Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
umesikika mkuu ila najitahidi kupost zaidi ya vipande 12 kwa wiki ni rate nzuri , ninaweza igawa 12 mara tatu ikawa vipande vinne nne na kupost mara tatu ila muda upande wangu si rafiki sana , kwanj lazima nitumie laptop kupost ili simulizi isipoteze Aya . na mtiririko mzuri wa usomaji hivyo naweza toa ahadi halafu nikashindwa tekeleza ndio maana nikishusha nashusha vya kutosha .mkuu singanojr hongera na asante kwa hii kazi......
ila mkuu ungekua unashusha vitu walau mara 3 kwa wiki ili wasomaji tusipoteze muunganiko wa matukio.....
hii kukaa siku 5 bila bila mtu unasahau hata ulipoishia, unakosa ule mvuto wa hii simulizi yako,...... mtu anakua anasoma as if kila kipande kinajitegemea,
btw, simulizi yako ni nzuri sana, tamu wala haichoshi, sema changamoto ni hio ya kukaa muda mrefu bila mwendelezo, inaondoa ladha ya simulizi kwa mfuatiliaji
Ahsante kwa burudani mkuu...utukumbuke na weekend hii kaka tupunguze stress za maisha.umesikika mkuu ila najitahidi kupost zaidi ya vipande 12 kwa wiki ni rate nzuri , ninaweza igawa 12 mara tatu ikawa vipande vinne nne na kupost mara tatu ila muda upande wangu si rafiki sana , kwanj lazima nitumie laptop kupost ili simulizi isipoteze Aya . na mtiririko mzuri wa usomaji hivyo naweza toa ahadi halafu nikashindwa tekeleza ndio maana nikishusha nashusha vya kutosha .
Leo itaendelea inshallah
umeeleweka mkuu, ilikua ushauri tu na nashukuru kwamba umechukulia positive, maana angekua mwingine angekuja na matusi/kejeli.........umesikika mkuu ila najitahidi kupost zaidi ya vipande 12 kwa wiki ni rate nzuri , ninaweza igawa 12 mara tatu ikawa vipande vinne nne na kupost mara tatu ila muda upande wangu si rafiki sana , kwanj lazima nitumie laptop kupost ili simulizi isipoteze Aya . na mtiririko mzuri wa usomaji hivyo naweza toa ahadi halafu nikashindwa tekeleza ndio maana nikishusha nashusha vya kutosha .
Leo itaendelea inshallah
kasema leo hapo ataendelezaAhsante kwa burudani mkuu...utukumbuke na weekend hii kaka tupunguze stress za maisha.
OhoooooKIJASUSI
Ep 01: Jiue Mwenyewe
Jiue Mwenyewe Sehemu ya Kwanza
IMEANDIKWA NA : RICHARD MWAMBE
Simulizi : Jiue Mwenyewe
Ni mara tano na zaisdi ames
CHAPISHO LA 01
1
DURBAN – AFRIKA KUSINI-Saa 3:21 asubuhi
NDANI ya jengo refu kuliko yote, Monte Blanc, lililopo katika jiji la Durban, jimbo la KwaZulu Natal, Afrika ya Kusini, ni mtu mmoja aliyekuwa akiwindwa kwa udi na uvumba. Ni mara sita kama si tano mtu huyo kakoswakoswa na muuaji hatari wa kike kutoka Marekani, Tracey Tasha. Mara hii kamfuata hukohuko katika ardhi ya nchi yake, Afrika ya Kusini.
Lamborghini Veneno, gari ya gharama kabisa duniani iliegeshwa taratibu katika maegesho Monte Blanc, nyuma yake ikasimama gari nyingine, BMW nyeusi, vijana wane wakakamavu waliovalia suti nyeusi zilizotanguliwa na mashati meupe na shingoni mwao kila mmoja alining’iniza tai ndefu nyeusi. Walikuwa kikazi zaidi; macho yao yakitazama kila upande kwa umakini wa hali ya juu, mmoja wao aliiendea ile gari, Lamborghini, akaufungua mlango na kuukinga upande wa juu kwa kiganja cha mkono wake wa kushoto ili atokaye ndani asijigonge. Kwa mtindo huu ilionekana atokaye ndani ya gari hiyo ni Mheshimiwa sana, delicate person.
The Great Khumalo kama alivyojiita, alitoka nje ya gari ile, akajiweka vizuri suti yake ya gharama, huku mkono wake wa kulia ukiwa kwenye kifundo cha tai ili kuirekebisha alianza kuvuta hatua ndogo ndogo na mwamvuli ukiwa umeshikiliwa juu yake ili manyunyu ya mvua yaliyokuwa yakinyurunyuta mudaasubuhi hiyo yasimletee tabu. Viajana wake walifuata nyuma wawili na mbele wawili, yeye alikuwa katikati. Ilikuwa ni ngumu kumgusa mtu huyu, tajiri sana katika jiji la Durban; nani asiyemjua Khumalo? Hakuna shule ambayo hajawahi kuifadhili katika jiji hilo, alijulikana, alipendwa, alitazamwa kama almasi. Anaitwa Gervas Khumalo aliyezaliwa na kukulia katika kitongoji cha Berea, alizaliwa katika familia yenye maisha ya kati, lakini iliyoweza kumlipia masomo yake ndani na nje ya nchi mpaka akawa mtu mkubwa.
Hatua zake zilimfikisha katika mlango mkubwa wa jengo hilo, ukafunguliwa kwani yeye hakutakiwa kushika sehemu yoyote, kila mtu alimhusudu, lakini hakukuwa na nafasi ya kumpa hata mkono kwani alikuwa akilindwa vilivyo, moja kwa moja wakaingia katika lifti ili kupanda juu katika ofisi Fulani ya jengo hilo. Monte Blanc, jengo lenye urefu wa mita 133, sakafu (ghorofa) 40, lililojengwa hapo tangu mwaka 1985. Ndani ya lifti hiyo alizungukwa pande zote na vijana wake waliosheheni silaha ndani ya makoti yao.
23, mmoja wao alibofya kitufe kilicho katika kuta ya dude hilo na mara tu likaanza kupanda juu. Lilipofika mahala lilipoamrishwa likasimama kitu kama kengele kikagonga kwa pigo moja laini, mlango ukafunguka, wakateremka na kutembea kuelekea mahala Fulani, wakaipita milango kadhaa. Kila mtu alipisha tajiri huyo apite. KwaZULU Beauty and Massage, wakasimama hapo, mlango wa kioo ukafunguka wawili wakaingia na tajiri wao na wawili wakabaki mlangoni kuhakikisha ulinzi. Khumalo moja kwa moja alienda katika kochi kubwa na kulikalia mara baada ya vijana wake kulihakikisha kuwa lina usalama wa kutosha. Muda huo huo mwanamke mrembo mweupe wa Kiafrika alijitokeza kwenye mapazia yaliyokuwa na nakshi za kumetameta. Ndani ya ofisi hiyo pana na nzuri kulikuwa na wasichana wane waliokuwa katika kazi zao za kila siku, mwingine mapokezi, mwingine kupokea pesa na kutoa risiti, mwingine usafi na mwingine kuongoza wageni kule wanakotakiwa kwenda.
“You are welcome Sir,” (karibu sana mheshimiwa) yule mwanamke akamsalimu. Ukimwangalia alivyo, utasema ni Malaika kashushwa kutoka Mbinguni lakini alikuwa ni Binadamu kama wengine.
“Thank you so much,” (asante sana) The Great Kumhalo akaitikia karibisho hilo, yule Mwanamke akampa ishara ya kumfuata naye akafanya hivyo.
Haikuwa mara ya kwanza kwa tajiri huyo na matajiri wengine wengi kufika sehemu hiyo, wote walifika hapa kwa minajiri ya kupata huduma ya kukandwa mwili, ili kuirudisha miili yao katika hali nzuri ya kiafya. Bwana Khumalo alikwishazoea mara nyingi kuja mahala hapo kwa ajili ya huduma hiyo, alikuwa amejipangia ratiba kabisa ya tendo hilo.
Akainuka na kumfuata yule mwanamke huku walinzi wake nao wakiwa nyuma yake, wakaingia katika mlango ule wa mapazia na kufuata korido ndefu, waliipita milango mingi ya vioo ambayo ndani yake kulikuwa na wanawake waliokuwa wakifanyiwa urembo wa mwili na nywele, vyumba vingine vilikuwa ni vya mazoezi ya viungo, kulikuwa na mabafu maalum kwa ajili ya wanaotaka kuusafisha mwili kwa mvuke.
Walifika kwenye moja ya milango ambayo daima huingia hapo, wale walinzi wakasimama nje ya mlango na bosi wao akaingia ndani pamoja na yule mwanamke kwa ajili ya kumpa huduma hiyo. Juu ya mlango ule kuliandikwa V.I.P.
Ohoooo
What do you mean????Ohooooo
Hades sijui kama atatoboa...mambo yake anafanya kizembe sana. Madem zake wanamcost mnooohuku Yan Buwen kapata damu ya hades, kule Anthena keshaanza kucheza karata zake na Dorisi, ........ aisee hii kitu inakoelekea sijui
kwanini hatofanya kazi mzee? siku Hdes akimjua huyu bwashee mtaka damu patachimbika maana jamaa kamwandama mnooo kisa anamtaka The Don.Sifa kubwa aliyonayo ni hurumaa ila ile damu haitafanya kazi
Ewhuuu! I've succeeded to catch up with you. I started reading this stuff 4 weeks ago. Congrats to me, but more congrats to the author- Your majesty SinganojrSEHEMU YA 313
Kwa maelezo ya Neema ni kwamba Mzee Chino alishambuliwa nyumbani kwake na watu wasiojulikana na kumjeruhi kwa kumpiga risasi na baada ya tukio hilo ndio Neema aliekuwa kazini kwake katika kampuni ya Maple ndio aliweza kupata taarifa ya tukio hilo na kuja mpaka hospitali ya Aghakhani na kukuta tayari mzee Chino akiwa katika chumba cha matibabu..
Kwahio muda ambao Roma alifika ndani ya hospitali ya Aghakani ni kwamba ndio Mzee Chino alikuwa na saa moja tokea afikishwe hapo na madaktari walikuwa wakiendelea na zoezi la kuokoa Maisha yake.
Roma alishangazwa na tukio hilo la kupigwa kwa lisasi kwa Mzee Chino na kujiuliza ni jambo gani ambalo linendelea hapa Tanzania mpaka matukio ya namna hio kutokea.
“Roma nitafanya nini mimi Mzee Chino na yeye akipoteza Maisha,, nitabaki mwenyewe Roma, Mzee chino ni ndugu pekee niliebakiwa nae hapa Duniani”Aliongea Neema huku akilia kwa kwikwi na kumfanya Roma kumuonea huruma mwanamke huyu , kwani alikuwa akimjua Neema kwa siku kadhaa alizoweza kufahamiana nae alikuwa ni mtu ambaye ana uwezo mkubwa wa kutawala hisia zake , sasa tukio hili na kwa jinsi ambavyo alikuwa akionekana ilikuwa ni dhahiri kwamba Mzee Chino alikuwa mtu muhimu sana kwake.
Roma kwa wakati huo kwa kweli hakuwa akijua cha kufanya na hata baadhi ya watu walioambatana na Neema walionekana kutuoelewa uhusiano uliokuwepo kati ya Neema na Roma , ila hakuna hata mmoja aliepata ujasiri wa kuuliza.
Roma ilibidi asubirie akiwa nje na Neema ili kuona ni kipi kitajili kwa afya ya Mzee Chino, wakati wote Neema alionekana kuomba baya lolote lisimkute mzee huyo na kumfanya Roma ajitahidi kumfariji Neema.
Lisaa limoja mbele hatimae Dokta Shukuru Omary mganga maarufu ndani ya hospitali hii alitoka kwenye chumba cha upasuaji , huku akionesha kuchoka mno lakini licha ya hivyo Neema hakutaka kumpa ahueni , alichotaka kujua muda huo ni maendeleo ya Baba yake wa hiari , yaani Mzee Chino.
Dokta alimwangalia Waziri na kuonyesha hali ya kukata tamaa na hilo Roma aliweza kulishuhudia.
“Tumeweza kutoa risasi mbili zilizompata begani , lakini moja iliompata kwenye uti wa mgongo imeshindikana kutoka na naweza kusema kwamba kwa sasa hatuwezi kabisa kuitoa na kuna uwezekano mdogo sana kutembea hata kama atapona”Aliongea Dokta Shukuru kwa hali ya huruma na kumfanya Neema kuangua kilio upya.
“Dokta nini kinapaswa kufanyika juu ya hali yake?”Aliuliza bwana aliekuwa amekuja na Neema ambaye amevalia Suti.
“Tunaweza kuitoa risasi kwa kumfanyia upasuaji lakini kwa hali aliokuwa nayo hata kama itatoka hakuna namna ya yeye kupona”
“Sasa Daktari kwanini msiitoe hio risasi muda huu na kuacha ikiendelea kubakia kwenye mwili kama uwezo huo mpo nao?”Aliuliza Roma.
“Kwa hali aliokuwa nayo hatuwezi kumfanyia upasuaji mkubwa wa namna hio , tunapaswa kumuacha kuona kama atarejewa na fahamu ndio tuanze utaratibu wakumfanyia upasuaji kwenye uti wa mgongo ,lakini…”
“Lakini nini Dokta?”Aliuliza Neema na Dokta Shukuru alimeza mate kidogo.
“Kadri risasi inavyobaki kwenye mwili wake ndio madhara Zaidi kwenye afya yake yanavyozidi kuongezeka anaweza akawa in ‘Vegetative condition’ Maisha yake yote”Aliongea na hapo ni kama alirusha bomu lingine kwa Neema kwani machozi yalimtoka mfululizo.
Vegetative state ni hali ambayo inaelezea mgonjwa ambaye hana uwezo wa kufanya chochote ilihali ya kwamba bado yupo hai , yaani hatokuwa na uwezo wa kuongea kutumia akili yake , au kufanya chochote kile kama binadamu wa kawaida.
“Dokta kwahio kama kuna uwezekano wa mgonjwa kurejewa na hali yake ya kawaida mnaweza kumfanyia upasuaji wa uti wa mgongo na kumuokoa katika madhara makubwa yanayoweza kumkumba?”Aliuliza Roma na kumfanya Dokta amwangalie kidogo kwa mshangao kwani swali la Roma lilionekana kuwa la kipumbavu.
“Kama kungekuwa na uwezekano huo, basi ninaweza kuandaa upasuaji wa haraka sana na matumaini ya hali ya afya yake kurudi kama zamani yanaweza kupanda kutoka asilimia sifuri mpaka sabini na tano”Aliongea lakini hata hivyo maneno hayo hayakuwa na nafuu kwa Neema kwani uwezekano huo wa kimiujiza haukuwepo.
“Nipelekeni nikaonane na mgonjwa”Aliongea Roma na kumfanya hata Neema aliekuwa akitoa machozi kushangaa.
“Roma hakuna jinsi ya kumsaidia ninapaswa kuukubali ukweli nitahakikisha waliohusika wanakamatwa na vyombo vya dola na kufia Gerezani”aliongea Neema.
“Mzee Chino anaonekana kuwa wa muhimu sana kwako Neema na mimi siwezi kukuangalia ukilia na kukosa furaha kwa ajili yake , nitafanya ambalo lipo kwenye uwezo wangu kuhakikisha anapona ,Dokta tusipoteze muda nataka kuonana na mgonjwa sasa hivi”Aliongea Roma na kumfanya Dokta Shukuru kushangaa ,kwani alishindwa kuelewa Roma anataka kufanya nini.
“Dokta muonyeshe Roma mgonjwa ,ni mpenzi wangu hivyo hakuna shida kama atamuona”Aliongea Neema tena awamu hii akimtambulisha Roma kama mpenzi, jambo ambalo lilimfanya Dokta Shukuru kushangaa mno , hakuamini kijana mdogo kama huyo anatoka kimapenzi na mwanamke mwenye heshima ndani ya taifa hili mwanbamke Tajiri na mwanasisiasa Neema Luwazo lakini kubwa Zaidi ni namna wawili hao walivyotofautiana umri ,hata kwa wale mabwana wawili waliokuwa pembeni walijikuta wakishangaa mno.
Ukumbuke maongezi haya yalikuwa yakifanyikia ndani ya ofisi ya Dokta Shukuru na watu wote waliomsindikiza Neema walikuwa kwenye chumba hiko , na hivyo neno mpenzi lilisikika kwa kila mtu, Roma mwenyewe baada ya neema kumtambulisha kama mpenzi licha ya tofauti kubwa kati yao , alijikuta kipande cha mahaba kwa Neema kikiongezeka , hio ilikuwa na maana kubwa kwamba Neema alishamkubali moja kwa moja kama mwanamke wake na yupo tayari kuuwaambia ulimwengu anatoka nae kimapenzi.
Dokta Shukuru kwasababu alikuwa na heshima kubwa kwa Mheshimiwa Waziri , basi aliona afanye kama alichoomba Roma na alinyanyuka na kuwaambai wamfate nyuma mpaka ICU.
Muda ambao Roma anatoka na Neema , madaktari wengine walikuwa wakitoka kwenye chumba ambacho Mzee Chino alikuwa akifanyiwa matibabu.
Itifaki za kuona mgonjwa ndani ya chumba cha ICU zilifuatwa na Roma pamoja na Neema waliweza kuingia sehemu ambayo Mzee Chino alikuwa akifanyiwa matibau kilikuwa ni chumba ambacho kimezungukwa na mashine nyingi za kufanyia upasuaiji wa dharula , hakukuwa na mwanga mwingi Zaidi ya taa kubwa zilizofungwa hapo ndani.
Neema baada ya kuona hali ya Mzee Chino , Chozi lilimtoka kwa kuona huruma kwa hali aliokuwa nayo , kwani alikuwa amelazwa kifudifudi , huku majeraha ya Risasi yakiwa yameelekezewa juu.
“Naomba mniache mwenyewe na mgonjwa ,Neema utanisubiri nje baada ya nusu saa nitatoka”
“Mr Roma nimeweza kukuruhusu kumuona mgonjwa , lakini siwezi kukuacha ukabaki nae kwani sio utararibu na unaweza fanya jambo baya Zaidi likahatarisha afya yake Zaidi”Aliongea Dokta Shukuru na Roma alimwangalia Neema kama kumpa ishara na Neema baada ya kuangaliwa kwa namna hio na Roma, akili zake haraka haraka zilisafiri siku ya kwenye kusanyiko, namna ambavyo Roma alipigwa risasi mgongoni , lakini licha ya hivyo kuonekana hana tatizo lolote.
“Dokta mimi kama ‘Guardian’ wa mgonjwa wangu ninaomba umpatie Roma ruhusa ya kubaki na mgonjwa kwa muda wa nusu saa”Aliongea Neema Luwazo huku akionyesha kuwa siriasi kwa maneno ambayo ameongea.
Dokta Shukuru kwakuwa ndio aliekuwa ameongoza kumhudumia Mzee chino basi hakuwa na haja ya kukataa ombo la Mheshimiwa Waziri, licha ya kwamba alikuwa akikiuka taratibu za hospitali.
“Roma sijui unataka kufanya nini , ila nakuombea unachotaka kufanya kifanikiwe”Aliongea Neema na kisha akaungana na Dokra Shukuru na wote kwa pamoja walitoka wakimuacha Roma akibaki na mgonjwa.
Roma baada ya kubaki mwenyewe alianza kuchunguza chumba chote na kuangalia Camera zilizofungwa kwenye chumba hiko na hakupata tabu ya kuzitafuta kwani alitumia uwezo wake wa kihisia na kuzipata zote na alijikuta akitabasamu mara baada ya kugundua kuna Camera Zaidi ya zile ambazo zinaonekana.
Upande mwingine katika ndani ya hospitali hii katika chumba cha kuongezea Camera ,anaonekana Yan Buwen akiwa peke yake akiangalia Skrini ambazo zilikuwa zikionyesha moja kwa moja chumba ambacho alilazwa Mzee Chino.
Haikueleweka waongozaji Camera wengine wako wapi , lakini ni Dhahiri kwamba alitaka kuona kila kinachofanywa na Roma yeye peke yake , pasipo mtu mwingine kushuhudia.
Sasa alikuwa ndani ya chumba hiko kwa takribani lisaa limoja , tokea muda ambao Roma anapita anaongea na Dokta Shukuru , lakini pia Roma alivyoingia kwenye chumba cha IC?U alicholazwa Mzee Chino, Yan Biuwen alikuwa akiona kila kitu.
Ukweli Yan Buwen ndio ambaye aliagiza watu kumjeruh Mzee Chino , huku akiamini kwamba kama Mzee Chino atakuwa kwenye hatihati ya kufa na Roma akapewa taarifa hizo basi ni lazima angechukua hatua ya kumponya kwa kutumia damu yake , huo ndio mpango wa Yan Buwen , kutumia ukaribu wa Neema Luwazo na Roma ili kumponya Mzee Chino na baada ya hapo ndio damu ya Roma ipatikane ili akaweze kufanya Cloning na kutumia jiwe la Kimungu.
Sasa baada ya kuona Roma kaachwa kwenye chumba cha matibabu alijikuta akitabasamu mno,na kujiona kama mshindi na alijiambia mafanikio yake ndio yanakaribia..
“F****ck! Ameziharibu Camera”Aliongea Yan Buwen mara baada ya Skrini zote kuwa giza na kuonyesha chenga chenga.
Yan Buwen mara baada ya kuona Camera zimezima alivuta tarakishi iliokuwa pembeni na kisha baada ya kuifungua aliandika mistari kadhaa ya kodi kwenye tarakishi hio na baada ya dakika mbili tu , Mawasiliano ya Camera yalirudi na Roma alionekana ndani ya chumba alicholazwa mzee chino na Yan Buwen kutabasamu huku akijipiga piga kifuani kwa kujiona yeye ndio jiniasi.
“Hades unajifanya mjanja sana , ndio maana nime install undetected Camera”aliongea mwenyewe huku akikaza macho yake kwenye tarakishi yake.
Roma alionekana kuchukua bomba la Sindano ambalo halikuwa limetumika na kisha akachukua na Sindano na kuunganisha na lile bomba , baada ya kumaliza kitendo hiko alikunja shati lake la mikono mirefu mpaka kwenye kiwiko cha mkono na baada ya kumaliza alitafuta mshipa wa damu kwenye mkono wake na ndani ya dakika alionekana kuupata na kwa kutumia mkono wake wa kushoto aliweza kujidunga ile sindano huku akiwa amekuja ngumi na alivyoachia tu alianza kuvuta na bomba lile lilionekana damu ikiwa inajaa.
Kitendo kile kilimfurahisha mno Yan Buwen kiasi cha kurusha mikono juu kwa furaha , hakuamini jambo lake linakwenda kuwa rahisi hivyo , kwani kitendo cha Roma kutoa damu yake kwenye mwili ndio alichotaka.
Roma alifanya kitendo kile cha kujitoa damu na kisha damu yake kuingiza kwenye Dripu ya damu ambayo alikuwa ametundikiwa Mzee Chino , alifanya kwa Zaidi ya mara tatu mpaka alipoweka bomba na sindano chini,.
Baada ya kumaliza alimsogelea tena mzee Chino na akamshika kwenye mbavu zake huku akiwa amefumba macho , na alianza kuongea maneno ambayo hayakueleweka yalikuwa yakimaanisha nini , lakini ni kama vile mchungaji anavyomwombea mtu.
Kadri alivyokuwa akifanya vile , kupauka kwa Mzee Chino kulianza kupotea na sasa alikuwa akionekana kama mtu ambaye yupo usingizini , Roma baada ya kukamilisha zoezi lile alitoa bendeji zote zilizofungwa mgongoni na hapo ndipo alipoachia tabasamu baada ya kuona majeraha yake yalikuwa yakivutana kwa kasi mno , yaani nyama za mwili za Mzee Chino ni kama zilikuwa zikicheza cheza kwa kuvutana..
Neema Luwazo aliekuwa nje , alionekana kuwa na wasiwasi kweli licha ya kwamba alikuwa akiamini huenda Roma akaweza kufanya maajabu kwa Mzee Chino , lakini hata hivyo aliogopa jambo hilo kutokufanikiwa na ndio maana alikuwa akikaa na kunyanyuka.
Baada ya lisaa limoja mbele hatimae mlango wa chumba cha ICU ulifunguliwa na kufanya watu wote waliokuwa wakimsubiri nje kusimama, akiwemo Neema Luwazo, wakitaka kujua hali aliokuwa nayo Mzee Chino.
SEHEMU YA 314.
HONGKONG
Ni moja ya mgahawa mkubwa na maarufu sana ndani yajiji la HongKong ,mgahawa unaofahamikakwajina la Ling Sichuan King anaonekana mrembo Clark akiwa kwenye meza moja na mwanaume kwenye Kona ndani ya mgahawa huo, mwanaume huyo akiwa ni mzungu, mwanaume huyu hakuwa mwingine bali alikuwa ni Edward kutoka ukoo wa Rothchild.
Huyu Edward ni yule aliekuwa akiambata na Malkia Catherine na tulimuona kule Ufaransa wakati akimleta Catherine katika chumba cha Roma kwa ajili ya ‘kunyanduliwa’.
Clark na Edward walionekana kuwa katika mazungumzo , huku wakijipatia nyama ya kopo , huku pembeni wakiwa na vinjwaji vya moto.
“Hades alikuwa na shida gani?”Aliuliza Edward huku akimwangalia mrembo Clark alievalia koti la manyoya aina ya leather , jaketi ambalo limtengenezwa na kampuni moja maarufu kutoka Italy.
“He is fine Edward , alikuwa na tatizo na lishaisha”Aliongea Clark .
“Nimesikia alikuwa Hokkaido kwa ajili ya mwanamke?”Aliongea Edward huku akimwangalia Clark usoni na Clark alitingisha kichwa kukubaliana nae.
“That isn’t good sign for you Clark”Aliongea Edward akimwambia Clark kwamba hio sio ishara njema kwake.
“That is none of your business I have said this before, I will decide myself on how I am getting along with Roma”
“Hio sio biashara yako , nishasema nitaamua mwenyewwe namna ambavyo nitakuwa naelewana na Roma”Aliongea Clark.
Unachotakiwa kuelewa hapa ni kwamba , alichokuwa akimaanisha Edward ni kwamba kitendo cha Roma kuongeza mwanamke mwingine ilihali kwa upande wa Clark hakuna maendeleo yoyote ndio alichokuwa akizungumzia na ndio maana akamwambia sio ishara njema kwa Roma kuongeza mwanamke mwingine ilihali kwake yeye kaachwa.
“Clark tatizo hujawahi hata kuongea nae juu ya hili swala , unafikiri ni kwa namna gani mahusiano yako na yeye yataimarika , kwa staili hio hauwezi kuuteka moyo wake na itafikia kipindi ushachelewa tayari hata kama ukichukua hatua”
“Hata kama mimi ndio daktari wake Edward na hatoweza kuniacha”Alijitetea Clark.
“Unafikiri ugonjwa wake usiporudi ataendelea kuwa na wewe, Clark unatakiwa kuelewa kwamba viongozi wa ukoo macho yao yote yapo upande wako kumteka Roma kihisia ili kuwa upande wetu”
“Edward katika ukoo nimechangia kwa kiasi kikubwa , kwanini natakiwa kuendelea kuishi kwa kutimiza malengo ya familia siku zote sio ya kwangu?”
“Clark unatakiwa kuelewa kwamba kwenye ukoo wetu wa Rothichild kuna Zaidi ya ndoa therathini mpaka sasa lakini licha ya hivyo damu yetu ya kifalme katika ukoo inazidi kupungua kutokana na miingiliano na makabila mengine ,tunachotaka sasa ni damu mpya katka ukoo wetu ambayo inachimbuko la kifalme moja kwa moja na macho yetu yapo kwa Hades na wewe ndio mwanamke pekee mrembo kwenye ukoo wetu ambaye unanafasi kubwa sana, urafiki wetu na Hades hautoshi bali akiwa mmoja kati yetu itakuwa rahisi Zaidi na hata makabila mengine hayatakuwa na nia ya kumsogelea na tutaendelea kuwa kabila kubwa ndani ya ulimwengu huu”Aliongea Edward kwa msisitizo.
“Edward najua wewe na Roma ni marafiki wa mudamrefu, je umekuwa na urafiki na yeye ili tu kupata faida kutoka kwake?”Aliuliza Clark.
“Ofcourse not , but other than being his friend , I am also a proud member of Rothchild clan, as well as a brother who hopes for his sister to be happy , Clark Stop being so cowardly ,this doesn’t look like you , you should confess to him since you love him, Even if he has Persephone as his wife and has other lovers at the same time ,it doesn’t mean you cant also be his love”
“Hapana , lakini licha ya kuwa rafiki yake , lakini pia mimi ni mwanaukoo wakujivunia wa Rothchild , lakini pia mimi ni kaka ambaye nataka dada yangu kuwa na furaha , Clark acha kuwa muoga , unaonekana kama sio wewe , unatakiwa kufunguka na kumueleza hisia zako kwasababu unampenda , hata kama anae Persephone kama mke wake lakini pia kuwa na wanawake wengine hii haimaanishi kwamba huna nafasi ya kuwa mpenzi wake pia”
“Edward nimechoka ninaondoka”Aliongea Clark huku akiinua mkoba wake na kuanza kupiga hatua kutoka nje ya mgahawa huo , lakini ile anakaribia kutoka alijikuta akigongana na mtu.
“Ooh!! Sorry”Aliongea mwanaume na kumuokotea mkoba wake Clark , sasa kitendo kile Edward alikiona na mtu aliekuwa mbele yake alikuwa akimfahamu sana kama moja ya mpishi namba moja duniani ambaye anamiliki pia mgahawa ambao walikuwa wakifanyia maongezi pamoja na migahawa mingine ndani ya China ,HongKong na Japani.
Mwaaume mwenyewe hakuwa mwingine bali alikuwa ni Poseidon , ambaye tulimuona kipindi kwenye siku ya kusanyiko la wafanyabiashara , mwanaume ambaye alimkamata Afshar Bahman.
“It`s okey”Aliongea Clark na kisha alichukua mkoba wake na kuanza kupiga hatua kutoka ndani ya eneo hilo pasipo kugeuka nyuma na Poseidon mara baada ya Clark kuondoka aliishia kumwangalia mpaka alipotokomea ndipo alipogeuza macho yake na kumwangalia Edward.
“Shemeji Edward kutoka Rothchild Family ni heshima kwangu umefanya mgahawa huu kama sehemu salama kutembelea hapa HongKong”Aliongea Poseidon mara baada ya kusogelea meza ya Edward.
“Mr Kelphin haina haja ya kuwa ‘humble’ kila mtu anatamani kuingia kwenye mgahawa wako ,na kwasisi ambao tunapesa siku zote tunajua hii ndio sehemu salama”Aliongea Edward na Poseidon ambaye sasa anafahamika kwa jina la Kelphin alitabasamu huku akiangalia nje.
“Niliona ulifanya makusudi kumgonga dada yangu”Aliongea Edward huku akitabasamu.
“Edward niseme tu nimetokea kuvutiwa sana na dada yako na ndio maana nilitanguliza neno Shemeji katika salamu yetu”Aliongea kwa Kingereza na kumfanya Edward kucheka.
“Macho yako yanaonyesha ,lakini nasikitika kukuambia kwamba moyo wake upo kwa mtu mwingine kabisa”Aliongea Edward.
“Unamaanisha moyo wake upo kwa yule mtanzania mpuuzi Hades?”Aliongea na Edward alitingisha mabega na Kelphin alitabasamu kwa kejeli.
“Koo zote za dunia hii mmekuwa mkitaka kuwa na ushirikiano na Hades kuliko sisi wengine ni kwanini?”
“Majibu yote yanajieleza Mr Kelphin ,ijapokuwa asilia yenu sio hapa duniani, lakini mkumbuke uwezo wenu ni mdogo pia , licha ya kwamba mmekuwa na uwezo mkubwa likija swala la kupambana lakini mchango wenu kwenye maendeleo ya dunia ni mdogo sana”Aliongea Edward
“Binadamu mnadharau sana lakini huyu Hades ambaye mnamuona wa maana nitamuua muda si mrefu”
“Ukifanikisha hilo siku moja, then dada yangu atakuwa ni wa kwako”Aliongea Edward huku akitabasamu na akanyanyuka baada ya kupiga mkupuo mmoja wa kinywaji chake na kumuacha Kelphin akiwa amekunja ngumi.
“Hades labda usikanyage maeneo ya China , ukijichanganya siku hio nitakuonyesha sitojali tena the Stupid “ Gods Treaty’ lazima nikuonyeshe kwamba wewe ni binadamu na sisi ndio miungu”Aliwaza Poseidon huku akinyanyuka haraka haraka baada ya kumuona mzee flani wa kichina alietangulizana na mabodigadi akiingia hapo ndani na Kelphin alimsogelea yule mzee na kuanza kumkaribisha kwa kumuinamia kwa heshima kubwa.
Kwa maigizo aliokuwa akiyafanya Poseidon usingejua miaka Zaidi ya Elfu moja iliopita alikuwa akiabudiwa mpaka pale alipokuja Christ Pamoja na mtumbe Muhamad.
******
Ulikuwa mshangao mkubwa sana kwa madaktari wote waliokuwa wakimtibia Mzee Chino , na sio kwao tu hata kwa Neema Luwazo mwenywe alijikuta akishangazwa na jambo hilo ,licha ya kwamba hakujua Roma amefanyaje , lakini afya ya Mzee Chino iliimarikika kwa kiasi kikubwa sana kiasi kwamba hata zile oksijeni ambazo zilikuwa zimewekwa kwenye pua zake kuondolewa.
“This is more than Miracle”Aliongea Dokta Shukuru Omary kwa mshangao mkubwa huku akiamini kilichotendeka sio kwa uwezo wa kisayansi bali ni kwa uweza wa kimungu Zaidi na aliamini huenda Roma alikuwa nabii , kwani amekuwa ni moja ya watu ambao washawahi kusikia Habari za miujiza , ila kwa kuwa alikuwa ni mwanasayansi hakuwahi kabisa kuamini , lakini kwa tukio ambalo limefanyika ,kwake aliona ni ile miujiza ambayo siku zote alikuwa akiidharau.
Neema Luwazo baada ya kushuhudia afya ya Mzee Chino kutengemeaa kwakiasi kikubwa alijikuta akitoka haraka haraka ndani ya chumba hiko ili kumuwahi Roma aliemuacha nje kwa ajili ya kumpa shukrani , lakini ile anafika hakuweza kumuona tena na ilibidi awasogelee vijana wawili waliokuwa eneo la kusubiria.
“Allly Roma kaelekea wapi?”Aliongea Neema Luwazo mwanamama huyu ambaye licha ya kwamba alikuwa akionekana kuwa mtu mzima lakini hakuacha kuvutia kwa kila anaemtazama.
“Amesema anaondoka anamuwahi mke wake”Aliongea Ally na kumfanya Neema Luwazo kupumua mara baadaya kusikia Roma kaondoka na alijiambia atampigia simu kwa ajili ya kumshukuru , licha ya kwmaba alikosa namna nzuri kwenye kichwa chake ambayo aliamini inaweza kuielezea na kwa jinsi gani amegusw ana msaada ambao Roma kafanya kwa ajili yake.
“He is right person for me ,Roma I will always love you”Alifikiria Neema Luwazo mpaka pale aliposhituliwa na madakrari waliokuwa nyuma yake.
“Mheshimiwa kwa hali ya mgonjwa ilivyotengemaa naweza kusema kwamba tunayo kila sababu ya kuandaa upasauaji ili kuitoa risasi iliopo kwenye uti wake wa mgongo”Aliongea Dokta Shukuru.
“Atakuwa na asilimia ngapi za kupona baada ya upasuaji huo?”Aliuliza Neema na Dokta shukuru akatabasamu.
“Shukrani ziende kwa mpenzi wako , nimeshangazwa sana na kilichotokea na mpaka hapa naweza kusema kwamba mafanikio yatakuwa ni Zaidi ya asilimia themanini”Aliongea kwa furaha na Neema Luwazo alitingishwa kichwa kukubaliana na madaktari.
Upande mwingine ndani ya chumba ambacho amelazwa Mzee Chino alionekana daktari mmoja wakihindi akimtoa damu mzee Chino na kuihifadhi kwenye kijichupa , alionekana kufanya haraka haraka mno , baada ya kutoa damu kwemye mkono, aligeukia Drip ambayo ilikuwa na kiasi kidogo cha damu iliokuwa ikiingia kwenye mwili wa mgonjwa na alitumia sindano na kuifyonza yote na akaihifadhi kwenye kijichupa kingine na baada ya zoezi lake kukamilika alichukua vile vijichupa viwili vyenye damu na kuweka kwenye koti lake na kutoka.
Dokta huyu hakushitukiwa kutokana na kwamba alikuwa ni moja ya madaktari ambao walikuwa wakimfanyia matibabu mzee Chino , hivyo wakati wenzake wanatoka yeye aliachwa ndani.
Dakika kama tano mbele wakati Neema Luwazo akiwa ndani ya ofisi ya Dokta Shukuru , upande wa maegeshoni dokta yule mhindi alisogelea gari moja aina ya V8 na kuingia ndani upande wa dereva na hapo ndio anaonekana Yan Buwen alieketi kwenye gari hilo akiwa hana wasiwasi kabisa.
“Hii hapa Mr Yan Buwen”Aliongea yule daktari na Yan Buwen alitabasamu na kupokea vile vijichupa.
“Kazi nzuri Dokta Jamshid, Mstaafu ataingiza kiasi cha pesa kama mlivyokubaliana”Aliongea Yan Buwen na Jamshid alitingisha kichwa na kisha akatoka kwenye gari hilo.
Yan Buwen baada ya kuangalia damu ile kwenye vile vijichupa alijikuta akiachia tabasamu flani hivi la kukera na kisha akawasha gari kwa mbwembwe kama zote.
“Kazi yangu hapa Tanzania imeanza , mrembo wangu The Doni muda si mrefu utanikubali kwa kitu ambacho ninakwenda kutengeneza “Aliwaza yan Buwen kwenye kichwa chake na dakika mbili mbele alitoa gari lake kabisa na kuingia barabarani.
SEHEMU YA 315.
Siku hio hio ya ijumaa ndani ya ofisi ya mrembo Edna , alionekana Amiri akiwa katika maongezi na Boss wake na maongezi hayo yalionyesha kuwa muhimu Zaidi kwani kuna muda Amiri alikuwa akimpatia baadhi ya karatasi na Edna alizisoma na ambapo hajaelewa ,Amiri alikuwa akipatolea maelezo.
Kitu ambacho Amiri alikuwa akimwabia Edna ilikuwa ni swala juu ya mkataba wa kibiashara uliovunjwa na serikali ya Jamhuri pamoja na kampuni yake juu ya ujenzi wa jengo la Bima ya Taifa miaka kadhaa nyuma.
Katika maelezo ambayo yalitokana na uchunguzi uliofanywa na Amiri akishirikiana na kikundi chake cha Athena , alibaini kwamba Innova haikuwa kampuni ya ujenzi wa magorofa , hivyo ni kama haikustahili kupewa tenda ya kumalizia jengo la Bima mara baada ya serikali kuvunja mkataba.
Amiri aliweza kumuonyesha Edna baadhi ya kazi ambazo zilikuwa zikihusiana na kampuni ya Innova na kwa maelezo hayo ilionyesha Dhahiri kabisa kwamba kampuni ya Innova haikuwa na uhusikaji wowote na ujenzi wa majengo.
“Kama hii kampuni inajihusisha Zaidi katika maswala ya utafiti wa kisayansi waliwezaje kupata tenda kutoka serikalini?”Aliuliza Edna
“Boss kilichofanyika kwa Innova ilikuwa ni kufungua kampuni ya kwenye makaratasi(Shell Company) , kampuni ambayo imesajiliwa kama ya ujenzi ambayo ipo chini ya uongozi wa taasisi ya Innova na hio kampuni ndio iliosaini mkataba wa umaliziaji wa jengo la Bima ya Taifa, lakini jambo la kufurahisha ni kwamba nina ‘data’ nyingine ambazo tulizichambua na kugundua huenda kuna Zaidi ya ujenzi uliokuwa ukikusudiwa kufanyika ndani ya jengo la Bima ya Taifa na ndio maana serikali ikavunja mkataba”
“Sababu zipi?”Aliuliza Edna na . Amiri alitoa karatasi na kumpatia Edna.
“Hayo ndio makubaliano ambayo Boss Raheli aliingia na serikali baada ya mkataba wa ujenzi na Vexto Construction kuvunjwa na hii ya pili ni karatasi ya pesa iliolipwa kwa ajili ya kuvunja mkataba”Aliongea Amiri na kumpatia karatasi za aina mbili Edna na akaanza kuzisoma na alijikuta akitoa macho.
“Why the government were this desparate?”Aliuliza Edna kwani serikali ililipa fidia kubwa mno kwa ajili tu ya kuvunja mkataba.
“Boss hilo ndio swali ambalo na sisi tulijiuliza kwanini walikuwa wakitaka kuvunja mkataba kwa namna yoyote ile , jambo la pili mkataba huu haukuvunjwa na Wizara bali ni mheshimiwa raisi mwenyewe ndio aliehusika, kwa maneno marahhisi maamuzi yote yalifanyikia ikulu na hata Boss Raheli alisaini ‘Breach of Contract’ na serikali akiwa Ikulu”Aliongea Amiri na Edna alikagua sahihi na kweli ilikuwa ni sahihi ilioasaniwa na Mheshimiwa Mstaafu Kigombola.
“Boss angalia pia na hii taarifa”Aliongea Amiri na kisha akampatia Edna karatasi nyingine na Edna alianza kuisoma kwa umakini , ilikuwa ni kaatasi iliokuwa ikionyesha pia kwamba licha ya kampuni ya Innova kuwa taasisi ya maswala ya kiutafiti lakini pia ilikuwa ikihusika na ujenzi wa ‘Laboratory facilities’ , na karatasi hio ilikuwa ni maelezo ya kina namna ambavyo Innova iliweza kuingia mkataba na kujenga maabara ya kiututafiti nchini Canada , maabara ambayo inamilikiwa na kampuni ya Maya.
Edna licha ya maelezo hayo aliona bado swala ambalo anataka kulifikia lilikuwa mbali, alikuwa akitaka kusikia ni kisasi gani ambacho mama yake alikuwa nacho mpaka kumwachia Flash ambayo ilikuwa na orodha ya makampuni mengi ndani ya Tanzania huku moja ya kampuni kubwa ikiwa ni Maya Group.
“Boss hitimisho ambalo tumeweza kufikia moja kwa moja ni kwamba katika kampuni ya Innova ilifanya ujenzi wa maabara ndani ya jengo la Bima ya Taifa na baada ya ukamilishaji wa ujenzi huo ndio wakaingia mkataba na Maya constructor kumalizia ujenzi wa jengo upande wa juu hivyo ninaamini sababu ya kampuni ya Vexto kutolewa kwenye mkataba wa ujenzi na serikali huenda ni kwa ajili ya kulinda siri ya maabara hio”Aliongea Amiri na Edna alifikiria kidogo.
“Amiri vipi kuhusu taarifa ya Dokta Hubery juu ya kifo chake?”aliuliza Edna na Amiri alinyamaza kidogo na kuonyesha sura ya huzuni kidoo.
“Tumejaribu kufatilia ndani ya familia yake na tumeweza kupata kugundua ni kweli alikuwa na ugonjwa wa moyo wa kuzaliwa nao?”Aliongea Amiri na Edna alikubali kwa kichwa.
“Amiri nashukuru kwa kazi kubwa mnayoifanya, kwasababu kazi ambayo niliwapa ni kujua kwanini kampuni yetu ilitolewa katika mkataba wa ujenzi wa jengo la Bima imekuwa na majibu ya kuridhisha, sidhani kama kuna faida ya kuendelea kuchimba Zaidi , kwani naamini jambo hili linaweza kuleta matokeo hasi kwa kampuni”Aliongea Edna na Amiri alielewa boss wake anachoongea.
Dakika kadhaa baada ya kupita baada ya Amiri kutokandani ya ofisi yake , Edna alimpigia simu Monica kumuita Benadetha ofisini kwake na ndani ya dakika tano tu , Benadetha alionekana akiingia ndani ya ofisi ya Edna.
“Boss nimeitikia wito”Aliongea Benadetha na Edna pasipo ya kubadili muonekano wake alivuta bahasha kwenye mtoto wa meza na kisha akamnyooshea Benadetha na vile anataka kuichukua Edna alirudisha mkono nyuma.
“Benadetha nakupatia hii Document uihifadhi kama mkuu wa idara ya Public Relation, ni nyaraka muhimu sana kwa kampuni ,imejaa mipango yote ya kampuni ya miaka mitano ijayo, nyaraka hii ikifika mikononi mwa makampuni ambayo ni washindani wetu wa kibiashara jua kwamba kampuni itaingia matatizoni”Aliongea Edna na kisha akamnyooshea Benadetha ili aichukue na mwanadada huyo kwa kutetemeka aliipokea , hakuelewa kwanini Boss wake alikuwa akimwamini na nyaraka muhimu namna hio.
“Nitaihifadhi vizuri boss”
“Okey unaweza Kwenda ni hayo tu niliokuitia”Aliongea Edna na Benadetha aliitikia kwa heshima na kisha kutoka.
“Benadetha…!!!”Benadetha ambaye alikuwa akiikaribia Lift alijikuta akigeuza macho nyuma mara baada ya kusikia jina lake linaitwa , aliemuita alikuwa ni Ernest Komwe CEO msaidizi wa kampuni ya Vexto.
“Naam!!”Aliitikia Benadetha kwa upole na Ernest Komwe alitabasamu , huku akimsogelea.
“Nimekuona unazikaribia lift ndio maana nikakuita tushuke wote , mimi naelekea Chini”Aliongea Ernest Komwe kwa bashasha huku akitabasamu na Benadetha na yeye alitabasamu na wote kwa Pamoja waliingia kwenye Lift macho ya Ernest Komwe muda wote yalikuwa kwenye nyaraka alioshikilia Benadetha.
“Benadetha kesho wikiend utakuwa na ratiba gani?”
“Mh! Mara nyingi wikiend naenda Beach kupunga upepo”Aliongea Benadetha.
“Na boyfriend wako?”
“Haha… sijui nisemeje ila naendaga mwenyewe”Aliongea Benadetha na Ernest Komwe alitabasamu.
“Kesho unaonaje nikikusindikiza nina siku nyingi sijaenda baharini , tukiwa wote itakuwa vizui Zaidi , isitoshe sio mwenyeji sana wa Tanzania”Aliongea Ernest na Benadetha alikubali kwa kichwa.
Dakika chache mbele Ernest alionekana akiongea na simu eneo la mapumziko chini kabisa ya jengo hili la kampuni.
“Boss nafikiri nishapata namna ya kuyumbisha hisa za kampuni, kuna Audio nimekutumia kupitia mtandao wa Watsapp”Aliongea .
“Ngoja niisikilize”Sauti upande wa pili ya mwanamke ilisikika na palepale simu ilikatwa na Ernest alitabasamu huku akinywa kidogo soda ya Pepsi ilio kwenye kopo na kabla hata hajamaliza soda yake simu iliita na alipokea mara baada ya kuona jina ni Boss.
“Hilo faili linaonekana kuwa muhimu pia kwa kampuni , licha ya kwamba ninachotaka ni Zaidi ya hiko”
“Boss napaswa kufanya nini?”
“Hilo sio swali , hakikisha unaipata hio nyaraka na mtafute Matilda na atajua cha kufanya”Aliongea mwanamke aliekua kwenye simu na Eresti Komwe aliitikia na kisha simu ilikatwa,
******
“Wife jumapili Mzee Kweka anataka tukamtembelee, unaonaje ukinisindikiza wewe na Lanlan”Aliongea Roma muda wa usiku baada ya kumkuta Edna akiwa amekaa kwenye masofa akiangalia taarifa ya Habari ITV.
“Sawa!!”Alijibu Edna pasipo hata ya kufikiria na Roma alitabasamu na kumsogelea.
“Halafu babe unapaswa umsikilize mdogo wako jinsi anavyo imba , Sophia ana kipaji kikubwa sana na namtabiria kuwa mwimbaji mkubwa”Aliongea Roma huku akikaa karibu na Edna na kupitisha mkono kwenye kiuno chake na kumfanya Edna aangalie mkono wa Roma jinsi ulivyotokeza upande wa pili.
“Mhmh sijamsikiliza , ila mama yake alishaniambia kama anakipaji cha kuimba na aliniomba nimsapoti”Aliongea Edna huku akijikausha akiacha mkono wa Roma uliokuwa ukimtekenya , lakini wakati huo huo akiomba mama yake na Roma asijitokeze hapo sebuleni kwani kitendo anachofanya Roma ni cha aibu..
Sasa Roma baada ya kusikia Edna akimtaja mama yake Sophia ni kama alikumbuka kitu , alikumbuka siku aliomdanganya Edna kama Sophia alikuwa mdogo wake waliotoka nae Marekani , lakini pia alikumbuka siku ambao Sophia alimwambai kwamba Edna alikuwa anajua wamemdaganya na Roma hakuwahi kuzungumza swala hilo na mke wake na pia hakuwahi kumuuliza Sophia waliyamaliza vipi na dada yake.
“Halafu mke wangu kwanini uliamua kujikausha mara baada ya kujua siku ile nilikudanganya?”Aliongea Roma na Edna alishika mkono wa Roma uliomshika kiuno na kuutoa na kisha akaegamia vizuri sofa.
“Kwaho ulitaka nije nianze kukulalamikia kwanini wewe na Sophia mlinidanganya , kwanza kwa taarifa yako nikueleze tu mama yake na Sophia alishaniambia kila kitu mlichopanga na balozi ila niliamua kukaa kimya”Aliongea Edna na kumfanya Roima kushangaa.
“Kakuambia nini Balozi?”
“Sophia alikuja kuishi na sisi kwasababu gani kuwa mkwel?”Aliuliza Edna, sasa wasichokujua ni kwamba Sophia pia alikuwa amesimama nyuma yao.
“Balozi alitaka nimfanye Sophia mke wangu wa pili , ila sikukubaliana nae ndio akaniomba niishi na Sophia kwa muda”Aliongea Roma bila kumungunya maneno.
“Sister Edna…!!!”Aliiita Sophia na kukimbia kupiga magoti mbele ya Edna na Roma na kumfanya Edna kushangaa kwani Sophia pia alianza kulia kwa kwikwi
ITAENDELEA SIKU YA JUMANNE.
wATSAPP CONTANCT:0687151346