Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ni swala la mda2...let us wait...jumatano naendelea
siku bado haijaisha.....Huyu so mtu wa ahadi
Sawasawa ila Monday asha tunyima tayari,ama naongea sana😂😂😂siku bado haijaisha.....
SHETANI RUDISHA AKILI ZETU
MTUNZI: SINGANOJR
SEASON 03
SEHEMU YA 61.
Frida alijua kabisa anakwenda kufa na kifo chake kuja kuwa utata , aliweza kuona kilichokuwa kimemkaba kooni ni kivuli lakini hakuweza kufanya chochote.
Kwa mtu wa kawaida unaweza useme Frida alikuwa amepatwa na ukichaa au ugonjwa wa ajabu lakini ukweli ni kwamba kuna nguvu iliokuwa ikimkaba kupitia kivuli.
Wakati akiwa amekata tamaa ghafla tu ule utulivu wa kile chumba ulitoweka , ilikuwa ni kama upepo umeongezeka kwa kiasi kikubwa na kufumba na kufumbua kivuli kile kilipotea na kumfanya Frida kuanza kukohoa kwa nguvu , mpaka anakuja kutulia alijikuta akishituka mara baada ya kugundua kuna mtu mwingine ndani ya chumba chake alievalia joho la rangi nyeusi, alitaka kupiga yowe lakini mtu yule alimpa ishara ya kutulia.
“Wewe ni nani?”Aliuliza Frida kwa sauti ya chini huku akiwa ameshika shingo yake , ilikuwa bado hakuamini kama alikuwa amepona.
“Msimamizi wako na mlinzi wako mpya”Aliongea kwa lugha ya kingereza na kumfanya Frida kuchangayikiwa.
“Sikuwa na msimamizi na mlinzi , kwanini unajitambulisha kama mlinzi wangu mpya , nataka kujua unatokea upande upi , Wiccan au Sinagogu?”Aliongea Frida kwa sauti kubwa kidogo.
“Mimi ni mu’ alkemi kutoka makao makuu ya Wiccan , nipo hapa kwa maagizo ya Madame, mlinzi wako wa zamani amepoteza maisha”Aliongea na kumfanya Frida kuzidi kuchanganyikiwa lakini mara baada ya kusikia mtu huyo yupo hapo kwa maagizo ya Madame alipata ahueni.
“Mlinzi wangu wa zamani , unamaanisha mlinzi gani?”
“Alietaka kukuua amemuua mlinzi wako , kwanzia sasa utakuwa chini ya ulinzi wa binadamu”Aliongea huku akisogea karibu na mlango.
“Nilikuwa na mlinzi kivuli!!?”
“Wewe ni wa muhimu sana kwa Madame kuwasiliana na waumini wa ulimwengu wa nje ya kivuli , kwa namna yoyote unapaswa kuwa salama”Aliongea.
“Kwanini alitaka kuniua?”Aliuliza Frida, alikuwa akijua mtu ambae alitaka kumuua ni kivuli au watu ambao wamepata umaarufu kwa jina la Night Shadows(Vivuli vya watu vinavyoonekana usiku).
“Sina majibu kuhusu swali lako lakini nina ujumbe kutoka makao makuu”Aliongea kama roboti.
“Ujumbe gani?”
“Hakikisha anatumia mshumaa kurekodi ndoto zake ndio utakuwa salama, kadri atakavyoota bila ndoto zake kurekodiwa mtiririko wa matukio utakosekana na mpango wote kuingia dosari”Aliongea.
“Unamaanisha Ha…”
“Sikutajiwa jina , huu ndio ujumbe kutoka makao makuu unaopaswa kufanyia kazi”Aliongea yule bwana. Frida alitaka kuuliza swali zaidi lakini alijua asingepata majibu.
Yule bwana alievalia joho la rangi nyeusi mara baada ya kuridhika kwa kuona Frida alikuwa ameelewa aliaga.
“Wakati wowote ukiwa katika hatari na kuhitaji msaada wangu tamka neno , Grishav nitaitikia wito wako”Aliongea na palepale bila ya Frida kujibu aliinama chini na kufumba na kufumbua alipotea.
Frida alijikuta akiingia katika maswali mengi na swali kubwa lilikuwa juu ya ule mshumaa , alijua maelekezo yale yalikuwa yakimlenga Hamza lakini alishangaa mara baada ya kuambiwa Hamza anapaswa kutumia mshumaa ule ili kurekodi ndoto zake.
Swali ambalo alijiuliza inakuwaje mshumaa ambao alipatiwa na Dokta Genesha kuwa na uwezo wa kurekodi ndoto , kitu ambacho Wiccan walitaka iwe hivyo , inamaana kuna mpango uliokuwa ukiendelea kati ya Dokta Genesha na Wiccan kiasi cha kumkabidhi Mshumaa wa Nuru kwa ajili ya kumpatia Hamza.
Frida alijiuliza ni kitu gani ambacho kinaendelea yeye hakijui na kwanini amenusurika katika kifo.
Alikumbuka kwamba asipofanikisha Hamza kutotumia mshumaa basi atakuwa hatarini lakini swali lingine liliibuka inamaana Hamza alikuwa akiota bila ya kutumia ule mshumaa.
Kitu ambacho Frida alikuwa akijua ni kwamba mshumaa ule ulikuwa ni kwa ajili ya kumletea Hamza ndoto tu ili kujua maisha yake ambayo ameyasahau , hayo ndio yalikuwa maelekezo kutoka kwa Dokta Genesha na hakuelezwa kwamba mshumaa ule ni kifaa cha kurekodi ndoto, alijiuliza kama ni hivyo kinarekodi vipi hizo ndoto , ni sayansi ya namna gani ambayo imetumika.
Alijikuta hata usingizi ukimpelea kabisa licha ya kwamba alijihisi uchomvu mkubwa , hofu ilimvaa na hisia zake zilimwambia pengine anachofanya sio kuhatarisha usalama wake tu bali anahatarisha na usalama wa Hamza.
“Sina jinsi kwasasa lazima nihakikishe Hamza anatumia mshumaa ili kuwa salama , wakati nikitafuta majibu ya maswali yangu yote. Lakini nitafanya nini kumfanya atumie mshumaa kama yeye mwenyewe haniamini vya kutosha mpaka kuutumia?”Aliwaza Frida.
******
Hamza mara baada ya Side na wenzake kuondoka alibakia na mrembo Dina , wote wawili hawakuwa na ile mudi ya kwenda floor za juu kwa ajili ya kulewa vileo na kufanya starehe zingine kama kucheza kamari.
Kitu pekee ambacho Dina alipenda ndani ya Club hio ni kutumia siraha kulenga shabaha na hata Hamza alikuwa akipenda kitu kama hiko , kwake hakuwa mpenzi sana wa vileo na kucheza disco.
Walitumia zaidi ya lisaa limoja na nusu kulenga shabaha kwa kutumia bunduki za aina mbalimbali.
Ilipotimia saa tano kasoro njaa zilikuwa zikiwauma na Hamza alipendekeza warudi Kijichi ndio wakapate chakula huko na Dina hakupiinga.
Mara baada ya kufika kijichi chakula kiliandaliwa na wote wakaanza kula pamoja.
“Unaonaje baada ya hapa ukaangalie maendeleo ya vijana wangu , tokea siku ile ulivyowafundisha kiasi namna ya kucheza Karate na Kung Fu hukuwaona tena”Aliongea Dina.
Hamza kipindi kabla ya kukutana na Regina alikuwa ameshawahi kuwafundisha vijana wa Dina mafunzo ya Karate na Kung Fu mara moja na hakuwahi kwenda tena kuwaona.
“Hakuna shida , kuna kitu pia nataka kwenda kukifanyia mazoezi”Aliongea Hamza.
“Kitu gani , ni kuvuna nishati za mbingu na ardhi au kitu kingine?”Aliuliza Dina kwa shauku alikuwa akijua Hamza ana mafunzo ya kuvuna nishati za nguvu ya asili ya ardhi na mbingu na alitamani kujifunza pia siku moja.
“Hutoelewa hata nikikuambia ni kama maneno ya kutamka nataka kuyafanyia majaribio”Aliongea Hamza.
Ukweli ni kwamba kitu ambacho alikuwa akienda kufanyia majaribio ni yale maneno ambayo Yonesi alimtajia wakati akiwa hospitalini , siku ile wakati akifanya tahajudi kwa kupitia yale maneno aliona sura ya mwanamke ambae anamuona katika ndoto , bado shauku yake juu ya tukio lile haikuwa imeisha na alitaka kwenda kujaribu tena.
Baada ya kumaliza kula Hamza alitoka akiongozana na Dina pamoja na Lawrence na kwenda katika ukumbi maalumu ambao ni kama eneo la mafunzo ya kimapigano.
Hakukuwa na matumizi ya siraha , ilikuwa ni sehemu ambayo watu wa Dina walikuwa wakijifunza namna ya kupigana kwa kutumia mbinu mbalimbali za sanaa ya mapigano , eneo hilo lilikuwa likitambulika hata kwa serikali na lilikuwa na kibali kabisa.
Ni eneo ambalo lilijengwa katika mgawanyo wa sehemu mbili , sehemu ya kwanza ilikuwa ni kwa kufanyia mazoezi ya kawaida kama Gym na mazoezi ya boksa, Karate na Judo upande mwingine ulikuwa ni wa tahajudi.
Katika sanaa ya mapigano tahajudi ilikuwa ni sehemu ya mazoezi kwa ajili ya kuujua mwili wako ulivo, ukifanya tahajudi kama binadamu utajuwa wapi kuna udhaifu wako na wapi nguvu zako zinakaa kwa wingi na namna gani ya kushinda udhaifu wako.
Hamza mara baada ya kuona vijana wa Dina wakichukua mazoezi aliridhika , aliweza kuona wengi walikuwa wamepiga hatua kwa kufuata maelekezo yake.
“Bro , unapanga kufanya mazoezi ya namna gani , unataka kufanya tahajudi?”Aliuliza Lauwrence mara baada ya kumuona Hamza akichagua upande wa wanaofanya Tahajudi.
Dina na Lawrence siku zote walikuwa na shauku ya kutaka kumuona Hamza akichukua mazoezi hivyo walimwangalia.
“Kaa kimya Lau acha maswali mengi”Aliongea Dina akimzuia Lau kutokumsumbua Hamza na maswali yake.
Kutokana na wale wanafunzi kumuona Hamza na wao wote waliacha na kumpatia Hamza nafasi , kwao ni kama kuna kitu ambacho walitaka kujifunza kwa kumuangalia ndio maana walisimama pembeni.
Wakati Hamza akiwa katika mkao wa kufanya tahajudi huku midomo yake ikicheza ghafla tu watu wote walijikuta wakikumbwa na msisimko wa ajabu , ilikuwa ni kama kuna kiumbe cha ajabu kimefika ndani ya eneo hilo na kuwafanya kuanza kushindwa hata kupumua vizuri huku eneo ambalo Hamza alikuwa amekaa anga lake ni kama lilikuwa likitingishika.
Dina alijikuta jasho la paji la uso likimtoka huku akimwangalia Hamza kwa wasiwasi , alipatwa na hisia kama vile Hamza amekuwa mfalme ghafla na yeye ni kijakazi wake.
Upande wa Hamza hakuwa hata akielewa kilichokuwa kikiendelea kwa nje , kama alivyotarajia maneno yale yalikuwa ni kama anamwita yule mwanamke , mara ya kwanza wakati alivyofanya kule wodini alimuona kwa mbali yule mwanamke , lakini wakati huo kadri alivyokuwa akiimarisha umakini wake wa ubongo na kuzidi kuyatamka yale maneno alimuona ni kama vile yule mwanamke mchawi anaemuona kwenye ndoto alikuwa akimsogelea kutoka angani kwa spidi ya ajabu.
Zilipita kama dakika nne tu yule mwanamke aliweza kumuona kwa ukaribu zaidi, lakini jambo ambalo lilimshangaza Hamza ni kitu ambacho alikuwa ameshikilia mkononi.
Kadri alivyokuwa akizidi kuongea yale maneno mwanamke yule alizidi kusogea , lakini ilifikia hatua ni kama hawezi kumfanya asogee zaidi na yule mwanamke ni kama alijua Hamza hawezi kumuita karibu zaidi na alichokifanya ilikuwa ni kunyoosha kile kitu alichoshikilia mkononi mwake na Hamza mara baada ya kuangalia vizuri alijikuta akipagwa , ulikuwa ni ule mshumaa ambao Frida alimpatia akimwambia umetoka kwa Dokta Genesha, Mshumaa wa Nuru.
Hamza alichanganyikiwa mshumaa wa nuru kwanini upo katika mikono ya huyo mwanamke , katika ndoto yule mwanake alimuona kama mchawi ambae anachomwa moto baada ya kukamatika lakini kwanini akashika kitu cha nuru ilihali nuru na uchawi ni vitu viwili tofauti.
Yule mwanamke ni kama alikuwa akitaka Hamza amsogeze karibu aweze kushika ule mshumaa , upande wa Hamza alionekana kusita kuupokea ule mshumaa na yule mwanamke ni kama aliliona hilo na alitamka neno kwa kunyanyua mdomo wake kwa juu bila kutoa sauti akihakikisha Hamza anasoma lipsi zake.
NISAIDIE!(Help me)
Ndio neno ambalo aliongea huku akimpa ishara Hamza kupokea ule mshumaa.
Muda uleule Hamza aliacha kutamka yale maneno na kitendo kile kilifanya yule mwanamke ni kama vile kuna nguvu iliokuwa ikimvuta na kuzidi kurudishwa nyuma mbali na yeye , lakini bado hakuacha kumnyooshea ule mshumaa kama ishara ya kumuomba amsaidie.
Muda ileule wakati kila mtu akiwa ameloa jasho kana kwamba eneo lote limekumbwa na joto kali Hamza aliweza kufungua macho yake huku akionyesha hali ya kuwashangaa waliokuwa wakimwangalia .
“Nini kimetokea, Dina mbona upo hivyo?”Aliuliza Hamza mara baada ya kumuona
“Bado tu unapata muda wa kuuliza , ni kitu gani ulichokuwa ukifanya?”Aliuliza Dina na kumfanya Hamza sasa kuelewa kilichokuwa kikiendelea , licha ya yeye mwenyewe kuwa na wasiwasi lakini aliishia kucheka.
“I am sorry !, hii ni mara yangu ya kwanza kujaribisha hiki kitu , sikuweza kujizuia kile kinachonizunguka”AliongeaHamza na kisha alipiga hatua kuondoka katika eneo hilo.
Na wakati wakianza kutembea ndio sasa waligundua paa la jengo hili lilitingishika sana na kutokana na mchwa kula mbao unga unga ulidondoka chini kwenye tailizi na kila walipokuwa wakipiga hatua walikuwa wakiacha nyuma alama za miguu.
“Muda umeenda sana , nataka nirudi nyumbani”Aliongea Hamza.
“Hamza ni mafunzo gani yale , ni nguvu ya ndani au nishati ya mbingu na maji?”
“Ilianza mbingu ikaja ardhi halafu mbingu ikaleta maji na uhai , hizi ni kanuni za mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi na ni kitu ninachoweza kufanya pia , lakini kuhusu nilichofanya sasa hivi hata sijui ni kitu gani , kama nilivyosema nipo kwenye utafiti”Aliongea Hamza
“Hata jina lake hujui?”Aliuliza Dina kwa mshangao.
“Ndio ila kwasasa nitaiita hii kama Wito, kwasababu ukiifanya ni kama kuna kitu unakiiita”
“Huwa haifurahishi kusikiliza pekee”Aliongea Dina kwa macho yaliojaa huzuni na shauku.
“Usiongee hivyo , hiki ni kitu ambacho siwezi kukuruhusu ufanye kabla sijakipatia majibu , nguvu yake ni kubwa kiasi kwamba ni kama sijakula kabisa”Aliongea Hamza huku akijihisi ni mwenye njaa kali.
Dina alimwambia twende ukale na Hamza hakuwa na aibu ya kukataa kwani alikuwa na njaa , muda huo hawakurudi kwenye mgahawa bali Hamza alienda mpaka yalipo makazi ya Dina mita kadhaa kutoka mgahawa wake ulipo na mfanyakazi aliagizwa kuandaa chakula na Hamza alikaa chini na kuanza kukifakamia huku Dina akimwangalia kwa macho yaliojaa mahaba.
“Unajua nilishangaa baada ya mstaafu Mgweno kunipigia simu akisema yaishe”Aliongea Dina.
“Kwanini yeye ndio kakupigia simu?”,
“Unaweza kushangaa , licha ya kwamba kwa nje inaonekana familia ya Benjamini ndio inataka Regina kuolewa na James lakini upange mwingine ni mipango ya Mheshimiwa Mgweno”Aliongea Dina.
“Unataka kumaanisha nini?”
“Labda utakuwa hujui tu , ila kampuni ya Dosam ni kubwa Tanzania na inachangia zaidi ya asilimia tatu ya pato lote la Taifa , imeshikilia uchumi wa nchi katika maeneo nyeti, Benki namba moja ya kibiashara inayoongoza kwa Tanzania na Afrika mashariki yote ni Dosam Commercial Bank huu ni kama utawala wa mzunguko wa fedha nchini , hapa bado hujazungumzia usafiri wa anga , mahoteli na usambazaji wa bidhaa mbalimbali kwa matumizi ya majumbani, Kabla ya mheshimiwa Mgweno hajaingia madarakani Kampuni ya Zena ilikuwa ya kawaida tu kulinganisha na Dosam lakini baada ya Mgweno kuingia madarakani ilikua kwa spidi ya hali ya juu na yote hii ilikuwa ni uwekezaji mkubwa ambao mheshimiwa alifanya kwa kuiba hela za wananchi”Aliongea Dina.
“Kwahio unachomaanisha ni kwamba kampuni ya Zena inamilikiwa na Mheshimiwa mstaafu Mgweno?”
“Ndio kwa asilimia zaidi ya arobaini na tisa, ukifuatilia wana hisa wa kampuni ya Zena utagundua wengi wanaomiliki hisa hizo ni kampuni kutoka nje ya nchi , ukifuatilia kampuni hizo nje ya nchi utagundua kwamba ni kampiuni ambazo zimepewa haki kisheria ya kumiliki hisa hizo na kampuni nyingine , mzunguko unaendelea hivyo hivyo, zote ni njama za Mgweno kuficha wananchi kwamba anaimiliki Zena , sio kampuni moja tu , kila kampuni kubwa ana ushawishi wa kimaamuzi”
“Zote hizo ni hela za rushwa!?”
“Ndio lakini hakuna ushahidi wa kuthibitisha kama ndio mmiliki, sehemu pekee ambapo amekosa umiliki na ushawishi ni kampiuni ya Dosam peke yake na hii ni kutokana na msimamo wa aliekuwa kuongozi wa kampuni yaani babu yake Regina”Aliongea Dina na sasa ni kama Hamza alikuwa akipata picha.
“Kwahio anajaribu kuitumia familia ya Benjamini kwa ajili ya kuingiza ushawishi wake katika kampuni ya Dosam?”
“Ipo hivyo , mwanzoni walijua mambo yataenda sawa kama Regina atakubali kuolewa na James lakini mambo yamekuwa magumu , Regina karithi tabia zote za waanzilishi wa ile kampuni”
“Unamaanisha bibi yake na babu yake, unachoongea kinaonekana kuwa sahihi”Aliongea Hamza.
“Mgweno anachotaka ni kuimiliki Tanzania katika kila nyanja , kwanzia mtandao wa biashara haramu , biashara halali na kisiasa , hii itaifanya familia yake kuwa ya kifalme na raisi ni kama waziri mkuu tu anaepokea maagizo kutoka kwao”
“Kama ndio anachowaza anajidanganya , kuna mifano mingi ya kihistoria ni ngumu sana kuuchimba msingi wa nchi na kutengeneza nyufa pasipo kushitua wamiliki wake”
“Pengine anaelewa ila anaona ni kheri kujaribu kuliko kufa bila ya kujaribu”
“Kwahio baada ya kuona familia ya mzee Benjamini imekwama njia pekee alioona ni kumuua Regina maana urithi utaenda kwa mtoto wa pili?”
“Ndio lakini mipango yake inaonekana kukwama kutokana na uwepo wako , niseme tu umetibua mambo mengi sana , najua hata kunipigia simu ni kutokana na kujua ukaribu wetu na anatangeneza mazingira ya kujihami, lakini kwa wanaojua Mgweno kuna kitu lazima anapanga, walijaribu hadi mbinu ya kutaka kumtengeneza mtu wao ambae yupo karibu zaidi na Regina”Aliongea Dina na kumshangaza kidogo Hamza.
“Unamaanisha wale wazee ambao Regina amewafurumusha?”Aliuliza.
“Huo haukuwa mpango , wale wazee walikuwa wakifahamika tokea kipindi kirefu wapo kinyume na uongozi wa Regina”
“Ni nani ambae walikuwa wakimlenga?”
“Mchepuko wako alieniingiza kwenye matatizo”Aliongea huku akivuta midomo”
“Eliza!?”
Dina alitingisha mabega lakini kabla ya Hamza hajauliza swali lingine mlango wa kuingilai uligongwa kwa nguvu na Lawrence alionekana akiingia kwa pupa.
“Kuna nini Lawrence?”Aliuliza.
“Nimeletewa taarifa muda huu na vijana , Mheshimiwa Jongwe amefariki dunia kwa ajali ya gari na jeshi la polisi limeishikilia familia ya Mzee Seif kama washukiwa namba moja”Aliongea Lawrence na habari ile ilimtoa macho Dina.
“Unamaanisha mgombea wa kiti cha uraisi kupitia chama tawala , Jongwe amefariki, tena kwa ajali , kwanini familia ya mzee Seif ihusishwe kama ni ajali?”Aliongea Dina.
“Inawezekana sio ajali ya kawaida”Aliongea Hamza.
“Kwa maelezo niliopatiwa gari ambayo alikuwa amepanda imelipuka na ndani yake alikuwa ameambatana na Mzee Martin”Aliongea Lawrence na alivyoongea ni kama alijua taarifa ile itamshitua bosi wake na ilikuwa kweli kwani Dina alijikuta akisimama akiwa kama haamini.
“Mzee Seif na Mzee Martini mbona kama ushawahi kunitajia hawa watu?”Aliuliza Hamza.
“Ndio Bro hawa ndio washirika wetu wakubwa, japo mara nyingi inaaminika Mzee Seif ana uadui wa kisiasa na Mzee Martini”Aliongea Lawrence.
“Kwanini inaaminika hivyo ?”
“Kwasababu wote ni wanasiasa wa vyama tofauti , Mzee Seif ni kutokea chama cha upinzani na Martini ni kutoka chama tawala na wamekuwa wakipishana kama wabunge katika jimbo moja kwa zamu , uchaguzi huu akishika mzee Martini mwaka mwingine anashika Mzee Seif , awamu hii inayoisha Mzee Seif anamaliza muda wake lakini uelekeo wa kura upo upande wa Mzee Martini , siasa zao mara nyingi ni za kurushiana maneno”Aliongea Lawrence.
“Kwahio jeshi limemkamata Mzee Seif kwa kuamini kwamba ametegesha bomu katika gari la Mzee Martini ili ashinde uchaguzi , kama ni hivyo mgombea wa uraisi wa chama tawala kwanini amekufa pamoja na Martini?”Aliuliza Hamza lakini ni kama alikuwa akiipata picha.
“Lazima kuna kitu Mgweno anajaribu kufanya , hizi zote ni hila za kutaka kubomoa mtandao wa Chatu”Aliongea Dina kwa hasira.
“Lakini Madam Mheshimiwa Jongwe ni mgombea ambae amepata sapoti kubwa kutoka kwa mheshimiwa Mgweno , kwanini afanye hila ya kumuua mgombea ilihali zimebakia wiki chache kabla ya wananchi kupiga kura”
“Kesho kutwa pia ndio ilitarajiwa mkutano wa mwisho wa chama tawala kufanyika ili kufunga kampeni”Aliendelea kuongea Lawrence.
“Kuna picha inanijia akilini”Aliongea Hamza lakini upande wa Dina alionekana kuwa katika majonzi ya kumpoteza Mzee Martini, alikuwa ni moja ya mhimili wa mtandao wake.
“Lawrence polisi wanamshikilia kituo gani Mzee Seif?”
“Nasikia hawajamkamata bali wameizingira nyumba yake huko Kigamboni Mbutu B”Aliongea Lawrence.
“Yaani baada ya dakika kadhaa mlipuko kutokea na kuua watu, tayari washafikia maamuzi Mzee Seif ndio muhusika , mbona haingii akilini , hii lazima ni njama ya kutaka sisi twende tukamsaidie”Aliongea Dina.
“Tena nina uhakika hata hao wanaoitwa polisi ni feki”Aliongea Hamza huku akiweka kijiko chini.
“Madam tunapaswa kufanya nini?”Aliuliza Lau.
“Kama ninachofikiria ni sahihi lazima hili linahusiana na kikao nilichofanya na mheshimiwa Mgweno siku kadhaa zilizopita , mtandao wetu wote unajua ni kwa namna gani Mzee Seif alikuwa mwaminifu , nisipoingilia na kulifanyia hili maamuzi unadhani nitaonekanaje , Lawrence kusanya vijana wote ambao hawako mbali tutaenda kuangalai kinachoendelea”Aliongea Dina.
“Lakini Madam ulitoa maelekezo ya vijana karibia wote wakae chimbo , waliopo karibu na mjini hawazidi hata hamsini?”
“Haina haja”Aliongea Hamza huku akisimama.
“Watu hamsini ni wengi sana na hili linaweza kuwa ni mtego , hebu ita wale kumi kutoka jumba la mazoezi waje hapa , wanatosha sana”
“Bro unataka na wewe…”
“Hamza na wewe unataka kwenda?”
“Nataka nikajionee kinachoendelea , kama kweli huu mpango kaupanga Mgweno basi atakuwa katumia akili , unadhani kwa katiba yao ya chama nini kinafuata mara baada ya mgombea mkuu wa chama kufariki ghafla?”Aliuliza Hamza.
SEHEMU YA 62.
“Sijui kuhusu katiba yao inachosema , ila nina uhakika mgombea Mwenza ndio atachukua nafasi, kwanini unauliza?”Aliuliza tena Dina maana alijua Hamza hakuwa mtu wa siasa.
“Nawaza kuna mchezo unaochezwa hapa na kuna nguvu mbili kubwa za kisiasa , nataka kujionea mwenyewe”Aliongea Hamza na Dina alitingisha kichwa , kwasababu Hamza alitaka kwenda hakuona haja ya kumzuia , isitoshe ilimpelekea kujiamini zaidi kudili na hali kama hio.
Upande wa Dina alijua lazima kuna mchezo unaofanywa na kama Mzee Seif atakubali kuhusika moja kwa moja itaaminika mtandao wake ndio umekamilisha swala hilo , jambo ambalo hakautaka litokee.
Nyumba ya Mzee Seif ilikuwa Kigamboni Mbutu B na gari mbili ziliendeshwa kuelekea huko ya mbele akiwemo Hamza na Dina na ya nyuma ilikuwa Noah iliowabeba Lawrence na kundi lake.
Kitendo cha kufika eneo la tukio waliweza kuona watu walioizingira nyumba ya Mzee Seif , jambo ambalo liliwashangazwa hakukuwa na uwepo wa polisi hata mmoja ni kama Hamza alivyotarajia.
“Mbona sio polisi kama taarifa ilivyosema?”Aliuliza Dina kama kwamba Hamza alikuwa na majibu.
Hamza alichunguza eneo lote hasa wale watu walioshikilia siraha na alijikuta akikunja sura mara baada ya kuona wazungu wawili ndani ya eneo lile wakiwa ni sehemu ya watu waliozunguka nyumba hio.
“Ni kama nilivyotarajia kuna kinachoendelea hapa”Aliongea Hamza.
“Lakini kama kweli walikuwa wakimshuku Mzee Seif kulipua gari ya mheshimiwa Jongwe kwanini hawajaja polisi?”Aliuliza.
“Tutapata majibu yote mara baada ya kuongea nao”Aliongea Hamza huku akitangulia kutoka nje ya gari.
Wale watu kama walinzi walioshikilia siraha wakiwa wamezingira nyuma hio waliongeza umakini kwa Dina na kundi lake.
“Kama tabia yako ya siku zote, Dina mrembo wa kujiamini , naona umekuja na watu wachache mno tofauti na nilivyotegemea”Sauti ya mwanaume ilisikika kwasababau ilikuwa kuna giza hawakumuona vizuri na mara baada ya kusogelea taa za mwanga wa gari ndio Dina aliweza kumuona.
“Pancho!, unafanya nini hapa?”Aliongea Dina na muda huo ni kama sasa alishaanza kupata picha ya kile kinachoendelea.
“Nimekuja kukusalimia kwa mara nyingine mara baada ya kukataa pendekezo ya dili nono”Aliongea na muda ule alitoa ishara na baada ya kupita dakika mmoja tu wanaume wanne walitoka katika nyumba hio na moja wapo ya wanaume wale alikuwa ni Mzee Seif alieshikiliwa na wanaume wawili weusi waliojazia mwili , mtu wa mwisho kutoka alikuwa ni Mzungu- Mjapani , yaani mtu aliechanganya rangi ya mjapani na Mzungu.
Kilichomfanya Dina kuanza kupandwa na hasira alijua mpango wote huu ulisukwa na Pancho.
Pancho alikuwa ni moja ya wasimamizi wa mtandao wao upande wa Congo na siku kadhaa nyuma Dina alipokea dili kupitia kwa Pancho kutoka kwa Wacanada ambao walitaka kuingiza siraha za kivita Congo kupitia Bandari ya Mtwara.
Dili hili liliungwa mkono na Mheshimiwa Mgweno lakini Dina aliona halikuwa na maslahi na kama angelikubali ni kama kujipiga risasi mguuni, ikizingatiwa siraha hizo zilipaswa kufikishwa kwa kundi lingine la waasi ndani ya Congo tofauti na lile ambalo wanashirikiana nalo kwa muda mrefu.
“Mzee Seif nini kimetokea , kwanini taarifa nilizopokea ni wewe kuhusika na kumuua Mzee Martini na mheshimiwa Jongwe?”Aliuliza Dina akimpotezea Pancho.
“Hawa ndio wahusika , wameiteka familia yangu na wanataka nikiri kuhusika kwa kushirikiana na wewe kumuua Jongwe au turejee mezani na kuanza mazungumzo ya kuingiza siraha Tanzania kwenda Congo”Aliongea Mzee Seif aliekuwa na hali ya hofu na kumfanya Pancho kutoa tabasamu.
“Pancho unajaribu kufanya nini , nani yupo nyuma yako?”
“Dina hakuna ambae yupo nyuma yangu?”Aliongea Pancho kwa kejeli.
“Kwa kumuua mgombea wa uraisi kupitia chama tawala, unasema hakuna ambae yupo nyuma yako?”Aliongea Dina kwa hasira na kumfanya Pancho kutoa tabasamu la kifedhuli.
“Nilitaka hili swala angalau ulichukulie kwa uzito wake, ushahidi wa wewe kuhusika katika shambulizi la kulipua bomu gari ya mgombea wa uraisi kupitia chama tawala upo , unaweza ukawa wa kutengeneza lakini jeshi la polisi lipo tayari kuuamini na kama likitoka uraiani , kitengo cha TISA kitakufanya mbuzi wa kafara, lakini huko kote ni kujisumbua kama upo tayari kuchagua chaguo zuri kati ya matatu alioongea Mzee Seif?”
Hamza muda huo alikuwa akiangalia mazingira yalivyo na watu wote waliokuwa hapo walikuwa na siraha za bunduki na haraka haraka kwa sheria ya Tanzania ilikua ngumu kwa watu hao kumiliki hizo siraha labda iwe kuna mtu ndani ya serikali ambae alikuwa akihusika.
Isitoshe safari yao kutoka kijichi mpaka kufka hapo , kama kweli jeshi la polisi lilikuwa sirasi kukamata watu hao waliomsababishia ajali mgombea wa kiti cha uraisi basi wangeshafika labda tu iwe kuna maagizo ambayo yamewafanya kuchelewa.
“Hizo siraha mnaotaka kuingiza Tanzania mnazitoa wapi?”Aliongea Hamza.
“Oh!, ahsante kwa kuuliza bwana mdogo , kidogo tu nimesahau kumtambulisha bosi wetu hapa , huyu ni Bosi Keita na ndio msingi wa haya maungumzo , kuhusu wapi siraha zinatoka ni juu yake”Aliongea Pancho kwa kujigamba.
“Pancho kama nilivyosema mtandao wetu haudili na maswala ya siraha bila ya utaratibu maalumu, kama unataka dili hili lipite lisimamie wewe mwenyewe na hela zako na sio za mtandao wa Chatu”Aliongea Dina na yule bwana mwenye asili ya kizungu na Kijapani alimpa ishara Pancho ya kuongea yeye.
“Miss Dina kama alivyoongea Pancho tunaweza kulimaliza hili swala kimya kimya na kusiwe na athari zozote kwa kila upande”Aliongea kwa Kingereza.
“Unamaanisha unaweza kuzima kesi ya kulipua gari ya mgombea wa Uraisi pamoja na Martini?”Aliuliza Lawrence.
“Itategemea na maamuzi ya Miss Dina?”
“Kwanini nahisi hata waliompendekeza Jongwe kupeperusha bendera ya Chama ni kama wanashangilia kifo chake?”Aliongea Hamza huku wakati huo Dina akiwa ametulia.
“Tunafanyaje?”Aliuliza Dina akimegemea Hamza , isitoshe ndie aliesema wasije na watu wengi.
“Wana siraha na hata kama tukishambuliana bila siraha hatuwezi kushinda bila kushitua raia , hawa watu wana mafunzo ya mapigano”Aliongea Hamza na kumfanya Dona kuwa na wasiwasi.
“Usiwaze hili naweza kulimaliza kwa amani na kisha utadili nao kujua nini kinaendelea kuhusu mgombea wa uraisi kulipuliwa”Aliongea Hamza na japo Dina alikuwa na wasiwasi aliamua kumwamini Hamza.
“Bwana Keita kwa ninavyojua huwezi kudili na siraha pasipo kuwakilisha shirika la giza unalotokea”Aliongea Hamza akitaka kujua Black Association ambayo Keita anatokea.
“Jungle Army Merchant ndio ninatokea”Aliongea bila ya kusita sita.
“Kumbe ni Jungle , hebu subiri kwanza nipige simu, nikimaliza utaamua cha kufanya”Aliongea.
“Umpigie nani?”
“Utajua nikimaliza’Aliongea Hamza.
“Mr Keita haina haja ya kupoteza muda na hawa watu , swala ni moja tu wachague chaguzi moja kati ya tatu tumalizane”Aliongea Pancho akionekana kukosa uvumilivu.
“Kimya! , sitaki unifundishe namna ya kufanya biashara”Aliongea Keira kwa kingereza na kumfanya Pancho kukaa kimya , isitoshe alikuwa akijua Jungle Army Merchant walikuwa wafanyabiashara wakubwa ndani ya Black Market kwa kuuza siraha za kila namna.
Muda huo Hamza alikuwa ashapiga simu tayari bila ya kuwa na wasiwasi kabisa.
*****
Magneto, Las Vegas- USA
Ni ndani ya jiji la Las Vegas , jiji ambalo kwa wacheza kamari hawakuhesabu muda , Usiku ni kama mchana na Mchana ni kama usiku tu ndani ya hili jiji.
Katika moja ya hoteli ya kifahri ya nyota tano ndani ya chumba cha hadhi ya raisi , alionekana mtu bonge mweusi mwenye kitambi akiwa amelala chali.
Alikuwa mrefu wa mita kama moja nukta tisa hivi , vidole vya mikono yake vilikuwa vimevishwa pete za madini ya almasi , Dhahabu na madini mengine ya thamani , shingoni alikuwa amevalia mikufu ya bei ghali.
Mtu yule bonge alijikuta akitandaza miguu yake vizuri huku akifumba fumba macho na kuyafumbua , katikati ya eneo la mapaja yake alionekana mwanamke mzungu mwenye nywele nyeupe(blonde) akiwa bize kumhudumia.
“Mr Mamen are you comfortable?”Aliuliza yule mwanamke kwa sauti tamu huku akiinua kichwa chake akimwangalia kwa macho malegevu , akimuuliza Big kama ni mwenye kuifurahia huduma.
Mwanaume yule bonge udenda ulikuwa ukitaka kumwagika kutoka kwenye midomo yake , alionekana alikuwa kwenye ulimwengu mwingine wa raha.
“Comfortable..!?, Deeper the better .”Aliongea akimaanisha azame chini zaidi ndio itakuwa vizuri.
“You’re so annoying , I’m realy tired ..”Aliongea yule mwanamke akimwambia anachukiza kwani amekwisha kuchoka.
Bonge yule mweusi kama msanii RickRoss alifungua droo ya meza pembeni na kitanda chake na kuchomoa maburungutu ya pesa za dola na kumtupia.
“Hakikisha najisikia vizuri mpaka kisogoni , nitakupa kiasi chochote cha pesa unachotaka”Aliongea Big na yule mwanamke uchomvu uliisha palepale na alijkuta akiongeza mashambulizi ya kuhakikisha Big anajisikia vizuri.
Dakika hio hio simu yake ilianza kuita , hata simu yake tu ilikuwa imetengenezwa kwa housing ya madini ghali sana na kuifanya ionekane kama kitu kisichokuwa cha kawaida kutokana na uthamani wake
“F*ck , kama ningejua ningeizima hii simu , nani ananipigia muda huu”Big alilaani huku akichukua ile simu na kuipokea maana namba ilikuwa mpya tena haikuwa ya taifa hilo
“Big naona kama kawaida yako sasa hivi unaringa , kwahio unaona sipaswi kukupigia hata kama ni swala linalohusu vita ya tatu ya dunia”Sauti ya kiume ilisikika katika simu ya Big.
Kitendo cha Mameni kusikia ile sauti mwili wake ulitetemeka na macho yake yalibadilika na kuwa mekundu na hata ule msisimko aliokuwa akisikia ulipotea.
Yule mwanamke aliekuwa bize kuhakikisha Big anafurahi alijikuta akipiga kelele mara baada ya kadudu kabig kupotea na kuwa kabamia.
“Boss!! , ni wewe kweli , naona hatimae umenipigia , nimekumisi sana”Aliongea Big huku sauti yake ikiwa imebadilika.
“Unafanya nini hapo , lazima utakuwa na m*laya kitandani , yaani ndio kwanza kunakucha wewe unahangaika na wanawake , kuna siku utafia kwenye kifua cha mwanamke”
“Hehe..Bosi wewe mwenyewe unanijua vizuri , isitoshe wewe ndio mtu pekee ulievunja rekodi yangu”Aliongea.
“F*ck you!”Alitukanwa.
“Bosi nasikia upo Tanzania , habari za siku nyingi , vipi naweza kuja huko?”
“Nina mambo mengi ya kufanya siku hizi tutaona kama unaweza kuja , nyie watu ni wasumbufu sana mkisikia nipo mahali mnataka kuja tu , sitaki usumbufu wenu nahitaji kutulia kwa sasa”
“Bosi kwa uwezo wako na ushawishi wako unaweza kuomba chumba mapumziko Ikulu na ukapatiwa na warembo kabisa , hayo sio mapumziko ila ni kujitia stress tu , mapumziko ni yale wafariji wanakuwa wanabadilika badilika kila siku kwenye kuusisimua mwili”
“Sterehe za kutumia hela hizo nishazichoka , hata nikikuambia ni namna gani nafurahia maisha ya sasa hivi hutonielewa Big”
“Kama ni hivyo bosi kwanini umenipigia simu , kuna dili jipya?”
“Hakuna dili lingine , nishastaafu hayo mambo”
“Sababu ni ipi sasa Bosi , au kuna sehemu nimekosea?”Aliuliza Big kwa upole.
“Kwenye biashara zako unamfahamu bwana anaefahamika kwa jina la Keita?”
“Ndio mwaka juzi niliingia dili na kundi moja linalofanya shughuli zao ndani ya Afrika kuiba madini Adimu na kuyauza kwenda kwenye moja ya kampuni ya maswala ya kiteknolojia nchini Ufaransa , linaongozwa na bwana Keita”Aliongea Big.
“Huyu bwana wako naona ana juhudi mno , muda huu nimeelekezewa mitutu ya bunduki ndio maana nimekupigia simu kuthibitisha , Big kwahio sasa hivi umeshaanza kuwa mkubwa kiasi cha kunisaliti kisa tu nnimetoka kwenye uringo?”
Big mara baada ya kusikia kauli hio kutoka kwa Hamza alijikuta mikono ikimtetemeka kiasi kwamba simu ilitaka kudondoka.
“Bosi , subiri kwanza , nitampigia simu sasa hivi , naomba kwanza nimfokee baada ya hapo unaweza kumuua”Aliongea Big na dakika ileile alikata simu na kuitafuta namba ya Keita.
“Mamen Babe! , unafanya nini sasa mbona imepotea!?”Yule kahaba wa kizungu aliongea lakini Mameni alimpotezea na mara baada ya kuipata namba ya Keita aliipiga palepale.
Mara baada ya Hamza kumaliza kuongea na simu hakuongea neno na alitulia akiangalia matokeo.
Ijapokuwa Keita hakujua Hamza alikuwa akiongea na nani kwenye simu lakini alihisi kuna kitu hakipo sawa.
Dakika ileile simu yake ilianza kuita na alisogea pembeni na kupogea lakini muda huo huo alianza kuonyesha ishara za kupaniki.
Upande wa pili ilikuwa ni sauti ya Big kutukana kimarekani kwa mara nyingi mfululizo kadri alivyoweza.
“Bosi nimefanya kosa gani?”
“Unataka kumuua nani sasa hivi?”
“Bosi umejuaje nataka kuua mtu?”
“Unaetaka kumuua ni bosi wangu”
“…”
Keita alijikuta akikosa neo , alishangaa mno kwa zaidi ya sekunde kumi , ni kama alikuwa akisharabu yale maneno.
“Ah!”
Alijikuta hofu ikimwingia na vigoti vya miguu yake vilianza kumlegea na alijikuta akigeuka na kumwangalia Hamza.
Upande wa Hamza alikuwa akimwangalia Keita tu kwa mbali na kwa jinsi alivyoonyesha kupaniki na woga alitamani kucheka.
“Mr Keita , Mr Keita , what happened?”Pancho aliuliza mara baada ya kuona mabadiliko.
Dina macho yake yalichanua alijua kabisa mabadiliko ya Keita ni kutokana na Hamza alipopiga simu na kwake aliona mwanaume Hamza alikuwa akimshangaza kila siku.
“Nini tatizo Mr Keita , mbona huongei?”Aliuliza Pancho kwa wasiwasi
“Hivi unajua mimi na vijana wangu tutakufa sasa hivi kutokana na ujinga wako na wale wanasiasa wapuuzi?”Aliongea kwa hasira.
“Unamaanisha nini Mr….”
Keita hakuchelewa alichomoa Desert Eagle kutoka kwenye kiuno chake na kumchapa risasi tatu Pancho palepale.
Mpaka Pancho anadondoka chini muonekano wake ulikuwa na shauku ya kutaka kujua kwanini Keita anamshambulia.
Keita mara baada ya kumalizana na Pancho alitoa maagizo kwa vijana wake kuwashambulia watu wa Pancho na walionekana kuwa shapu kweli kwani ndani ya sekunde wote walikuwa chini.
Baada ya Keita kuituliza hali alijikuta akimdondokea Hamza kwa magoti huku akiwa na wasiwasi mwingi akitia huruma.
“Prince Rich.. Bosi wangu ameniambia kila kitu , naomba unisamehe kwa ujinga wangu , sikubahatika kukutana na wewe ana kwa ana zaidi ya kusikia habari zako ndio maana nimekukosea…”
Kitendo kile kiliwashangaza mno Dina , Lawrence na wenzake , waliishia kujiuliza Hamza ni nani mpaka bwana yule kuwa na hofu namna ile kiasi cha kupiga magoti.
“Nipe bastora yako”Aliongea Hamza akiwa siriasi na kumfanya Keita kukakamaa mwili lakini alimpatiia.
‘Tafadhari naomba uwaache vijana wangu waondoke , walikuwa wakifuata maelekezo tu kutoka kwangu na wanazofamilia zinawategemea”Aliongea Keita lakini Hamza hakumjali na muda ule aliinua ile bastora na kujielekezea kwake kana kwamba anataka kujipiga risasi.
Tukio lile lilimshangaza kila mtu wakishindwa kuelewa Hamza anataka kufanya nini
“Hamza unataka kufanya nini , usipaniki..”Aliongea Dina lakini kabla hata hajamaliza Hamza alikuwa ashaachia risasi.
Bam!
Mlipuko ule wa bunduki ulimuogopesha mpaka Keita na wote walimwaangalia Hamza kwa mshangao na walishangaa zaidi baada ya kuona hakuna kilichotokea.
Risasi ambayo ilitoka katika ile bunduki ilikuwa katika vidole vya Hamza , haikueleweka amefanyaje lakini ilionekana aliikamata kabla ya kumfikia, tukio lile lilimfanya Keita kushindwa kuendelea kupiga magoti na kukaa chini kwa kunyoosha miguu huku mapigo yake ya moyo yakidunda kwa kasi.
“Kabla sijafanya chochote nataka muelezee kila kilichotokea… sababu ya kwamba umepiga magoti sio kwasabau ya bosi wako bali ni kwasababu yangu hivyo nataka majibu”Aliongea Hamza.
“Serafii.!!, nipo tayari kuongea”Aliongea Keita huku akipiga kichwa chini kiasi cha kutoka damu kwenye paji la uso.
“Anza kuelezea , kwanini kifo cha Mgombea wa uraisi na nani kahusika”Aliongea Hamza.
“Hatujahusika katika kumuua mtu , tupo hapa nchini kwa ajili ya mazungumzo ya biashara ya kupitisha Siraha Kwenda Congo kupitia bandari ya Mtwara , kitu pekee ambacho nafahamu kuhusu muhusika tulipewa kazi ya kumtorosha hapa nchini kupitia boti yetu”Aliongea na kauli ile ilimfanya Dina kusikiliza kwa umakini.
“Imekuwaje mkajiingiza , sitaki kuuliza maswali mengi elezea kila kitu ninachotaka kujua?”
“Mara ya mwisho nilivyokuja hapa nchini niliweza kukutana na mstaafu Mgweno kwa ajili ya kuingia dili la kupitisha siraha , lakini kutokana na usafirishaji wote wa Kimagendo kuwa chini ya Chatu hakutoa maamuzi badala yake aliwasiliana na Miss Dina ambae mara baada ya kuelekezwa kuhusu dili hili alikataa, Mstaafu baada ya ombi hili kukataliwa alituambia hana namna ya kutusaidia kwani njia pekee ya kupitisha siraha hizo ni moja tu ambayo ni Mtwara kutokana na bandari zote kuwa chini ya mwekezaji”
“Nini kiliendelea”
“Wakati tukifikiria namna ya kutafuta njia nyingine ya kukamilisha dili hili nilipokea simu kutoka kwa mtu ambae alijitambulisha ni msaidizi wa raisi”Aliongea.
“Unamaaniisha Mheshimiwa Eliasi Mbilu?”
“Ndio na alisema anataka kuonana na sisi kwa ajili ya mazungumzo ya namna ya kukamilisha kile tulichokuwa tukihitaji , kutokana na kuwa na haraka ya kufanikisha hili dili nilikubali na kupitia msaidizi wake alinipa maelekezo niwaache vijana na boti yetu nchini Tanzania kwa muda na nikutane nae jijini Kual Lampur nchini Malaysia ndani ya tarehe alionitajia wakati akiwa ziarani”
“Tokea tuzungumze kuhusu hili dili imeshapita mwezi miwili , inamaana huu mpango ulikuwa wa muda mrefu?”
“Inawezekana Miss Dina , kabla ya siku moja ya tarehe kufika , niliweza kufika Malaysia na nilikutana na mheshimiwa kwa siri sana kupitia msaidizi wake na nilitambulishwa kama mwekezaji”Aliongea Keitani kwa kutetemeka.
“Alitaka kuongea nini kwa siri namna hio?”Aliuliza Dina , ijapokuwa Keitani alijua alikuwa akitoa siri kubwa lakini hakuwa na jinsi.
“Aliniambia siku ya leo saa nne kamili za usiku mgombea wa kiti cha uraisi kupitia chama chake atafariki kwa ajali ya gari na atakaesababisha ajali hio napaswa kumtorosha nje ya nchi na kama ikishindikana nimuue kabla ya kukamatwa na polisi, kisha nitumie ushahidi feki wa tukio hilo kuhakikisha nakamilisha dili la kupitisha siraha”
“Ushahidi feki ni kutusingizia sisi ndio wahusika, si ndio?”
‘Ndio”
“Ameenda mbali mpaka kutengeneza ushahidi feki , yeye anafaidika nini katika hilo?”Aliuliza Lawrence.
“Kila kitu kipo wazi , naamini Jongwe sio chaguo lake na pili alitaka kujitengenezea njia za kupata maslahi hata akiwa amestaafu kupitia hili dili”Aliongea Hamza.
“Ndio , alitaka asilimia ishirini ya faida itakayopatikana na wakati huo huo Mgombea wa uraisi akiwa ni chaguo lake baada ya chaguo la Mgweno kufariki”Aliongea keita na kumfanya Dina sura kujikunja
“Mgweno na Eliasi wanataka kupinduana , madaraka huwa ni matamu sana”Aliongea Dina lakini upande wa Hamza hakujali nani anampindua nani.
“Vipi kuhusu muuaji ni nani?”
“Kuhusu mfungwa hatuna taarifa nyingi kuhusu yeye , tulipatiwa picha pekee na tuliambiwa ni mfungwa wa kidiplomasia aliefungwa kwa muda mrefu kwa siri”
“Yuko wapi kwasasa?”Aliuliza Hamza.
“Ametoweka mara baada ya tukio, tunaamini alikuwa na mpango wake binafsi wa kujitorosha baada ya kukamilisha misheni”Aliongea na kumfanya Hamza kuvuta pumzi.
“Picha yake ipo wapi”Aliuliza Hamza na Keita alimpa ishara bwana moja wa kizungu na alimsogezea Hamza simu na ilionekana picha ya mfungwa kwenye kioo cha simu na mara baada ya kuiangalia alijikuta macho yake yakichanua.
“What the f*ck!!”
Hamza alijikuta akitoa tusi na kumfanya Dina kusogea kuangalia picha hio ili kujua kwanini kashangaa.
ITAENDELEA.
Watsapp me kwa mwendelezo wa haraka haraka namba 0687151346
Umerudia mkuuSHETANI RUDISHA AKILI ZETU
MTUNZI: SINGANOJR
SEASON 03
SEHEMU YA 61.
Frida alijua kabisa anakwenda kufa na kifo chake kuja kuwa utata , aliweza kuona kilichokuwa kimemkaba kooni ni kivuli lakini hakuweza kufanya chochote.
Kwa mtu wa kawaida unaweza useme Frida alikuwa amepatwa na ukichaa au ugonjwa wa ajabu lakini ukweli ni kwamba kuna nguvu iliokuwa ikimkaba kupitia kivuli.
Wakati akiwa amekata tamaa ghafla tu ule utulivu wa kile chumba ulitoweka , ilikuwa ni kama upepo umeongezeka kwa kiasi kikubwa na kufumba na kufumbua kivuli kile kilipotea na kumfanya Frida kuanza kukohoa kwa nguvu , mpaka anakuja kutulia alijikuta akishituka mara baada ya kugundua kuna mtu mwingine ndani ya chumba chake alievalia joho la rangi nyeusi, alitaka kupiga yowe lakini mtu yule alimpa ishara ya kutulia.
“Wewe ni nani?”Aliuliza Frida kwa sauti ya chini huku akiwa ameshika shingo yake , ilikuwa bado hakuamini kama alikuwa amepona.
“Msimamizi wako na mlinzi wako mpya”Aliongea kwa lugha ya kingereza na kumfanya Frida kuchangayikiwa.
“Sikuwa na msimamizi na mlinzi , kwanini unajitambulisha kama mlinzi wangu mpya , nataka kujua unatokea upande upi , Wiccan au Sinagogu?”Aliongea Frida kwa sauti kubwa kidogo.
“Mimi ni mu’ alkemi kutoka makao makuu ya Wiccan , nipo hapa kwa maagizo ya Madame, mlinzi wako wa zamani amepoteza maisha”Aliongea na kumfanya Frida kuzidi kuchanganyikiwa lakini mara baada ya kusikia mtu huyo yupo hapo kwa maagizo ya Madame alipata ahueni.
“Mlinzi wangu wa zamani , unamaanisha mlinzi gani?”
“Alietaka kukuua amemuua mlinzi wako , kwanzia sasa utakuwa chini ya ulinzi wa binadamu”Aliongea huku akisogea karibu na mlango.
“Nilikuwa na mlinzi kivuli!!?”
“Wewe ni wa muhimu sana kwa Madame kuwasiliana na waumini wa ulimwengu wa nje ya kivuli , kwa namna yoyote unapaswa kuwa salama”Aliongea.
“Kwanini alitaka kuniua?”Aliuliza Frida, alikuwa akijua mtu ambae alitaka kumuua ni kivuli au watu ambao wamepata umaarufu kwa jina la Night Shadows(Vivuli vya watu vinavyoonekana usiku).
“Sina majibu kuhusu swali lako lakini nina ujumbe kutoka makao makuu”Aliongea kama roboti.
“Ujumbe gani?”
“Hakikisha anatumia mshumaa kurekodi ndoto zake ndio utakuwa salama, kadri atakavyoota bila ndoto zake kurekodiwa mtiririko wa matukio utakosekana na mpango wote kuingia dosari”Aliongea.
“Unamaanisha Ha…”
“Sikutajiwa jina , huu ndio ujumbe kutoka makao makuu unaopaswa kufanyia kazi”Aliongea yule bwana. Frida alitaka kuuliza swali zaidi lakini alijua asingepata majibu.
Yule bwana alievalia joho la rangi nyeusi mara baada ya kuridhika kwa kuona Frida alikuwa ameelewa aliaga.
“Wakati wowote ukiwa katika hatari na kuhitaji msaada wangu tamka neno , Grishav nitaitikia wito wako”Aliongea na palepale bila ya Frida kujibu aliinama chini na kufumba na kufumbua alipotea.
Frida alijikuta akiingia katika maswali mengi na swali kubwa lilikuwa juu ya ule mshumaa , alijua maelekezo yale yalikuwa yakimlenga Hamza lakini alishangaa mara baada ya kuambiwa Hamza anapaswa kutumia mshumaa ule ili kurekodi ndoto zake.
Swali ambalo alijiuliza inakuwaje mshumaa ambao alipatiwa na Dokta Genesha kuwa na uwezo wa kurekodi ndoto , kitu ambacho Wiccan walitaka iwe hivyo , inamaana kuna mpango uliokuwa ukiendelea kati ya Dokta Genesha na Wiccan kiasi cha kumkabidhi Mshumaa wa Nuru kwa ajili ya kumpatia Hamza.
Frida alijiuliza ni kitu gani ambacho kinaendelea yeye hakijui na kwanini amenusurika katika kifo.
Alikumbuka kwamba asipofanikisha Hamza kutotumia mshumaa basi atakuwa hatarini lakini swali lingine liliibuka inamaana Hamza alikuwa akiota bila ya kutumia ule mshumaa.
Kitu ambacho Frida alikuwa akijua ni kwamba mshumaa ule ulikuwa ni kwa ajili ya kumletea Hamza ndoto tu ili kujua maisha yake ambayo ameyasahau , hayo ndio yalikuwa maelekezo kutoka kwa Dokta Genesha na hakuelezwa kwamba mshumaa ule ni kifaa cha kurekodi ndoto, alijiuliza kama ni hivyo kinarekodi vipi hizo ndoto , ni sayansi ya namna gani ambayo imetumika.
Alijikuta hata usingizi ukimpelea kabisa licha ya kwamba alijihisi uchomvu mkubwa , hofu ilimvaa na hisia zake zilimwambia pengine anachofanya sio kuhatarisha usalama wake tu bali anahatarisha na usalama wa Hamza.
“Sina jinsi kwasasa lazima nihakikishe Hamza anatumia mshumaa ili kuwa salama , wakati nikitafuta majibu ya maswali yangu yote. Lakini nitafanya nini kumfanya atumie mshumaa kama yeye mwenyewe haniamini vya kutosha mpaka kuutumia?”Aliwaza Frida.
******
Hamza mara baada ya Side na wenzake kuondoka alibakia na mrembo Dina , wote wawili hawakuwa na ile mudi ya kwenda floor za juu kwa ajili ya kulewa vileo na kufanya starehe zingine kama kucheza kamari.
Kitu pekee ambacho Dina alipenda ndani ya Club hio ni kutumia siraha kulenga shabaha na hata Hamza alikuwa akipenda kitu kama hiko , kwake hakuwa mpenzi sana wa vileo na kucheza disco.
Walitumia zaidi ya lisaa limoja na nusu kulenga shabaha kwa kutumia bunduki za aina mbalimbali.
Ilipotimia saa tano kasoro njaa zilikuwa zikiwauma na Hamza alipendekeza warudi Kijichi ndio wakapate chakula huko na Dina hakupiinga.
Mara baada ya kufika kijichi chakula kiliandaliwa na wote wakaanza kula pamoja.
“Unaonaje baada ya hapa ukaangalie maendeleo ya vijana wangu , tokea siku ile ulivyowafundisha kiasi namna ya kucheza Karate na Kung Fu hukuwaona tena”Aliongea Dina.
Hamza kipindi kabla ya kukutana na Regina alikuwa ameshawahi kuwafundisha vijana wa Dina mafunzo ya Karate na Kung Fu mara moja na hakuwahi kwenda tena kuwaona.
“Hakuna shida , kuna kitu pia nataka kwenda kukifanyia mazoezi”Aliongea Hamza.
“Kitu gani , ni kuvuna nishati za mbingu na ardhi au kitu kingine?”Aliuliza Dina kwa shauku alikuwa akijua Hamza ana mafunzo ya kuvuna nishati za nguvu ya asili ya ardhi na mbingu na alitamani kujifunza pia siku moja.
“Hutoelewa hata nikikuambia ni kama maneno ya kutamka nataka kuyafanyia majaribio”Aliongea Hamza.
Ukweli ni kwamba kitu ambacho alikuwa akienda kufanyia majaribio ni yale maneno ambayo Yonesi alimtajia wakati akiwa hospitalini , siku ile wakati akifanya tahajudi kwa kupitia yale maneno aliona sura ya mwanamke ambae anamuona katika ndoto , bado shauku yake juu ya tukio lile haikuwa imeisha na alitaka kwenda kujaribu tena.
Baada ya kumaliza kula Hamza alitoka akiongozana na Dina pamoja na Lawrence na kwenda katika ukumbi maalumu ambao ni kama eneo la mafunzo ya kimapigano.
Hakukuwa na matumizi ya siraha , ilikuwa ni sehemu ambayo watu wa Dina walikuwa wakijifunza namna ya kupigana kwa kutumia mbinu mbalimbali za sanaa ya mapigano , eneo hilo lilikuwa likitambulika hata kwa serikali na lilikuwa na kibali kabisa.
Ni eneo ambalo lilijengwa katika mgawanyo wa sehemu mbili , sehemu ya kwanza ilikuwa ni kwa kufanyia mazoezi ya kawaida kama Gym na mazoezi ya boksa, Karate na Judo upande mwingine ulikuwa ni wa tahajudi.
Katika sanaa ya mapigano tahajudi ilikuwa ni sehemu ya mazoezi kwa ajili ya kuujua mwili wako ulivo, ukifanya tahajudi kama binadamu utajuwa wapi kuna udhaifu wako na wapi nguvu zako zinakaa kwa wingi na namna gani ya kushinda udhaifu wako.
Hamza mara baada ya kuona vijana wa Dina wakichukua mazoezi aliridhika , aliweza kuona wengi walikuwa wamepiga hatua kwa kufuata maelekezo yake.
“Bro , unapanga kufanya mazoezi ya namna gani , unataka kufanya tahajudi?”Aliuliza Lauwrence mara baada ya kumuona Hamza akichagua upande wa wanaofanya Tahajudi.
Dina na Lawrence siku zote walikuwa na shauku ya kutaka kumuona Hamza akichukua mazoezi hivyo walimwangalia.
“Kaa kimya Lau acha maswali mengi”Aliongea Dina akimzuia Lau kutokumsumbua Hamza na maswali yake.
Kutokana na wale wanafunzi kumuona Hamza na wao wote waliacha na kumpatia Hamza nafasi , kwao ni kama kuna kitu ambacho walitaka kujifunza kwa kumuangalia ndio maana walisimama pembeni.
Wakati Hamza akiwa katika mkao wa kufanya tahajudi huku midomo yake ikicheza ghafla tu watu wote walijikuta wakikumbwa na msisimko wa ajabu , ilikuwa ni kama kuna kiumbe cha ajabu kimefika ndani ya eneo hilo na kuwafanya kuanza kushindwa hata kupumua vizuri huku eneo ambalo Hamza alikuwa amekaa anga lake ni kama lilikuwa likitingishika.
Dina alijikuta jasho la paji la uso likimtoka huku akimwangalia Hamza kwa wasiwasi , alipatwa na hisia kama vile Hamza amekuwa mfalme ghafla na yeye ni kijakazi wake.
Upande wa Hamza hakuwa hata akielewa kilichokuwa kikiendelea kwa nje , kama alivyotarajia maneno yale yalikuwa ni kama anamwita yule mwanamke , mara ya kwanza wakati alivyofanya kule wodini alimuona kwa mbali yule mwanamke , lakini wakati huo kadri alivyokuwa akiimarisha umakini wake wa ubongo na kuzidi kuyatamka yale maneno alimuona ni kama vile yule mwanamke mchawi anaemuona kwenye ndoto alikuwa akimsogelea kutoka angani kwa spidi ya ajabu.
Zilipita kama dakika nne tu yule mwanamke aliweza kumuona kwa ukaribu zaidi, lakini jambo ambalo lilimshangaza Hamza ni kitu ambacho alikuwa ameshikilia mkononi.
Kadri alivyokuwa akizidi kuongea yale maneno mwanamke yule alizidi kusogea , lakini ilifikia hatua ni kama hawezi kumfanya asogee zaidi na yule mwanamke ni kama alijua Hamza hawezi kumuita karibu zaidi na alichokifanya ilikuwa ni kunyoosha kile kitu alichoshikilia mkononi mwake na Hamza mara baada ya kuangalia vizuri alijikuta akipagwa , ulikuwa ni ule mshumaa ambao Frida alimpatia akimwambia umetoka kwa Dokta Genesha, Mshumaa wa Nuru.
Hamza alichanganyikiwa mshumaa wa nuru kwanini upo katika mikono ya huyo mwanamke , katika ndoto yule mwanake alimuona kama mchawi ambae anachomwa moto baada ya kukamatika lakini kwanini akashika kitu cha nuru ilihali nuru na uchawi ni vitu viwili tofauti.
Yule mwanamke ni kama alikuwa akitaka Hamza amsogeze karibu aweze kushika ule mshumaa , upande wa Hamza alionekana kusita kuupokea ule mshumaa na yule mwanamke ni kama aliliona hilo na alitamka neno kwa kunyanyua mdomo wake kwa juu bila kutoa sauti akihakikisha Hamza anasoma lipsi zake.
NISAIDIE!(Help me)
Ndio neno ambalo aliongea huku akimpa ishara Hamza kupokea ule mshumaa.
Muda uleule Hamza aliacha kutamka yale maneno na kitendo kile kilifanya yule mwanamke ni kama vile kuna nguvu iliokuwa ikimvuta na kuzidi kurudishwa nyuma mbali na yeye , lakini bado hakuacha kumnyooshea ule mshumaa kama ishara ya kumuomba amsaidie.
Muda ileule wakati kila mtu akiwa ameloa jasho kana kwamba eneo lote limekumbwa na joto kali Hamza aliweza kufungua macho yake huku akionyesha hali ya kuwashangaa waliokuwa wakimwangalia .
“Nini kimetokea, Dina mbona upo hivyo?”Aliuliza Hamza mara baada ya kumuona
“Bado tu unapata muda wa kuuliza , ni kitu gani ulichokuwa ukifanya?”Aliuliza Dina na kumfanya Hamza sasa kuelewa kilichokuwa kikiendelea , licha ya yeye mwenyewe kuwa na wasiwasi lakini aliishia kucheka.
“I am sorry !, hii ni mara yangu ya kwanza kujaribisha hiki kitu , sikuweza kujizuia kile kinachonizunguka”AliongeaHamza na kisha alipiga hatua kuondoka katika eneo hilo.
Na wakati wakianza kutembea ndio sasa waligundua paa la jengo hili lilitingishika sana na kutokana na mchwa kula mbao unga unga ulidondoka chini kwenye tailizi na kila walipokuwa wakipiga hatua walikuwa wakiacha nyuma alama za miguu.
“Muda umeenda sana , nataka nirudi nyumbani”Aliongea Hamza.
“Hamza ni mafunzo gani yale , ni nguvu ya ndani au nishati ya mbingu na maji?”
“Ilianza mbingu ikaja ardhi halafu mbingu ikaleta maji na uhai , hizi ni kanuni za mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi na ni kitu ninachoweza kufanya pia , lakini kuhusu nilichofanya sasa hivi hata sijui ni kitu gani , kama nilivyosema nipo kwenye utafiti”Aliongea Hamza
“Hata jina lake hujui?”Aliuliza Dina kwa mshangao.
“Ndio ila kwasasa nitaiita hii kama Wito, kwasababu ukiifanya ni kama kuna kitu unakiiita”
“Huwa haifurahishi kusikiliza pekee”Aliongea Dina kwa macho yaliojaa huzuni na shauku.
“Usiongee hivyo , hiki ni kitu ambacho siwezi kukuruhusu ufanye kabla sijakipatia majibu , nguvu yake ni kubwa kiasi kwamba ni kama sijakula kabisa”Aliongea Hamza huku akijihisi ni mwenye njaa kali.
Dina alimwambia twende ukale na Hamza hakuwa na aibu ya kukataa kwani alikuwa na njaa , muda huo hawakurudi kwenye mgahawa bali Hamza alienda mpaka yalipo makazi ya Dina mita kadhaa kutoka mgahawa wake ulipo na mfanyakazi aliagizwa kuandaa chakula na Hamza alikaa chini na kuanza kukifakamia huku Dina akimwangalia kwa macho yaliojaa mahaba.
“Unajua nilishangaa baada ya mstaafu Mgweno kunipigia simu akisema yaishe”Aliongea Dina.
“Kwanini yeye ndio kakupigia simu?”,
“Unaweza kushangaa , licha ya kwamba kwa nje inaonekana familia ya Benjamini ndio inataka Regina kuolewa na James lakini upange mwingine ni mipango ya Mheshimiwa Mgweno”Aliongea Dina.
“Unataka kumaanisha nini?”
“Labda utakuwa hujui tu , ila kampuni ya Dosam ni kubwa Tanzania na inachangia zaidi ya asilimia tatu ya pato lote la Taifa , imeshikilia uchumi wa nchi katika maeneo nyeti, Benki namba moja ya kibiashara inayoongoza kwa Tanzania na Afrika mashariki yote ni Dosam Commercial Bank huu ni kama utawala wa mzunguko wa fedha nchini , hapa bado hujazungumzia usafiri wa anga , mahoteli na usambazaji wa bidhaa mbalimbali kwa matumizi ya majumbani, Kabla ya mheshimiwa Mgweno hajaingia madarakani Kampuni ya Zena ilikuwa ya kawaida tu kulinganisha na Dosam lakini baada ya Mgweno kuingia madarakani ilikua kwa spidi ya hali ya juu na yote hii ilikuwa ni uwekezaji mkubwa ambao mheshimiwa alifanya kwa kuiba hela za wananchi”Aliongea Dina.
“Kwahio unachomaanisha ni kwamba kampuni ya Zena inamilikiwa na Mheshimiwa mstaafu Mgweno?”
“Ndio kwa asilimia zaidi ya arobaini na tisa, ukifuatilia wana hisa wa kampuni ya Zena utagundua wengi wanaomiliki hisa hizo ni kampuni kutoka nje ya nchi , ukifuatilia kampuni hizo nje ya nchi utagundua kwamba ni kampiuni ambazo zimepewa haki kisheria ya kumiliki hisa hizo na kampuni nyingine , mzunguko unaendelea hivyo hivyo, zote ni njama za Mgweno kuficha wananchi kwamba anaimiliki Zena , sio kampuni moja tu , kila kampuni kubwa ana ushawishi wa kimaamuzi”
“Zote hizo ni hela za rushwa!?”
“Ndio lakini hakuna ushahidi wa kuthibitisha kama ndio mmiliki, sehemu pekee ambapo amekosa umiliki na ushawishi ni kampiuni ya Dosam peke yake na hii ni kutokana na msimamo wa aliekuwa kuongozi wa kampuni yaani babu yake Regina”Aliongea Dina na sasa ni kama Hamza alikuwa akipata picha.
“Kwahio anajaribu kuitumia familia ya Benjamini kwa ajili ya kuingiza ushawishi wake katika kampuni ya Dosam?”
“Ipo hivyo , mwanzoni walijua mambo yataenda sawa kama Regina atakubali kuolewa na James lakini mambo yamekuwa magumu , Regina karithi tabia zote za waanzilishi wa ile kampuni”
“Unamaanisha bibi yake na babu yake, unachoongea kinaonekana kuwa sahihi”Aliongea Hamza.
“Mgweno anachotaka ni kuimiliki Tanzania katika kila nyanja , kwanzia mtandao wa biashara haramu , biashara halali na kisiasa , hii itaifanya familia yake kuwa ya kifalme na raisi ni kama waziri mkuu tu anaepokea maagizo kutoka kwao”
“Kama ndio anachowaza anajidanganya , kuna mifano mingi ya kihistoria ni ngumu sana kuuchimba msingi wa nchi na kutengeneza nyufa pasipo kushitua wamiliki wake”
“Pengine anaelewa ila anaona ni kheri kujaribu kuliko kufa bila ya kujaribu”
“Kwahio baada ya kuona familia ya mzee Benjamini imekwama njia pekee alioona ni kumuua Regina maana urithi utaenda kwa mtoto wa pili?”
“Ndio lakini mipango yake inaonekana kukwama kutokana na uwepo wako , niseme tu umetibua mambo mengi sana , najua hata kunipigia simu ni kutokana na kujua ukaribu wetu na anatangeneza mazingira ya kujihami, lakini kwa wanaojua Mgweno kuna kitu lazima anapanga, walijaribu hadi mbinu ya kutaka kumtengeneza mtu wao ambae yupo karibu zaidi na Regina”Aliongea Dina na kumshangaza kidogo Hamza.
“Unamaanisha wale wazee ambao Regina amewafurumusha?”Aliuliza.
“Huo haukuwa mpango , wale wazee walikuwa wakifahamika tokea kipindi kirefu wapo kinyume na uongozi wa Regina”
“Ni nani ambae walikuwa wakimlenga?”
“Mchepuko wako alieniingiza kwenye matatizo”Aliongea huku akivuta midomo”
“Eliza!?”
Dina alitingisha mabega lakini kabla ya Hamza hajauliza swali lingine mlango wa kuingilai uligongwa kwa nguvu na Lawrence alionekana akiingia kwa pupa.
“Kuna nini Lawrence?”Aliuliza.
“Nimeletewa taarifa muda huu na vijana , Mheshimiwa Jongwe amefariki dunia kwa ajali ya gari na jeshi la polisi limeishikilia familia ya Mzee Seif kama washukiwa namba moja”Aliongea Lawrence na habari ile ilimtoa macho Dina.
“Unamaanisha mgombea wa kiti cha uraisi kupitia chama tawala , Jongwe amefariki, tena kwa ajali , kwanini familia ya mzee Seif ihusishwe kama ni ajali?”Aliongea Dina.
“Inawezekana sio ajali ya kawaida”Aliongea Hamza.
“Kwa maelezo niliopatiwa gari ambayo alikuwa amepanda imelipuka na ndani yake alikuwa ameambatana na Mzee Martin”Aliongea Lawrence na alivyoongea ni kama alijua taarifa ile itamshitua bosi wake na ilikuwa kweli kwani Dina alijikuta akisimama akiwa kama haamini.
“Mzee Seif na Mzee Martini mbona kama ushawahi kunitajia hawa watu?”Aliuliza Hamza.
“Ndio Bro hawa ndio washirika wetu wakubwa, japo mara nyingi inaaminika Mzee Seif ana uadui wa kisiasa na Mzee Martini”Aliongea Lawrence.
“Kwanini inaaminika hivyo ?”
“Kwasababu wote ni wanasiasa wa vyama tofauti , Mzee Seif ni kutokea chama cha upinzani na Martini ni kutoka chama tawala na wamekuwa wakipishana kama wabunge katika jimbo moja kwa zamu , uchaguzi huu akishika mzee Martini mwaka mwingine anashika Mzee Seif , awamu hii inayoisha Mzee Seif anamaliza muda wake lakini uelekeo wa kura upo upande wa Mzee Martini , siasa zao mara nyingi ni za kurushiana maneno”Aliongea Lawrence.
“Kwahio jeshi limemkamata Mzee Seif kwa kuamini kwamba ametegesha bomu katika gari la Mzee Martini ili ashinde uchaguzi , kama ni hivyo mgombea wa uraisi wa chama tawala kwanini amekufa pamoja na Martini?”Aliuliza Hamza lakini ni kama alikuwa akiipata picha.
“Lazima kuna kitu Mgweno anajaribu kufanya , hizi zote ni hila za kutaka kubomoa mtandao wa Chatu”Aliongea Dina kwa hasira.
“Lakini Madam Mheshimiwa Jongwe ni mgombea ambae amepata sapoti kubwa kutoka kwa mheshimiwa Mgweno , kwanini afanye hila ya kumuua mgombea ilihali zimebakia wiki chache kabla ya wananchi kupiga kura”
“Kesho kutwa pia ndio ilitarajiwa mkutano wa mwisho wa chama tawala kufanyika ili kufunga kampeni”Aliendelea kuongea Lawrence.
“Kuna picha inanijia akilini”Aliongea Hamza lakini upande wa Dina alionekana kuwa katika majonzi ya kumpoteza Mzee Martini, alikuwa ni moja ya mhimili wa mtandao wake.
“Lawrence polisi wanamshikilia kituo gani Mzee Seif?”
“Nasikia hawajamkamata bali wameizingira nyumba yake huko Kigamboni Mbutu B”Aliongea Lawrence.
“Yaani baada ya dakika kadhaa mlipuko kutokea na kuua watu, tayari washafikia maamuzi Mzee Seif ndio muhusika , mbona haingii akilini , hii lazima ni njama ya kutaka sisi twende tukamsaidie”Aliongea Dina.
“Tena nina uhakika hata hao wanaoitwa polisi ni feki”Aliongea Hamza huku akiweka kijiko chini.
“Madam tunapaswa kufanya nini?”Aliuliza Lau.
“Kama ninachofikiria ni sahihi lazima hili linahusiana na kikao nilichofanya na mheshimiwa Mgweno siku kadhaa zilizopita , mtandao wetu wote unajua ni kwa namna gani Mzee Seif alikuwa mwaminifu , nisipoingilia na kulifanyia hili maamuzi unadhani nitaonekanaje , Lawrence kusanya vijana wote ambao hawako mbali tutaenda kuangalai kinachoendelea”Aliongea Dina.
“Lakini Madam ulitoa maelekezo ya vijana karibia wote wakae chimbo , waliopo karibu na mjini hawazidi hata hamsini?”
“Haina haja”Aliongea Hamza huku akisimama.
“Watu hamsini ni wengi sana na hili linaweza kuwa ni mtego , hebu ita wale kumi kutoka jumba la mazoezi waje hapa , wanatosha sana”
“Bro unataka na wewe…”
“Hamza na wewe unataka kwenda?”
“Nataka nikajionee kinachoendelea , kama kweli huu mpango kaupanga Mgweno basi atakuwa katumia akili , unadhani kwa katiba yao ya chama nini kinafuata mara baada ya mgombea mkuu wa chama kufariki ghafla?”Aliuliza Hamza.
SEHEMU YA 62.
“Sijui kuhusu katiba yao inachosema , ila nina uhakika mgombea Mwenza ndio atachukua nafasi, kwanini unauliza?”Aliuliza tena Dina maana alijua Hamza hakuwa mtu wa siasa.
“Nawaza kuna mchezo unaochezwa hapa na kuna nguvu mbili kubwa za kisiasa , nataka kujionea mwenyewe”Aliongea Hamza na Dina alitingisha kichwa , kwasababu Hamza alitaka kwenda hakuona haja ya kumzuia , isitoshe ilimpelekea kujiamini zaidi kudili na hali kama hio.
Upande wa Dina alijua lazima kuna mchezo unaofanywa na kama Mzee Seif atakubali kuhusika moja kwa moja itaaminika mtandao wake ndio umekamilisha swala hilo , jambo ambalo hakautaka litokee.
Nyumba ya Mzee Seif ilikuwa Kigamboni Mbutu B na gari mbili ziliendeshwa kuelekea huko ya mbele akiwemo Hamza na Dina na ya nyuma ilikuwa Noah iliowabeba Lawrence na kundi lake.
Kitendo cha kufika eneo la tukio waliweza kuona watu walioizingira nyumba ya Mzee Seif , jambo ambalo liliwashangazwa hakukuwa na uwepo wa polisi hata mmoja ni kama Hamza alivyotarajia.
“Mbona sio polisi kama taarifa ilivyosema?”Aliuliza Dina kama kwamba Hamza alikuwa na majibu.
Hamza alichunguza eneo lote hasa wale watu walioshikilia siraha na alijikuta akikunja sura mara baada ya kuona wazungu wawili ndani ya eneo lile wakiwa ni sehemu ya watu waliozunguka nyumba hio.
“Ni kama nilivyotarajia kuna kinachoendelea hapa”Aliongea Hamza.
“Lakini kama kweli walikuwa wakimshuku Mzee Seif kulipua gari ya mheshimiwa Jongwe kwanini hawajaja polisi?”Aliuliza.
“Tutapata majibu yote mara baada ya kuongea nao”Aliongea Hamza huku akitangulia kutoka nje ya gari.
Wale watu kama walinzi walioshikilia siraha wakiwa wamezingira nyuma hio waliongeza umakini kwa Dina na kundi lake.
“Kama tabia yako ya siku zote, Dina mrembo wa kujiamini , naona umekuja na watu wachache mno tofauti na nilivyotegemea”Sauti ya mwanaume ilisikika kwasababau ilikuwa kuna giza hawakumuona vizuri na mara baada ya kusogelea taa za mwanga wa gari ndio Dina aliweza kumuona.
“Pancho!, unafanya nini hapa?”Aliongea Dina na muda huo ni kama sasa alishaanza kupata picha ya kile kinachoendelea.
“Nimekuja kukusalimia kwa mara nyingine mara baada ya kukataa pendekezo ya dili nono”Aliongea na muda ule alitoa ishara na baada ya kupita dakika mmoja tu wanaume wanne walitoka katika nyumba hio na moja wapo ya wanaume wale alikuwa ni Mzee Seif alieshikiliwa na wanaume wawili weusi waliojazia mwili , mtu wa mwisho kutoka alikuwa ni Mzungu- Mjapani , yaani mtu aliechanganya rangi ya mjapani na Mzungu.
Kilichomfanya Dina kuanza kupandwa na hasira alijua mpango wote huu ulisukwa na Pancho.
Pancho alikuwa ni moja ya wasimamizi wa mtandao wao upande wa Congo na siku kadhaa nyuma Dina alipokea dili kupitia kwa Pancho kutoka kwa Wacanada ambao walitaka kuingiza siraha za kivita Congo kupitia Bandari ya Mtwara.
Dili hili liliungwa mkono na Mheshimiwa Mgweno lakini Dina aliona halikuwa na maslahi na kama angelikubali ni kama kujipiga risasi mguuni, ikizingatiwa siraha hizo zilipaswa kufikishwa kwa kundi lingine la waasi ndani ya Congo tofauti na lile ambalo wanashirikiana nalo kwa muda mrefu.
“Mzee Seif nini kimetokea , kwanini taarifa nilizopokea ni wewe kuhusika na kumuua Mzee Martini na mheshimiwa Jongwe?”Aliuliza Dina akimpotezea Pancho.
“Hawa ndio wahusika , wameiteka familia yangu na wanataka nikiri kuhusika kwa kushirikiana na wewe kumuua Jongwe au turejee mezani na kuanza mazungumzo ya kuingiza siraha Tanzania kwenda Congo”Aliongea Mzee Seif aliekuwa na hali ya hofu na kumfanya Pancho kutoa tabasamu.
“Pancho unajaribu kufanya nini , nani yupo nyuma yako?”
“Dina hakuna ambae yupo nyuma yangu?”Aliongea Pancho kwa kejeli.
“Kwa kumuua mgombea wa uraisi kupitia chama tawala, unasema hakuna ambae yupo nyuma yako?”Aliongea Dina kwa hasira na kumfanya Pancho kutoa tabasamu la kifedhuli.
“Nilitaka hili swala angalau ulichukulie kwa uzito wake, ushahidi wa wewe kuhusika katika shambulizi la kulipua bomu gari ya mgombea wa uraisi kupitia chama tawala upo , unaweza ukawa wa kutengeneza lakini jeshi la polisi lipo tayari kuuamini na kama likitoka uraiani , kitengo cha TISA kitakufanya mbuzi wa kafara, lakini huko kote ni kujisumbua kama upo tayari kuchagua chaguo zuri kati ya matatu alioongea Mzee Seif?”
Hamza muda huo alikuwa akiangalia mazingira yalivyo na watu wote waliokuwa hapo walikuwa na siraha za bunduki na haraka haraka kwa sheria ya Tanzania ilikua ngumu kwa watu hao kumiliki hizo siraha labda iwe kuna mtu ndani ya serikali ambae alikuwa akihusika.
Isitoshe safari yao kutoka kijichi mpaka kufka hapo , kama kweli jeshi la polisi lilikuwa sirasi kukamata watu hao waliomsababishia ajali mgombea wa kiti cha uraisi basi wangeshafika labda tu iwe kuna maagizo ambayo yamewafanya kuchelewa.
“Hizo siraha mnaotaka kuingiza Tanzania mnazitoa wapi?”Aliongea Hamza.
“Oh!, ahsante kwa kuuliza bwana mdogo , kidogo tu nimesahau kumtambulisha bosi wetu hapa , huyu ni Bosi Keita na ndio msingi wa haya maungumzo , kuhusu wapi siraha zinatoka ni juu yake”Aliongea Pancho kwa kujigamba.
“Pancho kama nilivyosema mtandao wetu haudili na maswala ya siraha bila ya utaratibu maalumu, kama unataka dili hili lipite lisimamie wewe mwenyewe na hela zako na sio za mtandao wa Chatu”Aliongea Dina na yule bwana mwenye asili ya kizungu na Kijapani alimpa ishara Pancho ya kuongea yeye.
“Miss Dina kama alivyoongea Pancho tunaweza kulimaliza hili swala kimya kimya na kusiwe na athari zozote kwa kila upande”Aliongea kwa Kingereza.
“Unamaanisha unaweza kuzima kesi ya kulipua gari ya mgombea wa Uraisi pamoja na Martini?”Aliuliza Lawrence.
“Itategemea na maamuzi ya Miss Dina?”
“Kwanini nahisi hata waliompendekeza Jongwe kupeperusha bendera ya Chama ni kama wanashangilia kifo chake?”Aliongea Hamza huku wakati huo Dina akiwa ametulia.
“Tunafanyaje?”Aliuliza Dina akimegemea Hamza , isitoshe ndie aliesema wasije na watu wengi.
“Wana siraha na hata kama tukishambuliana bila siraha hatuwezi kushinda bila kushitua raia , hawa watu wana mafunzo ya mapigano”Aliongea Hamza na kumfanya Dona kuwa na wasiwasi.
“Usiwaze hili naweza kulimaliza kwa amani na kisha utadili nao kujua nini kinaendelea kuhusu mgombea wa uraisi kulipuliwa”Aliongea Hamza na japo Dina alikuwa na wasiwasi aliamua kumwamini Hamza.
“Bwana Keita kwa ninavyojua huwezi kudili na siraha pasipo kuwakilisha shirika la giza unalotokea”Aliongea Hamza akitaka kujua Black Association ambayo Keita anatokea.
“Jungle Army Merchant ndio ninatokea”Aliongea bila ya kusita sita.
“Kumbe ni Jungle , hebu subiri kwanza nipige simu, nikimaliza utaamua cha kufanya”Aliongea.
“Umpigie nani?”
“Utajua nikimaliza’Aliongea Hamza.
“Mr Keita haina haja ya kupoteza muda na hawa watu , swala ni moja tu wachague chaguzi moja kati ya tatu tumalizane”Aliongea Pancho akionekana kukosa uvumilivu.
“Kimya! , sitaki unifundishe namna ya kufanya biashara”Aliongea Keira kwa kingereza na kumfanya Pancho kukaa kimya , isitoshe alikuwa akijua Jungle Army Merchant walikuwa wafanyabiashara wakubwa ndani ya Black Market kwa kuuza siraha za kila namna.
Muda huo Hamza alikuwa ashapiga simu tayari bila ya kuwa na wasiwasi kabisa.
*****
Magneto, Las Vegas- USA
Ni ndani ya jiji la Las Vegas , jiji ambalo kwa wacheza kamari hawakuhesabu muda , Usiku ni kama mchana na Mchana ni kama usiku tu ndani ya hili jiji.
Katika moja ya hoteli ya kifahri ya nyota tano ndani ya chumba cha hadhi ya raisi , alionekana mtu bonge mweusi mwenye kitambi akiwa amelala chali.
Alikuwa mrefu wa mita kama moja nukta tisa hivi , vidole vya mikono yake vilikuwa vimevishwa pete za madini ya almasi , Dhahabu na madini mengine ya thamani , shingoni alikuwa amevalia mikufu ya bei ghali.
Mtu yule bonge alijikuta akitandaza miguu yake vizuri huku akifumba fumba macho na kuyafumbua , katikati ya eneo la mapaja yake alionekana mwanamke mzungu mwenye nywele nyeupe(blonde) akiwa bize kumhudumia.
“Mr Mamen are you comfortable?”Aliuliza yule mwanamke kwa sauti tamu huku akiinua kichwa chake akimwangalia kwa macho malegevu , akimuuliza Big kama ni mwenye kuifurahia huduma.
Mwanaume yule bonge udenda ulikuwa ukitaka kumwagika kutoka kwenye midomo yake , alionekana alikuwa kwenye ulimwengu mwingine wa raha.
“Comfortable..!?, Deeper the better .”Aliongea akimaanisha azame chini zaidi ndio itakuwa vizuri.
“You’re so annoying , I’m realy tired ..”Aliongea yule mwanamke akimwambia anachukiza kwani amekwisha kuchoka.
Bonge yule mweusi kama msanii RickRoss alifungua droo ya meza pembeni na kitanda chake na kuchomoa maburungutu ya pesa za dola na kumtupia.
“Hakikisha najisikia vizuri mpaka kisogoni , nitakupa kiasi chochote cha pesa unachotaka”Aliongea Big na yule mwanamke uchomvu uliisha palepale na alijkuta akiongeza mashambulizi ya kuhakikisha Big anajisikia vizuri.
Dakika hio hio simu yake ilianza kuita , hata simu yake tu ilikuwa imetengenezwa kwa housing ya madini ghali sana na kuifanya ionekane kama kitu kisichokuwa cha kawaida kutokana na uthamani wake
“F*ck , kama ningejua ningeizima hii simu , nani ananipigia muda huu”Big alilaani huku akichukua ile simu na kuipokea maana namba ilikuwa mpya tena haikuwa ya taifa hilo
“Big naona kama kawaida yako sasa hivi unaringa , kwahio unaona sipaswi kukupigia hata kama ni swala linalohusu vita ya tatu ya dunia”Sauti ya kiume ilisikika katika simu ya Big.
Kitendo cha Mameni kusikia ile sauti mwili wake ulitetemeka na macho yake yalibadilika na kuwa mekundu na hata ule msisimko aliokuwa akisikia ulipotea.
Yule mwanamke aliekuwa bize kuhakikisha Big anafurahi alijikuta akipiga kelele mara baada ya kadudu kabig kupotea na kuwa kabamia.
“Boss!! , ni wewe kweli , naona hatimae umenipigia , nimekumisi sana”Aliongea Big huku sauti yake ikiwa imebadilika.
“Unafanya nini hapo , lazima utakuwa na m*laya kitandani , yaani ndio kwanza kunakucha wewe unahangaika na wanawake , kuna siku utafia kwenye kifua cha mwanamke”
“Hehe..Bosi wewe mwenyewe unanijua vizuri , isitoshe wewe ndio mtu pekee ulievunja rekodi yangu”Aliongea.
“F*ck you!”Alitukanwa.
“Bosi nasikia upo Tanzania , habari za siku nyingi , vipi naweza kuja huko?”
“Nina mambo mengi ya kufanya siku hizi tutaona kama unaweza kuja , nyie watu ni wasumbufu sana mkisikia nipo mahali mnataka kuja tu , sitaki usumbufu wenu nahitaji kutulia kwa sasa”
“Bosi kwa uwezo wako na ushawishi wako unaweza kuomba chumba mapumziko Ikulu na ukapatiwa na warembo kabisa , hayo sio mapumziko ila ni kujitia stress tu , mapumziko ni yale wafariji wanakuwa wanabadilika badilika kila siku kwenye kuusisimua mwili”
“Sterehe za kutumia hela hizo nishazichoka , hata nikikuambia ni namna gani nafurahia maisha ya sasa hivi hutonielewa Big”
“Kama ni hivyo bosi kwanini umenipigia simu , kuna dili jipya?”
“Hakuna dili lingine , nishastaafu hayo mambo”
“Sababu ni ipi sasa Bosi , au kuna sehemu nimekosea?”Aliuliza Big kwa upole.
“Kwenye biashara zako unamfahamu bwana anaefahamika kwa jina la Keita?”
“Ndio mwaka juzi niliingia dili na kundi moja linalofanya shughuli zao ndani ya Afrika kuiba madini Adimu na kuyauza kwenda kwenye moja ya kampuni ya maswala ya kiteknolojia nchini Ufaransa , linaongozwa na bwana Keita”Aliongea Big.
“Huyu bwana wako naona ana juhudi mno , muda huu nimeelekezewa mitutu ya bunduki ndio maana nimekupigia simu kuthibitisha , Big kwahio sasa hivi umeshaanza kuwa mkubwa kiasi cha kunisaliti kisa tu nnimetoka kwenye uringo?”
Big mara baada ya kusikia kauli hio kutoka kwa Hamza alijikuta mikono ikimtetemeka kiasi kwamba simu ilitaka kudondoka.
“Bosi , subiri kwanza , nitampigia simu sasa hivi , naomba kwanza nimfokee baada ya hapo unaweza kumuua”Aliongea Big na dakika ileile alikata simu na kuitafuta namba ya Keita.
“Mamen Babe! , unafanya nini sasa mbona imepotea!?”Yule kahaba wa kizungu aliongea lakini Mameni alimpotezea na mara baada ya kuipata namba ya Keita aliipiga palepale.
Mara baada ya Hamza kumaliza kuongea na simu hakuongea neno na alitulia akiangalia matokeo.
Ijapokuwa Keita hakujua Hamza alikuwa akiongea na nani kwenye simu lakini alihisi kuna kitu hakipo sawa.
Dakika ileile simu yake ilianza kuita na alisogea pembeni na kupogea lakini muda huo huo alianza kuonyesha ishara za kupaniki.
Upande wa pili ilikuwa ni sauti ya Big kutukana kimarekani kwa mara nyingi mfululizo kadri alivyoweza.
“Bosi nimefanya kosa gani?”
“Unataka kumuua nani sasa hivi?”
“Bosi umejuaje nataka kuua mtu?”
“Unaetaka kumuua ni bosi wangu”
“…”
Keita alijikuta akikosa neo , alishangaa mno kwa zaidi ya sekunde kumi , ni kama alikuwa akisharabu yale maneno.
“Ah!”
Alijikuta hofu ikimwingia na vigoti vya miguu yake vilianza kumlegea na alijikuta akigeuka na kumwangalia Hamza.
Upande wa Hamza alikuwa akimwangalia Keita tu kwa mbali na kwa jinsi alivyoonyesha kupaniki na woga alitamani kucheka.
“Mr Keita , Mr Keita , what happened?”Pancho aliuliza mara baada ya kuona mabadiliko.
Dina macho yake yalichanua alijua kabisa mabadiliko ya Keita ni kutokana na Hamza alipopiga simu na kwake aliona mwanaume Hamza alikuwa akimshangaza kila siku.
“Nini tatizo Mr Keita , mbona huongei?”Aliuliza Pancho kwa wasiwasi
“Hivi unajua mimi na vijana wangu tutakufa sasa hivi kutokana na ujinga wako na wale wanasiasa wapuuzi?”Aliongea kwa hasira.
“Unamaanisha nini Mr….”
Keita hakuchelewa alichomoa Desert Eagle kutoka kwenye kiuno chake na kumchapa risasi tatu Pancho palepale.
Mpaka Pancho anadondoka chini muonekano wake ulikuwa na shauku ya kutaka kujua kwanini Keita anamshambulia.
Keita mara baada ya kumalizana na Pancho alitoa maagizo kwa vijana wake kuwashambulia watu wa Pancho na walionekana kuwa shapu kweli kwani ndani ya sekunde wote walikuwa chini.
Baada ya Keita kuituliza hali alijikuta akimdondokea Hamza kwa magoti huku akiwa na wasiwasi mwingi akitia huruma.
“Prince Rich.. Bosi wangu ameniambia kila kitu , naomba unisamehe kwa ujinga wangu , sikubahatika kukutana na wewe ana kwa ana zaidi ya kusikia habari zako ndio maana nimekukosea…”
Kitendo kile kiliwashangaza mno Dina , Lawrence na wenzake , waliishia kujiuliza Hamza ni nani mpaka bwana yule kuwa na hofu namna ile kiasi cha kupiga magoti.
“Nipe bastora yako”Aliongea Hamza akiwa siriasi na kumfanya Keita kukakamaa mwili lakini alimpatiia.
‘Tafadhari naomba uwaache vijana wangu waondoke , walikuwa wakifuata maelekezo tu kutoka kwangu na wanazofamilia zinawategemea”Aliongea Keita lakini Hamza hakumjali na muda ule aliinua ile bastora na kujielekezea kwake kana kwamba anataka kujipiga risasi.
Tukio lile lilimshangaza kila mtu wakishindwa kuelewa Hamza anataka kufanya nini
“Hamza unataka kufanya nini , usipaniki..”Aliongea Dina lakini kabla hata hajamaliza Hamza alikuwa ashaachia risasi.
Bam!
Mlipuko ule wa bunduki ulimuogopesha mpaka Keita na wote walimwaangalia Hamza kwa mshangao na walishangaa zaidi baada ya kuona hakuna kilichotokea.
Risasi ambayo ilitoka katika ile bunduki ilikuwa katika vidole vya Hamza , haikueleweka amefanyaje lakini ilionekana aliikamata kabla ya kumfikia, tukio lile lilimfanya Keita kushindwa kuendelea kupiga magoti na kukaa chini kwa kunyoosha miguu huku mapigo yake ya moyo yakidunda kwa kasi.
“Kabla sijafanya chochote nataka muelezee kila kilichotokea… sababu ya kwamba umepiga magoti sio kwasabau ya bosi wako bali ni kwasababu yangu hivyo nataka majibu”Aliongea Hamza.
“Serafii.!!, nipo tayari kuongea”Aliongea Keita huku akipiga kichwa chini kiasi cha kutoka damu kwenye paji la uso.
“Anza kuelezea , kwanini kifo cha Mgombea wa uraisi na nani kahusika”Aliongea Hamza.
“Hatujahusika katika kumuua mtu , tupo hapa nchini kwa ajili ya mazungumzo ya biashara ya kupitisha Siraha Kwenda Congo kupitia bandari ya Mtwara , kitu pekee ambacho nafahamu kuhusu muhusika tulipewa kazi ya kumtorosha hapa nchini kupitia boti yetu”Aliongea na kauli ile ilimfanya Dina kusikiliza kwa umakini.
“Imekuwaje mkajiingiza , sitaki kuuliza maswali mengi elezea kila kitu ninachotaka kujua?”
“Mara ya mwisho nilivyokuja hapa nchini niliweza kukutana na mstaafu Mgweno kwa ajili ya kuingia dili la kupitisha siraha , lakini kutokana na usafirishaji wote wa Kimagendo kuwa chini ya Chatu hakutoa maamuzi badala yake aliwasiliana na Miss Dina ambae mara baada ya kuelekezwa kuhusu dili hili alikataa, Mstaafu baada ya ombi hili kukataliwa alituambia hana namna ya kutusaidia kwani njia pekee ya kupitisha siraha hizo ni moja tu ambayo ni Mtwara kutokana na bandari zote kuwa chini ya mwekezaji”
“Nini kiliendelea”
“Wakati tukifikiria namna ya kutafuta njia nyingine ya kukamilisha dili hili nilipokea simu kutoka kwa mtu ambae alijitambulisha ni msaidizi wa raisi”Aliongea.
“Unamaaniisha Mheshimiwa Eliasi Mbilu?”
“Ndio na alisema anataka kuonana na sisi kwa ajili ya mazungumzo ya namna ya kukamilisha kile tulichokuwa tukihitaji , kutokana na kuwa na haraka ya kufanikisha hili dili nilikubali na kupitia msaidizi wake alinipa maelekezo niwaache vijana na boti yetu nchini Tanzania kwa muda na nikutane nae jijini Kual Lampur nchini Malaysia ndani ya tarehe alionitajia wakati akiwa ziarani”
“Tokea tuzungumze kuhusu hili dili imeshapita mwezi miwili , inamaana huu mpango ulikuwa wa muda mrefu?”
“Inawezekana Miss Dina , kabla ya siku moja ya tarehe kufika , niliweza kufika Malaysia na nilikutana na mheshimiwa kwa siri sana kupitia msaidizi wake na nilitambulishwa kama mwekezaji”Aliongea Keitani kwa kutetemeka.
“Alitaka kuongea nini kwa siri namna hio?”Aliuliza Dina , ijapokuwa Keitani alijua alikuwa akitoa siri kubwa lakini hakuwa na jinsi.
“Aliniambia siku ya leo saa nne kamili za usiku mgombea wa kiti cha uraisi kupitia chama chake atafariki kwa ajali ya gari na atakaesababisha ajali hio napaswa kumtorosha nje ya nchi na kama ikishindikana nimuue kabla ya kukamatwa na polisi, kisha nitumie ushahidi feki wa tukio hilo kuhakikisha nakamilisha dili la kupitisha siraha”
“Ushahidi feki ni kutusingizia sisi ndio wahusika, si ndio?”
‘Ndio”
“Ameenda mbali mpaka kutengeneza ushahidi feki , yeye anafaidika nini katika hilo?”Aliuliza Lawrence.
“Kila kitu kipo wazi , naamini Jongwe sio chaguo lake na pili alitaka kujitengenezea njia za kupata maslahi hata akiwa amestaafu kupitia hili dili”Aliongea Hamza.
“Ndio , alitaka asilimia ishirini ya faida itakayopatikana na wakati huo huo Mgombea wa uraisi akiwa ni chaguo lake baada ya chaguo la Mgweno kufariki”Aliongea keita na kumfanya Dina sura kujikunja
“Mgweno na Eliasi wanataka kupinduana , madaraka huwa ni matamu sana”Aliongea Dina lakini upande wa Hamza hakujali nani anampindua nani.
“Vipi kuhusu muuaji ni nani?”
“Kuhusu mfungwa hatuna taarifa nyingi kuhusu yeye , tulipatiwa picha pekee na tuliambiwa ni mfungwa wa kidiplomasia aliefungwa kwa muda mrefu kwa siri”
“Yuko wapi kwasasa?”Aliuliza Hamza.
“Ametoweka mara baada ya tukio, tunaamini alikuwa na mpango wake binafsi wa kujitorosha baada ya kukamilisha misheni”Aliongea na kumfanya Hamza kuvuta pumzi.
“Picha yake ipo wapi”Aliuliza Hamza na Keita alimpa ishara bwana moja wa kizungu na alimsogezea Hamza simu na ilionekana picha ya mfungwa kwenye kioo cha simu na mara baada ya kuiangalia alijikuta macho yake yakichanua.
“What the f*ck!!”
Hamza alijikuta akitoa tusi na kumfanya Dina kusogea kuangalia picha hio ili kujua kwanini kashangaa.
ITAENDELEA.
Watsapp me kwa mwendelezo wa haraka haraka namba 0687151346
Amechanganya maana kairudiamhm!! huyu jamaa kwel pasua kichwa...kwahiyo siku ndo imeisha hivyo au ulikuja kututemberea2???
😁😁😁umeandika kwa uchungu sana mkuusinganojr wewe ni mtu na heshima zako kama umafanya bahati mbaya kurudia unge tuomba radhi, kama ni kusudi basi sisi tuna shukuru.