Rogers luyangi
JF-Expert Member
- Sep 15, 2014
- 552
- 948
Arosto
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Simulixi nzuri sanaSEHEMU YA KUMI NA SABA
Kwa jinsi Roma alivyokuwa anaendesha gari , kila mtu alishangazwa na uwezo huo , Roma alikuwa akikwepa magari kama chizi kitendo ambacho wengi walidhania ni kama Muvi , dakika chache mbele alikuwa akiingia Mbagala , Roma aliendesha ndani ya mtaa huu uliokuwa na baadhi ya viwanda na kampuni za usafirishaji , lakini ile anakaribia nyumba anayoishi Najma , Alimuona Juma akiwa nje , alisimamisha Gari na kushuka haraka haraka.
“Niambie nini kimetokea?”Aliongea Roma huku akiona baadhi ya watu wakiwasogelea na walionekana kujua nini kimetokea.
“Kuna majambazi ambayo siyafahamu , yamekuja na kunitishia na bunduki na kisha wakamkamata Najma na kuondoka nae , huku wakiniachia maagizo kuwa nikitaka kumpata dada yangu akiwa mzima , niwasiliane na wewe na uende sehemu watakayo niambia”
“Sasa wamekuambia ni sehemu gani?”.
“Hawajaniambia wamesema watapiga simu ndani ya lisaa limoja”Aliongea Juma aliekuwa na wasiwasi huku wapangaji wakiwa wamewazunguka , kuna waliokuwa wakimwangalia Roma kwa wasiwasi ili kuona kama atakuwa na njia ya kumuokoa Najma , ila kuna wale waliokuwa wakishangaa mabadiliko ya Roma.
Baaada ya lisaa ni kweli simu ya Juma iliita na alipokea haraka haraka huku akiweka Loudspeaker na hata Roma kusikia.
“Dogo nadhani ushamwambia muhusika?”
“Ndio yuko hapa”
“Mpatie simu”Ilisikika sauti na Roma aliinyakua kutoka kwenye mikono ya Juma na kuweka silence huku akiiingia kwenye Gari yake na kufunga mlango.
“Ongea”.
“Roma hakikisha unakuja mahali ambapo tunakuambia kwa sasa na uje peke yako , ukifanya ujinga wa aina yoyote kama kutaarifu polisi Najma atakufa kifo cha kikatili sana”Ilisikika sauti hio.
“Nipe simu kwanza niongee na Najma siwezi kuja kabla sijasikia sauti yake mimi sio mjinga kiasi hiko”Aliongea Roma na dakika chache sauti ilisikika kwenye masikio yake.
“Najma uko salama?”
“Roma usije watakuua , wana siraha usifanye wanach..”Alipokonywa simu.
“Sikia Roma eneo ni Vikindu , hakikisha unakuja peke yako”Ilisikika sauti na kumfanya Roma akasirike na hio ni baada ya simu ile kukatwa na Roma hakujiuliza sana alitoa gari eneo hilo kwa spidi kiasi cha kufanya watu watumbue macho.
Roma alikuwa na hasira mno , kwanza kilichomkasirisha ni kwamba watu hao wamemuambia kwenda Vikindu lakini hawakuwa wameeleza Vikindu sehemu gani.
Roma baada ya kuingia ndani ya barabara ya Kongowe , alizidi kuendesha gari hio kwa spidi na ilikuwa na spidi kweli kwani zilikuwa zile gari za gharama ya hali ya juu , alikuwa akiyapita magari kama mwehu kiasi kilichofanya kuwanyanyua polisi wa barabarani.
“Shi**t huyu mpuuzi ni nani huyu anaendesha gari kwa spidi hivi kama hii nchi ya baba yake?”Alionekana mwanamke trafiki akiwa amekasirika mara baada ya kuisimamisha gari ya Roma lakini ilimpita bila ya kusimama na kumuachia upepo tu.
“Huyu hanijui vizuri ngoja nitamkamata tu”Aliongea mwanadada huyu mrembo huku wenzake wakiwa ni wenye kushangazwa na spidi ya gari iliowapita ndani ya eneo hili la Kongowe.
“Mage unaenda wapi?”
“Namfukuzia yule mshenzi, wasiliana na Trafiki wa mbele yetu uwape taarifa juu ya hio gari waizuie “Aliongea mrembo huyu mwenye kalio kubwa huku akikimbilia Pikipiki yake kubwa ya kijapani Kawasaki Ninja H2/R hii ni moja ya pikipiku ya kifahari sana na ni chache sana Tanzania , inaupiga mwingi sana hii pikipiki kwenye spidi , ina Zaidi ya 322bhp na imeingia kwenye kumi bora ya pikipiki zenye spidi sana duniani , thamani yake sio chini ya milioni 100 za kitanzania. .
Haikueleweka ni kivipi mtembo huyu Trafiki anaimiliki vipi kwani ni ya bei kubwa mno.
“Unafikiri ataifikia ile gari?”Aliuliza Trafiki wa kiume mweupe.
“Hio pikipiki ina upiga mwingi sana hio anaweza kuifikia ila inategemea na uwezo wake wa kuendesha”Aliongea Trafiki maji ya kunde.
Ni dakika chache tu Roma alikuwa ashafika Vikindu na kusimamisha gari huku akijiuliza ni uelekeo gani aelekee, alikuwa akiangalia daladala zilizokuwa zikiingia ndani ya stendi , lakini ile anajiuliza simu yake ilianza kuita tena.
Simama kwenye bango kubwa la Tigo hapo Stendi na kuna mtu atakufuata hapo”Roma aliangalia mahali sahihi pakuweka gari yake na kulisimamisha na kisha alishuka na kwenda kusimama chini ya Bango kubwa la Tigo.
“Hey! Brazaaa mambo ni vipi , kuna wana wameniambia nije nikuchukue nadhani wewe ndio Roma”Roma aliitikia kwa kichwa huku akimwangalia huyu kijana ambaye anaonekana kuharibiwa na madawa ya kulevya.
Baada ya dakika chache za kukata kona hatimae walivuka kiwanda kimoja amacho Roma hakukitambua kilikuwa cha nini , walipita upande wa kushoto na kusimama kwenye geti kubwa jeusi na mlango ukafunguliwa na Roma akaingia na hapa ndipo alipojua eneo hili ni la kuhifadhia nondo , kwani zilikuwa nyingi upande wa kulia , ni kama ghala.
Alitembea kwa kuongozwa na kijana huyo huku akiangalia baadhi ya mabaunsa waliokuwa wameshikilia bunduki za SMG wakilinda eneo hili kitendo ambacho kilimshangaza Roma , inakuwaje nhi yenye Amani kama hii kuna watu wanamiliki Siraha kiholela ila hakutaka kujisumbua maaana sio kazi yake, aliingia ndani na hapa ndipo alipomshuhudia Najma aliekuwa amefungwa kwenye nguzo, na kitambaa mdomoni , alionekana kuchoka kweli kweli alikuwa akitoa jasho kiasi kwamba baadhi ya Sehemu za Hijabu yake zimeloana.
Roma alimuonea huruma mrembo huyo kwa mateso aliokuwa akipitia , aligeuza macho na kuangalia mabaunsa haya Zaidi ya matano yakiwa na bastora na kisha aligeuka upande mwingine akimuangalia jamaa ambae alionekana kuwa ndio bosi kwani yeye hakushika siraha yoyote na alikuwa amekaa kwenye kiti na sigara yake mkononi.
“Roma unaonekana sana kumjali huyu mrembo, cheupe dawa mpaka ukajileta mwenyewe”Aliongea jamaa hili huku likionekana kutafuna bablishi.
“Nishafika mfungulieni Najma aondoke , ili tuongee shida yenu na mimi”Aliongea Roma kwa hasira.
“Acha upuuzi wewe , yaani unaniona mimi joka la kibisa , nimlete mrembo kama huyu ndani ya hili eneo halafu nimuache bila hata ya kumuonja”Aliongea Jambazi huyu huku akimshia kidevu Najma na kumuangalia kisha akaanza kumnusa usoni na shingoni.
“Kananukia vizuri na vijdomo vyake vidogo nadhani hata ka ‘K’ kake ni kadogo”Aliongea huyu jambazi mkuu na kumfanya Roma azidi kupandwa na hasira , ila hakutaka kufanya jambo lolote la kijinga kwani alihofia usalama wa Najma kwani watu hawa walikuwa wengi na wote walikuwa na siraha,Najma muda wote alikuwa mwenye kutokwa na machozi , alishindwa kuongea ila alionekana kumhurumia Roma kwani walikuwa wamemziba na matambala.
“Mfungeni kwanza , nataka nimfanye demu wake mbele yake”Aliamrisha na Roma alifungwa na yeye kwenye nguzo .
“Unajua kwanini nina shida na wewe fala?”.
“Wewe ndio umeniita hapa , naona unaanza kuuliza maswali ya kipuuzi”Aliongea Roma lakini alijikuta akianza kupigwa ngumi za Tumbo nyingi za haraka haraka na kisha akamaliziwa na Teke, kiasi cha kukohoa na kutema damu.
“Ulifanya kosa kubwa sana kulala na Rose,Mwanamke ambaye nimemhangaikia tokea anaingia ndani ya hili jiji , na wewe na hako kamashine kako ukajiona kidume, sasa leo nitahakikisha namto**mba huyu demu mbele yako , halafu nitahakikisha hautoki na hiko kibolo chako hapa ndani”Aliongea bwana huyu huku akionekana hakuwa ni mwenye utani kabisa.
“Hahaha .. sasa kama umemhangaikia ulishindwa nini kumpata , acha kuudhihirisha ubwege wako kwangu bwana , wewe ni fala tu”Aliongea Roma kwa hasira na kumfanya bwana huyo awaambie vijana wake wamsulubu Roma , kitendo ambacho kwa Najma kilimuumiza mno kwani ni kama alikuwa akipigwa yeye.
Roma alitema damu kwa mara nyingine na bwana huyu aliridhshwa na kipondo hiko na sasa kazi iliokuwa inafuata ni kukamilisha jambo lake kwa Najma.
“Ukimgusa huyo mwanamke nakuhakikisha nitakufanya kitu ambacho hutokisahau katika maisha yako”Aliongea Roma, kwani licha ya kupewa kichapo cha uhakika lakini alionekana kama hajapigwa vile.
“Ila lile jambazi kuu halikujali sana alimfungua Najma na kisha alimshika mkono kwa nguvu na akaanza kumvuta upande mwingine uliokuwa na maboksi.
“Kitendo kile kilimuuzi sana Roma kiasi kwamba mboni za macho yake zilianza kubadilika na kuwa za kijani na hata wale majambazi wengine walishuhudia hilo.
“Boss!”Aliita jambazi mmoja aliekuwa karibu na Roma , lakini kabla hajajibiwa alijikuta akiwa hewani na hakujua ni kwa namna gani , alipigwa na hapa Roma alikuwa amekata Kamba zote zilizokuwa zimemfunga .
“Mpige Risasi mbona mnamuangalia”Aliongea yule Jambazi kuu , lakini katika hali ambayo hata yeye hakujua imetokea vipi , aliskia sauti ‘Shwaa.. Shwaaa tiii …Aiii, Shwaa… Aiii..’ na mabodigai wote walikuwa chini huku wakiugulia maumivu.
Jambazi kuu alishangazwa na uwezo huo wa Roma na kuanza kutetemeka kwa woga , lakini sio yeye hata Najma alishangaa .
Wakati Jambazi hili kuu likiwa linashangaa , lilijikuta limefikiwa na Roma na kishikwa shingoni na kuning`inizwa hewani kwa mkono mmoja kitendo ambacho Najma ni kama alikuwa akiangalia Muvi za kihindi zile zenye uongo mwingi , yaani unakuta steringi kabeba gari na mkono mmoja.
“Sipendagi kutishiwa kwenye maisha yangu , pili Onyo mara moja ukirudia ni kifo, tatu sipendi watu wanaotumia watu wangu wa karibu kupambana na mimi Sababu hizo tatu zinanipa uhalali wa kukuondoa duniani maana wewe ni takataka”Ilikuwa sauti nzito kama ya Roboti.
“Najma Fumba macho mpaka nikwambie fumbua ”Aliongea Roma kwa sauti nzito na Najma alifumba kweli na ndani ya dakika mbili alimwambia fumbua na hapo ndipo Najma alipopigwa na mshangao , kwani majambazi yote manne yalikuwa yamelala chini huku yakiwa yamefunikwa na maboksi kwenye uso huku Roma akilipapasa lile jambazi kuu , lakini hakuambulia cha maana Zaidi ya pakiti ya sigara za SM na kuzichukua na kuweka mfukoni.
“Hawa wote ni maiti , ndugu zao watakuja kuchukua miili na sijui kama wanasafirisha au wanazika hapa hapa”Aliongea Roma bila wasiwasi na kumsogelea Najma ili amshike mkono , lakini Najma alirudi nyuma kwani alikuwa ni mwenye kutetemeka mno na alimuogopa Roma , hakumuona kama yule Roma aliekuwa akimjua na kumpenda ila huyu ni Roma mwinginekabisa mkatili na muuaji.
“Nifuate nyuma kama unaiogopa”Aliongea Roma na kuanza kupiga hatua na Najma japo alikuwa akimuogopa Roma ila alimkimbilia kwani aliogopa kukaa na maiti na isitoshe ilikuwa ni usiku.
Roma baada ya kukatiza kona ya chumba hiki alimwambia Asubiri kwa dakika chache lakini Najma hakusubiri , aitoka na kuangalia nje na hapo ndipo aliposhuhudia kwani alimuona Roma akitembea kama upepo flani hivi ulioambatana na kivuli cha mtu , na alichoweza kusikia ni ‘Crak shwaa..Aiii, Crak .. Shwaa ..Aii Crak.. Aiii Crak Crack;’.
Majambazi yote yalikuwa chini Roma akiwa ashayavunja shingo , yaani ni kitendo cha dakika moja tu , Roma ashamaliza kazi na aligeuka nyuma na kumuona Najma na kumuita kwa ishara ila Najma alizidi kumuogopa Roma.
“Najma nisamehe sana kwa kufanya mambo haya mbele yako , ila sikuwa na jinsi , sahau kabisa kilichotokea leo na nitahakikisha hakuna mtu anaekugusa tena”Aliongea Roma ila Najma hakujibu kitu aliishia kutoa machozi tu na kutangulia mbele.
Roma na yeye hakutaka kumuongelesha , alijuwa mwanake huyo atakuwa kwenye mshituko mkubwa sana , hivyo aliona muda pekee ndio utakao weza kumuweka sawa.
Baada ya kutembea kwa dakika kadhaa hatimae , walifika barabarani, alimuona kijana ambaye alikuja kumchukua akiendelea na upiga debe na Roma hakumjali sana , lakini ile anakaribia gari lake , aliona matrafiki wawili watatu wameegamia gari yake wawili wakiwa wanawake na mwingine akiwa ni mwanaume.
Na wakati huu macho yake yalikuwa yasharudi kwenye hali yake ya kawaida , na alikuwa Roma ambaye Najma alikuwa amemzoea , sio yule muaaji wa kutisha.
“Jamani habari zenu “Alisalimia Roma kama kawaida yake huku akitabasamu na Mage polisi aliekuwa akimfukuzia , aligeuza macho yake na kumwangalia Roma juu hadi chini, kwa muonekano wa Roma hakuonesha kuweza kumiliki ndinga kama hio na ndio maana baada ya kumuangalia kwa sekunde aligeuka na kuendelea kupiga stori na trafiki mwenzake wa kike huku akimuacha trafiki wa kiume akidili na Roma.
“Jamani mmesimama kwenye gari yangu nataka nikampumzishe huyu mrembo si , mnaona jinsi alivyochoka na pia giza kali hili”Hapo ndipo Mage aligeuka tena na kumwangalia Roma.
“Wewe ndio mwenye hii gari?”
“Ndio mrembo”
“Uko chini ya ulinzi kwanzia sasa , kwa kukiuka sheria za barabarani lakini pia kwa kuidharau serikali”.Aliongea Mage huku akiweka uso wa usiriasi.
“Mrembo nilikuwa na dharula ndio maana”
“Mpuuzi sana wewe , hata kama unadharula gani hii nchi sio ya baba yako kuendesha gari kama kichaa , unataka kusababisha ajali na usiku huu na mipombe yako”Aliongea Mage kwa hasira.
Roma aliona hana cha kujitetea , alimwangalia Najma alivyokuwa amechoka na kumuonea huruma.
“Utaenda na sisi mpaka polisi , usituletee shida kisa unaendesha gari la kuazima, Edwin endesha gari yake mpaka kituoni”Aliongea Mage na kumuamrisha trafiki wa kiume achukue funguo kwa Roma.Trafiki yule alitabasamu meno yote nje .
“Leo naenda kuonja kuendesha huu mchuma , Mungu anipe nini mimi nikimfikisha kituoni hata nikifa nitakuwa na Amani”Alijiwazia huyu trafiki kichwani mwake baada ya kupokea ufunguo
Najma , Roma waliingia kwenye gari na safari ya kuelekea kituoni ikaanza
SEHEMU YA KUMI NA NANE
Unaambiwa hakuna Trafiki aliekuwa akiwasumbua watu waliokuwa wakipita barabara ya Kongowe kama Mage, huyu Trafiki waendesha daladala na boda boda walikuwa wamembadilisha jina na kumuita ‘Mnaaa’, Mage alikuwa mzuri mno lakini hakuwa akifanania na usiriasi wake akiwa eneo lake la kazi , aliwanyoosha watu kisawasawa.
Mage anamiezi miwili tu tokea aanze kufanya kazi hii ya utrafiki na kilichomfanya kuwa trafiki ni adhabu aliokuwa amepewa , kwani Mage alikuwa ni Koplo polisi ndani ya kituo cha Osterbay jijini Dar es salaam , lakini kutokana na kumpiga mtuhumiwa mpaka kuzimia wakati akifanya nae mahojiano ndio kilichomfanya kupewa adhabu ya kufanya kazi kama Trafiki na kutolewa katika cheo chake.
Mwanzoni mkuu wa polisi alitaka amfukuze Mage lakini alishindwa kutokana na nguvu iliokuwa nyuma ya mrembo huyu , kwani inasemekana baba yake ni mtu mkubwa sana ndani ya ulingo wa siasa.
“Jina nani?”
“Roma Ramoni”
“Umri?”
“Miaka 24”
“Kabila”
“Mhehe”
“Uraia wako” Roma kimya .
“Jinsia yako?”
“Mwanamke”Jamaa yule wa kipolisi alimwangalia Roma kwa hasira na kisha kuendelea kuandika na baada ya dakika chache aliingia kwenye kijiofisi hiki afande mwingine.
“ Afande Dulla ,Mage amesema atadili mwenyewe na mtuhumiwa”Jamaa alionekana kukasirishwa sana jambo hili , kwani kwanza baada ya afande Dulla kuona gari kali ya Roma V8 aliamini huo ni mchongo Mungu amempatia usiku huo na aliona akiacha mchongo huo upite atakuwa fala.
“Huyu Mage ni mnoko sana tokea apangwe ukanda huu hakuna Amani na michongo imepungua”Aliongea Afande Dulla huku akitoka kwa hasira nje,hakuwa na cha kumfanya Mage kwani alikuwa akizijua tetesi kwamba Mage sio mtu wa kuwa nae adui.
Najma alikuwa asharudi nyumbani kwani hakuwa akihusika baada ya kutoa maelezo yake , aliekuwa amebaki kituoni alikuwa ni Roma , lakini jambo ambalo lililomkasirisha Roma ni kwamba Mage alichelewa sana , yaani alifika kituoni baada ya saa moja na Nusu.
“Kwanza huna leseni , pili nilivyokusimamisha ukajifanya mjuaji na kunipita , tatu spidi ya gari yako kwenye barabara hii yenye magari mengi ni kinyume na sheria , mpaka hapo una makossa matatu”Aliongea Mage , lakini wakati huu Roma alikuwa anamwangalia tu mrembo huyu huku akitafakari inakuwaje pisi kama hii ni Trafiki.
“Inakuwaje mrembo kama wewe ukawa polisi ,halafu unaonekana umeanza mzunguko wako wa mwezi jana”.Mage alizidi kukasirika.
“Huyu fala kajuaje nipo kwenye Period na nimeanza jana?”
“Wewe Nguruwe unadhani upo mtaani hapa, au kwasababu unaendesha V8 unataka kujiona upo kwenu hapa?”
“Hehe…Inaonekana nimepatia”Aliongea Roma na ilikuwa kitendo cha dakika tu alisikilizia maumivu kwenye mguu wake maana Mage alirusha buti yake yenye kisigino kirefu na kutua kwenye mguu wa Roma kiasi cha kumfanya Roma ainame huku akisikilizia maumivu.
Baada ya kupishana kwa muda hatimae Mage alimpa adhabu ya Roma kulipa faini milioni moja kwa makossa yake yote matatu.
*****
Ni usiku muda wa saa saba Edna hakuwa amelala, haikueleweka kwanini alikuwa hajalala , ila alionekana ameshikilia kitabu cha kingereza kilichokuwa na Title ‘HOW TO THINK POSITIVE akiwa anasoma , ni dakika chache pekee alizosoma alisikia simu yake ikiianza kuita mfululizo kiasi cha kuichukua haraka haraka ila alipoangalia jina ni ‘Mbakaji’Alikuta akiendelea kuangalia ikiendelea kuita.
Ilikatika na ikaita mara ya pili na hapa hakuwa na jinsi na kuipokea kisha akaweka sikioni.
“Unataka nini?”
“Bebi ,Usiniambie ulikuwa umelala mumeo sijarudi”
“Sema shida yako nina usingizi mimi?”.
“Kuna polisi mrembo hapa anataka kuongea na wewe”Aliongea Roma .
“Hellow! habari za Kiza kinene, nadhani huyu mlevi ni mumeo , basi hapa ni kituo cha polisi Chalambe tunamshikiria mumeo kwa kukiuka sheria za barabarani na kuidharau Mamlaka na atatoka iwapo atalipa kiasi cha milioni moja za kitanzania kama faini”.
“Sawa”Aliongea Edna na kukata simu.
Baada ya kukata simu ile alionekna ni mwenye kukasirishwa na jambo hilo , ila alifikiria kwa dakika na kuona ni jukumu lake kutatua matatizo ya ndoa , kwani licha ya wawili hao kutokuoana kwa mapenzi , ila walikuwa ni wanandoa kihalali na walikuwa na wajibu wa kusaidiana.
Edna alitafuta jina kwenye simu na kisha alipiga , japo muda ulikuwa umeenda sana , lakini simu hio iliopokelewa.
“Nataka aachiwe kwa sasa nadhani unakumbuka nilikusaidia kupandishwa cheo , sasa hivi ni usiku sana sitaki aendelee kuwa kituoni”Sentensi ya mwisho Edna alioongea na kisha akakata simu.
Upande wa huku Mbagala chalambe ,Mage alionekana kuwa ndani ya maliwato huku akiwa ameshusha jezi yake ya kitrafiki huku mkononi akiwa ameshikilia pedi , Alitoa ile aliokuwa amejifunga na kisha akachukua ile nyingine mpya na kuiweka vizuri na kisha akajivalisha vyema nguo yake ya ndani na kupandisha jezi yake hio nyeupe na akanawa mikono na kutupia ile pedi iliotumika kwenye dustibin.
“Hivi huyu choko kajuaje mimi niko kwenye period”Alijiongelesha huku akijigeuza geuza kwenye kioo kuangalia kama ana alama yoyote ya damu inayomuonesha yuko kwenye Period, alijikagua kwenye mpododo wake ambao ni ugonjwa wa wanaume wengi lakini hakuona kitu.
“Au hapa mbele pametuna sana ,Mh! Lakini panaonekana kawaida”Baada ya kumaliza alichukua mkoba wake na kutoka kwenye maliwato.
“Mage kuna simu yako kutoka kwa mkuu”Aliongea Edwin na Mage alipokea .
“Mkuu haiwezekani huyu ni muhalifu na sheria inapaswa kuchukua mkondo wake , kwanini tumuachie”
“Mage nakuambia muachie sasa hivi , huyo mtu uliemshikiria ana koneksheni na wenye nchi, sitaki kuhatarisha kibarua changu ninasomesha bado , muachie haraka , halafu acha ubishi mkuu wako wa kazi akikuambia achia , wewe achia ,nikikuambia jamba jikakamue jamba hio ndio maana ya mwanajeshi kutii amri Ala”Huku simu ikikatwa na Mage alitoa sonyo.
“Edwin mrudishie yule choko vitu vyake aondoke”Edwin alishangaa ila hakuwa na cha kuongea Zaidi ya kufanya hivyo.
“Hey!Mrembo usicheze na wenye nchi”Aliongea Roma ilimradi tu kumkasirisha Mage aliesimama karibu na barabara.
“Siku nyingine nikikukamata nakuapia lazima uozee jela”.
“Hehehe..Sawa bibie , ila naona ushabadilisha”
“Nishabadilisha nini?”Aliongea Mage kwa mshangao na Roma hakujibu aliingia kwenye gari lake na kuondoka kwa spidi huku Edwin akiliangalia gari kwa matamanio .
“Huyu choko ukute mchawi huyu kajuaje nimebadilisha pedi huyu”Alijiwazia Mage huku akijionea aibu , alikiri katika maisha yake ya kibabe kama mwanamke ashawahi kukutana na watu wengi ila hakuwahi kuyumbishwa kama alivyoyumbishwa usiku huo,alikasirika maradufu na alijiapiza siku atakayo mkamata Roma hata kama ana koneksheni atamtia kwanza ukilema na mengine yataendelea.
Ilikuwa ni asubuhi saa kumi na moja Roma alikuwa akikata kiuno huku mwanadada Rose akitoa miguno ya kimahaba ya kila aina , mwanadada huyu mrembo alikuwa mwekundu kama nyanya , kwani alikuwa anakunjwa , aligeuzwa geuzwa kama andazi linalokaangwa huku likirukaruka , alikuwa akibonyezwa bonyezwa kama embe huku ametoa ulimi kama anakata moto ni Zaidi ya dakika sabini zimepita Roma hajafunga goli hata moja huku yeye akipoteza hesabu ya idadi ya magoli aliokuwa ametupia.
“Roma tupumzike kwanza , kuna waka moto”.
“Tulia bebi namalizia chenga ya mwisho nitupie wavuni kama Mayele”Aliongea Roma na ndani ya dakika kumi alikuwa ametupia wavuni na kujitupa pembeni ya Rose.
“Bebi sidhani kama kuna mwanaume anajua kuto**mba kama wewe?”.
“Rose mpenzi usiniambie unawaza kufanya utafiti na ushapata idea”.
“Hahah.. yaani wewe , mimi nimeongea tu”Roma alitabasamu huku akimfinya Rose mashavu na muda huu wote wakiwa uchi.
“Halafu bebi ulitokea wapi jana , mbona ilikuwa usiku sana”.
“Halafu umenikumbusha , hebu kalete kwanza kiberiti nina sigara zangu kwenye suruali”Aliongea Roma na Rose alinyanyuka bila ya nguo na kwenda kuchukua kiberiti , alikuja nacho na kisha alipekua mfuko wa suruali ya Roma na kisha alitoa pakiti ya sigara na kuchomoa moja na kisha akampatia na kisha akawasha moto na kuunguza sigara ile na akaweka kiberiti pembeni na kurudi kwenye kitanda hiki kikubwa , huku Rose akiwa ameshikilia sahani flani ya udongo ,Roma alikuwa akivuta kidogo anaweka majivu kwenye ile sahani.
Ungemuona kitendo anachofanya Rose ungedhania ni wanawake wanaotumika kuwafurahisha wafalme kwenye majumba yao(maids) , hakuwa yule Rose ambae anaongoza kundi la Tembo na kuogopwa na walio chini yake.
“Kuna mpuuzi jana amemteka Najma , na kunitishia Amani huku akijinadi kwamba wewe ni wake na mimi nilikosea sana kulala na wewe”Rose alishangaa lakini pia aliwaza ni mtu gani mwenye uwezo wa kufanya jambo hilo na hapo hapo jibu alilipata.
“Unataka kuniambia Karimu ndio aliefanya hivyo?”
“Sitaki hata kumjua jina ni mpuuzi mmoja hivi mwenye nywele za kisomali”Huku akitoa moshi wa sigara na kufanya chumba kijae harufu ila Rose hakujali.
“Ni karimu bebi huyo , unakumbuka ile siku zile bia za ofa kwenye bethidei yangu , basi yeye ndioe alielipia gharama zote”Roma alielewa.
“Kwa hio ilikuwaje mpenzi?”
“Jibu unalo Rose”Alitoa macho.
“Unamaanisha..”
“Ndio nimemuua na vifaranga vyake vyote nadhani ndugu zake watakuwa wanaomboleza kwasasa kama wamepata taarifa”.
“Ila mpenzi ikijulikana wewe ndio umemuua inaweza ikakuletea shida , baba yake Karim ni meya , lakini pia ni mmiliki wa kundi la Black Mamba ni kundi kubwa sana kuliko la kwangu na linajihusisha na mambo mengi , kama kuuza viungo vya binadamu nje ya nchi , usafirishaji wa meno ya Tembo , Madawa na mengine mengi ambayo si halali katika ulimwengu unaonekana, na huyo Karimu ndio mkuu wa kundi hilo ila maagizo yote anapokea kwa baba yake , lakini pia inasemekana, baba yake Larim na The Doni wanaukaribu ambao unahisiwa kuwa ni undugu”Aliongea Rose kwa kirefu na kumshangaza Roma.
“The Doni?” Alishangaa Roma
ITAENDELEA
JAMANI KWENYE GRUPU INAENDELEA KWA SPIDI YA 4G NJOO NIKUUNGE , NICHEKI KWA NAMBA 0687151346 KILA ISKU NAPOSTI VIPANDE VITATU.
Sema Mwamba Roma anakula maisha ni balaa
Hii sio kawaida yake.labda ana dharura.Arosto
Story za humu ujiandae kisaikolojia.unaweza kupigwa na kizito kichwani muda wowote.kwahiyo usishangae game ndio imeisha hiyo.Kazi ipo
[emoji1787][emoji1787][emoji1787] sirogeki mimi, nashusha mwendelezo muda si mrefu nilibanwa na majukumuWamemroga [emoji848][emoji848][emoji848]
Woyoooooooo[emoji1787][emoji1787][emoji1787] sirogeki mimi, nashusha mwendelezo muda si mrefu nilibanwa na majukumu
Sent using Jamii Forums mobile app
Twakusubiria[emoji1787][emoji1787][emoji1787] sirogeki mimi, nashusha mwendelezo muda si mrefu nilibanwa na majukumu
Sent using Jamii Forums mobile app
Tulijua umetekwa na zero organization[emoji1787][emoji1787][emoji1787] sirogeki mimi, nashusha mwendelezo muda si mrefu nilibanwa na majukumu
Sent using Jamii Forums mobile app
Haya tunakusubiria mkuu[emoji1787][emoji1787][emoji1787] sirogeki mimi, nashusha mwendelezo muda si mrefu nilibanwa na majukumu
Sent using Jamii Forums mobile app
Zero hawateki bali wanakupyupyu moja kwa moja😆Tulijua umetekwa na zero organization
ninahisia mtoto wa Roma ataivunja ndoa ya Edina na Roma........khaaaaaaaaaSEHEMU YA 257
Edna hakutaka kumuachia kabisa Lanlan kuondoka na kwa Lanlan ilikuwa hivyo hivyo , hakupenda kuachiana na Edna na kurudi Bagamoyo na ilibidi Edna amshawishi Qiang mlezi wa Lanlan kukubali kubaki kwa siku kadhaa nyumbani kwake mpaka pale babu yake na Lanlan atakaporiudi.
Qiang licha ya mwanzo kumhofia Edna lakini aligudua Edna ni mtu mzuri hivyo ilibidi akubali.
“Mama , Lanlan anapenda bahari na anapenda na Wanyama”Aliongea Lanlan wakitoka kwenye mgahawa huu wa Best Bite na Edna alikuwa amemshikilia mkono 1anlan na walionekana mama na mwana kwa ukamili kabisa.
“Lanlan unataka nikupeleke ukaone bahari?”Aliuliza Edna na Lanlan alitingisha kichwa kuashiria ndio anataka kuona.
“Okey Lanlan bahari ipo upande wa pili nitakupeleka ukaone bahari”Aliongea Edna na Lanlan aliruka ruka kwa furaha mno.
“Lanlan anampenda sana mama yake”Aliongea Lanlan na kumfanya Edna kufurahi pia na walikuwa washasahau kama kuna watu wapo nyuma yao.
Roma na Qiang walikuwa wakiwaangalia na Roma haikueleweka alikuwa akiwaza nini , lakini kwa jinsi mke wake alivyoonekana kwenye macho yake alijiambia Edna atakuwa mama mzuri kama siku moja atakuja kupata mtoto wake.
Ukweli Roma licha ya kwamba Edna amefurahishwa na uwepo wa Lanlan lakini kwa upande wake ilikuwa tofuati ,kwake hakuwa sana mpenzi wa kucheza na Watoto , hususani wale ambao hakuwafahamu , lakini kwa upande wa Lanlan kuna kitu ambacho sio cha kawaida alikuwa akihisi kila anapomwangalia , lakini jambo lingine ni kwamba Lanlan hakuwa mtoto wa kawaida , kwani alikuwa na nguvu za ziada kwenye mwili wake.
“Roma nampeleka Lanlan kuona bahari , endesha kuelekea Coco”Aliongea Edna na kumfanya Roma kuachama kwa kuchoka na Edna alimwangalia.
“Kama umechoka unaweza kurudi nyumbani nitaendesha mimi mwenyewe”Aliongea na Roma alifikiria kidogo.
“Okey wife wewe utaendesha mimi naenda nyumbani kupumzika”Aliongea Roma na kisha akampatia Edna ufunguo na yeye alianza kutembea kusonga mbele kuelekea nyumbani kwani hapakuwa mbali.
“Roma mbona uko mwenyewe wakati umetoka hapa ukiwa na Edna?”Aliuliza Blandina aliekuwa amekaa nje kwenye bustani akiangalia maji ya Swimming pool na Roma alisogea mpaka alipokaa mama yake na kuketi kivivu huku akivuta hewa nzuri iliokuwa ikipuliza pua zake.
Nyumba ya Edna haikuwa mbali na Baharini , ni kama nyumba ileile ya kule Kigamboni utofauti wa nyumba hii na ya kile ni kwamba eneo la Baharini linaonekana kwa ukubwa Zaidi kama utakaa juu ya ghorofa kwenye balconi.
“Kapata mtoto na kampeleka kuona maji ya baharini , nimechoka nimerudi kupumzika”Aliongea Roma.
Ukweli Roma sio kama alikuwa amechoka ila alikuwa akitaka atulie kidogo muda uende aende nyumbani kwa Nasra, kwani juzi yake aliachana nae akiwa mwenye hasira hivyo aliamini kwenda kumpeti peti mrembo huyo anaweza kushusha hasira zake n ahata kumtunuku kitumbua.
“Mtoto gani tena kampata?”
“Alisema wiki iliopita mlikutana na mtoto kwenye kituo cha kulelea Yatima , ndio huyo ambaye tumekutana nae eneo la Mwenge na wanaonekana kuzoeana sana kiasi kwamba anamuona kama mtoto wake , hivyo kamchukua na kumpeleka ufukweni”Aliongea Roma na kumfanya Blandina kukumbuka.
“Ndio nakumbuka , kuna huyu mtoto alifanya mpaka akazimia”Roma alijikuta akishangaa baada ya kusikia neno kuzimia , hakuwa na taarifa ya Edna kuzimia.
“Unamaanisha nini kuzimia” Blandina alivuta pumzi na kisha akaanza kumuelezea tukio lilivyokuwa na Roma alijikuta akishangaa lakini pia hata kwake yeye alishindwa kujua sababu iliompelekea kuzimia ni nini , lakini pia akili yake ilianza kukumbuka jumapili ya wiki iliopita Edna alirudi nyumbani akiwa na mabadiliko makubwa kimwili.
“Mh! nini kimempata?”
“Hata mimi nilishindwa kuelewa na nilishangaa baada ya kushituka jina la kwanza kuuliza ni la huyo Lanlan , Roma jitahidini mpate mtoto na Edna, sipendi hivi nyie ni wanandoa na kulala vyumba tofauti”Aliongea Blandina.
“Mama hilo lisikuumize kichwa , Edna akiamua mwenyewe juu ya hilo mimi sina shida , kwasasa sitaku kumlazimisha kutokana na namna tulivyokutana”Aliongea Roma na kisha alinyanyuka kwa ajili ya kuelekea ndani , lakini muda huo huo geti la jumba lao lilifunguliwa na gari aina ya V8 ilionekana ikiingia na Roma baada ya kuangalia vizuri aligundua mmoja ya mwanamke aliekuwa ndani ya gari hilo, wa kwanza alikuwa ni Jestina na mwingine alikuwa ni mwanamke ambaye hakumfahamu vizuri , lakini mwanamke huyo alikuwa ni mdogo wake Raisi Senga afahamikae kwa jina la maarufu la Mama Theresia.
“Roma”Aliita Jestina huku akimsogelea Roma kwa furaha na kumsalimia.
“Roma huyu ni Shangazi yako anafahamika kwa jina maarufu la Mama Theresia”Aliongea Jesgtina na kumfanya Roma kutabasamu na kisha kumsailimia mwanamke ambaye ametambulishwa kwake kama Shangazi.
“Namkumbuka siku ambayo nilikuja kuonana na wewe ndani ya Landmark Hotel nilimuona akiwa nyuma yetu”Aliongea Roma na kumfanya Jestina kushangaa na kisha kucheka.
“Kwahio ulimuona?”
“Ndio nilimuona na nilifahamu siku ile alikuwa na wewe kwa namna yoyote ile kwani alikuwa akituangalia sana”
“Ni kweli , nisamehe mama yako , Roma unaweza usiamini ila mimi nilikufahamu tokea siku ya kwanza unafika ndani ya familia yetu kwenye ile sherehe nadhani unakumbuka hata baba alitaka kuongea na wewe ni kwasababu ulikuwa ukifanana kabisa na baba yako wakati akiwa katika ujana wake”Aliongea Jestina na Roma alitabasamu na kuona kumbe mama huyo kipindi kile alikuwa kwenye misheni yake , ila aliona sio jambo la kuzingaria sana.
“Mama Theresia!”Aliita Blandina na kusogeleana na Mama Theresia na kukumbatiana , ilikuwa ni mara yao ya kwanza kuonana tokea Blandina arudi kutoka Kenya, walionekana kukumbukana sana na Roma aliona hilo na hakuona haja ya kuendelea kusimama , kwani alitembea na kuingia ndani na alikutana moja kwa moja na Sophia.
“Broo..!!”Aliita Sophia na kumshika mkono Roma na kupandisha nae juu na kumpekea kwenye sebule ya juu upande wa Balconi.
“Kuna nini Sophia mbona una mchecheto hivyo?”Aliuliza Roma na kumfanya Sophia kupumua.
“Siri yetu imefichuka”Aliongea Sophia na kumfanya Roma kushangaa hakumuelewa Sophia alikuwa akimaanisha nini.
“Siri gani hio sijakuelewa”
“Nimetoka kuongea na mama hapa , anasema aliongea na Sister Edna muda tu juu ya mimi kukaa nyumbani kwake”Aliongea Sophia na kumfanya sasa Roma kuelewa anachomaanisha ni nini.
“Kwahio unamaanisha Edna alikuwa akifahamu wewe sio mdogo wangu kama tulivyomdanganya?”
“Ndio na mama kasema Sister Edna anajua kila kitu na inaonekana aliamua kukaa kimya”Aliongea Sophia huku akionekana kuwa na hatia na kwa upande wa Roma licha ya kwamba swala hilo halikuwa likimsumbua sana , ila hakujua kwanini Edna alikaa kimya baada ya kugundua kama walimdanganya.
“Nilikuambiaga mimi , Mke wangu ana akili nyingi na ni ngumu sana kumdanganya”
“Acha kumsifia mbele yangu ,mama ndio kaharibu , yaani anapenda kuingilia mipango yangu sana”Aliongea huku akionekana kumlaani mama yake.
“Wewe nae una mipango gani?”
“Hupswi kujua nina mipango gani , hapa nawaza namna ya kumuomba msahamaha Sister Edna , sijawa muaminifu kwake toka mwanzo huenda ananichukia ndani kwa ndani”Aliongea Sophia
“Mimi sidhani Edna yuko hivyo naamini aliamua kukaa kimya kwasababu anakuchukulia kama mdogo wake na ndio maana hajaonyesha utofauti wowote , ila inapaswa kuongea nae”Aliongea Roma na kisha akaanza kupiga hatua kuelekea kweney chumba chake kwa ajili ya kupumzika.
“Kwahio mimi ndio ninaepaswa kuongea nae peke yangu na hili halikuhusu?”Aliuliza Sophia.
“Hehe… kwani nani alilazmisha kuishi na mimi, wewe na baba yako ndio mlinifanya nikadanganya, hivyo Edna akinikasirikia nitamwambia tu ukweli kama unataka kuwa mke wangu wa pili simple”Aliongea Rsoma huku akitabasamu kifedhuli.
“Roma…!!!”Aliita kwa hasira Sophia huku akikunja ngumu , lakini Roma hakumjali na kupotea kwenye macho yake.
*********
Edna alionekana kufurahi kweli , yaani moyo wake ulikuwa mweupee na alijihisi dunia yote alikuwa akiimiliki , licha ya kwamba ni masaa machache sana ambayo aliweza kuonana na Lanlan lakini kwake ni kama miaka mingi.
Lanlan vilevile alionekana kufurahia uwepo Wa Edna alimuona Edna kama mama yake kamili na hakuona kabisa utofauti wa aina yoyote ile na ndio maana alijiachia atakavyo na kuomba kununuliwa anachotaka.
Takribani masaa mawili yote Edna , Qiang na Lanlan walikuwa wakifurahia upepo wa baharini .
Lanlan alikuwa akiogelea kiasi kwamba ilimfanya Edna kuwa na wasiwasi kumruhusu Lanlan kuingia kwenye maji , lakini Qiang alimtoa wasiwasi Edna na kumwambia Lanlan anaweza akaingia kwenye maji chini kabisa na kuzuia pumzi kwa takribani dakika nne.
“Unadanganya”Aliongea Edna huku akimwangalia Qiang.
“Ni kweli Miss , Lanlan sio mtoto wa kawaida na kadri unavyoishi nae ndio utagundua kuwa anaweza kufanya mambo mengi ambayo watu wa kawaida hawawezi kufanya , ndio maana hata Master hajawahi kufikiria kumpekea Shule kutokana na uwezo wake”Aliongea Qiang na kumfanya Edna kushangaa.
“Unataka kuniambia kuwa Lanlan hajawahi kusoma popote hata chekechea ,mbona anaonekana akili yake kukomaa tofauti na umri wake?”
“Ndio maana nakuambia Lanlan ana mambo mengi ya kukushangaza Miss Edna”Aliongea Qiang lakini muda huo huo Lanlan alitoka kwenye maji na kuwakimbilia.
“Mama , Aunt Qiang , Grandpaa amerudi”Aliongea Lanlan na kumfanya Edna kushangaa.
“U?nasema kweli Lanlan?”
“Ndio Grandpaa karudi , yule kule…”Kabla hajamaliza Sentesi yake alitoka nduki akiwa na kijichupi tu na kufanya watu wamshangae na Edna aligeuka na kumwambia asikimbie lakini Qiang alimzuia.
“Ni master”Aliongea Qiang na kumfanya Edna kushangaa na moyo wake kuuma maana alijua ujio wa babu wa Lanlan ndio kumkosa hivyo Lanlan, aliangalia upande wa kushoto kwake na kweli Lanlan alimkubaria kwa kumrukia mwanaume mmoja mweupe asiemfahamu ambaye alikuwa ni mchina.
“Yule ndio babu yake Lanlan?”Aliuliza Edna na Qiang alitingisha kichwa nayeye kuanza kukimbia kwa kutabasamu kuelekea upande wa kushoto alipo Lanlan na babu yake.
SEHEMU YA 258
“Linda unamaanisha nini kwamba ulikuwa ni mpango wako?”Aliuliza Raisi Senga kwani hata yeye alikuwa akimjua Linda na tena sio kumjua tu kama msaidizi wa karibu na mtu wa kuaminika kwa Senior , lakini pia alikuwa akimfahamu Linda kama mchepuko wa raisi Jeremy.
Mheshimiwa Jeremy alikuwa haamini kama ni kweli Linda alikuwa akijua mpango LADO muda wote na kumkalia kimya, alitaka kusikiliza kila kitu ndio aamini kwani aliona Linda ni kama alikuwa akimtania.
Linda alivuta pumzi na kisha alitembea na kwenda moja kwa moja kukaa kwenye huku akimwangalia Jeremy kwa huruma.
“Jeremy najua naweza usinisamehe kwa kile nilichokifanya lakini naomba usikie kila kitu na baada ya hapo nitakuwa tayari kupokea adhabu ya aina yoyote ile”Aliongea mwanamama Linda kwa huzuni na kumfanya hata Raisi Jeremy kushindwa kuongea.
“Linda tunakusikiliza unaweza kuongea kila kitu”Aliongea Raisi Senga na Linda alivuta kumbukumbu kurudi nyuma.
“Kabla ya yote mnatakiwa kutambua kwamba mimi ni CIA undercover Ajent”Aliongea Linda na kumfanya Jeremy mwili wake kukaa kitako pasipo ya akili yake kuelewa.
“Linda niambie unadanganya?”Aliongea Jeremy lakini Linda hakumjali , Zaidi ya kuingiza mkono kwenye mfuko wa koti lake na kutoa Flash Disk na kumkabidhi mheshimiwa Senga.
“Hii inanithibishia utambulisho wangu kama CIA , ni nyaraka kamili pia zinazotambulisha uraia wangu wa taifa la Marekani”Aliongea na Rasie Senga haraka haraka alisogelea Tablet na kuunganisha Flash ile.
“Password ni nini?”Aliuliza Mheshimiwa Raisi Senga baada ya kugundua Flash Disk inanywira.
“Oprah Fraklin”Aliongea Linda.
“Hili ndio jina lako halisi naamini , CIA hawajawah kutumia majina yao halisi”Aliongea Raisi Senga na kufungua faili moja lililokuwa kwa mfumo wa kama Software yaani ni faili ambalo baada ya kuligusa ni kama limeliwa na virusi kwani lilionyesha vijiboksi vidogo vidogo.
“This File is Corrupted Linda”Aliongea Senga na Linda alimpa ishara ya kumpatia hio Tablet na Senga alimkabidhi na jambo ambalo liliwashangaza ni kwamba Linda alianza kuandika kwa haraka haraka kwa kutumia ile Tablet na kila maneno ambayo anaandika vile vijiboksi vilianza kujikusanya kwa muundo falani hivi kama vile mchoro na ndani ya dakika tu vile vijiboksi vilitegeneza picha ‘ Logo’ ya shirika la kijasusi la CIA na chini kukaonekana ‘Form’ yaani hapa nikimaanisha fomu ya kilectroinics ambayo inamuhitaji Linda kuingiza jina lake halisi la kuzaliwa nalo , mwaka aliojiunga na CIA , pamoja na nywira ili kufungua akaunti yake.
“Kwa sheria za ma ajenti wote wa CIA tunapokuwa kazini hatubebi vitambilisho vinavyotuunganisha moja kwa moja na taifa la Marekani , bali tunabeba Flash Disk maalumu ambayo ukichomekwa na kifaa chochote huonekana kama Flash disk hio ina virusi ndani yake”Aliongea Linda na Senga aliitikia na kuona Yes hapa yupo na CIA mweyenyewe sio wa mchongo.
Linda aliingiza jina lake la Oprah Franklin na kisha palepale karatasi kama mfano wa vyeti unavyopewa shuleni au ukihitimu ilionekana kwenye Tablet na Linda alimpatia Raisi Jeremy.
“Huo ndio utambulisho wangu wa uraia wa Marekani , lakini pia nikionekana kama raia ninaelitumikia taifa langu nje na nyumbani”Aliongea Linda na Jeremy alipitia faili hilo na kisha hakuongea chchote na kumpatia Senga ambaye baada ya kusoma maelezo hayo aliamini maneno ya Linda na kuona ni kweli wapo na jasusi wa siri kutoka Idara ya CIA kutoka taifa la Marekani.
“Ukute hata Kabwe anaweza kuwa CIA na ananichora tu, Damn it lazima niende kwenye ibada ya mpasuko wa mwezi, kwa namna hiikuna majasusi wa CIA wa ngapi ndani ya hili taifa”Aliwaza Raisi Senga mwenyewe huku akimuangalia raisi Jeremy.
“Mhmh ! Hehe Senior anaonekana na yeye kupitishwa ubatizo wa moto, huenda hisia alizokuwa nazo ni kama nilizopitia nilivyofahamu Blandina na Denisi wapo hai , namuonea huruma”Aliendelea kuwaza huku akimwangalia Rafiki yake.
“Jeremy nakumbuka mara ya mwisho ulivyogundua uwezo wangu usio wa kawaida uliniuliza niliupatia wapi na nikakujibu ni kutoka kwa kundi la Yamaguchi , ni kweli kabla ya kuja Rwanda nilikuwa chini ya taasisi ya kininja ya Yamaguchi na ndiko nilipopatia mbini na nguvu zangu za ziada za kimapigano ambazo mtu wa kawaida hawezi kuwa nazo”
“Yamaguchi , sijawahi kusikia hio taasisi”Aliongea Senga.
“Ndio huwezi kuifahamu kwani ni taasisi za siri sana”
“Linda tafadhari ongea kila kitu nielewe wewe ni nani na kazi yako ya kuwa ndani ya ikulu ya Rwanda ni ipi , weka kila kitu wazi kwani baada ya hapa utakuwa mfu labda unipe sababu ya kutofanya hivyo , nachukia sana usaliti kwenye Maisha yangu”Aliongea Jeremy kwa hasira.
“Niliingizwa ikulu ya Rwanda kwa maagizo ya The Doni mara baada ya kumaliza mafunzo yangu ya kininja kutoka Yamaguchi na kazi yangu kubwa ni kukulinda mpaka pale nitakapopewa maagizo mengine, kabla ya kufanya mafunzo na kundi la Yamaguchi nilikuwa ni CIA Agent., hata kuingizwa ndani ya kundi hilo ni maagizo maalumu niliopewa na taifa langu la Marekani”
“Linda nadhani kwanza unielezee hili kundi la Yamaguchi kazi yake ni nini haswa na kwanini wanafundisha watu kuwa maninja , hebu elezea kila kitu kwanza”Aliongea Raisi Senga kwa mchecheto , alihitaji kujua kila kitu.
Kwa maelezo ya Linda ni kwamba Yamaguchi ni taasisi ya siri kutoka China ambayo inafadhiliwa kwa asilimia mia moja na serikali mbili yaani China na Japani, taasisi hii kazi yake kubwa ni kufundisha vijana wa kuanzia miaka kumi na moja mafunzo ya hali ya juu ya Uninja huku dhumuni kubwa ni kuua ndio wanachofundishwa.
Anaendelea kusema kwamba Yamaguchi baada ya kuwafundisha wanafunzi wake huko msituni na kufuzu mafunzo yote kuanzia ya kimapigano mpaka ya kichawi , maninja hao hufudishwa sheria maalumu ambazo zinawaongoza kufanya kazi zao baada ya kutoka mafunzoni na kuchangamana na watu wa kawaida na moja ya sheria hizo ni kutokutambuana na mwanafunzi mwingine wala kuwasiliana, Linda anasema kwamba baada ya wanafunzi kuhitimu mafunzo ya kimapigano moja kwa moja wanapangiwa majukumu(Target) kwa ajili ya kufanyia kazi, hivyo hata yeye baada ya kumaliza mafunzo alipangiwa Target yake ambayo ni Ikulu ya Rwanda.
“Kwahio wewe kazi yako uliopewa na Yamaguchi ni kumlinda Mheshimiwa Jeremy?”
“Hio ndio kazi yangu na sio kwa Jeremy tu , kama itatokea raisi mwingine akachaguliwa ndani ya Rwanda basi target yangu itabadilika”
“Hapo Yamaguchi walikuwa wakifahamu kama wew ni CIA?”
“Hawakua wakifahamu hilo kwani sikujitambulisha kwao kama CIA na pia niliingizwa kwenye mafunzo hayo kwa makusudi maalumu”
“Makusudi gani?”
“Misheni yangu ilikuwa ni kuingia kwenye kundi hilo na kutoa taarifa zote ya kile kinachoendelea na nilifanya hivyo na hata baada ya kumaliza mafunzo niliendelea kuwa chini ya Yamaguchi licha ya kutopokea maelekezo mengine kutoka CIA”Aliongea Linda.
“Sasa ilikuwaje ukahusika kwenye mpango LADO au Serikali ya Marekani walikuagiza kufanya hivyo”
“Serikali ya Marekani hawajawahi kunitafuta tokea nimalize mafunzo ndani ya Yamaguch na kuja hapa Rwanda kwasababu wanajua mpaka sasa hivi nimekufa”Aliongea Linda na kuwafanya waheshimiwa kuzidi kuchanganyikiwa Zaidi.
“Unamaanisha nini?” Aliuliza Jeremy na Linda alianza kushikwa na huzuni na kisha akanyamza na kuvuta kumbukumbu.
Kwa maelezo ya linda alisema kwamba baada ya kutoka kwenye kundi la Yamaguchi na kupangiwa tageti yake , serikali ya marekani ilitoa oda maalumu ya Linda kuuwawa mara moja , mpaka muda huo mwenyewe anashindwa kuelewa kwanini alikuwa akiwindwa na Serikali yake ilihali alikuwa amepewa misheni na aliifanya vizuri , ila alisema wakati akiwa katika harakati za kuingia Ikulu ya Rwanda ndipo alipoweza kupata taarifa iliokuwa ikihusu yeye kuuliwa kwa oda kutoka makao makuu.(Termination order)
“Nani alitoa hio oda ya wewe kuuliwa na kwanini na nani alikuletea taarifa hio”
“Mtu alieniambia hio taarifa simfahamu , ila ninachokumbuka ni kwamba nilikuwa kwenye nyumba yangu hapa Rwanda asubuhi na kwenye meza kulikuwa na karatasi iliokuwa ikithibitsha kwamba nawindwa na CIA , mwanzoni sikuamini karatasi hio na nilitumia marafiki zangu makao makuu kuthibitsha Ushahidi uliokuwa kwenye mikono yangu na walinithibitishia ni kweli na nikawauliza kwanini nawinda na serikali yangu ilihali nilikuwa kwenye misheni , ila hakukuwa na majibu maalumu na Rafiki yangu ndani ya CIA aliniambia nisije nikampigia tena na nijifiche kwa namna yoyote”
Ukweli raisi Senga bado alionekana kutokumuelewa kabisa Linda , kwanza mwanamke huyu alisema kwamba aliingia kwenye kundi la Yamaguachi akiwa kama CIA akiwa kwenye misheni maalumu huku akichukua mafunzo ya uninja ili kujifanyisha na yeye ni mwanfunzi na baada ya kumaliza mafunzo akapangiwa taget yake , sasa raisi Senga ambacho hajaelewa ni kwanini CIA hao hao ambao wamempa misheni kutoa oda ya kifo chake ilihali Linda bado alikuwa na umuhimu kwao, pili pia Linda anaeleza kwamba alijikuta akiwa nyumbani kwake asubuhi na alipoamka alikuta karatasi iliokuwa ikithibitisha oda ya kuuwawa kwake na mtu ambaye kamletea karatasi hio hakuwa akimfahamu, bado maelezo yake yalikuwa na maswali mengi.
Kwa upande wa Raisi Jeremy licha ya kwamba alikuwa na hasira na Linda lakini pia alikuwa akimuogoopa , alikuwa akijua uwezo wa kimapigano aliokuwa nao Linda , lakini pia uwezo wake wa kupotea kimazingara pia alikuwa akiufahamu na alijiambia kama Linda angekuwa mtu wa kawaida basi angemhoji akiwa chini ya chumba cha mateso kama ilivyokuwa kawaida yake na kwa muda huo alishiandwa hata kuuliza maswali kwani alikuwa kwenye hasira nyingi sana na ndio maana aliacha Rafiki yake Senga amuulize Linda maswali yote.
“Linda unayosayesma haya yote ni ya kweli au kuna jambo unatudanganya,?”
“Nimeamua leo kuweka ukweli wote wazi hivyo sina nia ya kuficha chochote, nitaeleza kile ninachofahamu kwa upande wangu”Aliongea Linda.
“Ilikuwaje ukahusika kwenye mpango LADO , tueleze hapo tuelewa kwanini nyaraka za mpango LADO zina sahihi yangu ya .senior na ya Rahel? Na kuonyesha kama sisi ndio wahusika wa mpango huo?”
SEHEMU YA 259
1997
Ni mwezi wa kumi na moja ndani ya ofisi ya mkuu wa majeshi , Jenerali Cammillius Kweka anaonekana Linda alievalia suti ya rangi nyeusi akiwa aneo la Mapokezi akiwa ameshikilia mkoba wake.
Linda alionekana kuwa na wasiwasi kweli licha ya kwamba yupo eneo ambalo lina ulinzi mkubwa sana nchini kutokana na maamuzi yote ya kijeshi kufanyikia hapo , lakini pia sehemu ambayo wafanyakazii wake wote ni wanajeshi.
Linda akiwa eneo la Mapokezi kwa takribani dakika kama kumi na tano hivi , huku akikagua kila mwanajeshi aliekuwa akiingia kwa wale waliokuwa na gwanda na wale ambao hawakuvaa gwanda , alifuatwa na mwanajeshi wa cheo cha Kapteni mwanaume mrefu mweusi wa umri mkubwa kuliko wake.
“Dada unaweza kunifuata , Jenerali ameridhia kuonana na wewe”Aliongea yule mwanajeshi na kumfanya Linda kutabasamu.
“Asante sana kaka kwa kunipelekea ombi langu”Aliongea Linda akiweka tabasamu na yule mwanajeshi alitabasamu pia na kupokea shukrani na kisha alianza kutembea kumpeleka Linda kwenye ofisi ya Afande Camllius Kweka.
“Nafikiri nimefanya maamuzi sahihi ya kuja ofisini kwake kuongelea hili swala”Aliwaza Linda huku akitembea kwa hali ya kujiamini.
Ukweli ni kwamba Linda kabla ya kuja hapa Tanzania kufanya maongezi na mkuu wa majeshi ya Tanzania , jana yake asubuhi kuna tukio ambalo lilimtokea na kumchanganya sana.
Jana yake mrembo huyu baada ya kurudi kutoka Ikulu ya Rwanda sehemu ambako anafanyia kazi kama katibu muhtasi wa raisi Jeremy , alivua nguo zake na kuzitundika vizuri kwenye kabati kama ilivyokuwa kawaida yake.
Linda ni moja ya wanawake ambao hawakuwa na mambo mengi na hii yote ni kutokana na mafunzo aliokuwa nayo ya kimapigano , alikuwa ni mwanamke ambaye hata mavazi yake karibia yote ni suti tupu na aina ya mavazi mengine ni kama tracksuit ambazo mara nyingi hutumia kuchukulia mazoezi ya kukimbia na pale anapokwenda Gym na ndio maana kwa mwaka huo wa tisini na saba katika moja ya nyumba za serikali alipokuwa akiishi , nyumba yake haikuwa na vitu vingi , kulikuwa na makochi ya mbao upande wa sebuleri na meza katikati ya mbao pia pamoja na Tv ya chogo , kwa upande wa chumbani kwake hakukuwa na vitu vingi Zaidi ya kabati la mbao analotumia kuhifadhia nguo na baadhi ya vitu vyake vya thamani.
Sasa siku ambayo mrembo huyu anaamka asubuhi nyumba yake ilikuwa sio ya kawaida kama alivyozoea , kwanza kabisa kwenye mwili wake kulikuwa na mabadiliko , katika paja lake kuna alama ambayo hata yeye mwenyewe hakujua alama hio imetoka wapi na alipoona hio alama ya tatoo ni kama vile yupo kwenye ndoto na atashituka na kuona alama hio kupotea , lakini hakukuwa na mabadiliko kwani mpaka inatimia saa mbili asubihi alama hio ipo , alijaribu kuifuta lakini haikuwezekana., alishangaa na kuogopa kwa wakati mmoja na kujiuliza alama hio imefikaje kwenye mwili wake , kwani jana alilala akiwa hana alama na hata kama kuna mtu aliingia nyumbani kwake na kumuwekea hio alama angetambua, kwani yeye alikuwa ni mwanajeshi na wanajeshi usingizi wao ni wa machale , lakini ajabu alilala fofofo na cha kushagnaza Zaidi anaamka asubuhi na kukuta ana alama kwenye mwili wake , alama ambayo haifutiki lakini pia hakujua inahusiana na nini.
Linda akiwa katika mawazo alitembea mpaka eneo la sebuleni huku akijihisi kuwa na uwoga wa ajabu kwa swala ambalo limemtokea na alikimbilia sebulni kwa ajili ya kuangalia usalama na ile anafika eneo la makochi ndipo alipoona bahasha ya khaki iliokuwa mezani na kumfanya kushangaa na kuanza kukagua nyumba nzima kuthibitisha usalama , lakini ajabu ni kwamba nyumba yake haikuonesha hali yoyote ya mtu kuingia kabisa kwani kama alivyofugna milango kabla ya kulala usiku wa jana , ndivyo alivyokuta asubuhi.
“So strange, what is happening , am I hallucinating”Aliongea mwenyewe huku akisogelea bahasha iliopo kwenye meza na kuiangalia juu yake.
“From X to Oprah Franklin”
Hayo ndio maneno yliosomeka juu ya bahasha hio na kumchangnya mno Linda , kwanza jina ambalo lipo juu ya Bahasha ni jina ambalo hajawahi kulitumia tokea afike nchini Rwanda na alishangaa imekuwaje fomu ikawekwa nyumbani kwake na ikawa na jina lake la utotoni , jina ambalo lipo kwenye database ya serikali ya Marekani tu , alishangaa na kujiuliza maswali na kutetemeka mikono kwa wakati mmoja.
“Itakuwa ni CIA hawa lazima tu, lakini hapana vipi kuhusu tatoo kwenye paja langu na yenyewe ni kutoka kwa CIA?”Aliwaza Linda huku akigeuza geuza bahasha ambayo ipo kwenye mikono yake.
“Usalama wote upo vizuri , hakuna sehemu inayoashiria mtu kuingia ndani lakini naamka asubuhi nikiwa na alama kwenye paja langu la mguu wa kushoto na sasa nimeshikilia bahasha ambayo sijui ndani yake kuna kitu gani , mtu aliefanya haya yote ni nani , je ni kundi la Yamaguchi, lakini hapana Yamaguchi hawafahamu jina langu halisi , sio wao naamini kuna mtu mwingine anaenifahamu”Aliwaza Linda lakini alijikuta akiwaza ujinga kwani aliamini huenda majibu yote yapo kwenye bahasha alioshikilia kwenye mikono yake.
Linda alikaaa chini harakaharaka na kuanza kufungua ile bahasha kwa kuchana na kisha akatoa karatasi nne zilizopo ndani yake na kuzishika mkononi na kuanza kusoma , lakini ajabu ni kwamba juu ya karatasi ya kwanza kuna alama ambayo ni kama iliokuwa kwenye paja lake la mguu.
“Nimeingia nyumbani kwako pasipo kuacha alama yoyote ya namna nilivyoingia , lakini pia nimeweza kukuchora tatoo kwenye paja lako la kushoto na nikaacha nyaraka ambayo unazisoma , Amini kwamba mimi sio mtu wakawaida na naweza kukufanya jambo lolote kwa muda ninaotaka” ndio sentensi ya kwanza iliokuwa juu ya nyaraka ya kwanza , moyo ulipiga kite na kuogopa Zaidi.
“Unatakiwa kutimiza kila maelekezo nilioandika kwenye nyaraka nilizoacha kama unataka kunifahamu , kwasasa utanitambua kwa jina la X na alama kwenye paja lako ni ya utambulisho kwamba wewe ni mwanachama”Sentensi ya pili kwenye Nyaraka na kumfanya Linda kuzidi kuchanganyikiwa.
Mwanachama , X , Tatoo alijiuliza vyote kwa pamoja na Linda kwa papara Zaidi alifungua ukurasa wa pili na alijikuta akishangaa kwani aliona picha ya mtu anaemjua.
Raheli mpenzi wa siri wa Raisi Jeremy ndio picha alioshikilia na kumfanya kushangaa Zaidi lakini alichana na picha hio na kuhamia nyaraka ya ta tu na hii ilikuwa ni nyaraka ya maandishi ambayo ina malekezo.
Malekezo no 1: “Mtafute Cammilius Kweka kutoka Tanzania kipengele namba mbili ndio anaepaswa kukisoma na kukuambia cha kufanya.”
Malekezo No 2: “Kweka huyo ni mshirika wako zidi ya Mpango LADO na nyaraka hii inamtambulisha”
Maelekezo no 3: “Kiongozi yoyote lazima asaini aidha kwa kukubali au kulazimishwa ili kuidhinisha mpango LADO na mzazi mmoja wa mhusika katika mpangon asaini ili kulinda mpango husika”
Linda alisoma vipengele vyote viwili na kujikuta akishangaa Zaidi lakini aliachana na nnyaraka ya tatu na kufungua nyaraka ya nne ambayo ilikuwa ikijitegemea na Linda baada ya kuisoma jasho lilianza kumtoka.
“Termination Order , Ajenti Flower Rain”Alisoma Linda maelezo hayo na kuangalia sahihi na muhuli na alichoka kwani Ajent Flower rain ni jina la kodi ndani ya CIA.
“Director Powel From CIA” ndio sahihi ambayo Linda asingeshindwa kuitambua na alijiuliza kwanini CIA wanamtaka kufa ni kipi ambacho amekosea ni kweli yupo Rwanda pasipo kutoa taarifa kwa wakubwa wake , lakini hakuweza kufanya hivyo kwasababu wao wenyewe ndio wa kwanza kumtafuta kwa njia wanazozijua wao, lakini Linda bado alikuwa kwenye maswali na mshangao , alijiuliza kama kweli CIA wametoa oda yake ya kufa inakuwaje mpaka sasa hivi yupo hai kwani alikuwa akifahamu uwezo wa shirika la CIA wakitoa oda jihesabie tayari ni mfu.
Linda kwa hasira akaanza kukung`uta ile bahasha kuhakikisha karatasi zote zimetoka na matarajio yake yalikuwa kweli kwani kulidondoka kikaratasi cha njano mfano wa kimemo.
“You are already dead when you go along with plan , you will be alive and hunted when you refuse to go along with plan, this notes only for you , I am X till second phase of plan”
“Wewe ni mfu tayari kama utaenda na mpango , utakuwa unaishi na kuwindwa kama utakataa kwenda na mpango , hiko kijimemo ni kwa ajili yako , mimi ni X mpaka hatua ya pili ya mpango” kijimemo aliweza kukisoma hivyo na kujikuta akishangaa Zaidi lakini ghafla Linda yupo Tanzania ndani ya makao makuu ya Jeshi la Tanzania akikubali kila kitu kilichoachwa nyumbani kwake na kuamini ni ukweli.
Kwanza anaanza vipi kuona sio kweli , yeye ni ninja wa hatari kutoka kwenye kundi la Yamaguchi lakini mtu anakuja nyumbani kwake na kumchora tatoo kwenye paja na kuacha maelezo pasipo yeye kutambua, aliamini huyo m mtu ni wa hatari sana na hivyo dakika ambayo atafanya kinyume basi ndio dakika ambayo kifo chake kitamkuta.
“No I am Dead , I will go along with plan”Aliwaza Linda wakati akifika mbele ya ofisi ya mkuu wa majeshi , jenerali Cammilius Kweka na mlango ukafunguliwa na akaingia ndani ya ofisi yanye ubaridi wa kiyoyozi wa hali ya juu , ofisi ambayo mkuu wa majeshi hufanyia maamuzi.
“Karibu Binti, nimesikia unataka kuonana na mimi na unatokea Ikulu ya Rwanda karibu sana”Sauti nzito ilimkaribisha Linda na Linda alitabasamu.
*********
Senga alijikuta akishangaa na kukosa cha kusema , kwahio mpango wote ule wa mwanae Denisi kupanda ndege , lakini pia Lorraine mtoto wa Jeremhy na Raheli ulisukwa na Senga pamoja na Linda, alijikuta akikaa chini na kuanza kuona baba yake ni mtu hatari sana na asipokufa mapema anaweza kuleta shida zaidi kwa taifa.
“Kwahio huyo mtu aliekuja nyumbani kwako na kukuchora alama kwenye paja ndio aliekupa maelekezo ya kufanya kila kitu”
“Ndio nilifanya kila kitu kwa maelekezo yake”
“Vipi kuhusu sahihi yangu , lakini pia mhuli wa raisi iliwezekana vipi maana sikumbuki kutia Saini wala kugonga muhuli karatasi ya mpango Zero”
“Ulifanya kila kitu kwa maelekezo yangu ninao uwezo huo na sio kwako tu hata kwa Raheli alitia sahihi pasipo ya kujitambua na kwako Senga hivyo hivyo , mbinu hio ni sehemu ya mafunzo kutoka kwa kundi la Yamaguchi, I have ability to hypnotize anyone and do things according to my wishes”
“Kwahio Linda mpango na ushauri ulionipa wa kumpeleka Lorraine kwenda China kupitia Malaysia ulikuwa ni mpango wako na Afande Kweka , lakini kwa maneno marahisi ni kwamba wewe ndio uliemuua mwanangu , ulimchukua mwanangu kutoka kwangu mtoto ambaye alikuwa ni kama zawadi kutoka kwa Rahel?” Aliongea Jeremy huku akianza kupandwa na jazba mdogo mdogo.
“Jeremy najua unahasira sana , lakini kumbuka kama isingekuwa mimi usingweza hata kufahamu kama una mtoto duniani , Raheli hakuwa na mpango wa kukuambia ila mimi nilikuambia kwa mapenzi yangu mwenyewe”
“Stupid woman!, you told me in order for your evil plan to work , umenifanya nimshawishi Rahel kuniachia mtoto mmoja kati ya mapacha ili iwe rahisi kwako”
“Hapana Jeremy huo haukua mpango wetu na nzee Kweka kwa mara ya kwanza , the plan was very simple na kama sio mimi usingesikia kabisa kuhusu Edna wala Lorraine, Jeremy tatizo lako uliamini Rahel anakupenda san ana hapo ndipo ulipokosea”
“How so, unataka kuniambia Rahel hanipendi?”Aliuliza kwa hasira mno kiasi cha misuli ya uso kusimama.
********
“Wewe ni miss Edna , mwanamke Tajiri ndani ya taifa hili?”Aliuliza Babu yake Lanlan.
“Ndio ni mimi” Alijibu Edna na hii ni baada ya kusalimiana na Babu yake Lanlan na Edna kushangazwa na babu hiyo kuwa wa umri mdogo.
“Nakiri kwamba unafanana kwa asilimia mia moja na mama yake Lanlan , lakini hio haikufanyi kuwa mama yake”
“Grandpa..”Aliingilia Lanlan kama vile alikuwa akielewa kinachoongelewa ila kwa upande wa Edna alijisikia vibaya ,mzee huyo alionyesha kuwa na maneno ya kuumiza lakini yanayoeleweka.
“Qiang mchukue mtoto na mnisubiri pale mbele”Aliongea kwa Kingereza na mlezi wa Lanlan alimchukua Lanlan.
“Hapana Lanlam anataka kuwa na mama yake”
“Lanlan nisikilize mimi babu yako huyu sio mama yako na nitakutafutia mama yako mwingine”Aliongea yule mzee na kumpa ishara Qiang kuondoka na Lanlan , lakini Lanlan alianza kulia na kumfanya Edna kukasirika .
“Huna haja ya kukasirika kwani huna haki yoyote ya kufanya hivyo”Aliongea yule mchina kwa maneno ya kejeli na Edna alijikuta akikasirika na kuumia lakini hakutaka kuonyesha aliona avumilie yapite kwa ajili ya Lanlan.
“Maneno yangu yanaweza kuonekana ya kejeli lakini huo ndio ukweli”
“Naomba uende moja kwa moja kwa ulichotaka kuongea”Aliongea Edna.
“Unaonekana kumpenda Lanlan sana na Lanlan pia anakupenda na tokea akuone amekuwa msumbufu na nikiri ni kweli Lanlan mama yake mpaka sasa hivi kashafariki hivyo hana mama, unaonaje kama utamlea kama utatimiza masharti yangu”Aliongea yule mzee na kumfanya Edna moyo wake kulipukwa na furaha.
“Kumlea , nipo tayari kumlea niambie masharti yako”Aliongea Edna pasipo hata ya kufikiria ukweli licha ya kwamba alikuwa akimpenda Lanlan lakini wazo la kumlea bado hakuwa nalo.
“Sidhani kama utayaweza masharti”Aliongea yule mwanaume na kutmbasamu kwa kejeli.
“Niambie ni masharti gani hayo unayoamini siyawezi?”
“Okey Miss Edna ukweli ni kwamba sharti ni moja tu na ukilitimiza unaweza kuondoka na Lanlan, kwanza mtoto wenyewe msumbufu kwangu na nina kazi nyingi kiasi cha kunifanya niondoke bila taarifa hivyo sifai kuwa mlezi wake”Alipumua na kisha akamwangalia Edna.
“Achana na mumeo kwa talaka na baada ya hapo nitakuruhusu umchukue Lanlan”
“Nini..!!”
“Ndio usishangae kama utaweza kuchanana Roma , basi Lanlan kuanzia leo atakuita mama , maamuzi unatakiwa kuyafanya sasa hivi , Je upo tayari kuachana na mume wako umchukue Lanlan au upo tayari kuendelea na mume wako umkose Lanlan? , kwa upande wa Lanlan naamini anaweza kuniacha mimi babu yake nilieteseka nae na kukuchagua wewe”Aliuliza yule mzee kwa Kingereza na kumfanya Edna kutoa macho , kwenye Maisha yake hajawahi kukutana na Dillema ya aina hio.
“Mama Lanlan anapenda kuishi na mama yake, usiniache tena”Aliongea LAnlana na kuanza kulia kilicho cha kwikwi huku akishika miguu ya Edna na Edna alimwangalia Lanlan na kuanza kutokwa na machozis.
“Miss Edna fanya maamuzi , Sharti ni dogo sana”Aliongea yule mwaume mchina na kuonyesha kejeli za waziwazi.
Unafikiri Edna atamuacha Roma na kumchukua Lanlan , nini kitendelea itaendelea kesho.
HAPPY WIKIEND KUTOKA KWA MWANDISHI SINGANO JR , NAMBA YANGU NI WATSAPP NI 0687151346 , USISITE KUNICHEKI UNAPOHITAJI MWENDELEZO
Hupatikani singano jrSEHEMU YA 257
Edna hakutaka kumuachia kabisa Lanlan kuondoka na kwa Lanlan ilikuwa hivyo hivyo , hakupenda kuachiana na Edna na kurudi Bagamoyo na ilibidi Edna amshawishi Qiang mlezi wa Lanlan kukubali kubaki kwa siku kadhaa nyumbani kwake mpaka pale babu yake na Lanlan atakaporiudi.
Qiang licha ya mwanzo kumhofia Edna lakini aligudua Edna ni mtu mzuri hivyo ilibidi akubali.
“Mama , Lanlan anapenda bahari na anapenda na Wanyama”Aliongea Lanlan wakitoka kwenye mgahawa huu wa Best Bite na Edna alikuwa amemshikilia mkono 1anlan na walionekana mama na mwana kwa ukamili kabisa.
“Lanlan unataka nikupeleke ukaone bahari?”Aliuliza Edna na Lanlan alitingisha kichwa kuashiria ndio anataka kuona.
“Okey Lanlan bahari ipo upande wa pili nitakupeleka ukaone bahari”Aliongea Edna na Lanlan aliruka ruka kwa furaha mno.
“Lanlan anampenda sana mama yake”Aliongea Lanlan na kumfanya Edna kufurahi pia na walikuwa washasahau kama kuna watu wapo nyuma yao.
Roma na Qiang walikuwa wakiwaangalia na Roma haikueleweka alikuwa akiwaza nini , lakini kwa jinsi mke wake alivyoonekana kwenye macho yake alijiambia Edna atakuwa mama mzuri kama siku moja atakuja kupata mtoto wake.
Ukweli Roma licha ya kwamba Edna amefurahishwa na uwepo wa Lanlan lakini kwa upande wake ilikuwa tofuati ,kwake hakuwa sana mpenzi wa kucheza na Watoto , hususani wale ambao hakuwafahamu , lakini kwa upande wa Lanlan kuna kitu ambacho sio cha kawaida alikuwa akihisi kila anapomwangalia , lakini jambo lingine ni kwamba Lanlan hakuwa mtoto wa kawaida , kwani alikuwa na nguvu za ziada kwenye mwili wake.
“Roma nampeleka Lanlan kuona bahari , endesha kuelekea Coco”Aliongea Edna na kumfanya Roma kuachama kwa kuchoka na Edna alimwangalia.
“Kama umechoka unaweza kurudi nyumbani nitaendesha mimi mwenyewe”Aliongea na Roma alifikiria kidogo.
“Okey wife wewe utaendesha mimi naenda nyumbani kupumzika”Aliongea Roma na kisha akampatia Edna ufunguo na yeye alianza kutembea kusonga mbele kuelekea nyumbani kwani hapakuwa mbali.
“Roma mbona uko mwenyewe wakati umetoka hapa ukiwa na Edna?”Aliuliza Blandina aliekuwa amekaa nje kwenye bustani akiangalia maji ya Swimming pool na Roma alisogea mpaka alipokaa mama yake na kuketi kivivu huku akivuta hewa nzuri iliokuwa ikipuliza pua zake.
Nyumba ya Edna haikuwa mbali na Baharini , ni kama nyumba ileile ya kule Kigamboni utofauti wa nyumba hii na ya kile ni kwamba eneo la Baharini linaonekana kwa ukubwa Zaidi kama utakaa juu ya ghorofa kwenye balconi.
“Kapata mtoto na kampeleka kuona maji ya baharini , nimechoka nimerudi kupumzika”Aliongea Roma.
Ukweli Roma sio kama alikuwa amechoka ila alikuwa akitaka atulie kidogo muda uende aende nyumbani kwa Nasra, kwani juzi yake aliachana nae akiwa mwenye hasira hivyo aliamini kwenda kumpeti peti mrembo huyo anaweza kushusha hasira zake n ahata kumtunuku kitumbua.
“Mtoto gani tena kampata?”
“Alisema wiki iliopita mlikutana na mtoto kwenye kituo cha kulelea Yatima , ndio huyo ambaye tumekutana nae eneo la Mwenge na wanaonekana kuzoeana sana kiasi kwamba anamuona kama mtoto wake , hivyo kamchukua na kumpeleka ufukweni”Aliongea Roma na kumfanya Blandina kukumbuka.
“Ndio nakumbuka , kuna huyu mtoto alifanya mpaka akazimia”Roma alijikuta akishangaa baada ya kusikia neno kuzimia , hakuwa na taarifa ya Edna kuzimia.
“Unamaanisha nini kuzimia” Blandina alivuta pumzi na kisha akaanza kumuelezea tukio lilivyokuwa na Roma alijikuta akishangaa lakini pia hata kwake yeye alishindwa kujua sababu iliompelekea kuzimia ni nini , lakini pia akili yake ilianza kukumbuka jumapili ya wiki iliopita Edna alirudi nyumbani akiwa na mabadiliko makubwa kimwili.
“Mh! nini kimempata?”
“Hata mimi nilishindwa kuelewa na nilishangaa baada ya kushituka jina la kwanza kuuliza ni la huyo Lanlan , Roma jitahidini mpate mtoto na Edna, sipendi hivi nyie ni wanandoa na kulala vyumba tofauti”Aliongea Blandina.
“Mama hilo lisikuumize kichwa , Edna akiamua mwenyewe juu ya hilo mimi sina shida , kwasasa sitaku kumlazimisha kutokana na namna tulivyokutana”Aliongea Roma na kisha alinyanyuka kwa ajili ya kuelekea ndani , lakini muda huo huo geti la jumba lao lilifunguliwa na gari aina ya V8 ilionekana ikiingia na Roma baada ya kuangalia vizuri aligundua mmoja ya mwanamke aliekuwa ndani ya gari hilo, wa kwanza alikuwa ni Jestina na mwingine alikuwa ni mwanamke ambaye hakumfahamu vizuri , lakini mwanamke huyo alikuwa ni mdogo wake Raisi Senga afahamikae kwa jina la maarufu la Mama Theresia.
“Roma”Aliita Jestina huku akimsogelea Roma kwa furaha na kumsalimia.
“Roma huyu ni Shangazi yako anafahamika kwa jina maarufu la Mama Theresia”Aliongea Jesgtina na kumfanya Roma kutabasamu na kisha kumsailimia mwanamke ambaye ametambulishwa kwake kama Shangazi.
“Namkumbuka siku ambayo nilikuja kuonana na wewe ndani ya Landmark Hotel nilimuona akiwa nyuma yetu”Aliongea Roma na kumfanya Jestina kushangaa na kisha kucheka.
“Kwahio ulimuona?”
“Ndio nilimuona na nilifahamu siku ile alikuwa na wewe kwa namna yoyote ile kwani alikuwa akituangalia sana”
“Ni kweli , nisamehe mama yako , Roma unaweza usiamini ila mimi nilikufahamu tokea siku ya kwanza unafika ndani ya familia yetu kwenye ile sherehe nadhani unakumbuka hata baba alitaka kuongea na wewe ni kwasababu ulikuwa ukifanana kabisa na baba yako wakati akiwa katika ujana wake”Aliongea Jestina na Roma alitabasamu na kuona kumbe mama huyo kipindi kile alikuwa kwenye misheni yake , ila aliona sio jambo la kuzingaria sana.
“Mama Theresia!”Aliita Blandina na kusogeleana na Mama Theresia na kukumbatiana , ilikuwa ni mara yao ya kwanza kuonana tokea Blandina arudi kutoka Kenya, walionekana kukumbukana sana na Roma aliona hilo na hakuona haja ya kuendelea kusimama , kwani alitembea na kuingia ndani na alikutana moja kwa moja na Sophia.
“Broo..!!”Aliita Sophia na kumshika mkono Roma na kupandisha nae juu na kumpekea kwenye sebule ya juu upande wa Balconi.
“Kuna nini Sophia mbona una mchecheto hivyo?”Aliuliza Roma na kumfanya Sophia kupumua.
“Siri yetu imefichuka”Aliongea Sophia na kumfanya Roma kushangaa hakumuelewa Sophia alikuwa akimaanisha nini.
“Siri gani hio sijakuelewa”
“Nimetoka kuongea na mama hapa , anasema aliongea na Sister Edna muda tu juu ya mimi kukaa nyumbani kwake”Aliongea Sophia na kumfanya sasa Roma kuelewa anachomaanisha ni nini.
“Kwahio unamaanisha Edna alikuwa akifahamu wewe sio mdogo wangu kama tulivyomdanganya?”
“Ndio na mama kasema Sister Edna anajua kila kitu na inaonekana aliamua kukaa kimya”Aliongea Sophia huku akionekana kuwa na hatia na kwa upande wa Roma licha ya kwamba swala hilo halikuwa likimsumbua sana , ila hakujua kwanini Edna alikaa kimya baada ya kugundua kama walimdanganya.
“Nilikuambiaga mimi , Mke wangu ana akili nyingi na ni ngumu sana kumdanganya”
“Acha kumsifia mbele yangu ,mama ndio kaharibu , yaani anapenda kuingilia mipango yangu sana”Aliongea huku akionekana kumlaani mama yake.
“Wewe nae una mipango gani?”
“Hupswi kujua nina mipango gani , hapa nawaza namna ya kumuomba msahamaha Sister Edna , sijawa muaminifu kwake toka mwanzo huenda ananichukia ndani kwa ndani”Aliongea Sophia
“Mimi sidhani Edna yuko hivyo naamini aliamua kukaa kimya kwasababu anakuchukulia kama mdogo wake na ndio maana hajaonyesha utofauti wowote , ila inapaswa kuongea nae”Aliongea Roma na kisha akaanza kupiga hatua kuelekea kweney chumba chake kwa ajili ya kupumzika.
“Kwahio mimi ndio ninaepaswa kuongea nae peke yangu na hili halikuhusu?”Aliuliza Sophia.
“Hehe… kwani nani alilazmisha kuishi na mimi, wewe na baba yako ndio mlinifanya nikadanganya, hivyo Edna akinikasirikia nitamwambia tu ukweli kama unataka kuwa mke wangu wa pili simple”Aliongea Rsoma huku akitabasamu kifedhuli.
“Roma…!!!”Aliita kwa hasira Sophia huku akikunja ngumu , lakini Roma hakumjali na kupotea kwenye macho yake.
*********
Edna alionekana kufurahi kweli , yaani moyo wake ulikuwa mweupee na alijihisi dunia yote alikuwa akiimiliki , licha ya kwamba ni masaa machache sana ambayo aliweza kuonana na Lanlan lakini kwake ni kama miaka mingi.
Lanlan vilevile alionekana kufurahia uwepo Wa Edna alimuona Edna kama mama yake kamili na hakuona kabisa utofauti wa aina yoyote ile na ndio maana alijiachia atakavyo na kuomba kununuliwa anachotaka.
Takribani masaa mawili yote Edna , Qiang na Lanlan walikuwa wakifurahia upepo wa baharini .
Lanlan alikuwa akiogelea kiasi kwamba ilimfanya Edna kuwa na wasiwasi kumruhusu Lanlan kuingia kwenye maji , lakini Qiang alimtoa wasiwasi Edna na kumwambia Lanlan anaweza akaingia kwenye maji chini kabisa na kuzuia pumzi kwa takribani dakika nne.
“Unadanganya”Aliongea Edna huku akimwangalia Qiang.
“Ni kweli Miss , Lanlan sio mtoto wa kawaida na kadri unavyoishi nae ndio utagundua kuwa anaweza kufanya mambo mengi ambayo watu wa kawaida hawawezi kufanya , ndio maana hata Master hajawahi kufikiria kumpekea Shule kutokana na uwezo wake”Aliongea Qiang na kumfanya Edna kushangaa.
“Unataka kuniambia kuwa Lanlan hajawahi kusoma popote hata chekechea ,mbona anaonekana akili yake kukomaa tofauti na umri wake?”
“Ndio maana nakuambia Lanlan ana mambo mengi ya kukushangaza Miss Edna”Aliongea Qiang lakini muda huo huo Lanlan alitoka kwenye maji na kuwakimbilia.
“Mama , Aunt Qiang , Grandpaa amerudi”Aliongea Lanlan na kumfanya Edna kushangaa.
“U?nasema kweli Lanlan?”
“Ndio Grandpaa karudi , yule kule…”Kabla hajamaliza Sentesi yake alitoka nduki akiwa na kijichupi tu na kufanya watu wamshangae na Edna aligeuka na kumwambia asikimbie lakini Qiang alimzuia.
“Ni master”Aliongea Qiang na kumfanya Edna kushangaa na moyo wake kuuma maana alijua ujio wa babu wa Lanlan ndio kumkosa hivyo Lanlan, aliangalia upande wa kushoto kwake na kweli Lanlan alimkubaria kwa kumrukia mwanaume mmoja mweupe asiemfahamu ambaye alikuwa ni mchina.
“Yule ndio babu yake Lanlan?”Aliuliza Edna na Qiang alitingisha kichwa nayeye kuanza kukimbia kwa kutabasamu kuelekea upande wa kushoto alipo Lanlan na babu yake.
SEHEMU YA 258
“Linda unamaanisha nini kwamba ulikuwa ni mpango wako?”Aliuliza Raisi Senga kwani hata yeye alikuwa akimjua Linda na tena sio kumjua tu kama msaidizi wa karibu na mtu wa kuaminika kwa Senior , lakini pia alikuwa akimfahamu Linda kama mchepuko wa raisi Jeremy.
Mheshimiwa Jeremy alikuwa haamini kama ni kweli Linda alikuwa akijua mpango LADO muda wote na kumkalia kimya, alitaka kusikiliza kila kitu ndio aamini kwani aliona Linda ni kama alikuwa akimtania.
Linda alivuta pumzi na kisha alitembea na kwenda moja kwa moja kukaa kwenye huku akimwangalia Jeremy kwa huruma.
“Jeremy najua naweza usinisamehe kwa kile nilichokifanya lakini naomba usikie kila kitu na baada ya hapo nitakuwa tayari kupokea adhabu ya aina yoyote ile”Aliongea mwanamama Linda kwa huzuni na kumfanya hata Raisi Jeremy kushindwa kuongea.
“Linda tunakusikiliza unaweza kuongea kila kitu”Aliongea Raisi Senga na Linda alivuta kumbukumbu kurudi nyuma.
“Kabla ya yote mnatakiwa kutambua kwamba mimi ni CIA undercover Ajent”Aliongea Linda na kumfanya Jeremy mwili wake kukaa kitako pasipo ya akili yake kuelewa.
“Linda niambie unadanganya?”Aliongea Jeremy lakini Linda hakumjali , Zaidi ya kuingiza mkono kwenye mfuko wa koti lake na kutoa Flash Disk na kumkabidhi mheshimiwa Senga.
“Hii inanithibishia utambulisho wangu kama CIA , ni nyaraka kamili pia zinazotambulisha uraia wangu wa taifa la Marekani”Aliongea na Rasie Senga haraka haraka alisogelea Tablet na kuunganisha Flash ile.
“Password ni nini?”Aliuliza Mheshimiwa Raisi Senga baada ya kugundua Flash Disk inanywira.
“Oprah Fraklin”Aliongea Linda.
“Hili ndio jina lako halisi naamini , CIA hawajawah kutumia majina yao halisi”Aliongea Raisi Senga na kufungua faili moja lililokuwa kwa mfumo wa kama Software yaani ni faili ambalo baada ya kuligusa ni kama limeliwa na virusi kwani lilionyesha vijiboksi vidogo vidogo.
“This File is Corrupted Linda”Aliongea Senga na Linda alimpa ishara ya kumpatia hio Tablet na Senga alimkabidhi na jambo ambalo liliwashangaza ni kwamba Linda alianza kuandika kwa haraka haraka kwa kutumia ile Tablet na kila maneno ambayo anaandika vile vijiboksi vilianza kujikusanya kwa muundo falani hivi kama vile mchoro na ndani ya dakika tu vile vijiboksi vilitegeneza picha ‘ Logo’ ya shirika la kijasusi la CIA na chini kukaonekana ‘Form’ yaani hapa nikimaanisha fomu ya kilectroinics ambayo inamuhitaji Linda kuingiza jina lake halisi la kuzaliwa nalo , mwaka aliojiunga na CIA , pamoja na nywira ili kufungua akaunti yake.
“Kwa sheria za ma ajenti wote wa CIA tunapokuwa kazini hatubebi vitambilisho vinavyotuunganisha moja kwa moja na taifa la Marekani , bali tunabeba Flash Disk maalumu ambayo ukichomekwa na kifaa chochote huonekana kama Flash disk hio ina virusi ndani yake”Aliongea Linda na Senga aliitikia na kuona Yes hapa yupo na CIA mweyenyewe sio wa mchongo.
Linda aliingiza jina lake la Oprah Franklin na kisha palepale karatasi kama mfano wa vyeti unavyopewa shuleni au ukihitimu ilionekana kwenye Tablet na Linda alimpatia Raisi Jeremy.
“Huo ndio utambulisho wangu wa uraia wa Marekani , lakini pia nikionekana kama raia ninaelitumikia taifa langu nje na nyumbani”Aliongea Linda na Jeremy alipitia faili hilo na kisha hakuongea chchote na kumpatia Senga ambaye baada ya kusoma maelezo hayo aliamini maneno ya Linda na kuona ni kweli wapo na jasusi wa siri kutoka Idara ya CIA kutoka taifa la Marekani.
“Ukute hata Kabwe anaweza kuwa CIA na ananichora tu, Damn it lazima niende kwenye ibada ya mpasuko wa mwezi, kwa namna hiikuna majasusi wa CIA wa ngapi ndani ya hili taifa”Aliwaza Raisi Senga mwenyewe huku akimuangalia raisi Jeremy.
“Mhmh ! Hehe Senior anaonekana na yeye kupitishwa ubatizo wa moto, huenda hisia alizokuwa nazo ni kama nilizopitia nilivyofahamu Blandina na Denisi wapo hai , namuonea huruma”Aliendelea kuwaza huku akimwangalia Rafiki yake.
“Jeremy nakumbuka mara ya mwisho ulivyogundua uwezo wangu usio wa kawaida uliniuliza niliupatia wapi na nikakujibu ni kutoka kwa kundi la Yamaguchi , ni kweli kabla ya kuja Rwanda nilikuwa chini ya taasisi ya kininja ya Yamaguchi na ndiko nilipopatia mbini na nguvu zangu za ziada za kimapigano ambazo mtu wa kawaida hawezi kuwa nazo”
“Yamaguchi , sijawahi kusikia hio taasisi”Aliongea Senga.
“Ndio huwezi kuifahamu kwani ni taasisi za siri sana”
“Linda tafadhari ongea kila kitu nielewe wewe ni nani na kazi yako ya kuwa ndani ya ikulu ya Rwanda ni ipi , weka kila kitu wazi kwani baada ya hapa utakuwa mfu labda unipe sababu ya kutofanya hivyo , nachukia sana usaliti kwenye Maisha yangu”Aliongea Jeremy kwa hasira.
“Niliingizwa ikulu ya Rwanda kwa maagizo ya The Doni mara baada ya kumaliza mafunzo yangu ya kininja kutoka Yamaguchi na kazi yangu kubwa ni kukulinda mpaka pale nitakapopewa maagizo mengine, kabla ya kufanya mafunzo na kundi la Yamaguchi nilikuwa ni CIA Agent., hata kuingizwa ndani ya kundi hilo ni maagizo maalumu niliopewa na taifa langu la Marekani”
“Linda nadhani kwanza unielezee hili kundi la Yamaguchi kazi yake ni nini haswa na kwanini wanafundisha watu kuwa maninja , hebu elezea kila kitu kwanza”Aliongea Raisi Senga kwa mchecheto , alihitaji kujua kila kitu.
Kwa maelezo ya Linda ni kwamba Yamaguchi ni taasisi ya siri kutoka China ambayo inafadhiliwa kwa asilimia mia moja na serikali mbili yaani China na Japani, taasisi hii kazi yake kubwa ni kufundisha vijana wa kuanzia miaka kumi na moja mafunzo ya hali ya juu ya Uninja huku dhumuni kubwa ni kuua ndio wanachofundishwa.
Anaendelea kusema kwamba Yamaguchi baada ya kuwafundisha wanafunzi wake huko msituni na kufuzu mafunzo yote kuanzia ya kimapigano mpaka ya kichawi , maninja hao hufudishwa sheria maalumu ambazo zinawaongoza kufanya kazi zao baada ya kutoka mafunzoni na kuchangamana na watu wa kawaida na moja ya sheria hizo ni kutokutambuana na mwanafunzi mwingine wala kuwasiliana, Linda anasema kwamba baada ya wanafunzi kuhitimu mafunzo ya kimapigano moja kwa moja wanapangiwa majukumu(Target) kwa ajili ya kufanyia kazi, hivyo hata yeye baada ya kumaliza mafunzo alipangiwa Target yake ambayo ni Ikulu ya Rwanda.
“Kwahio wewe kazi yako uliopewa na Yamaguchi ni kumlinda Mheshimiwa Jeremy?”
“Hio ndio kazi yangu na sio kwa Jeremy tu , kama itatokea raisi mwingine akachaguliwa ndani ya Rwanda basi target yangu itabadilika”
“Hapo Yamaguchi walikuwa wakifahamu kama wew ni CIA?”
“Hawakua wakifahamu hilo kwani sikujitambulisha kwao kama CIA na pia niliingizwa kwenye mafunzo hayo kwa makusudi maalumu”
“Makusudi gani?”
“Misheni yangu ilikuwa ni kuingia kwenye kundi hilo na kutoa taarifa zote ya kile kinachoendelea na nilifanya hivyo na hata baada ya kumaliza mafunzo niliendelea kuwa chini ya Yamaguchi licha ya kutopokea maelekezo mengine kutoka CIA”Aliongea Linda.
“Sasa ilikuwaje ukahusika kwenye mpango LADO au Serikali ya Marekani walikuagiza kufanya hivyo”
“Serikali ya Marekani hawajawahi kunitafuta tokea nimalize mafunzo ndani ya Yamaguch na kuja hapa Rwanda kwasababu wanajua mpaka sasa hivi nimekufa”Aliongea Linda na kuwafanya waheshimiwa kuzidi kuchanganyikiwa Zaidi.
“Unamaanisha nini?” Aliuliza Jeremy na Linda alianza kushikwa na huzuni na kisha akanyamza na kuvuta kumbukumbu.
Kwa maelezo ya linda alisema kwamba baada ya kutoka kwenye kundi la Yamaguchi na kupangiwa tageti yake , serikali ya marekani ilitoa oda maalumu ya Linda kuuwawa mara moja , mpaka muda huo mwenyewe anashindwa kuelewa kwanini alikuwa akiwindwa na Serikali yake ilihali alikuwa amepewa misheni na aliifanya vizuri , ila alisema wakati akiwa katika harakati za kuingia Ikulu ya Rwanda ndipo alipoweza kupata taarifa iliokuwa ikihusu yeye kuuliwa kwa oda kutoka makao makuu.(Termination order)
“Nani alitoa hio oda ya wewe kuuliwa na kwanini na nani alikuletea taarifa hio”
“Mtu alieniambia hio taarifa simfahamu , ila ninachokumbuka ni kwamba nilikuwa kwenye nyumba yangu hapa Rwanda asubuhi na kwenye meza kulikuwa na karatasi iliokuwa ikithibitsha kwamba nawindwa na CIA , mwanzoni sikuamini karatasi hio na nilitumia marafiki zangu makao makuu kuthibitsha Ushahidi uliokuwa kwenye mikono yangu na walinithibitishia ni kweli na nikawauliza kwanini nawinda na serikali yangu ilihali nilikuwa kwenye misheni , ila hakukuwa na majibu maalumu na Rafiki yangu ndani ya CIA aliniambia nisije nikampigia tena na nijifiche kwa namna yoyote”
Ukweli raisi Senga bado alionekana kutokumuelewa kabisa Linda , kwanza mwanamke huyu alisema kwamba aliingia kwenye kundi la Yamaguachi akiwa kama CIA akiwa kwenye misheni maalumu huku akichukua mafunzo ya uninja ili kujifanyisha na yeye ni mwanfunzi na baada ya kumaliza mafunzo akapangiwa taget yake , sasa raisi Senga ambacho hajaelewa ni kwanini CIA hao hao ambao wamempa misheni kutoa oda ya kifo chake ilihali Linda bado alikuwa na umuhimu kwao, pili pia Linda anaeleza kwamba alijikuta akiwa nyumbani kwake asubuhi na alipoamka alikuta karatasi iliokuwa ikithibitisha oda ya kuuwawa kwake na mtu ambaye kamletea karatasi hio hakuwa akimfahamu, bado maelezo yake yalikuwa na maswali mengi.
Kwa upande wa Raisi Jeremy licha ya kwamba alikuwa na hasira na Linda lakini pia alikuwa akimuogoopa , alikuwa akijua uwezo wa kimapigano aliokuwa nao Linda , lakini pia uwezo wake wa kupotea kimazingara pia alikuwa akiufahamu na alijiambia kama Linda angekuwa mtu wa kawaida basi angemhoji akiwa chini ya chumba cha mateso kama ilivyokuwa kawaida yake na kwa muda huo alishiandwa hata kuuliza maswali kwani alikuwa kwenye hasira nyingi sana na ndio maana aliacha Rafiki yake Senga amuulize Linda maswali yote.
“Linda unayosayesma haya yote ni ya kweli au kuna jambo unatudanganya,?”
“Nimeamua leo kuweka ukweli wote wazi hivyo sina nia ya kuficha chochote, nitaeleza kile ninachofahamu kwa upande wangu”Aliongea Linda.
“Ilikuwaje ukahusika kwenye mpango LADO , tueleze hapo tuelewa kwanini nyaraka za mpango LADO zina sahihi yangu ya .senior na ya Rahel? Na kuonyesha kama sisi ndio wahusika wa mpango huo?”
SEHEMU YA 259
1997
Ni mwezi wa kumi na moja ndani ya ofisi ya mkuu wa majeshi , Jenerali Cammillius Kweka anaonekana Linda alievalia suti ya rangi nyeusi akiwa aneo la Mapokezi akiwa ameshikilia mkoba wake.
Linda alionekana kuwa na wasiwasi kweli licha ya kwamba yupo eneo ambalo lina ulinzi mkubwa sana nchini kutokana na maamuzi yote ya kijeshi kufanyikia hapo , lakini pia sehemu ambayo wafanyakazii wake wote ni wanajeshi.
Linda akiwa eneo la Mapokezi kwa takribani dakika kama kumi na tano hivi , huku akikagua kila mwanajeshi aliekuwa akiingia kwa wale waliokuwa na gwanda na wale ambao hawakuvaa gwanda , alifuatwa na mwanajeshi wa cheo cha Kapteni mwanaume mrefu mweusi wa umri mkubwa kuliko wake.
“Dada unaweza kunifuata , Jenerali ameridhia kuonana na wewe”Aliongea yule mwanajeshi na kumfanya Linda kutabasamu.
“Asante sana kaka kwa kunipelekea ombi langu”Aliongea Linda akiweka tabasamu na yule mwanajeshi alitabasamu pia na kupokea shukrani na kisha alianza kutembea kumpeleka Linda kwenye ofisi ya Afande Camllius Kweka.
“Nafikiri nimefanya maamuzi sahihi ya kuja ofisini kwake kuongelea hili swala”Aliwaza Linda huku akitembea kwa hali ya kujiamini.
Ukweli ni kwamba Linda kabla ya kuja hapa Tanzania kufanya maongezi na mkuu wa majeshi ya Tanzania , jana yake asubuhi kuna tukio ambalo lilimtokea na kumchanganya sana.
Jana yake mrembo huyu baada ya kurudi kutoka Ikulu ya Rwanda sehemu ambako anafanyia kazi kama katibu muhtasi wa raisi Jeremy , alivua nguo zake na kuzitundika vizuri kwenye kabati kama ilivyokuwa kawaida yake.
Linda ni moja ya wanawake ambao hawakuwa na mambo mengi na hii yote ni kutokana na mafunzo aliokuwa nayo ya kimapigano , alikuwa ni mwanamke ambaye hata mavazi yake karibia yote ni suti tupu na aina ya mavazi mengine ni kama tracksuit ambazo mara nyingi hutumia kuchukulia mazoezi ya kukimbia na pale anapokwenda Gym na ndio maana kwa mwaka huo wa tisini na saba katika moja ya nyumba za serikali alipokuwa akiishi , nyumba yake haikuwa na vitu vingi , kulikuwa na makochi ya mbao upande wa sebuleri na meza katikati ya mbao pia pamoja na Tv ya chogo , kwa upande wa chumbani kwake hakukuwa na vitu vingi Zaidi ya kabati la mbao analotumia kuhifadhia nguo na baadhi ya vitu vyake vya thamani.
Sasa siku ambayo mrembo huyu anaamka asubuhi nyumba yake ilikuwa sio ya kawaida kama alivyozoea , kwanza kabisa kwenye mwili wake kulikuwa na mabadiliko , katika paja lake kuna alama ambayo hata yeye mwenyewe hakujua alama hio imetoka wapi na alipoona hio alama ya tatoo ni kama vile yupo kwenye ndoto na atashituka na kuona alama hio kupotea , lakini hakukuwa na mabadiliko kwani mpaka inatimia saa mbili asubihi alama hio ipo , alijaribu kuifuta lakini haikuwezekana., alishangaa na kuogopa kwa wakati mmoja na kujiuliza alama hio imefikaje kwenye mwili wake , kwani jana alilala akiwa hana alama na hata kama kuna mtu aliingia nyumbani kwake na kumuwekea hio alama angetambua, kwani yeye alikuwa ni mwanajeshi na wanajeshi usingizi wao ni wa machale , lakini ajabu alilala fofofo na cha kushagnaza Zaidi anaamka asubuhi na kukuta ana alama kwenye mwili wake , alama ambayo haifutiki lakini pia hakujua inahusiana na nini.
Linda akiwa katika mawazo alitembea mpaka eneo la sebuleni huku akijihisi kuwa na uwoga wa ajabu kwa swala ambalo limemtokea na alikimbilia sebulni kwa ajili ya kuangalia usalama na ile anafika eneo la makochi ndipo alipoona bahasha ya khaki iliokuwa mezani na kumfanya kushangaa na kuanza kukagua nyumba nzima kuthibitisha usalama , lakini ajabu ni kwamba nyumba yake haikuonesha hali yoyote ya mtu kuingia kabisa kwani kama alivyofugna milango kabla ya kulala usiku wa jana , ndivyo alivyokuta asubuhi.
“So strange, what is happening , am I hallucinating”Aliongea mwenyewe huku akisogelea bahasha iliopo kwenye meza na kuiangalia juu yake.
“From X to Oprah Franklin”
Hayo ndio maneno yliosomeka juu ya bahasha hio na kumchangnya mno Linda , kwanza jina ambalo lipo juu ya Bahasha ni jina ambalo hajawahi kulitumia tokea afike nchini Rwanda na alishangaa imekuwaje fomu ikawekwa nyumbani kwake na ikawa na jina lake la utotoni , jina ambalo lipo kwenye database ya serikali ya Marekani tu , alishangaa na kujiuliza maswali na kutetemeka mikono kwa wakati mmoja.
“Itakuwa ni CIA hawa lazima tu, lakini hapana vipi kuhusu tatoo kwenye paja langu na yenyewe ni kutoka kwa CIA?”Aliwaza Linda huku akigeuza geuza bahasha ambayo ipo kwenye mikono yake.
“Usalama wote upo vizuri , hakuna sehemu inayoashiria mtu kuingia ndani lakini naamka asubuhi nikiwa na alama kwenye paja langu la mguu wa kushoto na sasa nimeshikilia bahasha ambayo sijui ndani yake kuna kitu gani , mtu aliefanya haya yote ni nani , je ni kundi la Yamaguchi, lakini hapana Yamaguchi hawafahamu jina langu halisi , sio wao naamini kuna mtu mwingine anaenifahamu”Aliwaza Linda lakini alijikuta akiwaza ujinga kwani aliamini huenda majibu yote yapo kwenye bahasha alioshikilia kwenye mikono yake.
Linda alikaaa chini harakaharaka na kuanza kufungua ile bahasha kwa kuchana na kisha akatoa karatasi nne zilizopo ndani yake na kuzishika mkononi na kuanza kusoma , lakini ajabu ni kwamba juu ya karatasi ya kwanza kuna alama ambayo ni kama iliokuwa kwenye paja lake la mguu.
“Nimeingia nyumbani kwako pasipo kuacha alama yoyote ya namna nilivyoingia , lakini pia nimeweza kukuchora tatoo kwenye paja lako la kushoto na nikaacha nyaraka ambayo unazisoma , Amini kwamba mimi sio mtu wakawaida na naweza kukufanya jambo lolote kwa muda ninaotaka” ndio sentensi ya kwanza iliokuwa juu ya nyaraka ya kwanza , moyo ulipiga kite na kuogopa Zaidi.
“Unatakiwa kutimiza kila maelekezo nilioandika kwenye nyaraka nilizoacha kama unataka kunifahamu , kwasasa utanitambua kwa jina la X na alama kwenye paja lako ni ya utambulisho kwamba wewe ni mwanachama”Sentensi ya pili kwenye Nyaraka na kumfanya Linda kuzidi kuchanganyikiwa.
Mwanachama , X , Tatoo alijiuliza vyote kwa pamoja na Linda kwa papara Zaidi alifungua ukurasa wa pili na alijikuta akishangaa kwani aliona picha ya mtu anaemjua.
Raheli mpenzi wa siri wa Raisi Jeremy ndio picha alioshikilia na kumfanya kushangaa Zaidi lakini alichana na picha hio na kuhamia nyaraka ya ta tu na hii ilikuwa ni nyaraka ya maandishi ambayo ina malekezo.
Malekezo no 1: “Mtafute Cammilius Kweka kutoka Tanzania kipengele namba mbili ndio anaepaswa kukisoma na kukuambia cha kufanya.”
Malekezo No 2: “Kweka huyo ni mshirika wako zidi ya Mpango LADO na nyaraka hii inamtambulisha”
Maelekezo no 3: “Kiongozi yoyote lazima asaini aidha kwa kukubali au kulazimishwa ili kuidhinisha mpango LADO na mzazi mmoja wa mhusika katika mpangon asaini ili kulinda mpango husika”
Linda alisoma vipengele vyote viwili na kujikuta akishangaa Zaidi lakini aliachana na nnyaraka ya tatu na kufungua nyaraka ya nne ambayo ilikuwa ikijitegemea na Linda baada ya kuisoma jasho lilianza kumtoka.
“Termination Order , Ajenti Flower Rain”Alisoma Linda maelezo hayo na kuangalia sahihi na muhuli na alichoka kwani Ajent Flower rain ni jina la kodi ndani ya CIA.
“Director Powel From CIA” ndio sahihi ambayo Linda asingeshindwa kuitambua na alijiuliza kwanini CIA wanamtaka kufa ni kipi ambacho amekosea ni kweli yupo Rwanda pasipo kutoa taarifa kwa wakubwa wake , lakini hakuweza kufanya hivyo kwasababu wao wenyewe ndio wa kwanza kumtafuta kwa njia wanazozijua wao, lakini Linda bado alikuwa kwenye maswali na mshangao , alijiuliza kama kweli CIA wametoa oda yake ya kufa inakuwaje mpaka sasa hivi yupo hai kwani alikuwa akifahamu uwezo wa shirika la CIA wakitoa oda jihesabie tayari ni mfu.
Linda kwa hasira akaanza kukung`uta ile bahasha kuhakikisha karatasi zote zimetoka na matarajio yake yalikuwa kweli kwani kulidondoka kikaratasi cha njano mfano wa kimemo.
“You are already dead when you go along with plan , you will be alive and hunted when you refuse to go along with plan, this notes only for you , I am X till second phase of plan”
“Wewe ni mfu tayari kama utaenda na mpango , utakuwa unaishi na kuwindwa kama utakataa kwenda na mpango , hiko kijimemo ni kwa ajili yako , mimi ni X mpaka hatua ya pili ya mpango” kijimemo aliweza kukisoma hivyo na kujikuta akishangaa Zaidi lakini ghafla Linda yupo Tanzania ndani ya makao makuu ya Jeshi la Tanzania akikubali kila kitu kilichoachwa nyumbani kwake na kuamini ni ukweli.
Kwanza anaanza vipi kuona sio kweli , yeye ni ninja wa hatari kutoka kwenye kundi la Yamaguchi lakini mtu anakuja nyumbani kwake na kumchora tatoo kwenye paja na kuacha maelezo pasipo yeye kutambua, aliamini huyo m mtu ni wa hatari sana na hivyo dakika ambayo atafanya kinyume basi ndio dakika ambayo kifo chake kitamkuta.
“No I am Dead , I will go along with plan”Aliwaza Linda wakati akifika mbele ya ofisi ya mkuu wa majeshi , jenerali Cammilius Kweka na mlango ukafunguliwa na akaingia ndani ya ofisi yanye ubaridi wa kiyoyozi wa hali ya juu , ofisi ambayo mkuu wa majeshi hufanyia maamuzi.
“Karibu Binti, nimesikia unataka kuonana na mimi na unatokea Ikulu ya Rwanda karibu sana”Sauti nzito ilimkaribisha Linda na Linda alitabasamu.
*********
Senga alijikuta akishangaa na kukosa cha kusema , kwahio mpango wote ule wa mwanae Denisi kupanda ndege , lakini pia Lorraine mtoto wa Jeremhy na Raheli ulisukwa na Senga pamoja na Linda, alijikuta akikaa chini na kuanza kuona baba yake ni mtu hatari sana na asipokufa mapema anaweza kuleta shida zaidi kwa taifa.
“Kwahio huyo mtu aliekuja nyumbani kwako na kukuchora alama kwenye paja ndio aliekupa maelekezo ya kufanya kila kitu”
“Ndio nilifanya kila kitu kwa maelekezo yake”
“Vipi kuhusu sahihi yangu , lakini pia mhuli wa raisi iliwezekana vipi maana sikumbuki kutia Saini wala kugonga muhuli karatasi ya mpango Zero”
“Ulifanya kila kitu kwa maelekezo yangu ninao uwezo huo na sio kwako tu hata kwa Raheli alitia sahihi pasipo ya kujitambua na kwako Senga hivyo hivyo , mbinu hio ni sehemu ya mafunzo kutoka kwa kundi la Yamaguchi, I have ability to hypnotize anyone and do things according to my wishes”
“Kwahio Linda mpango na ushauri ulionipa wa kumpeleka Lorraine kwenda China kupitia Malaysia ulikuwa ni mpango wako na Afande Kweka , lakini kwa maneno marahisi ni kwamba wewe ndio uliemuua mwanangu , ulimchukua mwanangu kutoka kwangu mtoto ambaye alikuwa ni kama zawadi kutoka kwa Rahel?” Aliongea Jeremy huku akianza kupandwa na jazba mdogo mdogo.
“Jeremy najua unahasira sana , lakini kumbuka kama isingekuwa mimi usingweza hata kufahamu kama una mtoto duniani , Raheli hakuwa na mpango wa kukuambia ila mimi nilikuambia kwa mapenzi yangu mwenyewe”
“Stupid woman!, you told me in order for your evil plan to work , umenifanya nimshawishi Rahel kuniachia mtoto mmoja kati ya mapacha ili iwe rahisi kwako”
“Hapana Jeremy huo haukua mpango wetu na nzee Kweka kwa mara ya kwanza , the plan was very simple na kama sio mimi usingesikia kabisa kuhusu Edna wala Lorraine, Jeremy tatizo lako uliamini Rahel anakupenda san ana hapo ndipo ulipokosea”
“How so, unataka kuniambia Rahel hanipendi?”Aliuliza kwa hasira mno kiasi cha misuli ya uso kusimama.
********
“Wewe ni miss Edna , mwanamke Tajiri ndani ya taifa hili?”Aliuliza Babu yake Lanlan.
“Ndio ni mimi” Alijibu Edna na hii ni baada ya kusalimiana na Babu yake Lanlan na Edna kushangazwa na babu hiyo kuwa wa umri mdogo.
“Nakiri kwamba unafanana kwa asilimia mia moja na mama yake Lanlan , lakini hio haikufanyi kuwa mama yake”
“Grandpa..”Aliingilia Lanlan kama vile alikuwa akielewa kinachoongelewa ila kwa upande wa Edna alijisikia vibaya ,mzee huyo alionyesha kuwa na maneno ya kuumiza lakini yanayoeleweka.
“Qiang mchukue mtoto na mnisubiri pale mbele”Aliongea kwa Kingereza na mlezi wa Lanlan alimchukua Lanlan.
“Hapana Lanlam anataka kuwa na mama yake”
“Lanlan nisikilize mimi babu yako huyu sio mama yako na nitakutafutia mama yako mwingine”Aliongea yule mzee na kumpa ishara Qiang kuondoka na Lanlan , lakini Lanlan alianza kulia na kumfanya Edna kukasirika .
“Huna haja ya kukasirika kwani huna haki yoyote ya kufanya hivyo”Aliongea yule mchina kwa maneno ya kejeli na Edna alijikuta akikasirika na kuumia lakini hakutaka kuonyesha aliona avumilie yapite kwa ajili ya Lanlan.
“Maneno yangu yanaweza kuonekana ya kejeli lakini huo ndio ukweli”
“Naomba uende moja kwa moja kwa ulichotaka kuongea”Aliongea Edna.
“Unaonekana kumpenda Lanlan sana na Lanlan pia anakupenda na tokea akuone amekuwa msumbufu na nikiri ni kweli Lanlan mama yake mpaka sasa hivi kashafariki hivyo hana mama, unaonaje kama utamlea kama utatimiza masharti yangu”Aliongea yule mzee na kumfanya Edna moyo wake kulipukwa na furaha.
“Kumlea , nipo tayari kumlea niambie masharti yako”Aliongea Edna pasipo hata ya kufikiria ukweli licha ya kwamba alikuwa akimpenda Lanlan lakini wazo la kumlea bado hakuwa nalo.
“Sidhani kama utayaweza masharti”Aliongea yule mwanaume na kutmbasamu kwa kejeli.
“Niambie ni masharti gani hayo unayoamini siyawezi?”
“Okey Miss Edna ukweli ni kwamba sharti ni moja tu na ukilitimiza unaweza kuondoka na Lanlan, kwanza mtoto wenyewe msumbufu kwangu na nina kazi nyingi kiasi cha kunifanya niondoke bila taarifa hivyo sifai kuwa mlezi wake”Alipumua na kisha akamwangalia Edna.
“Achana na mumeo kwa talaka na baada ya hapo nitakuruhusu umchukue Lanlan”
“Nini..!!”
“Ndio usishangae kama utaweza kuchanana Roma , basi Lanlan kuanzia leo atakuita mama , maamuzi unatakiwa kuyafanya sasa hivi , Je upo tayari kuachana na mume wako umchukue Lanlan au upo tayari kuendelea na mume wako umkose Lanlan? , kwa upande wa Lanlan naamini anaweza kuniacha mimi babu yake nilieteseka nae na kukuchagua wewe”Aliuliza yule mzee kwa Kingereza na kumfanya Edna kutoa macho , kwenye Maisha yake hajawahi kukutana na Dillema ya aina hio.
“Mama Lanlan anapenda kuishi na mama yake, usiniache tena”Aliongea LAnlana na kuanza kulia kilicho cha kwikwi huku akishika miguu ya Edna na Edna alimwangalia Lanlan na kuanza kutokwa na machozis.
“Miss Edna fanya maamuzi , Sharti ni dogo sana”Aliongea yule mwaume mchina na kuonyesha kejeli za waziwazi.
Unafikiri Edna atamuacha Roma na kumchukua Lanlan , nini kitendelea itaendelea kesho.
HAPPY WIKIEND KUTOKA KWA MWANDISHI SINGANO JR , NAMBA YANGU NI WATSAPP NI 0687151346 , USISITE KUNICHEKI UNAPOHITAJI MWENDELEZO
Kwa Leo naishia hapaSimulizi mdefu sana hii ima inside stories nyingi hakikisha husahau majina ya kila muhusika ...nitajitahidi kuishusha hapa ila pia mochango yenu ni Muhimu GROUP tupo season 3
Sent from my TECNO-W5 using JamiiForums mobile app
Hahaha.. mimi ndio Hades mwenyewe , Karibu watsappUnajua singano kwanza naomba nikusifie(nyambafffff)isikute umetuletea story ya kweli wewe ndio Roma? unstumia akili kubwa sana kutunga bro,nitakutumia pesa unipe muendelezo