NILIMDHANIA KAHABA KUMBE BIKRA
MTUNZI: SINGANOJR
Mono no aware.
SEHEMU YA 625.
Roma mara baada ya kumuona Edna ameacha kuuliza maswali na kushangaa jiwe la madini aliompatia alijikuta akivuta pumzi ya ahueni maana alijua kama Edna angeendelea kuongea mwisho wa siku angeshia kumwambia ukweli wote.
“Nitamuambia Ron kutafuta mhunzi wa kuaminika , hilo jiwe ni kubwa sana na linaweza kukatwa katikati nakutegnenezwa vito vya vingi na unaweza kuchagua kinachokufaa”Aliongea Roma.
“Hapana , sioni inaweza kuwa salama kumpa mtu mwingine , isitoshe nitatafuta huyo mhunzi mimi mwenyewe , kama utalitoa wewe wanawake wengine wataliona na wanaweza wakataka uwapatie na wao”Aliongea na kumfanya Roma misuli yake ya uso kucheza.
“Babe kwahio unasema utalifiicha ndani milele bila watu kuliona?”Aliuliza na Edna alitingisha kichwa lakini hata hivyo akionekana kuwa na furaha kupatiwa jiwe hilo na hakujali kama litakaa ndani ili mradi tu awe na uwezo wa kuliangalia pale anapohitaji pasipo ya kuwafanya wanawake wa Roma kuliona.
Roma hakuongea neno lolote lakini wakati huo aliona kwamba alikuwa na majiwe kama hayo mengi tu ambayo ameyachukua kwa ajili ya hao wanawake, haraka sana hakutaka kumuonyesha Edna kwani angeweza kuyachukua yote hivyo aliona huko mbeleni angetafuta namna ya kuwakabidhi kwa siri.
“Nadhani umeniletea mimi tu , lakini nataka nikuonye , isije ikatokea nikagundua umewapa na wanawake wengine”Aliongea Edna akiwa siriasi.
“Ah.. kwanini nifanye hivyo sasa!?”Roma alijikuta akikosa ujasiri , ijapokuwa aliongea hivyo lakini kijasho cha baridi kilianza kumtoka , alijiambia huyo mwanamke ni kama anayajua mawazo yake , alikuwa akipanga kuwapatia wanawake wengine mawe hayo kwa siri lakini Edna alishaona tayari mpango wake.
Kumuona Edna akiwa ameshikilia jiwe hilo kwa mkono mmoja uzuri wake ulizidi kuongezeka na alikuwa ni kama ua huku tabasamu lake likizidi kuyafanya mapigo yake ya moyo kudunda kwa kasi zaidi , Roma mwishowe alishindwa kabisa kuvumilia njaa yake na kiu aliokuwa nayo kwa muda mrefu na palepale alimsogelea na kumrushia katikati ya kitanda huku jiwe lake likidondokea kwenye mto.
“Ah…nini wewe,, kwanini unaharaka hivyo , hebu kaoge kwanza..”Aliongea kujitetea lakini Roma hakujali maneno yake na tayari alikuwa ashajichimbbia katikati ya kifua chake.
“Siwezi kusubiri zaidi ,,, nimevumilia kwa muda mrefu..”
“Lakini ni siku nyingi zimepita kwanini ushindwe dakika chache za kuoga..”
“Basi tukaoge wote”
“Mh.. usinifanye mjijnga , najua mpango wako ni kufanyia bafuni”
“Kama ni hivyo tulia basi wewe mwanamke … halafu hii sketi ni ya namna gani , vishikizo vyake viko wapi?”
Roma alipeleka mkono kila mahali bila ya kujua kama kweli alikuwa akitafuta vishikio au ndio alikuwa akitaka kuminya makalio , dakika hio hio mkono wake ulikuwa ushatumbukia sehemu nyingine kabis akitafuta vishikizo.
Edna hakuwa hata na nguvu ya kumzuia anachotaka kufanya katikati ya mapaja yake na alijiambia kuziba na mkono ni kujisumbua tu , hivyo aliacha afanye anavyotaka isitoshe kwa wakati huo na yeye moto ulikuwa ushawaka kwenye mwili wake.
Ikiwa ni jioni Blandina alimwagiza kijakazi kwenda kuwaamsha kwani Lanlan alikuwa akiwahitaji lakini kijakazi huyo alirudi akiwa na sura iliokuwa imepata moto kutokana na kile alichokisikia na Blandina kwa uzoefu wake aliweza kujua nini kinaendelea na aliishia kutabasamu.
Alijiambia ni vizuri hivyo kwasababu wanaweza kupata mtoto mapema , hivyo alimsaidia Lanlan kukamilisha homework yake kazi ambayo ilikuwa ni ya Edna.
Katika kitanda cha sita kwa sita Edna Edna alionekana akiwa amejilaza kichomvu huku nusu ya mwili wake ukiwa juu ya Roma , katika hali kama hio kichwa chake kilikuwa kikiwaza vitu vingi.
Baadhi ya wanawake pengine hawawezi kupata uzoefu wa hali ya juu wa utamu ambao anaupata kwenye maisha yao yote lakini kwake yeye mume wake alikuwa akimfikisha kunako bila shida yoyote, hio ndio faida kubwa ambayo alikuwa akiipata kwa mwanaume huyo ambaye amekaa kihuni huni.
Upande wa Roma alikuwa amejiachia m mkono mmoja alikuwa ameupitishia begani kwa Edna akimfanya amlalie kifuani huku yeye akiwa na sigara yake kubwa aliotoka nacho China akiivuta huku akipuliza moshi wake kwa raha zote , hakujali kabisa kuhusu mwili wake uliokuwa uchi na muda huo kiungo chake kilikuwa kimesimama kama mlingoti wa bendera ya raisi.
Edna alijikalia kivivu kwa nusu saa na nguvu zake angalau ziliweza kumrudia , mafunzo ya kijini yalikuwa yamemsaidia sana kuendana na spidi ya Roma la sivyo kwa mikiki yake angepoteza fahamu, aliishia kutabasamu na kisha akampiga Roma busu la shavuni na kusimama kisha akalisogelea kabati na kutoa kipande cha khanga na kujifunga.
“Honey , nina wazo kuhusu Sophia….”Aliongea Edna na kumfanya Roma ambaye alikuwa katika hali ya utulivu kumwangalia.
“Wazo gani?”
“Wiki moja zilizopita kampuni ya Vexto upande wa habari na burudani tulipitisha zaidi ya bilioni nne za kitanzania zinazowenda kuwekezwa kwenye udhalishaji wa filamu mjongeo ya hadithi ya ‘Shetani Rudisha akili zetu” kutoka kwa mwandishi Singanojr , huu ni uwekezaji mkubwa wa kwanza kufanyika nchini Tanzania na kampuni ya Vexto Media and Entertainment ndio wasimamizi wakuu , mpango wetu ni muvi hii kufanya vizuri na sio kufeli au kwenda kinyume chake..:”
“Hebu subiri , kama ni hivyo Sophia anahusiake na hio bajeti?”Aliongea Roma huku akikunja sura.
“Sophia anakwenda kuwa Sterling wa kike kwenye hii filamu, muvi yake iliopita iliweza kufanya vizuri sana kwenye mtandao wa Netflix na kuibua hisia za watu wengi kutoka mataifa mbali mbali hususani Ulaya na Amerika , nadhani pengine ni kutokana na kuwa ‘endorsed’ na Christen ndio maana, viongozi wa Vexto wamekuja hapa na kunishawishi uhusika wa Sophia na kweli nimekuja kugundua ukiwa Star huwezi kukwepa Skendo , hivyo tofauti na kukimbia ni kuzichukulia Skendo hizo kuzidi kujipandisha ki umaarufu, hivyo wengi wameshauri kwamba Sophia ashiriki katika filamu hii kwani ni ‘Action Movie’ na ile iliotoka chini ya Director Lassay Sophia alifanya vizuri sana hususani upande wa mapigano”Aliongea huku Edna akikaa pembeni ya kitanda akijarbu kumwelezea.
“Edna usinifanye mimi mumeo ni mjinga , Sophia alishatangaza kuachana na maswala ya usanii inawezekanaje filamu ikafanya vizuri , labda unionyeshe ushahidi au unataka tu Sophia kurudi katika maswala ya usaniii?”
“Ndio nataka arudi , huu ni uwekezaji mkubwa na kama Sophia atahusika na filamu ikafanya vizuri kampuni yangu itaimarika na kuwa kubwa zaidi , sio Tanzania tu bali mpaka nje ya mipaka ya Tanzania na hayo ndio yalikuwa malengo yangu tokea mwanzo katika kuianzisha”Aliongea .
Roma alivuta moshi wa sigara mwingi na kabla Edna hajashituka moshi wote ulipulizwa usoni mwake na kuishia kukohoa kwa nguvu.
“Kwanini unannifanyia hivi..?”aliongea huku akimfinya.
“Nimefanya hivi ili kuirudisha akili yako katika mstari , Edna kwanini unapenda hela namna hio , ile kampuni ni tawi tu na hata ikifirishika huwezi kupata hasara kubwa , kwanini unataka kumrudisha Sophia ili kuikuza kampuni yako ili ujipatie pesa , halafu sio kwamba hela zenyewe huna , kwanini unataka kumsumbua kama yeye mwenyewe alitangaza hataki maswala ya usanii?”
“Nini ? Kwahio wewe ndio unajifanyisha sasa hivi ndio unamjali sana , Bibi yangu alinifunza jinsi ya kuwa mfanyabiashara tokea nikiwa mdogo , kama nisipojali hela kama mfanyabiashara kuna kipi kingine napaswa kujali , je napaswa kujali wanawake kama wewe , mimi sina njaa ya hela lakini vipi kuhusu wafanyakazi wangu , vipi kuhusu timu ya udhalishaji wa hio filamu , na wenyewe wanafamilia na ndoto za kukamilisha na walifanya kazi kubwa kumpaisha Sophia kimuziki lakini akaamua tu kuachana na usanii na kukimbia kwenda kujificha , kampuni sasa hivi haifanyi vizuri je unadhani ni sawa , sio kama nataka kumlazimisha kufanya kazi , ninachoatka ni yeye kurudi na kufanya kitu anachokipenda mbele ya kila mtu”
Roma aliona ni kweli watu wengi walifanya kazi kubwa kuhakikisha Sophia anaupata umaarufu na kupitia yeye wengine waliweza kupata ujira wao lakini akaacha na kufanya kampuni kuzorota na kuwapa watu mzigo wa kuirudisha katika uimara wake.
“Una uhakika na unachotaka kufanya , sitaki akawe topiki ya kila mmoja kama ilivyotokea , yule baba yake sio mtu mzuri sana jambo baya linapomkuta binti yake” Aliongea lakni Edna alimwangalia Roma kwa jicho la pembeni.
“Kuna kitu kinachoendelea kati yenu sio ndio na unanificha , kwanini hutaki akirudi?”
“Hamna kinachoendelea , naongea kama shemeji yake”
“Naamini hujawehuka na kumgusa na Sophia , itakufanya uonekane mnyama”
Maneno hayo yalimfanya Roma kuingiwa na majuto , alikuwa tayari ni zaidi ya mnyama , alijikatia tamaa yeye mwenyewe na tabia yake lakini hakuwa na la kufanya, Sophia alikuwa amekufa na kuoza juu yake , anaweza kuwa mpole lakini alikuwa siriasi kuhusu hisia zake.
Roma hakuwa akitaka Sophia arudi kwenye usanii kwani ingepelekea mwisho wa siku kugundulika alikuwa aki’dat’e nae , sasa alijiuliza atawezaje kuzuia swala hilo bila ya kuibua mashaka.
“Vipi simu ya Sophia inafanya kazi?”
“Nadhani itakuwa imezimwa”
“Kama ni hivyo basi nitamtafuta mama yake , nina namba yake , nitamweleza mpango wangu na nadhani lazima anikubalie”Aliongea Edna huku akisimama na kuisogelea simu yake.
“Sio lazima kuwa na haraka hivyo , isitoshe wewe sio CEO tena hio kazi anaweza kufanya mtu mwingine”
“Najua lakini Ernest hawezi kulifanyia kazi hili vizuri , hivyo napaswa kuhusika, kuna siku mbili tu ambazo zimewekwa kwa ajili ya kuchagua wahusika hivyo lazima nimshawishi Sophia ndani ya siku hizo”Aliongea na kumfanya Roma kufikiria kitu kingine cha kukwamisha mpango huo na palepale macho yake yalichanua.
“Ah .. Edna mke wangu hatuwezi kufanya hivyo kuna tatizo?”
“Tatizo gani tena?”
“Kumbuka nilikuambia Sophia yupo kwenye levo ya Nafsi kwa msaada wa Aoiline , lazima atapaswa kwenda ulimwengu wa kijini kama sheria inavyomtaka, atawezaje kuwa msainii?”Aliuliza na kumfanya Edna kufikiria kidogo na kisha alitoa tabasamu la kupata njia.
“Kwanini tusifanye hivi , nimesikia kikosi cha wachawi ndani ya Tanzania kimeunda ushirikiano wa maswala ya kijeshi na kikosi cha wachawi kutoka China ambacho ndio kina muunganiko mkubwa na Hongmeng , kwanini usiongee na Afande Tobwe akajaribu kufanya mawasiliano , isitoshe Sophia ni msanii mkubwa tu na kama mara ya mwisho uliweza kumhonga yule mjumbe wao na akakubali basi nadhani na la Sophia linawezekana ,isitoshe yupo hata Omari Tozo ambaye yupo levo ya nafsi na yupo uraiani”
“Unadhani njia hio itafanya kazi?”
“Naamini itafanya kazi, tunaweza kuwapa rushwa hata ya vidonge wakati watakapotaka kumchukua Sophia”Aliongea na kumfanya Roma ashindwe kuongea chochote , mpango wake aliona unaweza kufanya kazi vizuri na aliona kama ataendelea kukwamisha mpango wa Sophia kurudi basi inweza kuibua mashaka kwa mke wake.
Roma baada ya kuona hakuwa na chaguo lingine ilibidi awasiliane na Afande Tobwe na kumuelezea mpango wake kama anaweza kuwaungaisha na wajumbe wa Hongmeng wanaoishi duniani ili Sophia sheria isimguse na Afande Tobwe licha ya kutokuwa na uhakika lakini alisema atajitahidi.
Roma hakuacha kuuliza kuhusu habari za Edna kuua wanajeshi pamoja na wachina waliokuwa katika levo ya nusu mzunguko lakini upande wa Afande Tobwe mwenyewe hakuuwa na maelezo ya kutosha juu ya tukio hilo na hata uchunguzi ambao wamefanya haukuleta mwanga wa aina yoyote.
Baada ya Edna kutoka akimuacha Roma mwenyewe chumbani , Roma mawazo yake hayakuacha kumuwazia Aoiline juu ya kilichotokea baada ya yeye kuondoka.
Baada ya kuona hatoweza kuwa na majibu hata kama akiwaza aliachana na mawazo hayo na kuanza kuwazia juu ya uwezo wake wa kijini ambao hakuwa na uwezo wa kuutumia.
Alifikira namna ya kufanya na katika kuwaza kwake aliona mtu pekee ambaye anaweza kumshirikisha katika swla hilo ni Profesa Clark.
Hakutaka kupoteza muda palepale alitafuta simu yake na kisha akaitafuta namba ya Clark na kuipiga na ndani ya dakika chache tu iliweza kupoktelewa.
“My Dear Roma ramoni , is it reallly you? Are you really back ?”Aliuliza Clarka na kumfanya Roma kushangaa kwani alijua jambo la yeye kupotea lilikuwa siri kama alivyoelezewa na Afande Kweka.
SEHEMU YA 626.
“Clark ulikuwa unajua nilipotea?”Aliuliza Roma akiwa amekunja ndita kidogo akionyesha mshangao wake.
“Bila shaka , nilikuwa nikikufikiria sana lakini nipo huku mbali na sikujua ni wapi ulipo”Aliogea na kumfanya Roma kutabasamu , alijiambia siku zote ilileta raha pale unapojua kuna mtu anakujali.
“Clark vipi lakini kuhusu maendeleo ya mafunzo yako?”
“Naendelea taratibu sana , bado tu nipo kwenye levo ya mwanzo mwa nusu mzunguko, nimejiingiza katika mafunzo ya Kung Fu ili kupanda kwa haraka na kufanya viungo vyangu kufanya kazi vizuri, lakini niseme tokea nimeanza kujifunza kuna vitu nashindwa kuvielewa kisayansi”Aliongea na kumfanya Roma kucheka.
“Hebu kwanza tuachane na hayo , nina tatizo kwasasa na nahitaji unisaidie kunifanyia uchunguzi wa kiafya”
“Una tatizo!! , unapitia tena mavumivu ya kichwa?”Aliuliza Clark akiwa na sauti ya wasiwasi .
“Sio maumivu ya kichwa ni kitu kingine tofauti na hicho , kwasasa siwezi kutumia uwezo wangu wa kijini..”aliongea Roma huku akimwelezea kile ambacho kimetokea mwanzo hadi mwisho na Clark upande wa pili alionekana kusikiliza kwa umakini.
“Kama ni hivyo basi nadhani haina haja ya kusafiri mpaka huku Uingereza , nitakuja huko huko kujaribu kuangalia tatizo lako nikichukulia kama nafasi ya mapumziko , pia inaweza kupunguza macho ya wengi “Aliongea na Roma alijikuta akiguswa na maneno yake , kwa namna ambavyo alikuwa akiongea ni kama tatizo lake lilikuwa dogo lakini upande wake yeye aliliona ni kubwa lakini hata hivyo alimkubalia na kupanga wakutane Tanzania.
Upande mwigine Roma alikuwa na wasiwasi kwani yeye na Clark walikuwa ni wapenzi rasmi tokea siku ambayo alimuokoa , hivyo aliomba Edna asije akagundua hilo.
Ukweli ni kwamba Roma alikuwa na wasiwasi kwani mbele yake ana mizigo mitatu ya kumwambia Edna ambayo hakuwa na uhakika kama angeweza kuchukuliaje.
Edna alipaswa kujua kuhusu Lanlan , wakati huo huo Roma alikuwa ashafanya kosa na Magdalena mpaka kulala nae , bado yupo Sophia na Clark , wote alishaanzisha mahusiano nao na Edna hakuwa na uelewa wa maswala hayo , hivyo moja kwa moja ni kwamba uendelevu wa mambo hayo ni kama bomu ambalo linahesabu dakika kurudi nyuma na siku yoyote lingeweza kulipuka huku mwenyewe aishindwa kujua ni madhara ya aina gani ambayo yanaweza kutokea.
Wakati Roma akifikiria makosa yake ambayo yalikuwa nje ya uwezo wake kuyaeupuka palepale aliwakumbuka Rose na Magdalena ambao walikuwa katika visiwa vya bahari ya Mediterranian na ilikuwa ni muda mrefu hajawatafuta kujua maendeleo yao.
Roma palepale na wazo lingine liliibuka katika kichwa chake na kujiuliza kama Sophia anaweza kusamehewa na kuendelea kubakia uraini licha ya kuwa katika levo ya Nafsi , je na Magdalena anaweza kusamehewa, isitoshe Magdalena alikuwa katika mfumo wa kijeshi.
Roma baada ya kuwaza kwa muda mfupi kidogo aliamua kutafuta namba ya Magdalena na kumpigia na ilipokelewa kwa shangwe zote upande wa pili , kwani ilikuwa ni taarifa nzuri kwao kama Roma ameweza kurudi salama.
Roma alimpamba pamba na maneno ya hapa na pale na baada ya hapo alimwelezea swala la yeye pia kuruhusiwa kuishi kawaida licha ya kuwa katika levo ya Nafsi.
“Roma umeshashau kama Mzee Tobwe ni baba yangu? , alishaniuliza pia hilo kabla yako na kuniambia anaweza kutumia koneksheni zake niendelee kubakishwa uraiani”
“Sasa kwanini hukuniambia kuhusu hilo au ilikuwaje?”
“Sikutaka kumpa baba mzigo mkubwa , ulishasema ni sheria ambazo zimeweka kwa ajili ya kuimarisha usalama wa dunia hivyo sikutaka baba avunje sheria kwa ajili yangu , isitoshe sio kwamba ni kuhusu mimi tu kuna Rose na yeye, kwasasa nina furaha mazingira ya huku ni mazuri sana na ya amani pamoja na watu wake kuwa wakarimu , sina haja ya kuomba na mimi kuruhusiwa”
“Inaonekana hamna mpango tena wa kutaka kuishi karibu na mimi , wewe na Rose?”Aliuliza Roma.
“Sisi hatuna shida , tunaweza kuishi popote , tunaweza kurudi pia kama Edna hana shida”Aliongea Magdalena akijaribu kutania na kumfanya roma kucheka kivivu.
“Okey basi hakuna shida , nilidhani hamna furaha kuishi huko mbali na familia ila kama mko sawa basi hakuna shida , mpe simu na Rose niongee nae, nijue ana mishe gani siku hizi?”
“Rose hayupo hapa , anavua samaki anataka mchana wa leo kula chakula cha baharini tu , Mr Ron alituletea wapishi lakini Rose kawakataa na kusema atapika mwenyewe”Aliongea na maneno yake yalimfanya Roma kuona kweli warembo hao walikuwa wakifurahia maisha maana walionekana kuzoea mazingira tayari.
Upande huo mwingine wakati Roma akiongea na Magdalena , Rose alikuwa ameakaa juu ya jiwe kubwa lililotokezea majini huku akiwa amevalia miwani ya jua.
Alikuwa amevalia mavazi ya fukwe , mtindo unaofahamika kwa jina la Hawaian styled Bikini , mtindo ambao ulifanya umbo lake lote kuonekana na kuzidi kuvutia.
Dakika hio hio akiwa bize kusubiria ndoano yake kunasa samaki , alitokea Magdalena nyuma yake akiwa ameshikilia simu.
“Roma anataka kuongea na wewe”Aliongea Magdalena lakini Rose hakuonyesha mshangao zaidi ya kuweka umakini wake kwenye ndoano.
“Amerudi , amekuambia yupo salama?”
“Ndio yupo salama , vipi hutaki kuongea nae mwenyewe”
“Vizuri kama yupo salama .. subiri ,, Ah Magdalena angalia ndoano imekamata , Samaki mkubwa jamani”Aliongea huku akianza kuvuta kwa kuzungusha.
Rose hakuwa mtu ambaye alikuwa akifanya matembezi ya kusafiri , pengine ndio maana kila kitu kilichokuwa kwenye kisiwa hicho kilimshawishi kukifanya , alikuwa na ratiba zake maalumu kuna siku alikuwa akizama chini ya maji kuangalia viumbe hai , siku nyingine alizama msituni kuwinda , siku nyingine ndio kama hivyo alikuwa akivua samaki.
Alikuwa na mambo mengi ya kufanya lakini kwa bahati mbaya ni kwamba uwepo wao kisiwani hapo sio kwa ajili tu ya kustarehe .
Roma hakutaka kuwasumbua sana baada ya kuona wanafurahia maisha hivyo alikata simu na kuwaambia atakuja muda si mrefu kuwatembelea.
Siku iliofuata Roma mpango wake ni kurudi Dar es salaam akiwaacha Edna na Lanlan, alikuwa akitaka kurudi kwa ajili ya kumhoji Qiang Xi kwanini alimuweka gizani licha ya kupewa maagizo na Master Chi.
Roma mara baada ya kuaga wakati wa chakula cha usiku wengine wote hawakuwa na tatizo lakini kwa Edna alijua tu lazima atakuwa amewakumbuka wanawake wake waliopo Dar es salaam lakini hata hivyo hakuwa na muda wa kujali kile anachokwenda kufanya.
******
Wakati mengi na mengi yakiendelea katika maisha ya Roma ya kila siku , upande mwingine nchini Rwanda katika makazi ya Raisi Jeremy alionekana Master 4 akiwa ameketi kwenye Sofa huku akiwa ameshikilia kishikwambi cha kampuni ya Sumsung akipangusa kutoka kulia kwenda kushoto.
Inawezekana kabisa alikuwa ni jini kutoka miliki ya Panasi lakini haikumaanisha kwamba maisha yake yalikuwa tofauti sana na ya binadamu wa kawaida , kwa jinsi tu alivyokuwa akionekana kwa mtu wa kawaida hawezi kugundua kama sio mtu wa kawaida.
“Jeremy hizi ndio taarifa pekee ulizopata kuhusu Roma Ramoni au kuna zingine?”Aliliza .
Raisi Jeremy wakati huo alikuwa ameketi pembenii akimwangalia Master 4 aliekuwa akipekua taarifa alizompatia , ambazo zilikuwa katika mfumo wa kidigitali.
“Ndio Master 4 , ukiachana na taarifa nyingine za international underground organisation”aliongea na kumfanya Master 4 kuishia kuguna.
“Huyu Roma Ramoni ni mtu hatari sana , ndio kwanza yupo kwenye miaka yake ya ishirini kwenda therathini lakini ana mafanikio makubwa namna hii katika mataifa ya Ulaya na Amerika”
“Hakika , ni ngumu sana kushindana nae akiwa katika mataifa yaliondelea tofauti na akiwa huku Afrika ya mashariki , kila serikali kubwa duniani ina wasiwasi nae kutokana na koneksheni zake kuanzia kwenye jeshi na makampuni ya kutengeneza siraha , ni rahisi kusema kwamba kwasasa ndio mfalme wa underwold , bila kusahau pia anamiliki eneo kubwa ambalo amepatiwa hati ya umiliki na serikali ya Uingereza katika bahari ya Mediterranian , ni muunganiko wa visiwa ambavyo vinaitwa Visiwa vya wafu na ndio makao yake makuu na shughuli zake zote zinafanyikia hapo , wahalifu wakubwa walioamua kuachana na maisha yao ya nyuma hutafuta makazi ndani ya visiwa hivyo , ni kwa bahati mbaya kwamba hatuna uwezo wa kupata taarifa uelekeo wa eneo hilo kwani limetolewa katika mfumo wa ramani ya dunia na hata satilaiti zinashindwa kupokea taarifa katika hilo eneo”
“Mh.. hakika ni mtu hatari , ndio maana ni mtu wa majigambo sana , ni kwa bahati mbaya mtu kama huyu hawezi kufanya kazi na sisi ..”Aliongea huku akiendelea kukagua taarifa hizo kupitia Kishikwambi.
“Uwezo wake wa kijini ni mkubwa kiasi cha kufikirika , uongozi wa miliki umeniagiza kuipata mbinu yake ya mafunzo na kumfanya kuwa mmoja wetu lakini naona kabisa misheni hii haiwezi kuwa nyepesi , labda tuweze kupata udhaifu wake”Aliongea.
Wakati huo raisi Jeremy alionekana kuna kitu ambacho alikuwa akitaka kuongea lakini alikuwa akisita sita.
“Master 4 ile siku ya tatu yake baada ya mapambano hapa Rwanda Namba moja alinitafuta kwa ajili ya kikao”
“Namba moja alikutafuta yeye mwenyewe kwa ajili ya kikao?”Aliuliza kwa mshangao
“Ndio , ni muda mrefu sana tokea alivyofanya hivyo”
“Aliongea nini?”aliuliza Master 4 huku akikunja sura.
“Alisema tunavuka mpaka wa kisheria uliowekwa , watu wengi mnatoka katika ulimwengu wa kijini na kusumbua raia”
“Tokea kuundwa kwa umoja wa koo zote za kijini na Namba moja kuwa kiongozi wetu haijawahi kutokea akaingilia katika maswala yetu , sikutegemea awamu hii angezungumzia kuhusu hili”Aliongea Master 4 huku akionyesha wasiwas.
“Master 4 kwani anatisha sana mbona anaonekana wa kawaida?”
“Nakutahadharisha Jeremy , kama kweli Namba moja amesema tumevuka mipaka basi lazima atakuwa anatuchunguza kwa kila tunachofanya , mtu kama yule hawezi kukuita kutaka kuongea na wewe hivi hivi , jaribu kutumia akili yako kufikiria kuhusu hili , je kwanini haijawahi kutokea akabadilishwa na kuendelea kuishi maisha ya kawaida licha ya mambo mengi kutokea kwa zaidi ya miongo ?”Aliuliza na palepale alimfaya Raisi Jeremy kujikuta katika hali ya wasiwasi.
“Ila usiwe na wasiwasi , nadhani anajaribu kuwa makini tu na sheria , wewe bado ni kiongozi wa ukoo wetu katika ulimwengu wa kawaida, kama ungekuwa hufai basi ungeshaondolewa muda mrefu”Aliongea akijaribu kumtoa Jeremy wasiwasi na kisha akaendelea kupitia faili la Roma ambalo limesheheni kila mtu ambaye alikuwa na mahusiano nae.
Master 4 mara baada ya kuendelea kupitia kurasa za maisha ya Roma nchini Tanzania hususani wanawake aliokuwa nao katika mahusiano alijikuta akisimama kwenye picha ya msichana mdogo mweupe.
“Huyu msichana na yeye ni sehemu ya wanawake zake?”Aliuliza huku akimsogezea Jeremy kile kishikwambi.
“Ndio , jina lake anaitwa Rufi, kwa taarifa ambazo tunazo mama yake ni Wema Sufiani kijakazi wa muda mrefu katika familia ya Adebayo na ndio amemzaa huyu binti na mchina mmoja ambaye alikuwa ni machinga anaefahamika kwa jina la Kunlun na baada ya kuzaliwa kwa Rufi alipotea nae.
“Huyo msichana inasemekana alikutana na Roma nchini Marekani na kuanzia hapo ndio uhusiano wao ulipoanzia mpaka ilipoweza kufahamika ni mtoto wa Wema ,kwasasa anaishi na mama yake jijini Dar es ssalaam”Aliongea.
“Mozheng my friend .. hahaha… Rufi!! ni yeye namkumbika ,, hahaha.. inavutia , inavutia , Roma katoa wapi huu ujasiri kuwa na mahusiano na huyu msichana”Aliongea Master 4 alionekana kumfahamu Rufi na baba yake.
“Master 4 kuna kitu kingine kinachohusiana na huyo msichana?”
“Mh ,, hakuna kitu kikubwa zaidi kuhusu yeye lakini naweza kusema ni hazina kwa watengenezaji wa vidonge ,huwezi kuelewa kuhusu hili hata nikikuelezea , tunapaswa kutoa taarifa ya swala hili kwa wahusika wanaomtafuta ,… Roma unaweza ukawa mjanja na kujitosheleza lakini itafikia wakati utahitaji msaada wetu”Aliongea huku akitoa cheko kubwa la ushindi mara baada ya kupata taarifa muhimu ya aina hio.
******
Saa moja moja ndio muda ambao Roma aliweza kufika Dar , alikuwa amechelewa kufika kwasababu alikuwa amechelewa kutoka.
Roma alilaani kitendo chake cha kutoweza kutumia nguvu za kijini kwani pengine kwa muda aliotoka Iringa angeweza kufika Dar ndani ya dakika tu lakini kwa bahati mbaya uwezo huo hakuwa nao na kumbidi kuendesha gari umbali mrefu.
Saa moja na nusu ndio muda ambao aliweza kufika nje ya geti la nyumba ya Dorisi , mazingira yalikuwa yametulia na alitegemea iwe hivyo kwani Dorisi alikuwa akiishi peke yake tokea kuondoka kwa Rose na njia nzima alikuwa akimfikiria , ilikuwa kheri kwa Nasra ambaye Najma alikuwa ni rafiki yake hivyo hakuwa mpweke lakini Dorisi hakuwa na ndugu.
Roma mara baada ya kujifikiria aliona haina haja ya kugonga mlango zaidi ya kuruka ukuta na kwenda kutua ndani kwa ustadi wa hali ya juu.
Baada ya kukagua mazingira, taa za ndani zilikuwa zimewashwa na ilimwambia Dorisi alikuwa yupo hivyo palepale alitembea kitahadhari na kuingia ndani.
Baada ya kufungua mlango wa Sebuleni hakukuwa na ishara ya uwepo wa mtu na moja kwa moja alipandisha ngazi mpaka juu kwenye chumba chake na mara baada ya kufika nje ya mlango aliweza kusikia bomba la maji ya bafuni likitiririsha maji na kujiambia Dorisi muda huu atakuwa ndio anaoga.
Alitoa tabasamu na kisha akashika kitasa na kusukuma mlango taratibu na kuufungua na kitu cha kwanza alichoweza kuona ni nguo za ndani ambazo zilionekana kutoka kuvaliwa zikiwa zimetupwa ovyo juu ya kitanda na hapo hapo aliweza kujiambia hisia zake zipo sawa , Dorisi alikuwa akioga.
Roma macho yake yalivutiwa na nguo hizo na kutoa tabasamu la kifedhuli na kusogea kuelekea ndani ili mradi kuziangalia , lakini ile anapiga hatua ya kwanza na ya pili alijikuta akiguswa na kitu cha baridi kwenye kisogo chake, lakini haikuwa hivyo tu palepale mkono wa kulia wa mtu ambaye amemuwekea siraha kichwani alileta kisu usawa wa shingo na Roma kwa ustadi wa hali ya juu aliruka na kukwepa na kugeuka kwa wakati mmoja na kumshika adui yake mikono.
“Dorisi…!!!”
Roma alijikuta akishangaa mara baada ya kugundua aliekuwa akimshambulia ni Dorisi.
“Hubby ni wewe …!!”
Mapigo ya Dorisi yalikuwa juu juu na alijikuta akiwa na afadhali mara baada ya kugundua ni Roma.
Roma alishangaa kwani Dorisi muda huo alikuwa amevalia suti yake na ilikuwa ni dhahiri ndio kwanza anarudi tokea kazini.
“Babe Dorisi nashindwa kuamini nimeweza kuingia katika mtego ulioniwekea .. haha , umejifunzia wapi haya?”
“Kwaninni hukupiga simu na umekuja kimya kimya , nilijua ni jambazi ndio maana , hebu niachie mikono yangu unaniumiza”Aliongea Dorisi na Roma palepale alijua ni kweli alikuwa ameshikilia kwa nguvu mikono yake yenye siraha.
“Hii mbinu yako ni ya hatari , kama kweli angekuwa ni jambazi basi ungekuwa umemmaliza”
“Hehe.. sikuwa na jinsi , ukiishi mwenyewe unajikuta unatafuta namna ya kujilinda , nimeweza kujifunza hivi kupitia filamu”Aliongea huku akisogea na kwenda kukaa kitandani na kumfanya Roma kumwagalia kwa tabasamu.
Hakuwa amemuona mrembo huyo kwa muda mrefu na aliridhishwa na maendeleo yake kwani alionekana muda wowote angeweza kufika mwishoni mwa levo ya mzunguko kamili.
“Hii mbinu yako imenifurahisha sana Babe Dorisi nadhani tuendelee nayo hivi hivi , mimi nitakuwa kaka jambazi na wewe ni mwanamke unaetoka kazini na kuvamiwa na mimi kaka jambazi na sasa anataka kukubaka”Aliongea Roma na kumfanya Dorisi kuachia cheko huku akivuta mdomo na kumwangalia kwa jicho la pembeni.
“Sitaki kusikia huo ushenzi wako mimi…”
“Hehe leo tutaona , mimi jambazi ndio naanza mambo yangu hivyo”Aliongea Roma huku akimvamia Rose alieanza kujifanyisha analeta vurugu.
Ijapokuwa maneno yake hayakuendana na umri wake lakini ukweli yalimfurahisha Dorisi , inasemekana mtu akiwa mbele ya mpenzi wake anakuwa mtoto na ndio alichokiona Dorisi na alijikuta akikubali kuendelea na filamu yao huku akibakwa na kaka Jambazi.
“Eti wewe mwanamke mbona unaonekana kumpenda kaka Jambazi”
“Wewe kaka Jambazi utakuwa na kimzizi sio bure ..argghh ..Uwiiiii…”
*******
Siku iliofuata Roma alimpigia simu Nasra na kumwambia yupo kwa Dorisi na Nasra mara baada ya kusikia taarifa hio alisema anakuja kupatia kifungua kinywa huko kwani mama yake kasafiri.
Roma hakuwa na kipingamizi , isitoshe Dorosi na Nasra walikuwa ni marafiki wanaofanya kazi ndani ya kampuni moja.
Baada ya wote kukusanyika Roma alipata nao kifungua na warembo wake hao huku akijisikia raha kuwaona kwa mara nyingine na muda wa kwenda kazini ulipo wadia Dorisi na Nasra waliondoka na Roma ndipo sasa alipoanza safari ya kuelekea nyumbani kwa Bi Wema.
Qiang Xi alikuwa akiishi na Bi Wema tokea kuondoka kwa Edna kuelekea Iringa , hivyo Roma alitumia nafasi hio kwenda kumsalimia na Rufi pamoja na Bi Wema lakini pia kupata muda wa kumhoji Qiang Xi kwa kitendo chake cha kumficha juu ya Lanlan kuwa binti yake ilihali alipewa maagizo na Master Chi kumuelezea kila kitu.
Roma hakuwa na gari hivyo alitembea lakini wakati akiwa anakaribia kupita nje ya nyumba yake kuunganisha moja kwa moja kwenda kwa Bi Wema aliitwa nyuma yake upande wa kulia na sauti ya mtu aliemuita aliweza kuitambua ni ya Bi Wema.
“Mr Roma mmerudi!!?”Aliuliza Bi wema akiwa kwenye bashasha.
Bi Wema alionekana kunenepa na mwoneknao wake ulikuwa umebadilika na kurudi kwenye ujana zaidi , pengine ni kutokana kipindi hicho hakuwa akiishi kwa mawazo tena ndio maana uzee ulikuwa ukipotea.
“Nimerudi, Edna yeye bado nimemuacha Iringa na Lanlan”Aliongea Roma na Bi Wema alimuelewa na kumuuliza habari za Iringa.
Bi Wema hakuwa na taarifa za kupotea kwa Roma na kurudi kwake na alijua katika kipindi chote hicho Roma alikuwa Iringa na hakuuliza sana maswali hata alipokuwa akiongea na Edna alijua wapo wote nyumbani.
“Bi Wema ndio nilikuwa nikija kwako”
“Oh!.. ndio nakuja nyumbani , Qiang Xi amenitangulia , tulipanga kusafisha mazingira ya nje leo kwenye bustani”Aliongea na sasa Roma kuelewa na aliona hana haja ya kuendelea na safari bali aligeuza na kufungua gati na kuingia ndani akitangulizana na Bi Wema.
Nyumba ilikuwa imepooza mno , lakini licha ya hivyo ni kama kuna watu waliokuwa wakiishi , mazigira yake hayakuwa ya kipweke sana , hata hivyo hawakuwa wameondoka kwa muda mrefu , ilikuwa ni kama mwezi na siku kadhaa tokea waondoke kuelekea Iringa.
Roma mara baada ya kuona hakukuwa na mabadiliko makubwa zaidi ya nyasi ambazo hazikukaa vizuri aliiingia hadi ndani na ile anafika sebuleni aliweza kumuona Qiang Xi akielekea jikoni akiwa ameshikilia beseni.
“Mr Roma karibu nyumbani”Aliongea Qiang kwa lugha ya kiswahili ilioathiriwa na lugha ya kichina , Roma hakushngazwa na Qiang Xi kuongea lugha ya kisawahili hata hivyo alikuwa ameishi Tanzania kwa muda mrefu hivyo inaleta maana kuanza kuelewa kuongea.
SEHEMU YA 627.
Roma alijikuta akiishia kumwangalia Qiang Xi kwa macho ya kiuchnguzi , ukweli ni kwamba kutokana na upole aliokuwa nao ilikuwa ngumu kusema Qiang alikuwa mtu mbaya.
Baada ya Roma kuongea kidogo na Bi Wema alimwambia Qiang Xi amfuate kuelekea juu ana maongezi na yeye.
Bi Wema kidogo alishangazwa na jambo hilo kwani Roma alionekana kuwa siriasi lakini hakutaka kuuliza wala kujua nini kinachoendelea zaidi ya kujiweka bize kwa kile kilichomleta asubuhi ndani ya nyumba hio.
Upande wa Qiang alimkabidhi Bi Wema Beseni alilokuwa ameshikilia na kisha alipandisha juu kumfuata Roma pasipo ya kuwa na wasiwasi.
“Qiang , babu yake Lanlan kuna chochote ambacho alikuagiza baada ya kukuambia umlete Lanlan kwetu ?”Aliuliza Roma mara baada ya Qiang Xi kuingia katika chumba cha kujisomea cha Edna.
Swali la Roma lilimfanya Qiang Xi kushituka kidogo lakini alijituliza na kumwangalia Roma.
“Mr Roma sijajua ni nini unataka kumaanisha”
“Ni kweli huelewi ni nini namaanisha?”Aliuliza Roma huku sauti yake ikiwa juu kidogo.
“Sijui ndio..”
Aliongea na Roma palepale alitoa ule ushanga kama Rozari aliopewa na Master Chi akipewa maagizo kumpatia Lanlan kwani angeikumbuka na kumuonyesha Qiang Xi.
“Ushanga wa Master!!!, Mr Roma umezipatia wapi , umekutana na Master?”Aliuliza kwa mshangao huku macho yake yakichanua.
“Hio sio pointi , ninachotaka kusikia kutoka kwako ni barua ulioachiwa na Master Chi iko wapi pamoja na kithibitisho cha Lanlan kuwa binti yangu?”Aliuliza Roma na swali lake lilikuwa bomu kwaQiang Xi na palepale alijikuta mwili wake ukipauka kwa hofu na kuanza kutetemeka.
“Mr Roma , naomba unisikilize…”
“Viko wapi?”Aliongea Roma huku hasira zikianza kumpanda na palepale Qiang Xi akiwa anatetemeka na machozi yakianza kumvaa alijikuta akipiga magoti mbele ya Roma.
“Mr Roma , tafadhari naomba usikilize maelezo yangu , nilikuwa na sababu”
Roma alijikuta akimwangalia , licha ya kwamba alikuwa akitia huruma lakini bado hakuweza kupungza hasira zake mara baada ya kushikwa na hatia ya kuishi na Lanlan muda mrefu pasipo ya kufahamu ni binti yake.
Kwa wenza wa kawaida pengine kuambiana wanapendana ni jambo la kawaida lakini upande wa Roma na Seventeen ambao maisha yao yalikuwa ni ya kupambania maisha yao hawakupata muda hata wa kuelezana ni kwa namna gani wanapendana lakini licha ya yote hayo hisia zao ziliongea mpaka kufanikisha kupata mtoto , hisia zao za pamoja zilikuwa zimetengeneza mizizi ambayo ilikuwa ngumu kung’olewa.
Roma alijiambia pengine Qiang Xi ana bahati , kama jambo hilo lingetokea miaka kadhaa nyuma akiwa na ukichaa wake basi asingeweza kumpa hata nafasi ya kujielezea na muda huo angekuwa ashamuua.
Alijitahidi kuzuia hasira zake na kumwangalia Qiang Xi aliekuwa akitia hruma na kisha akavuta pumzi nyingi na kuzishusha.
“Niambie sababu zako”Aliongea Roma na palepale Qiang Xi alijikuta akishukuru na kufuta machozi yake na mkono
“Mr Roma ninaweza kusema kwamba wewe sio binadamu wa kawaida na hata sasa kwa wakati wote ambao nimeweza kuishi ndani ya hii nyumba naweza kusema wewe ni mungu mtu , kama ilivyokuwa kwa Master, na siwezi kuthubutu kufanya kinyume na maagizo yenu”
“Huwezi kuthubutu , ulinifanya niwe gizani kwa muda mrefu na pengine usingeniambia kama tu nisingekutana na Master”
“Hapana Mr Roma , najua nilifanya makosa lakini nilifanya hivi kwa ajili ya familia yako , kwa ajili yako , Madam na Lanlan”
“Usije kujaribu kunifanyia hila , unadhani mimi ni mwepesi kudanganyika”
“Siwezi kuthubutu , sina uelewa mkubwa na mimi sio msomi na niliacha masomo nikiwa primary tu, hakukuwa na faida yoyote kwa upande wangu miimi kukaa kimya”
“Kama ni hivyo kwanini hukuniambia”
“Nitakuambia kila kitu na sitothubutu kukuficha tena , niliangalia barua aliondika Master mara baada ya kuhisi hatari ya anachotaka kufanya .. nilifanya yote hayo kujua ni wapi anaenda , Master ni mtu ambaye aliniokoa nikiwa hatarini hivyo aligeuka kuwa wa thamani kwangu , hivyo yote nilifanya kuweza kupata kujua ni nini anapanga kufanya ,,, sikujua barua hio ilikuwa ikihusiana na wazazi wa Lanlan”
“Barua iko wapi pamoja na kisu ulichopewa?”Aliuliza Roma akiwa katika mwonekano ambao ni ngumu kujua anafikiria nini.
Qiang Xi mara baada ya kuulizwa swali lile aliwaza kidogo na kisha akasimama na kukimbilia nje na dakika kadhaa aliweza kurudi akiwa ameshikilia kipande cha kisu lakini mkono wa kulia alikuwa ameshikilia simu.
“Mr Roma naomba msamaha wako , barua sikuweza kuitunza lakini nilifanikiwa kui’scan’ kwa kutumia simu …”Aliongea huku akitetemeka.
Roma alimwangalia kwa hasira na kisha akapokea kile kisu na kisha akachukua simu ya Qiang Xi .
Roma alikuwa amezindiwa na hisia za huzuni wakati akiangalia kisu ambacho kipo mikononi mwake , kilikuwa ni kisu ambacho kimefungwa fungwa katika kitambaa cha rangi ya bluu cha hariri.
Hakikuwa kisu cha thamani kubwa lakini historia yake ndio ilimfanya Roma kuona kisu hicho kama cha thamani kubwa kwani mara baada tu ya kukiona mawazo yake yalisafiri miaka mingi iliopita.
Haikueleweka Qiang Xi alitoa wapi akili ya kuiscan barua alioachiwa na Master Chi na kuihifadhi kwa mfumo wa PDF , katika hali kama hio alishukuru kufanya hivyo.
Roma licha ya kukasirishwa na jambo hilo lakini aliishia kusoma barua hio mwanzo hadi mwisho na kila kitu kilikuwa sawa na alivyoelezwa na Master Chi namna ambavyo amekutana na Seventeen na kumuacha Lanlan , Master Chi mwishonni kabisa alikuwa ameandika maneno ya Codes ambayo Roma mara baada ya kuyasoma aliwweza kuyaelewa , yalikuwa ni maneno ambayo ni sawa na ‘signature’ ya barua hio kutbitisha kama yeye ndio ambae aliandika , hakuacha pia kumuusia kuhusu uwepo wa maadui wanaowinda mbinu ya kimaandiko ya urejesho.
“Mr Roma naomba unisamehe , sikuweza kukupatia barua hio na kufanya kama nilivyoagizwa kwani nilijua ukweli wote”
“Kwanini?”
“Mr Roma nimeishi kwa kumlea Lanlan kwa muda mrefu sana mpaka siku ambayo tuliweza kukutana na ninyi , tokea nimeanza kumlea Lanlan nilimchukulia kama binti yangu wa kumzaa lakini kwa upande wake hakuacha kumuulizia mama yake na baba yake , tuliweza kusafiri pamoja huku na kule tukiwa na Master , licha ya kwamba Master alikuwa akimpenda sana Lanlan na kumjali lakini bado Lanlan hakuacha kuulizia kuhusu wazazi wake kila mara alipoweza kuona watoto wakiongozana na wazazi wao , iliniumiza sana kipindi hicho kumuona Lanlan akiwa ni mwenye huzuni ya kukosa wazazi kama watoto wengine , alikuwa ni mtoto wa kipekee na watoto wa aina yake ambao wana akili na nguvu mara nyingi maisha yao huishia kuwa ya upweke , pengine angalau angezaliwa katika familia ya kawaida lakini kipindi hicho hakuwa hata na wazazi , hakuweza kupata kujua nini maana ya mapenzi ya wazazi , hakujua kama wazazi wake walikuwa wanaishi na aliishia kuwaonea watoto wengine wivu..”
“Mr Roma tokea siku ya kwanza Lanlan kumuona Miss Edna , kila siku alikuwa akienda kukaa pale nje ya geti akisubiria kumuona tena , kwa mara ya kwanza tokea nimlee niliweza kuona furaha yake , aliniambia ameweza kumpata mama yake lakini anaogopa ataondoka tena kwasababu hakuwa akimpenda , alikuwa akitia huruma sana na iliniumiza kumuona vile , bahati nzuri Miss Edna akatokea kumpenda Lanlan na kuanza kufikiria kumuasili , Lanlan alikuwa na furaha sana na kwa mara ya kwanza nilimuona akiwa katika hali ya kuridhika .. najua Miss Edna anaweza akafanana na mama yake mzazi lakini mimi kama mwanamke niliweza kuhisi Edna alikuwa akimjali sana Lanlan , alikuwa akimpenda kwa moyo wake wote kama mzazi na swala hilo lilinifanya niridhike na kutotaka kitu kingine zaidi , Lanlan hakuwa akipenda kulala kabisa nilipokuwa naishi nae lakini mara baada ya Madam kuja kwenye maisha yake alianza kulala vizuri na hashituki shituki usiku”Qiang Xi alijitahidi kujielezea , alionekana hakuwa akidanganya , alionekana alikuwa akijali furaha ya Lanlan.
Roma alijikuta akikumbuka namna Lanlan anavyolala na kujikuta moyo wake ukiwa wa moto.
“Mr Roma sijaishi kwenye familia yenu kwa muda mrefu lakini ninawashukuru sasa wewe na Miss Edna , Madam Blandina na Bi Wema na wengine wote ambao ni wazuri kwangu , mimi ni mgeni ndani ya taifa hili lakini niliamua kubakia hapa kwa ajili ya kuendelea kumuona Lanlan.. nashukuru hakuna ambaye amenibagua licha ya kwamba mimi sio wa taifa hili … Sikutaka kukuambia ukweli kwasababu niliogopa familia yako inaweza kuingia kwenye migogoro ambayo inaweza kuwa mikubwa kiasi cha kutengana na athari zikampata Lanlan , najua Miss Edna bado hayupo tayari kuwakubari wanawake wengine lakini hisia zao kwako ni za kweli na wewe ulikuwa ukijaribu kuimarisha familia yako kwa kujitahidi kumbembeleza mkeo ..
“Mimi si kitu , sijasoma lakini nilichotaka ni kumuona Lanlan akiwa na maisha mazuri , nilikuwa nikitaka kumuona akikua kwenye familia yenye furaha na upendo , nilikuwa mbinafsi ndio maana sikutaka kuondoka kwenye hii familia lakini …”Alijikuta akitoa kilio cha kwikwi.
Qiang Xi alijitahidi kujitetea na maneno yake kwa uzoefu wa Roma aliona hayakuwa na walakini , alionekana dhamira yake ilikuwa wazi , alichokuwa akitaka ni kumuona Lanlan akipata malezi stahiki.
Upande wa Roma aliona pengine ingekuwa sawa kama Lanlan angezaliwa na mwanamke mwingine , lakini Lanlan mama yake alikuwa ni Seventeen ambaye Edna anamchukulia kama mshindani wake.
Seveenteen alikuwa ameondoka moja kwa moja lakini kubaki kwa Lanlan kungemfanya kumkumbuka mara kwa mara.
Roma alijua Edna ni mtu ambae ana hasira za haraka ni ni mwepesi kubadilika na asingeweza kupotezea swala hilo kirahisi , pengine angeweza kumvumilia kwa kuwa na wanawake wengine nje lakini sio swala la Roma kuwa na mtu mwingine anaempenda zaidi yake.
Edna alikuwa akimvumilia Roma na kuendela kuishi nae kwa kujua kwamba ni yeye pekee ndio ambaye alikuwa akipendwa zaidi ya wengine wote.
Upande wa Roma aliona pengine Qiang Xi yupo sahihi , kama angejua mapema Lanlan ni binti yake kabla hata mahusiano yake na Edna kuimarika pengine maisha yake yangekuwa tofauti na sasa;.
Licha ya Roma kufikiria mengi lakini ni kwamba kwa wakati huo alikuwa akijua ukweli wote na asingeweza kwenda kinyume na hitajio la Seventeen la kumtambua Lanlan.
Roma mara baada ya kufikiria kwa muda aliishia kumwambia Qiang kwamba asimame na swala hilo alifanye siri mpaka atakapo mpa ruhusa ya kuongea na asiwe na hofu tena na aendelee kuishi nao na iang Xi alishukuru sana huku furaha yake ikionekana.
Mchina huyu alionekana kupenda mazingira ya Tanzania na katika kujitetea kwake alisema alikuwa Yatima huko kwao China na mara baada ya kukutana na Master Chi pamoja na Lanlan wakawa ni kama ndugu zake , sasa Master Chi ameondoka na Lanlan ameweza kumpata baba yake hivyo kama angerudi China ilikuwa ni kwenda kuanza moja, hivyo familia pekee alioona inamfaa ni ya Roma.
Alipenda wanafamilia hao walivyokuwa wakimjali mpaka kufikia hatua ya kumfundisha tamaduni za kitanzania na alikuwa ameridhika.
Roma akili yake ilikuwa imemjaa , alishindwa hata kujua ni kipi ambacho anapaswa kufanya kwa muda huo kwani kila kitu ni kama kipo hatarini kama ukweli utawekwa wazi alihofia familia yake kuvunjika , alihofia mapenzi yake kufikia tamati, dhamiri yake ilikuwa ikimsuta kwa wakati mmoja.
Roma mara baada ya kushuka chini aliweza kukutana na Bi Wema na kumpa maelezo kwamba yeye na Edna wangerudi januari baada ya mwaka mpya hivyo kama kuna tatizo lolote asisite kumpigia simu na Bi Wema hakuona tatizo na alikubali.
Roma siku hio hio alipanga kurudi Iringa , hakutaka kukutana na warembo wake kwani akili yake haikua sawa lakini hata hivyo alisita kuanza safari moja kwa moja kwani wakati akiwa njiani aliweka miadi ya kuonana na Najma nyumbani kwao kwani Juma alikuwa na sherehe ndogo ya kumtoa mtoto wake mara baada ya kutimiza siku arobaini.
Roma mara baada ya kukumbuka ahadi yake palepale alizama kwenye gereji yao ya magari na ksiha akatoka na Lexus na kuianza safari ya kuelekea Mbagala.
Hakuona haja ya kuwasiliana na Najma kwani walipanga kuonana huko huko yeye akishatoka kazini hivyo aliunganisha.
Ilikuwa mchana hivyo msongamano wa magari ulikuwa mdogo na aliweza kutumia dakika chache tu kufika Rangi tatu mbagala na kuchukua njia iliokuwa ikielekea Bias.
Alikuwa ameikumbuka hio mitaa , alikuwa na muda mrefu kidogo hajawahi kufika tokea mara ya mwisho kuja kujitambulisha mbele ya wanafamilia kama mchumba wa Najma na ilimshangaza kuona njia hio ilikuwa imewekwa rami yote na kupendeza tofauti na mwanzo.
Roma mara baada ya kukaribia karibu na nyumba ya Juma aliweza kuona gari zuri ya bei ghali aina ya Lamborgin ikisimama nje ya geti la nyumba ya Juma , mwanzoni wakati gari hio ilivyokuwa mbele aliishia kutoa tabasamu la uchungu kwa kujiambia magari hayo kuwepo Tanzania ni kama uharibifu wa hela kutokana na aina ya barabara kutoruhusu lakini mara baadda ya gari hio kusimama nje ya geti la nyumba ya Juma alijikuta akishikwa na shauku kubwa zaidi ya kumuona mmiliki.
Ni ndani ya dakika moja tu badala ya gari hio kusimama , ikiwa imekodolewa macho na watu wengi wa mtaa hio , hatimae aliweza kushuka mwanaume mtanashati aliekuwa amevalia suti nyeusi na kufungua mlango wa mbele kushoto na kisha alionekana mwanamke mrembo alievalia hijabu akishuka.
Roma aliishia kuguna mara baada ya kugundua mwanamke alieshuka kwenye gari hio alikuwa ni Najma.
SEHEMU YA 628.
Tokea kurudi kwa Najma ncini Tanzania na kuanza kufanya kazi wizarani alikuwa na mabadiliko makubwa , alikuwa ametoka katika usichana na kuwa mwanamke sasa ambaye alikuwa tamanio la wanaume wengi.
Najma alionekana kutotaka kumkaribisha mgeni aliemleta kwani alionyesha ishara ya kuaga ili kuingia ndani , lakini yule mwanaume alimzuia akionyesha kama vile kuna kitu anataka kuongea nae.
Hali hio ilimfanya Roma kuona pengine mwanaume huyo alikuwa katika harakati za kumpata Najma.
Alifikiria hivyo kwani hakuamini Najma ni mwanamke mwepesi ambaye anaweza kumsaliti , lakini licha ya hivyo hali ile haikumfanya kuwa katika hali ya utulivu na alizima gari yake na kisha akatoka nje na kisha akailoki na kuanza kupiga hatua kuwasogelea.
Roma mara baada ya kusogea karibu zaidi ndio sasa aliweza kumuona mwaname mwenyewe ambaye alionekana kuwa na pesa mpaka kumiliki gari kali la namna hio.
Alikuwa ni kijana mrefu wa saizi ya kati ambaye alikuwa na sura ya kihandsome kumzidi yeye na kwa haraka haraka alimkadira umri wa miaka yake inaweza kuwa ishirini na tano kuendelea..
Alikuwa akivutia kwani alionekana ni mtu wa mazoezi na kubwa zaidi alionekana kujiamini , pengine ni haki yake kuweza kumtongoza mwanamke mrembo kama Najma kwani kimuonekano ni sawa na kusema wanaendana.
Roma macho yake ya haraka haraka yaliweza kumkagua kwanzia suti yake ya Versace , viatu vya kung’aa vilivyoendana na mavazi yake pamoja na muonekano.
Upande wa Roma wakati huo alikuwa amevalia kikawaida sana, shati la mikono mirefu la drafti ya rangi ya kijani na nyeusi, jeans nyeusi pamoja na Moka na saa ya bei ghali alionunuliwa kama zawadi na Edna.
“Mheshimiwa nadhanni leo sio muda mzuri , unaonaje tukaweka miadi siku nyingine , naomba unisamehe..”Aliongea Najma huku akiwa kama mwanamke anaemkataa mtu kistaarabu.
“Najma nishakuambia uniite kwa jina langu tu inatosha , ila kwanini leo isiwe muda mzuri,isitoshe sio kama ni mara ya kwanza kukutana na kaka yako pamoja na ndugu zako , nina shauku pia ya kumuona mwanaume ambaye unatoka nae , hujawahi kuwa hivi leo umebadilika sana”
“Si..”
Najma alitaka kuongea lakini palepale alijikuta akiishia njiani mara baada ya kumuona Roma akiwasogelea na macho yake yalichanua huku furaha yake ikiupamba uso wake.
“Roma!!”
Roma alitembea na kumsogelea Najma huku akimpotezea mwanaume alieitwa mheshimiwa na kisha akamkumbatia na kumpiga Najma busu la Shavuni.
Kwa wakati huo Roma alitaka kwenda mbali zaidi na kumbusu mdomoni lakini alimheshimu Najma kutokana na watu wengi walikuwa wakiwaangalia.
Kitendo cha Najma kukumbatiwa kwa haraka hivyo mbele ya watu kidogo tu adondoshe pochi yake lakini aliishia kufurahi mara baada ya kuona Roma alikuwa na wivu na yeye.
Upande wa mwanaume alieitwa Mheshimiwa na yeye hakujali kitendo cha Roma cha ghafla bali alikuwa akimwangalia Najma na kwa uzoefu wake aliweza kuona Najma alionekana alikuwa amependa kweli na hata matumani yake kushuka zaidi na zaidi.
Jambo hilo lilimkasirisha mno kwani ni zaidi ya mwezi tokea aanze kumchombeza mrembo Najma amkubalie hata kumuahidi ndoa moja kwa moja .
Bahati tu ni kwamba alikuwa mzoefu kwani palepale alipotezea hasira zake za kupokonywa tonge mdomoni na mwanaume ambaye alikuwa na mwonekano wa kawaida kabisa.
“Babe huyu mwanaume ndio nani?”Aliuliza Roma huku akimwachia Najma na kujifanyisha ndio eti anamuona huyo mwanaume .
“Huyu ni naibu waziri wa elimu , Mr Salihi Ibuyawanga nilikuwa nikisubiria Uber ili kuanza safari ya kuja huku na aliniona na kunipa lift”Aliongea Najma kwa sauti ya chini.
Roma alishangazwa na maneno ya Najma kidogo , mwanaume aliekuwa mbele yake alikuwa ni mdogo mno kimuonekano lakini alikuwa ni Naibu waziri, alijiuliza ni kipi amefanya mpaka kuaminiwa kwa umri wake huo.
Roma pia aliona mwanaume huyo hakuwa wa kawaida maana kama kweli kazi yake pekee ni ya Unaibu waziri asingeweza kuendesha gari ya gharama kiasi hicho.
“Mr Roma , wewe ndio boyfriend wa Najma?”Aliuliza yule mwanaume , alionekana alikuwa akilijua jina la Roma pengine ni mara baada ya Najma kulitamka.
“Hapana sio sahihi kusema boyfriend , mimi ndio mwanaume wake”Alijibu.
“Oh ! kwahio unamaanisha umemuoa?”Aliuliza bwana Salihi.
Ukweli ni kwamba alishafanya uchunguzi kuhusu Najma na alishangazwa kwa kuona kwamba Najma hakuwa na skendo nyingi hata kipindi alichokuwa anasoma na jambo hilo ndio lilipa motisha ya kutaka kuwa nae karibu zaidi.
“Bado hatujafunga ndoa lakini nnitaendelea kumpenda mpaka siku ambayo yeye mwenyewe ataacha kunipenda”Alijiibu Roma kwa kujiamini.
Upande wa Najma alijikuta akiguswa na jibu la Roma lakini kwa wakati mmoja akiona aibu na alijiambia anawezaje kumuacha ilihali alimpigania kumpata kwa muda mrefu kiasi hicho.
“Hahaha.. wewe ni noma , kila mwanaume anahaki ya kutoka kimapenzi na mwanamke mrembo kama Najma, ila kwasababu hujamuoa natumaini huwezi kutuingilia sana kwani sitaki tuwe na wakati mgumu ilihali ndio mara yetu ya kwanza kukutana , kwasasa kuna maswala napaswa kuyashughulikia hivyo nitaondoka , natumaini tutaonana tena”Aliongea huku akimwangalia Roma kwa tabasamu ambalo limejaa kebehi na kisha akamgeukia Najma.
“Najma msalimie Shangazi na kaka yako Juma , nitawatembelea muda wowote m tafadhari naomba usinikatalie utaumiza nia utu wangu”
Mheshimiwa Salih hakusubiri jibu kutoka kwa Najma kwani palepale aliingia kwenye gari yake na kuigeuza kwa tambo na kuondoka.
Upande wa Roma alijikuta akiguswa na maneno ya kiuchokozi ya Salihi na alitamani kuipiga teke gari yake na kuiharibu palepale , lakini alijitahidi kujizuia.
“Najma ni kwa muda gani amekuwa akikusumbua?”Aliuliza Roma huku akijitahidi kujituliza na Najma alitoa kicheko cha utani kutokana na namna Roma alivyyobadilika.
“Sikuweza kufanya chochote , yeye ndio mkuu wangu wa kazi na nisingeweza kumkataa bila ustaarabu kwani ningefanya mazingira ya kazini kuwa magumu , naogopa pia kupoteza kazi yangu kwani mama ndio kanisaidia”
“Hilo sio tatizo , ninaweza kukuhamishia wizara nyingine kama anakuchukiza”Aliongea Roma kama vile yeye ndio raisi wa nchi.
“Hapana napenda nafasi yangu ya kazi kwa sasa kwani inaendana na nilichosomea na isitoshe unaweza kunihamishia sehemu nyingine na nikakutana na wanaume wengine ambao wananitaka , ni bora nilipo kwasasa kwani waziri Salihi kuonyesha kunitaka kumewafanya wengine wote kutothubutu kunisogelea”
Roma alijikuta akihema ndani kwa ndani na kujiambia Najma asingeacha kutongozwa kwani hakuwa amemuoa , ni swala ambalo halikuwa likiepukika labda tu aachane na maswala ya kazi.
Roma aliishia kukosa chaguo lingine na kuona ni kheri atulie tu licha ya kwamba hakupenda mwanamke wake kusumbuliwa kama hivyo.
“Babe naomba usiwe na wasiwasi , niamini mimi hakuna kitu ambacho kinaweza kutokea kati yetu , natembelea tu upepo kwa sasa , mwanaume wa aina yake ni wale ambao sio wavumilivu na muda wowote atajikatia tamaa , isitoshe kuna samaki wengi ziwani wa kuvua , pengine amevutiwa na mimi kwa muda tu na muda si mrefu anaweza kuona samaki mwingine, isitoshe tetesi ninazosikia anaweza kupandishwa cheo muda si mrefu”Aliongea Najma na kumfanya Roma kuguna.
“Familia yake ikoje , bado anaonekana mdogo na nafasi yake ni kubwa na unasema atapandishwa cheo?”
“Sijafatilia sana ila kwa ninavyosikia ni kwamba baba yake ni mfanyabiashara na kipindi ambacho raisi Senga yupo kwenye harakati za kampeni alisaidia kwa kiasi kikubwa kwenye kumfadhili , licha ya hivyo nasikia ametoka na GPA ya kwanza kutoka chuo cha Yale Marekani , hivyo ni sawa na kusema nafasi yake inalingana na elimu yake , ni mtu mwenye malengo na elimu ya Tanzania , mheshimiwa amemuweka kama naibu waziri mara baada ya kumpatia ubunge kutokana na mawazo yake ya kutaka kubadilisha mtaala wa elimu wa Tanzania ambao hauendani na kasi ya teknolojia hivyo inaaminika ili malengo yake kutimia atapandishwa cheo na kuwa waziri kamili au katibu mkuu wa Wizara , hizo ni fununu tu”Aliongea Najma kwa kirefu.
Ilikuwa ni kama Roma alivyotegemea , lakini hata hivyo alijiambia Najma hawezi kumuacha yeye na kwenda kwa ndugu naibu waziri Salihi.
Baada ya kuongea kwa dakika chache wakiwa pembeni ya geti Najma aliweza kuitwa na mwanamke ambaye Roma alimtambua ni shangazi yake na wote kwa pamoja waliona wasitishe mazungumzo na kuingia ndani.
Roma mara baada ya kuingia ndani aliweza kupokelewa na Juma ambaye alikuwa amevalia kanzu.
Mazingira ya nyumba ya Juma yalikuwa yamebadilika mno na kwa haraka haraka Roma aliamini nyumba haikuwa ikipangishwa tena kwani ilifanyiwa usafi kuanzia nje mpaka ndani na hata chumba chake cha kihistoria kilikuwa kimebadilishwa muonekano.
Sherehe ilionekana haijaanza bado na kuna wanawake wengi waliokuwa ndani ya geti wakionekana kuwa bize na mapishi , hata hivyo ilileta maana kwani muda ulikuwa ni saa nne za asubuhi kwenda saa tano.
“Bro..!!”Juma aliita huku akiweka tabasamu bashasha huku wakipeana kumbatio ambalo waswahili wa mtaani wanasema ni la kisela.
“Mazingira yamebadilika sana , naona hata room yangu imebadilika kimuonekano”
“Hahaha.. upo sahihi shem , kudra za mwenyezi Mungu zimefanya haya yote kuwezekana, karibu sana bro nyumbani , nilikuwa nikiona kila kinachoendelea hapo nje ila nilitulia kwanza muyamalize hahaha..”
“Hahaha.. kumbe ulikuwa ukituona?”
“Ndio nakuambia hivyo ndugu yangu , unapaswa kuchukua hatua mapema Najma anazidi kuwa maarufu na hadhi yake imepanda”
“Kwa maneno yako , inaonyesha sio mara ya kwanza kuletwa na gari?”Aliuiza Roma mara baada ya kukaa kwenye kiti cha plastiki chini ya turubai.
“Siwezi kusema ni mara nyingi kwani muda mwingine analala huko kwenye apartment yake , ila naweza kusema kila wakati anaokuja anaongozana na Naibu waziri , nadhani pia shida ya usafiri unachangia”Aliongea na kumfanya Roma aone tatizo lipo wapi na alitamani kujipiga kibao.
Aliweza kumsaidia Najma kupanga kwenye Apartment lakini akasahau kitu muhimu sana kumpatia,
Hakukumbuka kumnunulia gari , isitoshe Najma hadhi yake ilikuwa ya juu hivyo asingeweza kupanda daladala ,pengine pia Najma alihitaji usafiri lakini alishindwa kumwambia.
Roma palepale aliona hili haliwezi kuendelea hivi , ngoja atumie upluto wake kuhakikisha gari inasafirishwa hata kwa ndege kuja Tanzania.
Palepale alimwita Najma huku akiingia mtandaoni na kutafuta picha za magari tofauti tofauti ili kumuonyesha ni aina gani anapenda amuagizie.
ITAENDELEA KUHUSU SIKU NO PROMISE'S