Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Safi sana nipo na nishaagiza katoni ya popcorn kwa ajili ya kesho.
 
SEASON 2
SEHEMU YA 31

Ilikuwa ni Jumapili tulivu , kwa wale wakristo waliokuwa wakienda kanisani walikuwa wakienda na kwa wale ambao walikuwa ni wa dini nyingine walikuwa na pilipilika za mambo mengine za Maisha yao.

Roma kama kawaida yake aliamka asubuhi asubuhi na kwenda kufanya mazoezi ya hapa na pale ili kuweka mwili wake katika hali nzuri , kwa upande wa Bi wema alikuwa bize na kuandaa kifungua kinywa kwa siku hio na kwa upande wa Edna alikuwa bize na kusoma kama ilivyokuwa kawaida yake , aliamini matatizo yake yote yanaweza kutatuliwa na kusoma na ndio maana aliamini katika kusoma sana.

Alijitahidi kusoma kwa muda , lakini akili yake haikuwa ni yenye kutulia , alionekana kuna jambo lilikuwa likimuumiza kichwa kwani alikosa utulivu , baada ya kuona haelewi kile alichokuwa anakisoma alisogelea tarakishi yake ya mapakato na kuingia kwenye mtandao maarifu wa Google na kuanza kutafuta taarifa zinazohusiana na macho ya mtu kubadilika Rangi , lakini kila majibu yaliokuwa yamekuja yalionekana kutokumridhisha kabisa na kukosa jibu alilokuwa analitaka.

“Au nimuulize mimi mwenywe kwanini macho yake yanabadilika Rangi?” Aliwaza mrembo huyu huku akiwa amevalia kigauni chake kilichoufanya mwili wake mnene kiasi kupendeza.

“Ila naamini siku moja ataniambia mwenyewe kwanini yuko vile , sitakiwi kumuuliza”Alijijibu mwanamke huyu huku akiona hayupo kwenye nafasi ya kumuuliza mume wake Roma kwanini macho yake yanabadilika rangi anapokuwa na hasira kali.

Saa mbili kamili za asubuhi Edna alishuka chini kwa ajili ya kupata kifungua kinywa baada ya kuitwa na Bi Wema , Roma alikuwa tayari yupo mezani , na alikuwa anamsubiria mke wake waanze , baada ya Edna kuketi wanafamilia hawa watatu ndani ya jumba hili kubwa la kifahari walianza kupata kifungua kinywa chao ambacho kwa familia za Maisha ya chini wangedhania moja kwa moja aina hio ya chukula ni kwa ajili ya sherehe.

“Miss unaonaje ukienda na Mr Roma leo kituoni?”Aliongea Bi Wema na kupendekeza .

“Bi Wema kituo gani?”Aliuliza Roma

“Kuna kituo cha kulelea yatima kipo Mkoa wa pwani Bagamoyo Kiwangwa, Ni kituo ambacho kampuni inakifadhili na imekuwa utamaduni kila jumapili Miss Edna kwenda huko kuwatembelea Watoto hao na kuwapelekea baadhi ya mahitaji muhimu”Roma alishangaa.

Edna alimwangalia Roma , hakuwa akipinga swala hilo la kwenda nae , kwanza kabisa mrembo huyu alipanga kujiweka kidogo karibu na Roma ili kuweza kujua ni kwanini macho yake yanabadilika Rangi , aliamini kama watakuwa marafiki Roma anaweza kumfungukia.

“Bi Wema kama mke wangu anapenda kuongozana na mimi nipo tayari , isitoshe leo sina pakwenda na sijazoea kukaa ndani”Aliongea Roma.

“Roma itakuwa vizuri kama tutaenda wote , unisaidie kwenye kubeba mizigo ya kwenda nayo”Aliongea Edna na Roma aliitikia kwa kichwa.

Baada ya nusu saa Roma alikuwa ashajiandaa kwa ajili ya kuianza safari ya kuelekea Bagamoyo , alikuwa sebuleni akimsubiria Edna ambaye kama ilivyokuwa tabia ya wanawake kujiandaa muda mrefu Edna alichukua lisaa mpaka kuonekana akiwa anashuka.

Roma siku zote alikuwa akijivunia hata kuitwa mume wa Edna , kwani mwanamke huyu hata avae nini , alikuwa akipendeza sana na kuvutia,Edna alikuwa amevaa leo Suruali ya jeans rangi ya Bluu iliomfanya umbo lake kuonekana vyema, na kishati flani kitambaa mtelezo mikono mirefu , na akakikunJa hadi kwenye kiwiko cha mikono , chini akiwa amevalia viatu vyeupe kama Raba Rangi ya pink.

Edna alimpa Roma ufunguo na Roma alitangulia mpaka sehemu ya kuegeshea magari na kubonyeza Rimoti na Pickup aina ya Cadillac Escalade EX ili Tweak na kuwasha taa ,Roma alitabasamu na ufahari wa hii gari , aliitoa na kuleta mpaka katikati na Edna aliingia.

Bi Wema aliekuwa juu ya Gorofa alikuwa akitabasamu kwa furaha baada ya kuona Edna na Roma wakitoka , alijiambia ni mwenye akili sana kushauri waende pamoja.

“Kuanzia sasa misheni yangu ni kuhakikisha wanafanya mambo kwa pamoja , hii itawaongezea kuwa karibu” Aliwaza Bi Wema huku akijiona jasusi mbobezi likija swala la mapenzi.

Safari ya wanandoa hawa iliishia Mliman City , Watu waliokuwa ndani ya eneo hili waliwaangalia kwa macho ya tofauti kabisa huku kila mtu akiwa na mawazo yake ,Edna alikuwa amevalia miwani ambayo ilimfanya apendeze lakini yeye hakuvaa kwa ajili ya kupendeza , alikuwa amevaa kwa ajili ya kufanya watu wasimtambue.

Roma alievalia jeans lake Rangi nyeusi na koti la Ugolo alijongea upande upande na mke wake , huku akijisikia fahari namna ambavyo wanaume wa eneo hili walivyokuwa wanamwangalia kwa macho ya wivu.

Walinunua mahitaji mengi ndani maduka ya vyakula , baadhi ya nguo , taulo za kike na makolo koloo mengi sana ambayo yalikwa ni sehemu ya mahitaji ya Watoto , walichukua na baadhi ya zawadi kwa Watoto hao ikiwemo biskuti pipi na vitu vingine.

Baada ya kumaliza kufanya manunuzi , Roma kusaidiana na baadhi wafanya kazi walipakia huku Edna akiwa bize kulipia.

Wakati Roma akiwa bize kupandisha vitu , mara alisikia sauti iliokuwa ikimuita nyuma yake , sauti ya kike ambayo alikuwa akifahamu vyema, alikuwa ni mrembo Doris ambaye alikuwa akiegesha gari yake , akiwa yupo peke yake aliependeza kama kawaida.

“Doris !”Aliongea Roma kwa kushangaa baada ya kumuona mrembo huyu mbele yake.. wakati Doris anamwangalia Roma kwa mshangao mara alikuja Edna na kwenda kusimama karibu na Roma.

“Edna!”Macho yalimtoka Doris , hakuelewa ni kwanini wawili hao wako pamoja .

“Vipi Doris umekuja kufanya Shopping?”Aliuliza Edna wa kwanza baada ya kuona Dorisi yupo kwenye mshangao pasipo kuongea neno.

“Ndio Edna , lakini kwanini upo na Roma?”

“Nisamehe Dorisi rafiki yangu , nadhani unakumbuka nilikuambia nina mume?”

“Usiniambie Edna huyu ndio mumeo na siku zote huniambii?”.

“Ndio Dorisi huyu ni mke wangu,Tunaelekea Bagamoyo na muda unaenda tutaongea Zaidi”Aliongea Roma akikata mazungumzo hayo , hakutaka waendeleee kusimama ndani ya eneo hilo la maegeisho ya magari

“Nitakupigia simu Doris , tutaongea”Aliongea Edna na Roma alimshika bega Edna na kumsukumizia ndani na kufunga mlango na kisha akazunguka upande wa dereva na kuingia ndani na kuliwasha huku wakimwangalia Doris aliekuwa amesimama akiangalia gari yao ikitokomea.

“F**ck you Roma , siku zote unanichora tu kumbe mkeo ni Edna , halafu kwanini Edna hajaniambia”Alijiongelesha mwenyewe na kusahau kuwa baadhi ya watu walikuwa wakimshangaa , alifuta machozi kwa mkono ambayo yalikuwa yashaanza kujitengeneza ndani ya mboni za macho yake na kufungua mlango wa gari na kuingia na kisha akatoa gari ndani ya eneo hilo , alionekana kughairi , alichokuwa amefata hapo.

“Doris atakuwa amekasirika”Alianzisha maongezi Edna wakati wakipita Lugalo.

“Kwanini unasema hivyo?”

“Doris ni Rafiki yangu wa muda mrefu na niseme ni Zaidi ya Rafiki yangu , tumekuwa pamoja kwa muda mrefu kidogo , nilimwambia nimeolewa na kumuhaidi nitakutambulisha kwake lakini sikufanya hivyo na leo ametuona pamoja , kama marafiki atakasirika na kujisikia vibaya”.

“Mke wangu usiwe ni mwenye wasiwasi , Doris ni Rafiki yako na wewe ulikuwa pia na sababu za kutonitambulisha kwake mapema , hivyo atakuelewa , isitoshe hatuna muda mrefu tokea tumesajili ndoa yetu”.Edna aliitikia kwa kichwa.

“Kila jumapili unakujaga huku kutembelea kituo?”Aliuliza Roma kwa makusudi a ya kubadilisha stori.

“Ndio , imekuwa utamaduni , kila jumapili lazima nitembelee , napenda Watoto na najisikia faraja ninapokuwa nao karibu”.

“Mke wangu nilijua wewe ni kauzu kila sekta , kumbe una upande wako mwingine ambao sikuwa nikiufahamu”.

“Mimi sio kauzu ila napenda kuwa siriasi kwenye maeneo yanayonitaka kuwa hivyo , sipo kama wewe kila eneo haupo siriasi”.

“Kwa hio mke wangu wewe unataka niwe vipi?”Edna hakujibu aliendelea kukaza macho barabarani na Roma hakutaka kuongea Zaidi.

Ni masaa machache tu walikuwa washafika ndani ya kituo hiki , kilikuwa ni kituo kikubwa sana, kilikuwa na majengo makubwa kama chuo , jambo ambalo lilimshangaza Roma.

“Mke wangu hiki kituo ni kikubwa ni shirika gani limejenga hiki kituo?”

“Sio shirika ni mke wa raisi wa Kenya ndio amejenga hapa Tanzania”Roma alishangaa ,yaani mke wa raisi atoke Kenya kwao ambako kuna Watoto wengi waliozagaa mtaani aje ajenge Tanzania , alishangazwa na jambo hilo.

“Kwanini ajenge Tanzania sio Kwao Kenya?”

“Hata Kenya kajenga vituo vingi tu na sio Kenya wala Tanzania ,Uganda , Rwanda na Kongo kajenga vituo vinavyofanana hivi hivi, ni mwanamke ambaye ana moyo mzuri sana na anasifika sana ndani ya Afrika kwa kuisadia jamii.

Roma alitingisha kichwa baada ya kupewa jibu hilo na mke wake , aliona huyo mwanamama anapaswa kupewa tuzo kwa msaada mkubwa ambao anaufanya kwa jamii zenye uhitaji.

Kitendo cha kumaliza kuegesha Gari Tu ni kama Watoto waliokuwa ndani ya hili eneo walikuwa wakimsubiria Edna kwani kundi lote lilimkimbilia na kumzingira huku wakionyesha furaha yake na Edna na yeye hakuwa nyuma , alionekana kufurahi kweli uwepo wa Watoto na kwa mara ya kwanza Roma anamshuhudia Edna akiwa na furaha sana.

“Sikujua mke wangu kumbe mzuri hivi akicheka , halafu anaonekana kuwa na moyo mzuri sana , kanaigiza tu kuwa siriasi”Aliwaza Roma huku Watoto hao wakiwa hawana habari nae.

“Edna karibu” Aliongea mwanamama mmoja hivi mnene mwili wa kibonge mwenye umri si chini ya hamsini hivi alikuwa wa maji ya kunde.

“Asante Mama Issa ”Alijibu Edna aliekuwa akiwaangalia Watoto hawa , lakini kwa upande wa yule mama alimwangalia Roma na hapa ndipo Edna aliekuwa amemshau Roma akainuka.

“Mama Issa Watoto wamenifanya nisahau kukutambulisha , huyu ni mume wangu anaitwa Roma Ramoni” Mama huyu macho yalimtoka kwa mshangao huku Roma akiwa ni mwenye kutabasamu , alijiuliza huyu mwanaume ana nini mpaka kupata nafasi katika maisha ya Edna.

“Sikujua.. kumbe umepata mume Edna .. jamanii.. karibu baba mimi naitwa Tabea Singano ni mkuu wa hiki kituo”Aliongea mama huyu huku akionyesha furaha yake waziwazi , alionekana pia ni mtu ambaye alitamani siku moja Edna kumtambulisha mume wake kwake.

“Nashukuru sana kukufahamu Mama”.

“Karibu sana , unabahati sana kumpata Edna katika Maisha yako , umchunge sana”Aliongea mwanamama huyu huku Edna hata hakuwa akiwasikia , kwani alikuwa bize na Watoto aliokuwa akiwabeba mmoja mmoja juu.

Walishusha mizigo kwa kusaidiana na wafanya kazi wa hapa ndani , na Roma pia alisaidia katika kazi hio na baada ya zoezi hilo dogo kuisha Edna na Roma walichukua zawaidi walizokuwa wamekuja nazo na kuanza kuzigawa kwa Watoto hao .

Roma alimkubali sana aliejenga hiki kituo kutokana na wingi wa Watoto hao , kilikuwa mpaka na shule kubwa ya msingi mpaka sekondari , ni kituo ambacho kilionesha kujitosheleza sana kwa kila kitu.

Mama Issa alimchukua Roma na kuanza kumtembeza ndani ya kituo hichi , kwa kumuonesha baadhi ya huduma ambazo wanatoa kwa Watoto hawa ya kimalezi , mama huyu alionekana kuwa mkarimu sana.

“Edna ni msichana wa kipekee sana ,nimemuona akikua kwanzia alivyokuwa mdogo”Roma alishanga

“Mlikuwa maishi majirani?”.aliuliza Roma na mwanamama huyu alitabasamu.

“Hapana , wakati wa utoto wake alikuwa akija na bibi yake hapa mara kwa mara kucheza na Watoto na naweza kusema Muda wake wa utoto mwingi alicheza na Watoto ambao walikuwa kwenye hiki kituo”Aliongea mama huyu na kumfanya Roma ashangae , na wakati huu walikuwa wakiingia ndani ya mejengo ya ofisi hizi za kituo hiki kilichokuwa kinafahamika kwa jina la Son and Daughter Orphanage(SDO)..

Roma baada ya kuingia ndani ya hii ofisi kubwa ya mama Issa alijikuta akishangaa picha iliokuwa juu ya ukuta ,ilikuwa ni picha ya mwanamama mmoja maji ya kunde aliekuwa kwenye pozi la kutabasamu, kichwa chake kilianza kuuma na kupiga kama Radi na picha picha za matukio zikianza kupita .. macho yake yalianza kubadilika palepale na kuwa ya kijani.

SEHEMU YA 32

Roma alishindwa kuvumilia , alikuwa akishindana na hali iliokuwa ikiendelea kwenye mwili wake , alifumba macho yake haraka sana , ili Mama Issa asimuone akibadilika na kisha akageuka, Uzuri ni kwamba mwanamama huyu alikuwa amempa mgongo Roma na hakuwa akijua kilichokuwa kikiendelea kwenye kichwa chake.

Roma alikimbilia nje , lakini ile anatoka kwenye ofisi alijikuta akikumbana na Edna ambaye aliona hali yake ya macho Alitaka kumwepa lakini Edna hakufanya hivyo , alimshika mkono.

“Roma Calm Down”Aliongea Edna na Roma ni kama ameshituka kwani macho yake yaligeuka na kurudi katika hali yake ya kawaida na kumwangalia Edna.

“Am Sorry Edna”.

“Sorry ya nini?”

“Sijui …”Kabla Roma hajaibu walishitushwa na sauti ya Bi Tabea.

“Nilishangaa umeenda wapi kumbe umemfata mkeo”Aliongea Bi Tabea na Edna alitabasamu.

“Edna niseme tu hongera sana kwa kupata mume , Roma anaonekana kuwa kijana mzuri naamini mama yako na bibi yako watakuwa na furaha na wanaweza kupumzika kwa amani maana wewe..”

“Mama Issa Maana nini…”aliongea huku akicheka.

“Umekuwa mgumu sana , nakumbuka yule nani yule .. ee Elvice alikuwa akitoka jeshini lazima aje hapa kulalamika..”Mama huyu alijikuta akiishia njiani kuongea na kujiona ameropoka ila kwa Roma alikuwa amesikia kila kitu na akajiuliza kuna historia gani kati ya Elvice na Edna ambayo hakuwa akiijua , ila hakutaka kuuliza.

Saa moja kamili za jioni ndio muda ambao wawili hawa walitoka ndani ya kituo hiki kurudi nyumbani , Edna alionekana kuchoka kweli kutokana na kucheza na Watoto , kwa upande wa Roma yeye hakuwa amechoka , kwanza hakucheza kabisa na Watoto kwani sio mtu wakupenda sana kama ilivyokuwa kwa Edna.

Alimwangalia mke wake aliekuwa amesinzia pembeni na kujikuta moyo wake ukiwa wa moto , alitamani Maisha yake yawe kama hivyo kila siku ,awe anapendana na mke wake , watembee hapa na pale kurefresh mind, alitamani kufurahi na kuendeleza Maisha ya ukawaida , lakini Roma Maisha ya aina hio yalikuwa kwake ni ndoto.

“Hapana lazima nifanye juu chini nina kamilisha yote yalionileta Tanzania , nikishachimba swala hili kwa undani na kujua kwanini nilikuwa kwenye kile kisiwa cha mateso mimi na Seventeen na kuifahamu familia yangu nadhani nitatulia na mke wangu, Edna licha ya kwamba hatujaoana kimapenzi , lakini sidhani kama itakuja siku nitakuacha hata pale mkataba utakapoisha”Roma aliwaza mawazo hayo mchanganyiko huku akizidi kukanyaga pedeli kuelekea jijini Dar es salaam.

Wakati akiendelea kuendesha gari alikumbuka kauli ya Bi Issa kumuuliza hali ya kimaendeleao ya Nasra , alijiuliza kwanini mwanamama yule kauliza juu ya maendeleo ya Nasra ila alikosa majibu kwa wakati mmoja , alijiambia kuwa atafahamu kadri atakavyokuwa karibu na Nasra.

****

Doris alijikuta ni mwenye hasira sana , baada ya kujua kuwa Edna na Roma ni mume na mke , alikasirika sana , lakini na kuumizwa kwa wakati mmoja.

Alianza kukumbuka tukio ambalo Roma alimuomba hela ya nauli wakati akiwa anarudi nyumbani na kumpatia , alikumbuka usiku wao waliotumia na kufanya mapenzi na mwanadada huyu alizidi kutokwa na machozi ,alihisi moyo wake ulikuwa ukimuuma sana kiasi cha kwamba mwenyewe alishindwa kuelewa kwamba moyo wake ulikuwa ukimuuma kutokana na kwamba Edna na Roma walimficha na kumuona mjinga siku zote , au ni kwasababu alijua kuwa Roma mke wake ni Edna mwanamke mrembo na kilichokuwa kikimliza ni wivu wa kimapenzi.

Alisimama kukodolea maji ya baharini muda huu wa jioni huku machozi yakiwa yanamtoka , lakini kila alipokuwa akiangalia baadhi ya wapenzi waliokwa ndani ya fukwe hii ya Coco walivyokuwa wakifurahi na kuonyesheana mapenzi , aliijikuta akizidi kutoa machozi.

“Ninaonekana kutokuwa na bahati katika Maisha yangu , Edna nifanye nini mimi nahisi kumpenda sana mumeo , najiona kabisa siwezi kumuacha hata kidogo , kwanini iwe wewe rafiki yangu”Aliwaza mwanadada huyu na kuwazua huku akionekana ni mwenye kukosa jibu , alionekana alikuwa akishindana na hisia zake.

Doris licha ya kwamba alikuwa sio mwenye kuonyesha waziwazi mapenzi yake kwa Roma alikuwa ashampenda tokea siku ya kwanza wanaonana ,Roma alivyomuomba kiasi cha pesa , tokea siku ile alikuwa alikuwa ni mwenye kumkumbuka Roma , hakujua ni kwanini alikuwa akimkiumbuka mwanaume huyo , lakini picha yake haikuwa ni yenye kutoka kwenye kichwa chake.

Siku ambayo anamuona Roma kwa mara nyingine ndani ya kampuni yake , akija kufanya usaili , alijiambia kabisa ni Mungu ndie aliekuwa amewakutanisha kwa mara nyingine na hivyo hapaswi kuzarau kile Mungu alichompatia na ndio maana siku ile ile aliona atumie nafasi ile kumtambulisha Roma kwa mwanaume mzee aliekuwa akimsumbua , mwanaume aliekuwa akimfahamu kama Mr Kijembe .

Hakujali kabisa katika moyo wake kwamba Roma ameoa , alichokuwa akiamini ni Kwamba Roma alikuwa amepangiwa kuwa nae katika Maisha yao yote na mke aliemua ni makosa ambayo Roma alikuwa amefanya , hayo ndio yalikuwa mawazo ya mwanadada huyu mrembo , aliamini mke wa Roma sio mtu sahihi kwa Roma na yeye ndio alikuwa sahihi , kwani matukio yao ya kukutana ni kama Mungu aliwakutanisha.

Hata pale alipopata taarifa ya Roma kulala na mwanamke Neema Luwazo Mwanamke ambaye alikuwa akimjua sana tu, kwa kuwa na mahusiano na Raisi mstaafu , alijiambia kuwa ni mihemko tu ya Roma ya kukosa mtu sahihi wa kumtuliza na kama atampata basi Roma angetulia kwake na kuachana na mambo ya wanawake , kwani angempa kile kitu ambacho anakitafuta nje , kitu ambacho aliamini ni kwamba alikuwa akikikosa kwa mke wake.

Siku ya Jumapili ndio siku ambayo alipanga kutimiza jambo lake la kuanza kuweka ukaribu na Roma , aliamini anapaswa kufanikisha swala la yeye kuwa karibu kabla ya kwenda safari ya kikazi Japani , alitaka katika safari hio waitumie kama sehemu yao ya matembezi kama wapenzi , na ili kukamilisha swala hilo anachotakiwa kufanya ni kuhakikisha Roma anakuwa karibu yake anamzoea na hatimae kumpenda.

Baada ya kuwaza hayo , hatua ya kwanza aliofikiria ni kwenda kutafuta zawadi yoyote ambayo aliamini itamfurahisha Roma na eneo pekee alipoona panafaa kupata zawadi hio kwa siko hio ya jumapili ni Mlimani City.

Nwanadada huyu alijiandaa , alichukua kadi yake ya benki aina ya ‘Black Card’ kadi ambayo ilikuwa ikimruhusu kutoa kiasi chochote kile cha pesa na kuiweka katika mkoba wake , na kisha akachukua ufunguo wa gari yake na kutoka ndani ya jumba hili la kifahari alilokuwa akiishi mwenywe na wafanya kazi.,Jumba ambalo alikuwa amenunuliwa kama zawaidi na baba yake .

Lakini baada ya kufanya safari yake na kufika Mlimani anajikuta akishuhudia kitu ambacho moyo wake haukutarajia kukiona , alimuona mwanamke ambaye aliamini sio sahihi kwa Roma akiwa ni Edna , Rafiki yake kipenzi , bosi wake kazini, moyo wake ulipigwa na ganzi.

“Doris!!”Ilikuwa ni sauti ya mwanaume iliosikika nyuma yake na kumfanya mwanadada huyu ageuke ni nani anamuita , lakini ile anageika alikutana na uso wa Abu.

“Abu vipi , kwanini uko hapa ?”Aliuliza Doris kwa namna ya kushangaa.

“Nimekuja kupunga upepo kama wengine Doris , wewe vipi , kwanini uko hapa?”.

“Namini nipo kwa ajili ya kupunga upepo “Abu alijikuta akitabasamu .

“Doris najua unaonekana kuwa katika hali ya mawazo , lakini nimekuwa nikisubiria sana jibu lako”

Doris alishangaa na kuanza kuvuta pumzi kwa nguvu na kumgeukia Abuu….

Ni jibu gani ??

SEHEMU YA 33

2010 -KIGALI STATE HOUSE

Ni mwaka 2010 muda wa saa tano za Asubuhi mheshimiwa Jeremy alionekana ndani ya ofisi yake akifanya kazi kama kawaida, katika kuwatumikia wananchi wa Rwanda, lakini siku hii kwa mheshimiwa huyu hali yake ilionekana kuwa sio ya kawaida , kwani alionekana kuwa ni mwenye wasiwasi sana kuliko siku zote hali ambayo ilimfanya kukosa utulivu , kila saa alionekana kuangalia saa ya ukutani kama mtu ambae alikuwa na jambo ambalo alikuwa akilisubiria.Ilivyofika saa sita na nusu aliingia Linda mlinzi wa karibu wa Mheshimiwa Jeremy.

“Mheshimiwa Ashafika”Aliongea Linda na kumfanya mheshimiwa Jeremy avute pumzi .

“Mruhusu aingie”Aliongea mheshimiwa na kisha akatoka kwenye meza yake na kwenda kwenye masofa na hapo hapo mlango ulifunguliwa na aliingia mwanaume mmoja wa kizungu alievalia shati la Blue bahari na suruali ya kadeti , muonekano wa huyu jamaa ni kama vile hakuwa akiingia kuonana na mheshimiwa , kwani alivaa kikawaida sana kama muhuni flani hivi.

“Welcome Mr Viladkov”Aliongea mheshimiwa kwa kingereza.

“Asante sana mheshimiwa”Aliongea na kisha alitoa karamu nyeusi flani hivi pana kidogo lakini ya kawaida , kama zile za rangi na kisha alianza kuifungua kama mtu ambae anatoa ule mrija wa wino, na akatoa kifaa Fulani hivi kama kile kichwa cha kuchomekea kwenye Earphone lakini hiki kwa juu mwisho kina kitu kama kigoroli.

“Hili ndio faili mheshimiwa”Aliongea na kisha alimpatia Jeremy kile kidude na mheshimiwa alishangaa m inakuwaje kadude kama hako kawe ndio faili ambalo alikuwa akilisubiria kwa hamu.

‘”Usishangae mheshimiwa Hata Urusi sasa imeendelea kwenye teknolojia , na hio ni mbinu yetu mpya kuficha taarifa wakati wa kuzisafirisha” ’Mheshimiwa Jeremy hapa alishangaa na akachukua Tablet iliokuwa kwenye meza yake na kuchomeka kale kadude na baada ya tablet ile kusoma kama Earphone ilisoma kama memori , alishangaa na Viladkov akatabasamu.

“Ni taarifa nyeti sana hio , na serikali ya Urusi imelipa kiasi kikubwa kuinunua kwa mtu aliekuwa akiuza”Aliongea bwana huyu na mheshimiwa Jeremy aliifungua na ajabu ni kwamba alikutana na picha.

“Mbona ni picha sio kama faili nilivyokuwa nikitegemea?”

“Angalia kwanza hizo picha mheshimiwa kwa umakini na uniambie umegundua nini?”

Alianza kuangalia hizo picha kwa kuzizoom na katika picha hizo kulionekana meli kubwa ya mizigo ikiwa inashusha mavyuma , lakini baada ya mheshimiwa kuangalia kwa ukaribu Zaidi aligundua ni bawa la Ndege.

“Linaonekana kama bawa la Ndege”

“Angalia na hio nyingine” Aliangalia na pia yenyewe ilionekana kama baadhi ya vipandevvipande vya mabaki ya ndege.

“Hio meli inamilikiwa na kampuni Neptune , kampuni ambayo ni sehemu ya kampuni kubwa ya kuzalisha ndege ya kimarekani inayofahamika kwa jina la Ngebo Aeronautical”Mheshimiwa alionekana kushangaa , lakini pia alizidi kuongeza umakini.

“Hizo picha zilipigwa Tarehe saba March 1998”Aliongea na mheshimiwa huyu alishangaa sana.

“Unataka kumaanisha kwamba ni siku moja kabla ya ndege ya Malaysia kupotea?”

“Ndio kutoka sehemu ambayo meli hio ilipo na sehemu ambavyo ndege ya shirika M ilipotea ni umbali wa kilomita ishirini tu , kwa maana hio hayo ni mahesabu ambayo yamepigwa kabisa na hio meli ilitupa mabaki hayo unayoyaona kwenye hizo picha eneo hilo”Mheshimiwa Raisi alijikuta akitetemeka maana anacho ambiwa hapo ni taarifa nzito sana , tena nzito kweli kweli.

“Mheshimiwa hii ni siri ninayokupatia ambayo ni siri kubwa ndani ya taifa la Urusi na ni kama Asset kwetu , hivyo taarifa hii inapaswa kuwa siri , mheshimiwa Raisi Viladmn karuhusu upatiwe taarifa hio ili kwa ajili ya kushawishi mataifa ya Afrika kuingia kwenye Mpango TASAC”Mheshimiwa alishangaa Zaidi.

:Mheshimiwa chomoa hio flash na uichomeke tena” aliongea Viladkov na mheshimiwa alichomoa na kuichomeka tena na ikasoma tena kama memori , aligusa ten ana zile picha zikawa zimefutika ils sasa kulionekana faili lililokuwa kwa mfumo wa ‘Xml’ , mheshimiwa alilifungua na kuanza kusoma na hapa ndipo aliposhangaa.

“Hio ni barua ya wito iliotumwa kwa mashirika ya kijasusi makubwa yote duniani na katika hio barua inaonesha kulikuwa na makubaliano ambayo yalikuwa yanatakiwa kufanyika juu ya mpango ambao ulipewa jina la LADO ambapo sisi tulishindwa kung`amua kirefu cha neno hilo , na shirika letu pekee ndiio halikutuma muwakilishi kwenda kuhudhuria kikao hiko ambacho kilifanyikia nchini Italy”Mheshimiwa jasho lilimtoka maana kadiri anavyoambiwa ndio anavyoona siri hii kuzidi kuwa nzito na kuhofia Maisha yake.

“Kwa hio unamaanisha kwamba LADO na kupotea kwa ndege ya shirika la M ni swala ambalo lina muunganiko na limeratibiwa kwa makubaliano ya mashirika makubwa ya kijasusi duniani?” Aliuliza na jamaa alitingisha kichwa kukubaliana nae.

“Kwanini mmeamua kunipa hii taarifa?”

“Mpango TASAC ni mpango ambao unahusisha serikali ya Urusi kurudisha umoja wa Kisoviet , lakini hili ili liweze kufanikiwa , tunahitaji sapoti kutoka Afrika , tunahitaji udhaifu kutoka kwa mataifa makubwa ambao utatusaidia pale itakapobidi serikali yetu kuingia vitani , mataifa haya hayatoi msaada , lakini nyie wa mataifa ya Afrika mnapaswa kutuunga mkono kwa kukaa kimya.”

“Na ili swala hili lifanikiwe unapaswa kuhakikisha asiliamia sabini ya mataifa ya Afrika yanakuwa kwenye huu mpango TASAC na mheshimiwa Raisi wa Urusi amekuchagua wewe kutokana na uzoefu wako katika uongozi, ukifanikisha mpango huu basi serikali ya Urusi itafanya juu chini kubaini ni nini kipo ndani ya operesheni iliopewa jina la LADO”.

“Natakiwa kukubali swala hili hapa hapa?”

“Hapana mheshimiwa , swala hili lina umuhimu sana kwa nchi yetu na mheshimiwa Raisi atakupigia simu na mimi nipo hapa kwa ajili ya kukueleza haya , kwani tunajua kuwa wewe ni mmoja ya wahanga wa AJali ya ndege na unataka kulipiza kisasi , lakini kutokana na ukubwa wa tukio lenyewe na udogo wa taifa lako, hautoweza kupata hio nafasi ya kuujua ukweli”Aliongea bwana huyu na heshimiwa Jeremy alikubali kuwa kiongozi wa juu wa mpango TASAC.

****

“Sauron habari za muda huu?”

“Salama kabisa mfalme Pluto, habari za Tanzania?”

“Hapa ni kwema kabisa Sauron , nimekupigia kupata ripori ya yale tilioongea jana”

“Mfalme Pluto , nimeshayakamilisha yote na nimepanga vijana kumi wenye uwezo wa hali ya juu kwa ajili ya kuja nchini Tanzania, lakini kuna jambo moja nimeona nitoe pendekezo”

“Edelea kuongea Sauron nakusikiliza”

“Nimeona makomandoo hawa wakiingia nchini kama watalii hawatapata kibali cha muda mrefu cha kukaa hapo Tanzania , hivyo nimejaribu kuwasiliana na balozi ya Sweeden nchini Tanzania na kuwaomba watufanyie mpango wa kuwaingiza wanajeshi wetu kama wafanya kazi wao”Roma Alitabasamu.

“Sauron wewe unakili sana , hili sikulifikiria , ni kweli watapaswa kukaa nchini muda mrefu kidogo kwani pia nataka wamlinde mke wangu”Sauron alishangaa.

“Mfalme Pluto usiniambie umepata mke?”

“Ndio Sauron , sio muda mrefu sana nimefanikiwa kupata mke”

“Hongera sana mfalme Pluto , ila kwa hatua hio sidhani kama utarudi huku kisiwani”

“Yanayotokea kesho hatuyajui Sauonoi hivyo siwezi kuongea lolote juu ya hili”.

“Ni kweli Mheshimiwa Pluto , ila nitatamani kumuona malkia wetu”Roma alitabasamu

“Utamuona Sauron nitakuja nae siku moja , Sauron kuna jipya lolote kutoka The Zeros?”

“Mfalme Pluto vijana bado wanaendelea kufuatilia na naamini muda si mrefu watatupatia taarifa “

“Sawa Sauron , nadhani tutawasiliana baada ya vijana kufika Tanzania”Baada ya hapo waliagana na Roma akakata simu .

Muda huu Roma anawasiliana na Sauron ilikuwa ni saa moja kwenda saa mbili hivi , hivyo baada ya kumaliza tu aliitwa na Bi wema kwa ajili ya chakula cha usiku.

Baada ya kufika tu chini na Edna alikuwa akishuka alievalia kigauni kilichokuwa kikipeperuka kiasi kwamba kilimfanya Roma aliekuwa chini ya ngazi aone mapaja ya malaini ya Edna na alijikuta hisia za mapenzi zikimuandama.

“Kukaa na mwanamke kama Edna halafu hupati kitumbua chake ni swala ambalo nina uhakika madaktari wataniambia ni sumu kwa Afya yangu , nikimaliza hapa nduki kwa Rose nikapunguze kichupa”Aliwaza Roma huku akivuta kiti na kuketi.

Edna na yeye alijikuta akitabasamu baada ya kumuona Roma leo hajatoka kabakia nyumbani , kwani mara nyingi hakuwa akipenda sana Roma a tabia yake ya kutoka na kurudi asubuhi yeye kama mke aliona sio vizuri.

Wanafamilia hawa walikula wakashiba na baada ya hapo Edna aliungana na Bi wema kusafisha vyombo , lakini wakati Edna akiwa bize na vyombo upande wa jikoni Roma alimchungulia kwenye mlango.

“Bebi ndio natoka hivyo , hapa hadi kesho”Aliongea Roma na Edna ambaye alikuwa ameweka mikono yake kwenye Sink alijikuta akikunja ngumi kwenye maji na kung`ata meno , kwani kila ambacho kilikuwa kikimfurahisha dakika chache nyuma kimegeuka ndivyo sivyo,Edna aliishia kutingisha kichwa na Roma hakujali aliondoka.

“Yaani huyu mwanaume hatulii nyumbani”Aliongea Edna kwasauti pasipo kujua nyuma yake kasimama jasusi mbobezi wa mapenzi Bi Wema.

“Miss ulifikiri sasa atafanyaje , mmeoana lakini hamlali chumba kimoja , yule ni mwanaume na wanaume tendo la nndoa ni kama hitaji lao la msingi hawezi kukaa na mtoto mrembo kama wewe halafu akuangalie kama picha ya ukutani”Edna alifikiria kidogo.

“Bi Wema nitafanyaje , bado sina hisia nae na wewe unaelewa tumeoana kimkataba”.

“Naelewa ndio , lakini miss angalau jaribu kuufungua moyo kwa Roma , huenda ukampenda na mkawa Mume na mke kimapenzi sio kimkataba”Edna alitingisha kichwa kuelewa

Baada ya kufika chumbani kwake alionekana kuwaza maneno ya Bi Wema na kuona kidogo yana maana.

“Au nijaribu kumpa?”Aliwaza Edna akimaanisha ajaribu kumpa Roma kitumbua.
Unafikiri nini mwisho wa yote ....??
WIKIEND NJEMA TUONANE JUMATATU

CHANGIA KAZI HII KWA KULIPIA KUANZIA 2000 KUENDELEA NIKUUNGANISHE NA GRUPU UIFATILIE KWA VIPANDE VITATU KILA SIKU TUPO SEASON 2 KWENYE GRUPU

GRUPU NI KWA AJILI YA SIMULIZI HAKUNA KUCHAT

LIPIA NAMBA 0687151346 AIRTEL AU 0623367345 HALOPESA AU 0657195492 TIGOPESA JINA ISSAI SINGANO UKILIPA TUMA MESEJI YA MUAMALA NAMBA 0687151346 WATSAPP


View attachment 2336156

.
 
SEHEMU YA 57

Roma alitabasamu na aliona kabisa amejiingiza kwenye mtego wa Edna , na kujilaumu kwa kutokuwa makini na maneno yake , lakini alijiwazia kuwa sheria yake kubwa ni kuongea ukweli pale inapobidi kufanya hivyo.

“Nimelala na Dorisi ,Nasra , Rose na Neema Luwazo”Aliongea na kumfanya Edna akunje sura , kitendo cha Roma kujibu swali lake bila hatia kilimuuzi sana na alitamani agonge geti na gari

“Bebi wife umeridhika na jibu?”

“Ndio”Aliibu Edna na kisha hakutaka maoangezi tena , baada ya kuingiza gari ndani ya uzio , alichukua mkoba wake na kuingia ndani na hakuhangaika hata kuegesha gari.

“Bi Wema nimerudi”Roma alimsalimia Bi Wema kwa tabasamu.

“Karibu sana Mr Roma nyumbani kwako”

“Asante sana Bi Wema nimemisi chakula chako sana”Bi Wema alitabasamu.

“Karibu Mezani Mkeo leo aliamka mapema kukuandalia chai nzito na sasa ipo mezani”aliongea Bi Wema huku akiwa ni mwenye kutabasamu , lakini kwa Roma alishangaa kidogo , alijua Edna alikuwa akitiania alivyosema amemuandalia chakula.

Roma alijongea mezani huku akiwa na hamu ya kujua ni kipi Edna awamu hiia amepika.

“Bi Wema kaandaa Edna hizi tambi?”Aliuliza roma baada ya kula kidogo , alishangazwa na tambi hizo kuwa nzuri licha ya kwamba hazikuwa tamu kwa kiwango cha juu lakini zilikuwa tamu.

“Ndio Miss amekuwa akijifunza kupita tokea uondoke na amesema amepata rafiki anaemfundissha kupika”

Roma alijikuta akizidi kushangaa , alijiuliza ni rafiki gani huyo Edna mke wake amempata , kwani kwa namna ambavyo mke wake alikuwa kauzu, ilikuwa ni ngumu sana kuwa na marafiki kwani hata Dorisi ambaye alikuwa ni rafiki yake walionekana kama sio marafiki.

“Bi Wema ni rafiki gani Edna kampata?”

“Mimi sifahamu lakini ninachofahamu ni kwamba huyo rafiki yake ni mwalimu mpya ndani ya shule ya kituo cha kulelea yatima”.

Roma alitingisha kichwa hakutaka kuuliza sana maswali , lakini alikuwa na shauku ni rafiki Gani Edna kaweza kumpata ndani ya muda mfupi aliosafiri kuelekea Japai , alishangaa.

*****

Upande mwingine ndani ya makao makuu ya kampuni ya JR alioneakna Abuu akiwa ameketi kwenye kiti chake huku sura yake ikiwa katika hali ya wasiwasi sana na jambo ambalo lilimfanya bwana huyu kuwa na wasiwasi ni kutokana na Hisa za kampuni yao zinavyoendelea kushuka , kutokana na kushindwa kusaini mkataba wa Dili la Yamakuza, akiwa amekalia anaangaia tarakishi yake iliokuwa ikimuonesha chati ya Candlestick .

Mlango wa ofisi yake ulifunguliwa na alionekana Isack Makamu wa raisi wa Makapuni haya ya JR, huku mkononi akiwa ameshikilia karatasi.

“Kuna nini Isaack?”

“Abu kuna swala hapa ambalo sio la kawaida”

“Unamaanisha nini?”Aliuliza na Isack alimpatia Abu karatasi aliokuwa ameshikilia.

“Kama unavyona kwenye hio orodha ni baadhi ya watu ambao wamenuunua Hisa zetu baada ya kushuka kwa Thamani , lakini kuna mtu anaejiita Athena anaonekana kununua kiasi kikubwa sana cha hisa na hii ni hatari kwa kampuni , kwani mpaka sasa mtu huyu ana asilimia Zaidi ya therahini za umiliki wa kampuni”Abu macho yalimtoka , aliangalia na ni kweli kuna mtu kanunua hisa zao kwa kiwango kikubwa sana Zaidi ya bilioni mia mbili.

“Kana hisa zikiendelea kushuka Thamani kwa muda wa wiki , anaweza kununua Zaidi”Aliongea Abu.

“Ndio , inatakiwa kuwa na mpango wa kutatua hili tatizo zisishuke thamani Zaidi ya hapa”

“Huyu mtu unafikiri a anampango gani wa kununua hisa zote hizi?”Aliuliza Abuu

“Kuns mawili hapo huenda anataka kuwa na sehemu kubwa ya umiliki wa Kampuni , pili labda ni mtu ambaye ana matarajio chanya ya hisa za kampuni yetu kupanda thamanni baadae ,hivyo anatafuta faida”

“Okey Isack , lakini lazima tuwe makini na pesa yote hii ambayo imeingia kwenye Kampuni yetu , jaribu kutafura namna ya kuwasiliana na huyu mtu , ili tuweze kujua nia yake”

“Sawa boss” Baada ya Abuu kuongea na Isack ,aliingia marasta .

“Vipi Seif anaendeleaje Jose?”

“Anaendelea vizuri , bado yupo hospitalini anaendelea kuongezea Glucose na virtubisho mbalimbali ili mwili kupata nguvu”

“Okey Kazi nzuri”

“Lakini Boss hujaniambia , kwanini tunamtibu kizee kama yule?, sio kawaida yako”

“Jose wewe fanya kama ninavyoelekeza na acha maswali megni sawa”

“Sawa Bosi, Halafi Roma asharudi nchini leo asubuhi , kapokelewa na mke wake uwanja wa ndege na waliongea na Raisi”.Abu alitafakari kwa muda.

“Okey , waambie vijana waendelee kumfatilia kwa kila kitu anachokifanya na nataka taarifa zote zinazomuhusu”

“Sawa bosi”

Baada ya Marasta kutoka , aliingia Elvice ndani ya ofisi hii na kumfanya Abu atabasamu na kumkaribisha.

“Halafu Elvice haujaniambia kwanini mpango wa kumteka Edna ulishindwa kwa mara nyingine wakati nikiwa Japani , nilisahau hata kukuuliza maana niikuuwa nimechanganyikiwa.

“Nilituma vijana wangu kama kawaida , kutoka jeshini , lakini jambo la kushagnaza ni kwamba mpaka sasa sijui walipo , kwani mara ya mwisho niliwasiliana nao wakiwa nje ya nyumba ya Edna”Abuu alishangaa.

“Kwahio unamaanisah kwamba wamekukimbia au imekuwaje , sijaelewa mpaka hapo”.

“Sio wamekimbia , nilijaribu kufatilia kupitia polisi na majibu nilioyapata ni kwamba waliingia kabisa na kuwadhibiti walinzi wa Edna , lakini kwa maelezo ya polisi waliofika kwenye tukio ,Edna alieleza kuwa walidhibitiwa na Wazungu na kisha wakawabeba na kuondoka nao”

“Mh! , hii inaweza ikawa shida kwa upande wetu Elvice kama watakutaja?”

“Hawawezi , ni vijana kutoka jeshini ninao waamini sana na nina uhakika hawawezi kuniuza nimewatumia katika kazi nyingi”Abuu alitikia kwa kichwa kuonesha kuwa amekubali jibu hilo.

“Mpango wetu ni wikiend hii?”

“Ndio bado siku mbili tu kumuondosha yule shetani , japo bado nina wasiwasi?”

“Hupasi kuwa na wasiwasi , licha ya kwamba ulisema alibadillika kama shetani , lakini naamini Roma ni mwanadamu na hawezi kupona na risasi ya moyo”

“Naunga mkono hoja , cha msingi ni kuhakikisha tunamwandalia mazingira seif mazuri ya kufana kazi”

“Hilo muhimu”

*****

Ni Kaskazini mashariki ya Kiimwa kimwe na Kaskazini Mashariki ya Kirawe katikati ya haya maeneo ndipo ilipo Ikulu ya Wananchi wa Kenya , makazi ya mtawala wa Kenya aliemadarakani ndugu Kamau Kamau.

Ndani ya jengo hili ndani ya chumba wanachotumia kulala wanandoa, yaani mheshimiwa Kamau Kamau na mke wake Maina aliemaarufu kama ‘First lady’. Alionekana mheshimiwa Kamau Kamau kwenye kioo kikubwa huku akiwa anaweka suti yake sawa huku nyuma yake akiwa amejilaza mke wake Maina.

“Blandina , utamuepuka mpaka lini Senga , jambo hili linanikasirisha mara kwa mara, na kumuepuka kwako kunanifanya nione bado una hisia nae”

“Kamau hayo ni mawazo yako , ni miaka mingapi mpaka sasa tuwepamoja?”

“Miaka ishirini na tano ya ndoa yetu”

“Sasa nimeishi kwa miaka yote hio na wewe , kwanini bado hujiamini kama nakupenda?”

“Sio sijiamini Blandina , lakini huyu ni kiongozi na inapaswa tumpokee kwa pamoja, nataka ujiamini mbele ya Senga”.

“Sio kama sijiamini mbele ya Senga , lakini wewe ndio umenifanya kuwa hivi , miaka ile nilivyokuambiaa tumuambie Senga ukweli wote ukataka tumfiche huku ukinilazimisha kuishi kwa sura bandia , unafikiri napenda eh”Alianza kulia.

“Am sorry Blandina , yote nimefanya kwa ajili yako na mapenzi yetu , sikutaka Senga ayaingilie”

“You are Selfish Kamau , its always you as you , kwanini unaijali sana nafsi yako kuliko yangu Kamau , ni mapenzi ya aina gani hayo unayo juu yangu ,nimekuwa wakuishi kwa mateso miaka na miaka Kamau, lakini mpaka sasa hats mtoto wa kutoka kwenye tumbo langu sina….”Aliongea na kulia mno mwanamke huyu.

“Nisamehe sana Blandina ,, najua umeishi na mimi miaka na miaka na umekuwa ni mwenye kunifariji , huku ukiacha kuziishi ndoto zako , ni mapenzi makubwa sana ambayo umenipatia , Blandina naahidi baada ya mimi kustaafu I will make evertihing up for you mpenzi , nakupenda sana na nitaendelea kukupenda naomba usinikatie tamaa mapema hivi mke wangu sawa mama”

Kamau alionekana kumbembeleza mwanamama huyu ambaye ana majina mawili , yaani lile la Maina , ambalo lilikuwa likifahamika na watu wengi kama mke wa raisi , lakini pia alikuwa akifahamika kama Blandina , jina ambalo ni watu wachache sana waliokuwa wakilifahamu, na pia ni watu wachache ambao walikuwa wakijua kuwa Maina waliekuwa wakimjua ni feki.

Baada ya kubembelezana muda mrefu ,Maina kinyonge alikubali kujiandaa kwa ajli ya kuelekea uwanja wa ndege kumpokea Raisi senga, ambaye atakuwa hapo nchini kwa ziara ya siku moja.

Ni ndani ya nusu saa wanandoa hawa na baadhi ya viongozi wajuu walikuwa ndani ya uwanja wa kimataifa wa Jomo Kenyata kusubiria ujio wa Raisi senga.

Ilichukua takribani dakika kumi kwa ndege ya ATCL kutua na kusimama kabisa na pia kutoka kwa mheshimiwa Senga.

Maina alijikuta akigonganisha macho na Senga na Senga na yeye alimwangalia Maina huku kwenye kichwa cha Maina mambo mfululizo yakipita , haikueleweka mwanamke huyu alikuwa akifikiria nini kwa wakati mmoja .
 
SEHEMU YA 58

Mheshimiwa Senga baada tu ya kushuka kwenye Ndege alianza kusalimiana na mwenyeji wake Raisi Kamau ,aliekuwa ameambata na mke wake Maina .

Muda wote Maina alikuwa akimwangalia Senga , mwanamama huyu alionekana kuwa na majuto makuu , alionesha hali ya kujutia kwa kitendo cha kujivika sura bandia ili mradi asifahamike uwepo wake duniani kwa Senga.

Senga nae licha ya kwamba alikuwa akisalimiana na viongozi mbalimbali wa juu wa taifa hili la Kenya , lakini akili yale ilikuwa kwa Maina ,Senga alikuwa akijihisi kitu cha ajabu kila anapokutana na mke wa raisi mwenzake , hakujua ni kwanini anapata hisia ambazo ni kama amezisahau katika maisha yake .

"Karibu sana Kenya Mheshimiwa Senga"

"Asante sama Komredi , kila ninapokuja ndani ya taifa hili hua natoka na kitu kipya ni kama kuna nguvu ya Kimungu iliopo ndani ya hili taifa, nakiri Kenya imebarikiwa sana"

"Hahaha.. ni kweli ,Senga hata mimi mara ya mwisho kuja Tanzania niseme nilijisikia Amani na natamani baada ya kuachia madaraka nihamie Kwenye nchi yako" Aliongea Kamau na kwa namna ambavyo alikuwa akionekana kuongea usingemdhania kuwa alikuwa akificha mengi moyoni .

Waswahili wanasema Moyo wa mtu ni kichaka, na hili ndio lililokuwa likijidhihirisha mbele ya Maraisi hawa wa nchi jirani.

Baada ya salamu na mapokezi ya aina yake ya Raisi Senga hatimae walianza mazungumzo yao baada ya kuingia ndani ya Ikulu.

"Senga umekuwa sio wa kuambatana na mkeo mara kwa mara unapofika Kenya Au Damasi anakataa kuja Kenya , nimemkumbuka sana "

"Kamau yule mwanamke acha tu ni mvivu kupindukia na hapendi sana kuonekana hadharani na hio imekuwa tabia yake tokea namuoa".

"Ndio nakumbuka sana ,Sema tumetoka mbali sana Senga, ile mitihani tuliopitia kipindi kile katika kutafuta maisha ilikuwa ni ya aina yake , nakumbuka kila hali ilivyokuwa mbaya kwako na kujihisi kukata tamaa, Blandina ndio aliekuwa akikutia nguvu na neno moja la Blandina kwako la faraja ,ulionekana kuwa mpya na kupambana zaidi".

"Umenikumbusha mbali sana yaani, kama sio Blandina kufariki kwenye ile ajali pamoja na mwanangu Denisi huenda maisha yangu yangekuwa ya tofauti sana"Aliongea huku akiwa ni mwenye Huzuni na muda huo hio aliingia Maina.

Maina alionesha hali ya kutojiamini kabisa mbele ya raisi Senga , alikuwa ni mwenye kukwepesha macho kila mara wanapoangaliana.

"Maina niseme sana Asante kwa kujenga kile kituo kule Bagamoyo , hakika kimesaidia sana jamii ya wenye uhitaji , kimekuwa tumaimi kwa watoto ambao walipoteza wazazi wao wakiwa wadogo".

Asante sana Senga , moyo wangi unafarijika pale ninapo ona watoto wakiwa na furaha na kuishi katika mazingira salama"

"Ni kweli mchango wako kwa jamii za Afrika ni mkubwa sana na unapaswa kupewa tuzo"Maina alitabasamu namuda wote Kamau alikuwa akiwaangalia wawili hao walivyokuwa wakiongea ni kama alikuwa akitafuta jambo flani kupitia kukutana kwao.

Kwa namna ambavyo Senga alikuwa akiongea na raisi Kamau mabwana hawa walionekana kuwa na stori yao ambayo bado watu hawakua wakiifahamu, kwani kwa namna ambavyo waliweza kukumbushiana mambo yaliowatokea miaka ya nyuma , ilionekana walifahamiana kabla hata ya kufanikiwa ,haikueleweka mara moja ilikuwaje mpaka wote wakawa maraisi.

"Sijajua kwanini najisikia wa tofauti kila ninapokutana na Maina".Aliwaza Senga huku akiwa ameshilia picha ilioonekana kuchakaa , picha ambayo ameitoa kwenye mfuko wa koti lake ,ni picha ambayo ilikuwa ikimuonesha mwanamke mrembo , licha ya kwamba picha hio ilikuwa imechakaa , lakini mwanamke aliekuwa kwenye pivha hio alikuwa akionekana vyema kwa urembo wake.

***

Roma baada ya kumaliza kunywa chai ilioandaliwa na mke wake Edna , aliingia chumbani kwake na ndani ya madakika kadhaa alionekana kubadilisha nguo na sasa alikuwa amependeza huku mkononi akiwa ameshikilia ufunguo wa gari yake .

“Bi Wema mimi natoka kidogo nitarudi jioni”Aliongea Roma na Bi Wema akaitikia.

Wakati Roma anatoka Edna kama kawaida yake alikuwa juu ya Balconi akimwangalia Roma ambaye alikuwa akielekea uelekeo wa yalipokuwa yakiegeshwa magari.

“Zishaamka , yaani sijawahi pata ona mwanaume Malaya hivi , kama wanaume wote wako hivi , bora hata mimi niliolewa kwa mkataba, katumia zaidi ya siku tatu zote kuwa na Dorisi lakini saivi pale ni kwenda kutafuta mwanamke mwingine”Aliwaza Edna huku akiangalia Gari ya Roma inayotokomea nje .

Nimemmisi Rose , japo ni asubuhi ngoja nikaonanane nae”Aliwaza Roma huku akikanyaga pedeli kuchanja mbuga kuelekea Mbagala.

Dakika chache mbele kama nusu saa hivi , Roma alikuwa akiingiza gari ndani ya Club B.

Aliegesha gari yake na moja kwa moja aliingia kwenye Bar hii ambayo wakati wa mchana ni wateja wachache sana wanaokuwepo hapo.

“Mr Roma karibu sana”Aliongea Zonga mara baada ya kumuona Roma akiingia hapo ndani , lakini Roma kuna kitu alikiona kwenye macho ya Zonga , aliona hali ya wasiwasi.

“Rose yuko wapi na mbona leo naona hali ni kama nisivyoizoea?”

“Ndio Roma na bora hata umekuja , kwani Boss yupo kwenye hali mbaya”

“Nini kimempata Rose?” aliongea Roma kwa kushangaa huku akianza kupiga hatua kuelekea ilipo ofisi ya Rose.

“Boss yupo nyumbani kwake kajeruhiwa na risasi ya tumbo”Aliongea Zonga na kumfanya Roma ashangae na kuwa na wasiwasi pia , aligeuza na kutoka nje na kisha akaingia kwenye gari na kuipeleka mpaka ilipo nyumba ya mwanadada Rose.

Baada ya kuingia hapa ndani ,aliona kweli Rose alikuwa kwenye shida , kwani kulikuwa kimya mno , kiasi ambacho ungedhania kuwa wenyeji wamehama.

“Rose!”Aliita Roma mara baada ya kuingia kwenye sebule hii kubwa na kumkuta Rose ambaye amejilaza kwenye sofa huku akionekana kupauka kweli , ule uzuri wake ulikuwa umefifia na huyu alikuwa ni Roze anaeumwa.

“Huby!”Aliitikia Rose kwa sauti dhaifu na kumfanya Roma amuonee huruma mchepuko wake.

Roma baada ya kumsogelea , hakutaka kuongea sana alivuta juu blazia aliokuwa amevalia Rose na kuangalia jeraha la Risasi , na hapo Roma alijikuta akikumbuka siku alioingia Tanzania kwa mara ya kwanza ,alianza kukutana na Rose akiwa kwenye hali mbaya , hali ambayo ilikuwa ikifanana na hii anaiona sasa , kwani sehemu aliojeruhiwa Rose ni hio hio.

“Kwanini hujaenda hospitalini?”

“Ni jeraha la risasi , sikutaka kwenda hospitalini ingeleta shida kwa upande wangu na pia maadui zangu wangenimaliza kabla hata sijapona”

“Unamaanisha nini, mbona unaongea kama upo kwenye Vita?”Aliuliza Roma na Rose alionekana kusikia maumivu makali akongea na alijikuta akikohoa na Roma alilitambua hilo , na alichokifanya ni kumuwekea Rose mkono kwenye shavu la kulia na kushoto na palepale Rose alifumba macho , ni kama amepewa sindano ya ganzi.

Roma baada ya kuona Rose kalala , alienda mpaka jikoni na kisha akachukua kisu na kurudi nacho sebuleni, baada ya kukaa alifyonza kidole chake na kisha akamuweka Rose kwa kumlaza chali na kisha akafunua blazia na kutoa bendeji iliokuwa imeloana na damu nyingi.

Roma alichukua kisu na kuchana kiganja chake kwa kutumia kisu na damu zilianza kumtoka na hapohapo akasogeza mkono wake usawa wa jeraha la Rose na damu ile kuingia kwenye jeraha.

Ilikuwa ni kama kidonda cha Rose kilikuwa kikiungua kwa moto kwani ile sehemu ya jeraha kadiri Roma alivyokuwa akiruhusu damu kuingia , mvuke flani hivi mfano wa moshi ulianza kutoka , Roma alikata kiganja kingine na akaweka tena na mvuke ulizidi kuongezeka na ndani ya dakika tano alikuwa ashamaliza na sasa jeraha la Rose lilianza kuvutana na lilionekana kufunga taratibu na kadri dakika zilivyokuwa zikisogea ndipo jeraha lilipozidi kujifunga na ndani ya dakika kumi tu , ile sehemu iliokuwa na jeraha ilifanana na sehemu nyingine za mwili.

“Bebi Rose sasa hivi damu yako sio ya kawaida , umekuwa mtu wa kwanza kuhimili damu yangu yenye maambukizi ya kirusi kwa Zaidi ya mara mbili” .

Aliongea Roma huku akiwmangalia Rose aliekuwa amelala bila ya fahamu.

“Roma!!”Aliita Zonga aliesimama mlangoni , akimwangalia kwa hali ya wasiwasi , haikueleweka alisimama hapo kwa muda again.
 
SEHEMU YA 60

Roma Na Dorisi walipewa mapumziko ya siku mbili kabla ya kurejea kazini , hivyo Roma muda wote alibakia nyumbani , kiufupi hakukua na jambo kubwa sana ambalo lilikuwa limetokea ndani ya siku nzima.

Edna alionekana kuwa bize sana tokea Roma arudi nchini , Roma mwenyewe alishangazwa na ubize wa nke wake, Edna alikuwa akirudi usiku sana kwani alikuwa akifanya kazi Overtime,Kwa Roma hakutaka sana kumuuliza nini kinaendela kwenye kampuni mpaka mke wake kuwa bize kiasi hicho.

Siku ya ijumaa nzima Roma hakuwa ameonana na Edna , kwani ile anaamka mwanadada huyu alikuwa tayari ashaenda kazini.

Roma jambbo hili lilikuwa likimshangaza sana , hakuelewa Edna ni mwanamke wa aina gani , kwani alikuwa na pesa nyingi lakini alikuwa akifanya kazi Zaidi ya wale waliokuwa hawana hela na pia wafanyakazi wake yaani yeye ndio kama ameajiriwa.

Edna na Bi wema ni kama walikuwa wamesahau tikio la wao kuvamiwa , kwani Roma hakuwa na taarifa nalo , hakuwa akijua kama kuna watu ambao walikuja kuingia ndani ya nyumba yake, kwani hata jeshi lake hawakumpatia taarifa na Roma hakuwa ameenda kuwatembelea, alijiambia katika nafsi yake ngoja awape muda kidogo wa kufanya uchunguzi , ili akienda kuchukua ripoti iwe imeshiba.

Naam ni siku ya jumamosi,Roma aliamka vizuri na kujinyoosha na kisha alishuka kuelekea kwenye chumba cha mazoezi na ile anafika sebuleni , alikuta Bi Wema kama kawaida yake alikuwa ashaamka na sasa alikuwa akifanya usafi, na Roma alimsalimia.

“Bi Wema Edna jana alirudi?”Aliuliza Roma maana alienda kulala mapema kabla ya Edna kurudi.

“Miss jana hajarudi , alinipa taarifa kama atalala ofisini”Alijibu Roma na kushangaa.

“Bi Wema hii ya kulala ofisini imeanza juzi au ni mazoea?”.

“Ndio kuna siku hakuwa akirudi kabisa , na hii ni kama kuna jambo kubwa linaendelea ndani ya kampuni”

Alijibu Bi wema na Roma hakutaka kuongea Zaidi , licha ya kushangazwa na ufanyaji kazi wa Edna , hakujua k mke wake alikuwa akihitati kiasi gani cha pesa mpaka kuridhika , kwani kwa Roma ilikuwa ni jana tu aliweza kupata kuona taarifa ya Edna utajiri wake kuongezeka kwa dola bilioni moja kutokana na hisa za kampuni kupanda .

“Ilimradi wanajeshi wangu wapo makini na usalama wake , haina shida, ngoja afanye kazi”Alijiwazia Roma baada ya kuingia kwenye chumba cha mazoezi.

Baada ya kufanya mazoezi kwa madakika , alitoka na akaenda kuoga, kujiandaa kwa ajili ya kifungua kinywa na alitumia dakika chache tu alishuka na kukaa ,na leo hii alikuwa peke yake, kwani Bi Wema na yeye alitoa sababu za kutokunyuwa chai asubuhi hio na Roma hakujali sana , aliendelea kunywa zake chai taratibu, lakini chai ya hio ilionekana sio tamu kwake na mwenyewe alijishangaa kwanini leo hajisikii kunywa chai.

Wakati Roma anaendelea kunywa chai taratibu huku akiwa ni mwenye kukosa hamu , mara Bi Wema aliekuwa ameshikilia mfuko alionekana kushuka kutoka juu na alionekana alikuwa akitoka kwenye chumba cha Edna.

“Bi Wema mbona unaonekana kama unasafari?”Aliuliza Roma huku akimwangalia

“Nampelekea Miss chai, na baadhi ya nguo za kubadilisha,Jumamosi hakuna utaratibu wa wafanyakazi kufika kazini mpaka jumatatu”Aliongea Bi Wema na Roma alikuwa akielewa kuwa wafanyakazi wa Vexto Jumamosi walikuwa hawalazimishiwi kufika kazini na ni mara chache sana kukuta Kantini ya kampuni kuwa na wapishi siku za jumamosi.

“Bi Wema ngoja nimpelekee mimi , kwanza sina hamu ya kunywa chai leo”.Aliongea Roma na Bi Wema alitabasamu.

“Angejua nilikuwa nilikuja kumpa ampelekee asingeniomba maana ningemlazimisha”Aliwaza Bi Wema na alionekana alikuwa na mpango wake kichwani.

“Itakuwa vyema ukipeleka ndio”Aliongea Bi Wema na kisha aliandaa vitu ambavyo Roma antakiwa kwenda navyo, na ndani ya dakika kumi Roma alikuwa tayari kwa safari ya kuelekea kazini kwa mke wake huku Jasusi wa mapenzi akiwa ni mwenye kufarijika baada ya kumuona Roma akitoka na gari.

“Hivi ndio inatakiwa iwe”Aliwaza Bi Wema na kisha alirudi ndani kuendelea na majukumu yake ya kazi.

“Dakika chache mbele, Roma aliingiza gari yake sehemu ya maegesho , siku hii kweli aliona ni tofauti kwani magari yalikuwa machache mno,lakini kuna jambo moja lilimfurahisha Roma ni baada ya kuona Gari ya Chiara iliokuwa imepaki na Chiara alimuona Roma wakati anatoka na Roma alitabasamu na kutingisha kichwa kama ishara ya salamu.

“Wanajitahidi sana kumlinda Edna , nitamwambia Sauroni awaongeze mshahara”Aliwaza Roma wakati akiingia kwenye Lift.

Kampuni leo ilikuw imetulia kimya sana , ni wafanyakazi wachache sana ambao walionekana kuhudhuria siku ya leo.

Lift ilimchukua Roma mpaka Floor ya ofisi za wafanyakazi wa juu wa kampuni.

“Leo Miss Airport anaoneakana na yeye hajaja kazini”Aliwaza Roma huku akiwa na mfuko wake.

Roma hakujisumbua kugonga , alisukuma mlango na ulionekana kuwa wazi na akazama ndani , lakini alijikuta akishangaa na hii ni mara baada ya kumkuta Edna aliekuwa amejifunika na khanga , kwenye sofa akiwa amelala , Roma alishangazwa na jambbo hili na kuwaza kama mtu amechoka kwanini harudi nyumbani kulala.

Alisogea mpaka kwenye meza ya mke wake na kisha akaweka ule mfuko, na kugeuka na kutembea mpaka kwenye masofa na kumwangalia Edna alivyokuwa amelala.

“Mke wangu anaonekana mrembo Zaidi wakati akiwa amelala”Aliwaza Roma huku akivuta Khanga aliojifunika Edna na kumuweka vizuri kwani ilikuwa imeacha mwili na kuburuzika kwenye marumaru.

Roma hakutaka kumuamsha Edna , aliona ngoja amuache kwanza apumzike , na yeye alienda kukaa kwenye kiti cha mke wake.

Lakini Edna alionekana kuwa macho , kwani Roma ile anakaa kwenye kiti cha mzunguko cha mke wake ,Edna alifumbua macho na kumuangalia Roma na kisha akaendelea kulala.

Roma wakati anafungua tarakishi ya mke wake kwa ajili ya kucheza gemu , kuna karatasi juu ya faili ambalo lilikuwa pembenni , mbalo lilimvutia, alilichukua na kuanza kusoma.

Ilikuwa ni karatasi ambayo ilikuwa na majina ya kampuni za kitanzania ambazo zimezungushiwa kwa Wino , lakini sio zote, moja ya kampuni ambayo ilikuwa imezungushiwa kwa wino ilikuwa ni JR , alishangazwa na karatasi hio na kushindwa kuelewa ilikuwa ikihusu nini , hakutaka kujisumbua sana kama ilivyo kawaida yake, hakupenda kufikiria fikiria.

Edna ilionekana wakati alipokuwa peke yake alikuwa akikosa usingizi kutokana na wasiwasi , kwani kitendo cha Roma kuingia hapo ni kama ameruhusiwa , alilala muda mrefu mno kiasi kwamba hata Roma alijikuta akipitiwa na usingizi baada ya kuchoka kucheza gemu.

Mpaka inafika saa tisa na nusu bado hakuwa ameshituka,Roma alimwangalia Edna na kuishia kutabasamu , ukweli ni kwamba Roma aliona alikuwa na safari ndefu sana ya kumfahamu mke wake.

“Anaonekana hakulala usiku mzima, sijui ni kipi kinachomfanya kuwa bize kiasi cha kutolala” Aliwaza Roma na muda huohuo Edna alishituka huku akionekana ni kama alikuwa amekurupushwa.

“Wife unaonekana ulikuwa umechoka sana”Aliongea Roma huku akianza kuachama , kwani alihisi njaa.

“Saa ngapi?”Aliuliza Edna.

“Saa Tisa”Edna alijikuta akitoa macho hakujua kuwa amelala muda wote huo , alijishngaa kwani ilikuwa ni mara yake ya kwanza kulala ofisini Zaidi ya masaa sita.

“Nimepitiliza”Aliongea Edna huku akimwangalia Roma na macho yaliokuwa na usingizi bado.

“Ndio umelala sana mke wangu, yaani huwa nakushangaa Edna kwanini unafanya kazi kama huna hela”aliongea Roma lakini Edna hakutaka kumsikiliza alinyanyuka na kisha akazama kwenye mlango upande wa kulia , ulikuwa mlango wa maliwato kwani ofisi ya Edna ilikuwa imeunganishwa na choo na bafu kwa ndani.

Baada ya dakika kumi hivi kupita Edna alitoka huku akiweka nywele zake vizuri,ile chai ambayo Roma ameleta haikuwa na maana tena kwani muda ulikuwa umeenda na ilishapoa , Roma aliona jambo la maana hapo ni kutoka na Edna kwenda kupata chakula cha mchana.

“Wife nina njaa twende tukale kabla ya kwenda nyumbani”Aliongea Roma na nikama Roma alishitua njaa, na Edna alikumbuka hakuwa ameweka chochote tumboni tokea jana usiku, alimwangalia Roma na kisha akatingisha kichwa kukubali.

“Leo saa mbili nadhani hujasahau Roma”Aliongea Edna baada ya kuingia barabarani.

“Nishasahau mke wangu unaonaje ukinikumbusha”Aliongea Roma na ni kweli alikuwa ashasahau.

“Kusanyiko la wafanyabiashara ni leo , tukitoka kula unipeleke nikatafute nguo ya kuvaa maana nimesahau kuandaa”Aliongea

“Usijali mke wangu , nitaenda kukuchagulia mimi mwenywe , nguo itakayokupendeza , nataka usiku wa leo uonekane kama malkia kwa kupendeza , na hivyo ulivyomzuri mke wangu”Edna aliishia kutabasamu na kuangalia mbele.

Roma hakuwa akijua wapi asimamishe kwa ajili ya wao kupata chakula cha mchana , aliendesha taratibu , huku akiangaza macho kulia na kushoto na baada ya dakika kumi aliona sehemu ambayo ilikuwa ni nzuri kwa wao kukaa kwa ajili ya kula.

Ulikuwa ni mgahawa uliokuwa ndani ya posta , uliokuwa ukifahamika kwa jina la Rachel Dishes , ni mgahawa maarufu sana na ulikuwa umepakana na Mgahawa wa vyakula vya kichina.

Edna alipenda piam azingira ya mgahawa huo na waliangalia sehemu ambayo inawafaa kwa wao kukaa , sehemu hii ilikuwa na watu , licha ya kwamba sio wengi sana , maana muda ulikuwa umeenda.

Leo ndio ilikuwa mara ya kwanza kwa Roma kutoka na mke wake kwa ajili ya chakula tokea wafunge ndoa yao.

“Bebi unajua leo ndio siku yetu ya kwanza kutoka pamoja kama hivi kupata chakula”Aliongea Roma na Edna alimwangalia na kisha hakuongea chochote huku akiangalia chakula cha kuagiza kwenye kitabu cha orodha.

Baada ya dakika kama kumi na tano waliwekewa chakula chao na kuanza kula ,Roma alimwangalia Edna na wakakutanisha macho na Roma akatabasamu na kuendelea kula.

“Natamani maisha yangu yangekuwa hivi , ila naona kama nina safari ndefu”Aliwaza Roma.

****

Naam ni muda wa Saa mbili kamili za jioni ndani ya hoteli iliokuwa pembezoni mwa ufukwe wa Kunduchi , hoteli iliokuwa ikimilikiwa na Maple Group , hoteli ambayo ilikuwa maarufu sana ambayo ilikuwa ikifahamika kwa jina la Apple hoteli.

Hoteli hii ilikuwa imepakana na majengo mawili yaliokuwa yakifanana na yote yalikuwa yakimilikiwa na kampuni ya Maple , jengo la kulia lilikuwani la Apartment na jengo la kushoto kwake ndio ilikuwa hoteli hii nzuri ya kimataifa.

Hapa ndani ya hii hoteli ndio mahali ambapo kusanyiko la wafanyabiashara lilikuwa likifanyika na sasa ni muda wa saa mbili kamili za usiku gari za kifahari zilionekana kuingia ndani ya eneo hili kwa kupishana na kuegeshwa katika eneo maalumu,

Ni saa mbili kamili dakika kumi na tano,Gari ya kifahari aina ya Roly Royce iliingia hapa ndani na kwenda kusimama katika eneo la maegesho na baada ya gari hii kusimama, alishuka dereva ambaye alikuwa ni Roma Ramoni na kuzunguka upande wa pili na kufungua mlango na hapa ndipo alipoonekana mwanamke Mrembo sana akiingia na mwanamke huyu hakuwa mwingine bali ni Edna

Upande kulia wa jengo hili alionekana Seif Ramadhani mwanajeshi kutoka jeshi la Irani aliezamia nchini Tanzania kwa sababu ambazo hazikuwa zikifahamika , bwana huyu alionekana akiwa ndani ya jengo hili huku akiweka bunduki yake vizuri aina ya Assault Sniper Riffle Koflo 64 iliotengenezwa nchini Urusi.

Bwana seif alionekana kujiamini mno , baada ya kuweka standi ya kusapoti bunduki lake , aliweka jicho kwenye Lensi ya bunduki hii na na kuvuta pumzi kwa ishara ya ahueni.

“Target is clear in Position 12 O Clock”Alionekana alikuwa akiongea na mtu na kumwambia kuwa tageti yake inaonekana.

“Fanya haraka na kisha utoweke sehemu ya tukio”Ilisikika sauti ya upande wa pili.

Baada ya Seif kuruhusiwa , alimlenga vizuri , huku mtu aliekuwa akionekana kwenye lensi yake alikuwa ni mrembo Edna , bwana huyu alivuta pumzi nyingi na kuzizuia na kisha akazilekeza kifuani na palepale akavuta Triga na Risasi ikachomoka kuelekea ndani ya ukumbi uliokuwa ukifanyia kusanyiko.

MWISHO WA SEASON 02

UNAJUA NINI KIMETOKEA ..
ENDELEA KUTOA MCHANGO KUANZIA 2000 KUENDELEA KUNISAPOTI , UKILIPA UNATUMIWA SIMULIZI HII INBOX WATSAPP AU UNAUNGANISHWA NA GRUPU , TUKO SEHEMU YA 84 KWA SASA , UTATUMIWA VIPANDE VYOTE MPAKA TULIPOSIHIA

NAMBA ZA KULIPA NI 0687151346 AIRTEL AU 0743015453 M-PESA AU 0657195492 TIGO PESA AU 0623367345 HALOPESA JINAA ISSAI SINGANO
UKILIPA TUMA MESEII YA MUAMALA WATSAPP NAMBA NI 0687151346
 
SEHEMU YA 60

Roma Na Dorisi walipewa mapumziko ya siku mbili kabla ya kurejea kazini , hivyo Roma muda wote alibakia nyumbani , kiufupi hakukua na jambo kubwa sana ambalo lilikuwa limetokea ndani ya siku nzima.

Edna alionekana kuwa bize sana tokea Roma arudi nchini , Roma mwenyewe alishangazwa na ubize wa nke wake, Edna alikuwa akirudi usiku sana kwani alikuwa akifanya kazi Overtime,Kwa Roma hakutaka sana kumuuliza nini kinaendela kwenye kampuni mpaka mke wake kuwa bize kiasi hicho.

Siku ya ijumaa nzima Roma hakuwa ameonana na Edna , kwani ile anaamka mwanadada huyu alikuwa tayari ashaenda kazini.

Roma jambbo hili lilikuwa likimshangaza sana , hakuelewa Edna ni mwanamke wa aina gani , kwani alikuwa na pesa nyingi lakini alikuwa akifanya kazi Zaidi ya wale waliokuwa hawana hela na pia wafanyakazi wake yaani yeye ndio kama ameajiriwa.

Edna na Bi wema ni kama walikuwa wamesahau tikio la wao kuvamiwa , kwani Roma hakuwa na taarifa nalo , hakuwa akijua kama kuna watu ambao walikuja kuingia ndani ya nyumba yake, kwani hata jeshi lake hawakumpatia taarifa na Roma hakuwa ameenda kuwatembelea, alijiambia katika nafsi yake ngoja awape muda kidogo wa kufanya uchunguzi , ili akienda kuchukua ripoti iwe imeshiba.

Naam ni siku ya jumamosi,Roma aliamka vizuri na kujinyoosha na kisha alishuka kuelekea kwenye chumba cha mazoezi na ile anafika sebuleni , alikuta Bi Wema kama kawaida yake alikuwa ashaamka na sasa alikuwa akifanya usafi, na Roma alimsalimia.

“Bi Wema Edna jana alirudi?”Aliuliza Roma maana alienda kulala mapema kabla ya Edna kurudi.

“Miss jana hajarudi , alinipa taarifa kama atalala ofisini”Alijibu Roma na kushangaa.

“Bi Wema hii ya kulala ofisini imeanza juzi au ni mazoea?”.

“Ndio kuna siku hakuwa akirudi kabisa , na hii ni kama kuna jambo kubwa linaendelea ndani ya kampuni”

Alijibu Bi wema na Roma hakutaka kuongea Zaidi , licha ya kushangazwa na ufanyaji kazi wa Edna , hakujua k mke wake alikuwa akihitati kiasi gani cha pesa mpaka kuridhika , kwani kwa Roma ilikuwa ni jana tu aliweza kupata kuona taarifa ya Edna utajiri wake kuongezeka kwa dola bilioni moja kutokana na hisa za kampuni kupanda .

“Ilimradi wanajeshi wangu wapo makini na usalama wake , haina shida, ngoja afanye kazi”Alijiwazia Roma baada ya kuingia kwenye chumba cha mazoezi.

Baada ya kufanya mazoezi kwa madakika , alitoka na akaenda kuoga, kujiandaa kwa ajili ya kifungua kinywa na alitumia dakika chache tu alishuka na kukaa ,na leo hii alikuwa peke yake, kwani Bi Wema na yeye alitoa sababu za kutokunyuwa chai asubuhi hio na Roma hakujali sana , aliendelea kunywa zake chai taratibu, lakini chai ya hio ilionekana sio tamu kwake na mwenyewe alijishangaa kwanini leo hajisikii kunywa chai.

Wakati Roma anaendelea kunywa chai taratibu huku akiwa ni mwenye kukosa hamu , mara Bi Wema aliekuwa ameshikilia mfuko alionekana kushuka kutoka juu na alionekana alikuwa akitoka kwenye chumba cha Edna.

“Bi Wema mbona unaonekana kama unasafari?”Aliuliza Roma huku akimwangalia

“Nampelekea Miss chai, na baadhi ya nguo za kubadilisha,Jumamosi hakuna utaratibu wa wafanyakazi kufika kazini mpaka jumatatu”Aliongea Bi Wema na Roma alikuwa akielewa kuwa wafanyakazi wa Vexto Jumamosi walikuwa hawalazimishiwi kufika kazini na ni mara chache sana kukuta Kantini ya kampuni kuwa na wapishi siku za jumamosi.

“Bi Wema ngoja nimpelekee mimi , kwanza sina hamu ya kunywa chai leo”.Aliongea Roma na Bi Wema alitabasamu.

“Angejua nilikuwa nilikuja kumpa ampelekee asingeniomba maana ningemlazimisha”Aliwaza Bi Wema na alionekana alikuwa na mpango wake kichwani.

“Itakuwa vyema ukipeleka ndio”Aliongea Bi Wema na kisha aliandaa vitu ambavyo Roma antakiwa kwenda navyo, na ndani ya dakika kumi Roma alikuwa tayari kwa safari ya kuelekea kazini kwa mke wake huku Jasusi wa mapenzi akiwa ni mwenye kufarijika baada ya kumuona Roma akitoka na gari.

“Hivi ndio inatakiwa iwe”Aliwaza Bi Wema na kisha alirudi ndani kuendelea na majukumu yake ya kazi.

“Dakika chache mbele, Roma aliingiza gari yake sehemu ya maegesho , siku hii kweli aliona ni tofauti kwani magari yalikuwa machache mno,lakini kuna jambo moja lilimfurahisha Roma ni baada ya kuona Gari ya Chiara iliokuwa imepaki na Chiara alimuona Roma wakati anatoka na Roma alitabasamu na kutingisha kichwa kama ishara ya salamu.

“Wanajitahidi sana kumlinda Edna , nitamwambia Sauroni awaongeze mshahara”Aliwaza Roma wakati akiingia kwenye Lift.

Kampuni leo ilikuw imetulia kimya sana , ni wafanyakazi wachache sana ambao walionekana kuhudhuria siku ya leo.

Lift ilimchukua Roma mpaka Floor ya ofisi za wafanyakazi wa juu wa kampuni.

“Leo Miss Airport anaoneakana na yeye hajaja kazini”Aliwaza Roma huku akiwa na mfuko wake.

Roma hakujisumbua kugonga , alisukuma mlango na ulionekana kuwa wazi na akazama ndani , lakini alijikuta akishangaa na hii ni mara baada ya kumkuta Edna aliekuwa amejifunika na khanga , kwenye sofa akiwa amelala , Roma alishangazwa na jambbo hili na kuwaza kama mtu amechoka kwanini harudi nyumbani kulala.

Alisogea mpaka kwenye meza ya mke wake na kisha akaweka ule mfuko, na kugeuka na kutembea mpaka kwenye masofa na kumwangalia Edna alivyokuwa amelala.

“Mke wangu anaonekana mrembo Zaidi wakati akiwa amelala”Aliwaza Roma huku akivuta Khanga aliojifunika Edna na kumuweka vizuri kwani ilikuwa imeacha mwili na kuburuzika kwenye marumaru.

Roma hakutaka kumuamsha Edna , aliona ngoja amuache kwanza apumzike , na yeye alienda kukaa kwenye kiti cha mke wake.

Lakini Edna alionekana kuwa macho , kwani Roma ile anakaa kwenye kiti cha mzunguko cha mke wake ,Edna alifumbua macho na kumuangalia Roma na kisha akaendelea kulala.

Roma wakati anafungua tarakishi ya mke wake kwa ajili ya kucheza gemu , kuna karatasi juu ya faili ambalo lilikuwa pembenni , mbalo lilimvutia, alilichukua na kuanza kusoma.

Ilikuwa ni karatasi ambayo ilikuwa na majina ya kampuni za kitanzania ambazo zimezungushiwa kwa Wino , lakini sio zote, moja ya kampuni ambayo ilikuwa imezungushiwa kwa wino ilikuwa ni JR , alishangazwa na karatasi hio na kushindwa kuelewa ilikuwa ikihusu nini , hakutaka kujisumbua sana kama ilivyo kawaida yake, hakupenda kufikiria fikiria.

Edna ilionekana wakati alipokuwa peke yake alikuwa akikosa usingizi kutokana na wasiwasi , kwani kitendo cha Roma kuingia hapo ni kama ameruhusiwa , alilala muda mrefu mno kiasi kwamba hata Roma alijikuta akipitiwa na usingizi baada ya kuchoka kucheza gemu.

Mpaka inafika saa tisa na nusu bado hakuwa ameshituka,Roma alimwangalia Edna na kuishia kutabasamu , ukweli ni kwamba Roma aliona alikuwa na safari ndefu sana ya kumfahamu mke wake.

“Anaonekana hakulala usiku mzima, sijui ni kipi kinachomfanya kuwa bize kiasi cha kutolala” Aliwaza Roma na muda huohuo Edna alishituka huku akionekana ni kama alikuwa amekurupushwa.

“Wife unaonekana ulikuwa umechoka sana”Aliongea Roma huku akianza kuachama , kwani alihisi njaa.

“Saa ngapi?”Aliuliza Edna.

“Saa Tisa”Edna alijikuta akitoa macho hakujua kuwa amelala muda wote huo , alijishngaa kwani ilikuwa ni mara yake ya kwanza kulala ofisini Zaidi ya masaa sita.

“Nimepitiliza”Aliongea Edna huku akimwangalia Roma na macho yaliokuwa na usingizi bado.

“Ndio umelala sana mke wangu, yaani huwa nakushangaa Edna kwanini unafanya kazi kama huna hela”aliongea Roma lakini Edna hakutaka kumsikiliza alinyanyuka na kisha akazama kwenye mlango upande wa kulia , ulikuwa mlango wa maliwato kwani ofisi ya Edna ilikuwa imeunganishwa na choo na bafu kwa ndani.

Baada ya dakika kumi hivi kupita Edna alitoka huku akiweka nywele zake vizuri,ile chai ambayo Roma ameleta haikuwa na maana tena kwani muda ulikuwa umeenda na ilishapoa , Roma aliona jambo la maana hapo ni kutoka na Edna kwenda kupata chakula cha mchana.

“Wife nina njaa twende tukale kabla ya kwenda nyumbani”Aliongea Roma na nikama Roma alishitua njaa, na Edna alikumbuka hakuwa ameweka chochote tumboni tokea jana usiku, alimwangalia Roma na kisha akatingisha kichwa kukubali.

“Leo saa mbili nadhani hujasahau Roma”Aliongea Edna baada ya kuingia barabarani.

“Nishasahau mke wangu unaonaje ukinikumbusha”Aliongea Roma na ni kweli alikuwa ashasahau.

“Kusanyiko la wafanyabiashara ni leo , tukitoka kula unipeleke nikatafute nguo ya kuvaa maana nimesahau kuandaa”Aliongea

“Usijali mke wangu , nitaenda kukuchagulia mimi mwenywe , nguo itakayokupendeza , nataka usiku wa leo uonekane kama malkia kwa kupendeza , na hivyo ulivyomzuri mke wangu”Edna aliishia kutabasamu na kuangalia mbele.

Roma hakuwa akijua wapi asimamishe kwa ajili ya wao kupata chakula cha mchana , aliendesha taratibu , huku akiangaza macho kulia na kushoto na baada ya dakika kumi aliona sehemu ambayo ilikuwa ni nzuri kwa wao kukaa kwa ajili ya kula.

Ulikuwa ni mgahawa uliokuwa ndani ya posta , uliokuwa ukifahamika kwa jina la Rachel Dishes , ni mgahawa maarufu sana na ulikuwa umepakana na Mgahawa wa vyakula vya kichina.

Edna alipenda piam azingira ya mgahawa huo na waliangalia sehemu ambayo inawafaa kwa wao kukaa , sehemu hii ilikuwa na watu , licha ya kwamba sio wengi sana , maana muda ulikuwa umeenda.

Leo ndio ilikuwa mara ya kwanza kwa Roma kutoka na mke wake kwa ajili ya chakula tokea wafunge ndoa yao.

“Bebi unajua leo ndio siku yetu ya kwanza kutoka pamoja kama hivi kupata chakula”Aliongea Roma na Edna alimwangalia na kisha hakuongea chochote huku akiangalia chakula cha kuagiza kwenye kitabu cha orodha.

Baada ya dakika kama kumi na tano waliwekewa chakula chao na kuanza kula ,Roma alimwangalia Edna na wakakutanisha macho na Roma akatabasamu na kuendelea kula.

“Natamani maisha yangu yangekuwa hivi , ila naona kama nina safari ndefu”Aliwaza Roma.

****

Naam ni muda wa Saa mbili kamili za jioni ndani ya hoteli iliokuwa pembezoni mwa ufukwe wa Kunduchi , hoteli iliokuwa ikimilikiwa na Maple Group , hoteli ambayo ilikuwa maarufu sana ambayo ilikuwa ikifahamika kwa jina la Apple hoteli.

Hoteli hii ilikuwa imepakana na majengo mawili yaliokuwa yakifanana na yote yalikuwa yakimilikiwa na kampuni ya Maple , jengo la kulia lilikuwani la Apartment na jengo la kushoto kwake ndio ilikuwa hoteli hii nzuri ya kimataifa.

Hapa ndani ya hii hoteli ndio mahali ambapo kusanyiko la wafanyabiashara lilikuwa likifanyika na sasa ni muda wa saa mbili kamili za usiku gari za kifahari zilionekana kuingia ndani ya eneo hili kwa kupishana na kuegeshwa katika eneo maalumu,

Ni saa mbili kamili dakika kumi na tano,Gari ya kifahari aina ya Roly Royce iliingia hapa ndani na kwenda kusimama katika eneo la maegesho na baada ya gari hii kusimama, alishuka dereva ambaye alikuwa ni Roma Ramoni na kuzunguka upande wa pili na kufungua mlango na hapa ndipo alipoonekana mwanamke Mrembo sana akiingia na mwanamke huyu hakuwa mwingine bali ni Edna

Upande kulia wa jengo hili alionekana Seif Ramadhani mwanajeshi kutoka jeshi la Irani aliezamia nchini Tanzania kwa sababu ambazo hazikuwa zikifahamika , bwana huyu alionekana akiwa ndani ya jengo hili huku akiweka bunduki yake vizuri aina ya Assault Sniper Riffle Koflo 64 iliotengenezwa nchini Urusi.

Bwana seif alionekana kujiamini mno , baada ya kuweka standi ya kusapoti bunduki lake , aliweka jicho kwenye Lensi ya bunduki hii na na kuvuta pumzi kwa ishara ya ahueni.

“Target is clear in Position 12 O Clock”Alionekana alikuwa akiongea na mtu na kumwambia kuwa tageti yake inaonekana.

“Fanya haraka na kisha utoweke sehemu ya tukio”Ilisikika sauti ya upande wa pili.

Baada ya Seif kuruhusiwa , alimlenga vizuri , huku mtu aliekuwa akionekana kwenye lensi yake alikuwa ni mrembo Edna , bwana huyu alivuta pumzi nyingi na kuzizuia na kisha akazilekeza kifuani na palepale akavuta Triga na Risasi ikachomoka kuelekea ndani ya ukumbi uliokuwa ukifanyia kusanyiko.

MWISHO WA SEASON 02

UNAJUA NINI KIMETOKEA ..
ENDELEA KUTOA MCHANGO KUANZIA 2000 KUENDELEA KUNISAPOTI , UKILIPA UNATUMIWA SIMULIZI HII INBOX WATSAPP AU UNAUNGANISHWA NA GRUPU , TUKO SEHEMU YA 84 KWA SASA , UTATUMIWA VIPANDE VYOTE MPAKA TULIPOSIHIA

NAMBA ZA KULIPA NI 0687151346 AIRTEL AU 0743015453 M-PESA AU 0657195492 TIGO PESA AU 0623367345 HALOPESA JINAA ISSAI SINGANO
UKILIPA TUMA MESEII YA MUAMALA WATSAPP NAMBA NI 0687151346
Jaman imeishia patamu hivi pls kimoja tu[emoji120][emoji120]
 
Back
Top Bottom