Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #81
SEHEMU YA 70
"No. Usihofu kabisa, nakuhakikishia hii ndiyo njia salama ya kupata mzigo huo, unakumbuka kilichotokea Msumbuji na Congo? sasa una shaka gani?", Enock Jonson alihoji.
Baada ya majadiliano ya muda mrefu, hatimaye kikao kiliafiki kuwa, Hawa na Tony watoshwe. Carlos Dimera alipewa taarifa ya siri kuhusu mwafaka huo, akautafakari msimamo huo. Lakini hakuwa tayari kuutekeleza
Hali ya utulivu katika Jiji la Dar es Salaam, kiasi fulani ilikuwa imetoweka, Gabriel na George waliokuwa wamehitimu vizuri mafunzo ya ujasusi, katika nchi mbalimbali duniani, waliingia katika mitaa ya Jiji la Dar es Salaam kwa kazi moja tu, kumsaka Teacher. Majasusi hawa wakiendesha magari mawili tofauti, mmoja akiendesha Toyota Brevis yenye rangi ya Blue, mwingine alikuwa ndani ya Toyota Verosa yenye rangi ya Zambarau. Carlos Dimera aliuamini sana utendaji kazi wa vijana hawa, akasubiri kuona nini matokeo.
.
Mfano wa panya wa Suwa, wenye uwezo mkubwa wa kunusa na kutegua mabomu ardhini, majasusi hawa Gabriel na George, walianza kunusa harufu. Wakitumia mtambo maalumu wa kunasa mawasiliano, hatmaye walifanikiwa kuingilia mawasiliano ya Teacher, mara tu baada ya kuipata namba yake ya kiganjani. Mtambo huo maalumu uliweza kuonyesha mnara unaotumika kwa mawasiliano ya Teacher, baada ya kufanikiwa kuupata mnara huo, kazi ya majasusi hawa, ilikuwa kufuatilia uelekeo wa mahali mnara huo ulipo.
Carlos Dimera, alikuwa amewaeleza majasusi hawa kila kitu kuhusu Teacher, aliwaeleza jinsi Teacher alivyo mwepesi na mjanja wa kubaini mambo. Dimera alimwelezea Teacher kuwa ni mtu mwenye hisia kali katika tasnia hiyo. Hivyo aliwayaka walijiweka vizuri mara mia zaidi kwa ajili ya mapambano. iwapo hali hiyo itatokea.
Hatmaye mtambo ukawafikisha Kinyerezi, kila wanapotafuta uelekeo, mtambo nao unaonyesha mshale wa mawasiliano ya simu husika. kila waliposogea mlio fulani ulisikika ndani ya mtambo huo, kuashiria uelekeo ulikuwa sahihi. Hatmaye wakaifikia Hotel Bella, iliyoko Kinyerezi, nje kabisa ya Jiji la Dar es Salaam, eneo ambalo dakika chache zilizopita Teacher alikuwa amewasiliana na watu kadhaa. Majasusi hawa waliamini kuwa Teacher atakuwa amekia hotelini hapo kwa vile katika eneo hilo, hakukuwa na Hotel nyingine. wakajiweka sawa, wakapanga kuivamia.
Ukweli ni kwamba, baada ya Teacher kufanikiwa kuwaburuta mahakamani, Hawa na Tony, alikubaliana na wenzake Fred, Claud na Nyawaminza, kila mmoja apumzishe akili sehemu aliyoona inamfaa, wakisubiri mahakama kutoa hukumu dhidi ya watuhumiwa wa dawa za kulevya, Hawa na Tony. Akatafuta sehemu nzuri ya kupumzisha akili, sehemu ambayo si rahisi adui kuifikia, akajihifadhi Hotel Bella, kwa ajili ya usiku mmoja wa leo, akiisubiri kesho.
Kwa vile Hoteli Bella iko karibu na mitambo ya umeme wa ges ya SONGAS, baada ya majasusi hawa kufanya utafiti kuhusu eneo hilo, waliingia Hotelini hapo mmoja baada ya mwingine, wakikodi vyumba
"No. Usihofu kabisa, nakuhakikishia hii ndiyo njia salama ya kupata mzigo huo, unakumbuka kilichotokea Msumbuji na Congo? sasa una shaka gani?", Enock Jonson alihoji.
Baada ya majadiliano ya muda mrefu, hatimaye kikao kiliafiki kuwa, Hawa na Tony watoshwe. Carlos Dimera alipewa taarifa ya siri kuhusu mwafaka huo, akautafakari msimamo huo. Lakini hakuwa tayari kuutekeleza
Hali ya utulivu katika Jiji la Dar es Salaam, kiasi fulani ilikuwa imetoweka, Gabriel na George waliokuwa wamehitimu vizuri mafunzo ya ujasusi, katika nchi mbalimbali duniani, waliingia katika mitaa ya Jiji la Dar es Salaam kwa kazi moja tu, kumsaka Teacher. Majasusi hawa wakiendesha magari mawili tofauti, mmoja akiendesha Toyota Brevis yenye rangi ya Blue, mwingine alikuwa ndani ya Toyota Verosa yenye rangi ya Zambarau. Carlos Dimera aliuamini sana utendaji kazi wa vijana hawa, akasubiri kuona nini matokeo.
.
Mfano wa panya wa Suwa, wenye uwezo mkubwa wa kunusa na kutegua mabomu ardhini, majasusi hawa Gabriel na George, walianza kunusa harufu. Wakitumia mtambo maalumu wa kunasa mawasiliano, hatmaye walifanikiwa kuingilia mawasiliano ya Teacher, mara tu baada ya kuipata namba yake ya kiganjani. Mtambo huo maalumu uliweza kuonyesha mnara unaotumika kwa mawasiliano ya Teacher, baada ya kufanikiwa kuupata mnara huo, kazi ya majasusi hawa, ilikuwa kufuatilia uelekeo wa mahali mnara huo ulipo.
Carlos Dimera, alikuwa amewaeleza majasusi hawa kila kitu kuhusu Teacher, aliwaeleza jinsi Teacher alivyo mwepesi na mjanja wa kubaini mambo. Dimera alimwelezea Teacher kuwa ni mtu mwenye hisia kali katika tasnia hiyo. Hivyo aliwayaka walijiweka vizuri mara mia zaidi kwa ajili ya mapambano. iwapo hali hiyo itatokea.
Hatmaye mtambo ukawafikisha Kinyerezi, kila wanapotafuta uelekeo, mtambo nao unaonyesha mshale wa mawasiliano ya simu husika. kila waliposogea mlio fulani ulisikika ndani ya mtambo huo, kuashiria uelekeo ulikuwa sahihi. Hatmaye wakaifikia Hotel Bella, iliyoko Kinyerezi, nje kabisa ya Jiji la Dar es Salaam, eneo ambalo dakika chache zilizopita Teacher alikuwa amewasiliana na watu kadhaa. Majasusi hawa waliamini kuwa Teacher atakuwa amekia hotelini hapo kwa vile katika eneo hilo, hakukuwa na Hotel nyingine. wakajiweka sawa, wakapanga kuivamia.
Ukweli ni kwamba, baada ya Teacher kufanikiwa kuwaburuta mahakamani, Hawa na Tony, alikubaliana na wenzake Fred, Claud na Nyawaminza, kila mmoja apumzishe akili sehemu aliyoona inamfaa, wakisubiri mahakama kutoa hukumu dhidi ya watuhumiwa wa dawa za kulevya, Hawa na Tony. Akatafuta sehemu nzuri ya kupumzisha akili, sehemu ambayo si rahisi adui kuifikia, akajihifadhi Hotel Bella, kwa ajili ya usiku mmoja wa leo, akiisubiri kesho.
Kwa vile Hoteli Bella iko karibu na mitambo ya umeme wa ges ya SONGAS, baada ya majasusi hawa kufanya utafiti kuhusu eneo hilo, waliingia Hotelini hapo mmoja baada ya mwingine, wakikodi vyumba