Manyanza
JF-Expert Member
- Nov 4, 2010
- 16,464
- 35,629
Tupo tunasiikiliziakeshoo
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Tupo tunasiikiliziakeshoo
Toa location kabisa ya shughuli ya maziko, chachandu na tooth pick zipo standby hahaha😅😅aaaisee nimesoma Kwa presha sana hivi vipande.
abubakari safari hii tunamzika.
ratiba nzima anayo ROMA.Toa location kabisa ya shughuli ya maziko, chachandu na tooth pick zipo standby hahaha[emoji28][emoji28]
KHAAAAA HUU MZGO JMNSEHEMU YA 126
“Chino karibu sana”Aliongea Bi Wema kwa uchangamfu huku akimkaribisha Mzee Chino ambaye alionyesha pia kumfahamu Bi Wema.
“Asante sana Wema , ni muda sasa tokea mara ya mwisho tuonane”
“Ni kweli nadhani ni Zaidi ya miaka mitano sasa”Aliongea Bi Wema huku akiwa na tabasamu , lakini kwa Roma na Edna walikuwa kwenye hali ya mshangao, hawakuelewa kwanini yuke muhudumu wa mgahawa kutoka Upepo Beach Gaeden yupo nyumbani kwao akijitambulisha kama mwanasheria.
“Mr Roma , Miss Edna tunaonanatena , habari za toka jana?”.
“Salama Mzee Chino karibu sana”Alijibu Edna huku akimpatia mkono na Mzee Chino aliekuwa ameshikilia mkoba wake , alikaa chini kwenye masofa hayo.
“Kumbe Chino umeonana na Edna pamoja na Roma ?”
“Yeah nimeshaonana nao jana tu, walikuja kwenye mgahawa wangu”Aliongea Mzee Chino na kumfanya Roma atabasamu.
“Mzee Chino , Unaonekana kuwa na sura nyingi sana,najiuliza baada ya leo utanishangaza kwenye jambo lipi lingine”Aliongea Roma na kumfanya mzee huyu kutabasamu.
“Mr Roma nadhani na mimi pia napaswa kuzungumza hayo maneno”Aliongea.
“Miss Edna nadhani leo ni mara yetu ya pili kuonana, jana ulinifahamu kama mhudumu , lakini leo hii nipo hapa kama mwanasheria wa bibi yako Marium na nadhani mpaka sasa Wema ashakuambia baadhi ya mambo kutokana na kile kinachosambaa mtandaoni , si ndio?”Edna alitingisha kichwa.
“Okey basi nadhani kazi yangu itakuwa rahisi sana kwa siku ya leo”Aliongea huku akifungua mkoba wake uliokuwa pembeni na kutoa bahasha kubwa aina ya Khaki na kutoa karatasi kadhaa na kuziweka mkononi na kisha akarudisha ile bahasha kwenye sofa.
“Hii ni karatasi inayonitambulisha kama mwanasheria Binafsi wa Bibi yako Marium Adebayo”Aliongea na kumpatia Edna ambaye alipitisha macho yake haraka haraka na kuona kweli kulikuwa na sahihi ya mkataba wa kisheria kati ya Bibi yake na Mzee Chino.
“Hii nyingine ni mkataba ambao niliusiimamia miaka ishirini na tano nyuma , mkataba uliofanyika kati ya mama yako ,Adebayo na Bibi yako”Aliongea Mzee Chino na kumfanya Edna auchukue na kisha kuangalia na alijikuta macho yakimtoka mrembo huyu na Roma baada ya kuona Edna kashangaa , alimpokonya na kuangalia ni nini kilichoandikwa kwenye mkataba huo.
Na Roma aliweza kuona kipengele ambacho kilikuwa kikisomeka kwamba , Marium anakiri Edna kutokuwa mtoto halali wa Mzee Adebayo na Pia Raheli anakiri kwa Edna kutokuwa mtoto wa kuzaliwa wa Mzee Adebayo.
Kipengele Cha pili, Edna licha ya kutokuwa mtoto wa damu wa Mzee Adebayo, kupitia mkataba huu unamfanya Edna kuwa mtoto wa pekee wa familia ya Adebayo kutokana na makubaliano kati ya Raheli na Adebayo huku Marium akiwa Shahidi.
Yaani kwa maneno marahisi ni kwamba mkataba huo ulikuwa umesainiwa na watu watatu , Adebayo , Rahel , pamoja na Marium kama shahidi na huo mkataba ulikuwa ukimlinda Edna kama mwanafamilia halali wa kipekee wa familia ya Adebayo , lakini pia mkataba huo ulikuwa ukimzuia Edna kwa hali yoyote ile kutobadilisha jina lake , ama kutomkubali baba yake mzazi kwa namna yoyote ile na kama tu atakubali kuungana na baba yake mzazi basi atakosa haki ya umiliki wa mali zote za familia ya Adebayo.
“Miss Edna , mpaka hapo nadhani ushaelewa kwanini nimekuja siku hiii ya leo, kama utaangalia sehemu ya huo mkataba kuna sehemu haikusainiwa na hio sehemu inakuhusu wewe, na mimi kama mwanasheria wa Marium nitasimamia maamuzi yako ambayo utakwenda kufanya siku hii ya leo”Aliongea Mzee huyu kwa kujiamini na kumwangalia Edna ambaye alikuwa akisoma tena mkataba huo baada ya kuchukua kutoka kwenye mikono ya Roma.
“Kwa Jinsi nilivyoona hapa inaonesha kama nikisaini sitokuwa na haki ya kumtambua baba yangu na nitabakia kuwa mwanafamilia ya Adebayo?”
“Hakika Miss Edna , Kama utasaini hio karatasi , kwanzia siku hii ya leo utakuwa ni mtoto kamili wa familia ya Adebayo na hautakuwa na uwezo wa kubadilisha hapo baadae hata kama baba yako mzazi ajitokeze na kama utataka kuvunja mkataba huu muda wowote basi hautokuwa na haki ya umiliki wa aina yoyote ya mali za kampuni na moja kwa moja mali zote zitakuwa chini ya umiliki wa kituo cha kulelea watoto wa Son And Daughter Orphanage”Aliongea Mzee Chino na kumfanya Edna afikirie kidogo.
“Mzee Chino nadhani tumpe muda wa kufikiria mke wangu kwanza”Aliongea Roma na kumfanya Mzee Chino atingishe kichwa chake na Edna alishukua ile karatasi na kupandisha juu Ghorofani , ni hakika mrembo huyu alikuwa akitaka kufikiria , kwani swala la kusaini huo mkataba ni kwamba lingemzuia yeye kutokuja kumtambua baba yake mzazi katika maisha yake yote na hivyo ni swala ambalo hakutakiwa kukurupuka na pia ilionesha Edna hakupewa kusaini karatasi hio akiwa mdogo na alisubiriwa akiwa mkubw aili afanye maamuzi yake yeye mwenyewe.
Edna baada ya kukaa kwenye kitanda chake , alijikuta akiingia kwenye mawazo ya tokea akiwa mdogo , mrembo huyu alifikiria maisha yake yote alivyokuwa ameishi na bibi yake Marium , Edna katika kuwaza maisha ya Bibi yake Mariuma hakuweza kuona siku yoyote ambayo Marium ashawahi kuonyesha dalili zozote za kumchukia , Marium katika maisha ya Edna alionekana kama mwanamke mwenye upendo wa Dhati kabisa , na Kwa Edna alijitahidi kukumbuka namna yoyote ambayo bibi yake alionyesha kutompenda , lakini alishindwa kupata dosari , bibi yake alikuwa akimpenda kama mjukuu wake halisi na alimpa kila kitu alichokuwa akitaka kwenye maisha yake.
Edna alianza pia kukumbuka maisha ya mama yake na bibi yake yalivyokuwa , lakini mrembo huyu hakuona dosari yoyote kati ya bibi yake na mama yake , licha ya kwamba Mama yake alikuwa akionekana kuwa mpweke sana kwenye maisha yake , lakini siku zote alimuona Bibi yake alikuwa ni mtu wa kumfariji.
Edna aliweza pia kufikiria namna ambavyo aliweza kuishi na baba yake mzee Adebayo na aliona kweli kwa maisha ambayo aliweza kusihi na baba yake , hakuona dalili yoyote ya Mzee Adebayo kumpenda kama mtoto wake , hivyo kukosa kabisa radha ya mapenzi ya baba.
Mrembo huyu pia hakuacha kuwaza kazi aliokuwa ameachiwa na mama yake , juu ya swala la kulipiza kisasi , kisasi ambacho mpaka muda huu hakuwa akikifahamu kinahusiana na nini Zaidi ya kupewa muongozo wa kile cha kufanya , aliwaza na akawaza na akawazua kwa takribani nusu saa kupita na bado hakuwa amefikia kwenye maamuzi.
“Au The Protector ndio baba yangu mzazi?”Aliwaza Edna huku akijikuta akianza kukumbuka kwanzia siku ya kwanza alivyoanza kuwasiliana na mtu ambaye hakuwa akitaka kujitambulisha kwake Zaidi ya kujiita The Ptotector na kumsaidia katika mambo mbali mbali yanayohusiana na kampuni.
“Mr Roma jana nilishindwa kuongea mbele ya mkeo , ila niseme kijana una hatari sana”Aliongea Mzee Chino wakiwa wameketi na Roma sebuleni na muda huu Bi Wema alikuwa yupo jikoni akiandaa kifungua kinywa na Roma licha ya kuwa yupo hapo, lakini pia akili yake ilikuwa ikijiuliza Siphie yuko wapi.
“Mzee Chino kwanini unaongea hivyo?”
“Nadhani ushanielewa mpaka hapo Mr Roma”
“Aah Mzee Chino unamaanisha kuhusu Neema?”
“Ndio Mr Roma , Neema kwangu nikama mtoto wangu kabisa na tokea vifo vya wazazi wake , nimekuwa nikiishi kwa kuangalia kila mtu anaemzunguka kumpa usalama na hata mali ambazo aliachiwa na mama yake, nilisimamia mimi ili kiupata haki yake kisheria , licha ya kuwa na baadhi ya wadogo zake kutoka upande wa baba”Aliongea Mzee Chino na kumshanganza kidogo Roma.
“Point yangu Mr Roma ni kwamba mpaka sasa , Neema anaonekana kukupenda kwa dhati kabisa , jambo ambalo ni mara yake ya kwanza katika maisha yake , najua unaweza kushangaa na kujiuliza kwanini Neema ana mtoto na kisha nikasema ndio anapenda kwa mara ya kwanza , lakini naamini Neema mwenyewe atakuja kukuambia juu ya hilo”Roma alitingisha kichwa kumuelewa mzee Chino kwani wakati huu alionekana kuwa siriasi na sio kama yule aliekuwa muhudumu aliekuwa akipenda kuongea utani.
“Mzee Chino nini kiliwakuta wazazi wa Neema?”
“Kuna ajali ya ndege ilitokea miaka kadhaa iliopita , wakati Neema akiwa mdogo , ilikuwa inahusiana na kupotea kwa ndege ya shirika la M Airline”
“Kupotea kwa ndege?”
“Ndio Mr Roma , kuna ndege ambayo iliopotea miaka kadhaa nyuma ni miaka ya tisini hivi na wazazi wa Neema walikuwa ndani ya ndege hio , ilikuwa ni tukio ambalo lilimumiza sana Neema kwa wakati huo , kwani wazazi wake walikuwa wakienda kumsalimia Neema wakati akiwa yupo nchini China kimasomo”Aliongea Mzee Chino na kumfanya Roma kuelewa, lakini pia kushangaa.
“Mr Roma hakikisha maamuzi ambayo utayafanya kati yako na Neema hayatomuumiza”Aliongea Mzee Chino na wakati huo huo Edna alishuka kutoka juu akiwa ameshikilia ile karatasi na alionekana tayari ashafanya maamuzi.
“Mzee Chino nipo tayari kusaini”Aliongea Edna na kumfanya Roma kushangaa , kwani maamuzi hayo yalikuwa yakimaanisha kwamba Edna anamtelekeza baba yake mahali popote alipo na hatokuja kumtambua.
“Wife unauhakika na maamuzi yako?”Aliuliza Roma huku akimwangalia Edna.
“Ndio nipo na uhakika , kama kweli kuna mtu ambaye alikuwa ni baba yangu mzazi , kwanini mpaka leo nimekuwa mkubwa hivi hakuwahi kujitokea kwangu na kusema mimi ni baba yake na kunifanya niishi kwa kukosa malezi ya baba?”Aliongea Edna kwa msistizo na kumfanya Roma ashindwe hata kuongezea neno, kwanza alitegemea Edna kufanya maamuzi hayo.
Edna alitia sahihi kwenye mkataba huo ambao ulikuwa ni kama wosia kutoka kwa bibi yake Edna pamoja na mama yake.
Baada ya taratibu hizo kuisha, Mzee Chino aliaga na kuondoka licha ya kulazimishwa kusubiria chai , lakini mzee huyu aliwaambia kuwa anapaswa kuwahi kwenda kuhudumia wateja wake wa Mgahawa.
Ni kama simu ya Edna ilikuwa ikimsubiria Mzee Chino aondoke kwani ilianza kuita mfuluizo na kumfanya Edna akili yake sasa irudi na kuanza kukumbuka hali ya kile kinachoendelea ndani ya kampuni , baada ya kuangalia ni nani aliekuwa akipiga, aliona jina ni la Nasra, alipokea haraka haraka na kuweka sikioni.
“Bosi hali ni mbaya , hisa zinazidi kuporomoka mpaka sasa na sijui hata cha kufanya na pesa taslimu kupambana na soko hatuna”Aliongea Nasra kwa wasiwasi na kumfanya Edna awaze kidogo.
“Vipi kuhusu benki ambazo tunashirikiana nazo kibiashara , jaribu kuwasiliana nazo watusaidie kiasi cha pesa ili tuweze kukabiliana na tatizo”
“Bosi nimefanya hayo na ndio maana nimekupigia sasa hivi , hakuna benki ambayo ipo tayari kutukopesha kiasi chochote cha pesa?”
“Nini!!?”
“Ndio Bosi napaswa kufanya nini juu ya hili , nimechanganyikiwa kabisa na Director’s wanapiga simu kila dakika , wanasema kama hautolipatia ufumbuzi swala hili ndani ya muda mfupi ,wataitisha kikao kwa ajili ya kuchagua CEO Mwingine”Aliongea Nasra na kumfanya Edna akunje ngumi ,mrembo huyu tokea hapo ashajua kuna mchezo ambao unachezwa.
“Nitakupigia Nasra”Aliongea Edna na kisha akakata simu
SEHEMU YA 127
Roma alimwangalia Mke wake kwa jinsi alivyokuwa na wasiwasi na alijua kabisa kuna tatizo ambalo linaendelea kwenye kampuni.
“Kuna nini Mke wangu?”Aliongea Roma huku akimwangalia Edna ambaye alijikalisha kivivu kwenye Sofa.
“Inaonekana mtu ambaye amevujisha taarifa , alikuwa na mpango Zaidi ya huo”
“Kwanini , kuna jambo ambalo limetokea kwenye kampuni?”
“Ndio Roma , Benki hawataki kunikopesha licha ya kufanya nao biashara kwa miaka kadhaa”Aliongea Edna huku mrembo huyu kwa mara ya kwanza aliona tatizo lililokuwa mbele yake ni kubwa mno.
Na ni kweli mpaka wakati huo Edna mategemeo yake yote yalikuwa ni kwa upande wa Benki, aliamini hata kama aonyeshe mkataba aliokuwa amesaini muda mchache na Mzee Chino haitosaidia.
Wakati Edna akiwaza chakufanya simu yake ilianza kuita tena mfululizo na baada ya kuangalia jina la mpigaji moyo wake ulipiga kwa nguvu , kwani aliekuwa akipiga alikuwa ni Tikayi., Edna alipokea na kuweka sikioni.
“Miss Edna sisi kama kampuni tumesikitishwa na kinachoendelea kwenye kampuni yako , na kama swala hilo lisipopatiwa ufumbuzi ndani ya msaa kumi na mbili yajayo tutajitoa kwenye mktaba wa kiabishara na kampuni yenu kisheria kabisa kama vipengele vya mkataba vinavyosema”Yaani Tikayi alionesha kuwa na hasira kweli kwani hakutaka hata salamu Zaidi ya kwenda moja kwa moja kwenye dhumuni la kupiga simu.
Edna alijiona kama anachanganyikiwa kwa wakati huo na alijikuta akinyanyka na kukimbilia juu, huku Roma akiwmangalia kwa huzuni , kwa mara ya kwanza alimuona Edna akikosa maamuzi juu ya hali iliokuwa ikiendelea kwenye kampini , lakini pia yule mwanamke ambaye siku zote ambazo alikuwa ni mwenye kujiamini leo hii , alikuwa emekosa kujiamini na karuhusu hisia zimtawale.
Wakati Roma akiangalia kile kilichokuwa kikiendeela kwenye Runinga , mara simu yake ilianza kuita na aliichukua na kuangalia namba na kuona ni ya Ron.
“Leta habari Ron?”
“Mfalme Pluto nishakamilisha kazi na sasa Dokta yupo chini ya vijana wetu wa kazi na wanasubiria utaratibu mwingine,Kama utaniruhusu Mfalme Pluto nimlete chapu na lile Mwewe letu la kivita , nina hamu nalo kweli na nitahakikisha kila atakae nizuia namshushia mayai Viza ya kutosha”
“Nataka wamhoji ni mtu gani ambaye amemuuzia taarifa nyeti ya kihospitali inayomuhusu Jedi Adebayo”Aliongea Roma.
“Mheshimiwa Pluto mpaka hapo nimekuelewa kabisa , tunajua kile kinachoendelea juu ya Malkia na nitakupiga ndani ya muda mfupi na majibu”
“Okey Ron, Mkishafanikisha kupata taarifa kutoka kwake namhitaji Tanzania ndani ya masaa machache yajayo lakini usimlete na ndege ya kivita”Aliongea Roma na kukata simu na muda huu huu , alimuona Edna aliebadilisha nguo akishuka kutoka juu akiwa na mkoba wake.
“Edna kama hawataki kukukopesha utafanya nini? ,au unakwenda kuwapigia magoti wakusaidie kiasi cha pesa unachotaka?”Aliongea Roma na kumfanya Edna asimame.
“Kwenye wakati kama huu nitafanyaje Roma ? ,zaidi ya kwenda kuwabembeleza”
“Usahasema kuna watu wanacheza mchezo na naamini washachukua tahadhari zote kuhakikisha mpango wao unafanikiwa”Aliongea Roma na kisha alimsogegelea Edna ambaye mwenyewe alikuwa akifikiria tu kama Roma , wakati huo alitamani kupata mtu wa kumsaidia kutoka katika hio hali.
Roma alimshika mikono Edna na kumsogeza mpaka kwenye sofa , licha ya Edna kutotegemea kitu kikubwa kwa Roma , lakini wakati huu aijisikia vizuri kuwa na mtu kama Roma ambaye anaweza kumfariji na kuwa upande wake , kwani siku zote mrembo huyu alikuwa mpweke na mtu pekee aliekuwa upande wake alikuwa ni Bi wema.
“Edna licha ya kwamba naonekana kama masikini , lakini katika maisha yangu siwezi kumruhusu mke wangu apigie watu wengine magoti kisa pesa”Aliongea Roma kwa kuwa siriasi na kumfanya Edna amwangalie Roma usoni na kushindwa kujua ni jambo gani Roma anamaanisha , kwani hakuwa njia nyingine Zaidi ya yeye kwenda kupiga magoti na kubembeleza watu wa benki.
Roma baada ya kuona Edna hakuelewa maana ya maneno yake aliingiza mkono wake kwenye mfuko wa suruali na kuibuka na Pete ya ajabu ambayo Edna kwakuangalia tu , alikumbuka tatoo iliokuwa kwenye mgongo wa Roma, ni pete iliokuwa na jina la AIDES, Edna alijikuta akishangazwa na uzuri wa pete hio.
Roma alitabasamu kwa namna ambavyo Edna alikuwa na mshangao na yeye pasipo ya kuongea neno , alichukua mkono wake wa kushoto na kutumbukiza ile pete kwenye kidole cha Edna , na wakati huu Edna mwenyewe alishindwa kuongea chochote kwani alikuwa kwenye mshituko wa namna pete hio ambavyo ilikuwa ikionekana , ilikuwa ikiwaka huku katikati ikiwa na madini ambayo Edna mwenyewe alishndwa kujua ni madini gani.
“Wife si umesema unataka kunijua japo kidogo basi vaa hii pete kwa muda na ukishatatua tatizo ambalo liko mbele yako nitakuambia maana ya hii pete”Aliongea Roma na kumfanya Edna ainue mkono kwa kwa kuangalia , kwa jinsi alivyokuwa ikionekana ni, kama alikuwa amevalishwa pete ya uchumba kwa jinsi alivyokuwa akigeuza geuza mkono wake.
“Inahusiana na nini , kwanini inaonekana ya ajabu?”
“Utauliza baada ya kujua nguvu ya hii pete , kwasasa nenda kashughulikie tatizo linaloendelea kwenye kampuni yako”
“Kivipi Roma unanichanganya ujue , acha utani?”Aliongea Edna kwa sauti kavu kidogo bila kutoa macho yake kwenye hio pete.
“Nenda Swiss Bank , nina uhakika tawi lao lipo hapa Tanzania , si ndio?”
“Ndio lipo , lakini kwnaini niende Swiss Bank?”
“Wife unatakiwa kuniamini mumeo , ninachokuambia nenda Swiss na utapata kiasi cha pesa unachotaka, wewe ukifika omba kuonana na Meneja mkuu wa benki na muoneshe hio pete halafu muambia unahitaji nini?”
Aliongea Roma , lakini wakati huohuo , aliingia Sophia ambaye alionekana kuwa katika haraka na haikueleweka amelala wapi , kwani kwa muonekano wake alionyesha kabisa hakulala hapo nyumbani jana yake usiku.
Sophia mara baada ya kuingia moja kwa moja alienda kumkumbatia Edna , mrembo huyu alionekana alikuwa ashapata habari yakile kinachoendelea mtandaoni.
“Sister pole sana”Aliongea Sophie na kumfanya Edna ajisikie vizuri kuitwa dada.
“Ulilala wapi Sophie?”Aliuliza Roma na kumfanya Sophie amwangalie.
“Nililala kwa rafiki yangu”Aliongea Sophie na Roma alijikuta akishangaa ni rafiki gani huyo wa kulala nae usiku mzima , ila hakutaka kuongezea.
“Sister hii petee….!!”Aliongea Sophia huku akiangalia pete iliokuwa kwenye kidole cha Edna.
“Sophie ninaenda kazini , nitakuelezea nikirudi”Aliongea Edba huku akinyanyuka baada ya kuona muda ulikuwa ukisogea na Sophie aliishia kutoa mshangao kwa kuangalia hio pete kwenye kidole cha Edna na kisha akamgeukia Roma na kumwanagalia na Roma aliishia kutingisha mabega kwa ishara kama hajui kinachoendelea na asimuulize.
Baada ya kama nusu saa ya Edna kuondoka ,Roma alikuwaa kwenye meza akipata kifungua kinywa , huku akila kwa fujo bila wasiwasi wowote na kumfanya Sophie amwangalie kwa jinsi ambavyo Roma alikuwa akila.
“Mr Roma nina wasiwasi na Miss Edna na kinachoendelea kwenye kampuni”Aliongea Bi Wema baada ya kumuona Roma anakula bila wasiwsi huku mke wake akiwa na matatizo na Roma alipunguza spidi kidogo ya kula na kisha akamwangalia Bi Wema.
“Bi Wema wala usiwe na wasiwasi , mpaka sasa hivi tatizo lishaisha”Aliongea Roma na kisha akaendelea kunywa maziwa yaliokuwa kwenye glasi kwa mkupuo mmoja na kushsuha glasi yote chini.
“Wewe umejuaje kama tatizo limeisha?”Aliuliza Sophie huku akioneysha hali ya kukereka na Roma alimwangalia Sophie.
“Una uhakika jana ulikuwa kwa rafiki yako wewe , au unatudanganya tu”
“Kwahio hamini kama nilikuwa kwa rafiki yangu?, halafu kwannini unapenda kubadilisha topic?”
“Siwezi kukuamini”Aliongea Roma na kumfanya Sophie anune na kujisikia vibaya lakini kwa upande wa Bi Wema alijikuta akicheka kwa namna ambavyo Sophie aliweka uso wake, alidhihirisha utoto.
******
“Bebi una uhakika hakuna benki ambayo itamkopesha?”
“Matrida mpenzi unanichukuliaje kwa mfano , mimi ndio Musa Omary , Gavana wa benki ya Tanzania na kila benki inanisikiliza kwa maamuzi yangu na ushawishi wangu ni mkubwa , hivyo kaa kwa kutulia mpenzi , hili swala lako nishamaliza na hawezi kupata mkopo wowote, labda aende Swiss Bank lakini na wao hawatomkopesa maana hela zote sio za kwao”
Aliongea Gavana upande wa pili wa simu na asubuhi hii Matrida alikuwa ndani ya ofisi yake kubwa ambayo mwanzoni ilikuwa ikikaliwa na Abubakari Hamadi na mrembo huyu alikuwa akiongea na simu na mtu ambaye alikuwa akiitwa Musa Omary ,Gavana, ndio huyo ni mwanaume ambaye alikuwa ni Danga la Matrida na ndio aliemfanikisha Matrida baada ya kurudi masomoni kiuweza kupata cheo kikubwa ndani ya BOT.
“Lakini Edna anaonekana kuwa na ukaribu na mheshimiwa Senga , unadhani hatoingilia katika hili?”
“Kaa kwa kutulia mpenzi na swala lako hili likiisha baadaye hakikisha tunakutana kufanya yetu ,Raisi Senga licha ya kuwa Raisi , lakini hawezi kunipa maagizo na kutii, kuna nguvu ambayo hawezi kushindana nayo ndani ya Tanzania”Aliongea Mzee huyo kwenye simu na kumfanya Matrida atabasamu.
“Okey Baadae nitakupigia mpenzi”Aliongea na kukata simu na muda huo huo baada ya kukata simu aliingia Isack CEO msaidizi, akiwa na faili mkononi.
“Madam CEO”Aliita Isaack na Matrida alitabasamu na kunyanyuka alipokuwa ameketi na kumsoglea Isack na kubusiana , wawili hawa walionekana kuwa wapenzi kwa mahaba ambayo walikuwa wakifanya.
“Vipi mpango wako , unaenda kama ulivyopanga?”Aliuliza Isack na kumfanya mrembo Matrida kutabasamu na kisha kurudi kwenye kiti chake.
“Nimetokea kuongea na Gavana hapa anasema hakuna benki ambayo itaweza kumkopesha Edna”Aliongea
“Kama ni hivyo basi naamini mpango utafanikiwa kwa kiasi kikubwa sana ,lakini Matrida unauhakika unataka kumuacha Abubakari kuingiza pesa zake ndani ya Vexto , utanufaika vipi?”
“Hahaha…Isack nina mpango nae , Abubakari ni rahisi kushawishika sana , lakinni jambo la kufurahisha ni kwamba hela ambayo anaingiza ndani ya Vexto sio ya kwake”
“Unamaanisha nini?”
“Baba kaniambia kuwa Abubakari kakopeshwa na Dorisi , nimeshangazwa sana na Dorisi kuwa na uwezo wa kumkopesha Abubakari kiasi chote hiko, ila sitaki kujua Zaidi ni kwa namna gani Dorisi anapesa kiasi hiko , ila nitahakikisha Abubakari ashindwe kurudisha mkopo huo”Aliongea Matrida na kumfanya Isaack ashangae, hata yeye kwani alikuwa akimjua vizuri Dorisi.
“Halafu kuna swala nimekumbuka”
“Umekumbuka nini?”
“Dorisi mpenzi wake ni mfanyakazi mmoja wa Vexto , anaitwa Roma Ramoni kwa taarifa za chini ambazo nipo nazo , ni kwamba Edna na huyo Roma ni mke na mume na wafanyakazi wengi wa Vexto hawalitambui hilo na linafahamika kwa baadhi ya watu tu”
“Huyo Roma ana nini mpaka kuwa na mwanamkke kama Dorisi na Edna kwa wakati mmoja, anapesa kiasi gani?”Aliuliza Matrida kwamshangao.
“Siwezi kufahamu juu ya kiasi ambacho anacho , ila ni jamaa wa kawaida sana , kwani Zaidi ya kujua lugha nyingi , hakuna kitu Spesho kutoka kwake , ila anaonekana pia kuwa moja ya watu wenye uwezo mkubwa ndani ya Vexto kwani ndio aiefanikisha kusainishwa kwa dili lile na Yamakuza na kuifanya kampuni yetu kukosa saini”Aliongea Isack na kumfanya Matrida kushangaa Zaidi na kutaka kumjua hiyo Roma angalau kwa sura.
“Huyu Roma kama ni kweli ana mahusiano na wanawake warembo kama Edna na Dorisi ni kipi cha ziada kikawafanya wanawake wote wawili kumpenda kwa wakati moja nitajaribu kumfuatilia”Aliwaza Matrida lakini wakati huo huo simu yake ilianza kuita tena na kuangalia jina lilisomeka Rambo.
“Rambo nipe taarifa”
“Boss Edna namuona hapa anaingia kwenye jengo la Benki ya Swiss Bank”
“Umesema Swiss Bank?”
“Ndio madam ndani ya jengo la TPA”Aliongea mwanaume huyo upande wa pili na kumfanya Matrida ashangae kwanini Edna ameenda kwenye Bank Ya Swisi , kwani kwa jinsi a mabavyo alikuwa akielewa ni kwamba Benki ya Swiss haikuwa ikitoa aina yoyote ile ya mkopo Zaidi ya kuhifadhi pesa za watu tu na vito vya thamani.
“Jaribu kufatilia kujua ni jambo gani limempeleka hapo”Aliongea Matrida huku akikosa utulivyo kwenye macho yake.
SEHEMU YA 128
Upande mwingine ndani ya Ikulu ya mheshimiwa Senga , muda wa asubuhi wakati mheshimiwa huyu akiwa anaendelea na majukumu yake ya kazi kama kawaida , mara mlango wake ulifunguliwa na Msemaji wa Ikulu Miss Fatum Adinani.
“Mheshimiwa kuna taarifa mbaya imetufikia”Aliongea Fatuma na kumfanya Senga akae vizuri kwenye kiti , bwana huyu alikuwa ashazoea taarifa za kushitusha sana katika uongozi wake na alichukulia kama jambo la kawaida katika kazi yake hii ya uraisi.
“Inahusu nini Fatuma?”
“Profesa Peter Shelukindo pamoja na familia yake yote imeuwawa usiku wa jana muda wa saa tisa usiku baada ya kukatwa mapanga na mtumambaye mpaka sasa hivi hajafahamika”Aliongea Fatuma na kumfanya Mheshimiwa kutoa macho kwa taarifa hio na kuona ni kweli hio taarifa ilikuwa mbaya.
“Ni nani wa kufanya tukio la kinyama kama hilo?”Aliongea Senga huku akiwa na huzuni kwenye macho yake.
“Jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi mheshimiwa na nimewasiliana na IGP na ameniambia wanafatilia nani amefanya tukio hilo la kinyama”
“Fatuma hili ni tukio la kutisha sana kutokea kwa mtu muhimu kwa taifa kama Profesa Shelukindo ,nitawasiliana na IGP wafanye uchunguzi wa makini juu ya hilo , hebu toa taarifa ya ya kuomboleza na kusikitishwa na swala hilo”
“Sawa muheshimiwa” Aliongea Fatuma na kisha akatoka na kumuacha Mheshimiwa Senga kwenye mawazo , Raisi huyu alishindwa kujua ni nini kimesababisha kwa watu kwenda kumfanyia unyama huo Profesa Shelukindo , kwani alikuwa ni kama tegemeo la taifa kwa upande wa Sayansi ya kitafiti.
“Nitachimba hili swala mpaka nipate ukweli wote , hata wa kutumia majasusi wangu , hii ni aibu kwa mtu kama Shelukidno kufariki kifo cha kikatili namna hio pamoja na familia yake”Aliwaza Meheshimiwa Senga.
Profesa Shelukindo ni moja ya wasomi wakubwa ndani ya taifa na duniani ambao wamejizolea sifa kubwa sana katika medani za sayansi ya kiutafiti duniani , kiasi kwamba mataifa mengi yalikuwa yakimwangalia kwa ukaribu sana kwa kila kitu alichokuwa akikifanya ndani ya Tanzania.
Elimu yote ya Profesa Shelukindo aliipatia ndani ya chuo cha Harvard Marekani kwanzia ngazi ya Shahada mpaka PhD , akibobea Zaidi katika maswala ya sayansi inayohusiana na maswala ya Energy , na ndio mwafrika wa kwanza kiufundisha masongo kwa ngazi ya PhD ndani ya chuo cha Harvad na katika muda ambao amehudumu katika kufundisha ndani ya Harvard, Profesa Sheliuindo alijizoelea umaarufu baada ya kufanya tafiti mbalimbali zilizokuwa zikihusisha ‘Ant-Matter Energy’ na katika tafiti zake zote kutokana na ushahidi ambao aliweza kuwakilisha na kufanikiwa, ulikubalika na wanasayansi wengi duniani na kusaidia sana kutengeneza ‘formula’ ambayo ilikuwa ikihusisha namna ya kutengeneza aina hio ya Energy na kuitumia.
Moja ya wanasayansi nguli ambao wamepitia kwenye mikono ya Profesa Shelukindo ni Yan Buwen pamoja na Profesa Clark ,na hio ndio inamfanya profesa Shelukindo kufahamika duniani kote jambo ambalo pia lilifanya taifa la Tanzania kutambulika Zaidi kimataifa , mara baada ya Profesa kutangaza kuachana na ufundishaji ndani ya Harvard na kurudi Tanzania , jambo ambalo licha ya kuibua maswali mengi , liliwafanya wanasayansi wengi duniani kutaka kujua ni kwanini Profesa huyo mwenye heshima kubwa ndani ya ulimwengu wa Sayansi kutaka kurudi nchini Tanzania.
Lakini pia kulikuwa na tetesi za chini sana ambazo inasemakana kwamba Profesa amegundua siri kubwa sana juu ya vyanzo vya Energy mbalimbali ndani ya Dunia , siri ambayo ilikuwa ni kubwa sana kwake na Profesa huyo baada ya kugundua kanuni hizo ndio aliona kama hizo kanuni zitawafikia watu ambao wanania mbaya na dunia basi,kunaweza kutokea jambo baya sana ambalo linaweza kupelekea mwisho wa dunia na ndio maana profesa huyo kuharibu tafiti zote ambazo alifanyia kazi na kurudi Tanzania , hizo zilikuwa ni tetesi tu kutoka kwa vyanzo vya chini.
Kifo cha Profesa huyu huenda kikawa gumzo kubwa Zaidi ndani ya dunia , lakini pia kufanya tetesi ambazo zilikuwa zikisambaa , kurudi tena kwa kasi.
******
Ndani ya hoteli ya Serena anaonekana Yan Buwen akiwa amesimama kwenye dirisha akiwa kifua wazi huku mkono mmoja akiwa ameshikilia mvinyo na mkono mwingine akiwa ameshikilia simu mkononi na alionekana kuna mtu aliekuwa akiongea nae.
“Waziri hupaswi kuwa na wasiwasi , licha ya kwamba hata mimi nimeshangazwa na mtu wetu kumaliza familia nzima lakini naamini kuna sababu , hivyo hupaswi kabisa kuwa na wasiwasi juu ya swala hilo , nakuhakikisha hakunajambo baya ambalo linaweza kukufikia wewe na familia yako kama utaamua kukaa kimya”
“Mr Yan mimi mdomo wangu upo kimya na siwezi kuongea chochote , ni kwamba nimesikitishwa na familia nzima kufa kifo cha aina ile”
“Waziri achana na huruma zako za kipuuzi , unapaswa kuwa imara la sivyo jambo baya na wewe linaweza kukufikia , maana unaonesha udhaifu na unaweza kukwamisha mipango yangu ndani ya Tanzania”Aliongea Yan Buwena kwa hasira na kisha akakata simu. Na kisha kuachia tabasamu la kifedhuli.
“Watanzania ni watu waoga waoga sana , ni hatari kufanya nao kazi kwani hawako imara kihisia,ndio maana wengi wao ni masikini”Aliwaza Yan Buwen.
“The Don nishakamilisha kazi ya kwanza ambayo umeniagiza kuifanya ndani ya Tanzania , ni jukumu lako kuhakikisha Napata jiwe la kimungu , ili kuanza kulifanyia kazi, I will Become God Hahahaha.....,Hades baada ya kupata Jiwe la Kimungu hutakuwa na uwezo wa kuogopwa tena maana nitakudhibiti”Aliongea Yan Buwen na kisha akanywa kidogo mvinyo wake , lakini muda huo huo mlango wake ukagongwa .
“Scorpion anaonekana kuwa na mchecheto sana”Aliongea Yan Buwen na kuusogelea mlango na kwenda kufungua na kweli alikuwa ni Scorpion akiwa kwenye sura yake ile ile ngumu ambayo haikuonyesha Furaha wala huzuni na mwonekano wa Scorpion ulimridhisha sana Yan Buwen.
“Kuna haja gani sasa kuja na panga lako Scorpion..hahaha,,, unadhania sitotimiza ahadi yangu”Aliongea Yan Buwen huku akimruhusu Scorpion ambaye baada ya kuingia tu , maajabu upanga ulionekana kwenye mikono yake na alionekana kuuficha kimazingara na upanga bado unaonekana kuwa na damu. Yaani kwa mwonekano wa Scorpion usingedhania kama ni mwanamke alionekana kuwa Zaidi ya neno ukatili.
Roma aliekuwa akiangalia runinga hata yeye pia alijikuta akiwa ni mwenye kushitushwa na taarifa iliokuwa ikionyeshwa kwenye runinga , taarifa iliokuwa ikihusisha kifo cha profesa Shelukindo , Roma alikuwa akimjua vizuri Profesa Shelukindo kwani ni moja ya watu ambao walikuwa wamehusika na elimu ya Profesa Clark.
“Ashley na Profesa Clark watakuwa wapo kwenye maumivu baada ya kifo hiki na nadhani muda si mrefu watakuwa nchini Tanzania”Aliongea Roma huku akiwa sio mwenye kubadilisha mwonekano wake sana , ni kama mtu ambaye hakuwa akijali sana juu ya kifo cha Profesa Shelukindo.
Wakati Roma akiendelea kuangalia taarifa hio , simu yake ilianza kuita na baada ya kuangalia jina lilikuwa ni Diego.
Alipokea na kuweka sikioni kusikiliza kuna taarifa gani nyingine ambayo Deigo anayo.
*****
Edna licha ya kwamba Roma alimwambia kwenda ndani ya benki kubwa sana duniani ya Swisi Bank , lakini mrembo huyu alikuwa ni kama anabahatisha , hakuwa akiamini kabisa maneno ya Roma, aliendesha gari huku muda wote alikuwa akiangalia pete iliokuwa kwenye kidole chake, mrembo huyu alikuwa amevaa pete hio lakini aliogopa kwa kuoana kama inaweza kuibiwa kutokana na uzuri wake , kwa haraka haraka aliamini kabisa hio pete haikuwa ya kawaida sana na katika macho yake ilikuwa ikionekana kuwa na thamani kubwa mno.
Baada ya kuingiza gari lake ndani ya eneo hili la maegesho katika jengo hili refu ndani ya Tanzania , alishuka na kutembea kwa kujiamini na kuingia kwenye Floor ambayo ilikuwa ikionyesha ndio Benki ya Swiss ilipokuwa ikipatikana , baadhi ya wafanyakazi ndani ya jengo hili walimpa heshima yake , kwani walikuwa wakimfahamu na pia licha ya kuona habari iliokuwa ikiendelea mtandaoni.
Dakika kama moja na nusu aliingia ndani ya Floor ya Benki hii na kupokelewa kwa heshima kubwa sana na wafanyakazi , walionekana kumfahamu Edna kama moja ya ‘High Valued Customer’
“Karibu sana Miss Edna , Asante kwa kutembelea tawi letu kwa siku ya leo , nadhani upo hapa kwa ajili ya kuwithdrawal kiasi cha pesa ambacho umetunza kwetu”Aliongea mama mmoja hiivi wa kizungu ambaye alikuwa amevalia ‘uniform’ za nembo ya Benki hio.
“Hapana Madam , leo nipo hapa kwa ajili ya kuonana na Meneja wa Benki”Aliongea Edna na kumfanya mwanamama huyo wa kizungu kishangaa kidogo na kisha akatabasamu.
“Miss Edna naomba kuuliza kama una miadi nae?”
“Sina miadi nae , lakini ni muhimu kwa mimi kuonana nae ?”Aliongea Edna na ukweli ni kwamba huyu mama wa kizungu , alikuwa akimsemesha hivyo Edna kutokana na kwamba alikuwa akijua Edna alikuwa kwenye hali mbaya sana kiuchumi , na pia hata baada ya kumuona aliamini huenda Edna yupo kwa ajili ya kutoa kiasi cha pesa ambacho alikuwa amekihifadhi ndani ya benki hio.
Baada ya mama yule kuona Edna kaweka usiriasi kwenye macho yake , aliacha kuongea na kuingiza namba Fulani kwenye simu ya meza na kisha akaweka sikioni, hatua zilikuwa ni zile zile kama za Dorisi alivyofika ndani ya hii benki wiki kadhaa zilizopita.
“Miss Edna ,Menaja kakubali kuonana na wewe nenda Floor namba ishirini”Aliongea Mama huyu huku akitabasamu.
Ukweli wanawake wote ambao walikuwa wakifanya kazi ndani ya benki hii walikuw awakisikia sana , yaani walijiona kama wapo juu ya kila mfanyakazi ndani ya benki zote ndani ya Tanzania na ndio maana walikuwa wakitembea kwa mwendo wa kumaringo sana na hata Edna aliliona hilo ila hakujali sana.
“Okey Thank you”
“Okey Miss Edna , I wish you Good luck”Aliongea yule mzungu na Edna alitabasamu na kutembea mpaka kufikia lift na kisha akaingia , na kadiri lift ilivyokuwa ikipanda juu , mrembo huyu moyo wake ulikosa utulivu , alikuwa akiogopa kwa Roma kumdanganya na kuumbuka , lakini alipiga moyo Konde baada ya kukumbuka matukio ya ajabu ajabu ya Roma.
Ndani ya dakika kama mbili mlango wa lift ulifunguka na akapokelewa na Katibu Muhtasi mwanamke wa Kiafrika na akamuongoza mpaka ndani ya ofisi ya Meneja ilipo.
“Karibu sana Miss Edna”Aliongea Meneja Harris Pot huku akimuoneysha Edna kuketi kwenye masofa.
“Asante sana Mr Hariss naitwa…”
“No need for Introduction Miss Edna , We know all of our High Valued Customers”aliongea Harrisa na akaketi na yeye
“Enhe Miss Edna nadhani twende moja kwa moja kwenye swala ambalo limekufanya kutaka kuonana na mimi , maana sisi wafanyabiashara kwetu muda ni mali”
“Ni kweli Mr Harris , nimekuja hapa kwa maagizo ya mume wangu na ameniambia ni kuonyeshe hii pete”Aliongea Edna na muda wote alikuwa ameficha mkono uliokuwa na pete na baada ya kuongea hivyo , aliutoa na kumuonyesha Meneja Harriss na meneja huyu baada ya kuangalia ile pete alitoa macho.
“Miss Edna is it Original or Counterfelt one?”Aliuliza akimaanisha kama ni Original au ni feki na, Edna hakutaka kuongea sana , aliichomoa kwenye kidole na kisha akampatia.
“Nadhani una namna ya kujua hio pete ni Guinine or not Mr Harris ?”Aliongea Edna na kumkabidhi.
“Ofcourse yes Miss , Just Few minutes “Aliongea Harris na kunyanyka na kusogelea upande wa pili wa makabati na kufungua mlango wa kabati moja na baada ya kutoa baadhi ya vitu pembeni aliibuka na kifaa kama zile mashine za kupimia presha hospitalini na kwa mbele kikiwa kimeunganishwa na vifaa viwili , kimoja kikiwa kama ni mzani wa dukani lakini mdogo sana ambao haukuwa na uzto mkubwa na kifaa kingine kilikuwa ni kama pen ambayo ina tochi.
Edna alikuwa akimwangalia tu Harris kwa kila anachokifanya na alionekana kuwa na wasiwasi kweli , baada ya Harris kutoka na kile kifaa , alichomeka kifaa kile kwenye umeme na kukiweka mezani pamoja na ile peni na kile kipande kama Mashine za kupimia Presha na baada ya hapo alichukua ile pete na kuweka kwenye mzani.
Harrsi alioneysha kuwa na shauku kweli kwa kila alichokifanya , kwani hata mikono yake ilionekana kukosa utulivu kabisa, baada ya kuweka ile pete kwenye mzani aliangalia kile kimashine ambacho kipo kama Mashine ya Presha na kusoma uzito wa ile pete na macho yalimtoka.
“Precisely…!!,Precisely ..!!!”Aliwaza bwana huyu ba baada ya hapo , alichukua kile kifaa mfano wa pen za Tochi za kidaktari wanazotumia kumulikia wagonjwa na akabonyeza kwa upande wa juu na ile mashine ilitoa mwanga wa ‘laser’ mwekundu sana hivi na baada ya hapo , Harrisi kwa kutetemeka , akalengesha katikati ya neno ‘Aides’ na hapo hapo likatokea jambo la kushakangaza , kwani chumba chote kilibadilika rangi na kuwa na mwanga wa kijani tupu ambao unaumiza macho mno , mwanga uliotolewa na yale maneno ya Aides , Edna alijikuta akishangazwa na tukio hilo mpaka kumpelekea kusimama , lakini pale pale Harrisi , alidondoka chini haraka haraka hku akiweka ile pete kwenye viganja vyake vya mikono kama mtu anaepokea Baraka kutoka kwa Mungu akiwa amepiga magoti , huku ile pete ikiwa kwenye viganja vyake.
“Queen Peresephone”Aliongea Harris kwa kutetemaka huku akiinamisha kichwa chake chini kwa ishara ya heshima mbele ya Malkia .
ITAENDELEA JUMAMOSI JIONI ,ACHA MAONI YAKO HAPO CHINI
NICHEKI WATSAP UIFUATILIE KWA HARAKA , IPO SEHEMU YA 180 NAMBA NI 0687151346
SEHEMU YA 52
Ilikuwa ni kama kimbunga Jobo kilichokuwa kimejitengeneza ndani ya hili eneo kiasi kwamba ile mashua na Manuari pamoja na wanajeshi wa kikosi cha Dragoni walisukumwa mbali.
“Ni nguvu gani hii?”Aliongea Kibonge huku akiendelea kushangaa , kilichowashangaza Zaidi ni kwamba zilipita dakika kumi pasipo ya Roma na Tzeng kuonekana juu ya maji , ikimaanisha kwamba walikuwa wakipigana chini ya maji.
“Mbwa Mwitu kimbia..!”Aliongea Kobota baada ya kuona tukio la kutisha na hio ni mara baada ya eneo wanalopigana Tzeng maji yake kutengeneza barafu kwa spidi kiasi kwamba sehemu waliokuwa wamesima Kobota kuhisi ubaridi wa hali ya juu sana na maji yalikuwa yakigana kuelekea upande wao na kuwafanya waogelee kwenda kusimama mbali.
“What is happening?”Aliuliza Jessie kwa mshangao baada ya duara la Barafu kujitengeneza .
“That is Hades Jessie , I told you we have to stay here to enjoy this live show”A;iongea Jason akiwa amekalia ukingo wa Manuari yao ambao ilikuwa imefungua ufuniko kwa juu , licha ya kwamba walikuwa wakisikia barindi kali lakini hawakutaka kuondoka , walitaka waone mpaka mwisho wake.
Wakati wakiendelea kuongea Ghafla katikati ya lile barafu paliachia mpasuko wa nguvu kiasi kwamba kurusha vipande vya mabarafu juu na Tzeng Alionekana akichomoka kama mshale lakini wakati huo huo Hades na yeye alitokea , lakini sasa muonekano wa Roma uliwafanya kila mtu kushangaa…
“It`s yellow Glows not what I wanted to experience Jessie ,Tzeng is Disapointing”Aliongea Jason na kumfanya Jesie ashangae.
“What do you mean?”
“When his eyes emit Yellow glows mean he is using half of his power , I need to see red glows Come on Tzeng” Jesie alizidi kushangaa,huku Jason akionesha kutofurahishwa na uwezo wa Tzeng kwani alitegemea kuona macho ya Roma yakitoa mwanga mwekundu.
Roma Macho yake sasa hayakuwa ya kijani tena kama alivyokuwa amezeleka hapa macho yake yalikuwa ya njano huku yakitoa miale flani hivi kama mwanga wa jua lakini usio kuwa mwingi, kiasi kwamba haukuwa ukisambaa , na kutokana na eneo hili kuwa na giza alionekana vyema.
“Tzeng huna uwezo wa kunishinda , ikibidi kimbia kabla sijakufanya ukose hewa ya oksijeni”
Aliongea Roma kwa sauti nzito kama Roboti kiasi kwamba watu waliisikia mara mbili kwenye masikio yao kwani ilikuwa na mwangwi, huku Tzeng akionesha wasiwasi wake , ukweli ni kwamba Tzeng aliponea chupuchupi chini ya maji, kwani wakati wakiendelea kupigana Macho ya Roma yalikuwa yakitoa miale ya kijani kiasi kwamba bwana huyu aliogopa kubakia chini ya maji na akataka akimbie , lakini ni kama Roma alijua mawazo yake , kwani alikimbia juu yake na kisha kujikakamua kama mtu ambaye anataka kulazimisha ushuzi na hapohapo na mwili wake ulibadilika Rangi nangi na kuwa kama sanamu ambalo limejengwa kwa barafu huku likimomonyoka kama unga kwa spidi kubwa kiasi kwamba eneo la juu ndio lilianza kutengeneza barafu na hapa ndipo alipoweza kujua kuwa mtu ambae alikuwa akipambana nae hakuwa wa kawaida , yeye katika kusikia kwake kuhusu stori za Hades ni kwamba alikuwa na uwezo wa hali ya juu wa ‘Martial Art’ pamoa na mbinu za kichawi za kichina Lakini hakuwahi kuwaza kama anaweza kugandisha maji.
“Shi*t he is using power to control Density , I can’t Move”Aliwaza Tzeng huku akiwa amejawa na kiwewe.
Sasa kile kitendo ch Hades kugandisha maji kwa juu kilimfaya ashindwe kutoka juu na pia Pumzi ilikuwa ikimuishia na aliona akizembea anakufa kizembe na hapo ndipo alipoamua kutumia uchawi wake ambao ulimuongezea nguvu kiasi kwamba alikuwa akisukumwa kutoka chini kwenda juu kwa spidi ya hali ya juu na kuweza kutoboa barafu na upanga wake na kutokezea nje.
“Hapa inabidi nikimbie , huyu sio mtu wa kawaida nitakufa ,Ngoa nikajipange upya nitaomba mpambano tena”.Aliwaza Tzeng wakati akiwa amesimama kwenye barafu iliotengenezwa na Hades huku ikielea juu juu.
“Hades tutakutana tena ngoja nikajipange upya”Aliongea Tzeng na palepale aliposimama pakajitengeneza vitu kama majivu na vikapelerushwa na upepo kuelekea magharibi.
Baada ya Tzeng kukimbia Roma mwili wake ulianza kurudi katika hali ya kawaida , lakini sasa nguo zake zote zilikuwa zimechania yaani zilijiachia kama unga na kubakiwa uchi.
Jasona baada ya kuona Tzeng kashindwa pambano waliona hapo sio mahala pake kukaa ,kwani wote waliingia kwenye manuari na ikaanza kuzama chini na kukimbia.
“Jason , hatujachukua sanamu”Aliongea Jesie.
“Sanamu la nini?”
“Kwani tumekuja kufanya nini?”
“Jesie acha kuwa na kichwa kigumu , unafikiri tumekuja kuiba sanamu ambalo halina thamani kwetu”
“Kwa hio tumekuja kufanya nini?”
“Kurusha pambano live , ndio ilikuwa misheni yetu Jesie”Aliongea Jason
Kibonge hakutaka kabisa hata kumsogelea Roma , kwa matukio ambayo alikuwa ameyashuhudia kwa macho yake ni kama alikuwa kwenye ndoto ,alimwangalia Roma ambaye alikuwa amesimama kwenye mashua hii akiwa uchi sehemu ambayo alikuwa amesimama Tzeng kabla ya pambano lao.
Wale wakorea ambao walikuwa wapo pamoja na Tzeng baada ya kumuona Master wao kakimbia na wao walijirusha majini bila kujiuliza mara mbilimbili , mziki walioushuhudia kutoka kwa Roma waliziambia nafsi zao ni heli kujaribu kufia kwenye maji kuliko kuliko kukutana na adhabu ya shetani aliekuwa mbele yao..
Roma licha ya kwamba eneo hili la baharini kuwa na baridi kali kiasi kwamba kwa mtu wa kawaida ambaye hajazoea baridi anaweza kuzimia , lakini kwa Roma ni kama alikuwa amevaa nguo.
Mbwa mwitu alikuwa amesimama nyuma yake , kwenye boti , huku akimwangalia Roma kwa wasiwasi mwingi , kila akifikiria tukio ambalo limetokea dakika chache zilizopita , hakuwa akiamini kama mtu ambae amesimama mbele yake ndio alieweza kufanya yote hayo , zile dharau alizokuwa nazo zilikuwa zishaisha na sasa kilichokuwa kimebaki kwenye akili yake ni woga na hali ya kutokujiamini kila anapomuangalia Roma.
“Nilikuwa nikizisikia habari za Hades lakini sikuwa nikijua uwezo wake upo hivi”Aliongea Kobota mara baada ya kumsogelea Mbwa mwitu , muda huu wote wakiwa ndani ya boti hii.
“Nimeshaangazwa sana na kilichotokea dakika chache zilizopita Kobota huyu sio mtu”
“Kwani nani kasema ni mtu , wewe hujamsikia kampteni anamwita Mungu wa wafu?”
“Nilijua ni jina tu Kobota kama mimi ninavyoitwa Mbwa Mwitu”.
Kobota alitabasamu na bila kungea chochote alimgonga gonga begani Mbwa mwitu kama kitendo cha kumfariji na kisha akarudi ndani.
Baada ya Roma kusimama muda mrefu akiwa uchi aligeuka na kuanza kutembea na kuingia ndani ya chumba cha boti hii , huku akidhamiria kutafuta nguo kwa ajili ya kujisitiri.
Licha ya kutafuta kwakuchangua maboksi yaliokuwa kwenye hii boti hakuambulia chochote Zaidi ya kuona vitu ambavyo wale wakorea wameviiba,ni vitu ambavyo vilikuwa na thamani kwani kulikuwa na baadhi ya vifaa vya udongo ambavyo alipovichunguza kuna vilivyokuwa ni vya miaka mingi,ikiwemo uwepo wa ‘Porcelain’ ya ‘Song Dynastry’ na makolo kolo mengine
Roma baada ya kuona amekosa alirudi na kuungana na Kobota na Mbwa Mwitu waliokuwa wamekaa sehemu ile ile ambayo wale wakorea waikuwa wakinywa na kuongea , lakini kabla hajakaa chini kuna kitu kilimvutia, yalikuwa ni maboksi ya mbao mawili.
Aliyasogelea na kuanza kuyasukuma kwa mguu lakini yalikuwa mazito, Kobota na wenzake walikuwa wakimwangalia Roma kwani hata wao waliona hayo maboksi lakini hawakua na habari nayo , ni kama watu ambao walikuwa wamekosa na hamu ya kila kitu kutokana na kuponea chupuchupu kwenye kudunguliwa na ile Chopa na sasa walikuwa wakifikiria kurudi nchi kavu tu.
Roma baada ya kuona maboksi haya kuwa mazito , alibeba moja na kuligeuza kwa juu na kisha akafyatua kimlango ambacho kilikuwa kimegongelewa na chuma na hapo ndipo alipojikuta akishangaa , kwani ile anafungua tu boksi ,ulitokea mkono uliokuwa kwenye hali ya ulegevu na hapo ndipo alipojua kuwa ndani ya hayo maboksi kuna watu amba wamefungiwa.
Hata Kobota na wenzake walishangazwa na jambo hilo na walisimama na kumsogelea Roma.
Walikuwa ni wasichana wawili mmoja Mjapani na mwingine alikuwa ni muafrika kutokana na ngozi yake ,wasichana hawa walionekana kuzimia kutokana na baridi kali na kuelekea mpaka midomo yao kupasuka pasuka na kutengeneza nyufa.
“Wamepoteza fahamu , wanaonekana kuwa hai”Aliongea Roma kwa kijapani na kufanya Kobota na mbwa mwitu waangaliane na kisha kumgeukia Roma kwa mshangao.
“Hades tunapaswa kufanya nini kuwaokoa?”Aliuliza Kobota na Roma hakujibu chochote na kuinama huku akimwnaglaia yule mwanadada mwenye rangi ya chocolate ya kiafrika, baada ya kumwangalia kwa dakika aliweka mkono wake kwenye kifua cha yule mwanadada na kisha akafumba macho.
Kobota na kibonge walikuwa wakijiuliza Hades anafanya nini , lakini walitulia kuona mwisho wake , lakini ndani ya dakika kadhaa , walihisi joto kiasi na kumkazia macho Hades.
Roma alimuwekea mwanamke yule mweusi kiganja kwenye moyo na kisha akahamia kwenye uso kwa dakika kama tano hivi, na kilichotokea kiliwaacha kobota midomo wazi , kwani ngozi ya yule mwanamke iliokuwa imepauka ilirudi kama kawaida , licha ya kwamba alikuwa bado hajarejewa na fahamu lakini alionekana kuwa na afadhari kuliko alivyokuwa mwanzo.
“Hii ni ‘Endless Resolve restoration Energy’ nimejaribu kumuingizia na haitamchukua muda mrefu kurejewa na fahamu”Aliongea Roma.
Kobota na Mbwa mwitu waliangaliana kwa mshangao huku wakionekana kutoelewa kile ambacho Roma ameongea na Roma hakuwajali , alijua hawajaelewa ,alimsogelea na yule mwanadada wa kijapani na kisha akamuwekea kiganja cha mkono kwenye moyo na kisha akahamia kwenye uso na tumboni na ndani ya dakaika tano na yeye mwili wake ulionekana kurejea katika hali ya kawaida.
“Niko wapi?”Ilikuwa ni sauti ya msichana aliewekewa mikono na Roma wa kwanza, sasa kilichomshangaza Roma ni kwamba mwanadada huyu alitumia lugha ya Kiswahili kuuliza
Lugha ambayo Kobota na Mbwa mwitu hawakuweza kuielewa
UNAJUA NINI KIMETOKEA ..
ENDELEA KUTOA MCHANGO KUANZIA 2000 KUENDELEA KUNISAPOTI , UKILIPA UNATUMIWA SIMULIZI HII INBOX WATSAPP AU UNAUNGANISHWA NA GRUPU , TUKO SEHEMU YA 72 KWA SASA , UTATUMIWA VIPANDE VYOTE MPAKA TULIPOSIHIA
NAMBA ZA KULIPA NI 0687151346 AIRTEL AU 0743015453 M-PESA AU 0657195492 TIGO PESA AU 0623367345 HALOPESA JINAA ISSAI SINGANO
UKILIPA TUMA MESEII YA MUAMALA WATSAPP NAMBA NI 0687151346