariki lakini hajui nchi gani na huko ndio baba alienda kupandikiza mimba yake kwa binadamu wa kawaida ndipo nilipozaliwa , lakini niliogopa kukaa kwenye nchi hizi za Afrika mashariki kwani niliogopa ningekamatwa na kurudishwa ujinini , hivyo mara baada ya kumuona Roma ana nguvu kubwa za kijini mpaka kuniponyesha sumu iliokuwa ikinisumbua miaka na miaka ndio maana nikapata ujasiri wa kuja hapa Tanzania, nilihisi huenda pia nikabahatika kumuona mzazi wangu japo asilimia za kukutana nae ni sifuri”Aliongea.

“Ni levo ipi kubwa zaidi ambayo majini wamefikia?”Aliuliza Roma.

“Wengi ni levo ya Nafsi , lakini waliopitia levo ya kuipita dhiki pia wapo”Aliongea na kumfanya Roma kuguna mpaka hapo ilimaanisha wengi wapo sawa na yeye , lakini kubwa zaidi walikuwa pia na dhana.

“Nahitaji msaada wenu, sina mtu yoyote wa kunisaidia, sina ndugu wala wa kumtegemea , maisha yangu yote yamekuwa ya upweke na kuishi kwa wasiwasi”Aliongea.

“Ujio wako hapa Tanzania unaniweka kwenye matatizo Rufi”Aliongea Roma.

“Roma usiongee hivyo naomba umsaidie , hatuwezi kumuacha wakamchukua tena kwenda kumtesa”Aliongea Edna ambaye macho yake yalikuwa mekundu , hakuamini kuna watu waliokuwa wakipitia magumu kama Rufi.

“Edna hujamsikia alichosema , kuna majini yaliofikia levo ya Kuipita dhiki na sio mmoja bali wengi”Aliongea Roma kwa hofu , alijua akiamua kumsaidia Rufi ni kwamba anaingia vita na watu wanaomtaka.

“Najua chaguzi yangu ni ya kibinafsi , lakini sina pakwenda..”Aliongea na kuanza kulia kwa Kwikwi na Edna alijikuta akishindwa kuvumilia na kumsogelea kumkumbatia.

Roma alijikuta akifikiria kidogo lakini kuna kitu kilimjia katika kichwa chake na kumgeukia Rufi.

“Rufi umesema madawa ambayo walikuwa wakijaribisha kwenye mwili wako ni kwa ajili ya kuwasaidia kuweza kujifunza kwa urahisi mbinu za kuvuna nishati , si ndio?”Aliuliza Roma.

“Ndio ukiachana na dawa pia kuna maandiko maalumu ya mafunzo na hii imesiaidia sana wengi wao kuingia levo ya Nafsi na wale ambao wameshindwa kuingia levo ya nafsi walikosa hizo dawa , miliki nyingi zinatofautiana kutokanana umiliki wa dawa pamoja na hayo maandiko ya mafunzo”Aliongea na Roma alitabasamu.

Hehe…Kama nikienda ujinini kuiba hivyo vidonge na kuwapa wanawake wangu si wataingia levyo ya nafsi chapu tu”Aliwaza Roma

“Sina mpango wa kukusaidia kulipa kisasi , lakini kwasababu ya uwepo wa hayo madawa na maandiko ya mafunzo nadhani ni malipo tosha kwangu ambayo naweza kupata nikikusaidia”Aliongea Roma na kumfanya Rufi kutamani kuzimia palepale.

“Roma huwezi kuwaibia kabisa , labda nikuambie tu Hongmeng licha ya kuwa na nguvu kubwa lakini pia kukosa dawa ambazo zinawasiadia katika mafunzo , lakini hawakuhahji kuchukua hatua na kwenda kuvamia miliki ya kijini ya Luo au Kekexil kwa ajili ya kupata maandiko hayo wala mbinu zao za kutengeneza dawa, wana nguvu ambayo huwezi kushindana nayo”Aliongea Rufi na maneno yake yalimtisha Edna.

“Roma nakuonya usije ukaenda huko , ni hatari”Alionya Edna maana ashaona dalili za Roma kutafuta namna ya kuzamia.

Roma hakuwa na mpango wakwenda kizembe alijua ni kweli angeweza kufa , lakini kwasababu Rufi yupo lazima fursa ingejitokeza, siku zote alikuwa akitamani kwenda kwenye miliki hizo lakini hakujua namna ya kufika huko.

Baada ya Roma kuwaza kwa muda , alikumbuka jini mweusi aliepambana nae na kumuua kisha kuchukua dhana ya mfano wa medali na aliichomoa kwenye hifadhi ya anga na kisha akampatia Rufi kuiangalia.

“Wewe!!… kwanini unayo hii , umeipata wapi?”Aliuliza Rufi kwa mshangao. Na Roma ilibidi aelezee kila kitu walichokutana nacho siku hio na hapo ndipo Rufi alielewa kwanini walifika wakiwa wamechafuka na damu.

“Katika ulimwengu wa kijini Dhana zinapangiliwa katika levo tatu , Levo ya chini(‘Lower) , Levo ya kati(Middle) , Levo ya juu(Higher) , dhana za levo ya juu ni nadra sana , Hii Medali inafahamika kwa jina la Ganyua ipo katika kundi la Chini kwenda kati (Lower to middle) au unaweza kusema ni dhana yenye nguvu zaidi katika kundi la chini kukaribia kundi la kati , kazi yake kubwa inatumika kama ngao na inaweza kukinga mapigo zaidi ya levo ya kuipita Dhiki, kuhusu Daga uliozungumzia inaitwa Blood Dragoni ndio yenye nguvu kubwa sana na hata majini ambao wapo levo ya Kuipita Dhiki wanaihofia”Aliongea Rufi.

“Unajuaje yote hayo?”Aliuliza Roma.

“Licha ya kutumika katika majaribio ya dawa, lakini pia nilipewa nafasi ya kujifunza kuhusu namna majini wanavyovuna nishati za mbingu na ardhi lakini pia tamaduni zote”

Roma alijikuta akipata uraha ya ghafla mpaka hapo aliona Rufi angekuwa msaada mkubwa kwake , kwani angemsaidia kujibu maswali mengi ambayo siku zote alikuwa akijiuliza.

“Hakuna kitu kingine ulichokiona, naweza kukusaidia kutambua mtu uliepambana nae anatokea miliki ipi?”Aliuliza Rufi na kumfanya Roma kufikiria kwa dakika kadhaa na palepale alichukua karatasi na karamu na kuchora mchoro flani usioelezeka.

“Huu ni mchoro uliokuwa kwenye Dhana kama kibuyu alionipatia niingize nguvu ya kimaandiko , ja unaweza kutambua unamaanisha nini?”Aliuliza Roma na Rufi aliangalia ule mchoro kwa haraka.

“Huu sio mchoro”Aliongea na kumfanya Roma kushangaa.

“Kama sio mchoro ni nini?”

“Hii ni nembo ya miliki ya kijini ya Hongmeng, kama amesema kuna watu walimuagiza kuchukua uwezo wako wa kijini basi naweza kusema ni Hongmeng lakini sina uhakika”

“Nilijua Hongmeng ni jamii ya kichina pekee?”

“Ndio Hongmeng ni jamii ya kichina pekee , lakini wanaruhusu watu wa rangi tofauti kujifunza mbinu zao na tamaduni zao kama tu wataonyesha kuwa na faida kwao”Aliongea Rufi na Roma alielewa maneno yake maana hata Omari alitokea Hongmeng lakini hakuwa mchina.

“Kati ya Hongmeng na Koo zingine , ipi yenye nguvu zaidi?”Aliuliza Roma.

“Yenye nguvu zaidi ni Kekexil nilipotokea , hii nguvu yake kubwa ni kutokana na mchanganyiko wa watu , lakini pia ukiachana na nguvu za kijini pia wanamiliki madini mengi hasa ya dhahabu, Zipo jamii nyingi ambazo nimesikia zina nguvu kubwa kuzidi hata Kekexil moja wapo inafahamika kwa jina la PANAS , Hongmeng nguvu yao ipo chini sana na Luo wamewazidi , kinachowafanya Hongmeng kuwa na ushawishi mkubwa ni kutokana na kuidhibiti serikali ya China , jamii nyingine za kijini hazina miingiliano sana na binadamu wa kawaida kama ilivyo kwa Hongmeng”Aliongea Rufi.

“Panas hii miliki nimeisikia lakini niliambiwa ipo ni ya kufikirika tu?”Aliongea Roma.

“Inasemekana ipo na ni jamii kubwa ya kijini , kubwa sana na yenye maendeleo ambayo ni zaidi ya unavyofikiria na kuna utamaduni wa kipekee kabisa tofauti na jamii nyingine, katika hadhithi za kijini ili kuweza kwenda PANAS lazima kwanza utoke nje ya dunia ya kawaida ndio njia ya shorcurt”Aliongea Rufi na kumfanya Roma kujawa na shauku , alisikia hata nguvu yake ya kimaandiko asili yake ni huko Panas.

“Kwahio Roma kwasababu umemuua utakuwa tayari adui na jamii ya huko Hongmeng?”Aliuliza Edna ambaye alikuwa akijitahidi kuelewa maana alikuwa akiona giza tu , mambo mengine kwake hakuweza kuyakifikiria kimantiki wala kisayansi.

“Siamini hivyo , ni ngumu sana Hongmeng kuja mpaka huku kwa ajili ya kumtafuta Roma , kuna uwezekano alitokea kwenye jamii nyingine lakini alitaka tufahamu ametokea Hongmeng”Aliongea na hata Roma mwenywe alielewa.

“Upo sahihi na hata kama angetokea Hongmeng , kuja mpaka Tanzania na kuniletea vurugu ni kosa alilofanya , sheria zinaniruhusu kuua majini yote yanayoingilia maswala ya kibinadamu nje ya bara la Asia”Aliongea Roma.

“Kwahio unamaanisha hajatokea Hongmeng?”Aliuliza Edna.

“Miss Edna moja ya sifa kubwa ya koo ya Luo au Kekexil wanafanya lolote lile kuwawezesha kupanda levo za juu , hata kama ni kutoka duniani kwa ajili ya kutafuta msaada wa kuwasaidia , nadhani kuna kitu walikihitaji kutoka kwa Roma ndio maana akaja mpaka Tanzania na kama ulivyosema alionekana kuwa mweusi basi naamini sio wa Hongmeng kwani jamii niliotokea hakuna ubaguzi wa rangi na jini linao uwezo hata wa kuishi kwa mwonekano wa mnyama na likaheshimiwa kabisa na kuigia hata kwenye vikao vya wazee”Aliongea na kumfanya Edna kushangaa na kucheka.

“Rufi umenisaidia sana kwa kujibu baadhi ya maswali , lakini sidhani kama yameisha , kwasasa tutaishia hapa na kama nitahitaji msaada zaidi nitakutafuta , kuhusu usalama wako kwasababu upo Tanzania huna haja ya kuwa na wasiwasi nisipokupa ulinzi mimi , wapo wengine watakupa ulinzi”

“Unamaanisha nini wapo wengine?”Aliuliza Edna

“Kama Christen” Alijibu Roma kwa kumkonyeza na kumfanya Edna kuvuta mdomo na kisha alisimama kwani Bi Wema alishaanza kuita kwa ajili ya chakula cha mchana na alihisi njaa.

“Mom who is this aunt?”Lanlan aliuliza mara baada ya kumuona Rufi na Edna ilibidi amueleze kama ni mgeni na Lanlan alitingisha kichwa.

Roma alijikuta akitabasamu, kadri siku zinavyoenda Lanlan alizidi kuingia kwenye moyo wake na ukweli alikuwa akichangamsha nyumba mno alitamani kuwa na watoto zaidi ya mmoja.

Baada ya Rufi kuondoka Roma aliweza kufuata gari lake na kurudi nyumbani na ugomvi na mke wake uliisha, Edna hakuwa na kinyongo na Rufi tena , lakini alimpa onyo hakuna mahusiano kati yake na Roma na Rufi alikubali licha moyoni alitamani kuwa mpenzi wa Roma , penzi alilopewa na Roma lilishindwa kufutika kwenye akili yake.

Siku iliofuata Roma aliona sasa aharakishe swala la ndoa na mke wake , siku zilikuwa zimebaki chache mno kufikia mwezi aliomuahidi Edna ndoa.

Ni muda wa jioni Roma alipokea simu kutoka Visiwa vya wafu na mtu aliempigia alikuwa ni Ron.

“Ron is it ready?”Aliuliza Roma mara baada ya kusalimiana akimwambia kama tayari.

“Your Majesty Pluto , everything is ready , we may begine as soon as the following next month”

“Mfalme Pluto kila kitu kipo tayari tunaweza kuanza mapema mwezi unaofuata”Aliongea Rona na Roma aliangalia tarehe na kuona zimebaki siku chache sana , ilikuwa tarehe ishirini na mbili ya mwezi wa tatu kwa maana kwamba ni siku nane tu anapaswa kufunga ndoa na Edna.

Roma mara baada ya kuongea na Rona alienda hadi kwenye chmba cha Edna cha kujisomea na kumkuta akiwa anafanya kazi za kampuni.

“Vipi kuna nini mbona unaniangalia hivyo?” Aliuliza Edna.

“Maandalizi yashakamilika ndoa yetu ni mwanzoni mwa mwezi ujao”Aliongea Roma na kumfanya Edna kushangaa kidogo , lakini alijikuta akihisi aibu za kike na kutingisha kichwa kukubali huku akitabasamu.









SEHEMU YA 468.

Roma hakuwa na maandalizi makubwa na swala la kumuoa Edna kwa ndoa sio swala ambalo alifikiria sana , kwani sio kama walikuwa wachumba bali ni wanandoa tayari na kinachofanyika ni kama kuthibitisha ndoa yao mbele ya mashahidi tu.

Ndoa ilipangwa kufanyika tarehe kumi na nne ya mwezi wa nne tarkibani siku kumi na tano zinazofuatia.

Ni siku ya tano tokea Roma amwambie Edna tarehe ya ndoa , Edna alionekana kwenye mawazo. Licha ya kwamba alishaolewa na Roma , lakini ndoa yao ilikuwa ya kimkataba na haikuwa ya kimapenzi na inayokwenda kufanyika ilikuwa ya kimapenzi hivyo hisia zilikuwa zikimwambia kama ndio anakwenda kuyaishi sasa maisha ya ndoa rasmi mara baada ya kufunga ndoa na Roma.

Edna akiwa ofisini kwake akikamilisha taratibu za mwisho ili kuacha majukumu kwa Nasra kukaimu nafasi yake , alijikuta akiwa ni mwenye mawazo ya hapa na pale , kubwa zaidi ni swala la baba yake mzazi , kama mwanamke ambaye anaolewa alitamani angalau kusikia chochote kutoka kwa baba yake mzazi kwani ndio ndugu pekee aliebakia kwenye maisha yake , lakini tokea mara ya mwisho kumtumia ujumbe hakukuwa na majibu , the Protector alifahamu fika ni raisi Jeremy hisia hizo alikuwa na uhakika nazo na kama The Protector asingekuwa raisi Jeremy alijiambia basi angerudisha ujumbe aliotuma , kitendo cha kukaa kimya alijua kabisa The Protector ni raisi Jeremy.

Sasa kwa haraka haraka ni kama Edna alikuwa ashaishi maisha ya ukaribu na baba yake kwa zaidi ya miaka mitano tokea mama yake alipofariki , ijapokuwa raisi Jeremy hakujitambulisha kwa Edna , lakini msaada wake ulimgusa.

Edna akiwa ofisini kwake alikuwa amefungua barua pepe zilizotumwa na The Protector tokea alivyoanza kusimamia kampuni mpaka meseji ya mwisho na machozi yalianza kumdondoka , alianza kujishauri je amwambie kama anafunga ndoa au asimwambie.

Akiwa amekaa kwenye kiti chake cha kibosi akiwa na mawazo , mwishoe kabisa aliamua kuandika ujumbe wa meseji kwenda kwa The Protector kwa lugha ya kigereza. ‘Nafunga ndoa’ , ndio alivyoandika na kisha akazima tarakishi yake na siku hio hio aliamua kuitisha kikao na wafanyakazi kwamba ataenda likizo fupi ya miezi miwili hivyo madaraka ya kuongoza kampuni kumwachia Nasra.

Wakurugenzi wa bodi walishangazwa na Edna kuomba likizo lakini hakuwapa sababu maalumu kwanini anafanya hivyo , zaidi tu ya kuwaambia angekuwa anafanya maamuzi baadhi akiwa nje ya ofisi kwa kupitia Recho na Suzzane.

Ilikuwa lazima kuchukua likizo mapeka kwani Afande Kweka alimtaka Roma kufuata mila zao kwanza kabla ya kufunga ndoa rasmi na Edna.

Hivyo walipaswa kwenda Songea kijijini kwa Afande Kweka kwa ajili ya kufanya sherehe ya kimila na Edna kutambulishwa rasmi na kupewa baraka zote wakiwemo wanafamilia wote , lakini pia Afande Kweka alipanga siku hio kumtangaza Roma kama kiongozi wa ukoo moja kwa moja kurithi nafasi yake.

Afande Kweka alikuwa amekwisha kutangulia kijijini tayari , Blandina na Damasi wote walienda Songea kwa ajili ya maandalizi kwani familia nzima ya Afande Kweka ilipaswa kukusanyika kutoka pande zote za nchi na wale pia ambao walikuwa nje ya nchi.

Ulikuwa ni utamaduni kwa koo ya Afande Kweka kila mwanaume katika familia akitaka kufunga ndoa inaanza ya kimila kwanza na ndio ya kikanisa au imani nyingine ingefuatia , ukoo wao haukuwa ukilemea dini ya kikikristo wala uislamu na inasemekana mke wa Afande Kweka alikuwa muislamu na Afande Kweka mwenyewe alikuwa mkatoliki jina.

Hivyo Roma na Edna wakishafungishwa ndoa ya kitamaduni moja kwa moja wangeanza safari ya kuelekea visiwa vya wafu.

Moja ya watu ambao walikuwa na furaha kubwa sana ni Bi Wema , baada ya kupewa taarifa na Edna anaolewa rasmi na kuwa mke kwa kumpenda Roma, machozi yalimtoka na usiku alionekana akishikilia picha ya Raheli na Mariaum bibi yake Edna na kuziangalia kwa kutabasamu.

Alionyesha kutimiza misheni alioachiwa na watu hao kwenye picha , malezi ya Edna yalikuwa jukumu lake kubwa ambalo aliachiwa na Raheli lakini pia Bi Wema na alimjali sana Edna tokea vifo vya watu wake wa karibu na kuhakikisha sio mpweke kabisa.

Hata hivyo ilimfanya kujisikia vizuri na yale mawazo ya kupoteza mtoto yalipungua , hivyo alimuona Edna kama mtoto wake aliepoteza miaka mingi iliopita.

Bi Wema hakuelewa kabisa mtoto wake yupo karibu kuliko asivyokuwa akidhania .

Naam ilikuwa ni jioni siku ya ijumaa ndio muda ambao Edna alianza kupanga nguo zake kwenye pamoja na Za Lanlan , ilikuwa lazima kufanya hivyo kwani asingerudi kabisa Dar es salaam kwa maelezo ya Roma wangeunganisha kwenda Visiwa vya wafu kupitia uwanja wa ndege wa Songwe.

Upande wa Roma yeye alianza kuwaaga wachumba wake wote na kuwaeleza ukweli kwamba anaenda kufunga ndoa na Edna na kuwakaribisha kama kuna anaehitaji , lakini wote walikataa lakini walitamani sana kwenda na wao visiwa vya wafu na Roma hakuona hilo ni tatizo.

Aliwahidi baada ya ndoa yake na Edna angewapeleka , alichokifanya Roma ni kutaka kuwawekea mpaka kati yao na Edna kwamba mke wake atabakia kuwa Edna na hakuna mjadala.

Lakini hata hivyo Roma alijiambia kama Edna angekataa wasiende visiwa vya wafu basi asingeweza kupinga kwani hata hivyo alikuwa akienda kumtambulisha kama malkia kwa raia wake..

Siku iliofuata Edna , Roma na mtoto wao Lanlan walipanda kwenye Chopa ya kijeshi kuelekea Luhira Songea, ilikuwa ni safari ndefu ya gari ndio maana walichagua kupanda Helikopta iliotolewa na Afande Kweka.

Swala la kupanda chopa lilimfurahisha mno Lanlan, kwake ulikuwa uzoefu mpya na alifurahia.

Baada ya kufika Songea mjini walishushwa na kuchukuliwa na Range Rover Sport kuelekea Luhira , Edna alionyesha kuwa na wasiwasi mno kila alipokua akimwangalia Roma.

“Edna mbona una wasiwasi hivyo?”Aliongea Roma.

“Wasiwasi wangu ni juu yako”

“Mimi nina nini?”

“Vipi kama Denisi atakuwepo , vipi kuhusu baba yako mzazi Raisi Senga?”Aiongea Edna na Roma alishindwa kujibu lolote , alishasahau kama ana baba lakini mara baada ya kusikia kuhusu Raisi Senga alijikuta akifikiria.

Edna alikuwa amependeza kweli , alikuwa amevalia sketi ya kinidhamu ya Brand ya italia maarufu kama Botega Veneta , mkobwa wa Luis Vuiton na juu alikuwa amevalia blaza ya mikono mirefu iliomfunika mpaka shingo.

Lanlan mara baada ya kutoka kwenye Chopa moja kwa moja alisinzia kwenye mikono ya Roma.

Baada ya masaa muda mfupi tu gari iliweza kutoka kwenye njia iliokuwa ikielekea Ruhira na kukunja kushoto kuingia upande wa barabara ya vumbi ambayo pembeni yake kulikuwa na fensi ya michongoma , Roma alijikuta akitabasamu , ilionyesha kweli Afande Kweka huku alikuwa amejenga haswa kuliko ambavyo hajategemea kwani mbele zaidi kulikuwa na jumba kubwa likionekana.
 
SEHEMU YA 469.

Familia ya Afande Kweka ni moja ya familia ambazo zimejijenga sana kijeshi na hilo lilionyesha dhahiri.

Eneo lote la kuingia kwenye nyumba ya Afande Kweka palikuwa na walizi ambao wengi Roma alitambua ni wanajeshi wa nyota moja ambao walikuwa wameshiba kimazoezi haswa , mpaka Roma akafikia hatua ya kujiuliza mzee anaogopa nini mpaka kujiwekea ulinzi mkubwa namna hio , kwani uwepo wa Zenzhei kama mlinzi ilikuwa ni zaidi ya wanajeshi wote walioshikilia siraha.

Edna upande mwingine alijikuta akishangaa na kukosa urulivu , ijapokuwa alikwisha kwenda nyumbani kwa Mzee Kweka kujitambulisha na Roma miezi kadhaa iliopita , lakini awamu hii aliona utofauti mkubwa sana na ni kama ndio mara yake ya kwanza.

Unajua licha ya Roma kurudi nchini na kujitambulisha kwa babu yake pamoja na ndugu lakini hakupokelewa kimila , hivyo ujiio wake Songea ulikuwa ni kupokelewa kimila na kukaribishwa rasmi kwenye familia na tukio hilo linafanyika mbele ya wanafamilia wote.

Baada ya kuingia kwenye kijimsitu nyuma ya eneo hilo la Luhira gari yao ilisimama mbele ya geti kubwa ambalo lilifunguiwa kwa ndani na walinzi wawili na Roma kuwaangalia wote walikuwa ni wanajeshi wa vyeo vya kuruta.

“Huyu mzee anajifanya ndio raisi wa taifa hili?”Aliwaza Roma kwenye kichwa chake mara baada ya kutoka kwenye gari akiwa amembeba Lanlan.

Kilichomfanya kuwaza hivyo ni kutokana na ukubwa wa jumba hilo , ijapokuwa halikuwa na mwonekano kama ule wa kisasa kutokana na kujengwa zamani lakini mwonekano wake wa rangi nyeupe ulivutia lakini kubwa zaidi yalikuwa ni mazingira ya nje.

Eneo ndani ya ukuta lilikuwa kubwa mno ambalo lilikuwa na usafi wa hali ya juu ni kama vile alikuwa kwenye ikulu ndogo ya raisi.

Walipokewa na wahudumu waliokuwa nje huku mabegi yakitolewa nje kuingizwa ndani.

“Karibu sana Master Roma , Marshal alikuwa akisubiria kwa hamu ujio wenu”Aliongea mwanajeshi akimkaribisha Roma kwa saluti.

Roma alishangaa kuona bado babu yake anaitwa Marshal, aliona taifa la Tanzania lilikuwa likiwapa heshima sana hata wale wanajeshi waliostaafu.

Waliweza kuingia ndani eneo la sebuleni na kupokelewa na wahudumu watatu wakike waliowasalimia kwa heshima kwa kuinama mbele yao.

Edna alikuwa tajiri lakini hakuwa amezoea kabisa kunyenyekewa hivyo alionyesha kidogo kutojisikia vizuri kunyenyekewa na wahudumu.

“ My Boss wife mbona unaonyesha kuwa na wasiwasi au nikuchekeshe kidogo uwe vizuri”Aliuliza Roma akimwangalia Edna baada ya kuingia sebuleni ambayo bado ilionekana kutokuwa na watu wengi.

“Mh hili jumba ni kubwa na ni zuri , wahudumu pia wanaonyesha kuwa na mafunzo na hao wanajeshi ni kama wameandaliwa kwa ajili ya kutuigizia kuonyesha heshima”Aliongea Edna lakini Roma kabla hajajibu Blandina alijitokeza mbele yao kutokea mlango wa nuyuma.

“Jamani mmefika , niliwakumbukaje , nimemisi mjukuu wangu Lanlan kuliko kitu chochote”Aliongea huku akimsogelea Roma kumchukua Lanlan.

“Mimi hata sijakukummbuka kihiivyo”Aliongea Roma kwa utani.

“Wewe na utukutu wako , ndio maana unamfanya Edna kuonekana kuwa na wasiwasi , umemfanya nini?”Aliongea Blandina

“Mama hapana sina… “

“Usiwe na wasiwasi, hapa ni nyumbani kwenu sasa, hao wanajeshi unaowaona wapo wengi leo ni kwasababu kuna wageni pia kutoka jeshini wamefika”Aliongea Blandina na Roma alimwangalia mama yake kuona kama alikuwa na furaha na ilionyesha alikuwa hana tatizo lolote na lilimpa ahueni.

Baada ya Lanlan kuchukuliwa kwenda kulazwa Roma na Edna waliongozwa upande wa pili kuonana na Afande Kweka.

Afande Kweka alikuwa akiota moto huku akiwa amevalia sweta zito , ilionyesha eneo hilo lilikuwa maalumu kwa ajili ya kuota moto kwani lilikuwa na joto ambalo lilimfanya Edna kuhisi ahueni maana alikuwa akianza kuhisi ubaridi kwenye mwili wake, Zenzhei pia alikuwepo akiwa amesimama upande wa kulia.

“Baba washafika”Aliongea Blandina na kumfanya Afande Kweka kutingisha kichwa na kumwangalia Roma na Edna.

“Hatimae umerudi”Aliongea .

“Nimefika sijarudi”Alijibu Roma na kumfanya Afande kweka kutoa tabasamu la kifedhuli na kisha kumgeukia Edna.

“Edna hebu wewe niambie mmerudi au mmefika?”

“Tumerudi”Aijibu Edna

“Wife kulikoni kuungana na huyu mzee , tumekuja kutembelea asili yangu tu na hatujarudi kwani tulikuwa tumeenda wapi mpaka turudi?”

“Acha kuongea ujjinga na kujifanyisha mtukutu mbele ya babu yako”Aliongea Edna huku akimpiga Roma kofi la begani.

“Sawa mke wangu”Alijibu Roma.

“Hahaha…. Nilidhania unaendelea vizuri kwenye ndoa yako , ila hapa naona huna nguvu mbele ya mkeo”Aliongea Afande Kweka kwa utani huku akionyesha ishara ya kuketi.

……………………

Edna na Roma waliweza kukaa zaidi ya siku kumi ndani ya wilaya ya Songea , ilikuwa mara yake ya kwanza Edna kushiriki taratibu za kimila na alijifunza vitu vingi kwa siku zote alizokaa hapo , lakini pia aliweza kufahamina na wana ukoo wale ambao hakuwa akiwafahamu hata kujenga urafiki na baadhi yao.

Katika watu ambao aliweza kufahamiana nao na kuzoeana kwa haraka ni Eddy na mke wake Frola.

Eddy alikuwa ni raia wa Kenya na Flora ni raia wa Tanzania akiwa ni mjukuu pia wa Afande Kweka upande wa wakwe na ni moja ya wageni waliohudhuria sherehe za kimila, kilichomfanya Edna kufurahia kukutana na Eddy ni kutokana na kwamba Eddy alikuwa mfanyabiashara mkubwa ndani ya jiji la Nairobi .

Sasa kama ujuavyo watu wanaofanana kimtazamo wanapokutana huzoeana kwa haraka , basi ndio kilichotokea , Edna aliweza kuzoeana sana na Flora pamoja na mume wake Eddy na hata siku ambayo Eddy na Flora wanaaga kurudi Kenya walimlazimisha Edna baada ya kumaliza Honeymoon awatembelee Nairobi kwani atakuwa ameandaa zawadi kwa ajili yake , Edna alikubali na kutoa ahadi kwamba angefikana Romapamoja na Lanlan.

Sherehe ya kimila ilifana sana, Raisi Senga hakuhudhuria kwani alikuwa nchini Marekani kwenye mkutano wa umoja wa mataifa , kuhusu Denisi na yeye hakujitokeza kabisa na Roma alikuwa akitamaini kumuona tena ili amuue , lakini hakuwa amejitokeza na ilikuwa ahueni kwa Damasi pamoja na Blandina.

Tukio kubwa tu ambalo lilitokea ni kifo cha naibu waziri wa ujenzi ambaye alikuwa ameoa ndani ya familia ya Afande Kweka , kifo chake kilisababishwa na Roma baada ya kunyongwa na Roma mpaka umauti ulipomkuta mbele ya kadamnasi ya wana ukoo wote.

Naibu waziri alijitakia hata hivyo , haikueleweka alikuwa akifikiria nini kumpiga Roma hadharani na kumtukana tena mbele ya mke wake na hio yote ni mara baada ya Afande Kweka kumtangaza Roma kama mtu ambaye angeirithi nafasi yake, sasa huyo Naibu alikataa kwa kuweka pingamizi kwamba hawezi kumtambua Roma tofauti na Raisi Senga na kutaka kuhamasisha wengine, lakini mwisho wa siku aliweza kunyongwa.

Afande Kweka hakujali sana kuhusu kifo chake na alionyesha kama mtu ambaye alifurahishwa na jambo hilo kwani naibu waziri huo alionyesha pia kumtukana na kutokumheshimu kama kiongozi wa ukoo.

Inasemekana baba yake Afande Kweka hakuwa baba yake mzazi wa damu , bali Afande Kweka alikuwa amelelewa, sasa huyo naibu waziri aligusia hilo swala na kusema Roma na Afande Kweka hawana uhalali wa kurithishana uongozi wa ukoo ambao hauwahusu kwasababu Songea sio asili yao..

Ilikuwa siri ambayo iliwashangaza watu wengi na kutaka kujua kama alioyasema ni kweli lakini Afande Kweka alisema angelitolea swala hilo maelezo siku nyingine kwani huo sio muda wake.

Naam siku ya pili iliofuata Edna , Roma na Blandina walianza safari ya kuelekea visiwa vya wafu .

Afande Kweka alimzuia Edna asiongozane na Lanlan na kuwashauri wafanye hivyo mara baada ya ndoa, Edna hakupenda kutengana na Lanlan lakini mwishowe alikubali na kumuacha nyuma.

“Vipi kuhusu Bi Wema?”Aliuliza Edna kwa wasiwasi wakati walipokuwa kwenye gari wakielekea Songwe.

“Usijal Bi Wema atakuwa tayari ashafika muda huu”Aliongea Roma na kumfanya Edna kumwangalia Roma kwa shauku.

“Kwahio tunaelekea nchi gani?”Aliuliza na kumfanya hata Blandina kutaka kujua jibu maana licha ya kwamba alikuwa akimsindikiza mwanae kwa ajili ya harusi lakini hakuwa akielewa inaenda kufanyikia nchi gani.

“Nitawaambia tukishaingia kwenye ndege”Alijibu Roma

“Kwanini unanificha hata mimi mama yako , lazima nijue mwanangu anaenda kufanyia sherehe nchi gani”Aliongea Blandina lakini Roma aliishai kutabasamu na safari iliendelea.

Dakika chache mbele wote waliweza kuingia ndani ya uwanja wa kimataifa wa mkoa wa Songwe, shukrani kwa Dereva alitumia njia za mikato nyingi na kuwahi kufika , ilikuwa tayari ni alasili mchana wakati wanafika kiwanjani.

Na waliweza kupokelewa na wadada wawili wa kizungu waliovalia sare za uhudumu wa ndege, walikuwa warembo mno hasa pale walipompa heshima yake Roma kwa namna ya kutabasamu na kumfanya Edna amsogelee Roma karibu.

“Mbona kama nahisi kuna kinachoendelea.”Aliuliza Edna kwa utani maana aliona kila dalili wahudumu hao kumfahamu Roma.

“Hao ni wanajeshi , Wamevaa kama wahudumu wa ndege kwa ajili ya kurahisisha ulinzi”Aliongea Roma na kumfanya Edna kushangaa.

“Unamaanisha wanajeshi kitengo cha uhudumu wa ndege?”

“Hapana hao wapo kitengo kingine kabisa , labda naweza kusema ni Maninja ndio maana unaona ugumu wa kuwatambua kama wanajeshi”Aliongea Roma na kumfanya Edna kuchanganyikiwa na maelezo yake.

Kiwanjani hapo kulikuwa na ndege mbili , moja ndogo saizi ya ndege za Precision Air na nyingine ilikuwa kubwa kampuni ya Airbus, sasa Blandina na Edna walijuwa wanaenda kupanda ile ndogo lakini walijikuta wakitoa macho mara baada ya kuongozwa kwenye ile kubwa ambayo ilikuwa na jina la Arc Airline.

Roma alitambua mshituko wao na yeye ndio aliekuwa wa kwanza kutembea mpaka kwenye ngazi na kugeuka nyuma kuwaangalia wakiwa wamesimama.

“Mama mbona mnashangaaa na kusimama?” Aliongea na kauli yake ilimshitua Edna na kumsogelea Roma.

“Hii si Airbus A330?”Aliuliza Edna , alikuwa akizifahamu sana ndege kutokana na kwamba alishasafiri sana nje ya nchi, hivyo likija swala kuzitofautisha alikuwa vizuri kwanzia ndege za kampuni ya Boeng na Aribuss.

“Ndio, lakini kwanini upo kwenye mshangao , au kwasababu hatujaipamba , Babe tusingefanya hivyo kwani hatutoitumia mara kwa mara”Aliongea Roma kwa utani na wote waliingia taratibu huku wakipokelewa mlangoni na muhudumu.

Kilichowashangaza zaidi ni mara baada ya kuingia ndani, walitegemea kwamba wangekuta msururu wa siti za abiria kama walivyokuwa wakipanda ndege za kawaida lakini hii ilikuwa ni tofauti kabisa , eneo la ndani liligawanywa kwa vyumba na wao waliongoza mpaka sehemu iliokuwa kama sebule kwa mpangilio wake.

Usanifu wa ndani ulikuwa ni ule wa kifahari ukijumuisha samani za miti ya misandali, Jalidi za ngozi ya Elk na mapambo ya vito vya thamani, Chandelia za vioo ndio zilipangwa kwa mpangilio mnyoofu huku zikipitisha mwanga wa taa za kuvutia , chini ya sakafu kapeti nzito kutoka Irani maarufu kama Persian Carpet ilikuwa imetandazwa, kulikuwa na harufu ya marashi ya upekee sana,

Edna alikuwa tajiri lakini hakuwahi kupanda ndege yenye ufahari wa aina hio na alionekana kama mshamba tu na sio kwake tu hata kwa Blandina ilikuwa hivyo.

Unajua Blandina alikuwa akimuona Roma hana hela kumzidi Edna lna hata Roma alipoweka wazi swala la ndoa alitaka kuchangia , lakini Roma hakutaka mchango hata kidogo , safari yake hio ya kwenda kwenye harusi ilikuwa ya shauku kwake kwani Roma alimwambia ni baadhi ya maeneo ambayo yamejaza historia yake ya maisha ya nyuma.

Alishawahi kuwa mke wa raisi, kunyenyekewa alishazoea lakini kwa swala la ufahari wa hii ndege ulikuwa uzoefu mpya, aliishia kuwaza vitu vingi sana kwenye kichwa chake.

Roma baada ya kuketi kwenye sofa aliongea na wahudumu kwa lugha ambayo Edna hawakuielewa na ndani ya muda mfupi chakula na vinywaji mbalimbali vililetwa , Roma alikuwa na njaa maana hawakupata kula chochote.

“Mama jaribu hii , ni Vanila kutoka Ibiza naamini utaiona tamu”Aliongea Roma mara baaada ya wahudumu kuleta chupa za nyingi za bia na mvinyo, Blandina hakuwa akijua achague ipi kwani hakuwa mzoefu.

Blandina alichukua glass iliomiminiwa na kisa akanusa harufu yake na alimwangalia Roma kwa mshangao.

“Hii ni bia au Mvinyo ,mbona inanukia vizuri hivi”

“Ni kinywaji kama dawa na mara nyingi hutumika kuondoa uchomvu mwilini , ni bia ambayo haileweshi”Aliongea Roma na Blandina alijaribisha kunywa kidogo na kuonyesha kufurahia radha yake.

“Vipi kuhusu mimi?”Aliuliza Edna.

“Wewe chagua yoyote”Aliongea Roma huku akicheka

“Umemchagulia mama na mimi nataka unichagulie nichukue ipi hapa?”Aliongea na kumfanya Roma akune kichwa chake na kuanza kufikiria huku akiangalia chupa zilizokuwa kwenye trey.

“Hii infahamika kwa jina la ABSENTA kutoka Mediterranian lakini pia wengine wanaita Absinthe , ndio moja ya kinywaji changu pendwa , unaweza kujaribu”Aliongea Roma.

“Nishawahi kusikia kuhusu hii pombe na ipo kama spirit inakiwango kikubwa cha kulevya zaidi ya asilimia hamsini , nikinywa si nitalewa”

“Hii ni tofauti na toleo la zamani , Absinthe ya zamani ilifungiwa lakini hili nitoleo jipya na kiwango cha pombe ni kiduchu mno , ndani yake imewekewa asali hivyo huleta radha tamu kutokona na mchanganyiko wa Shamari”Aliongea Roma na kumfanya Edna kuguna , alikuwa hajawahi kunywa pombe hapo kabla zaidi ya mvinyo pekee, lakini aliamua kumuamini Roma na kunywa kidogo.

“Vipi radha yake unaionaje?”

“Ni tamu mno , ina radha nzuri”Aliongea Edna huku akianza kuangalia rangi yange ya kijani kwenye glasi na kufanya hata wahudumu kutabasamu , huku wengi wakionyesha wivu wa kuamani nafasi ya Edna ingekuwa ya kwao.

“Tuambie sasa ni wapi tunaelekea”Aliongea Edna.

“Kuwa mvumilivu mke wangu ni safari ndefu””

“Umbali wake ni wa kiasi gani?”Aliuliza Edna na Roma alimgeukia mhudumu na kumpa ishara ya kumsogelea na kisha akaanza kuongea kiitaliano

Edna na Blandina walishindwa kuelewa Roma anaongea nae nini lakini kwa mwonekano ni kama alikuwa akiuliza kitu..

“Amesema tunajiandaa kupaa lakini picha za satilaiti hazijawa tayari” Aliongea Roma kwa namna ya kutafsiri.

“Its fine”Aliongea Edna huku akimtingishia kichwa yule muhudumu huku akitabasamu.

“Rubani atatuonyesha picha za satilaiti punde baada ya kupaa na ndio nitawaeleza sehemu tunayo elekea”Aliongea Roma

Baada ya kufunga mikanda , hatimae dege hilo la Airbus iliruhusiwa kupaa na baada ya kutulia kwenye anga , picha za satilaiti zilionyweshwa kupitia LED skrini.

“Hapa ndio mwisho wa safari yetu”Aliongea Roma akionyesha kwa kidole.

“Hio si bahari ya Medetteranian?”

“Kwa usahihi zaidi ni Lonian Sea”alirekebisha Roma.

“Mbona sijawahi kusikia kuhusu Lonian Sea” Aliuliza Blandina.

“Bahari ya Lonian ni mwendelezo wa Ghuba ya bahari ya Mediteranian , Upande wa Kaskazini inaangaliana na bahari ya Adriatic ,upande wa kusini inafikia Cicily-Itally na upande wa mashariki ni Albania na Ugiriki , Kuna milipuko ya Volkano sana kutokana na misuguano wa sahani za kitetokniki chini ya uvungu wa bahari , tetemeko la Ardhi linatokea mara kwa mara kwenye hili eneo”

“Kwahio unasema unafanya harusi katikati ya bahari?”aliuliza Blandina kwa mshangao na kumfanya Roma atabasamu na kisha alionyesha baadhi ya viwingu viwingu vilivyoonekana katikati ya bahari kama vidoti doti.

“Nini hio?”

“Unavyoona hapo ni visiwa ninavyomiliki jina lake ni Islands of Dead(IOD) , ni visiwa ambavyo miaka iliopita vilikuwa chini ya serikali ya Uingereza kabla havijawa chini yangu ”

“Kwanini vinaitwa visiwa vya wafu?”

“Hilo utafahamu baadae”

“Kwahio unamaanisha kwamba hakuna mtu ambaye anaweza kwenda kwenye hivi visiwa kwasababu ni vya kwako?”Roma alitingisha kichwana kisha akaendelea kuelezea.

“Mwanzoni kabisa waliishi watu wa asili ya Australia(Aboriginal) kabla ya serikali ya Uingereza kuwaondoa , na kujenga magereza ya wahalifu wa daraja A, Wakati wa vita ya pili ya dunia wahalifu wote walifanikisha kutoroka kwenye magereza kutokana na wanajeshi wote waliokuwa wakilinda hilo eneo kwenda vitani , baada ya kuwa huru wakakosa usafiri wa kuwatoa kwenye visiwa hivyo na ndipo walichukua fursa ya kuviweka chini yao na kuanza maisha mapya na wakaamua kujiita The Lonians, waliishi hapo kwa amani sana na wakawa watu wasiokuwa chini ya serikali yoyote na jambo hili lilivutia zaidi baadhi ya wahalifu wengine ambao jamii haikuwataka na serikali kuwatafuta sana, kutokana na wengi wa watu waliokuwa wakitafuta hifadhi kuongezeka kwa kiwango kikubwa ikawa kama nchi sasa inayojitegemea, Sheria kubwa ya watu wote wanaoishi hapo lazima waachane na muunganiko wa maisha yao ya nyuma na kuanza upya kabisa , nikimaanisha hata ndugu zao ambao wapo katika nchi mbalimbali watengane nao na hata majina pia kuachana nayo na kuwa na majina mengine, ndio maana visiwa hivi vikaitwa vya wafu, kwa maana kwamba watu ambao wamekufa kwenye ulimwengu wa kawaida wanaanza maisha mapya ndani ya hivi visiwa”Aliongea Roma kwa kirefu.

Kwa lugha nyepesi ni kwamba asilimia kubwa ya wale wahalifu au magaidi wakubwa ambao washawahi kutikisa duniani , walienda kujificha kwenye hivi visiwa na hao ndio raia.

“Kwahio unamaanisha watu wanaoishi hayo maeneo ni wahalifu?”Aliuliza Blandina kwa wasiwasi.

“Mama unafikiria mbali , wale wafungwa walioishi hapo walishakufa na wengi wao waliohamia hapo ni kwa ajili ya kuishi kwa amani na wameachana na maisha yao ya zamani , siku yangu ya kwanza kwenda kwenye hivi visiwa ni bara baada ya kuisaidia familia ya kifalme kutoka Wales na ndio walionipatia hati miliki”Aliongea Roma.

Baada ya miaka kadhaa kupita visiwa vya wafu viliweza kupata kiongozi ambaye ni Hades wa Zamani na watu wote waliokuwa wakiishi ndani ya visiwa hivyo walimheshimu kwa kiasi kikubwa sana na yote hayo ni kutokana na ujasiri wake wa kuzuia serikali yoyote kutovitawala na kuendelea kubakia visiwa huru.

Lakini upande wa Ujingereza bado ilikuwa ikitaka kuvirudisha hivi visiwa kwasababu historia inaonyesha vilikuwa ni vya kwao , lakini walishindwa kuvipata kutokana na hila za Hades wa zamani.

Sasa Roma mara baada ya kukutana na Catherine na kumuokoa hatimae kumrejesha katika jumba la Kifalme na kuendeleza utawala wake , alipewa nafasi ya kuomba zawadi na ndipo alipotaka hatimiliki ya visiwa vyote vya wafu, lilikuwa ni ombi kichaa kwanni Serikali ya Uingereza ilitawala visiwa hivyo kimakaratasi tu lakini Roma auThirteen alikomalia kwamba serikali impatie hatimiliki za visiwa hivyo, kumbuka sasa wakati huo Visiwa hivyo vilikuwa chini ya Hades

Roma mara baada ya kupewa hatimiliki moja kwa moja alienda kwenye hivi visiwa kwa ajili ya kuviweka chini yake ,wakati huo alikuwa akiongoza kundi la Maninja lifahamikalo kwa jina la New Zero , akifahamika kama Ajent 13 na Seventeen akifahamika kwa jina la Agent 17 na alipanga kuweka makao yake hapo.

Sasa haikueleweka ilitokea nini lakini Hades wa zamani alimuachia Roma umiliki wa visiwa hivyo kama mrithi kwa hiari yake na Roma ndipo aliporithi jina la Hades kwanzia wakati huo , lakini hata hivyo mpaka Roma alipokuja kutambulika kama Hades ilikuwa ni zaidi ya mwaka tokea apewe hatimiliki ya umiliki wa visiwa hivyo na Serikali ya Uingereza , jambo moja kubwa ambalo lilimpa heshima kwa watu wa Visiwa vya wafu ni kwamba kitendo cha kupata hatimiliki kutoka Serikali ya Uingereza ni kama alileta uhuru na kwanzia hapo maisha yakawa ya amani na hakukuwana vita tena.

“Serikali ya Uingereza ilisaidia kuvitoa kwenye mfumo wa ramani ya kawaida ya dunia , ulinzi wake ni mkubwa kutokana na siiraha zenye teknolojia ya kipekee”

“Familia ya kifalme ulioisaidia ni Malkia Catherine mama yake Clark si ndio?”aliuliza Edna

“Upo sahihi na tokea visiwa hivi viwe chini yangu Catherine hutembelea mara kwa mara kwa ajili ya mapumziko, Babe unatakiwa kuelewa visiwa hivi vina mandhari nzuri ya kuvutia kutokana na milipuko ya Volkano na nina uhakika mtapenda mazingira yake na sitojali sana kama mtataka kuanzisha maisha moja kwa moja”

“Kuhusu hilo tutaongea muda mwingine, lakini sina mpango wa kuishi huko” aliongea Edna

“Roma kwahio unasema mataifa mengine duniani yalikuwa tayari kuondoa hivyo visiwa kutoka kwenye ramani kwa hiari yao?,naonekana kama sio uhaisia”Aliongea Blandina ambaye alikuwa akiyatafakari maelezo ya Roma na alionyesha kabisa kutokuamini.

“Mama je serikali ya Marekani inajali wapi kati ya New York na Visiwa vyangu?”

“Lazima wajali New Yok”

“Kwa jibu hilo basi sidhani watahitaji kuwa na mgogoro na mimi kisa tu namiliki visiwa, maana wangenibugudhi ningehakikisha hasara itakayopatikana ndani ya jiji la New York isingefidiwa Visiwa hivyo”Aliongea na kumfanya Blandina kukosa usemi , kwa maneno ya Roma ilionyesha Serikali ya Marekani ilikuwa ikimuogopa.

Kadri safari ilivyokuwa ikiendelea Edna aliawa sana na shauku ya kuona visiwa vyenyewe na watu wake, lakini pia upande mwingine alionyesha kukosa utulivu.

“Roma siamini kama tunaenda kufunga ndoa?”Aliongea Edna.

“Edna kwanini unaongea hivyo?”Aliongea Blandina mara baada ya kumuona hata Roma kushindwa kuielewa kauli ya Edna.

Roma yeye alichukulia kawaida , lakini upande wa Edna lilikuwa jambo kubwa kwake , yeye alihisi wakati alioishi na Roma ni wa uchumba na sio ndoa na sasa anakwenda kuolewa rasmi , upande wa Roma alihisi yeye ashaishi na Edna kwa muda mrefu na kinachowekda kufanyika ni kama kumbukumbu ya ndoa yao.

“Mama siamini kama hii siku imefika, kwenye maisha yangu sikuamini kama nitaolewa tena harusi kuwa sehemu ambayo sijawahi kufika , nahisi nipo ndotoni”

“Nikufinye uona kama upo kwenye ndoto au uhalisia?”

“Wewe usijaribu?”

“Haha… tunaonekana kama wanandoa wa kizamani tayari kuna haja gani kuwa na wasiwasi?”

“Wewe sisi sio wanandoa wa kizamani” aliongea Edna na kumfanya Blandina kuchekeshwa na maongezi yao lakini aliishia kutulia huku akionekana kuwaza, alishindwa kuelewa imekuwaje Roma akapotea kwenye ndege ya Malaysia Airline na kupona mpaka kuja kuwa mtu mzima na kumiliki visiwa , alikuwa na maswali mengi ambayo kwake majibu hakuwa nayo , lakini hakuwa na ujasiri pia wa kumuuliza Roma kile kilichotokea , alihisi huenda stori ya maisha yake ingekuwa ya maumivu sana na kumfanya kuishi kwa hatia maisha yake yote.

Baada ya masaa tisa kupita hatimae walikaribia mwisho wa safari yao baada ya Rubani kutangaza , Edna aliposhituka usingizini alipeleka macho nje kuangalia na alijikuta moyo wake ukienda mbio kwa mwonekano wa mandhari ya chini.











SEHEMU YA 470A.

“Hubby kwanini kuna visiwa vingi vidogo vidogo , Je Visiwa vya wafu ni kama Archipellago?”

Archiellago ni mkusanyiko wa visiwa vingi sana ni kama ilivyo kwa nchi ya Ugiriki.

“Unaweza kusema hivyo, ndio maana jina ni Visiwa na sio Kisiwa, harusi yetu itafanyikia kwenye kisiwa kikubwa zaidi , makao makuu”Aliongea Roma mara baada ya kuchungulia nje.

Baada ya muda kidogo walipewa taarifa kufunga mikanda kwani wanakaribia uwanja wa ndege kutua.

Kadri ndege hio ya Airbus ilivyokuwa ikishuka ndio mandhari yalivyozidi kuonekana , ni maji yaliozunguka pande zote na Edna aliweza kuoan baadhi ya fukwe za kupendeza mno zilizofanana kwa kiasi kikubwa na Santorini.

Aliweza pia kuona barabara za rami, nyumba pamoja na mashamba ,aliweza pia kuona baadhi ya meli za kivita za doria chini yake , lakini pia aliweza kuona baadhi ya Helicopta za doria upande wa pili zikiimarisha ulinzi.

Baada ya dakika ishirini kupita hatimae ndege iliweza kugusa njia ya kukimbilia , ilikuwa ni uwanja wa njia moja tu ambao umejengwa kwenye fukwe.

Baada ya wote kutoka waliweza kupokelewa na upepo pamoja na harufu ya bahari , hali ya hewa ilimfanya akili yake kuwa ya utulivu mkubwa pamoja na hisia zisizoelezeka , kwenye maisha yake hakuwahi kuona sehemu tulivu kama hio , alijikuta akigeuka geuka kama mtu asieamini.

Blandina na yeye alikuwa ni moja wapo ya watu ambao walikuwa kwenye mshangao mkubwa , walisahau kama kuna watu waliovalia suti wa kiwasubiria wakiwa wamepanga mstari kulia na kushoto kwa ajili ya kuwapokea.

“Ule ni mlina wa Volcano?”Aliuliza akiangalia upande wa kushoto kwake , akiangalia kisiwa ambacho kilikuwa na miti mingi lakini na kilele cha mlima wa Volcano.

“Ndio ni mlima wa Volcano , haujalipuka kwa zaidi ya miaka mia moja mpaka sasa , lakini ardhi inayozunguka mlima ina miti mizuri ya kijani kutokana na ardhi yake kuwa na rutuba ya utajiri wa madini

Edna alijikuta akikosa usemi kila kitu kilionekana kipya kwake , lakini kwa wakati mmoja kigeni machoni mwake.

Roma ndio aliekuwa wa kwanza kuongoza njia akiwa anatembea kwenye zulia la rangi nyekundu na kuanza kuwasalimia watu waliokuja kumpokea,moja wapo ya watu hao alikuwa Bi Wema.

Edna mara baada ya kumuona Bi Wema alishindwa kujizuia na kumkimbilia na kisha akamkumbatia , alionyesha kumkumbuka sana kwani hawakuonana kwa zaidi ya siku kumi na tano.

“Karibuni , watu wa hapa ni wakarimu sana sijawahi pata ona nimekutana pia na mswahili mwenzangu, lakini bado nahisi kuwa mgeni na kukosa utulivu”Aliongea Bi Wema.

Ni Blandina na Bi Wema pekee ambao wangeshuhudia harusi hio , kwani Sophia aligoma kuja na upande wa Familia ya ukoo wa Roma mhudhuriaji aalikuwa ni Ashley pekee ambaye alitoa taarifa.

Bi Wema alikuwa amevalia mavazi tofauti sana ambayo Edna hakuwahi kumuona nayo na Edna alimwangalia na kujikuta akitabasamu.

“Hili gauni kanitayarishia Ron , yule mwanaume wa kizungu pale ameniambia lingenifaa sana kwa ajili ya kuhudhuria harusi”Aliongea Bi Wema na kumfanya Edna na Bi Wema kumwangalia mwanaume wa kizungu ambaye ndio alieonekana kuongoza kundi la watu waliokuja kuwapokea.

“You Majestu Pluto , Welcome back to the IOD, Ron Von Konstantin at your service”

Kwa wale ambao mnatarajia kujiunga na gurpu letu la WAtsapp la VIP kwanzia wiki ijayo gharama itakuwa ni 5000…

ITAENDELEA SIKU KAMA YA LEO .

WATSAPP CONTACT -0687151346.
 
Mwisho wa story kumbe sio uhalisia bali ni Kila mtu anaota.

[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]
 
Maana story ilivyo ya moto toka mwanzo na hiki kipande Cha namna roma alivyopewa umiliki ya visiwa na jinsi alivyopewa uwezo wa hades nadhani kuna punje mbili tatu zimedondoka.

Ni story mojawapo ambayo haikuwahi kunipa arosto na mtunzi nimemkubari anatupia vipande vingi tena virefu mtu unasoma unatosheka.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…