Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
[emoji91][emoji91][emoji91]HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
Episode 27
Alifika huko akiwa hajui kwamba angeenda kufanya nini, alianza kufanya kazi ya kukaanga samaki na kuuza chakula huku uzuri wake ndio ukiwa mdhamana wake mkubwa wa kupata mtaji kutoka kwa wanaume mafisi ambao walikuwa wanavua samaki. Baadae alibahatika kufungua kimgahawa chake kidogo na haukupita muda sana akawa amejifungua mtoto wa kike ambaye jina lake alimuita Brandina na baba yake jina lake alikuwa anaitwa Elkana hivyo akaamua kumpatia jina halisi kabisa la baba yake.
Maisha kwake hayakuwa mazuri sana wala mabaya sana lakini alimshukuru Mungu kwani alifanikiwa kumlea vizuri sana mwanae huyo mpaka binti yake alipo anza kujitambua wote wakiwa wanasaidiana kazi ya mgahawa pale ambapo mwanae angetoka shule ambayo alikuwa anasoma. Mwanamama huyo alianza kuumwa na hali yake haikuwa nzuri kwa sababu kasi ya ugonjwa ambao alikuwa nao ulionekana kuwa na nguvu kulizidi tumaini ambalo alikuwa nalo na hakuchukua siku nyingi sana akawa amepoteza maisha huku akiwa amemwachia mwanae diary yake ambayo ilikuwa na taarifa zote za maisha yake.
Taarifa zilikuwa zinaelezea uhalisia wa maisha ambayo mama yake aliyaishi, maisha ambayo alikutana nayo wakati anaendelea wa kuishi lakini vitu vya kutisha ambavyo alifanyiwa akiwa anaishi mpaka siku anakufa. Brandina alidondosha chozi kwa huruma kubwa sana kwa sababu alihisi kwamba mama yake alikufa tu hivi hivi lakini aligundua kwamba mama yake alikufa kwa homa ya ini, homa ambayo aliandika kwamba aliambukizwa na wale watu ambao walimbaka ambao walikuwa ndugu wa yule bosi wake.
Mama yake alimsisitiza mwanae kwamba baba yake mzazi aliuawa na wanafamilia hao, mama yake alimkumbusha kwamba hiyo ndiyo familia ambayo ilimfanya yeye aishi maisha magumu sana kwani kama sio hao basi angezaliwa kwenye maisha ambayo yalikuwa mazuri lakini alimtaka mwanae asije kusahau kwamba wanafamilia hao ndio ambao walifanya mama yake mzazi kuweza kupoteza maisha hivyo lilikuwa ni jukumu lake na uamuzi wake kama alikuwa anahitaji kuwasamehe au asiwasamehe.
Brandina wakati anaisoma hiyo diary alikuwa ni binti ambaye alikuwa anakua kwa kasi sana, binti ambaye aliichukua sura na rangi ya mama yake ambayo ilimfanya kuwa mwanamke mrembo sana zaidi hata ya mama yake mzazi. Uzuri wake ulifanya akawa kivutio kikubwa sana kwa watu ambao walikuwa wanaenda kisiwani hapo, urembo wake ulikuwa habari ambayo ilikuwa inaenea mithili ya upepo uvumao kwa nguvu. Mgahawa wake ambao aliachiwa na mama yake ulizidi kupata wateja wengi kila siku huku kila mtu akiwa anatamani sana kuweza kuhudumiwa na mwanamke huyo ambaye alikuwa akitabasamu watu wengi walikuwa wanafurahia sana kuwa karibu naye.
Licha ya kuwa kwenye hali ambayo ilifanya biashara yake kuweza kukua kila siku, tangu alipo isoma diary ya mama yake, moyoni mwake alishindwa kabisa kupata amani, alishindwa kabisa kufanya maamuzi ya kuweza kuwasamehe watu wale ambao walimletea maumivu makali sana namna hiyo hivyo akajikuta anapatwa na kasi kubwa sana ya kisasi ndani yake, alitamani kuweza kuwaadhibu watu hao kwa namna ambayo angeona kwamba ingemfaa yeye ili wazazi wake waweze kupumzika kwa amani. Sasa angeweza vipi kuwalipizia watu hao ambao kwanza alisikia kwamba walikuwa wanaishi ndani ya jiji la Dar es salaam ambako hakuwahi kufika? Kichwani kwake alikuwa na wazo moja tu pekee ambalo aliona ndiyo itakuwa nafasi yake ya kuweza kulikamilisha hilo, wazo hilo lilikuwa ni kuweza kuutumia urembo wake, aliamini kwamba uzuri wake ungempatia kila alichokuwa anakihitaji kwenye maisha yake lakini alikuwa miongoni mwa wale wanawake wachache sana ambao walikuwa wanaamini kwamba nguvu ya mwanamke inapatikana katikati ya mapaja yake.
Akiwa anaendelea na biashara yake alimtafuta mwanamke mmoja ambaye alikuwa kungwi maarufu na mkubwa sana ambaye hakuna mwanafunzi wake hata mmoja aliwahi kuachika kwenye ndoa yake baada ya kupata mafunzo kwake. Alihitaji mwanamke huyo amfundishe namna nzuri ya kuweza kumkamata mwanaume yeyote yule, alihitaji kuwa gwiji wa mapenzi, alihitaji kuishika akili ya mwanaume yeyote yule kupitia zawadi ambayo ilikuwa katikati ya miguu yake. Ukawa mwanzo wake mzuri wa kujifunza kuhusu mapenzi.
Alijifunza kwa bidii sana kwa sababu hakuna kitu ambacho alikuwa anakijua kuhusu mapenzi na siku ya mwisho iliyokuwa inautimiza mwezi wa sita tangu aanze kufundishwa, alipewa mwanaume ambaye alikuwa kijana wa kungwi huyo kwa ajili ya kumfundisha mwanamke huyo kwa vitendo zaidi. Hiyo ndiyo ilikuwa siku yake ya kwanza kabisa kujihusisha na mapenzi, hakuyafaidi sana ila hakujutia kwani mwanaume huyo alikuwa fundi haswa na ilibaki kidogo tu aweze kumpenda ila moyo wake ulimuonya kwamba alikuwa anayafanya hayo kwa ajili ya kazi maalumu na sio kumpenda mtu. Mazoezi yalienda kwa wiki nzima mpaka pale alipofanikiwa kuiva kwa vitendo kabisa sasa akawa anawaza sehemu ambayo alitakiwa kuanzia kutimiza lile takwa lake ambalo alikuwa analitaka.
Ilikuwa ni siku ambayo ilidaiwa kwamba mkuu wa mkoa wa jiji la Mwanza alikuwa anatembelea kwenye kisiwa hicho akiwa na waziri wa uvuvi hivyo alifanya maandalizi makubwa sana kwenye mgahawa wake akiwa na imani kwamba kwa sababu huo ndio ulikuwa mgahawa maarufu zaidi ndani ya sehemu hiyo basi lazima wageni hao wangefikia hapo na hakutaka kufanya kosa lolote lile juu ya jambo hilo kwa sababu aliamini kwamba safari yake ya kulipa kisasi ilikuwa inaanzia siku hiyo.
Mchana wa jua kali kweli viongozi hao walipita ndani ya eneo hilo na kwa sababu wanasiasa walikuwa wanapenda sana mambo ya picha ili kuwadanganya raia wajinga jinsi wanavyo wajali raia wao, baada ya kufika kwenye mgahawa huo walianza kufanya hivyo na kumwaga sifa huku wasisitiza vijana kupiga kazi maana binti mdogo kama huyo alikuwa na biashara ambayo ilikuwa inafanya vizuri sana. Brandina alikuwa amevaa nguo za kuvutia sana na hesabu zake zilikuwa kwa mkuu wa mkoa ambaye jina lake alifahamika kama Philipo Tibaigana kwa sababu mwanaume huyo alizipata sifa zake kwa namna alivyokuwa anapenda wanawake hususani mabinti warembo hivyo akaamini kwamba akifanikiwa kumtia kwenye mkono wake huyo basi itakuwa ni hatua kubwa sana kwa upande wake.
Baada ya kumaliza shughuli zote ambazo ziliwapeleka huko kiongozi huyo alifanikiwa kuyapata mawasiliano ya mwanamke huyo ambaye naye alionekana kumhitaji, kwa urembo ambao alikuwa nao Brandina kiongozi huyo nafsi yake ilijiwekea nadhiri kwamba kama angemkosa mwanamke huyo basi hakuwa na maana yoyote ile kuwa hai au kuendelea kuishi ni bora angekufa tu.
Ukawa mwanzo mzuri wa hadithi ya mapenzi ya uongo kati ya watu hao wawili ambapo penzi lao lilishamiri sana mpaka siku moja ambapo Brandina aliamua kumuomba kiongozi huyo kama anaweza amsaidie kumuingiza ndani ya jeshi. Haikuwa kazi sana kwa sababu kabla ya kuwa mkuu wa mkoa aliwahi kuwa ruteni wa jeshi na ndiyo sababu kubwa ambayo ilimfanya Brandina kutaka kuwa naye karibu kwa sababu alikuwa ameipitia historia ya mtu huyo.
Penzi ambalo alikuwa anampatia kiongozi huyo lilimfanya asiwe na chaguo lingine zaidi ya kukubali kila kitu ambacho mwanamke huyo alikuwa anakitaka. Japo alitamani sana kuweza kujua sababu ya mwanamke huyo kutaka kwenda jeshi lakini jibu alilopewa ni kwamba aliacha shule baada ya mama yake kufariki na alikuwa anapenda sana jeshi hivyo nafasi hiyo aliona kama ilikuwa ya dhahabu sana kwake, basi akapata nafasi kiwepesi sana kuingia huko.
Safari yake ilikuwa nzuri hususani baada ya Philipo Tibaigana kuteuliwa kuwa waziri wa ulinzi, Brandina alizidi kupata nafasi kubwa sana huku akiwa kama mwanamke rasmi wa Philipo Tibaigana na baada ya muda mrefu kupita Philipo Tibaigana alifanikiwa kuipata nafasi ya kuwa mkurugenzi wa shirika la kijasusi la nchi ya Tanzania. Baada ya kuingia huko alifanikiwa kumchukua mrembo Brandina ambaye alikuwa ni moja kati ya wanajeshi hodari sana na kumfanya kuwa jasusi ndani shirika lake ili awe naye karibu zaidi.
Brandina baada ya kuona kwamba alikuwa na nafasi kubwa sana kwenye maisha yake na mali alikuwa nazo aliamua kuweza wazi ukweli wake kwa Philipo Tibaigana kwamba alifanya yale yote kwenye maisha yake ili kuweza kulipa kizazi kwa watu ambao walimuulia wazazi wake, alihitaji kuifuta ile familia kwenye uso wa dunia waungane na wazazi wake ambao aliamini kwamba walionewa na hawakustahili kuuawa bali kuishi. Mambo hayo yalimshtua sana mkurugenzi kwani lilikuwa ni jambo geni sana kwake lakini kwa mapenzi ambayo alikuwa nayo kwa mrembo huyo alimpa nafasi ya kufanya hilo tukio kwa msaada wa majasusi wengine na kisha angefuta ushahidi wote kwa sababu suala la usalama wa taifa lilikuwa lipo chini yake.
Mpango wa Brandina ulitimia kirahisi sana kwa sababu ya kuitumia fahari iliyopo katikati ya mapaja yake kama alivyokuwa anamini kwamba hapo ndipo ilipo nguvu ya kufanya jambo lolote duniani hata akitaka kuuendesha ulimwengu basi akiitumia sehemu hiyo vizuri kwake inakuwa kazi nyepesi sana. Baada ya kufanikisha hilo jambo kwa kuiua kikatili sana familia ile ambayo ilimfanya aishi kama yatima, Brandina hakuwa yule mwanamke tena ambaye alikuwa na roho ya huruma, hakuwa tena mwanamke ambaye alikuwa na roho ya kike bali kwa wakati huo alikuwa ni mwanamke mkatili sana, alikuwa ni mwanamke ambaye aliamini kwamba duniani anaweza kufanya jambo lolote lile na likafanikiwa.
Kilichokuwa kinampa jeuri kubwa ni kuwa karibu na mkurugenzi wa shirika la kijasusi huku akiamini kwamba hakuna mtu ambaye alikuwa anaweza kumgusa hivyo kwa wakati huo akawa ana hamu kubwa sana ya mafanikio makubwa, alitamani jina lake lije libaki kwenye kumbukumbu za maisha ya watu na lijulikane kila sehemu ili kuwaenzi wazazi wake. Akawa anatamani kupata nafasi kubwa ambapo aliahidiwa na Philipo Tibaigana kwamba siku moja angekuja kumuingiza mwanamke huyo kwenye siasa na kutokana na nguvu aliyokuwa nayo kwake lingekuwa suala dogo tu na miaka kadhaa huko mbele mwanamke huyo angejikuta kwenye vitengo vikubwa sana serikalini.
Kwa kumuonyesha mfano, Philipo yeye ndiye ambaye alimpenyeza na kufanikiwa kumuweka kwenye nafasi kubwa sana ya kuwa mlinzi mkuu wa raisi. Mwanamke huyo alifanikiwa kuipata nafasi hiyo kutoka kwa mwanaume ambaye alikuwa anamvulia nguo ikiwa ni kama malipo ya ufundi ambao alikuwa anampa kitandani.
Huyu ndiye Brandina ambaye kulipa kwake kisasi kulimfanya muda mwingi awe pembeni ya mtu mkubwa zaidi wa usalama ndani ya taifa la Tanzania, huyu ndiye Brandina ambaye moyo wake uliwaka moto na kuzihitaji nafasi kubwa sana akiamini kwamba siku moja jina lake litaimbwa kutoka kila sehemu na kila pande ya dunia. Huyu ndiye Brandina ambaye alitakiwa kutumika kukamilisha mpango wa Denis Kijazo wa kuweza kumteketeza mheshimiwa raisi wa taifa la Tanzania Teodensia Mpanzi na huyu ndiye Brandina ambaye ilikuwa ni karata ya mhimu sana kuusambaratisha umoja wa watu ambao walikuwa wapo kinyume na mwalimu wa mipango Denis Kijazo. Jina lake lilitakiwa kutumika vipi kuwamaliza na kukamilisha kazi zote hizo kwa wakati mmoja?
Usiku wa manane ilikuwa inasikika sauti ya mgugumio kitandani, sauti ya mwanaume ambaye alikuwa kwenye furaha kubwa sana ya kulifurahia penzi kuliko ilivyokuwa kwa mwanamke. Mwanamke hakuonekana kulifurahia sana penzi hilo bali kwa mwanaume ilikuwa ni tofauti sana maana alikuwa anahisi kama dunia yote ipo kwenye mkono wake. Kwenye hicho kitanda walikuwepo watu wawili Philipo Tibaigana na mrembo Brandina Elkana ambaye alikuwa ndiye mlinzi mkuu wa mheshimiwa raisi.
27 inafika mwisho.
Tchao.
We're waiting for 28,HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
Episode 27
Alifika huko akiwa hajui kwamba angeenda kufanya nini, alianza kufanya kazi ya kukaanga samaki na kuuza chakula huku uzuri wake ndio ukiwa mdhamana wake mkubwa wa kupata mtaji kutoka kwa wanaume mafisi ambao walikuwa wanavua samaki. Baadae alibahatika kufungua kimgahawa chake kidogo na haukupita muda sana akawa amejifungua mtoto wa kike ambaye jina lake alimuita Brandina na baba yake jina lake alikuwa anaitwa Elkana hivyo akaamua kumpatia jina halisi kabisa la baba yake.
Maisha kwake hayakuwa mazuri sana wala mabaya sana lakini alimshukuru Mungu kwani alifanikiwa kumlea vizuri sana mwanae huyo mpaka binti yake alipo anza kujitambua wote wakiwa wanasaidiana kazi ya mgahawa pale ambapo mwanae angetoka shule ambayo alikuwa anasoma. Mwanamama huyo alianza kuumwa na hali yake haikuwa nzuri kwa sababu kasi ya ugonjwa ambao alikuwa nao ulionekana kuwa na nguvu kulizidi tumaini ambalo alikuwa nalo na hakuchukua siku nyingi sana akawa amepoteza maisha huku akiwa amemwachia mwanae diary yake ambayo ilikuwa na taarifa zote za maisha yake.
Taarifa zilikuwa zinaelezea uhalisia wa maisha ambayo mama yake aliyaishi, maisha ambayo alikutana nayo wakati anaendelea wa kuishi lakini vitu vya kutisha ambavyo alifanyiwa akiwa anaishi mpaka siku anakufa. Brandina alidondosha chozi kwa huruma kubwa sana kwa sababu alihisi kwamba mama yake alikufa tu hivi hivi lakini aligundua kwamba mama yake alikufa kwa homa ya ini, homa ambayo aliandika kwamba aliambukizwa na wale watu ambao walimbaka ambao walikuwa ndugu wa yule bosi wake.
Mama yake alimsisitiza mwanae kwamba baba yake mzazi aliuawa na wanafamilia hao, mama yake alimkumbusha kwamba hiyo ndiyo familia ambayo ilimfanya yeye aishi maisha magumu sana kwani kama sio hao basi angezaliwa kwenye maisha ambayo yalikuwa mazuri lakini alimtaka mwanae asije kusahau kwamba wanafamilia hao ndio ambao walifanya mama yake mzazi kuweza kupoteza maisha hivyo lilikuwa ni jukumu lake na uamuzi wake kama alikuwa anahitaji kuwasamehe au asiwasamehe.
Brandina wakati anaisoma hiyo diary alikuwa ni binti ambaye alikuwa anakua kwa kasi sana, binti ambaye aliichukua sura na rangi ya mama yake ambayo ilimfanya kuwa mwanamke mrembo sana zaidi hata ya mama yake mzazi. Uzuri wake ulifanya akawa kivutio kikubwa sana kwa watu ambao walikuwa wanaenda kisiwani hapo, urembo wake ulikuwa habari ambayo ilikuwa inaenea mithili ya upepo uvumao kwa nguvu. Mgahawa wake ambao aliachiwa na mama yake ulizidi kupata wateja wengi kila siku huku kila mtu akiwa anatamani sana kuweza kuhudumiwa na mwanamke huyo ambaye alikuwa akitabasamu watu wengi walikuwa wanafurahia sana kuwa karibu naye.
Licha ya kuwa kwenye hali ambayo ilifanya biashara yake kuweza kukua kila siku, tangu alipo isoma diary ya mama yake, moyoni mwake alishindwa kabisa kupata amani, alishindwa kabisa kufanya maamuzi ya kuweza kuwasamehe watu wale ambao walimletea maumivu makali sana namna hiyo hivyo akajikuta anapatwa na kasi kubwa sana ya kisasi ndani yake, alitamani kuweza kuwaadhibu watu hao kwa namna ambayo angeona kwamba ingemfaa yeye ili wazazi wake waweze kupumzika kwa amani. Sasa angeweza vipi kuwalipizia watu hao ambao kwanza alisikia kwamba walikuwa wanaishi ndani ya jiji la Dar es salaam ambako hakuwahi kufika? Kichwani kwake alikuwa na wazo moja tu pekee ambalo aliona ndiyo itakuwa nafasi yake ya kuweza kulikamilisha hilo, wazo hilo lilikuwa ni kuweza kuutumia urembo wake, aliamini kwamba uzuri wake ungempatia kila alichokuwa anakihitaji kwenye maisha yake lakini alikuwa miongoni mwa wale wanawake wachache sana ambao walikuwa wanaamini kwamba nguvu ya mwanamke inapatikana katikati ya mapaja yake.
Akiwa anaendelea na biashara yake alimtafuta mwanamke mmoja ambaye alikuwa kungwi maarufu na mkubwa sana ambaye hakuna mwanafunzi wake hata mmoja aliwahi kuachika kwenye ndoa yake baada ya kupata mafunzo kwake. Alihitaji mwanamke huyo amfundishe namna nzuri ya kuweza kumkamata mwanaume yeyote yule, alihitaji kuwa gwiji wa mapenzi, alihitaji kuishika akili ya mwanaume yeyote yule kupitia zawadi ambayo ilikuwa katikati ya miguu yake. Ukawa mwanzo wake mzuri wa kujifunza kuhusu mapenzi.
Alijifunza kwa bidii sana kwa sababu hakuna kitu ambacho alikuwa anakijua kuhusu mapenzi na siku ya mwisho iliyokuwa inautimiza mwezi wa sita tangu aanze kufundishwa, alipewa mwanaume ambaye alikuwa kijana wa kungwi huyo kwa ajili ya kumfundisha mwanamke huyo kwa vitendo zaidi. Hiyo ndiyo ilikuwa siku yake ya kwanza kabisa kujihusisha na mapenzi, hakuyafaidi sana ila hakujutia kwani mwanaume huyo alikuwa fundi haswa na ilibaki kidogo tu aweze kumpenda ila moyo wake ulimuonya kwamba alikuwa anayafanya hayo kwa ajili ya kazi maalumu na sio kumpenda mtu. Mazoezi yalienda kwa wiki nzima mpaka pale alipofanikiwa kuiva kwa vitendo kabisa sasa akawa anawaza sehemu ambayo alitakiwa kuanzia kutimiza lile takwa lake ambalo alikuwa analitaka.
Ilikuwa ni siku ambayo ilidaiwa kwamba mkuu wa mkoa wa jiji la Mwanza alikuwa anatembelea kwenye kisiwa hicho akiwa na waziri wa uvuvi hivyo alifanya maandalizi makubwa sana kwenye mgahawa wake akiwa na imani kwamba kwa sababu huo ndio ulikuwa mgahawa maarufu zaidi ndani ya sehemu hiyo basi lazima wageni hao wangefikia hapo na hakutaka kufanya kosa lolote lile juu ya jambo hilo kwa sababu aliamini kwamba safari yake ya kulipa kisasi ilikuwa inaanzia siku hiyo.
Mchana wa jua kali kweli viongozi hao walipita ndani ya eneo hilo na kwa sababu wanasiasa walikuwa wanapenda sana mambo ya picha ili kuwadanganya raia wajinga jinsi wanavyo wajali raia wao, baada ya kufika kwenye mgahawa huo walianza kufanya hivyo na kumwaga sifa huku wasisitiza vijana kupiga kazi maana binti mdogo kama huyo alikuwa na biashara ambayo ilikuwa inafanya vizuri sana. Brandina alikuwa amevaa nguo za kuvutia sana na hesabu zake zilikuwa kwa mkuu wa mkoa ambaye jina lake alifahamika kama Philipo Tibaigana kwa sababu mwanaume huyo alizipata sifa zake kwa namna alivyokuwa anapenda wanawake hususani mabinti warembo hivyo akaamini kwamba akifanikiwa kumtia kwenye mkono wake huyo basi itakuwa ni hatua kubwa sana kwa upande wake.
Baada ya kumaliza shughuli zote ambazo ziliwapeleka huko kiongozi huyo alifanikiwa kuyapata mawasiliano ya mwanamke huyo ambaye naye alionekana kumhitaji, kwa urembo ambao alikuwa nao Brandina kiongozi huyo nafsi yake ilijiwekea nadhiri kwamba kama angemkosa mwanamke huyo basi hakuwa na maana yoyote ile kuwa hai au kuendelea kuishi ni bora angekufa tu.
Ukawa mwanzo mzuri wa hadithi ya mapenzi ya uongo kati ya watu hao wawili ambapo penzi lao lilishamiri sana mpaka siku moja ambapo Brandina aliamua kumuomba kiongozi huyo kama anaweza amsaidie kumuingiza ndani ya jeshi. Haikuwa kazi sana kwa sababu kabla ya kuwa mkuu wa mkoa aliwahi kuwa ruteni wa jeshi na ndiyo sababu kubwa ambayo ilimfanya Brandina kutaka kuwa naye karibu kwa sababu alikuwa ameipitia historia ya mtu huyo.
Penzi ambalo alikuwa anampatia kiongozi huyo lilimfanya asiwe na chaguo lingine zaidi ya kukubali kila kitu ambacho mwanamke huyo alikuwa anakitaka. Japo alitamani sana kuweza kujua sababu ya mwanamke huyo kutaka kwenda jeshi lakini jibu alilopewa ni kwamba aliacha shule baada ya mama yake kufariki na alikuwa anapenda sana jeshi hivyo nafasi hiyo aliona kama ilikuwa ya dhahabu sana kwake, basi akapata nafasi kiwepesi sana kuingia huko.
Safari yake ilikuwa nzuri hususani baada ya Philipo Tibaigana kuteuliwa kuwa waziri wa ulinzi, Brandina alizidi kupata nafasi kubwa sana huku akiwa kama mwanamke rasmi wa Philipo Tibaigana na baada ya muda mrefu kupita Philipo Tibaigana alifanikiwa kuipata nafasi ya kuwa mkurugenzi wa shirika la kijasusi la nchi ya Tanzania. Baada ya kuingia huko alifanikiwa kumchukua mrembo Brandina ambaye alikuwa ni moja kati ya wanajeshi hodari sana na kumfanya kuwa jasusi ndani shirika lake ili awe naye karibu zaidi.
Brandina baada ya kuona kwamba alikuwa na nafasi kubwa sana kwenye maisha yake na mali alikuwa nazo aliamua kuweza wazi ukweli wake kwa Philipo Tibaigana kwamba alifanya yale yote kwenye maisha yake ili kuweza kulipa kizazi kwa watu ambao walimuulia wazazi wake, alihitaji kuifuta ile familia kwenye uso wa dunia waungane na wazazi wake ambao aliamini kwamba walionewa na hawakustahili kuuawa bali kuishi. Mambo hayo yalimshtua sana mkurugenzi kwani lilikuwa ni jambo geni sana kwake lakini kwa mapenzi ambayo alikuwa nayo kwa mrembo huyo alimpa nafasi ya kufanya hilo tukio kwa msaada wa majasusi wengine na kisha angefuta ushahidi wote kwa sababu suala la usalama wa taifa lilikuwa lipo chini yake.
Mpango wa Brandina ulitimia kirahisi sana kwa sababu ya kuitumia fahari iliyopo katikati ya mapaja yake kama alivyokuwa anamini kwamba hapo ndipo ilipo nguvu ya kufanya jambo lolote duniani hata akitaka kuuendesha ulimwengu basi akiitumia sehemu hiyo vizuri kwake inakuwa kazi nyepesi sana. Baada ya kufanikisha hilo jambo kwa kuiua kikatili sana familia ile ambayo ilimfanya aishi kama yatima, Brandina hakuwa yule mwanamke tena ambaye alikuwa na roho ya huruma, hakuwa tena mwanamke ambaye alikuwa na roho ya kike bali kwa wakati huo alikuwa ni mwanamke mkatili sana, alikuwa ni mwanamke ambaye aliamini kwamba duniani anaweza kufanya jambo lolote lile na likafanikiwa.
Kilichokuwa kinampa jeuri kubwa ni kuwa karibu na mkurugenzi wa shirika la kijasusi huku akiamini kwamba hakuna mtu ambaye alikuwa anaweza kumgusa hivyo kwa wakati huo akawa ana hamu kubwa sana ya mafanikio makubwa, alitamani jina lake lije libaki kwenye kumbukumbu za maisha ya watu na lijulikane kila sehemu ili kuwaenzi wazazi wake. Akawa anatamani kupata nafasi kubwa ambapo aliahidiwa na Philipo Tibaigana kwamba siku moja angekuja kumuingiza mwanamke huyo kwenye siasa na kutokana na nguvu aliyokuwa nayo kwake lingekuwa suala dogo tu na miaka kadhaa huko mbele mwanamke huyo angejikuta kwenye vitengo vikubwa sana serikalini.
Kwa kumuonyesha mfano, Philipo yeye ndiye ambaye alimpenyeza na kufanikiwa kumuweka kwenye nafasi kubwa sana ya kuwa mlinzi mkuu wa raisi. Mwanamke huyo alifanikiwa kuipata nafasi hiyo kutoka kwa mwanaume ambaye alikuwa anamvulia nguo ikiwa ni kama malipo ya ufundi ambao alikuwa anampa kitandani.
Huyu ndiye Brandina ambaye kulipa kwake kisasi kulimfanya muda mwingi awe pembeni ya mtu mkubwa zaidi wa usalama ndani ya taifa la Tanzania, huyu ndiye Brandina ambaye moyo wake uliwaka moto na kuzihitaji nafasi kubwa sana akiamini kwamba siku moja jina lake litaimbwa kutoka kila sehemu na kila pande ya dunia. Huyu ndiye Brandina ambaye alitakiwa kutumika kukamilisha mpango wa Denis Kijazo wa kuweza kumteketeza mheshimiwa raisi wa taifa la Tanzania Teodensia Mpanzi na huyu ndiye Brandina ambaye ilikuwa ni karata ya mhimu sana kuusambaratisha umoja wa watu ambao walikuwa wapo kinyume na mwalimu wa mipango Denis Kijazo. Jina lake lilitakiwa kutumika vipi kuwamaliza na kukamilisha kazi zote hizo kwa wakati mmoja?
Usiku wa manane ilikuwa inasikika sauti ya mgugumio kitandani, sauti ya mwanaume ambaye alikuwa kwenye furaha kubwa sana ya kulifurahia penzi kuliko ilivyokuwa kwa mwanamke. Mwanamke hakuonekana kulifurahia sana penzi hilo bali kwa mwanaume ilikuwa ni tofauti sana maana alikuwa anahisi kama dunia yote ipo kwenye mkono wake. Kwenye hicho kitanda walikuwepo watu wawili Philipo Tibaigana na mrembo Brandina Elkana ambaye alikuwa ndiye mlinzi mkuu wa mheshimiwa raisi.
27 inafika mwisho.
Tchao.