NILIMDHANIA KAHABA KUME BIKRA
MTUNZI: SINGANOJR
Mono no ware.
SEHEMU YA 644.
Ni siku kadhaa baada ya mazungumzo kati ya Suzzane na Nadia kumalizika , huku Suzzane akiamua kufanya kazi ambayo itamuwezesha kukidhi vigezo ili kupata nafasi ya kupata uwanachama wa Ant-Illuminat.
Ikiwa ni siku ya jumamosi Suzzane aliweza kupokea ujumbe wa meseji kutoka kwa Nadia uliokuwa ukimtaarifu kwamba maombi ya miadi yake na Raisi Senga imeweza kufanikiwa na anapaswa kusafiri mpaka mkoani Dodoma makao makuu ya nchi kwa ajili ya kuonana nae.
Suzzane mara baada ya kupata taarifa hii mapigo yake ya moyo yalikuwa yakienda mbio sana , ijapokuwa alikuwaakijiamini katika mambo mengi , lakini swala ambalo ameamua kulifanyia kazi halikuwa swala dogo ambalo ni la kuongea na mheshimiwa Raisi tu na likaisha hapo bali ni mwanzo wa kitu kingine, dakika na sekunde ambayo atatamka kile ambacho kimemfanya kutaka kuongea na raisi huyo basi ni mwanzo wa maisha mapya.
Suzzane alijikuta akivuta pumzi nyingi na kuzishusha na alijitahidi kujiambia kwamba kila kitu kitafanikiwa kama alivyopanga.
Kilichokuwa kikimpa wasiwasi Suzzane ni kwamba Nadia alimwambia kwamba licha ya kwamba hatua yake ya kwanza katika misheni ya kumfanya Raisi Senga kuwa mwanachama wa Ant -Illuminat ni kuonana nae na kuongea nae kile alichomwambia lakini hatua ya pili hakuwa akiijua.
“Suzzane hatua ya kwanza unayotakiwa kufanya ni kuhakikisha Mheshimiwa Senga anakuamini , jambo hili sio jepesi kwasababu ‘trust is earned over time’ na ili uweze kufanikiwa lazima kwanza uwe na sababu binafsi ya yeye kukuamini”
“Sababu binafsi ya kuniamini? , hapo sijakuelewa” “Hakuna jaribio ambalo anapewa binadamu ambalo lipo nje ya uwezo wake , wewe kupewa hii kazi ili kukidhi vigezo ni kwasababu mahesabu yanaonyesha
ni swala ambalo unaweza kulifanyai kazi na likafanikiwa”
“Kwanini unahisi hili ni jaribio ambalo lipo ndani ya uwezo wangu?”
“Kwasababu ya historia yako na Dr Elvice , kitendo cha kuwa Single mpaka sasa ukiendelea kumuweka Elvice moyoni mwako licha ya kwamba amefariki muda mrefu ndio sababu, unajua Suzzane kwanini nilikuambia uniambie kuhusu historia yako na DrElvice wewe mwenyewe licha ya kwamba uliandika katika maombi yako?”
“Sijajua?”
“Nilitaka nikusome hisia zako wakati wa kumzungumzia Elvice , umeongea kwa hisia sana kiasi cha kuweza kunifanya ni kuamini , hiki ndio ambacho nilichokuwa nikitaka kuona kutoka kwako , mimi kama ‘Handler’ wako kwanzia sasa, Suzzane ili jaribio kama litafanikiwa pengine ni swala ambalo linaweza kukuweka huru na ili uelewe namaanisha nini lazima pia nikuambie ukweli namna ambavyo Elvice alifariki na nani alihusika”Aliongea Nadia na kumfanya Suzzane kumwangalia Nadia kwa macho yaliojaa umakini kuliko mwanzo.
“Unamjua aliemuua Elvice?”
“Najua alieagizwa kumuua Elvice lakini swala ambalo lipo nyuma ya kifo cha Dr Elvice ni swala ambalo Umoja ndio unajua”Aliongea Nadia na kumfanya Suzzane kupatwa na shauku ya kutaka kujua.
“Nataka kujua Nadia nani alimuua Elvice? , iwe ni
kwa kuagizwa au ni kwa kufanya maamuzi yeye mwenyewe”
Nadia alifikiria kidogo na kisha akaingiza mkono wake kwenye mkoba ambao amefika nao na kisha alitoa picha na kumpatia Suzzane.
“Huyo ndio ambaye amehusika na kifo cha mpenzi wako Elvice , kwa jina anaitwa Salim Shariff ni jasusi mstaafu wa kikosi cha Dhoruba nyekundu na kwasasa anafahamika kwa jina la Salimu Ibuyawanga ni baba yake Waziri wa Mazingira bwana Nguzo Ibuyawanga”Aliongea Nadia na kumfanya Suzzane mikono kumtetemeka huku machozi yakianza kujitengeneza kwenye mboni za macho yake.
“Una ushahidi gani wa kuniaminisha huyu ndio kahusika?”
“Suzzane hilo ni swali ambalo utaweza kulipata siku ambayo utakuwa mwanachama kamili wa umoja wa Ant – illuminat, Chriss umesema amekuambia Elvice alikuwa akipambana na ugonjwa ambao dalili zake zimeanza kujionyesha basi kama ni uonjwa maambukizi ya huo ugonjwa yameanzia kwa huyu mtu”Aliongea na Suzzane ambaye machozi yalikwa yameupamba uso wake aliyafuta na kisha akamwangalia Nadia.
“Unataka nifanye nini?”
“Ili uweze kufanikiwa kumfanya Raisi Senga kukuamini ni kumpatia mpango ambao utaweza kumuondoa huyu mtu hapa nchini, familia ya Ibuyawanga ni familia ambayo nguvu yake haionekani ambayo Serikali inaiogopa”
“Unamaanisha nini nguvu ambayo
haionekani?”Aliuliza Suzzane na kumfanya Nadia amwambie asogeze sikio amnong’neze na Suzzane alifanya hivyo na mara baada ya Nadia kuonekana kuongea jambo alijikuta akishangaa kwa kutoa macho.
“Hili swala ni la kweli?”
“Ni swala la kweli, Serikali ya Tanzania haina nguvu ya kumuondoa huyu mtu kwasababu ya hio nguvu yake lakini kama nguvu nyngine itajitokeza kutaka kuisaidia serikali kupambana na huyu mtu basi ni hakika atachukua hatua ni maswala ya kidiplomasia zaidi , wewe sasa itakuwa ni fursa kwako kumwelezea Raisi Senga juu ya nguvu hii ambayo ipo tayari kumsaidia huku ukitumia sababu yako binafsi ya kisasi zidi ya familia hio kumfanya Raisi Senga akuamini”
Suzzane alikuwa kwenye mfululizo wa kuwazia maongezi yake na Nadia mara ya mwisho kabla ya siku inayofuatia kuanza safari ya kuelekea Dodoma kwa ajili ya kuongea na mheshimiwa.
Kwanza kabisa Suzzane alipaswa kumwelezea
Mheshimiwa juu ya kisasi chake zidi ya familia ya
Ibuyawanga na baada ya hapo alipaswa kutumia
‘Codes’ katika kuelezea nguvu ambayo ingeweza kumsaidia Raisi Senga kupambana na nguvu ya ziada ambayo inaendesha nchi kwa mgongo wake.
“Suzzane hakikisha unapangilia maneno yako vizuri kama nilivyokuelekeza na baada ya hapo mpatie mheshimiwa mpango wako kwa kutumia tatizo analopitia, inawezekana asikubaliane na wewe hapo kwa hapo lakini lazima atakaa chini na kufikiria ulichomuambia na atafanya maamuzi”Alimalizia kuongea Nadia kauli ambayo na Suzzane pia alikuwa akiikumbuka vyema.
Suzzane kabla ya kuanza safari yake alianza kuandaa mpangilio wa maneno yake , ijapokuwa alikuwa akisifika kwa kujiamini tokea akiwa mdogo lakini mazingira mapya ambayo anaenda kukutana nayo siku ya kesho hakuwahi kuyapatia uzoefu hivyo presha ilikuwa juu na aliamini kitu pekee cha kupunguza wasiwasi wake ni kujiandaa vizuri.
Juu ya meza ambayo Suzzane alikuwa akifanyia kazi katika kujiandaa kulikuwa na picha kadha wa kadha ambazo zilikuwa zimepangiliwa , wakati huo huo alikuwa ameshikilia karatasi ambayo ina maandishi ya kurasa takribani nne ambayo ndani yake pia ina picha hizo hizo zilizokuwa zipo juu ya meza lakini ambazo zimetengenezewa kopi na kuambatanishwa, moja wapo ya picha hio ilikuwa ni ya Naibu Waziri Salihi mtoto wa Waziri wa mazingira.
******
Ni siku moja baada ya Raisi Senga kuweza kukutana na Suzzane na kufanya mazungumzo.
Katika saa zote ishirini na nne tokea mazungumzo hayo yamalizike Raisi Senga alipatwa na hisia tofauti tofauti sana , kwanza kabisa alipatwa na mshangao , alipatwa na hofu na pia akapatwa na wasiwasi.
Siku chache nyuma kupitia chaneli yake ya siri sana ya taarifa ya watu anaowaamini ndani ya Ikulu iliweza kumletea taarifa ambazo zilikuwa zikihusiana na mtu ambaye alikuwa akihitaji miadi ya kuonana nae akiwa ndani ya ikulu ya Dar es salaam , haikuwa taarifa tu ya mtu huyo kuomba miadi bali ni kwamba alietuma ujumbe huo aliambatanisha na sababu(bait) ya yeye kukubali kukutana nae.
“Need an appointment , I can help you avoid signing an unfair contract that is against Tanzanian Culture”
Ujumbe huo ulikuwa na tafsiri ya mtu kuhitaji miadi
, na mtu huyo anasema anao uwezo wa kumsaidia kuepusha kusaini mkataba ambao unaenda kinyume na Tamaduni za watanzania.
Siku ambayo mheshimiwa Senga aliweza kupokea huu ujumbe kwanza alipatwa na kiwewe , ni kweli kwamba kulikuwa na mkataba ambao alikuwa akilazimishwa na wakuu wake katika umoja wa siri aliojiunga kuusaini ili utekelezwe Tanzania lakini alishindwa kufanya hivyo kwa muda mrefu akiwa katika Dilema kwani kitendo cha kutia saini mkataba huo ilikuwa ni kwenda kinyume kabisa na kile alichokuwa akikiamini hata kabla ya kuwa raisi.
Ni kweli kwamba alikuwa ashafanya makosa makubwa ya kujinga katika umoja huo na kufanya au pengine kuendelea kufanya mambo ambayo yanaenda kinyume na kile alichokiamini lakini mkataba uliokuwa mbele yake ulikuwa ukivuka mpaka ambao kama angeuvuka basi ingekuwa ngumu kurudi tena.
Sasa wakati akiendelea kuwa katika Dilema anapokea ujumbe wa aina hio k wa kutumia chaneli ya siri ya mawasiliano ndani yake ambayo ni tofauti kabisa na mfumo wa kawaida wa mawasiliano ikulu.
“Kabwe ipo namna ya kurudisha jibu?”Aliuliza Raisi Senga siku mbili baada ya ujumbe huo kutumwa.
“Ndio mheshimiwa”
“Okey, nimekaa na nimefikiria juu ya hili swala kwa undani , mtu ambaye ametuma taarifa hii anaonekana sio wa kawaida sana kwani chaneli ya maswalisiano alioitumia tunaijua wachache sana , hivyo nitahitaji kwanza kuonana nae kabla ya kufatilia kosa limetokea wapi mpaka kutokea kwa chaneli yetu kuingiliwa”AliongeaMheshimiwa Senga.
“Lakini mheshimiwa…”
“Kabwe najua wasiwasi wako , lakini nishafanya maamuzi tayari, wasiliana nae na mpatie hizi taarifa”Aliongea Raisi Senga na kisha alimpatia Kabwe faili lililokuwa mbele yake.
Ijapokuwa Kabwe alionyesha wasiwasi lakini hakutaka kupinga maagizo ya mkuu wake wa kazi.
Sasa kilichomshangaza Raisi Senga ni kwamba alikuwa na shauku kwanza ya kutaka kujua ni nani aliekuwa amemtumia ujumbe na kutaka kuonana nae , mategemeo yake yalikuwa ni kuona mtu ambaye hajawahi kumuona katika macho yake , lakini alijikuta akishangaa mara baada ya kuoa mtu huyo alikuwa ni Suzzane.
Raisi Senga alikuwa akimjua Suzzane kwa muda mrefu tokea akiwa ni Sekretari na mwanasheria binafsi wa mama yake Edna.
Licha ya mshangao wake lakini hakutaka kudharau , alitaka kujua imekuwaje kuwaje pia akawa ni Suzzane mtu ambaye alikuwa akitegemea kwa hamu kuonana nae ndani ya Ikulu ya Chamwino tena kwa siri sana.
Raisi Senga baada ya kufanya mazungumzo na Suzzane mpaka kumaliza alijikuta akishangaa sana kile ambacho Suzzane alikuwa amemuambia , hakuwa akimwamini kabisa Suzzane kwa kile alichomwambia kwani kwa nafasi aliokuwa nayo Suzzane na kwa uzoefu wake asingekuwa na taarifa nyeti aliomwambia lakini pia asingeweza kujua kuna mkataba ambao anataka kusaini ambao unaenda kinyume na tamaduni za watanzania.
Ijapokuwa Suzzane hakumwambia ni watu gani wapo nyuma yake , lakini alipatwa na shauku zaidi na zaidi ya kuonana nao lakini hakuishia hapo tu saa na muda ambao Suzzane anaondoka ikulu tayari mheshimiwa ashaagiza watu kuanza kumfatilia na kumpatia taarifa ya kila mtu anaekutana nae.
Ikiwa ni siku moja sasa mara baada ya kuwaza kwa kina ,siku hio akiwa ndani ya ofisi yake aliamua kufanyia kazi mpango wa Suzzane huku akiwa na nia ya kutaka kujua nani yupo nyuma ya Suzzane mpaka kutaka kumsaidia.
Sasa ikiwa ni siku kadhaa tokea Suzzane kufanya mazungumzo na Raisi Senga, Raisi alifanya uteuzi kwa kumteua Salihi Nguzo kuwa mbunge na naibu waziri wa elimu.
Ulikuwa ni uteuzi ambao ni wa kushsangaza kwani Salihi alikuwa na umri mdogo sana kuaminiwa nafasi kubwa ndani ya serikali , tena mbaya zaidi ni kwamba Salihi alikosa udhoefu wa siasa za Tanzania kwani alikaa nje ya Tanzania kwa muda mrefu.
“Nadia hongera kwa kutimiza hatua ya kwanza ya misheni yako”Sauti ya mwanadada Nadia iliweza kusikika katika simu upande wa pili.
“Asante sana Nadia , yote haya yamefanikiwa kwa maelekezo yako mimi mchango wangu ni mdogo”
“Sio kweli Suzzane , ulichokifanya ni jambo ambalo linahitaji mtu jasiri na wewe umeweza kuonyesha ujasiri wako , hongera sana kwa hilo hii ni hatua nzuri ambayo inakuingiza katika kitu kingine”
“Asante sana , nini kinafuata baada ya hapa?, Mlengwa wetu wa kwanza ambaye ni Dorisi amebadilika , kwasasa kutakuwa na changes”
“Mlengwa mwingine ni nani?”
“Nitakutumia taarifa Suzzane kila kitu kikiwa
‘Confirmed’ kwasasa kaa ukiwa ‘Alert’ na usinitafute kwa muda mpaka nitakapokutafuta mimi”Aliongea Nadia na kisha simu ilikatwa palepale.
Wote walikuwa wakitumia simu za batani tena namba tofauti kabisa ya mtandao wa Safaricom na wakati Suzzane anawasiliana na Nadia alikuwa yupo bafuni.
Suzzane alikuwa akijua anafatiliwa na maafisa kipenyo hivyo alijitahidi kuchukua tahadhari.
SEHEMU YA 645.
Ilikuwa ni muda wa mchana Roma alionekana akitoka katika hoteli ya kimataifa ya Maple iliokuwa ikipatikana pembezoni mwa fukwe ya upepo Beach.
Roma wakati akitoka ndani ya hoteli hio alijikuta kumbukumbu zake zikimrudisha nyuma namna ambavyo alimlera Edna mahali hapo na kukisi nae kwa mara ya kwanza.
Moyo wake ulijikuta ukianza kuwa mzito mara baada ya kufikiria hali yake ya kimahusiano na mke wake, Roma alijiambia kuna mlima mkubwa mbele yake ambao anapaswa kuvuka ili tu kumrudisha Edna katika himaya yake na kumuondolea mawazo ya kutaka kuachana nae.
Roma wakati akishangaa shangaa mazingira , alitamani hata kumpigia simu Neema Luwazo ili waburudike muda huo wakiwa pamoja lakini hakuwa hata na hamu ya kufanya hivyo, isitoshe alijua pengine atakuwa kazini muda huo.
Ukweli mara nyingi anapokuwa na mgogoro na Edna ile hali ya kutaka kutembea na wanawake wengine ilikuwa ikipungua kwa kiasi kikubwa sana, ilikuwa ni kama vile anapokuwa na amani na Edna hisia zake zinakuwa wazi na anapata hamasa ya kutoka na wanawake wengine , lakini inapotokea ugomvi ndio utulivu wa akili yake hutoweka na kujikuta akikosa hamu ya kustarehe na warembo wake.
Pengine sio yeye tu ambaye alikuwa akijua kuhusu hilo , hata wanawake wake alikuwa wakiliona hilo na ndio maana walikuwa wakiomba Edna kuendelea na Roma ili tu Roma aweze kuwa na utulivu wa akili na wao kufurahia penzi.
Roma alikuwa hotelini hapo kwa ajili ya kuonana na Samweli Nguluma ambaye alikuwa na dili amempatia kwa ajili ya kumsaidia siraha za kimagendo ambazo alihitaji zisafirishwe mpaka mkoani Kilimanjaro.
Samweli Nguluma ambaye ni baba yake Benadetha na mkuu wa kundi la Zoa Zoa lenye makazi yake katika mkoa ya Mwanza na Shinyanga alionekana kuwa mzito kukubaliana na ombi la Roma.
Lakini faida ambayo Roma aliipendekeza kwake kama kile anachokwenda kufanya kitafanikiwa , ilimfanya kufikiria mara mbilimbili na baada ya maongezi ya muda mfupi ya kukubaliana katika masharti Samweli Nguluma alikubali kumsaidia Roma mahitaji yake huku akimpa onyo la kumtahadharisha kama isitokee akawa na uhusika wowote kama mambo yataenda kinyume na mipango yake na Roma alimtoa hofu na kumwambia hakuna wa kumtaja.
Upande wa Nguluma alishangazwa na kitendo cha Roma kuhitaji siraha ilihali alisifika kwa kuwa na nguvu kubwa zaidi ya bomu lakini hakutaka kuuliza maswali na alijitahidi kujenga nae urafiki bila ya kusahau kuchomekea topiki inayohusiana na binti yake Benadetha.
Licha ya bwana huyo kuingizia topiki hio Roma alibakia na msimamo wake uleule na kumwambia ni kama mara ya mwisho alivyomwambia walipokutana kwenye msiba wa babu yake Mzee Atanasi.
Mara ya mwisho Roma mara baada ya kukutana kwa mara ya kwanza na baba yake Benadetha aliweza kuambiwa na mzee huyo kwamba anataka kuwa mkwe wake , jambo ambalo Roma alikataa kata kata akisema hataki kuhusika na Benadetha kimapenzi.
Sasa siku hio ni kama Samweli nguluma aliendeleza pale alipoishia lakini Roma alionekana kumkatalia.
Roma alikuwa na haki ya kukataa isitoshe wakati huo alikuwa katika migogoro na mke wake Edna , hivyo hakutaka kuongeza tatizo lingine mbele ya safari ya jitihada za kumrudisha mke wake.
Roma alimuonea huruma Benadetha kwa kusikiliza maelezo ya baba yake , kulingana na maelezo ya Mzee Nguluma ni kwamba Benaetha amekataa kuwa na wanaume wote ambao baba yake amependekeza kuolewa nao na akaenda mbali kusema kwamba wanaume hao hawana vigezo anavyovitaka.
Baba yake Samweli Nguluma alijua tatizo pekee ni Roma , pengine Benadetha kwa kumuona Roma alishamchukulia kama ‘reference’ ya mwanamme anaemtaka jambo ambalo ni gumu kutekelezeka kwani Roma alikuwa ni tofauti na binadamu wa kawaida na kama Benadetha ataendelea kusimamia vigezo vya mwanaume anaemtaka kufanana na vya Roma basi atazeeka akiwa hajaolewa.
Wazazi wa benadetha waliishia kuangushia lawama kwa Roma ambaye amemchanganya mtoto wao.
Saa saba na nusu ndio muda ambao Roma aliweza kufika nyumbani na alishangaa mara baada ya kuingia eneo la sebuleni kumkuta Amina akiwa anacheza gemu na Lanlan.
Roma alikuwa amemkumbuka sana mrembo huyo kwani tokea atoke ulimwengu wa Majini pepo hakuwahi kumuona na alijikuta hata akishikwa na hatia kwa kutokumtafuta.
Nyumbani kwa Nasra ni kama yalikuwa ndio makazi mapya ya Roma , Nasra alikuwa akichakalika kweli kwani aliweza kubadilisha ratiba zake na kuhakikisha anaenda kazini na kurudi mapema na kupika chakula cha Roma na Lanlan kwa wakati na kisha kurejea kazini.
Amina alikuwa amependeza mno , alikuwa amevalia suti ya rangi ya Bluu na scarf nyeupe ya mua maua shingoni , alionekana kama vile ni wale wahudumu wa ndgea au wafanyakazi wa benki.
Amina mara baada ya kumuona Roma alisimama akitaka kumkimbilia amkubatie na Roma alichanua mikono vilevile kumpokea lakini kabla hata ya Amina hajamfikia Lanlan alishamuwahi na kujirusha kwenye mikono ya Roma na kuloki mikono yake kwenye shingo yake.
“Daddy needs to hug Lanlan first before hugging others”Aliongea Lanlan akimaanisha baba yake anapawa kumkumbatia yeye kwanza kabla ya wengine.
Roma alijikuta akitoa kicheko kwani ni kama Lanlan anamuonea wivu baba yake na kumwangalia Amina kwa kumchokoza.
“Babe wangu Amina sidhani kama kwa staili hii utakuwa na maelewano mazuri na watoto , hebu angalia namna ambavyo Lanlan ananipenda”Aliongea Roma na Amina alijikuta aking’ata meno yake kwa hasira na kujiambia atawezaje kujilinganisha na Lanlan mtoto wake wa damu.
“Lanlan unaonaje ukimuachia baba yako , nitahakikisha nakupeleka kucheza siku ya wikiend sawa”Aliongea Amina na Lanlan mara baada ya kusikia ofa hio palepale alimuachia Roma na kumkumbatia Amina.
“Aunt Amina wewe ni mzuri sana”Aliongea Lanlan kwa kingereza
Roma alikuwa anajua kabisa binti yake hakuwa mtu mwaminifu kabisa kutokana na matendo yake mengi ya kisaliti aliokuwa akiyafanya kutokana na ahadi za chakula pamoja na kutolewa our matembezini kucheza na licha ya yote hayo Edna alikuwa akiyavumilia.
Lakini upande wa Roma bado aliona hio sio sawa kwa Lanlan na anatakiwa kumfunza kwani ilikuwa na wajibu wake , aliona kama ataendelea kutokuwa na msimamo kutokana na kupewa zawadi ingekuwa tatizo huko mbeleni.
Baada ya chakula cha mchana kuweka mezani Lanlan alichukua fursa hio kuanza kumpamba Nasra kwamba chakula chake ni kizuri na maneno meingine ya kumtia moyo kiasi cha kumfanya Nasra kutamani kumpiga busu, lakini zote hizo ni mbinu za Lanlan kumtaka Nasra kuongeza ubunifu zaidi kwenye mapishi.
Roma hakutaka hata kujishugulisha na tabia ya Lanlan kwa wakati huo maana ilimfanya kutamani kumpiga atulie.
Baada ya chakula Roma alitumia nafasi hio kuongea na Amina na aliweza kugundua kuna mengi ambayo yalikuwa yakiendelea , ilionekana baadhi ya ndugu wa Amina upande wa baba yake walianza kutaka kujumuishwa katika maswala ya urithi kutokana na hali yake ya kiafya.
Lakini ukiachana na hilo pia Amina alionekana alikuwa na majukumu mengi kiasi cha kumfana kukosa muda wa kuendelea kujifunza mafunzo ya kunyonya nishati za mbingu na ardhi.
“Natamni Nasra uje kunisaidia , najiona kabisa sijazaliwa kwa ajili ya kufanya biashara maana nashndwa kabisa kuongea na wafanyabiashara na kukutana na baadhi ya wawekezaji , kama Nasra utakuwa tayari kuja katika kampuni yangu nitakupa asilimia tatu ya Equity ya kampuni yote ya Kanani Group”
“Asilimia tatu!? , kulingana na thamani ya kampuni yenu hapo asilimia tatu ni zaidi ya mabilioni ya hela”AliongeaNasra kwa mshangao kwani ni kiasi kikubwa cha pesa cha kumfanya bilionea.
“Wewe ni kama ndugu yangu kwasasa na maamuzi yangu sidhani kama yatapingwa na bodi ya wakurugenzi maana asilimia ninazokupa ni za kwangu … Nasra kusema ukweli Sister Edna ana nguvu kubwa sana hata pasipo ya uwepo wako wewe , uwepo wa Dorisi na Benadetha unamtosha kabisa , kwanini usifanye kazi kwenye kampuni yangu na ukawa CEO Msaidizi , nitakulipa mara mbili zaidi ya unachopokea ndani ya Vexto?”
“Kuna watu wengi sana wanataka kunitoa ndani ya kampuni ya Vextoila nilikataa , ijapokuwa nina asilimia chache za umiliki wa kampuni ya Vexto nataka kutimiza ahadi yangu niliowekeana na CEO aliepita kipindi cha nyuma, Kama Edna hatonichukia basi maisha yangu yote naweza nikafanyia kazi ndani ya Vexto”Aliongea Nasra akikataa ombi la Amina.
“Lakini Sister Edna na kipenzi chetu wanataka kuachana , hautojisikia vibaya kuwa mbele yake ukienda kazini ?”Aliongea kwa sauti ya chini huku akimwangalia Roma.
“Kwanini unaongea hivyo Amina , hatujaachana rasmi kwa maandishi lakini tayari ushaanza kutamani nafasi ya Edna?”Aliongea Roma na Amina alikataa haraka haraka kwa kutingisha kichwa.
“Huo ujasiri natoa wapi , hio nafasi yenyewe kwangu ni ndogo sana isitoshe ninachoona Sister Edna ana hasira tu kwasasa na zikiisha atarudi kama zamani , halafu kwanza hakuna ambaye alikuambia umguse Sophia yalikuuwa makosa yako hebu muone , ijapokuwa kwa sasa ni star wa kimataifa na unaweza kujihisi umefanikiwa kumuweka chini yako kama mwanaume wake lakini umefanya maamuzi ya kukurupuka”
Roma kusikia maneno hayo ni kama aliona hayajakaa sawa , kwani sio kama yeye ndio alimfosi Sophia kumpenda , alichofanya ni kutotaka kumuona akiendelea kuteseka kwa ajili yake.
“Anyway , Sophia siku hizi anaendeleaje , maana sijafatilia taarifa zake tokea nirudi?”Aliuliza Roma.
“Kurudi kwa Sophia kumeiinua kampuni ya Vexto Media sana , ukijumlisha na ufanyaji mzuri wa filamu yake ya mwisho alioigiza chini ya Penguin Production amekuwa maarufu kimataifa na kwasasa anapokea Dili nyingi za kibalozi na pia kuombwa kuhudhuria katika matamasha mbalimbali, kulingana na tafiti iliofanywa na kituo cha utafiti cha Yugen Africa kimakadirio inaonyesha filamu aliogiza Sophia imetazwamwa na watu bilioni moja , ‘Endorsement’ ya Christen imefanya kazi kubwa katika mafanikio haya na mashabiki zake wanatarajia kumuona katika filamu nyingine tofauti”Aliongea Nasra.
“Kupitia hio filamu ameingiza kiasi gani kwa kampuni na yeye binafsi?”Aliuliza Amina
“Kulingana na makato ya kimkataba na kampuni Sophia ameweza kupata kiasi cha bilioni tano za kitanzania na kampuni inapata bilioni saba za kitanzania , japo hizi ni namba ambazo hazipo Fixed kwani mauzo yanaendelea”
“Kwa maneno yako ni kwamba Sophia siku hizi amekuwa maarufu kuliko mwanzo”Aliongea Roma huku akiona hio ni hatari zaidi kwani kadri Sophia anavyozidi kuwa maarufu ndio ugumu wa mahusiano yao.
“Honey kwanini usimpigie simu , ukamjulia hali?”Aliuliza Amina.
“Kwasasa hapana, Sophia yupo makini na ni mueelewa na isitoshe kwasasa atakuwa bize , haina haja ya kumsumbua”
Baada ya kuongea na warembo hao kwa muda mfupi Amina na Nasra ndio waliokuwa wa kwanza kuondoka, huku kila mmoja akiwa na miadi ya kibiashara.
Roma yeye baada ya kucheza cheza gemu na Lanlan hatimae alianza kusinzia na Qiang alimchukua na kwenda kumlaza.
Roma mara baada ya kuona hana cha kufanya aliamua kutoka na kuelekea mjini kwa mara nyingine kumtafuta Rufi.
Ijapokuwa Rufi alikuwa akiishi na mama yake , lakini pia alikuwa akiishi katika Apartment aliokuwa akiishi mwanzo lakini alikuwa ameigeuza kama ‘Computer lab’ sehemu ya kufanyia maswala yake yanayohusiana na tehama.
Ilikuwa ni kama maabara kutokana na wingi wa tarakishi ambazo zliokuwa zimefungwa na Rufi mwenyewe.
Roma tokea mara ya mwisho kufika hapo hakuwahi kwenda tena na mara baada ya kufika awamu hio alishangaa kukuta vitu hivyo na alishindwa kuelewa ni kitu gani ambacho Rufi alikuwa akifanya kupitia hizo tarakishi lakini hata hivyo hakutaka kuhoji sana.
Lakini kwa wakati mmoja alishangazwa na uwezo wa Rufi , kwani Rufi maisha yake yote alikulia katika ulimwengu wa majini lakini muda mchache ambao aliishi katika ulimwengu wa kawaida alikuwa amekusanya maarifa mengi sana kuhusu tarakishi , lilikuwa jambo la kushangaza kwake kwa wakati mmoja.
“Umefanikiwa?”Aliuliza Roma mara baada ya kumsogelea Rufi aliekuwa amekondolea Code za Programng akionekana kuunda Software.
Upande wa Rufi alikuwa ashajua ujio wa Roma tokea muda mrefu kwani yeye ndio alifungua mlango kwa njia anazozijua yeye bila ya kuamka kwenye kiti chake cya mzunguko.
“Nimefanikiwa kwa urahisi , shukrani kwa kinipatia access terminal za satilaiti yako ya Crogo, kwasasa nilichoweza kuona hapa ni kwamba karibia wanafamilia wote wa ukoo wa Ibuyawanga wamekusanyika mkoani kilimanjaro na hakuna ambaye ametoka”
“Vipi kuhusu eneo alipo Asha?”Aliuliza Roma na palepale Rufi alibonyeza tarakishi haraka haraka na ndani ya sekunde tu ramani ya mkoa wa kilimanjaro na mkoa wa Arusha kwa pamoja iliweza kujitandaza kwenye skrini.
“Yupo pia ndani ya eneo moja , kwenye hiko kidoti chekundu”Aliongea Rufi , ilikuwa rahisi kupata uelekeo wa Asha mke wa Waziri wa
Mazingira kwa kutumia namba ya simu yake.
“Kazi nzuri Rufi , ninachotaka sasa ufanye ni kumtumia meseji kwa namba isiokuwa na jina ukimweleza kujileta yeye na mtoto wake mbele ya Najma na kuomba msamaha kwa kusujudu au vinginevyo makazi yao yatageuka majivu”Aliongea Roma.
“Vipi kama angefika na kuyamaliza , si ungemfanya Najma kutoa hasira zake kwa kumpiga?”Aliuliza Rufi.
Ukweli ni kwamba siku ambayo Roma alienda kumtoa Najma alimkuta akifanyishwa kazi na polisi mmoja aliefahamika kwa jina la Catheryn , kitendo kile ambacho Roma aliweza kushuhudia Najma akifanyiwa na Afande huyo kilimuuzi kabisa na alimlazimisha Najma kulipiza kisasi kwa kumvunja mkono huyo Afande , Najma mwanzonni alikataa lakini Roma alimlazimisha kwa kumfokea na mwisho wa siku Najma alitoka gerezani akiwa amevunja mkono wa Afande Catherine Bonge.
Ijapokuwa hayakuwa makosa ya Afande Catherine Bonge kumnyanyasa Najma lakini Roma aliona kitendo cha kukubali uovu kwa ajili ya hongo malipo yake ni maumivu.
Najma alikuwa mpole sana na hilo Roma halikumpendeza na aliona kama Najma ataendelea kuwa mpole basi haitokuwa na maana kabisa hata ya kujifunza mbinu za kuvuna nishati za mbingu na ardhi.
“Usiwe na shaka , najua hata kama tumtumie hizo meseji hawezi kuja , kwanza hata msamaha wenyewe hakujisumbua kuomba zaidi ya kutaka kunilipa hela , mtu kama huyu anajiona matawi ya juu na lazima ashushwe kwa lazima, mpango wangu ni kwenda kutia moto makazi yao leo usiku”Aliongea Roma.
“You are indeed Nasty”Aliongea Rufi ..
SEHEMU YA 647.
Upande mwingine mkoani Kilimanjaro katika makazi ya kifahari ya famiia ya Ibuyawanga alionekana Bi Asha au Farha kwa jina lake lingine akiwa amevalia mavazi ya kulalia huku mkononi akiwa ameshikilia mvinyo.
Alikuwa amesimama kwenye dirisha ambalo limetengenezwa kwa usanifu wa mtindo wa kifaransa(French Window) , mtindo ambao ulifanya dirisha kuwa kubwa kiasi cha kulingana na urefu wake na kumfanya kuweza kuangalia mandhari ya msitu akiwa ndani ya jumba hilo katika horofa ya tatu.
Baada ya kugeuza kichwa chake nyuma yake alikuwa ni mume wake waziri wa Mazingira aliekuwa amekaa juu ya kitanda kikubwa cha sita kwa sita huku pembeni yake kukiwa na tarakishi ya kampuni ya Apple na mbele yake kulikuwa na Runinga kubwa ya nchi 83 ya teknolojia ya Oled iliokuwa ikionyesha habari za kimataifa kupitia chaneli ya Aljazeera.
“Mpenzi , je hizo taarifa za kimpropaganda zinakuvutia zaidi kuliko mwanamke mrembo kama mim?”Aliongea kwa mapozi ya kimitego lakini Waziri hakuonyesha kumwangalia kwani alikuwa bize akiangalia habari ya kimapigano huko Urusi na Bi Asha ambaye alikuwa amevaa vazi la kimitego alisimama mbele ya mume wake.
“Huh.. uliniambia meneno matamu ya kuvutia kipindi ambacho ulikuwa ukinitongoza mpaka nikakubali kuolewa na wewe baada ya kifo cha mkeo , sasa ushanioa unaonyesha kutonitamani tena , hauogopi naweza kukuacha muda wowote , isitoshe sio kama nilikubali kuolewa na hela zako , kama ni hela baba anazo na ananipenda mno na kunidekeza”Aliongea.
Waziri mara baada ya kusikia neno ‘baba yangu’ palepale alishituka , hakutaka kukosa sapoti kutoka kwa familia ya mke wake kwani alikuwa na mpango wa kugombea uraisi mara baada ya Raisi Senga kumaliza uongozi wake.
Ukweli ni kwamba hakumuoa mwanamke huyo kutokana na kwamba alikuwa akimpenda bali alimuoa kwa ajili ya kutimiza mipango yake ya kuwa raisi wa nchi hii, hivyo hisia zake zidi ya mwanamke huyo zilikuwa ni za kufosi sana.
Ili kutomkasirisha mrembo huyo aliefanya upasuaji wa sura na umbo palepale alinyayua uso wake na kumwangalia na kisha akatoa tabasamu na kutoka kitandani na kisha alimshika kiuno chake na kumkalisha kwenye kitanda na kuanza kumfanyia Masaji.
Upande wa Asha alijiona mshindi na alitoa tabasamu la kejeli baada ya kuona kwamba alikuwa na uwezo wa kumfanya Waziri wa Mazingira kumfanyia masaji.
“Kutokana na ubize wangu najikuta nakosa muda wa kukaa kama hivi na kuangalia habari , lakini hebu muone unapenda kujifanyisha mtoto kila tunapokuwa pamoja , tumeona muda mrefu mno bado tu unataka kuwa kama msichana mdogo”Alijitahidi kubadilisha kutoridhika kwake kwa kuchomekea maneno ya kumpumbaza lakini pia na ya kijembe.
Asha alitaka kuchukua glasi ya mvinyo wake ili kunywa kidogo huku akichanua miguu yake kwa mtindo wa helufi V ili kumfanya mwanaume huyo kufanya kazi ya kumfurahisha lakini zoezi lake liliingiliwa na ujumbe wa meseji kwenye simu yake.
Baada ya kuchukua ile simu na kuangalia ujumbe wenyewe furaha yake ilipotea.
“Nini tatizo mke wangu?”Aliuliza mheshimwia baada ya kuona mabadiliko ya Asha.
“Ni ujumbe mwingine wa kunidhalilisha , hebu achana nayo tu”Aliongea lakini licha ya hivyo ilikuwa ngumu kwa Waziri Nguzo kupotezea swala hilo na alishikilia paja la mwanamke huyo kwa nguvu.
“Kuna kitu unanificha, kama ni swala kubwa unapaswa kunishirikisha”
“Kama huna mambo ya kufanya ni bora ukaweka
ubize kudili na watoto wako wawili wa kiume”Aliongea.
“Huh .. nini Tatizo la Ayubu na Salihi?”Aliuliza mheshimiwa huku akikunja sura.
“Tabia zao sio nzuri , hivi unajua kwamba Salihi jana alifanywa kubewa kurudishwa nyumbani baada ya kulewa yeye na kaka yake, kaka yako alikuwa akicheka sana matendo ya watoto wako kwasababu wa kwake wamekua katika maadili , ikiendelea hivi hakuna yeyote ambaye anaweza kupata urithi , leo ni siku ya ibada ya kimila na jini Husna bado hajachagua mrithi, lakini bado tu analewa , ataongozaje ibada ili hali ananuka pombe , unajua mwenyewe hawezi kuingia madhabahuni akiwa amejinajisi”Aliongea kwa kulalamika.
“Lakini hio ni kazi yako ya kuwaangalia , unajua mimi nipo bize na maswala yangu ya kisiasa na wewe ndio mama yao kwanini usiwazuie?”
“Unajua mwenywe wananiona kama kituko kwasababu tu mimi ni mama yao wa kambo , isitoshe mtoto wako mkubwa hata wewe mwenyewe sidhani kama anaweza kukusikiliza , au nasema uongo?”:
“Huyo mpuuzi anathubutu vipi , hebu leo toa maagizo Salihi atakaa na mimi karibu na Ayubu mwambie achukue nafasi ya Salihi kwani na yeye pia anaweza kuongoza ibada”Aliongea.
Asha aliishia kutoa tabasamu ambalo kwa nje lilionekana kama la roho nzuri lakini ndani yake limejaa unafiki , alijiambia huyu mwanaume anaonekana kujiamini lakini ni mdhaifu , nani angeweza kutegemea mwanaume ambaye anaheshimika kama waziri na pia mtoto wa pili wa mzee Sharifu kuwa dhaifu hivyo na sio tu mbele ya watoto wake lakini mpaka kitandani.
Hakupenda tu tabia ya kulewa kwa Salihi kwani mara nyingi huishia kulala na changudoa na kama sio hivyo asingejisumbua kumfatilia.
Baada ya Waziri kutoa maagizo hayo hakuongea zaidi na alijikuta akianza kumridhisha mke wake kwa kutumia mdomo na ulimi.
*****
Upande mwingine Roma mara baada ya kuachana na
Rufi aliweza kupokea ujumbe kutoka kwa Samweli
Nguluma ikimpa taarifa mzigo unakaribia kufika Kilimanjaro na ili kusitokee polisi kuunasa basi anapaswa kuwepo mwenyewe.
Roma mara baada ya taarifa hio alitoa tabasamu na kisha alianza safari ya kuelekea mkoa wa Kilimanjaro.
Alitaka kutumia usafiri wa gari lakini aliona ingemchukua muda mpaka kufika hivyo alichagua ndege kuelekea huko.
Ratiba za ndege kuelekea mkoani kilimanjaro zilikuwa ni nyingi sana kutokana na upande huo kuwa sehemu ya kitalii zaidi na wasafiri wengi wanaofika Dar es salaam walikuwa wakielekea Kilimanjaro hivyo saa kumi na moja na nusu Roma aliweza kupanda ndege ya shirika la Taifa.
Ilimchukua dakika kama sabini tu kuwa angani mpaka kufika Kilimanaro na kutoka nje ya uwanja wa ndege.
Roma ilikuwa ni mara yake ya kwanza kufika mkoani Kilimanjaro hivyo baada ya kushuka tu kwenye ndege alipiga namba ambayo alitumiwa na baba yake Benadetha na kutoa maagizo na ndani ya dakika hio hio alimpatia mwendesha Taksi simu na baada ya bwana yule kuongea kwa dakika akionekana kupokea maelekezo Roma aliingia ndani ya gari.
Giza lilikwua lishaingia tayari na baada ya Roma kutoka nje kidogo ya Wilaya ya Hai gari ile ilisimamishwa nje ya duka moja la vifaa vya spare za magari , sehemu iliokuwa na gereji pembeni na Roma alilipa na mwendesha Taksi aliondoka.
Roma mara baada ya kusogelea duka hilo aliweza kukutana na kijana alievalia Shati kubwa la mtumba oversize la draft na buti zake kubwa na Jeans akivuta sigara.
Roma hakushangazwa sana na mavazi hayo kutokaa na uzoefu wake wa maeneo mengi na alimsogelea na kisha akampatia tano.
“Wewe ndio Mr Roma!, Boss amenionyesha picha yako , unaweza kuniita Paskali au Mr P”Aliongea kwa rafudhi yake ya kichuga chuga huku akimpatia Roma sigara, Roma alikataa na kisha aliingiza mkono kwenye koti lake la suti na kisha akampa pakini nyingine ya sigara na bwana yule mara baada ya kuiangalia alionyesha kuona jina geni lakini alishukuru na kuiweka mfukoni.
“Asante kwa kunisubiria Mr P , vipi nimechelewa sana na kuharibu ratiba zako nyingine?”Aliongea Roma kwa upole na uongeaji wake ulimfanya bwana yule kuonyesha tabasamu na hali ya kujisikia vizuri.
Ijapokuwa alikuwa akiaminiwa sana na Bosi wake Samweli Nguluma na kupewa kazi zinazohitaji ufanisi wa hali ya juu lakini hata bosi wake hakuwa akimpa heshima kulingana na msaada wake , lakini Roma ambaye alikuwa akimjua kama mtu mzito alionyesha kuwa Humble , ilimfanya kujisikia vizuri.
Mwanzoni alijua Roma asingemjali sana kuhusu yeye na angekuwa ni kama mabosi wengine ambao anakutana nao lakini baada ya kumuona kama mtu asiejikweza ilimpa motisha ya kumsaidia.
“Hapana kabisa bosi wangu , hii ndio kazi yangu hivyo hata ungekfika usiku usingeniharibia ratiba”Aliongea akijitetea na Roma alitingisha kichwa kumuwelewwa.
“Vipi una mzigo wangu?”Aliuliza Roma huku akikagua mazingira ya watu waliopo , kulikuwa na mafundi makenikia waliokuwa wakihangaika na magari makubwa ya mizigo ndani ya hilo eneo.
“Ndio mzigo umefika mapema tu nusu saa iliopita, na jambo la bahati hakuna sehemu polisi walipotusimamisha na kutukagua”Aliongea Paskali huku akisimama na kutembea na Roma upande wa pili kwenye geti ambalo lilikuwa lina ukuta mkubwa ulioenda hewani na baada ya kuingia ndani waliweza kukutana na gari kubwa yenye bodi la Kontena nyeupe lenye nembo shirika la Bohari ya dawa MSD.
Paskali alifungua haraka haraka na kisha akamuonyesha Roma kilichopo ndani yake na kumfanya atoe tabasamu huku akimpongeza ndani kwa ndani Samweli nguruma kwa kuongoza kuwa mhalifu Tanzania maana kwa amani ya nchi hii hakuamini jambo lake lingekuwa rahisi namna hio.
“Asante bro , lakini vipi kuhusu hili gari , kuna uwezekano halitoweza kurudi tena hapa, kutakuwa na tatizo”
“Bila shaka bro , Bosi kaagiza kwamba kila kitu ni cha kwako , lakini unapaswa kuwa makini kwani mzigo huu ni hatari na unaweza kuigeuza hata hili gari kuwa majivu”
“Usiwaze , hivi vitu vinawafaa wao ila sio mimi”Aliongea Roma huku akijua kwamba uwezo wake hata kama gari hilo limlipukie hakuna uwezo wa kupata madhara.
Mwili wake ulikuwa sio wa kawaida na kulingana na data za Zeros organisation inaaminika kwamba kutokana na kumulikwa na miale ya teknoloijia ya jiwe la Kimungu anaweza kuwa hai hata akipigwa na bomu , hapo ni kabla haijajumuishwa uwezo wake wa kijini.
Paskali hakujua kuhusu hilo , pengine alikuwa akijua ni nani anakwenda kushindana nae , lakini bosi wake alimwambia kutokuuliza maswali mengi, lakini bado alikuwa akijiuliza inawezekanaje mtu mmoja kwenda kukamilisha kazi ya hatari namna hio.
Roma mara baada ya kukabidhiwa mzigo wake hakutaka kundelea kubakia hapo aliingia ndani ya gari hilo na kisha aliliwasha na kulitoa nje kwa mbwembwe na baada tu ya kuingia barabarani alimpigia simu Rufi.
“Rufi nipe uelekeo?” Aliongea Roma.
“Subiri kidogo?”
“Kuna tatizo”
“Uelekeao wa Asha naona umebadilika , tofauti na kwenda moja kwa moja geti la mbele yake , unapaswa kuzunguka nyuma , kilomita mbili kutoka ulipo kuna barabara inayoeleka kulia kwako chukua hio na utakuta geti mwisho kabisa wa barabara upande wa kusini karibu na msitu”
“Nini kimebadilika?”
“Nimejaribu kudukua mawasiliano ya mmoja ya wanafamilia , inaonekana kuna ibada ya kimizimu ambayo inafanyika kwenye Madhabahu yao iliopo maili moja kutoka yalipo makazi , inaangaliana na geti la upande wa kusini”Aliongea Rufi na palepale Roma alitoa tabasamu lililojaa uovu ndani yake.
“That is perfect , itaniokolea muda wangu kuzunguka zunguka sehemu moja kwenda nyingine , naona hata Mungu mwenyewe ananisaidia katika hili”Aliongea Roma.
“Babe hio familia inamiliki eneo kubwa mno , ninawasiwasi itakuwa ngumu kuharibu makazi yao yote, isitoshe wana watu wengi sana ambao pia ni wafuasi wao ,, kama mpango ni kuchoma moto basi uwezekano wa kuzimwa kabla haujakithiri ni mkubwa”Aliongea.
“Tutaona kitakachotokea , lakini hakikisha unanipatia taarifa kwa kila kinachotokea”Aliongea Roma na kisha alikata simu na kuseti ramani yake vizuri na kuendeleza safari.
Inasemekana kwamba ukiachana na Mzee Sharif wakati huo akijulikana kama muislamu alieshika dini lakini ilionekana ilikuwa ni kujionyesha tukwani alikuwa ikisalia kitu kingine kabisa.
Jambo hilo liliwakasirisha sana watu wa dini enzi hizo na kumpa onyo mara kwa mara kuachana na
Ukafiri wa kuasi dhidi ya dini ya kiislamu lakini
Mzee huyo hakutaka kuacha huku akiamini kwamba anachokifanya ni kuendeleza urithi ulioachwa na mababu zake.
Ilishangaza sana kwa mzee kama huyo kuwa na msimamo wa aina hio na hata baadhi ya watu walihoji kwanini alikuwa na msimamo wa aina hio , je kuna kipi cha siri juu ya mungu anaemsalia lakini hakukuwa na majibu kwani ilikuwa ni siri yake.
Mzee Sharif alikuwa ni raia wa nchi ya Kuwait na inasemekana alikuwa na utajiri wa kutisha sana unaotokana na madini pamoja na kumiliki visima vingi vya mafuta na hili lilimfanya kuogopwa na watu hata pale ambapo alikuwa akisalia miungu anayoijua yeye.
Upande wa serikali ya Marekani kupitia kitengo chao cha CIA walimtumia Tajiri Sharif kutaka kuipa kampuni yao ya Gulf Oil Corporation nguvu ya Ihtikar(Ukiritimba) wa kusafirisha mafuta yote kuingia nchini kwao lakini pia kuwa wasambazaji pande nyingine za dunia.
Serikali ya Marekani ilimtumia tajiri Sharif kutokana na kumuona kama ‘Weak point’ kutokana na msimamo wake wa kidini na waliweza kufanikiwa kwani waliweza kutumia tabia yake kwa manufaa , kwa mfano Mzee Sharif ukiachana na dini yake alipenda sana pesa na ni kupitia pesa iliomfanya kusaliti nchi yake na baada ya kushitukiwa ndio ikawa mwisho wa nguvu yake ndani ya taifa hilo kwani ilikiwa ni kama ule uvumilivu waliokuwa nao Raia juu ya Mzee huyo ulifika ukingoni..
Katika hatua za kujiokoa Mzee huyu aliweza kutolewa na serikali ya Marekani pamoja na mali zake na kukimbilia hapa nchini Tanzania na huo ndio ukawa mwisho wa kampuni ya Gulf Oil nchini Kuwait , kwani ilitaifishwa na serikali rasmi, hio ni historia iliomtokea Mzee Sharif miaka hio ya sabini.
Kabla ya kuja nchini Tanzania aliishi Marekani kwa miaka miwili mfululizo na katika miaka hio alitumiwa na Serikali ya Marekani kama Asset ya kutoa taarifa za uchimbaji wa mafuta nchini Kuwait , taarifa ambazo ziliifanya serikali hio kuweza kutengeneza mirija yao nchini humo.
Inasemekana baada ya kuishi miaka miwili nchini
Marekani ndipo alipofanya maamuzi kuhamia nchini Tanznia huku sababu kubwa alisema kwamba mungu anaemsalia kalichagua taifa hilo.
Serikali ya Marekani ikatumia ubabe wake na kuhakikisha Mzee huyo anapata eneo nchini Tanzania na permanent guaramtee protection , ni kweli raisi wa kipindi hicho aliweza kuidhinisha
Mzee Sharif kuuziwa eneo kubwa sana huko mkoani Kilimajaro na makazi yake yakaanzia hapo , ijapokuwa swala hilo mwanzoni liliibua sintofahamu kwa raia lakini ilikuwa ni kama upepo ambao huvuma ukiwa unasafiri mpaka kutoweka..
Baada ya kukaa nchini Tanzania mzee huyo alijenga eneo hilo makazi ya kifahari sana na mwanamke wa kwanza kumuoa alikuwa ni Mzanzibar na ilisemekana baada ya kujifungua tu alipoteza maisha hapo hapo , akaoa mwanamke mwingine ambaye alimzaa Waziri Nguzo na baada ya kujifungua na yeye alikufa hapo hapo.
Kitendo cha kufairki kila mwanamke ilianza kuibua maswali kwa ndugu wa familia ya mke lakini Mzee huyo aliweza kuzima kila skendo na maisha yakaendelea.
Lakini ajabu ni kwamba utaratibu huo haukuishia kwa yeye tu hata kwa watoto wake baaada ya kuoa kila mwanamke anaejifungua anakufa siku hio hio , lakini utofauti kidogo ulionekana kwa Waziri Nguzo kwani mke wake alijifungua mara mbili mtoto wake wa Kwanza ambaye alimwita jina la Ayubu na kisha baada ya kuzaliwa kwa Salihi ndio akafariki na ndipo alipokuja kumuoa Asha.
Asha mpaka wakati huo hakuwa amejifungua mtoto yoyote na Waziri na hakuwa na mpango huo wa kuzaa ili atolewe kafara.
Ukiachana na maswala ya ndani ya familia Mzee Sharifu alijitambulisha kama Mtanzania halisi na tokea kuishi kwake Tanzania alijijengea koneksheni za kisiasa kwa namna ya kipekee sana , kwanza hakuwa akichagua upande wowote wa kuungana nao bali alitumia pande zote ndani ya Tanzania kujinufaisha , ukichana na maswala ya kisiasa pia alikuwa ni tajiri mkubwa sana ambaye alikuwa na biashara nyingi za mabasi pamoja na vituo vya mafuta nchini, ukiachana na biashara zake za kihalali lakini pia alikuwa akijihusiha na biashara nyingi za kimagendo ikiwemo uuzaji wa madawa pamoja na pembe za Tembo.
Hivyo kuingia kwa Mzee Sharif nchini ilikuwa ni kwa msaada wa serikali ya Kimarekani.
Lakini ukiachana na hayo kuna mambo mengi sana ambayo yanaendelea ambayo ilifanya serikali ya Tanzania kutoweza kumgusa kwa kipindi kirefu sana.
Ndani ya eneo hilo familia nzima ilikuwa imekusanyika kama ilivyom desturi yao kukusanyika kila ifikapo mwisho wa mwaka na kufanya ibada za kimila kumsalia mungu wao.
Katika kipindi hicho familia inapokusanyika ulinzi unakuwa mkali sana kuliko siku zote na ikiwa ni saa mbili za usiku walinzi waliokuwa na siraha nzito walikuwa wakiimarisha ulinzi kiasi kwaba hata paka akitaka kuingia ndani ya eneo hilo angeweza kuonekana.
Sasa ikiwa ni mwisho mwisho wa ibada wakati wakipata chakula cha usiku ghafla tu walinzi walishituka mara baada ya kuona gari linalowasha taa kuja upande wa geti la kusini huku likiwa na kasi kubwa.
Eneo hilo licha ya kujengwa barabara nzuri ya viwango vya lami haikuwa ikitumika mara kwa mara hususani nyakati za usiku hivyo kusogea kwa gari hio kuliwapa mashaka walinzi.
Kilichoshangaza zaidi ni kwamba gari hio haikuonekana mwanzoni kabisa na ilikuja kuonekana
ikikaribia geti , pengne hata kama haikuwa ikinguruma vipi kuhusu taa zake.
Ukweli ni kwamba Roma alitumia mlima wa eneo hilo kuendesha gari pasipo ya kuiwasha na licha ya pia kuwa na giza hakuathirika kuendesha gari , alifanya hivyo ili kuwapa surprise na wakati anakaribia geti ndio aliwasha taa sasa na kupiga honi mfululizo.
Muda uleule walinzi kadhaa waliokuwa ndani walitoka nje ya geti na kisha wakasimama katikati ya barabara kuingia getini huku wakiipa ishara ya kusimamisha lakini kutokana na mwendo wa gari hio waliona kabisa hakuna dalili ya kutosimamishwa
Walinzi walijikuta wakipigwa na mshangao na walihofia pengine gari hio imekosa breki ndio maana ilikuwa kwenye mwendo mkali namna hio .
Hali ya makelele pamoja na msuguano wa tari za gari na barabara ilikuwa ni kama vile ni mnyama ambaye anakaribia kuwararua
Dakika ileile ambayo wanakumbuka siraha zao na kutaka kushambulia gari ilikuwa tayari ipo mbele yake na kabla hata hawajajipanga.
“Bang!!”
Gari ile iilingia na geti na kupita huku likiharibika na walijikuta wakitoa yowe huku baadhi ya walinzi wakipata majeruhi na Roma hakujali anaekufa.
SEHEMU YA 648.
Upande wa familia ya Mzee Sharif baada ya ibada walikusanyika katika eneo moja kwa ajili ya chakula cha usiku.
Ilikuwa ni familia kubwa kweli ikiunganishwa mpaka na pande za wajomba.
Mzee Sharif pengine ndio mtu ambaye ameishi miaka miaka mingi sana ndani ya taifa la Tanzania , inasemekana ana miaka mia moja na ishirini lakini bado alikuwa na nguvu zake licha ya kuonekana mzee sana.
Na swala hilo lilishangaza hata watu wa nje ya familia hio , lakini ukweli ni kwamba kuna siri nyingi sana juu ya Mzee Sharif mwenyewe ambazo pengine hata watoto wake hawakuwa wakizijua.
Wakati wakiongea kwa furaha na kucheka palepale alikuja kiongozi wa Walinzi bwana mweusi ambaye kwa kumwangalia tu ni Mmasai ambaye ameachana na tamaduni zao.
Kabla hata yule bwana hajaongea neno lolotea ghafla tu king’ora kilianza kutoa mlio na kufanya watu wote kukurupuka.
“Uvamizi!!”Mzee Sharif ndio aliekwua kwa kwanza kuongea hayo maneno huku watoto wake na wajukuu wake wake wakifatia kushangaa
Mfumo wa alarm ya nyumba hio tokea uwekwe ni zaidi ya miaka kumi iliopita na haijawahi kutokea hata siku moja ikatumika , hivyo swala hilo halikuwa la kawaida kabisa.
“Kimyaa..!!”
Mzee aliongea kwa sauti kubwa akitumia lugha ya kiswahili na sauti yake iliiibua hofu ambayo sio ya kawaida kwa wanafamilia hao , kwani aliogopesha , ijapokuwa alikuwa mzee lakini mkandamizo aliokuwa akisambaza haukuwa wa kawaida hata kidogo.
“Kuna nini?”Aliuliza akimwangalia yule mlinzi. “Kuna mtu amevamia geti na fuso na sasa inaonekana anaeleka upande huu bosi”Aliongea kwa hali ya kutetemeka.
“Unasema kuna mtu katuvamia na Fuso , tena ndani ya eneo langu haha… pamoja na uzee wangu huu wa kuishi miaka mingi sijawahi kutegemea mchezo
wa aina hii kutokea , pengine nakaribia kufa”Aliongea na palepale alimgeukia mtoto wake mkubwa ambaye ni mfanyabiashara.
“Wewe mtukutu , hebu chukua walinzi wote waliomo humu ndani tuelekea upande wa getini”Aliongea.
“Baba , ngoja nitafute mtu wa kumuua , wewe huna haja nya kujisumbua kuamka hapa unapaswa kuendelea kula chakula”Aliongea Waziri.
“F**ck you , acha kujifanyisha mjuaji mbele yangu?”Aliongea na palepale alimpiga teke Waziri na alijikuta akidondoka na kiti chake chini kama furushi.
Kila mmoja alishangazwa na jambo hilo , hakuna ambaye alitegemea mzee huyo angekuwa na nguvu ya kumpiga Waziri mwenye mwili mkubwa na kudondoka namna hio .
Naibu waziri Salihi , Asha na wengine wote walijikuta wakiwa katika mshituko kwani mzee ambaye siku zote walimzoea kumuona akitembea na mkongojo leo hii alionekana kuwa na nguvu kiasi cha kunyanyua mguu wake bila msaada wowote na kutoa kichapo.
Baadhi ya walinzi walioshuhudia tukio hilo hawakushangazwa ni kama walishamshuhudia mzee huyo kufanya kitu kama hicho na uzee wake.
Wanafamilia hao walikuwa wakijua kwamba utajiri wao na nguvu yao ndani ya Tanzania haikutegemea koneksheni , na utajiri waliokuwa nao bali kile walichokuwa wakimiliki, kitu cha siri sana ambacho pengine hakuna mtanzania wa aina yoyote angeweza kutegemea kama kinamilikiwa na Mzee huyo.
Ndio kitu ambacho kilimfanya Mzee huyo kufurumushwa kwenye nchi yake na kukimbilia nchini Tanzania na kuendelea kukiabudia.
Dakika ileile ni kama jeshi limekusanyika kwani kila ndani ya eneo hilo walinzi waliweza kukusanyika sehemu moja na Mzee huyo akiwa ametangulia alianza kutembea kueleka uelekao wa geti ambalo limevunjwa.
Jengo hilo la ibada ambalo hutumika kwa ibada ililikuwa lipo katikati ya eneo hilo , lakini likiwa karibu zaidi na geti kubwa ambalo ipo upande wa kusini , upande ambao una msitu mkubwa.
Geti la upande wa Kaskazini ndio ambalo lilikuwa karibu na makazi ya watu na la upande wa Kusini ndio ambalo lilikuwa likiunganisha na barabara inayoingia msituni.
Dakika ileile ambayo Mzee Sharif anafika akiongozana na familia yake , kila mmoja alijikuta akipagawa baada ya kuona tukio hio kwani kilichoharibiwa sio geti tu bali hata jengo lao la ibada eneo la mlangoni lilikuwa limevamiwa na gari hilo na ni vumbi tu lilikuwa limetanda.
Baada ya kufika karibu mzee alijikuta akipatwa na ahuenni mara baada a kungundua kilichoharibika ni uzio na mlango tu na eneo la ndani hakuna kilichoharibipka , pengine ni kutokana na uwepo wa ngazi nyingi kwenda juu kuingia madhabahuni.
Roma alikuwa akisbiria wote wakijikusanye eneo moja , mwanzoni alifurahi kwamba angewakuta wakifanya ibada lakini alichukia mara baada ya kugundua amechelewa na washasambaa, lakini hakujali baada ya kutoka nje ya gari alisimama juu ya ngazi na kutoa sigara yake na kuiwasha huku akisubiria wote wajitokeze.
Baada ya Asha na Salihi kumuona Roma walijikuta wakipigwa na mshituko wa aina yake na kujiuliza mtu huyo alikuwa kaifanya nini hapo.
Mzee Sharif akiwa na hali yake ya uzee alimwangalia Roma kwa macho ya mshangao kwani hakutegemea mtu aliefanya uharibifu nyumbani kwake kwa kuvamia alikuwa wa kawaida sana.
Eneo hilo licha ya kwamba lilikuwa ni usiku lakini taa za Spotlight zilikuwa zikimulika na kufanya liwe kama mchana.
“Hahaika una uasiri wa aina yake , wewe ni nani?”Aliuliza Mzee huyo kwa kiswahili fasaha.
“Baba haina haja ya kuongea nae , muue”Aliongea Waziri , hakumchukia baba yake licha ya kupokea kipondo cha teke.
“Kimya , hujaruhusiwa kuongea”
Roma alijikuta akishangaa mara baada ya kumkagua huyo mzee, ijapokuwa uwezo wake wa kijini ulikuwa dhaifu kuliko mwanzo lakini mara baada ya kumchunguza Mzee Sharif aliweza kugundua alikuwa na nguvu za kijini ndani yake.
Roma kama alivotarajia , hakuwa mtu wa kawaida kabisa mara baada ya kupewa historia ya mzee huyo pamoja na nguvu zake , ni kama kile alichoshuku kimepata majibu yake, lakini ilimshangaza kwa kuona mtu wa aina hio kujichimbia hapa Tanzania na kuitawala nchi nyuma ya pazia.
Kilichomleta Roma ukiachana na kutaka kulipiza kisasi chake , ni shauku yake aliokuwa nayo kulingana na maelezo ambayo ameyapata kutoka kwa Omari.
“Oii..Asha hapo , nimekutumia meseji mara kibao lakini ukaamua kunidharau , unafikiri nilichokuwa nikikuambia nilikuwa natania , vipi sasa hivi , je upo tayari kunisujudia?”Aliongea Roma akimnyooshea kidole mwanamke Asha aliekuwa amevalia Abaya ya rangi nyeusi.
Na muda huo huo Roma aliwasha sigara nyingine na kupiga pafu la moshi na kuutoa kwa pua kama vile ni gari moshi.
Asha miguu yake ilikuwa ikimtetemeka mno na watu wote walijikuta wakimwangalia kwa macho ya kiulizo.
“Asha nini kinaendelea?”Aliuliza Waziri wa Mazingira baada ya kukumbuka muda ambao alimuuliza mwanamke huyo na akapotezea swali lake.
Asha hakupata tena ujasiri wa kuongea uongo na palepale alisogea mbele ya Mzee Sharif.
“Baba nimekosea sana , nimekosea familia yote ya Sharif lakini nilikuwa na sababu zangu”Aliongea kimaigizo.
“Niambie nini kilichotokea?”Aliongea Mzee Sharif na palepale Asha alianza kuelezea tukio la Najma huku akibadilisha ukweli.
Alisema kwamba Najma alikuwa akimtega Salihi kwa ajili ya kupata nafasi kubwa zaidi ndani ya wizara na kusema kwamba alijaribu kumpa hadi onyo lakini kaishia kutukanwa hivyo akaagiza watu wake kumpa onyo kwa kuharibu gari yake na baada ya hapo polisi wakafika na kumpeleka kituoni kwa ajili ya mahojiano lakini Roma akafika na kumtoa huku akiongezea kwa kusema kumbe alikuwa akicheza kotekote.
“Baba walitaka niende nikawasujudie lakini mimi nikakataa na kuwaambia kwamba nitawafidia kwa kitu kingine lakini hakukubaliana na hilo , sikutegemea kama ataenda mbali hivi , ni makosa yangu baba naomba uniadhibu”Aliongea huku akicheza mchezo wa akili.
Kwa wanafamilia hao ambao walikuwa wakimjua tabia yake waliona pengine stori aliotoa ni ya kutengeneza lakini licha ya hivyo alikuwa akichukuliwa kama mwanafamilia
Licha ya kwamba familia ya Roma ilikuwa na nguvu haikumaanisha kwamba Familia ya Sharif ilikuwa ikimuogopa na hata kama ni mzee mwenyewe Sharif asingekubali mwanafamilia kujishusha na kumsujudia Roma.
Kwao taswira yao ndio ilikuwa kitu kikubwa sana , na mzee huyo alijiona yupo juu kuliko watanzania wote na inasemekana alikuwa ameua sana watanzania ambao wamefanyakazi kwake na kuonyesha utomvu wa nidhamu.
Isitoshe pia waliona Roma hakuwa na sabababu ya kuwavamia kwani mtu ambaye ameguswa sio kwamba ni mke wake bali ni mchepuko tu.
Muonekano wa Mzee Sharif ulikuwa ni ule usio wa kusomeka kwa wakati huo.
Wanafamilia wote walikuwa wakimjua Roma na wameweza kusikia pia alikuwa na nguvu za kijini na wengi walikuwa wakimjua kama mtu mkatili sana.
Tokea Mzee Sharif kujua nguvu ya Roma na ukichaa wake alitahadharisha watoto wake kuwa neutral na kuhakikisha kwamba hawachokozani nae kwa namna yoyote ile lakini kitu ambacho pengine amekosea mzee huyo ni kutokumuonya Asha , pengine ni kutokana na kutegemea mume wake angefanya kazi hio.
“Wewe mtoto , najua uwezo wako , lakini umevuka mipaka awamu hii”Aliongea Mzee Sharif.
Roma hakujisumbua na palepale alisogelea nyuma ya gari lake na kisha akafungua mlango kwa nyuma kuonyesha mzigo ambao amebeba na wale waliokuwa wakijua wanachokiona ni nini walijikuta wakishikwa na mshangao.
Ilikuwa ni gari zima ambalo limejaa aina flani ya mabomu ambayo yakikutana na moto hutengeneza mlipuko.
Roma mara baada ya kuongea na Mzee Samweli
Nguluma alikuwa akihitaji mabmu aina ya C4 au RDX mzee huyo alimwambia kwamba hana uwezo wa kupata aina hayo ya mabomu lakini anaweza kumsaidia kitu kingine cha kusababisha milipuko, mwenyewe akiyaita mawe ya kutengenezea fataki au mabomu ya kienyeji.
“Mnaonaje , mwenye macho haambiwi tazama , ijapokuwa haya hayana nguvu kubwa kama bomu la kisasa lakini kwa wingi huu wa gari zima yatakuwa na uwezo wa kuunguza hilo jengo lote la ibada zenu za kipuuzi, yaani leo itakuwa ni show ya kuwangalia milipuko ya fataki angani hehe..”Aliongea Roma na kufanya watu wote kushikwa na baridi.
“Asha,, wewe mjinga , kwanini umeyasababisha haya”Aliongea waziri akimfokea mke wake , alikuwa akiigiza ili kuepuka lawama kutoka kwa baba yake. “Nguzo usitake kumbebesha mwanangu kila kitu , kama ungekuwa makini haya yote
yasingetokea”Aliongea baba yake Asha Mzee flani mwenye muonekano wa kihindi , alikuwa akifahamika kwa jina la Mzee Hamisi Maya , alikuwa ni mtoto wa Tajiri Maya kutoka india.
Baada ya mzee yule kuongea vile palepale alimgeukia Roma na kumwangalia kwa kejeli huku akikumbuka tukio moja ambalo aliliratibu yeye mwenyewe linalohusiana na Raheli mke wa Adebayo , yaani mama yake Edna.
“Wewe mtoto , unafikiri nchi hii ni ya kwako kwasababu tu raisi ni baba yako na unatokea katika familia ya Kweka , nakuambia awamu hii umegusa sehemu mbaya sana , jaribu kulipua hili eneo uone , nitahakikisha natoa koromeo lako nje”
“Unaongea sana , wewe nitakufanya uwe mfano kabla ya show yenyewe kuanza”Aliongea Roma na kisha aligeukia gari lake na kuchukua bomu moja na kulishika mkononi na kisha akamsogelea lakini palepale walinzi waliinua siraha zao wakimkinga kwa mbele.
“Simama hapo hapo , nitakuchukulia hatua na kukupoteza kama utaendelea na ujeuri wako , hakuna anekuogopa hapa?”Aliongea Mzee Sharifu akionya lakini Roma hakutishika na maneno yake na baada ya kuona analeta ujeuri alitoa ruhusa ya kushambulia.
“Traa.. tata,, tatata,, ta..”
Milindimo ya milipuko ya risasi ilianza kusikika mfululizo kiasi cha kutengeneza kiwingu lakini mpaka wanakuja kumaliza wakijua wamemaliza kazi Roma alikuwa mzima na ni sigara yake tu ilioharibika.
“Wewe ni nani … usiniambie ni yule mtu”Aliongea Mzee Sharif kwa woga akishindwa kuamini macho yake.
Edna yuko wapi , atarudiana na Roma kama Amina anavyosema atatulia , usikose.