SEHEMU YA 151
Dorisi alikuja kushituka muda wa asubuhi kabisa ya saa moja , alijishangaa kwa kulala muda mrefu mno baada ya kuangalia saa, alikuwa akikumbuka mara ya mwisho jana alikuwa na Roma na alipotelea usingizini wakati wakiwa eneo la Sebuleni , hakutaka kufikiria sana kwani aliona ni lazima Roma alimleta hapo chumbani.
Aliangalia kulia na kushoto mwa chumba kama kulikuwa na dalili yoyote ya uwepo wa mtu , lakini hakuona dalili , alijinyanyua kivivu na kujikokota mpaka Bafuni ndani ya chumba hiko na kumaliza haja zake baada ya nusu saa na akatoka akiwa ameoga kabisa ,Dorisi hakuwa na utaratibu wa kwenda kazini ‘Overtime’ siku za jumamosi hivyo alipanga siku hio kushinda nyumbani.
Baada ya kujiweka sawa kwa kupaka mafuta kiasi usoni na kujifunga na taulo kubwa rangi nyeupe , alivaa visendo vya Manyoya rangi ya Pinki na kutoka ndani ya chumba hiko akielekea upande wa Sebuleni , alikuwa akihisi njaa , Dorisi hakuona utofauti ndani ya chumba chake ,kwani jana yake Roma alitoa picha ukutani na kushuka nayo Sebuleni.
“Hivi jana Roma hakuzima Tv kabla ya kuondoka?”aliwaza Mrembo huyu wakati akiwa anashuka na ngazi kwani alisikia kelele za sauti ya Televisheni.
Lakini alivyofika Sebuleni ni nje ya mategemeo yake kwani Roma alionekana akiangalia Runinga tena chaneli ya Aljazeera iliokuwa ikionyesha kwa kiarabu , Dorisi alishangaa kumuona Roma hajaondoka na kwa haraka haraka alimuona Roma alilala hapo ndani kwani alimuona alikuwa kifua wazi , kwa jinsi ambavyo Roma alikuwa akionekana ni kama baba mwenye nyumba.
“Roma...!!”Aliita Dorisi huku akimsogelea Roma aliekuwa amekaa kibosi kwenye masofa na kugeuka na kumwangalia mrembo Dorisi.
Dorisi na yeye alijikuta akimwangalia Roma kwa sekunde , mrembo huyu picha aliokuwa akiona kwa siku hio alitamani iwe endelevu , alikuwa akimpenda Roma sana na alitamani siku zote awe mwanaume wake , wawe wamefunga ndoa na kuishi pamoja na anachokiona asubuhi hio kiwe ni kitendo cha kudumu , yaani aamke asubuhi na amkute mume wake akiwa sebuleni kama hivyo akiangalia Runinga.
“Bebi Dorisi ..Mbona uniangalia hivyo,...njoo umkumbatie bebi wako”Aliongea Roma huku akitabasamu na Dorisi alimsogelea Roma na kwenda kumkumbatia kwa kupitisha mikono shingoni huku akikaa kwenye mapaja ya Roma na wakaanza kubusiana.
“Natamani ingekuwa hivi kila siku Roma”Aliongea Dorisi kwa sauti ya chini na kumfanya Roma amshike mabegani na kumwangalia usoni.
“Nini unataka iwe kila siku?”
“Kama hivi naamka na mwanaume ninaempenda anakuwa nyumbani.....Siku zote nimekuwa wa kuishi peke yangu najihisi mpweke mno kuishi kwenye hili jumba lote”Aliongea Dorisi kwa huzuni kidogo na kumfanya Roma atabasamu na kumshika Dorisi pua kama mtoto.
“Unachokiomba Dorisi hakiwezekani.. nadhani kabla ya mahusiano yetu kuanza ulishajua nina mke”Aliongea Roma na kumfanya Dorisi uso kubadilika lakini kwa Roma aliishia kutabasamu.
Roma aliona dawa pekee ya kuishi na hawa wanawake wote pasipo kuleta shida kwa upande wake ni kutowaahidi vitu vikubwa lakini pia kuwafanya wasifikirie vitu vikubwa zaidi ambavyo haviwezekani , yeye mwenyewe alijiambia katika akili yake kama Dorisi au mmoja ya wanawake aliokuwa nao wakiamua kumuacha, basi kiroho safi ataachana nao na hatozuia hata mmoja na kama watabakia kwake basi hivyohivyo atafanya juu chini kuhakikisha anafanya kile kilichokuwa ndani ya uwezo wake kuwafurahisha.
“Ila Dorisi hupaswi kuwaza sana , najua siwezi kukupa maisha unayotaka lakini naweza kukuahidi kitu kimoja......”Aliongea Roma huku akiwangalia Dorisi.
“Kitu gani?”
“Muda wowote utakaonihitaji nipigie simu na ntakuja mara moja labda kuwe na sababu ambayo ipo nje ya uwezo wangu”Aliongea Roma na kumfanya Dorisi kutabasamu , ukweli licha ya kwamba aliongea maneno hayo lakini aliona kwa upande wa Roma hayakuwa yakitekelezeka , hivyo aliona haina haja ya kuwa ‘Greed’ kwani kwanza mwanaume aliekuwa mbele yake alikuwa ameoa na hata mara yao ya kwanza kukutana alikuwa akilifahamu hilo , hivyo alitakiwa kuheshimu ndoa ya Roma na hata hivyo pia Roma alikuwa ni mume wa rafiki yake,hakutaka kujilinganisha na Edna lakini mwisho wa siku kila alipokuwa akimwangalia Edna juu ya urembo wake pamoja na mafanikio , aliona kushindana nae na kushinda ni ngumu sana na pia kwa upande wa Roma alionekana kutokuwa tayari kumucha Edna.
“Naenda andaa BreakFast”Aliongea Dorisi huku akinyanyuka na Roma alitabasamu huku akimshika Dorisi kalio na kuliminya kama Embe na kumfanya Dorisi alalamike na kumpiga kibao cha kimapozi na Roma aliishia kutabasamu huku akimsindikiza Dorisi kwa macho.
Baada ya kama nusu saa Roma na Dorisi walikuwa wakijipatia kifungua kinywa na Roma alionekana kuburudika , alijisemea moyoni kwamba kati ya wanawake wote aliokuwa nao ni mke wake pekee ambaye hakuwa akijua kupika , Dorisi na yeye alionekana kuwa mtaalamu kweli na hii ilimfanya Roma aone kweli kitendo cha Dorisi kuishi peke yake kimemfanya kuwa mpishi mzuri.
“Roma..Asante sana kwa kutoondoka jana”Aliongea Dorisi huku akimwangalia Roma.
“Bebi Dorisi nadhani baada ya hapa unapaswa kunieleza ni nini kinaendelea”Aliongea Roma na Dorisi alitingisha kichwa kukubali.
Basi walitumia nusu saa nzima kunywa chai , huku Roma akimwagia sifa Dorisi kwa kujua kupika na Dorisi alijisikia vizuri huku akimwahidi Roma kuja muda wowote ili ampikie chakula na Roma na yeye bila aibu aliitikia kuwa atakuwa anakuja mara kwa mara.
Dorisi alimuelezea Roma kila kitu kuhusu siku ya kwanza Abubakari Hamadi alivyoanza kumsumbua juu ya kadi ya benki aliokua akimiliki, kadi ambayo alikuwa ameachiwa na wazazi wake , alimuelezea Roma namna ambavyo Abubakari alimueleza kuwa kadi aliokuwa akimiliki ilikuwa ikitoa hela kwenye akaunti ambayo ilikuwa ikiingiziwa hela za biashara ya madawa ya kulevya , lakini pia mremabo huyo hakuacha kumuelezea Roma juu ya Taarifa chache alizopewa juu ya The Doni.
Dorisi pia alielezea namna ambavyo alivyoenda ndani ya Benki ya Uswisi kuangaia salio kujihakikishia maelezo ya Abubakari na Meneja Harrisi kumwambia kuwa haruhusiwi kuangalia Salio bali alikuwa na uwezo wa kutoa zaidi ya bilioni nne taslimu za Kimarekani,Dorisi pia alimuelezea pia Roma namna ambavyo wazazi wake walipotea.
Kwa maelezo ya Dorisi ni kwamba wazazi wake walipotea mara baada ya wao kuhamia jijini Dar Es Salaam , na kipindi ambacho walikuwa wakihamia ndani ya jiji hilo ni wakati ambao Dorisi alikuwa na umri wa miaka kumi na tano na ni mwaka 2010 na Dorisi alikuwa ndio anaanza kidato cha kwanza ndani ya shule ya Tanganyika , lakini jambo la kushangaza ni kwamba baada tu ya wiki moja kuisha baada ya kuhamia ndani ya jiji la Dar ndio wazazi waDorisi walipotoweka kwenye mazingira ambayo hayakueleweka , Dorisi alielezea siku moja kabla wazazi wake hawajapotea baba yake yaani Mzee Alex alimpatia hati ya jumba hilo ambalo alikuwa akiishi lakini pia pamoja na mama yake kumpatia kadi ya benki hio aina ya ‘Platinum Card’ kutoka benki ya Uswis na maelezo kidogo tu kwamba itamsaidia.
Maelezo yote ya Dorisi kwa iupande wa Roma yalimuacha na maswali , Roma alikuwa akijua juu ya ‘Black Card’ ambayo ilikuwa ikimilikiwa na Dorisi pamoja na Yan Buwen, kadi ambazo zote zilikuwa zikitoa hela kwenye akaunti yenye jina la Hegemoni , licha ya Roma kuwa na maswali mengi pamoja na Maelezo ya Dorisi ambayo hayakuwa na muunganiko hata kidogo na The Doni , aliona maswali ambayo anapaswa kumuuliza Dorisi yasiwe magumu na kumfanya Dorisi afahamu kama yeye alikuwa akijua kila kitu kuhusu kadi hio.
“So baada ya wazazi wako kupotea uliweza kuishi vipi peke yako?”aliuliza Roma.
“Sikuishi peke yangu , baada ya Baba na Mama kupotea niliishi na Mama Mdogo na aliondoka baada tu ya kuolewa”
“Na kuhusu mali ambazo mama yako na baba yako waliacha nini kilitokea?”
“Kuhusu mali mpaka sasa zipo chini ya familia ya ukoo wetu na zinasimamiwa na Baba Mdogo , nilichoachiwa na mama kikubwa ni hio kadi pamoja na hii nyumba na gari moja”Aliongea na Roma aliitikia kwa kichwa kukubaliana nae , lakini kuna kitu pia Roma alikumbuka na kunyanyuka na kusogelea picha aliokuwa ameifunika pembeni ya Tv na kuinyanyua na kumfanya Dorisi ashangae.
“Bebi unisamehe nilitoa hii picha chumbani kwako jana”Aliongea Roma na kumpatia Dorisi na Roma kuna kitu alikiona kwenye macho ya Dorisi wakati akiangalia picha hio, aliona hali ya huzuni.
“Dorisi hao wazungu ni wakina nani , haujawalezea kwenye maelezo yako?”Dorisi alimwangalia Roma kwa sekunde kadhaa na kisha akaiweka ile picha vizuri ili kumfanya Roma aone.
“Hawa walikuwa ni majirani zetu tulipokuwa Arusha,Huyu mama anaitwa Lucia na huyu Baba ni Luisi....”Aliongea Dorisi kwa sauti ndogo na alipofikia kwenye picha ya mtoto wa kike mrembo alitulia kidogo.
“Huyu ni dada yangu wa hiari, anaitwa Naira na ni mtoto wa hawa wazungu wawili “Aliongea Dorisi na kumfanya Roma kushangaa , kwanza maelezo ya kwanza ya Dorisi juu ya watu hao kuwa majirani zake yalimshangaza lakini pia yale maswali aliokuwa nayo kichwani juu ya mwanadada huyo aliekuwa kwenye picha kuonana nae aliona apotezee.
“Bado wanaishi Arusha?”
“Mh..!Hapana waliondoka Tanzania na kurudi nchini kwao , hii picha ilikuwa ni ya mwaka 2004 ilikuwa siku ya sherehe ya kuzaliwa kwangu,Nimemmisi sana Naira”Aliongea Dorisi na kumfanya Roma agundue kitu, Dorisi alionekana alikuwa na ukaribu mno na Naira.
“Inaonekana ulikuwa mkipendana sana?”
“Sana tulikuwa tukifanya mambo mengi pamoja na hata siku waliporudi nchini kwao nililia sana na hata Naira alilia sana”Roma hakuona haja ya kuendelea kuuliza maswali mengi , mpaka hapo hakuwa na kitu ambacho amepata kilichokuwa kikimuunganisha Dorisi na The Doni , lakini kadri kila alipokuwa akimwangalia Naira kwenye hio picha kuna jambo aliona halipo sawa kabisa , lakini kama ilivyokuwa kawaida yake , hakutaka kujiumiza kichwa sana , aliamua kupotezea baada ya maelezo ya Dorisi , lakinni jambo ambalo hakutaka kulipotezea ni juu ya wazazi wa Dorisi , kwa maelezo ya Diego na ya Dorisi aliona swala hilo anatakiwa kulitafutia ufumbuzi, kwani kama kadi ambayo Dorisi alikuwa akimiliki ilitolewa na mama yake , basi aliamini huenda kupotea kwao kunahusiana moja kwa moja na The Doni , lakini swali pia likabaki kwenye kichwa chake Roma , kama kweli wazazi wa Dorisi wana uhusiano wa karibu na The Doni kwanini wapotee, lakini pia aliona pia maelezo ya Dorisi hayakuwa sawa , kwani kwa maelezo yake , Roma aliona ni kama wazazi wake walikuwa wakijua kinachoenda kutokea, siku inayofuatia , kwani siku moja kabla ya kupotea ndio siku ambayo walimpatia Dorisi hati ya nyumba , lakini pia walimpatia kadi hio na hapo Roma aliona kuna jambo ambalo limetokea kwao na hilo ndio aliona kikosi chake cha The Eagles wanapaswa kufatilia.
SEHEMU YA 152
Roma alishinda siku nzima nyumbani kwa Dorisi na kufanya mambo mengi ambayo wapenzi hufanya na kwa Dorisi alijisikia furaha kuwa karibu na Roma tena tokea walivyotoka Japani.
Muda wa saa nane za jioni ndio muda ambao Roma aliweza kupata simu kutoka kwa Jestina akimuomba waonane siku inayofuuata yaani jumapili saa saba mchana , Roma alishangaa mualiko huo kutoka kwa Jestina, kwani hawakuwa na ukaribu ambao walipaswa kuonana , lakini Jestina alijitetea kwa kusema kuwa anataka arudishe fadhila kwa kile ambacho aliwafanyia kule Bagamoyo wakati wakienda kuoanana na Bladnina , na Roma hakuona haja ya kumkatalia mtu mzima aaetaka kuonana nae , kwani licha ya kauli ya Jestina kujitetea yeye alijua kuna jambo lingine ambalo mwanamama huyo alionekana kuhitaji kuongea nae.
“Sister unamuachaje mumeo kukaa nje ya nyumba mpaka muda huu?”Aliuliza Sophia , na kwa jinsi ambavyo alikuwa akiongekana ni kama yeye ndie alieolewa na hata Bi Wema aliliona hilo, na muda ambao Sophia alikuwa akiuliza swali hilo ilikuwa ni saa mbili za usiku na walikuwa mezani wakiendelea kula chakula cha usiku na mpaka muda huo Roma hakuwa amerudi nyumbani na hakuwa hata ametoa taarifa na Edna hakuona haja ya kumpigia , alijua Roma yupo kwa Dorisi na wanajiachia tu kwa raha zao na kila akifikiria hayo, roho yake ilimuuma na wivu juu , ni kwamba tu alikuwa akijikaza.
“Sophia kula ,Roma ni mtu mzima akijisikia kurudi nyumbani atarudi , hatupaswi kumchunga”Aliongea Edna kwa sauti kavu na kumfanya hata Bi wema amshangae Edna lakini hakutaka kuongea lolote na Sophia na yeye alitulia , hakutaka kuongea neno lolote.
“Miss mbona unaacha kula?”Aliuliza Bi wema mara baada ya Edna kuacha kula na kunyanyuka.
“Nimeshashiba Bi Wema”Aliongea Edna na kuanza kuzipandisha ngazi kuelekea juu , huku akiwaacha Bi Wema na Sophia katika hali ya mshangao , kwani Edna hakuwa amekula hata kidogo.
“Bi Wema unaonaje?”Aliuliza Sophia na kumfanya Bi wema atabasamu.
“Anaonekana kuwa na mawazo”
“Unadhani ni kwasababu ya Roma?”Aliuliza Sophia Kimbea na Bi wema alitabasamu huku akitingisha kichwa kukubaliana na Sophia , walionekana kuzoeana kweli.
Edna baada ya kuingia chumbani kwake macho yalitua kwenye Mdoli uliokuwa kwenye kitanda chake , aliuangalia kwa muda pasipo kueleweka anafikiria nini na kisha akaenda kukaa kitandani na kuchukua simu yake, lakini ni kama simu na yenyewe ilikuwa ikimsubiria aishike , kwani ilianza kuita na alipoangalia jina ni Roma, na haiikueleweka ni lini jina hilo lilikuwa limebadilishwa kwani mara ya mwisho alikuwa amemuandika kama Mbakaji , lakini leo hii Jina lilisomekaka kama ‘Roma’.
Edna aliacha simu iite kwa sekunde kadhaa na kisha kuipokea.
“Bebi Wife umeshindaje?”Ilikuwa ni sauti upande wa pili ya Roma.
“Safi”Aliitikia Edna kwa sauti ndogo.
“Nimekupigia nisikie sauti yako mke wangu”Aliongea Roma upande wa pili na kumfanya Edna ashindwe kujua ajibu nini , lakini mapigo ya moyo wake ni kama yalianza kwenda spidi.
“Sophia na Bi Wema wanauliza kwanini haurudi nyumbani..”
“Hehe.. Wife una uhakika ni Sophia ndio anaulizia?”.
“Kama huna chakuongea nakata simu”
“Okey! Wife nimekupigia kukutaarifu kuwa na leo sitorudi”
“Okey”
Alijibu Edna na kisha akakata simu , alionekana kuwa na hasria baada ya kuskia Roma tena hatorudi , ukweli mrembo huyo licha ya kwamba alijihisi bado hisia zake na Roma zilikuwa mbali , lakini kitendo cha wafanyakazi wake kumteka Roma kimapenzi aliona ni kama dharau kwake na ndio maaana siku nzima alikuwa na hasira , alikuwa na hasira na Dorisi ambaye alikuwa akijua kabisa Roma alikuwa ni mume wake lakini bado alikuwa akimng`ang`ania mpaka kumfanya asirudi nyumbani, lakini alikuwa pia na hasira na Nasra.
Edna aliweka simu chini na kuangalia mdoli uliokuwa kwenye kitanda kwa hasira na kisha akausukuma na mkono ukadondoka chini , lakini wakati huo huo mlango wake uligongwa na kumfanya anyanyuke na kwenda kuufungua , na aliekuwa mlangoni alikuwa ni Sophia.
“Naweza kuingia?”Aliuliza Sophia na Edna alitingisha kichwa na kurudi ndani na Sophia aliingia huku akifunga mlango kwa nyuma yake , Sophia licha ya kukaa kwa wiki kadhaa hapo ndani ya nyumba, hakuwahi kuingia kwenye chumba cha Edna licha ya kwamba vyumba vyao vilikuwa karibu , waliishia kuonana Sebuleni tu na kuongea na baada ya muda kila mtu angeenda kwenye chumba chake.
“Chumba chako kinapendeza”Aliongea kwa kusifia na kumfanya Edna amuangalie pasipo kuongea chochote alikuwa akijiuliza ni sababu gani ambayo imemfanya Sophia kuja kwenye chumba chake ,Sophia alisogea mpaka upande wa kulia wa kitanda na kuketi na macho yake yakatua kwenye mdoli uliokuwa umedondoka chini na Sophia baada ya kuuona tu alitabasamu na kuubeba kisha akamgeukia Edna.
“Kama sikosei huu mdoli amekupatia Bro Roma kama zawadi ?,Ni Mzuri”Aliuliza Sophia na Edna alimwangaliaSophia na kisha akauchukua ule mdoli na kuurudisha kitandani pasipo ya kumjibu.
“Sister Edna....”Aliita Sophia kama mtoto na kumfanya Edna amwangalie kwa namna ambavyo Sophia alikuwa akimwita.
“Unasemaje Sophia mbona huongei”
“Nimekuja kukupa mbinu”Aliongea Sophia na kumfanya Edna ashangae hakuelewa Sophia alikuwa akimaanisha nini.
“Mbinu za nini tena Sophia usiku wote huu”Aliongea Edna na kumfanya Sophia amwangalie Edna kidogo huku akigeuka na kukaa vizuri na kufanya mapaja yake kuonekana kwani alikuwa amevaa kijigauni chepesi
“Sister najua licha ya kwamba tumefahamiana kwa muda mfupi , lakini siku hizi chache tulizoishi nimejua mambo mengi yanayokuhusu na nikiri naendelea kukufahamu zaidi”
“Mh! na hizo siku ulizonifahamu uligundua jambo gani kuhusu mimi?”Aliuliza Edna kwa sauti kavu , alimuona Sophia kama mtu anaevuka mpaka na ndio maana aliweka sura ya usiriasi lakini Sophia hakujali.
“Sister unampenda sana Roma lakini haupo Romatic kabisa na ndio maana harudi nyumbani na kuishia kwe michepuko”Aliongea Sophia na kumfanya Edna awe mwekundu , sehemu ambayo ilimgusa zaidi ni hapo kwenye kumpenda Roma na Sophia aligundua mabadiliko ya Edna.
“Sister Edna bhana ... hupaswi kuonea aibu hisia zako”
“Nani kasema ninaonea hisia zangu aibu Sophia , una nini leo?”Ukweli ni kwamba licha ya Edna na Roma kulala vyumba tofauti lakini kwa upande wa Sophia hakuwa akijua kuwa wawili hao walikuwa wameoana kwa mkataba , aliekuwa akijua ni Bi Wema peke yake , lakini kwakuwa Sophia alikuwa mjanja na mwenye akili kuna kitu ambacho aligunda hakikuwa sawa baina ya Roma na Edna aliona kuna maigizo yanaendelea.
Kuhusu Sophia kwenda ndani ya chumba cha Edna ni pendekezo ,Bi Wema alimuona Sophia mjanja kuliko Edna na hivyo aliona kama atamtumia Sophia katika kumpa shule ya mapenzi Edna basi huenda mwisho wa siku Edna akawa mwepesi mbele ya Roma , hivyo kuwepo kwa Sophia ndani ya chumba cha Edna ni muendelezo wa misheni za Bi Wema juu ya kuwaunganisha Roma na Edna na waachane na mambo yao ya mkataba, lakini kwa upande wa Sophia pia alikuwa na mpango wake kichwani , yeye hakupenda kabisa Roma alivyokuwa na wanawake wengine jambo hilo lilimuumiza na kuona kama akiendelea kuzembea basi nafasi yake kama mkie wa pili wa Roma inaweza kuchukuliwa na wanawake wengine , hivyo aliona jambo pekee la kufanya kwa wakati huo ni kuungana na Edna ili kumdhibiti Roma asiifikirie michepuko yake.
“Sister hebu fikiria kwa uzuri huu ambao upo nao halafu mtu anasikia habari huko nje kama Roma anatoka nje ya ndoa , utajisikiaje Sister ?, Wewe unapenda tabia ya Roma kuondoka na kurudi muda anaotaka?”
“Sasa ulitaka nifanye nini wakati mtu mwenyewe kaamua kuwa na wanawake zake?”Aliongea Edna lwa sauti ndogo.
“Kwahio Sister unafikiri Bro Roma anajiamulia tu kulala na wanawake nje na kutorudi nyumbani kwa mkewe?”
“Sasa kama hajaamua unadhani kwannini mpaka sasa hivi hajarudi Sophia?”
“Hapo ndio unapo kosea dada yangu na ndio maana nasema haupo Romantic , Dada jifunze mbinu za kuhakikisha Roma haondoki , mimi najisikia vibaya”Aliongea Sophia na kumfanya Edna ashangae , alijiuliza inakuwaje mume ni wake yeye lakini aliekuwa akijisikia vibaya ni Sophia.
“Kwanini ujisikie Vibaya?”
“Sio picha nzuri kwa familia ndio maana najisikia vibaya , unaweza kuona ni jambo la kawaida ila watu wanaofahamu uhusiano wako na Roma wanaweza kumuona huko nje akiwa na wanawake , unafikiri ni picha gani itakayojitengeneza kwenye vichwa vyao?”Aliongea Sophia na kumfanya Edna amwangalie huku akifikiria , ni kweli pointi yake ilikuwa na mantiki Edna alifikiria ni watu wangapi mpaka muda huo alikuwa amewatambulisha kuwa Roma alikuwa mume wake, alijikuta akianza kuhesabu na kugundua ni wengi.
“Kwahio unataka nifanyeje?”Lilikuwa ni swali la Edna kwenda kwa Sophia na kumfanya Sophia aone kweli Edna alikuwa vizuri tu kwenye maswala ya biashara lakini likija swala la mapenzi alikuwa ‘Total Clueless’ lakini Sophia alitabasamu na kuona mambo yanakwenda kuwa rahisi.
SEHEMU YA 153
Ilikuwa ni siku ya jumapili asubuhi ndani ya familia ya Edna walionekana watu watatu wakiwa kwenye meza wakijipatia kifungua kinywa , aliwepo Bi Wema , Sophia pamoja na Edna , haikueleweka jana Sophia alimwambia mbinu gani Edna , ila Sophia na Edna walikuwa wakiangaliana na kisha kutabasamu.
“Bi Wema leo nitaenda na Sophia kutembelea watoto”Aliongea Edna na Bi Wema aliitikia kwa kichwa kuwa anakubali huku akitabasamu huku akimwangalia Sophia na kisha akamkonyeza pasipo ya Edna kuona,
Edna hakuwa akijua kuwa mbinu zote zilizokuwa akielezewa jana na Sophia zilikuwa ni mbinu ambazo zilikaliwa kikao na Jasusi mbobezi wa mapenzi Bi Wema pamoja na Sophia huku wakisaidiwa na Tamthilia waliokuwa wakiangalia kutengeneza Mbinu za kuhakikisha mwamba Roma anatulia na mke wake nyumbani.
Baada ya kumaliza kujipatia kifungua kinywa Edna na Sophia walienda kujiandaa kwa ajili ya kuelekea Kiwangwa kwa ajili ya kutembelea watoto yatima na kuwapelekea baadhi ya mahitaji kama ilivyo desturi.
Edna leo hii alikuwa na hamu ya kwenda Kiwangwa kutokana na kwamba alikuwa amemmisi sana Najma , alikuwa akitamani kuonana nae na kumuelekeza pia baadhi ya mambo ya upishi.
Baada kama ya lisaa kupita , hatimae Edna pamoja na Sophia waliokuwa wamependeza walishuka kutoka juu kwenye vyumba vyao wakiwa tayari kwa safari.
Bi Wema aliwaangalia na kisha kutabasamu na Edna ndio aliekuwa wa kwanza kutoka akimuacha Sophia nyuma.
“Bi Wema baadae”Aliongea Sophia kwa kutabasamu na kisha akatoka kuelekea nje na kuingia ndani ya gari.
Edna ndio aliekuwa akiendesha, na ndani ya dakika kadhaa tu walikuwwa washapotelea barabarani na kumuacha Bi Wema akisililizia mngurumo wa gari aina ya Pick Up.
Edna alikuwa ashaandaa baadhi ya mahitaji ya kwenda nayo kwenye kituo cha Son and Daughter Orphangea jana yake mchana , kwahio safari yao ilikuwa ni ya moja kwa moja, ndani ya madakika kadhaa tu, Edna alikunja kulia kuingia upande wa kituo hiki cha Son And Daughter.
“Sister kuna mtoto getini”Aliongea Sophia baada ya kumuona mtoto mdogo wa kike alievalia jezi ndogo mfano wa Singlend , kama zile za kuhcezea Basketbal na suruali ya Jeans, alikuwa ni mtoto wa rangi ya Chocolate rangi yake ya sura.
“Nimemuaona”Aliongea Edna huku akipunguza mwendo kabisa na kusimamisha gari na kisha kushuka , Edna alishangazwa na uwepo wa mtoto huyo nje ya geti na kujiuliza alikuwa akifanya nini , kwani geti lilikuwa limefungwa , hata Sophia na yeye alitoka kwenye Gari.
Yule mtoto aligeuka baada ya kuhisi kuna watu waliokuwa wakija nyuma yake na baada ya kugeuka aliwafanya Sophia na Edna kumuona Vizuri , alikuwa ni mtoto mzuri kweli kiasi kwamba Edna alijikuta akishindwa kuzuia tabasamu.
Lakini sasa katika hali ya kushangaza ni kwamba baada ya mtoto yule kumwangalia Edna , alimkimbilia na kumkumbatia kwenye miguu.
“Mom...!!!!” Ndio maneno alioyatamka yule mtoto na kumfanya Hata Edna mwenyewe ashangae na sio kwake tu hata kwa Sophia.
Baada ya Edna kuona mtoto huyo kamshikilia pasipo kumuachia ilibidi na yeye achutame chini.
“Hey! Mtoto mzuri unaitwa nani?”Aliuliza Edna huku akimwangalia mtoto aliekuwa mbele yake.
“Sister Unafanana nae”Aliongea Sophia huku akimwangalie Edna na mtoto huyo mdogo wa kike ambaye kimakadirio umri hakua chini ya miaka minne.
“Mom ,I don`t understand Swahili Language”Aliongea yule mtoto na kumfanya Edna atabasamu na kushangaa , hakujua kuwa mtoto aliekuwa mbele yake hakuwa akijua lugha ya kiswahili.
“What is your Name?”Aliongea Edna kwa kingereza
“My name is LanLan”Aliongea yule mdoto na kumfanya Edna atabasamu , mtoto aliekuwa mbele yake alikuwa akivutia kwa vitu vingi , sio kwa sura yake tu ya kitoto iliokuwa ikivutia , bali pia namna ambavyo mtoto huyo alikuwa akiongea alikuwa ni mtoto ambaye alikuwa na afya nzuri mno , kwani alikuwa mnene.
“Sister!! lanlan ni jina la kichina”Aliongea Sophia kwa kishwahili na kumfanya Edna ashangae kidogo.
“Lanlani kwanini upo hapa , wazazi wako wako wapi?”Aliuliza Edna kwa shauku huku akigeuza shingo kuangalia kama kuna mtu yupo na Lanlan na ni kweli ile anaangalia umbali kama wa mita ishirini hvi alionekana mwanamke aliekuwa akija Spidi Spidi upande wao , alikuwa ni mwanamke wa kichina kwa kumwangalia tu na hata Sophia alimuona.
“Lanlani..!”Aliita yule mwanadada kwa wasiwasi na kumshika Lanlani na kumtoa kwenye mikono ya Edna haraka haraka kama mtu anaemkinga mtoto na watu wabaya.
“Lanlan unajua ni kwa kiasi gani nimekutafuta kwaninni umekuja huku tena?”Aliongea yule mchina kwa lugha ya kingereza na kuwaacha Sophia na Edna wawaangalie , lakini kwa upande wa Lanlani macho yake yalikuwa kwa Edna muda wote.
“Aunti Qian.... Anafanana na mama”Aliongea Lanlan na kumfanya yule mdada wa kichina kuwaangalia wanawake waliokuwa mbele yake , alikuwa na wasiwasi sana kiasi kwmaba hata wanawake waliokuwa mbele yake hakuwa amewaangalia vizuri , alimwangalia Edna kwa sekunde kadhaa na kisha akainamisha kichwa kwa heshima na kumshika mkono Lanlan.
“Babu yako asharudi ,Turudi nyumbani”Aliongea yule mchina kwa kingereza na baada ya mtoto huyu kusikia babu yake karudi , alitoka mbio pasipo kuangalia nyuma na kuwafanya Edna na Sophia kutabasamu.
“Miss Lanlan, you must be careful. Don’t trip on… my gosh, my…”Yule mchina alionekana kuwa na wasiwasi mno kwani Spidi ambayo Lanlani alitoka nayo haikuwa ya kawaida , ni kama kuna mtu aliekuwa akikimbizwa na kumfanya yule mchina awe na wasiwasi.
“Ni kazuri”Aliongea Edna akimwangalia yule mtoto akitokomea kwenye macho yake upande wa juu barabarani wakiingia kwenye makazi ya watu.
“Sana..! Wazazi wake watakuwa na bahati kuwa na mtoto mzuti kama yule”Aliongea Sophia huku wakirudi kwenye gari na kupiga honi kuingia kituoni.
Upande mwingine baada ya yule Mchina na Lanlani kufika upande mwingine mita kadhaa kutoka kwenye hiko kituo , waliingia kwenye nyumba moja ambayo ilionekana kuwa mpya , kwani hata mazingira ya nje yaliashiria watu waliokuwa wakiishi hapo hawakuwa na muda mrefu kwani kuna michanga ambayo ilikuwa imejazana kwa mbele.
Sasa Lanlani baada ya kufika ndani ya hii nyumba alipitiliza moja kwa mooja mpaka ndani ya sebule ambayo haikuwa na masofa zaidi ya viti peke yake na meza ...
“Grandpaaa...”Aliongea Lanlani na kuchomoka kwa Spidi na kwenda kumrukia mwanaume mmoja hivi wa makamo ambaye kama ungemuona ungeshangaa kwanini Lanlani alikuwa akimwita mwanaume huyo babu na sio baba , licha ya Mwanaume huyo kuwa Mchina , lakini alikuwa bado na umri wa ujana unaofikai ukingoni , alikuwa sio chini ya miaka Therathini na sita.
“Lanlan, you didn’t bully other kids again, did you?”
“Lanlani huajawachokoza watoto wengine tena si ndio?”Aliuliza babu yake Lanlan.
“Grandpa, there’s this aunty who looks just like my mom”Aliongea Lanlani akimaanisha kwamba kuna mwanamke mmoja ambaye anafanana na mama yake na kumfanya huyu mzee kushangaa na kumgeukia yule mwanamke wa Kichina , ni kama alikuwa akitaka maelezo kutoka kwake.
“Sir, Miss Lanlan saw a really pretty woman`s over at the gate of orphanage and thought she looked just like her mother.”
“Sir Lanlan alimuona mwanamke kwenye nje ya geti la kituo ambaye anafikiri anafanana kama mama yake”Yule Mzee baada ya kuambiwa maneno hayo , alimwangalia Lanlan kwa muda.
“Lanlan, Grandpa understands that you miss your mother. But I’ve said time and time again, your mother has gone to a faraway place and cannot return. As for your dad, when the time is right I’ll take you to meet him. When that day comes, you will have a father and mo...”
“Lanlan Babu yako naelewa umemkumbuka sana mama yako , lakini nimekuwa nikikuambia mara nyingi kuwa mama yako ameenda sehemu ya mbali sana na hawezi kurudi na kuhusu baba yako nitakupeleka ukakutane nae muda ukiwadia , hio siku ikifika utakuwa na baba pamoja na ma..”
“Lanlan has a mummy, and Lanlan’s mummy will never leave Lanlan alone!”Aliongea yule mtoto kwa namna ya kuamrisha kwa kukasirika na sauti kubwa na kumfanya yule mchina kumwangalia Lanlan kwa sekunde
“Alright, alright, Lanlan’s mummy will surely come back. It’s Grandpa’s fault this time.”
“Haya sawa ,Mama wa Lanlani ni hakika atarudi nimekosa mimi babu yako”Aliongea Yule mchina na kumfanya yule mtoto kutabasamu.
“Lanlan, we’re going to stay here in Tanzania from now on. How are you liking it?”Lanlan tutaishi hapa Tanzania kuanzia leo , umepapenda?”
“Grandpa, you said you were going to take me to meet Daddy. Now that we’re staying here, does this mean Daddy is here?”
“Banu umesema unaenda kunikutanisha na baba , kwasababu sasa hivi tunaishi hapa , ni kwasababu baba na yeye anaishi hapa?”
“Oh, you little....”Aliongea huyu mzee kwa kukosa maneno , kwani kila akiongea hivi Lanlani alikuwa akimjibu hivi na muda wote alikuwa akimuwazia baba yake tu.
“Then why won’t you take me to see Daddy?”
“Sasa kwanini hunipeleki kumuona baba?”Aliongea Lanlani na kumfanya huyu Mchina kuvuta pumzi na kuzitoa na kumwangalia Mjukuu wake ambaye hakuwa akifanana nae hata kidogo kutokana na rangi yake.
“Oh Lanlan, Grandpa will do what’s best for you and your dad too. That means that there will be some waiting to do on your part, alright?”
“Oh Lanlani Babu yako nitahakikisha nafanya kile unachotaka na kwa baba yako pia , hivyo unapaswa kuwa na subira kabla sijakamilisha jambo lako , Sawa?”Aliongea yule mzee huku akishika nywele za Lanlani na mtoto yule aliitikia kwa kichwa kukubali
SEHEMU YA 154
Ni muda wa saa Saba za mchana Roma Ramoni alionekana akiegesha gari yake ndani ya hoteli ya Landmark , Roma alikuwa ndani ya hoteli hio kwa ajili ya kutii wito wa kuonana na mke wa Tajiri Azizi.
Baada ya kutoka kwenye gari alipiga hatua kuingia moja kwa moja ndani ya hoteli hii upande wa mgahawa , kwani ndio alivyopewa maelekezo na Jestina, na kweli ile anaingia tu ndani ya mgahawa huu wa kisasa uliokuwa ndani ya hoteli hii kubwa ya nyota tano , alimuona Jestina akiwa ameketi peke yake upande wa kulia nyuma , lakini nyuma yake akiwepo mwanamke mwingine ambaye roma hakuweza kumtambua, alikuwa ni Mama Theresia na haikueleweka kwanini hakuwa amekaa meza moja na Jestina.
“Nimechelewa sana?”Aliuliza Roma baada ya kumfikia Jestina na kuvuta kiti na kukaa.
“Hapana ndio kwanza nimefika”Alionngea mke wa Tajiri Azizi na muda huo huo alikuja muhudumu kwa ajili ya kuchukua oda yao na kwakua ilikuw ni mchana ya saa saba Roma aliagiza Ugali na Samaki pamoja na juisi na jestina akaagiza Pilau na mhudumu akaondoka,Jestina muda wote alikuwa akimuangalia Roma na hatra Toma aliligundua hilo.
“Roma mara ya mwisho