Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

kuhus nadia nakumbuk aliwah kupokea sim akifokewa kua kapew kz aifanye kuhus roma ila bado hajaikamilisha na boss wake alikasirik sana, nadhan bos mwenyew alikua ni apollo fek
Inawezekana Kaka! Ngoja tuone majibu atakayotoa pind akiulizwa amifika ufaransa kwa sababu zipi!! Maana Edna nae yupo duniani kimwili tu.. akili bado hazijamkaa sawa
 
NILIMDHANIA KAHABA KUMBE BIKRA

MTUNZI:SINGANOJR KING

SEHEMU YA 206

Tukio ambalo lilitokea hapo bandarini kwa upande wa Roma alikosa maelezo mazuri ya kulielezea kabisa, jambo hilo halikuwa dogo na lilimkera sana Roma , kwani ni mara ya pili hii anakutana na mtu huyu ambaye uwezo wake ni mkubwa sana kuliko wa kwake.

Roma hakuona haja ya kubakia ndani ya hilo eneo Zaidi ya kurejea kwenye gari, Edna alikuwa vilevile kama alivyomuacha , hakuongea chochote hata pale Roma alivyorudi kwenye gari, na kutokana na Roma kutokuwa kwenye mudi nzuri kutokana na tukio la teknolojia ya siraha ya Thanatos kuchukuliwa na mtu mwenye uwezo mkubwa kuliko yeye hakutaka pia kuongea chochote Zaidi ya kuendesha gari kuelekea upande wa hoteli ya Sofiteli.

Ni madakika kadhaa tu Roma alikuwa ashafika ndani ya hoteli hio na ile anasimamisha gari tu, Edna ndio aliekuwa wa kwanza kutoka na kupiga hatua kuelekea ndani na kumfanya Roma aishie kumwangalia, pasipo kujua ni kipi kimempata Edna kwa wakati huo kwani kama ni Edna kumchunia aliona huo mchunio sio wa kawaida hata kidogo.

Upande wa ndani ya hoteli Goodman alikuwa ndani ya chumba chake akiwa anakunywa bia kwa kujipongeza kile ambacho alikuwa amekikamilisha mchana wa siku hio , alikuwa na furaha kweli kwani aliamini kwa asilimia mia moja Edna asingeweza kutoka kwenye mikono ya Apollo.

Mziki wa mahadhi ya Waltz aliokuwa ameufungulia ulimfanya bwana huyu kucheza kwa kujiachia ndani ya chumba chake cha kifahari ndani ya hoteli hii , huku akiwa amevalia taulo na mkononi akiwa ameshikilia Glass ya iliojazwa kwa kimiminika cha rangi nyekundu.

“Hahaha…Vexto inakwenda kuwa yangu,What a great Achivement!”Aliongea Goodman huku akiendelea kucheza kwa furaha akiwa amefumba macho akisikilizia mziki kutoka kwenye spika zilizokuwa zimefungwa ndani ya chumba hiko.

Wakati akiendelea kusikiliza mziki na kucheza kwa furaha, burudani yake ya kucheza Pamoja na kufurahia mvinyo ilikatishwa na mtu aliekuwa akigonga nje ya mlango.

Goodman akiwa kwenye hali ya kukereka pasipo kufikiria ni nani aliekuwa akigonga alifungua kwa jaziba na palepale macho yake yakatua kwa mtu ambaye hakutegemea kumuona mbele yake muda huo , kwani alitegemea mtu huyo kuwa mfu kwa wakati huo.

“ Mr Roma..ho…how did… how did you…”Goodman alijikuta akiwa ni mwenye kubabaika kwani hakutegemea kumuona Roma Ramoni wakati huo na kwa upande wa Roma hakujali Goodman aliekuwa ni mwenye kubabaika bali palepale kwa kutumia mguu wake wa kulia alimpiga teke Goodman na kumfanya kudondokea ndani na Roma aliingia ndani na kufunga mlango huku Goodman akitoa ukulele wa maumivu.

Ukweli Roma hakuwa na haja ya kumuuliza Nadia ilikuwaje mpaka akawa sehemu ya mateka na hii ni kwasababu alikuwa na maelezo kutoka kwa Stern na Alice ambao walimwambia Goodman ndie aliekuwa mhusika mkuu aliefika hospitalini akiwa na magaidi na kuwateka , hivyo Roma aliamini maelezo yote atayapata kupiga Goodman.

Roma baada ya kumpiga Goodman teke na kudondokea ndani , alimshika Goodma kwenye kiuno kwa kutumia mkono mmoja tu na kisha akamnyanyua juu na kumfanya Goodman kuelea hewani.

“Mr Roma uantaka kufanya nin…”Aliongea Goodman huku akiwa kwenye hali ya wasiwasi mno , lakini Roma hakuwa ni mwenye kuongea neno , alichokifanya ni kumbeba Goodman kwa staili ileile na kisha akafungua mlango uliokuwa ukimruhusu kutokezea kwenye Balconi.

Roma akiwa amemshikilia kisawasawa Goodman kwenye kiuno alijirusha kutoka juu ya Balconi na kupotea ndani ya hoteli hii ya Sofitel.

“Shwaaa…..!!!”

Ni maji yaliokuwa na mchanganyiko wa harufu mbaya ndio yalioweza kumzindua Goodman aliekuwa amepoteza fahamu.

“Hey! Wewe nguruwe mweupe naona umezinduka”Ilikiwa ni sauti ambayo Goodman hakuweza kuitambua na kutokana na ubaridi aliokuwa akihisi kwenye mwili wake aligundua hakuwa na nguo yoyote mwilini na alikuwa uchi.

“Nyie ni wakina nani na hapa nipo wapi?”Aliuliza Goodman baada ya kugundua amezungukwa na wananaume Weusi Zaidi ya wanne wakiwa wanamwangalia , huku taa za eneo hili zikiwa haififu mno na zenye rangi mbalimbali , ni kama vile alikuwa ndani ya Casino kwa muonekano wa eneo hili.

“Huna haja ya kuuliza maswali wewe nguruwe mweupe , haha… unaiona hii?”Aliongea mwanaume mwingine mweusi aliekuwa na ndevu nyingi huku akimwonyesha Goodman kiungo chake cha siri na Goodman baada ya kugundua kitu ambacho kinatarajiwa kufanyika kwake a;ijikuta akitamani hata kupoteza fahamu.

Ile furaha aliokuwa nayo dakika kadhaa nyuma ilikuwa imegeuka na kuwa majuto makuu , hakuamini kwenye Maisha yake anaweza kuwa kwenye eneo kama hilo akiwa hana msaada na huku mbele yake kukiwa na wanaume ambao wanataka kumfanyizia kitendo ambacho hakuwahi kukifikiria kwenye Maisha yake kama kitakuja kumtokea.

“Hey!Mshikilieni vizuri , nataka nianze mimi”Aliongea jamaa mmoja mwingine huku akivua bukta lake.

“Subi… subirini kwanza , nisikilizeni nitawapa pesa nying…”Goodman alianza kuweweseka , lakini palepale mlango ulifunguliwa na Roma aliekuwa ameshikilia bia aina ya Martel akiigida kwa fujo.

“Mr Roma naomba unisiadie tafadhari … nitakupa kiasi chochote cha hela unachotaka ,usinifanyie hivi , nimekosa mimi naomba unisamehe”aliongea Goodman maneno mfululizo , lakini kwa Roma hayakuwa yakimwingia hata kidogo Zaidi ya kupandwa na hasira , kila alipokuwa akikumbuka namna Edna alivyokua amemchunia alijihisi hasira zikizidi kupanda.

“Sina sababu ya kukusamehe …. Nitahakikisha hawa wanaume wanakufanya kwa zamu mpaka waliridhike na nikishamaliza nitatekeleza kifo chako”Aliongea Roma ambaye hakuhangaika na sauti za miziki zilizokuwa zikisikika kutoka nje.

Ndio sehemu ambayo Goodman alikuwa amekamatwa na kufungwa ni ndani ya ya mtaa wa Moulin Rouge upande wa Montmartre ndani ya jiji hili la Paris , hii ndio mitaa ambayo ilikuwa imechangamka sana wakati wa usiku kwa kuwa na Macasino mengi ,Bar na biashara nyingi haramu ambazo zilikuwa zikifanyika, maatufu kama Grey Business.

“Mr Roma …Pleaase….”Aliongea Goodman huku machozi yakianza kumtoka.

“Mr Goodman unaonaje kabla ya kujitetea ukaelezea tukio zima kwanza ili nielewe nia yako halisi ni ipi?”Aliongea Roma ambaye alikuwa amekaa kwenye kiti cha sofa kilichokuwa pembeni ya Goodman.

Goodman baada ya kupewa nafasi hio hakuona haja ya kuficha chochote , aliona njia pekee ya kukwepa kifo na adhabu ambayo Roma alikuwa amemuandalia ni kuongea ukweli.

“Mr Roma nitakueleza kila kitu ,, naomba usiniue tafathari”Aliongea Goodman na kumfanya Roma atabasamu kifedhuli na kisha akampa ishara jamaa mmoja ambae dakika chache nyuma alitaka aanze yeye kumfanyizia Goodman, na jamaa yule baada ya kupewa ishara alimsogelea Goodman huku akiwapa ishara vijana wake wamshike vizui kwa kumuinamisha.

“Nitaongea…nitaongea”Goodman baada ya kugundua anachotaka kufanyiziwa palepale alijitetea kwa kusema ataongea ukweli na Roma aliwapa ishara kumsimamisha vizuri ili aweze kuongea.

********

Nahita , Rahel na Kizwe walikuwa ni wanachuo walioshibana sana ndani ya chuo cha Durban South Africa na urafiki wao ulitokana na kukaa chumba kimoja ndani ya hosteli za chuo hiko zilizokuwa ndani ya Campus namba moja.

Licha ya kila mmoja kuchukua kozi tofauti tofauti kati yao, hio haikuwafanya wanadada hao warembo na maarufu kutokuwa marafiki ,wakati Raheli akichukua masomo ya uhasibu, upande wa Nahita alikuwa akichukua masomo ya uongozi wa biashara, huku mwanadada mrembo Kizwe na yeye akichukua masomo ya Lugha.

Nahita alikuwa ni mjapani, huku Raheli yeye akiwa ni mtanzania na kwa upandewa Kizwe yeye akiwa ni Mrwanda, urafiki wa wadada hawa wa mataifa tofauti ulikuwa mkubwa kiasi kwamba walikuwa wakifanya mambo mengi kwa Pamoja.

Kutokana na urembo wao lakini pia namna ambavyo walikuwa wakifanya matanuzi ndani ya South Africa iliwafanya warembo hawa kuwa maarufu sana kwa wakati huo.

Mwanadada mrembo kutoka Rwanda yaani Kizwe, kwa upande wake yeye alikuwa tayari yupo kwenye ndoa na makamu wa raisi wa Rwanda mheshimiwa Jeremy Paul wakati akiwa masomoni, upande wa Nahita yeye pia alikuwa na mpenzi wake Muingereza, ila kwa upande wa Raheli bado hakuwa na mpenzi kwa wakati huo, licha ya wanaume wengi kumtakakimahusiano, na hio ni kwasababu wanaume wote walionekana kutomvutia kabisa, na hii yote ni kutokana na tabia ya Raheli kuchagua chagua wanaume.

Raheli tofauti na marafiki zake , yeye pekee ndie aliekuwa hapo chuoni kwa ufadhili maalumu wa masomo yake kutoka serikalini, hivyo unaweza kusema kwamba Raheli hakuwa mtoto wa kishua kama ilivyokuwa kwa marafiki zake Nahita na Kizwe.

Mwaka wao wa mwisho ndio Kizwe aliweza kuwatambulisha Raeli na Nahita kwa Mheshimiwa Jeremy Paul kwenye mahafali yao ya kumaliza, na pale mheshimiwa Jeremy Paul baada ya macho yake kutua kwa mrembo Rahel, alijikuta akimpenda hapo hapo(Love in first sight) na sio kwa Jeremy tu hata kwa Raheli pia baada ya macho yake kutua kwa Mheshimiwa Jeremy alijikuta akivutiwa nae mno na kutokea kumpenda, na kwa mara ya kwanza Raheli akajikuta anampenda Jeremy kwa mapenzi ya dhati pasipo kujali kuwa Jeremy alikuwa ni mume wa mtu , tena mume wa rafiki yake Kizwe.

Baada ya marafiki hao kuhitimu masomo yao kila mmoja alirejea katika taifa lake ,Nahita alitejea Japani kabla ya kuhamia uingereza baada ya kufunga ndoa na mwanaume aliekuwa akipendana nae na kwa upande wa Kizwe alirejea nchini kwao Rwanda kuendelea kuitumikia ndoa yake.

Lakini jambo ambalo Kizwe hakulifahamu, ni kwamba Raheli na Mheshimiwa Jeremy tayari walikuwa na mawasiliano ya karibu sana , mawasiliano ambayo yalipelekea mapenzi mazito ya wawili hao, na mheshimiwa Jeremy kutokana na penzi lake kwa Raheli aliamua kufadhili masomo yake ngazi ya Masters ndani ya taifa la Urusi na huko ndio sehemu ambazo mheshimiwa Jeremy alitumia sana kukutana mara kwa mara na Raheli na kufurahia penzi lao.

Upande wa Nahita mara baada ya kufunga ndoa na mzungu wake miaka miwili baadae ndipo alipopata kujifungua mtoto wa kiume na kumpa jina la Goodman.

Huku upande wa Raheli yeye alikuwa tayari ashamaliza masomo yake na alikuwa asharejea nchini Tanzania kuendelea na Maisha yake na wakati Nahita anajifungua ,kwa upande wa Raheli alikuwa mjamzito tayari na alikuwa ameshaolewa na Adebayo, na kwa upande wa Jeremy wakati Raheli ana ujuaito yeye ndio kwanza alikuwa akiingia madarakani kama Raisi wa Taifa la Rwanda huku Kizwe mke wake akipanda cheo na kuitwa rasmi First Lady huku jina Kizwe likikosa umaarufu .

Sasa haikueleweka ni wakati gani Kizwe aliweza kugundua mahusiano ya Jeremy na Raheli , lakini wawili hao waliendelea kuwa marafiki kwa muda mrefu sana mpaka ambapo Edna mtoto wa Raheli kufikisha umri mkubwa.

Kutokana na ushauri wa Nahita na bibi yake Edna yaani Mariaum walikubaliana na Raheli kwa Edna Kwenda kusoma ndani ya chuo cha Oxford na kipindi ambacho Edna anaanza masomo, kwa upande wa Goodman alikuwa tayari yupo chuoni na alikuwa amemtangulia Edna kwa mwaka mmoja.

Kwahio hapa tunaona kwamba Kosa alilolifanya Kizwe ni kuwatambulisha marafiki zake kwa mume wake , kwani tokea siku hio mume wake aliacha kumpenda na mapenzi yake yote yalihamia kwa mrembo Raheli kutoka Babati.
 
SEHEMU YA 207

Kwahio Edna baada ya kufika Oxford Uingereza ni kama waangalizi wake walikuwa ni familia yote ya Nahita na hapo ndipo Goodman alipoweza kukutana kwa mara ya kwanza na mrembo Edna.

Baba yake Goodman na malkia Elizabeth walikuwa ni ndugu wa damu kabisa , hivyo Goodman alikuwa na damu ya kifalme na kutokana na jambo hilo Goodman alikuwa akitumia jina la ukoo wake kupata warembo wa kila aina ndani ya chuo cha Oxford na alikuwa akishobokewa mno kutokana na kwamba ilikuwa ni ndoto ya wanawake wengi kutoka na mtoto mwenye damu ya kifalme.

Sasa uhuni wa Goodman wote ulijuka kukwama mbele ya mrembo Edna , kwani tokea siku ambayo Goodman anatambulishwa kwa Edna na mama yake Nahita , kwanzia siku hio alimpenda sana Edna.

Lakini kwa upande wa Edna mambo yalikuwa tofauti , licha ya kuwa mrembo lakini hakuwa na Habari kabisa na wanaume, na kuna muda hata Goodman mwenyewe alimuona Edna kama mwanamke ambaye amepungukiwa na baadhi ya homioni za kike , kwani muda wote alimuona mrembo huyo kuwa siriasi na masomo na kwa jinsi Edna alivyokuwa akikomaa na kitabu kwa wabongo wangesema mrembo huyo alikuwa akisoma kama anasomea Kijiji.

Lakini sasa licha ya Goodman mbinu zake zote za kiushawishi kukwama hakukata tamaa kabisa na alimfanya Edna kuwa rafiki yake wa karibu huku akitafuta mbinu nyingine ya kumuweka mikononi Edna na hamasa yake ya kumpata Edna iliongezeka pale alipokuja kugundua kuwa Edna alikuwa Bikra bado na kama ilivyo kwa wanaume wengi ukishagundua jambo hili basi ni lazima ile nguvu ya kumsaka mrembo iongezeke marafudu na jambo hilo ndio lilimpelekea Goodman kuanza kumshawishi mama yake Nahita kuongea na Rafiki yake, yaani Raheli kwa ajili ya kuandaa namna ya kufanya Edna na yeye wapate kuona hapo baadae.

Jambo hili kwa Nahita hakulikataa kabisa kutokana na kwamba alikuwa akimpenda mwanae , lakini pia hakuona ni jambo baya kwa Edna kuwa kimapenzi na Goodman kwani ingewaongezea nafasi ya yeye na Raheli kuwa karibu Zaidi na familia zao kuwa ndugu.

Na pale ambapo Nahita alipofikisha swala hilo kwa rafiki yake Raheli halikupata pingamizi ,ila jambo ambalo Raheli alimwambia Nahita ni kwamba wamuache kwanza Edna asome na atahakikisha wawili hao wanaona baada ya kumaliza masomo.

Goodman ndio aliekuwa wakwanza kumaliza masomo , hivyo baada tu ya kumaliza alipata nafasi ya kazi ndani ya kampuni ya Athena Trading Company ambayo ilikuwa ndio kwanza inaanzishwa ndani ya jiji la Paris Ufaransa, na Goodman alikubali kazi hio kwa misinigi ya kwamba ukaribu wake na Edna ungeongezeka Zaidi lakini pia Raheli angetimiza ahadi yake ya kumfanya Edna kuwa mke wake.

Lakini Rahel alikumbwa na umauti kabla ya kutimiza ahadi yake aliokuwa amewekeana na Mama yake Goodman yaani Nahita , Pamoja na Goodman mwenyewe , lakini licha ya hivyo Goodman hakukata tamaa kwani mpaka wakati huo alikuwa akiwasiliana kwa ukaribu kabisa na mrembo Edna na kuna kipindi Goodman alikuwa akifika Tanzania kwa ajili tu ya kumsalimia Edna.

Upande wa Edna alikuwa akijua kabisa Goodman ana hisia nae za kimapenzi , lakini kwa upande wake yeye hakuwa kabisa na hisia za kimapenzi na Goodman na alimchukulia kama rafiki wa kawaida kabisa na hata pale ambapo Goodman alipoacha tabia yake ya kumtaka kimapenzi aliona huenda Goodman kwa wakati huo alikuwa akimchukulia kama rafiki na hana hisia nae tena , hivyo Edna alizidi kumuamini Goodman na kujiachia mbele yake.

Kwa upande wa Goodman alikuwa akiishi Ufaransa , lakini macho yake yote yalikuwa Tanzania kwa mrembo Edna, Goodman alikuwa na watu wake ambao amewaweka kumpeleleza Edna na alijikuta akiridhika pale alipogundua Edna hakuwa na mpenzi kabisa na alikuwa na bikra yake vile vile.

“Edna siku nitakapo itoa bikra yako ndio siku ambayo utakuwa mke wangu” Goodman alionekana kuwaza baada ya Edna kumtumia Selfie , wakati akiwa ndani ya jengo la Kampuni akiendelea na kazi.

Kwahio ndoto ya Goodman ilikuwa ni kutoa bikra ya Edna , ndoto ambayo ilikuja kuzimwa na Mfalme Pluto a.k.a Hades a.k. a Roma Ramoni.

Siku ambayo Goodman anakuja kujua ukweli juu ya Edna kufunga ndoa kwa siri na Roma Ramoni , moyo ulimuuma kiasi kwamba alitoa machozi akiwa ndani ya kampuni ya Athena akiendelea na kazi.

Sasa kipindi hayo yote yanatokea Goodman na Depney walikuwa ni marafiki wakubwa sana na urafiki wao ulianzia kwenye viwanja vya kula bata ndani ya jiji la Paris.

Depney alikumkubali Goodman kutokana na kwamba Goodman alikuwa na akili nyingi lakini wakati huo huo akiwa na damu ya kifalme, na kutokana na mipango na mikakati ya Depney kutaka kutawala taifa la Ufaransa ndio maana alimpenda Goodman.

Urafiki wa Goodman na Depney ulikuwa mkubwa kiasi kwamba kupelekea Goodman kumwambia Depney juu ya swala lake linalomuumiza moyo.

“Kwahio unamaanisha kwamba huyu ndio mwanaume ambaye kafunga ndoa na Edna!!?”Aliuliza Depney siku ambayo walikutana kwenye harakati zao za kula bata na Goodman alimwonyesha Depney picha ya Roma.

“Ndio huyo , lakini mbona kama unamfahamu?”Aliuliza Goodman.

“Namfahamu ndio”Aliongea Depney na kumfanya Goodman kushangaa

“Unamfahamu vipi?”Aliuliza Goodman kwa kifaransa.

“Huyu ndio fala ambaye Nadia kaniambia anampenda”Aliongea Goodman huku huku akionyesha hasira kwenye macho yake na kumfanya hata Goodman kushangaa mno.

Depney na Nadia pia wana historia ndefu mno, kwa mara ya kwanza Depney anakutana na Nadia ni nchini Korea Kusini kipindi ambacho Nadia alikuwa katika harakati za kusimamia kesi ya Raisi Kim ambaye alikuwa ameshitakiwa na serikali ya Korea kusini kama Fisadi.

Sasa kutokana na Ufaransa kuwa karibu sana na raisi Kim kipindi cha uongozi wake , katika kesi hio ya ufisadi walikuwa nae bega kwa beda, na katika kuonyesha kwamba wapo tayari kumsaidia kutoka kwenye mikono ya sheria ndipo walipotuma wafanyakazi wake wa kitendo cha Kijasusi nchini Korea ili kumsaidia Raisi mstaafu Kim, na katika majasusi waliotumwa Korea kusini , mmoja wapo alikuwa ni Depney.

Kutokana na mwanasheria mkubwa aliekuwa akisimamia kesi ya Kim ni Nadia Alfonso ilipelekea Depney na Nadia kukutana mara kwa mara kwa ajili ya kuzungumza namna ya kushinda kesi hio, na hapo ndio wakati ambao Depney alikufa na akaoza kwa Nadia , lakini kwakua walikuwa katikati ya harakati za kushinda kesi Depney hakuweza kumwabia Nadia juu ya jambo hilo.

Kesi ya Kim ilikuwa ikimwendea vibaya sana Nadia Alfonso kutokana na wanasiasa ambao walikuwa ndani ya serikali kusimama kidete kuhakikisha Kim anafungwa gerezani , jambo hili hata kwa majasusi waliotumwa kutoka Ufaransa hawakuleta matokeo chanya juu ya mwenendo wa kesi ya bwana Kim na hii yote ni kutokana na Serikali ya Marekani pia kuingiza propaganda zao za kutaka Raisi Kim afungwe gerezani kutokana na maslahi yao.

Katika dakika za mwisho za Nadia kukata tamaa juu ya mwenendo wa kesi ya mheshimiwa Kim , mambo yote yalibadilika baada ya mtaalamu Roma Ramoni kutoka visiwa vya wafu kuingilia kati.

Unaambiwa kutoka taarifa za siri za Korea kusini , wale wote ambao walikuwa wakitaka Mheshimiwa Kim kufungwa gerezani walitoa Ushahidi ambao ulimwezesha Kim kushinda mahakamani lakini pia walikufa kwa kucharangwa charangwa mapanga na muuaji kutoka kundi la New Zero Asssasin.

Kwahio Nadia aliweza kushinda kesi hio baada ya kupewa Ushahidi na Roma Ramoni.

“Huu ni Ushahidi utakao kufanya ushinde kesi , kuhusu namna nilivyoupata hilo halikuhusu”

“Wewe ni nani?”

“Nafahamika kwa jina la kodi, Ajenti Thirteen?”

Hii ilikuwa ni siku moja kabla ya siku ya hukumu ya mheshimiwa Kim , wakati Nadia akiwa amelela ndani ya chumba cha hoteli ndipo alikuja kuvamiwa na mwanaume ambaye alimpatia Ushahidi, mwanaume ambaye baada ya kujitambulisha kwa jina la Thirteen hakuongea neno lolote Zaidi ya kupotea kimazingara ndani ya chumba chake.

Sasa haikueleweka ilikuwa vipi mpaka kwa Nadia kuweza kumfahamu Roma Ramoni kama ndio mtu aliempatia Ushahidi , lakini kwanzia siku hio Nadia Alfonso aliishi kwa kumpenda sana mwanaume aliekuwa na jina la Thirteen na kutokana na ushaihidi aliopewa , aliweza kushinda kesi na jina lake kuwa maarufu.

Hivyo unaweza kusema kwamba mafanikio ya Nadia yalitokana na Ushahidi ambao Roma alimpatia.

Kwa upande wa Depney baada ya kesi kuisha alijaribu kumuweka karibu Nadia na kumueleza hisia zake , lakini Nadia alimuweka wazi kuwa hana hisia nae na mapenzi yake yote yapo kwa Ajenti Thirteen.

Depney baada ya kuuanza kufukunyua taarifa zinazomuhusu Ajenti Thirteen ndipo alipokuja kugundua kuwa Ajenti Thirteen alikuwa ni Mfalme Pluto A.k.a Hades , na aliweza kupata taarifa zake zote , mpaka picha zake , lakini sasa baada ya kupata taarifa hizo alishindwa kupata kujua ni sehemu gani anaweza kumpata Hades , kwani licha ya kusikia kuhudu Visiwa Vya wafu hakuweza kupata uelekeo kutokana na visiwa hivyo kutokuwepo kwenye Ramani ya Dnunia.

Sasa siku ambayo Goodman alipomwonyesha picha ya Roma kama mwanaume aliefunga ndoa na Edna, aligundua kuwa Roma Ramoni au Hades alikuwa nchini Tanzania.

“Goodman nitakusaidia kumpata Edna lakini kuna jambo namimi pia nataka unisaidie”Aliongea Depney.

“Jambo gani hilo , nipo tayari kwa jambo lolote”Aliongea Goodman na Depney alimpa ishara ya kwamba ainamishe kichwa chake amnong`oneze na Goodman alifanya hivyo na kujikuta akishangaa sana.

“Kweli!!”

“Ndio kama upo tayari nitawasiliana na bosi wangu na kila kitu kitaenda kama unavyotaka”

“Nipo tayari kwa hilo”Alijibu Goodman.

“Sasa sikiliza hakikisha mwezi wa tisa mwishoni unahakikisha Edna anakuja hapa Ufaransa”Aliongea Depney na Goodman alifikiria kidogo na kisha akatabasamu.

“Hilo linawezekana kabisa”Aliongea Goodman na kumfanya Depeny kutabasamu.

Sasa Depney kwakua alikuwa ndio Apollo feki ilibidi amtumie taarifa Nadia Alfonso juu ya mtu anaemtafuta kuwa ndani ya Tanzania akiwa ameoa , jambo hili lilikuwa la maumivu sana kwa Nadia baada ya kusikia mwanaume ambaye alikuwa anampenda na kumtafuta alikuwa ashaoa na yupo Tanzania.

Lakini licha ya maumivu aliokuwa nayo Nadia alishangaa kwamba mwanaume aliekuwa akimpenda siku zote alikuwa mtanzania.

“This is Fate”Aliwaza Nadia Alfonso alivyokuwa Amsterdam hotelini , aliamini kama kweli Roma Ramoni alikuwa mtanzania na wakakutana katika mazingira kama yale ndani ya taifa la Korea basi , wawili hao walipangwa kuwa Pamoja , hivyo swala la Roma kuoa halikumpa shida kabisa na hapo ndipo alipoanza kupanga mikakati ya kurudi Tanzania kwa ajili ya Roma Ramoni.

Lakini licha ya Nadia kurudi nchini Tanzania kwa ajili ya Roma Ramoni , alikuwa na wasiwasi mno juu ya Apollo na hii yote ni kwamba Nadia hakumfahamu Apollo kuwa ni Depney na alikuwa akimhofia Apollo kutokana na yale ambayo alikuwa akiyasikia chini chini juu ya uwezo wake.

Misheni ambayo Nadia alikuwa amepewa na Apollo wakati anarudi Tanzania ni kuhakikisha Edna ana aachana na Roma Ramoni , hivyo bosi ambaye alikuwa akiwasiliana na Nadia alikuwa ni Depney a. k,a Apollo wa mchongo.

Sasa siku ambayo Nadia anapata kufahamu Roma yupo kwenye hatari baada ya kupigiwa simu na Boss ilibidi afanye safari ya Dharula ya kuja Paris kwa ajili ya kumuokoa Roma na mtu wa kwanza kuwasiliana nae akiwa njiani kuja Paris alikuwa ni Depney.

Nadia alijiambia kama Depney atakuwa tayari kumsaidia ili jambo baya lisimpate Roma , basi yupo tayari kumkabidhi kitumbua, na jambo hili baada ya kufika kwenye masikio ya Depney alilipokea kwa mikono miwili , lakini ile Nadia anatua ndani ya uwanja wa ndege wa kimataifa wa Charles De Gaullie aliishiwa kutekwa kama ilivyokuwa kwa Edna na Roma..

Sasa mpaka hapo utakuwa na picha Boss aliekuwa nani , lakini pia ushaelewa uhusiano wa First Lady wa Rwanda na mama yake Rahel.

Sasa je kifo cha Raheli kilisababishwa na First Lady?, Hayo yote utayajua.
 
SEHEMU YA 208

Roma aliweza kusikiliza maelezo yote ya Goodman na kuona kumbe hata mpango wa kuja hapa Paris ulikuwa ni wa kupangwa na Apollo Pamoja na Goodman?.

Ukweli mpaka hapo kwa sheria zake hakuona sababu kabisa ya kumsamehe Goodman kabisa, aliona ni kifo peke yake ndio ambacho kingeweza kumaliza hasira zake.

Lakini pia aliona safari ya kuja hapo Paris imemfanya kutatua baadhi ya matatizo , kwa mfano kwa maelezo ya Goodman mpaka kufikia point hio alishajua kabisa kwamba Nadia alikuwa ndani ya kampuni ya mke wake kwa ajjili ya kuwaachanisha.

“Sio mbaya hii safari imejaa baraka hata hivyo”Aliwaza Roma kwenye kichwa chake huku akimwangalia Goodman aliekuwa uchi akiwa mbele yake.

“Mr…Mr Roma, I’m really sorry. Please let me go. I’ll give you anything you want, all my wealth. I won’t dare to hold any absurd intentions in the future anymore,”

“Mr Roma , naomba unisahehe sana , tafadhari niachia , nitakupa kila kitu unachotaka , utajiri wangu wote ,Sitothubutu kuwa na nia yoyot ya kijinga tena”Aliongea Goodman kwa kujitetea.

“Mh! Kama mtu anaweza kusamehewa makosa yake kwasababu tu ya utajiri na mali, Hio si inaonyesha kabisa matajiri watakuwa na uwezo wa kuua masikini?”Aliuliza Roma , lakini Goodman alishindwa kua na jibu la moja kwa moja Zaidi ya kuonyesha wasiwasi ambao umeufunika uso wake.

“Mr Goodman sasa hivi sipo kwenye mudi ya kuua kabisa , kuna mchezo naupenda sana kwenye Maisha yangu na kama utanifurahisa kwa kuucheza vizuri basi upo huru kuishi”Aliongea Roma na kumfanya Goodman asiamini kama anakwenda kusamehewa kwa kucheza mchezo tu.

“May I know what the performance it is?”Aliuliza Goodman kwa wasiwasi akimaanisha anaomba kujua ni mchezo gani ambao Roma anataka acheze.

“Bungee jumping.”

“Kuruka Bunge”Aliongea Roma pasipo kuwa na huzuni wala furaha , lakini kwa upande wa Goodman ilikuwa ni kilio.

Kuruka Bunge Au Bungee Jumping ni mchezo ambao mara nyingi unahusisha kuruka kutoka umbali mrefu kwa mfano mlima au Gorafa mpaka chini huku ukiwa umefungwa Kamba mgongoni na mara nyingi watu wanaoruka wanakwenda kutua kwenye mto mkubwa au baharini , Zanzibar watalii wanafanya sana huu mchezo.

Sasa Goodman alikuwa akiujua sana huu mchezo wa kuruka Bunge , licha ya kwamba hakuwahi kuufanya ila alikuwa akiufahamu na alikuwa pia akiuogopa sana, lakini kwakua Maisha yake yalikuwa hatarini, aliona afanye jambo lolote lile kujiokoa.

“Uko tayari Mr Goodman?”Aliuliza Roma.

“Ndio .. Ndio nipo tayari” Aliongea Goodman kwa haraka haraka , huku tumaini la kuishi likirudi upya.

Roma baada ya kuona Goodman kakubali kucheza mchezo wa Bungee Jumping palepale aliwapa ishara wale watu Weusi wamfungue mikono , na walifanya hivyo kwa haraka haraka na baada ya Goodman kufunguliwa alifurahi mno kwani aliona ni hatua nyingine ya matumaini ya kuishi.

“Pesa yenu mtachukua kwa Dosi”Aliongea Roma akiwaamrisha wale watu Weusi kwamba watapata pesa yao ya malipo kwa Dosi , sasa haikueleweka Dosi ni nani , lakini wote kwa Pamoja waliitikia na Roma palepale akamshika Goodman mguu wa kushoto na kumning`iniza kichwa chini miguu juu na palepale alipotea kimazingara ndani ya jengo lile la Club na kufanya wale watu Weusi kushangaa jambo lile.

Naam sasa ni saa saba za usiku lakini jiji la Paris lilionekana ni kama vile ni mchana kwa mataa yake yaliokuw ayakiwaka kila kona , jengo la Arc de Triomphe,Jumba la makumbusho la Louvre, Place De La Concorde , Champ Elysee ni sehemu ambazo zilikuwa zikionekana kupendezesha sana jiji hili.

Roma aliekuwa juu kabisa ya mnara maarufu ndani ya Ufaransa wa Eifell Tower alionekana akiwa amesimama huku upepo ukimpuliza kwa kasi kiasi cha kuepelekea hata shati lake aliovaa kuganda mwilini na kuonyesha mwili wake uliojengeka kimazoezi.

Chini ya miguu ya Roma anaonekana Goodman aliekuwa amelala chini akiwa uchi na ilionekana alipoteza fahamu wakati wa usafiri wa kuletwa juu ya mnara huo na sasa wakati huo ndio kwanza alikuwa akishituka.

Goodman hakuwa mjinga kiasi cha kutogundua kama yupo juu ya mnara wa Eifelli Tower, na hii yote ni kutokana na namna ambavyo aliweza kuona jiji lote la Paris.

Haikuwa mara yake ya kwanza ya Goodman kufika juu ya mnara huo kama ilivyokuwa kwa watalii wengi ambao wakifika Ufaransa lazima wafike kwenye huo mnara na kuupanda ili kuweza kupata uono mzuri wa jiji , lakini ilikuwa mara yake ya kwanza kwa Goodman kufika hapo akiwa uchi wa mnyama.

“Mr Roma why did you bring me here? Didn’t you mention bungee jumping?”

“Mr Roma , kwanini umenileta hapa , si ulisema mchezo ni Kuruka Bunge?”Aliuliza Goodman aliekuwa kwenye wasiwasi akimwangalia Roma ambaye alionekana kutokuwa na wasiwasi na alionekana kama vile ndio ilikuwa mara yake ya kwanza kusimama juu ya mnara huo kutokana na namna alivyokua akiangalia mandhari ya jiji.

Ukweli Goodman hakuelewa amefika vipi juu ya huo mnara , kwani ulikuwa ni mrefu mno na kama ni mtu kupanda basi ingemchukua muda na nguvu nyingi kupanda.

“That is Right , Bungee Jumping , you will be jumping from here”.

“Yeah ni sahihi, nilisema mchezo wa kuruka Bunge , hivyo utaruka kutoka hapa juu mpaka chini”Aliongea Roma.

“Unasema…!!!”

Goodman hakuamini kama mchezo wa Kuruka Bunge ambao Roma alikuwa akimaanisha ulikuwa ukifanyikia juu ya mnara wa Eifell Tower tena kutoka kileleni kabisa na ukilinganisha pia na namna ambavyo mnara ulikuwa umejengwa, juu ni kwembamba na chini ni kupana , hivyo aliona kuruka kutoka juu pasipo ya kuwa na vifaa maalumu ni sawa na kujiua.

“Mbona unashangaa.. nasubiria ujirushe , usisahau uliniahidi mwenyewe kama unakubaliana na mchezo”

“Mr Roma hakuna vifaa vyovyote vya kufanyia mchezo wa kuruka hapa , nikijitosa kutoka hapa mpaka chini sio mchezo bali ni kujiua”

“Uliniahidi mwenyewe upo tayari kwa ajili ya huu mchezo na mimi sikukuahidi kama kutakuwa na Kamba , huu ni mchezo wa kuruka Bunge bila Kamba hivyo acha kupoteza muda na fanya kuruka”Aliongea Roma lakini kabla hata Goodman hajajianda alisukumwa na mguu wa kushoto na alishindwa kupata hata pakushika kwani aliporomoka kama furushi Kwenda chini na kujipigizakwenye mavyuma ya mnara huo.

Naam na huo ndio ukawa mwisho wa Goodman, Roma licha ya Goodman kufa kwake hakua hata na tone na kujutia wala kuwa na wasiwasi hata kidogo , kwake aliona ni jambo la kawaida tu , lakini pia Goodman ndio aliechangua kucheza mchezo wa kuruka bunge hivyo aliamini hakuwa na kosa , lakini pia alijiambia hata kama polisi watafute chanzo cha kifo, usalama wa taifa kwa muda huo iulikuwa chini ya Fodesa hivyo wasingemfanya chochote.

Roma baada ya kusimama juu ya mnara kwa dakika chache hatimae aliamua kurudi zake hotelini kwa ajili ya kupumzika na njia aliotumia kufika juu ya mnara huo ndio njia ambayo alitumia kurudia na kufumba na kufumbua alikuwa nje ya Balconi ya chumba chake, na alisukuma mlango kuingia ndani.

Na ile Roma anaingia alishangazwa na mahadiliko yaliokuwa kwenye chumba chake na kilichomshangaza Zaidi ni aina ya mavazi ya mwanamke aliekuwa mbele yake.
 
SEHEMU YA 209

Mwanamke aliekuwa mbele ya Roma alikuwa ni Lilith , haikueleweka alifikaje hapo ndani ila nia yake ilionekana wazi kabisa mbele ya Roma , Lilith alionekana kuja hapo ndani kwa ajili ya kuomba mchezo na mfalme Pluto.

“Nikajua ushaondoka na baba yako kuelekea Uingereza?”Aliuliza Roma akijongea kivivu mpaka kwenye kitanda na kuketi.

“Nisingeweza kuondoka kabla hatujaonana?”Aliongea Lilith huku akijirembulisha.

“Lilith najua kwanini upo hapa , ila nikuambie tu sipo kwenye mudi nzuti kabisa na nitapenda uondoke”aliongea Roma.

“Mfalme Pluto huwezi kunifukuza na nimekuja mpaka hapa naomba japo kidogo ulichofanya na Malkia wa Wales”aliongea Lilith na kumfanya Roma amwangalie , hakua akifahamu kama Lilith alikuwa akijua kuwa ana mahusiano na Catherine.

“Lilith haina haja ya kujilinganisha na Catherine , Kuwa na mahusiano na Catherine haimaanishi kwamba kila mwanamke nitakubali kuwa nae”Aliongea Roma , lakini kwa upande wa Lilith alionekana kutokata tamaa , mpango wake ni kuhakikisha anashusha kiu yake usiku huo.

“Mfalme Pluto sijilinganishi na Catherine , ila naomba unipokee kama sehemu ya shukrani kwa kile ambacho umetutendea mimi na baba yangu”

“Kuhusu nilichokifanya kule kisiwani kisikusumbue kichwa kabisa , sijawaua Wavatican kwasababu yenu , ila nimefanya vile kutokana na Vatican walichonifanyia miaka kadhaa nyuma , hivyo hauna haja ya kunilipa na naomba uondoke”Aliongea Roma huku akiweka uso wa usiriasi.

“Mfalme Pluto hivi unajua tofauti ya wanawake Vampire na binadamu wa kawaida?”Aliongea Lilith huku akiacha paja wazi na Roma alionekana kutokumuelewa.

“Binadamu damu yao ni ya moto , hivyo pia kwa miili yao kuwa ya moto ndani na nje , lakini kwetu sisi Vampire damu yetu ni ya baridi kama barafu nje na ndani”Aliongea na kumfanya Roma amwangalie Lilith.

Ukweli baada ya maneno hayo kutoka kwa Lilith Roma alijikuta akifikiria kwamba hajawahi kukutana na kitu cha baridi , hivyo shauku ya kujaribu kitu kipya ilimvaa palepale na kwa upande wa Lilith alijua maneno yake yamemgusa penyewe Mfalme Pluto , na alimsogelea na kisha akamkalia mapajani.

“Mfalme Pluto sidhani kama haifanyi kazi”Aliongea Lilith huku akimsogelea Roma kwenye uso na kama ilivyokuwa kwa wanaume wote wasivyopenda kauli ya kudharauliwa ndio kilichotokea kwani Lilith alichapwa bakora za kimkakati.

*******

Saa saba mchana siku iliofuat, ndio muda ambao Edna na Roma waliiacha ardhi ya Ufaransa kurejea Tanzania kwa kutumia ndege ya kampuni ya Fly Emirate.

Edna alishamaliza kile ambacho kilimpeleka Ufaransa ,licha ya kusaini mkataba mnono na kampuni ya mavazi na mitindo ya Luis Vuitton ,lakini pia aliweza kuchagua mtu mwingine wa kuongoza kampuni yake ya Athena na hakubadili tu viongozi wa juu , lakini pia aliweza kupangua mfumo wote wa kiuongozi wa kampuni yake na hii ni kuhakikisha anaepusha ufisadi ndani ya kampuni kutokana na kile kilichotokea kwa Goodman na kwa jinsi alivyoweza kubadili uongozi wa kampuni ilimshangaza Roma kwani ni kama Edna alikuwa na mpango huo tokea anatoka Tanzania , kwani swala la kubadili uongozi kama ni kufanyika lingechukua muda , lakini kwa pande wa Roma hakuuliza.

Taarifa za Goodman kufariki alizipata , lakini licha ya kupata taarifa hizo hakumuuliza Roma chochote , kwani alijua fika kifo cha Goodman ni lazima kimetelekezwa na Roma.

Ukweli tokea siku ya jana yake ya kujikuta kwenye meli ya kivita hakuongea neno lolote na Roma ,yaani alikuwa amemchunia moja kwa moja na hata safari yao ya kurudi Tanzania ilikuwa ni ya kimya kimya, licha ya Roma kiuingiza maneno ya utani kwa Edna lakini hakukua na majibu na Roma hakuona namna ya kumaliza hio vita baridi ilioanzishwa na mke wake na ilimuwia kuwa ngumu mno kutokana na kwamba hakuweza kujua Edna anafikiria nini kwa wakati huo.

Saa tatu kamili Edna na Roma walikamilisha taratibu zote baada ya kufika ndani ya uwanja wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere na walitoka nje ya jengo la kufikia wageni na kupokelewa na Innocent ambaye alikuwa ni dereva wa kampuni na moja kwa moja safari ya Kwenda Kigamboni ilianza.

Kwa upande wa Roma safari nzima alikuwa akiwaza mambo mawili mpaka anafika ndani ya jiji la Dar , jambo la kwanza alilokuwa akiwaza ni juu ya mwanamke aliekuwa amekutana nae ndani ya meli ya Loius XVI, mwanamke aliejitambulisha kwake kama Zoe Kovac , kilichomfanya Roma kumfikiria huyu mwanamke ni kutokana na kwamba aliguswa na sehemu ya Stori ya Zoe pale aliposema alikutana na mwanamke anaemfahamu ndani ya visiwa vya Maldives , jambo hilo lilimfikirisha kwani kwa wanawake wake wote ambao alikuwa nao hapo kabla hawakuwa wakimfahamu kwa jina la Hades na hata wale wanawake ambao alikuwa na uhusiano nao wa karibu ambao walikuwa wakimfahamu, ni ngumu sana Kwenda visiwa vya Maldives na kuamza kuzungumza Habari zake.

Swala la pili ambalo Roma alikuwa akilifikiria ni juu ya mtu ambaye amehusika na kumpokonya HollyGrail Pamoja na Teknolojia ya Thanatos, hisia mbalimbali ziliibuka katika kichwa cha Roma kila alipokumbuka nguvu aliokuwa nayo mtu huyo kiasi cha kwamba hata namna ambavyo alikuwa akitokea alishindwa kabisa kuilelewa.

“Nitatumia Godstone chambo cha kupambana nae tena?”Aliwaza Roma huku akijiambia atatumia Jiwe la kimungu kama chambo kwa ajlii ya kupambana nae tena , na wazo hili lilimjia baada ya kufika Kigamboni.

“Sister Edna..!!!”Ilikuwa ni sauti ilioambatana na kivuli kilichojitokeza mbele ya Edna ambaye ndio kwanza alikuwa akipiga hatua kuelekea ndani huku Roma akiwa nyuma yake.

“Yezi..!”Aliita Edna na kukumbatia na Yezi , hakufahamu ilikuwaje Yezi akawa yupo nyumbani kwake.

*****

Damasi mke wa Raisi Senga alishangazwa na maneno ya mume wake , hakuamini kama siku zote hizo baba mkwe wake alikuwa akifahamu Denisi na Blandina walikuwa hai na alikuwa kimya muda wote pasipo kumwambia mtoto wake..

Alimuonea sana huruma Mume wake , kwani aliamini ni maumivu makubwa sana kudanganywa kwa miaka mingi na mtu ambaye alikuwa akimpenda, kiufupi aliona ni watu wengi ambao walihusika kumdanganya mume wake , Afande kweka mkwe wake , Blandina na Mheshimiwa Kamau ni watu ambao mme wake alikuwa akiwaheshimu sana na kuwapenda sana , lakini watu hao walimuweka kizani kwa miaka yote hio , aliona ni jambao la ajabu sana ambalo wamelifanya na alimuonea huruma sana mume wake juu ya jambo hilo , na aliona ana haki kuwa katika hali aliokuwa nayo, lakini licha ya hivyo yeye alikuwa ndio mke halali wa Senga hivyo hakutaka kumuoana Senga akiumia Zaidi, aliona pasipo kumpa ushauri mzuri mume wake, lakini pia maneno ya Faraja kwa ajili ya kumtuliza , huenda akafanya jambo ambalo sio zuri na likampelekea kuwa katika matatizo.

Na hata pale ambapo Senga alipomueleza mke wake juu ya safari ya Kwenda Kenya siku inayofuata alipinga sana swala hilo.

“Senga sipo tayari kukuona ukienda Kenya?”Aliongea Damasi kwa msisititizo.

“Damasi lazima hili swala nilimalize ,siwezi kuendelea kukaa hapa bila kufanya lolote”

“Baba Ashley, mume wangu , najua ni kipindi kigumu unapitia sasa , lakini licha ya hivyo unatakiwa kutambua kuwa kuna Denisi na Ashley ambao wanakutegemea kama baba , lakini pia usisahau pia kuwa wewe ni raisi wangu wa taifa hili , mimi Pamoja na Raia wote tunakutegemea, maamuzi ya Kwenda Kenya siyaafiki kabisa”Aliongea Damasi kwa msisitizo.

“Damasi unataka nifanye nini kwenye hali kama hii , nikikaa kimya watazidi kuniona mpumbavu na dhaifu ,lazima hili swala nilimalize kwa namna yoyote ile”Aliongea Senga kwa hasira huku akipumua kwa kasi mno na kusababisha kifua chake kupanda na kushuka kwa kasi.

“Kama kweli unataka Kwenda Kenya , ni hatua gani unakwenda kuichukua , je utakwenda kuanza kupigana na Kamau kwa ajili ya kukusaliti au unakwenda kumgombeza Blandina kwa ajili ya kujificha kwa sura ya Maina , Nipe sababu ya kueleweka Senga kwa ajili ya wewe Kwenda Kenya?”Aliongea Damasi huku akianza kupandwa na hasira hata yeye, lakini maswali yake yalionekana kuwa ya maana sana mbele ya raisi Senga , ni kweli alikuwa akitaka Kwenda Kenya , ila mpaka wakati huo hakuwa nasababu maaliuamu ya Kwenda kenya na alishindwa hata kumjibu Damasi swali lake.

“Damasi sijui hata nini napanga kufanya mpaka sasa”

“Ni haki yako Senga kutokufahamu kipi unapaswa kufanya kwa wakati huu , ni kwasababu unapitia wakati mgumu na mimi kama mkeo nipo hapa kwa ajili ya kukusaidia kuvuka katika hali hii unayopitia , ukishatulia utakuwa na majibu sahihi”Aliongea Damasi na kumfanya Senga amwangalie mke wake kwa dakika kadhaa na kisha akamsogelea na kumkumbatia.

“Nakupenda sana mke wangu”Aliongea Mheshimiwa Senga kwa hisia kubwa.

“Nakupenda sana mume wangu”

Maongezi ya Damasi na mume wake Raisi Senga yaliishia kwa Senga kughairisha safari yake ya Kwenda Kenya.

*******

Raisi Kamau tokea siku ambayo Gumilla alirudi pasipo kukamilisha misheni aliompatia hakuwa na amani kabisa , moyo wake ulikuwa kwenye wasiwasi na maumivu mengi , licha ya kwamba ni maamuzi yake mwenyewe aliofanya miaka kadhaa nyuma ya kuhakikisha Blandina anakaa mbali na Senga na hata kuamua kumuoa kabisa , lakini bwana huyu leo hii baada ya rafiki yake wa muda mwingi Senga kuambiwa juu ya uwepo wa Blandina ulimfanya kukosa amani na kujutia kwa matendo yake.

Leo ni siku ya tano mke wake Blandina hakuwa tayari kuongea nae kabisa na alikuwa amemchunia na msimamo wake wa kutotaka kuendelea kubaki hapo ikulu ukiwa upo vilevile.

“Njiro hakikisha ulinzi unaongezeka kwa mke wangu sitaki mtu yoyote kuonana nae”

“Sawa mheshimiwa” Aliitikia Njiro mara baada ya kuitwa ofisini na mheshimiwa Kamau.

“Pia haruhusiwi kupata kifaa chochote cha mawasiliano ukitokea uzembe wa aina yoyote kama uliotokea Tanzania basi jua kazi huna tena”

“Sawa mheshimiwa nitazingatia”

“Okey unaweza Kwenda”Aliongea na Njiro alievalia suti na viatu vyake vya Skuna alitoka ndani ya ofisi hio ya mheshimiwa kwa ajili ya Kwenda kuendelea na majukumu ya kumlinda Maina ili asiweze kuonana na mtu yoyote.

Baada ya Maina kutoka , aliingia na Deo ndani ya ofisi ya mheshimiwa na alionekana na yeye aliitwa ndani ya ofisi hio.

“Nipe Ripoti”

“Hakuna hatua yoyote ambayo mheshimiwa Senga amechukua mpaka sasa”Aliongea Deo.

“Okey , hakikisha unanipa taarifa ya kile kinachoendelea , wasiliana na wanausalama wetu Tanzania kuongeza umakini”

“Sawa mheshimiwa”

“Deo..!!”Aliita Mheshimiwa baada ya Deo kukaribia mlango wa kutokea.

“Ndio mheshimiwa”

“Nataka pia taarifa zinazomuhusu Roma Ramoni kwa kila anachokifanya ndani ya Tanzania , Tafuta mtu kwa ajili ya kazi hio”

“Sawa mheshimiwa”Alijibu Deo na kisha akatoka nje.

Licha ya Kamau kumfungia Maina , lakini alikuwa na hofu na Roma mno aliamini yeye ndio enaeweza kuwa kikwazo cha kumzuia Blandina kubakia ndani ya ikulun, taarifa ya Roma aliokuwa nayo haikuwa ndogo kabisa na alijua kwa uwezo aliokuwa nao Roma kama atajua mama yake amefungiwa ndani ya ikulu yake ni Dhahiri angechukua hatua
 
SEHEMU YA 210

Kwa maelezo ya Bi Wema ni kwamba Yezi alivamiwa sehemu aliokuwa amepanga na majambazi maarufu kama Panya Road na kumpokonya kila kitu na tukio hilo mara baada ya kumfikia Mama Issa kutoka kituo cha kuelelea Yatima aliomba Yezi Akaishi kwanza kwa Edna, huku akitafuta namna nzuti ya kuhakikisha anaishi kwenye mazingira yaliosalama.

Baada ya Edna na Roma kusikia maelezo hayo kutoka kwa Bi Wema walijikuta wakiwa na wasiwasi mno lakini pia kushukuru kwa wakati mmoja kwa Yezi kutopata Majeraha makubwa na waliona ni jambo zuri kwa Yezi kuja kuishi hapo, licha ya Mama Issa kuomba Yezi kukaa kwa muda , ila kwa Edna aliona litakuwa jambo zuri kama Yezi atakaa moja kwa moja.

“Yezi utaishi na sisi haina haja ya kuhama na Kwenda kupanga sehemu nyingine”Aliongea Edna.

“Lakini site…”

“Wife umeongea pointi ,,, Yezi kwanzia leo utaishi na sisi…. hakuna cha lakini… utaishi na sisi hapa ili kumpunguzia Mama Issa wasiwasi”Aliongea Roma na kuanza kupiga hatua kuelekea kwenye chumba chake kwani alikuwa amechoka muda huo kutokana na safari na hivyo hivyo kwa upande wa Edna.

Sophia aliekuwa eneo la Sebuleni aliona jambo ambalo halipo sawa kwa wanandoa hawa , kwani walivyoondoka sio kama walivyorudi, kitendo cha Edna kutokumuanngalia Roma machoni kilionyesha hali isiokuwa ya kawaida.

Sio kwa Sophia tu hata kwa Bi Wema pia aliona ni kama umbali kimahusiano uliokuwa kati ya Edna na Roma umeongezeka na sio kupungua , Bi Wema ukweli alikuwa akitegemea kuona wawili hao wakirudi kuwa wanandoa halisi ambao wapo tayari kwa ajili ya kulala chumba kimoja, lakini pia kuona mapenzi moto moto kutoka kwa Edna Kwenda kwa Roma.

Bi Wema na Sophia waliishia kuangaliana machoni na kisha wakatingisha vichwa vyo kuonyesha ishara ya masikitiko na kumfanya Yezi ambaye hakuwa akielewa chochcote asielewe kinachoendelea.

Naam ilikuwa ni siku nyingine ya jumatatu Edna baada ya Edna kuelekea kazini , Roma ndio kwanza alikuwa akiamka na alijishangaa kwa siku hio kulala muda mrefu kuliko isivyokuwa kawaida na leo kwasababu alikuwa amechelewa kuamka hakuona sababu ya Kwenda kuchukua mazoezi kama ilivyokuwa ratiba yake, bali alikua na jambo lingine kichwani.

Na baada ya kusalimia na Bi Wema aliekuwa bize na kazi za ndani ,moja kwa moja alielekea ndani ya chumba cha kufanyia mazoezi na kufungua sehemu ambayo alificha kiboksi ambacho alitoka nacho Mhagala , kiboksi ambacho alikuwa akikitumia kuhifadhia jiwe la Kimungu.

Baada ya kutoa kiboksi kile na kukishika mkononi alikifungua ndani na kisha akatoa Jiwe la kimungu na kulikweka mkononi na kufanya chumba chote kuwa na rangi ya bluu na ya rangi nyeupe ambayo imechanganyika , mwanga ambao ulisababishwa na mng`ao uliokuwa ukitolewa na jiwe ambalo lilionekana kuwa kama kitenesi kwenye mikono ya Roma.

Haikueleweka Roma alikuwa na mpango gani na jiwe hilo , ila alilitia mfukoni kwenye Tracksuit na kisha akafunga kile kiboksi na kurudi chumbani kwake ,na baada ya kuingia ndani ya chumba chake alibadilisha mavazi yake na kuvaa tisheti na Jeans Pamoja na Raba na kisha alitoa lile jiwe na kuliweka mfukoni na akachukua na ufunguo wa gari na kutoka.

“Mr Roma kifungua kinywa kipo tayari?”Aliongea Bi Wema

“Bi Wema usijali leo nitakunywa mbele kwa mbele kuna sehemu ninaenda mara moja”Aliongea Roma na Bi Wema hakuwa na haja ya kumlazimisha na aliishia kumwangalia akitokomea nje kabisa.

Roma baada ya kutoka na gari yake moja kwa moja alichukua uelekeo wa Mbutu na ndani ya dakika chache tu aliingiza gari yake ndani ya geti la kambi ya wanajeshi wake wa The Eagles na kusimamisha gari.

“Mfalme Pluto karibu sana?”Aliongea Diego mara baada ya Roma kutoka kwenye gari na Roma alimshika Diego begani kwa kumpiga piga na kutangulia ndani.

“Diego leo sijaja kwa ajili ya kupata ripoti ila kama kuna jambo muhimu sana nataka mnieleze baada ya kumaliza kazi yangu”Aliongea Roma na kumfanya Diego ashangae , hakuelewa Roma alikuwa akimaanisha nini akisema kazi yake.

“Mfalme kuna msaada wowote unataka kutoka kwetu juu ya kazi yako?”Aliongea Diego na kumfanya Roma afikirie kidogo na kisha akamwangalia Diego.

“Kuna njia yoyote ya kuweza kugundua namna ya mtu anavyoweza kucheza na muda”

“Mudaa..!!, Mfalme sijakuelewa bado”Aliongea Diego ni kweli hakuelewa kwani neno aliloongea Roma lilikuwa nje ya fani yake.

“Ndio nataka kujua kama kuna kanuni ambayo inamuwezesha mtu kucheza na kanunuzi za Anga na kufanya muda kusimama au kurudi nyuma”

“Mfalme Pluto jambo ambalo unazungumza hatujawahi kulisikia”Aliongea Diego na kumfanya Roma atabasamu , aliona nikweli alichoongea kisingeleta mantiki kwenye kichwa cha Diego ndio maana kila jambo linalotokea na kumhusu mtu mwenye nguvu kuliko yeye alishindwa kulielezea.

“Diego hupaswi kufikiria sana , kwasababu umeshindwa kuelewa swali langu naamini ni jambo ambalo pia haliwezekani na nashindwa kulitolea maelezo”

“”Mfalme Pluto naomba niyafikirie maneno yako kwa muda huenda nikayaelewa”

“Usisumbuke Diego, nipo kwenye bustani nje , nikimaliza kazi yangu nitarejea hapa kwa ajili ya maelezo mengine”Aliongea Roma huku akinyanyka na kutoka ndani ya jumba hili la kifahari la Rose ambalo Roma aliligeuza kama sehemu ya makazi ya wanajeshi wake.

Kutokanana ukubwa wa Eneo la jumba hili, ilifanya kubakie eneo kubwa ambalo Rose alilifanya kama bustani na Roma mara baada ya kukagua eneo lote alionyesha hali ya kuridhika na kisha akajongea mpaka katikati.

Baada ya kusimama sehemu ambayo alihisi inafaa , alitoa jiwe la kimungu na kuliweka kwenye mikono yake na kufanya jiwe hilo litowe mwanga mkali wa kuumiza macho baada ya kupigwa na jua.

Roma akiwa ameangalia jiwe lililokuwa kwenye mikono yake palepale alibadilisha macho yake na kuwa mekundu huku kiini cha jicho lake kikibadilika rangi na kuwa cha Rangi ya Maji(Aqua), Roma haikueleweka anafanya nini , lakini palepale macho yake yote aliyaelekeza kwenye jiwe la kimungu pasipo kupepesa macho na kufanya mwanga mkali wa kuvutia uliokuwa ukitoka kwenye jiwe la Kimungu kupinda na kujikusanya wote kwa Pamoja na kugonga kwenye macho ya Roma kwa kasi mno, huku Roma na yeye kutokuonyesha hali yoyote ya kudhurika na mwanga huo.

Kitendo ambacho alikuwa akikifanya Roma kiliendelea kwa dakika kama mbili tu na jiwe ambalo lilikuwa kwenye mkono wake lilionekana kuongezeka ukubwa marafudufu kiasi kwamba lilionekana kama mpira unatoa mwanga wa rangi ya Ultraviolet na awamu hii jiwe halikuegamia kwenye mikono ya Roma ila lilielea juu kwa nchi kadhaa kutoka kwenye kiganja cha mkono na kufanya lizunguke kwa spidi huku mwanga wake kama wa Laser ukiendelea kujikusanya kwenye macho ya Roma na kutengeneza alama ya V. ilioinamishwa.

“Arrggh…!!!”Roma alitoa mlio wa mamivu na palepale macho yake yakarudi kwenye hali ya kawaida na jiwe lile lilirudi kwenye ukubwa wake halisi huku likitua mikononi.

“Hii mbinu haifanyi kazi”Aliwaza Roma na kuchukua jiwe lake na kuliingiza mfukoni na kugeuka na kuanza kupiga hatua kuelekea ndani.

Lakini sasa kabla hajamaliza kunyanyua mguu mwingine , alijikutuka akidondoka kama vile mtu aliepigwa mtama na ile anataka kutua chini , alijikuta akiinuliwa kwa kasi ya ajabu sana Kwenda juu na kumfanya miguu iwe juu na kichwa kiwe chini na kutokana ughafla wa kitendo kile alijikuta akipata akili na kupelekea mikono yake kuelekea upande wa mfukoni , lakini ni kama amechelewa kwani ile anafikisha mkono kwenye mfuko wake wa suruali ambao alikuwa amehifadhia jiwe la Kimungu, mwili wake uliganda hewnai yaani licha ya kwamba mwanzoni alikuwa akielea pasipo kujua ni nguvu gani iliomshikilia na kumfanya aeleee , lakini muda huo huo mkono wake uliganda Ghalfa.

“Sh*****t! muda muda umesimama”Aliwaza Roma huku macho yake yakibadilika rangi na kuwa ya njano.

“Puu…!!!”

Roma alidondoka chini kama gunia baada ya nguvu iliokuwa imeshikilia kumuachia na haraka haraka , alisimama na kupeleka mikono yake kwenye mifuko wake wa Suruali kwa ajili ya kutafuta lile jiwe lakini alichokutana nacho kilimfanya macho kuongezeka ukubwa palepale.

Roma kwenye mfuko wake wa Suruali aliweza kutoa kichuma flani hivi cha mstatiri kidogo sana kama holder ya Ufunguo kilichofungwa na mkufu wa madini ya Silver.

“Athena” Ndio maneno yaliokuwa yameandikwa upande wa kulia , The Doni ndio maneno yalioandikwa upande wa Nyuma.

Akili ya Roma ni kama haikuwa ikifanya kazi vizuri , mpaka hapo ashaelewa mtu ambaye hakuwa na nguvu za kawaida sasa anamfahamu kwa jina lake halisi

“The Doni kumbe ndio Athena kwanini sikufikiria hili mapema!!!???”Roma alijiuliza kwa mshangao mkubwa.

MWISHO WA SEASON 7 NICHEKI WATSAPP 0687151346

NGOJA TUPATE WADHAMINI , ITAKUJA KUENDELEA
 
SEHEMU YA 210

Kwa maelezo ya Bi Wema ni kwamba Yezi alivamiwa sehemu aliokuwa amepanga na majambazi maarufu kama Panya Road na kumpokonya kila kitu na tukio hilo mara baada ya kumfikia Mama Issa kutoka kituo cha kuelelea Yatima aliomba Yezi Akaishi kwanza kwa Edna, huku akitafuta namna nzuti ya kuhakikisha anaishi kwenye mazingira yaliosalama.

Baada ya Edna na Roma kusikia maelezo hayo kutoka kwa Bi Wema walijikuta wakiwa na wasiwasi mno lakini pia kushukuru kwa wakati mmoja kwa Yezi kutopata Majeraha makubwa na waliona ni jambo zuri kwa Yezi kuja kuishi hapo, licha ya Mama Issa kuomba Yezi kukaa kwa muda , ila kwa Edna aliona litakuwa jambo zuri kama Yezi atakaa moja kwa moja.

“Yezi utaishi na sisi haina haja ya kuhama na Kwenda kupanga sehemu nyingine”Aliongea Edna.

“Lakini site…”

“Wife umeongea pointi ,,, Yezi kwanzia leo utaishi na sisi…. hakuna cha lakini… utaishi na sisi hapa ili kumpunguzia Mama Issa wasiwasi”Aliongea Roma na kuanza kupiga hatua kuelekea kwenye chumba chake kwani alikuwa amechoka muda huo kutokana na safari na hivyo hivyo kwa upande wa Edna.

Sophia aliekuwa eneo la Sebuleni aliona jambo ambalo halipo sawa kwa wanandoa hawa , kwani walivyoondoka sio kama walivyorudi, kitendo cha Edna kutokumuanngalia Roma machoni kilionyesha hali isiokuwa ya kawaida.

Sio kwa Sophia tu hata kwa Bi Wema pia aliona ni kama umbali kimahusiano uliokuwa kati ya Edna na Roma umeongezeka na sio kupungua , Bi Wema ukweli alikuwa akitegemea kuona wawili hao wakirudi kuwa wanandoa halisi ambao wapo tayari kwa ajili ya kulala chumba kimoja, lakini pia kuona mapenzi moto moto kutoka kwa Edna Kwenda kwa Roma.

Bi Wema na Sophia waliishia kuangaliana machoni na kisha wakatingisha vichwa vyo kuonyesha ishara ya masikitiko na kumfanya Yezi ambaye hakuwa akielewa chochcote asielewe kinachoendelea.

Naam ilikuwa ni siku nyingine ya jumatatu Edna baada ya Edna kuelekea kazini , Roma ndio kwanza alikuwa akiamka na alijishangaa kwa siku hio kulala muda mrefu kuliko isivyokuwa kawaida na leo kwasababu alikuwa amechelewa kuamka hakuona sababu ya Kwenda kuchukua mazoezi kama ilivyokuwa ratiba yake, bali alikua na jambo lingine kichwani.

Na baada ya kusalimia na Bi Wema aliekuwa bize na kazi za ndani ,moja kwa moja alielekea ndani ya chumba cha kufanyia mazoezi na kufungua sehemu ambayo alificha kiboksi ambacho alitoka nacho Mhagala , kiboksi ambacho alikuwa akikitumia kuhifadhia jiwe la Kimungu.

Baada ya kutoa kiboksi kile na kukishika mkononi alikifungua ndani na kisha akatoa Jiwe la kimungu na kulikweka mkononi na kufanya chumba chote kuwa na rangi ya bluu na ya rangi nyeupe ambayo imechanganyika , mwanga ambao ulisababishwa na mng`ao uliokuwa ukitolewa na jiwe ambalo lilionekana kuwa kama kitenesi kwenye mikono ya Roma.

Haikueleweka Roma alikuwa na mpango gani na jiwe hilo , ila alilitia mfukoni kwenye Tracksuit na kisha akafunga kile kiboksi na kurudi chumbani kwake ,na baada ya kuingia ndani ya chumba chake alibadilisha mavazi yake na kuvaa tisheti na Jeans Pamoja na Raba na kisha alitoa lile jiwe na kuliweka mfukoni na akachukua na ufunguo wa gari na kutoka.

“Mr Roma kifungua kinywa kipo tayari?”Aliongea Bi Wema

“Bi Wema usijali leo nitakunywa mbele kwa mbele kuna sehemu ninaenda mara moja”Aliongea Roma na Bi Wema hakuwa na haja ya kumlazimisha na aliishia kumwangalia akitokomea nje kabisa.

Roma baada ya kutoka na gari yake moja kwa moja alichukua uelekeo wa Mbutu na ndani ya dakika chache tu aliingiza gari yake ndani ya geti la kambi ya wanajeshi wake wa The Eagles na kusimamisha gari.

“Mfalme Pluto karibu sana?”Aliongea Diego mara baada ya Roma kutoka kwenye gari na Roma alimshika Diego begani kwa kumpiga piga na kutangulia ndani.

“Diego leo sijaja kwa ajili ya kupata ripoti ila kama kuna jambo muhimu sana nataka mnieleze baada ya kumaliza kazi yangu”Aliongea Roma na kumfanya Diego ashangae , hakuelewa Roma alikuwa akimaanisha nini akisema kazi yake.

“Mfalme kuna msaada wowote unataka kutoka kwetu juu ya kazi yako?”Aliongea Diego na kumfanya Roma afikirie kidogo na kisha akamwangalia Diego.

“Kuna njia yoyote ya kuweza kugundua namna ya mtu anavyoweza kucheza na muda”

“Mudaa..!!, Mfalme sijakuelewa bado”Aliongea Diego ni kweli hakuelewa kwani neno aliloongea Roma lilikuwa nje ya fani yake.

“Ndio nataka kujua kama kuna kanuni ambayo inamuwezesha mtu kucheza na kanunuzi za Anga na kufanya muda kusimama au kurudi nyuma”

“Mfalme Pluto jambo ambalo unazungumza hatujawahi kulisikia”Aliongea Diego na kumfanya Roma atabasamu , aliona nikweli alichoongea kisingeleta mantiki kwenye kichwa cha Diego ndio maana kila jambo linalotokea na kumhusu mtu mwenye nguvu kuliko yeye alishindwa kulielezea.

“Diego hupaswi kufikiria sana , kwasababu umeshindwa kuelewa swali langu naamini ni jambo ambalo pia haliwezekani na nashindwa kulitolea maelezo”

“”Mfalme Pluto naomba niyafikirie maneno yako kwa muda huenda nikayaelewa”

“Usisumbuke Diego, nipo kwenye bustani nje , nikimaliza kazi yangu nitarejea hapa kwa ajili ya maelezo mengine”Aliongea Roma huku akinyanyka na kutoka ndani ya jumba hili la kifahari la Rose ambalo Roma aliligeuza kama sehemu ya makazi ya wanajeshi wake.

Kutokanana ukubwa wa Eneo la jumba hili, ilifanya kubakie eneo kubwa ambalo Rose alilifanya kama bustani na Roma mara baada ya kukagua eneo lote alionyesha hali ya kuridhika na kisha akajongea mpaka katikati.

Baada ya kusimama sehemu ambayo alihisi inafaa , alitoa jiwe la kimungu na kuliweka kwenye mikono yake na kufanya jiwe hilo litowe mwanga mkali wa kuumiza macho baada ya kupigwa na jua.

Roma akiwa ameangalia jiwe lililokuwa kwenye mikono yake palepale alibadilisha macho yake na kuwa mekundu huku kiini cha jicho lake kikibadilika rangi na kuwa cha Rangi ya Maji(Aqua), Roma haikueleweka anafanya nini , lakini palepale macho yake yote aliyaelekeza kwenye jiwe la kimungu pasipo kupepesa macho na kufanya mwanga mkali wa kuvutia uliokuwa ukitoka kwenye jiwe la Kimungu kupinda na kujikusanya wote kwa Pamoja na kugonga kwenye macho ya Roma kwa kasi mno, huku Roma na yeye kutokuonyesha hali yoyote ya kudhurika na mwanga huo.

Kitendo ambacho alikuwa akikifanya Roma kiliendelea kwa dakika kama mbili tu na jiwe ambalo lilikuwa kwenye mkono wake lilionekana kuongezeka ukubwa marafudufu kiasi kwamba lilionekana kama mpira unatoa mwanga wa rangi ya Ultraviolet na awamu hii jiwe halikuegamia kwenye mikono ya Roma ila lilielea juu kwa nchi kadhaa kutoka kwenye kiganja cha mkono na kufanya lizunguke kwa spidi huku mwanga wake kama wa Laser ukiendelea kujikusanya kwenye macho ya Roma na kutengeneza alama ya V. ilioinamishwa.

“Arrggh…!!!”Roma alitoa mlio wa mamivu na palepale macho yake yakarudi kwenye hali ya kawaida na jiwe lile lilirudi kwenye ukubwa wake halisi huku likitua mikononi.

“Hii mbinu haifanyi kazi”Aliwaza Roma na kuchukua jiwe lake na kuliingiza mfukoni na kugeuka na kuanza kupiga hatua kuelekea ndani.

Lakini sasa kabla hajamaliza kunyanyua mguu mwingine , alijikutuka akidondoka kama vile mtu aliepigwa mtama na ile anataka kutua chini , alijikuta akiinuliwa kwa kasi ya ajabu sana Kwenda juu na kumfanya miguu iwe juu na kichwa kiwe chini na kutokana ughafla wa kitendo kile alijikuta akipata akili na kupelekea mikono yake kuelekea upande wa mfukoni , lakini ni kama amechelewa kwani ile anafikisha mkono kwenye mfuko wake wa suruali ambao alikuwa amehifadhia jiwe la Kimungu, mwili wake uliganda hewnai yaani licha ya kwamba mwanzoni alikuwa akielea pasipo kujua ni nguvu gani iliomshikilia na kumfanya aeleee , lakini muda huo huo mkono wake uliganda Ghalfa.

“Sh*****t! muda muda umesimama”Aliwaza Roma huku macho yake yakibadilika rangi na kuwa ya njano.

“Puu…!!!”

Roma alidondoka chini kama gunia baada ya nguvu iliokuwa imeshikilia kumuachia na haraka haraka , alisimama na kupeleka mikono yake kwenye mifuko wake wa Suruali kwa ajili ya kutafuta lile jiwe lakini alichokutana nacho kilimfanya macho kuongezeka ukubwa palepale.

Roma kwenye mfuko wake wa Suruali aliweza kutoa kichuma flani hivi cha mstatiri kidogo sana kama holder ya Ufunguo kilichofungwa na mkufu wa madini ya Silver.

“Athena” Ndio maneno yaliokuwa yameandikwa upande wa kulia , The Doni ndio maneno yalioandikwa upande wa Nyuma.

Akili ya Roma ni kama haikuwa ikifanya kazi vizuri , mpaka hapo ashaelewa mtu ambaye hakuwa na nguvu za kawaida sasa anamfahamu kwa jina lake halisi

“The Doni kumbe ndio Athena kwanini sikufikiria hili mapema!!!???”Roma alijiuliza kwa mshangao mkubwa.

MWISHO WA SEASON 7 NICHEKI WATSAPP 0687151346

NGOJA TUPATE WADHAMINI , ITAKUJA KUENDELEA
Daaah Mkuu ngoma inapamba moto....., Huu mzigo unaendelea leo au[emoji39][emoji39][emoji39]
 
Halafu mnaopenda kulalamika kabla ya siku tuliyo ahidiwa kutumiwa simulizi haijaisha muwe mnaona aibu kama mna haraka muwe mnalipia mtumiwe whatsapp.

Mkuu singanojr Asante sana Kaka. Halafu nilikuuliza nikiitaka hii simulizi yote kutoka Sehemu ya kwanza inakuwa ni shilling ngapi? Hukunijibu

Sent from my SM-J700H using JamiiForums mobile app
 
SEHEMU YA 210

Kwa maelezo ya Bi Wema ni kwamba Yezi alivamiwa sehemu aliokuwa amepanga na majambazi maarufu kama Panya Road na kumpokonya kila kitu na tukio hilo mara baada ya kumfikia Mama Issa kutoka kituo cha kuelelea Yatima aliomba Yezi Akaishi kwanza kwa Edna, huku akitafuta namna nzuti ya kuhakikisha anaishi kwenye mazingira yaliosalama.

Baada ya Edna na Roma kusikia maelezo hayo kutoka kwa Bi Wema walijikuta wakiwa na wasiwasi mno lakini pia kushukuru kwa wakati mmoja kwa Yezi kutopata Majeraha makubwa na waliona ni jambo zuri kwa Yezi kuja kuishi hapo, licha ya Mama Issa kuomba Yezi kukaa kwa muda , ila kwa Edna aliona litakuwa jambo zuri kama Yezi atakaa moja kwa moja.

“Yezi utaishi na sisi haina haja ya kuhama na Kwenda kupanga sehemu nyingine”Aliongea Edna.

“Lakini site…”

“Wife umeongea pointi ,,, Yezi kwanzia leo utaishi na sisi…. hakuna cha lakini… utaishi na sisi hapa ili kumpunguzia Mama Issa wasiwasi”Aliongea Roma na kuanza kupiga hatua kuelekea kwenye chumba chake kwani alikuwa amechoka muda huo kutokana na safari na hivyo hivyo kwa upande wa Edna.

Sophia aliekuwa eneo la Sebuleni aliona jambo ambalo halipo sawa kwa wanandoa hawa , kwani walivyoondoka sio kama walivyorudi, kitendo cha Edna kutokumuanngalia Roma machoni kilionyesha hali isiokuwa ya kawaida.

Sio kwa Sophia tu hata kwa Bi Wema pia aliona ni kama umbali kimahusiano uliokuwa kati ya Edna na Roma umeongezeka na sio kupungua , Bi Wema ukweli alikuwa akitegemea kuona wawili hao wakirudi kuwa wanandoa halisi ambao wapo tayari kwa ajili ya kulala chumba kimoja, lakini pia kuona mapenzi moto moto kutoka kwa Edna Kwenda kwa Roma.

Bi Wema na Sophia waliishia kuangaliana machoni na kisha wakatingisha vichwa vyo kuonyesha ishara ya masikitiko na kumfanya Yezi ambaye hakuwa akielewa chochcote asielewe kinachoendelea.

Naam ilikuwa ni siku nyingine ya jumatatu Edna baada ya Edna kuelekea kazini , Roma ndio kwanza alikuwa akiamka na alijishangaa kwa siku hio kulala muda mrefu kuliko isivyokuwa kawaida na leo kwasababu alikuwa amechelewa kuamka hakuona sababu ya Kwenda kuchukua mazoezi kama ilivyokuwa ratiba yake, bali alikua na jambo lingine kichwani.

Na baada ya kusalimia na Bi Wema aliekuwa bize na kazi za ndani ,moja kwa moja alielekea ndani ya chumba cha kufanyia mazoezi na kufungua sehemu ambayo alificha kiboksi ambacho alitoka nacho Mhagala , kiboksi ambacho alikuwa akikitumia kuhifadhia jiwe la Kimungu.

Baada ya kutoa kiboksi kile na kukishika mkononi alikifungua ndani na kisha akatoa Jiwe la kimungu na kulikweka mkononi na kufanya chumba chote kuwa na rangi ya bluu na ya rangi nyeupe ambayo imechanganyika , mwanga ambao ulisababishwa na mng`ao uliokuwa ukitolewa na jiwe ambalo lilionekana kuwa kama kitenesi kwenye mikono ya Roma.

Haikueleweka Roma alikuwa na mpango gani na jiwe hilo , ila alilitia mfukoni kwenye Tracksuit na kisha akafunga kile kiboksi na kurudi chumbani kwake ,na baada ya kuingia ndani ya chumba chake alibadilisha mavazi yake na kuvaa tisheti na Jeans Pamoja na Raba na kisha alitoa lile jiwe na kuliweka mfukoni na akachukua na ufunguo wa gari na kutoka.

“Mr Roma kifungua kinywa kipo tayari?”Aliongea Bi Wema

“Bi Wema usijali leo nitakunywa mbele kwa mbele kuna sehemu ninaenda mara moja”Aliongea Roma na Bi Wema hakuwa na haja ya kumlazimisha na aliishia kumwangalia akitokomea nje kabisa.

Roma baada ya kutoka na gari yake moja kwa moja alichukua uelekeo wa Mbutu na ndani ya dakika chache tu aliingiza gari yake ndani ya geti la kambi ya wanajeshi wake wa The Eagles na kusimamisha gari.

“Mfalme Pluto karibu sana?”Aliongea Diego mara baada ya Roma kutoka kwenye gari na Roma alimshika Diego begani kwa kumpiga piga na kutangulia ndani.

“Diego leo sijaja kwa ajili ya kupata ripoti ila kama kuna jambo muhimu sana nataka mnieleze baada ya kumaliza kazi yangu”Aliongea Roma na kumfanya Diego ashangae , hakuelewa Roma alikuwa akimaanisha nini akisema kazi yake.

“Mfalme kuna msaada wowote unataka kutoka kwetu juu ya kazi yako?”Aliongea Diego na kumfanya Roma afikirie kidogo na kisha akamwangalia Diego.

“Kuna njia yoyote ya kuweza kugundua namna ya mtu anavyoweza kucheza na muda”

“Mudaa..!!, Mfalme sijakuelewa bado”Aliongea Diego ni kweli hakuelewa kwani neno aliloongea Roma lilikuwa nje ya fani yake.

“Ndio nataka kujua kama kuna kanuni ambayo inamuwezesha mtu kucheza na kanunuzi za Anga na kufanya muda kusimama au kurudi nyuma”

“Mfalme Pluto jambo ambalo unazungumza hatujawahi kulisikia”Aliongea Diego na kumfanya Roma atabasamu , aliona nikweli alichoongea kisingeleta mantiki kwenye kichwa cha Diego ndio maana kila jambo linalotokea na kumhusu mtu mwenye nguvu kuliko yeye alishindwa kulielezea.

“Diego hupaswi kufikiria sana , kwasababu umeshindwa kuelewa swali langu naamini ni jambo ambalo pia haliwezekani na nashindwa kulitolea maelezo”

“”Mfalme Pluto naomba niyafikirie maneno yako kwa muda huenda nikayaelewa”

“Usisumbuke Diego, nipo kwenye bustani nje , nikimaliza kazi yangu nitarejea hapa kwa ajili ya maelezo mengine”Aliongea Roma huku akinyanyka na kutoka ndani ya jumba hili la kifahari la Rose ambalo Roma aliligeuza kama sehemu ya makazi ya wanajeshi wake.

Kutokanana ukubwa wa Eneo la jumba hili, ilifanya kubakie eneo kubwa ambalo Rose alilifanya kama bustani na Roma mara baada ya kukagua eneo lote alionyesha hali ya kuridhika na kisha akajongea mpaka katikati.

Baada ya kusimama sehemu ambayo alihisi inafaa , alitoa jiwe la kimungu na kuliweka kwenye mikono yake na kufanya jiwe hilo litowe mwanga mkali wa kuumiza macho baada ya kupigwa na jua.

Roma akiwa ameangalia jiwe lililokuwa kwenye mikono yake palepale alibadilisha macho yake na kuwa mekundu huku kiini cha jicho lake kikibadilika rangi na kuwa cha Rangi ya Maji(Aqua), Roma haikueleweka anafanya nini , lakini palepale macho yake yote aliyaelekeza kwenye jiwe la kimungu pasipo kupepesa macho na kufanya mwanga mkali wa kuvutia uliokuwa ukitoka kwenye jiwe la Kimungu kupinda na kujikusanya wote kwa Pamoja na kugonga kwenye macho ya Roma kwa kasi mno, huku Roma na yeye kutokuonyesha hali yoyote ya kudhurika na mwanga huo.

Kitendo ambacho alikuwa akikifanya Roma kiliendelea kwa dakika kama mbili tu na jiwe ambalo lilikuwa kwenye mkono wake lilionekana kuongezeka ukubwa marafudufu kiasi kwamba lilionekana kama mpira unatoa mwanga wa rangi ya Ultraviolet na awamu hii jiwe halikuegamia kwenye mikono ya Roma ila lilielea juu kwa nchi kadhaa kutoka kwenye kiganja cha mkono na kufanya lizunguke kwa spidi huku mwanga wake kama wa Laser ukiendelea kujikusanya kwenye macho ya Roma na kutengeneza alama ya V. ilioinamishwa.

“Arrggh…!!!”Roma alitoa mlio wa mamivu na palepale macho yake yakarudi kwenye hali ya kawaida na jiwe lile lilirudi kwenye ukubwa wake halisi huku likitua mikononi.

“Hii mbinu haifanyi kazi”Aliwaza Roma na kuchukua jiwe lake na kuliingiza mfukoni na kugeuka na kuanza kupiga hatua kuelekea ndani.

Lakini sasa kabla hajamaliza kunyanyua mguu mwingine , alijikutuka akidondoka kama vile mtu aliepigwa mtama na ile anataka kutua chini , alijikuta akiinuliwa kwa kasi ya ajabu sana Kwenda juu na kumfanya miguu iwe juu na kichwa kiwe chini na kutokana ughafla wa kitendo kile alijikuta akipata akili na kupelekea mikono yake kuelekea upande wa mfukoni , lakini ni kama amechelewa kwani ile anafikisha mkono kwenye mfuko wake wa suruali ambao alikuwa amehifadhia jiwe la Kimungu, mwili wake uliganda hewnai yaani licha ya kwamba mwanzoni alikuwa akielea pasipo kujua ni nguvu gani iliomshikilia na kumfanya aeleee , lakini muda huo huo mkono wake uliganda Ghalfa.

“Sh*****t! muda muda umesimama”Aliwaza Roma huku macho yake yakibadilika rangi na kuwa ya njano.

“Puu…!!!”

Roma alidondoka chini kama gunia baada ya nguvu iliokuwa imeshikilia kumuachia na haraka haraka , alisimama na kupeleka mikono yake kwenye mifuko wake wa Suruali kwa ajili ya kutafuta lile jiwe lakini alichokutana nacho kilimfanya macho kuongezeka ukubwa palepale.

Roma kwenye mfuko wake wa Suruali aliweza kutoa kichuma flani hivi cha mstatiri kidogo sana kama holder ya Ufunguo kilichofungwa na mkufu wa madini ya Silver.

“Athena” Ndio maneno yaliokuwa yameandikwa upande wa kulia , The Doni ndio maneno yalioandikwa upande wa Nyuma.

Akili ya Roma ni kama haikuwa ikifanya kazi vizuri , mpaka hapo ashaelewa mtu ambaye hakuwa na nguvu za kawaida sasa anamfahamu kwa jina lake halisi

“The Doni kumbe ndio Athena kwanini sikufikiria hili mapema!!!???”Roma alijiuliza kwa mshangao mkubwa.

MWISHO WA SEASON 7 NICHEKI WATSAPP 0687151346

NGOJA TUPATE WADHAMINI , ITAKUJA KUENDELEA
9L678F5AFLN Imethibitishwa. ISSAI SINGANO amepokea 2000.00 tarehe 20221206214735.
Nimelipia huko ila sijaipata mwendelezo na WhatsApp hujibu.
 
Halafu mnaopenda kulalamika kabla ya siku tuliyo ahidiwa kutumiwa simulizi haijaisha muwe mnaona aibu kama mna haraka muwe mnalipia mtumiwe whatsapp.

Mkuu singanojr Asante sana Kaka. Halafu nilikuuliza nikiitaka hii simulizi yote kutoka Sehemu ya kwanza inakuwa ni shilling ngapi? Hukunijibu

Sent from my SM-J700H using JamiiForums mobile app
Simulizi na3ndelea kuandika ipo sehemu ya 270 season 9 unaweza kunicheki watsapp utatumiwa kuanzia 210 mpaka 270
 
Back
Top Bottom