Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

majini-watu majini-pepo majini majini majini maniji 😬 😬 😬 😬 😬 😬 😬 bikira ukahaba illuminant freemason VEXTO amina edna yezi doris rose lanlan visiwa vya wafu 🤣🤣🤣🤣🤣🤣hongmeng kekexil panas wema recho . . . .benadetha ernest najma monica maimuna rufi lekcha aoiline desmond sharif kweka zhenzhei pluto Persephone Diego zero Omari Poseidon . . . .

NJOONI MMALIZIE MAJINA MAANA NI MENGIII . . . .

Hata hivyo, mwamba SINGANO ameupiga wa ukweliiii
 
Visiwa vya malidives,seventeen, jeremy, desmond,blandina,bibi wema,the don,mr wadudu,mfalume wuja,mr Kuo, rufi etc.
ila ep moja imenifanya niirudie zaidi ya mara tatu ile inayoelezea kumbe roma yuko mikononi mwa shirika fulani na ndo linamuongoza bila mwenyewe kujua, na kumbe kifo cha seventeen ni feki, na kumbe ili wajue wako huru wakaruhusu walipue maabala ya shirika aisee hii dunia ina mengi. sasa atakuwa wapi huyu seventeen au ndo edina mwenyewe au ndo yule dada aliyebaki ulimwengu gani sijui ule unaomeza watu kupitia mnala maana roma kafichwa vitu vingi hata master wake alijificha wakati anakutana nae mara kwa mara akiwa na lanlan.

Hii simulizi ni ndefu sana hii na ya kuvutia haichoshi hata kidogo.uzuri na mwandishi yuko vema anatupia mapande kadhaa raia tukimaliza tunabaki bila kiu hadi wakati mwingine.
 
Ok
 
NILIMDHANIA KAHABA KUMBE BIKRA.

BY SINGANOJR

Mono no aware.

SEHEMU YA 725.
Tulipoishia Roma anaingia katika mtego wa Jini Anjiu na kumfanya afanikishe kupitia mapigo ya radi kwa kutumia Chungu chake na baada ya tukio hilo anajigamba kwa kumwambia Roma kwamba amemshindwa na hamuwezi tena kutokana na uwezo wake.
Roma alijua palepale alichokuwa akifanya Anjiu ni mashambulizi ya kimaneno ili kumfanya asijiamini , Roma alijua uwezo wake ulikuwa umeongezeka sana hivyo haikumaanisha moja kwa moja alikuwa amepoteza pambano.
Lakini sasa baada ya kuona namna ambavyo amechezewa akili na Anjiu alishindwa kujizuia na kuonyesha hasira waziwazi.
“Nani kapoteza?, sio kwa namna unavyofikiri , ingawa umeweza kuivuka Dhiki, kwa upande wangu nimefaidika sana na huna uwezo wa kushindana na ukubwa wa nguvu yangu ya ukweli ya nishati za mbingu na ardhi….Kwamba ndio nini sasa kama umweza kupita levo ya Dhiki ya radi .je unao uwezo wa kutengeneza siraha za kimaajabu ninazo tengeneza mimi?, hio mbinu yako unayojivunia nayo ya moto wa ndege na radi yako ya Zambarau haviwezi kuniua zaidi ya kunisababishia maumivu tu au unataka kuonja radha ya moto wangu mweusi?”
Anjiu uso wake ulijikunja baada ya kushangazwa kidogo na namna ambavyo Roma hakuingia kwenye mtego wake wa maneno ili kumfanya asijiamini.
Jini huyo alijua licha ya kwamba alikuwa na uwezo mkubwa katika kujifunza mbingu za nishati ya mbingu na ardhi alijua Roma angepatwa na hofu kutokana na maneno yake.
Alionekana kutokujua kitu kimoja kuhusu Roma, malezi yake yalikuwa ya tofauti kabisa na binadamu wa kawaida , katika maisha ya Roma maisha yake yote ni kupambania maisha yake na hicho ndio alichokuwa akielewa na siku zote aliamini kushindwa maana yake ni kifo hivyo ni ngumu sana kukubali kushindwa kirahisi.
Hata Athena ambaye alikuwa na uwezo mkubwa wa kumfanya kuwa na adabu hakuwahi kukubali kushindwa na Athena na alijua siku moja tu lazima na yeye amshikishe adabu.
Sasa kama hamuogopi Athena anamuogopaje jini Anjiu ambaye ndio kwanza ameonja radha halisi ya mapigo ya radi jambo ambalo yeye alipitia miezi mingi iliopita.
Likija swala la vita hata Anjiu mwenyewe hamfikii Roma hata kidogo kwa uzoefu.
Baada ya kuona namna ambavyo Roma alikuwa hana wasiwasi Rufi aljikuta akipatwa na ahueni vinginevyo angekuwa na wasiwasi na kuona kwamba hawawezi kushinda katika vita hio.
“Sawa tu , kwasababu unajikuta kujiamini sana nitakuonyesha utofauti uliopo kati yako na mimi”
“Askari wa kipepo ungana na mimi!!!”
Dakika ileile ambayo aliongea lile pepo ambalo lilikuwa limejigawa kutoka kwenye mwili wake lilimrudia kama kivuli na kuwa mtu mmoja.
Ghafla tu mkandamizo wa nguvu za mbingu na ardhi wa Jini Anjiu uliongezeka kwa kiasi kikubwa sana kwa zaidi ya asilimia therathini.
Ijapokuwa Roma alikuwa na utulivu lakini alishangazwa na namna ambavyo uwezo wa Anjiu ulivyoongezeka kwa sekunde.
“Uwezo wangu wa kijini kama nilivyokwisha kukueleza nilikuwa nimeupunguza na kuuhifadhi katika Askari pepo wangu , kwa sasa nishapitia Dhiki hivyo sina hofu ya kumiliki uwezo wangu wote, halafu bado tu unajiona unao uwezo wa kunishinda?”
Roma aliishia kutoa tabasamu la kejeli na bila ya kuongea neno lolote alitumia Chungu cha maafa ambacho kilikuwa kikizunguka angani ili kumshikilia Anjjiu mwili wake.
“Hakuna utofauti wowote wa namna ulivyokuwa na nguvu , kadri unavyokuwa na nguvu ndio vizuri zaidi kwangu kwani nitakuua na kutumia nguvu zako kama virutubisho”Aliwaza Roma.
Anjiu alikuwa katika kiwewe , alijua kwa kuunganisha uwezo wake wote ingemfanya Roma kuogopa na kuacha vita na yeye lakini Roma hakuwa na dalili ya kuacha kabisa vita hio.
Kitu ambacho hakuwa akikijua Anjiu ni kwamba mbinu yake ya kutumia pepo kama namna ya kukuza uwezo wake wa kijini Roma alikuwa anaijua sana hio mbinu kwani alibahatika kuingia katika ulimwengu wa majini pepo.
Ulimwengu ambao majini huvuna nishati kwa ajili ya kuamsha mapeppo yao ya ndani tofauti na kuyamaliza kama ilivyokuwa kwenye ulimwengu wa majini watu.
Ijapokuwa uwezo wa pepo lake ulikuwa na nguvu lakini ukweli ni kwamba faida ya kutumia pepo ni katika kujiimarisha katika utimamu wa kimwili tu na sio katika kufanya mashambulizi.
Ndio mara nyingi faida kubwa ya majini ambao wanatumia mbinu ya kuamsha mapepo yao ya ndani ni kwamba wanakuwa na miili yenye nguvu mno.
Hivyo Roma alijua Askari pepo huyo alikuwa akimtumia tu kama vile ni Dhana ya kuhifadhia nishati mbingu zake lakini pia kumuwezesha kupitia levo ya Dhiki.
Kitu kingine ni kwamba licha ya Anjiu kuwa na uwezo wa kutumia pepo lake lakini msingi wake wa nguvu za kijini sio ule wa majini pepo , yeye alitumia sehemu ya nguvu zake za kijini katika kuamsha pepo lake lakini majini pepo wenyewe hawatumii sehemu ya nguvu zao katika kuvuna nishati bali uwezo wao huongozwa na pepo kikamilifu.
Kwa lugha nyepesi ni kwamba Anjiu yeye pepo lake alilitumia kama Dhana ya kumsaidia katika mashambulizi lakini majini pepo wao pepo ndio uhalisia wao.
Chungu cha maafa kilikuwa kimeongezeka uwezo wake maradufu tofauti na ilivyokuwa mwanzo kabla ya kumeza nishati ya radi.
Kutokana na asili ya chungu hicho kuwa na nguvu ya giza kiliweza kumuona Anjiu kama chakula bora kabisa kula hivyo kilianza kuonyesha makali yake na kutaka kummeza.
“Shit!!”
Anjjiu mara baada ya kuhisi mvuto mkubwa kutoka kwa chungu hicho aliishia kutoa tusi na palepale alijitahidi kujitoa katika eneo hilo ili kuondoka katika mvutano huo kwa kutumia uwezo wake lakini ilionekana kuwa ngumu.
“Alama ya mkono ya Daloshoo..!!!!”
Anjiu aliinua mkono wake mmoja juu angani mara baada ya kutamka kauli hio na palepale alama za kimaandishi za michoro(runes) zilichomoza zikiwa na mwanga wa kustaajabisha hewani na sekunde ileile zote zilijikusanya pamoja na kutengeneza umbo la Alama ya mkono(handprint).
Vidole vya mkono ule vililikuwa vimetawalia na elementi zote tano na nguvu ya mbingu na ardhi ilitoka kwenye vidole vile kama vile mlango wa bwawa la maji umefunguliwa.
Chungu cha maafa palepale kilisogelea kwa kasi alama ile ya vidole na kwenda kupigana na ile nguvu lakini kilishindwa kufika kwani alama ile ya vidole vya Daloshoo vilikuwa na nguvu kubwa ya msukumo.
Kutokana na chungu kushindana na nguvu ile ya alama Anjiu palepale alitumia fursa ile kujichomoa katika ile kani ya mvutano na kuanza kumshambulia Roma.
Kutokana na Roma kumshikilia Rufi na mkono mmoja hakutaka kumsogelea Anjiu karibu hivyo palepale alitengeneza moto wa rangi ya Zambarau na kuanza kumshambulia nao.
Mara baada ya mashambulizi yao yote kukutana kati ulitokea mlipuko ambao uliangaza eneo lote lakini muda ulule Roma aliongeza mashambulizi ya kasi zaidi na kitendo cha Anjiu kuchelewa kwa sekunde tu mashambulizi ya Roma yalimfikia na kutokana na kasi yake alishindwa kutoa shambulizi la kupangua na aliishia kuruka na kukwepa shambbulizi lile.
“Scorching sun and fire rain!!!”(Jua la kuchoma na Mvua ya moto).
Dakika ileile mwili wa Jini Anjiu uligeuka kwa mara nyingine na kuonekana kama vile ni malaika wa moto wa jua na palepale mwili wake ni kama vile nguo ilioloana inayokun’gutwa kwani matone ya moto yalimtoka na kwenda kumvaa Roma kama vile ni matone ya mvua.
Mvua hio ya moto ambayo imetokana na mbinu ya Golden Crow ilikuwa na spidi kubwa mno tofauti na Roma alivyofikiri, katika spidi ya kupepesa jicho walikuwa washafikiwa na moto ule na kufunikwa.
Licha ya Roma kutengeneza ngao ya moto wa Zambarau lakini moto ule uliweza kupita lakini Roma hakutaka kuumia kizembe hivyo alitengeneza maji ya Kiroho kushindana na moto ule lakini wakati huo akijua hio sio nia kamilifu ya kuweza kushindana na moto huo hivyo bahati nzuri ni kwamba Chungu hakikuwa na matumizi hivyo alikipa maelekezo kupitia fahamu zake na kumshambulia Anjiu.
Anjiu ni kama alikuwa amejiandaa kwani wakati Chugnu kinaanza kumsogelea alituma shambulizi la moto kwenda kukipiga na alionekana kufanikiwa kumaliza kasi yake ya kumsogelea kwa muda na aliishia kutoa sauti ya chini ya kuzomea na ngurumo kama vile alikuwa amechangayikiwa.
Mara baada ya kupita dhiki ya radi tisa uwezo wa mbinu yake ya Ndege wa Dhahabu na yenyewe ilikuwa imeimarika mno.
Roma alishikwa na huzuni ya ghafla na kujiambia kama angekuwa na uwezo wa kudhibiti radi kama siraha angekuwa ashamaliza pambano hilo muda tu.
Ijapokuwa aliweza kupata mashambulizi matatu ya radi lakini bado hakuwa na uelewa wa namna ya kuidhibiti radi na kuitumia kama siraha na alijua kama mashambulizi ya namna hio yataendelea atashindwa kumlinda Rufi na atashindwa kutoka hapo akiwa hai.
“Daloshoo safu ya elementi tano!!”
Ghafla tu safu tano za mwanga wa vidoti doti zilitokeza katika pande zote na mara baada ya kumfikia Roma zilimzingira na kutengeza umbo la nyota kwa staili ya kumuweka katikati.
Roma alijikuta akishngazwa na jambo lile na kujiuliza ni mbingu gani hio , inakuwaje jini huyu kuwa na safu nyingi za siri namna hio.
Roma kabla hata hajajua kinachoendelea lile umbo la nyota lilianza kutengeneza rangi za ajabu na kuanza kuzunguka kwa spidi kubwa na kuanza kutengeneza kimbunga cha rangi na kumfanya ashindwe kuona kinachoendelea kwa nje..
Roma alishangazwa na jambo lile na kugundua uhatari wa mbinu hio na hakutaka kufanya ujinga na palepale aliita chungu ili kuanza kuanza kunyonya nguvu ile
Kimbunga kile kilipunguza spidi na Roma alitumia nafasi hio kutengeneza moto wa rangi ya Zambarau na kupiga umbo lile la nyota. Na hatimae alifanikiwa kutoka katika kimbunga kile ambacho kilikuwa kimemznigira kwa kumuweka kati.
“Ndege wa Dhahabu , Mkuki wa kiuungu!!!”:
Ilikuwa ni kama vile Anjiu alitegema Roma kitu ambacho atafanya na alikuwa akisubiria nafasi hio na palepale moto wake uligeuka na kutengeneza umbo la mkuki na kutokana na Roma kuchelewa na kutotegemea shambulizi lile hakuwa na muda wa kukwepa na aliishia kumshika Rufi na kugeuka ili kuruhusu mkuki ule kumchoma mgongoni wakati huo mwili wake akiuzingira na nguvu ya kiroho.
“Boom!!!”
Mkuki ule ulilipuka lakini cheche zake ziliweza kupita katika ngao ya Roma na kufikia mwili wake kwa nguvu ya kutosha , kama mwili wa Roma usingekuwa timamu basi palepale angegeuzwa kifusi cha nyama.
“Hubby!!!”
Rufi masikio yake yalikuwa yakigonga kengele na aliishia kutoa kilio kuliita jina la mpenzi wake tu.
Lakini aliishia kutemewa damu nyingi usoni na Roma, Maumivu alioyaskia katika mgongo wake iikuwa ni kama vile viungo vya ndani ya mwili vimegeuzwa mshikaki , ngozi yake iliungua katika kiwango ambacho hakuwa akihisi maumivu tena.
Akili yake ilimpotea kwa sekunde kadhaa , ilikuwa ni kipindi kirefu kidogo kupitia maumivu kama hayo na Roma hakuwa ameyazoea kabisa na palepale alijua kabisa mtu ambaye anaweza kumpatia shambulizi hilo basi anao uwezo wa kumuua pia.
“Duuh bado upo hai tu , hakika mbinu yako ya andiko sio ya kawaida”Jini Anjiu kwa mara yingine alijikuta akionyesha mshangao wake waziwazi.
“Ungeachana na huyo mwanamke pangine ungekuwa na uwezo wa kushindana na mimi lakini nikuambie tu huna uwezo wa kunishinda ukiwa utaendelea kumlinda”
Roma akiwa katika hasira aligeuka kwa spidi akiwa na moto wake wa rangi ya samawati na kumrushia anjiu na Anjiu hakuwa mzembe kwani kwa kupigisha kiganja chake hewani tu moto wake wa ndege wa Dhahabu uliweza kuzimisha shambulizi lile.
“Hata kama umeweza kunyonya nishati ya radi bado hunniwezi , nina mbinu ya moto wa Ndege wa Dhahabu licha y moto wako huo wa kimbingu na wa kiroho haileti tofauti yoyote na mashambulizi yako hayawezi kuwa na madhara kwangu na ninazo mbinu nyingi za kukushinda , ijapokuwa Cauldron uwezo wake ni mkubwa lakini bado uwezo wake ni wa kati , kitendo cha kupitia mapigo ya radi kimeleta mshituko katika ulimwengu wote wa majini na wazee wakubwa watafika hapa muda sio mrefu kujua nini kinaendelea na muda huo huotokuwa na nafasi ya kujiokoa tena nakushauri nipatie andiko la urejesho na mimi kama mkuu wa miliki ya Xia nitakuachia huru wewe na mwanamke wako kuondoka”
Licha ya maumivu ya Roma kupona kwa kasi lakini maneno ya Anjiu yalimshitua kidogo na aliishia kutoa tabasamu na kutoa meno yake ambayo yamechafuka na damu.
“Ushapitia mapigo ya radi lakini bado unahitaji mbinu yangu?”
“Hakuna ambaye anaweza kukataa mbinu nzuri ya mafunzo , tunataka kujua ni kwanini mwili wako ni imara namna hio?”
Ukiachana na uwezo wa Roma kupona haraka kutokana na mbinu ya andiko, majini hao wanajua utimamu wa mwili wa Roma umetokana na nguvu za kijini, wasichokijua ni historia kamili ya Roma.
Roma ni sehemu ya matokeo ya projekti LADO na ndio iliomfanya kuwa na mwili wa namna hio , hata kama hatumii mbinu hio ya andiko virusi ambavyo vipo katika mwili wake vikiamshwa uwezo wake wa kupona unakuwa mkubwa.
“Kama haya yataendelea nafasi yangu ya kushinda itazidi kushuka , leo nilifanya makosa , sikutegemea Anjiu kuwa na hila namna hii , nimekuja hapa kumuokoa Rufi na nilichotaka ni kumlipia kisasi lakini nadhani kwasasa bado mpaka nitakapoweza kudhibiti radi”Aliwaza Roma huku akiwa katika hali ya kimaamuzi ya kutaka kuondoka na kuachana na maswala ya kupambana.
Lakini sasa dakika ambayo alikuwa akijiandaa kukimbia aliweza kuhisi nguvu za aina sita za mbingu na ardhi kubwa zikisogelea eneo hilo kutoka pande zote , ni nguvu za majini ambao wapo katikati mwa levo za maji ya upako na mwishoni.
“Kwanini ndio unataka kuondoka ilihali ndio wazee wetu sita wamekwisha kufika, unadhani unaweza kuondoka kirahisi hivyo?”
Roma uso wake ulizidi kuwa mweusi na Rufi aliishia kumwangalia Roma kwa wasiwasi na alishiia kujilaumu kwa kuwa mzigo kwake na Roma ni kama alishajua Rufi alichokuwa akiwaza na alimwangalia kwa tabasamu.
“Usiwe na wasiwasi nilishakuambia nitakulinda kwa namna yoyote ile”
“Hehe … mnao muda tu wa kuonyesheana mapenzi ?”Aliongea Anjiu kwa kejeli.
Kwa jinsi nguvu za majini wengine wakubwa waliokuwa wakisogea hilo eneo ni kama wanatengeneza duara kwa kila mtu kuwa na uwezo wa kulinda kilomita kadhaa za eneo lake , ilikuwa ni kama vile wanafanya ushirikiao kwa kuhakikisha hakuna kitu kinachowapita.
Kufumba na kufumbua hatimae Roma aliweza kuona sura za wanaume watatu majini wa makamo , wazee wawili na mwanamke mmoja wa makamo.
Mwanamke pamoja na Mzee alievalia joho rangi nyeusi kwa pamoja uwezo wao ilikuwa mwishoni mwa levo ya maji ya kiroho kama ilivyo kwa Anjiu na ilionyesha muda wowote wangeweza kupitia Dhiki ya radi.
Majini wengine wanne wote waalikuwa na uwezo sawa na wa Ajuza Tigola wa miliki ya Kekexi.
Ukubwa wa miliki ya Xia hatimae ulikuwa wazi na Roma alijua ongezeko la hawa majini ni tishio kwake.
Majini wa miliki ya Xia walishia kutoa shangwe za utukufu mara baada ya ujio wa wazee hao wa miliki.
Yaani ukisikia baraza la wazee ambalo ndio uchangua nani awe kiongozi wa miliki basi huundwa na hao majini ambao wote wapo katika levo ya maji ya upako.
Majini wale wote mara baada ya kumwangalia Roma kwa macho yaliojaa utukufu waligeuza sura zao na kuangalia lijichungu ambalo lilikuwa likizunguka hewani kwa maringo na walionyesha mshangao wa waziwazi na palepale waligeuza sura zao na kumwangalia Anjiu.
“Anjiu umefanikiwa kuingia levo ya Dhiki ya radi ya mapigo tisa?”Mzee ambaye alikuwa mwishoni mwa levo ya maji ya upako aliongea.
“Ndio babu nimeweza kupata Epifania muda mfupi uliopita na kuweza kushinda jaribio”
Ilionekana huyo mzee alikuwa ndio babu yake Anjiu , kwa umri wa Anjiu ungeshangaa kuwa na babu lakini majini umri wao ulikuwa ni mkubwa mno kuliko binadamu.
Roma alikumbuka kauli ya jini Sui kwamba ndio huyo mzee ambaye aliweza kuchukua nafasi ya baba yake Laofi kuwa mkuu wa miliki.
Huyo mzee jina lake halisi ni Senji na ndio ambaye alikuwa na mchango mkubwa kwa Anjiu kuwa na nafasi aliokuwa nao wakati huo.
“Siamini kama umeweza kulipita jaribio , nadhani kwasasa hatuna thamani tena”Mwanamke ambaye alikuwa katika muonekano wa ukauzu aliongea.
“Bibi Sena umeniona nikikua na wewe ni msingi wa miliki yetu, nimepata bahati tu na kila kitu nilichokuwa nacho leo hii ni kutokana na maelekezo yenu tokea nikiwa mdogo.”
Ijapokuwa Anjiu hakuwa kijana lakini alijishusha na kuwa kama mtoto mbele ya wazee hao na kauli yake ilimfanya Sena kujisikia vizuri.
“Ni nani huyu mtoto, uwezo wake wa kijini ni mkuu mno na hilo Jungu lake , Usiniambie ndio chungu ambacho tuliweza kusoma tu katika hadithi?”
“Inaonekana ni chungu cha maafa ndio , huyu binadamu anaonekana kuwa mtoto mdogo lakini ameweza kufikia uwezo huo wa nishati za mbingu na ardhi na hebu angalia mwanamke ambaye amembeba anakiwango kikubwa cha nishati ya Yin , mwili mzuri wa kufanyia majaribio ya vidonge, Anjiu hebu tuelezee hii hali?”Aliongea Senji.
Ilikuwa ni haki yao kuwa katika mshangao wa hali ilivyo kwani hawakuwa katika makao makuu ya miliki kwa miaka mingi na hawajui ambacho kilikuwa kikiendelea.
Anjiu mkuu wa miliki alielezea tukio zima kwa kusema Roma ni binadamu mwizi ambaye amevamia miliki yao na kumuua Lao mtumishi na mzee Laofi na kundi la majini wa levo ya maji ya meupe na barafu na hakuishia hapo tu alielezea na kilichotokea miliki ya Kekexil.
Malezo hayo yote yaliwafanya wale wazee kupatwa na hasira ya kutaka kumchuna ngozi Roma.
“Haha… Panas na Xia hatujawahi kukwaruzana , nimekuwa mbali na miliki kwa miaka hamsini hadi sasa lakini miliki yetu imevamiwa na mtoto mdogo tena binadamu , Anjiu hii ndio namna ambavyo unaongoza hii miliki?”Aliongea Senji.
“Huyu mwanaharamu uwezo wake ni wa ajabu, sio tu kwamba mwili wake sio wa kawaida lakini pia anao uwezo wa kutengeneza maji ya kiroho , moto wa kiroho na moto wa bluu siraha ambazo mashambulizi yake ni makubwa mno kuliko za kwetu , sio mwepesi kudili nae”
Baada ya kusikia maelezo hayo wazee hao walijikuta wakishangazwa lakini kwa wakati mmoja tamaa zilianza kujitengeneza katika nyuso zao.
“Imetosha kwa huu ujinga , kamata huyu mtoto na chukua mbinu yake , mlazmishe pia kutueleza namna ambavyo amefanikiwa kujifunza kwa muda mfupi , huyo mwanamke pia chukua na awe ni kifaa rasmi cha majaribio , kulingana na hadithi katika kumbukumbu zetu Chungu cha Maafa ndio kilitumika kumfungia mnyama wa machafuzi aliewahi kuwepo , ni Dhana ya kikale ya mababbu zetu , hazina ambayo inazidi Dhana zote , tukiwa nayo haitokuwa ngumu kuunganisha miliki zote na kuwa chini yetu kama Anjiu utatumia uwezo wako kuiendesha”Aliongea moja wapo ya wale wazee.
“Umeongea pointi, angalau kwa wakati huu tumepata kitu cha thamani”Aliongea Sena kwa tabasamu la furaha.
“Huyu mtoto uwezo wake sio wa kuchukulia poa lakini pia kushindana na chungu cha maafa sio rahisi , kwanini tusishambulie wote kwa pamoja na kumfanya asiwe na nguvu?”
Wale wazee wote waliangaliana na kisha wakatingishiana vichwa kuonyesha ishara ya makubaliano na ilionekana washaamua na kuona hio ndio mbinu rahisi ya kumdhibiti Roma.
Wakati huo walikuwa wakiendeshwa na tamaa, kwanza kupata mbinu ya Roma ya mafunzo , pili kumkamata Rufi ili kuwa kifaa cha majaribio na tatu kubwa kuliko yote kupata Dhana ya kilijendi ya Chungu au Sufuria la maafa.











SEHEMU YA 726.
Roma mara baada ya kusikiliza maneno yao aliishia kushikwa na hasira na aliona kabisa hao wazee wa kijini hawakuwa kabisa na aibu, yaani licha ya kuwa na umri zaidi ya miaka elfu mbili kama utawaunanisha wote lakini bado wanapanga kushambuliana na yeye ambae ana miaka ishirini kupanda.
Ukweli ni kwamba kwasababu ya wazee hao kuishi muda mrefu , hawakujali kabisa maneno ya wengine , kwao aibu sio kitu na wakati huo malengo yao ni kupata kitu cha thamani kilichokuwa mbele yao.
“Mimi na Sena tutashambulia , nyie wanne zungukeni hilo Jungu la maafa na muanze utarafibu wa kulikamata , Anjiu wewe ungana na sisi tumalize hili swala haraka iwezekanavyo”Aliongea Senji ki amri.
“Umeeleweka”
Sena alikuwa tayari katika mkao wa kumshambulia Roma na alitoa nguvu kubwa ya kijini ya andiko la Roshinisutra.
“Joka la sanaa ya wino - Jozi Majoka katika dansi moja!!”
Palepale ghafla tu Kizingia(vortex) cheusi kilianza kumtoka , ilikuwa ni kitu kinachofanana na wiuo wa karamu kama maji maji mazito hivi ambayo yamebeba Aura ambayo sio ya kawaida . ni aura ambayo inafanana nae kabisa.
Sekunde tu wino ule mwingi uligeuka na kuwa nyoka mfano wa Cobra na kuanza kucheza cheza.
Yaani kilichokuwa kikionekana ni kama wale watu wanaocheza na mijoka ikiwa imewazingira mwili, sasa jini Sena alikuwa amezingirwa na majoka mawili meusi kama wino yaliokuwa yamekaa kulia na kushoto yakichezesha vichwa vyao , yalikuwa makubwa mno na ya kuogofya.
Roma hakutaka kuzembea na palepale aligeuza nguvu zake za nishati ya mbingu na ardhi na kuwa moto wa bluu unaofanana na nyoka pia wa rangi ya bluu ili kupambana na zile nyoka za wino.
Sena alikuwa mwepesi mno na palepale yale majoka yake yaliongezeka urefu na kufyatuka kuelekea kwa Roma lakini Roma na yeye alifyatua nyoka zake ambazo zilikuwa katika moto wa bluu na kwenda kupambana.
Kitendo cha nyoka wale wa bluu kugusana na wale wa wino palepale walisambaratishwa na nguvu zao zilizobakia zilimsogelea Sena kwa kasi lakini alikuwa mwepesi mno kwani palepale alitoaDhana iliokuwa ikifanana na mkuki lakini ambayo imemgawanyo katikati kama vile ni Uma ya Tuni(Tuning fork).
“Onja Dhana yangu ya ‘Kilio pepo’”
Jini Sena alikuwa tayari ashafanya miujiza yake na kuifyatua siraha yake ya Kilio cha pepo na kutengeneza wimbi kali la nguvu za kijini.
Roma palepale alizuia shambulizi lile na nguvu zake za kijini lakini shambulizi lile lilikuwa limeambatana na sauti kali za kuchafua akili , ilikuwa ni sauti kali mno za vilio.
“Arghh…!!”
Rufi aliweza kusikia sauti zile pia na alijikuta akitoa yowe na damu kuanza kumtoka midomoni.
Muonekano huo ulimfanya Roma kupatwa na ukichaa , hio siraha ya ‘Kilio Pepo ‘ ilikuwa ni shambulizi la sauti(Sonic attack) ukijumlisha na aura yake iliendana na jina lake.
Roma alijua kama ni hivyo asingeweza kuizuia na alijua ni vizuri kuikwepa kwani kama atakumbana nayo moja kwa moja basi inaweza kuharibu masikio ya Rufi.
Lakini sasa kabla hata hajachukua maamuzi nguvu kubwa ya kijini ilimsogelea kwa kasi na kwa mara moja tu aliweza kuona mamia ya nguvu za kijini ambazo zipo katika rangi , ilikuwa ni kama vile ni nyota katika mstari kutoka angani zinamdondokea.
“Mkondo Nyota …Anguko la ngurumo!!!”
Ulikuwa ni uchawi uliotoka kwa Senji huku macho yake yalikuwa yakiwaka waka kama vile yanaungua na moto na kitendo kile cha kutingisha mkono tu vitu ambvyo vilikuwa katika umbo la nyora vilianza kumdondokea Roma
Roma aliishia kutoa mlio wa sauti huku akigeuza nguvu yake ya kijini na kuwa moto wa Zambarau na kuzingira mwili wake na palepale akituma mashambulizi kushambulia zile nyota na zilisambaratishwa palepale na ni muda huo huo aliita Jungu lake na kwenda kumvaa Sena ambaye alikuwa karibu yake.,
“Unatoa wapi ujeuri huo?”
Sena alishikwa na hasira na ile siraha yake ya Kilio pepo ilianza kuzunguka na kutengeneza mchoro wa kuvutia macho na palepale alianza kuongea kwa sauti kubwa kama wale wachungaji wanaokemea pepo.
“Joka sanaa ya wino –Wino mzito!!!”
Palepale ulifyatuka ujiuji wa wino kama kamba na kwenda kukifunga kile chungu na kuanza kukivutia mbali ili kukipunguza nguvu na alitumia fursa hio kujiondoa katika kani mvutano wake.
Hakuishia kujitoa tu bali aliendelea kuipigisha hewani ile siraha yake na kufyatua mawimbi ya sauti na kumfanya Roma kuyakwepa haraka, ijapokuwa alikuwa na uwezo wa kupambana nayo lakini alifanya hivyo ili kuepusha madhara kwa Rufi,
Anjiu mara baada ya kuona Pambano ndio linaelekea ukingoni kutokana na Roma kuzidiwa na mashambulizi alitoa tabasamu la kejeli na palepale aligeuka na kuwa kama jua.
“Ndege wa Dhahabu wa miguu mitatu , Kusanyiko la ndege elfu moja”
Makundi ya ndege katika mamia mamia yalianza kumsogelea Roma kwa kasi lakini Roma hakuwa akidili na yeye tu , hali ilikuwa inazidi kumuia vigumu zaidi na zaidi.
Huku alikuwa akipambana na mkondo wa nyota , huku anapambana na majoka wino na sauti na kumfanya akose muda wa kukipa chungu maagizo.
Wakati huo sasa Roma ngao yake ilianza kukosa nguvu na ilionekana muda wowote ingeangushwa na mashambulizi ya ndege wale wa moto.
Ilikuwa ni vita ya pata shika kwani majini watatu wa nguvu za juu walikuwa wakimshambulia na kwa mtu yoyote mwenye akili timamu lazima angeona Roma hachomoki kwa namna yoyote ile.
Majini wa miliki hio waliokuwa wakiangalia mapambano hayo kwa mbali walikuwa katika furaha lakini kwa namna moja walimkubali Roma kutokana na namna ambavyo alikuwa akijilinda na mashambulizi bila kusahahu alikuwa na mwanamke amemshikilia na mkono mmoja.
Xiao ambaye alikuwa akiangalia aliishia kushika gauni ake kwa nguvu kama anataka kulichana vile huku michirizi ya machozi ikiwa imepamba uso wake , alionekana alikuwa akimlilia Roma lakini kwa wakati huo hakuwa na cha kufanya kabisa.
“Kwanini nipo hivi , kwanini naumia , si alitaka kuniua , sielewei kadri anavyoshambuliwa naumia mimi?”
Mrembo huyo nusu jini alikuwa katika hali ya maswali mazito akipambana na hisia zake za mapenzi kwenda kwa mwamba Hades.
Roma sasa alianza kuona nguvu zake za mbingu na ardhi zinaenda kombo kwani upande maadui ulikuwa na nguvu kubwa ambazo ni zaidi ya za kwake.
Ingekuwa sio kwa mwili wake kuwa na uwezo usiokuwa wa kawaida basi angekufa.
Haikuwa habari nzuri kwa Roma hio, ijapokuwa alikuwa akipigaina nao kwa maji ya kiroho na moto wa bluu lakini licha ya kutumia Chungu chake matokeo hayakuwa mazuri.
Na alijua akiendelea hivyo anaweza kufanya kosa na kupoteza uwezo wake wa kijini wote au kuishiwa nguvu.
Kilichomsumbua Roma sana wakait huo alijua majini hao bado hawakutumia hata nusu yote ya uwezo wao na hata kama asingekuwa amemshikilia Rufi na kumlinda wakitumia asilimia zote za uwezo wao basi hatokuwa na nafasi tena ya kuwa hai.
“Napaswa kufanya nini?”
Swali liliibuka katika kichwa chake na palepale Roma alikiona kifo chake kikikaribia.
******
Wakati huo huo upande mwingine kusini magharibi mwa miliki hio hio ya Xia alionekana Mkuu wa miliki ya Panas yaani Gefu akiwa amesimama juu ya msitu maili mia moja mbali na pambano linapoendelea.
Alikuwa na muonekano usioelezeka na alikuwa kimya akionekana kuwa katika subira ya jambo flani.
Hakuwa peke yake , nyuma yake walikuwa ni majini wazee Chotara ambao wamevalia kanzu wote kimya wakiwa katika hali ya subira pia.
Majini hao wawili walikuwa ni wanaume na wawili walikuwa ni wanawake wakitengeneza jumla ya majini wanne na mkuu huyo alikuwa ni wa tano.
Ukiachana na majini hao ambao wapo eneo moja nusu kilomita kutoka waliposimama kulikuwa na majini wengine makundi kwa makundi ambao wote wapo katika levo ya maji ya barafu na meupe wakiwa katika hali ya wasiwasi.
Yaani walionekana kama vile wapo katika hali ya tahadhari ya kuingia vitani muda wowote.
Dakika chache mbele alionekana jini ambaye yupo katika levo ya maji meupe akipaa kuwasogelea kutoka chini kuja juu na aliinamisha kichwa mbele ya Mkuu huyo mara baada ya kumkaribia.
Jini huyo alikuwa ni shushu ambaye alikuwa ameingizwa katika miliki ya Xia kwa ajili ya kutoa taarifa ya kila kinachoendelea.
Kutokana na wingi wa majini ambao walikuwa na ruhusa ya kufanya watakvyo katika miliki ya Xia ingekuwa ngumu kukosekana kwa mashushu.
“Kwanini umecheleawa , hali ipoje , nini kimetokea?”Aliuliza Gefu,
“Niwie radhi namba moja , nimechelewa kwasababu hali ilivyo ni ya kushitusha sana , Anjiu ameweza kupita Dhiki ya radi”Aliongea yule shushu katika sauti iliojaa kitetemeshi.
Sekunde ambayo maneno hayo yanatoka mdomoni majini wote waliosikia walijikuta wakishikwa na sura mpauko.
“Roma hali yake ikoje?”
“Hali yake haionekani kuwa nzuri , sidhani kama atadumu kwa muda mrefu , Wazee wote sita wa miliki ya Xia wamefika na kuna uwepo wa Sena jini maarufu wa miaka ile pamoja na Senji mkuu wa miliki aliepita , wazee wngine wote ni wataalamu ambao walipata umaarufu miaka mia moja iliopita ,Roma kamshindwa Anjiu ataweza kupambana nao wote saba? , ijapokuwa anajitahidi lakini ni swala la muda tu kabla hajauliwa au kukamatwa”Aliongea na kumfanya Gefu kuonyesha wasiwasi kiasi lakini alijituliza.
“Nimekuelewa rudi Xia na hakikisha hukamatwi”
“Sawa”
Dakika ileile yule shushu jini aliondoka katika hilo eneo na Gefu aliinua uso wake juu angani akionekana kufikiria jambo.
“Wazee radhi zangu kwenu , inaonekana wote mmekuja hapa bure tu”
“Hatuja poteza muda wetu kuja hapa , kwasababu tushajua mafanikio ya Anjiu hili linamaanisha hata sisi pia tunayo nafasi , lakini elewa baadae nguvu ya miliki ya Xia itakuwa kubwa zaidi hivyo unapaswa kuwa nao makini”
“Sio mbaya , licha ya mipango yetu mikubwa inayoendelea katika ulimwengu wa binadamu lakini pia nguvu za nishati ya mbingu na ardhi ni muhimu pia ili kuimarisha eneo letu , Gefu unapaswa kujifunza kutoka kwa Rozu , tunafikiri huyu msichana ndio tumaini letu kubwa kwasasa katika vijana ambao wataweza kushindana na Anjiu”
“Asante kwa ukumbusho wenu wazee wangu , sitosahau busara zenu”
Wazee hao wanne walinzi wakuu wa miliki ya Panas hawakuongea neno lingine , mpango wao ulikuwa ni kumsaidia Roma lakini mara baada ya kusikia Anjiu ameweza kuvuka Dhiki ya radi uwezo huo wa kumsaidia hamna na Roma anakwenda kufa.,
Hivyo hawakutaka kusikia neno lingine kutoka kwa Gefu hivyo waliamua kuondoka katika spidi ya kupepesa macho na kutokomea.
“Kwahio tunaachana na misheni yetu”
Jini ambaye alikuwa katika levo ya maji ya barafu alisogea na kuongea na Gefu.
“Tukiendelea ni sawa na kujitoa kafara tu , kwanini tuhatarishe maisha yetu kwa kutaka kumsaidiia Roma? , ni muda wa kurudi Panas”
Baada ya kauli hio Gefu aliongoza njia na kupaa kuelekea mbali kurudi katika miliki yao.
Ilionekana walikuwa hapo kwa ajili ya kumpa sapoti Roma ili awapatie mbinu ya Andiko kutokana na msaada wao lakini hatari waliiona hivyo waliamua kuufyata mkia na kukimbia.









SEHEMU YA 727.
Roma akiwa katika wasiwasi wa kupotea maisha akiwa na Rufi mawazo yalikataa kabisa kushindwa mara baada ya kumkumbuka Lanlana na wanawake wake wanaomsubiri nyumbani.
Licha ya ukinzani wake katika kuzuia mashambulizi lakini alikuwa akipoteza nguvu sana katika kukusanya nishati ya mbingu na ardhi.
Roma alikuwa akisikia mapigo yake ya moyo na pumzi wake lakini kwa wakati mmoja aliweza kuhisi hali ya Rufi imekuwa dhaifu sana kutokana na mashambulizi ya sauti.
Chungu kilijitahidi katika kushambulia na kuwalinda lakini haikutosha kabisa kwani maadui walikuwa wengi na Roma aliishia kuimarisha uzio wake tu bila kufanya shambulizi..
Licha ya kwamba Cauldon ilikuwa na uwezo lakini ilikuwa ni swala la muda tu kushindwa, wakati huo mashambulizi ya ndege wa moto , Majoka ya wino na Mkondo wa nyota vilimfanya ashindwe hata kuona hata wale majini walikuwa wakifanya nini wala kupanga.
Yaani ki ufupi ni kwamba Roma alikuwa amezingirwa pande zote na alikuwa ni kama vile amefunikwa na mashabulizi na hakuwa akishambulia bali alikuwa akijilinda tu kama vile anasubiri mtu kuja kumuokoa.
Lakini sasa akiwa hajui ni kipi anapaswa afanye ufahamu mwingine uliibuka katika akili yake na kuanza kuongea na ufahamu wake, ilikuwa ni kama vile yupo ndotoni bila ya kufumba macho.
“Heheee…!!!”
Ilikuwa ni sauti ambayo Roma alikuwa akiitambua , sauti ambayo ilikuwa katika hali ya kuchokoza kama vile inamcheka kwa kile anachopita.
Jambo lile lilimshangaza Roma , uwezo wake wa kiuungu palepale ulisisimka kwa dakika na ndani ya akili yake aliishia kutamka maneno’chaos’ yaani Roho ya mnyama wa maafa.
Katika ufahamu wake Roma kama vile anaota hatimae aliweza kuona sura yake iliokuwa ikimwangalia kwa muonekano wa kichokozi.
“Ni muda mrefu hatujaonana Dogo”Roho ya mnyama iliokuwa katika sura ya Roma iliongea kwa dharau.
“Ina,,,inawezekana..!!” Roma aliishia kuonyesha mshangao huku bila ya kujielewa akiendelea kuzuia mashambulizi katika uhalisia.
“Naona unashangaa na kujiuliza kwanini bado nipo hai kwenye ufahamu wako … hehe ulidhani ulinizimisha kwa kujimezesha lile lijikifaa la Kibuddha. Hakika wewe ni binadamu kilaza, Mimi ndio Mnyama wa Kiuungu, mkuu wa Enzi na Enzi nisiekufa niliezaliwa kabla hata ya uwepo wa majini na binadamu , hicho mlichokiita moyo wa kibuddha ni kakifaa kakipuuzi tu kalikotengenezwa na bindamu kichaa wa karne zile , binadamu ambaye naweza kummeza hata akiungana na wenzake mia moja, halafu eti umejikaza mwenyewe na kujimezesha bila hata ya kujishtukia”Mnyama wa kimaafa alikuwa akiongea na ufahamu wa Roma kwa vichambo.
Roma palepale alijua nini kinachoendelea na alijikuta akiwa kwenye hamani.
“Ulifanya makusudi sio?”
“Hahaa… umechelewa kugundua mpango wangu , kama nisingejifanyisha kumalizwa na wewe nisingepata fursa ya kuendelea kumeza majini na kurudisha uwezo wangu kimya kimya kwasababu ulikataa knnipatia uwezo wako”
Roma alijikuta akijidharau kwa ujinga wake sio tu kwamba alidanganywa na Anjiu lakini hata roho ya mnyama imemdanganya na kuingia mtegoni.
Chaos ni Jini mharibifu aliekuwa katika umbo la mnyama ambaye aliwahi kuwepo na mara baada ya kuuliwa roho yake na nafsi vilifungwa katika Cauldron na akaweza kuishi kwa maeflu au mamilioni ya miaka, hivyo licha ya kuwa katika umbo la mnyama uwezo wake wa akili ni mkubwa sana kuliko wa binadamu.
Ni sawa ufanananishe majini Joka na Chaos wote ni majini ambao maumbo yao ni ya mnyama lakini fahamu zao ni kubwa na zenye akili.
Sasa mara baada ya kuona Roma yupo hatarini ndio roho hio ikajitokeza ndani ya Roma.
Sasa hapa unaweza ukashangaa lakini ukweli ni kwamba Chungu ni Chungu na Roho ni roho , kitendo cha Roma kumiliki Chungu inamaana alimiliki Roho sasa mara baada ya kumeza ule moyo wa Kibudha Roma aliamini ile nguvu ya kiroho ameweza kuidhibiti na kuishikilia katika Chungu lakini haikuwa hivyo Roho hio ilijifanyisha kuwa chini ya Roma na kuendelea kujifanyisha kuwa ndani ya Chungu ili kuendelea kumeza majini kujijengea uwezo kimya kimya.
“Kama ni hivyo kwanini ndio umejitokeza sasa hivi?”
“Hivi unafikiri unaweza kuidhibiti hii hali ya hatari uliopo kama nisingejitokeza? , ungekuwa na uwezo wa kudhibiti Radi ungekipa nguvu kubwa Cauldron na kuweza kumeza mashambulizi yao lakini kwasasa uwezo wako ni wa chini sana na hutoweza kuishi kama utaendelea”
“Siamini , huna uwezo wa kushambulia kwasababu ya uwezo wangu mdogo au kwasababu unafanya yote haya makusudi , hukuonyesha kujali mara baada ya kumeza radi na kila kinachoendelea lazima ni mpango wako”
“Huna haja ya kukasirika dogo , kwangu wewe ni kama kajimdoli tu nisingejisumbua hata kujiileta kwako kama sio mwili wako imara ambao unanifaa sana , ndio nikiamua kupambana mimi mwenyewe mambo sijui ya radi na upuuzi mwingine haviwezi kunitisha , ninao uwezo wa kumeza kila aina ya radi lakini kwanini nikusaidie kama mimi mwenyewe sifaidiki, hata hivyo nimekusaidia katika vingi mpaka sasa hivi?”
“Hujanisaidia kwa chochote unachofanya ni kutimiza mipango yako ya baadae tu kwa kunitumia”Ufahamu wa Roma uliongea.
“Hahaha… ndio unatakaje sasa kama nakutumi ,kila sekunde ambayo nimemeza na kutafuna majini au kusharabu nishati ya radi nakugawia kiasi cha nguvu hio ili kukufanya uwezo wako uongezeke na mwili wako pia kuimarika . ingawa nafanya haya yote ili kuhakikisha mwili wako unakuwa katika hali nzuri kwa ajili ya kuutumia baadae lakini huwezi kukataa ukweli kwamba nilikusaidia sana”
Ukichaa ulianza kumshika Roma palepale , ilikuwa ni kama vile yeye analelewa na roho hio ya mnyama kwasababu tu ilikuwa ikihitaji kutumia mwili wake.
Kitendo cha ufahamu wake kushikiliwa ilimfanya Roma kupandwa na Jazba na ukichaa kwa wakati mmoja lakini roho ya mnyama haikujisumbua na ukinzani wa Roma.
“Ushauri wangu kwako ni kupunguza jazba, kama unakili unapaswa kuelewa huna uwezo wa kushindana na hawa majini , kama unatamani kuondoka hapa pamoja na mchumba wako bila madhara niazimishe mwili wako kwa muda nikusaidie”
Roma aliishia kuwa katika bumbuwazi , ijapokuwa katika uhalisia akili yake ilikuwa ikifanya kazi lakini upande mwingine alikuwa akijibishana na roho hio katika akili.
Roma alimwangalia Rufi namna ambavyo midomo yake ilivyopauka na alijihisi moyo wake kuumia.
“Hubby unaendeleaje…Koho,,,koho…”Rufi alitaka kujua hali ya Roma lakini aliishia kukohoa na kutoa damu nyingi mdomoni ikionyesha Dhahiri alikuwa amepata majeraha ya ndani.
Maongezi ya Roma na roho ya mnyama hakuna jini yoyote ambaye alikuwa akijua wala kuhisi.
Dakika hio Roma alijisi maumivu katika moyo wake , ilikuwa ni kama vile moyo wake unapasuka.
“Ndio kama nitaendelea na huu ukiburi wangu Rufi atafia mikononi mwangu , hata kama hatokufa atapitia mateso makali mno pia hakuna namna hawa majini wakawaacha na wanawake wangu waliopo nyumbani kuishi kwa amani”Roma aliwaza.
Roho ya mnyama ni kama ilikuwa ikipiga chabo Roma anafikiria nini na palepale ilipigilia msumari katika ushawishi wake.
“Zingatia watu wako unaotaka kuwalinda lakini pia jali juhudi zao kwako , unataka kuona maisha yao yakiamuliwa na wengine , kama utaniacha nitumie mwili wako naapia kwa damu ya ukuu wangu wa kitakatifu wa wanyama wote nitakulipa kwa kuwalinda wanawake wako wote na familia yako kwa ujumla , nitammeza kila adui ambaye atataka kuwadhuru … vilevile hawa majini hapa nitawafyeka wote bila kuacha ushahidi wa mifupa yao nyuma , unaonaje ofa yangu?”
Roma hakutaka kuthubutu kuamini maneno yake , kama ilikuwa ikijua kutii ahadi isingeitwa Roho ya mnyama wa maafa.
Roho hio haikuwa na haraka kutaka majibu kutoka kwa Roma na iliishia kutoa tabasamu katika sura ya Roma katika hali ya utulivu kabisa.
Ijapokuwa ilikuwa na uwezo wa kushindana na ufahamu wa Roma lakini ingekupambana na ukinzani na kushindwa kutimiza mpango wake hivyo moja kwa moja ilitumia kanuni ya ushawishi ya kutokuwa na papara ili Roma kujileta mwenyewe.
Roma na yeye alikuwa akifurukuta na kushindwa kuchukua maamuzi ya haraka juu ya hali aliokuwa nayo.
Upande wa majjini hao wa miliki waliokuwa wakimshambulia walikuwa wakikosa subira na walikuwa wakipanga kutumia uwezo wao wote ku,maliza Roma haraka iwezekanayo.
“Mhmh..!! Hiki Chungu cha maafa hakika kinaendana na sifa zake , ni Dhana ipitayo Dhana zote , sijaamini kitakuwa na uwezo wa kuhimili mashambulizi muda mrefu hivi ?”Aliongea Sena huku akionyesha hali ya kuchanganyikiwa kidogo.
“Nafikiri ashafikia mwishoni mwa uwezo wake na hana njia ya kujiokoa tena , mnaonaje sisi wote saba tukishambulia kwa shambulizi moja la wakati mmoja?”Alishauri Senji,
Baada ya kuthibitisha Roma hakuwa na uwezo wa kujiokoa tena wote walikusanya nguvu zao za kiiijini katika kiwango cha juu kabisa.
Anjiu hakuwa na maoni juu ya pendekezo hilo ijapokuwa alijua wakipiga shambulizi moja watamuua Roma moja kwa moja na kukosa mbinu ya andiko lakini hakutaka kupinga.
Ghafla tu Roma aliweza kuhisi ongezeko kubwa la nguvu za kijini ambazo zinajiandaa kumvamia kwa nje , Roma palepale alijuliza majini hao ndio kwamba wana usongo wa kumuua kiasi hicho?.
“Sina jinsi napaswa kucheza kamari ya pata potea”Aliongea Roma na kisha alimwangalia Rufi aliekuwa akitia huruma kwenye mikono yake.
“Rufi sina jinsi nitabetia roho ya mnyama wa maafa , I am sorry”
Rufi alijikuta akikosa neno baada ya kusikia maneno yake na dakika ileile mara baada ya kuhisi nguvu ya ajabu kumzingira Roma alishajua anamaanisha nini.
“Hubby .. umeamua ..”Rufi alishindwa hata kumalizia sentensi yake na machozi palepale yaliupamba uso wake baada ya kujua Roma tayari amekwisha kufanya maamuzi na kuruhusu roho ya mnyama kutawala mwili wake.
Hata kauli yake aliotoa haikuweza kusikiwa tena na Roma kwani alishapotea kwa wakati huo na mmiliki wa mwili wake ni Chaos.
Hatimae Roho ya mnyama Chaos ilifurahi mara baada ya kupata hatimiliki ya mwili wa Roma na ilionekana kweli ilikuwa ikijikusanyia nguvu za kijini kwa kipindi kirefu kimya kimya kwani mara baada ya umiliki wa mwili huo uwezo wake ulipaa kileleni kwa sekunde tu.
Ingawa uwezo wake haukuwa mkubwa kama ilivyokuwa hapo mwanzo lakini majini hayo yasingekuwa na uwezo wa kushinda mbele yake, kumiliki mwili wa Roma ilikuwa ni hatua nzuri sana kwake ya kurudisha utukufu wake uliopotea.
Upande wa majini kila mmoja alikuwa amekusanya nguvu kubwa kwa ajili ya mashambulizi na kutokana na wote kuwa profesheno kwenye mbinu yao ya miliki ya Roshinisutra , waliamini mashambulizi hayo Roma hawezi kupona hata iweje kwani ingekuwa ni mara mbili ya bomu la nyuklia.
“Ni muda wa kumuua kwa shambulizi moja sasa”Aliongea kwa nguvu Senji na ndani ya sekunde iliofata nguvu zao za kijini ilikuwa ni kama Tsunami ambayo inaelekea kumfunika Roma.
“BOOM!!!
Mwanga ulitokana na mlipuko huo ulikuwa mkubwa kiasi cha kufanya miliki yote ya Xia kuwa angavu kama vile ni wakati wa mchana.
Mtikisiko wa muunganisho wa mshambulizi hayo ya majini saba wa levo za juu ni kama vile unataka kudondosha ulimwengu wote wa kijini.
Wakati huo walikuwa washajua Roma yupo mwishoni mwa uwezo wake na shambulizi lao hilo ni hukumu yake ya kifo kwa kujifanya mjuaji kuja ulimwengu wa kijini na kuwachokoza, katika akili zao walikua wakiamini kabisa hapo hachomoki.
Mlipuko na mwanga mpaka unakuja kuisha na kupotea ile sehemu ya mlipuko Roma na Rufi hawakuoekana tena , yaani palikuwa peupe .
Wakati huo huo jungu la maafa lilikuwa likizunguka juu angani na nguvu yake ilionekana kufifia.
“Its over”(Imekwisha).”Aliongea Sena.
“Ilipaswa kuisha muda mrefu”Alijibu Senji.
Majini wa miliki hio waliokuwa wakiangalia kwa mbali walipiga yowe la shangwe mara baada ya kuona mafanikio hayo na ile hali ya kujiamini ilikuwa imerudi.
Lakini sasa dakika ileile Anjiu sura yake ilijikunja huku macho yake yakisinyaa na palepale aligeuza kichwa chake na kuangalia angani upande wa mbali kama vile anaangalia jua.
“Imewe,,, imewezakana vipi !!!”
Mshituko wake uliwashutia na wale wazee wengine na wote kwa pamoja waliangalia juu angani na kila mmoja alijikuta akishikwa na butwaa kiasi cha kushindwa kuvuta hewa.
Kulikuwa na kivuli kilichokuwa kimesimama mamia ya kilomita kutoka kilipo chungu cha maafa.
Upepo wa baridi ulikuwa ukimpuliza Roma ambaye alikuwa ameshikilia Rufi kwa mkono mmoja huku mwingine ukiparaza paraza mashavu yake kimahaba.
Kiini cha macho ya Roma kilikuwa ni rangi nyekundu tii na muonekano wake licha ya umbo kuwa la kawaida lakini hakuonyesha ishara yoyote ya kuwa na ubinadamu ndani yake.
Alionekana kuzingirwa na ukungu uliokuwa ukimtoka katika mwili wake kama vile ni mvuke ambao ulitoa msisimko ambao ni kuogofya na wa kikale.
“Haiwezekani… amewezaje kuokoka , hata kujua hatujui lakini ameweza kukwepa shambulizi letu , kivipi nauliza!!?”Sena alikuwa katika bumbuwazi na hamaki ya karne.
Katika Anga mtu ambaye aliitwa ‘Roma Ramoni’ alishusha macho yake ya rangi ya balbu nyekundu na kuwaangalia watu hao kwa tabasamu la uovu , huku akilamba lipsi zake akionyesha ishara kamili ya tamaa kama Simba ambaye ameona swala.
Roma huyu hakuwa katika umbo la mnyama kwasababu virusi ambavo walikuwa wakifanya kazi ya kupanua mwili wake wamelala kutokana na nguvu ya kijini lakini wale waliohusika kumtengeneza, yaani Zeros kwa kumwangalia Roma wangeweza kujua alikuwa katika kiwango cha juu mno cha uhatari kutokana na macho yake tu.
 
Shukhran mkuu ubarikiwe
 
Ok
 
Totally good
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…