FEBIANI BABUYA
JF-Expert Member
- Mar 5, 2022
- 1,916
- 3,850
- Thread starter
- #21
HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
Episode 7
“Sijajua ulifanikiwa vipi kuwa raisi wa taifa hili hilo unalijua wewe na njia ulizopita kwani siasa ni michezo ya kijinga tu ambayo kuna muda wajinga ndiyo wanakuwa washindi huku wananchi wakipumbazwa kwamba kuna haki, sijui demokrasi na ujinga mwingine lakini kichwa chako hakikufaa kabisa uwe kwenye nafasi kubwa kama hizo maana uwezo wako ni mdogo sana kichwani. Wakati unamuinua huyo changudoa na kumpa hiyo nafasi kubwa ambayo umempa ulisahau kitu kimoja Denis”
“Kipi hicho?”
“Ulisahau kwamba madaraka huwa yanawabadilisha watu, umesahau kwamba madaraka huwa yanawafanya watu wajihisi kwamba wana nguvu kubwa sana sehemu yoyote ile ambayo wanakuwa wanaenda ndiyo sababu wakisha yapata huwa hawakumbuki tena kuhusu nyuma walikotoka wala watu ambao wamewatoa huko. Wewe hapo ulishikwa mkono na watu wengi sana ambao wamekufikisha hapo ulipo leo lakini si unakumbuka ulichokuja kuwafanya kwa baadae? Ulihisi kama watakuwa tishio kwako ukaamua kuwaua wote ili utawale kila kitu, je wewe uliwahi kuwaza hili kwa mtu ambaye ulikuwa unampa nafasi kwamba anaweza kuwa kama wewe? Kosa kubwa ambalo umelifanya ni kumchukulia kwa udogo huyo mwanamke na huenda kama ungemchukulia kwa ukubwa zaidi usingekuja kunililia hapa nikupe ushauri”
“Mhhh mze nadhani bado haujanielewa vizuri, sijaja hapa kwa ajili ya kutaka unipe shule kwamba nimeshindwa kumdhibiti huyu mwanamke au kanishinda hapana, hapa nipo nahitaji ushauri mmoja tu wa ndiyo au hapana basi, hivyo ulitakiwa kulisikiliza swali langu kwanza kabla ya kuanza kunisomea risala yako hapa”
“Unataka kumuua?” mzee huyo ni kama alielewa mapema sana dhamira ya mtu huyo licha ya kujifanya kwamba alikuwa anazunguka nayo sana.
“Ndiyo, nimekuja hapa ili unishauri kama kumuua mapema hivi itakuwa ni sawa? Maana kama nikiendelea kumpa muda anaweza kuniharibia mambo mengi sana kwa sababu hivi ninavyo zungumza nikiwa njiani kuja huku tayari kuna akaunti zangu za benki zimezuiliwa yaani haziruhusiwi kufanya miamala kitu ambacho kimenichukiza sana kufanyiwa jambo la kijinga na mwanafunzi wangu mwenyewe nadhani natakiwa kulifanyia maamuzi haraka sana”
“Hilo ndilo litakuwa kosa lako kubwa zaidi kuwahi kulifanya kwenye maisha yako”
“Una maanisha?”
“Najua kwa sasa una watu wengi sana kwa upande wako ambao wanakusikiliza na kukutii kwa lolote na wapo tayari hata kufa kwa ajili yako pia na natambua kwamba kwa sasa huenda una mengi ambayo umejifunza ila umeniacha mimi hai kwa ajili ya kuendelea kukupa maarifa ila hivi umewaza kwamba ni kwa sababu gani labda mwanamke huyo ameamua kubadilika haraka sana namna hiyo wakati anakujua kabisa kwamba wewe ni binadamu mkatili sana?”
“Nadhani bado hajanijua vizuri ndiyo maana anahisi anaweza kunimudu”
“Najua kwamba huwa unaigiza kwa tabasamu lako mbele za watu ndilo linalo wafanya watu wahisi kwamba wewe ni mtu muungwana sana ila hawajui binadamu aliyepo nyuma ya hilo tabasamu, huenda ni kweli umeishi hivyo hata kwake pia kwa kumuigizia kwamba wewe ni mtu mwepesi tofauti na ulivyo wewe lakini unatakiwa kujiuliza kwamba kwa muda wote huo ambao huyo binti alikuwa na wewe unahisi hakuutambua udhaifu wako hata kidogo? Unahisi hajui baadhi ya mambo yako ya siri ambayo unahisi hayajui? Unadhani nini kinampa jeuri ya kuanza kukugeuka tena unasema ameanza mapema kabisa hivi?”
“Unanishauri nini?”
“Nitakuelekeza kwa mfano halisi. Biashara ya kuuza miili kwa wanawake imeandikwa tangu miaka na miaka huko kabla hata sisi hatupo kwenye dunia hii kama ambavyo vitabu vitakatifu vinaeleza hivyo ni biashara endelevu ya vizazi na vizazi kama ambavyo sisi tunaendelea kuzaliwa. Kwahiyo hii inaonyesha kwamba hii biashaara haiwezi kuja kuisha hapa duniani ni mpaka siku ya mwisho iweze kufika kama ambavyo tumeahidiwa kwenye vitabu vya dini. Kuna baadhi ya viongozi waliwahi kujaribu sana kuiua biashara hii hata kabla ya vita vya kwanza vya dunia kufanyika lakini walishindwa na hata dunia ya sasa kwa miaka takribani hamsini viongozi wa dini wanajitahidi sana kukemea hii biashara iishe kwani inahatarisha sana mmomonyoko wa maadili na kuleta tamaduni mbaya za kutoka magharibi ambazo zinafanya tamaduni zetu kufa lakini wameshindwa licha ya mamlaka zenye nguvu kuingilia na kupinga kwa nguvu lakini bado imeshindikana. Unahisi ni kwanini jambo hilo limeshindikana kabisa kuisha?
“Ni kwa sababu ni biashara ambayo ina manufaa makubwa sana duniani kwa sasa na watu ambao wanaihitaji ni wengi zaidi ya wale ambao wanahitaji ipotee kwenye mifumo”
“Umejibu sahihi lakini hiyo ni sababu nyepesi sana ambayo haiwezi kuwa na mashiko ya kuifanya isipotee au washindwe kuipoteza kabisa. Uhalisia ni kwamba kwa makusudi au kwa bahati mbaya hawa ambao wanataka hii biashara ifungwe wameshindwa kabisa kujua chanzo chake hasa ni nini wanaishia kukomaa na matokeo yake tu, huwezi kulikomesha jambo kwa kupambana na matokeo yake kwa sababu hata kama utayamaliza yale matokeo ilimradi hicho kitu bado kipo basi kitaendelea kuleta matokeo mengine kila kuitwapo leo na ndiyo maana biashara hiyo haiwezi kuja kuisha kamwe. Kuna wanawake wanafanya hiyo biashara kwa sababu maisha ni magumu sana na kuna watu wengi sana ambao wanawategemea nyuma yao hivyo inafika mahali wanakuwa hawana namna tena zaidi ya kuifanya tu ili wajikwamue kimaisha lakini kuna wengine wanaifanya kwa sababu watu mnaokabidhiwa nafasi kubwa ndani ya nchi hamjali lolote, mnajaza ndugu zenu ambao ni wapumbavu kupitiliza kwenye mifumo ya ajira huku vijana ambao wanastahili mkiwanyima ajira halafu kila siku mnaanza kuwatukana na kuwadhihaki kwamba wanauza miili yao, mara wanawake wote ni Malaya tu, hivi ulishawahi kukaa chini ukajiuliza haya maswali kama kiongozi? Nakuhakikishia hii biashara haiwezi kuisha kamwe kama vyanzo vyake havijajulikana, kuna wanawake wanafanya hivyo kwa sababu ya msukumo wa maisha mazuri ambayo wanayaona kwa wenzao lakini kuna wengine wanafanya ikiwa ni madhara mabaya ya utumiaji wa mitandao ya kijamii bila kusahau msukumo wa marafiki na baadhi ya mambo mengi sana ambayo najua unayafahamu kwenye kichwa chako. Umenielewa nilicho maanisha kutokana na jambo lako ambalo ulikuwa unahitaji msaada?” Denis Kijazo alibaki anacheka tu akiwa anamwangalia mzee huyo, alikuwa ni mzee mwenye akili sana kwa sababu hata elimu yake ilikuwa ni kubwa mno ndiyo maana aliaminiwa mpaka kuwa gavana wa benki kuu ya taifa la Tanzania.
“Moja kati ya ushindi mkubwa ambao niliupatia mezani ni kukuacha wewe hai, kuna muda nawaza kama ningekuua mapema basi ningekuwa nakosa maamuzi ya busara kwenye mambo yangu mengi sana ambayo huenda kwa baadae yangekuja kunileta madhara makubwa sana. Huyu mwanamke natakiwa kujua kwanza ni kitu gani kinampa sana kiburi lakini pia huenda kuna watu ambao wanampa kiburi na kama ulivyosema kwamba nilimchukulia kwa udogo huenda aliitumia nafasi hiyo kutengeneza watu wake ambao alijua hata kukiwa na matatizo wanaweza kumlinda na ndiyo maana anajiamini sana” mzee huyo alitikisa kichwa kuonyesha kukubaliana na jambo hilo kwamba alitakiwa kwanza kujua chanzo na sababu ya mwanamke huyo kubadilika ghafla sana ilikuwa ni nini na ni nani na nani ambao walikuwa wanamzunguka kiasi kwamba wakampa hiyo nguvu ya kuweza kujiamini sana kiasi hicho.
“Ukishindwa kuzimudu hisia zako ambazo zinakuletea mihemko kwenye mwili wako basi duniani mtu yeyote anaweza kukuendesha. Nimemaliza kukueleza ulicho kijia naomba sana niione familia yangu japo kwa picha tu” alipogusia jambo la familia yake aliongea kwa kutia huruma sana na mwanaume ambaye alikuwa mbele yake aliitoa simu yake na kumuonyesha mzee huyo picha ambayo ilimtoa sana machozi. Alikuwa anawaona watu wanne kwenye picha moja ambapo alikuwa ni mkewe, mtoto wake wa kwanza wa kike pamoja na mapacha wawili wa kiume ambao ndio walikuwa ni watoto wake wa mwisho.
“Usijali familia yako ipo salama na inaishi kwa furaha kabisa na kesho ni siku ya kuzaliwa ya hao mapacha. Wote wanajua kwamba wewe ulishakufa tayari wameanza kukusahau kwa sasa zaidi ya kuzikumbuka picha zako tu, moja kati ya makosa ambayo uliwahi kuyafanya kwenya maisha yako ni kuamua kupingana na kile ambacho mimi nilikuwa nakitaka kama ambavyo huyu mwanamke naye ameamua kufanya, huenda yeye atakuwa na majuto makali zaidi hata ya wewe. Kwaheri Professor Mande” alitamka huku akiwa ananyanyuka na kutoka ndani ya chumba hicho ambacho baada ya yeye kutoka tu kiliweza kujifunga chenyewe, aliingia humo akiwa na hasira sana lakini alitoka akiwa mwepesi na akiwa anajua ni wapi ambapo alitakiwa kuanzia ili kuweza kutimiza jambo hilo kwa usahihi pasipo kujulikana kwamba alikuwa anahusika na lolote lile huku professor Mande akibaki kwenye majozi makubwa sana kwani ulipita muda mrefu sana bila kuweza kuiona familia yake huku familia hiyo ikiwa inajua kwamba yeye alishakufa muda mrefu sana.
Chumba kilikuwa kina kiza kila sehemu kasoro katikati tu ya chumba hicho ndipo palikuwa na mwanga ambapo wanaume wanne walikuwa wamemzunguka mwanaume mmoja wote wakiwa vifua wazi bila mashati. Mmoja alizunguka kwa sarakasi huku akijipinda ya kuyatuma mateke yake kwa mwanaume ambaye alikuwa katikati yao lakini mahesabu yake hayakwenda sawa baada ya ngumi nzito kutua kwenye bega lake na kumfanya adondoke vibaya chini lakini alifanikiwa kutanguliza mkono mmoja ambao ulifanikiwa kuupa balansi mwili wake usiweze kwenda wote kabisa chini ila kwa bahati mbaya wakati anatua na mkono huo ulipigwa na teke lenye kilo nyingi na kuvunjika ambapo alipiga kelele sana ila alitulia baada ya teke kutua kwenye uso wake na kumpeleka ukutani ambako kulikuwa na kiza.
Tukio lilikuwa la sekunde ishirini tu wakati mwanaume huyo ambaye alikuwa pekeyake akiyakwepa mateke na ngumi za wanaume wengine watatu, alipigwa ngumi ya mbavu na mwanaume mmoja ambapo baada ya kugeuka kwa hasira alimkita na viganja mwanaume mmoja kwenye masikio yake mpaka masikio yakaziba kabisa akawa hasikii kile ambacho kilikuwa kinaendelea hapo, alipigwa ngumi nyingi za kifua ambapo alibaki anatetemeka huku akiwa anashuka chini taratibu na mdomoni akiwa na damu nyingi sana. Wawili walikuwa wanamshangaa mwenzo alivyokuwa anashuka kama utani, walikwenda kwa pamoja mmoja akiwa chini na mwingine akilenga upande wa juu. Mwanaume huyo alijigeuza haraka sana ambapo alimkwepa wa chini ambaye alishika sakafu na kuyazungusha mateke yake kwa kasi ya ajabu hivyo aliyakwepa kwa sarakasi kisha akakutana na wa juu ambaye alimpiga double kick mbili za haraka haraka ambazo zilimzoa mpaka ukutani ambako kilisikika kishindo kikali sana na sauti ya mtu mara moja tu ikiwa inapiga kelele kisha kukawa kimya ghafla sana.
Wakati anatua chini yule mmoja alikuwa amezungusha mateke mengine lakini yeye alitua nyuma kidogo kwa hatua moja hivyo mateke hayakumpata lakini wakati yule ambaye alikuwa chini ananyanyuka alikuwa ameshika kisu mkononi ambacho bila shaka alikificha kwenye kiuno kwake maana kwenye buti isingewezekana kwa sababu wote walikuwa miguu mitupu bila viatu. Hivyo alikizungusha kisu chake ambacho kilimkosa mwenzake shingoni mkono ukawa umepitiliza. Wakati anahitaji kuurudisha mkono huo ukiwa na kisu shingoni kwa mwanaume huyo, alikuwa ameukwepa na kufanikiwa kuudaka ambapo aliubinya kwa nguvu mshipa mmoja wa mkono wa mwanaume aliyekuwa amekishika kisu hicho akaishia kupiga kelele kwa maumivu hali ambayo ilipelekea kisu hicho kumponyoka kwenye mkono wake na kutua kwenye mkono wa mwanaume ambaye alikuwa anakabiliana naye.
Mwanaume huyo baada ya kukidaka kisu hicho alijizungusha kwa kasi kwenye mkono wa mwenzake na kukizamisha kisu hicho juu ya bega kwa nguvu kisha akakichomoa kwa nguvu na kuuchana chana vibaya sana mkono. Mwanaume huyo alipokea maumivu makali sana, upigaji wake wa kelele ulifanya apokee ngumi nzito ya shingo ambayo ilimfanya apoteze fahamu na kudondokea chini. Dakika moja tu pekee na sekunde chache sana zilifanya mwanaume huyo aimalize kazi. Ulisika mlio wa makofi mtu akiwa anapongea kile kilichokuwa kimefanyika hapo na baada ya muda mfupi taa iliwashwa humo ndani akawa anaonena mheshimiwa raisi Teodensia Mpanzi ndiye ambaye alikuwa anapiga makofi hayo kumpongeza kijana wake.
Episode 7 nasema bye.
Tchao
Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
Episode 7
“Sijajua ulifanikiwa vipi kuwa raisi wa taifa hili hilo unalijua wewe na njia ulizopita kwani siasa ni michezo ya kijinga tu ambayo kuna muda wajinga ndiyo wanakuwa washindi huku wananchi wakipumbazwa kwamba kuna haki, sijui demokrasi na ujinga mwingine lakini kichwa chako hakikufaa kabisa uwe kwenye nafasi kubwa kama hizo maana uwezo wako ni mdogo sana kichwani. Wakati unamuinua huyo changudoa na kumpa hiyo nafasi kubwa ambayo umempa ulisahau kitu kimoja Denis”
“Kipi hicho?”
“Ulisahau kwamba madaraka huwa yanawabadilisha watu, umesahau kwamba madaraka huwa yanawafanya watu wajihisi kwamba wana nguvu kubwa sana sehemu yoyote ile ambayo wanakuwa wanaenda ndiyo sababu wakisha yapata huwa hawakumbuki tena kuhusu nyuma walikotoka wala watu ambao wamewatoa huko. Wewe hapo ulishikwa mkono na watu wengi sana ambao wamekufikisha hapo ulipo leo lakini si unakumbuka ulichokuja kuwafanya kwa baadae? Ulihisi kama watakuwa tishio kwako ukaamua kuwaua wote ili utawale kila kitu, je wewe uliwahi kuwaza hili kwa mtu ambaye ulikuwa unampa nafasi kwamba anaweza kuwa kama wewe? Kosa kubwa ambalo umelifanya ni kumchukulia kwa udogo huyo mwanamke na huenda kama ungemchukulia kwa ukubwa zaidi usingekuja kunililia hapa nikupe ushauri”
“Mhhh mze nadhani bado haujanielewa vizuri, sijaja hapa kwa ajili ya kutaka unipe shule kwamba nimeshindwa kumdhibiti huyu mwanamke au kanishinda hapana, hapa nipo nahitaji ushauri mmoja tu wa ndiyo au hapana basi, hivyo ulitakiwa kulisikiliza swali langu kwanza kabla ya kuanza kunisomea risala yako hapa”
“Unataka kumuua?” mzee huyo ni kama alielewa mapema sana dhamira ya mtu huyo licha ya kujifanya kwamba alikuwa anazunguka nayo sana.
“Ndiyo, nimekuja hapa ili unishauri kama kumuua mapema hivi itakuwa ni sawa? Maana kama nikiendelea kumpa muda anaweza kuniharibia mambo mengi sana kwa sababu hivi ninavyo zungumza nikiwa njiani kuja huku tayari kuna akaunti zangu za benki zimezuiliwa yaani haziruhusiwi kufanya miamala kitu ambacho kimenichukiza sana kufanyiwa jambo la kijinga na mwanafunzi wangu mwenyewe nadhani natakiwa kulifanyia maamuzi haraka sana”
“Hilo ndilo litakuwa kosa lako kubwa zaidi kuwahi kulifanya kwenye maisha yako”
“Una maanisha?”
“Najua kwa sasa una watu wengi sana kwa upande wako ambao wanakusikiliza na kukutii kwa lolote na wapo tayari hata kufa kwa ajili yako pia na natambua kwamba kwa sasa huenda una mengi ambayo umejifunza ila umeniacha mimi hai kwa ajili ya kuendelea kukupa maarifa ila hivi umewaza kwamba ni kwa sababu gani labda mwanamke huyo ameamua kubadilika haraka sana namna hiyo wakati anakujua kabisa kwamba wewe ni binadamu mkatili sana?”
“Nadhani bado hajanijua vizuri ndiyo maana anahisi anaweza kunimudu”
“Najua kwamba huwa unaigiza kwa tabasamu lako mbele za watu ndilo linalo wafanya watu wahisi kwamba wewe ni mtu muungwana sana ila hawajui binadamu aliyepo nyuma ya hilo tabasamu, huenda ni kweli umeishi hivyo hata kwake pia kwa kumuigizia kwamba wewe ni mtu mwepesi tofauti na ulivyo wewe lakini unatakiwa kujiuliza kwamba kwa muda wote huo ambao huyo binti alikuwa na wewe unahisi hakuutambua udhaifu wako hata kidogo? Unahisi hajui baadhi ya mambo yako ya siri ambayo unahisi hayajui? Unadhani nini kinampa jeuri ya kuanza kukugeuka tena unasema ameanza mapema kabisa hivi?”
“Unanishauri nini?”
“Nitakuelekeza kwa mfano halisi. Biashara ya kuuza miili kwa wanawake imeandikwa tangu miaka na miaka huko kabla hata sisi hatupo kwenye dunia hii kama ambavyo vitabu vitakatifu vinaeleza hivyo ni biashara endelevu ya vizazi na vizazi kama ambavyo sisi tunaendelea kuzaliwa. Kwahiyo hii inaonyesha kwamba hii biashaara haiwezi kuja kuisha hapa duniani ni mpaka siku ya mwisho iweze kufika kama ambavyo tumeahidiwa kwenye vitabu vya dini. Kuna baadhi ya viongozi waliwahi kujaribu sana kuiua biashara hii hata kabla ya vita vya kwanza vya dunia kufanyika lakini walishindwa na hata dunia ya sasa kwa miaka takribani hamsini viongozi wa dini wanajitahidi sana kukemea hii biashara iishe kwani inahatarisha sana mmomonyoko wa maadili na kuleta tamaduni mbaya za kutoka magharibi ambazo zinafanya tamaduni zetu kufa lakini wameshindwa licha ya mamlaka zenye nguvu kuingilia na kupinga kwa nguvu lakini bado imeshindikana. Unahisi ni kwanini jambo hilo limeshindikana kabisa kuisha?
“Ni kwa sababu ni biashara ambayo ina manufaa makubwa sana duniani kwa sasa na watu ambao wanaihitaji ni wengi zaidi ya wale ambao wanahitaji ipotee kwenye mifumo”
“Umejibu sahihi lakini hiyo ni sababu nyepesi sana ambayo haiwezi kuwa na mashiko ya kuifanya isipotee au washindwe kuipoteza kabisa. Uhalisia ni kwamba kwa makusudi au kwa bahati mbaya hawa ambao wanataka hii biashara ifungwe wameshindwa kabisa kujua chanzo chake hasa ni nini wanaishia kukomaa na matokeo yake tu, huwezi kulikomesha jambo kwa kupambana na matokeo yake kwa sababu hata kama utayamaliza yale matokeo ilimradi hicho kitu bado kipo basi kitaendelea kuleta matokeo mengine kila kuitwapo leo na ndiyo maana biashara hiyo haiwezi kuja kuisha kamwe. Kuna wanawake wanafanya hiyo biashara kwa sababu maisha ni magumu sana na kuna watu wengi sana ambao wanawategemea nyuma yao hivyo inafika mahali wanakuwa hawana namna tena zaidi ya kuifanya tu ili wajikwamue kimaisha lakini kuna wengine wanaifanya kwa sababu watu mnaokabidhiwa nafasi kubwa ndani ya nchi hamjali lolote, mnajaza ndugu zenu ambao ni wapumbavu kupitiliza kwenye mifumo ya ajira huku vijana ambao wanastahili mkiwanyima ajira halafu kila siku mnaanza kuwatukana na kuwadhihaki kwamba wanauza miili yao, mara wanawake wote ni Malaya tu, hivi ulishawahi kukaa chini ukajiuliza haya maswali kama kiongozi? Nakuhakikishia hii biashara haiwezi kuisha kamwe kama vyanzo vyake havijajulikana, kuna wanawake wanafanya hivyo kwa sababu ya msukumo wa maisha mazuri ambayo wanayaona kwa wenzao lakini kuna wengine wanafanya ikiwa ni madhara mabaya ya utumiaji wa mitandao ya kijamii bila kusahau msukumo wa marafiki na baadhi ya mambo mengi sana ambayo najua unayafahamu kwenye kichwa chako. Umenielewa nilicho maanisha kutokana na jambo lako ambalo ulikuwa unahitaji msaada?” Denis Kijazo alibaki anacheka tu akiwa anamwangalia mzee huyo, alikuwa ni mzee mwenye akili sana kwa sababu hata elimu yake ilikuwa ni kubwa mno ndiyo maana aliaminiwa mpaka kuwa gavana wa benki kuu ya taifa la Tanzania.
“Moja kati ya ushindi mkubwa ambao niliupatia mezani ni kukuacha wewe hai, kuna muda nawaza kama ningekuua mapema basi ningekuwa nakosa maamuzi ya busara kwenye mambo yangu mengi sana ambayo huenda kwa baadae yangekuja kunileta madhara makubwa sana. Huyu mwanamke natakiwa kujua kwanza ni kitu gani kinampa sana kiburi lakini pia huenda kuna watu ambao wanampa kiburi na kama ulivyosema kwamba nilimchukulia kwa udogo huenda aliitumia nafasi hiyo kutengeneza watu wake ambao alijua hata kukiwa na matatizo wanaweza kumlinda na ndiyo maana anajiamini sana” mzee huyo alitikisa kichwa kuonyesha kukubaliana na jambo hilo kwamba alitakiwa kwanza kujua chanzo na sababu ya mwanamke huyo kubadilika ghafla sana ilikuwa ni nini na ni nani na nani ambao walikuwa wanamzunguka kiasi kwamba wakampa hiyo nguvu ya kuweza kujiamini sana kiasi hicho.
“Ukishindwa kuzimudu hisia zako ambazo zinakuletea mihemko kwenye mwili wako basi duniani mtu yeyote anaweza kukuendesha. Nimemaliza kukueleza ulicho kijia naomba sana niione familia yangu japo kwa picha tu” alipogusia jambo la familia yake aliongea kwa kutia huruma sana na mwanaume ambaye alikuwa mbele yake aliitoa simu yake na kumuonyesha mzee huyo picha ambayo ilimtoa sana machozi. Alikuwa anawaona watu wanne kwenye picha moja ambapo alikuwa ni mkewe, mtoto wake wa kwanza wa kike pamoja na mapacha wawili wa kiume ambao ndio walikuwa ni watoto wake wa mwisho.
“Usijali familia yako ipo salama na inaishi kwa furaha kabisa na kesho ni siku ya kuzaliwa ya hao mapacha. Wote wanajua kwamba wewe ulishakufa tayari wameanza kukusahau kwa sasa zaidi ya kuzikumbuka picha zako tu, moja kati ya makosa ambayo uliwahi kuyafanya kwenya maisha yako ni kuamua kupingana na kile ambacho mimi nilikuwa nakitaka kama ambavyo huyu mwanamke naye ameamua kufanya, huenda yeye atakuwa na majuto makali zaidi hata ya wewe. Kwaheri Professor Mande” alitamka huku akiwa ananyanyuka na kutoka ndani ya chumba hicho ambacho baada ya yeye kutoka tu kiliweza kujifunga chenyewe, aliingia humo akiwa na hasira sana lakini alitoka akiwa mwepesi na akiwa anajua ni wapi ambapo alitakiwa kuanzia ili kuweza kutimiza jambo hilo kwa usahihi pasipo kujulikana kwamba alikuwa anahusika na lolote lile huku professor Mande akibaki kwenye majozi makubwa sana kwani ulipita muda mrefu sana bila kuweza kuiona familia yake huku familia hiyo ikiwa inajua kwamba yeye alishakufa muda mrefu sana.
Chumba kilikuwa kina kiza kila sehemu kasoro katikati tu ya chumba hicho ndipo palikuwa na mwanga ambapo wanaume wanne walikuwa wamemzunguka mwanaume mmoja wote wakiwa vifua wazi bila mashati. Mmoja alizunguka kwa sarakasi huku akijipinda ya kuyatuma mateke yake kwa mwanaume ambaye alikuwa katikati yao lakini mahesabu yake hayakwenda sawa baada ya ngumi nzito kutua kwenye bega lake na kumfanya adondoke vibaya chini lakini alifanikiwa kutanguliza mkono mmoja ambao ulifanikiwa kuupa balansi mwili wake usiweze kwenda wote kabisa chini ila kwa bahati mbaya wakati anatua na mkono huo ulipigwa na teke lenye kilo nyingi na kuvunjika ambapo alipiga kelele sana ila alitulia baada ya teke kutua kwenye uso wake na kumpeleka ukutani ambako kulikuwa na kiza.
Tukio lilikuwa la sekunde ishirini tu wakati mwanaume huyo ambaye alikuwa pekeyake akiyakwepa mateke na ngumi za wanaume wengine watatu, alipigwa ngumi ya mbavu na mwanaume mmoja ambapo baada ya kugeuka kwa hasira alimkita na viganja mwanaume mmoja kwenye masikio yake mpaka masikio yakaziba kabisa akawa hasikii kile ambacho kilikuwa kinaendelea hapo, alipigwa ngumi nyingi za kifua ambapo alibaki anatetemeka huku akiwa anashuka chini taratibu na mdomoni akiwa na damu nyingi sana. Wawili walikuwa wanamshangaa mwenzo alivyokuwa anashuka kama utani, walikwenda kwa pamoja mmoja akiwa chini na mwingine akilenga upande wa juu. Mwanaume huyo alijigeuza haraka sana ambapo alimkwepa wa chini ambaye alishika sakafu na kuyazungusha mateke yake kwa kasi ya ajabu hivyo aliyakwepa kwa sarakasi kisha akakutana na wa juu ambaye alimpiga double kick mbili za haraka haraka ambazo zilimzoa mpaka ukutani ambako kilisikika kishindo kikali sana na sauti ya mtu mara moja tu ikiwa inapiga kelele kisha kukawa kimya ghafla sana.
Wakati anatua chini yule mmoja alikuwa amezungusha mateke mengine lakini yeye alitua nyuma kidogo kwa hatua moja hivyo mateke hayakumpata lakini wakati yule ambaye alikuwa chini ananyanyuka alikuwa ameshika kisu mkononi ambacho bila shaka alikificha kwenye kiuno kwake maana kwenye buti isingewezekana kwa sababu wote walikuwa miguu mitupu bila viatu. Hivyo alikizungusha kisu chake ambacho kilimkosa mwenzake shingoni mkono ukawa umepitiliza. Wakati anahitaji kuurudisha mkono huo ukiwa na kisu shingoni kwa mwanaume huyo, alikuwa ameukwepa na kufanikiwa kuudaka ambapo aliubinya kwa nguvu mshipa mmoja wa mkono wa mwanaume aliyekuwa amekishika kisu hicho akaishia kupiga kelele kwa maumivu hali ambayo ilipelekea kisu hicho kumponyoka kwenye mkono wake na kutua kwenye mkono wa mwanaume ambaye alikuwa anakabiliana naye.
Mwanaume huyo baada ya kukidaka kisu hicho alijizungusha kwa kasi kwenye mkono wa mwenzake na kukizamisha kisu hicho juu ya bega kwa nguvu kisha akakichomoa kwa nguvu na kuuchana chana vibaya sana mkono. Mwanaume huyo alipokea maumivu makali sana, upigaji wake wa kelele ulifanya apokee ngumi nzito ya shingo ambayo ilimfanya apoteze fahamu na kudondokea chini. Dakika moja tu pekee na sekunde chache sana zilifanya mwanaume huyo aimalize kazi. Ulisika mlio wa makofi mtu akiwa anapongea kile kilichokuwa kimefanyika hapo na baada ya muda mfupi taa iliwashwa humo ndani akawa anaonena mheshimiwa raisi Teodensia Mpanzi ndiye ambaye alikuwa anapiga makofi hayo kumpongeza kijana wake.
Episode 7 nasema bye.
Tchao
Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app