Spartacus boy
JF-Expert Member
- Sep 22, 2020
- 1,727
- 3,464
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Matendo ya mapacha yanasikitisha. Haya ni matokeo ya KUWADEKEZA ktk malezi.SEHEMU YA 495.
Roma alishangazwa na kupatwa na huzuni ya taarifa hio ya kifo kwani siku hio hio ndio walipanga kwenda yeye Edna na Lanlan kumtembelea, kwao ilikuwa ni kama wamechelewa kwenda , lakini hata hivyo hakujilaumu sana kwa kutowahi kwenda kumuona.
Mzee Atanasi ni moja wapo ya wazee waliokula chumvi nyingi na alikuwa akikaribia kutimiza miaka mia moja na moja na kwa uzito wake ndani ya serikali ya Tanzania ni sahihi kuitwa babu wa taifa.
Ndio mwanajeshi pekee aliebaki ambaye alipigania uhuru wa Tanzania pamoja na Raisi Nyerere.
Roma hakuwa na haraka ya kwenda moja kwa moja msibani , alitaka kwanza kumaliza kilichomfikisha hapo na kisha ndio arudi nyumbani na kuelekea huko , ile safari yao ya kwenda kwa ajili ya kusalimia iligeuka na kuwa safari ya kwenda msibani.
Roma baada ya kukata simu kwa kumpa mama yake pole aliwageukia Diego na kuwapa taarifa hio ya msiba na Diego na Bram walimpatia pole.
Roma aligeukia kwa mara ya pili picha iliokuwa ikionekana kwenye skrini , picha ya mwanaume aliefahamika kwa jina la Bikindi , alikuwa ni baba mzazi wa Lekcha na Roma alimkumbuka kwasababu ni moja ya wanasayansi wa Zeros organisaiton aliowaua.
“Mfalme Pluto unamfahamu huyu mwanaume?”Aliuliza Diego na Roma alitingisha kichwa kuashiria anamjua.
“Mmefanikisha kuchunguza taarifa za Joseph Bikindi za hivi karibuni”
“Ndio mfalme Pluto kwa taarifa tulizoweza kupata kutoka Rwanda mpaka miezi michache iliopita alikuwa mkufunzi wa chuo kikuu cha taifa lakini kwa wiki kadhaa sasa ameripotiwa kutoonekana chuoni bila ya taarifa”.
“Endeleeni kumchunguza kwa ukaribu zaidi na sura yake iunganishe na mfumo wetu wa ‘facial recognition’ ili kama itatokea akiwepo Tanzania tuweze kutambua mara moja”Aliongea Roma huku akipata hisia huenda Lekcha alikuwa Tanzania kwa kutafuta namna ya kulipiza kisasi na kwa muda huo ambao Kizwe alionekana kutokuwa wa kawaida aliamini huenda wapo wote na wanajiandaa na mipango ya kulipiza kisasi , hakusahau na Denisi alikuwa hivyo hivyo tu ndio maana alihitaji kuchukua tahadhari mapema.
Jambo lingine ambalo lilimfanya kuwa na wasiwasi ni juu ya Athena ,tokea apewe cheo cha Hades hakuwahi kujionyesha kwake na alikuwa akijua ana mzunguka lakini hakuwa akijua sababu ni ipi ,lakini alijiambia maadamu yupo hai basi kuna siku tu wataonana na atathibitisha maswali yake yote.
“Vipi kuhusu uchunguzi wa Chriss mlikamilisha?”
“Mfalme Pluto taarifa za Chriss imekuwa ngumu sana kuzipata na mpaka sasa hatujapiga hatua lakini kuna jambo moja tu ambalo tulifanikiwa kupata”
“Mmepata nini?”Aliuliza Roma kwa shauku na Diego alitoka ndani ya chumba hiko na ndani ya muda mfupi aliweza kurudi na mfuko wa plastic ambao ndani yake ulionekana kuwa na mkufu uliofungwa na kishaufu cha madini ya almasi.
“Huu ni…”
“Ni mkufu ambao unaonyesha Chriss alikuwa mwanachama wa Freemason”Aliongea Diego na kumfanya Roma kuchukua na kuangalia vizuri na kweli aliweza kugundua maana ya mchoro uliokuwa kwenye kishaufu(Pendant).
Ijapokuwa sasa ameweza kuanza kupata ukweli wa Chriss alikuwa akitokea jamii ya siri ya freemason lakini ilikuwa ngumu kwake kuweza kuamini kama watu wa jamii hio ya siri ndio walitaka kumuua mke wake na moja kwa moja alijua huenda majibu yapo kwenye mchoro.
Roma ilibidi kwanza amuelezee Diego na Bram kile ambacho alikuwa akitambua kuhusu Chriss.
“Mfalme Pluto hata sisi tunashindwa kuelewa kama Chriss alikuwa mwachama wa Ant- illuminat”
“Kwanini mnaamini hawezi kuwa mwanachama unajua taarifa zote za umoja huo?”
“Ndio mfalme Pluto najua taarifa zote zinazohusiana na umoja wa ant- illuminat na baadhi ya mipango yao ya mbeleni japo mpaka sasa hakuna uthibitisho kwani ni taarifa ambazo ni kama uzushi”
“Ni taarifa gani ambazo unafahamu?”
“Mfalme Pluto ushawahi kusikia kuhusu mpango TASAC?”
“Mpango TASAC!, si huu ulioanzishwa na serikali ya Urusi kuyafanya mataifa ya Afrika kutounga mkono wala kukataa vamizi anazozifanya Raisi wa Urusi nchini Ukraine?”
“Ndio mfalme Pluto lakini ni ngumu kusema mpango TASAC umeanzishwa na Urusi”
“Kwanini?”
“Taarifa za siri za daraja la tatu zinaonyesha mpango TASAC waanzilishi ni Ant- illuminat”Aliongea na kumfanya Roma kuguna ilikuwa habari mpya kwake na huenda angekuwa anafatilia sana maswala ya siasa angekuwa ashaijua , huenda ilikuwa sahihi kwa Christen kumwambia hayuko ‘flexible’ kama mtangulizi wake”
“Uzushi mwingine unaoenezwa kuhusu Ant-illuminat ni juu ya mataifa ya kiarabu kuwekeza zaidi katika mataifa yalioendelea ya kimagharibi katika nyanja ambazo zinagusa moja kwa moja hisia za watu mfano kwenye vilabu vya mpira na kadhalika”Aliongea Bram.
“Na pia ndio kinara wa mapambano ya sarafu ya Dola ya kimarekani kutaka kuiangusha”Aliongezea Diego.
“Inaongekana mnapenda sana uzushi”
“Your Majesty if no Somke no Fire “Aliongea Diego akiingiza msemo ambayo unaoendana na ule wa kiswahili usemao yasemwayo yapo na kama hayapo yaja au penye moshi hapakosi moto.
Roma hakutaka kukaa sana hapo kwani kuna msiba ambao ulikuwa ukimuhusu na mpango wake ni kuunganisha kwanza msibani kujua kile kinachoendelea na kujua taratibu zinazofuatia, hivyo alitoa msisitizo wa usalama zaidi wa watu wake wa karibu kuzingatiwa hususani muda huo ambao alijua na Lekcha ni adui yake mpya alieingia kwenye orodha.
Akiwa garini alijaribu kuwasiliana na mke wake kumuulizia kama kapata taarifa na ilionyesha Edna alikuwa na taarifa na alikuwa akijiandaa kwa ajili ya kufika msibani pamoja na Bi Wema na Roma alimwambia angemkuta huko huko kwani anatangulia.
Baada ya kufika Masaki nyumbani kwa Tajiri Azizi aliweza kuona watu wengi waliokuwa wakiingia ndani ya nyumba hio na kutoka na pia kulikuwepo na baadhi ya waandishi wa habari.
Kwa haraka haraka Roma alishajua msiba huo ni wa kitaifa hivyo wageni wengi lazima wangefika kutoa salamu zao za pole.
Roma hakuingiza gari ndani ilibidi apaki pembeni kwa kuhofia ndani kusingekuwepo na nafasi na baada ya kuegesha aliingia moja kwa moja ndani na alikuta tayari maturubai yashasimamishwa pamoja na viti ambavyo vilikuwa vikipangwa.
Mtu wa kwanza kuonana nae alikuwa ni Kassimu mtoto mkubwa wa tajiri Azizi ambaye alikuwa akipokea wageni na alimkaribisha Roma na kumpeleka kuonana na mama yake pamoja na wanafamilia wengine.
Dakika chache mbele na Edna aliweza kufika na kutoa pole , msiba haukuwa na vilio sana zaidi ya sura za majonzi tu huenda ni kwasababu mzee huyo kaishi miaka mingi na muda wake umewadia hivyo alipaswa kutangulia mbele za haki .
Ratiba ya msiba ilikuwa ni siku inayofauta mwili kuagwa katika viwanja vya Karimjee na kisha safari ya kuelekea Kilosa kijijini ingeanza ili kumpumzisha Babu Atanasi.
Katika watu ambao walikuja kutoa salamu za pole ni Samweli Nguruma kiongozi wa kundi la ZoaZoa na ilikuwa ni kama amekuja kumtafuta Roma kuongea nae.
Roma alishawahi kuwasiliana na bwana huyo kwa kupitia simu ila hakuwahi kukutana nae ana kwa ana na siku hio ndio waliweza kufahamina kwa mara ya kwanza.
Samweli Nguruma baba yake na Benadetha alikuwa ni kama bosi mtu mwenye kitambi na kipara cha nywele na ilikuwa ngumu kuamini ndio ambaye alikuwa akijihusisha na biashara za magendo lakini hata hivyo Roma hakutaka kumtoa dosari ukizingatia hata Rose hakuwa na mwonekano wa kuongoza kundi la Tembo.
“Mr Roma unamwonaje mtoto wangu Benadetha?”Aliuliza Samweli Nguruma na kumfanya Roma kushangazwa na swali hilo.
Ilikuwa ni saa za mwisho mwisho za kuaga mwili ili safari ya kuelekea Morogoro ianze ndio maana Roma alishangaa.
“Kwanini unauliza hivyo mzee?”.
“Nataka kujua maoni yako, umefanya nae kazi kwa muda mrefu kidogo hivyo sio dhambi kutoa maoni yako unavyomuona na tabia yake kwa ujumla”Roma ijapokuwa muda huo aliona hakupaswa kujibu swali hilo kutokana na muda kutokuwa mzuri lakini aliona ni kheri kujibu kile anachokiona kwa Benadetha.
“Namuona kama msichana mzuri mwenye sheria zake na inaonyesha ashatambua mapema kama mwanamke anataka nini katika maisha yake”Alijibu Roma na kumfanya Samweli nguruma kutabasamu.
“Upo sahihi Benadetha ni binti mwenye msimamo na mara nyingi uwezo wake mkubwa wa kujielewa unanifanya hata mimi baba yake kumhofia”
“Hongera kwa malezi, kwa ninavyomuona atakuja kuwa na maisha yenye furaha sana mbeleni”
“Furaha ya mwanamke inakamilika pale akiridhika na kila kitu kunachomzunguka, asipo ridhika ataishia kutangatanga kukidhi haja ya moyo wake”Aliongea
“Ndio maana nikasema Benadetha atakuja kuwa na furaha kwasababu kama mwanamke ukishafahamu kwenye maisha unataka nini mapema ni rahisi pia kuridhika”
“Upo sahihi Mr Roma lakini ushawahi kujiuliza kwanini kipindi Benadetha alipopelekwa kituoni na mkeo nilitaka wewe ufanye kazi ya kumtoa?”
“Kwanini?””
“Nilijua tayari mkeo ashafahamu hisia za Benadetha kwako”Aliongea na kumfanya Roma ashangae.
“Mzee labda utakuwa haujamfahamu Benadetha vizuri , mimi na yeye hatuna ukaribu huo na hata kama Benadetha anipende mimi kama mwanaume siwezi kumpokea kwani tayari nina mke”Aliongea Roma bila ya wasiwasi.
“Haha.. Mr Roma nimekutana na vijana wengi ila ujasiri wako na kujiamini ni wa viwango”
“Na wewe pia ujasiri wako ni wa viwango kumnadi mtoto wako wa kike kwangu ilihali tayari nina mke sio jambo la kawaida kabisa kwa tamaduni za kiafrika”
“Upo sahihi imenichukua ujasiri kuongea na wewe kuhusu maswala ya binti yangu na nimetidhika pia kama huna nia ya kumfanya kuwa sehem ya wanawake wako”Aliongea na kumfanya Roma kumchanganya na kuona huenda habari za yeye kuwa na wanawake wengi zilikuwa zikifahamika kwa watu wengi.
*********
Tokea kumalizika kwa maziko ya Babu Atanasi siku zilienda haraka haraka mno na katika watu ambao walikuwa wako bize basi ni Roma ,kuna muda alijiambia uwepo wa Lanlan kidogo ulikuwa umesaidia sana kupunguza migogoro yake na Edna.
Kwani kitendo cha Lanlan kung’ang’ania kulala na mama yake ilimpa nafasi Roma ya kila usiku kutembelea wanawake wake kwa zamu na hilo pia lilisaidia sana kuyafatilia maendeleo yao.
Vidonge ambavyo aliweza kuvipata baada ya kuwaua watu wa hongmeng vilisaidia sana katika kumfanikisha Rose kupanda levo na Roma aliona kabisa muda si mrefu Rose angefanikisha kupata ufunuo wa nguvu ya mbingu na Ardhi jinsi ya kutumia elementi zote za dunia.
Katika mafunzo ya kijini kila mmoja alitofautiana na mwenzake katika kupata ufunuo wa namna ya kutengeneza maajabu kwa kutumia elementi za dunnia na hicho ndio ambacho kilimfanya Roma kupatwa na hamu kubwa ya kuwaona wakifikia levo ya kupata ufunuo.
Mage na yeye hakuwa mbali sana na ilionyesha juhudi zake zilionyesha manufaa kwani alianza kuelewa levo ya nusu mzunguko kikamilifu na Roma aliona kabisa muda si mrefu angeweza kuingia levo ya mzunguko na alijiambia kama atafanikisha mpango wake wa kutengeneza vidonge vyenye nguvu basi huenda ndani ya mwaka mmoja kila mmoja anaweza kuingia kwenye levo ya Nafsi na matumaini ya kuweza kupata mtoto yangekuwa juu.
Upande wa Amina msukumo wa ndani zaidi kujifunza mafunzo hayo ni kwa ajili ya kutunza urembo wake na kufanya tahajudi muda mrefu haikuwa kazi kubwa kwake, ,ijapokuwa maendeleo yake yalikuywa ya taratibu lakini alileta matumaini na hata hivyo Roma alifurahi kuona Amina alikuwa mzoefu wa mazoezi ya Yoga na hilo ndio lilirahisisha.
Neema Luwazo ndio ambaye alikuwa akijifunza kwa fujo sana na tamaa kubwa ya kufikia levo za juu na Roma aliona huenda ni kwasababau alikuwa akiukaribia utu uzima ndio maana alitaka kupanda levo kwa haraka ili asiendelee kuzeeka na kubakia na mwonekano wa ujana.
Lakini licha ya fujo alizokuwa nazo za kutaka kujifunza maendeleo yake yalikuwa ni ya taratibu mno kulinganisha na wengine wote kutokana na utu uzima wake kwani ilikuwa rahisi kwa vijana kujifunza na kupanda levo kwa haraka tofauti na watu wazima na Roma ilibidi achukue jukumu la kumtuliza.
“Roma nimeachia majukumu kabisa ya kampuni kwa Alhaji kwa ajili ya kujifunza”Aliongea Neema usiku Roma alipomtembelea.
“Umefanya vizuri lakini unatakiwa kwelewa mbinu hizi huwa zinaendana na utulivu wako wa akili ukiwa na tamaa ya kupanda levo kwa haraka utakosa utambuzi wa kunyaka kila viashiria vinavyokujia wakati wa kufanya Tahajudi na ndio maana nakushauri usichukulie sana hili swala siriasi lifanye kama ni moja wapo ya starehe, kama unavyokaa kwenye Jakuzi ukiwa umeshikilia glasi ya mvinyo ukiyafurahia mafanikio yako”Aliongea Roma nakumfanya Neema kutabasamu.
Na alfajiri Roma alijaribu kufanya nae mafunzo na sasa angalau aliona akili yake ilikuwa imetulia , ilionekana maneno yake ya jana usiku yalikuwa yamefanya kazi.
Upande wa Edna na Nasra maendeleo yao yalikuwa ya kinyonga lakini yalioleta mabadiliko kwenye miili yao.
Zamani Edna alikuwa akimhofia Lanlan kumrukia kutokana na uzito wake lakini kwa kipindi chote alichokuwa akichukua mazoezi alikuwa ameimarika na kumudu hata uzito wa Lanlan vizur.
*******
Ni baada ya wiki moja kupita hatimae Omari na Queen waliweza kufunga ndoa yao rasmi kwa tamaduni za dini ya kiislamu ambazo zilimtaka Queen kubadili dini jambo ambalo Mzee Alex hakupinga, hata hivyo ni Omari pekee ambaye alionyesha kumpenda mtoto wake kwa mapenzi ya dhati licha ya kwamba alikuwa mjamzito hivyo hata swala la Queen kubadili dini kuwekwa mezanni kwake hakuwa na kipingamizi.
Saa tano na nusu za usiku ndio muda ambao Roma na Edna walirudi kutoka kwenye sherehe ya harusi hio ya Omari na Queen na wakati Roma anaingiza gari ndani ya geti alishangazwa kuona nyumba bado inatoa mwanga wa taa kutokea sebuleni kwani kwa muda huo aliamini wanafamilia wote wangekuwa washalala.
Roma usiku huo akiwa njiani alikuwa akipanga kwenda kuburudika na mke wake Edna usiku kucha kwa kuamini muda huo Lanlan angekuwa tayari amekwisha kulala na Qiang Xi.
Lakini sasa ile wanaingia sebuleni lile tumaini lake lote lilipotea baada ya kumkuta Qiang Xi na Lanlan wakiwa wamekaa sebuleni na hata Edna mwenyewe alishangaa kuwakuta hapo kwani muda ulikuuwa umeenda.
“Qiang mbona mpaka muda huu Lanlan hajalala na asubuhi anatakiwa kuwahi kuamka”
“Madam nimejaribu kumfanya alale lakini hana usingizi na anasema anakusubiria”Aliongea Qiang Xi huku akionyesha hali ya uchomvu ilionekana alikuwa akijitahidi kuwa macho kwasababu ya Lanlan na alikuwa amechoka.
“Lanlan kwanini unashindwa kulala?”
“Mama sipati usingizi , Lanlan anataka kulala karibu na mama”Aliongea na kumfanya Roma akunje sura alijiambie kama watoto wake watakuja kuwa kama Lanlan basi maisha yake yangekuwa magumu sana.
Edna alimuonea huruma kuona alikosa usingizi na swala hilo lilikuwa likimsumbua kichwa namna ya kulitatua kuishia kujiuliza kama siku nyingine asingekuwepo na Lanlan angelala vipi.
Upande wa Roma alishajua kwanini Lanlan alikuwa akikosa usingizi , sababu ilikuwa ni kutokana na damu yake kuchemka kila wakati na kumfanya kukosa utulivu wa akili ndio maana alikuwa akikosa usingizi na njia pekee ambayo aliona huenda ingemsaidia Lanlan ni kumfundisha ya mbinu ya kimaandiko ya urejesho ili aweze kudhibiti uwezo wake lakini alimuona Lanlan ni mdogo na hata kama angejaribu kumfundisha kutamka maneno ya maandiko na kuyageuza kuwa nguvu ingekuwa ngumu kwake.
Hivyo suluhisho la muda mfupi ambalo aliona lingefaaa kwa muda huo ni Lanlan kuendelea kulala na Edna mpaka atakapogundua namna ya kumsaidia kupata usingizi bila ya uwepo wa Edna.
Roma mara baada ya kurudi kwenye chumba chake akijiandaa kwenda bafuni kujimwagia maji alale simu yake ilitoa mlio wa ishara ya mwaliko wa mtu kumpigia kwa njia ya Vidio Call.
Baada ya kuangalia inatoka kwa nani aligundua ni Sauron na alijikuta akiwa na shauku ya kumsikia maana ni kama mwezi unakaribia kuisha tokea ampatie Sauroni kazi ya kusambaza vijana kutafuta maeneo walioishi binadamu enzi za kale , maeneo ambayo yalifanikisha ukuaji wa mila na tamaduni za kijamii za mwanzo kabisa(Ancient Civilization) lakini baada ya muda maeneo hayo yakatelekezwa , aliamini upatikanaji wa maeneo hayo ingekuwa rahisi kwake kuweza kupata mimea anayojitaji itakayosaidia katika utengenezaji wa vidonge vya kijini.
SEHEMU YA 496.
Licha ya mwonekano wa kutisha kutokana na mtindo wake wa nywele nyingi alizokuwa nazo kwa upande wa Roma alikuwa ashamzoea na kumuona mtu wa kawaida lakini kwa mwingine huenda mwonekano wa Sauroni ungemkosesha amani hususani wakati anapokuwa siriasi.
Ilionekana muda huo Sauroni upande wa kwao kulikuwa ni mchana maana alionekana ndani ya ofisi huku kwenye meza yake kukiwa na mafaili mengi, huku yeye mwenyewe akiwa amevalia miwani ya kusomea.
Roma mara baada ya kupokea simu na kubadilishana salamu na Sautoni ilibidi amwambie aende moja kwa moja kwani alitaka kulala.
“Mfalme Pluto nishakutumia mafaili yanayohusiana na taarifa ulizo omba kupitia barua pepe yako , tumefanikisha kupata maeneo nane yanayofanana na sifa ulizotupatia”Aliongea Sauroni
“Asante sana Sautoni kwa juhudi zako zilizopelekea kufanikisha , vipi kuna changamoto yoyote uliweza kupata?”
“Sijapata changamoto kubwa mfalme Pluto lakini nina shauku ya kufahamu kwanini unahitaji taarifa za hayo maeneo kwani kwa uelewa wangu hayo maeneo sasa hivi hayakaliwi na binadamu na huenda hata uwepo wa hio mimea ni kwasababu hio na binadamu wa kawaida ambaye angesafiri kwenda kwenye hayo maeneo asingeweza kutoka hai”Aliongea na kumfanya Roma kucheka kidogo
“Maeneo ambayo watu waliishi na sasa hawaishi ndio ambayo ninayatafuta kwani naamini inaweza kufanikisha kupata kile ninachohitaji , najua una shauku lakini nitakuelezea siku nyingine kwasasa taarifa hii ulionitumia nitaipitia na kuanza na mikakati ya kuelekea huko”Aliongea Roma na Sauroni aikubali na kisha akakata mawasiliano
Roma alighairi kwanza kwenda kuoga na kuanza kupitia taarifa ambazo ametumiwa na Sauroni na ilionekana ziliandikwa vizuri ili kueleweka kwa urahisi, ni ‘Document’ ambayo ilikuwa na peji nane ambazo zilikuwa zikielezea maeneo husika ambayo yalikuwa yakikidhi vigezo.
Na mpaka anakuja kumaliza alikwisha kupata sehemu ambayo aliona inafaa kuanzia kutafuta mimea hio lakini kwakuwa hakuwa mzoefu sana alitaka kwanza kusikia maoni kutoka kwa Rufi na kwasababu muda huo ulikuwa ni usiku sana aliona angewasiliana nae asubuhi.
Siku iliofauta jambo la kwanza ilikuwa ni kuwasiliana na Rufi na akamtumia na faili la taarifa alizotumiwa na Sauroni na wote walijikuta wakiachana na baadhi ya maeneo yalio orodheshwa kwa sababu za aina moja, waliachana na eneo la Eveglades ambalo lipo kusini mwa Marekani , Msitu wa Panama , msitu wa Amazoni na maeneo mengine na wakaja kuchagua eneo lililofahamika kwa jina la Arnhem Land ambalo lipo kaskazini mwa bara na nchi ya Australia.
Arnhem Land ni eneo ambalo walichagua kutokana na historia yake kwani sio tu kwamba miaka ya hivi karibuni halikukalika lakini miaka mingi iliopita lilikaliwa na watu wa asili zaidi wa nchi ya Australia na ilikuwa ni eneo ambalo ni kama tamaduni nyingi zilizaliwa na hivyo ndio vigezo ambavyo Rufi alipendekeza.
Eneo ambalo lilikaliwa na watu wa asili na kuzaa tamaduni na mila ndio ambalo lingekuwa na mkusanyiko wa nguvu nyingi za kiroho ambazo zingefanikisha upatikanani wa malighafi za Alchemy.
Roma alikuwa akielewa Australia ilikuwa kusini mwa ncha ya dunia na kwa mwezi huo wa nne kwenda wa tano ni kipindi cha Vuli na kama angevuta muda vuta muda basi mwezi wa sita ingekuwa ni hatari zaidi kwenda kwani ingekuwa ni kipindi cha baridi kali na kwasababu hakuwa akienda mwenyewe alitakiwa pia kuzingatia hali ya kiafnya ya Rufi na ndio maana aijiambia ni kheti kuharakisha kufanya safari na kwenda kutafuta hio mimea na kuanza harakati zingine.
Rufi alikuwa ashakubali kuongozana nae kwani hakuwa na shughuli ya maana ya kufanya Tanzania na maisha yake yalikuwa ya upweke sana na aliona ingekuwa kama utalii kwake kusafiri mpaka Australia.
Tatizo ambalo Roma aliona ni changamoto ambayo alipaswa kuitatua ni kwa mke wake , alijua akimuaga kwamba anaelekea Australia na Rufi angemuwekea ngumu lakini hata hivyo aliona lazima akubaliane na matakwa yake kwani anachokifanya sio kwa faida yake mwenyewe bali ni kwa faida ya wote.
Usiku baada ya Roma kupata chakula aliona ndio wakati muafaka wa kumweleza Edna mpango wake wa kusafiri na Rufi na Roma alimsubiria kwanza Edna amalize kumwandaa Lanlan kwa ajili ya kulala na ndio aongee nae.
Roma mara baada ya kukaa chini na kumuelezea anachopanga mwanzoni hakushangazwa na taarifa hio lakini Roma alipokuja kusema anataka kwenda na Rufi alihisi hatari.
Tokea aanze kuwa na ukaribu zaidi na mume wake alikuwa mwangalifu mno hakutaka Roma aongeze mwanamke kabisa na ndio maana hakutaka mazoea kati ya Rufi na Roma kuongezeka kwani mwisho wake usingekuwa wa kheti kwake.
“Najua unaweza kuona sio sawa mimi kwenda na Rufi lakini hili ni swala ambalo napaswa kulifanya na hata hivyo Arnhem sio sehemu ambayo ipo kiburudani ni kama gereza na kila kitu ni msitu hivyo kwenda na Rufi kule ni kama nampeleka kuzimu, hivyo mke wangu usiwe na wasiwasi na toa ruhusa yako niweze kuondoka nae”Aliongea Roma kwa unyenyekevu baada ya kuona mabadiliko yake.
Edna alifikiria na alionekana kama mtu ambaye amechanganyikiwa, moyo wake siku hizo za karibuni ulikuwa tofauti na zamani, alikuwa tayari kuona Roma akiendelea na wanawake wale wale aliokuwa nao na asione wivu lakini kumuona mwaamke mwingine mpya kwake ilimuuma na kumuogopesha kwa wakati mmoja na hata yeye mwenyewe alijishangaa na hata Roma alivyoweka wazo hilo akili yake ilimwambia na yeye aungane nae ili aweze kumlinda vizuri , lakini alifikiria uwepo wa Lanlan aliona asingeweza kuongozana na Roma na kumuacha peke yake.
Wazo moja tu ambalo lilimjia katika akili yake na kuona ndio njia mbadala ni kumteua mtu mwingine wa kuongozana nae kwenda huko na ingekuwa rahisi kuzuia mahusiano kuibuka zaidi na zaidi
“Nimekubali unaweza kwenda nae lakini lazima uende na mtu mwingine pia”Aliongea Edna na kumfanya Roma kushangaa.
“Mtu mwingine kwenda nae sio tatizo kwangu , nani unaona anafaaa kunisindikiza?”
“Mage”Aliomngea akiwa ni mwenye sura iliojaa usirias na kumfanya Roma moyo wake kupiga kite , alikuwa na mahusiano na Mage lakini alikuwa akiyafanya siri Edna asifahamu.
“Unashangaa nini Mage ndio mtu pekee ambaye unaweza kwenda nae ningewaruhusu mwingine lakini kwa walivyokuwa wadhaifu kwako wasingeweza kukuzuia kufanya jambo la kishenzi?”Aliongea na kumfanya Roma kukuna kichwa.
Roma alikuwa na mahusiano na Mage lakini hakuwahi luyaweka wazi na ndio maana alikuwa kwenye mshangao bara baada ya Edna kutaja mtu wa kuongozana nae kwenda Australia kuwa Mage, hali hio ilimfanya kuvhanganyikiwa yeye mwenyewe kwa kuona Edna alikuwa akifahamu siri yake halafu alikaa kimya.
"Mbona uko hivyo au Mage hafai ?"
"Sio kwamba hafai lakini kuna ulazima wa kutangulizana na mwanamke?"
"Ndio nataka utangulizane na mwanamke tena mwanamke huyo akiwa Mage ndio mtu pekee ambaye anaweza kukuzuia usifanye ujinga na Rufi na ndio sharti langu"Aliongea
"Edna ulifahamu lini?"
"Kuhusu nini?"
"Mimi na Mage tuna mahusiano" Aliongea Roma kwa ujasiri lakini kwa hofu ndani yake na swali lake lilimfanya Edna kucheka kidogo kwa uchungu.
"Hilo swali muulize Mage mwenyewe atakuwa na majibu" Aliomgea Edna na kisha hakutaka mazungumzo zaidi na kuondoka kwenye chumba hiko cha kujisomea na kumuacha Roma bado akiwa kwenye sintofahamu.
Ni kweli alikuwa na mahusiano na Mage lakini siku zote alikosa ujasiri wa kumuweka wazi Edna , lakini alishangaa Edna kutambua juu ya hilo bado lakimi aka kaa kimya bila ya kuzungumza.
Roma alijiuliza Edna alifahamu lini maana kama ingekuwa ni siku hio basi huenda angemnunia siku nzima lakini ajabu walikuwa sawa na hata siki yao iliisha bila shida.
Ila kitendo sasa cha Edna kuondoka wakiwa hawajamaliza mazungumzo alijua lazima angekuwa na hasira na yeye kutokumuambia ukweli lakini hata hivyi asingejuwa namna ya kujitetea kama hajui ni lini ameweza kujua ukweli.
Roma hapohapo aliona majibu ayapate kuroka kwa Mage mwenyewe , muda ulikuwa umeenda lakini alijua lazima Mage atakuwa macho na kweli baada ya simu yake kuita muda mfupi ilipokelewa haraka.
"Babe Mage mbona kama ulikuwa ukisubiria simu yangu"
"Mh ..! Roma vipi kuhusu Edna"
"Edna ana nini?"
"Mama leo kaharibu kila kitu"
"Kaharibu nini??"
"Sijui kaongea nini na Mkeo ila kamwambia kuhusu sisi baada ya Magdalena kakataa mchumba anaetaka kumuoa...."
Kwa maelezo ya Mage ni kwamba mtoto wa waziri wa sayansi na teknolojia afahamikae kwa jina la Jumbe alifika nyumbani kwa Mage na kuweka nia yake wazi ya kutaka kumuoa Magdalena jambo ambalo lilipokelewa kwa mikono miwili na Mama T.
Mwanamama huyu alikuwa ashachoshwa kuona watoto wake wa kike wakikosa ndoa ilihali wakina mama ambao ni marafiki zake watoto wao walikuwa wakiolewa na kuoa kwa sherehe kubwa na yeye kuishia kutoa michango pekee.
Na kilichompa shida zaidi ni kila mara alipofikiria Mage hawezi kuolewa tena kwa kuamua kuwa mchepuko wa Roma jambo ambalo hata mume wake alilibariki hivyo tumaini lake kubwa ilikuwa ni kwa Magdalena.
Alielewa watu wakiona Mage hajaolewa wangemnyooshea vidole na kumsema lakini kwasababu ilikuwa ni kwa ajili ya furaha yake hakutaka kumzuia lakini jambo hilo hilo hakutaka kuona likitokea kwa Magdakena pia na ndio maana Jumbe alupoweka nia yake wazi ya kutaka kumuoa mtoto wake alipokea taarifa hio kwa mikono miwili.
Lakini sasa kilichomshangaza ni baada ya Magdakena kukataa akisema hawezi kuolewa na Jumbe kauli ambayo ilimfanya kuhisi uchizi.
"Magdalena kama humtaki Jumbe inamaana tayari una mchumba kama ni hivyo mlete tumuone na nikiridhika nae nitakuruhusu uolewe nae" Aliongea Mama na kumfanya Mage aliekuwa amekaa upamde wa kushoto kushindwa kuongea chochote na kumuonea huruma dada yake kwani alikuwa akijua kike kilichokuwa kikiendelea kwenye moyo wake.
"Mama sina mchumba ila sipo tayari kuolewa na Jumbe" Alijibu Magdalena na kumfanya Mama T kushindwa hata kuelewa watoto wake wamekumbwa na nini , kwenye maisha ykje alijitahidi kuwalea kimaadili na kutegemea waje kuolewa na kuwa na furaha kakini imegeuka kuwa tofauti .
"Mume wangu mbona huongei chochote jamani hawa watoto wanataka kunitia uchizi?"
Afande Tobwe alikosa cha kusema kabisa kwani alikuwa ashajua muda mrefu sababu ya Magdalena kukataa ndoa na Jumbe , alikumbuka vizuri siku ya Roma alipokuwa akipambana na Yan Buwen namna ambavyo Magdalena alitaka kumuokoa Roma kwa kujitoa Muhanga yeye mwenyewe uhai wake.
Kwanzia kipindi hiko alikuwa akishindwa kujua tatizo la Magdakena linaisha vipi , kwenye maisha yake licha ya kuwa mwanajeshi likija swala ka familia yake alikuwa akizingatia zaidi watoro wake waje kuishi na furaha na ndio maana hata Mage alipo onyesha kuwa na mapenzi na Roma hakusita kumruhusu licha ya kujua Roma ana mke tayari na mwanae angekwenda kuwa mchepuko tu, lakini swala la Magdalena ilikuwa ngumu kumruhusu kuwa na mahusiano na Roma na wakati huo na pacha wake akiwa na mahusiano na Roma.
Jambo hilo kama angeruhusu jamii isingemuelewa na sio hivyo ru hata dini yake ilimzuia kuruhusu kitu kama hiko.
"Magdalena kama huna mahusiano, Jumbe anakufaa usikatae , najua kwa zama za sasa wazazi hawapaswi kuwachaguliwa watoto wao wachumba lakii siku zote mzazi anamuombea mtoro wake kuwa na furaha hivyo kuelewa ni kipi bora kwako , Jumbe anakupenda hivyo hata kama humpendi utajifunza"Aliongea Afande Tobwe kwa usiriasi na kisha akaamka na kuondokaneneo hilo la sebuleni.
Huku nyuma akiacha sura ya Magdalena kuwa katika hali isioelezeka , alitarajia baba yake kumuunga mkono lakini akaishia kumkandamiza kwa.kusimama upande wa mama yake.
Wakati wa mchana Edna alipofika dukani kwa ajili ya kutafuatilia mwenendo wa mauzo ya mavazi alioingiza sokoni kupitia kampuni yake kwa kutumia malighafi mpya ndio alipokutana na Mama T.
Walikuwa hawajaonana muda mrefu tokea Edna asafiri kwa ajili ya harusi yake hivyo waliongea sana huku Mama T akitaka kuona Edna alipendezaje na katika mwendelezo wa stori ndipo Mama T alipojikuta akiropoka kuhusu mtoto wake Mage kuwa na mahusiano na Roma.
Mwanzoni Edna alihisi kuna kitu kinaendelea kati ya Mage na mume wake lakini alikosa ushahidi wa wazi wa kuthibitisha kile anachowazia.
******
Upande mwingine nchini Rwanda mheshimiwa Jeremy alikuwa akizunguka zunguka kwenye ofisi yake huku na huko akionyesha kama mtu mwenye hasira nyingi na hio yote ni mara baada ya kupata taarifa ambazo zilithibitisha Kizwe ndio ambaye alimtorosha Desmond hospitalini wiki kadhaa zilizopita.
Raisi Jeremy mara baada ya kumtoa Desmond Tanzania moja kwa moja alimsafirisha mpaka India kwa ajili ya matibabu , hakuwa akiamini maneno ya daktari wa Tanzania kwamba mtoto wake hawezi kupona kiungo chake cha uzazi na ndio maana alikuwa radhi kufanya lolote kwa ajili ya mtoto wake huyo na isitoshe ndio ambaye alikuwa ni mrithi wake akitaratjia siku za usoni kumwachia nchi aiendeshe , lakini akajiuliza kama Demsond hatokuwa na uanaume wake je angeweza kuendesha nchi kisawasawa na jibu lilikuwa hapana.
Upande wa Desmond mara baada ya kushituka katika kupoteza fahamu na kujua hakuwa na uwezo tena wa kumfanya chochote mwanamke wakiwa kitandani alilia sana na kuomboleza na maumivu yake yalikuwa ni zaidi ya siku aliopokea taarifa za kifo cha mama yake.
Mpaka muda huo alijiona hakuwa ni wa thamani tena kama mwanaume na ndio maana alijawa na huzuni isiokuwa ya kifani huku lawama zote akimwangushia baba yake mzazi ,kwani aliamini kama sio matendo yake basi huenda asingepatwa na kadhia hio.
Ilikuwa ni adhabu kubwa mno ambayo Roma alikuwa amemfanyia , ilikuwa ni zaidi ya kifo kwake na hakujiona wa thamani kabisa.
Hata pale raisi Jeremy alipomtembelea katika wodi aliolazwa hakutaka kumuona kabisa na alitangaza waziwazi kwamba anamchukia na hali ilio iliamsha sana huzuni kwa Raisi Jeremy ,hakujua ni kwa namna gani angemsaidia mtoto wake kupona kwani alishakuwa tayari Eunuch ,kwa mtazamo wake hata kama angetaka kulipiza kisasi kwa Roma asingeweza na pia ingekuwa laana kwake kushindana na mkwe wake.
Kuna muda aliona huenda matendo yake ndio yaliokuwa yakimfikisha katika hali kama hio, alikuwa na mafanikio katika uongozi wake lakini likija swala la familia alikuwa amefeli pakubwa na alijiona kama mtu ambaye hakuwa na bahati.
Madaktari wa kihindi walijitahidi kufanya juhudi za kila namna ili kumponyesha Desmond tatizo lake lakini majibu hayakuwa na tofauti sana na yale ambayo yalitolewa Tanzania.
Kwa ufupi ni kwamba mtoto wake hakuwa mwanaume mwenye makali tena , taarifa ambayo ilikuwa mbaya sana na kuishia kumlaani Roma kwa kumfanyia hivyo mtoto wake.
Wakati akiendelea kutafakari namna gani ya kumsaidia Desmond akiwa nchini India kwa siri, ndipo alipopokea taarifa za Desmond kutoweka hospitalini kwa hali isiokuwa ya kueleweka jambo ambalo lilimshangaza mno na sio kwake tu hata vitengo vya ulinzi vya hospitali vilishangazwa na jambo hilo kwani hakukuwa na Kamera yoyote ilionasa tukio la Desmond kutoroshwa na kitu kingine zaidi ni kwamba CCTV Kamera zote zilikuwa zikifanya kazi.
Kwa maelezo hayo mafupi alioyapata Raisi Jeremy alijua moja kwa moja Kizwe atakuwa anahusika katika hilo.
Tokea siku ambayo aliweza kupata taarifa za Kizwe kuwa hai kutoka kwa Linda ilimshangaza sana Raisi Jeremy kwani ilikuwa ni taarifa ambayo kwake ni kama anaambiwa mfu kafufuka , alishuhudia yeye mwenyewe kifo cha mke wake na kumuona akizikwa inakuwaje akawa hai.
Linda hata yeye mwenyewe alishindwa kuamini kama Kizwe alikuwa hai , aliweza kupata kuigundua sura ya Kizwe siku kadhaa wakiwa wanafanya uchunguzi ndani ya chuo cha taifa cha Rwanda mara baada ya Lekcha kupotea na walipoangalia kamera za Chuo ndio walipoweza kuona sura ya mwanamke anaefanana na Kizwe kabisa akiwa katika ujana.
Tena inasemekana wakati Kizwe anaondoka na Lekcha katika chuo hicho Kizwe aliangalia Kamera ya ulinzi na kisha akatabasamu kifedhuli na kutamka maneno kwa namna ya kuonyesha ishara za midomo yake, alifanya hivyo kama mtu ambaye aliamini kabisa Footage za sura yake zingemfikia Jeremy.
Katika rekodi hio ya camera Kizwe alikuwa akionyesha ishara kama ya kumtahadharisha Jeremy kwa kumwambia kwamba anarudi kulipiza kisasi.
Baada ya taarifa ya mwanamke anaefanana na Kizwe kumfikia raisi Jeremy kwanza kabisa hakuamini na aliweza kupitia hatua zote tano za mshituko ili kujibu hali ya taarifa hio na baada ya masaa mengi ya kufikiria ndio uamuzi wa kufukuliwa kaburi(exhumation) la Kizwe kwa siri sana ufanyike nyakati za usiku kazi ambayo iliongozwa na Linda.
Na ilichukua siku tatu kwa mchakato wote kumalizika na mara baada ya raisi Jeremy kuwekewa majibu mezani alijikuta akipagawa , mwili ambao ulifukiwa haukuwa wa mke wake Kizwe kwani vinasaba vilithibtisha hilo.
Sio kwake tu ambaye alishangazwa na hilo lakini hata Linda pia alishangaa na kutaka kuthibitisha hilo na hapo ndipo walipoanza kuwasiliana na wanasayansi na vitengo vya serikali nyingine ili kuweza kuthibitisha uwezekano wa mtu aliefariki kufufuka na katika majibu mengi ambayo walipokea moja wapo ni kesi ya siri sana iliomtokea raisi mstaafu wa China lakini kesi hio hio ikajirudia nchini Tanzania baada ya mwili mtoto wa tajiri wa makampuni ya Maya kuonekana akiwa hai mara baada ya kifo chake kuthibitishwa.
Taarifa zilikusanywa kwa kutumia idara za kitelijensia na zilipomfikia Raisi Jeremy ndipo alipotambua sasa jina la mwanasayansi Yan Buwen ambaye alikuwa amepewa hifadhi ya kufanya majaribio yake nchini Tanzania.
Intellijensia ya Rwanda iliweka kila kitu wazi na kweli Yan Buwen wakati wa maombolezo ya kifo cha Firsr lady alionekana kuingia nchini Rwanda , muunganiko huo wa matukio ndio ulikamilisha uchunguzi wa kuamini Kizwe alikuwa hai bado na aliehusika kumrudisha hai ni Yan Buwen.
Na Raisi Jeremy alijiona mjinga kwa kuona alizidiwa akili na mke wake na hata kitendo cha Lekcha kumbakisha hai ulikuwa pia ni mpango uliosukwa , hatari aliweza kuiona mbele yake na kuanza kumuogopa Mwanamke aliekuwa ni mke wake na hata ulinzi wake aliongeza maradufu huku akihakikisha Desmond mtoto wake hafahamu ukweli wowote kuhusu hilo.
Asichokijua raisi Jeremy ni kwamba Desmond ndio moja wapo ya watu walioshuhudia mama yake mzazi akifufuliwa na Yan Buwen na hata nyakati za maombolezo ya taifa alikuwa akijifanyisha tu kuwa na huzuni.
Baada ya kifo cha raisi Kigombola pamoja na Yan Buwen Raisi Jeremy alipata unafuu na safari yake ya kuhudhuria maziko ya raisi Kigombola ilikuwa na sababu ya ziada ambayo ni kuona uwezekano wowote ambao ungemkutanisha na mke wake.
Siku ambayo Fredi aliandaa Party ya kusherehekea siku yake ya kuzaliwa na Edna na Roma kualikwa ndio siku ambayo pia hata yeye mwenyewe aliweza kupokea ujumbe kutoka kwa Kizwe akimwambia afike Maple speed Resort kama anataka kuonana nae.
Lakini Kizwe hakuwa na mpango wa kuonana na Jeremy bali aliandaa mpango wa kumfanya Jeremy kushuhudia Kaka akimbaka mdogo wake kwa macho yake lakini kwa bahati mbaya mpango wake huo ukaja kufeli mara baada ya bangili aliovalishwa Edna kuingilia kati na matokeo yake ni Desmond kuharibiwa uanaume wake.
Sasa zikawa zimepita siku kadhaa tokea Desmond apotee nchini India huku akiamini moja kwa moja muhusika ni Kizwe ambaye amebadilika na kuwa wa tofauti sana , sio tu kwamba alikuwa amefufuka lakini pia akarudi ujana.
Asubuhi hio aliokuwa akizunguka katika ofisi yake ni mara baada ya Kizwe kumthibitishia Jeremy kwamba yupo na Desmond na ajiandae kuachia uongozi wa nchi , kauli ya Kizwe kwake ilikuwa kama ya vitisho na ndio maana alikuwa na hasira na kuzunguka huku na huko huku akikosa namna ya kumshughulikia mwanamke huyo ambaye muda huo hakumuona kama mke wake tena bali alimuona kama shetani.
Mbaya zaidi aliogopa kwa kuamini na Desmond atakuwa amejazwa ujinga na mama yake kwa wakati huo .
Ilikuwa kama laana kwake kwa baba wa familia kushindana na familia yake na jambo hilo lilimkosesha amani kabisa.
ITAENDELEA.
... mwandishi anaupiga mwingi kama YangaMatendo ya mapacha yanasikitisha. Haya ni matokeo ya KUWADEKEZA ktk malezi.
Boss Edna anao moyo kwa kweli. Michepuko ya Mfalme Pluto inamtia jakamoyo na simanzi ya hasira.
Ulinzi kwa Familia ndicho kipaumbele kwa kila Baba. Roma anauweka rehani usalama wa familia yake kutokana na arrogance na hivyo kuongeza wigo wa maadui.
Rufi ana lake jambo. Pamoja na kuleta hadithi za kuhuzunisha, shabaha ni kumnasa Roma na hatimaye kumtia msuko suko mkubwa atakapofika milki za Majini.
Hata hivyo, mwandishi na mtunzi ameonesha kipaji cha hali ya juu ktk kupangilia matukio na hivyo riwaya kuwa na mtirirko mzuri na hivyo kistahili PONGEZI nyingi sana.
Adios.
Anakera sana huyu jamaa,nakuteteaga lakini unakera,jibu sms za inbox... mwandishi anaupiga mwingi kama Yanga
HatariSEHEMU YA 568.
Stern mara baada ya kuona kitu kibaya kinakwenda kutokea , palepale alisogea na kumshika Ares ili asije kuleta malumbano na Magdalena.
“Kwasababu ni mwanamke wa karibu na Hades basi ni mmoja wetu , Ares hasira zako za haraka haziwezi kubadilika hata kama utapewa miaka elfu therathini ya kuishi , kwasasa wote turudini hotelini muda ambao Poseidon na Hermes watafika hapa tutasalimiana na marafiki zetu”Aliongea Stern
“Nitaacha hili lipite kwa leo”Aliongea Stern huku akimwangalia Magdalena kwa hasira kubwa na kisha akaondoka katika hilo eneo.
*********
Anga la Norway katika bahari licha ya kwamba kulikuwa na jua lakini bado kulikuwa na ubaridi wa aina yake.
Mbele yake ni bahari isionekana mwisho wake , na alichoweza kuona ni mawingu ambayo yanatawanyika kila pande.
Usiku ulikuwa ushapita tayari , Roma alikuwa ametafuta katika kila sehemu ambazo hazikuwa na watu wengi sana na kutofikika kwa urahisi hususani milimani na katika pembezoni mwa bahari katika maeneo yote ya Kaskazini mwa Ulaya
Alianzia Gotland katika bahari ya Baltic akaeda Stockholm halafu Oslo na Bergen , katika maeneo yote hayo kulikwa na vituo nane ambavyo vyote vilikuwa ni vya kimitengo ambavyo vimetengenezwa na wahalifu ili kuchanganya watu wanaowatafuta.
Roma aliweza kupata moja wapo ya kambi ya siri katika kijiji kimoja lakini licha ya hivyo hakuweza kuona dalili yoyote ya majaribio ya sayansi ya nyuklia .
Mpaka hapo aliona kabisa ilikuwa sahihi kuja yeye kutafuta , kwani kama ni watu wake wasingefanikisha chochote, yeye licha ya spidi yake kubwa lakini bado tu hakuwa amefanikisha kumpata Clark.
Roma alitoa simu maalumu aliokabidhiwa na Sauron ili kuwasiliana nae moja kwa kwa moja kupitia satilaiti.
“Sauron wapi kumebakia?”Aliuliza.
“Mfalme Pluto kutoka bahari ya Norway kwenda Kaskazin kuna kituo katika eneo la Wilwick na ukielekea magharibi zaidi kuna meli inayoelekea Iceland na nyingine inaelekea Nuuk Greanland , Kusini kutoka sehemu ulipo pia kuna kituo cha Rotterdam nchini Uholanzi , Leipzig nchini Ujerumani , Marseille nchini Ufaransa na Lodz nchini Poland na kuendelea”Aliongea Sauron kupitia simu na kumfanya Roma kung’ata meno yake kwa hasira.
“Pumbavu kabisa yaani wamefanya makusudi kutengeneza vituo hewa vingi ili wasikamatike kirahisi”.
Ukumbuke hapa kwamba Roma anachofatilia ni uelekeo wa madini adimu yalikosafirishwa hivyo vituo anavyozungumzia Sauron ni vile ambavyo wanaamini meli iliosafirisha mzigo ilisimama.
Kama kutakuwa na sehemu meli imesimama na kushusha mzigo moja kwa moja ingemaanisha kwamba katika ukanda huo wote kutakuwa na maabara ya siri na hicho ndio ambacho Roma alikuwa akitafuta.
“Mfalme Pluto nafikiria kwamba tachane na baadhi ya vituo , kwa mfano maeneo ya Ufaransa yapo karibu sana na bahari ya Mediterranian na yana idadi kubwa ya watu hivyo kukosa sifa kujificha na uwezekano wa wao kufanyia majaribio ya sayansi ya nyuklia katika maeneo hayo , lakini pia hawawezi kuyachagua kwani wangehofia kukamatwa haraka na jeshi , hivyo nashauri uelekee upande wa magharibi na mimi nitaamrisha vikosi kutafuta upande wa miji ya Kaskazini”
“Mimi nashauri tufanye kinyume chake , tutaanza kuafuta kutoka katika latitiudo za chini kwenda latitudo za juu , miji na maeneo ambayo yapo zaidi karibu na bahari ya Mediterranian tutaanza kutafuta huko kwanza”
“Mfalme Pluto unadhania kwamba wamefikiria kinyume makusudi kuchagua maeneo ambayo sisi hatwezi kufikiria kama wameyachagua si ndio?”
“Haiwezi kuwa rahisi Sauron , nakumbuka umesema haiwezekani kwa maabara kuwepo katika watu wengi waliozagaa , njia zuri kwa kundi la watu wengi kama hao kujificha basi kwa angalau miaka ni katika maeneo ambayo yana idadi kubwa ya watu, kwahio nafikiri maeneo sahihi ya kutengeneza maabara ni katika maeneo hayo , hata hivyo kwasasa ni makisio yangu tu lakini tunaweza pia kuotea baadhi ya maeneo tofauti na kutafuta bila uelekeo”
“Uko sahihi nitawaagiza vijana kuanza kutafua upande wa kusini sasa hivi?”Aliongea Sauron na palepale walikatisha maongezi yao
Baada ya Roma kukata simu palepale aliichukua safari ya kuelekea Marseille nchini Ufaransa , ijapokuwa anakwenda kuonekana katika maeneo hayo kukiwa mchana kweupe lakini hakujali kama anaweza kuibua taharuki , alijiambia akifika katika hayo maeneo atatumia spidi kubwa kuzunguka ili hata kama kuna mtu atakae weza muona asiweze kuamini kama ni mtu bali maluweluwe.
Alikuwa akifikiria kinachoendelea Sicilly kwa muda huo katika mashindano ya Caesar Conference na kwa haraka haraka alijua mpaka muda huo mashindano hayo yatakuwa yamefunguliwa rasmi , lakini hata hivyo alijituliza kwa kujiambia hakuna baya ambalo linaweza kutokea kama tu Christen atakuwa ametaarifu miungu wenzake kufika katika.
*******
Wakati Roma akielekea Ufaransa upande mwingine katika jiji la Palermo karibu na bandari kulikuwepo na Colloseum kubwa ya kizamani iliokuwa imejazwa na makelele.
Ukumbuke Colloseum ni uwanja au Ulingo unaotumika kwa michezo ambayo huhusisha damu na hicho ndio ambacho kilikuwa kikienda kuanza ndani ya uwanja huo.
Ulikuwa ni uwanja mkubwa sana uliokaa kama duara na kwa upande wa nje ulionekana kama vile ni jengo la Ghorofa la froo nne liliojengwa kama duara.
Licha ya kwamba ni jengo ambalo lipo kama makumbusho lakini lilikuwa limefanyiwa maboresho makubwa na umoja wa makundi ya kimafia ya Sicilly kwa kazi maalumu ya kufundishia watu wao , kwa nje ni jengo lililoonekana kuwa na muundo wa kizamani lakini ndani yake lilikuwa na mwonekano wa kisasa zaidi kama vile kiwanja cha mpira.
Ni Ulingo uliokuwa ukiruhusu zaidi ya watu elfu therathini kwa mpigo na cha kushangaza sana asilimia kubwa katika siti zote hujazwa na wanajeshi wa makundi mbalimbali duniani ambao hushiriki.
Ukichana na watu hao kuwa wanajeshi lakini kwa jinsi walivyoketi katika viti vyao ni kama vile ni mashabiki wa mpira , kwani waliongea lugha mbalimbali na kufanya zogo kubwa kusikikika katika rafudhi mbalimbali.
Katika eneo la VIP , Magddalena na Rose walikuwa tayari washachukua siti zao mapema sana , katika eneo hilo alikuwepo Stern na dada yake Alice , vilevile alikuwepo mrembo Christen na kwa upande wa Ron na mtoto wake Fidero walikuwa wapo pembeni yao wakihakikisha kuwahudumia kwa kila kitu watakachotaka.
“Wanaanza kupigana saa ngapi ni zadii ya lisaa tokea sherehe za ufunguzi kumalizika?”Aliongea Rose aliekuwa na shauku ya kuona mapambano haraka iwezekanavyo.
“Unaonaje tukicheza raundi moja ya kadi ili kupoteza muda?”Aliogea Magdalena kwa kutania huku akicheka na kumfanya Rose kubetua midmo.
“Cheka uridhike mama, nimepoteza hela nyingi kwenye kamari lakini kwangu sio tatizo , wale watu hata hivyo walikuwa na maprofesheno kwenye kucheza kamari ingeshangaza mimi kushinda”Aliongea , ilionyesha siku ya jana alikuwa amepoteza hela nyingi sana.
“Oh! Miss Christen nimekumbuka , je napaswa kukuita Venus si ndio?”Aliuliza Rose.
Wakati huo Christen na Alice alikuwa wameshikiria jarida na fasheni na mitindo wakiangalia baadhi ya picha za nguo ambazo zimewekwa.
“Vyovyote utakavyoniita sawa tu lakini usije kuniita Venus kwenye kundi la watu”Aliongea.
Kitendo cha Rose kuwa karibu na Roma kwenye maisha yake kimemfanya kujua uwepo wa hao viumbe kutoka sayari nyingine ambao serikali nyingi duniani kubwa hujaribu kuficha uwepo wao.
“Nataka nikuulize swali , je unafahamu wale watu wa mavazi meupe?”
Baada ya kuulizwa swali hio alionyesha upande wa kulia kwake katika eneo la VIP , kulikuwepo na wanaume watatu waliokuwa wamekaa , alikuwepo Poseidon ambaye amevalia kombati za jeshi la Marekani lakini pia Ares na Hermes ambao walikuwa wamevalia suti na viatu vya ngozi wakiwa kawaida.
Majamaa hao hawakuwa wakipendelea sana kukaa karibu na wanawake kutokana na kwamba hawakupenda sana kuongea ongea lakini kitu kingine ukiachana na Hermes , Ares na Poseidon walikuwa wakifanana kitabia walikuwa wakipenda sana fujo.
“Angalia na wale wanasubiri kama sisi tu , tutaweza kuthibitisha wakati watakapotokea na isitoshe Hades hayupo hapa na Athena pia hayupo , haitakuwa rahisi kama tutaweza kukutana na maadui wetu wa zama zile”Aliongea.
Maneno yake ni kama yalizidi kumuongezea Rose shauku ya kutaka kujua watu hao ni wakina nani na alitamani muda huo hata Roma aweze kurudi mapema baada ya kumpata Clark , lakini akili yake haikuwa mbali na kufikiria kama kuna uwezekano wa kitu kibaya kimetokea.
Wakati wa watu kuanza kuchoka hatimae msherehesaji katika jukwaa maarufu alitangaza kwamba raundi ya kwanza ya mapigano ingeanza .
Kutokana na timu nyingi ambazo zilikuwa zikishiriki siku ya kwanza kulikuwa na raudi ya mtoano , kulikuwa na timu sita ambazo zilikuwa zinacheza kila raundi na kila mshindi atakae toka katika kila pambano basi atakuwa ameingia katika nafasi ya kucheza siku inayofuata.
Mkutano wa Kaisari mara nyingi huzuia mauaji ndani ya ulingo lakini kama itatokea kifo cha bahati mbaya au kumpelekea mshiriki kupata ukilema basi hawezi kukosa vigezo kuendelea na hayo ni makubaliano ambayo yanasainiwa na kila timu kabla ya kuanza.
Ukweli ni kwamba licha ya kwamba kuna makundi ya wanajeshi wapiganaji ambao walikuwa na asilimia ndogo za kushinda lakini walikuwa na uwezo wa kibunifu wa kuweza kutoroka pale wanapozidiwa na hilo limesaidia sana kupunguza mauaji yanayotokea katika ulingo kwa zaidi ya miaka nane mfululizo.
Uwanja ulikuwa umegawiwa katika maeneo matatu na muda huo mwanajeshi mmoja baada ya mwingine aliweza kutoka na kwenda kusimama katika eneo ambalo ameelekezwa.
Kulikuwa na ulingo tatu ambazo zote zilipaswa kila timu kupigana na mshindani wake katika mgawanyo wa timu mbilimbili.
Kilichomkatisha tamaa Rose ni kuona The Eagles sio timu ya kwanza ambayo imeanza katika randi hio , lakini palepale alionekana mtu mmoja aliekuwa kwenye mavazi meupe ambae aliingia katika ulingo akiwa peke yake na kuonyesha kutaka kushindana na timu ya watu watano.
Yaani mtu mmoja wa mavazi meupe alikuwa akitaka kudili na timu ya watu watano na ilifanya hali ya hewa kuwa katika ukimya wa hali ya juu kuangalia kinachokwenda kutokea.
Baada ya watu hao kujitokeza Christne na wenzake wote walijikuta wakisimama na kumwaangalia mtu yule kwa mshangao.
“It is real hem .. how did they come back”Aliongea Hermes akisema ndio wenyewe , wamewezaje kurudi.
“Kuna haja gani ya kuwa na wasiwasi , hili ni jambo zuri pia, kipindi kile tuliwaacha hai nadhani muda huu itakuwa nafasi nzuri kuwamaliza kabisa”Aliongea Ares.
Upande wa Poseidon yeye alionekana mwenye kujiamini wala kutokuwa na mshangao mkubwa na alikunja sura baada ya kumuangalia namna ambavyo Ares anaongea kwa kujigamba.
“Unasema kuwamaliza , hivi unafikiri wewe ni Zeus au Athena?Unafikrii unaweza kuwamaliza wewe kama wao walishindwa? , kwasababu wameweza kurudi lazima watakuwa na njia yao maalumu ya kuingia na kutoka , kama sio hivyo wasingekuwa ni wenye kujiamini kujitokeza mbele yetu”Aliongea Poseidon mpishi huyo na mwanajeshi kwa wakati mmoja.
“Poseidon nafikiri unaishi nyuma ya muda na unazidi kupoteza kujiamini , hawa ni kundi tu la wezi na wauaji wa miungu , hata baada ya miaka elfu ishirini hawawezi kubadili kilichopo ndani yao”
“Acheni kulumbana mara moja, muda huu lazima tufikirie namna ya kumtaarufu Athena ,Wakati huu Zeus hayupo na hatujui kama Hera na Dionysus wameamka , kama hatokuja hapa sijui namna ya kudhibiti hali’Aliongea Hermes.
“Umeanza lini kumkubali Athena wewe , si siku zote ulikuwa ni mwenye kumchukia na kutaka kuonyesha una uwezo mkubwa kuliko yeye?”Aliongea Ares kwa kejeli huku akicheka.
“Hata kama namchukia lakini kwasasa tupo upande mmoja kushindana na adui mmoja”
“Acha unafiki”
“Hehehe ..vyovyote unavyofikiria”
Kila aina ya kelele na vifijo vilisikika katika uwanja mzima , watu wengine walikuwa kwenye mchecheto mara baada ya kuona labda ni majivuno na kujiamini kwingi kwa timu ya kundi la DEICIDE kutuma mtu mmoja kushindana na timu ya watu watano.
Ni wakati huo huo kundi la wapiganaji ambalo lilijiatambulisha kama wawakilishi wa Afrika kumvamia yule mtu wa mavazi meupe kwa fujo zote.
Hawa Masenari wa kiafrika walikuwa na miili mikubwa mno na ni wenye nguvu ,ijapokuwa namna wanavyopigana sio kwa utaratibu maalumu na kwa wepesi lakini walikuwa na spidi na walichagua maeneo muhimu ya kumpiga adui
Mtu wa mavazi meupe aliekuwa na sura iliofunikwa na Mask ya madini ya Dhahabu alisimama katika eneo moja bila ya kusogea na hata maadui zake walivyomsogela hakufanya chochote na aliwaacha wafanye wanachotaka, walijaribu kurusha ngumi kumpiga katika maeneo ya kifuani , usoni na kwenye kiuno kwa kuunganisha nguvu lakini hawakuweza kumsogeza hata inchi., ni kama vile mtu anapojaribu kupunguza maji chumvi ya maji ya bahari kwa kumwaga maji safi.
Tukio hilo liliwafanya wale watu kushindwa kujua ni kipi cha kufanya zaidi , maana wamepiga kwa kutumia mbinu zao zote , lakini hakukuwa na matokeo ya adui yake kuonysha kuumia ni kama wanajaribu kulima jiwe kwa kutumia majembe.
Muda uleule kulisikika sauti isiokuwa ya kawaida,ilioashiria dharau kutoka kwa yule mtu wa mavazi meupe na palepale wale waafrika wenzetu ni kama vile walikuwa wakivutwa kwani wote walirushwa pembeni na nguvu isiokuwa ya kwaida na kwenda kudondokea mbali nje ya ulingo.
Ijapokuwa hawakuwa wameumia , lakini mshindani wao aliwashangaza na kumuona sio wakawaida kabisa kwa namna ambavyo anapambana na walikosa ujasiri wa kueondelea na palepale kengere ya refarii kupitia vifaa vya Eletronik ilisikika na kutangaza timu ya DEICIDE imeshinda kuingia raundi nyingine.
Licha ya hivyo mtu wa mavazi meupe alionekana kama vile hakuwa hata na haja ya kuingia raundi nyingine bali alikuwa amesimama akiwa ameangalia upande mmoja ambao ni wa VIP.
Miungu sita iliokuwa katika eneo la VIP ndio walengwa wake wakuu na macho yake kama yalivyoonekana katika Mask yalikuwa ni yale aliokuwa na dharau lakini pia ya kiuchokozi.
“Haiwezi kuwa makosa , muonekano wao na nguvu bila ya kuwa na msisimko wowote wa nguvu ya kiroho , ni wao bila shaka”Aliongea Sten huku akikunja sura.
“Lakini kama kweli ni wao na wametoka walipokuwa , kwanini wameshiriki katika mashindano ya binadamu , si maadui zake ni sisi?”Aliuliza Alice.
“Sina uhakika kwasasa , lakini kwasababu tayari washatangaza vita basi haitakuwa rahisi kama miaka elfu ishirini iliopita na inaweza kusababisha dunia kuingia katika taharuki , tunapaswa kuona mambo yatakavyokwenda”Alijibu .
“Hao ni wakina nani , kwasababu unaonekana unajua kwanini na sisi usitutoe gizani?”Aliuliza Rose , yeye na Magdalena hawakuwa wakijua chochote na Christen alivuta pumzi na kuzishusha na kisha akaongea.
“Have you heard about .. A race named GIANT?”Aliuliza akisema je ashawahi kusikia kabila la watu waliofahamika kwa majina ya GIANT.
“Giant!!?”Aliongea Magdalena huku akionyesha mshangao na kuonekana akifikiri.
SEHEMU YA 568.
Magdalena mara baada ya kufikiria kwa muda alikumbuka maneno ya Roma na Ron walivyokuwa wakizungumzia kuhusu kundi la Kimasenari ambalo linajiia Ps linalohusiana na Cyclops.
“Nimesikia mshindi wa mashindano yaliopita ni kutoka kwa familia iliopewa jina la Cyclop ?”
“Upo sahihi , Cyclops ni sehemu ya Giants(Majitu) wana uhusiano wa karibu pia na Centimani , kulingana na historia Centimani iliwakirisha majitu mia moja katika vita , Hadithi za miungu kuna nyingine ni za uongo na nyingine ni za ukweli ambazo zilikuwepo enzi hizo zilizoandikwa na binadamu, kabila la Cyclop ni uzao mchanganyiko kati ya Giants na binadamu wa kawaida , hivyo unaweza kusema Cyclop wamerithi tu damu yao na sio muonekano. licha ya hivyo uwezo wao ulikuwa mkubwa kushinda makundi yote ya kimasenari katika mapigano.
Sasa basi hawa Cyclops halisi pamoja na Centmani wanatokea katika uzao mmoja ambao ni sawa na wa kwetu lakini hayo ni mambo ya zamani sana ambayo yametukia katika sayari yetu , nguvu zao za kimwili ni kubwa mno kuliko za kwetu lakini nguvu zao za kiroho hazikuwa kubwa kutupita hivyo wakawa na uwezo mdogo sana wa kutumia kanuni za anga na sio washindani wetu kabisa kipindi hicho na katika sayari yetu walikuwa ni kabila lenye hadhi ya chini kabisa ambalo lilikuwa chini yetu lakini mara baada ya sayari yetu kukosa uwezo wa kusapoti maisha sisi tlikuja duniani lakini wakati huo sio kama tulikuja duniani tukiwa peke yetu, baadhi ya Cyclops na Centiman walikuja duniani kwa kupewa msaada na Hepheastus ambaye alikuwa ni mwanasayansi aliebobea katika utengenezaji wa dhana , utofauti wa hawa Majitu na sisi wao walivyofika duniani waliweza kuhimili mazingira lakini kwetu sisi tulishindwa hivyo uwezo wetu wa kuendeleza kizazi chetu ukawa mdogo sana na ni kipindi ambacho waliweza kugundua tulikuwa tumeivaa miili ya binadamu ili kuweza kuishi walituchukulia kama dhaifu sana na baada ya kuona hilo hawakutaka tena kuwa chini yetu bali juu yetu na walianza kutuwinda ili watuue lakini matokeo yake Zeus akagundua mipango yao na akatumia kauuni za anga kupitia siraha yake ya Thunder na kuwafungia katika ‘Dimension’ mbalimbali na kwanzia hapo ndipo walipoweza kupotea katika uso wa dunia , lakini hakuna ambae alitarajia leo hii wataonekana tena kwa zaidi ya miaka elfu ishirini katika miili ya kibinadamu”Aliongea
“Kama ulivyosema ni sahihi , mbona hawaonekani kuwa na uwezo mkubwa, kwanini Zeus hakuwaua kabisa”Aliuliza Rose
“Ilikuwa ni ngumu sana kuwaua kwasababu ya miili yao ndio maana Zeus akaamua kuwafungia kwenye Dimension nyingine kwa kutumia kanuni za anga, ijapokuwa hatuwaogopi lakini ni ngumu sana kupambana nao na zaidi ya yote kama wametoka wakiwa hivi inamaana wanao uwezo mubwa na kama sio hivyo wasingetokea”
“Kama Zeus ndio aliekuwa na nguvu kuliko wote na alishindwa vipi kuhusu sasa hivi?”
“Kama tungekuwa na miili yetu kama kwenye sayari yetu na nguvu zetu kuwa asilimia mia moja wasingekuwa na ubavu hata wa kutusogelea”
“Unamaanisha nini?”
“Haha..Usiulize maswali mengi , Inabidi mjaribu kuwasiliana na Hades arudi haraka iwezakanavyo”Aliongea Christen huku akicheka
*****
Ni katika nchi ya Ujerumanni katika ukanda wa eneo la Bavaria , Roma ndio kwanza alikuwa amefika katika eneo hilo akitokea Marseille Ufaransa akijiandaa kuelekea Leipzig.
Sasa wakati akiwa anapita katika jiji la Munich alisimama ghafla , wakati huo alikuwa akiongea na Sauron ili kumpa maelekezo lakini mfumo wa mawasiliano ulionekana kuingiliwa na kumfanya Roma kusimama.
“Mfalme Pluto kuna kitu umepata?”Aliuliza Sauron mara baada ya kuona Roma yupo kimya.
“Sauron hii njia ya mawasiliano tunayotumia si mtandao wake unajitegema na tunatumia satilaiti binafsi?”
“Ndio Mfalme , njia hii inazuia baadhi ya taasisi nyingine kuingilia mawasiliano yetu na kutudukua, tumeweza pia kuweka nywira ili isiwe rahisi”
“Kwahio inamaanisha kwamba kama itatokea mawasiliano yakayumba inamaana kuna mtu alieingilia kutoka ndani si ndio anaejua mfumo wetu?”
“Ndio Mfalme na kama ni hivyo basi nakubaliana na wewe kwani mawasiliano yetu yalikuwa mazuri tokea tuanze msako”Aliongea na kumfanya Roma kufikiria huku akianza kuchunguza kila upande na aliweza kusikia tena mawimbi ya frikwensi yakiingiliana na mawasiliano yao
“Hebu jaribu kuangalia kama kuna sehemu gani ndani ya eneo la ukanda wa Bavaria ambalo kuna uwezekano wa uwepo wa kambi”Aliongea Roma na Sauron alichukua agizo hilo na kulifanyia kazi.
“Mfalme Pluto hilo eneo ni mahususi kwa ajili ya Viwanda na hakuna kingine ukiachana na sehemu mbili zilizotelekezwa ambazo kuna migodi mwili ya makaa ya mawe iliotelekezwa kwa miaka mingi”
“Migodi ya makaa ya mawe , unamaanisha ambayo ilichimbwa miaka mingi iliopita?”
“Upo sahihi lakini hata kama ni ya zamani ilikuwa ni mikubwa mno na inaenda sana chini na imetawaliwa na joto la kiwango cha juu , hivyo eneo hilo haliwezekani kuwa sahihi kwa ujenzi wa maabara”
“Umekosea Sauron , huu ndio ufunguo kwasababu jotoridi kuwa juu inafanya eneo hili kuwa sahihi kujenga maabara”Aliongea Roma na kumfanya Sauron upande wa pili kushangaa.
“Could it be.. Geotharmal energy”Aliongea Sauron akimaanisha je wanatumia nguvu ya umeme wa mvuke.
Maabara ya siri ya utafiti wa siraha kubwa za nyuklia ingeweza kugundulika kwa haraka kama tu ingetumia umeme kutoka katika gridi ya taifa kwani wangekuwa na matumzi makubwa sana ya umeme hivyo wagetiliwa mashaka , lakini kama ni umeme unatokana na mvuke ingekuwa rahisi sana kwani ni wa kujitegemea.
Sauron alishngaa kuona Roma aliweza kufikira jambo la namna hio lakini upande wa Roma hakutaka kufikiria mara mbilimbili kwani aliweza kushuka moja kwa moja mpaka chini.
Eneo lote la Bavarian lilikuwa na utajiri wa kutisha ndio kitomvu cha utajiri wa taifa la Ujerumani , lakini licha ya kuwepo kwa viwanda vingi vinavyofanya kazi na maendeleo makubwa ya jiji lakini kulikuwepo na maeneo ambayo yalikuwa wazi , hususani yale ya migodi kama hio ya makaa ya mawe.
Roma mara tu baada ya kukanyaga chini na kukagua eneo hilo aliweza kutumia uwezo wake kukagua mazingira kutoka juu kwenda chini na hatimae aliweza kuona utofati wa eneo moja kuwa na muundo ambao ulikuwa ukitofautiana na baadhi ya migodi mingine na alijiambia huenda ikawa eneo ambalo alikuwa akitafuta.
****
Dakika kumi zilizopita lwenye maabara , alionekana Clark ambaye alikuwa amesimama kwenye kioo chenye uwezo mkubwa wa kuzuia mionzi akiangalia kwa umakini upande wa pili namna mkono wa Roboti ulivyokuwa ukifanya kazi kutoa majibu ya kikanuni ambayo umepewa maelekezo yake.
Mkono huo uliokuwa ukifanya kazi kiotomatiki ulikuwa ushafanikisha kudhalisha vitu viwili vyenye maumbo makubwa muundo wa risasi.
Jerry akiwa na macho ya furaha aliangalia matokeo hayo kwa tamaa huku muda wote akicheka cheka kama chizi.
“FURY hatimae upo mbele yangu , Profesa naamini unafuraha pia hii ni Masterpice ambayo itabadilisha kabisa ustaarabu wa dunia mzima wa kibinaadamu , hata miungu hawatoweza kuwa na nguvu ya kuhimili si ndio?”
“Sijawai kufikiria ingefika siku ningetengeeza kitu kama hichi , kama bado unanichukulia kama mwalimu wako fuata ushauri wangu , usije ukaitumia..”
“Haha..”Alicheka na muda uleule alibonyeza kitufe na kuruhusu zile Fury zilizokamilika kutoka katika eneo la matengenezo na kuingia upande mwingine kwa ajili ya matumizi.
“Usijali Profesa kama yule shetani atashuruti , bila shaka sitakuwa na haja ya kuitumia lakini kabla ya hapo lazima tutengeneze mtaji mkubwa ambao hata siku tukisema tuiharibu dunia inawezekana , kwasasa wafadhili wa hii projekti wanasubiri “
“Ijapokuwa sijui nani yupo nyuma yako na ni taasisi ipi lakini nguvu ya FURY haiwezi kuogozwa na binadamu , nakwambia utajutia hili”Aliongea kwa kujaribu kumbembeleza.
“Profesa au hapana kwanzia sasa nitakuita Clark , mimi nido napaswa kukushauri kuanzia sasa hivyo acha maigizo , wewe na mimi ni sawa tu , sisi wote ni watu ambao tunatumia juhudi kubwa kaika kufanya tafiti bila kujali athari zake na mwisho wa safari yetu ni pale ambapo tutapita vizingiti vyote alivyowekewa binadamu na kujua nini maana ya msingi wa ulimwengu , kama hukuwa na mpango wa kutengeneza FURY na kuvuka mipaka ya kibinadamu katika siraha za nyuklia basi usingethubutu hata kufikiria hii tafiti , wewe si ulisoma maswala ya tiba kwanini ukajiunga na maswala ya tafiti za siraha , Hawa binadamu wote ni wapuuzi kwako na unawachukulia kama vifaa vya majaribio , hawana utofauti na panya wa maabara waliofngiwa kusubiria wakati muafaka kufanyiwa majaribio kwani hakuna utofauti , kama hukutegneneza Fury kwa ajili ya kuharibu dunia nina uhakika ulikuwa ukisubiria madhara yake, Au nakosea Clark?”
“Sijatarajia utanifikiria mimi hivyo , nilisoma maswala ya tiba kwa ajili ya mwanaume ninampenda kuondokana na maumivu na nilitengeneza Fury nikiwa na matarajio kwamba itasaidia binadamu kuweza kutumia nishati kwa kiwango kikubwa zaidi ya ilivyosasa kupitia teknolojia iliopo lakini licha ya hivyo niliishia njiani kwasababu niliogopa kama itatumiwa na taifa kutengenezea siraha , upo sahihi maisha yangu yote yatakuwa ni kufanya tafiti lakini sio hapo tu , kuna vitu vingi katika dunia hii ambavyo vinahitaji hasira zetu lakini hatupaswi kuwa watumwa wa hasira na chuki”
“Acha kuongea upumbavu wako , usijifanye wewe ndio mtakatifu, unaweza kuwa mwalimu wangu lakini sasa wewe ni mateka wangu na mimi ndio master wako”Aliongea na palepale alimsogelea Clark na kisha akakikumbatia kiuno chake na Clark kwasababu alikuwa amengalia upande wa mbele yake hakuweza kutegemea kitendo kile kutoka kwa Jerry aliekuwa nyuma yake.
“Jerry unataka kufanya nini?”Aliongea huku akijitoa kwake.
“Unaiuliza tena , huu ni muda sasa wa kurelax baada ya kumaliza kazi yangu nzito , kwanini nisifurahie uzuri wako, itakuwa hasara kumuacha mtu mwingine”
“Wewe, mimi ni mwalimu wako uthithubutu”
“Acha ujinga , sijali wewe ni nani , kwanza kabisa wewe ni mdogo kwangu kwa miaka miatu , unafikiri nitakuabudu kwasababu tu ulikuwa mwalimu wangu na uwezo wako ni mkubwa , sahau katika kichwa chako na kwanzia sasa hivi hakuna kitu kinachoitwa mwalimu na mwanafunzi, hapa ni mwanaume na msichana ambaye anajiandaa kuwa mwanamke”Aliongea huku akimsogelea tena.
Clark alikuwa na uwezo wa kumdhibiti Jerry kwa wakati huo kwani alikua yupo peke yake katka hilo eneo kwasababu ya kuwa na mafunzo ya kujilinda lakini alisita kufanya hivyo..
Upande wa Jerry mara baada ya kuona Clark anakwenda kuleta ugumu palepale alichomoa bastora na kumnyooshea Clark.
“Samahani najua kabisa wewe ni mgumu hivyo niliandaa kabisa bunduki , kukwambia tu ukweli nje ya hii maabara kuna walinzi kibao wanalinda na hauwezi kutoroka”Aliongea na kumfanya Clark kukunja ngumi yake na kung’ata lipsi kwa wakati mmoja .
“Unaota nini , vua nguo haraka , nina sehemu ya kwenda pia kuonyesha mafanikio kwa wakubwa zangu, nimeisubiri hii siku kwa zaidi ya miaka mitatu kufanya mapenzi na wewe na hatimae leo ninapata nilichokuwa nikipania sana , hivyo naomba unirhuhsu nifurahi kistaarabu kabisa..”
“Nipige risasi kama una ujasiri huo”Aliongea Clark akiwa katika ukauzu.
“Kama unakitaka kifo utakipata lakini kama hutotoa ushirikiano basi wale watoto ndani ya kanisa la Santa Maria nitawaua kwa bomu tena nikuambie nitaenda mbali kuharibu shule ambayo umewekeza”
“Ushetani””
“Ndio ujue sasa mimi ni shetani , hivyo vua haraka”Aliongea na kumfanya Clark amwangalie kwa huzuni kubwa na palepale aliingiza mkono wake katika mfuko wa koti na kutoa kijichupa kidogo na kupeleka mdomoni na kuonekana alikuwa akinywa kimiminika.
“Unafanya nini?”Aliongea Jerry kwa mshangao na kumfanya Clark kucheka kwa dharau.
“Wewe huoni , ni kheri nife kuliko kuruhusu shetani kama wewe kuunajisi mwili wangu , kama hutojali mwili wenye sumu na wa baridi unaweza kunitumia utakavyo..”Aliongea na muda uleule sura ya Clark ilianza kubadilika na kupauka na alianza kuhema kwa shida na palepale alikosa mhimili na kudondoka chini huku povu likianza kumtoka mdomoni na palepale macho yake yaliongezeka ukubwa.
“Wewe umewezaje kupata sumu..”Aliongea kwa kutetemeka akiwa haamini.
Muda huo huo ndio aliweza kukumbuka kauli yake masaa kadhaa yaliopita kwamba anajaribu kuangalia usafi wa elementi.
Wakati ule hakuwa akielewa ni mchanganyo gani wa kemikali aliokuwa akitengeneza , lakini sasa anajua kumbe ilikuwa ni simu aliokuwa akitengeneza.
Baada ya kuona kwamba mwanamke huyu alimdaganya jana na kujitengenezea sumu alijikuta hasira zikimvaa na alimsogelea kwa kasi na kumpiga teke tumboni na kumfanya Clark kudhidi kutapatapa akielekea kupoteza maisha.
“Mh hata hivyo sina tamaa kihiivyo ya mwili wako , lakini siwezi kukuacha ukafia hapa ndani , tutakutoa na kufanya wanyama wakali wa msituni kukufanya chakula , itashangaza baade ikija kugundulika mwanamke mwenye busara kama wewe umejiua na sumu”Aliongea na baada ya kumaliza hakujali tena na alirudisha siraha yake kibindoni na kugeuka ili kuondoka hilo eneo.
BOOM!
Wakati akiwa anajiandaa kutoka alijikuta akisimama na kufunga masikio yake baada ya mlango wa kuingilia kudondoka chini kwa kuonyesha kwamba umepigwa na nguvu isiokuwa ya kawaida.
Na mpaka akili yake inamkaa sawa na kuamsha kichwa kuangalia knachoendelea , alijikuta akiachama mara baada ya kuona sura ya mtu ambaye hakuitarajia kuiona hapo ndani , alikuwa ni Roma.
ITAENDELEA.
NaaamSEHEMU YA 570.
Jerry alidhani alikuwa akiota , mlango huo ulikuwa ni wa chuma kigumu sana , imewezekanaje ukabobolewa kirahisi namna hio.
Muda huo ni shoti pekee za umeme ambazo zilikuwa zikisikika ndani ya eneo hilo na Roma wala hakujali kabisa aliingia kama vile ni mnyama.
Nyuma yake kulikuwepo na damu nyingi ambazo zilikuwa zimetengeneza mfereji mkubwa wa damu kuingia ndani mara baada ya mlango kuvunjika.
Zilikwa ni damu za walinzi ambao walikuwa walilinda katika hilo eneo na ilionekana dhahiri kabisa Roma aliwapasua pasua viungo vyao pasipo huruma.
Roma mara baada ya kugundua eneo ni lenyewe , alitolea hasira zake zote za kutafuta usiku kucha kwa walinzi hao na aliwaua vifo vibaya sana, huenda ni aina ya vifo ambavyo havijawahi kutekelezwa hapa duniani , vilikuwa ni vya ukatili wa hali ya juu sana.
“Clark!!”Aliita mara baada ya kumuona Clark aliekuwa yupo chini sakafutni akitetema kama mgonjwa mwenye kifafa na palepale alimkimbilia na kumkalisha.
“Nini kimetokea ?Umepewa sumu?”Aliuliza Roma kwa wasiwasi mkubwa na hakuacha kujaribu kumchunguza kwa kumuingizia nguvu za kimaandiko.
“I… I knew it ..you.. would save me ..just like ten years ago..”Aliongea kwa tabu sana akisema kwamba alijua tu atakuja kumuokoa kama miaka kumi iliopita.
Roma macho yake yalianza kuwa mekundu hakuwa na uwezo wa kujua ni aina gani ya sumu ambayo ipo kwenye mwili wa Clark , alikuwa na uwezo wa kuhisia sumu iliokuwa kwenye mwili wake ilikuwa ikinyong’onyesha saa utendaji kazi wa mwili.
Lakini alishindwa kumponyesha kwani sumu iliokuwa kwenye mwili wake iliionekana tayari ishaingia kwenye mfumo wa damu moja kwa moja na wakati akiwa amemshikilia palepale alitema damu nyingi nje mara baada ya Roma kujaribu kumponyesha.
“Ni sumu ya aina gani hii , niambie namna ya kukuponyesha”Aliongea Roma akijaribu kumtingisha lakini Clark aliishia kutingisha kichwa chake akimuonyesha ishara kwamba hakuna namna ya kumponyesha.
“Ni sumu ambayo niliiandaa dakika ya mwisho kabisa na ili kuhakikisha hawawezi kuniponyesha nilitumia mbinu ya kipekee ambayo inafanya viungo vya mwili kutofanya kazi sawasawa .. kwasasa haiwezekani kitu”Aliongea kwa tabu na kumfanya Roma palepale kumgeukia Jerry ambaye alikuwa amemsahau kwa muda.
“Wewe mnyama , yote haya ni kwasababu yako , kama utafanikisha kumponyesha mwalimu wako nitakuua lakini mwili wako sitouharibu”Aliongea Roma kimkwara huku akisambaza msisimko wa hali ya juu wa nguvu za kijini ili kumuogopesha Jerry.
Muda huo Jerry alikuwa ameshikwa na ubaridi wa aina yake hasa baada ya kuona damu nyingi zikiingia ndani kutokea nje , lakini licha ya hivyo chuki yake zidi ya Roma ziliifunika hofu yake na kaunza kucheka kama kichaa.
“Wewe shetani ijapokuwa sijui namna ulivyoipata hii sehemu lakini nakuambia hivi hakuna namna ya kumuokoa , sumu ambayo Clark ametengeneza anaweza kutengenza dawa yeye mwenyewe , inatia huruma kwamba anakufa kwenye mikono yako ukiwa huwezi kumsaidia “
“Unakiomba kifo wewe..”Aliongea Roma huku akitaka kumshambulia lakini Jerry alimzuia kwa kumpigia makelele.
“Usinisogelee, ukinigusa tu hii maabara yote italipuka na zile FURY mbili zitalipuka, madhara hayatakuwa kwako tu lakini kwa ukanda wote wa eneo la Bavaria, Ujerumani yote itageuka na kuwa toharani ya dunia, Je upo tayari kutoa kafara mamilioni ya watu kwa ajili ya kuniua mimi?”Aliongea na kumfanya Roma kunasa neno FURY.
“FURY siraha aliotaja je ndio sababu ambayo imewafanya wakuteke?”Alimuuliza Clark.
“Ndio .. niliipatia jila hilo ikimaanisha neno kisasi”Aliongea .
“Inahusiana na nini?”
“Ni aina ya siraha ya nyuklia ambayo teknolojia yake imeboreshwa zaidi … risasi yake moja ni sawa na risasi mia tano za bomu la Hydrojeni”
“Nini..!!”
Roma alishangaa kwa uhatari wa siraha hio , kama kweli risasi moja ni sawa na risasi mia tano za bomu la Hyrdrojeni si ni hatari hio , maana kama siraha hio ikatumika basi mionzi yake isingeathiri tu Ujerumani huenda na nchi za karibu.
Alijiuliza inakuwaje watu wa North Buyeo na kundi la kigaidi kutafuta teknolojia ya namna hio, ni kipi ambacho wanalenga?.
“Hehe.. sasa nadhani tayari ushajua ukuu wake, ninataka kuona kama utathubutu kuniua …Wewe shetani utapata maumivu makubwa sana baada ya mwanamke unaempenda akifa mbele yako …Hahaa, nimesubiria hii sku kwa muda mrefu sana , na unastahili kwa kila kitu , unapaswa kwenda jehanamu”Aliongea kwa hasira .
Roma alikuwa katika kiwango cha juu cha hasira na alitamani kumfanya kitu kibaya , lakini hakuweza kuthubutu kufanya maamuzi ya haraka kwani maisha ya watu zaidi ya mamilioni yalikuwa hatarini.
“Nini tatizo , Umekosa ujasiri tena?, Umejileta mwenyewe hata hivyo , ninakwenda kulipiza kisasi cha vifo vya familia yangu , baba yangu , mama yangu na dada yangu ambaye alikuwa na miaka mitatu tu”
“Kisasi? Ni kipi nimekufanyia mpaka kutaka kulipiza kisasi?”
“Bila shaka hukumbuki , umeua watu wengi sana unawezaje kuwakumbuka wote , umesahau ulichokifanya miaka mitano iliopita pale Simbokrog nchini Belarus kwenye kijiji cha Wozic si ndio?”
“Kijiji cha Wozic ?”Aliongea Roma huku akikunja sura , hakuwa akikumbuka kabisa kama kuna sehem kama hio na isitoshe kulikuwa na maeneo mengi madogo madogo aliopita ambayo hakuyakumbuka na kote hhuko huenda aliua.
“Unaonekana hukumbuki , Kijiji chetu kilikuwa na watu 186, kati yao therathini walikuwa ni watoto na wakati huo ni mimi pekee ambaye sikuwepo nyumbani kutokana na kwamba nilienda shuleni kwenye mji mwingine wa pembeni , lakini wewe ukaja na kufyeka kila mtu uliemkuta kijijini bila kujali wana hatia au hawana kwasababu tu adui yako alikuja kwenye kijiji chetu , kwanini usingeacha hata maisha ya watoto wadogo ambao walikuwa hawana hatia , kwanini ulivyomaliza ukawachoma na moto…”Aliongea Jerry kwa hasira kubwa na kauli yake ilimfanya Roma sasa kukumbuka lakini hakuwa akikimbuka vizuri sana , kipindi anafanya hivyo alikuwa katika hali ya ukichaa na ugonjwa wake ulikuwa ndio unaitawala akili yake.
Alikumbuka kabisa kitendo cha kuua watu wa kijiji kile ndio kilichosababisha Seventeen kumkimbia na mwisho wa siku akaingia kwenye mikono ya maadui na kumuua akiwa na ujauzito tumboni mbele ya macho yake.
Roma alishindwa kujizuia kusikia uchungu kutokana na maelezo ya Jerry , haikujalisha alikuwa akitamani kuwa na maisha ya amani , lakini mambo ambayo ameyafanya miaka iliopita yalimfanya kutengeneza maadui wengi ambao muda wowote watataka kulipza kisasi na aliona hata kwa Jerry ni mwanzo tu.
Lakini licha ya hayo yote , kipindi hicho akili yake ni kama ilikuwa ikiendeshwa kwa rimoti , ugonjwa wake ulikuwa mkubwa kiasi kwamba alikuwa ni kama shetani na bila kumwaga damu kwa siku hakuweza kutulia.
“Naona sasa unakumbuka ..?”Aliongea Jeryy huku akifuta machozi .
“Unapaswa kuadhibiwa pia , mwanzoni wakubwa waliniahidi watanisaidai katika kulipiza kisasi , na nikaamua kuishi na chuki na kuvumilia mpaka leo hii , lakini kwa leo kwasababu umepajua hapa sina mpango wa kuondoka hapa nikiwa hai”
“Unapanga kufanya nini , je unafikiri kulipua hilo bomu la FURY na kuniua kutakufanya ulipize kisasi cha ndugu zako , sahau kabisa hizo ni ndoto za kufikirika utaua watu wengi kuliko mimi”
“Inanihusu nini , ni matendo yako ya kishetani ndiio ambayo yamenifanya kuwa katika hali hii , usijaribu kunidanganya, hata kaam nitaondoka leo utanitafuta na kuniua , ni kheri niende na mamia ya watu katika kaburi langu , maisha ya hawa watu yatakuwa yametolewa kafara kwa sababu yako hahahaa..”
Baaada ya kuongea huku akicheka kwa kejeli palepale alisogea upande wa kulia wa kile kioo cha kuzuia mionzi na kukipiga ngumi kwa nguvu kubwa.
“Twiii , Twi, Twiit”
Ilionekana ndio namna maabara ilivyotengenezwa ili kuilipua njia ya mkato ya kuwasha bomu ni kupiga ngumi kioo na hicho ndio ambacho kilikuwa kikienda kutokea , hata hivyo maabara nyingi za kufanya majaribio ya siraha hutegeshewa bomu la kuiharibu kabisa pale panapotokea tatizo.
Muda uleule alivyoopiga ngumi kile kioo sauti kutoka kwenye tarakishi humo ndani ilisikika ikiwatahadharisha.
“Destruction Mode has been turned on , the labaratory will be exploding after the countdown , thirty .. twenty nine…”
“Ni mwisho haha , hatimae imekuwa mwisho”Aliongea Jeryy.
Roma alishangaa , hakutaka kumuua Jerry kwasababbu aliogopa siraha hio ya FURY ingelipuka , lakini sasa hivi maabara yote inakwenda kulipika , ilikuwa haiwezekani kwa yeye kuzuia kutokulipuka kwa bomu hilo la nyuklia.
Roma aligeuza macho yake na kumwangalia Clark aiekuwa kwenye mikono yake ambaye afya yake inaelekea ukingoni alijikuta aking’ata meno yake kwa hasira
Baada ya kuona hana uwezo wa kuzuia mlipuko wa maabara hio pamoja na mlipuko wa FURY kitu pekee ambacho aliona angeweza kufanya ni kujiuoko yeye na Clark kuondoka katika hilo eneo.
Kufumba na kufumbua alikuwa ashatoka nae na kwenda kutua mbali kabisa na eneo hilo katika mlima na msitu usiokaliwa na watu, Kusini mwa nchi ya Austria.
Alikadiria kwa umbali huo hata kama bomu hilo la nyuklia litalipuka upande wa Ujerumani halitowaathiri kwa muda kupitia mionzi yake.
Baada ya kutafuta sehemu yenye majani makavu aliamua kumuweka Clark chini na kuanza kumfanyia uchunguzi wa mwili wake.
Haikuleta maana kwake kuomba msaada kwa muda huo , kwani aliona asingepata msaada huo ndani ya muda , hivyo kitu pekee ambacho alitaka kujaribu kufamnya ni kumpontysha yeye.
Mapigo ya moyo ya Clark yalikua ya chini mno na yalikuwa yakiendelea kuwa ya chini na muda wowote yangeacha kabisa kudunda na kupelekea kifo chake.
Roma alijikuta akijikatia tamaa mara baada ya kumungizia nishati ya mbingu na Ardhi kwa kuunganisha na ya Urejesho lakini bado alishindwa kumponyesha.
Mwili wake ulikuwa ni kama vile seli zake zinaoza ndani kwa ndani na hiko ndio kilichomuogopesha zaidi , kwani aliona dakika yoyote Clark angeweza kufa kwenye mikono yake maana tayari alishaanza kuwa wa baridi.
“Damn it … Clark , jarobu hata kuongea kidogo , ninaweza vipi kukuokoa?”Roma ujasiri wake wote ulimwishia na aliishia kuukumbatia mwili wa Clark huku akishindwa kuzuia machozi yaliochanganyika na hofu.
Ni mwanamke huyo ambaye hakulala usiku na mchana kwa ajili tu ya kumtengenezea dawa, na katika kipindi chote ambacho alihisi kuwa mpweke ni yeye pekee ambaye alifanya kila liwezekanalo kumsaidai , lakini sasa mwanamke huyo anafia kwenye mikono yake bila ya kuwa na msaada kwake.
Aliogopa kwamba bado hakuwa amelipa fadhila zake zote kwa yale aliomfanyia , alijilaumu na kuona yatakuwa makosa yake kuruhusu akifariki kwenye mikono yake kwani itamaanisha kwamba alishindwa kumlinda na maadui ambao aliwatengeneza yeye mwenyewe.
Clark alijitahidi kuamsha kinyonge sana mkono wake akimfuta machozi roma ,Roma hakujua hata alikuwa akilia alihisi maji yanaririka katika mashavu yake , lakini hakujua kama ni machozi yake .
“Ni sawa … wewe .. usilie tena .. nina furaha , mtu wa mwisho ninaemuona .. ni wewe”Aliongea Clark kwa kukata kata maneno.
Alishindwa kujizuia zaidi na zaidi mara baada ya mwanamke huyo kuongea kauli hio na alizidi kutoa machozi na kulia kwa kwikwi.
“Huwezi kuondoka hivi … utakuwa umenikatili sana ,,,, siwezi kujisamehe tena , umeniokoa mara nyingi sana na umefanya mambo mengi kwa ajili yangu ,, lakini mimi nashindwa kukukoa ,, sina thamani kabisa kwako , mimi ni mjinga”Aliongea huku akiinua mkono wake na kujipiga kibao kwa nguvu na kutokana kutumia nguvu za kijini ilisababisha mpaka majani ya miti kuanza kudondoka lakini bado aliendelea kujipiga vibao mara nyingi zaidi na kumfanya Clark azidi kutoa machozi ya kumuonea huruma na huzuni kwa wakati mmoja.
“Usi.. usi , fanye hivyo”Alijitahidi kuongea.
“Clark naomba usife , naomba usife tafadhari , siwezi kufikiria nitakuwa na maisha ya namna gani ukishaniach…”Alianza kulia kama mtoto huku akimwangalia mwanamke huyo kwa kuomba.
“Na.. naomba,, nikuulize swali na unijibu kabla sijafa?”
“Niulize chochote na nitakujibu”Aliongea haraka haraka.
“Roma … nataka tu .. kujua kama .., je .. unanipenda?”
“Ndio , Nakupenda , siku zote nilikuwa nikikupenda sana ,… wewe ni moja wapo ya wanawake ninaowapenda sana..”Roma aliongea bila kujiuma uma , hayo ni maneno ambayo hakupanga kumwambia mwanamke huyo katika maisha yake.
Zamani hakutaka kabisa kumsogelea mwanamke huyo kutokana na madhambi ya umwagaji damu alioyafanya, lakini baada ya kurudi Tanzania na kujipatia mke ndio kabisa hakutaka kumfanya mwanamke huyo mchepuko kwa kuamini alistahili kitu kikubwa zaidi.
Roma hakuwa na mashaka kabisa juu ya mapenzi yake kwa Clark, ni mapenzi ambayo hayakuanza jana wala leo , ni tokea alivyokuwa mdogo na kadri mrembo huyo alivyokuwa anakuwa alizidi kumpenda.
Mapenzi yake kwa mwanamke huyo yalikuwa sio ya kawaida ambayo yanaweza kueleweka kirahisi kwa binadamu.
Pengine katika dunia kuna wanawake wengi ambao aliwapenda na wao pia kumpenda na kumpa kila kitu na yeye kufanya kila kitu kushinda magumu yote kwa ajili yao lakini mapenzi yake ya kweli katika kumbukumbu zake yapo kwa Seventeen na katika uhalisia yapo kwa Edna na mpenzi anaemuona kama ndoto ni Clark.
“Kweli!?”Aliuliza Clark akiwa kama haamini na alijitahidi kufumbua macho yake ..
“Ni kweli , nilichokwisha kukisema ni ukweli , na unapaswa kuniamini , sijawahi kukuweka wazi kwasababu tu niliona hustahili kuwa na mtu kama mimi , … samahani sikukuambia hili mapema”Macho ya Clark yalionyesha kabisa kufurahishwa na kauli yake na tabasamu la furaha lilifunika uso wake .
“Honey … I knew it , you loved me..”Aliongea.
Roma alikuwa akilia hivyo hakuwa akiongea zaidi ya kutingisha kichwa tu kumwaminisha ni namna gani anamkubali huyo mwanamke.
Clark alipanua mdomo wake huku akiinamisha kichwa chini na alionekana kama anataka kung’ata kitu flani..”
Roma aliweza kuona lakini hakujua Clark anataka kufanya nini na alimwangalia kwa kuchanganikiwa.
“Collar …”Aliongea Clark kwa sauti dhaifu akimaanisha Kola ya koti lake.
Roma palepale alielewa sasa anataka kung’ata nini na alifanya haraka na kumsaidia kumpelekea karibu Kola ya koti ili kuweza kugusanisha na lipsi zake.
“Clark unafanya nini, kwanini unamg’ata Kola ya koti, ni kwa ajili ya nini?”Aliuliza lakini Clark hakuongea neno na muda huo alikuwa kama mtoto anaetafuna nguo kwani alifyonza kwa nguvu ule ukola wa koti mpaka ukaanza kujaa mate.
Ni muda huo huo aliweza kuona Ukola ule wa shati ukibadilika rangi na kuwa wa bluu ambayo haijakolea sana na kama sio kwa kuloana basi isingetokea
Wakati akishangaa palepale aliweza kushangaa mara baada ya Clark kuvuta pumzi nyingi na kuzishusha baada ya kuonekana kumaliza alichokuwa akifanya na kadri dakika zilivyokuwa zikisogea ndio ambavyo alizidi kurudi katika hali yake ya kawaida.
“Unashangaa nini mpenzi? , sijafufuka ni kwamba tu sijafa”Aliongea huku akitabasamu.
“Wewe , umewezaje kufanya hivyo.. nini..?”
“Unataka kuuliza nimewezaje kurudi katika hali ya kawaida si ndio , basi ni kwasababu nimejiponyesha mwenyewe”Aliongea huku akijaribu kukusanya nguvu na kukaa mwenyewe chini.
Roma aliangalia ile Kola ya koti kwa mara nyingine jinsi ilivyokuwa na doa la rangi ya bluu na kisha akamgeukia Clark aliekuwa na uso wa furaha .
“Ulinidanganya?”
“Nani kakuambia udanganyike kizembe , mimi ni nani , mimi ni Profesa Clark, mwalimu wa mwanafunzi mjinga kama Jerry , hivi unadhani naweza kuzidiwa akili na mwanafunzi niliemfundisha mimi?”
Roma alikosa cha kusema, alimwangalia mwanamke huyo namna ambavyo aliweza kurudi katika hali yake ya kawaida kwa haraka sana na alijikuta akichoka kabisa na kujikalia chini.
“Huu ulikuwa ni mpango wako?”Aliuliza Roma.
“Ndio , hivi unafikiri ungeweza kunipata kwa kubahatisha , wakati nilipokuwa nikitumia tarakishi zao nilituma Link kwa siri katika satilaiti yenu , kama mwalimu nilimjua Jerry hakuwa vizuri kwenye maswala ya Compyuta hivyo hakuweza kujua ninachokifanya kabisa , nilijua tu kama mtafika maeneo ya karibu na nilipo basi mngehisi mawasiliano ni kama yameingiliwa kutoka ndani”Aliongea na kumfanya Roma asipinge kwani ndio alivyoweza kumpata.
“Kama ni hivyo vipi kuhusu Sumu ni nini kile?”
“Ile ni sumu kweli , niliweza kuchanganya aina mpya ya sumu nilioitengeneza pale, ni sumu ambayo inavilegeza viungo vya mwili na kukufanya uonekakane kama umekufa na kama hutachukua dawa yake basi utakuwa wa baridi kwa masaa ishirini na nne na ikiisha makali yake mwili utarudiwa na joto lake na utaweza kuamka , nilipanga kama wataniona nimekufa watatafuta sehemu ya kunizika au kunipatia matibabu na ndio nitajua namna ya kutoroka ,lakini hio ilikuwa ni mpango wangu wa mwisho kabisa kwani sikuwa na uhakika kama hawatachoma mwili wangu lakini nilipanga kama hakuna ambae atakuja kuniokoa basi moja kwa moja nitadanganya nimekufa ili kuepuka wasinidhuru, lakini bahati nzuri umeweza kuja ndani ya muda hivyo nikatumia mpango B”Aliongea na kisha akashika Kola ya koti lake.
“Nililoanisha hii Kola na dawa maalumu ya sumu ,ilihitajika tu mimi kunyonya na ndani ya lisaa limoja ninarudi kuwa sawa tena”
“Kama ni hivyo kwanini ulinichezea hila hata mimi , hivi ulijua ni kwa kiasi gani moyo wangu uliuma?”Aliongea Roma huku akisimama na palepale mrembo huyo alisimama na kupitisha mikono yake yote mwili katika shingo ya Roma na kumbusu kwenye paji la uso..
“Kama nisingetumia fursa hii , usingeweza kuniambia nilichotoka kusikia kutoka kwako kwa muda mrefu”Aliongea na wakati Roma anataka kuongea neno alizuiwa na lipsi laini za mwanamke huyo.
Baada ya busu jepesi , Clark alionyesha uso wa kuomba huku macho yake yakionyesha hali ya kutia huruma.
“Honey usinikasirikie , nilitaka tu kuwa na wewe kama mpenzi wako , nilijua kama hutoniambia nitakuwa na huzuni milele”
Roma alijiambia ile siku ambayo alikuwa akiiepuka kwa miaka mingi hatimae imewadia na hakujua anakwenda vipi kumwelezea mke wake kwa maneno marahisi na kumuelewa.
“Umeandaa mpango wako , ili kunifanya niingie katika mtego na ukanifanya nilie kama mtoto , aisee inatia aibu Daah”Aliongea Roma huku akitabasamu kwa uchungu na kumfanya Clark amwangalie kwa macho ya utani huku akimtolea ulimi nje kama anamcheka.
“Nilikuwa nikienda na hali inavyoruhusu , Jerry alinitishia kwenda kuwaua wale watoto wsio na hatia , sikuwa na chaguo lingine..”Baada ya kusikia hivyo alijikuta akikumbuka kitu alichosahau.
“Oh nimesahau kuhusu FURY Ujerumani ndio kwaheri”Aliongea.
“Haha.. nilikuambia kila kitu nilipanga mimi , unadhani ninaweza kutengeneza kitu hatari namna hio”
“Kwahio ulichotengeneza ni nini , ni feki pia?”
“Hebu fikiria , unadhani ninaweza kuhatarisha maisha ya mamilioni ya watu kwasababu ya watoto , hata kama niwe kwenye hali gani siwezi kwenda mbali kiasi hivyo , teknolojia ya FURY kwasasa ipo katika nadharia tu , inawezekana vipi kuitengeneza ndani ya siku mbili au moja? , kutengeneza tu elementi ya mwisho inayokamilisha kanuni inahitajika mchanganyo wa kikemia ambao unaweza kuchukua mwaka mzima kutoa matokeo”
“Kwahio unasema sasa hivi Jerry atakuwa na hasira sana mara baada ya kuona umemdanganya?”
“Labdal , Ujerumani naamini watashughulika na tatizo hilo , kwasasa ninafuraha ya nilichoweza kutimiza baada ya muda mrefu , Roma naomba unibusu japo kidogo tu”
“Nini!”
“Umesema unanipenda hivyo unapaswa kunifidia kwa miaka yote nilioteseka kwa ajili yako”Baada ya kuongea alifumba macho na kunyanyua kichwa chake juu kuweka mdomo vizuri ubusiwe.
Roma aliangalia Lips zake zilizokuwa nyekundu kutokana na weupe wake wa kizungu na kisha palepale alitoa tabasamu la kifedhuli na kumshika kiuno kisha akamvutia kwake.
Clark mpaka hapo alijua kabisa alikuwa amefanya kosa kwa kujirahisisha mbele ya mwanaume ambaye alikuwa kama Simba mwenye njaa.
Dakika moja mbele wote walikuwa kwenye ulimwengu mwingine kabisa ulioitwa Busu, inasemekana wazungu wapo vizuri sana kwenye Kubusu na hicho ndio kilichompagawisha Roma.
MWISHO WA SEASON YA 19
SEHEMU YA 571.
Katika jiji la Palermo giza tayari lilikuwa lishatawala na katika uwanja wa kivita uliokuwa ukifanyia mashindano , ulikuwa mtupu kwa wakati huo ikimaanisha kwamba mashindano kwa siku hio yamesha mpaka siku inayofuata.
Katika siku hio ya kwanza hakukua na maajabu makubwa kwani wale wanajeshi kutoka mashindano yaliopita wote kwa pamoja wameweza kuingia raundi inayofuata na kwa wale wahudhuriaji wenyewe wanasema mapigano yenyewe yanaanza siku inayofuata katika raundi ya pili.
Katika Moja ya Balkonni ya hoteli ya Cassano , mwanaume wa makamo mzungu alievalia mavazi ya upishi meupe alionekana akiwa bize kucharanga samaki aina ya Salmoni kwa haraka sana na kwa ufanisi mkubwa.
Kila kipande cha samaki kilikuwa kikilingana na kingine ni hivyo tu kwamba vilikuwa na ukubwa kidogo ambao unamuwezesha mlaji kutafuna kipande kimoja chote kwa wakati mmoja.
Mbali kidogo na alipokuwa anafanyia kazi mwanaume huyo kulikuwa na meza kubwa ambayo wahudumu wawili walionekana wakiwa bize kumsaidia kuhudumia kila anachokamilisha kupika na kuweka mezani.
Katika meza Christen alinyanyua Glasi yake ya Champagne na kumnyooshea Rose kugonga zao Cheers ambaye alikuwa karibu yake.
“Aphrodite, unaonekana kutokuwa kabisa na wasiwasi , vipi kuhusu hiko kinywaji?”Ares ambaye alikuwa ameegamia kwenye kiti kivivu aliongea kwa kuonyesha sura ya dhihaka.
“Wasiwasi wa nini , nipo hapa kwa ajili ya burudani sio kuteseka”Baada ya kusema hivyo alimgeukia Poseidon ambaye alikuwa akikomaa na upishi.
“Poseidon vipi hiko chakula bado tu? Nina njaa mimi”
“Hakuna mtu kugusa chakula kabla sijamaliza ,atakae fanya hivyo nitahakikisha hali chakula nilichopika mimi”
Upande wa Magdalena aliekuwa kimya alikuwa kwenye mshangao , bila shaka alikuwa akimjua Poseiodon ni mpishi maarufu duniani aliefahamika kwa jina la Mr Kelphin lakini hakuwahi kuwaza mtu huyo huyo kuwa mwanajeshi wa jeshi la Marekani upande wa majini.
“Christen kuna haja gani ya kusubiria amalize kila kitu , kwanini tusianze kula?”Aliuliza Magdalena ambaye alikuwa na njaa.
“Ndio sheria ya Poseidon hio kama atajitolea kupika chakula basi hataki mtu akiguse mpaka aridhike kimekamilika , anajali sana mlo kamilifu kuliko kitu kingine chochote”
“Kwa maneno marahisi Miss Magdalena ni kwamba bwana huyo ni mpishi Mbishi sana kwahi kutokea”Aliongezea Stern na Rose na Magdalena waliishia kushangaa tu.
Dakika chache mbele Poseidon aliweza kukamilisha sahani za Sashimi na kuwekwa kwenye meza hio kubwa , katika meza hio kilichoonekana ni aina mbalimbali ya vitoweo vya baharini ambavyo vimepikwa katika ubora wa hali ya juu.
Na kabla ya kuwaruhusu kula aliwaambia wasiguse kwanza chakula chake mpaka apige Selfie na palepale alitoa simu yake ya I Phone Toleo la juu na kupiga picha mbalimbali ya chakula chake na kisha kupost mtandaoni kwenye akaunti yakeiliokuwa ikifuatiliwa na watu zaidi ya milioni.
Baada ya kutaniwa na ndugu zake kutoka sayari nyingine , hatimae aliweza kukaa sasa na kuwaambia wale wahudumu waondoke.
Ukweli Magdalena na Rose walipata fursa ya kushiriki kwasababu ya heshima ya Roma pekee , lakini chakula hicho cha usiku ni kama vile kimeandaliwa kwa ajili ya ndugu hao ambao ni mara chache sana hukusanyika pamoja kama hivyo.
“Hermes tayari upo ndani ya hoteli , kwanini usivue hilo lisuti lako , huoni kwamba ni wewe tu hapa ulievaa suti na joto lote hili?”Aliongea Christen huku akimwangalia Raphaeli aliekuwa amekaa pembeni yake.
“Kuwa na amani sisi Vampire miili yetu ni ya baridi”
“Mwacheni nani anajali kama anahisi baridi au Joto , kwanza unaweza kunywa damu na ukaishi , kuna haja gani ya kula na sisi?”
“It’s recognition to Poseidon ‘s Culinary arts”Alijibu.
“Haina haja , chakula changu kipo Perfect”Aliongea Poseidon akijigamba.
Rose na Magdalena waliishia kuangaliana pasipo kuongea chochote , na walijiambia Poseidon na yeye ni kama Roma tu hana aibu kabisa kwa matendo yake.
Chakula kilichokuwa mbele ya Ares kilipotea kwa haraka sana na baada ya kumaliza kila kitu alisimama na kuelekea upande wa Balkoni.
“Ares unaenda wapi?”Aliuliza Stern.
“Hilo nalo ni swali gani?”
“Sio muda sahihi wa kuwatafuta, au unadhania unaweza kuwashinda?”
“Sina muda wa kupoteza kula na nyie mpaka usiku wa manane mimi wala sitamani kuangalia mapigano ya kibinadamu ya Caesar Conference nipo hapa kwa ajili ya kupigana nao”
“Hey Bro unataka kuzaliwa upya katika mwili mwingine labda?”
“So what , nevet try never know , I am not interested in their conspiracies , I dare to go if you don’t”(“Kwani vipi , usipo jaribu huwezi kujua , sina matamanio ya uzushi wao , ninathubutu kwenda kama wewe huwezi”Aliongea na kumfanya Stern na Alcie kukunja sura zao kutokana na ukichaa wa Ares.
Muda huo huo Rose na Magdalena waliweza kuhisi msisimko maalumu ambayo ni kama vile ni mawasiliano yao na Roma na walijikuta wote wakiangalia upande wa nje na waliweza kumuona Roma akiwasogelea kwa kasi na walijikuta wakiwa na furaha.
Kufumba na kufumbua Roma aliweza kutua katika Balkoni huku akiwa na tabasamu pana.
“The Annoying Hades , you finally came back , we thought you run away in fear”Aliongea Christen akimtania kama walidhania amekimbia kutokana na uoga.
Roma aliangalia kila mmoja aliekuwepo na alionekana kuridhika kupitia macho yake.
“Naona kila mmoja ameweza kufika , hakuna chochote kilichotokea wakati nilipokuwa sipo, nilienda Scotland ndio maana nimchelewa kuja”Aliongea.
Alikuwa amempeleka Clark Scotland kwani walikuwa na jukumu la kushiriki katika sherehe za Summer Bank Holliday , yeye na mama yake.
“Kwasasa bado lakini ni swala la muda tu”Aliiongea Stern huku akimwangalia Ares.
Baada ya hapo Roma aliongea na wanawake wake na kuwatoa hofu kwamba tayari alifanikiwa kumpata Clark na kumrudisha nyumbani.
Baada ya kuelezea kwa ufupi kwa upande wake na yeye alimuuliza Christen kile kilichotokea wakati ambao hakuwepo na alielezewa kila kitu kwa ufupi na namna ambavyo Ares anapanga kutoka hapo na kwenda kuwatafuta akiwa peke yake.
Upande wa Roma hakuwa na msingi mzuri wa historia nzuri juu ya hadithi ya miungu ya kigiriki hivyo hakuwa na uelewa mkubwa na licha ya kusikia stori zinazohusiana na majitu hakuwahi kuamini kama kweli walikuwepo.
“Nakushauri usiende kwanza mpaka ufahamu mbinu zao zote”Alishauri Roma.
“Acha kunidharau , Hades usijifanye wewe una nguvu kunishinda mimi kwasababu tu mara ya mwisho ulinishinda , kipindi kile sikuwa makini na nilikudharau na mbinu zako za kichawi”
“Kama unajiamini basi hakuna wa kukuzuia kufanya kile unachotaka, ni sawa kama unataka kufa lakini haitakuwa vizuri kwasisi kuja kuulizwa baadae”Aliongea Roma na kisha akajifanyisha kufikiria.
“Unaonaje ikawa hivi , kwasababu una uhitaji wa mtu wa kupigana nae , kwanini usipigane na Raphaeli”
“Damn it Hades , unanitania , nani anataka kupigana nae?”Alijitetea Hermes.
Ares baada ya kuambiwa pigane na Raphaeli alionyesha kuwa katika hali ya furaha mno , ukweli ni kwamba mikono yake ilikuwa ikimuwasha muda wote , hakujali kama angeweza kushinda au kushindwa alitaka kupigana tu.
“Hehe.. Hermes wewe ndio ulijifanyisha kuwa Farid kule Tanzania si ndio?”
“Farid !!, yupi huyo?”
“Haishagazi kwa mtu kama wewe kukosa makando kando na haina haja ya kujifanyisha hujui ninachomaanisha, ijapokuwa sijui kwanini ulileta mkanda wa kichawi feki Tanzania lakini haitokei tu ukaamua kunichokoza mimi peke yangu”
“Unamaanisha nini? , Hermes ule mkanda wangu feki ulionekana Tanzania wewe ndio uliehusika na kuzusha habari hizo?”Aliuliza Christen kwa mshangao.
“Aphrodite unaamini vipi anachoongea , kwanini nifanye kitu cha namna hio kwa faida ipi kwa mfano?”
“Acha kongea ujinga , Hades hawezi kuongea bila kuwa na ushahidi na zaidi ya yote Hermes tumejuana kwa muda mrefu tokea katika syari yetu, siku zote ukidanganya unakuwa na utulivu wa hali ya juu mno”
“Wewe..”Alitaka kuongea lakini aliishia kimwangalia Poseidon na wengine wanavyochukulia swala hilo.
“Mnaonaje na nyie , mnadhani ni mimi niliefanya kitendo hiko , mnamuamini Hades anachoongea tofauti na mimi , nitapata faida gani nikifanya hivyo kwanza?”Alijitetea. na Stern na Alice hawakuongea chochote na kuweka sura za maigizo.
“Hermes your skills in deception is not as good as your illusions”Aliongea Poseidon akimwambia uwezo wake wa kudanganya ni mdogo kuliko uwezo wake wa kutengeneza udanganyifu.
“Poa, nakubali kwamba wote nyie mnanijua vizuri , na nakubali nilifanya mimi , lakini sababu kubwa ni kwamba nilikuwa ninajisikia vibaya hivyo nikaona nikamchokoze Hades , kuna ttatizo juu ya hilo?”Aliongea kinafiki alikuwa akijua anadanganya.
“Hehe.. Hermes sijali sana kuhusua mambo yako ya kishenzi unayoyafanya , kama kweli umekasirika sasa hivi kwanini usitolee hasira zako kwangu kwa kujaribbu kunipiga”Aliongea Ares.
“Pumbavu , nina hasira kweli , lazima nikufundishe adabu wewe mshenzi”Aliongea kwa hasira huku akisimama na alimwangalia Roma kwa dakika kadhaa na kisha alisogelea Balkoni na kupotea nje na mabawa yake kama vile ni Makerubi akimfukuzia Ares.
“Aphrodite , Hermes ndio aliezusha uzushi juu ya mkanda wako wa kichawi , huna mpango wa kwenda kuungana na Ares kumshikisha adabu Hermes?”Aliuliza Alice akitania.
“Hapana, uwezekano wa sisi kushinda au wa Hermes kutushinda ni asilimia hamsini kwa hamsini, nilikuwa nikijaribu kukaa upande wa Hades tu hapa , sijali kati yenu anaetumia jina langu kwa mambo yenu”
“Vyovote vile , lakini kumuacha Hermes kwenda kushindana na yule kichaa ili tu kutoa hasira zake ni sawa na kupigana na yale Majitu tu”Aliongezea Stern huku akicheka.
“Ni wazi kabisa wametuleta hapa kwa makusudi , vinginevyo wasingeenda ndani ya hoteli ambayo ulipanga kukaa Hades , inaonekana wanasubiria wote tuwe sehemu moja ndio watushambulia , hivyo kwa muda kama huu kama tutakuwa na haraka na kukosa mpango lazima tutaingia kwenye mtego wao , hivyo tunapaswa kusubiri kuona ni nini wanatuandalia , isitoshe Athena hayupo hapa na hatuwezi kujihakikishia ushindi wa moja kwa moja”Aliongea Poseidon.
“Mbona unamuamini sana Athena?”Aliuliza Roma.
“Tayari nasikia umekutana nae na kuona uwezo wake , je sipaswi kujiamini?”Aliuliza na kumfanya Roma kushindwa kuongea chochote , ukweli ni kwamba katika nyakati zoe ambazo aliweza kukutana na Athena hakuweza kufanya chochote mbele yake , tukio la Korea kusini halikuwa limefutika katika akili yake na kila siku alikuwa akifikiria ni kwa namna gani anaweza kuwa katika levo za juu kumpita Athena.
Lakini kwa wakati mmoja alishindwa kuelewa ni kwa namna gani hao watu wenye asili ya Ujitu wametoa wapi hali ya kujiamini mpaka kujitokeza na kuanza kuwachokoza makusudi.
****
Siku nyingine ya mashindano iliwadia katika jiji la Palermo , watu wengi walikuwa wakitarajia kwanzia siku hio mashindano yangekuwa ya moto sana kwani makundi makubwa makubwa ndio ambayo yalikuwa yakikutana.
Kila mmoja aliekuwa akimfahamu Roma alifurahi kwamba amerudi na alikuwa akishiriki , Kwa Sauron alonekana kama vile amezeeka tu ndani ya siku mbili zilizopita lakini mara baada ya kumfuata Roma hotelini asubuhi kidogo hali yake ya utulivu ilimrejea.
Roma hakuwazuia wasiendelee na uchunguzi, alihitaji kujua zaidi kuhusu tukio lile , alitaka kujua kuhusu kundi la kigaidi ambalo limemteka Clark na kutaka kuunda siraha ya kimaangamizi ya teknolojjia ya FURY.
Kwa wakati huo uchunguzi ulikuwa ni rahisi kutokana na kwamba Umoja wa Norh Buyeo kutoka Korea ulikuwa ukijihusisiha , hivyo Roma alimpa kazi Makedon na wengine kujaribu kutafuta nguvu ambayo ipo nyuma yao na pamoja na mipango yao yote.
Wakati mashindano yanaanza Roma alikuwa eneo la VIP huku kulia na kushoto akiwa na Mage na Magdalena.
Upande wa Magdalena alikuwa na aibu sana asubuhi hio kumwangalia Roma usoni , pengine huenda ni kwasababu ya kile kilichotokea usiku kucha.
Ukweli ni kwamba baada ya chakula cha usiku Rose yeye alichukuana na Christen na kusingizia wanaenda kufanya Shopping , ilikuwa ni usiku ndio kakini maduka katika jiji la Palermo yalifanya kazi masaa ishirini na nne na watu ambao walikua ni maarufu maarufu wanaofika katika jiji hilo walikuwa wakifanya Shopping usiku ili kuepuka macho ya wengi.
Sasa kilichotokea ni kama kuna mpango ambao Rose na Magdalena walikuwa wamepanga , kwani wakati Rose alivyotaka kwenda kufanya Shopping Magdalena yeye alisema amechoka na alitaka kulala, upande wa Roma na yeye alikuwa amechoka kwa kutolala siku mbili mfululizo hivyo alitaka kupumzika.
………….
Kutokana na wote kupewa chumba kimoja basi ilitokea , Roma na Magdalena wakalala kitanda kimoja.
“Magdalena vinauma?”Ni sauri ya mwanaume iliosikika usiku wa jana katika chumba cha hadhi ya juu alichokuwa akilala mfalme Pluto.
Licha ya mwanaume kuuliza swali la namna hio , hakukuwa na majibu kutoka kwa mwanamke mrembo aliekuwa amelaliwa kwa juu na mwanaume aliejengeka mwili kimazoezi, upande wa yule mwanamke alionekana kuwa katika raha ya ajabu kiasi kwamba alitumia miguu yake na kuipitisha katika kiuno cha mwanaume yule.
“Arggh..”Mwanamke alitoa mguno huku akiachama kama vile kabanwa na mlango , alionekana alikuwa akipitia hali ya maumivu na raha kwa wakati mmoja
“Samahani , lakini inaonekana kubanwa sana ndio maana unasikia maumivu”Aliongea mwanaume kwa sauti ya kunong’ona, ilionekana kwa upande wa mwanamke kinachoendelea kwake kilikuwa ni mara yake ya kwanza kufanyiwa.
“Ni sawa tu , nitapona kwa haraka , isitoshe na mimi pia sio wa kawaida”Ilisikika sauti nyororo ya mwanamke.
“Kama ni hivyo basi nitaanza kuchezesha kiuno”
“Sawa , usije kunifanya niijutie hii siku”
“Usijali , nitahakikisha hii siku unaikumbuka katika maisha yako yote”Aliongea yule mwanaume kwa besi na kisha makalio yake yalionekana kubonyea chini.
“Argh…!!”
…………….
Naam hayo ndio maongezi yaliosikika nje ya mlango wa chumba cha mfalme Pluto usiku wa jana.
Sasa wakati wakisubiria pambano lianze , ndio Roma alimuuliza mrembo Rose namna usiku wake wa Shopping ulivyokuwa na mrembo huyo alimwelezea kwa ufupi.
“Hakuna kikubwa kilichotokea”Alijibu Rose.
“Pengine anaona aibu , jana kanunua nguo za ndani kibao ambazo zimekaa kiuchokozi uchokozi”Aliongea Christen bila aibu na kumfanya Rose amkazie macho na alijikuta akiona aibu, Bahati tu waliokuwepo karibu yao ni Stern na Alice , angejisikia aibu sana kama Ron na Sauron wangekuwepo hapo.
Christen hakujali namna Rose alivyokuwa akimwangalia na alitoa ulimi kumtania na kisha akageuza shingo yake mbele.
“Kama ni hivyo , hakikisha unanunua za kutosha”Aliongea Roma akiwa na uso uliokaa kifisi.
“Haikuwa hivyo..Usimsikilize Christen”
“Najua , mimi natoa maoni yangu tu , ila usisahau usiku wa leo nataka kuona namna utakavyopendez… sawa Babe?”
………………
Wakati wakiendelea kuongea hatimae ilifikia zamu ya The Eagles , washindani wao ilikuwa ni kundi la Kimasenari lifahamikalo kwa jina la Odin Mercenary Corp, walikuwa na makazi yao Kaskazini mwa ncha ya dunia.
Rose na Magdalena mara baada ya kuona ni watu wa Roma waliweza kuongeza umakini , lakini upande wa Roma alionekana kabisa kutopenda sana kuangalia maishindano ya aina hio kwani yalikuwa ya kawaida sana kwake.
Lakini licha ya hivyo alifurahi kuona wanajeshi wake walikuwa wameimarika sana , hususani Maninja upande wa New Zero kwani walionyesha uwezo mkubwa katika kupambana na wapiganaji wa kundi la Odin, mpaka kipenga cha mwisho kinapulizwa The Eagles waliibuka washndi na kuigia katika hatua inayofuatia.
Roma ndio aliekuwa wa kwanza kuondoka na hakuwa na mpango kabisa wa kurudi tena, upande wa Rose mara baada ya kuona Roma kaondoka katika hilo eneo na yeye alifuata nyuma nyuma lakini kwa Magdalena yeye alisema ataangalia mashindano hayo mpaka mwisho
Ukweli ni kwamba alitaka kuendelea kuangalia , ila tu kumpa nafasi na Rose kuwa karibu na Roma kwani usiku wa jana kama sio Rose basi huenda asingeweza kuonja dunia ya mapenzi kwa mara ya kwanza katika maisha yake, alikuwa na raha na akili yake yote ilikuwa ikiwaza usiku wa jana wote aliofanya mapenzi na Roma.
Hakuwaza rena kama Roma alikuwa mpenzi wa pacha mwenzake au mume wa rafiki yake wa utotoni Edna , bali muda huo alijiambia amefanya maamuzi sahihi kufata kile moyo wake unachotaka.
Wakati Roma na Rose wanakaribia hotelini waliweza kukutana na mwanaume wa Kijapani , Rose alionekana kumfahamu mwanaume huyo na upande wa Roma pia alikuwa akikumbuka sura ya mwanaume huyo, alikumbika kipindi alichosafiri kwenda Japani akiwa na Dorisi aliweza kukutana na huyo mwaname katika kambi ya jeshi wakati akienda kumpatia mateso Kapteni Kisu Mvunjiko na alishangaa kumuona akiwa hapo kwani alikuwa na cheo kikubwa mno serikalini.
Roma ilibidi kwanza amhoji Rose inakuwaje akawa anamfahamu huyo Mjapani na ndipo alipomuelezea kwamba alikutana nae usiku wa jana akiwa na Christen na huyo mwanaume ndio aliewasogelea na kuwachombeza kwa ajili ya kwenda kumpa huduma usiku kucha kwa malipo ya hela , lakini Christen akamjibu kwa kumwambia yeye atamlipa kwa kila pigo atakalompiga na ndio akaondoka na kuwaacha.
Roma mara baada ya kusikia hivyo aliguna , aliona sio jambo la kawaida kigogo wa serikali kutoka Japani ghafla tu kumsogelea Christen na Rose na kuwataka wampatie huduma.
Baada ya kuingiwa na wasiwasi ya uwepo wa mwanaume huyo hapo Sicilly haraka sana alimpigia simu Sauron na kumpa maelekezo ya kumfanyia uchunguzi , hisia zake zilimwambia huenda alikuwa akihusika na wale watu wa mavazi meupe au kundi la Cyclops.
*****
Ikiwa ni muda wa jioni kabisa wakati Roma akiwa ameuchapa usingizi mara baada ya kazi nzito alioifanya na Rose mlango wa chumba chao ulifunguliwa na Magdalena.
Mara baada ya kuona namna Rose na Roma walivyolala wakiwa hawana nguo mwilini alijikuta akiona aibu , lakini alijitahidi kujikaza na kwenda kumuamsha Roma.
Roma mara baada ya kuamka hakuona aibu licha ya kwamba alikuwa uchi yeye na Rose na alienda mbali kumtania Magdalena na kumwambia ajiunge na yeye lakini Magdalena aligoma na kumwambia kwamba amekuja hapo kumpa taarifa kwamba wenzake wanamuhitaji katika eneo lileile la siku ya jana kwa ajili ya maongezi.
Roma mara baada ya kupewa taarifa hio hakuwa na muda wa kupoteza , alikuwa na hamu kubwa ya kuwajua kiundani watu alioambiwa wana aasii ya Ujitu ndani yake hivyo ndani ya dakika chache tu alikuwa tayari amekwisha kujiandaa na kutoka.
Roma mara baada ya kufika aliweza kukuta kila mmoja alikuwa amekaa katika nafasi yake na yeye pia alisogelea kiti na kuketi , lakini wakati huo akiangalia barua iliokuwa juu ya meza.
“Nini kinaendelea hapa , hio ni nini?”Aliuliza Roma na kumfanya Christen aliekuwa akimwangalia Roma muda wote katika eneo la chini ya kiuno chake palivyotuna kuvuta mdomo na kisha kuchukua ile barua na kumpatia.
“Je ungependa kujifunza lugha yetu?”Aliuliza na kumfanya Roma kuangalia ile barua ilioandikwa kwa herufi zisizoeleweka na kumrudishia Christen.
“Haina haja , ninajua lugha nyingi sitaki kuongeza nyingine kwenye kichwa changu , niambie barua hii inahusu nini”
“Ni rahisi tu , ni kwamba kiongozi wa Cyclops anaefahaika kwa jina la Brontes ametutumia mwaliko , anatualika sisi wote kwenda kupata chakula cha mchana katika mgahawa siku ya kesho baada ya awamu ya kwanza ya mashindano ya asubuhi”Aliongea Poseidon.
“Kwanini wanataka kukutana na sisi? , hawajawahi kututafuta hapo kabla”Aliuliza Roma.
“Hata sisi imetushagnaza pia , wanaonekana kama hawatafuti kulipiza kisasi na wanajaribu kutualika namna hii , wanajaribu kufanya nini?”Aliongea Stern.
“Kwanini tujali wanachotaka , huenda wametualika kwa ajili ya kumaliza tofauti zetu , lakini kama wanataka kupigana na sisi tutapigana na kama wanataka amani tutawaacha waendelee kuishi”Aliongea Ares na kufanya wote wamwangalie kwa mshangao kidogo lakini haa hivyo washazoea Ares amekaa kifujo fujo.
“Hivi wasiwasi wenu ni kwamba tunaweza tusiweze kupambana nao?”Aliuliza Roma baada ya kimya cha muda mfupi.
“Kama tungekua kwenye sayari yetu , wasingethubutu hata kutusogelea na ningewapiga mimi mwenyewe, lakinii sasa hivi mambo ni tofuati bila ya Athena na Zeus tunaweza tusifanikiwe kuwashinda ijapokuwa tutakuwa na uwezo wa kujilinda”Aliongea Hermes.
“Mimi nipo , yupo pia Rose na Magdalena ambao wote wapo katika levo ya Nafsi , je bado tu haitoshi , kwanini tuwaogope?”Aliuliza Roma.
“Hades unawachukulia poa hawa majitu , ngoja nikuambie Cyclops na Hecatoncheires wanao uwezo mkubwa kuliko jamii zote za majini na hawaathiriki na nguvu za mbingu na ardhi kwasababu wana damu ya kizazi chetu , Damu ya Titan”Aliongea Artemis.
“Damu ya Titan!!?”Aliuliza Roma kwa mshangao.
“Ndio …”Alice aliwaangalia wenzake kuona kama kuna ambaye anajaribu kumzuia na baada ya kuona wapo kimya aliendelea.
“Damu ya Titan ndio asili yetu kamili na sisi ni mwendelezo wa kizazi cha damu yake , ndio chanzo kikubwa cha nguvu zetu wakati tulipokuwa kwenye sayari yetu m sababu ambayo imetufanya uwezo wetu kushuka kufikia asilimia therathini ni kwasababu tulikosa miili yetu yenye asili ya damu ya Titan , hawa Majitu wenyewe ni sehemu ya uzao wetu hivyo wana asili ya damu ya Titan na kama tulivyosema mwanzo, wao walikuja duniani na wakaweza kuishi kwa miili yao lakini sisi ikashindikana, Mpaka sasa hivi damu yetu ipo Sealed”
“Hebu subiri kwanza , nilikuwa nataka siku zote kuuliza ilikuwaje miungu mkapoteza uwezo wenu kwa kiasi kikubwa , kama kweli hii damu ya Titan ndio chanzo cha nguvu zenu , kwanini ipo ‘Sealed’ mpaka sasa , je swala hili lina uhusiano na moyo wa Gaia?”Aliuliza Roma.
“Kuhusu hilo..”Alice alitaka kuongea lakini alisita lakini palepale Christen na yeye aliingilia.
“Usiulize maswali Hades , kwetu kumbukumbu hizo ni maumivu makali kila zinapojirudia .. nitaendelea kukuelezea kwa niaba ya Alice, hawa majitu wanao uwezo mkubwa kutokana na kuwa na damu ya Titan na ndio maana hawaogopi kabisa watu wanaovuna nishati za mbingu na ardhi , kwasababu ni nishati ya muunganiko wa dunia hii , Damu ya Titan unaweza kusema ina nguvu ya Kiroho kama mnavyopenda kuita hapa duniani , sasa unatakiwa kujua ni Zeus pekee ambaye alikuwa na uwezo wa kutumia mwanga kuifubaza nguvu za damu hio na kuwafanya wawe dhaifu , hivyo hakuna mtu ambaye anaweza kuwashinda hata Athena mwenyewe hakuwa na uwezo huo”
“Kwa maelezo yenu mnaamaanisha kwamba tunapaswa kufa kwenye mikono yao si ndio?”Aliuliza Roma huku akitabasamu kwa uchungu
“Hatuwezi kwenda mbali hivyo , kwasasa hatujui ni ipi mipango yao na isitoshe una nafasi kubwa , angalau unaweza kutumia kanuni za anga pamoja na nguvu za nishati ya mbingu na ardhi , lakini hata hivyo inatia huzuni kwasababu haupo kwenye levo ya juu zaidi ya kuweza kudhibiti Radi kama Majinni tuliokutana nayo kipindi tunafika la sivyo ungekuwa tishio kwao”Aliongea Poseidon.
Roma alijiambia hata kama hakuwa katika levo za juu kama watu waliowakuta miaka hio , lakini yeye alikuwa na chungu cha maafa hivyo alijiambia kwamba mwisho wa kila kitu bado haujulikani kama watapambana.
Hao watu kilichomuudhi sana ni kwamba ni wasiri sana kuhusu hio damu ya Titan na alijua kabisa ameelezwa nusu na ni kitu ambacho kinahusiana na moyo wa Gaia
Baada ya mazungumzo ya muda mfupi Poseion alimtaka Hermes kunagalia Ulingo kama haujawekwa mtego ili kuwa salama na haikuwa tatizo kwa Hermes kulingana na spidi yake
******
Siku ya tatu hatimae iliweza kuwadia na makundi therathini na mbili yalikuuwa ndo yamebakia , wawakilishi mbalimbali kutoka serikalini walikuwepo.
Kama kawaida Poseidon , Hermes na Ares walikuwa katika eneo lao la sku zote na Roma , Magdalena , Rose Alice , Stern na Christine wlaikuwa wamekaa katika eneo moja.
Kabla ya mashindano kuanza Roma aliweza kupokea ripoti kutoka kwa Makedoni juu ya baadhi ya chunguzi alizomwambia Sauron afanyie kazi.
Na kwa maelezo yake ni kwamba mwanaume wa Kijapani aliemuona katika hoteli ya Cassano alikuwa akifahamika kwa jina laKagawa Chusho na ni waziri wa ulinzi wa Japani na hana uhusiano wowote na kundi la watu wa mavazi meupe , lakini alimwambia kwamba wakati ambao alimuona hotelini ilionekana kulikuwa na kikao kilichokwisha kufanyika hivyo hawakuwa na uelelwa nini kilitokea au kilizungumzwa katika kikao hicho ndani ya hoteli ya Cassano.
Roma kuna hisia ambazo zilimwambia kabisa huenda serikali ya Japani ilikuwa ikihusika kabisa na uwepo wa hawa Majitu hapo Sicilly lakini hakuwa na namna ya kuthibtisha dukuduku lake kutokana na kwamba alijua fika kikao ambacho kilifanyika ndio kilikuwa na taarifa kamili lakini kwa bahati mbaya walichelewa kugundua mapema..
Wakati ambao Roma alikuwa katika mawazo alikuja kushituliwa na Sauron aliekuwa anakuja mbio mbio kwake .
“Your Majesty Pluto something is wrong”Aliongea Sauron akimwambia kuna tatizo.
“What are you saying?”(Unaongea nini?”);
‘Hapa , hebu angalia wahusika ambao wanakwenda kushiriki katika mecho inayofuatia”Aliongea Sauron na kushika Kishikwambi alichokuwa ameshikilia Sauron.
“Mechi inayofuata ni The Eagles na Deicide?”Aliongea Roma kwa mshangao akimaanisha kwamba mechi inayokwneda kuanza ni kati ya Majitu wanaojiita godkiller na wanajeshi wake wa The Eagles.
“Nini kimetokea , nilijua wanakwenda kukutana katika nusu fainali tu?”Aliuliza Roma huku akiwa na wasiwasi na kuanza kupitia orodha ya wanajeshi wake ambao wanakwenda kushindana katika mechi inayofuata.
“Kuna mtu ambaye amebadilisha na meneja anasema ni makosa tu yaliofanyika , nadhani ni makusudi kabisa wanataka tukutane kwanza na hao wauaji ili watudhalilishe kututoa katika mashindano mapema“Aliongea Sauron kwa hasira.
Lakini licha ya hivyo ni kama washachelewa , kwani tayari wanajeshi wa The Eagles walionekana wakiingia kwenye ulingo na walionekan kuwa na mchecheto mara baada ya kusikia wanakwenda kupambana na kundi la Deicide watu waliowaonyeshea kiburi katika hoteli ya Federico.
Wakati Nasri na wenzake wakiwa na shauku ya kulipiza kisasi kwa kuwashikisha adabu watu hao, upande wa Roma alikuwa na wasiwasi kwa kile kinachokwenda kutoktea kwa kuamini kwamba wanajeshi wake hao hawana uwezo wa kushinda na kwa mara ya kwanza jeshi lake linakwenda kudhalilishwa.
Makofi ya shangwe na vifijo yalisikika pande zote baada ya wanajeshi wa mavazi meupe kuingia kwa mbwembwe zote na baada ya kufika katikati waligeuka upande ambao wamekaa Poseidon , Roma na ndugu zake na kuwaangalia , ijapokuwa sura zao hazikuwa zikioneana kwa kuvaa Mask lakini likuwa ni kama vile walikuwa na sura za kejeli.
ITAENDELEA WIKIEND NJOO WATSAPP TUPIGE STORI NAMBA 0687151346
[emoji15][emoji15][emoji7]SEHEMU YA 570.
Jerry alidhani alikuwa akiota , mlango huo ulikuwa ni wa chuma kigumu sana , imewezekanaje ukabobolewa kirahisi namna hio.
Muda huo ni shoti pekee za umeme ambazo zilikuwa zikisikika ndani ya eneo hilo na Roma wala hakujali kabisa aliingia kama vile ni mnyama.
Nyuma yake kulikuwepo na damu nyingi ambazo zilikuwa zimetengeneza mfereji mkubwa wa damu kuingia ndani mara baada ya mlango kuvunjika.
Zilikwa ni damu za walinzi ambao walikuwa walilinda katika hilo eneo na ilionekana dhahiri kabisa Roma aliwapasua pasua viungo vyao pasipo huruma.
Roma mara baada ya kugundua eneo ni lenyewe , alitolea hasira zake zote za kutafuta usiku kucha kwa walinzi hao na aliwaua vifo vibaya sana, huenda ni aina ya vifo ambavyo havijawahi kutekelezwa hapa duniani , vilikuwa ni vya ukatili wa hali ya juu sana.
“Clark!!”Aliita mara baada ya kumuona Clark aliekuwa yupo chini sakafutni akitetema kama mgonjwa mwenye kifafa na palepale alimkimbilia na kumkalisha.
“Nini kimetokea ?Umepewa sumu?”Aliuliza Roma kwa wasiwasi mkubwa na hakuacha kujaribu kumchunguza kwa kumuingizia nguvu za kimaandiko.
“I… I knew it ..you.. would save me ..just like ten years ago..”Aliongea kwa tabu sana akisema kwamba alijua tu atakuja kumuokoa kama miaka kumi iliopita.
Roma macho yake yalianza kuwa mekundu hakuwa na uwezo wa kujua ni aina gani ya sumu ambayo ipo kwenye mwili wa Clark , alikuwa na uwezo wa kuhisia sumu iliokuwa kwenye mwili wake ilikuwa ikinyong’onyesha saa utendaji kazi wa mwili.
Lakini alishindwa kumponyesha kwani sumu iliokuwa kwenye mwili wake iliionekana tayari ishaingia kwenye mfumo wa damu moja kwa moja na wakati akiwa amemshikilia palepale alitema damu nyingi nje mara baada ya Roma kujaribu kumponyesha.
“Ni sumu ya aina gani hii , niambie namna ya kukuponyesha”Aliongea Roma akijaribu kumtingisha lakini Clark aliishia kutingisha kichwa chake akimuonyesha ishara kwamba hakuna namna ya kumponyesha.
“Ni sumu ambayo niliiandaa dakika ya mwisho kabisa na ili kuhakikisha hawawezi kuniponyesha nilitumia mbinu ya kipekee ambayo inafanya viungo vya mwili kutofanya kazi sawasawa .. kwasasa haiwezekani kitu”Aliongea kwa tabu na kumfanya Roma palepale kumgeukia Jerry ambaye alikuwa amemsahau kwa muda.
“Wewe mnyama , yote haya ni kwasababu yako , kama utafanikisha kumponyesha mwalimu wako nitakuua lakini mwili wako sitouharibu”Aliongea Roma kimkwara huku akisambaza msisimko wa hali ya juu wa nguvu za kijini ili kumuogopesha Jerry.
Muda huo Jerry alikuwa ameshikwa na ubaridi wa aina yake hasa baada ya kuona damu nyingi zikiingia ndani kutokea nje , lakini licha ya hivyo chuki yake zidi ya Roma ziliifunika hofu yake na kaunza kucheka kama kichaa.
“Wewe shetani ijapokuwa sijui namna ulivyoipata hii sehemu lakini nakuambia hivi hakuna namna ya kumuokoa , sumu ambayo Clark ametengeneza anaweza kutengenza dawa yeye mwenyewe , inatia huruma kwamba anakufa kwenye mikono yako ukiwa huwezi kumsaidia “
“Unakiomba kifo wewe..”Aliongea Roma huku akitaka kumshambulia lakini Jerry alimzuia kwa kumpigia makelele.
“Usinisogelee, ukinigusa tu hii maabara yote italipuka na zile FURY mbili zitalipuka, madhara hayatakuwa kwako tu lakini kwa ukanda wote wa eneo la Bavaria, Ujerumani yote itageuka na kuwa toharani ya dunia, Je upo tayari kutoa kafara mamilioni ya watu kwa ajili ya kuniua mimi?”Aliongea na kumfanya Roma kunasa neno FURY.
“FURY siraha aliotaja je ndio sababu ambayo imewafanya wakuteke?”Alimuuliza Clark.
“Ndio .. niliipatia jila hilo ikimaanisha neno kisasi”Aliongea .
“Inahusiana na nini?”
“Ni aina ya siraha ya nyuklia ambayo teknolojia yake imeboreshwa zaidi … risasi yake moja ni sawa na risasi mia tano za bomu la Hydrojeni”
“Nini..!!”
Roma alishangaa kwa uhatari wa siraha hio , kama kweli risasi moja ni sawa na risasi mia tano za bomu la Hyrdrojeni si ni hatari hio , maana kama siraha hio ikatumika basi mionzi yake isingeathiri tu Ujerumani huenda na nchi za karibu.
Alijiuliza inakuwaje watu wa North Buyeo na kundi la kigaidi kutafuta teknolojia ya namna hio, ni kipi ambacho wanalenga?.
“Hehe.. sasa nadhani tayari ushajua ukuu wake, ninataka kuona kama utathubutu kuniua …Wewe shetani utapata maumivu makubwa sana baada ya mwanamke unaempenda akifa mbele yako …Hahaa, nimesubiria hii sku kwa muda mrefu sana , na unastahili kwa kila kitu , unapaswa kwenda jehanamu”Aliongea kwa hasira .
Roma alikuwa katika kiwango cha juu cha hasira na alitamani kumfanya kitu kibaya , lakini hakuweza kuthubutu kufanya maamuzi ya haraka kwani maisha ya watu zaidi ya mamilioni yalikuwa hatarini.
“Nini tatizo , Umekosa ujasiri tena?, Umejileta mwenyewe hata hivyo , ninakwenda kulipiza kisasi cha vifo vya familia yangu , baba yangu , mama yangu na dada yangu ambaye alikuwa na miaka mitatu tu”
“Kisasi? Ni kipi nimekufanyia mpaka kutaka kulipiza kisasi?”
“Bila shaka hukumbuki , umeua watu wengi sana unawezaje kuwakumbuka wote , umesahau ulichokifanya miaka mitano iliopita pale Simbokrog nchini Belarus kwenye kijiji cha Wozic si ndio?”
“Kijiji cha Wozic ?”Aliongea Roma huku akikunja sura , hakuwa akikumbuka kabisa kama kuna sehem kama hio na isitoshe kulikuwa na maeneo mengi madogo madogo aliopita ambayo hakuyakumbuka na kote hhuko huenda aliua.
“Unaonekana hukumbuki , Kijiji chetu kilikuwa na watu 186, kati yao therathini walikuwa ni watoto na wakati huo ni mimi pekee ambaye sikuwepo nyumbani kutokana na kwamba nilienda shuleni kwenye mji mwingine wa pembeni , lakini wewe ukaja na kufyeka kila mtu uliemkuta kijijini bila kujali wana hatia au hawana kwasababu tu adui yako alikuja kwenye kijiji chetu , kwanini usingeacha hata maisha ya watoto wadogo ambao walikuwa hawana hatia , kwanini ulivyomaliza ukawachoma na moto…”Aliongea Jerry kwa hasira kubwa na kauli yake ilimfanya Roma sasa kukumbuka lakini hakuwa akikimbuka vizuri sana , kipindi anafanya hivyo alikuwa katika hali ya ukichaa na ugonjwa wake ulikuwa ndio unaitawala akili yake.
Alikumbuka kabisa kitendo cha kuua watu wa kijiji kile ndio kilichosababisha Seventeen kumkimbia na mwisho wa siku akaingia kwenye mikono ya maadui na kumuua akiwa na ujauzito tumboni mbele ya macho yake.
Roma alishindwa kujizuia kusikia uchungu kutokana na maelezo ya Jerry , haikujalisha alikuwa akitamani kuwa na maisha ya amani , lakini mambo ambayo ameyafanya miaka iliopita yalimfanya kutengeneza maadui wengi ambao muda wowote watataka kulipza kisasi na aliona hata kwa Jerry ni mwanzo tu.
Lakini licha ya hayo yote , kipindi hicho akili yake ni kama ilikuwa ikiendeshwa kwa rimoti , ugonjwa wake ulikuwa mkubwa kiasi kwamba alikuwa ni kama shetani na bila kumwaga damu kwa siku hakuweza kutulia.
“Naona sasa unakumbuka ..?”Aliongea Jeryy huku akifuta machozi .
“Unapaswa kuadhibiwa pia , mwanzoni wakubwa waliniahidi watanisaidai katika kulipiza kisasi , na nikaamua kuishi na chuki na kuvumilia mpaka leo hii , lakini kwa leo kwasababu umepajua hapa sina mpango wa kuondoka hapa nikiwa hai”
“Unapanga kufanya nini , je unafikiri kulipua hilo bomu la FURY na kuniua kutakufanya ulipize kisasi cha ndugu zako , sahau kabisa hizo ni ndoto za kufikirika utaua watu wengi kuliko mimi”
“Inanihusu nini , ni matendo yako ya kishetani ndiio ambayo yamenifanya kuwa katika hali hii , usijaribu kunidanganya, hata kaam nitaondoka leo utanitafuta na kuniua , ni kheri niende na mamia ya watu katika kaburi langu , maisha ya hawa watu yatakuwa yametolewa kafara kwa sababu yako hahahaa..”
Baaada ya kuongea huku akicheka kwa kejeli palepale alisogea upande wa kulia wa kile kioo cha kuzuia mionzi na kukipiga ngumi kwa nguvu kubwa.
“Twiii , Twi, Twiit”
Ilionekana ndio namna maabara ilivyotengenezwa ili kuilipua njia ya mkato ya kuwasha bomu ni kupiga ngumi kioo na hicho ndio ambacho kilikuwa kikienda kutokea , hata hivyo maabara nyingi za kufanya majaribio ya siraha hutegeshewa bomu la kuiharibu kabisa pale panapotokea tatizo.
Muda uleule alivyoopiga ngumi kile kioo sauti kutoka kwenye tarakishi humo ndani ilisikika ikiwatahadharisha.
“Destruction Mode has been turned on , the labaratory will be exploding after the countdown , thirty .. twenty nine…”
“Ni mwisho haha , hatimae imekuwa mwisho”Aliongea Jeryy.
Roma alishangaa , hakutaka kumuua Jerry kwasababbu aliogopa siraha hio ya FURY ingelipuka , lakini sasa hivi maabara yote inakwenda kulipika , ilikuwa haiwezekani kwa yeye kuzuia kutokulipuka kwa bomu hilo la nyuklia.
Roma aligeuza macho yake na kumwangalia Clark aiekuwa kwenye mikono yake ambaye afya yake inaelekea ukingoni alijikuta aking’ata meno yake kwa hasira
Baada ya kuona hana uwezo wa kuzuia mlipuko wa maabara hio pamoja na mlipuko wa FURY kitu pekee ambacho aliona angeweza kufanya ni kujiuoko yeye na Clark kuondoka katika hilo eneo.
Kufumba na kufumbua alikuwa ashatoka nae na kwenda kutua mbali kabisa na eneo hilo katika mlima na msitu usiokaliwa na watu, Kusini mwa nchi ya Austria.
Alikadiria kwa umbali huo hata kama bomu hilo la nyuklia litalipuka upande wa Ujerumani halitowaathiri kwa muda kupitia mionzi yake.
Baada ya kutafuta sehemu yenye majani makavu aliamua kumuweka Clark chini na kuanza kumfanyia uchunguzi wa mwili wake.
Haikuleta maana kwake kuomba msaada kwa muda huo , kwani aliona asingepata msaada huo ndani ya muda , hivyo kitu pekee ambacho alitaka kujaribu kufamnya ni kumpontysha yeye.
Mapigo ya moyo ya Clark yalikua ya chini mno na yalikuwa yakiendelea kuwa ya chini na muda wowote yangeacha kabisa kudunda na kupelekea kifo chake.
Roma alijikuta akijikatia tamaa mara baada ya kumungizia nishati ya mbingu na Ardhi kwa kuunganisha na ya Urejesho lakini bado alishindwa kumponyesha.
Mwili wake ulikuwa ni kama vile seli zake zinaoza ndani kwa ndani na hiko ndio kilichomuogopesha zaidi , kwani aliona dakika yoyote Clark angeweza kufa kwenye mikono yake maana tayari alishaanza kuwa wa baridi.
“Damn it … Clark , jarobu hata kuongea kidogo , ninaweza vipi kukuokoa?”Roma ujasiri wake wote ulimwishia na aliishia kuukumbatia mwili wa Clark huku akishindwa kuzuia machozi yaliochanganyika na hofu.
Ni mwanamke huyo ambaye hakulala usiku na mchana kwa ajili tu ya kumtengenezea dawa, na katika kipindi chote ambacho alihisi kuwa mpweke ni yeye pekee ambaye alifanya kila liwezekanalo kumsaidai , lakini sasa mwanamke huyo anafia kwenye mikono yake bila ya kuwa na msaada kwake.
Aliogopa kwamba bado hakuwa amelipa fadhila zake zote kwa yale aliomfanyia , alijilaumu na kuona yatakuwa makosa yake kuruhusu akifariki kwenye mikono yake kwani itamaanisha kwamba alishindwa kumlinda na maadui ambao aliwatengeneza yeye mwenyewe.
Clark alijitahidi kuamsha kinyonge sana mkono wake akimfuta machozi roma ,Roma hakujua hata alikuwa akilia alihisi maji yanaririka katika mashavu yake , lakini hakujua kama ni machozi yake .
“Ni sawa … wewe .. usilie tena .. nina furaha , mtu wa mwisho ninaemuona .. ni wewe”Aliongea Clark kwa kukata kata maneno.
Alishindwa kujizuia zaidi na zaidi mara baada ya mwanamke huyo kuongea kauli hio na alizidi kutoa machozi na kulia kwa kwikwi.
“Huwezi kuondoka hivi … utakuwa umenikatili sana ,,,, siwezi kujisamehe tena , umeniokoa mara nyingi sana na umefanya mambo mengi kwa ajili yangu ,, lakini mimi nashindwa kukukoa ,, sina thamani kabisa kwako , mimi ni mjinga”Aliongea huku akiinua mkono wake na kujipiga kibao kwa nguvu na kutokana kutumia nguvu za kijini ilisababisha mpaka majani ya miti kuanza kudondoka lakini bado aliendelea kujipiga vibao mara nyingi zaidi na kumfanya Clark azidi kutoa machozi ya kumuonea huruma na huzuni kwa wakati mmoja.
“Usi.. usi , fanye hivyo”Alijitahidi kuongea.
“Clark naomba usife , naomba usife tafadhari , siwezi kufikiria nitakuwa na maisha ya namna gani ukishaniach…”Alianza kulia kama mtoto huku akimwangalia mwanamke huyo kwa kuomba.
“Na.. naomba,, nikuulize swali na unijibu kabla sijafa?”
“Niulize chochote na nitakujibu”Aliongea haraka haraka.
“Roma … nataka tu .. kujua kama .., je .. unanipenda?”
“Ndio , Nakupenda , siku zote nilikuwa nikikupenda sana ,… wewe ni moja wapo ya wanawake ninaowapenda sana..”Roma aliongea bila kujiuma uma , hayo ni maneno ambayo hakupanga kumwambia mwanamke huyo katika maisha yake.
Zamani hakutaka kabisa kumsogelea mwanamke huyo kutokana na madhambi ya umwagaji damu alioyafanya, lakini baada ya kurudi Tanzania na kujipatia mke ndio kabisa hakutaka kumfanya mwanamke huyo mchepuko kwa kuamini alistahili kitu kikubwa zaidi.
Roma hakuwa na mashaka kabisa juu ya mapenzi yake kwa Clark, ni mapenzi ambayo hayakuanza jana wala leo , ni tokea alivyokuwa mdogo na kadri mrembo huyo alivyokuwa anakuwa alizidi kumpenda.
Mapenzi yake kwa mwanamke huyo yalikuwa sio ya kawaida ambayo yanaweza kueleweka kirahisi kwa binadamu.
Pengine katika dunia kuna wanawake wengi ambao aliwapenda na wao pia kumpenda na kumpa kila kitu na yeye kufanya kila kitu kushinda magumu yote kwa ajili yao lakini mapenzi yake ya kweli katika kumbukumbu zake yapo kwa Seventeen na katika uhalisia yapo kwa Edna na mpenzi anaemuona kama ndoto ni Clark.
“Kweli!?”Aliuliza Clark akiwa kama haamini na alijitahidi kufumbua macho yake ..
“Ni kweli , nilichokwisha kukisema ni ukweli , na unapaswa kuniamini , sijawahi kukuweka wazi kwasababu tu niliona hustahili kuwa na mtu kama mimi , … samahani sikukuambia hili mapema”Macho ya Clark yalionyesha kabisa kufurahishwa na kauli yake na tabasamu la furaha lilifunika uso wake .
“Honey … I knew it , you loved me..”Aliongea.
Roma alikuwa akilia hivyo hakuwa akiongea zaidi ya kutingisha kichwa tu kumwaminisha ni namna gani anamkubali huyo mwanamke.
Clark alipanua mdomo wake huku akiinamisha kichwa chini na alionekana kama anataka kung’ata kitu flani..”
Roma aliweza kuona lakini hakujua Clark anataka kufanya nini na alimwangalia kwa kuchanganikiwa.
“Collar …”Aliongea Clark kwa sauti dhaifu akimaanisha Kola ya koti lake.
Roma palepale alielewa sasa anataka kung’ata nini na alifanya haraka na kumsaidia kumpelekea karibu Kola ya koti ili kuweza kugusanisha na lipsi zake.
“Clark unafanya nini, kwanini unamg’ata Kola ya koti, ni kwa ajili ya nini?”Aliuliza lakini Clark hakuongea neno na muda huo alikuwa kama mtoto anaetafuna nguo kwani alifyonza kwa nguvu ule ukola wa koti mpaka ukaanza kujaa mate.
Ni muda huo huo aliweza kuona Ukola ule wa shati ukibadilika rangi na kuwa wa bluu ambayo haijakolea sana na kama sio kwa kuloana basi isingetokea
Wakati akishangaa palepale aliweza kushangaa mara baada ya Clark kuvuta pumzi nyingi na kuzishusha baada ya kuonekana kumaliza alichokuwa akifanya na kadri dakika zilivyokuwa zikisogea ndio ambavyo alizidi kurudi katika hali yake ya kawaida.
“Unashangaa nini mpenzi? , sijafufuka ni kwamba tu sijafa”Aliongea huku akitabasamu.
“Wewe , umewezaje kufanya hivyo.. nini..?”
“Unataka kuuliza nimewezaje kurudi katika hali ya kawaida si ndio , basi ni kwasababu nimejiponyesha mwenyewe”Aliongea huku akijaribu kukusanya nguvu na kukaa mwenyewe chini.
Roma aliangalia ile Kola ya koti kwa mara nyingine jinsi ilivyokuwa na doa la rangi ya bluu na kisha akamgeukia Clark aliekuwa na uso wa furaha .
“Ulinidanganya?”
“Nani kakuambia udanganyike kizembe , mimi ni nani , mimi ni Profesa Clark, mwalimu wa mwanafunzi mjinga kama Jerry , hivi unadhani naweza kuzidiwa akili na mwanafunzi niliemfundisha mimi?”
Roma alikosa cha kusema, alimwangalia mwanamke huyo namna ambavyo aliweza kurudi katika hali yake ya kawaida kwa haraka sana na alijikuta akichoka kabisa na kujikalia chini.
“Huu ulikuwa ni mpango wako?”Aliuliza Roma.
“Ndio , hivi unafikiri ungeweza kunipata kwa kubahatisha , wakati nilipokuwa nikitumia tarakishi zao nilituma Link kwa siri katika satilaiti yenu , kama mwalimu nilimjua Jerry hakuwa vizuri kwenye maswala ya Compyuta hivyo hakuweza kujua ninachokifanya kabisa , nilijua tu kama mtafika maeneo ya karibu na nilipo basi mngehisi mawasiliano ni kama yameingiliwa kutoka ndani”Aliongea na kumfanya Roma asipinge kwani ndio alivyoweza kumpata.
“Kama ni hivyo vipi kuhusu Sumu ni nini kile?”
“Ile ni sumu kweli , niliweza kuchanganya aina mpya ya sumu nilioitengeneza pale, ni sumu ambayo inavilegeza viungo vya mwili na kukufanya uonekakane kama umekufa na kama hutachukua dawa yake basi utakuwa wa baridi kwa masaa ishirini na nne na ikiisha makali yake mwili utarudiwa na joto lake na utaweza kuamka , nilipanga kama wataniona nimekufa watatafuta sehemu ya kunizika au kunipatia matibabu na ndio nitajua namna ya kutoroka ,lakini hio ilikuwa ni mpango wangu wa mwisho kabisa kwani sikuwa na uhakika kama hawatachoma mwili wangu lakini nilipanga kama hakuna ambae atakuja kuniokoa basi moja kwa moja nitadanganya nimekufa ili kuepuka wasinidhuru, lakini bahati nzuri umeweza kuja ndani ya muda hivyo nikatumia mpango B”Aliongea na kisha akashika Kola ya koti lake.
“Nililoanisha hii Kola na dawa maalumu ya sumu ,ilihitajika tu mimi kunyonya na ndani ya lisaa limoja ninarudi kuwa sawa tena”
“Kama ni hivyo kwanini ulinichezea hila hata mimi , hivi ulijua ni kwa kiasi gani moyo wangu uliuma?”Aliongea Roma huku akisimama na palepale mrembo huyo alisimama na kupitisha mikono yake yote mwili katika shingo ya Roma na kumbusu kwenye paji la uso..
“Kama nisingetumia fursa hii , usingeweza kuniambia nilichotoka kusikia kutoka kwako kwa muda mrefu”Aliongea na wakati Roma anataka kuongea neno alizuiwa na lipsi laini za mwanamke huyo.
Baada ya busu jepesi , Clark alionyesha uso wa kuomba huku macho yake yakionyesha hali ya kutia huruma.
“Honey usinikasirikie , nilitaka tu kuwa na wewe kama mpenzi wako , nilijua kama hutoniambia nitakuwa na huzuni milele”
Roma alijiambia ile siku ambayo alikuwa akiiepuka kwa miaka mingi hatimae imewadia na hakujua anakwenda vipi kumwelezea mke wake kwa maneno marahisi na kumuelewa.
“Umeandaa mpango wako , ili kunifanya niingie katika mtego na ukanifanya nilie kama mtoto , aisee inatia aibu Daah”Aliongea Roma huku akitabasamu kwa uchungu na kumfanya Clark amwangalie kwa macho ya utani huku akimtolea ulimi nje kama anamcheka.
“Nilikuwa nikienda na hali inavyoruhusu , Jerry alinitishia kwenda kuwaua wale watoto wsio na hatia , sikuwa na chaguo lingine..”Baada ya kusikia hivyo alijikuta akikumbuka kitu alichosahau.
“Oh nimesahau kuhusu FURY Ujerumani ndio kwaheri”Aliongea.
“Haha.. nilikuambia kila kitu nilipanga mimi , unadhani ninaweza kutengeneza kitu hatari namna hio”
“Kwahio ulichotengeneza ni nini , ni feki pia?”
“Hebu fikiria , unadhani ninaweza kuhatarisha maisha ya mamilioni ya watu kwasababu ya watoto , hata kama niwe kwenye hali gani siwezi kwenda mbali kiasi hivyo , teknolojia ya FURY kwasasa ipo katika nadharia tu , inawezekana vipi kuitengeneza ndani ya siku mbili au moja? , kutengeneza tu elementi ya mwisho inayokamilisha kanuni inahitajika mchanganyo wa kikemia ambao unaweza kuchukua mwaka mzima kutoa matokeo”
“Kwahio unasema sasa hivi Jerry atakuwa na hasira sana mara baada ya kuona umemdanganya?”
“Labdal , Ujerumani naamini watashughulika na tatizo hilo , kwasasa ninafuraha ya nilichoweza kutimiza baada ya muda mrefu , Roma naomba unibusu japo kidogo tu”
“Nini!”
“Umesema unanipenda hivyo unapaswa kunifidia kwa miaka yote nilioteseka kwa ajili yako”Baada ya kuongea alifumba macho na kunyanyua kichwa chake juu kuweka mdomo vizuri ubusiwe.
Roma aliangalia Lips zake zilizokuwa nyekundu kutokana na weupe wake wa kizungu na kisha palepale alitoa tabasamu la kifedhuli na kumshika kiuno kisha akamvutia kwake.
Clark mpaka hapo alijua kabisa alikuwa amefanya kosa kwa kujirahisisha mbele ya mwanaume ambaye alikuwa kama Simba mwenye njaa.
Dakika moja mbele wote walikuwa kwenye ulimwengu mwingine kabisa ulioitwa Busu, inasemekana wazungu wapo vizuri sana kwenye Kubusu na hicho ndio kilichompagawisha Roma.
MWISHO WA SEASON YA 19
SEHEMU YA 571.
Katika jiji la Palermo giza tayari lilikuwa lishatawala na katika uwanja wa kivita uliokuwa ukifanyia mashindano , ulikuwa mtupu kwa wakati huo ikimaanisha kwamba mashindano kwa siku hio yamesha mpaka siku inayofuata.
Katika siku hio ya kwanza hakukua na maajabu makubwa kwani wale wanajeshi kutoka mashindano yaliopita wote kwa pamoja wameweza kuingia raundi inayofuata na kwa wale wahudhuriaji wenyewe wanasema mapigano yenyewe yanaanza siku inayofuata katika raundi ya pili.
Katika Moja ya Balkonni ya hoteli ya Cassano , mwanaume wa makamo mzungu alievalia mavazi ya upishi meupe alionekana akiwa bize kucharanga samaki aina ya Salmoni kwa haraka sana na kwa ufanisi mkubwa.
Kila kipande cha samaki kilikuwa kikilingana na kingine ni hivyo tu kwamba vilikuwa na ukubwa kidogo ambao unamuwezesha mlaji kutafuna kipande kimoja chote kwa wakati mmoja.
Mbali kidogo na alipokuwa anafanyia kazi mwanaume huyo kulikuwa na meza kubwa ambayo wahudumu wawili walionekana wakiwa bize kumsaidia kuhudumia kila anachokamilisha kupika na kuweka mezani.
Katika meza Christen alinyanyua Glasi yake ya Champagne na kumnyooshea Rose kugonga zao Cheers ambaye alikuwa karibu yake.
“Aphrodite, unaonekana kutokuwa kabisa na wasiwasi , vipi kuhusu hiko kinywaji?”Ares ambaye alikuwa ameegamia kwenye kiti kivivu aliongea kwa kuonyesha sura ya dhihaka.
“Wasiwasi wa nini , nipo hapa kwa ajili ya burudani sio kuteseka”Baada ya kusema hivyo alimgeukia Poseidon ambaye alikuwa akikomaa na upishi.
“Poseidon vipi hiko chakula bado tu? Nina njaa mimi”
“Hakuna mtu kugusa chakula kabla sijamaliza ,atakae fanya hivyo nitahakikisha hali chakula nilichopika mimi”
Upande wa Magdalena aliekuwa kimya alikuwa kwenye mshangao , bila shaka alikuwa akimjua Poseiodon ni mpishi maarufu duniani aliefahamika kwa jina la Mr Kelphin lakini hakuwahi kuwaza mtu huyo huyo kuwa mwanajeshi wa jeshi la Marekani upande wa majini.
“Christen kuna haja gani ya kusubiria amalize kila kitu , kwanini tusianze kula?”Aliuliza Magdalena ambaye alikuwa na njaa.
“Ndio sheria ya Poseidon hio kama atajitolea kupika chakula basi hataki mtu akiguse mpaka aridhike kimekamilika , anajali sana mlo kamilifu kuliko kitu kingine chochote”
“Kwa maneno marahisi Miss Magdalena ni kwamba bwana huyo ni mpishi Mbishi sana kwahi kutokea”Aliongezea Stern na Rose na Magdalena waliishia kushangaa tu.
Dakika chache mbele Poseidon aliweza kukamilisha sahani za Sashimi na kuwekwa kwenye meza hio kubwa , katika meza hio kilichoonekana ni aina mbalimbali ya vitoweo vya baharini ambavyo vimepikwa katika ubora wa hali ya juu.
Na kabla ya kuwaruhusu kula aliwaambia wasiguse kwanza chakula chake mpaka apige Selfie na palepale alitoa simu yake ya I Phone Toleo la juu na kupiga picha mbalimbali ya chakula chake na kisha kupost mtandaoni kwenye akaunti yakeiliokuwa ikifuatiliwa na watu zaidi ya milioni.
Baada ya kutaniwa na ndugu zake kutoka sayari nyingine , hatimae aliweza kukaa sasa na kuwaambia wale wahudumu waondoke.
Ukweli Magdalena na Rose walipata fursa ya kushiriki kwasababu ya heshima ya Roma pekee , lakini chakula hicho cha usiku ni kama vile kimeandaliwa kwa ajili ya ndugu hao ambao ni mara chache sana hukusanyika pamoja kama hivyo.
“Hermes tayari upo ndani ya hoteli , kwanini usivue hilo lisuti lako , huoni kwamba ni wewe tu hapa ulievaa suti na joto lote hili?”Aliongea Christen huku akimwangalia Raphaeli aliekuwa amekaa pembeni yake.
“Kuwa na amani sisi Vampire miili yetu ni ya baridi”
“Mwacheni nani anajali kama anahisi baridi au Joto , kwanza unaweza kunywa damu na ukaishi , kuna haja gani ya kula na sisi?”
“It’s recognition to Poseidon ‘s Culinary arts”Alijibu.
“Haina haja , chakula changu kipo Perfect”Aliongea Poseidon akijigamba.
Rose na Magdalena waliishia kuangaliana pasipo kuongea chochote , na walijiambia Poseidon na yeye ni kama Roma tu hana aibu kabisa kwa matendo yake.
Chakula kilichokuwa mbele ya Ares kilipotea kwa haraka sana na baada ya kumaliza kila kitu alisimama na kuelekea upande wa Balkoni.
“Ares unaenda wapi?”Aliuliza Stern.
“Hilo nalo ni swali gani?”
“Sio muda sahihi wa kuwatafuta, au unadhania unaweza kuwashinda?”
“Sina muda wa kupoteza kula na nyie mpaka usiku wa manane mimi wala sitamani kuangalia mapigano ya kibinadamu ya Caesar Conference nipo hapa kwa ajili ya kupigana nao”
“Hey Bro unataka kuzaliwa upya katika mwili mwingine labda?”
“So what , nevet try never know , I am not interested in their conspiracies , I dare to go if you don’t”(“Kwani vipi , usipo jaribu huwezi kujua , sina matamanio ya uzushi wao , ninathubutu kwenda kama wewe huwezi”Aliongea na kumfanya Stern na Alcie kukunja sura zao kutokana na ukichaa wa Ares.
Muda huo huo Rose na Magdalena waliweza kuhisi msisimko maalumu ambayo ni kama vile ni mawasiliano yao na Roma na walijikuta wote wakiangalia upande wa nje na waliweza kumuona Roma akiwasogelea kwa kasi na walijikuta wakiwa na furaha.
Kufumba na kufumbua Roma aliweza kutua katika Balkoni huku akiwa na tabasamu pana.
“The Annoying Hades , you finally came back , we thought you run away in fear”Aliongea Christen akimtania kama walidhania amekimbia kutokana na uoga.
Roma aliangalia kila mmoja aliekuwepo na alionekana kuridhika kupitia macho yake.
“Naona kila mmoja ameweza kufika , hakuna chochote kilichotokea wakati nilipokuwa sipo, nilienda Scotland ndio maana nimchelewa kuja”Aliongea.
Alikuwa amempeleka Clark Scotland kwani walikuwa na jukumu la kushiriki katika sherehe za Summer Bank Holliday , yeye na mama yake.
“Kwasasa bado lakini ni swala la muda tu”Aliiongea Stern huku akimwangalia Ares.
Baada ya hapo Roma aliongea na wanawake wake na kuwatoa hofu kwamba tayari alifanikiwa kumpata Clark na kumrudisha nyumbani.
Baada ya kuelezea kwa ufupi kwa upande wake na yeye alimuuliza Christen kile kilichotokea wakati ambao hakuwepo na alielezewa kila kitu kwa ufupi na namna ambavyo Ares anapanga kutoka hapo na kwenda kuwatafuta akiwa peke yake.
Upande wa Roma hakuwa na msingi mzuri wa historia nzuri juu ya hadithi ya miungu ya kigiriki hivyo hakuwa na uelewa mkubwa na licha ya kusikia stori zinazohusiana na majitu hakuwahi kuamini kama kweli walikuwepo.
“Nakushauri usiende kwanza mpaka ufahamu mbinu zao zote”Alishauri Roma.
“Acha kunidharau , Hades usijifanye wewe una nguvu kunishinda mimi kwasababu tu mara ya mwisho ulinishinda , kipindi kile sikuwa makini na nilikudharau na mbinu zako za kichawi”
“Kama unajiamini basi hakuna wa kukuzuia kufanya kile unachotaka, ni sawa kama unataka kufa lakini haitakuwa vizuri kwasisi kuja kuulizwa baadae”Aliongea Roma na kisha akajifanyisha kufikiria.
“Unaonaje ikawa hivi , kwasababu una uhitaji wa mtu wa kupigana nae , kwanini usipigane na Raphaeli”
“Damn it Hades , unanitania , nani anataka kupigana nae?”Alijitetea Hermes.
Ares baada ya kuambiwa pigane na Raphaeli alionyesha kuwa katika hali ya furaha mno , ukweli ni kwamba mikono yake ilikuwa ikimuwasha muda wote , hakujali kama angeweza kushinda au kushindwa alitaka kupigana tu.
“Hehe.. Hermes wewe ndio ulijifanyisha kuwa Farid kule Tanzania si ndio?”
“Farid !!, yupi huyo?”
“Haishagazi kwa mtu kama wewe kukosa makando kando na haina haja ya kujifanyisha hujui ninachomaanisha, ijapokuwa sijui kwanini ulileta mkanda wa kichawi feki Tanzania lakini haitokei tu ukaamua kunichokoza mimi peke yangu”
“Unamaanisha nini? , Hermes ule mkanda wangu feki ulionekana Tanzania wewe ndio uliehusika na kuzusha habari hizo?”Aliuliza Christen kwa mshangao.
“Aphrodite unaamini vipi anachoongea , kwanini nifanye kitu cha namna hio kwa faida ipi kwa mfano?”
“Acha kongea ujinga , Hades hawezi kuongea bila kuwa na ushahidi na zaidi ya yote Hermes tumejuana kwa muda mrefu tokea katika syari yetu, siku zote ukidanganya unakuwa na utulivu wa hali ya juu mno”
“Wewe..”Alitaka kuongea lakini aliishia kimwangalia Poseidon na wengine wanavyochukulia swala hilo.
“Mnaonaje na nyie , mnadhani ni mimi niliefanya kitendo hiko , mnamuamini Hades anachoongea tofauti na mimi , nitapata faida gani nikifanya hivyo kwanza?”Alijitetea. na Stern na Alice hawakuongea chochote na kuweka sura za maigizo.
“Hermes your skills in deception is not as good as your illusions”Aliongea Poseidon akimwambia uwezo wake wa kudanganya ni mdogo kuliko uwezo wake wa kutengeneza udanganyifu.
“Poa, nakubali kwamba wote nyie mnanijua vizuri , na nakubali nilifanya mimi , lakini sababu kubwa ni kwamba nilikuwa ninajisikia vibaya hivyo nikaona nikamchokoze Hades , kuna ttatizo juu ya hilo?”Aliongea kinafiki alikuwa akijua anadanganya.
“Hehe.. Hermes sijali sana kuhusua mambo yako ya kishenzi unayoyafanya , kama kweli umekasirika sasa hivi kwanini usitolee hasira zako kwangu kwa kujaribbu kunipiga”Aliongea Ares.
“Pumbavu , nina hasira kweli , lazima nikufundishe adabu wewe mshenzi”Aliongea kwa hasira huku akisimama na alimwangalia Roma kwa dakika kadhaa na kisha alisogelea Balkoni na kupotea nje na mabawa yake kama vile ni Makerubi akimfukuzia Ares.
“Aphrodite , Hermes ndio aliezusha uzushi juu ya mkanda wako wa kichawi , huna mpango wa kwenda kuungana na Ares kumshikisha adabu Hermes?”Aliuliza Alice akitania.
“Hapana, uwezekano wa sisi kushinda au wa Hermes kutushinda ni asilimia hamsini kwa hamsini, nilikuwa nikijaribu kukaa upande wa Hades tu hapa , sijali kati yenu anaetumia jina langu kwa mambo yenu”
“Vyovote vile , lakini kumuacha Hermes kwenda kushindana na yule kichaa ili tu kutoa hasira zake ni sawa na kupigana na yale Majitu tu”Aliongezea Stern huku akicheka.
“Ni wazi kabisa wametuleta hapa kwa makusudi , vinginevyo wasingeenda ndani ya hoteli ambayo ulipanga kukaa Hades , inaonekana wanasubiria wote tuwe sehemu moja ndio watushambulia , hivyo kwa muda kama huu kama tutakuwa na haraka na kukosa mpango lazima tutaingia kwenye mtego wao , hivyo tunapaswa kusubiri kuona ni nini wanatuandalia , isitoshe Athena hayupo hapa na hatuwezi kujihakikishia ushindi wa moja kwa moja”Aliongea Poseidon.
“Mbona unamuamini sana Athena?”Aliuliza Roma.
“Tayari nasikia umekutana nae na kuona uwezo wake , je sipaswi kujiamini?”Aliuliza na kumfanya Roma kushindwa kuongea chochote , ukweli ni kwamba katika nyakati zoe ambazo aliweza kukutana na Athena hakuweza kufanya chochote mbele yake , tukio la Korea kusini halikuwa limefutika katika akili yake na kila siku alikuwa akifikiria ni kwa namna gani anaweza kuwa katika levo za juu kumpita Athena.
Lakini kwa wakati mmoja alishindwa kuelewa ni kwa namna gani hao watu wenye asili ya Ujitu wametoa wapi hali ya kujiamini mpaka kujitokeza na kuanza kuwachokoza makusudi.
****
Siku nyingine ya mashindano iliwadia katika jiji la Palermo , watu wengi walikuwa wakitarajia kwanzia siku hio mashindano yangekuwa ya moto sana kwani makundi makubwa makubwa ndio ambayo yalikuwa yakikutana.
Kila mmoja aliekuwa akimfahamu Roma alifurahi kwamba amerudi na alikuwa akishiriki , Kwa Sauron alonekana kama vile amezeeka tu ndani ya siku mbili zilizopita lakini mara baada ya kumfuata Roma hotelini asubuhi kidogo hali yake ya utulivu ilimrejea.
Roma hakuwazuia wasiendelee na uchunguzi, alihitaji kujua zaidi kuhusu tukio lile , alitaka kujua kuhusu kundi la kigaidi ambalo limemteka Clark na kutaka kuunda siraha ya kimaangamizi ya teknolojjia ya FURY.
Kwa wakati huo uchunguzi ulikuwa ni rahisi kutokana na kwamba Umoja wa Norh Buyeo kutoka Korea ulikuwa ukijihusisiha , hivyo Roma alimpa kazi Makedon na wengine kujaribu kutafuta nguvu ambayo ipo nyuma yao na pamoja na mipango yao yote.
Wakati mashindano yanaanza Roma alikuwa eneo la VIP huku kulia na kushoto akiwa na Mage na Magdalena.
Upande wa Magdalena alikuwa na aibu sana asubuhi hio kumwangalia Roma usoni , pengine huenda ni kwasababu ya kile kilichotokea usiku kucha.
Ukweli ni kwamba baada ya chakula cha usiku Rose yeye alichukuana na Christen na kusingizia wanaenda kufanya Shopping , ilikuwa ni usiku ndio kakini maduka katika jiji la Palermo yalifanya kazi masaa ishirini na nne na watu ambao walikua ni maarufu maarufu wanaofika katika jiji hilo walikuwa wakifanya Shopping usiku ili kuepuka macho ya wengi.
Sasa kilichotokea ni kama kuna mpango ambao Rose na Magdalena walikuwa wamepanga , kwani wakati Rose alivyotaka kwenda kufanya Shopping Magdalena yeye alisema amechoka na alitaka kulala, upande wa Roma na yeye alikuwa amechoka kwa kutolala siku mbili mfululizo hivyo alitaka kupumzika.
………….
Kutokana na wote kupewa chumba kimoja basi ilitokea , Roma na Magdalena wakalala kitanda kimoja.
“Magdalena vinauma?”Ni sauri ya mwanaume iliosikika usiku wa jana katika chumba cha hadhi ya juu alichokuwa akilala mfalme Pluto.
Licha ya mwanaume kuuliza swali la namna hio , hakukuwa na majibu kutoka kwa mwanamke mrembo aliekuwa amelaliwa kwa juu na mwanaume aliejengeka mwili kimazoezi, upande wa yule mwanamke alionekana kuwa katika raha ya ajabu kiasi kwamba alitumia miguu yake na kuipitisha katika kiuno cha mwanaume yule.
“Arggh..”Mwanamke alitoa mguno huku akiachama kama vile kabanwa na mlango , alionekana alikuwa akipitia hali ya maumivu na raha kwa wakati mmoja
“Samahani , lakini inaonekana kubanwa sana ndio maana unasikia maumivu”Aliongea mwanaume kwa sauti ya kunong’ona, ilionekana kwa upande wa mwanamke kinachoendelea kwake kilikuwa ni mara yake ya kwanza kufanyiwa.
“Ni sawa tu , nitapona kwa haraka , isitoshe na mimi pia sio wa kawaida”Ilisikika sauti nyororo ya mwanamke.
“Kama ni hivyo basi nitaanza kuchezesha kiuno”
“Sawa , usije kunifanya niijutie hii siku”
“Usijali , nitahakikisha hii siku unaikumbuka katika maisha yako yote”Aliongea yule mwanaume kwa besi na kisha makalio yake yalionekana kubonyea chini.
“Argh…!!”
…………….
Naam hayo ndio maongezi yaliosikika nje ya mlango wa chumba cha mfalme Pluto usiku wa jana.
Sasa wakati wakisubiria pambano lianze , ndio Roma alimuuliza mrembo Rose namna usiku wake wa Shopping ulivyokuwa na mrembo huyo alimwelezea kwa ufupi.
“Hakuna kikubwa kilichotokea”Alijibu Rose.
“Pengine anaona aibu , jana kanunua nguo za ndani kibao ambazo zimekaa kiuchokozi uchokozi”Aliongea Christen bila aibu na kumfanya Rose amkazie macho na alijikuta akiona aibu, Bahati tu waliokuwepo karibu yao ni Stern na Alice , angejisikia aibu sana kama Ron na Sauron wangekuwepo hapo.
Christen hakujali namna Rose alivyokuwa akimwangalia na alitoa ulimi kumtania na kisha akageuza shingo yake mbele.
“Kama ni hivyo , hakikisha unanunua za kutosha”Aliongea Roma akiwa na uso uliokaa kifisi.
“Haikuwa hivyo..Usimsikilize Christen”
“Najua , mimi natoa maoni yangu tu , ila usisahau usiku wa leo nataka kuona namna utakavyopendez… sawa Babe?”
………………
Wakati wakiendelea kuongea hatimae ilifikia zamu ya The Eagles , washindani wao ilikuwa ni kundi la Kimasenari lifahamikalo kwa jina la Odin Mercenary Corp, walikuwa na makazi yao Kaskazini mwa ncha ya dunia.
Rose na Magdalena mara baada ya kuona ni watu wa Roma waliweza kuongeza umakini , lakini upande wa Roma alionekana kabisa kutopenda sana kuangalia maishindano ya aina hio kwani yalikuwa ya kawaida sana kwake.
Lakini licha ya hivyo alifurahi kuona wanajeshi wake walikuwa wameimarika sana , hususani Maninja upande wa New Zero kwani walionyesha uwezo mkubwa katika kupambana na wapiganaji wa kundi la Odin, mpaka kipenga cha mwisho kinapulizwa The Eagles waliibuka washndi na kuigia katika hatua inayofuatia.
Roma ndio aliekuwa wa kwanza kuondoka na hakuwa na mpango kabisa wa kurudi tena, upande wa Rose mara baada ya kuona Roma kaondoka katika hilo eneo na yeye alifuata nyuma nyuma lakini kwa Magdalena yeye alisema ataangalia mashindano hayo mpaka mwisho
Ukweli ni kwamba alitaka kuendelea kuangalia , ila tu kumpa nafasi na Rose kuwa karibu na Roma kwani usiku wa jana kama sio Rose basi huenda asingeweza kuonja dunia ya mapenzi kwa mara ya kwanza katika maisha yake, alikuwa na raha na akili yake yote ilikuwa ikiwaza usiku wa jana wote aliofanya mapenzi na Roma.
Hakuwaza rena kama Roma alikuwa mpenzi wa pacha mwenzake au mume wa rafiki yake wa utotoni Edna , bali muda huo alijiambia amefanya maamuzi sahihi kufata kile moyo wake unachotaka.
Wakati Roma na Rose wanakaribia hotelini waliweza kukutana na mwanaume wa Kijapani , Rose alionekana kumfahamu mwanaume huyo na upande wa Roma pia alikuwa akikumbuka sura ya mwanaume huyo, alikumbika kipindi alichosafiri kwenda Japani akiwa na Dorisi aliweza kukutana na huyo mwaname katika kambi ya jeshi wakati akienda kumpatia mateso Kapteni Kisu Mvunjiko na alishangaa kumuona akiwa hapo kwani alikuwa na cheo kikubwa mno serikalini.
Roma ilibidi kwanza amhoji Rose inakuwaje akawa anamfahamu huyo Mjapani na ndipo alipomuelezea kwamba alikutana nae usiku wa jana akiwa na Christen na huyo mwanaume ndio aliewasogelea na kuwachombeza kwa ajili ya kwenda kumpa huduma usiku kucha kwa malipo ya hela , lakini Christen akamjibu kwa kumwambia yeye atamlipa kwa kila pigo atakalompiga na ndio akaondoka na kuwaacha.
Roma mara baada ya kusikia hivyo aliguna , aliona sio jambo la kawaida kigogo wa serikali kutoka Japani ghafla tu kumsogelea Christen na Rose na kuwataka wampatie huduma.
Baada ya kuingiwa na wasiwasi ya uwepo wa mwanaume huyo hapo Sicilly haraka sana alimpigia simu Sauron na kumpa maelekezo ya kumfanyia uchunguzi , hisia zake zilimwambia huenda alikuwa akihusika na wale watu wa mavazi meupe au kundi la Cyclops.
*****
Ikiwa ni muda wa jioni kabisa wakati Roma akiwa ameuchapa usingizi mara baada ya kazi nzito alioifanya na Rose mlango wa chumba chao ulifunguliwa na Magdalena.
Mara baada ya kuona namna Rose na Roma walivyolala wakiwa hawana nguo mwilini alijikuta akiona aibu , lakini alijitahidi kujikaza na kwenda kumuamsha Roma.
Roma mara baada ya kuamka hakuona aibu licha ya kwamba alikuwa uchi yeye na Rose na alienda mbali kumtania Magdalena na kumwambia ajiunge na yeye lakini Magdalena aligoma na kumwambia kwamba amekuja hapo kumpa taarifa kwamba wenzake wanamuhitaji katika eneo lileile la siku ya jana kwa ajili ya maongezi.
Roma mara baada ya kupewa taarifa hio hakuwa na muda wa kupoteza , alikuwa na hamu kubwa ya kuwajua kiundani watu alioambiwa wana aasii ya Ujitu ndani yake hivyo ndani ya dakika chache tu alikuwa tayari amekwisha kujiandaa na kutoka.
Roma mara baada ya kufika aliweza kukuta kila mmoja alikuwa amekaa katika nafasi yake na yeye pia alisogelea kiti na kuketi , lakini wakati huo akiangalia barua iliokuwa juu ya meza.
“Nini kinaendelea hapa , hio ni nini?”Aliuliza Roma na kumfanya Christen aliekuwa akimwangalia Roma muda wote katika eneo la chini ya kiuno chake palivyotuna kuvuta mdomo na kisha kuchukua ile barua na kumpatia.
“Je ungependa kujifunza lugha yetu?”Aliuliza na kumfanya Roma kuangalia ile barua ilioandikwa kwa herufi zisizoeleweka na kumrudishia Christen.
“Haina haja , ninajua lugha nyingi sitaki kuongeza nyingine kwenye kichwa changu , niambie barua hii inahusu nini”
“Ni rahisi tu , ni kwamba kiongozi wa Cyclops anaefahaika kwa jina la Brontes ametutumia mwaliko , anatualika sisi wote kwenda kupata chakula cha mchana katika mgahawa siku ya kesho baada ya awamu ya kwanza ya mashindano ya asubuhi”Aliongea Poseidon.
“Kwanini wanataka kukutana na sisi? , hawajawahi kututafuta hapo kabla”Aliuliza Roma.
“Hata sisi imetushagnaza pia , wanaonekana kama hawatafuti kulipiza kisasi na wanajaribu kutualika namna hii , wanajaribu kufanya nini?”Aliongea Stern.
“Kwanini tujali wanachotaka , huenda wametualika kwa ajili ya kumaliza tofauti zetu , lakini kama wanataka kupigana na sisi tutapigana na kama wanataka amani tutawaacha waendelee kuishi”Aliongea Ares na kufanya wote wamwangalie kwa mshangao kidogo lakini haa hivyo washazoea Ares amekaa kifujo fujo.
“Hivi wasiwasi wenu ni kwamba tunaweza tusiweze kupambana nao?”Aliuliza Roma baada ya kimya cha muda mfupi.
“Kama tungekua kwenye sayari yetu , wasingethubutu hata kutusogelea na ningewapiga mimi mwenyewe, lakinii sasa hivi mambo ni tofuati bila ya Athena na Zeus tunaweza tusifanikiwe kuwashinda ijapokuwa tutakuwa na uwezo wa kujilinda”Aliongea Hermes.
“Mimi nipo , yupo pia Rose na Magdalena ambao wote wapo katika levo ya Nafsi , je bado tu haitoshi , kwanini tuwaogope?”Aliuliza Roma.
“Hades unawachukulia poa hawa majitu , ngoja nikuambie Cyclops na Hecatoncheires wanao uwezo mkubwa kuliko jamii zote za majini na hawaathiriki na nguvu za mbingu na ardhi kwasababu wana damu ya kizazi chetu , Damu ya Titan”Aliongea Artemis.
“Damu ya Titan!!?”Aliuliza Roma kwa mshangao.
“Ndio …”Alice aliwaangalia wenzake kuona kama kuna ambaye anajaribu kumzuia na baada ya kuona wapo kimya aliendelea.
“Damu ya Titan ndio asili yetu kamili na sisi ni mwendelezo wa kizazi cha damu yake , ndio chanzo kikubwa cha nguvu zetu wakati tulipokuwa kwenye sayari yetu m sababu ambayo imetufanya uwezo wetu kushuka kufikia asilimia therathini ni kwasababu tulikosa miili yetu yenye asili ya damu ya Titan , hawa Majitu wenyewe ni sehemu ya uzao wetu hivyo wana asili ya damu ya Titan na kama tulivyosema mwanzo, wao walikuja duniani na wakaweza kuishi kwa miili yao lakini sisi ikashindikana, Mpaka sasa hivi damu yetu ipo Sealed”
“Hebu subiri kwanza , nilikuwa nataka siku zote kuuliza ilikuwaje miungu mkapoteza uwezo wenu kwa kiasi kikubwa , kama kweli hii damu ya Titan ndio chanzo cha nguvu zenu , kwanini ipo ‘Sealed’ mpaka sasa , je swala hili lina uhusiano na moyo wa Gaia?”Aliuliza Roma.
“Kuhusu hilo..”Alice alitaka kuongea lakini alisita lakini palepale Christen na yeye aliingilia.
“Usiulize maswali Hades , kwetu kumbukumbu hizo ni maumivu makali kila zinapojirudia .. nitaendelea kukuelezea kwa niaba ya Alice, hawa majitu wanao uwezo mkubwa kutokana na kuwa na damu ya Titan na ndio maana hawaogopi kabisa watu wanaovuna nishati za mbingu na ardhi , kwasababu ni nishati ya muunganiko wa dunia hii , Damu ya Titan unaweza kusema ina nguvu ya Kiroho kama mnavyopenda kuita hapa duniani , sasa unatakiwa kujua ni Zeus pekee ambaye alikuwa na uwezo wa kutumia mwanga kuifubaza nguvu za damu hio na kuwafanya wawe dhaifu , hivyo hakuna mtu ambaye anaweza kuwashinda hata Athena mwenyewe hakuwa na uwezo huo”
“Kwa maelezo yenu mnaamaanisha kwamba tunapaswa kufa kwenye mikono yao si ndio?”Aliuliza Roma huku akitabasamu kwa uchungu
“Hatuwezi kwenda mbali hivyo , kwasasa hatujui ni ipi mipango yao na isitoshe una nafasi kubwa , angalau unaweza kutumia kanuni za anga pamoja na nguvu za nishati ya mbingu na ardhi , lakini hata hivyo inatia huzuni kwasababu haupo kwenye levo ya juu zaidi ya kuweza kudhibiti Radi kama Majinni tuliokutana nayo kipindi tunafika la sivyo ungekuwa tishio kwao”Aliongea Poseidon.
Roma alijiambia hata kama hakuwa katika levo za juu kama watu waliowakuta miaka hio , lakini yeye alikuwa na chungu cha maafa hivyo alijiambia kwamba mwisho wa kila kitu bado haujulikani kama watapambana.
Hao watu kilichomuudhi sana ni kwamba ni wasiri sana kuhusu hio damu ya Titan na alijua kabisa ameelezwa nusu na ni kitu ambacho kinahusiana na moyo wa Gaia
Baada ya mazungumzo ya muda mfupi Poseion alimtaka Hermes kunagalia Ulingo kama haujawekwa mtego ili kuwa salama na haikuwa tatizo kwa Hermes kulingana na spidi yake
******
Siku ya tatu hatimae iliweza kuwadia na makundi therathini na mbili yalikuuwa ndo yamebakia , wawakilishi mbalimbali kutoka serikalini walikuwepo.
Kama kawaida Poseidon , Hermes na Ares walikuwa katika eneo lao la sku zote na Roma , Magdalena , Rose Alice , Stern na Christine wlaikuwa wamekaa katika eneo moja.
Kabla ya mashindano kuanza Roma aliweza kupokea ripoti kutoka kwa Makedoni juu ya baadhi ya chunguzi alizomwambia Sauron afanyie kazi.
Na kwa maelezo yake ni kwamba mwanaume wa Kijapani aliemuona katika hoteli ya Cassano alikuwa akifahamika kwa jina laKagawa Chusho na ni waziri wa ulinzi wa Japani na hana uhusiano wowote na kundi la watu wa mavazi meupe , lakini alimwambia kwamba wakati ambao alimuona hotelini ilionekana kulikuwa na kikao kilichokwisha kufanyika hivyo hawakuwa na uelelwa nini kilitokea au kilizungumzwa katika kikao hicho ndani ya hoteli ya Cassano.
Roma kuna hisia ambazo zilimwambia kabisa huenda serikali ya Japani ilikuwa ikihusika kabisa na uwepo wa hawa Majitu hapo Sicilly lakini hakuwa na namna ya kuthibtisha dukuduku lake kutokana na kwamba alijua fika kikao ambacho kilifanyika ndio kilikuwa na taarifa kamili lakini kwa bahati mbaya walichelewa kugundua mapema..
Wakati ambao Roma alikuwa katika mawazo alikuja kushituliwa na Sauron aliekuwa anakuja mbio mbio kwake .
“Your Majesty Pluto something is wrong”Aliongea Sauron akimwambia kuna tatizo.
“What are you saying?”(Unaongea nini?”);
‘Hapa , hebu angalia wahusika ambao wanakwenda kushiriki katika mecho inayofuatia”Aliongea Sauron na kushika Kishikwambi alichokuwa ameshikilia Sauron.
“Mechi inayofuata ni The Eagles na Deicide?”Aliongea Roma kwa mshangao akimaanisha kwamba mechi inayokwneda kuanza ni kati ya Majitu wanaojiita godkiller na wanajeshi wake wa The Eagles.
“Nini kimetokea , nilijua wanakwenda kukutana katika nusu fainali tu?”Aliuliza Roma huku akiwa na wasiwasi na kuanza kupitia orodha ya wanajeshi wake ambao wanakwenda kushindana katika mechi inayofuata.
“Kuna mtu ambaye amebadilisha na meneja anasema ni makosa tu yaliofanyika , nadhani ni makusudi kabisa wanataka tukutane kwanza na hao wauaji ili watudhalilishe kututoa katika mashindano mapema“Aliongea Sauron kwa hasira.
Lakini licha ya hivyo ni kama washachelewa , kwani tayari wanajeshi wa The Eagles walionekana wakiingia kwenye ulingo na walionekan kuwa na mchecheto mara baada ya kusikia wanakwenda kupambana na kundi la Deicide watu waliowaonyeshea kiburi katika hoteli ya Federico.
Wakati Nasri na wenzake wakiwa na shauku ya kulipiza kisasi kwa kuwashikisha adabu watu hao, upande wa Roma alikuwa na wasiwasi kwa kile kinachokwenda kutoktea kwa kuamini kwamba wanajeshi wake hao hawana uwezo wa kushinda na kwa mara ya kwanza jeshi lake linakwenda kudhalilishwa.
Makofi ya shangwe na vifijo yalisikika pande zote baada ya wanajeshi wa mavazi meupe kuingia kwa mbwembwe zote na baada ya kufika katikati waligeuka upande ambao wamekaa Poseidon , Roma na ndugu zake na kuwaangalia , ijapokuwa sura zao hazikuwa zikioneana kwa kuvaa Mask lakini likuwa ni kama vile walikuwa na sura za kejeli.
ITAENDELEA WIKIEND NJOO WATSAPP TUPIGE STORI NAMBA 0687151346
Jomba leo umefunguka na kutema ya moyoni.Anakera sana huyu jamaa,nakuteteaga lakini unakera,jibu sms za inbox
Shukrani sana mwana singanojr tutasubiri tu hata ikiwa mwakani fresh tu
Kesho usiku ni subjective