Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Problem sio token na kujichokea kusoma.aweke no hapa pm ayapata token zake na atume link huko huko pm.process ya kule ni mambo privacy.Ila wabongo😅😅
Mmepewa link kbs ya kujimiminia venye mnataka lakn bado mnaweka MB za 2000 kuja kusoma kipande kimoja wakt ukilipia tokeni hyo 2000 unasoma mpk ujichokee 🙌🙌
Naunga mkono hojaProblem sio token na kujichokea kusoma.aweke no hapa pm ayapata token zake na atume link huko huko pm.process ya kule ni mambo privacy.
Na wengine hatuwezi kujiunga privacy zetu kwaajili ya hadithi tu.
Aseme hapa atapewa kilaini tu.
Well saidProblem sio token na kujichokea kusoma.aweke no hapa pm ayapata token zake na atume link huko huko pm.process ya kule ni mambo privacy.
Na wengine hatuwezi kujiunga privacy zetu kwaajili ya hadithi tu.
Aseme hapa atapewa kilaini tu.
Mkuu nani anajua Babu Kijana unatumia namba 06871513... au Hii ID yako ndio jina lako la NIDA? Kule huulizwi Id yako labda uamue kujitambulisha which is unnecessary.Wewe endelea kusubiri mwendelezo hapa utawekwa kwa udhamini wa wale wanaoniunga mkono.Problem sio token na kujichokea kusoma.aweke no hapa pm ayapata token zake na atume link huko huko pm.process ya kule ni mambo privacy.
Na wengine hatuwezi kujiunga privacy zetu kwaajili ya hadithi tu.
Aseme hapa atapewa kilaini tu.
Amani iwe nawe mkuu, shukrani sanaSEHEMU YA 181
Palepale wanaume waliojazia miili ambao pia walikuwa ni wafuasi wa sinagogu walitokeza mbele , wakiwa na visu mikononi mwao na haraka sana walianza kumshambulia Hamza..
Hamza aliishia kushika vile visu upande unaokata na kuvuta kwa nguvu lakini hakuonekana kuumia kabisa.
Kwa wakati mmoja alimpiga teke mwanaume yule na kisha alitumia kisu kile na kumkata mwingine shingo.
Ijapokuwa mbinu za mapigano za wafuasi hao zilikuwa sio za kawaida , lakini spidi yao ilikuwa ndogo mno kulinganisha na ya Hamza.
Hamza kila alipokwepa shambulizi aliweza kumuua mshambuliaji kwa urahisi kabisa na ndani ya sekunde chache tu watu kadhaa walikuwa wamedondoka chini wakiwa hawana uhai.
Mara baada ya kuona uwezo usiokuwa wa kawaida wa Hamza kupigana, Blue palepale alikamata bunduki aina ya AK-47 kutoka chini ya meza ya jiwe na kuanza kumlenga Hamza.
Hamza hakutaka risasi kumfikia , ingawa asingeweza kufa lakini zilikuwa zikiuma.
Alichokifanya alikimbia upande wa waumini wale na kufanya risasi zile ziue baadhi yao.
Kundi hilo la waumini walionekana hawakukiogopa kifo na walianza kumzingira Hamza wakitaka kumpiga.
Hamza aliishia kufyatua mateke akiwashambulia na kutengeneza njia ili kumfikia Blue, na alifanikiwa kutoka na kumpokonya paroko ile bunduki.
Hamza aliona ingekuwa kazi kuwaua kwa kutumia mikono yake na ili kuharakisha kazi aliona atumie bunduki hio.
“F*ck you zenu nyie wendawazimu msio na akili , kufaaaa!”aliongea Hamza na palepale alianza kuwafyatulia risasi na kufumba na kufumbua watu wengi ndani ya eneo hilo walidondoka chini.
Lakini baadhi ya waumini wakiungana na wale ambao walimteka Aira walionekana kuwa na bunduki zao pia na walianza kumshambulia Hamza.
Hamza alikuwa na wasiwasi risasi za bunduki zao zingemdhuru Aira hivyo alisogelea juu ya ile meza ya jiwe aliolazwa na kumsukumia upande mwingine chini na kisha alikimbia upande uliokuwa na wafuasi wengi na kuendeleza mashambulizi.
Waumini hao walikuwa ni kama vichaa , tofauti na kukimbia wote walikuwa wakimsogelea Hamza kama misukule na kumfanya Hamza kukosa jinsi na kuendelea kuwapasua vichwa na risasi.
Ndani ya dakika mbili eneo lote lilikuwa limejaa maiti na damu . Hamza aliishia kutoa pumzi ya masikitiko , ilipita muda mrefu kidogo mpaka kuuwa watu wengi kwa wakati mmoja kama siku hio , lakini hata hivyo alikuwa hana jinsi.
Watu hao hawakuwa katika akili zao , walikuwa wamegeuzwa kifikra na alijua kama wangetoka uraiani wangesababishia wenzao madhara.
Hamza mara baada ya kumalizana na wale wenye bunduki palepale alimsogelea Blue ambae uso wake bado ulionekana kuvimba . hakuwa na woga bali macho yake yalikuwa yamejaa chuki mno. Lakini Hamza hakumjali na palepale alimshika shingo kwa kumkwida.
“Jibu kila nitakachokuuliza la sivyo nitakugeuza maiti”Aliongea Hamza akiamini bwana huyo lazima atakuwa anajua baadhi ya siri za jamii hio ya wasinagogu.
Lakini mtu yule alionekana kabisa kutojali na palepale alitoa tabasamu la uvovu.
“Huwezi kupata chochote kutoka kwangu. Uishi milele mfalme wa masinagogu! Uishi milele Devasi…”
Hamza alishangazwa kwa sekunde na palepale ndio alipoweza kumuona Blue akitema damu huku mboni za macho yake zikizunguka na ndani ya sekunde kadhaa alipoteza pumzi.
Hamza aliishia kutupa chini mwili ule . Hakuamini bwana huyo atakunywa sumu kwa ajili ya kulinda umoja huo. Aliona watu wa Sinagogu kweli walikuwa ni hatari na kama mafunzo yao ni hayo aliamini hata kule Tanzania kuhusu makanisa ya kibrazili basi ni hatari pia kuendelea kuwepo.
Muda huo Hamza alivyogeuka aliweza kuona macho ya rangi ya bluu yalikuwa yakimwangalia kwa wasiwasi. Alikuwa ni Princess Airami ambae kwa macho yake tu alionekana kuwa katika hofu na kutia huruma.
“Princess Aira , haina haja ya kuwa na hofu . Kila kitu kipo sawa sasa”Aliongea Hamza akiwa na tabasamu.
Aira alionekana kuona ukarimu wa Hamza na palepale taratibu taratibu alisimama . Alionekana alishituka mara baada ya Hamza kumsukumia chini na makelele ya mirindimo ya bunduki ilikuwa ni ngumu kutokurejewa na fahamu..
“Wewe ni nani?”Aliuliza Aira kwa lugha ya kifaransa , huku macho yake yakionyesha kuwa na aibu kubwa . Wakati huo alipokuwa akiongea alikuwa ameegamia upande na hakuthubutu kumwangalia Hamza usoni.
Tofauti na wanafamilia wengi wa kifalme , ambao waliona kawaida sana kuonekana hadharani , lakini kwa Aira ilikuwa tofauti, alisifika kwa kuwa na aibu mno na ndio maana mara nyingi alipotokea katika kusanyiko alivaa Nikabu.
Aibu za Aira zilimfanya kumvutia Hamza . kwa uzuri wake usiokuwa wa kawaida na urefu wa mita moja nukta saba , ilikuwa ngumu sana kuona dosari katika uumbaji wake. Dosari pekee alioweza kuona ni kutokujiamini kwake.
“Jina langu naitwa Hamza , nilikuwa nikipita tu na kugundua umetekwa na ndio maana nikaja kukuokoa. Usikifirie sana kuhusu unachokiona”Aliongea Hamza.
“A.. amzha..”Alionekana kushindwa kutamka vizuri , hakuwahi kusikia jina hilo kabla na kama amelisikia pengine hakuwahi kulitamka.
“Amzah tupo wapi hapa?”Aliuliza kwa sauti ya unyonge.
Hamza mara baada ya kuulizwa swali hilo hata yeye mwenyewe alijishangaaa, wakati wa kuwafuatilia majambazi hakutilia umakini juu ya eneo walipo hivyo hakuwa na uelewa eneo hilo ni wapi.
“Princess , subiri tutoke nje , nikiona alama barabarani nitajua tupo wapi”Aliongea Hamza na kumfanya Aira kupepesa macho yake mazuri na baada ya sekunde kadhaa kupita alionekana kuanza kucheka.
“Princess ! mbona unacheka au nimekosea?”Aliuliza Hamza akiwa katika mshangao maana aliamini maneno yake hakuna alilosema likawa linachekesha.
“Hamna tu , samahani sio kama nakucheka bali ulivyojibu inachekesha , nilikuwa nauliza hapa ndani ni wapi? Kuna haja ya kuangalia alama za barabarani?”Aliuliza na Hamza palepale alijikuta akijidharau.
“Kumbe ulikuwa ukiuliza kuhusu hapa , Humu ndani ni chumba chini ya ardhi ndani ya kanisa , itakuwa ndio kambi ya hawa waumini.Tukiachana na hayo Princess , je unajua kuhusu wauamini wa Sinagogu? Nahisi sio kawaida kwa wao kukuteka , kuna sababu yoyote ambayo unaifahamu?”Aliuliza Hamza na Airami alitingisha kichwa kukataa.
“Nimefika hapa nchini kwa ajili ya kushiriki katika sherehe za kukata utepe , wakati nikitokea Airport kwenda hotelini nilihisi tu harufu nzuri ndani ya gari na nikapitiwa na usingizi”
Hamza alitingisha kichwa kuelewa , kwa maelezo hayo Hamza aliamini mlipuko ule wa bomu haukuwa ukihusiana na kutekwwa kwa Princess Aira bali ilikuwa ni kuwachanganya polisi kwakutengeneza machafuko.
“Princess nitakuondoa hapa kukurudisha , Umetekwa hivyo watu wengi watakuwa na wasiwasi juu yako”
Princess huyo mara baada ya kusikia hivyo alitngisha kichwa kukubali.
“Sawa , nadhani napaswa kukusumbua tena , Hamza”Aliongea akijitahidi kuita jina la Hamza kwa usahihi.
“Usijali kwangu ni swala dogo sana , kumuokoa mwanamke mrembo ni jukumu langu kama mwanaume , isitoshe pia wewe ni princess”
Aira mara baada ya kusikia hivyo alishikwa na aibu tena na aliishia kushika mikono yake huku akianza kumfuata Hamza kwa nyuma.
Wakati Hamza akiongoza kuitafuta njia ya kutokea , palepale alionekana kufikiria kitu na aligeuka na kumwangalia Aira.
“Princess , unaonekana kuwa jasiri mno , huogopi maiti zote hizo tulizopita?”Aliuliza na kumfanya Aira kushangaa kwa sekunde.
“Nilisahau”
“Umesahau?!”
“Ndio nimesahau kama kuna watu wamekufa pale”Aliongea akiwa ameinamisha kichwa chini akikwepesha macho yake na Hamza.
Hamza alijikuta akikosa usemi , aliona princess huyo ukilaza wake ulivutia mno , kilichomshangaza zaidi ni namna ambavyo alikuwa na aibu.
Hamza palepale alielewa kwanini mfalme Ingridi alikuwa akimficha binti yake katika macho ya watu. Kwa aibu hizo alimuonea huruma.
Mara baada ya kutoka nje ya kanisa hakukuwa na watu kuzunguka eneo hilo . Lakini kulikuwa na magari kadhaa yaliokuwa yameegeshwa kando ya barabara.
Hamza aliangalia mpangilio wa magari hayo na aliamini lazima magari hayo yatakuwa ni ya wale waumini, na kwa sababu alishawaua wote aliona magari hayo hayana mmiliki tena.
Hamza aliachana na magari ya kifahari na kutafuta gari ambalo lilionekana kuchakaaa na kisha palepale alivunja kioo na kufungua mlango kupitia ndani na mara baada ya kuingia ndani alianza kulazimisha gari hio kuwaka kwa kuchezesha nyaya.
Princess Aira ambae alikuwa akifuatisha nyuma nyuma alionekana kuwa na shauku kutokana na mambo aliokuwa akiyafanya Hamza.
“Hamza unataka turudi kwa gari?”Aliuliza.
“Ndio . Au unataka kupiga simu na kuwaambia upo salama?”Aliuliza Hamza.
“Hapana , kwasababu matatizo yamenitokea nikiwa katika gari ambayo imeandaliwa na walinzi nikifika Airport. Kuna uwezekano moja ya walinzi wangu ni msaliti. Nikipiga simu na kuwaambia nilipo ni sawa na kuwaambia waje kuniteka kwa mara ya pili, Au wewe unaonaje?”Aliuliza
Hamza mara baada ya kusikia hivyo alionekana kushangaa mno kuona alikuwa na uwezo wa kuchanganua mambo.
“Upo sahihi kabisa , unaonekana uko vuzuri kichwani Princess. Nilikudhania ni msichana mjinga”Aliongea Hamza akiwa na tabasamu na kumfanya Aira kuangalia pembeni kutokana na aibu kumzidia.
“Hapana , nimejifikiria mimi mwenyewe , maana mpaka sasa sijui kwanini nimetekwa”
Hamza licha ya kumuita msichana mjinga , Aira alionekana kutojali kabisa.
Hamza kadri alivyokuwa akimwangalia Aira alivyo, alijiambia itakuwa furaha kubwa sana kwake akija kupata mtoto wa kike kama yeye hapo baadae.
“Princess , ingia sasa tuondoke”Aliongea Hamza akimfungulia mlango wa nyuma na Aira alitingisha kichwa na kuingia ndani.
“Hamza kwanini usingechagua Mercedenz benz au Audi naona yapo mengi , ila hii Renault imechoka mno”Aliuliza Aira.
“Kwasababu ni magari ya zamani pekee yanayowaka kwa kuchezesha nyaya , hayo unayosema bila funguo hayawezi waka”
“Oh! Wewe ni Agent au mwanajeshi? Una nguvu na uwezo zaidi ya walinzi wa baba yangu”
Muda huo Hamza alikuwa ashaondosha gari hilo mkabala na kanisa hilo na kuianza safari ya kurudi mjini Parisi.
“Mimi ni mtu wa kawaida tu ambae nikiona tukio la uovu linatendeka naonyesha uwezo wangu mdogo wa mapigano”Aliongea Hamza lakini maneno yake ambayo hayakuwa na maana ya moja kwa moja yalimfanya Aira kuonekana kuwa na shauku zaidi na kuanza kumuuliza Hamza maswali kama vile ni raia wa nchi gani , anafanya kazi gani na yupo Paris kwa ajili ya nini.
Ijapokuwa princess huyo alikuwa na aibu sana , lakini kitendo cha kukaa nyuma mbali na macho ya Hamza alionekana kuongea sana.
Hamza upande wake alijibu na kumwambia anatokea Tanzania nchi kutoka Afrika , kazi yake ni msaidizi wa bosi ndani ya kampuni na amekuja Parisi na bosi wake kwa ajili ya shughuli za kibiashara.
Hakuchoka kumjibu , alifurahishwa na namna anavyoongea na alikuwa akimtania hapa na pale , lakini Aira alionekana kukubali kila Hamza anachoongea akishindwa kujua Hamza alikuwa akitania tu na kumjibu uongo baadhi ya maswali. Lakini kutokana na kuongea kwao ilifanya safari yao kutochosha kabisa.
Kitu ambacho hawakufahamu ni kwamba ile wanaondoka tu katika kanisa lile , watu waliovalia mavazi ya suti walifika nje ya kanisa na kuingia ndani. Kiongozi wa watu hao alikuwa na chata la mfupa kwenye shingo yake na X na alionekana dhahiri alikuwa ni mwanachama wa umoja huo wa Sinagogu.
Ukweli ni kwamba ibada zote za Sinagogu duniani zilikuwa zikirekodiwa na kamera za siri na kusambazwa moja kwa moja makao makuu, hususani zile za kikafara , Hivyo uvamizi wa Hamza ulishuhudiwa lakini ilichukua muda kwa watu hao kufika katika kanisa hilo kuzuia kutokana na kuwa mbali.
“Pumbavu! Ni wapi huyu mtu katokea , amewezaje kumuokoa Princess Aira?”Aliongea kiongozi akionekana kukasirika mno “Tukiruhusu Princess kurudi Paris itakuwa ngumu kumteka tena”Aliendelea kuongea.
“Kiongozi nadhani nafasi bado tunayo , tunaweza kuwasiliana na wenzetu ili kuwazuia kwa mbele”Aliongea mwanaume aliekuwa pembeni.
“Lakini huyu mtu ni hatari mno . Wasiwasi wangu hata wakijaribu kumzuia wataishia kupoteza maisha tu”Aliongea mwingine.
“Tunamtaka Princess Aira kwa namna yoyote ile , haijalishi awe amekufa au yupo hai . Misheni yetu ni kuhakikisha tunamrekodi tukimdhalilisha na kisha kuposti mtandaoni … lengo kuu la hii misheni ni…”
“Bosi unajaribu kusema…”Wanaume wawili waliokuwa pembeni yake walianza kucheka kishetani . Walionekana kuelewa kiongozi wao anachomaanisha bila ya kuongea.
*****
Ndani ya gari la kizamani la kampuni ya Renault , Hamza alikuwa akiongea kwa furaha na Princess Airami.
“Hamza , Tanzania ni kuzuri eh? Nasikia kuna wanyama wengi wakubwa na wakali kama Simba na Tembo , nina miaka ishirini na mbili ila sijawahi kufika Bara la Afrika”Aliongea Aira kinyonge.
“Wewe ni Princess si una huru wa kwenda popote?”
“Hapana , nikisafiri kidogo tu baba anatuma watu wanirudishe nyumbani na kila ninapoenda nakosa uhuru kwasababu ya kuwa na walinzi wengi na itifaki nyingi za ki usalama”
“Kama ni hivyo , siku nyingine mwambiae baba yako nataka kwenda nchi inayoitwa Tanzania na utakuwa chini yangu”Aliongea Hamza kwa kujiamini.
“Kweli? Lakini baba ataweza kuamini kweli na kunikubalia?”
“Nitakuachia namba yangu ya simu ,Ukitaka kuja nitamwagiza mtu aongee na baba yako , nina uhakika atakuruhusu”Aliongea Hamza
“Unafahamiana na baba yangu?”Aliuliza Aira akioneakna kuwa katika mshangao na Hamza aliishia kutoa tabasamu tu.
“Ndio , wewe niamini mimi , nina uhakika baba yako ataelewa nikishaongea nae”Aliongea Hamza na kumfanya Aira kupepesa macho yake.
“Sawa mimi nakuamini Hamza kwasababu umeweza kuniokoa . Lakini nitajie namba yako”Aliongea na Hamza alimtajia namba yake na Aira alionekana kuirudia rudia kuhakikisha ilikuwa sahihi.
“Wakati wa kunipigia hakikisha unaweka code za Tanzania kwanza , ukipiga hivyo hivyo haitofanya kazi Au tumia Watsapp”Aliongea Hamza.
“Oh sawa , sijawahi kumpigia mtu nje ya nchi bado na simu yangu haipo hapa nitakwenda kujaribisha..”
Wakati wakiendelea na safari . Hamza aligundua Aira alikuwa ameacha kuongea na alionekana kumwemwesa midomo kama vile kuna kitu anachoongea lakini hakikuweza kusikika.
“Princess , unaongea nini?”Hamza hakuelewa lakini swali lake lilimfanya Aira kuona aibu.
Narudia rudia kukariri namba yako ya simu , sina mahali pa kuiandika , nikijikumbusha mara nyingi sitoisahau”
Hamza mara baada ya kusikia hivyo hakujua acheke ama alie , hakujua kama angekuwa siriasi hivyo kwenye kukariri namba yake tu.
“Princess , huna haja ya kupata tabu namna hio , nitakuandikia kwenye karatasi tukishafika Paris au nitakutumia namba yangu kupitia Email”Aliongea Hamza na kumfanya Aira kufurahi.
“Lakini sina Email , tukifika Parisi niandikie”Aliongea.
Sauti hio ya kumtoa nyoka pangoni ilimpagashiwa mno Hamza , alitamani kuruka nyuma na kufanya jambo , ashawahi kuwa na wanawake warembo wa kizungu wengi hapo kabla lakini Aria aliwazidi kila kitu.
Wakati wanafika nusu safari kuingia Paris , hatimae waliweza kuona gari ya polisi mbele yao . Gari hio ilikuwa imesimama na polisi walikuwa wakimuwashia taa nyekundu kumwashiria asimame.
Hamza palepale alihisi kuna kitu hakipo sawa na kujiuliza au amegundulika ameiba gari maana eneo hilo kusimamishwa ni kama ilikuwa kinyume sana.
Kwa uzoefu wa Hamza Trafiki wa Ulaya hawakuwa na ufanisi mkubwa nje ya mji mpaka kuweka kambi , hivyo aliona ni ngumu kuamini wapo hapo kwa ajili ya doria.
Hata hivyo Hamza hakutaka kuwaza sana na palepale alisimamisha gari pembeni na kushusha kioo.
“Afisa kuna tatizo?”Aliuliza na mzungu huyo trafiki alimwangalia Hamza bila ya hisia zozote na kisha macho yake yakatua kwa Aira nyuma ya gari.
“Tafadhari onyesha leseni yako”Aliongea.
“Hii gari ni ya rafiki yangu na leseni haipo ndani ya gari”Aliongea Hamza huku akijiambia kama kweli polisi hao walikuwa wakitaka kuona leseni yake , anatakchofanya ni kumpigia tu mtu na kutatua tatizo
Yule trafiki wa kifaransa aliishia kutingisha kichwa na kisha alimwambia Hamza asubiri kidogo.
Muda ule polisi alienda mpaka kwenye gari yao na kuungana na mwenzake kisha alionekana kuchukua kitu.
Mara baada ya kugeuka Hamza alijua palepale hali haikuwa shwari, Kwani polisi wote walionekana kuvaa Mask usoni za kujikinga na hewa chafu.
Muda ule Hamza akipanga kuchukua hatua, polisi wale wawili walirusha mabomu mawili ya gesi.
“F*ck! “Hamza alijikuta akitoa tusi baada ya kugundua polisi hao mpango wao ulikuwa ni kuwaua kwa sumu na kisha ndio wachukue maiti zao.
Bomu lile la gesi lilitoa moshi mzito ambao ulizingira gari yao na muda uleule wale polisi walichomoa bastora zao na kuanza kushambulia kioo cha mbele cha gari ya Hamza.
Kutokana na ukale wa gari hio hazikuhitajika risasi nyingi, moja tu ilitosha kusambaratisha kioo na kufanya moshi ule wa sumu kuingia ndani.
Kwa mwendelezo zaidi , tembelea tovuti yetu ya fasihinet.com kuendelea , kipande cha 182 na 183 ni bure kabisa nenda na link;- SEHEMU YA 182
Pamoja mkuuSingano jr Mungu akubariki mkuu kazi yako ni njema Sana sana
Roma alikuwa mvuna nishati za mbingu n aardhi na kupanda levo kwa mapigo ya radi , Roma alikuwa ni mtu aliekuwa modified kisayansi mwili wake na kuwa na uwezo usio na kawaida , Roma alikuwa sehemu ya miungu ya kigiriki aka Hades mungu wa kuzimu , vibe kutoka dayari nyingine ...Zipo sifa nyingi tu ..Alafu Kaka singano nauliza tofauti za hawa wataalamu Roma na Hamza ni nini?
Episode 12Singano jr mi na elimu yangu ya menkwa hii Wala bado sijaelewa,Kwa hii simulizi ya shetani hamza nimeisoma hapa hapa jukwaani na nimeishia hiyo sehem ya 182,nataka unielimishe process ya malipo uko fasihinet,mfano nikilipa Elfu 2 nasoma episode ngapi?.