Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Simulizi imekaa unyama sana Big up BroHamza mara baada ya kuongea hivyo , palepale alisimama kwa ajili ya kuondoka , lakini muda huo Rehema ambae alikuwa amebeba kikombe cha kahawa kwa ajili ya Hamza aliingia na alishangaa kumuona Hamza anataka kuondoka.
“Mr Hamza unaondoka baada ya kufika tu?”Aliongea na Hamza alichukua kikombe kile na bila kujali kahawa ilikuwa ya moto ama ya baridi aliipiga yote kwa mkupuo kama maji na kisha akampatia kikombe chake.
“Sister Rehema , asante kwa jitihada zako , ila mimi ndio naondoka hivyo”
“Mr Hamza tafadhari usikasirike! Mzee Mboma ndio alivyo , ila tunahitaji sana msaada wako. Mimi naamini Afande Simba na Afande Himidu kukualika hapa ni kwasababu wanazo sababu zao za msingi”Aliongea Rajabu.
“Balozi huna haja ya kuwa na wasiwasi. Kwasababu nilishakubaliana na Himidu, nitatimiza baadhi ahadi zangu. Lakini kutokana na baadhi yenu tofauti ya kuongea kuhusu ushirikiano ila mnaanza kunihoji, sioni haja ya kuendelea kubakia hapa”Aliongea Hamza na Balozi Rajabu alikuwa na wasiwasi mno.
“Mzee Mbomba ni vizuri ukimwomba radhi Mr Hamza”
“Muache aondoke kama anataka , lazima amechaguliwa kwasababu za kindugu . Kama hana vigezo kwanini tumlazimishe. Kwa uzee wangu huu nishaona watu wengi wa aina yake. Kama wasiwasi ni juu ya ulinzi nitaweka mpango mzuri kwa kushirikiana na majasusi ndani ya Kitengo cha usalama . Pili Baraza la maksi licha ya kuwa la siri lakini pia limeundwa kwa ajili ya kuimarisha amani duniani baina ya makundi , sidhani kama itatokea mtu akataka kutuvamia bila sababu”
“Mzee.. kwanini ni mgumu sana kuelewa…” Balozi alishindwa kujua cha kufanya baada ya kuona Hamza ameshaondoka tayari na haraka sana alimpa maagizo sekretari wake kumsindikiza Hamza.
Katika kikao hicho Balozi alizidi kumshutumu Mboma , kwamba alifanya makusudi kumfanya Hamza kuondoka. Akienda mbali na kusema hata kama Hamza amechaguliwa kutokana na koneksheni na Mshauri mkuu hakupaswa kuongea kwa namna ya kumdhalilisha.
Ukweli ni kwamba watu wote wlaiokuwa katika kikao hicho walikuwa na mtazamo sawa na Mboma. Walikosa tu ujasiri wa kuelezea hisia zao , ila Hamza alionekana wa kawaida sana licha ya kuwa maarufu kupitia tukio la Kisiwani Chole.
Walipata kusikia tu habari za kisiwani na hakuna hata mmoja hapo ambae aliona Hamza akipambana moja kwa moja.
Mboma upande wake hakujali kile ambacho Balozi anaongea na aliishia kukunja midomo kumkejeli , akiamini kabisa alichofanya ni sahihi.
Upande wa nje Rehema alifanikiwa kumuona Hamza akitaka kuingia kwenye taksi na alimwita kwa kumkimbilia.
“Mr Hamza tafadhari usijali sana juu ya kilichotokea. Wote tunamjua mzee Mboma ni mtu anaeongea bila ya kufikiria , hususani likija swala la ukaribu wako na Himidu”Aliongea.
“Kuna tatizo gani mimi kuwa na ukaribu na Himidu?”Aliuliza Hamza
“Afande Mboma alikuwa moja ya watu waliokuwa wakiaminiwa sana na Afande Simba , lakini baada ya kutokea kwa Himidu nafasi yake ilichukuliwa na akaanza kujiona sio wa muhimu tena mbele ya wakubwa. Hakuwahi kupenda namna ambavyo Himidu alipanda cheo haraka haraka mpaka kufikia kuwa mshauri mkuu”Aliongea Rehema.
“Ndio maana , kumbe nimejiingiza katika ushindani wao?”Aliongea Hamza akitingisha kichwa lakini hata hivyo aliona hayo hayamuhusu. Kwanza mwanzoni hakutaka hata kushiriki na ni hila tu za Afande Simba.Ila hata hivyo hakutaka kuweka mambo moyoni kutokana na kile ambacho Mboma alisema kuhusu mpango wa jeshi kutaka kugawa baadhi ya taarifa zinazhohusianisha teknolojia ndani ya Earth Axis, aliona kuna haja ya kuwa siriasi kwani lolote lingetokea, ingekuwa hasara kwa serikali na wasingeridhishwa nae.
Hamza hakujali sana , alipanga kufuatilia swala hilo kwa namna anayoijua yeye, hivyo palepale aliagana na Rehema ambae alikuwa akiomba radhi kwa niaba ya Mboma mpaka anatia huruma.
Hamza hakupanga kurudi hotelini na badala yake alimpa uelekeo mwingine dereva nje kabisa ya jiji mpaka kumfanya dereva yule kushangaa kidogo.Wakati akiwa njiani, Hamza alipokea simu kutoka kwa Afande Himidu.
“Bosi nimesikia kilichotokea . Mboma ni mtu mgumu sana kuelewa licha ya cheo chake na ni mtu wa kukuza hata vitu vidogo visivyo na maana,naomba usimzingatie sana”
“Nawezaje kukasirika kwa kitu kidogo namna hio? Unawaza sana na wewe”Aliongea Hamza huku akicheka.
“Haha.. bosi nilikuwa na wasiwasi tu utaacha kunisaidia ndio maana. Bosi kama sio uwepo wako ndani ya Tanzania sidhani tungekuwa na amani mpaka sasa”Aliongea Himidu.
“Wewe ni muhuni sana , kwahio kumbe hili kongamano lenu lina mpango mwingine wa kugawa siri za Earth Axis lakini ukakaa kimya. Au ulitaka nije kuyajulia hukuhuku?”
“Haha.,. samahani sana bosi , tumeamua kuvujisha taarifa za Earth axis makusudi kurahisishia kazi , ila naamini kwa uwezo wako hakuna tatizo kabisa”
“Hakukuwa na utofauti hata ungeniambia mapema. Ila taarifa mlizowabebesha hawa wanajeshi ni kama kuwashikisha kiazi cha moto”
“Upo sahihi , ila taarifa ambazo tumetoa ni za juu juu sana kuhusiana na mazingira na mfumo mpya wa viwanda na mbinu nyingine za kuboresha zaidi maisha ya binadamu . Hata kama watuibie hawataweza kutengeneza siraha za hatari. Hivyo sidhani kutakuwa na shida kubwa”
“Lazima itakuwa mbinu uliofikiria , mnataka kutoa ushirikiano wa kugawa teknolojia ambayo haihusiani na mambo ya siraha ili kujiimarisha kidiplomasia na kuongeza ushawishi wenu katika siasa ili msiwe wanyonge katika kupambana na nchi kubwa kama Amerika. Himidu hata kama hii mbinu yako itafanya kazi pointi ya msingi ni kwamba , hata wakijua mnachotaka kugawa hakina uhusiano na utengenezaji wa siraha na mambo mengine , unadhani watakubali?. Lazima watafikiri mnajaribu kuwasaidia China na Urusi mahasimu wao wakubwa kiuchumi na kijeshi ili kujijenga, hivyo sidhani kama watakubali kupitwa kirahisi ?”
“Ndio maana tunakutegemea wewe bosi , mazungumzo haya yakikamilika, tutakuwa na washirika wengi kutoka mataifa makubwa na mikataba mingi itasainiwa. Na kwanzia hapo tutakuwa hatuna hofu tena kama taifa dogo, hata kama tukiwa katika ushirikiano mbaya na America lakini bado tutakuwa na sapoti ya kutosha kujilinda kutoka kwingine. Wasiwasi wangu ni kama ambavyo nimekwambia bosi , tunahofia kabla ya makubaliano, taarifa za Earth Axis zitakuwa zimekwisha kuvuja mahali tusipotaka zifike kupitia mashushu wao ndani ya jeshi letu na kama kila mtu akiwa na hizi taarifa za kiteknolojia zitakosa thamani na itakuwa ngumu kufanya makubaliano na haya mataifa na wakakubali”Aliongea na kumfanya Hamza kutaka kucheka.
“Tabu zote hizo ni kwa ajili ya kutaka kunufaika mwenyewe na Earth Axis! Unadhani utaweza kuificha mpaka mwisho , si mshirikiane tu ?”
“Bosi mpango sio kwa ajili ya kuhimili mpaka mwisho , tunachotaka ni kupata muda wa kutosha wa kujijenga , tukifikia hatua ya kuwa na teknolojia ambayo hakuna mwingine alienayo, hakuna taifa litaweza kutugusa kirahisi. Hii ni bahati yetu kuinuka kiuchumi kama taifa na Arika nzima. Licha ya kwamba itakuwa safari ndefu yenye vikwazo vya kila namna”
Hamza mara baada ya kusikia hivyo , alionekana kuwa katika hali ya kuwaza , ukweli alichokuwa akimaanisha Himidu ni kwamba wanahitaji muda wa kutosha kwa ajili ya Yulia kukwamua kila taarifa iliopo ndani ya Earth axis.
Aliona Yulia alikuwa na kazi ngumu sana, maana kwa mpiganaji kama yeye alichoweza zaidi ni kuufanya mwili wake kuwa imara zaidi na kufikia levo za juu lakini sio katika maswala ya teknolojia.
“Bosi ..”Aliita Himidu mara baada ya kuona Hamza ameacha kuongea na alishindwa kujua anachowaza ndio maana aliita kwa nguvu.
“Bosi lazima utakuwa umekasirika si ndio?”
“Hapana , kuna kitu nilichokuwa nikifikiria , ila niseme umenipa hamasa”Aliongea Hamza
“Hamasa gani bosi?”
“Kufunuliwa ni chanzo cha hamasa , usiulize sana, na usiwe na wasiwasi, japo sipendi kuwasaidia katika mipango yenu ila kwa ajili yako sina jinsi zadi ya kwenda kuonana na Roho Mchafu”
Himidu mara baada ya kusikia kauli hio alijikuta akishangaa na palepale alianza kucheka.
“Haha… , boss kweli unashangaza mno , umefikiria la maana sana. Kwasababu upo Paris sio mbaya kuonana mshikaji wetu , usisahau kunifikishia salamu zangu kwa Roho mchafu”
Hamza hakuendelea hata kujibishana na Himidu tena na palepale alikata simu ile.
Taksi ile iposimama Hamza ni kama alikuwa nje kabisa ya jiji la Paris kutokana na eneo hilo kuwa kama limetelekezwa hivi.
Majengo mengi yaliokuwa katika eneo hilo yalikuwa ni yale ya kale na yenye kuota uozo.
Hamza mara baada ya kusogelea upande wa kulia kuingia katika majengo , watu wengi walikuwa wakimnyooshea vidole na ilionekana walikuwa wakiongea kwa kumtukana.
Lakini hata hivyo Hamza hakuonekana kujali kabisa na aliendelea kutembea kukata mitaa na mara baada ya kuingia katika uchochoro wa nyumba mbili pande kwa pande ndio jinsi aeneo hilo lilivyozidi kuwa tulivu na watu kutoonekana.
Hamza alitembea katika uchochoro huo bila ya wasiwasi , akionyesha alikuwa akijua anakoelekea na dakika chache mbele aliweza kutokezea kwenye uzio uliokuwa na geti kubwa la chuma la rangi nyeusi.
Getini hapakuwa na mlinzi , hivyo Hamza alipita na ile anafika ndani aliweza kukuta eneo kama vile ni mapokezi ya hotelini ndani ya jengo hilo lililoenda hewani na kulikuwa na mtu eneo la Kaunta , mzee hivi mzungu, aliekuwa amelala fofofo na kupiga miayo , ilionekana alikuwa amelewa pombe chakali.
Pembeni ya kaunta kulikuwa na vyungu vya maua ambavyo mimea yake ilionekana kukauka kutokana na kukosa maji . Kulikuwa na vipisi vingi vya sigara katika vyungu hivyo.
Ni eneo ambalo lilikuwa na uchafu ambao sio wa kawaida na giza tupu na hio yote ni kutokana kati ya taa chafu za glasi ambazo zimening’inizwa, ni mbili tu ambazo zilikuwa zinawaka na mwanga wake ulikingwa na kutu.
Hamza baada ya kusogea kwenye lile eneo la kaunta alipeleka mkono na kuvuta kitabu kilichokuwa pembeni ya yule mlevi , lakini ile anavuta tu mwanaume yule mzungu alikikandamiza na mkono wake bila kuinua uso kuangalia nani anavuta kitabu huku akiendelea kupiga usingizi.
Hamza aliishia kutoa tabasamu na kujiambia huyu mzee lazima atakuwa anaota na palepale hakutaka kumchelewesha kwani alivuta kile kitabu kwa nguvu na kumsukuma na kumfanya adondoke chini kama furushi na palepale ndio alishituka na kujua kumbe kulikuwa mgeni.
Alisimama haraka haraka na kumwangalia Hamza na kisha alichukua karamu na lile daftari.
“Unaitwa nani?”Aliuliza kwa kifaransa.
“Hamza”
“Sijui linavyoandikwa , hebu andika mwenyewe”Aliongea na kumsogezea Hamza karamu na daftari.
Hamza alitamani kucheka kwa visingizio vya mzee huyo , lakini hata hivyo aliandika jina lake.
“Raisi wako yupo?”Aliuliza Hamza na mzungu yule mara baada ya kusikia Hamza akiuliza hivyo alimwangalia kwa macho ya uchunguzi.
“Unamtafuta raisi wangu kwa ajili ya kukumbushia yaliopita?”
“Ndio , sisi ni mrafiki”
“Lakini ametoka”Aliongea.
“Ameenda wapi?”Aliuliza Hamza akiona hakuwa na bahati.
“Mbugani”
Hamza mara baada ya kusikia hivyo , alionekana kukumbuka kitu palepale na kutabasamu.
“Kama ni hivyo nitamsubiri”Aliongea na palepale yule mzungu alinyoosha kidole kuelekea kwenye korido iliokuwa na giza.
“Chukua huo uelekeo kwenda mbele , utaona ofisi ya Raisi , unaweza kuingia na kupumzika”Aliongea yule mzungu bila kujali Hamza ni nani na Hamza mara baada ya kuondoka palepale aliendelea kulala.
Hamza alichukua korido hio mdogo mdogo akijali mambo yake na mara baada ya kutembea ndani zaidi hatimae aliweza kukuta eneo ambalo kulikuwa na bendera mbalimbali zilizosimamishwa pembeni , pamoja na medali zilizofungiwa kwenye kabineti za makabati ya vioo.
Kama mtu angeangalia medali hizo kwa umakini, asingekosa maneno haya: World number one Assassin Guild - Baffold (Shirika namba moja duniani la Wauaji - Baffold), World Ranking of Assassins (Cheo cha Dunia cha Wauaji), Golden Blade Awards (Tuzo ya Upanga wa Dhahabu), World Assassin Guild (Shirika la Dunia la Wauaji), Best Trade Union – Baffold Annihilations (Muungano Bora wa Biashara – Baffold Annihilations), Assassin Guild Lifetime Achievements Awards – Asmuntis (Tuzo za Mafanikio ya Maisha ya Shirika la Wauaji – Asmuntis), Honorary Chairman of the Assassin's Society – Asmuntis (Mwenyekiti wa Heshima wa Jumuiya ya Wauaji – Asmuntis).
Ilikuwa ni kawaida sana kwa kundi la kimauaji kupokea medali za aina hio , hasa kwa yale ambayo yanashikiria namba moja duniani.
Asilimia kubwa ya bendera ambazo zimening’inizwa zilikuwa ni kutoka kwa wateja ambao waliridhika na kazi na namna ya kushukuru kwa kazi nzuri mara nyingi hutuma bendera ya nchi misheni ilipofanyikia na kukamilika.
Kadri wingi wa bendera ulivyo ilimaanisha idadi ya waliokufa , ambao wengi wao ni viongozi wakubwa wa kisiasa na matajiri. Kulikuwa na bendera hadi ya Tanzania katika makabati hayo.
Hamza wakati huo akikagua hizo medali na bendera macho yake yalionyesha kuwa na hali ya majuto na kuridhika , akisifia ndani kwa ndani kwa kusema Roho mchafu umefanya kazi nzuri ya kuendeleza kuwa mchafu.
Ukiachana na medali hizo pamoja na bendera , kulikuwa na vyumba tofauti katika korido hio , vingi vikiwa ni vya mafunzo , Gym na hata swimming pools.
Kwa bahati ukiachana na maeneo mengi kuwa machafu eneo la mafunzo ya kulenga shabaha lilikuwa safi mno.
Hamza mara baada ya kusogea ndani ya eneo hilo kuchungulia aliweza kuona watu wengi wa kila rangi watoto na watu wazima wakiwa bize kujifunza namna mbalimbali za kimafunzo na kwa macho ya haraka tu walionekan mafunzo yao sio kwa ajili ya ulinzi bali kummaliza mtu.
Hamza alitembea kuvuka eneo hilo na kwenda ndani zaidi katika mlango wa mbao , usiokuwa na loki kabisa na kisha akausukuma na ile anaingiza mguu mmoja kuingia ndani , mwili ulimsisimka kwa kuhisi hatari , lakini hakujizuia na kukubali kile kinachokwenda kumtokea.
Na pale pale kisu kikali kiliwekwa shingoni kwake na aliekuwa amemuwekea kisu hicho alikuwa ni mwanamke alievalia nguo za kininja za kumbana huku akiwa hana utani hata kidogo.endelea nayo bure:- SEHEMU YA 186