Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #101
SEHEMU YA MWISHO
COUNT DOWN - 8
Hivyo, alijifanya mnyonge zaidi. Akajiweka kitini hapo katika hali iliyotosha kumsumbua mwanamume yeyote. Von alikwisha timiza Fula yake ya kimwili kwa Nuru. Hata hivyo, Nuru alijua fika kwamba, kutokana na tabia ya roho ya Fula ya mwanaume; dakika chache baadaye angerudiwa na Fula ileile kwa kiwango kikubwa zaidi.
“Wewe ni mshenzi…” alimchokoza tena ili atazamwe wakati huohuo akiyalegeza macho yake na kuzidi kujiweka juu ya kochi kinamna fulani.
*********
Kitu hiki ambacho asili kiliwekwa baina ya mwanaume na mwanamke, kitu ambacho hakielezekai kikamilifu kwa maneno, kilitimiza wajibu wake. Nuru alibaini kuwa Von na ukatili wake, pamoja na kuamini kwake kuwa ametosheka na kukinai, alianza upya kutaabika. Macho yake hayakuweza tena kutulia, mikono yake ilikuwa haikai pamoja. Alihangaika, akienda hapa na pale na kushika hiki na kile. Tahamaki akawa ameketi kochi moja na Nuru, mkono wake mmoja ukikosa kochi na kuangukia juu ya paja nono la Nuru.
“Wewe ni mtu mbaya sana,” Nuru alisema, sauti ikiwa laini, huku akijitia kusogea kando kidogo.
“Sikiliza…”
Nuru alijitia kumsikiliza. Alichofanya hasa ilikuwa kuupima uwezekano wa kumzidi Von maarifa aikwapue bastola yake ambayo ilikuwa imara kama hirizi katika mkono wake wa pili.
Von hakuwa mgeni kwa silaha hii ambayo ilikuwa ikitumiwa na Nuru. Alifahamu fika kuwa msichana huyu alikuwa akitumia mbinu ili ayaokoe maisha yake. Lakini kufahamu huko hakukukata shauku yake ya kutamani tena. Alitamani tena, kwa mara ya mwisho. Nuru angefanya nini? Kama kuna kisu basi Nuru alikuwa ameshika makali yake yeye akiwa ameshikilia mpini. Hata hivyo, alijua kuwa anacheza mchezo hatari, anacheza na nyoka. Haikuwa busara kuchezea roho kando ya shimo la mauti lililowazi kiasi hicho. Ni hilo ambalo lilimfanya aendelee kuishikilia bastola kama roho yake.
Wakati huo Von alikwishaibonyeza mitambo yake ambayo alisema ingemwezesha kuiona setilaiti hiyo ikishuka taratibu toka angani na kuiendea anga ya Tanzania ambapo ingesubiri muda uliopangwa kabla ya kuanza kuachia dhoruba za hewa ambayo ingezusha moto wa kutisha. Katika kioo hicho waliweza kuyaona mawingu mazitomazito yakipita katika kioo. Kisha dude la ajabu likajitokeza. Lilikuwa kubwa, jeusi lenye muundo wa ndege aina ya kunguru. Lilikuwa likisafiri kwa mwendo mkali sana kama linaloifuata televisheni hiyo.
Von aliinuka ghafla huku ameshikwa na mshangao. Aliiendea meza iliyokuwa na chombo chenye vidude vingi alivyokuwa akivibonyeza na kuvikagua kwa makini. Alibonyezabonyeza na kutazama tena katika kioo. Alikuwa kama ambaye hakuyaamini macho yake kuliona dude hilo likizidi kusogea. Mara jiji la johanesburg likajitokeza katika kioo hicho, majumba fulanifulani makubwa yakitoa nuru nyekundu kama gari linaloonyesha linaelekea upande upi. Nuru hiyo ilipokelewa au kujibiwa na dalili hiyo ya moto kutoka katika domo la chombo hicho ambacho sasa kilikuwa kikielea juu ya mji..
COUNT DOWN - 8
Hivyo, alijifanya mnyonge zaidi. Akajiweka kitini hapo katika hali iliyotosha kumsumbua mwanamume yeyote. Von alikwisha timiza Fula yake ya kimwili kwa Nuru. Hata hivyo, Nuru alijua fika kwamba, kutokana na tabia ya roho ya Fula ya mwanaume; dakika chache baadaye angerudiwa na Fula ileile kwa kiwango kikubwa zaidi.
“Wewe ni mshenzi…” alimchokoza tena ili atazamwe wakati huohuo akiyalegeza macho yake na kuzidi kujiweka juu ya kochi kinamna fulani.
*********
Kitu hiki ambacho asili kiliwekwa baina ya mwanaume na mwanamke, kitu ambacho hakielezekai kikamilifu kwa maneno, kilitimiza wajibu wake. Nuru alibaini kuwa Von na ukatili wake, pamoja na kuamini kwake kuwa ametosheka na kukinai, alianza upya kutaabika. Macho yake hayakuweza tena kutulia, mikono yake ilikuwa haikai pamoja. Alihangaika, akienda hapa na pale na kushika hiki na kile. Tahamaki akawa ameketi kochi moja na Nuru, mkono wake mmoja ukikosa kochi na kuangukia juu ya paja nono la Nuru.
“Wewe ni mtu mbaya sana,” Nuru alisema, sauti ikiwa laini, huku akijitia kusogea kando kidogo.
“Sikiliza…”
Nuru alijitia kumsikiliza. Alichofanya hasa ilikuwa kuupima uwezekano wa kumzidi Von maarifa aikwapue bastola yake ambayo ilikuwa imara kama hirizi katika mkono wake wa pili.
Von hakuwa mgeni kwa silaha hii ambayo ilikuwa ikitumiwa na Nuru. Alifahamu fika kuwa msichana huyu alikuwa akitumia mbinu ili ayaokoe maisha yake. Lakini kufahamu huko hakukukata shauku yake ya kutamani tena. Alitamani tena, kwa mara ya mwisho. Nuru angefanya nini? Kama kuna kisu basi Nuru alikuwa ameshika makali yake yeye akiwa ameshikilia mpini. Hata hivyo, alijua kuwa anacheza mchezo hatari, anacheza na nyoka. Haikuwa busara kuchezea roho kando ya shimo la mauti lililowazi kiasi hicho. Ni hilo ambalo lilimfanya aendelee kuishikilia bastola kama roho yake.
Wakati huo Von alikwishaibonyeza mitambo yake ambayo alisema ingemwezesha kuiona setilaiti hiyo ikishuka taratibu toka angani na kuiendea anga ya Tanzania ambapo ingesubiri muda uliopangwa kabla ya kuanza kuachia dhoruba za hewa ambayo ingezusha moto wa kutisha. Katika kioo hicho waliweza kuyaona mawingu mazitomazito yakipita katika kioo. Kisha dude la ajabu likajitokeza. Lilikuwa kubwa, jeusi lenye muundo wa ndege aina ya kunguru. Lilikuwa likisafiri kwa mwendo mkali sana kama linaloifuata televisheni hiyo.
Von aliinuka ghafla huku ameshikwa na mshangao. Aliiendea meza iliyokuwa na chombo chenye vidude vingi alivyokuwa akivibonyeza na kuvikagua kwa makini. Alibonyezabonyeza na kutazama tena katika kioo. Alikuwa kama ambaye hakuyaamini macho yake kuliona dude hilo likizidi kusogea. Mara jiji la johanesburg likajitokeza katika kioo hicho, majumba fulanifulani makubwa yakitoa nuru nyekundu kama gari linaloonyesha linaelekea upande upi. Nuru hiyo ilipokelewa au kujibiwa na dalili hiyo ya moto kutoka katika domo la chombo hicho ambacho sasa kilikuwa kikielea juu ya mji..