Simulizi ya kijasusi: Shetani Rudisha akili zetu na mke wangu

Simulizi ya kijasusi: Shetani Rudisha akili zetu na mke wangu

SHETANI RUDISHA AKILI ZETU
MTUNZI:SINGANOJR

SEHEMU YA 60.
Hamza akiwa ndani ya gari na Dina alimwambia kile ambacho kimetokea mpaka namna alivyojiandikisha na Regina na kuwa wanandoa kisheria.
Ijapokuwa Dina alikuwa mtulivu wakati wa kumsikiliza Hamza , lakini mara baada ya kusikia Hamza alikuwa amesajili ndoa na mwanamke mwingine alijikuta akishikwa na huzuni.
Lakini hata hivyo aliona haiwezekani yeye kuja kuwa mke wa Hamza kwani hakuwa na vigezo hivyo.
“Kwahio kwanzia sasa utakuwa chini ya ulinzi wa mke wako na kuwa ngumu kwetu kuonana , sijui mimi Dina nimekosea wapi katika ulimwengu huu”Aliongea na kumfanya Hamza asijue alie au acheke.
“Hapo ndio unapokosea , kasema licha ya kuandikisha ndoa niharakishe kutafuta mwanamke na ataachana na mimi baada ya nafasi yake katika kampuni kuimarika”Aliongea Hamza
Dina mara baada ya kusikia hivyyo alijikuta akimuonea huruma na kumdharau kwa wakati mmoja Regina.
“Regina ni mwanamke asiejua ana bahati kiasi gani lakini anachezea, kuolewa na mtu kama wewe ni zaidi ya faida ya vizazi na vizazi”Aliongea Dina.
“Dina huwezi kurahisisha mambo , kwa nafasi yake huwezi kumlaumu yeye sio kama sisi tuliozea kuona damu , nadhani baada ya kugundua nimeua mtu jana ameona hata swala la kuandikisha ndoa amekurupuka”Aliongea Hamza lakini upande wa Dina alimuona Hamza kama anatafuta sehemu ya kulalamikia.
“Naona unafikiria sana , sio kawaida yako, kwa haraka haraka unaonekana kumpenda, ni kitu gani cha pekee ambacho kimekuvutia kutoka kwake?”
“Ushaanza kujilingansha sasa , hebu acha kufikiria mbali kwangu mimi wewe ni mtu muhimu ambae siwezi kukupoteza.. Regina sijafahamiaa nae kwa muda mrefu na kuna uwezekano pia naweza nisiendelee kuwa nae muda wowote lakini angalau najua wewe huwezi kunikimbia”Aliongea Hamza na kumfanya Dina kujisikia utamu.
“Sawa , ila acha sasa kufikiria maswala ya Regina , mimi naamini anakupenda pia na muda wowote atazielewa hisia zake , leo ngoja ukapoteze mawazo yako Club”
“Ni Club gani tunaelekea?”
“Tanganyika Club ushawahi kuingia?”Aliuliza Dina.
“Naionaga sijawahi kuingia”
“Sasa Tanganyika ndio moja ya Club ya kifahari hapa nchini yenye kila aina ya starehe kuna hadi sehemu ya kujifunza kutumia bunduki halisi kulenga shabaha, kiingilio cha chini kwa mwezi ni milioni therathini na tano na pia lazima upendekezwe na mwanachama, wanaoingia humo ni wa hadhi ya juu mno”
“Mbona kama unapanga kunipeleka kulenga shabaha na bunduki?”
“Ni mpango wangu pia, nimekuona mara kadhaa ukipigana lakini sijawahi kukuona ukitumia bunduki , nataka nione kama unanizidi”
“Dina unajua unazidi kuwa tofauti na wanawake wa kawaida kutokana na hobi zako”
“Kwahio unamaanisha hupendi.. kama ndio hivyo turudi”Aliongea Dina na Hamza aliishia kutingisha kichwa chake kukataa na kuendelea kuendesha gari.
Dakika kadhaa mbele waliweza kufika Posta na kuingia kwenye jengo kubwa ambalo halijaenda sana hewani , lilikuwa limejengwa kwa kuigiza muundo wa meli , sehemu hio ndio ilikuwa ikipatikana Club na hoteli maarufu ya matajiri ya Tanganyika.
Licha ya Club hii kuwa ndani ya Tanzania lakinni ni asilimia kumi tu pengine pungufu zaidi ya walioingia ndani ya Club hio kuwa watanzania, ukiachana na kwamba matajiri wa kibongo huingia ndani ya club hio ila ni wachache sana, raia wengi wa Kigeni ambao walikuwa wakiingia nchini kwa ajili ya kufanya anasa lazima wafikie katika hio Club , ilikuwa maarufu Afrika mashariki na kati yote.
Taarifa ambazo hazikuthibirishwa ilisemekana inamilikiwa na familia moja ya kitajiri kutoka Scotland maarufu kama Keswick kupitia asset zao ndani ya Mandarlin oriental luxury hospitality,Uwekezaji huo mkubwa ulitekelezwa kipindi cha uongozi wa Mheshimiwa Mgweno.
Mara baada ya kuingia ndani ya lango la hoteli na Club hio Hamza alikabidhi funguo kwa Valet na kutokana na Dina pia kuwa moja ya wanachama ndani ya Club hio alikuwa akiruhsiwa kuingia na tafiki.
Mara baada ya kuingia katika Korido ndeefu Dina alikunja kulia kwake na kuhamia katika Korido nyingine na hapa ndio Hamza alijua ni kipi kinaendelea , ndani ya eneo hilo kulikuwa na skrini zilizofungwa ukutani kama TV na zilikuwa zikionyesha kila aina ya Bunduki inayopatikana kwa ajili ya kulengea shabaha.
Kila mtu alikuwa na starehe yake na hili lilizingatiwa ndani ya hoteli hio , wengine starehe yao pengine ni kuzima shauku zao katika matumizi ya siraha na sio kuishia kuziona kwenye filamu tu na hiki ndio kilichokuwa kikipatikana ndani ya club hio , ukitaka kuwa Mdunguaji ama kujifunza kuwa Mdunguaji basi hio ndio sehemu yenyewe.
Upande wa Hamza kila bunduki alioweza kuona alikwua ashaitumia hivyo ni kama hakuwa na ile shauku kubwa.
“Dina!!”
Ghafla tu sauti ya kiume iliita kutoka nyuma yao na kufanya wageuke.
Alikuwa ni bwana mmoja mwenye muonekano wa kipole alievalia suti nyyeupe pamoja na miwani.
“Huyu mwanaume ni nani , usiniambie ndio boyfriend wako?”Aliongea mara baada a kuwakaribia na alimwangalia Hamza kwa macho yasiokuwa na ishara ya urafiki, alikuwa hajapenda kabisa namna ambavyo Hamza na Dina walivyoshikana mikono.
“Robert umekuwa na shauku ya kumjua , huyu sasa ndio mpenzi wangu”Aliongea Dina na kisha alimtambulisha Hamza.
“Hamza huyu ni Robert mtoto wa Eliasi mheshimiwa raisi anaemaliza muda wake, ni Mbunge na msimamizi mkuu wa mahoteli yote ya Tanganyika”Aliongea Dina.
“Hello Mr Robert!”Aliongea Hamza na kunyoosha mkono kusalimiana nae.
“Sijaona ubora wowote uliokuwa nao tofauti na mimi , ukiachana na muonekano wako wa kuchanganya rangi, nimemfuatilia Dina kwa mwaka sasa lakini kila siku ananikataa , nataka kujua ni kipi ambacho kinakufanya kuwa bora zaidi yangu”Aliongea Robert na kumfanya Hamza kucheka.
“Sijajua anachonipendea labda ni kwasababu mimi ni handsome zaidi kuliko wewe”Aliongea na kumfanya Dina kumpiga Hamza na kiwiko akimwambia atulie.
“Haiwezekani , kinachokubeba ni huo muonekano wako wa kuchanganya rangi lakini kimavazi na kila kitu nimekuzidi “
“Labda nikwasababu namridhisha kwenye sita kwa sita wanawake hawajawahi kueleweka wanachopenda kwa mwanaume”Aliongea Hamza.
“Hebu acha kuongea , unamaanisha nini?” Dina hakutaka Hamza aendelee kuongea maana alijikuta akishikwa na aibu.
“Dina kwahio ndio sababu ya kunikataa , kwanini usingeongea tu , niko vizuri pia kwenye sita kwa sira na kama usingeridhika ningetumia hata mkongo kwa ajili yako”
“Robert usimsikilize Hamza anakutania tu , sijakukataa kwasababu huna vigezo ni kwasababu kazi yangu haieandani vyema na kazi yako na ya baba yako, sidhani pia kama natosha kwako , isitoshe hili ni swala la kihisia zaidi”
“Hilo sio tatizo Dina , nilikupenda siku ya kwanza nilipokuona ndani ya mgahawa wako…”
“Robert naomba unisamehe lakini sitaki kuendelea na haya mazungumzo mbele ya Hamza”Aliongea na kumfanya Robert kuonekana kutoridhika hasa alipomuangalia Hamza.
Upande wa Hamza aliona huyo bwana anafurahisha , alikuwa ni kama mtoto ambae amekasirika baada ya kunyimwa hitajio lake , kariba ambayo kwa bahati mbaya haikuendana na Dina kabisa.
Muda huo Wenza wengine waliingia ndani ya eneo hilo na kumfanya Hamza kuwashangaa baada ya kuwajua .
Alikuwa ni bosi Side Mkrugenzi wa Vodocum Tanzania alieambatana na Salma ambae alidhalilika mbele ya Fellini wa kamapuni ya kimavazi ya Zara..
“Mr Hamza?”Aliita Saidi.
“Bwana Saidi kumbe na wewe ni mhudhuriaji hapa?”Aliongea Hamza huku akitoa tabasamu la utulivu.
“Side unamfahamu?”Aliongea Salma akijifanyisha eti hamjui Hamza.
“Ndio namfahamu , mbona kama na wewe unamjua?”Aliongea Saidi na kumfanya Salma mwili wake kukakamaa , alihitaji kujizuia kadri awezavyo asije kuongea upuuzi kama wakati ule.
“Ndio nilifahamiana nae katika harakati za kazi”Aliongea Salma.
“Kumbe mnafahamiana ne , Hamza huyu ni Side rafiki yangu , Salma ni mpenzi wake na rafiki yangu pia”Aliongea Robert na kumfanya Hamza kuishia kujisemea Side hakuonekana mzembe , Salma alikuwa mwanamke matawi pia na mrembo na kwa kuangalia tu ilionekana Salma ndio kapenda zaidi ya Side.
“Robert si ulisema ulimfukuzia Dina kwa zaidi ya mwaka , inamaana huyu ndio mtu aliekubia?”Aliongea Salma hakukoma tu.
Hata kwa Side aliweza kuona ukaribu uliokuwepo kati ya Dina na Hamza na alizidi kujawa na hisia mchanganyiko , siku ile Prisila alimtambulisha kama mpenzi wake lakini leo hii Hamza yupo na Dina , wanawake hao wote kwake ni ngumu kuwapata licha ya cheo chake kazini .
“Salma haina haja ya kusema hivyo , bado sijakubali kumpoteza Dina , lazima nimuonyeshe mimi ni zaidi ya Hamza”Aliongea na muda uleule alimgeukia Hamza.
“Si mmekuja upande huu kulenga shabaha na bunduki , kwanini tusishindane , kama kweli wewe ni mwanaume tucheze pambano moja na atakae shinda rasmi atatoka kimapenzi na Dina”
“Robert!, mimi sio tuzo kwamba nitajikabidhi kwa yoyote anaeshinda , kwanini unanigeuza kuwa kifaa?”
“Dina usinifikirie vibaya , nadhani utanipa nafasi angalau ya kukupigania , kama wasemavyo huwezi kuona ubora wa kitu pasipo ya kukilinganisha na kingine , siwezi kukubali kushindwa bila ya kuijua sababu”
“Lakini mimi sitaki kushindana”Aliongea Hamza
“Wewe sema hujui kutumia bunduki acha kuzunguka, Dina ni mwanamke anaeweza kulenga shabaha kwa kiwango kikubwa unaweza vipi kuwa mpenzi wake kama hata kutumia bunduki hujui?”
“Najua lakini sitaki kushindana”Aliongea Hamza akionyesha kukereka.
“Kama unajua tushindane acha kuwa mwanamke , jiamini bro kama nikishinda utaachana na Dina kama ukishinda nitaacha kumsumbua Dina , unaonaje hapo?”
“Robert huwezi kuzipangia hisia zangu nani wa kumpenda kupitia mashindano?”AliongeaDina akionekana kuanza kukasirika lakini Hamza alimzuia huku akitoa tabasamu lililojaa kejeli.
“Sio mbaya muda mwingine wanaume kwa wanaume kushindana japo huwa sipendelei , kama hili ni swala la kuonyesha nani mwanaume zaidi kati yetu basi nipo tayari”
Hamza hakutaka kuonekana mdhaifu mbele ya Dina hivyo alitaka kuuonyesha Robert nini maana ya kulenga shabaha.
Side na Salma walioneysha hali ya dharau kwa Hamza , walikuwa wakimjua Robert Eliasi likija swala la kulenga shabaha alikuwa fundi kuzidi hata wanajeshi wa vikosi maalumu.
“Hamza upo tayari kushindana na Robert kweli! , ngoja umpoteze bosi Dina kwa Robert”Aliongea Salma.
“Hatujaanza kushindana lakini ushaanza kuleta dharau zako kama siku ile?”Aliongea Hamza na kumfanya Salma kupandwa na hasira, bado alikuwa na kinyongo na Hamza kwa kumsababishia kukosa ushirikiano wa kibiashara kati ya Kampuri yao ya S Corporation na Zara Group kwa Hamza kuleta habari zake za Mshona nguo kutoka Ulaya.
“Dina usiwe na wasiwasi , huwa sijawahi kushindwa”Aiongea Hamza akimtoa wasiwasi.
Dina hakuwa na cha kumfanya Hamza kutokana tayari ashaafanya maamuzi , licha ya kwamba alionekana kama anatania lakini aliamini Hamza hawezi kufanya kitu ambacho hajiamini nacho.
Wote kwa pamoja walisogea mpaka eneo la Shooting Range.
“Tutatumia bastora ya Smith & wesson toleo la tatu , yenye uwezo wa kuachia risasi ukubwa wa Kaliba arobaini na tano, kila mtu raundi kumi , mita hamsini kutoka kwenye shabaha , tutashinda kwa kuangalia nani ana maksi kubwa”Aliongea Robert na kumfanya Hamza kuchukua bastora na kuanza kuipima uzito wake na aligundua ilikuwa ni orijino kutoka kiwandani kabisa na sio feki na alijiambia hii hoteli sio ya kawaida.
Eneo hilo lilikuwa na soundproof kiasi kwamba hata ukifyatua bunduki sauti yake inamezwa na haiwezi kufika floor za juu kwenye makasino na vyumba vya kulala lakini pia bunduki nyingi zilikuwa na mfumo wa Suppressor wa kuzuia makelele.
“Hakuna shida, nani anaanza?”
“Yoyote yule , mimi niko freshi”
“Kama ni hivyo wewe anza”Aliongea Hamza na Robert hakujali zaidi ya kutoa tabasamu lililojaa kejeli na aliijaza bunduki na risasi na kisha akaiweka katika usalama na kuanza kulenga shabaha za duara zilizokuwa mita hamsini umbali.
“Bang , Bang , Bang..”
“Bahati mbaya kwako umenikuta nikiwa na hali nzuri ya kulenga , alama hizi ni karibia na alama zangu za juu katika ulengaji , kama utaamua kukata tamaa mapema naweza kukuelewa”
Alikuwa ameweza kulenga duara namba nane na namba saba , kwa umbali wa mita hamsini ana uwezo wa kulenga kiganja cha mkono wa mtu , ni uwezo wa juu ambao mtu wa kawaida hawezi kufikia kabisa, lazima uwe na mafunzo ya miaka mingi , maana msukumo wa nguvu inayokurudisha nyuma ulikuwa mkubwa mno bila kusahau bastora aliokuwa akitumia ina mdomo(Calliber au Kaliba) mkubwa hivyo kuwa na msukumo mkubwa.
Dina hata yeye aliingiwa na wasiwasi , licha ya kwamba uwezo wake wa kulenga shabaha ni mzuri lakini ilikuwa ni mara chache sana kufikia alama alizopata Robert kwa kufyatua risasi mara kumi mfululizo na aliona Hamza anaweza asimfikie.
Hamza hakuongea neno na taratibu alichukua risasi moja moja na kuijaza kwenye bunduki.
Ni kweli aliona Robert alikuwa na uwezo mzuri wa kulenga kwa kugusa duara namba 8 na 7 , wasiwasi wake mkubwa ni kupata maksi za juu kabisa ambazo sio za kawaida na kufanya hao watu kumshitukia.
Baada ya kuwaza hivyo aliona kidogo aonyeshe ubinadamu kwa kujikosesha.
Bang , Bang , Bang
Hamza aliishikilia bunduki kwa mikono miwili kana kwamba alikuwa akimuigiza Robert lakin ukweli ni kwamba hakuangalia hata anapolenga, kwa umbali huo aliiona anaweza kupata maksi mia ya mia hata kama amefumba macho yake.
Mara baada ya kukamilisha mizunguko kumi , haraka sana Robert alibonyeza kitufe cha kuonyesha alama Hamza alizopata.
“”Nane .. tisa ,,, nane , nane , nane!!”Robert alijikuta akishikwa na hasira huku akisaga meno akiwa haamini macho yake
“Samahani mkuu nimeshinda”Aliongea Hamza.
“Wewe .. unaonekana kuwa na bahati sana”
“Kwahio bado hujakubali nimeshinda”
“Turudie tena , tufanye iwe mbili kwa tatu”Aliongea Robert akionyesha kutokukubali kushindwa.
“Tulikubaliana atakaepata maksi kubwa ndio mshindi lakini sasa hivi unaanza kubadilisha sheria, siwezi kushindana na mtu ambae anaenda kiunyume na ahadi yake”
“Sio hivyo…”
Kilichomfanya Robert kukasirika ni kwasababu alijua angekosa nafasi ya kuombata tena tunda kutoka kwa Dina.
Salma alimwangalia Saidi na kisha alimgeukia Hamza na alionekana kuna kitu alichokiwaza.
“Mnaonaje tukifanya hivi, kama marafiki Saidi atashindana kwa ajii ya Robert , akishinda tutafanya shindano la mwanzo ni suruhu”Aliongea huku akishika mkono wa Saidi akiupangusa kwa mapozi.
“Side naomba umsaidie Robert , naona kama haki haijatendeka”Aliongea lakini Side alionekana kutofurahishwa na alichosema Salma.
“Hili ni wazo zuri Salma , vipi upo tayari kupambana na saidi?”Aliongea Robert akimwangalia Hamza
“Bado hatujamaliza tu hili na mnataka tena, sidhani kama kuna faida yoyote”Aliongea Hamza lakini Side alionekana kulifikiria lile wazo.
“Unaonaje tukifanya hivi kama nikishinda, pambano kati ya Hamza na Robert ni batili na kama Hamza akishinda nitampatia dola laki moja , Robert chukulia hio hela kama ufadhili wangu kwenye uchaguzi wa kutetea jimbo lako”Aliongea Side.
“Haha… Side ndio maana nakukubali sana rafiki yangu , hili limepita”
Hamza alijikuta akiishia kutingisha kichwa kwa masikitiko , ilionyesha Side alitaka kushindana nae kwa kiasi kikubwa mpaka kuweka rehani kiasi kikubwa hivyo cha pesa.
“Kuwa makini , Saidi uwezo wake wa kulenga shabaha sio wa kawaida , ndio mwenye rekodi ya juu tokea kuanzishwa kwa hii club, huwa hashuki chini ya pointi tisini”Aliongea Dina lakini Hamza wala hakujali.
“Unaonekana kuwa na nia ya dhati kabisa kupambana na mimi hivyo sio vizuri kukukatalia , tuanze mechi”Aliongea Hamza na Side alitingisha kichwa na kisha alisogea na kuanza kuload risasi na kuanza kushuti.
Baada ya awamu kumi kuisha Side hata hakujali kuangalia matokeo kwani alisogea pembeni na kazi hio ilifanywa na Robert.
“Side umevunja rekodi tena , umepata pointi tisini na nane umekosa mbili tu”Aliongea Robert ikimaanisha amelenga kwenye duara namba kumi mara nane na tisa mara moja.
“Babe upo vizuri sana ndio maana nakupenda”Aliongea Salma akimwangalia Side na macho yaliolegea.
Dina alimwangalia Hamza na aliona ni ngumu kwa Hamza kuzidi hizo maksi mbili tu ambazo Side alikosa.
“Unaweza kukubali kushindwa hakuna atakae kucheka”Aliongea Side.
Hamza aliona yupo kwenye hali ngumu na hawezi kuigiza tena , isitoshe iwe tisini na tisa au mia hakuna ambae ataona kama anadanganya.
“Usiwaze , ngoja nijaribu na mimi”Aliongea Hamza na kisha alisogea na kuanza kujaza bastora na risasi na kisha aliinua mkono mmoja wa kushoto na kuanza kupiga , hakupumzika hata kwa sekunde ilikuwa ni mfululizo wa risasi kutoka.
Dakika ambayo Hamza aliweka bunduki chini , kwa haraka sana Robert aliangalia matokeo na mara baada ya namba nyekundu kuonekana wote na Dina ambao walionekana kuwa na shauku macho yaliwatoka , huku Side na Salma wakimwangalia Hamza kwa mshangao mkubwa.
“100!?”
Robert alikuwa akiangalia namba hio kwa muda mrefu kana kwamba alidhania macho yake yanamdanganya.
“Wewe ni binadamu kweli!?”Aliuliza Robert maana hakuamini mfuatano wa risasi zile zote zimegonga shabaha kwa asilimia mia.
“Leo inaonekana nina bahati sana”Aliongea Hamza akicheka , ijapokuwa watu wote waliokuwa wakimwangalia hawakuwa wajinga , lakini ilikuwa ni uhalisia Hamza hakutumia uwezo wake wote.
“Kupoteza ni kupoteza tu , ikitokea mtaalamu zaidi yako utaishia kushindwa , Hamza nitajie namba za akaunti yako ya benki nikuingizie kiasi nilichoahidi”Aliongea Saidi.
“Potezea , Side sisi sio wageni kwetu , chukulia kama tulikuwa tukicheza”Aliongea Hamza hakutaka kufanya mambo kuwa magumu kwa Saidi.
“Huwa sichukulii kiwepesi ahadi zangu , nikisema ni laki ni laki , nimekubali kushindwa hivyo usinifanye kwenda kinyume na ahadi”
“Babe nitampatia mimi”Aliongea Salma.
“Haina haja”
Salma alionekana kujutia kupendekeza shindano lile na kumfanya Saidi kuingia hasara na aliona hasira ya Side kabisa, lakini alipendekeza vile kwani hakuamini kama Hamza anaweza kumzidi Saidi.
Hamza mara baada ya kuona Side anataka kukasirika aliona asiikatae ile hela.
“Dina mtajie akaunti yako ya benki akuingizie hela , chukulia kama malipo ya siku zote nilizokula na kunywa bure kwenye mgahawa wako”
“Ni hela yako hio , sioni kama ni vizuri kuitumia kama malipo”Aliongea Dina lakini hata hivyo alimtajia Saidi akaunti yake ya benki na alichukua sekunde kadhaa muamala ulisoma milioni mia mbili hamsini, ijapokuwa aliahidi atalipia kwa dola lakini alilipa kwa hela za kitanzania na baada ya hapo alionekana hakuwa hata na mudi kwani aligeuka na kuondoka na kumfanya Salma kumkimbilia.
“Side inaonekana kakasirika, sio kwasababu ya kupoteza hela ila kwasababu ya kushindwa”Aliongea Robert
“Wewe vipi hujakasirika, siku nyingine unapaswa kutimiza wajibu wako wa kutumikia wananchi na sio kumsumbua mpenzi wangu”
“Nimekubali kushindwa Bro , kama nilivyoahidi nitatekeleza’Aliongea Robert kisha alimsogelea Hamza na kumpatia mkono.
“Hamza unaonaje tukishikana mikono kama ishara ya kuwa marafiki kwanzia sasa?, natumaini utamfanya Dina kuwa na furaha”Aliongea na kumfanya Hamza amuone kweli bwana huyo ni mwanasiasa lakini hata hivyo aliishia kunyoosha mkono kumkubalia.
Upande wa maegesho ya magari mara baada ya bosi Side kuingia ndani ya gari yake Audi R8 aliweza kumuona Salma akiwa ameshaingia tayari.
“Shuka!”Aliongea kikauzu na kumfanya Salma kutia huruma.
“Side naomba unisamehe mpenzi wangu , sikujua kama Hamza angekuwa na bahati kiasi kile , naomba usikasirike”
“Eti bahati , kuna bahati ya namna ile mtu kuweza kulenga shabaha eneo moja kwa mara zote kumi au unaongea upuuzi?”
“Lakini kwanini upo hivi Side , kuna kingine tofauti na hiki kilichotokea , tumekuwa wapenzi kwa zaidi ya miaka minne sasa na nimeamua kurudi kwa ajili yako , lakini kwanini kadri siku zinavyosogea unazidi kuwa mkali kwangu?”
“Kama unadhani nimekuwa mkali kwako , basi rudi China ukaendelee na mambo yako sikukuambia urudi kwa ajili yangu”
“Sirudi tena China, awamu hii nimerudi ili unioe”
“Nani kasema nitakuoa , hebu toka kwenye gari yangu kabla sijakufanya kitu kibaya”Aliongea na kumfanya Salma kuzidi kuona Side anamkosea na alishuka kwa hasira na kuondoka lakini hata hivyo Side hakujali , mara baada ya kuingia katika gari yake alianza kutafuta majina katika simu yake na kuweka sikioni ikionyesha anapiga simu.
“Side , naona leo umepata muda wa kunipigia?”Sauti ya kike ilisikika.
“Lea hebu acha maneno yako , kuna kitu nataka unisaidie nitakulipa hela”
“Kila unapoongelea hela ujue una stress , haya niambie ni kipi unataka nikusaidie?”
“Leo nimegundua siri ambayo Hamza anaificha , nataka umwambie Prisila…”Aliongea Saidi huku akiwa na tabasamu lililojaa uovu.
******
Upande mwingine ndani ya makazi ya mrembo na Daktari , Frida Franklin katika chumba cha Master alionekana mrembo huyo akiwa amejilaza na kukoroma kabisa , alionekana alikuwa amechoka kwa namna alivyokuwa amelala.
Taa ya kitandani ilionekana haijazimwa na pembeni yake kuna kitabu kilichokuwa kimefunguliwa , ikionyesha alipitiwa na usingizi wakati akiwa anasoma.
Zilipita sekunde chache tu muda ule hali ya hewa ya kile chumba ilibadilika , ilikuwa ni kama upepo umeongezeka na kumfanya Frida kuanza kujinyoosha kitandani.
Mara ghafla tu chumba kile kilirudi katika hali ya utulivu wa hali ya juu na kumfanya Frida kujigeuza na kulala chali , lakini utulivu ule uliambatana na maajabu yake kwani ghafla tu kilionekana kivuli kikitokea kwenye pembe ya chumba hicho.
Ajabu ni kwamba kifizikia ili kivuli kitokee kinahitaji mwanga lakini kivuli hicho kilitokea bila ya kuwa na chanzo cha mwanga.
Kile kivuli kilikuwa na umbo la mtu lakini kwa namna moja ama nyingine kama ni mtu katika uhalisia basi angekuwa akitisha kutokana na eneo lake la kichwa kukosa mpangilio mzuri.
Wakati Frida akiwa hana hili wala lile mkono wa kivuli kile cha mtu wa ajabu ulinyooka ni kama ulikuwa ukirefuka kutoka eneo kilipo mpaka kwenye kitanda , mkono ule ukimlenga Frida katika shingo yake.
Ghafla tu ni kama Frida alishituka lakini alianza kurusha miguu kama mtu ambae amekabwa shingoni , alijikuta akirusha Miguu huku akijitahidi kuvuta hewa.
Lakini mwanamke mrembo huyo alionekaa kushindwa kabisa kupambana na mkono ule wa Kivuli cha mtu na ulionekana ni kama umedhamiria kumuua.
Frida alijikuta kadri sekunde zinavyoenda ndio ambavo alikuwa akikosa nguvu kutokana na kutoweza kuvuta pumzi ,aliishia kurusha rusha miguu huku akionekana muda wowote atakata roho.
MWISHO WA SEASON 2
ITAENDELEA.

0687151346 WhatsApp
 
SHETANI RUDISHA AKILI ZETU
MTUNZI:SINGANOJR

SEHEMU YA 60.
Hamza akiwa ndani ya gari na Dina alimwambia kile ambacho kimetokea mpaka namna alivyojiandikisha na Regina na kuwa wanandoa kisheria.
Ijapokuwa Dina alikuwa mtulivu wakati wa kumsikiliza Hamza , lakini mara baada ya kusikia Hamza alikuwa amesajili ndoa na mwanamke mwingine alijikuta akishikwa na huzuni.
Lakini hata hivyo aliona haiwezekani yeye kuja kuwa mke wa Hamza kwani hakuwa na vigezo hivyo.
“Kwahio kwanzia sasa utakuwa chini ya ulinzi wa mke wako na kuwa ngumu kwetu kuonana , sijui mimi Dina nimekosea wapi katika ulimwengu huu”Aliongea na kumfanya Hamza asijue alie au acheke.
“Hapo ndio unapokosea , kasema licha ya kuandikisha ndoa niharakishe kutafuta mwanamke na ataachana na mimi baada ya nafasi yake katika kampuni kuimarika”Aliongea Hamza
Dina mara baada ya kusikia hivyyo alijikuta akimuonea huruma na kumdharau kwa wakati mmoja Regina.
“Regina ni mwanamke asiejua ana bahati kiasi gani lakini anachezea, kuolewa na mtu kama wewe ni zaidi ya faida ya vizazi na vizazi”Aliongea Dina.
“Dina huwezi kurahisisha mambo , kwa nafasi yake huwezi kumlaumu yeye sio kama sisi tuliozea kuona damu , nadhani baada ya kugundua nimeua mtu jana ameona hata swala la kuandikisha ndoa amekurupuka”Aliongea Hamza lakini upande wa Dina alimuona Hamza kama anatafuta sehemu ya kulalamikia.
“Naona unafikiria sana , sio kawaida yako, kwa haraka haraka unaonekana kumpenda, ni kitu gani cha pekee ambacho kimekuvutia kutoka kwake?”
“Ushaanza kujilingansha sasa , hebu acha kufikiria mbali kwangu mimi wewe ni mtu muhimu ambae siwezi kukupoteza.. Regina sijafahamiaa nae kwa muda mrefu na kuna uwezekano pia naweza nisiendelee kuwa nae muda wowote lakini angalau najua wewe huwezi kunikimbia”Aliongea Hamza na kumfanya Dina kujisikia utamu.
“Sawa , ila acha sasa kufikiria maswala ya Regina , mimi naamini anakupenda pia na muda wowote atazielewa hisia zake , leo ngoja ukapoteze mawazo yako Club”
“Ni Club gani tunaelekea?”
“Tanganyika Club ushawahi kuingia?”Aliuliza Dina.
“Naionaga sijawahi kuingia”
“Sasa Tanganyika ndio moja ya Club ya kifahari hapa nchini yenye kila aina ya starehe kuna hadi sehemu ya kujifunza kutumia bunduki halisi kulenga shabaha, kiingilio cha chini kwa mwezi ni milioni therathini na tano na pia lazima upendekezwe na mwanachama, wanaoingia humo ni wa hadhi ya juu mno”
“Mbona kama unapanga kunipeleka kulenga shabaha na bunduki?”
“Ni mpango wangu pia, nimekuona mara kadhaa ukipigana lakini sijawahi kukuona ukitumia bunduki , nataka nione kama unanizidi”
“Dina unajua unazidi kuwa tofauti na wanawake wa kawaida kutokana na hobi zako”
“Kwahio unamaanisha hupendi.. kama ndio hivyo turudi”Aliongea Dina na Hamza aliishia kutingisha kichwa chake kukataa na kuendelea kuendesha gari.
Dakika kadhaa mbele waliweza kufika Posta na kuingia kwenye jengo kubwa ambalo halijaenda sana hewani , lilikuwa limejengwa kwa kuigiza muundo wa meli , sehemu hio ndio ilikuwa ikipatikana Club na hoteli maarufu ya matajiri ya Tanganyika.
Licha ya Club hii kuwa ndani ya Tanzania lakinni ni asilimia kumi tu pengine pungufu zaidi ya walioingia ndani ya Club hio kuwa watanzania, ukiachana na kwamba matajiri wa kibongo huingia ndani ya club hio ila ni wachache sana, raia wengi wa Kigeni ambao walikuwa wakiingia nchini kwa ajili ya kufanya anasa lazima wafikie katika hio Club , ilikuwa maarufu Afrika mashariki na kati yote.
Taarifa ambazo hazikuthibirishwa ilisemekana inamilikiwa na familia moja ya kitajiri kutoka Scotland maarufu kama Keswick kupitia asset zao ndani ya Mandarlin oriental luxury hospitality,Uwekezaji huo mkubwa ulitekelezwa kipindi cha uongozi wa Mheshimiwa Mgweno.
Mara baada ya kuingia ndani ya lango la hoteli na Club hio Hamza alikabidhi funguo kwa Valet na kutokana na Dina pia kuwa moja ya wanachama ndani ya Club hio alikuwa akiruhsiwa kuingia na tafiki.
Mara baada ya kuingia katika Korido ndeefu Dina alikunja kulia kwake na kuhamia katika Korido nyingine na hapa ndio Hamza alijua ni kipi kinaendelea , ndani ya eneo hilo kulikuwa na skrini zilizofungwa ukutani kama TV na zilikuwa zikionyesha kila aina ya Bunduki inayopatikana kwa ajili ya kulengea shabaha.
Kila mtu alikuwa na starehe yake na hili lilizingatiwa ndani ya hoteli hio , wengine starehe yao pengine ni kuzima shauku zao katika matumizi ya siraha na sio kuishia kuziona kwenye filamu tu na hiki ndio kilichokuwa kikipatikana ndani ya club hio , ukitaka kuwa Mdunguaji ama kujifunza kuwa Mdunguaji basi hio ndio sehemu yenyewe.
Upande wa Hamza kila bunduki alioweza kuona alikwua ashaitumia hivyo ni kama hakuwa na ile shauku kubwa.
“Dina!!”
Ghafla tu sauti ya kiume iliita kutoka nyuma yao na kufanya wageuke.
Alikuwa ni bwana mmoja mwenye muonekano wa kipole alievalia suti nyyeupe pamoja na miwani.
“Huyu mwanaume ni nani , usiniambie ndio boyfriend wako?”Aliongea mara baada a kuwakaribia na alimwangalia Hamza kwa macho yasiokuwa na ishara ya urafiki, alikuwa hajapenda kabisa namna ambavyo Hamza na Dina walivyoshikana mikono.
“Robert umekuwa na shauku ya kumjua , huyu sasa ndio mpenzi wangu”Aliongea Dina na kisha alimtambulisha Hamza.
“Hamza huyu ni Robert mtoto wa Eliasi mheshimiwa raisi anaemaliza muda wake, ni Mbunge na msimamizi mkuu wa mahoteli yote ya Tanganyika”Aliongea Dina.
“Hello Mr Robert!”Aliongea Hamza na kunyoosha mkono kusalimiana nae.
“Sijaona ubora wowote uliokuwa nao tofauti na mimi , ukiachana na muonekano wako wa kuchanganya rangi, nimemfuatilia Dina kwa mwaka sasa lakini kila siku ananikataa , nataka kujua ni kipi ambacho kinakufanya kuwa bora zaidi yangu”Aliongea Robert na kumfanya Hamza kucheka.
“Sijajua anachonipendea labda ni kwasababu mimi ni handsome zaidi kuliko wewe”Aliongea na kumfanya Dina kumpiga Hamza na kiwiko akimwambia atulie.
“Haiwezekani , kinachokubeba ni huo muonekano wako wa kuchanganya rangi lakini kimavazi na kila kitu nimekuzidi “
“Labda nikwasababu namridhisha kwenye sita kwa sita wanawake hawajawahi kueleweka wanachopenda kwa mwanaume”Aliongea Hamza.
“Hebu acha kuongea , unamaanisha nini?” Dina hakutaka Hamza aendelee kuongea maana alijikuta akishikwa na aibu.
“Dina kwahio ndio sababu ya kunikataa , kwanini usingeongea tu , niko vizuri pia kwenye sita kwa sira na kama usingeridhika ningetumia hata mkongo kwa ajili yako”
“Robert usimsikilize Hamza anakutania tu , sijakukataa kwasababu huna vigezo ni kwasababu kazi yangu haieandani vyema na kazi yako na ya baba yako, sidhani pia kama natosha kwako , isitoshe hili ni swala la kihisia zaidi”
“Hilo sio tatizo Dina , nilikupenda siku ya kwanza nilipokuona ndani ya mgahawa wako…”
“Robert naomba unisamehe lakini sitaki kuendelea na haya mazungumzo mbele ya Hamza”Aliongea na kumfanya Robert kuonekana kutoridhika hasa alipomuangalia Hamza.
Upande wa Hamza aliona huyo bwana anafurahisha , alikuwa ni kama mtoto ambae amekasirika baada ya kunyimwa hitajio lake , kariba ambayo kwa bahati mbaya haikuendana na Dina kabisa.
Muda huo Wenza wengine waliingia ndani ya eneo hilo na kumfanya Hamza kuwashangaa baada ya kuwajua .
Alikuwa ni bosi Side Mkrugenzi wa Vodocum Tanzania alieambatana na Salma ambae alidhalilika mbele ya Fellini wa kamapuni ya kimavazi ya Zara..
“Mr Hamza?”Aliita Saidi.
“Bwana Saidi kumbe na wewe ni mhudhuriaji hapa?”Aliongea Hamza huku akitoa tabasamu la utulivu.
“Side unamfahamu?”Aliongea Salma akijifanyisha eti hamjui Hamza.
“Ndio namfahamu , mbona kama na wewe unamjua?”Aliongea Saidi na kumfanya Salma mwili wake kukakamaa , alihitaji kujizuia kadri awezavyo asije kuongea upuuzi kama wakati ule.
“Ndio nilifahamiana nae katika harakati za kazi”Aliongea Salma.
“Kumbe mnafahamiana ne , Hamza huyu ni Side rafiki yangu , Salma ni mpenzi wake na rafiki yangu pia”Aliongea Robert na kumfanya Hamza kuishia kujisemea Side hakuonekana mzembe , Salma alikuwa mwanamke matawi pia na mrembo na kwa kuangalia tu ilionekana Salma ndio kapenda zaidi ya Side.
“Robert si ulisema ulimfukuzia Dina kwa zaidi ya mwaka , inamaana huyu ndio mtu aliekubia?”Aliongea Salma hakukoma tu.
Hata kwa Side aliweza kuona ukaribu uliokuwepo kati ya Dina na Hamza na alizidi kujawa na hisia mchanganyiko , siku ile Prisila alimtambulisha kama mpenzi wake lakini leo hii Hamza yupo na Dina , wanawake hao wote kwake ni ngumu kuwapata licha ya cheo chake kazini .
“Salma haina haja ya kusema hivyo , bado sijakubali kumpoteza Dina , lazima nimuonyeshe mimi ni zaidi ya Hamza”Aliongea na muda uleule alimgeukia Hamza.
“Si mmekuja upande huu kulenga shabaha na bunduki , kwanini tusishindane , kama kweli wewe ni mwanaume tucheze pambano moja na atakae shinda rasmi atatoka kimapenzi na Dina”
“Robert!, mimi sio tuzo kwamba nitajikabidhi kwa yoyote anaeshinda , kwanini unanigeuza kuwa kifaa?”
“Dina usinifikirie vibaya , nadhani utanipa nafasi angalau ya kukupigania , kama wasemavyo huwezi kuona ubora wa kitu pasipo ya kukilinganisha na kingine , siwezi kukubali kushindwa bila ya kuijua sababu”
“Lakini mimi sitaki kushindana”Aliongea Hamza
“Wewe sema hujui kutumia bunduki acha kuzunguka, Dina ni mwanamke anaeweza kulenga shabaha kwa kiwango kikubwa unaweza vipi kuwa mpenzi wake kama hata kutumia bunduki hujui?”
“Najua lakini sitaki kushindana”Aliongea Hamza akionyesha kukereka.
“Kama unajua tushindane acha kuwa mwanamke , jiamini bro kama nikishinda utaachana na Dina kama ukishinda nitaacha kumsumbua Dina , unaonaje hapo?”
“Robert huwezi kuzipangia hisia zangu nani wa kumpenda kupitia mashindano?”AliongeaDina akionekana kuanza kukasirika lakini Hamza alimzuia huku akitoa tabasamu lililojaa kejeli.
“Sio mbaya muda mwingine wanaume kwa wanaume kushindana japo huwa sipendelei , kama hili ni swala la kuonyesha nani mwanaume zaidi kati yetu basi nipo tayari”
Hamza hakutaka kuonekana mdhaifu mbele ya Dina hivyo alitaka kuuonyesha Robert nini maana ya kulenga shabaha.
Side na Salma walioneysha hali ya dharau kwa Hamza , walikuwa wakimjua Robert Eliasi likija swala la kulenga shabaha alikuwa fundi kuzidi hata wanajeshi wa vikosi maalumu.
“Hamza upo tayari kushindana na Robert kweli! , ngoja umpoteze bosi Dina kwa Robert”Aliongea Salma.
“Hatujaanza kushindana lakini ushaanza kuleta dharau zako kama siku ile?”Aliongea Hamza na kumfanya Salma kupandwa na hasira, bado alikuwa na kinyongo na Hamza kwa kumsababishia kukosa ushirikiano wa kibiashara kati ya Kampuri yao ya S Corporation na Zara Group kwa Hamza kuleta habari zake za Mshona nguo kutoka Ulaya.
“Dina usiwe na wasiwasi , huwa sijawahi kushindwa”Aiongea Hamza akimtoa wasiwasi.
Dina hakuwa na cha kumfanya Hamza kutokana tayari ashaafanya maamuzi , licha ya kwamba alionekana kama anatania lakini aliamini Hamza hawezi kufanya kitu ambacho hajiamini nacho.
Wote kwa pamoja walisogea mpaka eneo la Shooting Range.
“Tutatumia bastora ya Smith & wesson toleo la tatu , yenye uwezo wa kuachia risasi ukubwa wa Kaliba arobaini na tano, kila mtu raundi kumi , mita hamsini kutoka kwenye shabaha , tutashinda kwa kuangalia nani ana maksi kubwa”Aliongea Robert na kumfanya Hamza kuchukua bastora na kuanza kuipima uzito wake na aligundua ilikuwa ni orijino kutoka kiwandani kabisa na sio feki na alijiambia hii hoteli sio ya kawaida.
Eneo hilo lilikuwa na soundproof kiasi kwamba hata ukifyatua bunduki sauti yake inamezwa na haiwezi kufika floor za juu kwenye makasino na vyumba vya kulala lakini pia bunduki nyingi zilikuwa na mfumo wa Suppressor wa kuzuia makelele.
“Hakuna shida, nani anaanza?”
“Yoyote yule , mimi niko freshi”
“Kama ni hivyo wewe anza”Aliongea Hamza na Robert hakujali zaidi ya kutoa tabasamu lililojaa kejeli na aliijaza bunduki na risasi na kisha akaiweka katika usalama na kuanza kulenga shabaha za duara zilizokuwa mita hamsini umbali.
“Bang , Bang , Bang..”
“Bahati mbaya kwako umenikuta nikiwa na hali nzuri ya kulenga , alama hizi ni karibia na alama zangu za juu katika ulengaji , kama utaamua kukata tamaa mapema naweza kukuelewa”
Alikuwa ameweza kulenga duara namba nane na namba saba , kwa umbali wa mita hamsini ana uwezo wa kulenga kiganja cha mkono wa mtu , ni uwezo wa juu ambao mtu wa kawaida hawezi kufikia kabisa, lazima uwe na mafunzo ya miaka mingi , maana msukumo wa nguvu inayokurudisha nyuma ulikuwa mkubwa mno bila kusahau bastora aliokuwa akitumia ina mdomo(Calliber au Kaliba) mkubwa hivyo kuwa na msukumo mkubwa.
Dina hata yeye aliingiwa na wasiwasi , licha ya kwamba uwezo wake wa kulenga shabaha ni mzuri lakini ilikuwa ni mara chache sana kufikia alama alizopata Robert kwa kufyatua risasi mara kumi mfululizo na aliona Hamza anaweza asimfikie.
Hamza hakuongea neno na taratibu alichukua risasi moja moja na kuijaza kwenye bunduki.
Ni kweli aliona Robert alikuwa na uwezo mzuri wa kulenga kwa kugusa duara namba 8 na 7 , wasiwasi wake mkubwa ni kupata maksi za juu kabisa ambazo sio za kawaida na kufanya hao watu kumshitukia.
Baada ya kuwaza hivyo aliona kidogo aonyeshe ubinadamu kwa kujikosesha.
Bang , Bang , Bang
Hamza aliishikilia bunduki kwa mikono miwili kana kwamba alikuwa akimuigiza Robert lakin ukweli ni kwamba hakuangalia hata anapolenga, kwa umbali huo aliiona anaweza kupata maksi mia ya mia hata kama amefumba macho yake.
Mara baada ya kukamilisha mizunguko kumi , haraka sana Robert alibonyeza kitufe cha kuonyesha alama Hamza alizopata.
“”Nane .. tisa ,,, nane , nane , nane!!”Robert alijikuta akishikwa na hasira huku akisaga meno akiwa haamini macho yake
“Samahani mkuu nimeshinda”Aliongea Hamza.
“Wewe .. unaonekana kuwa na bahati sana”
“Kwahio bado hujakubali nimeshinda”
“Turudie tena , tufanye iwe mbili kwa tatu”Aliongea Robert akionyesha kutokukubali kushindwa.
“Tulikubaliana atakaepata maksi kubwa ndio mshindi lakini sasa hivi unaanza kubadilisha sheria, siwezi kushindana na mtu ambae anaenda kiunyume na ahadi yake”
“Sio hivyo…”
Kilichomfanya Robert kukasirika ni kwasababu alijua angekosa nafasi ya kuombata tena tunda kutoka kwa Dina.
Salma alimwangalia Saidi na kisha alimgeukia Hamza na alionekana kuna kitu alichokiwaza.
“Mnaonaje tukifanya hivi, kama marafiki Saidi atashindana kwa ajii ya Robert , akishinda tutafanya shindano la mwanzo ni suruhu”Aliongea huku akishika mkono wa Saidi akiupangusa kwa mapozi.
“Side naomba umsaidie Robert , naona kama haki haijatendeka”Aliongea lakini Side alionekana kutofurahishwa na alichosema Salma.
“Hili ni wazo zuri Salma , vipi upo tayari kupambana na saidi?”Aliongea Robert akimwangalia Hamza
“Bado hatujamaliza tu hili na mnataka tena, sidhani kama kuna faida yoyote”Aliongea Hamza lakini Side alionekana kulifikiria lile wazo.
“Unaonaje tukifanya hivi kama nikishinda, pambano kati ya Hamza na Robert ni batili na kama Hamza akishinda nitampatia dola laki moja , Robert chukulia hio hela kama ufadhili wangu kwenye uchaguzi wa kutetea jimbo lako”Aliongea Side.
“Haha… Side ndio maana nakukubali sana rafiki yangu , hili limepita”
Hamza alijikuta akiishia kutingisha kichwa kwa masikitiko , ilionyesha Side alitaka kushindana nae kwa kiasi kikubwa mpaka kuweka rehani kiasi kikubwa hivyo cha pesa.
“Kuwa makini , Saidi uwezo wake wa kulenga shabaha sio wa kawaida , ndio mwenye rekodi ya juu tokea kuanzishwa kwa hii club, huwa hashuki chini ya pointi tisini”Aliongea Dina lakini Hamza wala hakujali.
“Unaonekana kuwa na nia ya dhati kabisa kupambana na mimi hivyo sio vizuri kukukatalia , tuanze mechi”Aliongea Hamza na Side alitingisha kichwa na kisha alisogea na kuanza kuload risasi na kuanza kushuti.
Baada ya awamu kumi kuisha Side hata hakujali kuangalia matokeo kwani alisogea pembeni na kazi hio ilifanywa na Robert.
“Side umevunja rekodi tena , umepata pointi tisini na nane umekosa mbili tu”Aliongea Robert ikimaanisha amelenga kwenye duara namba kumi mara nane na tisa mara moja.
“Babe upo vizuri sana ndio maana nakupenda”Aliongea Salma akimwangalia Side na macho yaliolegea.
Dina alimwangalia Hamza na aliona ni ngumu kwa Hamza kuzidi hizo maksi mbili tu ambazo Side alikosa.
“Unaweza kukubali kushindwa hakuna atakae kucheka”Aliongea Side.
Hamza aliona yupo kwenye hali ngumu na hawezi kuigiza tena , isitoshe iwe tisini na tisa au mia hakuna ambae ataona kama anadanganya.
“Usiwaze , ngoja nijaribu na mimi”Aliongea Hamza na kisha alisogea na kuanza kujaza bastora na risasi na kisha aliinua mkono mmoja wa kushoto na kuanza kupiga , hakupumzika hata kwa sekunde ilikuwa ni mfululizo wa risasi kutoka.
Dakika ambayo Hamza aliweka bunduki chini , kwa haraka sana Robert aliangalia matokeo na mara baada ya namba nyekundu kuonekana wote na Dina ambao walionekana kuwa na shauku macho yaliwatoka , huku Side na Salma wakimwangalia Hamza kwa mshangao mkubwa.
“100!?”
Robert alikuwa akiangalia namba hio kwa muda mrefu kana kwamba alidhania macho yake yanamdanganya.
“Wewe ni binadamu kweli!?”Aliuliza Robert maana hakuamini mfuatano wa risasi zile zote zimegonga shabaha kwa asilimia mia.
“Leo inaonekana nina bahati sana”Aliongea Hamza akicheka , ijapokuwa watu wote waliokuwa wakimwangalia hawakuwa wajinga , lakini ilikuwa ni uhalisia Hamza hakutumia uwezo wake wote.
“Kupoteza ni kupoteza tu , ikitokea mtaalamu zaidi yako utaishia kushindwa , Hamza nitajie namba za akaunti yako ya benki nikuingizie kiasi nilichoahidi”Aliongea Saidi.
“Potezea , Side sisi sio wageni kwetu , chukulia kama tulikuwa tukicheza”Aliongea Hamza hakutaka kufanya mambo kuwa magumu kwa Saidi.
“Huwa sichukulii kiwepesi ahadi zangu , nikisema ni laki ni laki , nimekubali kushindwa hivyo usinifanye kwenda kinyume na ahadi”
“Babe nitampatia mimi”Aliongea Salma.
“Haina haja”
Salma alionekana kujutia kupendekeza shindano lile na kumfanya Saidi kuingia hasara na aliona hasira ya Side kabisa, lakini alipendekeza vile kwani hakuamini kama Hamza anaweza kumzidi Saidi.
Hamza mara baada ya kuona Side anataka kukasirika aliona asiikatae ile hela.
“Dina mtajie akaunti yako ya benki akuingizie hela , chukulia kama malipo ya siku zote nilizokula na kunywa bure kwenye mgahawa wako”
“Ni hela yako hio , sioni kama ni vizuri kuitumia kama malipo”Aliongea Dina lakini hata hivyo alimtajia Saidi akaunti yake ya benki na alichukua sekunde kadhaa muamala ulisoma milioni mia mbili hamsini, ijapokuwa aliahidi atalipia kwa dola lakini alilipa kwa hela za kitanzania na baada ya hapo alionekana hakuwa hata na mudi kwani aligeuka na kuondoka na kumfanya Salma kumkimbilia.
“Side inaonekana kakasirika, sio kwasababu ya kupoteza hela ila kwasababu ya kushindwa”Aliongea Robert
“Wewe vipi hujakasirika, siku nyingine unapaswa kutimiza wajibu wako wa kutumikia wananchi na sio kumsumbua mpenzi wangu”
“Nimekubali kushindwa Bro , kama nilivyoahidi nitatekeleza’Aliongea Robert kisha alimsogelea Hamza na kumpatia mkono.
“Hamza unaonaje tukishikana mikono kama ishara ya kuwa marafiki kwanzia sasa?, natumaini utamfanya Dina kuwa na furaha”Aliongea na kumfanya Hamza amuone kweli bwana huyo ni mwanasiasa lakini hata hivyo aliishia kunyoosha mkono kumkubalia.
Upande wa maegesho ya magari mara baada ya bosi Side kuingia ndani ya gari yake Audi R8 aliweza kumuona Salma akiwa ameshaingia tayari.
“Shuka!”Aliongea kikauzu na kumfanya Salma kutia huruma.
“Side naomba unisamehe mpenzi wangu , sikujua kama Hamza angekuwa na bahati kiasi kile , naomba usikasirike”
“Eti bahati , kuna bahati ya namna ile mtu kuweza kulenga shabaha eneo moja kwa mara zote kumi au unaongea upuuzi?”
“Lakini kwanini upo hivi Side , kuna kingine tofauti na hiki kilichotokea , tumekuwa wapenzi kwa zaidi ya miaka minne sasa na nimeamua kurudi kwa ajili yako , lakini kwanini kadri siku zinavyosogea unazidi kuwa mkali kwangu?”
“Kama unadhani nimekuwa mkali kwako , basi rudi China ukaendelee na mambo yako sikukuambia urudi kwa ajili yangu”
“Sirudi tena China, awamu hii nimerudi ili unioe”
“Nani kasema nitakuoa , hebu toka kwenye gari yangu kabla sijakufanya kitu kibaya”Aliongea na kumfanya Salma kuzidi kuona Side anamkosea na alishuka kwa hasira na kuondoka lakini hata hivyo Side hakujali , mara baada ya kuingia katika gari yake alianza kutafuta majina katika simu yake na kuweka sikioni ikionyesha anapiga simu.
“Side , naona leo umepata muda wa kunipigia?”Sauti ya kike ilisikika.
“Lea hebu acha maneno yako , kuna kitu nataka unisaidie nitakulipa hela”
“Kila unapoongelea hela ujue una stress , haya niambie ni kipi unataka nikusaidie?”
“Leo nimegundua siri ambayo Hamza anaificha , nataka umwambie Prisila…”Aliongea Saidi huku akiwa na tabasamu lililojaa uovu.
******
Upande mwingine ndani ya makazi ya mrembo na Daktari , Frida Franklin katika chumba cha Master alionekana mrembo huyo akiwa amejilaza na kukoroma kabisa , alionekana alikuwa amechoka kwa namna alivyokuwa amelala.
Taa ya kitandani ilionekana haijazimwa na pembeni yake kuna kitabu kilichokuwa kimefunguliwa , ikionyesha alipitiwa na usingizi wakati akiwa anasoma.
Zilipita sekunde chache tu muda ule hali ya hewa ya kile chumba ilibadilika , ilikuwa ni kama upepo umeongezeka na kumfanya Frida kuanza kujinyoosha kitandani.
Mara ghafla tu chumba kile kilirudi katika hali ya utulivu wa hali ya juu na kumfanya Frida kujigeuza na kulala chali , lakini utulivu ule uliambatana na maajabu yake kwani ghafla tu kilionekana kivuli kikitokea kwenye pembe ya chumba hicho.
Ajabu ni kwamba kifizikia ili kivuli kitokee kinahitaji mwanga lakini kivuli hicho kilitokea bila ya kuwa na chanzo cha mwanga.
Kile kivuli kilikuwa na umbo la mtu lakini kwa namna moja ama nyingine kama ni mtu katika uhalisia basi angekuwa akitisha kutokana na eneo lake la kichwa kukosa mpangilio mzuri.
Wakati Frida akiwa hana hili wala lile mkono wa kivuli kile cha mtu wa ajabu ulinyooka ni kama ulikuwa ukirefuka kutoka eneo kilipo mpaka kwenye kitanda , mkono ule ukimlenga Frida katika shingo yake.
Ghafla tu ni kama Frida alishituka lakini alianza kurusha miguu kama mtu ambae amekabwa shingoni , alijikuta akirusha Miguu huku akijitahidi kuvuta hewa.
Lakini mwanamke mrembo huyo alionekaa kushindwa kabisa kupambana na mkono ule wa Kivuli cha mtu na ulionekana ni kama umedhamiria kumuua.
Frida alijikuta kadri sekunde zinavyoenda ndio ambavo alikuwa akikosa nguvu kutokana na kutoweza kuvuta pumzi ,aliishia kurusha rusha miguu huku akionekana muda wowote atakata roho.
MWISHO WA SEASON 2
ITAENDELEA.

0687151346 WhatsApp
Very nice 👍👍👍
 
SHETANI RUDISHA AKILI ZETU

MTUNZI: SINGANOJR

SEASON 03
SEHEMU YA 61.
Frida alijua kabisa anakwenda kufa na kifo chake kuja kuwa utata , aliweza kuona kilichokuwa kimemkaba kooni ni kivuli lakini hakuweza kufanya chochote.
Kwa mtu wa kawaida unaweza useme Frida alikuwa amepatwa na ukichaa au ugonjwa wa ajabu lakini ukweli ni kwamba kuna nguvu iliokuwa ikimkaba kupitia kivuli.
Wakati akiwa amekata tamaa ghafla tu ule utulivu wa kile chumba ulitoweka , ilikuwa ni kama upepo umeongezeka kwa kiasi kikubwa na kufumba na kufumbua kivuli kile kilipotea na kumfanya Frida kuanza kukohoa kwa nguvu , mpaka anakuja kutulia alijikuta akishituka mara baada ya kugundua kuna mtu mwingine ndani ya chumba chake alievalia joho la rangi nyeusi, alitaka kupiga yowe lakini mtu yule alimpa ishara ya kutulia.
“Wewe ni nani?”Aliuliza Frida kwa sauti ya chini huku akiwa ameshika shingo yake , ilikuwa bado hakuamini kama alikuwa amepona.
“Msimamizi wako na mlinzi wako mpya”Aliongea kwa lugha ya kingereza na kumfanya Frida kuchangayikiwa.
“Sikuwa na msimamizi na mlinzi , kwanini unajitambulisha kama mlinzi wangu mpya , nataka kujua unatokea upande upi , Wiccan au Sinagogu?”Aliongea Frida kwa sauti kubwa kidogo.
“Mimi ni mu’ alkemi kutoka makao makuu ya Wiccan , nipo hapa kwa maagizo ya Madame, mlinzi wako wa zamani amepoteza maisha”Aliongea na kumfanya Frida kuzidi kuchanganyikiwa lakini mara baada ya kusikia mtu huyo yupo hapo kwa maagizo ya Madame alipata ahueni.
“Mlinzi wangu wa zamani , unamaanisha mlinzi gani?”
“Alietaka kukuua amemuua mlinzi wako , kwanzia sasa utakuwa chini ya ulinzi wa binadamu”Aliongea huku akisogea karibu na mlango.
“Nilikuwa na mlinzi kivuli!!?”
“Wewe ni wa muhimu sana kwa Madame kuwasiliana na waumini wa ulimwengu wa nje ya kivuli , kwa namna yoyote unapaswa kuwa salama”Aliongea.
“Kwanini alitaka kuniua?”Aliuliza Frida, alikuwa akijua mtu ambae alitaka kumuua ni kivuli au watu ambao wamepata umaarufu kwa jina la Night Shadows(Vivuli vya watu vinavyoonekana usiku).
“Sina majibu kuhusu swali lako lakini nina ujumbe kutoka makao makuu”Aliongea kama roboti.
“Ujumbe gani?”
“Hakikisha anatumia mshumaa kurekodi ndoto zake ndio utakuwa salama, kadri atakavyoota bila ndoto zake kurekodiwa mtiririko wa matukio utakosekana na mpango wote kuingia dosari”Aliongea.
“Unamaanisha Ha…”
“Sikutajiwa jina , huu ndio ujumbe kutoka makao makuu unaopaswa kufanyia kazi”Aliongea yule bwana. Frida alitaka kuuliza swali zaidi lakini alijua asingepata majibu.
Yule bwana alievalia joho la rangi nyeusi mara baada ya kuridhika kwa kuona Frida alikuwa ameelewa aliaga.
“Wakati wowote ukiwa katika hatari na kuhitaji msaada wangu tamka neno , Grishav nitaitikia wito wako”Aliongea na palepale bila ya Frida kujibu aliinama chini na kufumba na kufumbua alipotea.
Frida alijikuta akiingia katika maswali mengi na swali kubwa lilikuwa juu ya ule mshumaa , alijua maelekezo yale yalikuwa yakimlenga Hamza lakini alishangaa mara baada ya kuambiwa Hamza anapaswa kutumia mshumaa ule ili kurekodi ndoto zake.
Swali ambalo alijiuliza inakuwaje mshumaa ambao alipatiwa na Dokta Genesha kuwa na uwezo wa kurekodi ndoto , kitu ambacho Wiccan walitaka iwe hivyo , inamaana kuna mpango uliokuwa ukiendelea kati ya Dokta Genesha na Wiccan kiasi cha kumkabidhi Mshumaa wa Nuru kwa ajili ya kumpatia Hamza.
Frida alijiuliza ni kitu gani ambacho kinaendelea yeye hakijui na kwanini amenusurika katika kifo.
Alikumbuka kwamba asipofanikisha Hamza kutotumia mshumaa basi atakuwa hatarini lakini swali lingine liliibuka inamaana Hamza alikuwa akiota bila ya kutumia ule mshumaa.
Kitu ambacho Frida alikuwa akijua ni kwamba mshumaa ule ulikuwa ni kwa ajili ya kumletea Hamza ndoto tu ili kujua maisha yake ambayo ameyasahau , hayo ndio yalikuwa maelekezo kutoka kwa Dokta Genesha na hakuelezwa kwamba mshumaa ule ni kifaa cha kurekodi ndoto, alijiuliza kama ni hivyo kinarekodi vipi hizo ndoto , ni sayansi ya namna gani ambayo imetumika.
Alijikuta hata usingizi ukimpelea kabisa licha ya kwamba alijihisi uchomvu mkubwa , hofu ilimvaa na hisia zake zilimwambia pengine anachofanya sio kuhatarisha usalama wake tu bali anahatarisha na usalama wa Hamza.
“Sina jinsi kwasasa lazima nihakikishe Hamza anatumia mshumaa ili kuwa salama , wakati nikitafuta majibu ya maswali yangu yote. Lakini nitafanya nini kumfanya atumie mshumaa kama yeye mwenyewe haniamini vya kutosha mpaka kuutumia?”Aliwaza Frida.
******
Hamza mara baada ya Side na wenzake kuondoka alibakia na mrembo Dina , wote wawili hawakuwa na ile mudi ya kwenda floor za juu kwa ajili ya kulewa vileo na kufanya starehe zingine kama kucheza kamari.
Kitu pekee ambacho Dina alipenda ndani ya Club hio ni kutumia siraha kulenga shabaha na hata Hamza alikuwa akipenda kitu kama hiko , kwake hakuwa mpenzi sana wa vileo na kucheza disco.
Walitumia zaidi ya lisaa limoja na nusu kulenga shabaha kwa kutumia bunduki za aina mbalimbali.
Ilipotimia saa tano kasoro njaa zilikuwa zikiwauma na Hamza alipendekeza warudi Kijichi ndio wakapate chakula huko na Dina hakupiinga.
Mara baada ya kufika kijichi chakula kiliandaliwa na wote wakaanza kula pamoja.
“Unaonaje baada ya hapa ukaangalie maendeleo ya vijana wangu , tokea siku ile ulivyowafundisha kiasi namna ya kucheza Karate na Kung Fu hukuwaona tena”Aliongea Dina.
Hamza kipindi kabla ya kukutana na Regina alikuwa ameshawahi kuwafundisha vijana wa Dina mafunzo ya Karate na Kung Fu mara moja na hakuwahi kwenda tena kuwaona.
“Hakuna shida , kuna kitu pia nataka kwenda kukifanyia mazoezi”Aliongea Hamza.
“Kitu gani , ni kuvuna nishati za mbingu na ardhi au kitu kingine?”Aliuliza Dina kwa shauku alikuwa akijua Hamza ana mafunzo ya kuvuna nishati za nguvu ya asili ya ardhi na mbingu na alitamani kujifunza pia siku moja.
“Hutoelewa hata nikikuambia ni kama maneno ya kutamka nataka kuyafanyia majaribio”Aliongea Hamza.
Ukweli ni kwamba kitu ambacho alikuwa akienda kufanyia majaribio ni yale maneno ambayo Yonesi alimtajia wakati akiwa hospitalini , siku ile wakati akifanya tahajudi kwa kupitia yale maneno aliona sura ya mwanamke ambae anamuona katika ndoto , bado shauku yake juu ya tukio lile haikuwa imeisha na alitaka kwenda kujaribu tena.

Baada ya kumaliza kula Hamza alitoka akiongozana na Dina pamoja na Lawrence na kwenda katika ukumbi maalumu ambao ni kama eneo la mafunzo ya kimapigano.
Hakukuwa na matumizi ya siraha , ilikuwa ni sehemu ambayo watu wa Dina walikuwa wakijifunza namna ya kupigana kwa kutumia mbinu mbalimbali za sanaa ya mapigano , eneo hilo lilikuwa likitambulika hata kwa serikali na lilikuwa na kibali kabisa.
Ni eneo ambalo lilijengwa katika mgawanyo wa sehemu mbili , sehemu ya kwanza ilikuwa ni kwa kufanyia mazoezi ya kawaida kama Gym na mazoezi ya boksa, Karate na Judo upande mwingine ulikuwa ni wa tahajudi.
Katika sanaa ya mapigano tahajudi ilikuwa ni sehemu ya mazoezi kwa ajili ya kuujua mwili wako ulivo, ukifanya tahajudi kama binadamu utajuwa wapi kuna udhaifu wako na wapi nguvu zako zinakaa kwa wingi na namna gani ya kushinda udhaifu wako.
Hamza mara baada ya kuona vijana wa Dina wakichukua mazoezi aliridhika , aliweza kuona wengi walikuwa wamepiga hatua kwa kufuata maelekezo yake.
“Bro , unapanga kufanya mazoezi ya namna gani , unataka kufanya tahajudi?”Aliuliza Lauwrence mara baada ya kumuona Hamza akichagua upande wa wanaofanya Tahajudi.
Dina na Lawrence siku zote walikuwa na shauku ya kutaka kumuona Hamza akichukua mazoezi hivyo walimwangalia.
“Kaa kimya Lau acha maswali mengi”Aliongea Dina akimzuia Lau kutokumsumbua Hamza na maswali yake.
Kutokana na wale wanafunzi kumuona Hamza na wao wote waliacha na kumpatia Hamza nafasi , kwao ni kama kuna kitu ambacho walitaka kujifunza kwa kumuangalia ndio maana walisimama pembeni.

Wakati Hamza akiwa katika mkao wa kufanya tahajudi huku midomo yake ikicheza ghafla tu watu wote walijikuta wakikumbwa na msisimko wa ajabu , ilikuwa ni kama kuna kiumbe cha ajabu kimefika ndani ya eneo hilo na kuwafanya kuanza kushindwa hata kupumua vizuri huku eneo ambalo Hamza alikuwa amekaa anga lake ni kama lilikuwa likitingishika.
Dina alijikuta jasho la paji la uso likimtoka huku akimwangalia Hamza kwa wasiwasi , alipatwa na hisia kama vile Hamza amekuwa mfalme ghafla na yeye ni kijakazi wake.
Upande wa Hamza hakuwa hata akielewa kilichokuwa kikiendelea kwa nje , kama alivyotarajia maneno yale yalikuwa ni kama anamwita yule mwanamke , mara ya kwanza wakati alivyofanya kule wodini alimuona kwa mbali yule mwanamke , lakini wakati huo kadri alivyokuwa akiimarisha umakini wake wa ubongo na kuzidi kuyatamka yale maneno alimuona ni kama vile yule mwanamke mchawi anaemuona kwenye ndoto alikuwa akimsogelea kutoka angani kwa spidi ya ajabu.
Zilipita kama dakika nne tu yule mwanamke aliweza kumuona kwa ukaribu zaidi, lakini jambo ambalo lilimshangaza Hamza ni kitu ambacho alikuwa ameshikilia mkononi.
Kadri alivyokuwa akizidi kuongea yale maneno mwanamke yule alizidi kusogea , lakini ilifikia hatua ni kama hawezi kumfanya asogee zaidi na yule mwanamke ni kama alijua Hamza hawezi kumuita karibu zaidi na alichokifanya ilikuwa ni kunyoosha kile kitu alichoshikilia mkononi mwake na Hamza mara baada ya kuangalia vizuri alijikuta akipagwa , ulikuwa ni ule mshumaa ambao Frida alimpatia akimwambia umetoka kwa Dokta Genesha, Mshumaa wa Nuru.
Hamza alichanganyikiwa mshumaa wa nuru kwanini upo katika mikono ya huyo mwanamke , katika ndoto yule mwanake alimuona kama mchawi ambae anachomwa moto baada ya kukamatika lakini kwanini akashika kitu cha nuru ilihali nuru na uchawi ni vitu viwili tofauti.
Yule mwanamke ni kama alikuwa akitaka Hamza amsogeze karibu aweze kushika ule mshumaa , upande wa Hamza alionekana kusita kuupokea ule mshumaa na yule mwanamke ni kama aliliona hilo na alitamka neno kwa kunyanyua mdomo wake kwa juu bila kutoa sauti akihakikisha Hamza anasoma lipsi zake.
NISAIDIE!(Help me)
Ndio neno ambalo aliongea huku akimpa ishara Hamza kupokea ule mshumaa.
Muda uleule Hamza aliacha kutamka yale maneno na kitendo kile kilifanya yule mwanamke ni kama vile kuna nguvu iliokuwa ikimvuta na kuzidi kurudishwa nyuma mbali na yeye , lakini bado hakuacha kumnyooshea ule mshumaa kama ishara ya kumuomba amsaidie.
Muda ileule wakati kila mtu akiwa ameloa jasho kana kwamba eneo lote limekumbwa na joto kali Hamza aliweza kufungua macho yake huku akionyesha hali ya kuwashangaa waliokuwa wakimwangalia .
“Nini kimetokea, Dina mbona upo hivyo?”Aliuliza Hamza mara baada ya kumuona
“Bado tu unapata muda wa kuuliza , ni kitu gani ulichokuwa ukifanya?”Aliuliza Dina na kumfanya Hamza sasa kuelewa kilichokuwa kikiendelea , licha ya yeye mwenyewe kuwa na wasiwasi lakini aliishia kucheka.
“I am sorry !, hii ni mara yangu ya kwanza kujaribisha hiki kitu , sikuweza kujizuia kile kinachonizunguka”AliongeaHamza na kisha alipiga hatua kuondoka katika eneo hilo.
Na wakati wakianza kutembea ndio sasa waligundua paa la jengo hili lilitingishika sana na kutokana na mchwa kula mbao unga unga ulidondoka chini kwenye tailizi na kila walipokuwa wakipiga hatua walikuwa wakiacha nyuma alama za miguu.
“Muda umeenda sana , nataka nirudi nyumbani”Aliongea Hamza.
“Hamza ni mafunzo gani yale , ni nguvu ya ndani au nishati ya mbingu na maji?”
“Ilianza mbingu ikaja ardhi halafu mbingu ikaleta maji na uhai , hizi ni kanuni za mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi na ni kitu ninachoweza kufanya pia , lakini kuhusu nilichofanya sasa hivi hata sijui ni kitu gani , kama nilivyosema nipo kwenye utafiti”Aliongea Hamza
“Hata jina lake hujui?”Aliuliza Dina kwa mshangao.
“Ndio ila kwasasa nitaiita hii kama Wito, kwasababu ukiifanya ni kama kuna kitu unakiiita”
“Huwa haifurahishi kusikiliza pekee”Aliongea Dina kwa macho yaliojaa huzuni na shauku.
“Usiongee hivyo , hiki ni kitu ambacho siwezi kukuruhusu ufanye kabla sijakipatia majibu , nguvu yake ni kubwa kiasi kwamba ni kama sijakula kabisa”Aliongea Hamza huku akijihisi ni mwenye njaa kali.
Dina alimwambia twende ukale na Hamza hakuwa na aibu ya kukataa kwani alikuwa na njaa , muda huo hawakurudi kwenye mgahawa bali Hamza alienda mpaka yalipo makazi ya Dina mita kadhaa kutoka mgahawa wake ulipo na mfanyakazi aliagizwa kuandaa chakula na Hamza alikaa chini na kuanza kukifakamia huku Dina akimwangalia kwa macho yaliojaa mahaba.
“Unajua nilishangaa baada ya mstaafu Mgweno kunipigia simu akisema yaishe”Aliongea Dina.
“Kwanini yeye ndio kakupigia simu?”,
“Unaweza kushangaa , licha ya kwamba kwa nje inaonekana familia ya Benjamini ndio inataka Regina kuolewa na James lakini upange mwingine ni mipango ya Mheshimiwa Mgweno”Aliongea Dina.
“Unataka kumaanisha nini?”
“Labda utakuwa hujui tu , ila kampuni ya Dosam ni kubwa Tanzania na inachangia zaidi ya asilimia tatu ya pato lote la Taifa , imeshikilia uchumi wa nchi katika maeneo nyeti, Benki namba moja ya kibiashara inayoongoza kwa Tanzania na Afrika mashariki yote ni Dosam Commercial Bank huu ni kama utawala wa mzunguko wa fedha nchini , hapa bado hujazungumzia usafiri wa anga , mahoteli na usambazaji wa bidhaa mbalimbali kwa matumizi ya majumbani, Kabla ya mheshimiwa Mgweno hajaingia madarakani Kampuni ya Zena ilikuwa ya kawaida tu kulinganisha na Dosam lakini baada ya Mgweno kuingia madarakani ilikua kwa spidi ya hali ya juu na yote hii ilikuwa ni uwekezaji mkubwa ambao mheshimiwa alifanya kwa kuiba hela za wananchi”Aliongea Dina.
“Kwahio unachomaanisha ni kwamba kampuni ya Zena inamilikiwa na Mheshimiwa mstaafu Mgweno?”
“Ndio kwa asilimia zaidi ya arobaini na tisa, ukifuatilia wana hisa wa kampuni ya Zena utagundua wengi wanaomiliki hisa hizo ni kampuni kutoka nje ya nchi , ukifuatilia kampuni hizo nje ya nchi utagundua kwamba ni kampiuni ambazo zimepewa haki kisheria ya kumiliki hisa hizo na kampuni nyingine , mzunguko unaendelea hivyo hivyo, zote ni njama za Mgweno kuficha wananchi kwamba anaimiliki Zena , sio kampuni moja tu , kila kampuni kubwa ana ushawishi wa kimaamuzi”
“Zote hizo ni hela za rushwa!?”
“Ndio lakini hakuna ushahidi wa kuthibitisha kama ndio mmiliki, sehemu pekee ambapo amekosa umiliki na ushawishi ni kampiuni ya Dosam peke yake na hii ni kutokana na msimamo wa aliekuwa kuongozi wa kampuni yaani babu yake Regina”Aliongea Dina na sasa ni kama Hamza alikuwa akipata picha.
“Kwahio anajaribu kuitumia familia ya Benjamini kwa ajili ya kuingiza ushawishi wake katika kampuni ya Dosam?”
“Ipo hivyo , mwanzoni walijua mambo yataenda sawa kama Regina atakubali kuolewa na James lakini mambo yamekuwa magumu , Regina karithi tabia zote za waanzilishi wa ile kampuni”
“Unamaanisha bibi yake na babu yake, unachoongea kinaonekana kuwa sahihi”Aliongea Hamza.
“Mgweno anachotaka ni kuimiliki Tanzania katika kila nyanja , kwanzia mtandao wa biashara haramu , biashara halali na kisiasa , hii itaifanya familia yake kuwa ya kifalme na raisi ni kama waziri mkuu tu anaepokea maagizo kutoka kwao”
“Kama ndio anachowaza anajidanganya , kuna mifano mingi ya kihistoria ni ngumu sana kuuchimba msingi wa nchi na kutengeneza nyufa pasipo kushitua wamiliki wake”
“Pengine anaelewa ila anaona ni kheri kujaribu kuliko kufa bila ya kujaribu”
“Kwahio baada ya kuona familia ya mzee Benjamini imekwama njia pekee alioona ni kumuua Regina maana urithi utaenda kwa mtoto wa pili?”
“Ndio lakini mipango yake inaonekana kukwama kutokana na uwepo wako , niseme tu umetibua mambo mengi sana , najua hata kunipigia simu ni kutokana na kujua ukaribu wetu na anatangeneza mazingira ya kujihami, lakini kwa wanaojua Mgweno kuna kitu lazima anapanga, walijaribu hadi mbinu ya kutaka kumtengeneza mtu wao ambae yupo karibu zaidi na Regina”Aliongea Dina na kumshangaza kidogo Hamza.
“Unamaanisha wale wazee ambao Regina amewafurumusha?”Aliuliza.
“Huo haukuwa mpango , wale wazee walikuwa wakifahamika tokea kipindi kirefu wapo kinyume na uongozi wa Regina”
“Ni nani ambae walikuwa wakimlenga?”
“Mchepuko wako alieniingiza kwenye matatizo”Aliongea huku akivuta midomo”
“Eliza!?”
Dina alitingisha mabega lakini kabla ya Hamza hajauliza swali lingine mlango wa kuingilai uligongwa kwa nguvu na Lawrence alionekana akiingia kwa pupa.
“Kuna nini Lawrence?”Aliuliza.
“Nimeletewa taarifa muda huu na vijana , Mheshimiwa Jongwe amefariki dunia kwa ajali ya gari na jeshi la polisi limeishikilia familia ya Mzee Seif kama washukiwa namba moja”Aliongea Lawrence na habari ile ilimtoa macho Dina.
“Unamaanisha mgombea wa kiti cha uraisi kupitia chama tawala , Jongwe amefariki, tena kwa ajali , kwanini familia ya mzee Seif ihusishwe kama ni ajali?”Aliongea Dina.
“Inawezekana sio ajali ya kawaida”Aliongea Hamza.
“Kwa maelezo niliopatiwa gari ambayo alikuwa amepanda imelipuka na ndani yake alikuwa ameambatana na Mzee Martin”Aliongea Lawrence na alivyoongea ni kama alijua taarifa ile itamshitua bosi wake na ilikuwa kweli kwani Dina alijikuta akisimama akiwa kama haamini.
“Mzee Seif na Mzee Martini mbona kama ushawahi kunitajia hawa watu?”Aliuliza Hamza.
“Ndio Bro hawa ndio washirika wetu wakubwa, japo mara nyingi inaaminika Mzee Seif ana uadui wa kisiasa na Mzee Martini”Aliongea Lawrence.
“Kwanini inaaminika hivyo ?”
“Kwasababu wote ni wanasiasa wa vyama tofauti , Mzee Seif ni kutokea chama cha upinzani na Martini ni kutoka chama tawala na wamekuwa wakipishana kama wabunge katika jimbo moja kwa zamu , uchaguzi huu akishika mzee Martini mwaka mwingine anashika Mzee Seif , awamu hii inayoisha Mzee Seif anamaliza muda wake lakini uelekeo wa kura upo upande wa Mzee Martini , siasa zao mara nyingi ni za kurushiana maneno”Aliongea Lawrence.
“Kwahio jeshi limemkamata Mzee Seif kwa kuamini kwamba ametegesha bomu katika gari la Mzee Martini ili ashinde uchaguzi , kama ni hivyo mgombea wa uraisi wa chama tawala kwanini amekufa pamoja na Martini?”Aliuliza Hamza lakini ni kama alikuwa akiipata picha.
“Lazima kuna kitu Mgweno anajaribu kufanya , hizi zote ni hila za kutaka kubomoa mtandao wa Chatu”Aliongea Dina kwa hasira.
“Lakini Madam Mheshimiwa Jongwe ni mgombea ambae amepata sapoti kubwa kutoka kwa mheshimiwa Mgweno , kwanini afanye hila ya kumuua mgombea ilihali zimebakia wiki chache kabla ya wananchi kupiga kura”
“Kesho kutwa pia ndio ilitarajiwa mkutano wa mwisho wa chama tawala kufanyika ili kufunga kampeni”Aliendelea kuongea Lawrence.
“Kuna picha inanijia akilini”Aliongea Hamza lakini upande wa Dina alionekana kuwa katika majonzi ya kumpoteza Mzee Martini, alikuwa ni moja ya mhimili wa mtandao wake.
“Lawrence polisi wanamshikilia kituo gani Mzee Seif?”
“Nasikia hawajamkamata bali wameizingira nyumba yake huko Kigamboni Mbutu B”Aliongea Lawrence.
“Yaani baada ya dakika kadhaa mlipuko kutokea na kuua watu, tayari washafikia maamuzi Mzee Seif ndio muhusika , mbona haingii akilini , hii lazima ni njama ya kutaka sisi twende tukamsaidie”Aliongea Dina.
“Tena nina uhakika hata hao wanaoitwa polisi ni feki”Aliongea Hamza huku akiweka kijiko chini.
“Madam tunapaswa kufanya nini?”Aliuliza Lau.
“Kama ninachofikiria ni sahihi lazima hili linahusiana na kikao nilichofanya na mheshimiwa Mgweno siku kadhaa zilizopita , mtandao wetu wote unajua ni kwa namna gani Mzee Seif alikuwa mwaminifu , nisipoingilia na kulifanyia hili maamuzi unadhani nitaonekanaje , Lawrence kusanya vijana wote ambao hawako mbali tutaenda kuangalai kinachoendelea”Aliongea Dina.
“Lakini Madam ulitoa maelekezo ya vijana karibia wote wakae chimbo , waliopo karibu na mjini hawazidi hata hamsini?”
“Haina haja”Aliongea Hamza huku akisimama.
“Watu hamsini ni wengi sana na hili linaweza kuwa ni mtego , hebu ita wale kumi kutoka jumba la mazoezi waje hapa , wanatosha sana”
“Bro unataka na wewe…”
“Hamza na wewe unataka kwenda?”
“Nataka nikajionee kinachoendelea , kama kweli huu mpango kaupanga Mgweno basi atakuwa katumia akili , unadhani kwa katiba yao ya chama nini kinafuata mara baada ya mgombea mkuu wa chama kufariki ghafla?”Aliuliza Hamza.





SEHEMU YA 62.
“Sijui kuhusu katiba yao inachosema , ila nina uhakika mgombea Mwenza ndio atachukua nafasi, kwanini unauliza?”Aliuliza tena Dina maana alijua Hamza hakuwa mtu wa siasa.
“Nawaza kuna mchezo unaochezwa hapa na kuna nguvu mbili kubwa za kisiasa , nataka kujionea mwenyewe”Aliongea Hamza na Dina alitingisha kichwa , kwasababu Hamza alitaka kwenda hakuona haja ya kumzuia , isitoshe ilimpelekea kujiamini zaidi kudili na hali kama hio.
Upande wa Dina alijua lazima kuna mchezo unaofanywa na kama Mzee Seif atakubali kuhusika moja kwa moja itaaminika mtandao wake ndio umekamilisha swala hilo , jambo ambalo hakautaka litokee.
Nyumba ya Mzee Seif ilikuwa Kigamboni Mbutu B na gari mbili ziliendeshwa kuelekea huko ya mbele akiwemo Hamza na Dina na ya nyuma ilikuwa Noah iliowabeba Lawrence na kundi lake.
Kitendo cha kufika eneo la tukio waliweza kuona watu walioizingira nyumba ya Mzee Seif , jambo ambalo liliwashangazwa hakukuwa na uwepo wa polisi hata mmoja ni kama Hamza alivyotarajia.
“Mbona sio polisi kama taarifa ilivyosema?”Aliuliza Dina kama kwamba Hamza alikuwa na majibu.
Hamza alichunguza eneo lote hasa wale watu walioshikilia siraha na alijikuta akikunja sura mara baada ya kuona wazungu wawili ndani ya eneo lile wakiwa ni sehemu ya watu waliozunguka nyumba hio.
“Ni kama nilivyotarajia kuna kinachoendelea hapa”Aliongea Hamza.
“Lakini kama kweli walikuwa wakimshuku Mzee Seif kulipua gari ya mheshimiwa Jongwe kwanini hawajaja polisi?”Aliuliza.
“Tutapata majibu yote mara baada ya kuongea nao”Aliongea Hamza huku akitangulia kutoka nje ya gari.
Wale watu kama walinzi walioshikilia siraha wakiwa wamezingira nyuma hio waliongeza umakini kwa Dina na kundi lake.
“Kama tabia yako ya siku zote, Dina mrembo wa kujiamini , naona umekuja na watu wachache mno tofauti na nilivyotegemea”Sauti ya mwanaume ilisikika kwasababau ilikuwa kuna giza hawakumuona vizuri na mara baada ya kusogelea taa za mwanga wa gari ndio Dina aliweza kumuona.
“Pancho!, unafanya nini hapa?”Aliongea Dina na muda huo ni kama sasa alishaanza kupata picha ya kile kinachoendelea.
“Nimekuja kukusalimia kwa mara nyingine mara baada ya kukataa pendekezo ya dili nono”Aliongea na muda ule alitoa ishara na baada ya kupita dakika mmoja tu wanaume wanne walitoka katika nyumba hio na moja wapo ya wanaume wale alikuwa ni Mzee Seif alieshikiliwa na wanaume wawili weusi waliojazia mwili , mtu wa mwisho kutoka alikuwa ni Mzungu- Mjapani , yaani mtu aliechanganya rangi ya mjapani na Mzungu.
Kilichomfanya Dina kuanza kupandwa na hasira alijua mpango wote huu ulisukwa na Pancho.
Pancho alikuwa ni moja ya wasimamizi wa mtandao wao upande wa Congo na siku kadhaa nyuma Dina alipokea dili kupitia kwa Pancho kutoka kwa Wacanada ambao walitaka kuingiza siraha za kivita Congo kupitia Bandari ya Mtwara.
Dili hili liliungwa mkono na Mheshimiwa Mgweno lakini Dina aliona halikuwa na maslahi na kama angelikubali ni kama kujipiga risasi mguuni, ikizingatiwa siraha hizo zilipaswa kufikishwa kwa kundi lingine la waasi ndani ya Congo tofauti na lile ambalo wanashirikiana nalo kwa muda mrefu.
“Mzee Seif nini kimetokea , kwanini taarifa nilizopokea ni wewe kuhusika na kumuua Mzee Martini na mheshimiwa Jongwe?”Aliuliza Dina akimpotezea Pancho.
“Hawa ndio wahusika , wameiteka familia yangu na wanataka nikiri kuhusika kwa kushirikiana na wewe kumuua Jongwe au turejee mezani na kuanza mazungumzo ya kuingiza siraha Tanzania kwenda Congo”Aliongea Mzee Seif aliekuwa na hali ya hofu na kumfanya Pancho kutoa tabasamu.
“Pancho unajaribu kufanya nini , nani yupo nyuma yako?”
“Dina hakuna ambae yupo nyuma yangu?”Aliongea Pancho kwa kejeli.
“Kwa kumuua mgombea wa uraisi kupitia chama tawala, unasema hakuna ambae yupo nyuma yako?”Aliongea Dina kwa hasira na kumfanya Pancho kutoa tabasamu la kifedhuli.
“Nilitaka hili swala angalau ulichukulie kwa uzito wake, ushahidi wa wewe kuhusika katika shambulizi la kulipua bomu gari ya mgombea wa uraisi kupitia chama tawala upo , unaweza ukawa wa kutengeneza lakini jeshi la polisi lipo tayari kuuamini na kama likitoka uraiani , kitengo cha TISA kitakufanya mbuzi wa kafara, lakini huko kote ni kujisumbua kama upo tayari kuchagua chaguo zuri kati ya matatu alioongea Mzee Seif?”
Hamza muda huo alikuwa akiangalia mazingira yalivyo na watu wote waliokuwa hapo walikuwa na siraha za bunduki na haraka haraka kwa sheria ya Tanzania ilikua ngumu kwa watu hao kumiliki hizo siraha labda iwe kuna mtu ndani ya serikali ambae alikuwa akihusika.
Isitoshe safari yao kutoka kijichi mpaka kufka hapo , kama kweli jeshi la polisi lilikuwa sirasi kukamata watu hao waliomsababishia ajali mgombea wa kiti cha uraisi basi wangeshafika labda tu iwe kuna maagizo ambayo yamewafanya kuchelewa.
“Hizo siraha mnaotaka kuingiza Tanzania mnazitoa wapi?”Aliongea Hamza.
“Oh!, ahsante kwa kuuliza bwana mdogo , kidogo tu nimesahau kumtambulisha bosi wetu hapa , huyu ni Bosi Keita na ndio msingi wa haya maungumzo , kuhusu wapi siraha zinatoka ni juu yake”Aliongea Pancho kwa kujigamba.
“Pancho kama nilivyosema mtandao wetu haudili na maswala ya siraha bila ya utaratibu maalumu, kama unataka dili hili lipite lisimamie wewe mwenyewe na hela zako na sio za mtandao wa Chatu”Aliongea Dina na yule bwana mwenye asili ya kizungu na Kijapani alimpa ishara Pancho ya kuongea yeye.
“Miss Dina kama alivyoongea Pancho tunaweza kulimaliza hili swala kimya kimya na kusiwe na athari zozote kwa kila upande”Aliongea kwa Kingereza.
“Unamaanisha unaweza kuzima kesi ya kulipua gari ya mgombea wa Uraisi pamoja na Martini?”Aliuliza Lawrence.
“Itategemea na maamuzi ya Miss Dina?”
“Kwanini nahisi hata waliompendekeza Jongwe kupeperusha bendera ya Chama ni kama wanashangilia kifo chake?”Aliongea Hamza huku wakati huo Dina akiwa ametulia.
“Tunafanyaje?”Aliuliza Dina akimegemea Hamza , isitoshe ndie aliesema wasije na watu wengi.
“Wana siraha na hata kama tukishambuliana bila siraha hatuwezi kushinda bila kushitua raia , hawa watu wana mafunzo ya mapigano”Aliongea Hamza na kumfanya Dona kuwa na wasiwasi.
“Usiwaze hili naweza kulimaliza kwa amani na kisha utadili nao kujua nini kinaendelea kuhusu mgombea wa uraisi kulipuliwa”Aliongea Hamza na japo Dina alikuwa na wasiwasi aliamua kumwamini Hamza.
“Bwana Keita kwa ninavyojua huwezi kudili na siraha pasipo kuwakilisha shirika la giza unalotokea”Aliongea Hamza akitaka kujua Black Association ambayo Keita anatokea.
“Jungle Army Merchant ndio ninatokea”Aliongea bila ya kusita sita.
“Kumbe ni Jungle , hebu subiri kwanza nipige simu, nikimaliza utaamua cha kufanya”Aliongea.
“Umpigie nani?”
“Utajua nikimaliza’Aliongea Hamza.
“Mr Keita haina haja ya kupoteza muda na hawa watu , swala ni moja tu wachague chaguzi moja kati ya tatu tumalizane”Aliongea Pancho akionekana kukosa uvumilivu.
“Kimya! , sitaki unifundishe namna ya kufanya biashara”Aliongea Keira kwa kingereza na kumfanya Pancho kukaa kimya , isitoshe alikuwa akijua Jungle Army Merchant walikuwa wafanyabiashara wakubwa ndani ya Black Market kwa kuuza siraha za kila namna.
Muda huo Hamza alikuwa ashapiga simu tayari bila ya kuwa na wasiwasi kabisa.
*****
Magneto, Las Vegas- USA
Ni ndani ya jiji la Las Vegas , jiji ambalo kwa wacheza kamari hawakuhesabu muda , Usiku ni kama mchana na Mchana ni kama usiku tu ndani ya hili jiji.
Katika moja ya hoteli ya kifahri ya nyota tano ndani ya chumba cha hadhi ya raisi , alionekana mtu bonge mweusi mwenye kitambi akiwa amelala chali.
Alikuwa mrefu wa mita kama moja nukta tisa hivi , vidole vya mikono yake vilikuwa vimevishwa pete za madini ya almasi , Dhahabu na madini mengine ya thamani , shingoni alikuwa amevalia mikufu ya bei ghali.
Mtu yule bonge alijikuta akitandaza miguu yake vizuri huku akifumba fumba macho na kuyafumbua , katikati ya eneo la mapaja yake alionekana mwanamke mzungu mwenye nywele nyeupe(blonde) akiwa bize kumhudumia.
“Mr Mamen are you comfortable?”Aliuliza yule mwanamke kwa sauti tamu huku akiinua kichwa chake akimwangalia kwa macho malegevu , akimuuliza Big kama ni mwenye kuifurahia huduma.
Mwanaume yule bonge udenda ulikuwa ukitaka kumwagika kutoka kwenye midomo yake , alionekana alikuwa kwenye ulimwengu mwingine wa raha.
“Comfortable..!?, Deeper the better .”Aliongea akimaanisha azame chini zaidi ndio itakuwa vizuri.
“You’re so annoying , I’m realy tired ..”Aliongea yule mwanamke akimwambia anachukiza kwani amekwisha kuchoka.
Bonge yule mweusi kama msanii RickRoss alifungua droo ya meza pembeni na kitanda chake na kuchomoa maburungutu ya pesa za dola na kumtupia.
“Hakikisha najisikia vizuri mpaka kisogoni , nitakupa kiasi chochote cha pesa unachotaka”Aliongea Big na yule mwanamke uchomvu uliisha palepale na alijkuta akiongeza mashambulizi ya kuhakikisha Big anajisikia vizuri.
Dakika hio hio simu yake ilianza kuita , hata simu yake tu ilikuwa imetengenezwa kwa housing ya madini ghali sana na kuifanya ionekane kama kitu kisichokuwa cha kawaida kutokana na uthamani wake
“F*ck , kama ningejua ningeizima hii simu , nani ananipigia muda huu”Big alilaani huku akichukua ile simu na kuipokea maana namba ilikuwa mpya tena haikuwa ya taifa hilo
“Big naona kama kawaida yako sasa hivi unaringa , kwahio unaona sipaswi kukupigia hata kama ni swala linalohusu vita ya tatu ya dunia”Sauti ya kiume ilisikika katika simu ya Big.
Kitendo cha Mameni kusikia ile sauti mwili wake ulitetemeka na macho yake yalibadilika na kuwa mekundu na hata ule msisimko aliokuwa akisikia ulipotea.
Yule mwanamke aliekuwa bize kuhakikisha Big anafurahi alijikuta akipiga kelele mara baada ya kadudu kabig kupotea na kuwa kabamia.
“Boss!! , ni wewe kweli , naona hatimae umenipigia , nimekumisi sana”Aliongea Big huku sauti yake ikiwa imebadilika.
“Unafanya nini hapo , lazima utakuwa na m*laya kitandani , yaani ndio kwanza kunakucha wewe unahangaika na wanawake , kuna siku utafia kwenye kifua cha mwanamke”
“Hehe..Bosi wewe mwenyewe unanijua vizuri , isitoshe wewe ndio mtu pekee ulievunja rekodi yangu”Aliongea.
“F*ck you!”Alitukanwa.
“Bosi nasikia upo Tanzania , habari za siku nyingi , vipi naweza kuja huko?”
“Nina mambo mengi ya kufanya siku hizi tutaona kama unaweza kuja , nyie watu ni wasumbufu sana mkisikia nipo mahali mnataka kuja tu , sitaki usumbufu wenu nahitaji kutulia kwa sasa”
“Bosi kwa uwezo wako na ushawishi wako unaweza kuomba chumba mapumziko Ikulu na ukapatiwa na warembo kabisa , hayo sio mapumziko ila ni kujitia stress tu , mapumziko ni yale wafariji wanakuwa wanabadilika badilika kila siku kwenye kuusisimua mwili”
“Sterehe za kutumia hela hizo nishazichoka , hata nikikuambia ni namna gani nafurahia maisha ya sasa hivi hutonielewa Big”
“Kama ni hivyo bosi kwanini umenipigia simu , kuna dili jipya?”
“Hakuna dili lingine , nishastaafu hayo mambo”
“Sababu ni ipi sasa Bosi , au kuna sehemu nimekosea?”Aliuliza Big kwa upole.
“Kwenye biashara zako unamfahamu bwana anaefahamika kwa jina la Keita?”
“Ndio mwaka juzi niliingia dili na kundi moja linalofanya shughuli zao ndani ya Afrika kuiba madini Adimu na kuyauza kwenda kwenye moja ya kampuni ya maswala ya kiteknolojia nchini Ufaransa , linaongozwa na bwana Keita”Aliongea Big.
“Huyu bwana wako naona ana juhudi mno , muda huu nimeelekezewa mitutu ya bunduki ndio maana nimekupigia simu kuthibitisha , Big kwahio sasa hivi umeshaanza kuwa mkubwa kiasi cha kunisaliti kisa tu nnimetoka kwenye uringo?”
Big mara baada ya kusikia kauli hio kutoka kwa Hamza alijikuta mikono ikimtetemeka kiasi kwamba simu ilitaka kudondoka.
“Bosi , subiri kwanza , nitampigia simu sasa hivi , naomba kwanza nimfokee baada ya hapo unaweza kumuua”Aliongea Big na dakika ileile alikata simu na kuitafuta namba ya Keita.
“Mamen Babe! , unafanya nini sasa mbona imepotea!?”Yule kahaba wa kizungu aliongea lakini Mameni alimpotezea na mara baada ya kuipata namba ya Keita aliipiga palepale.
Mara baada ya Hamza kumaliza kuongea na simu hakuongea neno na alitulia akiangalia matokeo.
Ijapokuwa Keita hakujua Hamza alikuwa akiongea na nani kwenye simu lakini alihisi kuna kitu hakipo sawa.
Dakika ileile simu yake ilianza kuita na alisogea pembeni na kupogea lakini muda huo huo alianza kuonyesha ishara za kupaniki.
Upande wa pili ilikuwa ni sauti ya Big kutukana kimarekani kwa mara nyingi mfululizo kadri alivyoweza.
“Bosi nimefanya kosa gani?”
“Unataka kumuua nani sasa hivi?”
“Bosi umejuaje nataka kuua mtu?”
“Unaetaka kumuua ni bosi wangu”
“…”
Keita alijikuta akikosa neo , alishangaa mno kwa zaidi ya sekunde kumi , ni kama alikuwa akisharabu yale maneno.
“Ah!”
Alijikuta hofu ikimwingia na vigoti vya miguu yake vilianza kumlegea na alijikuta akigeuka na kumwangalia Hamza.
Upande wa Hamza alikuwa akimwangalia Keita tu kwa mbali na kwa jinsi alivyoonyesha kupaniki na woga alitamani kucheka.
“Mr Keita , Mr Keita , what happened?”Pancho aliuliza mara baada ya kuona mabadiliko.
Dina macho yake yalichanua alijua kabisa mabadiliko ya Keita ni kutokana na Hamza alipopiga simu na kwake aliona mwanaume Hamza alikuwa akimshangaza kila siku.
“Nini tatizo Mr Keita , mbona huongei?”Aliuliza Pancho kwa wasiwasi
“Hivi unajua mimi na vijana wangu tutakufa sasa hivi kutokana na ujinga wako na wale wanasiasa wapuuzi?”Aliongea kwa hasira.
“Unamaanisha nini Mr….”
Keita hakuchelewa alichomoa Desert Eagle kutoka kwenye kiuno chake na kumchapa risasi tatu Pancho palepale.
Mpaka Pancho anadondoka chini muonekano wake ulikuwa na shauku ya kutaka kujua kwanini Keita anamshambulia.
Keita mara baada ya kumalizana na Pancho alitoa maagizo kwa vijana wake kuwashambulia watu wa Pancho na walionekana kuwa shapu kweli kwani ndani ya sekunde wote walikuwa chini.
Baada ya Keita kuituliza hali alijikuta akimdondokea Hamza kwa magoti huku akiwa na wasiwasi mwingi akitia huruma.
“Prince Rich.. Bosi wangu ameniambia kila kitu , naomba unisamehe kwa ujinga wangu , sikubahatika kukutana na wewe ana kwa ana zaidi ya kusikia habari zako ndio maana nimekukosea…”
Kitendo kile kiliwashangaza mno Dina , Lawrence na wenzake , waliishia kujiuliza Hamza ni nani mpaka bwana yule kuwa na hofu namna ile kiasi cha kupiga magoti.
“Nipe bastora yako”Aliongea Hamza akiwa siriasi na kumfanya Keita kukakamaa mwili lakini alimpatiia.
‘Tafadhari naomba uwaache vijana wangu waondoke , walikuwa wakifuata maelekezo tu kutoka kwangu na wanazofamilia zinawategemea”Aliongea Keita lakini Hamza hakumjali na muda ule aliinua ile bastora na kujielekezea kwake kana kwamba anataka kujipiga risasi.
Tukio lile lilimshangaza kila mtu wakishindwa kuelewa Hamza anataka kufanya nini
“Hamza unataka kufanya nini , usipaniki..”Aliongea Dina lakini kabla hata hajamaliza Hamza alikuwa ashaachia risasi.
Bam!
Mlipuko ule wa bunduki ulimuogopesha mpaka Keita na wote walimwaangalia Hamza kwa mshangao na walishangaa zaidi baada ya kuona hakuna kilichotokea.
Risasi ambayo ilitoka katika ile bunduki ilikuwa katika vidole vya Hamza , haikueleweka amefanyaje lakini ilionekana aliikamata kabla ya kumfikia, tukio lile lilimfanya Keita kushindwa kuendelea kupiga magoti na kukaa chini kwa kunyoosha miguu huku mapigo yake ya moyo yakidunda kwa kasi.
“Kabla sijafanya chochote nataka muelezee kila kilichotokea… sababu ya kwamba umepiga magoti sio kwasabau ya bosi wako bali ni kwasababu yangu hivyo nataka majibu”Aliongea Hamza.
“Serafii.!!, nipo tayari kuongea”Aliongea Keita huku akipiga kichwa chini kiasi cha kutoka damu kwenye paji la uso.
“Anza kuelezea , kwanini kifo cha Mgombea wa uraisi na nani kahusika”Aliongea Hamza.
“Hatujahusika katika kumuua mtu , tupo hapa nchini kwa ajili ya mazungumzo ya biashara ya kupitisha Siraha Kwenda Congo kupitia bandari ya Mtwara , kitu pekee ambacho nafahamu kuhusu muhusika tulipewa kazi ya kumtorosha hapa nchini kupitia boti yetu”Aliongea na kauli ile ilimfanya Dina kusikiliza kwa umakini.
“Imekuwaje mkajiingiza , sitaki kuuliza maswali mengi elezea kila kitu ninachotaka kujua?”
“Mara ya mwisho nilivyokuja hapa nchini niliweza kukutana na mstaafu Mgweno kwa ajili ya kuingia dili la kupitisha siraha , lakini kutokana na usafirishaji wote wa Kimagendo kuwa chini ya Chatu hakutoa maamuzi badala yake aliwasiliana na Miss Dina ambae mara baada ya kuelekezwa kuhusu dili hili alikataa, Mstaafu baada ya ombi hili kukataliwa alituambia hana namna ya kutusaidia kwani njia pekee ya kupitisha siraha hizo ni moja tu ambayo ni Mtwara kutokana na bandari zote kuwa chini ya mwekezaji”
“Nini kiliendelea”
“Wakati tukifikiria namna ya kutafuta njia nyingine ya kukamilisha dili hili nilipokea simu kutoka kwa mtu ambae alijitambulisha ni msaidizi wa raisi”Aliongea.
“Unamaaniisha Mheshimiwa Eliasi Mbilu?”
“Ndio na alisema anataka kuonana na sisi kwa ajili ya mazungumzo ya namna ya kukamilisha kile tulichokuwa tukihitaji , kutokana na kuwa na haraka ya kufanikisha hili dili nilikubali na kupitia msaidizi wake alinipa maelekezo niwaache vijana na boti yetu nchini Tanzania kwa muda na nikutane nae jijini Kual Lampur nchini Malaysia ndani ya tarehe alionitajia wakati akiwa ziarani”
“Tokea tuzungumze kuhusu hili dili imeshapita mwezi miwili , inamaana huu mpango ulikuwa wa muda mrefu?”
“Inawezekana Miss Dina , kabla ya siku moja ya tarehe kufika , niliweza kufika Malaysia na nilikutana na mheshimiwa kwa siri sana kupitia msaidizi wake na nilitambulishwa kama mwekezaji”Aliongea Keitani kwa kutetemeka.
“Alitaka kuongea nini kwa siri namna hio?”Aliuliza Dina , ijapokuwa Keitani alijua alikuwa akitoa siri kubwa lakini hakuwa na jinsi.
“Aliniambia siku ya leo saa nne kamili za usiku mgombea wa kiti cha uraisi kupitia chama chake atafariki kwa ajali ya gari na atakaesababisha ajali hio napaswa kumtorosha nje ya nchi na kama ikishindikana nimuue kabla ya kukamatwa na polisi, kisha nitumie ushahidi feki wa tukio hilo kuhakikisha nakamilisha dili la kupitisha siraha”
“Ushahidi feki ni kutusingizia sisi ndio wahusika, si ndio?”
‘Ndio”
“Ameenda mbali mpaka kutengeneza ushahidi feki , yeye anafaidika nini katika hilo?”Aliuliza Lawrence.
“Kila kitu kipo wazi , naamini Jongwe sio chaguo lake na pili alitaka kujitengenezea njia za kupata maslahi hata akiwa amestaafu kupitia hili dili”Aliongea Hamza.
“Ndio , alitaka asilimia ishirini ya faida itakayopatikana na wakati huo huo Mgombea wa uraisi akiwa ni chaguo lake baada ya chaguo la Mgweno kufariki”Aliongea keita na kumfanya Dina sura kujikunja
“Mgweno na Eliasi wanataka kupinduana , madaraka huwa ni matamu sana”Aliongea Dina lakini upande wa Hamza hakujali nani anampindua nani.
“Vipi kuhusu muuaji ni nani?”
“Kuhusu mfungwa hatuna taarifa nyingi kuhusu yeye , tulipatiwa picha pekee na tuliambiwa ni mfungwa wa kidiplomasia aliefungwa kwa muda mrefu kwa siri”
“Yuko wapi kwasasa?”Aliuliza Hamza.
“Ametoweka mara baada ya tukio, tunaamini alikuwa na mpango wake binafsi wa kujitorosha baada ya kukamilisha misheni”Aliongea na kumfanya Hamza kuvuta pumzi.
“Picha yake ipo wapi”Aliuliza Hamza na Keita alimpa ishara bwana moja wa kizungu na alimsogezea Hamza simu na ilionekana picha ya mfungwa kwenye kioo cha simu na mara baada ya kuiangalia alijikuta macho yake yakichanua.
“What the f*ck!!”
Hamza alijikuta akitoa tusi na kumfanya Dina kusogea kuangalia picha hio ili kujua kwanini kashangaa.
ITAENDELEA.
 
SHETANI RUDISHA AKILI ZETU

MTUNZI: SINGANOJR

SEASON 03
SEHEMU YA 61.
Frida alijua kabisa anakwenda kufa na kifo chake kuja kuwa utata , aliweza kuona kilichokuwa kimemkaba kooni ni kivuli lakini hakuweza kufanya chochote.
Kwa mtu wa kawaida unaweza useme Frida alikuwa amepatwa na ukichaa au ugonjwa wa ajabu lakini ukweli ni kwamba kuna nguvu iliokuwa ikimkaba kupitia kivuli.
Wakati akiwa amekata tamaa ghafla tu ule utulivu wa kile chumba ulitoweka , ilikuwa ni kama upepo umeongezeka kwa kiasi kikubwa na kufumba na kufumbua kivuli kile kilipotea na kumfanya Frida kuanza kukohoa kwa nguvu , mpaka anakuja kutulia alijikuta akishituka mara baada ya kugundua kuna mtu mwingine ndani ya chumba chake alievalia joho la rangi nyeusi, alitaka kupiga yowe lakini mtu yule alimpa ishara ya kutulia.
“Wewe ni nani?”Aliuliza Frida kwa sauti ya chini huku akiwa ameshika shingo yake , ilikuwa bado hakuamini kama alikuwa amepona.
“Msimamizi wako na mlinzi wako mpya”Aliongea kwa lugha ya kingereza na kumfanya Frida kuchangayikiwa.
“Sikuwa na msimamizi na mlinzi , kwanini unajitambulisha kama mlinzi wangu mpya , nataka kujua unatokea upande upi , Wiccan au Sinagogu?”Aliongea Frida kwa sauti kubwa kidogo.
“Mimi ni mu’ alkemi kutoka makao makuu ya Wiccan , nipo hapa kwa maagizo ya Madame, mlinzi wako wa zamani amepoteza maisha”Aliongea na kumfanya Frida kuzidi kuchanganyikiwa lakini mara baada ya kusikia mtu huyo yupo hapo kwa maagizo ya Madame alipata ahueni.
“Mlinzi wangu wa zamani , unamaanisha mlinzi gani?”
“Alietaka kukuua amemuua mlinzi wako , kwanzia sasa utakuwa chini ya ulinzi wa binadamu”Aliongea huku akisogea karibu na mlango.
“Nilikuwa na mlinzi kivuli!!?”
“Wewe ni wa muhimu sana kwa Madame kuwasiliana na waumini wa ulimwengu wa nje ya kivuli , kwa namna yoyote unapaswa kuwa salama”Aliongea.
“Kwanini alitaka kuniua?”Aliuliza Frida, alikuwa akijua mtu ambae alitaka kumuua ni kivuli au watu ambao wamepata umaarufu kwa jina la Night Shadows(Vivuli vya watu vinavyoonekana usiku).
“Sina majibu kuhusu swali lako lakini nina ujumbe kutoka makao makuu”Aliongea kama roboti.
“Ujumbe gani?”
“Hakikisha anatumia mshumaa kurekodi ndoto zake ndio utakuwa salama, kadri atakavyoota bila ndoto zake kurekodiwa mtiririko wa matukio utakosekana na mpango wote kuingia dosari”Aliongea.
“Unamaanisha Ha…”
“Sikutajiwa jina , huu ndio ujumbe kutoka makao makuu unaopaswa kufanyia kazi”Aliongea yule bwana. Frida alitaka kuuliza swali zaidi lakini alijua asingepata majibu.
Yule bwana alievalia joho la rangi nyeusi mara baada ya kuridhika kwa kuona Frida alikuwa ameelewa aliaga.
“Wakati wowote ukiwa katika hatari na kuhitaji msaada wangu tamka neno , Grishav nitaitikia wito wako”Aliongea na palepale bila ya Frida kujibu aliinama chini na kufumba na kufumbua alipotea.
Frida alijikuta akiingia katika maswali mengi na swali kubwa lilikuwa juu ya ule mshumaa , alijua maelekezo yale yalikuwa yakimlenga Hamza lakini alishangaa mara baada ya kuambiwa Hamza anapaswa kutumia mshumaa ule ili kurekodi ndoto zake.
Swali ambalo alijiuliza inakuwaje mshumaa ambao alipatiwa na Dokta Genesha kuwa na uwezo wa kurekodi ndoto , kitu ambacho Wiccan walitaka iwe hivyo , inamaana kuna mpango uliokuwa ukiendelea kati ya Dokta Genesha na Wiccan kiasi cha kumkabidhi Mshumaa wa Nuru kwa ajili ya kumpatia Hamza.
Frida alijiuliza ni kitu gani ambacho kinaendelea yeye hakijui na kwanini amenusurika katika kifo.
Alikumbuka kwamba asipofanikisha Hamza kutotumia mshumaa basi atakuwa hatarini lakini swali lingine liliibuka inamaana Hamza alikuwa akiota bila ya kutumia ule mshumaa.
Kitu ambacho Frida alikuwa akijua ni kwamba mshumaa ule ulikuwa ni kwa ajili ya kumletea Hamza ndoto tu ili kujua maisha yake ambayo ameyasahau , hayo ndio yalikuwa maelekezo kutoka kwa Dokta Genesha na hakuelezwa kwamba mshumaa ule ni kifaa cha kurekodi ndoto, alijiuliza kama ni hivyo kinarekodi vipi hizo ndoto , ni sayansi ya namna gani ambayo imetumika.
Alijikuta hata usingizi ukimpelea kabisa licha ya kwamba alijihisi uchomvu mkubwa , hofu ilimvaa na hisia zake zilimwambia pengine anachofanya sio kuhatarisha usalama wake tu bali anahatarisha na usalama wa Hamza.
“Sina jinsi kwasasa lazima nihakikishe Hamza anatumia mshumaa ili kuwa salama , wakati nikitafuta majibu ya maswali yangu yote. Lakini nitafanya nini kumfanya atumie mshumaa kama yeye mwenyewe haniamini vya kutosha mpaka kuutumia?”Aliwaza Frida.
******
Hamza mara baada ya Side na wenzake kuondoka alibakia na mrembo Dina , wote wawili hawakuwa na ile mudi ya kwenda floor za juu kwa ajili ya kulewa vileo na kufanya starehe zingine kama kucheza kamari.
Kitu pekee ambacho Dina alipenda ndani ya Club hio ni kutumia siraha kulenga shabaha na hata Hamza alikuwa akipenda kitu kama hiko , kwake hakuwa mpenzi sana wa vileo na kucheza disco.
Walitumia zaidi ya lisaa limoja na nusu kulenga shabaha kwa kutumia bunduki za aina mbalimbali.
Ilipotimia saa tano kasoro njaa zilikuwa zikiwauma na Hamza alipendekeza warudi Kijichi ndio wakapate chakula huko na Dina hakupiinga.
Mara baada ya kufika kijichi chakula kiliandaliwa na wote wakaanza kula pamoja.
“Unaonaje baada ya hapa ukaangalie maendeleo ya vijana wangu , tokea siku ile ulivyowafundisha kiasi namna ya kucheza Karate na Kung Fu hukuwaona tena”Aliongea Dina.
Hamza kipindi kabla ya kukutana na Regina alikuwa ameshawahi kuwafundisha vijana wa Dina mafunzo ya Karate na Kung Fu mara moja na hakuwahi kwenda tena kuwaona.
“Hakuna shida , kuna kitu pia nataka kwenda kukifanyia mazoezi”Aliongea Hamza.
“Kitu gani , ni kuvuna nishati za mbingu na ardhi au kitu kingine?”Aliuliza Dina kwa shauku alikuwa akijua Hamza ana mafunzo ya kuvuna nishati za nguvu ya asili ya ardhi na mbingu na alitamani kujifunza pia siku moja.
“Hutoelewa hata nikikuambia ni kama maneno ya kutamka nataka kuyafanyia majaribio”Aliongea Hamza.
Ukweli ni kwamba kitu ambacho alikuwa akienda kufanyia majaribio ni yale maneno ambayo Yonesi alimtajia wakati akiwa hospitalini , siku ile wakati akifanya tahajudi kwa kupitia yale maneno aliona sura ya mwanamke ambae anamuona katika ndoto , bado shauku yake juu ya tukio lile haikuwa imeisha na alitaka kwenda kujaribu tena.

Baada ya kumaliza kula Hamza alitoka akiongozana na Dina pamoja na Lawrence na kwenda katika ukumbi maalumu ambao ni kama eneo la mafunzo ya kimapigano.
Hakukuwa na matumizi ya siraha , ilikuwa ni sehemu ambayo watu wa Dina walikuwa wakijifunza namna ya kupigana kwa kutumia mbinu mbalimbali za sanaa ya mapigano , eneo hilo lilikuwa likitambulika hata kwa serikali na lilikuwa na kibali kabisa.
Ni eneo ambalo lilijengwa katika mgawanyo wa sehemu mbili , sehemu ya kwanza ilikuwa ni kwa kufanyia mazoezi ya kawaida kama Gym na mazoezi ya boksa, Karate na Judo upande mwingine ulikuwa ni wa tahajudi.
Katika sanaa ya mapigano tahajudi ilikuwa ni sehemu ya mazoezi kwa ajili ya kuujua mwili wako ulivo, ukifanya tahajudi kama binadamu utajuwa wapi kuna udhaifu wako na wapi nguvu zako zinakaa kwa wingi na namna gani ya kushinda udhaifu wako.
Hamza mara baada ya kuona vijana wa Dina wakichukua mazoezi aliridhika , aliweza kuona wengi walikuwa wamepiga hatua kwa kufuata maelekezo yake.
“Bro , unapanga kufanya mazoezi ya namna gani , unataka kufanya tahajudi?”Aliuliza Lauwrence mara baada ya kumuona Hamza akichagua upande wa wanaofanya Tahajudi.
Dina na Lawrence siku zote walikuwa na shauku ya kutaka kumuona Hamza akichukua mazoezi hivyo walimwangalia.
“Kaa kimya Lau acha maswali mengi”Aliongea Dina akimzuia Lau kutokumsumbua Hamza na maswali yake.
Kutokana na wale wanafunzi kumuona Hamza na wao wote waliacha na kumpatia Hamza nafasi , kwao ni kama kuna kitu ambacho walitaka kujifunza kwa kumuangalia ndio maana walisimama pembeni.

Wakati Hamza akiwa katika mkao wa kufanya tahajudi huku midomo yake ikicheza ghafla tu watu wote walijikuta wakikumbwa na msisimko wa ajabu , ilikuwa ni kama kuna kiumbe cha ajabu kimefika ndani ya eneo hilo na kuwafanya kuanza kushindwa hata kupumua vizuri huku eneo ambalo Hamza alikuwa amekaa anga lake ni kama lilikuwa likitingishika.
Dina alijikuta jasho la paji la uso likimtoka huku akimwangalia Hamza kwa wasiwasi , alipatwa na hisia kama vile Hamza amekuwa mfalme ghafla na yeye ni kijakazi wake.
Upande wa Hamza hakuwa hata akielewa kilichokuwa kikiendelea kwa nje , kama alivyotarajia maneno yale yalikuwa ni kama anamwita yule mwanamke , mara ya kwanza wakati alivyofanya kule wodini alimuona kwa mbali yule mwanamke , lakini wakati huo kadri alivyokuwa akiimarisha umakini wake wa ubongo na kuzidi kuyatamka yale maneno alimuona ni kama vile yule mwanamke mchawi anaemuona kwenye ndoto alikuwa akimsogelea kutoka angani kwa spidi ya ajabu.
Zilipita kama dakika nne tu yule mwanamke aliweza kumuona kwa ukaribu zaidi, lakini jambo ambalo lilimshangaza Hamza ni kitu ambacho alikuwa ameshikilia mkononi.
Kadri alivyokuwa akizidi kuongea yale maneno mwanamke yule alizidi kusogea , lakini ilifikia hatua ni kama hawezi kumfanya asogee zaidi na yule mwanamke ni kama alijua Hamza hawezi kumuita karibu zaidi na alichokifanya ilikuwa ni kunyoosha kile kitu alichoshikilia mkononi mwake na Hamza mara baada ya kuangalia vizuri alijikuta akipagwa , ulikuwa ni ule mshumaa ambao Frida alimpatia akimwambia umetoka kwa Dokta Genesha, Mshumaa wa Nuru.
Hamza alichanganyikiwa mshumaa wa nuru kwanini upo katika mikono ya huyo mwanamke , katika ndoto yule mwanake alimuona kama mchawi ambae anachomwa moto baada ya kukamatika lakini kwanini akashika kitu cha nuru ilihali nuru na uchawi ni vitu viwili tofauti.
Yule mwanamke ni kama alikuwa akitaka Hamza amsogeze karibu aweze kushika ule mshumaa , upande wa Hamza alionekana kusita kuupokea ule mshumaa na yule mwanamke ni kama aliliona hilo na alitamka neno kwa kunyanyua mdomo wake kwa juu bila kutoa sauti akihakikisha Hamza anasoma lipsi zake.
NISAIDIE!(Help me)
Ndio neno ambalo aliongea huku akimpa ishara Hamza kupokea ule mshumaa.
Muda uleule Hamza aliacha kutamka yale maneno na kitendo kile kilifanya yule mwanamke ni kama vile kuna nguvu iliokuwa ikimvuta na kuzidi kurudishwa nyuma mbali na yeye , lakini bado hakuacha kumnyooshea ule mshumaa kama ishara ya kumuomba amsaidie.
Muda ileule wakati kila mtu akiwa ameloa jasho kana kwamba eneo lote limekumbwa na joto kali Hamza aliweza kufungua macho yake huku akionyesha hali ya kuwashangaa waliokuwa wakimwangalia .
“Nini kimetokea, Dina mbona upo hivyo?”Aliuliza Hamza mara baada ya kumuona
“Bado tu unapata muda wa kuuliza , ni kitu gani ulichokuwa ukifanya?”Aliuliza Dina na kumfanya Hamza sasa kuelewa kilichokuwa kikiendelea , licha ya yeye mwenyewe kuwa na wasiwasi lakini aliishia kucheka.
“I am sorry !, hii ni mara yangu ya kwanza kujaribisha hiki kitu , sikuweza kujizuia kile kinachonizunguka”AliongeaHamza na kisha alipiga hatua kuondoka katika eneo hilo.
Na wakati wakianza kutembea ndio sasa waligundua paa la jengo hili lilitingishika sana na kutokana na mchwa kula mbao unga unga ulidondoka chini kwenye tailizi na kila walipokuwa wakipiga hatua walikuwa wakiacha nyuma alama za miguu.
“Muda umeenda sana , nataka nirudi nyumbani”Aliongea Hamza.
“Hamza ni mafunzo gani yale , ni nguvu ya ndani au nishati ya mbingu na maji?”
“Ilianza mbingu ikaja ardhi halafu mbingu ikaleta maji na uhai , hizi ni kanuni za mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi na ni kitu ninachoweza kufanya pia , lakini kuhusu nilichofanya sasa hivi hata sijui ni kitu gani , kama nilivyosema nipo kwenye utafiti”Aliongea Hamza
“Hata jina lake hujui?”Aliuliza Dina kwa mshangao.
“Ndio ila kwasasa nitaiita hii kama Wito, kwasababu ukiifanya ni kama kuna kitu unakiiita”
“Huwa haifurahishi kusikiliza pekee”Aliongea Dina kwa macho yaliojaa huzuni na shauku.
“Usiongee hivyo , hiki ni kitu ambacho siwezi kukuruhusu ufanye kabla sijakipatia majibu , nguvu yake ni kubwa kiasi kwamba ni kama sijakula kabisa”Aliongea Hamza huku akijihisi ni mwenye njaa kali.
Dina alimwambia twende ukale na Hamza hakuwa na aibu ya kukataa kwani alikuwa na njaa , muda huo hawakurudi kwenye mgahawa bali Hamza alienda mpaka yalipo makazi ya Dina mita kadhaa kutoka mgahawa wake ulipo na mfanyakazi aliagizwa kuandaa chakula na Hamza alikaa chini na kuanza kukifakamia huku Dina akimwangalia kwa macho yaliojaa mahaba.
“Unajua nilishangaa baada ya mstaafu Mgweno kunipigia simu akisema yaishe”Aliongea Dina.
“Kwanini yeye ndio kakupigia simu?”,
“Unaweza kushangaa , licha ya kwamba kwa nje inaonekana familia ya Benjamini ndio inataka Regina kuolewa na James lakini upange mwingine ni mipango ya Mheshimiwa Mgweno”Aliongea Dina.
“Unataka kumaanisha nini?”
“Labda utakuwa hujui tu , ila kampuni ya Dosam ni kubwa Tanzania na inachangia zaidi ya asilimia tatu ya pato lote la Taifa , imeshikilia uchumi wa nchi katika maeneo nyeti, Benki namba moja ya kibiashara inayoongoza kwa Tanzania na Afrika mashariki yote ni Dosam Commercial Bank huu ni kama utawala wa mzunguko wa fedha nchini , hapa bado hujazungumzia usafiri wa anga , mahoteli na usambazaji wa bidhaa mbalimbali kwa matumizi ya majumbani, Kabla ya mheshimiwa Mgweno hajaingia madarakani Kampuni ya Zena ilikuwa ya kawaida tu kulinganisha na Dosam lakini baada ya Mgweno kuingia madarakani ilikua kwa spidi ya hali ya juu na yote hii ilikuwa ni uwekezaji mkubwa ambao mheshimiwa alifanya kwa kuiba hela za wananchi”Aliongea Dina.
“Kwahio unachomaanisha ni kwamba kampuni ya Zena inamilikiwa na Mheshimiwa mstaafu Mgweno?”
“Ndio kwa asilimia zaidi ya arobaini na tisa, ukifuatilia wana hisa wa kampuni ya Zena utagundua wengi wanaomiliki hisa hizo ni kampuni kutoka nje ya nchi , ukifuatilia kampuni hizo nje ya nchi utagundua kwamba ni kampiuni ambazo zimepewa haki kisheria ya kumiliki hisa hizo na kampuni nyingine , mzunguko unaendelea hivyo hivyo, zote ni njama za Mgweno kuficha wananchi kwamba anaimiliki Zena , sio kampuni moja tu , kila kampuni kubwa ana ushawishi wa kimaamuzi”
“Zote hizo ni hela za rushwa!?”
“Ndio lakini hakuna ushahidi wa kuthibitisha kama ndio mmiliki, sehemu pekee ambapo amekosa umiliki na ushawishi ni kampiuni ya Dosam peke yake na hii ni kutokana na msimamo wa aliekuwa kuongozi wa kampuni yaani babu yake Regina”Aliongea Dina na sasa ni kama Hamza alikuwa akipata picha.
“Kwahio anajaribu kuitumia familia ya Benjamini kwa ajili ya kuingiza ushawishi wake katika kampuni ya Dosam?”
“Ipo hivyo , mwanzoni walijua mambo yataenda sawa kama Regina atakubali kuolewa na James lakini mambo yamekuwa magumu , Regina karithi tabia zote za waanzilishi wa ile kampuni”
“Unamaanisha bibi yake na babu yake, unachoongea kinaonekana kuwa sahihi”Aliongea Hamza.
“Mgweno anachotaka ni kuimiliki Tanzania katika kila nyanja , kwanzia mtandao wa biashara haramu , biashara halali na kisiasa , hii itaifanya familia yake kuwa ya kifalme na raisi ni kama waziri mkuu tu anaepokea maagizo kutoka kwao”
“Kama ndio anachowaza anajidanganya , kuna mifano mingi ya kihistoria ni ngumu sana kuuchimba msingi wa nchi na kutengeneza nyufa pasipo kushitua wamiliki wake”
“Pengine anaelewa ila anaona ni kheri kujaribu kuliko kufa bila ya kujaribu”
“Kwahio baada ya kuona familia ya mzee Benjamini imekwama njia pekee alioona ni kumuua Regina maana urithi utaenda kwa mtoto wa pili?”
“Ndio lakini mipango yake inaonekana kukwama kutokana na uwepo wako , niseme tu umetibua mambo mengi sana , najua hata kunipigia simu ni kutokana na kujua ukaribu wetu na anatangeneza mazingira ya kujihami, lakini kwa wanaojua Mgweno kuna kitu lazima anapanga, walijaribu hadi mbinu ya kutaka kumtengeneza mtu wao ambae yupo karibu zaidi na Regina”Aliongea Dina na kumshangaza kidogo Hamza.
“Unamaanisha wale wazee ambao Regina amewafurumusha?”Aliuliza.
“Huo haukuwa mpango , wale wazee walikuwa wakifahamika tokea kipindi kirefu wapo kinyume na uongozi wa Regina”
“Ni nani ambae walikuwa wakimlenga?”
“Mchepuko wako alieniingiza kwenye matatizo”Aliongea huku akivuta midomo”
“Eliza!?”
Dina alitingisha mabega lakini kabla ya Hamza hajauliza swali lingine mlango wa kuingilai uligongwa kwa nguvu na Lawrence alionekana akiingia kwa pupa.
“Kuna nini Lawrence?”Aliuliza.
“Nimeletewa taarifa muda huu na vijana , Mheshimiwa Jongwe amefariki dunia kwa ajali ya gari na jeshi la polisi limeishikilia familia ya Mzee Seif kama washukiwa namba moja”Aliongea Lawrence na habari ile ilimtoa macho Dina.
“Unamaanisha mgombea wa kiti cha uraisi kupitia chama tawala , Jongwe amefariki, tena kwa ajali , kwanini familia ya mzee Seif ihusishwe kama ni ajali?”Aliongea Dina.
“Inawezekana sio ajali ya kawaida”Aliongea Hamza.
“Kwa maelezo niliopatiwa gari ambayo alikuwa amepanda imelipuka na ndani yake alikuwa ameambatana na Mzee Martin”Aliongea Lawrence na alivyoongea ni kama alijua taarifa ile itamshitua bosi wake na ilikuwa kweli kwani Dina alijikuta akisimama akiwa kama haamini.
“Mzee Seif na Mzee Martini mbona kama ushawahi kunitajia hawa watu?”Aliuliza Hamza.
“Ndio Bro hawa ndio washirika wetu wakubwa, japo mara nyingi inaaminika Mzee Seif ana uadui wa kisiasa na Mzee Martini”Aliongea Lawrence.
“Kwanini inaaminika hivyo ?”
“Kwasababu wote ni wanasiasa wa vyama tofauti , Mzee Seif ni kutokea chama cha upinzani na Martini ni kutoka chama tawala na wamekuwa wakipishana kama wabunge katika jimbo moja kwa zamu , uchaguzi huu akishika mzee Martini mwaka mwingine anashika Mzee Seif , awamu hii inayoisha Mzee Seif anamaliza muda wake lakini uelekeo wa kura upo upande wa Mzee Martini , siasa zao mara nyingi ni za kurushiana maneno”Aliongea Lawrence.
“Kwahio jeshi limemkamata Mzee Seif kwa kuamini kwamba ametegesha bomu katika gari la Mzee Martini ili ashinde uchaguzi , kama ni hivyo mgombea wa uraisi wa chama tawala kwanini amekufa pamoja na Martini?”Aliuliza Hamza lakini ni kama alikuwa akiipata picha.
“Lazima kuna kitu Mgweno anajaribu kufanya , hizi zote ni hila za kutaka kubomoa mtandao wa Chatu”Aliongea Dina kwa hasira.
“Lakini Madam Mheshimiwa Jongwe ni mgombea ambae amepata sapoti kubwa kutoka kwa mheshimiwa Mgweno , kwanini afanye hila ya kumuua mgombea ilihali zimebakia wiki chache kabla ya wananchi kupiga kura”
“Kesho kutwa pia ndio ilitarajiwa mkutano wa mwisho wa chama tawala kufanyika ili kufunga kampeni”Aliendelea kuongea Lawrence.
“Kuna picha inanijia akilini”Aliongea Hamza lakini upande wa Dina alionekana kuwa katika majonzi ya kumpoteza Mzee Martini, alikuwa ni moja ya mhimili wa mtandao wake.
“Lawrence polisi wanamshikilia kituo gani Mzee Seif?”
“Nasikia hawajamkamata bali wameizingira nyumba yake huko Kigamboni Mbutu B”Aliongea Lawrence.
“Yaani baada ya dakika kadhaa mlipuko kutokea na kuua watu, tayari washafikia maamuzi Mzee Seif ndio muhusika , mbona haingii akilini , hii lazima ni njama ya kutaka sisi twende tukamsaidie”Aliongea Dina.
“Tena nina uhakika hata hao wanaoitwa polisi ni feki”Aliongea Hamza huku akiweka kijiko chini.
“Madam tunapaswa kufanya nini?”Aliuliza Lau.
“Kama ninachofikiria ni sahihi lazima hili linahusiana na kikao nilichofanya na mheshimiwa Mgweno siku kadhaa zilizopita , mtandao wetu wote unajua ni kwa namna gani Mzee Seif alikuwa mwaminifu , nisipoingilia na kulifanyia hili maamuzi unadhani nitaonekanaje , Lawrence kusanya vijana wote ambao hawako mbali tutaenda kuangalai kinachoendelea”Aliongea Dina.
“Lakini Madam ulitoa maelekezo ya vijana karibia wote wakae chimbo , waliopo karibu na mjini hawazidi hata hamsini?”
“Haina haja”Aliongea Hamza huku akisimama.
“Watu hamsini ni wengi sana na hili linaweza kuwa ni mtego , hebu ita wale kumi kutoka jumba la mazoezi waje hapa , wanatosha sana”
“Bro unataka na wewe…”
“Hamza na wewe unataka kwenda?”
“Nataka nikajionee kinachoendelea , kama kweli huu mpango kaupanga Mgweno basi atakuwa katumia akili , unadhani kwa katiba yao ya chama nini kinafuata mara baada ya mgombea mkuu wa chama kufariki ghafla?”Aliuliza Hamza.





SEHEMU YA 62.
“Sijui kuhusu katiba yao inachosema , ila nina uhakika mgombea Mwenza ndio atachukua nafasi, kwanini unauliza?”Aliuliza tena Dina maana alijua Hamza hakuwa mtu wa siasa.
“Nawaza kuna mchezo unaochezwa hapa na kuna nguvu mbili kubwa za kisiasa , nataka kujionea mwenyewe”Aliongea Hamza na Dina alitingisha kichwa , kwasababu Hamza alitaka kwenda hakuona haja ya kumzuia , isitoshe ilimpelekea kujiamini zaidi kudili na hali kama hio.
Upande wa Dina alijua lazima kuna mchezo unaofanywa na kama Mzee Seif atakubali kuhusika moja kwa moja itaaminika mtandao wake ndio umekamilisha swala hilo , jambo ambalo hakautaka litokee.
Nyumba ya Mzee Seif ilikuwa Kigamboni Mbutu B na gari mbili ziliendeshwa kuelekea huko ya mbele akiwemo Hamza na Dina na ya nyuma ilikuwa Noah iliowabeba Lawrence na kundi lake.
Kitendo cha kufika eneo la tukio waliweza kuona watu walioizingira nyumba ya Mzee Seif , jambo ambalo liliwashangazwa hakukuwa na uwepo wa polisi hata mmoja ni kama Hamza alivyotarajia.
“Mbona sio polisi kama taarifa ilivyosema?”Aliuliza Dina kama kwamba Hamza alikuwa na majibu.
Hamza alichunguza eneo lote hasa wale watu walioshikilia siraha na alijikuta akikunja sura mara baada ya kuona wazungu wawili ndani ya eneo lile wakiwa ni sehemu ya watu waliozunguka nyumba hio.
“Ni kama nilivyotarajia kuna kinachoendelea hapa”Aliongea Hamza.
“Lakini kama kweli walikuwa wakimshuku Mzee Seif kulipua gari ya mheshimiwa Jongwe kwanini hawajaja polisi?”Aliuliza.
“Tutapata majibu yote mara baada ya kuongea nao”Aliongea Hamza huku akitangulia kutoka nje ya gari.
Wale watu kama walinzi walioshikilia siraha wakiwa wamezingira nyuma hio waliongeza umakini kwa Dina na kundi lake.
“Kama tabia yako ya siku zote, Dina mrembo wa kujiamini , naona umekuja na watu wachache mno tofauti na nilivyotegemea”Sauti ya mwanaume ilisikika kwasababau ilikuwa kuna giza hawakumuona vizuri na mara baada ya kusogelea taa za mwanga wa gari ndio Dina aliweza kumuona.
“Pancho!, unafanya nini hapa?”Aliongea Dina na muda huo ni kama sasa alishaanza kupata picha ya kile kinachoendelea.
“Nimekuja kukusalimia kwa mara nyingine mara baada ya kukataa pendekezo ya dili nono”Aliongea na muda ule alitoa ishara na baada ya kupita dakika mmoja tu wanaume wanne walitoka katika nyumba hio na moja wapo ya wanaume wale alikuwa ni Mzee Seif alieshikiliwa na wanaume wawili weusi waliojazia mwili , mtu wa mwisho kutoka alikuwa ni Mzungu- Mjapani , yaani mtu aliechanganya rangi ya mjapani na Mzungu.
Kilichomfanya Dina kuanza kupandwa na hasira alijua mpango wote huu ulisukwa na Pancho.
Pancho alikuwa ni moja ya wasimamizi wa mtandao wao upande wa Congo na siku kadhaa nyuma Dina alipokea dili kupitia kwa Pancho kutoka kwa Wacanada ambao walitaka kuingiza siraha za kivita Congo kupitia Bandari ya Mtwara.
Dili hili liliungwa mkono na Mheshimiwa Mgweno lakini Dina aliona halikuwa na maslahi na kama angelikubali ni kama kujipiga risasi mguuni, ikizingatiwa siraha hizo zilipaswa kufikishwa kwa kundi lingine la waasi ndani ya Congo tofauti na lile ambalo wanashirikiana nalo kwa muda mrefu.
“Mzee Seif nini kimetokea , kwanini taarifa nilizopokea ni wewe kuhusika na kumuua Mzee Martini na mheshimiwa Jongwe?”Aliuliza Dina akimpotezea Pancho.
“Hawa ndio wahusika , wameiteka familia yangu na wanataka nikiri kuhusika kwa kushirikiana na wewe kumuua Jongwe au turejee mezani na kuanza mazungumzo ya kuingiza siraha Tanzania kwenda Congo”Aliongea Mzee Seif aliekuwa na hali ya hofu na kumfanya Pancho kutoa tabasamu.
“Pancho unajaribu kufanya nini , nani yupo nyuma yako?”
“Dina hakuna ambae yupo nyuma yangu?”Aliongea Pancho kwa kejeli.
“Kwa kumuua mgombea wa uraisi kupitia chama tawala, unasema hakuna ambae yupo nyuma yako?”Aliongea Dina kwa hasira na kumfanya Pancho kutoa tabasamu la kifedhuli.
“Nilitaka hili swala angalau ulichukulie kwa uzito wake, ushahidi wa wewe kuhusika katika shambulizi la kulipua bomu gari ya mgombea wa uraisi kupitia chama tawala upo , unaweza ukawa wa kutengeneza lakini jeshi la polisi lipo tayari kuuamini na kama likitoka uraiani , kitengo cha TISA kitakufanya mbuzi wa kafara, lakini huko kote ni kujisumbua kama upo tayari kuchagua chaguo zuri kati ya matatu alioongea Mzee Seif?”
Hamza muda huo alikuwa akiangalia mazingira yalivyo na watu wote waliokuwa hapo walikuwa na siraha za bunduki na haraka haraka kwa sheria ya Tanzania ilikua ngumu kwa watu hao kumiliki hizo siraha labda iwe kuna mtu ndani ya serikali ambae alikuwa akihusika.
Isitoshe safari yao kutoka kijichi mpaka kufka hapo , kama kweli jeshi la polisi lilikuwa sirasi kukamata watu hao waliomsababishia ajali mgombea wa kiti cha uraisi basi wangeshafika labda tu iwe kuna maagizo ambayo yamewafanya kuchelewa.
“Hizo siraha mnaotaka kuingiza Tanzania mnazitoa wapi?”Aliongea Hamza.
“Oh!, ahsante kwa kuuliza bwana mdogo , kidogo tu nimesahau kumtambulisha bosi wetu hapa , huyu ni Bosi Keita na ndio msingi wa haya maungumzo , kuhusu wapi siraha zinatoka ni juu yake”Aliongea Pancho kwa kujigamba.
“Pancho kama nilivyosema mtandao wetu haudili na maswala ya siraha bila ya utaratibu maalumu, kama unataka dili hili lipite lisimamie wewe mwenyewe na hela zako na sio za mtandao wa Chatu”Aliongea Dina na yule bwana mwenye asili ya kizungu na Kijapani alimpa ishara Pancho ya kuongea yeye.
“Miss Dina kama alivyoongea Pancho tunaweza kulimaliza hili swala kimya kimya na kusiwe na athari zozote kwa kila upande”Aliongea kwa Kingereza.
“Unamaanisha unaweza kuzima kesi ya kulipua gari ya mgombea wa Uraisi pamoja na Martini?”Aliuliza Lawrence.
“Itategemea na maamuzi ya Miss Dina?”
“Kwanini nahisi hata waliompendekeza Jongwe kupeperusha bendera ya Chama ni kama wanashangilia kifo chake?”Aliongea Hamza huku wakati huo Dina akiwa ametulia.
“Tunafanyaje?”Aliuliza Dina akimegemea Hamza , isitoshe ndie aliesema wasije na watu wengi.
“Wana siraha na hata kama tukishambuliana bila siraha hatuwezi kushinda bila kushitua raia , hawa watu wana mafunzo ya mapigano”Aliongea Hamza na kumfanya Dona kuwa na wasiwasi.
“Usiwaze hili naweza kulimaliza kwa amani na kisha utadili nao kujua nini kinaendelea kuhusu mgombea wa uraisi kulipuliwa”Aliongea Hamza na japo Dina alikuwa na wasiwasi aliamua kumwamini Hamza.
“Bwana Keita kwa ninavyojua huwezi kudili na siraha pasipo kuwakilisha shirika la giza unalotokea”Aliongea Hamza akitaka kujua Black Association ambayo Keita anatokea.
“Jungle Army Merchant ndio ninatokea”Aliongea bila ya kusita sita.
“Kumbe ni Jungle , hebu subiri kwanza nipige simu, nikimaliza utaamua cha kufanya”Aliongea.
“Umpigie nani?”
“Utajua nikimaliza’Aliongea Hamza.
“Mr Keita haina haja ya kupoteza muda na hawa watu , swala ni moja tu wachague chaguzi moja kati ya tatu tumalizane”Aliongea Pancho akionekana kukosa uvumilivu.
“Kimya! , sitaki unifundishe namna ya kufanya biashara”Aliongea Keira kwa kingereza na kumfanya Pancho kukaa kimya , isitoshe alikuwa akijua Jungle Army Merchant walikuwa wafanyabiashara wakubwa ndani ya Black Market kwa kuuza siraha za kila namna.
Muda huo Hamza alikuwa ashapiga simu tayari bila ya kuwa na wasiwasi kabisa.
*****
Magneto, Las Vegas- USA
Ni ndani ya jiji la Las Vegas , jiji ambalo kwa wacheza kamari hawakuhesabu muda , Usiku ni kama mchana na Mchana ni kama usiku tu ndani ya hili jiji.
Katika moja ya hoteli ya kifahri ya nyota tano ndani ya chumba cha hadhi ya raisi , alionekana mtu bonge mweusi mwenye kitambi akiwa amelala chali.
Alikuwa mrefu wa mita kama moja nukta tisa hivi , vidole vya mikono yake vilikuwa vimevishwa pete za madini ya almasi , Dhahabu na madini mengine ya thamani , shingoni alikuwa amevalia mikufu ya bei ghali.
Mtu yule bonge alijikuta akitandaza miguu yake vizuri huku akifumba fumba macho na kuyafumbua , katikati ya eneo la mapaja yake alionekana mwanamke mzungu mwenye nywele nyeupe(blonde) akiwa bize kumhudumia.
“Mr Mamen are you comfortable?”Aliuliza yule mwanamke kwa sauti tamu huku akiinua kichwa chake akimwangalia kwa macho malegevu , akimuuliza Big kama ni mwenye kuifurahia huduma.
Mwanaume yule bonge udenda ulikuwa ukitaka kumwagika kutoka kwenye midomo yake , alionekana alikuwa kwenye ulimwengu mwingine wa raha.
“Comfortable..!?, Deeper the better .”Aliongea akimaanisha azame chini zaidi ndio itakuwa vizuri.
“You’re so annoying , I’m realy tired ..”Aliongea yule mwanamke akimwambia anachukiza kwani amekwisha kuchoka.
Bonge yule mweusi kama msanii RickRoss alifungua droo ya meza pembeni na kitanda chake na kuchomoa maburungutu ya pesa za dola na kumtupia.
“Hakikisha najisikia vizuri mpaka kisogoni , nitakupa kiasi chochote cha pesa unachotaka”Aliongea Big na yule mwanamke uchomvu uliisha palepale na alijkuta akiongeza mashambulizi ya kuhakikisha Big anajisikia vizuri.
Dakika hio hio simu yake ilianza kuita , hata simu yake tu ilikuwa imetengenezwa kwa housing ya madini ghali sana na kuifanya ionekane kama kitu kisichokuwa cha kawaida kutokana na uthamani wake
“F*ck , kama ningejua ningeizima hii simu , nani ananipigia muda huu”Big alilaani huku akichukua ile simu na kuipokea maana namba ilikuwa mpya tena haikuwa ya taifa hilo
“Big naona kama kawaida yako sasa hivi unaringa , kwahio unaona sipaswi kukupigia hata kama ni swala linalohusu vita ya tatu ya dunia”Sauti ya kiume ilisikika katika simu ya Big.
Kitendo cha Mameni kusikia ile sauti mwili wake ulitetemeka na macho yake yalibadilika na kuwa mekundu na hata ule msisimko aliokuwa akisikia ulipotea.
Yule mwanamke aliekuwa bize kuhakikisha Big anafurahi alijikuta akipiga kelele mara baada ya kadudu kabig kupotea na kuwa kabamia.
“Boss!! , ni wewe kweli , naona hatimae umenipigia , nimekumisi sana”Aliongea Big huku sauti yake ikiwa imebadilika.
“Unafanya nini hapo , lazima utakuwa na m*laya kitandani , yaani ndio kwanza kunakucha wewe unahangaika na wanawake , kuna siku utafia kwenye kifua cha mwanamke”
“Hehe..Bosi wewe mwenyewe unanijua vizuri , isitoshe wewe ndio mtu pekee ulievunja rekodi yangu”Aliongea.
“F*ck you!”Alitukanwa.
“Bosi nasikia upo Tanzania , habari za siku nyingi , vipi naweza kuja huko?”
“Nina mambo mengi ya kufanya siku hizi tutaona kama unaweza kuja , nyie watu ni wasumbufu sana mkisikia nipo mahali mnataka kuja tu , sitaki usumbufu wenu nahitaji kutulia kwa sasa”
“Bosi kwa uwezo wako na ushawishi wako unaweza kuomba chumba mapumziko Ikulu na ukapatiwa na warembo kabisa , hayo sio mapumziko ila ni kujitia stress tu , mapumziko ni yale wafariji wanakuwa wanabadilika badilika kila siku kwenye kuusisimua mwili”
“Sterehe za kutumia hela hizo nishazichoka , hata nikikuambia ni namna gani nafurahia maisha ya sasa hivi hutonielewa Big”
“Kama ni hivyo bosi kwanini umenipigia simu , kuna dili jipya?”
“Hakuna dili lingine , nishastaafu hayo mambo”
“Sababu ni ipi sasa Bosi , au kuna sehemu nimekosea?”Aliuliza Big kwa upole.
“Kwenye biashara zako unamfahamu bwana anaefahamika kwa jina la Keita?”
“Ndio mwaka juzi niliingia dili na kundi moja linalofanya shughuli zao ndani ya Afrika kuiba madini Adimu na kuyauza kwenda kwenye moja ya kampuni ya maswala ya kiteknolojia nchini Ufaransa , linaongozwa na bwana Keita”Aliongea Big.
“Huyu bwana wako naona ana juhudi mno , muda huu nimeelekezewa mitutu ya bunduki ndio maana nimekupigia simu kuthibitisha , Big kwahio sasa hivi umeshaanza kuwa mkubwa kiasi cha kunisaliti kisa tu nnimetoka kwenye uringo?”
Big mara baada ya kusikia kauli hio kutoka kwa Hamza alijikuta mikono ikimtetemeka kiasi kwamba simu ilitaka kudondoka.
“Bosi , subiri kwanza , nitampigia simu sasa hivi , naomba kwanza nimfokee baada ya hapo unaweza kumuua”Aliongea Big na dakika ileile alikata simu na kuitafuta namba ya Keita.
“Mamen Babe! , unafanya nini sasa mbona imepotea!?”Yule kahaba wa kizungu aliongea lakini Mameni alimpotezea na mara baada ya kuipata namba ya Keita aliipiga palepale.
Mara baada ya Hamza kumaliza kuongea na simu hakuongea neno na alitulia akiangalia matokeo.
Ijapokuwa Keita hakujua Hamza alikuwa akiongea na nani kwenye simu lakini alihisi kuna kitu hakipo sawa.
Dakika ileile simu yake ilianza kuita na alisogea pembeni na kupogea lakini muda huo huo alianza kuonyesha ishara za kupaniki.
Upande wa pili ilikuwa ni sauti ya Big kutukana kimarekani kwa mara nyingi mfululizo kadri alivyoweza.
“Bosi nimefanya kosa gani?”
“Unataka kumuua nani sasa hivi?”
“Bosi umejuaje nataka kuua mtu?”
“Unaetaka kumuua ni bosi wangu”
“…”
Keita alijikuta akikosa neo , alishangaa mno kwa zaidi ya sekunde kumi , ni kama alikuwa akisharabu yale maneno.
“Ah!”
Alijikuta hofu ikimwingia na vigoti vya miguu yake vilianza kumlegea na alijikuta akigeuka na kumwangalia Hamza.
Upande wa Hamza alikuwa akimwangalia Keita tu kwa mbali na kwa jinsi alivyoonyesha kupaniki na woga alitamani kucheka.
“Mr Keita , Mr Keita , what happened?”Pancho aliuliza mara baada ya kuona mabadiliko.
Dina macho yake yalichanua alijua kabisa mabadiliko ya Keita ni kutokana na Hamza alipopiga simu na kwake aliona mwanaume Hamza alikuwa akimshangaza kila siku.
“Nini tatizo Mr Keita , mbona huongei?”Aliuliza Pancho kwa wasiwasi
“Hivi unajua mimi na vijana wangu tutakufa sasa hivi kutokana na ujinga wako na wale wanasiasa wapuuzi?”Aliongea kwa hasira.
“Unamaanisha nini Mr….”
Keita hakuchelewa alichomoa Desert Eagle kutoka kwenye kiuno chake na kumchapa risasi tatu Pancho palepale.
Mpaka Pancho anadondoka chini muonekano wake ulikuwa na shauku ya kutaka kujua kwanini Keita anamshambulia.
Keita mara baada ya kumalizana na Pancho alitoa maagizo kwa vijana wake kuwashambulia watu wa Pancho na walionekana kuwa shapu kweli kwani ndani ya sekunde wote walikuwa chini.
Baada ya Keita kuituliza hali alijikuta akimdondokea Hamza kwa magoti huku akiwa na wasiwasi mwingi akitia huruma.
“Prince Rich.. Bosi wangu ameniambia kila kitu , naomba unisamehe kwa ujinga wangu , sikubahatika kukutana na wewe ana kwa ana zaidi ya kusikia habari zako ndio maana nimekukosea…”
Kitendo kile kiliwashangaza mno Dina , Lawrence na wenzake , waliishia kujiuliza Hamza ni nani mpaka bwana yule kuwa na hofu namna ile kiasi cha kupiga magoti.
“Nipe bastora yako”Aliongea Hamza akiwa siriasi na kumfanya Keita kukakamaa mwili lakini alimpatiia.
‘Tafadhari naomba uwaache vijana wangu waondoke , walikuwa wakifuata maelekezo tu kutoka kwangu na wanazofamilia zinawategemea”Aliongea Keita lakini Hamza hakumjali na muda ule aliinua ile bastora na kujielekezea kwake kana kwamba anataka kujipiga risasi.
Tukio lile lilimshangaza kila mtu wakishindwa kuelewa Hamza anataka kufanya nini
“Hamza unataka kufanya nini , usipaniki..”Aliongea Dina lakini kabla hata hajamaliza Hamza alikuwa ashaachia risasi.
Bam!
Mlipuko ule wa bunduki ulimuogopesha mpaka Keita na wote walimwaangalia Hamza kwa mshangao na walishangaa zaidi baada ya kuona hakuna kilichotokea.
Risasi ambayo ilitoka katika ile bunduki ilikuwa katika vidole vya Hamza , haikueleweka amefanyaje lakini ilionekana aliikamata kabla ya kumfikia, tukio lile lilimfanya Keita kushindwa kuendelea kupiga magoti na kukaa chini kwa kunyoosha miguu huku mapigo yake ya moyo yakidunda kwa kasi.
“Kabla sijafanya chochote nataka muelezee kila kilichotokea… sababu ya kwamba umepiga magoti sio kwasabau ya bosi wako bali ni kwasababu yangu hivyo nataka majibu”Aliongea Hamza.
“Serafii.!!, nipo tayari kuongea”Aliongea Keita huku akipiga kichwa chini kiasi cha kutoka damu kwenye paji la uso.
“Anza kuelezea , kwanini kifo cha Mgombea wa uraisi na nani kahusika”Aliongea Hamza.
“Hatujahusika katika kumuua mtu , tupo hapa nchini kwa ajili ya mazungumzo ya biashara ya kupitisha Siraha Kwenda Congo kupitia bandari ya Mtwara , kitu pekee ambacho nafahamu kuhusu muhusika tulipewa kazi ya kumtorosha hapa nchini kupitia boti yetu”Aliongea na kauli ile ilimfanya Dina kusikiliza kwa umakini.
“Imekuwaje mkajiingiza , sitaki kuuliza maswali mengi elezea kila kitu ninachotaka kujua?”
“Mara ya mwisho nilivyokuja hapa nchini niliweza kukutana na mstaafu Mgweno kwa ajili ya kuingia dili la kupitisha siraha , lakini kutokana na usafirishaji wote wa Kimagendo kuwa chini ya Chatu hakutoa maamuzi badala yake aliwasiliana na Miss Dina ambae mara baada ya kuelekezwa kuhusu dili hili alikataa, Mstaafu baada ya ombi hili kukataliwa alituambia hana namna ya kutusaidia kwani njia pekee ya kupitisha siraha hizo ni moja tu ambayo ni Mtwara kutokana na bandari zote kuwa chini ya mwekezaji”
“Nini kiliendelea”
“Wakati tukifikiria namna ya kutafuta njia nyingine ya kukamilisha dili hili nilipokea simu kutoka kwa mtu ambae alijitambulisha ni msaidizi wa raisi”Aliongea.
“Unamaaniisha Mheshimiwa Eliasi Mbilu?”
“Ndio na alisema anataka kuonana na sisi kwa ajili ya mazungumzo ya namna ya kukamilisha kile tulichokuwa tukihitaji , kutokana na kuwa na haraka ya kufanikisha hili dili nilikubali na kupitia msaidizi wake alinipa maelekezo niwaache vijana na boti yetu nchini Tanzania kwa muda na nikutane nae jijini Kual Lampur nchini Malaysia ndani ya tarehe alionitajia wakati akiwa ziarani”
“Tokea tuzungumze kuhusu hili dili imeshapita mwezi miwili , inamaana huu mpango ulikuwa wa muda mrefu?”
“Inawezekana Miss Dina , kabla ya siku moja ya tarehe kufika , niliweza kufika Malaysia na nilikutana na mheshimiwa kwa siri sana kupitia msaidizi wake na nilitambulishwa kama mwekezaji”Aliongea Keitani kwa kutetemeka.
“Alitaka kuongea nini kwa siri namna hio?”Aliuliza Dina , ijapokuwa Keitani alijua alikuwa akitoa siri kubwa lakini hakuwa na jinsi.
“Aliniambia siku ya leo saa nne kamili za usiku mgombea wa kiti cha uraisi kupitia chama chake atafariki kwa ajali ya gari na atakaesababisha ajali hio napaswa kumtorosha nje ya nchi na kama ikishindikana nimuue kabla ya kukamatwa na polisi, kisha nitumie ushahidi feki wa tukio hilo kuhakikisha nakamilisha dili la kupitisha siraha”
“Ushahidi feki ni kutusingizia sisi ndio wahusika, si ndio?”
‘Ndio”
“Ameenda mbali mpaka kutengeneza ushahidi feki , yeye anafaidika nini katika hilo?”Aliuliza Lawrence.
“Kila kitu kipo wazi , naamini Jongwe sio chaguo lake na pili alitaka kujitengenezea njia za kupata maslahi hata akiwa amestaafu kupitia hili dili”Aliongea Hamza.
“Ndio , alitaka asilimia ishirini ya faida itakayopatikana na wakati huo huo Mgombea wa uraisi akiwa ni chaguo lake baada ya chaguo la Mgweno kufariki”Aliongea keita na kumfanya Dina sura kujikunja
“Mgweno na Eliasi wanataka kupinduana , madaraka huwa ni matamu sana”Aliongea Dina lakini upande wa Hamza hakujali nani anampindua nani.
“Vipi kuhusu muuaji ni nani?”
“Kuhusu mfungwa hatuna taarifa nyingi kuhusu yeye , tulipatiwa picha pekee na tuliambiwa ni mfungwa wa kidiplomasia aliefungwa kwa muda mrefu kwa siri”
“Yuko wapi kwasasa?”Aliuliza Hamza.
“Ametoweka mara baada ya tukio, tunaamini alikuwa na mpango wake binafsi wa kujitorosha baada ya kukamilisha misheni”Aliongea na kumfanya Hamza kuvuta pumzi.
“Picha yake ipo wapi”Aliuliza Hamza na Keita alimpa ishara bwana moja wa kizungu na alimsogezea Hamza simu na ilionekana picha ya mfungwa kwenye kioo cha simu na mara baada ya kuiangalia alijikuta macho yake yakichanua.
“What the f*ck!!”
Hamza alijikuta akitoa tusi na kumfanya Dina kusogea kuangalia picha hio ili kujua kwanini kashangaa.
ITAENDELEA.
Bingo
 
Back
Top Bottom