Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #101
SEHEMU YA 85
Shamla shamla ziliendelea mitaani. ulikuwa ushindi mkubwa kwa Serikali. Lakini ghafla habari hii ikagauka msiba. Masaa kadhaa baada ya hukumu, taarifa zikaenea kuwa Hakimu aliyesikiliza kesi hiyo na kutoa hukumu amepigwa risasi na kuuawa ofisini kwake. Hofu ikatawala. Wakati viongozi wakitafakari kuhusu tukio hili. Habari nyingine inasambaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa, askari kadhaa wameuawa na wengine kujeruhiwa vibaya baada ya kutokea mapigano makali wakati wakisindikiza wafungwa.
Taarifa hii ilieleza kuwa wafungwa wawili waliotuhumiwa kuingiza dawa za kulevya nchini, Hawa Msimbazi na Tony Sime, waliokuwa wakipelekwa katika gereza moja Jijini Dar es Salaam wametoroshwa wakiwa wakiwa chini ya ulinzi mkali wa polisi. Wananchi wakapatwa na masikitiko, Mzee mmoja wa makamo aliposikia taarifa hizi kwenye vyombo vya habari alitoa machozi.
.
Habari zinamfikia Kanali Beny Emilly, anashindwa kuyaamini masikio yake, anasimama sekunde kadhaa mbele ya kiti chake, hofu inamwingia, anajaribu kwa mara nyingine kuinua simu yake ya kiganjani kuwasiliana na Teacher. Bahati mbaya simu hiyo haipatikani anaelekea kuchanganyikiwa, furaha yake inageuka kalaha, machozi yanamlengalenga.
"Nini hii?", Kanali Emilly anajiuliza wakati akielekea nje ya ofisi yake.
Taarifa hii inawafikia wakubwa wa nchi, vikao vya dharura vinakaa. "Nini kumetokea", anahoji mkuu wa nchi. "Hili haliwezekani katika nchi hii", anasisitiza bila kupata majibu. Wasaidizi wake wanajaribu kueleza msimamo.
Simu zinapigwa huku na huko bila mafanikio, "Nani hasa wameshiriki katika tukio hili", Kanali Emilly anajiuliza kwa mara nyingine.
*************************************
Nilijaribu bila mafanikio kutambua wapi tulipofichwa. Tulikuwa tumesimamishwa mbele ya watu hawa huku mikono na miguu yetu ikiwa imefungwa barabara kwa kamba ngumu. Pamoja na mazoezi makali ninayofanya karibu kila siku, lakini hapa niliyasikia maumivu kutokana na staili iliyotumika kutufunga hizi kamba. Ukweli hata uwe na mazoezi kiasi gani kwa mtindo huu lazima utasikia maumivu.
Wote watatu tulifungwa kwa mtindo mmoja, yaani miguu yetu ikiwa imefungwa kamba, mikono nayo ikiwa imefungwa vizuri kwa nyuma halafu kamba hizo zimevutwa na kufungwa sehemu ya juu. Kwa maana hiyo mikono yetu ilivutwa nyuma ikaangalia juu na kutusababishia maumivu makali sana.
Kelele za mashine na baadhi ya watu zilisikika, hali hii ilinifanya nikabaini kuwa eneo hili lilikuwa la viwanda. Niliwaza na kujiuliza mambo mengi, nilimuomba mungu angalao awanusuru wenzangu Julius Nyawaminza na Claud Mwita ili mimi nichukue nafasi yao.
Nilijilaumu kwa kuweka tahadhali ndogo wakati naingia pale hotelini, hata hivyo sikupaswa kulaumu sana maana tayari nilikuwa katika mikono ya mauti. Hasira na chuki kwa watu hawa zilinijia, nikatamani kufanya miujiza lakini sikuweza tena.
Shamla shamla ziliendelea mitaani. ulikuwa ushindi mkubwa kwa Serikali. Lakini ghafla habari hii ikagauka msiba. Masaa kadhaa baada ya hukumu, taarifa zikaenea kuwa Hakimu aliyesikiliza kesi hiyo na kutoa hukumu amepigwa risasi na kuuawa ofisini kwake. Hofu ikatawala. Wakati viongozi wakitafakari kuhusu tukio hili. Habari nyingine inasambaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa, askari kadhaa wameuawa na wengine kujeruhiwa vibaya baada ya kutokea mapigano makali wakati wakisindikiza wafungwa.
Taarifa hii ilieleza kuwa wafungwa wawili waliotuhumiwa kuingiza dawa za kulevya nchini, Hawa Msimbazi na Tony Sime, waliokuwa wakipelekwa katika gereza moja Jijini Dar es Salaam wametoroshwa wakiwa wakiwa chini ya ulinzi mkali wa polisi. Wananchi wakapatwa na masikitiko, Mzee mmoja wa makamo aliposikia taarifa hizi kwenye vyombo vya habari alitoa machozi.
.
Habari zinamfikia Kanali Beny Emilly, anashindwa kuyaamini masikio yake, anasimama sekunde kadhaa mbele ya kiti chake, hofu inamwingia, anajaribu kwa mara nyingine kuinua simu yake ya kiganjani kuwasiliana na Teacher. Bahati mbaya simu hiyo haipatikani anaelekea kuchanganyikiwa, furaha yake inageuka kalaha, machozi yanamlengalenga.
"Nini hii?", Kanali Emilly anajiuliza wakati akielekea nje ya ofisi yake.
Taarifa hii inawafikia wakubwa wa nchi, vikao vya dharura vinakaa. "Nini kumetokea", anahoji mkuu wa nchi. "Hili haliwezekani katika nchi hii", anasisitiza bila kupata majibu. Wasaidizi wake wanajaribu kueleza msimamo.
Simu zinapigwa huku na huko bila mafanikio, "Nani hasa wameshiriki katika tukio hili", Kanali Emilly anajiuliza kwa mara nyingine.
*************************************
Nilijaribu bila mafanikio kutambua wapi tulipofichwa. Tulikuwa tumesimamishwa mbele ya watu hawa huku mikono na miguu yetu ikiwa imefungwa barabara kwa kamba ngumu. Pamoja na mazoezi makali ninayofanya karibu kila siku, lakini hapa niliyasikia maumivu kutokana na staili iliyotumika kutufunga hizi kamba. Ukweli hata uwe na mazoezi kiasi gani kwa mtindo huu lazima utasikia maumivu.
Wote watatu tulifungwa kwa mtindo mmoja, yaani miguu yetu ikiwa imefungwa kamba, mikono nayo ikiwa imefungwa vizuri kwa nyuma halafu kamba hizo zimevutwa na kufungwa sehemu ya juu. Kwa maana hiyo mikono yetu ilivutwa nyuma ikaangalia juu na kutusababishia maumivu makali sana.
Kelele za mashine na baadhi ya watu zilisikika, hali hii ilinifanya nikabaini kuwa eneo hili lilikuwa la viwanda. Niliwaza na kujiuliza mambo mengi, nilimuomba mungu angalao awanusuru wenzangu Julius Nyawaminza na Claud Mwita ili mimi nichukue nafasi yao.
Nilijilaumu kwa kuweka tahadhali ndogo wakati naingia pale hotelini, hata hivyo sikupaswa kulaumu sana maana tayari nilikuwa katika mikono ya mauti. Hasira na chuki kwa watu hawa zilinijia, nikatamani kufanya miujiza lakini sikuweza tena.