Simulizi ya kijasusi: Shetani Rudisha akili zetu na mke wangu

Simulizi ya kijasusi: Shetani Rudisha akili zetu na mke wangu

Mkuu singano shusha mzigo leo kwa jina la mama samia rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania,,,,,
 
SHETANI RUDISHA AKILI ZETU.
MTUNZI:SINGANOJR

SEHEMU YA 63.
Kitendo cha Hamza kuonyesha kuishangaa ile picha kama vile mtu huyo anamfahamu ilimpa na Dina shauku ya kutaka kujua ni nani, baada ya kuangalia na kuona ni mwanaume wa kizungu aliekuwa amevalia mavazi ya kifungwa huku akiwa na kipara alimwangalia Hamza.
“Unamjua huyu ni nani?”Aliuliza Dina.
“Naweza kusema ndio namfahamu , lakini hata nikuelezee ni nani huwezi mfahamu, kinachonishangaza sio kwamba huyu ni nani bali ni kuitwa mfungwa wa muda mrefu”Aliongea Hamza.
“Unamaanisha nini?”Aliuliza Dina akiwa hajamuelewa Hamza kabisa.
“Unadhani kuwa mfungwa wa muda mrefu ni kama miaka mingapi hivi?”
“Inaweza kuwa miaka ishirini na zaidi”Aliongea Dina na kauli ile ilimfanya Hamza kutabasamu , lakini tabasamu lake lilikuwa na maana flani hivi.
“Kama hii sura ni ya mtu ninaemfahamu mimi basi huyu hajawahi kuwa mfungwa na kama ni kweli alikuwa mfungwa hapa Tanzania basi aliamua kulifanya Gereza makazi yake ya muda mrefu”Aliongea na kauli ile ilimfanya Dina kushangaa na kujiuliza kuna mfungwa wa aina hio , yaani wa kuweza kukaa ndani ya gereza kwa hiari yake.
“Kwa unavyoongea , kama kweli kahusika kumuua mgombea wa uraisi , unadhani jeshi la polisi litaweza kumkamata?”Aliuliza Dina.
“Kwa asilimia tisini nina uhakika hawatoweza kukamata hata kivuli chake”Aliongea Hamza na kumfanya Dina kumwangalia Hamza kwa shauku , alitamani kumjua huyo mtu ni nani lakini kwa muda huo alishindwa kuuliza hata kwa Lawrence hivyo hivyo.
Keita yeye hakuwa akijua kiswahili, hivyo hakuweza kusikia wanachozungumza ni kitu gani.
Hamza alionyesha kuridhika na ile picha na kisha alimrudishia yule bwana aliemkabidhi simu.
******
Upande wa Las Vegas Big alionekana kuwa na wasiwasi mno , zilikuwa zimepita dakika kumi na tano na kadri dakika zilivyokuwa zikiongezeka ndio jasho lilivyozidi kumtoka.
Mara baada ya simu yake kunguruma ikiashiria kuna ujumbe uliongia haraka haraka aliangalia na kukuta ni wa Keita.
“Bosi tumesamehewa…”Ndio ujumbe ulivyosomeka kwa liugha ya kingereza na kumfanya Big kupumua kwa nguvu ikionyesha amepata ahueni.
Ijapokuwa Keita alijiingiza mwenyewe katika anga za bosi wake lakini alikuwa akiomba asiuliwe , katika watu ambao amefanya nao kazi na waliomwingizia pesa ndefu na wenye ufanisi wa hali ya juu ni Keita, hivyo kama angekufa kwake ingekuwa hasara.
“Mr Mamen , huyo mwanaume kutoka Tanzania ni muhimu sana kiasi hicho , hii hoteli pamoja na Casino vyote ni vyako , kwanini unamuogopa sana?”Aliongea yule mwanamke wa kizungu , alikuwa ameshasikia mtu aliekuwa akiongea nae yupo Tanzania.
“Acha kuongea ujinga , huna unachokielewa”Aliongea Bonge kwa kufoka huku akimsukumia pembeni maana mudi ilikuwa ishapotea tayari.
“Hebu kwanza ondoka , sitaki huduma yako tena”Aliongea Big na mara baada ya yule mwanamke kusikia kauli hio kama nyoka alijikumbatisha katika mwili wa Big.
“Usifanye hivyo mpenzi , bado nina mbinu nyingi ambazo sijakuonyesha bado”
“Sitaki tena mbinu zako”Aliongea Big huku akinyoosha mkono wake kwenye kimeza na kuchukua sigara moja katika pakti na kuiwasha kisha kuanza kuvuta.
Yule kahaba wa kizungu aliona ni kama mpango wake wa kupata maokoto umevurugika na lawama zote alimpelekea Mtanzania aliekuwa akiongea na Big kwenye simu , isitoshe mpaka kupata nafasi ya kumhudumia Big alikuwa amefanya juhudi kubwa za kujilengesha.
“Haya yote ni kutokana na huyu Mtanzania , yeye ndio kaniharibia na kukufanya kukosa mudi ya kuendelea na mimi , Mr Mameni wewe ni mtu mzuri sana kwake lakini kwanini inaonekana hakujali kama rafiki , kama ni kweli anakuheshimu asingekutafuta muda mbovu kama huu”Aliongea akilalama
Kitendo cha kusikia kauli ile kutoka kwa huyo mwanamke , hasira zilimvaa Big palepale na alimkaba shingoni.
“Arghhhhhh..!”
Kahaba yule wa kizungu alijikuta akihangaika kujinasua kutoka kwa Mamen lakini hakutaka kumwachia.
“Wewe mwanamke mpumbavu sana , wewe ni nani mpaka kumsema vibaya bosi wangu”
“Mr Mameni nisamehe , sikujua unamheshimu kiasi hicho , naomba usiniue”Aliongea kwa kuomba lakini Mameni hakuwa na mpango wa kumwachia kabisa na alizidi kumkaba.
“Kumheshimu? , huyo mtu kwangu ndio imani”Aliongea akimaanisha Hamza kwake ndio imani yake na mara baada ya kauli ile alikaza mkono na kuizungusha shingo ya yule mwanamke na palepale alilegea.
Big hakuwa na hatia hata kidogo , baada ya kuona amekwisha kumuua yule mwanamke aliupiga mwili teke na kudondokea chini kwenye Zuria la kiajemi na kisha bila ya nguo alitoka kitandani na kwenda kusimama katika dirisha huku akivuta moshi mwingi wa sigara.
Katika macho yake alionekana kama mtu ambae ameingia katika kumbukumbu ya maisha yaliopita.

******
Hamza alimsamehe Keita na kumwambia aondoke Tanzania na watu wake mara moja na aachane na maswala ya madili ya siraha katika ardhi hii.
Keita alishukuru kusamehewa na kwa haraka sana aliongoza watu wake na kutoweka katika eneo hilo huku wakifuta ushahidi wote wa wao kuwepo nchini.
Kuhusu maswala yaliobakia alimwachia Dina adili nayo , kutokana yamekaa sana kisiasa na hakutaka kujiingiza huko.
Dina alitoa maelekezo ya Mzee Seif kupelekwa Safehouse kwa muda mpaka mambo yatulie na vijana wake walifanya kazi hio.
“Unapanga kufanya nini?”Aliuliza Hamza mara baada ya kungia kwenye gari , alitaka kujua ni hatua gani ambayo Dina atachukua kuhusu swala la kifo cha mgombea wa uraisi.
“Mpaka sasa nimeshindwa kuamini kama Eliasi ameenda mbali namna hii mpaka kumuua mgombea wa uraisi tena wa chama chake huku yeye akiwa mwenyekiti wa Chama, kuna kitu kinaniambia hili hajalitekeleza yeye peke yake , pengine kuna nguvu ilionyuma yake”
“Unamaanisha nguvu ambayo inataka kumpindua Mgweno?”Aliuliza Hamza.
“Ndio , Eliasi ninaemjua mimi sio jasiri kiasi hichi , ijapokuwa Mgweno amekuwa akiitawala hii nchi nyuma ya pazia lakini haimaanishi ana nguvu kila mahali, katika uongozi wake alikuwa na maadui zake pia na ndio namna ambavyo hata mtandao wetu wa Chatu uliweza kuendelea kuwepo licha ya kuupiga vita kwa kipindi kirefu akitaka kuumiliki”Aliongea Dina.
“Kwa ninavyoona kwasasa huu ni mpango ambao haujaisha bado , muuaji kakimbia na sidhani kama wanaweza kumpata tena , pili upande wa Keita mpango umevurugika kwa asilimia kadhaa , kama unavyosema ni sahihi basi nina uhakika pengine Keita alikuwa Plan B ya mpango mzima”Aliongea Hamza na kumfanya Dina kidogo kushangaa.
“Unataka kumaanisha nini?”
“Wewe hebu chukulia , kazi kubwa ya Keita ilikuwa nini katika huu mpango , ni kumtorosha muuaji lakini Keita amemkosa muuaji hii maana yake walikuwa wakiujua uwezo wa muuaji kujitorosha yeye mwenyewe”
“Vipi kitendo cha kutaka kunisingizia mimi kama muhusika?”Aliuliza Dina.
“Ni kukujulisha kinachoendelea kabla ya kukisikia kwenye taarifa ya habari , yule Pancho alikuwa chambo tu”Aliongea Hamza na kumfanya Dina kuanza kufikiri.
“Maana yake ni kwamba hata kama ningeenda mwenyewe ningeweza kuujua ukweli kutoka kwa Keita?”
“Nina uhakika huo licha ya kwamba ingekuwa ngumu, lakini kama ni kweli basi nguvu iliopo nyuma ya Eliasi inamtafutia udhaifu pia”Aliongea Hamza na upande wa Dina mara baada ya kuanza kufikiria kimantiki, ni kama sasa anaanza kuelewa pointi ambayo Hamza analenga.
“Babu aliweza kuulinda mtandao wa Chatu kwa kuushikilia udhaifu wa mheshimiwa Mgweno lakini hili lililotokea leo pia nimepata ushahidi wa Eliasi kupanga njama na kumuua mgombea wa kiti cha uraisi , hii maana yake Eliasi na Mgweno wote wapo kiganjani kwangu, kuhusu nani atarithi nafasi ya Jongwe lazima atakuwa upande wa Eliasi na kuna uwezekano pia amehusika katika huu mpango.Kama ni hivyo basi napata picha nani yupo nyuma ya Eliasi” Aliongea Dina kana kwamba anajaribu kuunganisha matukio na kumfanya Hamza kutabasamu.
“Naamini atakuwa yule raisi wa Rwanda”Aliongea Hamza huku akimshika Dina kiuno.
“Wewe umajuaje?”
“Babe si ushawahi kuniambia babu yako alifanikisha kumfunga mikono Mgweno kutokana na kumtengenezea udhaifu wa kashfa ya kuuza rasilimali za nchi nchini China kwa ajili ya kumuokoa mtoto wake na mpango ulisukwa na rafiki yake mkubwa raisi wa Rwanda”Aliongea Hamza na kumfanya Dina kuitikia kwa kichwa huku akimwangalia Hamza kwa macho malegevu.
“Huyu mzee anataka kuitawala Afrika mashariki nzima , naona anajaribu kumuweka raisi anaemtaka madarakani huku wakati mmoja akiizima nguvu ya Mgweno ambae ni adui yake mkubwa”Aliongea Dina.
“Mtu wa nje anaweza kuona ni kiongozi mwenye akili sana , lakini upande mwingine wa shilingi sababu ya kuwa na mipango mingi ni kutawala kwa muda mrefu na kuamini nchi ni yake na anajaribu kila namna kuiendeleza licha ya kuwa na rasilimali chache”Aliongea Hamza huku akitabasamu na Dina alitingisha kichwa kukubaliana nae.
“Mbona huniulizi swali lolote licha ya sura yako kuoneysha ina maswali mengi?”Aliongea Hamza mara baada ya kuona Dina alikuwa akimwangalia sana.
“Ndio nina maswali mengi kwa kilichotokea leo lakini kwasasa naona ngoja lipite”
“Ukiuliza nitakuambia kila kitu”Aliongea Hamza.
Ukweli aliona Dina sio Regina anaweza kumweleza kila kitu na wala asipate mabadiliko zaidi ya ushangaa tu.
“Kwasasa sitaki kujua vitu vingi , nahisi bado sina vigezo , siku za baadae nikijihisi kustahili kukujua nitakuuliza, sitaki kujua sasa hivi inaweza kunifanya niwe na mawazo kwa kuona tuna gepu kubwa kati yetu”Aliongea Dina na kumfanya Hamza kutabasamu , hakudhani Dina angekuwa na mawazo ya namna hio.
Mpango wa Dina ilikuwa ni kujiimarisha zaidi uwezo wake binafsi , alikuwa akijua kuna mbinu nyingi za kuwa na uwezo mkubwa ikiwemo mbinu za kujifunza kanuni za mbingu na ardhi , kuamsha nguvu ya ndani, uchawi na mengineyo.
Hamza alikwua ni mtu ambae anaamini ana mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi na alitaka ajifunze kutoka kwake na kufikia hatua ambayo atajiona yupo tayari kumjua Hamza.
Kutokana na muda ulikuwa umeenda Hamza hakupanga kurudi nyumbani , ukweli ni kwamba angetaka kurudi ingekuwa rahisi tu maana alikuwa karibu na mji wa kisasa wa Egret lakini aliamua kurudi Kijichi na mrembo Dina.
Mara baada ya kufika nyumbani hakukuwa na chakufanya zaidi ya kwenda kulala , kulikuwa na vyumba vingi vya wageni ndani ya jumba la mrembo huyo lakini Dina alilazimisha walale pamoja.
Hamza licha ya kukubali alijitahidi asimfanye chochote mwanamke huyo, baada ya Dina kuuliza maswali kibao kuhusu namna ya kuwa bora katika eneo la mapigano na kujua nguvu iliojificha katika mwili wake hatimae alipotelea usingizini , lakini upande wa Hamza kama mwanaume rijali ilikuwa ngumu kwake kulala , alijikuta akikaa macho mpaka kunakucha.
*****
Wakati ikiwa ni siku nzuri kwa watu wengine upande mwingine haikuwa siku nzuri kabisa kwa mheshimiwa mstaafu Mgweno.
Taarifa ya kifo cha mheshimiwa Jongwe aliweza kuzisikia usiku wa manane saa saba na tokea apate taarifa hizo hakuweza kupata usingizi kabisa , kwanza anaanza vipi kupata huo usingizi , kitendo cha kuuwawa na bomu kwa Jongwe tena akiwa ndani ya gari ilimaanisha kuna mtu anataka kumpindua ki nguvu ndani ya Tanzania , jambo ambalo hakuwa tayari kuona likitimia, lakini hata hivyo kama ilikuwa kweli aliona wanaotaka kumpindua walikuwa wamepiga hatua.
Usiku mzima kwa kuambizana na msaidizi wake Jonathani Machete walipanga kila aina ya mpango wa kurudisha hali hio katika mstari wake. Hata mtoto wake ambae alikuwa kwenye siasa akifuata nyayo zake alimpigia simu kumweleza kile kinachoendelea.
“Baba tunafanyaje juu ya hili swala?”Kijana huyo aliuliza kwa wasiwasi mkubwa , nafasi yake ya Uwaziri mkuu alikuwa akiona ikienda na maji.
Kitu ambacho Mgweno alikosea ni kukubaliana na Eliasi Mbilu kwamba kutokana na yeye kuweka mtu ambae ni chaguo lake kuwania kiti cha uraisi basi Mbilu yeye ataweka makamu wa raisi ambae ni chaguo lake , sasa wakati huo alipokaa chini na kufikiria aliona kabisa alijipiga risasi mguuni , ilionekana Mbilu tokea muda mrefu alikuwa na mipango ya kumuweka raisi anaemtaka madarakani kwa namna yoyote ile.
“Bakari wahi nyumbani asubuhi , kwasasa sina cha kukuambia”Aliongea Mheshimiwa.
“Sawa baba, nitapanda ndege binafsi kufika asubuhi na mapema”Aliongea Bakari Mgweno , alikuwa nyumbani kwao mkoani ambako ndio jimbo analogombea lilipo , kama angetaka kuwa Waziri Mlkuu ilimpasa kushinda kwanza ubunge.
Mheshimiwa usiku huo mara baada ya kukata simu alimgeukia Jona Machete ambae alikuwa bize.
“Vipi Machete umefanikiwa kuwasiliana nao wote”
“Ndio mheshimiwa nimetoa taarifa na wote asubuhi watakuwepo kwenye kikao”Aliongea Machete na kumfanya Mheshimiwa kukaa kwenye sofa huku akionekana kuwaza , bado hakuonekana kuridhika licha ya hatua ya kwanza kuichukua.
“Kabla ya asubuhi kuingia wasiliana na meneja wa Benki wa Sychelles napaswa kujiandaa kwa lolote”Aliongea Mheshimiwa.
“Sawa Mheshimiwa”
Mgweno kuna kila hisia mbaya ambayo ilikuwa ikimtawala, alijua fika Eliasi alikuwa akihusika katika hili lakini ushahidi wa moja kwa moja hakuwa nao.
“Mheshimiwa, Bi Zalha anasema ameshindwa kuunganisha mawasiliano na mheshimiwa Eliasi”Aliongea Jona akipokea simu kutoka kwa Zalha katibu wake ndani ya ofisi ya mheshimiwa mstaafu Oysterbay.
“Ametoa sababu ,inawezekana vipi raisi wa nchi kutopatikana hewani”
“Wanasema mheshimiwa kapata dharula ya kiafya, yupo chumba cha uangalizi katika hospitali ya Rufaa ya Gleneagles nchini Malaysia”Aliongea Jona na kumfanya Mgweno kutoa tabasamu la kifedhuli.
“Eliasi ana maigizo sana , ila hajui kwamba mimi ni mtoto wa mjini na ndio nilimwingiza Ikulu”Aliongea huku aking’ata meno kwa hasira na Jona aliishia kukaa kimya.
“Wasiliana na IGP nahitaji taarifa kutoka kwake sasa hivi juu ya mshukiwa wa mauaji”Aliongea na Jona dakika ileile alifanya mawasiliano na mara baada ya simu kupokeleiwa alifowadi kwenda kwa simu ya mheshimiwa
“IGP yupo hewani mheshimiwa”Aliongea na Mgweno alitoa simu yake na kupokea haraka haraka na kuweka sikioni.
“Mheshimiwa nadhani tumewasiliana dakika ishirini zilizopita”Sauti upande wapili iliongea.
“Sanga tumekubaliana kila baada ya dakika kumi unanipa ripoti , dakika ishirini zimepita naona kimya”Aliongea.
“Mheshimiwa hakuna ripoti ya kukupatia mpaka sasa , vijana wapo eneo la tukio , maiti ya mheshimiwa Jongwe na Mzee Martini pamoja na dereva zimefikishwa hospitalini kwa ajili ya kuhifadhiwa”
“Nataka ripoti Afande , kwanini Jongwe alikuwa kwenye gari la Martini tena usiku akiwa hana ulinzi wa kutosha?”
“Msaidizi wake namba mbili hakuwa na taarifa ya mheshimiwa kutoka , kuhusu msaidizi wake namba moja mpaka sasa hatujapata taarifa zake, hakuwepo kwenye ajali ya gari lakini pia nyumbani kwake hayupo”Aliongea IGP akiwa mpole lakini upande wa Mgweno aliishia kung’ata meno yake kwa hasira.
Katika taarifa ya tukio hili ilisemekana Mheshimiwa Jongwe alikuwa nyumbani kwa mzee Martini na wakati wa kuondoka alitoka na Martini na ndipo gari yao ilipolipuka mara baada ya kusafiiri kwa umbali wa kilomita nne kutoka nyumbani kwa Martini, swali lilikuwa moja , licha ya kwamba inafahamika Martini na Jongwe ni marafiki lakini ilikuwaje Jongwe akatoka nyumbani kwake bila ya wasaidizi wake kujua na akaenda kwa Mzee Martini.
Mheshimiwa alijiuliza maswali mengi lakini aliamua kufuata ule msemo wa ‘The dead have no tales to tell’ yaani mfu hana stori tena ya kusimulia.
Sasa akiwa ameshapanga mikakati ya kuchukua , hatimae asubuhi ikaingia akiwa hajalala kabisa na muda huo alikuwa akisubiria viongozi waliokuwa upande wake ndani ya chama kufika nyumbani kwake kwa ajili ya kikao cha siri na cha dharula kabla ya kifo cha Jongwe kutangazwa,alikuwa amezuia kifo hicho kisitangazwe kabla ya muafaka wa kuamua nani aingie Ikulu.
Saa mbili kamili ilikuwa ndio muda wa kikao lakini ajabu mpaka inafika saa mbili na nusu viongozi waliofika kwa ajili ya kikao walikuwa saba tu tena watatu kati yao wakiwa sio wale wenye vyeo vikubwa kwenye Chama.
“Jona mbona hawajafika mpaka muda huu , una uhakika ulifanya mawasiliano nao?”
“Ndio mheshimiwa na niliwapa muda sahihi wa kikao ni saa mbili kamili”Aliongea Jona na kumfanya mheshimiwa kuanza kuzunguka chumba kama vile amekuwa kichaa.
“Kuna jambo halipo sawa, hebu ongea na vijana wafuatilie sasa hivi unipe majibu”
“Mheshimiwa pengine wamechelewa tu , kwanini tusiwape muda angalau nusu saa?”
“Jona mimi sio mjinga kukuambia ongea na vijana wafuatilie , umeanza lini kwenda kinyume na ninachoagiza?”Alifoka mstaafu.
“Nitawasiliana na vijana mara moja mheshimiwa”Aliongea Jona na kutoka katika sebuleni na muda huo alipishana na mke wa Mstaafu akingia akiwa amebeba Trey.
“Mgweno punguza wasiwasi , hebu kunywa chochote kwanza ndio mengine yafuate”
“Mama Bakari unadhani kwa kinachoendelea nina muda wa kuweka kitu mdomoni?”Aliongea akiwa kakereka na kumfanya Mama Rahma kuweka ile Tray kwenye meza na kuanza kuandaa.
“Mume wangu hivi sio namna nilivyokuzoea, tumekuwa pamoja kwa muda mrefu na tumepitia makubwa kuliko hili na kipindi chote hicho hukuwahi kupoteza utulivu wako , wewe mwenyewe unamwambia Bakari kila siku hatua ya kwanza ya kutatua tatizo ni kujipa utulivu lakini naona unaenda kinyume na maneno yako”Aliongea na muda ule ni kama amekumbushwa kuhusu Bakari.
“Kuhusu Bakari mpaka sasa hivi hajafika tu?”Aliuliza
“Baba nipo hapa , hebu kwanza angalia taarifa ya habari”Sauti ya mtu kuingia ndani ya sebule hio mkuku mkuku ilisikika.
“Bakari kuna nini?”Aliongea mama yake lakini Bakari alikuwa mwepesi mno kuikimbilia rimoti ya TV na kuweka taarifa ya habari.
Kitendo cha Mstaafu Mgweno kuona ile habari alijikuta vigoti vya miguu vikilegea , ilikuwa ni habari ya kifo cha Jongwe mgombea wa Chama, licha ya kwamba Mgweno hakuruhusu taarifa hizo kutolewa kilichomlegeza ni sababu ya kifo cha Jongwe.
Kulingana na uchunguzi wa jeshi la polisi wanasema ni kweli mheshimiwa Jongwe amefariki na wamethibitisha mhusika mkuu ni Yohana Kamote msaidizi namba mmoja wa mheshimiwa Jongwe, polisi wanasema wamemkuta Kamote hotelini akiwa amejinyonga na kuacha wosia , akisema kwamba mheshimiwa Jongwe alimuiba mpenzi wake Janeth yaani mke wa Mheshimiwa Jongwe , Kamote anadai alikuwa kwenye mapenzi na Janeth kabla ya kuolewa na Jongwe na mapenzi yao yaliendelea hata wakati Janeth akiwa ameolewa tayari na wamezaa mtoto mmoja ambae anafahamika ni wa Jongwe , Kamote anasema Janeth alianza kubadiika baada ya mume wake kupewa dhamana ya kupeperusha bendera ya Chama na kutokana na wivu ameamua kumuua Jongwe na kujiua yeye mwenyewe kumkomoa Janeth, Polisi wanasema Janeth ameshikiliwa na jeshi la polisi kwa ajili ya mahojiano kuthibitisha kama kuna ukweli juu ya maneno ya Marehemu Kamote.
Mstaafu Mgweno alijikuta akinyong’onyea , upande wa Mama Rahma pia hata ile mudi ya kumlazimisha mume wake kunywa chai haikuwepo kabisa.
“Jamani mama Lebroni nili…!!”
Mke wa Mstaafu alijikuta akiropoka na kumfanya Bakari na mume wake kumwangalia kwa macho yaliojaa maswali.
“Mama unajua nini?”Aliuliza Bakari na Mama Rahma alianza kumwangalia mume wake kwa wasiwasi.
“Mama Bakari unajua nini , mbona huongei unaniangalia , usiniambie kinachosemwa na Polisi ni cha kweli?”
“Mume wangu naomba unisamehe sikukuambia kuhusu hili maana sikuwahi kuona ni muhimu , ni kweli nimejua muda mrefu Janeth alikuwa akitembea na Marehemu …”Alijikuta akishindwa kuendelea kuongea na kuanza kulia.
Mgweno alitamani kumvamia mke wake kumdunda lakini Bakari alionekana kuwa makini na baba yake kumsogelea mama yake , sio kwamba alikuwa akimtetea mama yake , lakini baba yake alikuwa na tabia ya kumpiga mama yake na hakuwa akipenda.
Mgweno hakutaka kusikiliza neno lingine na alitoka ndani ya sebule hio na kuelekea moja kwa moja kwenye ukumbi wa mikutano lakini mara baada ya kuona hakuna ambae ameongezeka alijikuta hofu ikimwingia.
“Mheshimiwa kuna ujumbe wako”Sauti ya Jonna ilisikika na kumfanya mstaafu na wale waliokuwa ndani ya ukumbi kumwangalia Jona kwa shauku.
“Taarifa imefika ofisini kwako asubuhi hii , unahitajika kwenye kikao cha dharula cha Halmashauri kuu ya Chama , saa tatu kamili ndio kinaanza ukumbi wa makao makuu”Aliongea Jonna.
“Kikao saa tatu kamili taarifa naeletewa saa mbili na nusu , Jona nini kinaendelea?”
“Mheshimiwa hata mimi nimeshangaa ila ni Zalha ndio kafikisha hii taarifa”Aliongea Jonna na mheshimiwa alimwangalia msaidizi wake kwa udadisi na hakuongea neno alihisi harufu kubwa ya usaliti kwa vijana wake aliowaamini.
“Ahirisha hiki kikao , tunaelekea makao makuu”Aliongea Mgweno huku akitoka ndani ya eneo hilo kwa pupa.
Kuna jambo alikuwa akiliwaza katika akili yake lakini hakutaka kulipa kipaumbele kwa wakati huo , alitaka kuwahi kwanza maana kama akichelewa na maamuzi yakifanyika hata kama ana ushawishi mkubwa hatokuwa na uwezo wa kupinga maamuzi ya watu wengi.
*****
Hamza asubuhi na mapema alikuwa ashaondoka nyumbani kwa Dina.
Siku hio mpango wake ni kwenda kazini na kisha akutane na Eliza amweleze kuhusu ndoa feki aliofunga na Regina.
Hamza hakutaka kabisa kumkosa Eliza lakini aliona sio vizuri pia kumdanganya.
Baada ya kufika ndani ya kampuni alikuwa amewahi sana na hata Eliza hakuwa amefika bado , hivyo hakuwa na chaguzi zaidi ya kwenda ofisini kwake na kuangalia kazi ambazo anapaswa kufanya.
Na mara baada ya kufika tu Linda alionekana kumtafuta na alimwangalia Hamza kwa ukauzu mkubwa.
“Umekuwaje wewe , unasiku ngapi hujaripoti kazini na kwanini unachelewa , yaani bosi kafika wewe ndio unaingia kazini?”Aliuliza Linda kana kwamba yeye ndio bosi.
Hamza alitaka kumwambia mwanamke huyo yeye ni nani wa kumpandishia ilihali amemuoa bosi wake ila alijizuia.
“Nilikuwa na maswala binafsi ndio maana?”
“Hii ni tabia gani unayojaribu kuonyesha, maswala binafsi ni ya kwako na hayapaswi kuingiliana na maswala yako ya kazi , usijione kwasababu unajua watu maarufu ndio unaweza kufanya chochote kile unachotaka”Hamza alifokewa na alijifanyisha mzembe kama kawaida na kutingisha kichwa lakini upande wa Linda ni kama hajaridhika aliishia kuchukia mara baada ya kuona hakuna dalili ya woga kabisa kutoka kwa Hamza.
Alikuwa na kila haki ya kukasirika, wote na Hamza walikuwa nafasi sawa lakini yeye muda wote alikuwa bize kuhakikisha ratiba za bosi wake zinaenda sawa , sasa Hamza ambae wapo nafasi sawa anafanya anachotaka , aliishia kumwangalia Hamza kwa macho mabaya na kisha aligeukia ofisi ya bosi wake na kwenda ndani.
Regina muda huo alikuwa ameshafika kazini tayari na aliwahi kwani alikuwa na viporo vingi vya kufanyia kazi.
Hata pale jana aliporudi na kutokumkuta Hamza nyumbani wala hakujali kabisa na kila alipohisi kupandwa na hasira alijiambia cheti chao cha ndoa ni kwa ajili ya kupata hisa za bibi yake tu na hakuna kingine.
“Bosi…”Aliita Linda kwa unyenyekevu mara baada ya kuingia katika ofisi ya Regina na aliongea mara baada ya Regina kumwangalia.
“Kuna tatizo nataka kukushirikisha”
“Tatizo gani?”Aliongea Regina huku akirudisha macho yake kwenye karatasi aliokuwa akiangalia.
“Ni kuhusu Hamza”Aliongea Linda na kauli yake ilimfanya Regina mikono yake kutetemeka kidogo na kisha alimwangalia Linda kwa shauku.
“Nini kimemtokea?”
“Anaonyesha tabia ambayo si nzuri kazini , kwanzia siku ziliozopita anafika kazini kwa kuchelewa na siku zingine haonekani kabisa na hakuna taarifa , tukimuacha akiendelea kama hivi ni taswira mbaya kwa kampuni”
“Unaona tumfanye nini sasa?”Aliuliza Regina lakini Linda kidogo alishangaa maana ni mara chache sana kwa Regina kuuliza swali kama hilo , ki ufupi alikuwa na majibu kwa kila kitu.
“Naona ni vizuri tukimfukuza tu”
“Hapana”Aliongea Regina haraka na kumfanya Linda kuinamisha kichwa chake chini kwa kusikitika
“Bosi ni kwasababu anafahamiana na Master Alec?”
“Hapana , ni kwasababu hawezi kuachishwa kazi”
“Lakini…”
“Unaonaje tukifanya hivi .. muandalie kazi ambazo zinahitaji muda na nguvu , wewe mpe kazi hakikisha muda wote ana kitu cha kufanya”Aliongea Regina na Linda alikubali na kutoka ofisini.
Linda akiwa kwenye ofisi yake alikuwa ashaona ni kazi gani ambayo anapaswa kumpatia Hamza, kulikuwa na kesi mbalimbali ambazo zimetoka kwenye kampuni tanzu na moja ya kesi iliokuwepo ni kutoka idara ya Sales and Business development , walikuwa wakitoa taarifa juu ya kampuni ya Dede kutoka Bagamoyo wamepitiliza siku za kulipa pesa wanaozodaiwa na walijaribu kufanya mawasiliano na kampuni hio lakini wametoa taarifa kwamba watalipa kwa Cash na anaepaswa kufuata hayo malipo ni Eliza meneja wa idara ya mauzo.
Kipindi ambacho kampuni ya Dede inaingia katika tenda ya kibiashara na Dosam dili hilo lilisimamiwa na meneja wa idara ya mauzo yaani Eliza, lakini kutokana na Dede kukosa kiasi chote cha pesa waliomba kufanikishiwa tenda yao na watalipa kiasi kilichobakia katika muda wa miezi mitatu na Eliza aliweza kuidhinisha.
Ilikuwa ni ngumu kuona kampuni inamuwekewa masharti mtu ambae amemkopesha , hii ni kwasababu ya nguvu ya kampuni hio ya Dede , ndio kampuni ilioaminika kuongoza kwa utapeli , ilikuwa kampuni ambayo inamilikiwa na Mmasai na huyo mmasai alikuwa akiaminisha wamasai wenzake kwamba hio ni kampuni ya kabila lao.
Sasa ilishangaza wamiliki wa kampuni hio kumtaka Eliza ndio akachukue malipo , ilionekana ni kama kuna mtego, sasa mara baada ya Linda kukumbuka Hamza anajua mbinu kadhaa za mapigano aliiona ni kazi ambayo inamfaa sana.
“Linda kuna kazi ninayopaswa kufanya?”Aliuliza Hamza mara baada ya kumuona Linda akiingia ofisini kwake.
“Ndio ila sio kutafsiri kama ulivyozoea , leo kuna kazi nyingine nje ya ofisi, kuna malipo yetu ya mwisho ya mwisho ya mauzo na tunaowadai wanataka twende tukachukue Cash”
“Kwanini mimi nikamilishe hayo malipo , hii ni kazi ambayo inapaswa kufanya na idara ya mikopo , ya fedha au mauzo kwanini niwe mimi?”Aliuliza Hamza.
“Upo sahihi lakini kampuni tunayoidai kidogo ina upekee wake , hivyo tusipomtuma mtu ambae sio makini anaweza kupata matatizo, umeonyesha una uwezo wa kupigana , hivyo utaenda kama bodigadi kuhakikisha Meneja Eliza hapati shida”Aliongea Linda.
“Ni kampuni gani?”Aliuliza Hamza maana baada ya kusikia ataenda na Eliza kidogo aliingiwa na utayari wa kwenda lakini alitaka kujua ni kampuni gani kwanza.
“Inaitwa Dede Entertainment”Aliongea na kumfanya Hamza kuona huyu Linda ni kama anamtafutia matatizo, Hamza aliwahi kusikia kuhusu hio kampuni mtandaoni lakini hakuwahi kuingia , kulikuwa na taarifa za malalamishi kibao kwenye mitandao zikiilalamikia serikali kuhusu watu wengi kupotea ndani ya kampiuni hio na hakuna hatua zozote zinazochukuliwa.
“Hili swala wameweka masharti watalipa Cash tunataka kuona kama kweli wanayonia ya kulipa na kama hawana tuchukue hatua za kisheria kuwadai , lakini kama tukiwashitaki itachukua muda mwingi mpaka kushinda kesi hivyo kama wapo tayari kulipa kwa Cash haina haja ya kukataa kwenda kuzichukua hizo hela”Aliongea Linda.
Hamza mara baada ya kumwangalia huyu mwanamke alivyokuwa akimpa maelekezo aliona ni kama anataka kumwingiza matatizoni.
Lakini kwasababu hakuwa na mpango wa kuendelea kubishana na huyo mwanamke ambae ni kama anamuonea wivu kwa kula bata kazini aliamua kukubali na alitoka ofisini kwenda kumtafuta Eliza.









SEHEMU YA 64,
Hamza mara baada ya kuonana na Eliza, mrembo huyo alionekana kama amechoka mno licha ya kwamba ilikuwa asubuhi, ni kama vile alikuwa ameachwa na mpenzi.
“Eliza kwanini unaonekana kuchoka hivyo?”Aliuliza Hamza na mara bada ya Eliza kukutanisha macho na Hamza alionyesha kulazimisha tabasamu.
“Labda ni kwasababu nilikosa usingizi jana , vipi kwanini umekuja ofisini kwangu?”
“Linda kasema kuna hela za malipo unazokwenda kukusanya leo , ameniambia niende na wewe kama mlinzi”
“Kwahio tunaenda pamoja?”
“Ndio”
“Nikweli nilikubali kwenda lakini pamoja na Kapteni Yonesi kama mlinzi wangu”Aliongea Eliza.
Ombi la kampuni hio kutaka Eliza kwenda kuchukua hayo malipo lililetwa kabla ya Yonesi kupatwa na matatizo mpaka kulazwa.
“Hivi hii kampuni ya Dede inatisha namna hio , nimewahi kusoma mtandaoni kuna mdau analalamika ndugu yake kupoteea ndani ya kampuni hio”Aliongea Hamza.
“Kumekuwa na taarifa nyingi kuielezea lakini haijulikani kama ni za kweli ama za uongo, polisi pia hawajawahi kukanusha ndio maana wafanyakazi wengi wanaogopa , lakini wana wateja wengi tu wapenda starehe”Aliongea Eliza , ilionekana hata yeye hakuwa na uhakika kama hio kampuni ina shida.
“Kama kampuni haijulikani uendeshwaji wake kwanini mnafanya nayo biashara?”
“Mteja huwezi kumkatalia kumhudumia kwasababu umesikia tetesi ni mtu mbaya , labda kuwe na ushahidi wa wazi unaothibitisha hayo madai , vinginevyo kama amekidhi vigezo ukimkatalia lazima umpe sababu ya kuelezeka, Kampuni ni taasisi na haikopeshi wateja kulingana na tabia zao, inaangalia vigezo”Aliongea Eliza na kumfanya Hamza kutingisha kichwa kukubaliana nae.
“Kama ni hivyo angetafutwa mtu mwingine wa kwenda , kampuni ina watu wengi wa kudai madeni sio lazima wewe?”
“Mara ya mwisho alienda mtu kwa niaba yangu lakini hakuweza kukutana kabisa na mkurugenzi wao, lakini ilisemekana alikuwepo na baada ya kuwatishia kuwachukulia hatua za kisheria ndio bosi wao akasema anataka mimi niende nikapatiwe cash”
“Huoni sasa kuna mtego?”
“Najua ndio maana sikutaka kwenda mwenyewe , nilipanga kwenda na Kapteni Yonesi”Aliongea Eliza.
Mara baada ya wawili hao kutoka nje ya lift sehemu ya maegesho , Eliza alisogelea gari ya mjerumaini Porsche Macan ya rangi nyekundu , ilionekana ile gari ya Toyota ambayo ilipata ajali ilibadilishwa na kupewa gari nyingine.
“Eliza ni lini umenunua gari kali namna hii?”Aliuliza Hamza kwa mshangao maana ilikuwa ni gari ya hadhi mno na kwa haraka haraka alijua sio chini ya milioni mia thamani yake.
“Sijanunua mimi , hii ni zawadi kanipa Regina kutokana na kufanikisha dili la ile kampuni kutoka Morogoro?, ni gari ya bei sana najua lakini nilishindwa kuikataa maana mwenyewe ndio kanipa”Aliongea Eliza na kumfanya Hamza kushangaa , ilionekana Regina alikuwa akimjali mno Eliza lakini bado ni kama kuna kitu kilimpa ishara tofauti , ilionekana kulikuwa na zaidi ya sababu kwa Regina kumpatia Eliza gari ya bei ghali namna hio.
“Hata mimi naona hukuwa na haja ya kukataa , isitoshe unahitaji usafiri”Aliongea Hamza.
“Ndio , bosi ananijali ndio maana sitaki kumwangusha”Aliongea Eliza huku akiwa na muonekano usioweza kuelezeka ni wa furaha au wa huzuni.
Kwa namna ambavyo Eliza alikuwa akiongea ilizidi kumpa wasiwasi Hamza na kujiambia kuna kitu ambacho hakipo sawa kabisa lakini hakuelewa nini kinaendelea, isitoshe Eliza pia alionekana kutokuwa na raha kabisa.
Kwasababu Hamza ndio aliekuwa akiendesha Eliza alisema analala kidogo.
Kampuni hio ilikuwa maeneo ya Msata-Bagamoyo hivyo ilikuwa ni safari ya kama masaa mawili hivi.
Kutokana na Eliza kulala Hamza aliendesha gari kwa spidi kubwa ya wastani na ndani ya muda mfupi aliweza kufika na kuingia kwenye barabara inayokunja kushoto akipishana na kituo cha kujazia mafuta cha Lake oil.
Dede licha ya kwamba ilikuwa ikiitwa kampuni lakini ilikuwa ni kama hoteli tu.
Tajiri Laizer mara baada ya kupata madini makubwa yaliompa zaidi ya utajiri wa dolla milioni kumi za Kimarekani ndio alijenga katika eneo hilo ambalo ilikuwa ni shamba lao kabla hata ya kutajirika.
Hamza mara baada ya kuegesha gari Eliza aliweka nywele zake vizuri na wote wakashuka na kuanza kutembea kulisogelea geti na mara baadaya kufika getini hawakuweza kuigia maana lilikuwa limefungwa na waliishia kugonga.
“Mnaenda wapi?”Sauti ya mmasai ilisikika kupitia kijidirisha kidogo.
“Tunatokea kampuni ya Dosam , tuna miadi na Mr Laizer ”Aliongea Eliza.
“Dosam?, hebu subiri kwanza tutoe taarifa”Aliongea yule mlinzi na kisha kidirisha kilifungwa , walionekana kuwa makini kama vile wanafanya biashara haramu humo ndani.
Mpaka dakika tano zinaisha ndio mlango wa geti dogo ulifunguliwa na mwanamke alievalia sare za uhudumu.
“Nadhani utakuwa unaitwa Eliza meneja kutoka kampuni ya Dosam , unaweza kunifuata”Aliongea yule mwanamke na Hamza na Eliza waliingia ndani.
Lilikuwa eneo kubwa mno lenye bustani zilizotengenezwa na kuvutia , kulikuwa hadi na sanamu kubwa ya ng’ome katikati ya bustani.
Jengo la kampuni hio lilikuwa limeenda hewani kwa floor kama nne hivi na pana.
Ukweli licha ya kuambiwa hio ni kampuni lakini alishindwa kuelewa ni kampuni ya aina gani , Hamza alijiambia pengine ni biashara ilioandikishwa kama kampuni pekee lakini sio kampuni.
Walimfuata yule mhudumu ambae aliwaingiza katika korido ndefu iliokuwa na kila aina ya michoro ya wamasai ikiwemo Morani na viongozi wakubwa wa kimasai waliowahi kutamba katika historia , kulikuwa hadi na picha za baadhi ya tamaduni zao ikiwemo vinyago na mengineyo.
Licha ya michoro hio, jengo hilo lilinukia harufu ya kitajri , ni aina flani ya harufu hata benki unaweza kuweza kuinusa.
Waliweza kupishana na watu tofauti tofauti ikiwemo wanawake na wanaume na walikuwa wamevaa na wakapendeza mavazi ya pesa nyingi na kuna hata wale ambao Hamza aliweza kuona walikuwa na mafunzo ya mapigano.
Eliza alikuwa mwanamke mrembo na kitendo cha kuingia eneo hilo ilikuwa ni kama anaingia kwenye shamba lililojaa mbwa mwitu, kila mwanaume aliekuwa akimwangalia alionekana kumtamani.
Hata Hamza aliweza kuona namna ambavyo Eliza alikuwa na wasiwasi lakini hakuongea chochote , ili kumuondolea wasiwasi aliamua kumshika mkono
Eliza mara baada ya kushikwa mkono na Hamza alishituka kidogo lakini kwa wakati mmoja alionekana kujisikia vizuri kwenye moyo wake , lakini macho yake alipokuwa akimwangalia Hamza ni kama alikuwa akionyesha hisia za mwanamke mpweke, ni kama zile hisia ambazo michepuko wanakuwa nazo wakati wakiwasindikiza kwa macho waume za watu wakirudi nyumbani kuonana na familia zao.
Mara baada ya kutembea kwa takribani dakika saba waliweza kufika katika eneo ambalo lilikuwa kama sebule , kulikuwa na kila aina ya samani za bei ghali na kulikuwa hadi na kitanda chembaba cha kupumzikia.
“Mtasubiri hapa chumba cha mapokezi kwa dakika chache , bosi kwasasa yupo bize na baadhi ya kazi”Aliongea yule mhudumu na kisha akaondoka na kuacha ukimya ndani ya eneo hilo, kulikuwa na runinga pekee ambayo ilikuwa ikionyesha habari za kifo cha mgombea wa uiraisi wa chama tawala ambazo hazikumvutia Eliza kwa muda huo
“Hili eneo ni kama vile tupo Ikulu , ndio maana kuna malalamishi mengi kuhusu hili eneo”Aliongea Hamza maana ukimya wa hilo eneo ni kama vile hakuna kinachoendelea.
“Nimepitia mengi na kuna kila dalili zinazoniambia kuna kitu hakipo sawa , tunapaswa kuwa makini”Aliongea Eliza na kumfanya Hamza atake kumuuliza swala ambalo aliambiwa na Dina kutaka kutengenezwa na mheshimiwa Mgweno kama shushu wao wa karibu na Regina.
“Una hisi hivyo?”
“Ndio , unaweza ukawa hujapitia changamoto nyingi lakini kama meneja wa idara ya mauzo nimekutana na kila aina ya wateja kukamilisha mauzo ,hatujaambiwa hata ni muda gani tunakutana na Mr Laizer hii inaonyesha wametukalisha hapa makusudi kuvuta muda”Aliongea na kumfanya Hamza kutabasamu.
“Eliza wa nyumbani ni tofauti sana na wa kazini unaonekana kuwa makini mno”Aliongea Hamza.
“Sina utofauti wowote nyumbani na kazini nipo makini”Aliongea Eliza kwa kulalamika lakini kitendo cha kulainisha midomo na mate ni kama ilimpa hamasa Hamza kutaka kumkisi hapo hapo baada ya kuona wapo wenyewe tu na alichowaza ndio alifanya , alimshika kiuno Eliza na kumsogelea.
“Ah , wewe unafanya nini?”Aliongea lakini alionekana kulegea mbele ya Hamza na ilikuwa ni kama ishara nzuri kwa Hamza na kuzidi kumsogelea ili kumkisi lakini Eliza aliwahi kumziba Hamza mdomo na kiganja chake.
“Hamza usiwe hivi bwana , hatuwezi..”Aliongea Eliza akijitahidi kuwa siriasi na muda huo ni kama Hamza na yeye alikumbuka kuhusu swala la ndoa kwamba bado hajamuambia ukweli.
“Sorry Eliza , shida ni kwamba tukiwa wenyewe hivi nashindwa kujizuia kukuangalia unavyovutia”Aliongea Hamza.
“Kwasasa tuwe bize na kazi kwanza”Aliongea Eliza kikauzu huku akisogea mbali kidogo na Hamza na kitendo kile kilimfanya Hama kuona huyu sio Eliza aliemzoea.
Walikaa kwa zaidi ya dakika ishirini bila ya mtu yoyote kufika na hawakukaribishwa hata kinywaji , Hamza alijikuta akianza kuchoka na kuanza kupiga miayo na walisubiri kwa nusu saa nyingine lakini hakutokea mtu na muda wa chakula cha mchana ulifika na kumfanya Hamza kuhisi njaa.
“Inaonekana wanataka kuendelea kutukalisha hapa”Aliongea Hamza
“Tusubiri kidogo?”
“Mimi naona tunapoteza tu muda , kwanini tusiende kumtafuta wenyewe,tunaweza hata kuuliza wafanyakazi watuambie ofisi yake ilipo”Aliongea
“Unafikiri itakuwa rahisi wafanyakazi kutuambia?”Aliongea Eliza na muda huo huo mlango ulifunguliwa na alionekana mwanaume aliejazia mwili alievalia singlend tu kama mcheza basketball.
Mwanaume huyo alikuwa akinuka pombe tu na alikuwa ameshikilia chupa ya Whiskey mkononi na macho yake yalikuwa kwa Eliza muda wote kama vile anamtathimini.
“Mrembo nilieandaliwa leo naona hana ubaya mwenye , kazurii..”Aliongea huku akitabasamu kifedhuli na kauli yake ilimfanya Eliza kubadilika.
“Wewe ni nani?”Aliuliza Eliza na swali lile ni kama lilikuwa kichekesho kwa yule mwanaume kwani alianza kucheka kwa sauti huku akimsogelea Eliza.
“Unauliza nini wakati umeletwa kwa ajili yangu , halafu kwanini umevaa nguo nyingi namna hii au ndio unatunza joto , hii mbinu nimeipenda”Aliongea kilevi huku akinyoosha mkono kutaka kushika kola ya shati la Eliza lakini Hamza alikuwa ashamkinga Eliza kwa mbele tayari.
“Bro , nadhani umekosea chumba?”Aliongea Hamza na kumfanya yule bwana kumwangalia Hamza kwa macho yaliojaa ukauzu.
“Dogo wewe ni nani , kwanini unanizuia kuigusa mali yangu?”
“Narudia tena , Bro umekosea chumba “Aliongea Hamza na kumfanya yule mlevi kukasirika na aliinua chupa yake na kutaka kumpiga nayo Hamza ya kichwa na kitendo kile kilimfanya Eliza kupiga kelele , lakini Hamza aliweza kuidaka kabla hata haijampiga na ni pombe tu ilioishia kumwagikia usoni na aliishia kulamba maji maji yaliomfikia mdomoni.
“Sijui nafanya nini , hata mimi naona nishalewa”Aliongea Hamza.
Lakini yule mlevi alijikuta akikasirika zaidi na aliinua mkono kutaka kumpiga Hamza kibao lakini kabla ya kumfikia Hamza alikuwa ashainua mguu na kumpiga nao tumboni.
“Bang!!”
Yule mlevi alijikuta akishindwa kuhimili nguvu iliomsukuma na kwenda kuvaa pot ya maua na kudondoka nayo
“Fuc*k you”
Bwana yule alijkuta akitukana na alisimama kwa tabu na kumsogela Hamza kwa mara nyingine huku akiwa amekunja ngumi , lakini Hamza alisimama katika eneo moja na baada ya kumkaribia alimpiga ngumi ya kifuani iliomfanya yule bwana kudondoka tena chini huku akiwa amepiga magoti na kuanza kutapika pombe iliochangayikana na damu.
Eliza aliekuwa nyuma aliweza kuona Hamza alikuwa amemuadhibu yule mlevi kwa mashambulizi mawili tu mpaka kutapika damu , alishindwa kujizuia na kuishia kushikwa na hofu asijue cha kufanya.
Hamza alimsogelea yule mwanaume na kisha alimkanyaga mgongoni na kumfanya alale kifundi fudi.
“Sema wapi alipo Laizer”Aliongea Hamza
“Unajitafutia kifo , mimi ni mgeni hapa unathubutu vipi kunishambulia?”Aliongea kijeuri na kumfanya Hamza anyanyue mguu na kumkandamiza kwa nguvu kwenye bega lake na kumfanya apige mayowe kwa maumivu makali.
“Ongea wapi alipo Laizer?”Alirudia Hamza.
“Sijui alipo , mimi sijui kweli”Mtu yule wa miraba minne alijikuta akianza kuingiwa na woga .
“Unaendelea kujifanya mtiifu sio , mpaka muda huu bado unaigiza?”Aliongea Hamza huku akizidi kumkandamiza kwenye bega lake.
“Nilikuwa nikifuata maagizo tu , mimi sijui kweli alipo”Aliongea yule bwana na muda huo ni kama Eliza alishituka.
“Hamza anasema ametumwa na Mr Laizer?”.
“Kuna haja hata ya kuuliza , huyu katumwa kuja kukuigizia hapa kukuogopesha ili usahau hata kuulizia hela”Aliongea Hamza.
“Mbona wameenda mbali hivyo , sidhani Mr Laizer anaweza kukosa milioni themanini iliobaki”
******
Upande wa makao makuu, Regina akiwa ndani ya ofisi yake alijaribu kumpigia Hamza lakini ajabu alikuwa akiambiwa simu yake haipatikani.
Na alianza kushikwa na wasiwasi kutokana na bibi yake alimsisitizia kupitia simu anataka kuonana na Hamza siku hio bila ya kukosa , sasa kwa mtu ambae alikuwa siku za mwisho mwisho ombi lake lilipaswa kutimizwa bila ya kuchelewa ndio maana Regiina alikuwa na wasiwasi.
Lakini anajaribu kupiga simu yake sasa haipatikani , muda uleule aliamua kumuita Linda ofisini kwake.
“Mkurugenzi kuna maagizo yoyote?”Aliongea Linda.
“Hamza yupo wapi?”Aliuliza na kumfanya Linda mwili kumkakamaa.
“Ametoka nje ya ofisi kikazi?”
“Kwenda nje kikazi , nje ya wapi na ni kazi gani?”Aliuliza Regina kutokana na kwamba hata yeye alishangaa kusikia kauli hio.
“Kuna zile pesa zilizobakia za tenda kutoka kampuni ya Dede Bagamoyo , mkurugenzi wao alipiga simu na kusema atafanya malipo ya Cash na Meneja Eliza anapaswa kuyafuata leo , ilipangwa Eliza kwenda na Kapteni Yonesi kama mlinzi wake lakini bado hajapona kabisa , hivyo nilimpa kazi hio Hamza kwenda nae , maana anaonekana kuwa na nguvu zaidi ya Kapteni..”Aliongea Linda na kumfanya Regina ukauzu kumvaa.
“Nani kakuambia umpangie kazi ya namna hio?”
“Lakini bosi si ulisema nimpe kazi asikae bure”
“Hebu nyamaza , Hamza ni msaidizi wangu mimi , inakuwaje atoke hapa aende kuwa bodigadi wa meneja wa idara ya mauzo , nimekwambia mpangie kazi na sio kumhamisha idara , akili yako inawaza nini?, hivi unadhani mimi nimekuwa kipofu , hata kama una wivu kutokana na uwezo wake kwenye baadhi ya mambo hupaswi kuonyesha wivu wako kwa kufanya maamuzi ya namna hii , yaani umefanya kazi na mimi kwa zaidi ya miaka mitatu lakini unashindwa kukua kimawazo” Regina alibadilika na kuwa mbongo na kuanza kumfokea sekretari wake.
Linda macho yaligeuka kuwa mekundu huku akiinamisha kichwa kwa hofu kubwa.
“Nisamehe bosi , nimekosea.. , nitampigia mara moja arudi’Aliongea Linda akijitetea.
“Haina haja nishampigia mara kadhaa na simu yake haipo hewani , nadhani kaizima au hakuna mtandao”
“Lakini bosi wanazimaje simu , wameenda Msata makao makuu ya Dede kwanini mtandao usipatikane”Aliongea Linda na muda ule ni kama Regina anasikia vizuri sasa.
“Dede si wana ofisi yao Posta na ndio tulikubaliana makabidhiano ya malipo yatafanyikia hapo , kwanini wameenda Msata?”Aliuliza Regina ni kama aliona kuna taarifa ambazo hajaletewa.
“Ndio walivyotoa maelekezo , mara ya mwisho siku yao ya kulipa waliomba kuongezewa siku mpaka leo na Eliza ndio afuate Cash, idara ya mauzo ndio walifanya makubaliano na Dede na ofisi ya Finance wameipa siku kumi idara ya sales kukamilisha hesabu la sivyo wataripoti idara ya sheria…”
“Kwahio wamemwambia Eliza aende na akakubali kwenda , hivi ni habari ngapi mmesikia kuhusu mambo yanayofanyika huko Msata , ukute hata hizo Cash wanazotaka kutoa ni kwa ajili ya kutakatisha hela , mlipaswa kuwakatalia na sio kwenda kichwa kichwa ,si walikubaliana wakutane Posta kwenye makabidhiano?”Aliuliza Regina lakini Linda hakuwa na jibu zaidi ya kukaa kimya
“Dede wanafahamika kwa kutapeli watu kupitia madeni yao , wakikataaa deni lao Eliza ana uzoefu wa kutolazimisha na kuacha sheria ichukue mkondo wake , lakini wewe umemjumuisha Hamza ambae anapenda kujichukulia sheria mkononi , unataka akaibue matatizo mengine?”Aliongea Regina huku akimwangalia Linda kwa macho ya kukatishwa tamaa.
“Nisamehe bosi sikufikiria mbali”Alijitetea lakini Regina hakuwa na mudi kabisa ya kuendelea kumuona.
“Unaweza kuondoka , unapaswa kuomba yasitokee matatizo na warudi wakiwa salama la sivyo jiandae kuandika barua ya kuacha kazi”Aliongea Regina kikauzu na kumfanya Linda kuinua uso wake huku akimwangalia bosi wake kwa kutoamini.
“Bosi , kwani Hamza ni wa muhimu sana?”Aliuliza Linda.
“Ndio ni wa muhimu”Aliongea kikauzu na kauli yake ilimfanya Linda kutetemeka na aliishia kuondoka kwa hatua hafifu na kufunga mlango.
Ukweli ni kwamba Regina hakujua kwanini alikuwa na wasiwasi Hamza angesababisha matatizo huko Msata , kulikuwa na mambo mengi yanaendelea nchini ikiwemo taarifa za mgombea wa uraisi kuuliwa na mengineyo na aliona Hamza anaweza kutibua zaidi hali.
Baada ya kukaa akiwaza cha kufanya palepale alichukua simu yake na kuitafuta namba ya Meneja wa hoteli yao ya nyota tano Bagamoyo mjini.
“Mkurugenzi habari za mchana , kuna maagizo yoyote?”Sauti ya mwanaume ikiongea kwa heshima ilisikika.
“Hebu tuma mtu yoyote kutoka hotelini aende Dede kuangalia kinachoendelea, Meneja Eliza na msaidizi wangu wapo huko na hawapatikani hewani”Aliongea
“Sawa Mkurugenzi nina mtu yupo maeneo ya Msata nadhani itakuwa rahisi kwenda kuangalia nitakupa majibu muda si mrefu”Aliognea mkurugenzi na Regina alikata simu.
Hamza ametengenezwa mpango wa kwenda Dede bila kujua , ngoja uone.

0687151346 -Watsapp only
 
SHETANI RUDISHA AKILI ZETU

MTUNZI: SINGANOJR

SEASON 03
SEHEMU YA 61.
Frida alijua kabisa anakwenda kufa na kifo chake kuja kuwa utata , aliweza kuona kilichokuwa kimemkaba kooni ni kivuli lakini hakuweza kufanya chochote.
Kwa mtu wa kawaida unaweza useme Frida alikuwa amepatwa na ukichaa au ugonjwa wa ajabu lakini ukweli ni kwamba kuna nguvu iliokuwa ikimkaba kupitia kivuli.
Wakati akiwa amekata tamaa ghafla tu ule utulivu wa kile chumba ulitoweka , ilikuwa ni kama upepo umeongezeka kwa kiasi kikubwa na kufumba na kufumbua kivuli kile kilipotea na kumfanya Frida kuanza kukohoa kwa nguvu , mpaka anakuja kutulia alijikuta akishituka mara baada ya kugundua kuna mtu mwingine ndani ya chumba chake alievalia joho la rangi nyeusi, alitaka kupiga yowe lakini mtu yule alimpa ishara ya kutulia.
“Wewe ni nani?”Aliuliza Frida kwa sauti ya chini huku akiwa ameshika shingo yake , ilikuwa bado hakuamini kama alikuwa amepona.
“Msimamizi wako na mlinzi wako mpya”Aliongea kwa lugha ya kingereza na kumfanya Frida kuchangayikiwa.
“Sikuwa na msimamizi na mlinzi , kwanini unajitambulisha kama mlinzi wangu mpya , nataka kujua unatokea upande upi , Wiccan au Sinagogu?”Aliongea Frida kwa sauti kubwa kidogo.
“Mimi ni mu’ alkemi kutoka makao makuu ya Wiccan , nipo hapa kwa maagizo ya Madame, mlinzi wako wa zamani amepoteza maisha”Aliongea na kumfanya Frida kuzidi kuchanganyikiwa lakini mara baada ya kusikia mtu huyo yupo hapo kwa maagizo ya Madame alipata ahueni.
“Mlinzi wangu wa zamani , unamaanisha mlinzi gani?”
“Alietaka kukuua amemuua mlinzi wako , kwanzia sasa utakuwa chini ya ulinzi wa binadamu”Aliongea huku akisogea karibu na mlango.
“Nilikuwa na mlinzi kivuli!!?”
“Wewe ni wa muhimu sana kwa Madame kuwasiliana na waumini wa ulimwengu wa nje ya kivuli , kwa namna yoyote unapaswa kuwa salama”Aliongea.
“Kwanini alitaka kuniua?”Aliuliza Frida, alikuwa akijua mtu ambae alitaka kumuua ni kivuli au watu ambao wamepata umaarufu kwa jina la Night Shadows(Vivuli vya watu vinavyoonekana usiku).
“Sina majibu kuhusu swali lako lakini nina ujumbe kutoka makao makuu”Aliongea kama roboti.
“Ujumbe gani?”
“Hakikisha anatumia mshumaa kurekodi ndoto zake ndio utakuwa salama, kadri atakavyoota bila ndoto zake kurekodiwa mtiririko wa matukio utakosekana na mpango wote kuingia dosari”Aliongea.
“Unamaanisha Ha…”
“Sikutajiwa jina , huu ndio ujumbe kutoka makao makuu unaopaswa kufanyia kazi”Aliongea yule bwana. Frida alitaka kuuliza swali zaidi lakini alijua asingepata majibu.
Yule bwana alievalia joho la rangi nyeusi mara baada ya kuridhika kwa kuona Frida alikuwa ameelewa aliaga.
“Wakati wowote ukiwa katika hatari na kuhitaji msaada wangu tamka neno , Grishav nitaitikia wito wako”Aliongea na palepale bila ya Frida kujibu aliinama chini na kufumba na kufumbua alipotea.
Frida alijikuta akiingia katika maswali mengi na swali kubwa lilikuwa juu ya ule mshumaa , alijua maelekezo yale yalikuwa yakimlenga Hamza lakini alishangaa mara baada ya kuambiwa Hamza anapaswa kutumia mshumaa ule ili kurekodi ndoto zake.
Swali ambalo alijiuliza inakuwaje mshumaa ambao alipatiwa na Dokta Genesha kuwa na uwezo wa kurekodi ndoto , kitu ambacho Wiccan walitaka iwe hivyo , inamaana kuna mpango uliokuwa ukiendelea kati ya Dokta Genesha na Wiccan kiasi cha kumkabidhi Mshumaa wa Nuru kwa ajili ya kumpatia Hamza.
Frida alijiuliza ni kitu gani ambacho kinaendelea yeye hakijui na kwanini amenusurika katika kifo.
Alikumbuka kwamba asipofanikisha Hamza kutotumia mshumaa basi atakuwa hatarini lakini swali lingine liliibuka inamaana Hamza alikuwa akiota bila ya kutumia ule mshumaa.
Kitu ambacho Frida alikuwa akijua ni kwamba mshumaa ule ulikuwa ni kwa ajili ya kumletea Hamza ndoto tu ili kujua maisha yake ambayo ameyasahau , hayo ndio yalikuwa maelekezo kutoka kwa Dokta Genesha na hakuelezwa kwamba mshumaa ule ni kifaa cha kurekodi ndoto, alijiuliza kama ni hivyo kinarekodi vipi hizo ndoto , ni sayansi ya namna gani ambayo imetumika.
Alijikuta hata usingizi ukimpelea kabisa licha ya kwamba alijihisi uchomvu mkubwa , hofu ilimvaa na hisia zake zilimwambia pengine anachofanya sio kuhatarisha usalama wake tu bali anahatarisha na usalama wa Hamza.
“Sina jinsi kwasasa lazima nihakikishe Hamza anatumia mshumaa ili kuwa salama , wakati nikitafuta majibu ya maswali yangu yote. Lakini nitafanya nini kumfanya atumie mshumaa kama yeye mwenyewe haniamini vya kutosha mpaka kuutumia?”Aliwaza Frida.
******
Hamza mara baada ya Side na wenzake kuondoka alibakia na mrembo Dina , wote wawili hawakuwa na ile mudi ya kwenda floor za juu kwa ajili ya kulewa vileo na kufanya starehe zingine kama kucheza kamari.
Kitu pekee ambacho Dina alipenda ndani ya Club hio ni kutumia siraha kulenga shabaha na hata Hamza alikuwa akipenda kitu kama hiko , kwake hakuwa mpenzi sana wa vileo na kucheza disco.
Walitumia zaidi ya lisaa limoja na nusu kulenga shabaha kwa kutumia bunduki za aina mbalimbali.
Ilipotimia saa tano kasoro njaa zilikuwa zikiwauma na Hamza alipendekeza warudi Kijichi ndio wakapate chakula huko na Dina hakupiinga.
Mara baada ya kufika kijichi chakula kiliandaliwa na wote wakaanza kula pamoja.
“Unaonaje baada ya hapa ukaangalie maendeleo ya vijana wangu , tokea siku ile ulivyowafundisha kiasi namna ya kucheza Karate na Kung Fu hukuwaona tena”Aliongea Dina.
Hamza kipindi kabla ya kukutana na Regina alikuwa ameshawahi kuwafundisha vijana wa Dina mafunzo ya Karate na Kung Fu mara moja na hakuwahi kwenda tena kuwaona.
“Hakuna shida , kuna kitu pia nataka kwenda kukifanyia mazoezi”Aliongea Hamza.
“Kitu gani , ni kuvuna nishati za mbingu na ardhi au kitu kingine?”Aliuliza Dina kwa shauku alikuwa akijua Hamza ana mafunzo ya kuvuna nishati za nguvu ya asili ya ardhi na mbingu na alitamani kujifunza pia siku moja.
“Hutoelewa hata nikikuambia ni kama maneno ya kutamka nataka kuyafanyia majaribio”Aliongea Hamza.
Ukweli ni kwamba kitu ambacho alikuwa akienda kufanyia majaribio ni yale maneno ambayo Yonesi alimtajia wakati akiwa hospitalini , siku ile wakati akifanya tahajudi kwa kupitia yale maneno aliona sura ya mwanamke ambae anamuona katika ndoto , bado shauku yake juu ya tukio lile haikuwa imeisha na alitaka kwenda kujaribu tena.

Baada ya kumaliza kula Hamza alitoka akiongozana na Dina pamoja na Lawrence na kwenda katika ukumbi maalumu ambao ni kama eneo la mafunzo ya kimapigano.
Hakukuwa na matumizi ya siraha , ilikuwa ni sehemu ambayo watu wa Dina walikuwa wakijifunza namna ya kupigana kwa kutumia mbinu mbalimbali za sanaa ya mapigano , eneo hilo lilikuwa likitambulika hata kwa serikali na lilikuwa na kibali kabisa.
Ni eneo ambalo lilijengwa katika mgawanyo wa sehemu mbili , sehemu ya kwanza ilikuwa ni kwa kufanyia mazoezi ya kawaida kama Gym na mazoezi ya boksa, Karate na Judo upande mwingine ulikuwa ni wa tahajudi.
Katika sanaa ya mapigano tahajudi ilikuwa ni sehemu ya mazoezi kwa ajili ya kuujua mwili wako ulivo, ukifanya tahajudi kama binadamu utajuwa wapi kuna udhaifu wako na wapi nguvu zako zinakaa kwa wingi na namna gani ya kushinda udhaifu wako.
Hamza mara baada ya kuona vijana wa Dina wakichukua mazoezi aliridhika , aliweza kuona wengi walikuwa wamepiga hatua kwa kufuata maelekezo yake.
“Bro , unapanga kufanya mazoezi ya namna gani , unataka kufanya tahajudi?”Aliuliza Lauwrence mara baada ya kumuona Hamza akichagua upande wa wanaofanya Tahajudi.
Dina na Lawrence siku zote walikuwa na shauku ya kutaka kumuona Hamza akichukua mazoezi hivyo walimwangalia.
“Kaa kimya Lau acha maswali mengi”Aliongea Dina akimzuia Lau kutokumsumbua Hamza na maswali yake.
Kutokana na wale wanafunzi kumuona Hamza na wao wote waliacha na kumpatia Hamza nafasi , kwao ni kama kuna kitu ambacho walitaka kujifunza kwa kumuangalia ndio maana walisimama pembeni.

Wakati Hamza akiwa katika mkao wa kufanya tahajudi huku midomo yake ikicheza ghafla tu watu wote walijikuta wakikumbwa na msisimko wa ajabu , ilikuwa ni kama kuna kiumbe cha ajabu kimefika ndani ya eneo hilo na kuwafanya kuanza kushindwa hata kupumua vizuri huku eneo ambalo Hamza alikuwa amekaa anga lake ni kama lilikuwa likitingishika.
Dina alijikuta jasho la paji la uso likimtoka huku akimwangalia Hamza kwa wasiwasi , alipatwa na hisia kama vile Hamza amekuwa mfalme ghafla na yeye ni kijakazi wake.
Upande wa Hamza hakuwa hata akielewa kilichokuwa kikiendelea kwa nje , kama alivyotarajia maneno yale yalikuwa ni kama anamwita yule mwanamke , mara ya kwanza wakati alivyofanya kule wodini alimuona kwa mbali yule mwanamke , lakini wakati huo kadri alivyokuwa akiimarisha umakini wake wa ubongo na kuzidi kuyatamka yale maneno alimuona ni kama vile yule mwanamke mchawi anaemuona kwenye ndoto alikuwa akimsogelea kutoka angani kwa spidi ya ajabu.
Zilipita kama dakika nne tu yule mwanamke aliweza kumuona kwa ukaribu zaidi, lakini jambo ambalo lilimshangaza Hamza ni kitu ambacho alikuwa ameshikilia mkononi.
Kadri alivyokuwa akizidi kuongea yale maneno mwanamke yule alizidi kusogea , lakini ilifikia hatua ni kama hawezi kumfanya asogee zaidi na yule mwanamke ni kama alijua Hamza hawezi kumuita karibu zaidi na alichokifanya ilikuwa ni kunyoosha kile kitu alichoshikilia mkononi mwake na Hamza mara baada ya kuangalia vizuri alijikuta akipagwa , ulikuwa ni ule mshumaa ambao Frida alimpatia akimwambia umetoka kwa Dokta Genesha, Mshumaa wa Nuru.
Hamza alichanganyikiwa mshumaa wa nuru kwanini upo katika mikono ya huyo mwanamke , katika ndoto yule mwanake alimuona kama mchawi ambae anachomwa moto baada ya kukamatika lakini kwanini akashika kitu cha nuru ilihali nuru na uchawi ni vitu viwili tofauti.
Yule mwanamke ni kama alikuwa akitaka Hamza amsogeze karibu aweze kushika ule mshumaa , upande wa Hamza alionekana kusita kuupokea ule mshumaa na yule mwanamke ni kama aliliona hilo na alitamka neno kwa kunyanyua mdomo wake kwa juu bila kutoa sauti akihakikisha Hamza anasoma lipsi zake.
NISAIDIE!(Help me)
Ndio neno ambalo aliongea huku akimpa ishara Hamza kupokea ule mshumaa.
Muda uleule Hamza aliacha kutamka yale maneno na kitendo kile kilifanya yule mwanamke ni kama vile kuna nguvu iliokuwa ikimvuta na kuzidi kurudishwa nyuma mbali na yeye , lakini bado hakuacha kumnyooshea ule mshumaa kama ishara ya kumuomba amsaidie.
Muda ileule wakati kila mtu akiwa ameloa jasho kana kwamba eneo lote limekumbwa na joto kali Hamza aliweza kufungua macho yake huku akionyesha hali ya kuwashangaa waliokuwa wakimwangalia .
“Nini kimetokea, Dina mbona upo hivyo?”Aliuliza Hamza mara baada ya kumuona
“Bado tu unapata muda wa kuuliza , ni kitu gani ulichokuwa ukifanya?”Aliuliza Dina na kumfanya Hamza sasa kuelewa kilichokuwa kikiendelea , licha ya yeye mwenyewe kuwa na wasiwasi lakini aliishia kucheka.
“I am sorry !, hii ni mara yangu ya kwanza kujaribisha hiki kitu , sikuweza kujizuia kile kinachonizunguka”AliongeaHamza na kisha alipiga hatua kuondoka katika eneo hilo.
Na wakati wakianza kutembea ndio sasa waligundua paa la jengo hili lilitingishika sana na kutokana na mchwa kula mbao unga unga ulidondoka chini kwenye tailizi na kila walipokuwa wakipiga hatua walikuwa wakiacha nyuma alama za miguu.
“Muda umeenda sana , nataka nirudi nyumbani”Aliongea Hamza.
“Hamza ni mafunzo gani yale , ni nguvu ya ndani au nishati ya mbingu na maji?”
“Ilianza mbingu ikaja ardhi halafu mbingu ikaleta maji na uhai , hizi ni kanuni za mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi na ni kitu ninachoweza kufanya pia , lakini kuhusu nilichofanya sasa hivi hata sijui ni kitu gani , kama nilivyosema nipo kwenye utafiti”Aliongea Hamza
“Hata jina lake hujui?”Aliuliza Dina kwa mshangao.
“Ndio ila kwasasa nitaiita hii kama Wito, kwasababu ukiifanya ni kama kuna kitu unakiiita”
“Huwa haifurahishi kusikiliza pekee”Aliongea Dina kwa macho yaliojaa huzuni na shauku.
“Usiongee hivyo , hiki ni kitu ambacho siwezi kukuruhusu ufanye kabla sijakipatia majibu , nguvu yake ni kubwa kiasi kwamba ni kama sijakula kabisa”Aliongea Hamza huku akijihisi ni mwenye njaa kali.
Dina alimwambia twende ukale na Hamza hakuwa na aibu ya kukataa kwani alikuwa na njaa , muda huo hawakurudi kwenye mgahawa bali Hamza alienda mpaka yalipo makazi ya Dina mita kadhaa kutoka mgahawa wake ulipo na mfanyakazi aliagizwa kuandaa chakula na Hamza alikaa chini na kuanza kukifakamia huku Dina akimwangalia kwa macho yaliojaa mahaba.
“Unajua nilishangaa baada ya mstaafu Mgweno kunipigia simu akisema yaishe”Aliongea Dina.
“Kwanini yeye ndio kakupigia simu?”,
“Unaweza kushangaa , licha ya kwamba kwa nje inaonekana familia ya Benjamini ndio inataka Regina kuolewa na James lakini upange mwingine ni mipango ya Mheshimiwa Mgweno”Aliongea Dina.
“Unataka kumaanisha nini?”
“Labda utakuwa hujui tu , ila kampuni ya Dosam ni kubwa Tanzania na inachangia zaidi ya asilimia tatu ya pato lote la Taifa , imeshikilia uchumi wa nchi katika maeneo nyeti, Benki namba moja ya kibiashara inayoongoza kwa Tanzania na Afrika mashariki yote ni Dosam Commercial Bank huu ni kama utawala wa mzunguko wa fedha nchini , hapa bado hujazungumzia usafiri wa anga , mahoteli na usambazaji wa bidhaa mbalimbali kwa matumizi ya majumbani, Kabla ya mheshimiwa Mgweno hajaingia madarakani Kampuni ya Zena ilikuwa ya kawaida tu kulinganisha na Dosam lakini baada ya Mgweno kuingia madarakani ilikua kwa spidi ya hali ya juu na yote hii ilikuwa ni uwekezaji mkubwa ambao mheshimiwa alifanya kwa kuiba hela za wananchi”Aliongea Dina.
“Kwahio unachomaanisha ni kwamba kampuni ya Zena inamilikiwa na Mheshimiwa mstaafu Mgweno?”
“Ndio kwa asilimia zaidi ya arobaini na tisa, ukifuatilia wana hisa wa kampuni ya Zena utagundua wengi wanaomiliki hisa hizo ni kampuni kutoka nje ya nchi , ukifuatilia kampuni hizo nje ya nchi utagundua kwamba ni kampiuni ambazo zimepewa haki kisheria ya kumiliki hisa hizo na kampuni nyingine , mzunguko unaendelea hivyo hivyo, zote ni njama za Mgweno kuficha wananchi kwamba anaimiliki Zena , sio kampuni moja tu , kila kampuni kubwa ana ushawishi wa kimaamuzi”
“Zote hizo ni hela za rushwa!?”
“Ndio lakini hakuna ushahidi wa kuthibitisha kama ndio mmiliki, sehemu pekee ambapo amekosa umiliki na ushawishi ni kampiuni ya Dosam peke yake na hii ni kutokana na msimamo wa aliekuwa kuongozi wa kampuni yaani babu yake Regina”Aliongea Dina na sasa ni kama Hamza alikuwa akipata picha.
“Kwahio anajaribu kuitumia familia ya Benjamini kwa ajili ya kuingiza ushawishi wake katika kampuni ya Dosam?”
“Ipo hivyo , mwanzoni walijua mambo yataenda sawa kama Regina atakubali kuolewa na James lakini mambo yamekuwa magumu , Regina karithi tabia zote za waanzilishi wa ile kampuni”
“Unamaanisha bibi yake na babu yake, unachoongea kinaonekana kuwa sahihi”Aliongea Hamza.
“Mgweno anachotaka ni kuimiliki Tanzania katika kila nyanja , kwanzia mtandao wa biashara haramu , biashara halali na kisiasa , hii itaifanya familia yake kuwa ya kifalme na raisi ni kama waziri mkuu tu anaepokea maagizo kutoka kwao”
“Kama ndio anachowaza anajidanganya , kuna mifano mingi ya kihistoria ni ngumu sana kuuchimba msingi wa nchi na kutengeneza nyufa pasipo kushitua wamiliki wake”
“Pengine anaelewa ila anaona ni kheri kujaribu kuliko kufa bila ya kujaribu”
“Kwahio baada ya kuona familia ya mzee Benjamini imekwama njia pekee alioona ni kumuua Regina maana urithi utaenda kwa mtoto wa pili?”
“Ndio lakini mipango yake inaonekana kukwama kutokana na uwepo wako , niseme tu umetibua mambo mengi sana , najua hata kunipigia simu ni kutokana na kujua ukaribu wetu na anatangeneza mazingira ya kujihami, lakini kwa wanaojua Mgweno kuna kitu lazima anapanga, walijaribu hadi mbinu ya kutaka kumtengeneza mtu wao ambae yupo karibu zaidi na Regina”Aliongea Dina na kumshangaza kidogo Hamza.
“Unamaanisha wale wazee ambao Regina amewafurumusha?”Aliuliza.
“Huo haukuwa mpango , wale wazee walikuwa wakifahamika tokea kipindi kirefu wapo kinyume na uongozi wa Regina”
“Ni nani ambae walikuwa wakimlenga?”
“Mchepuko wako alieniingiza kwenye matatizo”Aliongea huku akivuta midomo”
“Eliza!?”
Dina alitingisha mabega lakini kabla ya Hamza hajauliza swali lingine mlango wa kuingilai uligongwa kwa nguvu na Lawrence alionekana akiingia kwa pupa.
“Kuna nini Lawrence?”Aliuliza.
“Nimeletewa taarifa muda huu na vijana , Mheshimiwa Jongwe amefariki dunia kwa ajali ya gari na jeshi la polisi limeishikilia familia ya Mzee Seif kama washukiwa namba moja”Aliongea Lawrence na habari ile ilimtoa macho Dina.
“Unamaanisha mgombea wa kiti cha uraisi kupitia chama tawala , Jongwe amefariki, tena kwa ajali , kwanini familia ya mzee Seif ihusishwe kama ni ajali?”Aliongea Dina.
“Inawezekana sio ajali ya kawaida”Aliongea Hamza.
“Kwa maelezo niliopatiwa gari ambayo alikuwa amepanda imelipuka na ndani yake alikuwa ameambatana na Mzee Martin”Aliongea Lawrence na alivyoongea ni kama alijua taarifa ile itamshitua bosi wake na ilikuwa kweli kwani Dina alijikuta akisimama akiwa kama haamini.
“Mzee Seif na Mzee Martini mbona kama ushawahi kunitajia hawa watu?”Aliuliza Hamza.
“Ndio Bro hawa ndio washirika wetu wakubwa, japo mara nyingi inaaminika Mzee Seif ana uadui wa kisiasa na Mzee Martini”Aliongea Lawrence.
“Kwanini inaaminika hivyo ?”
“Kwasababu wote ni wanasiasa wa vyama tofauti , Mzee Seif ni kutokea chama cha upinzani na Martini ni kutoka chama tawala na wamekuwa wakipishana kama wabunge katika jimbo moja kwa zamu , uchaguzi huu akishika mzee Martini mwaka mwingine anashika Mzee Seif , awamu hii inayoisha Mzee Seif anamaliza muda wake lakini uelekeo wa kura upo upande wa Mzee Martini , siasa zao mara nyingi ni za kurushiana maneno”Aliongea Lawrence.
“Kwahio jeshi limemkamata Mzee Seif kwa kuamini kwamba ametegesha bomu katika gari la Mzee Martini ili ashinde uchaguzi , kama ni hivyo mgombea wa uraisi wa chama tawala kwanini amekufa pamoja na Martini?”Aliuliza Hamza lakini ni kama alikuwa akiipata picha.
“Lazima kuna kitu Mgweno anajaribu kufanya , hizi zote ni hila za kutaka kubomoa mtandao wa Chatu”Aliongea Dina kwa hasira.
“Lakini Madam Mheshimiwa Jongwe ni mgombea ambae amepata sapoti kubwa kutoka kwa mheshimiwa Mgweno , kwanini afanye hila ya kumuua mgombea ilihali zimebakia wiki chache kabla ya wananchi kupiga kura”
“Kesho kutwa pia ndio ilitarajiwa mkutano wa mwisho wa chama tawala kufanyika ili kufunga kampeni”Aliendelea kuongea Lawrence.
“Kuna picha inanijia akilini”Aliongea Hamza lakini upande wa Dina alionekana kuwa katika majonzi ya kumpoteza Mzee Martini, alikuwa ni moja ya mhimili wa mtandao wake.
“Lawrence polisi wanamshikilia kituo gani Mzee Seif?”
“Nasikia hawajamkamata bali wameizingira nyumba yake huko Kigamboni Mbutu B”Aliongea Lawrence.
“Yaani baada ya dakika kadhaa mlipuko kutokea na kuua watu, tayari washafikia maamuzi Mzee Seif ndio muhusika , mbona haingii akilini , hii lazima ni njama ya kutaka sisi twende tukamsaidie”Aliongea Dina.
“Tena nina uhakika hata hao wanaoitwa polisi ni feki”Aliongea Hamza huku akiweka kijiko chini.
“Madam tunapaswa kufanya nini?”Aliuliza Lau.
“Kama ninachofikiria ni sahihi lazima hili linahusiana na kikao nilichofanya na mheshimiwa Mgweno siku kadhaa zilizopita , mtandao wetu wote unajua ni kwa namna gani Mzee Seif alikuwa mwaminifu , nisipoingilia na kulifanyia hili maamuzi unadhani nitaonekanaje , Lawrence kusanya vijana wote ambao hawako mbali tutaenda kuangalai kinachoendelea”Aliongea Dina.
“Lakini Madam ulitoa maelekezo ya vijana karibia wote wakae chimbo , waliopo karibu na mjini hawazidi hata hamsini?”
“Haina haja”Aliongea Hamza huku akisimama.
“Watu hamsini ni wengi sana na hili linaweza kuwa ni mtego , hebu ita wale kumi kutoka jumba la mazoezi waje hapa , wanatosha sana”
“Bro unataka na wewe…”
“Hamza na wewe unataka kwenda?”
“Nataka nikajionee kinachoendelea , kama kweli huu mpango kaupanga Mgweno basi atakuwa katumia akili , unadhani kwa katiba yao ya chama nini kinafuata mara baada ya mgombea mkuu wa chama kufariki ghafla?”Aliuliza Hamza.





SEHEMU YA 62.
“Sijui kuhusu katiba yao inachosema , ila nina uhakika mgombea Mwenza ndio atachukua nafasi, kwanini unauliza?”Aliuliza tena Dina maana alijua Hamza hakuwa mtu wa siasa.
“Nawaza kuna mchezo unaochezwa hapa na kuna nguvu mbili kubwa za kisiasa , nataka kujionea mwenyewe”Aliongea Hamza na Dina alitingisha kichwa , kwasababu Hamza alitaka kwenda hakuona haja ya kumzuia , isitoshe ilimpelekea kujiamini zaidi kudili na hali kama hio.
Upande wa Dina alijua lazima kuna mchezo unaofanywa na kama Mzee Seif atakubali kuhusika moja kwa moja itaaminika mtandao wake ndio umekamilisha swala hilo , jambo ambalo hakautaka litokee.
Nyumba ya Mzee Seif ilikuwa Kigamboni Mbutu B na gari mbili ziliendeshwa kuelekea huko ya mbele akiwemo Hamza na Dina na ya nyuma ilikuwa Noah iliowabeba Lawrence na kundi lake.
Kitendo cha kufika eneo la tukio waliweza kuona watu walioizingira nyumba ya Mzee Seif , jambo ambalo liliwashangazwa hakukuwa na uwepo wa polisi hata mmoja ni kama Hamza alivyotarajia.
“Mbona sio polisi kama taarifa ilivyosema?”Aliuliza Dina kama kwamba Hamza alikuwa na majibu.
Hamza alichunguza eneo lote hasa wale watu walioshikilia siraha na alijikuta akikunja sura mara baada ya kuona wazungu wawili ndani ya eneo lile wakiwa ni sehemu ya watu waliozunguka nyumba hio.
“Ni kama nilivyotarajia kuna kinachoendelea hapa”Aliongea Hamza.
“Lakini kama kweli walikuwa wakimshuku Mzee Seif kulipua gari ya mheshimiwa Jongwe kwanini hawajaja polisi?”Aliuliza.
“Tutapata majibu yote mara baada ya kuongea nao”Aliongea Hamza huku akitangulia kutoka nje ya gari.
Wale watu kama walinzi walioshikilia siraha wakiwa wamezingira nyuma hio waliongeza umakini kwa Dina na kundi lake.
“Kama tabia yako ya siku zote, Dina mrembo wa kujiamini , naona umekuja na watu wachache mno tofauti na nilivyotegemea”Sauti ya mwanaume ilisikika kwasababau ilikuwa kuna giza hawakumuona vizuri na mara baada ya kusogelea taa za mwanga wa gari ndio Dina aliweza kumuona.
“Pancho!, unafanya nini hapa?”Aliongea Dina na muda huo ni kama sasa alishaanza kupata picha ya kile kinachoendelea.
“Nimekuja kukusalimia kwa mara nyingine mara baada ya kukataa pendekezo ya dili nono”Aliongea na muda ule alitoa ishara na baada ya kupita dakika mmoja tu wanaume wanne walitoka katika nyumba hio na moja wapo ya wanaume wale alikuwa ni Mzee Seif alieshikiliwa na wanaume wawili weusi waliojazia mwili , mtu wa mwisho kutoka alikuwa ni Mzungu- Mjapani , yaani mtu aliechanganya rangi ya mjapani na Mzungu.
Kilichomfanya Dina kuanza kupandwa na hasira alijua mpango wote huu ulisukwa na Pancho.
Pancho alikuwa ni moja ya wasimamizi wa mtandao wao upande wa Congo na siku kadhaa nyuma Dina alipokea dili kupitia kwa Pancho kutoka kwa Wacanada ambao walitaka kuingiza siraha za kivita Congo kupitia Bandari ya Mtwara.
Dili hili liliungwa mkono na Mheshimiwa Mgweno lakini Dina aliona halikuwa na maslahi na kama angelikubali ni kama kujipiga risasi mguuni, ikizingatiwa siraha hizo zilipaswa kufikishwa kwa kundi lingine la waasi ndani ya Congo tofauti na lile ambalo wanashirikiana nalo kwa muda mrefu.
“Mzee Seif nini kimetokea , kwanini taarifa nilizopokea ni wewe kuhusika na kumuua Mzee Martini na mheshimiwa Jongwe?”Aliuliza Dina akimpotezea Pancho.
“Hawa ndio wahusika , wameiteka familia yangu na wanataka nikiri kuhusika kwa kushirikiana na wewe kumuua Jongwe au turejee mezani na kuanza mazungumzo ya kuingiza siraha Tanzania kwenda Congo”Aliongea Mzee Seif aliekuwa na hali ya hofu na kumfanya Pancho kutoa tabasamu.
“Pancho unajaribu kufanya nini , nani yupo nyuma yako?”
“Dina hakuna ambae yupo nyuma yangu?”Aliongea Pancho kwa kejeli.
“Kwa kumuua mgombea wa uraisi kupitia chama tawala, unasema hakuna ambae yupo nyuma yako?”Aliongea Dina kwa hasira na kumfanya Pancho kutoa tabasamu la kifedhuli.
“Nilitaka hili swala angalau ulichukulie kwa uzito wake, ushahidi wa wewe kuhusika katika shambulizi la kulipua bomu gari ya mgombea wa uraisi kupitia chama tawala upo , unaweza ukawa wa kutengeneza lakini jeshi la polisi lipo tayari kuuamini na kama likitoka uraiani , kitengo cha TISA kitakufanya mbuzi wa kafara, lakini huko kote ni kujisumbua kama upo tayari kuchagua chaguo zuri kati ya matatu alioongea Mzee Seif?”
Hamza muda huo alikuwa akiangalia mazingira yalivyo na watu wote waliokuwa hapo walikuwa na siraha za bunduki na haraka haraka kwa sheria ya Tanzania ilikua ngumu kwa watu hao kumiliki hizo siraha labda iwe kuna mtu ndani ya serikali ambae alikuwa akihusika.
Isitoshe safari yao kutoka kijichi mpaka kufka hapo , kama kweli jeshi la polisi lilikuwa sirasi kukamata watu hao waliomsababishia ajali mgombea wa kiti cha uraisi basi wangeshafika labda tu iwe kuna maagizo ambayo yamewafanya kuchelewa.
“Hizo siraha mnaotaka kuingiza Tanzania mnazitoa wapi?”Aliongea Hamza.
“Oh!, ahsante kwa kuuliza bwana mdogo , kidogo tu nimesahau kumtambulisha bosi wetu hapa , huyu ni Bosi Keita na ndio msingi wa haya maungumzo , kuhusu wapi siraha zinatoka ni juu yake”Aliongea Pancho kwa kujigamba.
“Pancho kama nilivyosema mtandao wetu haudili na maswala ya siraha bila ya utaratibu maalumu, kama unataka dili hili lipite lisimamie wewe mwenyewe na hela zako na sio za mtandao wa Chatu”Aliongea Dina na yule bwana mwenye asili ya kizungu na Kijapani alimpa ishara Pancho ya kuongea yeye.
“Miss Dina kama alivyoongea Pancho tunaweza kulimaliza hili swala kimya kimya na kusiwe na athari zozote kwa kila upande”Aliongea kwa Kingereza.
“Unamaanisha unaweza kuzima kesi ya kulipua gari ya mgombea wa Uraisi pamoja na Martini?”Aliuliza Lawrence.
“Itategemea na maamuzi ya Miss Dina?”
“Kwanini nahisi hata waliompendekeza Jongwe kupeperusha bendera ya Chama ni kama wanashangilia kifo chake?”Aliongea Hamza huku wakati huo Dina akiwa ametulia.
“Tunafanyaje?”Aliuliza Dina akimegemea Hamza , isitoshe ndie aliesema wasije na watu wengi.
“Wana siraha na hata kama tukishambuliana bila siraha hatuwezi kushinda bila kushitua raia , hawa watu wana mafunzo ya mapigano”Aliongea Hamza na kumfanya Dona kuwa na wasiwasi.
“Usiwaze hili naweza kulimaliza kwa amani na kisha utadili nao kujua nini kinaendelea kuhusu mgombea wa uraisi kulipuliwa”Aliongea Hamza na japo Dina alikuwa na wasiwasi aliamua kumwamini Hamza.
“Bwana Keita kwa ninavyojua huwezi kudili na siraha pasipo kuwakilisha shirika la giza unalotokea”Aliongea Hamza akitaka kujua Black Association ambayo Keita anatokea.
“Jungle Army Merchant ndio ninatokea”Aliongea bila ya kusita sita.
“Kumbe ni Jungle , hebu subiri kwanza nipige simu, nikimaliza utaamua cha kufanya”Aliongea.
“Umpigie nani?”
“Utajua nikimaliza’Aliongea Hamza.
“Mr Keita haina haja ya kupoteza muda na hawa watu , swala ni moja tu wachague chaguzi moja kati ya tatu tumalizane”Aliongea Pancho akionekana kukosa uvumilivu.
“Kimya! , sitaki unifundishe namna ya kufanya biashara”Aliongea Keira kwa kingereza na kumfanya Pancho kukaa kimya , isitoshe alikuwa akijua Jungle Army Merchant walikuwa wafanyabiashara wakubwa ndani ya Black Market kwa kuuza siraha za kila namna.
Muda huo Hamza alikuwa ashapiga simu tayari bila ya kuwa na wasiwasi kabisa.
*****
Magneto, Las Vegas- USA
Ni ndani ya jiji la Las Vegas , jiji ambalo kwa wacheza kamari hawakuhesabu muda , Usiku ni kama mchana na Mchana ni kama usiku tu ndani ya hili jiji.
Katika moja ya hoteli ya kifahri ya nyota tano ndani ya chumba cha hadhi ya raisi , alionekana mtu bonge mweusi mwenye kitambi akiwa amelala chali.
Alikuwa mrefu wa mita kama moja nukta tisa hivi , vidole vya mikono yake vilikuwa vimevishwa pete za madini ya almasi , Dhahabu na madini mengine ya thamani , shingoni alikuwa amevalia mikufu ya bei ghali.
Mtu yule bonge alijikuta akitandaza miguu yake vizuri huku akifumba fumba macho na kuyafumbua , katikati ya eneo la mapaja yake alionekana mwanamke mzungu mwenye nywele nyeupe(blonde) akiwa bize kumhudumia.
“Mr Mamen are you comfortable?”Aliuliza yule mwanamke kwa sauti tamu huku akiinua kichwa chake akimwangalia kwa macho malegevu , akimuuliza Big kama ni mwenye kuifurahia huduma.
Mwanaume yule bonge udenda ulikuwa ukitaka kumwagika kutoka kwenye midomo yake , alionekana alikuwa kwenye ulimwengu mwingine wa raha.
“Comfortable..!?, Deeper the better .”Aliongea akimaanisha azame chini zaidi ndio itakuwa vizuri.
“You’re so annoying , I’m realy tired ..”Aliongea yule mwanamke akimwambia anachukiza kwani amekwisha kuchoka.
Bonge yule mweusi kama msanii RickRoss alifungua droo ya meza pembeni na kitanda chake na kuchomoa maburungutu ya pesa za dola na kumtupia.
“Hakikisha najisikia vizuri mpaka kisogoni , nitakupa kiasi chochote cha pesa unachotaka”Aliongea Big na yule mwanamke uchomvu uliisha palepale na alijkuta akiongeza mashambulizi ya kuhakikisha Big anajisikia vizuri.
Dakika hio hio simu yake ilianza kuita , hata simu yake tu ilikuwa imetengenezwa kwa housing ya madini ghali sana na kuifanya ionekane kama kitu kisichokuwa cha kawaida kutokana na uthamani wake
“F*ck , kama ningejua ningeizima hii simu , nani ananipigia muda huu”Big alilaani huku akichukua ile simu na kuipokea maana namba ilikuwa mpya tena haikuwa ya taifa hilo
“Big naona kama kawaida yako sasa hivi unaringa , kwahio unaona sipaswi kukupigia hata kama ni swala linalohusu vita ya tatu ya dunia”Sauti ya kiume ilisikika katika simu ya Big.
Kitendo cha Mameni kusikia ile sauti mwili wake ulitetemeka na macho yake yalibadilika na kuwa mekundu na hata ule msisimko aliokuwa akisikia ulipotea.
Yule mwanamke aliekuwa bize kuhakikisha Big anafurahi alijikuta akipiga kelele mara baada ya kadudu kabig kupotea na kuwa kabamia.
“Boss!! , ni wewe kweli , naona hatimae umenipigia , nimekumisi sana”Aliongea Big huku sauti yake ikiwa imebadilika.
“Unafanya nini hapo , lazima utakuwa na m*laya kitandani , yaani ndio kwanza kunakucha wewe unahangaika na wanawake , kuna siku utafia kwenye kifua cha mwanamke”
“Hehe..Bosi wewe mwenyewe unanijua vizuri , isitoshe wewe ndio mtu pekee ulievunja rekodi yangu”Aliongea.
“F*ck you!”Alitukanwa.
“Bosi nasikia upo Tanzania , habari za siku nyingi , vipi naweza kuja huko?”
“Nina mambo mengi ya kufanya siku hizi tutaona kama unaweza kuja , nyie watu ni wasumbufu sana mkisikia nipo mahali mnataka kuja tu , sitaki usumbufu wenu nahitaji kutulia kwa sasa”
“Bosi kwa uwezo wako na ushawishi wako unaweza kuomba chumba mapumziko Ikulu na ukapatiwa na warembo kabisa , hayo sio mapumziko ila ni kujitia stress tu , mapumziko ni yale wafariji wanakuwa wanabadilika badilika kila siku kwenye kuusisimua mwili”
“Sterehe za kutumia hela hizo nishazichoka , hata nikikuambia ni namna gani nafurahia maisha ya sasa hivi hutonielewa Big”
“Kama ni hivyo bosi kwanini umenipigia simu , kuna dili jipya?”
“Hakuna dili lingine , nishastaafu hayo mambo”
“Sababu ni ipi sasa Bosi , au kuna sehemu nimekosea?”Aliuliza Big kwa upole.
“Kwenye biashara zako unamfahamu bwana anaefahamika kwa jina la Keita?”
“Ndio mwaka juzi niliingia dili na kundi moja linalofanya shughuli zao ndani ya Afrika kuiba madini Adimu na kuyauza kwenda kwenye moja ya kampuni ya maswala ya kiteknolojia nchini Ufaransa , linaongozwa na bwana Keita”Aliongea Big.
“Huyu bwana wako naona ana juhudi mno , muda huu nimeelekezewa mitutu ya bunduki ndio maana nimekupigia simu kuthibitisha , Big kwahio sasa hivi umeshaanza kuwa mkubwa kiasi cha kunisaliti kisa tu nnimetoka kwenye uringo?”
Big mara baada ya kusikia kauli hio kutoka kwa Hamza alijikuta mikono ikimtetemeka kiasi kwamba simu ilitaka kudondoka.
“Bosi , subiri kwanza , nitampigia simu sasa hivi , naomba kwanza nimfokee baada ya hapo unaweza kumuua”Aliongea Big na dakika ileile alikata simu na kuitafuta namba ya Keita.
“Mamen Babe! , unafanya nini sasa mbona imepotea!?”Yule kahaba wa kizungu aliongea lakini Mameni alimpotezea na mara baada ya kuipata namba ya Keita aliipiga palepale.
Mara baada ya Hamza kumaliza kuongea na simu hakuongea neno na alitulia akiangalia matokeo.
Ijapokuwa Keita hakujua Hamza alikuwa akiongea na nani kwenye simu lakini alihisi kuna kitu hakipo sawa.
Dakika ileile simu yake ilianza kuita na alisogea pembeni na kupogea lakini muda huo huo alianza kuonyesha ishara za kupaniki.
Upande wa pili ilikuwa ni sauti ya Big kutukana kimarekani kwa mara nyingi mfululizo kadri alivyoweza.
“Bosi nimefanya kosa gani?”
“Unataka kumuua nani sasa hivi?”
“Bosi umejuaje nataka kuua mtu?”
“Unaetaka kumuua ni bosi wangu”
“…”
Keita alijikuta akikosa neo , alishangaa mno kwa zaidi ya sekunde kumi , ni kama alikuwa akisharabu yale maneno.
“Ah!”
Alijikuta hofu ikimwingia na vigoti vya miguu yake vilianza kumlegea na alijikuta akigeuka na kumwangalia Hamza.
Upande wa Hamza alikuwa akimwangalia Keita tu kwa mbali na kwa jinsi alivyoonyesha kupaniki na woga alitamani kucheka.
“Mr Keita , Mr Keita , what happened?”Pancho aliuliza mara baada ya kuona mabadiliko.
Dina macho yake yalichanua alijua kabisa mabadiliko ya Keita ni kutokana na Hamza alipopiga simu na kwake aliona mwanaume Hamza alikuwa akimshangaza kila siku.
“Nini tatizo Mr Keita , mbona huongei?”Aliuliza Pancho kwa wasiwasi
“Hivi unajua mimi na vijana wangu tutakufa sasa hivi kutokana na ujinga wako na wale wanasiasa wapuuzi?”Aliongea kwa hasira.
“Unamaanisha nini Mr….”
Keita hakuchelewa alichomoa Desert Eagle kutoka kwenye kiuno chake na kumchapa risasi tatu Pancho palepale.
Mpaka Pancho anadondoka chini muonekano wake ulikuwa na shauku ya kutaka kujua kwanini Keita anamshambulia.
Keita mara baada ya kumalizana na Pancho alitoa maagizo kwa vijana wake kuwashambulia watu wa Pancho na walionekana kuwa shapu kweli kwani ndani ya sekunde wote walikuwa chini.
Baada ya Keita kuituliza hali alijikuta akimdondokea Hamza kwa magoti huku akiwa na wasiwasi mwingi akitia huruma.
“Prince Rich.. Bosi wangu ameniambia kila kitu , naomba unisamehe kwa ujinga wangu , sikubahatika kukutana na wewe ana kwa ana zaidi ya kusikia habari zako ndio maana nimekukosea…”
Kitendo kile kiliwashangaza mno Dina , Lawrence na wenzake , waliishia kujiuliza Hamza ni nani mpaka bwana yule kuwa na hofu namna ile kiasi cha kupiga magoti.
“Nipe bastora yako”Aliongea Hamza akiwa siriasi na kumfanya Keita kukakamaa mwili lakini alimpatiia.
‘Tafadhari naomba uwaache vijana wangu waondoke , walikuwa wakifuata maelekezo tu kutoka kwangu na wanazofamilia zinawategemea”Aliongea Keita lakini Hamza hakumjali na muda ule aliinua ile bastora na kujielekezea kwake kana kwamba anataka kujipiga risasi.
Tukio lile lilimshangaza kila mtu wakishindwa kuelewa Hamza anataka kufanya nini
“Hamza unataka kufanya nini , usipaniki..”Aliongea Dina lakini kabla hata hajamaliza Hamza alikuwa ashaachia risasi.
Bam!
Mlipuko ule wa bunduki ulimuogopesha mpaka Keita na wote walimwaangalia Hamza kwa mshangao na walishangaa zaidi baada ya kuona hakuna kilichotokea.
Risasi ambayo ilitoka katika ile bunduki ilikuwa katika vidole vya Hamza , haikueleweka amefanyaje lakini ilionekana aliikamata kabla ya kumfikia, tukio lile lilimfanya Keita kushindwa kuendelea kupiga magoti na kukaa chini kwa kunyoosha miguu huku mapigo yake ya moyo yakidunda kwa kasi.
“Kabla sijafanya chochote nataka muelezee kila kilichotokea… sababu ya kwamba umepiga magoti sio kwasabau ya bosi wako bali ni kwasababu yangu hivyo nataka majibu”Aliongea Hamza.
“Serafii.!!, nipo tayari kuongea”Aliongea Keita huku akipiga kichwa chini kiasi cha kutoka damu kwenye paji la uso.
“Anza kuelezea , kwanini kifo cha Mgombea wa uraisi na nani kahusika”Aliongea Hamza.
“Hatujahusika katika kumuua mtu , tupo hapa nchini kwa ajili ya mazungumzo ya biashara ya kupitisha Siraha Kwenda Congo kupitia bandari ya Mtwara , kitu pekee ambacho nafahamu kuhusu muhusika tulipewa kazi ya kumtorosha hapa nchini kupitia boti yetu”Aliongea na kauli ile ilimfanya Dina kusikiliza kwa umakini.
“Imekuwaje mkajiingiza , sitaki kuuliza maswali mengi elezea kila kitu ninachotaka kujua?”
“Mara ya mwisho nilivyokuja hapa nchini niliweza kukutana na mstaafu Mgweno kwa ajili ya kuingia dili la kupitisha siraha , lakini kutokana na usafirishaji wote wa Kimagendo kuwa chini ya Chatu hakutoa maamuzi badala yake aliwasiliana na Miss Dina ambae mara baada ya kuelekezwa kuhusu dili hili alikataa, Mstaafu baada ya ombi hili kukataliwa alituambia hana namna ya kutusaidia kwani njia pekee ya kupitisha siraha hizo ni moja tu ambayo ni Mtwara kutokana na bandari zote kuwa chini ya mwekezaji”
“Nini kiliendelea”
“Wakati tukifikiria namna ya kutafuta njia nyingine ya kukamilisha dili hili nilipokea simu kutoka kwa mtu ambae alijitambulisha ni msaidizi wa raisi”Aliongea.
“Unamaaniisha Mheshimiwa Eliasi Mbilu?”
“Ndio na alisema anataka kuonana na sisi kwa ajili ya mazungumzo ya namna ya kukamilisha kile tulichokuwa tukihitaji , kutokana na kuwa na haraka ya kufanikisha hili dili nilikubali na kupitia msaidizi wake alinipa maelekezo niwaache vijana na boti yetu nchini Tanzania kwa muda na nikutane nae jijini Kual Lampur nchini Malaysia ndani ya tarehe alionitajia wakati akiwa ziarani”
“Tokea tuzungumze kuhusu hili dili imeshapita mwezi miwili , inamaana huu mpango ulikuwa wa muda mrefu?”
“Inawezekana Miss Dina , kabla ya siku moja ya tarehe kufika , niliweza kufika Malaysia na nilikutana na mheshimiwa kwa siri sana kupitia msaidizi wake na nilitambulishwa kama mwekezaji”Aliongea Keitani kwa kutetemeka.
“Alitaka kuongea nini kwa siri namna hio?”Aliuliza Dina , ijapokuwa Keitani alijua alikuwa akitoa siri kubwa lakini hakuwa na jinsi.
“Aliniambia siku ya leo saa nne kamili za usiku mgombea wa kiti cha uraisi kupitia chama chake atafariki kwa ajali ya gari na atakaesababisha ajali hio napaswa kumtorosha nje ya nchi na kama ikishindikana nimuue kabla ya kukamatwa na polisi, kisha nitumie ushahidi feki wa tukio hilo kuhakikisha nakamilisha dili la kupitisha siraha”
“Ushahidi feki ni kutusingizia sisi ndio wahusika, si ndio?”
‘Ndio”
“Ameenda mbali mpaka kutengeneza ushahidi feki , yeye anafaidika nini katika hilo?”Aliuliza Lawrence.
“Kila kitu kipo wazi , naamini Jongwe sio chaguo lake na pili alitaka kujitengenezea njia za kupata maslahi hata akiwa amestaafu kupitia hili dili”Aliongea Hamza.
“Ndio , alitaka asilimia ishirini ya faida itakayopatikana na wakati huo huo Mgombea wa uraisi akiwa ni chaguo lake baada ya chaguo la Mgweno kufariki”Aliongea keita na kumfanya Dina sura kujikunja
“Mgweno na Eliasi wanataka kupinduana , madaraka huwa ni matamu sana”Aliongea Dina lakini upande wa Hamza hakujali nani anampindua nani.
“Vipi kuhusu muuaji ni nani?”
“Kuhusu mfungwa hatuna taarifa nyingi kuhusu yeye , tulipatiwa picha pekee na tuliambiwa ni mfungwa wa kidiplomasia aliefungwa kwa muda mrefu kwa siri”
“Yuko wapi kwasasa?”Aliuliza Hamza.
“Ametoweka mara baada ya tukio, tunaamini alikuwa na mpango wake binafsi wa kujitorosha baada ya kukamilisha misheni”Aliongea na kumfanya Hamza kuvuta pumzi.
“Picha yake ipo wapi”Aliuliza Hamza na Keita alimpa ishara bwana moja wa kizungu na alimsogezea Hamza simu na ilionekana picha ya mfungwa kwenye kioo cha simu na mara baada ya kuiangalia alijikuta macho yake yakichanua.
“What the f*ck!!”
Hamza alijikuta akitoa tusi na kumfanya Dina kusogea kuangalia picha hio ili kujua kwanini kashangaa.
ITAENDELEA.
Watsapp me kwa mwendelezo wa haraka haraka namba 0687151346

Umerudia
 
SHETANI RUDISHA AKILI ZETU

MTUNZI: SINGANOJR

SEASON 03
SEHEMU YA 61.
Frida alijua kabisa anakwenda kufa na kifo chake kuja kuwa utata , aliweza kuona kilichokuwa kimemkaba kooni ni kivuli lakini hakuweza kufanya chochote.
Kwa mtu wa kawaida unaweza useme Frida alikuwa amepatwa na ukichaa au ugonjwa wa ajabu lakini ukweli ni kwamba kuna nguvu iliokuwa ikimkaba kupitia kivuli.
Wakati akiwa amekata tamaa ghafla tu ule utulivu wa kile chumba ulitoweka , ilikuwa ni kama upepo umeongezeka kwa kiasi kikubwa na kufumba na kufumbua kivuli kile kilipotea na kumfanya Frida kuanza kukohoa kwa nguvu , mpaka anakuja kutulia alijikuta akishituka mara baada ya kugundua kuna mtu mwingine ndani ya chumba chake alievalia joho la rangi nyeusi, alitaka kupiga yowe lakini mtu yule alimpa ishara ya kutulia.
“Wewe ni nani?”Aliuliza Frida kwa sauti ya chini huku akiwa ameshika shingo yake , ilikuwa bado hakuamini kama alikuwa amepona.
“Msimamizi wako na mlinzi wako mpya”Aliongea kwa lugha ya kingereza na kumfanya Frida kuchangayikiwa.
“Sikuwa na msimamizi na mlinzi , kwanini unajitambulisha kama mlinzi wangu mpya , nataka kujua unatokea upande upi , Wiccan au Sinagogu?”Aliongea Frida kwa sauti kubwa kidogo.
“Mimi ni mu’ alkemi kutoka makao makuu ya Wiccan , nipo hapa kwa maagizo ya Madame, mlinzi wako wa zamani amepoteza maisha”Aliongea na kumfanya Frida kuzidi kuchanganyikiwa lakini mara baada ya kusikia mtu huyo yupo hapo kwa maagizo ya Madame alipata ahueni.
“Mlinzi wangu wa zamani , unamaanisha mlinzi gani?”
“Alietaka kukuua amemuua mlinzi wako , kwanzia sasa utakuwa chini ya ulinzi wa binadamu”Aliongea huku akisogea karibu na mlango.
“Nilikuwa na mlinzi kivuli!!?”
“Wewe ni wa muhimu sana kwa Madame kuwasiliana na waumini wa ulimwengu wa nje ya kivuli , kwa namna yoyote unapaswa kuwa salama”Aliongea.
“Kwanini alitaka kuniua?”Aliuliza Frida, alikuwa akijua mtu ambae alitaka kumuua ni kivuli au watu ambao wamepata umaarufu kwa jina la Night Shadows(Vivuli vya watu vinavyoonekana usiku).
“Sina majibu kuhusu swali lako lakini nina ujumbe kutoka makao makuu”Aliongea kama roboti.
“Ujumbe gani?”
“Hakikisha anatumia mshumaa kurekodi ndoto zake ndio utakuwa salama, kadri atakavyoota bila ndoto zake kurekodiwa mtiririko wa matukio utakosekana na mpango wote kuingia dosari”Aliongea.
“Unamaanisha Ha…”
“Sikutajiwa jina , huu ndio ujumbe kutoka makao makuu unaopaswa kufanyia kazi”Aliongea yule bwana. Frida alitaka kuuliza swali zaidi lakini alijua asingepata majibu.
Yule bwana alievalia joho la rangi nyeusi mara baada ya kuridhika kwa kuona Frida alikuwa ameelewa aliaga.
“Wakati wowote ukiwa katika hatari na kuhitaji msaada wangu tamka neno , Grishav nitaitikia wito wako”Aliongea na palepale bila ya Frida kujibu aliinama chini na kufumba na kufumbua alipotea.
Frida alijikuta akiingia katika maswali mengi na swali kubwa lilikuwa juu ya ule mshumaa , alijua maelekezo yale yalikuwa yakimlenga Hamza lakini alishangaa mara baada ya kuambiwa Hamza anapaswa kutumia mshumaa ule ili kurekodi ndoto zake.
Swali ambalo alijiuliza inakuwaje mshumaa ambao alipatiwa na Dokta Genesha kuwa na uwezo wa kurekodi ndoto , kitu ambacho Wiccan walitaka iwe hivyo , inamaana kuna mpango uliokuwa ukiendelea kati ya Dokta Genesha na Wiccan kiasi cha kumkabidhi Mshumaa wa Nuru kwa ajili ya kumpatia Hamza.
Frida alijiuliza ni kitu gani ambacho kinaendelea yeye hakijui na kwanini amenusurika katika kifo.
Alikumbuka kwamba asipofanikisha Hamza kutotumia mshumaa basi atakuwa hatarini lakini swali lingine liliibuka inamaana Hamza alikuwa akiota bila ya kutumia ule mshumaa.
Kitu ambacho Frida alikuwa akijua ni kwamba mshumaa ule ulikuwa ni kwa ajili ya kumletea Hamza ndoto tu ili kujua maisha yake ambayo ameyasahau , hayo ndio yalikuwa maelekezo kutoka kwa Dokta Genesha na hakuelezwa kwamba mshumaa ule ni kifaa cha kurekodi ndoto, alijiuliza kama ni hivyo kinarekodi vipi hizo ndoto , ni sayansi ya namna gani ambayo imetumika.
Alijikuta hata usingizi ukimpelea kabisa licha ya kwamba alijihisi uchomvu mkubwa , hofu ilimvaa na hisia zake zilimwambia pengine anachofanya sio kuhatarisha usalama wake tu bali anahatarisha na usalama wa Hamza.
“Sina jinsi kwasasa lazima nihakikishe Hamza anatumia mshumaa ili kuwa salama , wakati nikitafuta majibu ya maswali yangu yote. Lakini nitafanya nini kumfanya atumie mshumaa kama yeye mwenyewe haniamini vya kutosha mpaka kuutumia?”Aliwaza Frida.
******
Hamza mara baada ya Side na wenzake kuondoka alibakia na mrembo Dina , wote wawili hawakuwa na ile mudi ya kwenda floor za juu kwa ajili ya kulewa vileo na kufanya starehe zingine kama kucheza kamari.
Kitu pekee ambacho Dina alipenda ndani ya Club hio ni kutumia siraha kulenga shabaha na hata Hamza alikuwa akipenda kitu kama hiko , kwake hakuwa mpenzi sana wa vileo na kucheza disco.
Walitumia zaidi ya lisaa limoja na nusu kulenga shabaha kwa kutumia bunduki za aina mbalimbali.
Ilipotimia saa tano kasoro njaa zilikuwa zikiwauma na Hamza alipendekeza warudi Kijichi ndio wakapate chakula huko na Dina hakupiinga.
Mara baada ya kufika kijichi chakula kiliandaliwa na wote wakaanza kula pamoja.
“Unaonaje baada ya hapa ukaangalie maendeleo ya vijana wangu , tokea siku ile ulivyowafundisha kiasi namna ya kucheza Karate na Kung Fu hukuwaona tena”Aliongea Dina.
Hamza kipindi kabla ya kukutana na Regina alikuwa ameshawahi kuwafundisha vijana wa Dina mafunzo ya Karate na Kung Fu mara moja na hakuwahi kwenda tena kuwaona.
“Hakuna shida , kuna kitu pia nataka kwenda kukifanyia mazoezi”Aliongea Hamza.
“Kitu gani , ni kuvuna nishati za mbingu na ardhi au kitu kingine?”Aliuliza Dina kwa shauku alikuwa akijua Hamza ana mafunzo ya kuvuna nishati za nguvu ya asili ya ardhi na mbingu na alitamani kujifunza pia siku moja.
“Hutoelewa hata nikikuambia ni kama maneno ya kutamka nataka kuyafanyia majaribio”Aliongea Hamza.
Ukweli ni kwamba kitu ambacho alikuwa akienda kufanyia majaribio ni yale maneno ambayo Yonesi alimtajia wakati akiwa hospitalini , siku ile wakati akifanya tahajudi kwa kupitia yale maneno aliona sura ya mwanamke ambae anamuona katika ndoto , bado shauku yake juu ya tukio lile haikuwa imeisha na alitaka kwenda kujaribu tena.

Baada ya kumaliza kula Hamza alitoka akiongozana na Dina pamoja na Lawrence na kwenda katika ukumbi maalumu ambao ni kama eneo la mafunzo ya kimapigano.
Hakukuwa na matumizi ya siraha , ilikuwa ni sehemu ambayo watu wa Dina walikuwa wakijifunza namna ya kupigana kwa kutumia mbinu mbalimbali za sanaa ya mapigano , eneo hilo lilikuwa likitambulika hata kwa serikali na lilikuwa na kibali kabisa.
Ni eneo ambalo lilijengwa katika mgawanyo wa sehemu mbili , sehemu ya kwanza ilikuwa ni kwa kufanyia mazoezi ya kawaida kama Gym na mazoezi ya boksa, Karate na Judo upande mwingine ulikuwa ni wa tahajudi.
Katika sanaa ya mapigano tahajudi ilikuwa ni sehemu ya mazoezi kwa ajili ya kuujua mwili wako ulivo, ukifanya tahajudi kama binadamu utajuwa wapi kuna udhaifu wako na wapi nguvu zako zinakaa kwa wingi na namna gani ya kushinda udhaifu wako.
Hamza mara baada ya kuona vijana wa Dina wakichukua mazoezi aliridhika , aliweza kuona wengi walikuwa wamepiga hatua kwa kufuata maelekezo yake.
“Bro , unapanga kufanya mazoezi ya namna gani , unataka kufanya tahajudi?”Aliuliza Lauwrence mara baada ya kumuona Hamza akichagua upande wa wanaofanya Tahajudi.
Dina na Lawrence siku zote walikuwa na shauku ya kutaka kumuona Hamza akichukua mazoezi hivyo walimwangalia.
“Kaa kimya Lau acha maswali mengi”Aliongea Dina akimzuia Lau kutokumsumbua Hamza na maswali yake.
Kutokana na wale wanafunzi kumuona Hamza na wao wote waliacha na kumpatia Hamza nafasi , kwao ni kama kuna kitu ambacho walitaka kujifunza kwa kumuangalia ndio maana walisimama pembeni.

Wakati Hamza akiwa katika mkao wa kufanya tahajudi huku midomo yake ikicheza ghafla tu watu wote walijikuta wakikumbwa na msisimko wa ajabu , ilikuwa ni kama kuna kiumbe cha ajabu kimefika ndani ya eneo hilo na kuwafanya kuanza kushindwa hata kupumua vizuri huku eneo ambalo Hamza alikuwa amekaa anga lake ni kama lilikuwa likitingishika.
Dina alijikuta jasho la paji la uso likimtoka huku akimwangalia Hamza kwa wasiwasi , alipatwa na hisia kama vile Hamza amekuwa mfalme ghafla na yeye ni kijakazi wake.
Upande wa Hamza hakuwa hata akielewa kilichokuwa kikiendelea kwa nje , kama alivyotarajia maneno yale yalikuwa ni kama anamwita yule mwanamke , mara ya kwanza wakati alivyofanya kule wodini alimuona kwa mbali yule mwanamke , lakini wakati huo kadri alivyokuwa akiimarisha umakini wake wa ubongo na kuzidi kuyatamka yale maneno alimuona ni kama vile yule mwanamke mchawi anaemuona kwenye ndoto alikuwa akimsogelea kutoka angani kwa spidi ya ajabu.
Zilipita kama dakika nne tu yule mwanamke aliweza kumuona kwa ukaribu zaidi, lakini jambo ambalo lilimshangaza Hamza ni kitu ambacho alikuwa ameshikilia mkononi.
Kadri alivyokuwa akizidi kuongea yale maneno mwanamke yule alizidi kusogea , lakini ilifikia hatua ni kama hawezi kumfanya asogee zaidi na yule mwanamke ni kama alijua Hamza hawezi kumuita karibu zaidi na alichokifanya ilikuwa ni kunyoosha kile kitu alichoshikilia mkononi mwake na Hamza mara baada ya kuangalia vizuri alijikuta akipagwa , ulikuwa ni ule mshumaa ambao Frida alimpatia akimwambia umetoka kwa Dokta Genesha, Mshumaa wa Nuru.
Hamza alichanganyikiwa mshumaa wa nuru kwanini upo katika mikono ya huyo mwanamke , katika ndoto yule mwanake alimuona kama mchawi ambae anachomwa moto baada ya kukamatika lakini kwanini akashika kitu cha nuru ilihali nuru na uchawi ni vitu viwili tofauti.
Yule mwanamke ni kama alikuwa akitaka Hamza amsogeze karibu aweze kushika ule mshumaa , upande wa Hamza alionekana kusita kuupokea ule mshumaa na yule mwanamke ni kama aliliona hilo na alitamka neno kwa kunyanyua mdomo wake kwa juu bila kutoa sauti akihakikisha Hamza anasoma lipsi zake.
NISAIDIE!(Help me)
Ndio neno ambalo aliongea huku akimpa ishara Hamza kupokea ule mshumaa.
Muda uleule Hamza aliacha kutamka yale maneno na kitendo kile kilifanya yule mwanamke ni kama vile kuna nguvu iliokuwa ikimvuta na kuzidi kurudishwa nyuma mbali na yeye , lakini bado hakuacha kumnyooshea ule mshumaa kama ishara ya kumuomba amsaidie.
Muda ileule wakati kila mtu akiwa ameloa jasho kana kwamba eneo lote limekumbwa na joto kali Hamza aliweza kufungua macho yake huku akionyesha hali ya kuwashangaa waliokuwa wakimwangalia .
“Nini kimetokea, Dina mbona upo hivyo?”Aliuliza Hamza mara baada ya kumuona
“Bado tu unapata muda wa kuuliza , ni kitu gani ulichokuwa ukifanya?”Aliuliza Dina na kumfanya Hamza sasa kuelewa kilichokuwa kikiendelea , licha ya yeye mwenyewe kuwa na wasiwasi lakini aliishia kucheka.
“I am sorry !, hii ni mara yangu ya kwanza kujaribisha hiki kitu , sikuweza kujizuia kile kinachonizunguka”AliongeaHamza na kisha alipiga hatua kuondoka katika eneo hilo.
Na wakati wakianza kutembea ndio sasa waligundua paa la jengo hili lilitingishika sana na kutokana na mchwa kula mbao unga unga ulidondoka chini kwenye tailizi na kila walipokuwa wakipiga hatua walikuwa wakiacha nyuma alama za miguu.
“Muda umeenda sana , nataka nirudi nyumbani”Aliongea Hamza.
“Hamza ni mafunzo gani yale , ni nguvu ya ndani au nishati ya mbingu na maji?”
“Ilianza mbingu ikaja ardhi halafu mbingu ikaleta maji na uhai , hizi ni kanuni za mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi na ni kitu ninachoweza kufanya pia , lakini kuhusu nilichofanya sasa hivi hata sijui ni kitu gani , kama nilivyosema nipo kwenye utafiti”Aliongea Hamza
“Hata jina lake hujui?”Aliuliza Dina kwa mshangao.
“Ndio ila kwasasa nitaiita hii kama Wito, kwasababu ukiifanya ni kama kuna kitu unakiiita”
“Huwa haifurahishi kusikiliza pekee”Aliongea Dina kwa macho yaliojaa huzuni na shauku.
“Usiongee hivyo , hiki ni kitu ambacho siwezi kukuruhusu ufanye kabla sijakipatia majibu , nguvu yake ni kubwa kiasi kwamba ni kama sijakula kabisa”Aliongea Hamza huku akijihisi ni mwenye njaa kali.
Dina alimwambia twende ukale na Hamza hakuwa na aibu ya kukataa kwani alikuwa na njaa , muda huo hawakurudi kwenye mgahawa bali Hamza alienda mpaka yalipo makazi ya Dina mita kadhaa kutoka mgahawa wake ulipo na mfanyakazi aliagizwa kuandaa chakula na Hamza alikaa chini na kuanza kukifakamia huku Dina akimwangalia kwa macho yaliojaa mahaba.
“Unajua nilishangaa baada ya mstaafu Mgweno kunipigia simu akisema yaishe”Aliongea Dina.
“Kwanini yeye ndio kakupigia simu?”,
“Unaweza kushangaa , licha ya kwamba kwa nje inaonekana familia ya Benjamini ndio inataka Regina kuolewa na James lakini upange mwingine ni mipango ya Mheshimiwa Mgweno”Aliongea Dina.
“Unataka kumaanisha nini?”
“Labda utakuwa hujui tu , ila kampuni ya Dosam ni kubwa Tanzania na inachangia zaidi ya asilimia tatu ya pato lote la Taifa , imeshikilia uchumi wa nchi katika maeneo nyeti, Benki namba moja ya kibiashara inayoongoza kwa Tanzania na Afrika mashariki yote ni Dosam Commercial Bank huu ni kama utawala wa mzunguko wa fedha nchini , hapa bado hujazungumzia usafiri wa anga , mahoteli na usambazaji wa bidhaa mbalimbali kwa matumizi ya majumbani, Kabla ya mheshimiwa Mgweno hajaingia madarakani Kampuni ya Zena ilikuwa ya kawaida tu kulinganisha na Dosam lakini baada ya Mgweno kuingia madarakani ilikua kwa spidi ya hali ya juu na yote hii ilikuwa ni uwekezaji mkubwa ambao mheshimiwa alifanya kwa kuiba hela za wananchi”Aliongea Dina.
“Kwahio unachomaanisha ni kwamba kampuni ya Zena inamilikiwa na Mheshimiwa mstaafu Mgweno?”
“Ndio kwa asilimia zaidi ya arobaini na tisa, ukifuatilia wana hisa wa kampuni ya Zena utagundua wengi wanaomiliki hisa hizo ni kampuni kutoka nje ya nchi , ukifuatilia kampuni hizo nje ya nchi utagundua kwamba ni kampiuni ambazo zimepewa haki kisheria ya kumiliki hisa hizo na kampuni nyingine , mzunguko unaendelea hivyo hivyo, zote ni njama za Mgweno kuficha wananchi kwamba anaimiliki Zena , sio kampuni moja tu , kila kampuni kubwa ana ushawishi wa kimaamuzi”
“Zote hizo ni hela za rushwa!?”
“Ndio lakini hakuna ushahidi wa kuthibitisha kama ndio mmiliki, sehemu pekee ambapo amekosa umiliki na ushawishi ni kampiuni ya Dosam peke yake na hii ni kutokana na msimamo wa aliekuwa kuongozi wa kampuni yaani babu yake Regina”Aliongea Dina na sasa ni kama Hamza alikuwa akipata picha.
“Kwahio anajaribu kuitumia familia ya Benjamini kwa ajili ya kuingiza ushawishi wake katika kampuni ya Dosam?”
“Ipo hivyo , mwanzoni walijua mambo yataenda sawa kama Regina atakubali kuolewa na James lakini mambo yamekuwa magumu , Regina karithi tabia zote za waanzilishi wa ile kampuni”
“Unamaanisha bibi yake na babu yake, unachoongea kinaonekana kuwa sahihi”Aliongea Hamza.
“Mgweno anachotaka ni kuimiliki Tanzania katika kila nyanja , kwanzia mtandao wa biashara haramu , biashara halali na kisiasa , hii itaifanya familia yake kuwa ya kifalme na raisi ni kama waziri mkuu tu anaepokea maagizo kutoka kwao”
“Kama ndio anachowaza anajidanganya , kuna mifano mingi ya kihistoria ni ngumu sana kuuchimba msingi wa nchi na kutengeneza nyufa pasipo kushitua wamiliki wake”
“Pengine anaelewa ila anaona ni kheri kujaribu kuliko kufa bila ya kujaribu”
“Kwahio baada ya kuona familia ya mzee Benjamini imekwama njia pekee alioona ni kumuua Regina maana urithi utaenda kwa mtoto wa pili?”
“Ndio lakini mipango yake inaonekana kukwama kutokana na uwepo wako , niseme tu umetibua mambo mengi sana , najua hata kunipigia simu ni kutokana na kujua ukaribu wetu na anatangeneza mazingira ya kujihami, lakini kwa wanaojua Mgweno kuna kitu lazima anapanga, walijaribu hadi mbinu ya kutaka kumtengeneza mtu wao ambae yupo karibu zaidi na Regina”Aliongea Dina na kumshangaza kidogo Hamza.
“Unamaanisha wale wazee ambao Regina amewafurumusha?”Aliuliza.
“Huo haukuwa mpango , wale wazee walikuwa wakifahamika tokea kipindi kirefu wapo kinyume na uongozi wa Regina”
“Ni nani ambae walikuwa wakimlenga?”
“Mchepuko wako alieniingiza kwenye matatizo”Aliongea huku akivuta midomo”
“Eliza!?”
Dina alitingisha mabega lakini kabla ya Hamza hajauliza swali lingine mlango wa kuingilai uligongwa kwa nguvu na Lawrence alionekana akiingia kwa pupa.
“Kuna nini Lawrence?”Aliuliza.
“Nimeletewa taarifa muda huu na vijana , Mheshimiwa Jongwe amefariki dunia kwa ajali ya gari na jeshi la polisi limeishikilia familia ya Mzee Seif kama washukiwa namba moja”Aliongea Lawrence na habari ile ilimtoa macho Dina.
“Unamaanisha mgombea wa kiti cha uraisi kupitia chama tawala , Jongwe amefariki, tena kwa ajali , kwanini familia ya mzee Seif ihusishwe kama ni ajali?”Aliongea Dina.
“Inawezekana sio ajali ya kawaida”Aliongea Hamza.
“Kwa maelezo niliopatiwa gari ambayo alikuwa amepanda imelipuka na ndani yake alikuwa ameambatana na Mzee Martin”Aliongea Lawrence na alivyoongea ni kama alijua taarifa ile itamshitua bosi wake na ilikuwa kweli kwani Dina alijikuta akisimama akiwa kama haamini.
“Mzee Seif na Mzee Martini mbona kama ushawahi kunitajia hawa watu?”Aliuliza Hamza.
“Ndio Bro hawa ndio washirika wetu wakubwa, japo mara nyingi inaaminika Mzee Seif ana uadui wa kisiasa na Mzee Martini”Aliongea Lawrence.
“Kwanini inaaminika hivyo ?”
“Kwasababu wote ni wanasiasa wa vyama tofauti , Mzee Seif ni kutokea chama cha upinzani na Martini ni kutoka chama tawala na wamekuwa wakipishana kama wabunge katika jimbo moja kwa zamu , uchaguzi huu akishika mzee Martini mwaka mwingine anashika Mzee Seif , awamu hii inayoisha Mzee Seif anamaliza muda wake lakini uelekeo wa kura upo upande wa Mzee Martini , siasa zao mara nyingi ni za kurushiana maneno”Aliongea Lawrence.
“Kwahio jeshi limemkamata Mzee Seif kwa kuamini kwamba ametegesha bomu katika gari la Mzee Martini ili ashinde uchaguzi , kama ni hivyo mgombea wa uraisi wa chama tawala kwanini amekufa pamoja na Martini?”Aliuliza Hamza lakini ni kama alikuwa akiipata picha.
“Lazima kuna kitu Mgweno anajaribu kufanya , hizi zote ni hila za kutaka kubomoa mtandao wa Chatu”Aliongea Dina kwa hasira.
“Lakini Madam Mheshimiwa Jongwe ni mgombea ambae amepata sapoti kubwa kutoka kwa mheshimiwa Mgweno , kwanini afanye hila ya kumuua mgombea ilihali zimebakia wiki chache kabla ya wananchi kupiga kura”
“Kesho kutwa pia ndio ilitarajiwa mkutano wa mwisho wa chama tawala kufanyika ili kufunga kampeni”Aliendelea kuongea Lawrence.
“Kuna picha inanijia akilini”Aliongea Hamza lakini upande wa Dina alionekana kuwa katika majonzi ya kumpoteza Mzee Martini, alikuwa ni moja ya mhimili wa mtandao wake.
“Lawrence polisi wanamshikilia kituo gani Mzee Seif?”
“Nasikia hawajamkamata bali wameizingira nyumba yake huko Kigamboni Mbutu B”Aliongea Lawrence.
“Yaani baada ya dakika kadhaa mlipuko kutokea na kuua watu, tayari washafikia maamuzi Mzee Seif ndio muhusika , mbona haingii akilini , hii lazima ni njama ya kutaka sisi twende tukamsaidie”Aliongea Dina.
“Tena nina uhakika hata hao wanaoitwa polisi ni feki”Aliongea Hamza huku akiweka kijiko chini.
“Madam tunapaswa kufanya nini?”Aliuliza Lau.
“Kama ninachofikiria ni sahihi lazima hili linahusiana na kikao nilichofanya na mheshimiwa Mgweno siku kadhaa zilizopita , mtandao wetu wote unajua ni kwa namna gani Mzee Seif alikuwa mwaminifu , nisipoingilia na kulifanyia hili maamuzi unadhani nitaonekanaje , Lawrence kusanya vijana wote ambao hawako mbali tutaenda kuangalai kinachoendelea”Aliongea Dina.
“Lakini Madam ulitoa maelekezo ya vijana karibia wote wakae chimbo , waliopo karibu na mjini hawazidi hata hamsini?”
“Haina haja”Aliongea Hamza huku akisimama.
“Watu hamsini ni wengi sana na hili linaweza kuwa ni mtego , hebu ita wale kumi kutoka jumba la mazoezi waje hapa , wanatosha sana”
“Bro unataka na wewe…”
“Hamza na wewe unataka kwenda?”
“Nataka nikajionee kinachoendelea , kama kweli huu mpango kaupanga Mgweno basi atakuwa katumia akili , unadhani kwa katiba yao ya chama nini kinafuata mara baada ya mgombea mkuu wa chama kufariki ghafla?”Aliuliza Hamza.





SEHEMU YA 62.
“Sijui kuhusu katiba yao inachosema , ila nina uhakika mgombea Mwenza ndio atachukua nafasi, kwanini unauliza?”Aliuliza tena Dina maana alijua Hamza hakuwa mtu wa siasa.
“Nawaza kuna mchezo unaochezwa hapa na kuna nguvu mbili kubwa za kisiasa , nataka kujionea mwenyewe”Aliongea Hamza na Dina alitingisha kichwa , kwasababu Hamza alitaka kwenda hakuona haja ya kumzuia , isitoshe ilimpelekea kujiamini zaidi kudili na hali kama hio.
Upande wa Dina alijua lazima kuna mchezo unaofanywa na kama Mzee Seif atakubali kuhusika moja kwa moja itaaminika mtandao wake ndio umekamilisha swala hilo , jambo ambalo hakautaka litokee.
Nyumba ya Mzee Seif ilikuwa Kigamboni Mbutu B na gari mbili ziliendeshwa kuelekea huko ya mbele akiwemo Hamza na Dina na ya nyuma ilikuwa Noah iliowabeba Lawrence na kundi lake.
Kitendo cha kufika eneo la tukio waliweza kuona watu walioizingira nyumba ya Mzee Seif , jambo ambalo liliwashangazwa hakukuwa na uwepo wa polisi hata mmoja ni kama Hamza alivyotarajia.
“Mbona sio polisi kama taarifa ilivyosema?”Aliuliza Dina kama kwamba Hamza alikuwa na majibu.
Hamza alichunguza eneo lote hasa wale watu walioshikilia siraha na alijikuta akikunja sura mara baada ya kuona wazungu wawili ndani ya eneo lile wakiwa ni sehemu ya watu waliozunguka nyumba hio.
“Ni kama nilivyotarajia kuna kinachoendelea hapa”Aliongea Hamza.
“Lakini kama kweli walikuwa wakimshuku Mzee Seif kulipua gari ya mheshimiwa Jongwe kwanini hawajaja polisi?”Aliuliza.
“Tutapata majibu yote mara baada ya kuongea nao”Aliongea Hamza huku akitangulia kutoka nje ya gari.
Wale watu kama walinzi walioshikilia siraha wakiwa wamezingira nyuma hio waliongeza umakini kwa Dina na kundi lake.
“Kama tabia yako ya siku zote, Dina mrembo wa kujiamini , naona umekuja na watu wachache mno tofauti na nilivyotegemea”Sauti ya mwanaume ilisikika kwasababau ilikuwa kuna giza hawakumuona vizuri na mara baada ya kusogelea taa za mwanga wa gari ndio Dina aliweza kumuona.
“Pancho!, unafanya nini hapa?”Aliongea Dina na muda huo ni kama sasa alishaanza kupata picha ya kile kinachoendelea.
“Nimekuja kukusalimia kwa mara nyingine mara baada ya kukataa pendekezo ya dili nono”Aliongea na muda ule alitoa ishara na baada ya kupita dakika mmoja tu wanaume wanne walitoka katika nyumba hio na moja wapo ya wanaume wale alikuwa ni Mzee Seif alieshikiliwa na wanaume wawili weusi waliojazia mwili , mtu wa mwisho kutoka alikuwa ni Mzungu- Mjapani , yaani mtu aliechanganya rangi ya mjapani na Mzungu.
Kilichomfanya Dina kuanza kupandwa na hasira alijua mpango wote huu ulisukwa na Pancho.
Pancho alikuwa ni moja ya wasimamizi wa mtandao wao upande wa Congo na siku kadhaa nyuma Dina alipokea dili kupitia kwa Pancho kutoka kwa Wacanada ambao walitaka kuingiza siraha za kivita Congo kupitia Bandari ya Mtwara.
Dili hili liliungwa mkono na Mheshimiwa Mgweno lakini Dina aliona halikuwa na maslahi na kama angelikubali ni kama kujipiga risasi mguuni, ikizingatiwa siraha hizo zilipaswa kufikishwa kwa kundi lingine la waasi ndani ya Congo tofauti na lile ambalo wanashirikiana nalo kwa muda mrefu.
“Mzee Seif nini kimetokea , kwanini taarifa nilizopokea ni wewe kuhusika na kumuua Mzee Martini na mheshimiwa Jongwe?”Aliuliza Dina akimpotezea Pancho.
“Hawa ndio wahusika , wameiteka familia yangu na wanataka nikiri kuhusika kwa kushirikiana na wewe kumuua Jongwe au turejee mezani na kuanza mazungumzo ya kuingiza siraha Tanzania kwenda Congo”Aliongea Mzee Seif aliekuwa na hali ya hofu na kumfanya Pancho kutoa tabasamu.
“Pancho unajaribu kufanya nini , nani yupo nyuma yako?”
“Dina hakuna ambae yupo nyuma yangu?”Aliongea Pancho kwa kejeli.
“Kwa kumuua mgombea wa uraisi kupitia chama tawala, unasema hakuna ambae yupo nyuma yako?”Aliongea Dina kwa hasira na kumfanya Pancho kutoa tabasamu la kifedhuli.
“Nilitaka hili swala angalau ulichukulie kwa uzito wake, ushahidi wa wewe kuhusika katika shambulizi la kulipua bomu gari ya mgombea wa uraisi kupitia chama tawala upo , unaweza ukawa wa kutengeneza lakini jeshi la polisi lipo tayari kuuamini na kama likitoka uraiani , kitengo cha TISA kitakufanya mbuzi wa kafara, lakini huko kote ni kujisumbua kama upo tayari kuchagua chaguo zuri kati ya matatu alioongea Mzee Seif?”
Hamza muda huo alikuwa akiangalia mazingira yalivyo na watu wote waliokuwa hapo walikuwa na siraha za bunduki na haraka haraka kwa sheria ya Tanzania ilikua ngumu kwa watu hao kumiliki hizo siraha labda iwe kuna mtu ndani ya serikali ambae alikuwa akihusika.
Isitoshe safari yao kutoka kijichi mpaka kufka hapo , kama kweli jeshi la polisi lilikuwa sirasi kukamata watu hao waliomsababishia ajali mgombea wa kiti cha uraisi basi wangeshafika labda tu iwe kuna maagizo ambayo yamewafanya kuchelewa.
“Hizo siraha mnaotaka kuingiza Tanzania mnazitoa wapi?”Aliongea Hamza.
“Oh!, ahsante kwa kuuliza bwana mdogo , kidogo tu nimesahau kumtambulisha bosi wetu hapa , huyu ni Bosi Keita na ndio msingi wa haya maungumzo , kuhusu wapi siraha zinatoka ni juu yake”Aliongea Pancho kwa kujigamba.
“Pancho kama nilivyosema mtandao wetu haudili na maswala ya siraha bila ya utaratibu maalumu, kama unataka dili hili lipite lisimamie wewe mwenyewe na hela zako na sio za mtandao wa Chatu”Aliongea Dina na yule bwana mwenye asili ya kizungu na Kijapani alimpa ishara Pancho ya kuongea yeye.
“Miss Dina kama alivyoongea Pancho tunaweza kulimaliza hili swala kimya kimya na kusiwe na athari zozote kwa kila upande”Aliongea kwa Kingereza.
“Unamaanisha unaweza kuzima kesi ya kulipua gari ya mgombea wa Uraisi pamoja na Martini?”Aliuliza Lawrence.
“Itategemea na maamuzi ya Miss Dina?”
“Kwanini nahisi hata waliompendekeza Jongwe kupeperusha bendera ya Chama ni kama wanashangilia kifo chake?”Aliongea Hamza huku wakati huo Dina akiwa ametulia.
“Tunafanyaje?”Aliuliza Dina akimegemea Hamza , isitoshe ndie aliesema wasije na watu wengi.
“Wana siraha na hata kama tukishambuliana bila siraha hatuwezi kushinda bila kushitua raia , hawa watu wana mafunzo ya mapigano”Aliongea Hamza na kumfanya Dona kuwa na wasiwasi.
“Usiwaze hili naweza kulimaliza kwa amani na kisha utadili nao kujua nini kinaendelea kuhusu mgombea wa uraisi kulipuliwa”Aliongea Hamza na japo Dina alikuwa na wasiwasi aliamua kumwamini Hamza.
“Bwana Keita kwa ninavyojua huwezi kudili na siraha pasipo kuwakilisha shirika la giza unalotokea”Aliongea Hamza akitaka kujua Black Association ambayo Keita anatokea.
“Jungle Army Merchant ndio ninatokea”Aliongea bila ya kusita sita.
“Kumbe ni Jungle , hebu subiri kwanza nipige simu, nikimaliza utaamua cha kufanya”Aliongea.
“Umpigie nani?”
“Utajua nikimaliza’Aliongea Hamza.
“Mr Keita haina haja ya kupoteza muda na hawa watu , swala ni moja tu wachague chaguzi moja kati ya tatu tumalizane”Aliongea Pancho akionekana kukosa uvumilivu.
“Kimya! , sitaki unifundishe namna ya kufanya biashara”Aliongea Keira kwa kingereza na kumfanya Pancho kukaa kimya , isitoshe alikuwa akijua Jungle Army Merchant walikuwa wafanyabiashara wakubwa ndani ya Black Market kwa kuuza siraha za kila namna.
Muda huo Hamza alikuwa ashapiga simu tayari bila ya kuwa na wasiwasi kabisa.
*****
Magneto, Las Vegas- USA
Ni ndani ya jiji la Las Vegas , jiji ambalo kwa wacheza kamari hawakuhesabu muda , Usiku ni kama mchana na Mchana ni kama usiku tu ndani ya hili jiji.
Katika moja ya hoteli ya kifahri ya nyota tano ndani ya chumba cha hadhi ya raisi , alionekana mtu bonge mweusi mwenye kitambi akiwa amelala chali.
Alikuwa mrefu wa mita kama moja nukta tisa hivi , vidole vya mikono yake vilikuwa vimevishwa pete za madini ya almasi , Dhahabu na madini mengine ya thamani , shingoni alikuwa amevalia mikufu ya bei ghali.
Mtu yule bonge alijikuta akitandaza miguu yake vizuri huku akifumba fumba macho na kuyafumbua , katikati ya eneo la mapaja yake alionekana mwanamke mzungu mwenye nywele nyeupe(blonde) akiwa bize kumhudumia.
“Mr Mamen are you comfortable?”Aliuliza yule mwanamke kwa sauti tamu huku akiinua kichwa chake akimwangalia kwa macho malegevu , akimuuliza Big kama ni mwenye kuifurahia huduma.
Mwanaume yule bonge udenda ulikuwa ukitaka kumwagika kutoka kwenye midomo yake , alionekana alikuwa kwenye ulimwengu mwingine wa raha.
“Comfortable..!?, Deeper the better .”Aliongea akimaanisha azame chini zaidi ndio itakuwa vizuri.
“You’re so annoying , I’m realy tired ..”Aliongea yule mwanamke akimwambia anachukiza kwani amekwisha kuchoka.
Bonge yule mweusi kama msanii RickRoss alifungua droo ya meza pembeni na kitanda chake na kuchomoa maburungutu ya pesa za dola na kumtupia.
“Hakikisha najisikia vizuri mpaka kisogoni , nitakupa kiasi chochote cha pesa unachotaka”Aliongea Big na yule mwanamke uchomvu uliisha palepale na alijkuta akiongeza mashambulizi ya kuhakikisha Big anajisikia vizuri.
Dakika hio hio simu yake ilianza kuita , hata simu yake tu ilikuwa imetengenezwa kwa housing ya madini ghali sana na kuifanya ionekane kama kitu kisichokuwa cha kawaida kutokana na uthamani wake
“F*ck , kama ningejua ningeizima hii simu , nani ananipigia muda huu”Big alilaani huku akichukua ile simu na kuipokea maana namba ilikuwa mpya tena haikuwa ya taifa hilo
“Big naona kama kawaida yako sasa hivi unaringa , kwahio unaona sipaswi kukupigia hata kama ni swala linalohusu vita ya tatu ya dunia”Sauti ya kiume ilisikika katika simu ya Big.
Kitendo cha Mameni kusikia ile sauti mwili wake ulitetemeka na macho yake yalibadilika na kuwa mekundu na hata ule msisimko aliokuwa akisikia ulipotea.
Yule mwanamke aliekuwa bize kuhakikisha Big anafurahi alijikuta akipiga kelele mara baada ya kadudu kabig kupotea na kuwa kabamia.
“Boss!! , ni wewe kweli , naona hatimae umenipigia , nimekumisi sana”Aliongea Big huku sauti yake ikiwa imebadilika.
“Unafanya nini hapo , lazima utakuwa na m*laya kitandani , yaani ndio kwanza kunakucha wewe unahangaika na wanawake , kuna siku utafia kwenye kifua cha mwanamke”
“Hehe..Bosi wewe mwenyewe unanijua vizuri , isitoshe wewe ndio mtu pekee ulievunja rekodi yangu”Aliongea.
“F*ck you!”Alitukanwa.
“Bosi nasikia upo Tanzania , habari za siku nyingi , vipi naweza kuja huko?”
“Nina mambo mengi ya kufanya siku hizi tutaona kama unaweza kuja , nyie watu ni wasumbufu sana mkisikia nipo mahali mnataka kuja tu , sitaki usumbufu wenu nahitaji kutulia kwa sasa”
“Bosi kwa uwezo wako na ushawishi wako unaweza kuomba chumba mapumziko Ikulu na ukapatiwa na warembo kabisa , hayo sio mapumziko ila ni kujitia stress tu , mapumziko ni yale wafariji wanakuwa wanabadilika badilika kila siku kwenye kuusisimua mwili”
“Sterehe za kutumia hela hizo nishazichoka , hata nikikuambia ni namna gani nafurahia maisha ya sasa hivi hutonielewa Big”
“Kama ni hivyo bosi kwanini umenipigia simu , kuna dili jipya?”
“Hakuna dili lingine , nishastaafu hayo mambo”
“Sababu ni ipi sasa Bosi , au kuna sehemu nimekosea?”Aliuliza Big kwa upole.
“Kwenye biashara zako unamfahamu bwana anaefahamika kwa jina la Keita?”
“Ndio mwaka juzi niliingia dili na kundi moja linalofanya shughuli zao ndani ya Afrika kuiba madini Adimu na kuyauza kwenda kwenye moja ya kampuni ya maswala ya kiteknolojia nchini Ufaransa , linaongozwa na bwana Keita”Aliongea Big.
“Huyu bwana wako naona ana juhudi mno , muda huu nimeelekezewa mitutu ya bunduki ndio maana nimekupigia simu kuthibitisha , Big kwahio sasa hivi umeshaanza kuwa mkubwa kiasi cha kunisaliti kisa tu nnimetoka kwenye uringo?”
Big mara baada ya kusikia kauli hio kutoka kwa Hamza alijikuta mikono ikimtetemeka kiasi kwamba simu ilitaka kudondoka.
“Bosi , subiri kwanza , nitampigia simu sasa hivi , naomba kwanza nimfokee baada ya hapo unaweza kumuua”Aliongea Big na dakika ileile alikata simu na kuitafuta namba ya Keita.
“Mamen Babe! , unafanya nini sasa mbona imepotea!?”Yule kahaba wa kizungu aliongea lakini Mameni alimpotezea na mara baada ya kuipata namba ya Keita aliipiga palepale.
Mara baada ya Hamza kumaliza kuongea na simu hakuongea neno na alitulia akiangalia matokeo.
Ijapokuwa Keita hakujua Hamza alikuwa akiongea na nani kwenye simu lakini alihisi kuna kitu hakipo sawa.
Dakika ileile simu yake ilianza kuita na alisogea pembeni na kupogea lakini muda huo huo alianza kuonyesha ishara za kupaniki.
Upande wa pili ilikuwa ni sauti ya Big kutukana kimarekani kwa mara nyingi mfululizo kadri alivyoweza.
“Bosi nimefanya kosa gani?”
“Unataka kumuua nani sasa hivi?”
“Bosi umejuaje nataka kuua mtu?”
“Unaetaka kumuua ni bosi wangu”
“…”
Keita alijikuta akikosa neo , alishangaa mno kwa zaidi ya sekunde kumi , ni kama alikuwa akisharabu yale maneno.
“Ah!”
Alijikuta hofu ikimwingia na vigoti vya miguu yake vilianza kumlegea na alijikuta akigeuka na kumwangalia Hamza.
Upande wa Hamza alikuwa akimwangalia Keita tu kwa mbali na kwa jinsi alivyoonyesha kupaniki na woga alitamani kucheka.
“Mr Keita , Mr Keita , what happened?”Pancho aliuliza mara baada ya kuona mabadiliko.
Dina macho yake yalichanua alijua kabisa mabadiliko ya Keita ni kutokana na Hamza alipopiga simu na kwake aliona mwanaume Hamza alikuwa akimshangaza kila siku.
“Nini tatizo Mr Keita , mbona huongei?”Aliuliza Pancho kwa wasiwasi
“Hivi unajua mimi na vijana wangu tutakufa sasa hivi kutokana na ujinga wako na wale wanasiasa wapuuzi?”Aliongea kwa hasira.
“Unamaanisha nini Mr….”
Keita hakuchelewa alichomoa Desert Eagle kutoka kwenye kiuno chake na kumchapa risasi tatu Pancho palepale.
Mpaka Pancho anadondoka chini muonekano wake ulikuwa na shauku ya kutaka kujua kwanini Keita anamshambulia.
Keita mara baada ya kumalizana na Pancho alitoa maagizo kwa vijana wake kuwashambulia watu wa Pancho na walionekana kuwa shapu kweli kwani ndani ya sekunde wote walikuwa chini.
Baada ya Keita kuituliza hali alijikuta akimdondokea Hamza kwa magoti huku akiwa na wasiwasi mwingi akitia huruma.
“Prince Rich.. Bosi wangu ameniambia kila kitu , naomba unisamehe kwa ujinga wangu , sikubahatika kukutana na wewe ana kwa ana zaidi ya kusikia habari zako ndio maana nimekukosea…”
Kitendo kile kiliwashangaza mno Dina , Lawrence na wenzake , waliishia kujiuliza Hamza ni nani mpaka bwana yule kuwa na hofu namna ile kiasi cha kupiga magoti.
“Nipe bastora yako”Aliongea Hamza akiwa siriasi na kumfanya Keita kukakamaa mwili lakini alimpatiia.
‘Tafadhari naomba uwaache vijana wangu waondoke , walikuwa wakifuata maelekezo tu kutoka kwangu na wanazofamilia zinawategemea”Aliongea Keita lakini Hamza hakumjali na muda ule aliinua ile bastora na kujielekezea kwake kana kwamba anataka kujipiga risasi.
Tukio lile lilimshangaza kila mtu wakishindwa kuelewa Hamza anataka kufanya nini
“Hamza unataka kufanya nini , usipaniki..”Aliongea Dina lakini kabla hata hajamaliza Hamza alikuwa ashaachia risasi.
Bam!
Mlipuko ule wa bunduki ulimuogopesha mpaka Keita na wote walimwaangalia Hamza kwa mshangao na walishangaa zaidi baada ya kuona hakuna kilichotokea.
Risasi ambayo ilitoka katika ile bunduki ilikuwa katika vidole vya Hamza , haikueleweka amefanyaje lakini ilionekana aliikamata kabla ya kumfikia, tukio lile lilimfanya Keita kushindwa kuendelea kupiga magoti na kukaa chini kwa kunyoosha miguu huku mapigo yake ya moyo yakidunda kwa kasi.
“Kabla sijafanya chochote nataka muelezee kila kilichotokea… sababu ya kwamba umepiga magoti sio kwasabau ya bosi wako bali ni kwasababu yangu hivyo nataka majibu”Aliongea Hamza.
“Serafii.!!, nipo tayari kuongea”Aliongea Keita huku akipiga kichwa chini kiasi cha kutoka damu kwenye paji la uso.
“Anza kuelezea , kwanini kifo cha Mgombea wa uraisi na nani kahusika”Aliongea Hamza.
“Hatujahusika katika kumuua mtu , tupo hapa nchini kwa ajili ya mazungumzo ya biashara ya kupitisha Siraha Kwenda Congo kupitia bandari ya Mtwara , kitu pekee ambacho nafahamu kuhusu muhusika tulipewa kazi ya kumtorosha hapa nchini kupitia boti yetu”Aliongea na kauli ile ilimfanya Dina kusikiliza kwa umakini.
“Imekuwaje mkajiingiza , sitaki kuuliza maswali mengi elezea kila kitu ninachotaka kujua?”
“Mara ya mwisho nilivyokuja hapa nchini niliweza kukutana na mstaafu Mgweno kwa ajili ya kuingia dili la kupitisha siraha , lakini kutokana na usafirishaji wote wa Kimagendo kuwa chini ya Chatu hakutoa maamuzi badala yake aliwasiliana na Miss Dina ambae mara baada ya kuelekezwa kuhusu dili hili alikataa, Mstaafu baada ya ombi hili kukataliwa alituambia hana namna ya kutusaidia kwani njia pekee ya kupitisha siraha hizo ni moja tu ambayo ni Mtwara kutokana na bandari zote kuwa chini ya mwekezaji”
“Nini kiliendelea”
“Wakati tukifikiria namna ya kutafuta njia nyingine ya kukamilisha dili hili nilipokea simu kutoka kwa mtu ambae alijitambulisha ni msaidizi wa raisi”Aliongea.
“Unamaaniisha Mheshimiwa Eliasi Mbilu?”
“Ndio na alisema anataka kuonana na sisi kwa ajili ya mazungumzo ya namna ya kukamilisha kile tulichokuwa tukihitaji , kutokana na kuwa na haraka ya kufanikisha hili dili nilikubali na kupitia msaidizi wake alinipa maelekezo niwaache vijana na boti yetu nchini Tanzania kwa muda na nikutane nae jijini Kual Lampur nchini Malaysia ndani ya tarehe alionitajia wakati akiwa ziarani”
“Tokea tuzungumze kuhusu hili dili imeshapita mwezi miwili , inamaana huu mpango ulikuwa wa muda mrefu?”
“Inawezekana Miss Dina , kabla ya siku moja ya tarehe kufika , niliweza kufika Malaysia na nilikutana na mheshimiwa kwa siri sana kupitia msaidizi wake na nilitambulishwa kama mwekezaji”Aliongea Keitani kwa kutetemeka.
“Alitaka kuongea nini kwa siri namna hio?”Aliuliza Dina , ijapokuwa Keitani alijua alikuwa akitoa siri kubwa lakini hakuwa na jinsi.
“Aliniambia siku ya leo saa nne kamili za usiku mgombea wa kiti cha uraisi kupitia chama chake atafariki kwa ajali ya gari na atakaesababisha ajali hio napaswa kumtorosha nje ya nchi na kama ikishindikana nimuue kabla ya kukamatwa na polisi, kisha nitumie ushahidi feki wa tukio hilo kuhakikisha nakamilisha dili la kupitisha siraha”
“Ushahidi feki ni kutusingizia sisi ndio wahusika, si ndio?”
‘Ndio”
“Ameenda mbali mpaka kutengeneza ushahidi feki , yeye anafaidika nini katika hilo?”Aliuliza Lawrence.
“Kila kitu kipo wazi , naamini Jongwe sio chaguo lake na pili alitaka kujitengenezea njia za kupata maslahi hata akiwa amestaafu kupitia hili dili”Aliongea Hamza.
“Ndio , alitaka asilimia ishirini ya faida itakayopatikana na wakati huo huo Mgombea wa uraisi akiwa ni chaguo lake baada ya chaguo la Mgweno kufariki”Aliongea keita na kumfanya Dina sura kujikunja
“Mgweno na Eliasi wanataka kupinduana , madaraka huwa ni matamu sana”Aliongea Dina lakini upande wa Hamza hakujali nani anampindua nani.
“Vipi kuhusu muuaji ni nani?”
“Kuhusu mfungwa hatuna taarifa nyingi kuhusu yeye , tulipatiwa picha pekee na tuliambiwa ni mfungwa wa kidiplomasia aliefungwa kwa muda mrefu kwa siri”
“Yuko wapi kwasasa?”Aliuliza Hamza.
“Ametoweka mara baada ya tukio, tunaamini alikuwa na mpango wake binafsi wa kujitorosha baada ya kukamilisha misheni”Aliongea na kumfanya Hamza kuvuta pumzi.
“Picha yake ipo wapi”Aliuliza Hamza na Keita alimpa ishara bwana moja wa kizungu na alimsogezea Hamza simu na ilionekana picha ya mfungwa kwenye kioo cha simu na mara baada ya kuiangalia alijikuta macho yake yakichanua.
“What the f*ck!!”
Hamza alijikuta akitoa tusi na kumfanya Dina kusogea kuangalia picha hio ili kujua kwanini kashangaa.
ITAENDELEA.
Watsapp me kwa mwendelezo wa haraka haraka namba 0687151346
Umerudia mkuu
 
singanojr wewe ni mtu na heshima zako kama umafanya bahati mbaya kurudia unge tuomba radhi, kama ni kusudi basi sisi tuna shukuru.
 
Back
Top Bottom