Mchenjeuke
Member
- Mar 16, 2014
- 45
- 18
Tunakushukuru singano
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Not yet , Bdo vipande kumi sita ifike tamatihivi sezoni 3 imeisha yote
Namkubali sana Issai ila tumuunge mkono Kwa kamchangomkuu BIG UP! kazi nzuri
Shukrani mkuuMkuu singanojr kazi nzuri na imetulia sana kwakweli nakupongeza mkuu.umedadavua mengi ambayo hapo katika ulimwengu wetu huu. Wafanyabiasha na Wanasiasa imewaweka wazi aisee.
Shukrani mkuuNamkubali sana Issai ila tumuunge mkono Kwa kamchango
Movies ambazo zinazohusiana na Greek God's zipoHii habari ya Roma naitaja Kwa mtindo wa movie. Issai inapatikana hii??
Soft copy au
Duuuh imeishia patamu balaaa aseeeeSEHEMU YA 60
Roma Na Dorisi walipewa mapumziko ya siku mbili kabla ya kurejea kazini , hivyo Roma muda wote alibakia nyumbani , kiufupi hakukua na jambo kubwa sana ambalo lilikuwa limetokea ndani ya siku nzima.
Edna alionekana kuwa bize sana tokea Roma arudi nchini , Roma mwenyewe alishangazwa na ubize wa nke wake, Edna alikuwa akirudi usiku sana kwani alikuwa akifanya kazi Overtime,Kwa Roma hakutaka sana kumuuliza nini kinaendela kwenye kampuni mpaka mke wake kuwa bize kiasi hicho.
Siku ya ijumaa nzima Roma hakuwa ameonana na Edna , kwani ile anaamka mwanadada huyu alikuwa tayari ashaenda kazini.
Roma jambbo hili lilikuwa likimshangaza sana , hakuelewa Edna ni mwanamke wa aina gani , kwani alikuwa na pesa nyingi lakini alikuwa akifanya kazi Zaidi ya wale waliokuwa hawana hela na pia wafanyakazi wake yaani yeye ndio kama ameajiriwa.
Edna na Bi wema ni kama walikuwa wamesahau tikio la wao kuvamiwa , kwani Roma hakuwa na taarifa nalo , hakuwa akijua kama kuna watu ambao walikuja kuingia ndani ya nyumba yake, kwani hata jeshi lake hawakumpatia taarifa na Roma hakuwa ameenda kuwatembelea, alijiambia katika nafsi yake ngoja awape muda kidogo wa kufanya uchunguzi , ili akienda kuchukua ripoti iwe imeshiba.
Naam ni siku ya jumamosi,Roma aliamka vizuri na kujinyoosha na kisha alishuka kuelekea kwenye chumba cha mazoezi na ile anafika sebuleni , alikuta Bi Wema kama kawaida yake alikuwa ashaamka na sasa alikuwa akifanya usafi, na Roma alimsalimia.
“Bi Wema Edna jana alirudi?”Aliuliza Roma maana alienda kulala mapema kabla ya Edna kurudi.
“Miss jana hajarudi , alinipa taarifa kama atalala ofisini”Alijibu Roma na kushangaa.
“Bi Wema hii ya kulala ofisini imeanza juzi au ni mazoea?”.
“Ndio kuna siku hakuwa akirudi kabisa , na hii ni kama kuna jambo kubwa linaendelea ndani ya kampuni”
Alijibu Bi wema na Roma hakutaka kuongea Zaidi , licha ya kushangazwa na ufanyaji kazi wa Edna , hakujua k mke wake alikuwa akihitati kiasi gani cha pesa mpaka kuridhika , kwani kwa Roma ilikuwa ni jana tu aliweza kupata kuona taarifa ya Edna utajiri wake kuongezeka kwa dola bilioni moja kutokana na hisa za kampuni kupanda .
“Ilimradi wanajeshi wangu wapo makini na usalama wake , haina shida, ngoja afanye kazi”Alijiwazia Roma baada ya kuingia kwenye chumba cha mazoezi.
Baada ya kufanya mazoezi kwa madakika , alitoka na akaenda kuoga, kujiandaa kwa ajili ya kifungua kinywa na alitumia dakika chache tu alishuka na kukaa ,na leo hii alikuwa peke yake, kwani Bi Wema na yeye alitoa sababu za kutokunyuwa chai asubuhi hio na Roma hakujali sana , aliendelea kunywa zake chai taratibu, lakini chai ya hio ilionekana sio tamu kwake na mwenyewe alijishangaa kwanini leo hajisikii kunywa chai.
Wakati Roma anaendelea kunywa chai taratibu huku akiwa ni mwenye kukosa hamu , mara Bi Wema aliekuwa ameshikilia mfuko alionekana kushuka kutoka juu na alionekana alikuwa akitoka kwenye chumba cha Edna.
“Bi Wema mbona unaonekana kama unasafari?”Aliuliza Roma huku akimwangalia
“Nampelekea Miss chai, na baadhi ya nguo za kubadilisha,Jumamosi hakuna utaratibu wa wafanyakazi kufika kazini mpaka jumatatu”Aliongea Bi Wema na Roma alikuwa akielewa kuwa wafanyakazi wa Vexto Jumamosi walikuwa hawalazimishiwi kufika kazini na ni mara chache sana kukuta Kantini ya kampuni kuwa na wapishi siku za jumamosi.
“Bi Wema ngoja nimpelekee mimi , kwanza sina hamu ya kunywa chai leo”.Aliongea Roma na Bi Wema alitabasamu.
“Angejua nilikuwa nilikuja kumpa ampelekee asingeniomba maana ningemlazimisha”Aliwaza Bi Wema na alionekana alikuwa na mpango wake kichwani.
“Itakuwa vyema ukipeleka ndio”Aliongea Bi Wema na kisha aliandaa vitu ambavyo Roma antakiwa kwenda navyo, na ndani ya dakika kumi Roma alikuwa tayari kwa safari ya kuelekea kazini kwa mke wake huku Jasusi wa mapenzi akiwa ni mwenye kufarijika baada ya kumuona Roma akitoka na gari.
“Hivi ndio inatakiwa iwe”Aliwaza Bi Wema na kisha alirudi ndani kuendelea na majukumu yake ya kazi.
“Dakika chache mbele, Roma aliingiza gari yake sehemu ya maegesho , siku hii kweli aliona ni tofauti kwani magari yalikuwa machache mno,lakini kuna jambo moja lilimfurahisha Roma ni baada ya kuona Gari ya Chiara iliokuwa imepaki na Chiara alimuona Roma wakati anatoka na Roma alitabasamu na kutingisha kichwa kama ishara ya salamu.
“Wanajitahidi sana kumlinda Edna , nitamwambia Sauroni awaongeze mshahara”Aliwaza Roma wakati akiingia kwenye Lift.
Kampuni leo ilikuw imetulia kimya sana , ni wafanyakazi wachache sana ambao walionekana kuhudhuria siku ya leo.
Lift ilimchukua Roma mpaka Floor ya ofisi za wafanyakazi wa juu wa kampuni.
“Leo Miss Airport anaoneakana na yeye hajaja kazini”Aliwaza Roma huku akiwa na mfuko wake.
Roma hakujisumbua kugonga , alisukuma mlango na ulionekana kuwa wazi na akazama ndani , lakini alijikuta akishangaa na hii ni mara baada ya kumkuta Edna aliekuwa amejifunika na khanga , kwenye sofa akiwa amelala , Roma alishangazwa na jambbo hili na kuwaza kama mtu amechoka kwanini harudi nyumbani kulala.
Alisogea mpaka kwenye meza ya mke wake na kisha akaweka ule mfuko, na kugeuka na kutembea mpaka kwenye masofa na kumwangalia Edna alivyokuwa amelala.
“Mke wangu anaonekana mrembo Zaidi wakati akiwa amelala”Aliwaza Roma huku akivuta Khanga aliojifunika Edna na kumuweka vizuri kwani ilikuwa imeacha mwili na kuburuzika kwenye marumaru.
Roma hakutaka kumuamsha Edna , aliona ngoja amuache kwanza apumzike , na yeye alienda kukaa kwenye kiti cha mke wake.
Lakini Edna alionekana kuwa macho , kwani Roma ile anakaa kwenye kiti cha mzunguko cha mke wake ,Edna alifumbua macho na kumuangalia Roma na kisha akaendelea kulala.
Roma wakati anafungua tarakishi ya mke wake kwa ajili ya kucheza gemu , kuna karatasi juu ya faili ambalo lilikuwa pembenni , mbalo lilimvutia, alilichukua na kuanza kusoma.
Ilikuwa ni karatasi ambayo ilikuwa na majina ya kampuni za kitanzania ambazo zimezungushiwa kwa Wino , lakini sio zote, moja ya kampuni ambayo ilikuwa imezungushiwa kwa wino ilikuwa ni JR , alishangazwa na karatasi hio na kushindwa kuelewa ilikuwa ikihusu nini , hakutaka kujisumbua sana kama ilivyo kawaida yake, hakupenda kufikiria fikiria.
Edna ilionekana wakati alipokuwa peke yake alikuwa akikosa usingizi kutokana na wasiwasi , kwani kitendo cha Roma kuingia hapo ni kama ameruhusiwa , alilala muda mrefu mno kiasi kwamba hata Roma alijikuta akipitiwa na usingizi baada ya kuchoka kucheza gemu.
Mpaka inafika saa tisa na nusu bado hakuwa ameshituka,Roma alimwangalia Edna na kuishia kutabasamu , ukweli ni kwamba Roma aliona alikuwa na safari ndefu sana ya kumfahamu mke wake.
“Anaonekana hakulala usiku mzima, sijui ni kipi kinachomfanya kuwa bize kiasi cha kutolala” Aliwaza Roma na muda huohuo Edna alishituka huku akionekana ni kama alikuwa amekurupushwa.
“Wife unaonekana ulikuwa umechoka sana”Aliongea Roma huku akianza kuachama , kwani alihisi njaa.
“Saa ngapi?”Aliuliza Edna.
“Saa Tisa”Edna alijikuta akitoa macho hakujua kuwa amelala muda wote huo , alijishngaa kwani ilikuwa ni mara yake ya kwanza kulala ofisini Zaidi ya masaa sita.
“Nimepitiliza”Aliongea Edna huku akimwangalia Roma na macho yaliokuwa na usingizi bado.
“Ndio umelala sana mke wangu, yaani huwa nakushangaa Edna kwanini unafanya kazi kama huna hela”aliongea Roma lakini Edna hakutaka kumsikiliza alinyanyuka na kisha akazama kwenye mlango upande wa kulia , ulikuwa mlango wa maliwato kwani ofisi ya Edna ilikuwa imeunganishwa na choo na bafu kwa ndani.
Baada ya dakika kumi hivi kupita Edna alitoka huku akiweka nywele zake vizuri,ile chai ambayo Roma ameleta haikuwa na maana tena kwani muda ulikuwa umeenda na ilishapoa , Roma aliona jambo la maana hapo ni kutoka na Edna kwenda kupata chakula cha mchana.
“Wife nina njaa twende tukale kabla ya kwenda nyumbani”Aliongea Roma na nikama Roma alishitua njaa, na Edna alikumbuka hakuwa ameweka chochote tumboni tokea jana usiku, alimwangalia Roma na kisha akatingisha kichwa kukubali.
“Leo saa mbili nadhani hujasahau Roma”Aliongea Edna baada ya kuingia barabarani.
“Nishasahau mke wangu unaonaje ukinikumbusha”Aliongea Roma na ni kweli alikuwa ashasahau.
“Kusanyiko la wafanyabiashara ni leo , tukitoka kula unipeleke nikatafute nguo ya kuvaa maana nimesahau kuandaa”Aliongea
“Usijali mke wangu , nitaenda kukuchagulia mimi mwenywe , nguo itakayokupendeza , nataka usiku wa leo uonekane kama malkia kwa kupendeza , na hivyo ulivyomzuri mke wangu”Edna aliishia kutabasamu na kuangalia mbele.
Roma hakuwa akijua wapi asimamishe kwa ajili ya wao kupata chakula cha mchana , aliendesha taratibu , huku akiangaza macho kulia na kushoto na baada ya dakika kumi aliona sehemu ambayo ilikuwa ni nzuri kwa wao kukaa kwa ajili ya kula.
Ulikuwa ni mgahawa uliokuwa ndani ya posta , uliokuwa ukifahamika kwa jina la Rachel Dishes , ni mgahawa maarufu sana na ulikuwa umepakana na Mgahawa wa vyakula vya kichina.
Edna alipenda piam azingira ya mgahawa huo na waliangalia sehemu ambayo inawafaa kwa wao kukaa , sehemu hii ilikuwa na watu , licha ya kwamba sio wengi sana , maana muda ulikuwa umeenda.
Leo ndio ilikuwa mara ya kwanza kwa Roma kutoka na mke wake kwa ajili ya chakula tokea wafunge ndoa yao.
“Bebi unajua leo ndio siku yetu ya kwanza kutoka pamoja kama hivi kupata chakula”Aliongea Roma na Edna alimwangalia na kisha hakuongea chochote huku akiangalia chakula cha kuagiza kwenye kitabu cha orodha.
Baada ya dakika kama kumi na tano waliwekewa chakula chao na kuanza kula ,Roma alimwangalia Edna na wakakutanisha macho na Roma akatabasamu na kuendelea kula.
“Natamani maisha yangu yangekuwa hivi , ila naona kama nina safari ndefu”Aliwaza Roma.
****
Naam ni muda wa Saa mbili kamili za jioni ndani ya hoteli iliokuwa pembezoni mwa ufukwe wa Kunduchi , hoteli iliokuwa ikimilikiwa na Maple Group , hoteli ambayo ilikuwa maarufu sana ambayo ilikuwa ikifahamika kwa jina la Apple hoteli.
Hoteli hii ilikuwa imepakana na majengo mawili yaliokuwa yakifanana na yote yalikuwa yakimilikiwa na kampuni ya Maple , jengo la kulia lilikuwani la Apartment na jengo la kushoto kwake ndio ilikuwa hoteli hii nzuri ya kimataifa.
Hapa ndani ya hii hoteli ndio mahali ambapo kusanyiko la wafanyabiashara lilikuwa likifanyika na sasa ni muda wa saa mbili kamili za usiku gari za kifahari zilionekana kuingia ndani ya eneo hili kwa kupishana na kuegeshwa katika eneo maalumu,
Ni saa mbili kamili dakika kumi na tano,Gari ya kifahari aina ya Roly Royce iliingia hapa ndani na kwenda kusimama katika eneo la maegesho na baada ya gari hii kusimama, alishuka dereva ambaye alikuwa ni Roma Ramoni na kuzunguka upande wa pili na kufungua mlango na hapa ndipo alipoonekana mwanamke Mrembo sana akiingia na mwanamke huyu hakuwa mwingine bali ni Edna
Upande kulia wa jengo hili alionekana Seif Ramadhani mwanajeshi kutoka jeshi la Irani aliezamia nchini Tanzania kwa sababu ambazo hazikuwa zikifahamika , bwana huyu alionekana akiwa ndani ya jengo hili huku akiweka bunduki yake vizuri aina ya Assault Sniper Riffle Koflo 64 iliotengenezwa nchini Urusi.
Bwana seif alionekana kujiamini mno , baada ya kuweka standi ya kusapoti bunduki lake , aliweka jicho kwenye Lensi ya bunduki hii na na kuvuta pumzi kwa ishara ya ahueni.
“Target is clear in Position 12 O Clock”Alionekana alikuwa akiongea na mtu na kumwambia kuwa tageti yake inaonekana.
“Fanya haraka na kisha utoweke sehemu ya tukio”Ilisikika sauti ya upande wa pili.
Baada ya Seif kuruhusiwa , alimlenga vizuri , huku mtu aliekuwa akionekana kwenye lensi yake alikuwa ni mrembo Edna , bwana huyu alivuta pumzi nyingi na kuzizuia na kisha akazilekeza kifuani na palepale akavuta Triga na Risasi ikachomoka kuelekea ndani ya ukumbi uliokuwa ukifanyia kusanyiko.
MWISHO WA SEASON 02
UNAJUA NINI KIMETOKEA ..
ENDELEA KUTOA MCHANGO KUANZIA 2000 KUENDELEA KUNISAPOTI , UKILIPA UNATUMIWA SIMULIZI HII INBOX WATSAPP AU UNAUNGANISHWA NA GRUPU , TUKO SEHEMU YA 84 KWA SASA , UTATUMIWA VIPANDE VYOTE MPAKA TULIPOSIHIA
NAMBA ZA KULIPA NI 0687151346 AIRTEL AU 0743015453 M-PESA AU 0657195492 TIGO PESA AU 0623367345 HALOPESA JINAA ISSAI SINGANO
UKILIPA TUMA MESEII YA MUAMALA WATSAPP NAMBA NI 0687151346
muendelezo lini ndugu ?
Leo jioni nitawawekea vipande viwili hapamuendelezo lini ndugu ?
Poa poa twasubilia
Fanya hata vitatu kamanda