SHETANI RUDISHA AKILI ZETU.
MTUNZI: SINGANOJR
SEHEMU YA 68.
MALAYSIA-KUALA LAMPUR.
Wakati Tanzania ikiwa ni saa sita za mchana ndani ya jiji la Kuala Lampur nchini Malaysia ilikuwa ni saa kumi na moja za jioni.
Nje ya mlango wa kuingilia wodi ya VVIP katika hospitali ya Gleneeagles walionekana wanausalama wakiimarisha ulinzi , kwa jinsi sura zao zilivyokuwa zikionekana hazikuwa za wasiwasi wala huzuni bali ni za umakini zaidi kama kwamba wanahakikisha kile kinachoendelea ndani ya hio wodi kubakia kuwa siri.
Dakika kama kumi hivi alionekana mwanaume wa umri wa makamo maji ya kunde akisogelea eneo hilo , alikuwa ni msaidizi wa mheshimiwa Raisi Samweli Elias Mbilu ambae anafahamika kwa jina la Maulidi .
Maulidi anashikiria majukumu yote ya Chief of Staff lakini licha ya hivyo alikuwa ni moja ya watu ambao wanaaminiwa sana na mheshimiwa.
“Nipo hapa kwa ajili ya kuonana na mheshimiwa , Kanali”Aliongea Maulidi akiomba ruhusa kutoka kwa kitengo cha ulinzi kinachongozwa na mpambe wa raisi Kanali Ashrak Chipyangu.
Afande Ashrak aliangalia saa yake na alionekana kutingisha kichwa kwa ishara ya kukataa.
“Mheshimiwa katoa maagizo kuruhusu mlango wake kugongwa baada ya dakika therathini, yupo na mgeni”Aliongea Ashrak na kauli ile ilimfanya Maulidi kukunja sura , alijua lazima mgeni atakuwa mwanamke maana kauli hizo ni kama ashazizoea.
Maulidi hakuwa na hiyana zaidi ya kusubiri , isitoshe alikuwa akimjua bosi wake alikuwa akiongoza kwa kupenda wanawake.
Dakika kumi za kusubiri zilipita na hatimae mlango wa wodi hio ulifunguliwa kwa ndani na alionekana mwanamke mrembo akitoka.
Mwanamke yule mara baada ya kukutanisha macho na Maulidi alimkonyeza kwa ishara ya kichokozi na kisha kimadaha akaanza kuzipiga hatua kuondoka ndani ya hilo eneo.
“Kanali naungana na wewe kumchukia huyu kahaba”Aliongea Maulidi akimwangalia Kanali Ashrak kwa tabasamu la uchokozi.
“Sijawahi kusema namchukia Mr Maulidi”Aliongea Kanali kikauzu.
“Hata mimi naona Afande, unaonekana kumpenda sana”Aliongea na Kanali hakujali maneno ya kinafiki ya Maulidi na alimpa ishara ya kusubiri wakati akimtaarifu mheshimiwa ujio wake.
“Mheshimiwa Mr Maulidi yupo hapa anataka kuonana na wewe”Aliongea Kanali na bila sauti upande wa ndani kusikika Kanali alimfungulia Maulidi mlango na kisha kuingia.
“Mheshimiwa sijawahi kumpenda huyu Tresha hasa katika nyakati kama hizi”Aliongea Maulidi akimwangalia mheshimiwa Eliasi ambae alikuwa akifunga mkanda wa Bathrobe vizuri.
“Kama ungempenda inamaanisha hana vigezo vya kuwa na mimi , nani asiejua Maulidi anachukia wanawake warembo”Aliongea Mheshimiwa Eliasi huku akitoa tabasamu lililojaa kejeli akisogelea chupa na kujaza mvinyo kwenye glasi.
“Nazungumzia kwa kujali usalama wa misheni zetu mheshimiwa , huu ni muda wa kuwa makini”
“Shida yako upo siriasi sana , wakati huu wengi wakijua nipo hospitalini nadhani ingekuwa vizuri kuonana na madaktari ili kutibu shida yako ya kisaikolojia ya kuogopa wanawake warembo”
Ilikuwa ni kweli Maulidi Ally Mfinanga ni mgonjwa wa Caligynephobia,ugonjwa ambao unamfanya mtu kuogopa wanawake warembo , inasemekana wakati akiwa katika misheni nje ya nchi aliwahi kupatwa na tukio ambalo lilimpelekea kupata ugonjwa huo wa kisaikolojia.
“Nipatie habari za kinachoendelea”.
“Nimepokea taarifa kutoka Tanzania, mstaafu ameridhia Abubakari Kassimu kuchukua nafasi ya Marehemu Jongwe, japo maamuzi hayajatangazwa kwa wanachama wote lakini huo ndio msimamo wa chama kwa sasa”Aliongea na kauli yake haikumbadilisha muonekano Eliasi.
“Sijawahi kumuona Mgweno kukubali kirahisi namna hii , inaonekana familia ya Wanyika wamefanikiwa kumuweka mkononi”Aliongea huku akipiga pafu la mvinyo.
“Mheshimiwa licha hili kuwa na faida kwa upande wako lakini nina wasiwasi na matokeo yake kwa nchi yetu”Aliongea Mauidi.
“Niambie Mzalendo, wasiwasi wako ni nini?”
“Licha ya kwamba inaonekana Wanyika ndio wamesimamia kila kitu lakini udhaifu wa mheshimiwa Mgweno upo chini ya Raisi Habimana”
“Papa ni mkali baharini akitolewa nje ya maji anakuwa Kambale, Habinana anaweza kuwa na udhaifu wa Mgweno lakini hauna nguvu yoyote pasipo ya msaada wa Wanyika”Aliongea na kumfanya kuchanganyikiwa kidogo.
“Unadhani mimi Eliasi Mbilu naweza shiriki katika kitu ambacho kinahatarisha usalama wa taifa , wengi wanaamini nipo chini ya Mgweno lakini mimi nipo mwenyewe, Ushawahi kujiuliza kwanini Wanyika licha ya kutokuwa na umaarufu ndani ya Tanzania lakini wana nguvu kubwa?”Aliuliza Eliasi.
“Mara nyingi nimekuwa wa kujiuliza hili swali , ukilinganisha na familia ya Mgweno, Wanyika utajiri wao na umaarufu wao ni mdogo mno?”
“Ushawishi ni nguvu, katika dunia hii ili uwe na nguvu ya ushawishi sio lazima uwe tajiri au mwanasiasa, kinachoangaliwa ni ushawishi unaobebwa na historia katika kuchangia kile wanachokiita Lengo Kuu moja la Dunia, Mgweno ana ushawishi ndio lakini katika jamii ya kimataifa inayosimamia Lengo kuu moja la Dunia haimtambui kwasababu ushawishi wake ni wa msimu na umetokana na siasa na si vinginevyo, lakini tukija kwa Wanyika wanatambulika kama Chimbuko, kama familia inayobeba damu asilia ya nchi, damu ambayo ambayo wanaamini ina mchango mkubwa kuyafikia malengo”Aliongea na kumfanya Maulidi kuonekana kama hajaelewa.
“Huwezi kuelewa ninachomaanisha kwasasa , wengi hawajawahi kuelewa , hata Mgweno hajawahi kuelewa, lakini sasa hivi atakuwa anaanza kuelewa, hata hivyo tukiachana na hilo, sijasikia taarifa yoyote kutoka kwa Keita”Aliongea Mheshimiwa na kumfanya Maulidi kukamaa mwili.
“Mheshimiwa hilo lilikuwa swala la pili kuripoti”
“Nini kimetokea?”
“Keita katuma taarifa ya kuvunja mkataba na malengo yake ya kupitisha siraha kupitia bandari za Tanzania atafikiria upya”Aliongea na kumfanya mheshimiwa kukunja sura.
“Vipi kuhusu misheni tuliompatia , ameweza kumtorosha Chindez?”
“Hakutoa maelezo ya kutosha nilipomuuliza , ila kuna taarifa ambayo imenifikia kutoka kwa chanzo chetu, Keita mara baada ya kukutana na Hamza alimgeuka Pancho na kumuua na bado haijaeleweka sababu ya kufanya hivyo”Aliongea na kauli ile ilimfanya kushangaa.
“Kwanini kila mara nasikia hili jina la Hamza katika kila mpango ulioharibika?”Aliongea huku akiwa amekunja sura.
“Bado tunaendelea kumfutilia mheshimiwa ili kumjua ni nani haswa”Aliongea lakini hata hivyo mheshimiwa alionekana kutokuwa na wasiwasi.
“Yulia anasemaje juu ya hili?”
“Amesema Keita ulikuwa ni mpango wa dharula”Aliongea na kumfanya Eliasi kumwangalia Maulidi kana kwamba hakuwa amemsikia vizuri.
“Yaani wamenitoa Tanzania kuja kujifanyisha mgonjwa hapa Malaysia kwa ajili ya mpango wa Dharula?”
“Mheshimiwa sidhani kuwepo hapa ni mpango wa Dharula , labda kuna kinachoendelea pasipo ya sisi kujua”
“Hilo ni jukumu lako la kujua kila kitu kinachoendelea na kunitaarifu , unadhani nakulipa posho ili uje kunielezea vitu vya kukisia?”
“Nitafuatilia mara moja mheshimiwa”Aliongea Maulidi akijitetea.
“Ili niweze kuishi kwa amani baada ya kustaafu ni kutokufungamana upande wowote , Wanyika wanaweza kumdhibiti Mgweno kwasasa lakini mimi namjua Mgweno sio mtu wa kukubali kirahisi kupokonywa ufalme wake , isitoshe mizizi yake imesambaa kila kona ya nchi”
“Mheshimiwa unapanga kuchukua hatua gani?”
“Licha ya kwamba mpango wa kumuua Jongwe ulipangwa na Wanyika kuna uwezekano mkubwa mpango huu ukanitengenezea udhaifu na hata nikistaafu madili yangu mengi kukwama kutokana na kukosa nguvu serikalini ,Maulidi unadhani ni kwanini Mgweno licha ya kuonekana kuwa na ushawishi mkubwa bado ameshindwa kutimiza malengo yake?”.Aliuliza na kumfanya Maulidi kufikitiria kidogo.
“Moja ya sababu kubwa ni kushindwa kuimarisha ushawishi wake upande wa underworld Societies”
“Safi kabisa, tafsiri ya underworld ni jamii ya watu ambao wapo nje ya mfumo wa kawaida wa kimaisha , katika jamii hizi kinachoangaliwa zaidi ni nani anaunganisha mtandao kutoka eneo moja kwenda eneo lingine , Mgweno alichokosa ni mtandao ndio maana mara zote alikuwa akipambana kuumiliki mtandao wa Chatu lakini tamaa zake zimemfanya kujiingiza kitanzini yeye mwenyewe”
“Mheshimiwa unamaanisha nini kuhusu tamaa?”
“Tamaa ni kufanyia kazi malengo mengi kwa wakati mmoja. Wasiliana na Dina nikirudi nchini nataka kuonana nae”Aliongea Mheshimiwa na kumfanya Maulidi kushangaa kidogo.
“Mheshimiwa lakini kuna uwezekano Dina anafahamu mpango wa kutaka kusingizia kundi lake kujihusisha na kifo cha Jongwe”.
“Kama ingekuwa rahisi kusingizia mtandao wa Chatu kuhusika na mauaji na kuondoa nguvu yake basi Mgweno angefanikiwa muda mrefu sana , Mtandao wa Chatu sio mtandao ambao unaweza kuharibiwa kwa hila nyepesi nyepesi, ukisikia Chatu ni kama wamiliki wa geti ndani ya ukanda wa Afrika mashariki na kati la kuingilia kuzimu , Mgweno alijaribu na matokeo yake akatengenezewa udhaifu ambao unamfunga mpaka leo hii”
“Mheshimiwa kama walikuwa wakiamini Chatu haiingiliki imekuwaje wakaandaa mpango wa namna hii?”
“Kuna uwezekano ni hila za Yulia kutaka kumfahamu Hamza au kuna sababu nyijngine nisioijua, Kadri huyu Hamza anavyozidi kujihusisha katika haya maswala ndio anavyozidi kujiweka wazi yeye ni nani haswa , nafikiria hii ndio sababu , isitoshe si amekuambia Keita ni mpango B wakati mwanzoni alituaminisha ni mpango A , licha ya kumwambia ni mpango kichaa”
“Mheshimiwa nadhani naanza kupata kitu pia, Yulia anajaribu kumtengenezea Hamza matatizo kumzunguka ili kadri atakavyojaribu kuyatatua ndio anavyozidi kujiweka wazi yeye ni nani?”
“Nadhani ushaanza kupata picha”
“Kwaninni sasa mheshimiwa unataka kuwasiliana na Dina?”
“Maulidi , inamaana hukunielewa maana ya maneno yangu tokea mwanzo”
“Sijakuelewa moja kwa moja mheshimiwa”
“Wasiliana na Dina nataka kuonana nae , kama nilivyosema Chatu ni Lango la kuingilia kuzimu na mimi nataka kuingia huko ila lazima niwe na mtu wa kuniongoza, sitaki kuwa kama Mgweno ambae anadhani kila kitu kinaweza kuwa chake kwa kutumia mabavu”
“Mheshimiwa kwahio mpango wako ni kuimiliki Chatu kidogo kidogo?”
“Yes! Slow but sure”
*****
“Nani kakuambia?”Aliuliza Hamza.
“Haina haja ya kubadilika kiasi hicho , hujafanya dhambi hii ni taarifa njema”Aliongea Eliza.
“Eliza nilipaswa kukuambia mapema kuhusu hili , nilikuwa nikipanga kukuambia tokea muda mrefu”
“Huna haja ya kujielezea Hamza, naelewa unachomaanisha , hata hivyo sidhani mapenzi yetu yalikuwa siriasi kihivyo , siwezi kusema umenisaliti au nini, isitoshe pia nashindwa hata kujua namna ya kukushukuru kwa kunisaidia kumpeleka mama yangu nje ya nchi kwa ajili ya kutibiwa , sio hivyo tu umeniokoa mara kibao , kwangu wewe nakuchukulia kama mtu mzuri , hivyo nakutakia wewe na bosi Regina furaha…”
Eliza alikuwa akiongea huku akiwa ametabasamu lakini upande wa Hamza maneno hayo yalimfanya kujihisi ni kama anatambaliwa na mdudu mgongoni.
“Eliza haya maneno yako ni ya kweli?”Aliuliza Hamza huku akiwa amekunja ndita.
“Kabisa, nawatakia kila la kheri , sisi ni watu wazima hakuna haja ya kudanganyana , isitoshe wewe kuoa haimaanishi hatuwezi kuwa marafiki”
“Lakini Eliza nakupenda mno ,usiniambie hukua na hisia zozote juu yangu?”
Eliza alijikuta mwili wake ukikakamaa wakati cheche za mapenzi zikionekana kwenye macho yake , alionekana alikuwa akijitahidi kujizuia kwa kuvuta pumzi nyingi.
“Eliza kadri unavyoonyesha kuwa sawa unazidi kunipa wasiwasi ujue”
“Usijali Hamza , mimi nipo sawa kabisa , japo ni kweli nahisi kujutia lakini bado najihisi ni mwenye bahati kukutana na wewe pamoja na bosi Regina , wote ni watu wazuri mno kwangu”
Ukweli ni kwamba Hamza alikuwa anakosa ujasiri wa kusema ndoa yake ni ya mkataba kwa ajili ya kumsaidia Regina kupata hisa za kampuni kutoka kwa bibi yake, aliona hata akisema, ingekuwa kisingizio kisichokuwa na msingi, maana iwe ni kwa mkataba au kwa mapenzi hakulazimishwa kufanya maamuzi.
Hamza aliishia kumwangalia Eliza bila kupata neno la kuongea , kosa kubwa kwake lilikuwa ni kumdanganya Eliza tokea mwanzo.
“Usiniangalie hivyo , najua unampenda sana Bosi , ile siku tulivyopata ajali na namna ulivyowahi kuwaza usalama wake niliweza kuona ni kwa namna gani ni mtu wa muhimu kwako , kwanzia sasa sitaki niwe kikwazo kwenye mahusiano yenu ya ndoa, hivyo naomba mambo yetu yaishie kwenye maswala ya kikazi”
Ilionekana Eliza aliweza kugundua nafasi yake ndani ya moyo wa Hamza kutokana na ile ajali , kwake aliamini kama kweli Hamza alikuwa akimpenda basi siku ile asingemwacha akiwa na hofu vile na kumkimbilia Regina , kimantiki ilikuwa ni sawa kwa Hamza kukimbilia kwenda kuona usalama wa Regina lakini kihisia kwa Eliza alipatwa na hisia za kutelekezwa njiani.
“Eliza ijapokuwa naweza kuonekana kama nimekosa aibu , lakini ukweli ni kwamba wewe na Regina ni watu muhimu kwangu , sitaki kukupoteza kwasababu ya ndoa yangu na Regina”
‘Wewe…!”Eliza alijikuta akikosa neno na alimwangalia Hamza kwa mshangao ni kama hakutegemea ile kauli.
“Kwasababu tumefikia hapa sina haja ya kukuficha chochote , lakini ukweli ukiachana wewe na Regina kuwa watu muhimu kwangu lakini vilevile nina mwanamke mwingine”Aliongea Hamza akiwa siriasi.
“Hamza kwanini unanifanyia hivi?”Aliuliza Eliza huku akijikuta ni kama mtu anaejutia , hakujutia kwasababu anaachana na Hamza bali kwasababu tayari ashafungua moyo wake kwa Hamza muda mrefu tu na anashindwa namna ya kuufunga.
“Kwasababu mimi ni mimi na sina haja ya kukudanganya tena”
“Wewe ni mbinafsi”
“Ndio mimi ni mbinafsi , na ndio maana sitaki kukupoteza”
Eliza alikuwa na hasira mnno na kama ni mwanamke mwingine kwa jinsi ambavyo alikuwa akijisikia kutokana na alichokisema Hamza , angekuwa ashampiga kibao tayari, hakuamini mwanaume ambae alikuwa akianza kumpenda alikuwa na mwanamke mwingine , kwa Regina tu imemfanya kukosa usingizi lakini kuna mwingine.
Lakini hata hivyo kutokana na utu uzima wake na uzoefu katika maisha yake hakutaka kuruhusu akili yake kudanganywa na moyo wake , mtu kama Hamza ambae ameonyesha uwezo wa tofauti tofauti usio kuwa wa kawaida , ilikuwa ni ngumu kuwa Single , isitoshe pia hakujua maisha ya Hamza ya nyuma yalivyokuwa.
‘Nadhani nakuelewa , isitoshe sina ninachojua kuhusu maisha yako ya nyuma , lakini ninaweza kuotea wewe sio mtu wa kawaida , unaonekana kuwa na nguvu kubwa, upande wangu mimi ni msichana kutoka familia ya kawaida niliebahatika kuajiriwa katika kampuni kubwa sioni kama nina haki ya kukukosoa wala kukuhukumu , kitu pekee ninachoweza kufanya ni kuishinda aibu ya moyo wangu”
“Eliza unajaribu kumaanisha nini?”
“Ninachomaanisha ni kwamba siwezi kukataa kama sikuwa na hisia za kimapenzi kwako na upo tayari kuzipokea, lakini licha ya hivyo najali utu wangu , hata kama sistahili kukataa mwanaume kama wewe, sitaki kumsaliti Regina”
“Nimekuelewa , lakini vipi kama Regina anakubaki tuendelee na mahusiano yetu , bado utaniacha?”
“Labda..”
“Regina hana shida na sisi kuwa katika mahusiano , kwanza hanipendi la sivyo asingeniambia nitafute mwanamke mwingine”
“Sio kweli , Regina anaweza kuonekana hakupendi lakini ukweli anakupenda la sivyo asingekubali mfunge ndoa, nimemjua bosi kwa muda mrefu sana na nailewa tabia yake , kama angekuwa hakupendi hata angepigwa mpaka kufa asingekubali”Aliongea Eliza.
Hamza mara baada ya kusikia maneno hayo alishindwa kujiuia na kuona yana ukweli wake , ilionekana swala la wao kusajili ndoa halikuwa la kimkataba pekee ila kuna sababu nyingine , vinginevyo kwa ukiburi aliokuwa nao Regina asingekubali ndoa kirahisi hata kama ni kuikosa kampuni.
Eliza alionekana kuhitaji muda zaidi , alikuwa akimpenda Hamza lakini vilevile hakutaka kuwa mchepuko , katika maisha yake alitamani kuitwa mke wa mtu na sio mchepuko wa mtu , ijapokuwa ni kweli alikuwa akimpenda Hamza hakutaka kuziruhusu hisia zake kumpelekesha , alitaka kukaa chini na kufikiria.
Mara baada ya chakula cha mchana safari ya kurudi ilianza na hawakuchukua muda mrefu barabarani mpaka kufika, Eliza alimsisitizia Hamza kwa kipindi hicho wapunguze ukaribu wao na uendelee kuwa wa kikazi zaidi , Kwasababu Eliza alionekana kuwa siriasi Hamza hakuona haja ya kuendelea kumpa wakati mgumu , isitoshe yeye ndio alieonekana kuwa na makosa , lakini alimuahidi ikitokea Regina akikubali waendelee basi atahakikisha hampotezi.
Baada ya Eliza kuelekea idara ya Finance upande wa Hamza alichukua lift iliompelekea moja kwa moja mpaka juu , akitaka kwenda kuonana na Regina maana alimpigia kuwahi.
Dakika ambayo lift inafunguka Regina alikuwa mbele yake akionekana alikuwa tayari ashamaliza siku.
“Huna haja ya kutoka tunaelekea hospitalini”Aliongea Regina huku akimwangalia Hamza bila ya kubadilisha muonekano wake
Muda huo wakati Hamza akimwangalia mrembo huyo ni kama anakumbuka maneno ya Eliza kwamba Regina anampenda ila ni kutokana na kwamba anamwigizia tu na ilimfanya kutabasamu.
Hamza anaweza kuonekana kutokuwa mtu wa kawaida na ambae ana uzoefu wa aina tofauti tofauti lakini ni mwanaume kama mwanaume mwingine tu, hakuna mwanaume ambae hatojisikia vizuri kuhisi mwanamke mrembo kama Regina anampenda.
“Sawa bosi , nitaendesha gari”Aliongea huku akiwa na tabasamu kama pana usoni , Regina kwa jinsi alivomuona Hamza akitabasamu alishindwa kujizuia na kujihisi kitu cha ajabu moyoni mwake lakini hisia za bibi yake kutokuwa na muda mrefu kuishi zilizima hali ile haraka.
Wakati Hamza akiendesha gari kuelekea hospitalini , alikuwa amefungulia mziki laini ambao ulimkonga moyo wake na kujikuta akiangalia kio cha nyuma kuona kama na Regina anafurahia mziki.
“Wife , vipi nizime mziki?”
“Usiniite na hilo jina lako”
“Bado hasira hazijaisha tu, basi nitakuitwa babe” Aliongea lakini Regina hakutaka kujibishana nae.
“Mmewezaje kupata hela yote?”Aliuliza Regina , ukweli ni kwamba tokea mwanzo alishachukulia deni lao kwa kampuni ya Dede ni hasara maana haliwezi kulipwa, licha ya kwamba bosi Laizer alikuwa na uwezo wa kulipa lakini ni ngumu kutoa milioni mia nane yote kwa wakati mmoja.
Hamza muda huo aliona hio ndio nafasi adhimu kumpigia debe Eliza ili hata ikitokea wakiendeleza mahusiano yao Regina atoe baraka zote.
“Mimi sikufanya chochote kila kitu alimaliza Lizzie, ana uwezo mkubwa sana likija swala la kazi , ni mwanamke mmoja mwenye msimamo sana , tukija kwenye tabia yaani hata usiseme..”
“Lizzie!”Regina alijikuta akimkatisha Hamza mara baada ya kusikia Hamza akitaja jina la Eliza kwa kulibadilisha kuwa Lizzie.
“Naona leo ndio unakiri , Eliza ndio mpenzi wako”
“Kwani nilishawahi kukataa . halafu unajua tokea muda mrefu unajikausha , kama ungekuwa hujui ungemwambia kuhusu kusajili ndoa?”
“Unaongea ujinga gani wewe , ni saa ngapi niliongea na Eliza kuhusu kusajili ndoa? , nilishasema hii ni siri yetu , kama ni kujua mna mahusiano zilikuwa hisia tu baada ya ile siku wakati wa mashindano niliona namna mlivyokuwa mkionyesheana ishara za kimapenzi”Aliongea Regina kwa sauti kubwa kana kwamba Hamza alikuwa na shida ya masikio.
“Haha.. Regina unajua nini huna haja ya kuficha wakati kila kitu kipo wazi , leo Eliza kaniambia anajua kuhusu sisi kusajili ndoa , kama sio wewe uliemwambia nani mwingine?”
“Sijui hata unaongea nini!, Hamza nakwambia ukweli sijaongea chochote na Eliza kuhusu maswala ya ndoa”
“Kama sio wewe ni nani sasa?”Aliongea Hamza lakini kwa jinsi Regina alivyokuwa akionekana , ilionyesha hakuwa akidanganhya.
“Mimi sijui lakini kweli sio mimi”
“Nilivyoona umempatia gari la bei ghali na alivyoniambia anajua kuhusu sisi nilijua umempa gari kwa ajili ya kumtuliza , kumbe sio wewe?”
Kwa bahati nzuri au mbaya , kitendo cha Hamza kutamka hayo maneno hayakumfurahisha kabisa Regina na alinuna palepale zaidi ya alivyokuwa mwanzo
“Unaongea nini wewe , kwahio unadhani nimempa gari ili niwe na wewe, unajikuta nani kwa mfano”
Hamza mara baada ya kusikia sauti hio ya chuki kutoka kwa Regina alijikuta akinywea , hakujua kama maneno yake yalikuwa na zaidi ya maana
“Sijamaanisha hivyo , wewe ni mwanamke unaejiamini na mrembo huna haja ya kujishusha mbele yake , ninachomaanisha niliamini kutokana na moyo wako mzuri umempa kwa nia njema tu…”
Hamza alitaka kujielezea kadri awezavyo lakini aliona kadri alivyokuwa akiongea ni kama anazidi kukosea.
Regina upande wake alikuwa na hasira kiasi kwamba kifua kilikuwa kikipanda na kushuka.
“Kwahio unadhani nakupenda sana kiasi cha kutaka kukugombania na Eliza , mshenzi wewe shuka kwenye gari yangu?”
“Regina usiwe na hasira , nimekosea kweli , sikumaanisha hivyo , sijui hata ubongo wangu unafikiria nini mpaka kuonge ahivyo , nisamehe”
“Eti nimekosea , hiko ndio kilichopo ndani ya moyo wako”
“Hamna, sio kweli”
“Ndio unachowaza”
“Kila mtu anakosea Regina , haina haja ya kutafuna meneno yangu kama yalivyo”
“Kutafuna!, kwahio unaniona nimekuwa mbuzi ,unamaanisha naongea kitu ambacho hakina msingi?”
“No, no , no , no… Regina sio hivyo…, punguza jazba basi , mwenyewe nina mawazo kibao hapa , yaani hata sijui nani kamwambia nimekuoa?”
“Shenzi wewe , mjinga… usije kuniongelesha tena”
Regina alikuwa amekasirika kiasi cha kutaka kutukana kila aina ya tusi analolijua lakini alishindwa kupata matusi na kujikuta macho yakiwa mekundu , aliishia kugeuzia macho yake nje ya dirisha la gari ili asionekane anataka kulia.
Hamza alijikuta akihema kwa nguvu na kujiambia anapaswa kujifunza vizuri kiswahili maana kauli zake zinaonyesha kubeba zaidi ya maana na kumkasirisha mrembo huyo kila akiongea,
Mara baada ya kufika hospitalini na kwenda wodi ya Bibi Mirium walichokiona kiliwashangaza , Bibi yake Regina ni kama alikuwa ameshapona na amekaa kitandani akipiga stori na Shangazi huku wakicheka.
“Bibi hali yako imeimarika , naona dawa zimefanya kazi”Aliongea Regina huku akiwa na furaha kubwa , lakini upande wa Hamza alizidi kushikwa na huzuni .
Hamza alijua fika unafuu huo aliokuwa nao Bibi Mirium ni ishara kwamba muda wake wa kuondoka umewadia , hio ni kutokana na uzoefu wake.
Bibi huyo aliishia kuinua mkono wake na kumshika Regina mashavu huku wakati mmoja akimwangalia Hamza
“Hamza kuna kitu nataka kukwambia mimi mwenyewe”
“Nakusikiliza bibi niambie ni kitu gani”
“Kuna kitu ambacho mume wangu alinipatia kwa kuniusia nimpatie mume wake Regina na kwasababu ni wewe nadhani ndio muda wa kupokea”Aliongea na kumfanya Hamza mwili wake kumsisimka , pengine bibi huyu alikuwa akiharakisha swala la yeye kufunga ndoa na Regina kwa ajili ya kukamisiha misheni yake ya kumpatia kitu hicho.
Muda huo Bi Mirium alipandisha mikono yake shingoni na kufungua mkufu aliokuwa ameuvaa na palepale ilionekana pete iliokuwa imening’inizwa katika huo mkufu , ilikuwa ni pete ambayo licha ya kwamba ilionekana kama ya kawaida lakini ilikuwa ni ya aina yake, Hata Hamza alishindwa kuelewa imetengengezwa na madini gani.
Regina upande wake alionekana kutokuwa na mshangao , ni kama ameshawahi kuona hio pete muda mrefu.
“Bibi kwanini unataka kumpatia hio pete wakati sio mwanafamilia?”Aliongea Regina , ukweli ni kwamba hata yeye alishangazwa na maneno ya bibi yake , alikuwa akiijua hio pete ilikuwa ni ya thamani sana kwa babu yake na hakuwahi kuivua kipindi cha uhai wake.
“Hamza Tayari ni mume wako hivyo ni mwanfamilia na dakika anayovaa hii pete amerithi nafasi ya babu yako kama kiongozi wa familia”Aliongea Bibi Mirium huku akionekana kuwa siriasi.
Lakini upande wa Regina alijikuta akisaga meno baada ya kuona hana uwezo wa kumkatalia bibi yake , aliamua kutulia huku akijiambia atampokonya Hamza baadae.
Upande wa Hamza alijikuta akiingiwa na furaha akitamani kuona pete hio , hivyo kwa tabasamu kama lote aliipokea kwa mikono miwili na unyenyekevu mkubwa kama vile anapokea mkate wa sakramenti kanisani.
“Bibi wewe ni mkarimu mn…”
Hamza alitaka kuanza kumsifia Bibi Mirium lakini alijikuta akiishia katikati mara baada ya kuona kitu kisichokuwa cha kawaida juu ya pete hio.
Kulikuwa na mchoro wa ajabu juu ya hio pete na kwa namna ulivyowekwa ni kama vile ni pete ya kupigia mhuli.
Hamza alijikuta mapigo yake yakienda mbio huku akizidi kuikodolea macho.
“Unakodoa macho ya nini sasa, hujawahi kuona pete zenye mchoro wa mhuli”Aliongea Regina huku ikionyesha ni dhahiri hakufurahishwa Hamza kupewa ile pete.
Tofauti na Hamza hakuwa akishangaa kama pete hio ni ya muhuli , alikuwa akishangaa mchoro uliokuwa katika pete hio huku akijiuliza maswali babu yake Regina aliitolea wapi.
“Bibi hii pete inaonekana ni ya thamani kubwa… sioni kama ni sahihi kuopokea”
“Unaongea nini , inamaana unakataa zawadi yangu?”Aliongea huku tabasamu lake likimpotea.
Hamza alijikuta akikosa namna ya kujitetea , aliona kitu pekee cha kuepukana na hio pete ni kumtelekeza Regina lakini kama atakubali kuwa nae karibu basi atabeba majukumu yote yanayoambatana na hio pete.
“Kila maamuzi yana gharama yake , kumuoa huyu mwanamke inaonekana naenda kulipa gaharama kubwa mno , sijui nini kinakwenda kutokea”Aliwaza Hamza kwenye moyo wake huku wasiwasi ukimvaa.
Licha ya wasiwasi huo kwasababu yeye ndio alifanya maamuzi aliona hana cha kufanya zaidi ya kukubali.
Hamza hakuwa mtu wa kuogopa kitu , kwa mtu mwingine kwa namna ambavyo amekutana na Regina na pete hio kumfikia mkononni mwake angeweza kujiita mtu mwenye bahati lakini kwa jicho lingine inaweza kuwa zaidi ya bahati.
“Sio kama naikataa bibi , ni kwamba nimeona ni ya thamani sana”Aliongea Hamza akijibaraguza na kumfanya Bibi Marium kutabasamu huku muda huo akiangaliana na Shangazi kwa macho yaliojaa zaidi ya maana.
“Hamza nina maombi mawili”
“Nakusikiliza bibi”
“Kwanza katika kipindi chote Regina akiitwa mkeo naomba usiivue ili ikuletee bahati ya kupata watoto haraka , pili naomba kati ya watoto wako, wapili kuzaliwa jina lake la ukoo aitwe Dosam”Aliongea na kumfanya Hamza kuona maneno ni kama yanazaidi ya maana ila hata hivyo aliishia kukubali.
“Nitatimiza bibi”Aliongea Hamza na kauli ile ilimfanya Bibi Mirium kulipukwa na furaha.
Upande wa Regina alikuwa mwekundu kama yai , kadri dakika zilivyokuwa zikienda akiwa na Hamza ni kama mahusiano yao yanazidi kuwa siriasi.
“Asante sana kwa kuahidi , ya kwangu ni hayo tu , unaweza kuondoka sasa, kuna vitu nataka kuongea na Regina”
Hamza hakuwa na hiyana hivyo aliwaacha na kutoka nje.
“Bibi kwanini umempa ile pete ya babu?”Aliongea Regina kwa sauti ya kubembeleza kana kwamba anataka kumwambia bii yake ampokonye Hamza hio pete.
“Kwasababu amekubali kuipokea mwenyewe hii inamaanisha yupo tayari kuwa na wewe , hili pia ni jaribio kwako”
“Lakini bibi mimi simpendi , namchukia na napanga kuachana nae , kwanini umekazania mimi kuolewa nae?”
“Hebu acha kuongea ujinga, unaongeaje hivyo wakati ndio kwanza umeolewa?”Aliongea kwa kufoka kidogo lakini alijua amemfokea hivyo alimshika mkono tena kwa ishara ya kumbembeleza.
“Mjukuu wangu najua Hamza anaonekana kuwa na mapugufu mengi, lakini unapaswa kuniamini mimi bibi yako , ndio mwanaume pekee anaekufaa dunia hii”
“Kwanini bibi?”
“Kwasasa hata nikikuelezea huwezi kuelewa , ila baadae utakuja kunielewa”
“Bibi naogopa nitakuangusha maana sina muda wa kusubiri mpaka baadae , wakati tunakuja hapa nilitaka kumtoa kwenye gari yangu.Mtu hawezi kuchuma ua na akapenda zaidi mti wake , kwake mbele ya kila mwanamke mrembo ni dhaifu na masaa yote kila kinachomtoka kwenye mdomo wake ni uongo”Aliongea Regina.
“Regina ni kweli humpendi Hamza?”Aliuliza Bibi Mirium huku akiwa na hali ya wasiwasi.
SEHEMU YA 69.
Regina mara baada ya kuulizwa swali hilo ni kama moyo wake uliingia katika hali ya mkanganyiko na akili yake , lakini mara baada ya kufikiria kwa umakini alionekana kupata jibu.
“Kabisa bibi, yaani simpendi”Aliongea na kumfanya Bibi Mirium kuonesha hali ya kukata tamaa.
“Hata iwe hivyo hakikisha huachani nae , ukihisi kutaka kuachana nae kumbuka maneno ya bibi yako , ukiona huko mbeleni umeshindwa kumpenda kabisa basi jifanyishe unampenda . mchukulie kama kete , mtumie kwa faida yako huku ukihakikisha haondoki”Aliongea Bibi Mirium na maneno yale yalimshangaza mno Regina.
“Bibi wewe….”Aliongea lakini muda huo Bibi Mirium alionekana kuwa siriasi na kile abacho anaongea.
“Mjukuu wangu unadhani mimi bibi yako ni kipofu na sionni kinachoendelea kati yenu , lakini sitaki kuongea sana kuhusu hayo , hakikisha unamshikilia hata kama huna hisia nae”
“Lakinni bibi kwanini…”
“Hakuna cha kwanini Regina , nataka uniahidi hutoachana na Hamza”Aliongea na kumfanya Regina kuishia kung’ata lips zake.
“Bibi nimekuelewa”Aliongea na kumfanya Bibi kucheka kicheko cha ahueni.
“Mjukuu wangu wewe ni mwanamke mrembo sana , umewazidi wengi kwa uzuri , ukiongeza mbinu kidogo tu unaweza kumfanya Hamza kufa kuoza kwako na kumfanya akutii kwa kila kitu , mimi bibi yako nakuamini sana”Aliongea na kumfanya Regina mwili wake kusisimka.
Alijiuliza inamaana ndoa hudumu kutokana na kudanganyana , Regina alijikuta akijihisi vibaya kwenye moyo wake , kadri alivyokuwa akiangalia swala hilo ni kama bibi yake alikuwa na sababu kubwa
Bibi Mirium alionekana kama vile ni mtu ambae amekuwa na amani ghafla na ki uchomvu sana aliegamia mto wake.
“Nimechoka sasa , nenda kamtafute Hamza , haina haja ya kuendelea kuja kuniona”Aliongea
Regina alijikuta akishikwa na huzuni baada ya kuona bibi yae anazidi kuwa mdhaifu , alijikuta pia akishikwa na mshagao akijiuliza kwanini bibi yake alionekana kuwa na ahueni lakini ghafla tu hali yake inabadilika.
“Bibi unajisikiaje , mbona ghafla tu umekuwa…”Regina alitaka kuongea lakini alizuwa na Shangazi Mariposa.
“Regina kwasasa nendeni nyumbani kwanza na umuache apumzike”
Regina licha ya kuwa na wasiwasi mwingi alijikuta akitii na kugeuka na kutoka nje , moyo wake ulikuwa mzito mno kuondoka.
Baada ya Regina kutoka Shangazi alijikuta akivuta pumzi nyingi na kuzishusha kwa ahueni na alinyoosha mkono wake na kushika mkono wa Marium na macho yake ni kama yamebadilika ghafla na kutoa miale kama ya jua.
Alimwangalia Bibi yake Regina kwa namna ambavyo ni kama anamsindikiza huko aendako.
*******
Regina mara baada ya kutoka nje aliweza kumkuta Hamza akiwa ameegamia boneti ya gari huku akionekana kama mtu ambae anafikiria kitu, aliishia kuangalia pete ambayo amevaa kidoleni kwa sekunde kadhaa na macho yake yalionyesha kutoridhika.
“Tunza hio pete vizuri , ni mali ya familia yetu”Aliongea na kumshitua Hamza.
“Unaonaje nikikuachia uitunze”
“Sitaki , kwasababu bibi ndio kakukabidhi kwasasa siwezi kukupokonya , isitoshe haina maana hata nikiichukua”Aliongea na kumfanya Hamza asijue alie ama acheke , ukweli ni kwamba alikuwa akiwaza kama kweli pete hio ni kama ambavyo anafikiria basi kuendelea kuivaa ni kujitafutia matatizo.
“Regina wapi tunaenda?”
“Naenda kumtembelea Yonesi hospitalini”Aliongea na kumfanya Hamza pia kukumbuka alimuacha Yonesi hospitalini , hivyo aliona sio mbaya kama ataenda kumuona pia.
Muda ambao Hamza anafika ndani ya hospitali ambayo Yonesi amelazwa alijikuta akimwangalia Regina na kujiangalia na kuona hawakuwa wamebeba chochote.
“Regina tunaenda kumuona mgonjwa lakini hakuna tulichobeba?”Aliongea na kumfanya Regina kushangaa na kuona ilikuwa ni kweli hakuna walichobeba.
“Ila tungebeba nini?”Aliuliza na kumfanya Hamza kufikiria kidogo na baada ya kugeuza macho upande wa kulia waliweza kuona kijana ambae anauza maua na kadi.
Hamza alisogelea na kisha alinunua ua na kadi ya kumtakia Yonesi kupona haraka na kisha waliongozana kuingia hospitalini upande wa wodi.
“Hili ua nikiliangalia vizuri naona kama linakufaa mno mke wangu”Aliongea Hamza.
“Halafu huelewi tu , nishakuambia usiniite hivyo”Aliongea huku akizidi kuongeza ukauzu lakini alikuwa akihema kwa nguvu kiasi kwamba alihisi kutokana na udogo wa lift Hamza atasikia mapigo yake ya moyo yalivyokuwa yakidunda.
“Acha wasiwasi , sina mpango wa kukupa zawadi ya ua”Aliongea Hamza na kumfanya Regina kuzidi kuwa kauzu.
“Bora ufanye hivyo , siku ukijipendekeza na vimaua maua hupati mshahara”Aliongea na kumfanya Hamza kuishia kutingisha mabega, ilionekana Regina kutaja mara kwa mara neno mshahara ni kumkumbusha kwamba uhusiano wao ni wa kikazi pekee na hakuna zaidi.
Wakati Hamza akiwaza hilo lift ilifungukka katika wodi ya daraja la watu muhimu na walitembea mpaka kwenye wodi namba nne , kitendo cha kusukuma mlango na kuingia ndani Hamza alijikua sura yake ikikunjamana mara baada ya kuona ndani kuna mtu tena akiwa amevalia Kombati za jeshi zilizochafuka kwa vyeo.
******
Ni muda wa saa tisa za jioni alionekana Kanali Dastani akiingia makao makuu ya kitengo cha MALIBU, huku kwa kiasi flani hatua zake zikionyesha alikuwa na haraka.
Muda huo baadhi ya wafanyakazi walikuwa wakianza kutoka kazini wakipisha zamu za jioni.
Mara baada ya kuingia kwenye lift alibonyeza kitufe cha floo ya juu zaidi, floor ambayo ofisi za wakuu zaidi yake zilipatikana.
Yeye alikuwa akiendesha idara yake kama Kanali na ofisi yake ilikuwa floor ya kumi na tisa huku ya bosi wake ikiwa floor ya ishirini.
Kitendo cha kutoka katika floor hio mtu wa kwanza kukutana nae alikuwa ni Afande Msuya mkuu msaidizi wa kitengo cha MALIBU,licha ya kwamba kivyeo wote walikuwa ni makanali lakini Msuya yeye alikuwa ni mwandamizi hivyo Dastani ilibidi kumpa heshima yake.
“Jambo afande”Alisalimia Kanali.
“Dastani hivi unajua katika hiki kitengo wewe ndio unaonekana kuwa bize sana , nimeshauriana na Afande Doswe na kuona pengine tukupunguzie majukumu”Aliongea Msuya huku akionyesha hali ya kutoridhishwa na Kanali.
“Sio kweli Afande , nilikuwa nje ya ofisi kikazi ndio maana nimechelewa kuripoti”Aliongea
“Vizuri kama ulikuwa nje ya ofisi kikazi , sasa niambie ni kazi gani hio ambayo timu yako hata hawaijui”Aliongea na kumfanya Afande Dastani wasiwasi kumvaa.
“Dastani unanipotezea muda”Sauti nyuma yao ilisikika na kumfanya Afande Msuya bila kugeuka kukunja ndita.
“Nakuja afande”Aliongea na kisha alitoa ishara ya heshima kwa Msuya na kisha kupita huku akonekana kuvuta pumzi ya ahueni.
Ukweli ni kwamba licha ya Afande Msuya kuwa mkubwa wake kazini lakini hakuwa akimuamini ni moja ya Ma’Afande ambao walijaa rushwa na hata nafasi yake hio ya umakamu aliipata kutokana na kuwa mkwe kwa Makamu wa raisi.
Kwake mtu aliekuwa akimheshimu alikuwa Afande Doswe, lakini kutokana na mara nyingi kujihusisha na maswala mengi yanayomuhusu Mheshimiwa Mbilu, Kanali Doswe alikuwa akimuweka pembeni katika misheni nyingi na watu waliokuwa wakiaminiwa ni kama Amosi na wengineo.
“Jambo Afande”.
“Kaa chini Dastani, muda umeenda nina kikao sehemu nyingine”Aliongea kwa kuamrisha na Dastani alikaa chini.
“Nimeitikia wito Afande”
“Dastani naungana na Msuya , upo bize sana kama nisingekuwa na Siwalima katika idara yako mambo mengi yangekuwa hayaendi , kwasasa umegeuka kuwa Field officer tofauti na Command officer , kama unataka naweza kukuondoa ofisini”Aliongea Afande Doswe na kumfanya Dastani kuanza kukuna kichwa akikosa jibu.
“Nadhani umezipata taarifa za kifo cha Jongwe huko ulipokuwa umejichimbia mpaka simu yako kutopatikana hewani”
“Ndio Afande , nimezipata tokea jana usiku”Aliongea.
“Jana usiku ya saa ngapi?!!”Aliuza Afande Doswe huku akionyesha mshangao kidogo.
“Usiku wa saa tano kwenda sita hivi”Aliongea huku akionyesha hali ya kuchangahyikiwa kidogo.
“Mimi mkuu wa kitengo taarifa nimepatiwa saa nane usiku, wewe umezipata saa saa tano, kwanini hukutoa taarifa mapema?”
“Afande taarifa sikuzipata”
“Unamaanisha nini?”
“Nilikuwa eneo la tukio wakati ajali inatokea”Aliongea Dastani na kauli ile kidogo ilimshangaza Afande Doswe.
“Inamaana ulishuhudia wakati ajali inatokea , ilikuwaje mpaka ukawa aneo la tukio?”Aliongea na kumfanya Kanali kukuna kichwa huku akionyesha hali ya wasiwasi.
“Ongea kanali una dakika kumi tu za kunielewesha la sivyo nakubadilishia majukumu”
“Afande nilikuwa nikiendelea na uchunguzi wa kesi namba 99”Aliongea na kumfanya Afande Doswe sura kujikunja.
“Hii kesi si imetolewa chini ya idara yako na kupatiwa Amosi?, hukupaswa kuigusa mpaka tuhuma zinazokukabili kuthibitishwa , inamaana muda wote ulikuwa bize kuvunja utaratibu wa Kitengo?”
“Afande najua ni kweli nilikuwa nikivunja utaratibu lakini yote ni kwasababu ya faida ya Kitengo chetu”
“Faida kivipi?”
“Afande nadhani hata wewe unajiuliza mpaka sasa Amosi yupo wapi, kesi namba tisini na tisa ni nyeti sana na inahitajika kutafutiwa ufumbuzi wa haraka , lakini mpaka sasa hakuna taarifa yoyote kutoka kwa Amosi , tokea mwanzo niliona hii ni kesi ambayo naweza kuitatua”Aliongea na kumfanya Afande Doswe kuvuta pumzi na kuzishusha na kisha akaangalia saa yake , ilionekana maneno ya Dastani yalikuwa na ukweli, mpaka muda huo Amosi hakujulikana alipo.
“Muda umeenda , niambie kwanini ulikuwa eneo la tukio?”
“Jana usiku wakati nikitokea Mpiji nilitumiwa ujumbe kwenye simu yangu ukinitaarifu Chendezi ametolewa Gerezani”Aliongea.
“Chendezi!”
“Ndio Afande , mfungwa wa kesi ya Ajenti Sedekia”
“Endelea”
“Wakati nikitafakati namna ya kudili na ujumbe huo nilipokea simu kutoka kwa Afande Norbert na kunipa habari juu ya ujumbe aliotumiwa na yeye”
“Unamaanisha Norbert na yeye katumiwa ujumbe kama wako?”
“Ndio katumiwa ujumbe lakini tofauti na wangu?”
“Wa kwake unasemaje?”
“Jongwe yupo hatarini”Aliongea na kumfanya Afande Doswe macho yake kucheza.
“Norbert aliniambia yupo hospitalini hivyo hawezi kutoka na alinipigia kuuliza maoni yangu juu ya ujumbe huo na nilimwambia kuhusu ujumbe wangu na ndipo tulipokubaliana mimi nifuatilie kwa undani kama ni taarifa ambayo ni sahihi”
“Kwahio ulianza kumfuatilia Jongwe”
“Ndio Afande”
“Baada ya hapo nini kilitokea?”
“Afande nilienda nyumbani kwa Jongwe baada ya kuambiwa yupo kwake lakini wakati nafika niliambiwa mheshimiwa alikuwa na kikao na Mzee Martini na kuambiwa kama nataka kuonana nae nije kesho, ila nililazimisha ni jambo muhimu sana nataka kuonana nae usiku huo hivyo nitasubiri , lakini baada ya kuonyesha msimamo wangu mtoto wa Mzee Jongwe alinipa taarifa mheshimiwa hana mgeni, bali ametoka kwenda kwenye kikao cha siri nyumbani kwa Mzee Martini , baada ya taarifa hio kuipata machale yalinicheza na haraka nilianza safari ya kwenda nyumbani kwa Mzee Martini , lakini wakati nakaribia kiwanda cha Binsulm ndio nilishuhudia gari ikilipuka”Aliongea Kanali na kumfanya Afande Doswe kupatwa na utulivu wa kutaka kusikia zaidi.
“Kama ni hivyo kwanini hukutoa taarifa?”
“Sikuwa na muda, mwanzoni sikujua gari ile ilikuwa ni ya mheshimiwa Jongwe , umakini wangu niliuelekeza katika pikipiki iliokuwa nyuma ya gari hio , kwa namna gari ilivyolipuka niliweza kugundua ni bomu mara moja kutokana na uzoefu wangu na mtu aliekuwa kwenye pikipiki nilimtilia mashaka kushika rimoti mara baada ya kuigeuza na kurudi alikotokea uzuri tulikuwa uelekeo sawa”
“Kwa maana hio ulianza kumfukuzia?”
“Ndio Afande”Aliongea na kumfanya Afande Doswe uso wake kucheza kidogo.
“Hilo lilikuwa swala la kutaarifu polisi na hata kama ulitaka kuhusisha kitengo ungempigia mkuu wa TISA, Wewe na Norbert kama mlipata ujumbe wa namna hio mlipaswa kuwasilisha makao makuu ili kuchakatwa, huo ndio utaratibu, Dastani huu nin muda wa kikao na sina muda wa kusikiliza mpaka mwisho , andika ripoti ya tukio zima na kisha unitumie kwenye barua pepe yangu, hata kama nikujirekodi fanya hivyo na unitumie kabla sijafika makao makuu ya TISA”Aliongea na kusimama.
“Ndio afande”.
“Usishahu na kuandika vifungu vya sheria ulivyovunja, asubuhi naitaka barua yako hapa na nitajua namna ya kudili na wewe”Aliongea akiwa kauzu na kisha alitoka ofisini.
Lakini kitendo cha kufungua mlango atoke alijikuta akisimama mara baada ya kuona sura aliokuwa akiitafuta.
“Amosi!!”
“Jambo Afande!!” Alisaluti Amosi.
ITAENDELEA WIKIEND NAWQKUMBUSHA TU KWENYE GRUPU IPO.SEHEMU YA 103
0687151346 -nicheki