singanojr
JF-Expert Member
- Sep 24, 2020
- 1,974
- 10,361
- Thread starter
-
- #1,021
SEHEMU YA 188
Edna alionekana kuwa na hasira , alionekana alikuwa na mambo mengi ambayo alikuwa ameyaweka moyoni muda mrefu , mrembo huyu kama ilivyokuwa tabia yake , tabia ya kutopenda kuuliza , lakini pia tabia ya kutopenda kujielezea ilimfanya kuficha mambo mengi sana na kuyakalia kimya , kwa mfano Edna tokea anafika Ufaransa alikuwa akifikiria swala la Roma Kwenda kujitambulisha nyumbani kwa Nasra, lakini swala lingine Edna alikuwa akifahamu Roma alichokifanya mara baada ya kupotea kwake , siku ambayo alienda kupigana na Ares na baada ya kurudi akaenda kuua watu wa kundi la Fupa Faru kwa ajili ya Rose, mambo yote hayo Edna yalikuwa kwenye moyo wake na hakuyatafutia maelezo kabisa licha ya kuyafahamu, wala kutaka kuuliza Zaidi ya kukaa kimya, lakini mbaya Zaidi ni baada ya kumuona mwanamke akitoka kwenye chumba cha Roma asubuhi, Edna alijiambia Roma hakuwa siriasi na yeye na alikuwa akimchukulia kabisa kama mwanamke wa mkataba pekee ndio maana anafanya mambo anavyotaka hata kumuahidi Nasra Kwenda kujitambulisha ukweni .
Roma mwenyewe alishangaa , hakuwa akifahamu kama Edna alikuwa akijua kama aliua watu wa kundi la Fupa Faru kwa ajili ya Rose, alijiuliza ni mambo mangapi Edna alikuwa akiyajua na ameyakalia kimya.
Lakini alijiambia huenda Edna pointi yake ni ya msingi , alijiuliza kama Edna atajua ukweli wote wa Maisha yake ya nyuma ni kipi ambacho angefanya ,Je angekuwa na furaha na kumkumbali yeye kama mume na kujitoa jumla jumla kwake , hilo ni moja ya maswali mengi yaliopita katika kichwa cha Roma.
“Edna maneno yako yanaumiza”Aliongea Roma na kumfanya Edna amwangalie Roma na kisha kuvuta pumzi ndefu kama mtu ambaye anakusanya ujasiri.
“Kama kweli unapenda nikuulize , basi naomba nikuulize swali moja tu”Aliongea Edna
“Unaweza kuuliza?”alijibu Roma.
“Niambie kuhusu Seventeen?”Aliongea Edna na kumfanya Roma ashangae hapo hapo na kujiuliza Edna aliwezaje kujua hilo jina,kwani katika kumbukumbu zake hakuwahi kulitamka , lakini katika kufikiria hapo hapo jina la Clark liliibuka katika kichwa chake , aliamini kama Edna amejua hilo jina basi ni kupitia Clark.
*******
WIKI KADHAA NYUMA
Ni siku ambayo Edna alikuwa hospitalini , siku ambayo Roma , Sophia na Profesa Clark walienda kumtembelea Edna baada ya kupewa taarifa ya Edna kudhirai akiwa ndani ya hoteli ya Paridise siku ambayo aliweza kugundua kuwa baba yake mzazi ambaye alikuwa akimchukia kwa miaka mingi alikuwa sio baba yake mzazi.
Sasa muda huu wa jioni wakati Roma anaongea na simu nje mpaka kusimamishwa na Queen baada ya kugongana nae , upande wa ndani Sophia Edna na Clark walikuwa wakiongea.
“Edna nikiri kwamba unafanana kila kitu na Seventeen”Aliongea Profesa Clark na kumfanya Edna kushangaa , kwani ilikuwa ni mara yake ya kwanza kusikia hilo jina na sio kwake tu hata kwa Sophia.
“Profesa!, Seveenteen ni nani?”Aliuliza Edna na kumfanya Clark kushangaa na mpaka hapo alijua ameropoka neno ambalo hakupaswa kuongea , maana kama Edna hakuwa akimjua Seventeen, basi ni hakika kwamba Roma hakuwa amemueleza Edna juu ya jambo hilo.
Sophia ilibidi waangaliane na Edna na kisha wakageuza macho yote kwa Profesa Clark wakitaka maelezo ya kumjua Seventeen ni nani.
“Jamani kama hamumjui Seventeen basi naamini Roma hajawaambia bado na naamini anayo sababu ya kutofanya hivyo”
“Profesa tuambie Seventeen ni nani?”Aliongea Sophia huku akimshika mkono Profesa Clark ili kueleza Seventeen ni nani.
“Edna naamini siku moja Roma atakwambia kuhusu Seventeen kwa undani Zaidi , ninachoweza kukuambia tu ni kwamba Seventeen ndio mwanamke pekee ambaye Roma aliwahi kumpenda sana.. Sijui nini kilitokea ila kwa maelezo ya Roma Seventeen alijiua akiwa mjamzito”Aliongea Profesa Clark huku akionyesha kujutia kwa kitendo chake cha kuropoka mbele ya Edna.
“Kwanini alijiua?”Aliuliza Sophia. Na kumfanya Edna amwangalie Clark.
“Kuhusu hilo sifahamu ,jamani najua sikupaswa kuwaambia juu ya hili ,Roma akijua nimewaambia anaweza kukasirika, naombeni msiongee chochote kwa sasa mpaka atakapotaka kuwaambia yeye mwenyewe”Aliongea na kuwafanya Sophia na Edna watingine vichwa kubaki na siri hio moyoni.
Na hata pale Roma aliporudi ndani ya chumba alicholazwa Edna hakuweza kuona mabadiliko ya aina yoyote , Zaidi ya Edna na Sophia kumuangalia.
Sasa hii ndio siku ambayo Edna alipata kujua jina la Seventeena kwenye Maisha ya Roma , lakini licha ya mrembo huyu kupata kujua kuna mtu anaeitwa Sventeen kwenye Maisha ya Roma , hakuwa tayari kumuuliza Roma juu ya huyo mtu na kukaa na jambo hilo moyoni.
“Sipo tayari kuona mwanamke wa pili anapoteza uhai
kwa ajili yangu”Edna alikumbuka hio kauli ya Roma , siku ambayo alionana kwa mara ya pili na Roma na kupendekza swala la Roma kumuoa na pale Roma alipokataa na kutishia kujirusha na ndio Roma alipomzuia na kutamka kauli hio.
Edna baada ya kuunganisha matukio aliamini huenda maneno hayo yalikuwa yanamhusu Seventeen, lakini kama kawaida ya Edna hakuuliza , alilihifadhi moyoni.
*******
Taswira ya mto Seine ndani ya siku hii ilionekana kuvutia macho ya wengi waliokuwa wamekaa kandokando yake ,ni mto ambao umezungukwa na miti mikubwa aina ya London Platanus, miti iliogubikwa na majani ya kijani kibichi na manjano , huku kila upepo unapovuma juu ya miti hii hufanya majani ya manjano kupeperuka , kuna yale yaliokuwa yakitua kwenye reli na kuna yale yaliokuwa yakienda moja kwa moja ndani ya mto, Roma alikuwa ni moja ya watu waliokuwa wakiangalia namna majani hayo yalivyokuwa yakipeperushwa , huku akionekana kuingia kwenye mawazo, huku Edna akiwa upande wake wa kulia akiwa anasubiria jibu.
“Kwahio ushamfahamu tayari?”Aliuliza Roma.
“Vipi!,unaonekana haujapenda nilipotaja hilo jina , huenda nisingepaswa kukuuliza” Aliongea Edna.
“Sidhani kama napaswa kushangaa juu ya hilo,naamini Clark ndio kakuambia”
“Alitamka hilo jina tu , huku akianiambia nafanana kwa asilimia kubwa na mtu anaefahamika kwa Seventeen , hakunipa maelezo mengine , nataka nisikie kutoka kwako kuhusu Seventeen , lakini kama haupo tayari kuniambia usijilazimishe”Aliongea Edna.
“Nadhani sipaswi kukuficha juu ya hilo, ni mambo yaliopita na kila mtu katika Maisha lazima awe na kumbukumbu za maisha yaliopita , sio swala la mtu kuona aibu kuwa na kumbukumbu za nyuma , ziwe za kusikitisha au za kufurahisha,kuhusu Seventeen sidhani kama nitakuja kumsahau kwenye Maisha yangu na angalau imekuwa vyema umeweza kumfahamu kupitia Clark”
“Bado unampenda?”Aliuliza Edna.
“Mapenzi!, Sina uhakika kama bado nampenda au lah,Nimejuana na Seventeen miaka Zaidi ya ishirini na mbili iliopita kabla sijarudi Tanzania , Seventeen kwangu alikuwa ndio kila kitu , alikuwa ndio sababu ya mimi kuishi licha ya kupitia kipindi cha maumivu makali nikiwa katika utoto wangu , kila nilipofikiria kukata tamaa na kumwangalia Seventeen ambaye bado alinihitaji nilipata nguvu upya , hatukuwa wapenzi kwasababu hatukuwahi kutongozana na kuambiana tunapendana wala kupeana zawadi , muunganiko wetu ulikuwa ni Zaidi ya wapenzi , ,Seventeen alinihitaji ili aishi na mimi nilimhitaji vilevile ili niweze kuishi,huenda ningemwambia kama nampenda na akawa mpenzi wangu , huenda asingechukua maamuzi ya kijinga alioyafanya… Seventeen ni mwanamke wa kipekee sana kwenye Maisha, aliebaki katika kumbukumbu zangu…”Roma alijikuta akiishia njiani , kwa mara ya kwanza aliongea pasipo kuwa na tabasamu kwenye macho yake, huku macho yakiwa mekundu mno , ilionesha Maisha alioishi na Seventeen yalikuwa ya kuumiza sana , kiasi kwamba hakutaka kabisa kukumbuka yaliowatokea, Edna na yeye alijihisi moyo kuuma kwa jinsi Roma alivyokuwa akiongea.
“Umeuliza kama na mpenda! , kwangu Seventeen sikuwahi kumtamkia neno nampenda hata siku moja na yeye hakuwahi kuniambia ananipenda, tulizungumza maneno machache sana kuhusu mapenzi , vitu tuulivyongea ni namna ya kuweza kushinda kiza kilichokuwa mbele yetu , kwangu kuwa karibu yake ilikuwa ni Faraja, ukiniuliza kama nampenda ukweli sijui namna ya kujibu hilo swali”Aliongea Roma.
“Clark alisema nafanana nae kwa kiasi kikubwa , hilo ni kweli?”
“Ndio mnafanana kwa asilimia kubwa sana na Seventeen , ila utofauti wenu ni kwamba wewe ni mtembo Zaidi kuliko Seventeen , usisikilize maneno ya Clark , hana anachojua kuhusu Seventeen Zaidi ya kuona picha yake tu”Aliongea Roma.
“Kwahio unavyoniona kwako unanichukulia kama mbadala wa Seventeen?”Aliuliza Edna na kumfanya Roma kushangaa kidogo.
“Seventeen ni Seventeen na wewe ni mke wangu kwa sasa, Seventeen kwangu amebakia kuwa kumbukumbu nisizoweza kuzisahau, kama ningekuwa nakuchulia kama Seventeen nisingejali hisia zako”Edna alionekana kuridhishwa na jibu alilipewa na Roma.
“Unakumbuka mara yangu ya pili na wewe kukutana ndani ya hoteli , wakati nilivyokuambia kuwa nataka unioe na ukanikataa , na hata pale nilipolazimisha kujirusha kwenye lile jengo ukabadilika ghafla na kunizuia, nahisi ile siku nilikukumbusha kuhusu Seventeen , ndio maana ulikiubali kunioa”Roma alifikiria kidogo , ukweli siku ile ni kweli kitendo cha Edna kutaka kujirusha kwenye lile jengo la hoteli kilimrudishia kumbukumbu za nyuma juu ya kitendo alichokifanya Seventeen.
“Siwezi kupinga , ulinifanya nikumbuke kilichotokea miaka ya nyuma ndio maana nikakubaliana na wewe , lakini hata hivyo sijawahi kukuchukulia kama mbadala wa Seventeen”
“Kama ni hivyo basi naamini ninapaswa kushukuru uwepo wa Seventeen kwenye hii dunia, kama sio yeye huenda Maisha yangu mpaka sasa yangekuwa yashabadilika , huenda baba yangu mzazi angeniua , lakini pia hunda ningekuwa kwenye Maisha ya ndoa na mtu nisiekuwa nikimpenda…”Aliongea Edna na kuishia njiani huku akianza kulia na kumshangaza Roma na kumfanya ageuze macho kuangalia watu waliokuwa ndani ya eneo hili , kwani aliogopa watu wakishuhudia Edna akilia mbele yake,aliamini Wazungu wangemshangaa kwa kumfanya mwanamke mrembo kama Edna kulia na alishukuru uwepo wa Sauroni , kwani watu walikuwa wametawanyishwa.
“Edna nyamaza basi , kama kuna sehemu hujaridhika na majibu yangu niambie”Aliongea Roma , huku akishindwa ni hatua gani azichukue kwa wakati huo , siku zote amemzoea Edna kuwa kauzu na mtu wa kuficha hisia zake , lakini mabadiliko ya leo ya Ghafla yamemfanya kushangaa kidogo.
Licha ya Edna kumwambia Edna anyamaze , lakini Edna hakunyamaza Zaidi ya kuangalia chini na kudondosha machozi.
“Edna nishasema wewe ni Edna na Seventeen ni Seventeen, Sijui unafikiria nini lakini sijui cha kufanya kwenye hali uliokuwa nayo”Aliongea Roma na Edna alinyanyua kichwa chake na kumwangalia Roma.
“Clark aliniambia kuwa Seventeen alikuwa na ujauzito wako, Ni kweli?”Aliuliza Edna na Roma alitingisha kichwa kukubali.
Ukweli kwa upande wa Roma hakupenda kukumbuka tukio la miaka kadhaa iliopita , kitendo cha Seventeen aliekuwa na ujauzito wake kujirusha kwenye bahari iliokuwa imejaa mabarafu ,tena mbele yake kilikuwa ni cha kuumiza sana na kwake ndio sababu nyingine iliomfanya Roma kuchukulia wanawake kama chombo cha Starehe , Alikuwa akitumia wanawake kwa ajili ya kujipoza na maumivu , lakini maumivu hayakupita na kadri maumivu ya moyo yalivyozidi kumuendesha ,ndipo tatizo lake la ubongo kuwa kubwa Zaidi , Profesa Clark alijaribu kumsaidia Roma ili aweze kupunguza mawazo , lakini alishindwa kabisa na kuogopa mno na kushindwa kujua cha kufanya, na hata pale Roma alipompa taarifa ya kuondoka nchini hakuwa tayari , lakini pia hakuweza kumzuia Roma.
Hivyo ndio ilivyokuwa, moja ya sababu kubwa ya Roma kurudi Tanzania , aliamini kwa kuishi Maisha ya kawaida , huenda ingekuwa rahisi kwake kumsahau Seventeen na hata pale aliporudi nchini hakuwa tayari kujihusisha na wanawake kabisa , kwani aliona wanawake hawakuwa wakimsaidia Zaidi ya kumfanya kumkubuka Sevcenteen.
“Kama ni kweli Seventeen alikuwa na ujauzito wako , naomba nikuulize swali la mwisho”
“Okey unaweza kuuliza”
“Kama Seventeen yupo hai na akajitokeza kwako , akiwa na mtoto wako na yupo tayari kwa ajili ya kuanza upya na wewe ,je utaendelea kuwa na mimi au utaenda kwa Seventeen?”
“Nyamazaa….!!!!”Aliongea Roma kwa sauti kubwa na mwonekano wake ulibadilika palepale na hata macho yake yalibadilika na kuwa ya kijani.
SEHEMU YA 189.
Edna licha ya Roma kubadilika , alionekana kutohofia kitu chochote , alimwangalia Roma pasipo hata ya kupepesa macho na alionekana alitaka jibu lake licha ya Roma kubadilika.
“Seventeen….. Seventeen na mtoto wake walishakufa zamani na sitaki tena kusikia ukilitamka hilo jina mbele yangu”Aliongea Roma kwa sauti isio ya kawaida.
“Huna haja ya kuzificha hisia zako, unaonekana kabisa kwenye moyo wako unashindwa kututofautisha mimi na Seventeen , ndio maana unaonesha kunijali na kutaka kunilinda”Aliongea Edna huku akiangaliana na Roma kwenye macho, pasipo ya kuogopa kabisa , ni kama mtu aliekuwa akijiambia licha ya Roma kubadilika asingeweza kumdhuru..
“Edna nakuambia kwa mara nyingine kaa kimya”Roma aliongea huku akimsogelea kabisa Edna karibu kama mtu ambaye anajaribu kumuogopesha kwa muonekano wake.
Roma mwenyewe alishindwa kujielewa kwanini alikuwa na hasira za namna hio, baada ya Edna kutaja jina la Seventeen mfululizo.
“Roma acha kujidanganya, ninachojua huwezi kunitofautisha mimi na Seventeen na unajishawishi tu kusema kama sisi ni tofauti , ila unafanya hivyo kwa ajili ya kujipozapoza maumivu yako yakuachwa ,hukutaka kuwa na mwanamke mwingine kwasababu ulihisi utakuwa dhaifu ,kutokana na kumbukumbu za Seventeen na kwako mimi ni kama kitulizo cha mateso yako, Kama kweli unaweza kunitofautisha na Seventeen kwanini ukaamua kumuacha Rose , mwanamkie ambaye naamini anakupenda na wewe unampenda na kukubali kuoana na mimi ambaye kwangu ninachojali zaidi ni kazi , sikuwahi kukupa hata nafasi ya kuingia kwenye chumba changu wala kuonyesha ishara yoyote ya kukupenda upo na mimi kwasababu nafanana na Seventeen huo ndio ukweli.
Maneno ya Edna yalikuwa ni makali kiasi kwamba yalikuwa yakipita kwenye masikio ya Roma kwa kujirudia rudia na kumfanya kichwa chake kuanza kuuma.
“Edna tafadhari , nakuomba uache kuongea tena kuhusu Seventeen”
“Nisamehe kama maneno yangu yanaonekana kuwa makali , lakini huo ndio ukweli haukuwahi kunichukulia mimi kama mimi , najua ni mengi umenisaidia kwa muda mfupi tuliokuwa Pamoja , lakini tokea siku Clark aliponiambia kuhusu Seventeen , nilikuwa nikiwaza sana , haikuwa rahisi kwangu kama unavyofikiria na angalau leo hii nimeweka wazi kile kilichopo ndani ya moyo wangu”Aliongea Edna ila kwa upande wa Roma alishindwa kujibu chochote , aliona anaweza kushindwa kujizuia muda wowote ndio maana akaugeukia mto.
“Mimi nishamaliza na narudi ndani kuendelea kuangalia maonyesho , kama hujisikii kuungana na mimi unaweza kurudi kupumzika ila naamini pia rafiki yako yupo hapa kwa ajili ya kuongea na wewe”Aliongea Edna na kujiweka sawa na kuanza kupiga hatua kurudi ndani.
Edna licha ya kujiweka sawa , lakini macho yake hayakujificha kama alikuwa akilia , Stern na Alice waligundua pia hilo , ila hawakutaka kuuliza lolote na kuendelea kuangalia mbele.
“Miss Edna tunaweza kuanza tukio?”Aliuliza Meneja na kumfanya Edna amwangalie.
“Kwanini unaniuliza mimi?”
“Tulikuwa tukisubiri uwepo wenu ndio tuanze”Aliongea Meneja.
“Mnaweza kuanza tu , kilichotokea hapa ni maswala binafsi”Aliongea Edna na Meneja alitabasamu na kisha kuinamisha kichwa chake kwa heshima na kusogea jukwaani na kumnong`oneza mshereheshaji kuanza tukio.
Upande wa nje Roma alitulia kwa dakika kama mbili hivi mpaka alipoinua mkono wake na kumpa ishara Sauroni ya kumsogelea na Sauroni alifanya hivyo.
“Sauron, I’m going to ask you something, be honest with me.”
“Sauroni nitakuuliza kitu na naomba uwe mkweli na mimi”
“Your Majesty Pluto, I never lie.”
“Mfalme Pluto , Mimi sidanganyi”
“Tell me then, in your eyes, am I someone who will cower in the face of my own weaknesses…”
“Hebu niambie kwenye macho yako ,naonekana kama mtu ambaye naweza kuogopa kudili na udhaifu wangu”
“Mfalme Pluto ijapokuwa mimi ni mshirika wako , lakini kwa umri wako naamini hilo swali ni la kitoto”Aliongea Sauroni na kumfanya Roma kucheka.
“Kwa kauli hio naamini Swali langu ni la kijinga”
“Mfalme Pluto ninachoamini ni kwamba muda mwingine inakuwa ngumu kwa mtu kuutambua uongo na ukweli , ila ilimradi unaweza kutambua kusudio halisi ndani ya moyo wako basi hupaswi kujiuliza maswali , Nguvu ya kweli haitegemei nguvu ya kimwili bali ni ule uwezo wa kukabiliana na matatizo na kuyatafutia ufumbuzi”
“Haha.. Sauroni nadhani kweli swali langu lilikuwa la kipumbavu , ulichoongea ni sahihi , kama kweli nina uwezo wa kukabiliana na matatizo yangu , kuwa imara au dhaifu sio swala la kujionea aibu”Aliongea Roma na Sauroni alitabasamu baada ya kuona mapokeo ya Roma.
“Mheshimiwa Pluto,Sidhani kama unataarifa juu ya mkutano wa siri wa Kimataifa unaofanyikia hapa Paris chini ya DGSE?”Aliuliza Sauroni na kumfanya Roma kushangaa.
“Mkutano wa siri?” Sijawahi kusikia juu ya hilo Sauroni”
“Nadhani umechelewa tu kupata taarifa juu ya huu mkutano Mfalme Pluto , kiufupi ni kwamba huu ni mkutano ulioandaliwa na Serikali ya Ufaransa na unahusisha , mashirika ya kijasusi , Vikosi maalumu na baadhi ya mashirika pia yanayotumia nguvu za ziada na kwa kile tulichogundua ni kwamba moja ya ajenda za mkutano huo pia unahusika”
“Unamaanisha nini Sauroni kama nahusika?”
“Your Majest!, “It’s about the gods”
“Kwanini kikao kiwe ni kwasababu ya The Gods Sauroni”
“Mfalme kwa maelezo ambayo hatuna uhakika nayo ni kwamba Mataifa ya Ulaya Pamoja na Marekani wanajiandaa kuingia Vitani na Appolo, licha ya kwamba ni tetesi tu kwa sasa , ila naamini kuna jambo kubwa linaendelea”
“Sauroni sijafautalia maswala haya kwa muda mrefu kidogo”
“Ndio Mfalme Pluto ,Tokea umerudi nchini Tanzania , Appolo Pamoja na jeshi lake waliweza kushambulia baadhi ya kambi za kijeshi za Urusi , EU pamoja na NATO, lakini mbaya Zaidi ni kwamba Appolo ameenda mbali na kuanza kuandikia barua za vitisho baadhi ya viongozi wa kubwa wa nchi , akiwemo Raisi wa Ufaransa, , Kwa taarifa tulizopata ni kwamba Appolo pia amehusika na kuteka baadhi ya matajiri wakubwa waliohudhuria maonyesho ya Fasheni hapa Paris”
“Sauroni hata mimi pia pamoja na mke wangu ni moja ya wahanga wa tukio hilo”Aliongea Roma na Sauroni akatabasamu.
“Sikudhani Umeweza kukutana na mkasa huo Mfalme Pluto , Nimefika hapa kwa ajili ya kumuona Madam Persephone lakini pia kulizungumzia swala hili”
“Haha.. Sauroni hebu niambie kwanza mmeweza kumfahamu Appolo mpaka sasa hivi?”Sauroni alitingisha kichwa akimaanisha Hapana.
“Mfalme ninachotaka kukuambia ni kwamba kwenye mkutano utakaofanyika siku ya kesho licha ya ajenda kuu ni juu ya kutafuta namna ya kumuangamiza Appolo na kundi lake , lakini pia kuna swala ambalo linahusiana na wewe?”
“Swala gani tena Sauroni?”
“Ni juu ya majadiliano juu ya umiliki halali wa teknolojia iliotumika kutengenezea siraha aliopoteza Mfalme Pluto wa kwanza”
“Sauroni unamaanisha Thanatos!?”Roma alishangaa , alikuwa akijua sana juu ya Teknolojia iliokuwa imepewa jina la Thanatos , Teknolojia ambayo ilivumbuliwa na wanasayansi kutoka kisiwa cha wafu na mfalme Pluto wa kwanza kabla hajamrithi.teknolojia ambayo ilikuwa ikifanyika kwa kucheza na DNA za mwili na kumfanya mtu kuwa kama sumu kwa Maisha ya binadamu , kwani kama mwili wako utatengenezwa kwa tekonolojia hio basi utakuwa hata na uwezo wa kumuua mtu kwa kumgusa tu ndio maana ikaitwa kwa jina la Thanatos.
Sasa kwa kumbukumbu za Roma ni kwamba, Mfalme Pluto wa kwanza alipoteza kanuni za kutengeneza siraha hio , huku mwanasayansi aliehusika na utafiti kufariki .
“Ndio mfalme Pluto ,kwasasa taarifa zinaonyesha teknolojia hio ipo chini ya Serikali ya Ufaransa na Appolo ni moja ya watu wanaotaka hio teknolojia kwa nguvu ndio maana akatishia hata kuteka baadhi ya matajiri , lakini pia kumpa siku saba Raisi wa Ufaransa kusalimisha hio Teknolojia kabla ya kuvamia ikulu na kumuua”
“Sauroni nina hamu ya kutaka kuona uwezo wa hio teknolojia , lakini nahisi kwangu haina matumizi makubwa”
“Mfalme naamini hio teknolojia ni moja ya sehemu ya Urithi wako kutoka kwa Mfalme Pluto wa kwanza na ni haki yako kuimiliki, Mfalme Pluto kama unaona hutaki kujiingiza kwenye matatizo sisi The Eagles tutakusaidia katika hilo na kuhakikisha Teknolojia hio inarudi kwenye mikono yako”
“Sauroni unaweza usinielewe ila kwangu hio teknolojia haina maana , nadhani Appolo anaitaka kwa ajili ya kujiongezea nguvu , lakini sio kwa upande wangu”Aliongea Roma.
“Naamini kwa asilimia kubwa mtu aliechukua HollyGrail ile siku na kwenye huu mkutano anaweza akawepo ,ni muhimu nikashiriki na mimi ili kama atawepo niweze kumjua zaidi”Aliwaza Roma kwenye kichwa chake.
“Sauroni kikao kinafanyikia sehemu gani?”
“Sauron, where will the secret meeting be held tomorrow night?”
“Kitafanyikia ndani ya kambi ya kijeshi ya Le Havre ,usafiri Kwenda hujo ni kwakutumia meli ya Louis XVI mfalme”
“Sauroni nadhani kuna umuhimu wa mimi kuhudhuria”
ITAENDELEA
ITAENDELEA
Edna alionekana kuwa na hasira , alionekana alikuwa na mambo mengi ambayo alikuwa ameyaweka moyoni muda mrefu , mrembo huyu kama ilivyokuwa tabia yake , tabia ya kutopenda kuuliza , lakini pia tabia ya kutopenda kujielezea ilimfanya kuficha mambo mengi sana na kuyakalia kimya , kwa mfano Edna tokea anafika Ufaransa alikuwa akifikiria swala la Roma Kwenda kujitambulisha nyumbani kwa Nasra, lakini swala lingine Edna alikuwa akifahamu Roma alichokifanya mara baada ya kupotea kwake , siku ambayo alienda kupigana na Ares na baada ya kurudi akaenda kuua watu wa kundi la Fupa Faru kwa ajili ya Rose, mambo yote hayo Edna yalikuwa kwenye moyo wake na hakuyatafutia maelezo kabisa licha ya kuyafahamu, wala kutaka kuuliza Zaidi ya kukaa kimya, lakini mbaya Zaidi ni baada ya kumuona mwanamke akitoka kwenye chumba cha Roma asubuhi, Edna alijiambia Roma hakuwa siriasi na yeye na alikuwa akimchukulia kabisa kama mwanamke wa mkataba pekee ndio maana anafanya mambo anavyotaka hata kumuahidi Nasra Kwenda kujitambulisha ukweni .
Roma mwenyewe alishangaa , hakuwa akifahamu kama Edna alikuwa akijua kama aliua watu wa kundi la Fupa Faru kwa ajili ya Rose, alijiuliza ni mambo mangapi Edna alikuwa akiyajua na ameyakalia kimya.
Lakini alijiambia huenda Edna pointi yake ni ya msingi , alijiuliza kama Edna atajua ukweli wote wa Maisha yake ya nyuma ni kipi ambacho angefanya ,Je angekuwa na furaha na kumkumbali yeye kama mume na kujitoa jumla jumla kwake , hilo ni moja ya maswali mengi yaliopita katika kichwa cha Roma.
“Edna maneno yako yanaumiza”Aliongea Roma na kumfanya Edna amwangalie Roma na kisha kuvuta pumzi ndefu kama mtu ambaye anakusanya ujasiri.
“Kama kweli unapenda nikuulize , basi naomba nikuulize swali moja tu”Aliongea Edna
“Unaweza kuuliza?”alijibu Roma.
“Niambie kuhusu Seventeen?”Aliongea Edna na kumfanya Roma ashangae hapo hapo na kujiuliza Edna aliwezaje kujua hilo jina,kwani katika kumbukumbu zake hakuwahi kulitamka , lakini katika kufikiria hapo hapo jina la Clark liliibuka katika kichwa chake , aliamini kama Edna amejua hilo jina basi ni kupitia Clark.
*******
WIKI KADHAA NYUMA
Ni siku ambayo Edna alikuwa hospitalini , siku ambayo Roma , Sophia na Profesa Clark walienda kumtembelea Edna baada ya kupewa taarifa ya Edna kudhirai akiwa ndani ya hoteli ya Paridise siku ambayo aliweza kugundua kuwa baba yake mzazi ambaye alikuwa akimchukia kwa miaka mingi alikuwa sio baba yake mzazi.
Sasa muda huu wa jioni wakati Roma anaongea na simu nje mpaka kusimamishwa na Queen baada ya kugongana nae , upande wa ndani Sophia Edna na Clark walikuwa wakiongea.
“Edna nikiri kwamba unafanana kila kitu na Seventeen”Aliongea Profesa Clark na kumfanya Edna kushangaa , kwani ilikuwa ni mara yake ya kwanza kusikia hilo jina na sio kwake tu hata kwa Sophia.
“Profesa!, Seveenteen ni nani?”Aliuliza Edna na kumfanya Clark kushangaa na mpaka hapo alijua ameropoka neno ambalo hakupaswa kuongea , maana kama Edna hakuwa akimjua Seventeen, basi ni hakika kwamba Roma hakuwa amemueleza Edna juu ya jambo hilo.
Sophia ilibidi waangaliane na Edna na kisha wakageuza macho yote kwa Profesa Clark wakitaka maelezo ya kumjua Seventeen ni nani.
“Jamani kama hamumjui Seventeen basi naamini Roma hajawaambia bado na naamini anayo sababu ya kutofanya hivyo”
“Profesa tuambie Seventeen ni nani?”Aliongea Sophia huku akimshika mkono Profesa Clark ili kueleza Seventeen ni nani.
“Edna naamini siku moja Roma atakwambia kuhusu Seventeen kwa undani Zaidi , ninachoweza kukuambia tu ni kwamba Seventeen ndio mwanamke pekee ambaye Roma aliwahi kumpenda sana.. Sijui nini kilitokea ila kwa maelezo ya Roma Seventeen alijiua akiwa mjamzito”Aliongea Profesa Clark huku akionyesha kujutia kwa kitendo chake cha kuropoka mbele ya Edna.
“Kwanini alijiua?”Aliuliza Sophia. Na kumfanya Edna amwangalie Clark.
“Kuhusu hilo sifahamu ,jamani najua sikupaswa kuwaambia juu ya hili ,Roma akijua nimewaambia anaweza kukasirika, naombeni msiongee chochote kwa sasa mpaka atakapotaka kuwaambia yeye mwenyewe”Aliongea na kuwafanya Sophia na Edna watingine vichwa kubaki na siri hio moyoni.
Na hata pale Roma aliporudi ndani ya chumba alicholazwa Edna hakuweza kuona mabadiliko ya aina yoyote , Zaidi ya Edna na Sophia kumuangalia.
Sasa hii ndio siku ambayo Edna alipata kujua jina la Seventeena kwenye Maisha ya Roma , lakini licha ya mrembo huyu kupata kujua kuna mtu anaeitwa Sventeen kwenye Maisha ya Roma , hakuwa tayari kumuuliza Roma juu ya huyo mtu na kukaa na jambo hilo moyoni.
“Sipo tayari kuona mwanamke wa pili anapoteza uhai
kwa ajili yangu”Edna alikumbuka hio kauli ya Roma , siku ambayo alionana kwa mara ya pili na Roma na kupendekza swala la Roma kumuoa na pale Roma alipokataa na kutishia kujirusha na ndio Roma alipomzuia na kutamka kauli hio.
Edna baada ya kuunganisha matukio aliamini huenda maneno hayo yalikuwa yanamhusu Seventeen, lakini kama kawaida ya Edna hakuuliza , alilihifadhi moyoni.
*******
Taswira ya mto Seine ndani ya siku hii ilionekana kuvutia macho ya wengi waliokuwa wamekaa kandokando yake ,ni mto ambao umezungukwa na miti mikubwa aina ya London Platanus, miti iliogubikwa na majani ya kijani kibichi na manjano , huku kila upepo unapovuma juu ya miti hii hufanya majani ya manjano kupeperuka , kuna yale yaliokuwa yakitua kwenye reli na kuna yale yaliokuwa yakienda moja kwa moja ndani ya mto, Roma alikuwa ni moja ya watu waliokuwa wakiangalia namna majani hayo yalivyokuwa yakipeperushwa , huku akionekana kuingia kwenye mawazo, huku Edna akiwa upande wake wa kulia akiwa anasubiria jibu.
“Kwahio ushamfahamu tayari?”Aliuliza Roma.
“Vipi!,unaonekana haujapenda nilipotaja hilo jina , huenda nisingepaswa kukuuliza” Aliongea Edna.
“Sidhani kama napaswa kushangaa juu ya hilo,naamini Clark ndio kakuambia”
“Alitamka hilo jina tu , huku akianiambia nafanana kwa asilimia kubwa na mtu anaefahamika kwa Seventeen , hakunipa maelezo mengine , nataka nisikie kutoka kwako kuhusu Seventeen , lakini kama haupo tayari kuniambia usijilazimishe”Aliongea Edna.
“Nadhani sipaswi kukuficha juu ya hilo, ni mambo yaliopita na kila mtu katika Maisha lazima awe na kumbukumbu za maisha yaliopita , sio swala la mtu kuona aibu kuwa na kumbukumbu za nyuma , ziwe za kusikitisha au za kufurahisha,kuhusu Seventeen sidhani kama nitakuja kumsahau kwenye Maisha yangu na angalau imekuwa vyema umeweza kumfahamu kupitia Clark”
“Bado unampenda?”Aliuliza Edna.
“Mapenzi!, Sina uhakika kama bado nampenda au lah,Nimejuana na Seventeen miaka Zaidi ya ishirini na mbili iliopita kabla sijarudi Tanzania , Seventeen kwangu alikuwa ndio kila kitu , alikuwa ndio sababu ya mimi kuishi licha ya kupitia kipindi cha maumivu makali nikiwa katika utoto wangu , kila nilipofikiria kukata tamaa na kumwangalia Seventeen ambaye bado alinihitaji nilipata nguvu upya , hatukuwa wapenzi kwasababu hatukuwahi kutongozana na kuambiana tunapendana wala kupeana zawadi , muunganiko wetu ulikuwa ni Zaidi ya wapenzi , ,Seventeen alinihitaji ili aishi na mimi nilimhitaji vilevile ili niweze kuishi,huenda ningemwambia kama nampenda na akawa mpenzi wangu , huenda asingechukua maamuzi ya kijinga alioyafanya… Seventeen ni mwanamke wa kipekee sana kwenye Maisha, aliebaki katika kumbukumbu zangu…”Roma alijikuta akiishia njiani , kwa mara ya kwanza aliongea pasipo kuwa na tabasamu kwenye macho yake, huku macho yakiwa mekundu mno , ilionesha Maisha alioishi na Seventeen yalikuwa ya kuumiza sana , kiasi kwamba hakutaka kabisa kukumbuka yaliowatokea, Edna na yeye alijihisi moyo kuuma kwa jinsi Roma alivyokuwa akiongea.
“Umeuliza kama na mpenda! , kwangu Seventeen sikuwahi kumtamkia neno nampenda hata siku moja na yeye hakuwahi kuniambia ananipenda, tulizungumza maneno machache sana kuhusu mapenzi , vitu tuulivyongea ni namna ya kuweza kushinda kiza kilichokuwa mbele yetu , kwangu kuwa karibu yake ilikuwa ni Faraja, ukiniuliza kama nampenda ukweli sijui namna ya kujibu hilo swali”Aliongea Roma.
“Clark alisema nafanana nae kwa kiasi kikubwa , hilo ni kweli?”
“Ndio mnafanana kwa asilimia kubwa sana na Seventeen , ila utofauti wenu ni kwamba wewe ni mtembo Zaidi kuliko Seventeen , usisikilize maneno ya Clark , hana anachojua kuhusu Seventeen Zaidi ya kuona picha yake tu”Aliongea Roma.
“Kwahio unavyoniona kwako unanichukulia kama mbadala wa Seventeen?”Aliuliza Edna na kumfanya Roma kushangaa kidogo.
“Seventeen ni Seventeen na wewe ni mke wangu kwa sasa, Seventeen kwangu amebakia kuwa kumbukumbu nisizoweza kuzisahau, kama ningekuwa nakuchulia kama Seventeen nisingejali hisia zako”Edna alionekana kuridhishwa na jibu alilipewa na Roma.
“Unakumbuka mara yangu ya pili na wewe kukutana ndani ya hoteli , wakati nilivyokuambia kuwa nataka unioe na ukanikataa , na hata pale nilipolazimisha kujirusha kwenye lile jengo ukabadilika ghafla na kunizuia, nahisi ile siku nilikukumbusha kuhusu Seventeen , ndio maana ulikiubali kunioa”Roma alifikiria kidogo , ukweli siku ile ni kweli kitendo cha Edna kutaka kujirusha kwenye lile jengo la hoteli kilimrudishia kumbukumbu za nyuma juu ya kitendo alichokifanya Seventeen.
“Siwezi kupinga , ulinifanya nikumbuke kilichotokea miaka ya nyuma ndio maana nikakubaliana na wewe , lakini hata hivyo sijawahi kukuchukulia kama mbadala wa Seventeen”
“Kama ni hivyo basi naamini ninapaswa kushukuru uwepo wa Seventeen kwenye hii dunia, kama sio yeye huenda Maisha yangu mpaka sasa yangekuwa yashabadilika , huenda baba yangu mzazi angeniua , lakini pia hunda ningekuwa kwenye Maisha ya ndoa na mtu nisiekuwa nikimpenda…”Aliongea Edna na kuishia njiani huku akianza kulia na kumshangaza Roma na kumfanya ageuze macho kuangalia watu waliokuwa ndani ya eneo hili , kwani aliogopa watu wakishuhudia Edna akilia mbele yake,aliamini Wazungu wangemshangaa kwa kumfanya mwanamke mrembo kama Edna kulia na alishukuru uwepo wa Sauroni , kwani watu walikuwa wametawanyishwa.
“Edna nyamaza basi , kama kuna sehemu hujaridhika na majibu yangu niambie”Aliongea Roma , huku akishindwa ni hatua gani azichukue kwa wakati huo , siku zote amemzoea Edna kuwa kauzu na mtu wa kuficha hisia zake , lakini mabadiliko ya leo ya Ghafla yamemfanya kushangaa kidogo.
Licha ya Edna kumwambia Edna anyamaze , lakini Edna hakunyamaza Zaidi ya kuangalia chini na kudondosha machozi.
“Edna nishasema wewe ni Edna na Seventeen ni Seventeen, Sijui unafikiria nini lakini sijui cha kufanya kwenye hali uliokuwa nayo”Aliongea Roma na Edna alinyanyua kichwa chake na kumwangalia Roma.
“Clark aliniambia kuwa Seventeen alikuwa na ujauzito wako, Ni kweli?”Aliuliza Edna na Roma alitingisha kichwa kukubali.
Ukweli kwa upande wa Roma hakupenda kukumbuka tukio la miaka kadhaa iliopita , kitendo cha Seventeen aliekuwa na ujauzito wake kujirusha kwenye bahari iliokuwa imejaa mabarafu ,tena mbele yake kilikuwa ni cha kuumiza sana na kwake ndio sababu nyingine iliomfanya Roma kuchukulia wanawake kama chombo cha Starehe , Alikuwa akitumia wanawake kwa ajili ya kujipoza na maumivu , lakini maumivu hayakupita na kadri maumivu ya moyo yalivyozidi kumuendesha ,ndipo tatizo lake la ubongo kuwa kubwa Zaidi , Profesa Clark alijaribu kumsaidia Roma ili aweze kupunguza mawazo , lakini alishindwa kabisa na kuogopa mno na kushindwa kujua cha kufanya, na hata pale Roma alipompa taarifa ya kuondoka nchini hakuwa tayari , lakini pia hakuweza kumzuia Roma.
Hivyo ndio ilivyokuwa, moja ya sababu kubwa ya Roma kurudi Tanzania , aliamini kwa kuishi Maisha ya kawaida , huenda ingekuwa rahisi kwake kumsahau Seventeen na hata pale aliporudi nchini hakuwa tayari kujihusisha na wanawake kabisa , kwani aliona wanawake hawakuwa wakimsaidia Zaidi ya kumfanya kumkubuka Sevcenteen.
“Kama ni kweli Seventeen alikuwa na ujauzito wako , naomba nikuulize swali la mwisho”
“Okey unaweza kuuliza”
“Kama Seventeen yupo hai na akajitokeza kwako , akiwa na mtoto wako na yupo tayari kwa ajili ya kuanza upya na wewe ,je utaendelea kuwa na mimi au utaenda kwa Seventeen?”
“Nyamazaa….!!!!”Aliongea Roma kwa sauti kubwa na mwonekano wake ulibadilika palepale na hata macho yake yalibadilika na kuwa ya kijani.
SEHEMU YA 189.
Edna licha ya Roma kubadilika , alionekana kutohofia kitu chochote , alimwangalia Roma pasipo hata ya kupepesa macho na alionekana alitaka jibu lake licha ya Roma kubadilika.
“Seventeen….. Seventeen na mtoto wake walishakufa zamani na sitaki tena kusikia ukilitamka hilo jina mbele yangu”Aliongea Roma kwa sauti isio ya kawaida.
“Huna haja ya kuzificha hisia zako, unaonekana kabisa kwenye moyo wako unashindwa kututofautisha mimi na Seventeen , ndio maana unaonesha kunijali na kutaka kunilinda”Aliongea Edna huku akiangaliana na Roma kwenye macho, pasipo ya kuogopa kabisa , ni kama mtu aliekuwa akijiambia licha ya Roma kubadilika asingeweza kumdhuru..
“Edna nakuambia kwa mara nyingine kaa kimya”Roma aliongea huku akimsogelea kabisa Edna karibu kama mtu ambaye anajaribu kumuogopesha kwa muonekano wake.
Roma mwenyewe alishindwa kujielewa kwanini alikuwa na hasira za namna hio, baada ya Edna kutaja jina la Seventeen mfululizo.
“Roma acha kujidanganya, ninachojua huwezi kunitofautisha mimi na Seventeen na unajishawishi tu kusema kama sisi ni tofauti , ila unafanya hivyo kwa ajili ya kujipozapoza maumivu yako yakuachwa ,hukutaka kuwa na mwanamke mwingine kwasababu ulihisi utakuwa dhaifu ,kutokana na kumbukumbu za Seventeen na kwako mimi ni kama kitulizo cha mateso yako, Kama kweli unaweza kunitofautisha na Seventeen kwanini ukaamua kumuacha Rose , mwanamkie ambaye naamini anakupenda na wewe unampenda na kukubali kuoana na mimi ambaye kwangu ninachojali zaidi ni kazi , sikuwahi kukupa hata nafasi ya kuingia kwenye chumba changu wala kuonyesha ishara yoyote ya kukupenda upo na mimi kwasababu nafanana na Seventeen huo ndio ukweli.
Maneno ya Edna yalikuwa ni makali kiasi kwamba yalikuwa yakipita kwenye masikio ya Roma kwa kujirudia rudia na kumfanya kichwa chake kuanza kuuma.
“Edna tafadhari , nakuomba uache kuongea tena kuhusu Seventeen”
“Nisamehe kama maneno yangu yanaonekana kuwa makali , lakini huo ndio ukweli haukuwahi kunichukulia mimi kama mimi , najua ni mengi umenisaidia kwa muda mfupi tuliokuwa Pamoja , lakini tokea siku Clark aliponiambia kuhusu Seventeen , nilikuwa nikiwaza sana , haikuwa rahisi kwangu kama unavyofikiria na angalau leo hii nimeweka wazi kile kilichopo ndani ya moyo wangu”Aliongea Edna ila kwa upande wa Roma alishindwa kujibu chochote , aliona anaweza kushindwa kujizuia muda wowote ndio maana akaugeukia mto.
“Mimi nishamaliza na narudi ndani kuendelea kuangalia maonyesho , kama hujisikii kuungana na mimi unaweza kurudi kupumzika ila naamini pia rafiki yako yupo hapa kwa ajili ya kuongea na wewe”Aliongea Edna na kujiweka sawa na kuanza kupiga hatua kurudi ndani.
Edna licha ya kujiweka sawa , lakini macho yake hayakujificha kama alikuwa akilia , Stern na Alice waligundua pia hilo , ila hawakutaka kuuliza lolote na kuendelea kuangalia mbele.
“Miss Edna tunaweza kuanza tukio?”Aliuliza Meneja na kumfanya Edna amwangalie.
“Kwanini unaniuliza mimi?”
“Tulikuwa tukisubiri uwepo wenu ndio tuanze”Aliongea Meneja.
“Mnaweza kuanza tu , kilichotokea hapa ni maswala binafsi”Aliongea Edna na Meneja alitabasamu na kisha kuinamisha kichwa chake kwa heshima na kusogea jukwaani na kumnong`oneza mshereheshaji kuanza tukio.
Upande wa nje Roma alitulia kwa dakika kama mbili hivi mpaka alipoinua mkono wake na kumpa ishara Sauroni ya kumsogelea na Sauroni alifanya hivyo.
“Sauron, I’m going to ask you something, be honest with me.”
“Sauroni nitakuuliza kitu na naomba uwe mkweli na mimi”
“Your Majesty Pluto, I never lie.”
“Mfalme Pluto , Mimi sidanganyi”
“Tell me then, in your eyes, am I someone who will cower in the face of my own weaknesses…”
“Hebu niambie kwenye macho yako ,naonekana kama mtu ambaye naweza kuogopa kudili na udhaifu wangu”
“Mfalme Pluto ijapokuwa mimi ni mshirika wako , lakini kwa umri wako naamini hilo swali ni la kitoto”Aliongea Sauroni na kumfanya Roma kucheka.
“Kwa kauli hio naamini Swali langu ni la kijinga”
“Mfalme Pluto ninachoamini ni kwamba muda mwingine inakuwa ngumu kwa mtu kuutambua uongo na ukweli , ila ilimradi unaweza kutambua kusudio halisi ndani ya moyo wako basi hupaswi kujiuliza maswali , Nguvu ya kweli haitegemei nguvu ya kimwili bali ni ule uwezo wa kukabiliana na matatizo na kuyatafutia ufumbuzi”
“Haha.. Sauroni nadhani kweli swali langu lilikuwa la kipumbavu , ulichoongea ni sahihi , kama kweli nina uwezo wa kukabiliana na matatizo yangu , kuwa imara au dhaifu sio swala la kujionea aibu”Aliongea Roma na Sauroni alitabasamu baada ya kuona mapokeo ya Roma.
“Mheshimiwa Pluto,Sidhani kama unataarifa juu ya mkutano wa siri wa Kimataifa unaofanyikia hapa Paris chini ya DGSE?”Aliuliza Sauroni na kumfanya Roma kushangaa.
“Mkutano wa siri?” Sijawahi kusikia juu ya hilo Sauroni”
“Nadhani umechelewa tu kupata taarifa juu ya huu mkutano Mfalme Pluto , kiufupi ni kwamba huu ni mkutano ulioandaliwa na Serikali ya Ufaransa na unahusisha , mashirika ya kijasusi , Vikosi maalumu na baadhi ya mashirika pia yanayotumia nguvu za ziada na kwa kile tulichogundua ni kwamba moja ya ajenda za mkutano huo pia unahusika”
“Unamaanisha nini Sauroni kama nahusika?”
“Your Majest!, “It’s about the gods”
“Kwanini kikao kiwe ni kwasababu ya The Gods Sauroni”
“Mfalme kwa maelezo ambayo hatuna uhakika nayo ni kwamba Mataifa ya Ulaya Pamoja na Marekani wanajiandaa kuingia Vitani na Appolo, licha ya kwamba ni tetesi tu kwa sasa , ila naamini kuna jambo kubwa linaendelea”
“Sauroni sijafautalia maswala haya kwa muda mrefu kidogo”
“Ndio Mfalme Pluto ,Tokea umerudi nchini Tanzania , Appolo Pamoja na jeshi lake waliweza kushambulia baadhi ya kambi za kijeshi za Urusi , EU pamoja na NATO, lakini mbaya Zaidi ni kwamba Appolo ameenda mbali na kuanza kuandikia barua za vitisho baadhi ya viongozi wa kubwa wa nchi , akiwemo Raisi wa Ufaransa, , Kwa taarifa tulizopata ni kwamba Appolo pia amehusika na kuteka baadhi ya matajiri wakubwa waliohudhuria maonyesho ya Fasheni hapa Paris”
“Sauroni hata mimi pia pamoja na mke wangu ni moja ya wahanga wa tukio hilo”Aliongea Roma na Sauroni akatabasamu.
“Sikudhani Umeweza kukutana na mkasa huo Mfalme Pluto , Nimefika hapa kwa ajili ya kumuona Madam Persephone lakini pia kulizungumzia swala hili”
“Haha.. Sauroni hebu niambie kwanza mmeweza kumfahamu Appolo mpaka sasa hivi?”Sauroni alitingisha kichwa akimaanisha Hapana.
“Mfalme ninachotaka kukuambia ni kwamba kwenye mkutano utakaofanyika siku ya kesho licha ya ajenda kuu ni juu ya kutafuta namna ya kumuangamiza Appolo na kundi lake , lakini pia kuna swala ambalo linahusiana na wewe?”
“Swala gani tena Sauroni?”
“Ni juu ya majadiliano juu ya umiliki halali wa teknolojia iliotumika kutengenezea siraha aliopoteza Mfalme Pluto wa kwanza”
“Sauroni unamaanisha Thanatos!?”Roma alishangaa , alikuwa akijua sana juu ya Teknolojia iliokuwa imepewa jina la Thanatos , Teknolojia ambayo ilivumbuliwa na wanasayansi kutoka kisiwa cha wafu na mfalme Pluto wa kwanza kabla hajamrithi.teknolojia ambayo ilikuwa ikifanyika kwa kucheza na DNA za mwili na kumfanya mtu kuwa kama sumu kwa Maisha ya binadamu , kwani kama mwili wako utatengenezwa kwa tekonolojia hio basi utakuwa hata na uwezo wa kumuua mtu kwa kumgusa tu ndio maana ikaitwa kwa jina la Thanatos.
Sasa kwa kumbukumbu za Roma ni kwamba, Mfalme Pluto wa kwanza alipoteza kanuni za kutengeneza siraha hio , huku mwanasayansi aliehusika na utafiti kufariki .
“Ndio mfalme Pluto ,kwasasa taarifa zinaonyesha teknolojia hio ipo chini ya Serikali ya Ufaransa na Appolo ni moja ya watu wanaotaka hio teknolojia kwa nguvu ndio maana akatishia hata kuteka baadhi ya matajiri , lakini pia kumpa siku saba Raisi wa Ufaransa kusalimisha hio Teknolojia kabla ya kuvamia ikulu na kumuua”
“Sauroni nina hamu ya kutaka kuona uwezo wa hio teknolojia , lakini nahisi kwangu haina matumizi makubwa”
“Mfalme naamini hio teknolojia ni moja ya sehemu ya Urithi wako kutoka kwa Mfalme Pluto wa kwanza na ni haki yako kuimiliki, Mfalme Pluto kama unaona hutaki kujiingiza kwenye matatizo sisi The Eagles tutakusaidia katika hilo na kuhakikisha Teknolojia hio inarudi kwenye mikono yako”
“Sauroni unaweza usinielewe ila kwangu hio teknolojia haina maana , nadhani Appolo anaitaka kwa ajili ya kujiongezea nguvu , lakini sio kwa upande wangu”Aliongea Roma.
“Naamini kwa asilimia kubwa mtu aliechukua HollyGrail ile siku na kwenye huu mkutano anaweza akawepo ,ni muhimu nikashiriki na mimi ili kama atawepo niweze kumjua zaidi”Aliwaza Roma kwenye kichwa chake.
“Sauroni kikao kinafanyikia sehemu gani?”
“Sauron, where will the secret meeting be held tomorrow night?”
“Kitafanyikia ndani ya kambi ya kijeshi ya Le Havre ,usafiri Kwenda hujo ni kwakutumia meli ya Louis XVI mfalme”
“Sauroni nadhani kuna umuhimu wa mimi kuhudhuria”
ITAENDELEA
ITAENDELEA