Simulizi ya kweli: Niliishi kuzimu siku saba

Simulizi ya kweli: Niliishi kuzimu siku saba

SEHEMU YA 42

ILIPOISHIA:
“Una..ta..ka kufa…nya ni…ni,” sikumalizia kauli yangu, akawa tayari ameshafika pale kitandani, tukagusanisha ndimi zetu huku Shamila akionesha kweli kudhamiria kile alichokitaka. Hakuogopa kabisa kwamba pale ni wodini.
SASA ENDELEA…
Nilijaribu kumzuia lakini haikusaidia kitu, alishadhamiria na kwa ilivyoonesha, alikuwa tayari kufanya chochote ili apate alichokuwa anakitaka. Tuliendelea kugusanisha ndimi zetu huku mikono yake laini ikitalii kwenye viunga mbalimbali vya mwili wangu, nikaanza kuhisi hali ya tofauti.
Unajua jambo ambalo nitaendelea kulisema kila siku, hakuna jambo baya kama kuyajaribu mapenzi. Wazee wetu waliosema kwamba mapenzi hayajaribiwi, walikuwa sahihi kabisa. Wakati naanza uhusiano wa kimapenzi na Shamila, nilikuwa najua kabisa kwamba tayari ninaye Raya ambaye ananipenda sana na tumeshaahidiana vitu vingi, tena kibaya zaidi mimi ndiyo nikiwa mwanaume wa kwanza maishani mwake.
Akilini mwangu nilijua kwamba hata nikimkubalia Shamila, haiwezi kuwa na tatizo lolote kwa sababu kiukweli sikuwa nimempenda kutoka ndani ya moyo wangu na nilipanga kumtumia kama daraja tu la kunifanya nipate nilichokuwa nakitaka kwa urahisi.
Hata hivyo, tangu Shamila alipoanza kua karibu na mimi, nilijikuta akiingia kwa kasi kwenye moyo wangu kuliko hata nilivyotegemea. Jambo ambalo sikuwahi kulijua tangu awali ni kwamba kumbe Shamila alikuwa mzuri kuliko Raya, kuanzia mwonekano, shepu, uchangamfu, uelewa wa mambo mpaka kwenye ufundi wa ‘uwanja wa fundi seremala’.
Ilifika mahali mwenyewe nikawa najiona kabisa kwamba nimeanza kumpenda Shamila kuliko Raya, jambo ambalo sikujua mwisho wake utakuja kuwa nini. Nawasihi kwa mara nyingine wanaume, hasa vijana kama sisi, hakuna kosa baya kama kucheza na hisia za wanawake wanaokupenda kwa wakati mmoja.
Basi Shamila aliendelea na mbwembwe, ‘Jamal’ wangu akachaji ile mbaya, nikajikuta mimi ambaye mwanzo nilikuwa navungavunga ndiyo nimekuwa nyota wa mchezo, kwa umakini wa hali ya juu nikajibinua, Shamila akawa chini mimi juu, tukawa tunatazamana kama majogoo yanayotaka kupigana, kila mmoja pumzi zikimtoka kwa nguvu.
Sikuwa na muda wa kusubiri, nilianza kusakata kambumbu kwa mtindo wa kushambulia mfululizo, huku nikiwa makini nisijitoneshe jeraha langu la kifuani, Shamila akawa anayapokea mashambulizi yangu kwa miguno flan’ hivi ambayo ilizidi kunipandisha wazimu.
Ilifika mahali nikabadili mfumo wa kusakata kabumbu, nikawa nakimbia na mpira kwenye chaki kama Christiano Ronaldo vile, nikawa nahama pande zote na kumfanya Shamila apoteze ‘netiweki’, akaanza kutoa miguno kwa nguvu akiwa amesahau kabisa kwamba hatukuwa kwenye mazingira rafiki.
Niliongeza kasi, naye akaongeza kasi ya kunikaba, dakika chache baadaye nilitangaza kuzifumania nyavu zake lakini kabla sijamuwahi, na yeye alishatangaza kuzifumania zangu, ikawa ngoma droo!
Harakaharaka nilishuka pale kwenye kitanda changu na kuvaa vizuri nguo zangu ambazo hata sikumbuki nilizitupa saa ngapi sakafuni. Harakaharaka nikajiweka vizuri na kumsogelea Shamila ambaye eti tayari alikuwa ameanza kukoroma kwa mbali, akionesha kuchoshwa mno na mpambano ule wa kushtukiza.
Nikamtingisha kwa nguvu, akawa ananisukuma kama anayesema ‘niache nipumzike bwana’. Nilipozidi kumsumbua, aliinuka, naye akavaa magwanda yake, safari hii akiwa hataki kabisa kunitazama usoni. Akajizoazoa mpaka kwenye ofisi ya manesi ambako nako kulikuwa na kitanda, akajitupa kitandani.
Ilibidi mimi ndiyo niwe na kazi ya ziada ya kuondoa ushahidi wote eneo la tukio, nikaenda kufungua mapazia, nikafungua na milango na kuiweka kama inavyotakiwa kuwekwa, nikaongeza spidi ya feni na kurudi kitandani, nikajilaza huku moyoni nikijipongeza kwa kumtolea uvivu Shamila ambaye alikuwa akicheza na sharubu za simba.
Muda mfupi baadaye, niliona kivuli cha mtu akipita dirishani kwa nje, akaenda upande mmoja kisha muda mfupi baadaye akarudi na kusimama pale mlangoni, ilionesha kama ni mtu ambaye hakuwa na uhakika sana wa mahali anakokwenda. Kwa kuwa pale nje ya wodi za ‘private’ kulikuwa na walinzi, nilisikia wakimsemesha.
Kama kawaida yangu, nikawahi kujihami kwa kushuka pale kitandani haraka na kwenda kujibanza nyuma ya mlango ili hata kama ni miongoni mwa wale wanaoisaka roho yangu, akiingia tu niwahi kuchomoka.
Katika mahojiano yake, niligundua kwamba ni msichana, tena bado mdogo na alikuwa akitaka kuniona mimi maana niliwasikia akiwatajia mpaka jina langu. Baada ya kumhoji sana, wale walinzi walimruhusu kuingia, nadhani ni kwa sababu walishapewa maelekezo na Shamila juu ya kuwa makini na watu wanaokuja kwa lengo la kuniona. Akafungua mlango na kuanza kuangalia juu ya vitanda viwili vilivyokuwa ndani ya wodi hiyo.
“Firyaal,” nilisema baada ya kumtambua kuwa ni yule mdogo wake Shenaiza ambaye nilipewa maagizo ya kwenda nyumbani kwao kuonana naye, ambaye ndiye aliyenipa ‘hard disk’ iliyokuwa na siri nyingi kuhusu ushetani uliokuwa ukifanywa na baba yake.
“Jamal! Alisema huku akitetemeka, uso wake ukionesha dhahiri jinsi alivyokuwa na hofu kubwa ndani ya moyo wake.
“Vipi mbona hivyo? Tulia kisha uniambie nini kinachokusumbua,” nilisema huku nikifunga mlango na kusogea naye mpaka pale kwenye kitanda changu.
“Baba anatarajiwa kurudi kesho nchini na tayari walinzi wake wamegundua kwamba kuna kitu kwenye kompyuta yake kimechomolewa, wakijua kwamba mimi na dada Shenaiza tunahusika hata sijui itakuwaje.
“Nipo chini ya miguu yako nakuomba unirudishie ile ‘hard disk’, nimefanya kazi kubwa sana kukutafuta, hospitali nzima hawajui umelazwa wodi gani,” alisema Firyaal, nikashusha pumzi ndefu na kumtazama.
“Usijali Firyaal kila kitu kitakuwa sawa,” nilimwambia na kuanza kumtuliza, nikamhakikishia kwamba kabla ya hiyo kesho, ataipata ‘hard disk’ yake, pia nikamwambia kuhusu matatizo yaliyokuwa yanamkabili dada yake.
“Tusaidie kama unaweza, najua baba akija maisha ya dada yapo hatarini sana, anaweza hata kuamuru auawe, yaani sijui baba siku hizi amekuwaje,” alisema Firyaal huku akianza kuangua kilio. Niliendelea kumtuliza huku nikitafuta mbinu ya kuwasaidia wote kwani kwa jinsi ilivyoonesha, baba yao alikuwa mtu hatari hata ndani ya familia yake mwenyewe.
Nadhani mazungumzo yetu yalimzindua Shamila aliyekuwa usingizini, akakurupuka na kutoka, akapigwa na butwaa kumuona mdogo wake Shenaiza. Alimkumbuka vizuri kwa sababu hata siku niliyoenda kuichukua ile ‘hard disk’, nilikuwa nimeongozana naye ingawa yeye alibaki ndani ya teksi.
“He, vipi imekuwaje? Binti nani amekuruhusu kuingia humu?” alihoji Shamila huku akijiweka vizuri nguo zake pamoja na nywele ambazo bado zilikuwa zimevurugika. Ilibidi nimtulize na kumweleza kilichomleta pale. Kwa bahati nzuri Shamila ni mwelewa sana, harakaharaka alielewa, kwa pamoja tukawa tunajadiliana nini cha kufanya.
“Inabidi kwanza hiyo ‘hard disk’ yake irudishwe haraka kisha baada ya hapo inabidi tufanye mpango wa kumtorosha Shenaiza wodini haraka iwezekanavyo, hayo yote yanatakiwa kufanyika usiku wa leo.
“Hata wewe hapa siyo mahali salama tena pa kuendelea kukaa, ngoja kwanza nimesahau kuuliza kitu muhimu. Wewe binti upo upande upi? Unamuunga mkono baba yako au na wewe unamsimamo kama wa dada yako?” Shamila alimuuliza swali muhimu.
Msichana huyo mdogo alituhakikishia, tena kwa kujiapiza kwamba kamwe hajawahi kumuunga mkono baba yake lakini amekuwa akikosa mtu wa kumsaidia kupambana naye.
Kauli yake hiyo ilitufurahisha sana mimi na Shamila, tukawa na uhakika kwamba sasa kazi itakuwa nyepesi kwa sababu tayari tutakuwa na mtu kutoka ndani kabisa, ambaye angetusaidia kutimiza lengo letu la kupambana na mtu huyo hatari.
Je, nini kitafuatia?
 
SEHEMU YA 43

ILIPOISHIA:
Kauli yake hiyo ilitufurahisha sana mimi na Shamila, tukawa na uhakika kwamba sasa kazi itakuwa nyepesi kwa sababu tayari tutakuwa na mtu kutoka ndani kabisa, ambaye angetusaidia kutimiza lengo letu la kupambana na mtu huyo hatari.
SASA ENDELEA…
“Kwa hiyo tunaanzia wapi?” nilimuuliza Shamila, akawa ni kama anayetafakari kitu kisha akaniambia ameshapata majibu.
“Ngoja niende kwanza na huyu binti nikampe hiyo hard disk yake,” alisema Shamila.
“Utaweza kuichomoa kwenye kompyuta?”
“Mimi naweza, nasomea Information Technology niko mwaka wa pili,” alisema Firyaal ambaye alikuwa amefanana sana na Shenaiza, yaani hata bila kuuliza ungemjua tu kwamba ni ndugu yake.
“Sijamaliza kukopi data ninazozihitaji lakini.”
“Nitakusaidia pia, ninayo ‘back up’ kubwa tu nyumbani, naweza kuhamisha data zote na kukuletea,” alisema msichana huyo, nikawa namtazama usoni kwani aliyokuwa akiyasema hayakuwa yakifanana na umri wake.
Kwa kumtazama alionekana kama msichana mdogo ambaye kwa makadirio ungeweza kudhani yupo kidato cha pili au cha tatu lakini kumbe tayari alishafika kidato cha sita na sasa alikuwa chuoni.
“Nitashukuru sana ukinisaidia dada’angu,” nilisema kwa sauti ya kiungwana, Firyaal akanitazama usoni, na mimi nikamtazama, macho yetu yakagongana, harakaharaka akakwepesha macho yake huku aibu za kikekike zikiwa zimemtawala.
“Basi usitoke kwenda sehemu yoyote, mimi ngoja niende naye nyumbani,” alisema Shamila, akanisogelea pale kitandani na kunibusu kisha harakaharaka akamshika mkono Firyaal na kuanza kutoka naye nje.
>>>Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
Walipofika mlangoni, nilimuona Firyaal akigeuka na kunitazama, na mimi nikamtazama, macho yetu yakagongana kwa mara nyingine. Tofauti na mwanzo, safari hii hakukwepesha macho yake, tukaendelea kutazamana mpaka walipotoka nje. Sikuelewa sababu iliyofanya awe ananitazama vile kwa sababu kimsingi hiyo haikuwa mara ya kwanza mimi na yeye kuonana.
Ilikuwa ni mara ya pili. Hata hivyo sikutilia sana maanani, nikampotezea.
Nikashusha pumzi ndefu na kutulia kitandani, mawazo mengi yakiendelea kupita ndani ya kichwa changu. Ni kweli nilikuwa bado sijapona vizuri lakini ilikuwa ni lazima niondoke hospitalini hapo kabla mambo hayajaharibika. Kutokana na sifa nilizokuwa nazisikia, nilijikuta nikimuogopa mno baba yake Shenaiza kama malaika mtoa roho.
Niliendelea kutulia pale kitandani, japokuwa Shamila aliniambia nisitoke, nilipata wazo la kwenda kwenye wodi aliyokuwa amelazwa Shenaiza kwenda kuangalia anaendeleaje. Hata hivyo, nilipomkumbuka yule mtu aliyekuwa akinitazama sana kwa makini mle ndani ya wodi ya vichaa, nilijikuta nikipatwa na hofu moyoni, nikaghairi.
Kwa hesabu zangu za harakaharaka ukichanganya na maelezo niliyoyapata kutoka kwa Shamila, nilikuwa nimekaa hospitalini hapo kwa wiki mbili mfululizo, huku kati ya hizo, siku saba nikiwa nimepoteza kabisa fahamu.
Nilijaribu kuvuta kumbukumbu ya mambo yote yaliyotokea ndani ya kipindi hicho nilichokuwa hospitalini hapo, ungeweza kudhani kama nimekaa hospitalini kwa kipindi cha mwaka mzima. Kila kitu kilikuwa kikitokea kwa kasi kubwa mno kiasi cha kufanya hata akili yangu isipate muda wa kupumzika.
Kitu ambacho kilinipa faraja kubwa ndani ya moyo wangu, ni kuona jinsi wafanyakazi wenzangu pamoja na bosi wetu walivyokuwa wakinijali. Japokuwa nilikuwa chini ya uangalizi maalum ambapo watu hawakuwa wakiruhusiwa kuja mara kwa mara kunitazama, Raya alinihakikishia kwamba katika zile siku nilizokuwa nimepoteza fahamu karibu kila siku watu kutoka kazini walikuwa wakija kunitazama.
Baada ya kama dakika arobaini tangu Shamila na yule mdogo wake Shenaiza waondoke, Raya alikuja tena. Kiukweli japokuwa nilikuwa nikimuendea kinyume, Raya alikuwa akijitahidi sana kuwa karibu na mimi.
>>>Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
Muda wote yeye alikuwa akinifikiria mimi tu kiasi cha kumfanya kazini asiwe anaenda wala nyumbani kwao asiwe anatulia, muda wote ilikuwa ni kiguu na njia, kuja hospitali na kurudi kwao.
“Vipi unaendeleaje mume wangu,” alisema Raya kwa sauti ya chini, akionesha kuwa na mawazo lukuki ndani ya kichwa chake.
“Naendelea vizuri mke wangu, vipi mbona nakuona kama mudi yako iko chini sana, nini kinakusumbua,” nilimwambia Raya kwa upole, akajisogeza na kupitisha mkono wake mmoja shingoni kwangu, akanibusu kwenye paji langu la uso na kuanza kuniambia kwamba tangu nilipomweleza ukweli wa kilichokuwa kinaendelea nyuma ya pazia, alikosa raha kabisa.
“Nahisi kama nitakupoteza mpenzi wangu na mimi siwezi kuishi bila wewe, hata sijui itakuwaje,” alisema kwa huzuni, nikashusha pumzi ndefu na kuanza kumtuliza. Nikamwambia asiwe na wasiwasi, hakuna jambo lolote baya litakalotokea nakuhakikishia,” nilimwambia.
Kidogo kujiamini kwangu kulimfanya naye aanze kuona kwamba kumbe halikuwa tatizo kubwa mbele yetu, nikamueleza pia juu ya mipango ya kutoroka tuliyokuwa tumeipanga kwa ajili ya kumkimbia baba yake Shenaiza. Nilimuona naye akiniunga mkono, nadhani hata yeye hakuwa na imani kabisa juu ya usalama wangu hospitalini hapo.
Tulizungumza mambo mengi, Raya akawa ananisisitiza kwamba yeye amejitoa kwa asilimia mia moja kunisaidia, isije ikatokea kwamba nikamgeuka na kumuona hana maana tena. Kauli yake iliugusa sana moyo wangu kwa sababu ni kweli Raya alikuwa amejitoa kwa kila kitu lakini kwa bahati mbaya sana shetani alionekana kunizidi nguvu.
Nikawa namhakikishia kwamba asiwe na wasiwasi lakini ukweli, sikuwa namaanisha kile nilichokuwa nakisema. Akaniambia kwamba atashirikiana na Shamila kuhakikisha wananitorosha hospitalini hapo usiku bila mtu yeyote kujua, swali likawa nikishatoroshwa nitaenda kukaa wapi?
Raya alisema anataka nikakae nyumbani kwao kwa sababu pale kuna usalama zaidi, nikamwambia ni rahisi wabaya zangu kujua kwamba niko pale kwa sababu kuna baadhi ya watu walikuwa wakijua kuhusu uhusiano wetu wa kimapenzi. Nikatumia nafasi hiyo kumpigia chapuo Shamila, nikamwambia Raya kwamba amesema yupo tayari kunificha nyumbani kwake.
Nilimuona Raya akishtushwa kidogo na nilichokisema lakini nikamtoa wasiwasi na kumwambia kwamba mimi na yeye tutakuwa pamoja kwa hiyo asiwe na wasiwasi wowote. Akakubali kwa shingo upande, nadhani bado alikuwa na wivu juu ya ukaribu wangu na Shamila.
Muda ulizidi kuyoyoma, baadaye Shamila alirudi akiwa peke yake, akaniambia kwamba kila kitu kimeenda kama tulivyokubaliana, akaniambia kwamba Firyaal alikuwa mtundu sana kwenye mambo ya kompyuta na kwamba tayari alishanikopia data zote na kuziacha pale nyumbani kwake kama tulivyokubaliana, tukaanza kupanga mipango ya namna ya kutoroka usiku huku Raya naye akiwepo.
Jambo ambalo kuanzia mwanzo Raya hakuwa akilijua, ni kwamba katika mpango wetu huo ilikuwa ni lazima pia tumtoroshe na Shenaiza, akashtuka kusikia hivyo.
Bado nikaendelea kumsisitiza kwamba ilikuwa ni lazima tuondoke na Shenaiza kwa sababu bila yeye mimi nisingeingia kwenye mtego huo na kuanzia mwanzo alikuwa akinisisitiza kwamba mimi ndiye mtu pekee ninayeweza kumsaidia.
“Usiwe na wasiwasi, hawa wote wataenda kukaa nyumbani kwangu, mimi nina nyumba kubwa, hata na wewe ukitaka tukae pamoja tusaidiane kuwahudumia wagonjwa haina shida,” alisema Shamila, nikamuona Raya akishusha pumzi ndefu na kunitazama, akatingisha kichwa kama ishara ya kukubaliana na mimi.
Ilibidi Raya abaki palepale hospitalini mpaka usiku ili iwe rahisi kufanya kazi yetu, muda ukazidi kuyoyoma na hatimaye giza likaingia, ule muda tuliokuwa tukiusubiri kwa hamu ukawa umewadia.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue
 
SEHEMU YA 44
ILIPOISHIA:
Ilibidi Raya abaki palepale hospitalini mpaka usiku ili iwe rahisi kufanya kazi yetu, muda ukazidi kuyoyoma na hatimaye giza likaingia, ule muda tuliokuwa tukiusubiri kwa hamu ukawa umewadia.
SASA ENDELEA…
“Tunakusikiliza wewe Shamila!”
“Yaah! Inabidi mnisikilize kwa makini vinginevyo hakuna kitakachofanikiwa.”
“Tunaanzia wapi?” nilimuuliza Shamila huku mapigo ya moyo wangu yakinienda mbio.
“Tulia Jamal, mbona una haraka namna hiyo,” alisema Shamila, nikashusha pumzi ndefu na kutulia, hakuna muda ambao nilikuwa nahitaji msaada wake kama huo na kubwa zaidi, sikuwa mimi tu ambaye nilikuwa nahitaji msaada wake, bali Shenaiza pia.
Shamila aliingia kwenye chumba cha kubadilishia nguo, muda mfupi baadaye alitoka akiwa na gauni jingine, akampa Raya na kumuelekeza kuingia kule ndani kwenda kubadilisha nguo. Kweli akatii alichoambiwa, muda mfupi baadaye akatoka akiwa ndani ya mavazi ya kinesi, usingeweza kumtambua kwamba hakuwa nesi.
“Sasa wewe kazi yako itakuwa ni kutoka na mgonjwa mpaka nje, unaona hili faili lake, inatakiwa ulishike na kufuata maelekezo ya nitakachokuwa nakwambia. Ukikosea tu basi hakuna kitakachowezekana,” alisema Shamila wakati akimpa maelekezo Raya, akatingisha kichwa kwa utiifu kuonesha kwamba alikuwa ameelewa alichokuwa ameambiwa.
“Inabidi pia njia ambayo itatumika kukutoa wewe itumike pia kwa Shenaiza, tena kwa wakati mmoja kwa hiyo tutaongozana wote, sijui kama mnanielewa,” alisema Shamila huku akiwa amevaa uso wa ‘usiriaz’, wote tukaitikia kuonesha kwamba tulikuwa tumemuelewa.
>>>Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
“Mimi nitaenda kumchukua Shenaiza wakati huo nyie mtakuwa mkinisubiri hapo chini, tutatoka pamoja mpaka pale getini, mimi nitaongea na walinzi, wakituruhusu kutoka tu, Firyaal yupo nje anatusubiri na gari la familia yao kwa hiyo hakutakuwa na muda wa kupoteza, tumeelewana?” alisema Shamila ambaye aligeuka na kuwa mwalimu wa kutuelekeza, sisi kazi yetu ikawa ni kuitikia tu.
“Nifuate,” alimwambia Raya huku akinitaka na mimi nivae vizuri nguo maalum za wagonjwa.
“Kamanda, huyu mgonjwa inatakiwa akafanyiwe kipimo cha MRI kesho sasa kwa sababu mashine ya hapa hospitalini ni mbovu na kesho kutakuwa na foleni kubwa, tumeomba akafanyiwe kipimo hicho usiku huu pale kwenye maabara za Lancert zilizopo nje ya hospitali,” Shamila alimwambia mlinzi aliyekuwa nje ya wodi ile kwa sauti ya juu, japokuwa mimi nilikuwa ndani niliweza kusikia kila kitu, nikatabasamu na kutikisa kichwa kwani ama kwa hakika mbinu ya Shamila ilikuwa kali mno.
Muda mfupi baadaye, nilisikia mlango ukifunguliwa, Shamila akatangulia kuingia, nyuma yake akafuatia Raya aliyekuwa akisukuma kiti cha magurudumu (wheel chair) huku akionesha dhahiri jinsi alivyokuwa na hofu kubwa moyoni mwake.
“Inatakiwa uchangamke, ukiwa unatetemeka hivyo watatushtukia, muone kwanza,” Shamila alimshushua Raya kwa sauti ya chini, nikanyamaza kimya kama sijasikia chochote. Wakasogeza ile wheel chair mpaka pale pembeni ya kitanda changu, Shamila akaniambia anajua ninao uwezo wa kutembea mwenyewe lakini ni lazima nikubali kusukumwa kwenye kiti cha magurudumu ili isiwe rahisi kwa mtu yeyote kutushtukia.
Basi nikashuka kitandani na kukaa kwenye kitanda cha magurudumu, Shamila akamuelekeza Raya namna ya kukisukuma na akarudia kumsisitiza kwamba anatakiwa kuchangamka. Ilibidi vitu vyangu vingine vyote niviache mlemle wodini, tukatoka mpaka kwenye korido, nikamuona yule mlinzi akisimama na kutusaidia kubonyeza kitufe kwenye lifti.
Hakuwa na mawazo kabisa kwamba ndiyo tunamtoka kiaina. Nikiri wazi kwamba hilo halikuwa zoezi langu la kwanza kutoroka hospitalini kwa sababu tayari nilishamtorosha Shenaiza lakini hali haikuwa tete kama ilivyokuwa muda huo, na kikubwa kilichokuwa kikinipa hofu kubwa ndani ya moyo wangu ni kujua aina ya watu niliokuwa nadili nao; baba yake Shenaiza na watu wake.
“Inawezekana kabisa kuna watu wamepandikizwa hapa hospitalini na baba yake Shenaiza kufuatilia nyendo zako na binti yake, kwa hiyo unatakiwa kujiinamia muda wote ili mtu yeyote asikuone usoni, mtanisubiri nikamchukue Shenaiza,” alisema Shamila wakati tukiwa ndani ya lifti tukishuka chini, tukamuitikia.
>>>Usiache kutembelea Simulizi za Majonzi
Tulishuka mpaka chini, akatuelekeza kufuata korido mpaka mbele ambapo alisema tumsubiri, Raya akawa ananisukuma taratibu, yeye akaelekea kwenye wodi ya wagonjwa wa akili alikokuwa amelazwa Shenaiza.
“Im scared Jamal, I cant take it!” (Naogopa Jamal, siwezi!)
“You need to do this my love, do it for me!” (Unatakiwa kufanya mpenzi wangu, fanya kwa ajili yangu) Raya alinisemesha kwa Kimombo si unajua tena yeye alikuwa akitoka familia bora? Nikawa naendelea kumpa maneno ya kumtia nguvu, tukawa tunaendelea kutembea taratibu kwenye korido huku Raya pia akiwa na faili langu.
“Hivi akitokea mlinzi hapa na kutuuliza tunaenda wapi usiku huu tutajibu nini?”
“Tunaenda kufanyiwa kipimo cha MRI pale nje kwenye maabara za Lancert kwa sababu mashine za humu ndani zimeharibika,” nilijibu kwa kujiamini, nikaona hofu ikipungua ndani ya moyo wake.
“Maelezo haya inabidi wewe nesi ndiyo uyatoe, sio mimi mgonjwa,” nilisema kwa msisitizo, Raya akawa ananiitikia lakini jambo ambalo bado hakuweza kulidhibiti, ni hofu iliyokuwa ndani ya moyo wake.
Tulifika mpaka pale Shenaiza alipotuambia kwamba tumsubiri, tukasimama na kuanza kuangalia uelekeo wa wodi ya wagonjwa wa akili alikokuwa ameelekea. Hata hivyo, hakutokea haraka kama tulivyodhani, muda ukaanza kuyoyoma mara dakika tano zikakatika, kimya! Tano nyingine zikakatika bila Shamila kurudi, tukaanza kuingiwa na hofu.
Pale tulipokuwa tumesimama, wauguzi na ndugu za wagonjwa mbalimbali walikuwa wakitupita lakini hakuna aliyekuwa na habari na sisi kwani walijua tupo kwenye taratibu za kawaida za tiba.
“Tunavyozidi kusimama hapa ndivyo tunavyozidi kujiweka kwenye hatari zaidi, wanaweza kutushtukia.”
“Sasa tufanyeje?” nilimuuliza Raya lakini kama bahati, kwa mbali tuliona mlango wa wodi ya wagonjwa wa akili ukifunguliwa, Shamila akatoka akiwa anasukuma kitanda cha magurudumu kama kile nilichokuwa nimekalia, wote tukashusha pumzi ndefu na kumshukuru Mungu kwani tulishaanza kuchanganyikiwa.
Kwa mbali akatuonesha ishara kwamba tuendelee kusonga mbele, naye akawa anakuja huku akikisukuma kile kitanda ambacho hata bila kuuliza, niligundua kwamba aliyekuwa amekaa pale alikuwa ni Shenaiza.
Akazidi kutukaribia na muda mfupi baadaye, tayari alikuwa ametufikia, tukawa tunatembea bila yeyote kati yetu kumsemesha mwenzake. Kwa watu ambao hawakuwa wakielewa kinachoendelea, wangedhani kwamba ni manesi walikuwa wakiwapeleka wagonjwa wao kupata matibabu ya kawaida.
Kwa mbinu ile ilikuwa vigumu sana kwa mtu yeyote kutushtukia, tukazidi kusonga mbele huku nikijitahidi kuibia macho pembeni na kumtazama Shenaiza ambaye alikuwa amekaa kwenye kiti cha magurudumu akiwa haelewi chochote kilichokuwa kinaendelea.
Nguo maalum aliyofunikwa upande wa kichwani, ilifanya iwe vigumu kwa mtu yeyote kumtambua, tukaendelea kusonga mbele mpaka tulipofika kwenye geti la kutokea nje ya hospitali, hapo tukakumbana na kipingamizi ambacho hakuna aliyekitegemea, mapigo ya moyo wangu yakawa yananienda mbio kuliko kawaida.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue
 
SEHEMU YA 45


ILIPOISHIA:
Nguo maalum aliyofunikwa upande wa kichwani, ilifanya iwe vigumu kwa mtu yeyote kumtambua, tukaendelea kusonga mbele mpaka tulipofika kwenye geti la kutokea nje ya hospitali, hapo tukakumbana na kipingamizi ambacho hakuna aliyekitegemea, mapigo ya moyo wangu yakawa yananienda mbio kuliko kawaida.
SASA ENDELEA...
“Haroo! Mnaenda wapi usiku? Harafu hao wagonjwa mbona mumewafunika sura, wafunueni, hima,” alisema askari aliyekuwa amevalia sare maalum, mkononi akiwa ameshika bunduki. Ilibidi Shamila atumie mbinu ya ziada kumtuliza kwani tayari alishaonesha wasiwasi nao.
“Kamanda, ina maana hata mimi hunijui? Hiki hapa ni kitambulisho changu, naitwa Shamila, nawapeleka wagonjwa wangu hapo kwenye maabara za Lancet hapo nje kwenye kipimo cha MRI, si unajua humu ndani hakuna na isitoshe kesho asubuhi kutakuwa na foleni kubwa sana,” alisema Shamila kwa lafudhi laini ambayo ilimfanya yule mlinzi awe anamtazama tu usoni.
“Ooh! Nesi Shamira, kumbe ni wewe, basi wapereke ila ukitoka basi uje hapa nina mazungumzo na wewe kidogo sawa nesi,” alisema mlinzi huyo kwa lafudhi ambayo ilionesha dhahiri kwamba ni Mkurya, kwa kutambua udhaifu wake, Shamila alimbania kijicho kimoja, akawa anachekacheka mwenyewe na kwenda kufungua geti.
Nilimsifu sana Shamila kwa sababu aliutumia vizuri uzuri wa sura na umbo lake, kama asingewahi kumkabili mlinzi yule, ni dhahiri lazima angekuja kunifunua usoni na angeenda kumfunua pia Shenaiza na hapo picha ingeungua, lazima tungeishia pabaya.
Kweli alifungua geti, Shamila na Raya wakaendelea kusukuma vitanda vile vya magurudumu huku kila mmoja kijasho chembamba kikimtoka, hakuna aliyemsemesha mwenzake mpaka tulipozamia gizani, Shamila ndiye aliyevunja ukimya kwa kumuelekeza Raya mahali gari lilipokuwa.
Kwa kuwa tayari tulishafika mbali, ilibidi nijifunue usoni, kwa mbali nikawa naliona gari jeusi, Toyota Noah likiwa limepaki pembeni ya barabara, niligeuka nyuma na kutazama kule tulikotoka, hakukuwa na mtu yeyote aliyekuwa akitufuatilia.
Niliona kama Raya ananichelewesha, nilisimama kwenye kile kiti cha magurudumu na kuanza kutembea mwenyewe, jambo lililoonesha kumchukiza Shamila, hakusema kitu lakini uso wake tu ulionesha hivyo, nikajikaza kiume na kutembea mpaka lile gari lilipokuwa limepaki.
Tulipofika tu, mdogo wake Shenaiza, Firyaal alishuka na kuja kutufungulia mlango, nikawa wa kwanza kuingia. Nilitegemea nitamkuta mtu mwingine mle ndani ya gari kwani bado sikuwa naamini kwamba Firyaal anaweza kuendesha gari peke yake, kutoka nyumbani kwao, Kurasini.
Hata hivyo, hakukuwa na mtu mwingine yeyote ndani ya gari, wote tukaingia, Shamila akakaa siti ya mbele pamoja na Firyaal ambaye ndiye aliyekuwa nyuma ya usukani, safari ikaanza. Sikuamini jinsi Firyaal alivyokuwa na ‘control’ ya gari kwani alilitoa pale alipokuwa amepaki kwa spidi kubwa na kulingiza barabarani, akakanyaga mafuta na kulifanya liwe linakimbia kwa kasi kubwa.
Mbele kidogo alikata kona kali na kuzidi kukanyaga mafuta, tukaingia Barabara ya Umoja wa Mataifa ambako aliendelea kukanyaga mafuta kwa nguvu, gari likawa linakimbia kama tupo kwenye mashindano. Nadhani alikuwa na wasiwasi kwamba huenda kuna watu wanatufuatilia kwa nyuma.
Safari iliendelea, Shamila akawa anamuelekeza njia ya kupita kuelekea nyumbani kwake. Kitu ambacho sikukishtukia kuanzia mwanzo, kumbe wakati Firyaal akiendesha gari, mara kwa mara alikuwa akinitazama kupitia kioo cha juu ya dereva (driving mirror). Hata sijui kwa nini alikuwa akinitazama sana.
Safari iliendelea huku Raya akiwa kimya kabisa pembeni yangu, Shenaiza yeye akiwa amelazwa kwenye siti ya nyuma, akiwa haelewi chochote kilichokuwa kinaendelea. Hatimaye tulifika salama nyumbani kwa Shamila, akashuka na kwenda kufungua geti, Firyaal akaliingiza gari kinyumenyume mpaka ndani.
Nilimvulia kofia msichana huyo, japokuwa alikuwa akionekana kama mdogo, ilionesha na ujuzi wa vitu vingi sana ndani ya kichwa chake. Baada ya kuingiza gari, nilishuka, akafuatia Raya, ndani ya gari akawa amebaki Shenaiza. Ilibidi watatu hao wasaidiane kumshusha kwani mimi nilikuwa nikihofia kujitonesha tena kidonda changu.
Wakamshusha na kumuingiza mpaka ndani, wakampeleka moja kwa moja mpaka kwenye chumba cha wageni, mimi nikakaa pale sebuleni huku nikiangaza macho huku na kule. Nilitaka kujiaminisha kwamba hapo ndani palikuwa salama kama nilivyopaacha.
Muda mfupi baadaye, walitoka chumbani, wakaja mpaka pale sebuleni.
“Kumbe wewe ni dereva mzuri?” nilimuuliza Firyaal, akacheka kwa aibu na kujiinamia chini, wote tukatulia.
“Sasa hapa ndiyo patakuwa ‘safe house’ yetu, mipango yote itapangwa kutokea hapa lakini cha msingi ni kuhakikisha hakuna anayejua kama mpo hapa na njia pekee itakayofanya iwezekane ni kila mmoja kuwa makini. Hata ukibanwa vipi kamwe usije kusema chochote Firyaal, umenielewa,” alisema Shamila, msichana yule akaitikia kwa kutingisha kichwa kisha akanitazama, macho yetu yakagongana kisha haraka akayakwepesha.
Bado sikuwa nimeelewa sababu ya msichana huyo kuwa ananitazama mara kwa mara, hata hivyo sikuwa na haraka, nilijiambia mwenyewe moyoni kwamba ‘nitajua tu’. Shamila alimuonesha ishara Raya kwamba amfuate, wakaelekea jikoni nadhani kwa lengo la kwenda kuandaa chakula maana jioni sikuwa nimekula chochote, pale sebuleni tukabaki na Firyaal.
“Nambie!” nilivunja ukimya, Firyaal akainua uso wake na kunitazama huku aibu za kikekike zikiwa zimemjaa, akaishia kuchekacheka tu.
“Kwani wewe unaishi na nani?” aliniuliza swali ambalo hata sikuelewa kwa sababu gani ameniuliza. Nilikuwa na uhakika kwamba alikuwa anajua naishi peke yangu kwa sababu hata siku ya kwanza kumsaidia dada yake, nilimpeleka nyumbani kwangu kabla ya baadaye kuja kuvamiwa na kuponea kwenye tundu la sindano.
“Naishi mwenyewe, vipi kwani.”
“Nilitaka kujua tu,” alisema kwa lafudhi laini huku akijitahidi sauti yake iwe ya chini. Nadhani hakutaka mtu yeyote ajue kwamba nazungumza naye.
“Wewe ni mchumba’ake dada Shenaiza?” aliniuliza swali lingine ambalo lilinifanya nicheke.
“Hapana, niliamua tu kumsaidia.”
“Kwani we mchumba wako ni nani?” aliniuliza swali lingine, kabla sijamjibu niligeuka huku na kule, nilipohakikisha Raya na Shamila walikuwa jikoni, nilimgeukia na kumuuliza swali juu ya swali.
“Mbona unaniuliza maswali mengi kama polisi?”
“Hamna, nilitaka tu kujua, samahani kama nimekuudhi.”
“Hujaniudhi chochote, kwani we mchumba wako anaitwa nani?”
“Mi sina wala sijawahi kuwa naye.”
“Unataka kusema we humjui mwanaume?” nilimuuliza kwa pupa, akatingisha kichwa kuashiria kwamba ni kweli hakuwa akimjua mwanaume, moyo ukanilipuka paah! Nikageuka na kutazama tena kule jikoni, nikamgeukia Firyaal.
“Kwa nini ulikuwa unaniuliza kuhusu mchumba wangu?”
“Nilitaka kujua tu.”
“Kwa sasa sina, nipo mwenyewe kama unavyoniona,” nilimdanganya, nikamuona tabasamu pana likichanua kwenye uso wake, akaanza kung’atang’ata kucha huku akinitazama kwa macho ya wizi, taratibu nikajikuta nikianza kufikiria mambo tofauti kuhusu Firyaal.
“Ina maana ananipenda? Lakini mbona kama mdogo?” nilijiuliza huku nikiendelea kumkodolea macho Firyaal ambaye naye alishaanza kunifanyia vituko.
Akawa ni kama anataka kukaa vizuri, sketi yake ikafunuka upande mmoja na kunifanya niyaone mapaja yake yaliyokuwa yamejaa vizuri, yenye rangi ya weupe wa kung’aa, mapigo ya moyo wangu yakaanza kunienda mbio.
Ni kama alijua kwamba namtazama, akazidi kunifanyia vituko, akawa na kazi ya kubadilisha mikao, jambo lililomfanya ‘Jamal’ wangu aanze kuchachamaa, nikameza funda la mate kama fisi aliyeona mfupa. Kwa muda nilisahau kabisa kwamba nipo kwenye matatizo makubwa.
“Humu ndani kuna joto,” alisema Firyaal na kufungua kifungo cha blauzi aliyokuwa amevaa, maembe ‘bolibo’ mawili yaliyojaa vizuri yakawa yanaonekana na kunifanya nizidi kuwa kwenye wakati mgumu.
“Ulisema unasomea IT, hebu chukua ile laptop pale uje hapa unisaidie kitu,” nilimtega, naye ni kama alikuwa akiisubiri nafasi hiyo, harakaharaka aliinuka pale alipokuwa amekaa, akaenda kuchukua laptop ya Shamila na kuja nayo kwenye lile kochi nililokuwa nimekaa, akaja kukaa karibu kabisa na mimi kiasi cha kunifanya niwe nalisikia joto la mwili wake, lililonakshiwa kwa manukato mazuri aliyokuwa amejipulizia.
Mara mlango wa jikoni ukafunguliwa.
Je, nini kitafuatia?
 
SEHEMU YA 46

“Ulisema unasomea IT, hebu chukua ile laptop pale uje hapa unisaidie kitu,” nilimtega, naye ni kama alikuwa akiisubiri nafasi hiyo, harakaharaka aliinuka pale alipokuwa amekaa, akaenda kuchukua laptop ya Shamila na kuja nayo kwenye lile kochi nililokuwa nimekaa, akaja kukaa karibu kabisa na mimi kiasi cha kunifanya niwe nalisikia joto la mwili wake, lililonakshiwa kwa manukato mazuri aliyokuwa amejipulizia.
Mara mlango wa jikoni ukafunguliwa.
SASA ENDELEA...
“Vipi?” Shamila aliuliza huku akiwa ni kama ameshtuka f’lani hivi kuniona nikiwa nimekaa jirani namna ile na Firyaal.
“Kuna kazi namuelekeza anisaidie.”
“Ooh! Tena huyo atakufaa zaidi, si amesema anajuajua mambo ya IT?”
“Ndiyo japo bado sijathibitisha,” nilisema huku nikijifanya kumkandamiza Firyaal ili kuua soo, naye ni kama alijua kilichokuwa ndani ya akili yangu, akatulia kiasi cha kufanya iwe vigumu kwa Shamila kuelewa kilichokuwa kikiendelea kati yangu na msichana huyo mdogo lakini mrembo.
Akaenda kwenye friji na kuchukua baadhi ya vifaa kisha akarudi jikoni, akaniacha nikiwa bize nikijifanya namuelekeza kitu Firyaal ambaye naye alikuwa akiitikia kwa umakini, alipoingia jikoni tukatazamana.
“Hapa siyo sehemu sahihi, watatushtukia sasa hivi,” nilimnong’oneza, harakaharaka akanikubalia kwa kutingisha kichwa. Nikamwambia anisaidie kutafuta majina ya watu wote ambao walikuwa ‘wamesaidiwa’ na Shirika la Black Heart lililokuwa likiongozwa na baba yake kwenye zile data tulizoziiba kwenye ile ‘hard disk’ aliyonipa.
Akahama pale alipokuwa amenifuata na kurudi kwenye kiti chake, akajiinamia kwenye laptop na kuanza kufanya ile kazi niliyomuagiza. Shamila alitoka tena jikoni na alipoona kweli Firyaal amejiinamia na kompyuta, wala hakuhisi jambo lolote baya, akawa ananitazama kwa macho fulani hivi ambayo nilimuelewa alichokuwa anamaanisha.
Firyaal aliendelea na kazi, Shamila na Raya nao waliendelea na kazi, mimi nikawa nimekaa zangu pale kwenye kochi nikiwa naendelea kuwaza hili na lile. Nikiri wazi kwamba kabla ya matatizo hayo hayajaanza kunikumba, sikuwa napenda kukaa karibu na wasichana kabisa, yaani kama ungekuja kwangu, kama usingenikuta natazama ‘movie’ basi ungenikuta nacheza gemu za ‘Playstation’.
Tangu nilipoanza kukutana kimwili na Raya, akili zilikuwa ni kama zimezibuka, nikawa najilaumu kwa kuchelewa kuvumbua ‘hazina’ iliyojificha kwa kipindi chote hicho. Kabla sijaendelea, naomba niliweke wazi hili kwa manufaa ya wengine. Wanaume wengi huwa wanaharibikiwa maishani kwa sababu ya kuruka vipengele fulani katika hatua za ukuaji.
Unakuta mtu ule muda ambao alitakiwa afanye mambo ya ‘kitoto’ yeye anakuwa bize na masomo au kazi. Akishaingia kwenye ndoa ndiyo anazibuka na kuanza kuona kama alikuwa anachelewa, matokeo yake ndiyo unakuta mwanaume ana mke mzuri lakini kila siku anasaliti ndoa yake kwa sababu kuna hatua ya ukuaji aliiruka.
Muda mfupi baadaye, chakula kilikuwa tayari, Raya na Shamila wakaandaa chakula, Raya akiwa hajui kabisa kwamba aliyekuwa akishirikiana naye kwa kila kitu alikuwa ni ‘mke mwenzie’, Firyaal naye akijifanya anawaheshimu sana dada zake hao kumbe na yeye alikuwa akijilengesha kwangu.
Baada ya kumaliza kuandaa, tulianza kula huku Shamila akitusisitiza kwamba tusiwe na wasiwasi kuhusu Shenaiza, akatuambia kwamba atamshughulikia na baada ya muda mfupi atarejewa na fahamu zake. Sote tulikuwa kimya kabisa, mtu pekee aliyekuwa akizungumza alikuwa ni Shamila.
Baada ya kumaliza kula, tulikaa pamoja sebuleni hapo na kuanza kupanga namna ya kukabiliana na baba yake Shenaiza. Nilimuuliza Firyaal amefikia wapi kwenye kazi niliyompa, akaniambia ameshapata majina ya watu wote waliosaidiwa na shirika hilo pamoja na anuani zao za makazi pamoja na ndugu zao waliokuwa hapa nchini.
“Basi naomba uunganishe na yale majina ambayo nilishayapata kuanzia mwanzo,” nilisema, Firyaal naye akaitikia kwa adabu kabisa, watu wote wakazidi kutuamini kwamba kweli tulikuwa kikazi zaidi.
Bado ule mchezo wake wa kunitazama kwa kuibia hakuwa ameuacha lakini kwa kuwa sasa Raya na Shamila walikuwa pale sebuleni, nilijifanya sijui chochote kinachoendelea kwa sababu nilihofia wanaweza kutufuma tukitazamana halafu wakatufikiria vibaya.
Tuliendelea kupanga mipango yetu na mwisho tukakubaliana kwamba kwa kuwa ushahidi wote tayari tulikuwa nao, twende tukatoe taarifa polisi ili watusaidie kupambana na genge hatari la baba yake Shenaiza.
Kilichonipa moyo kwamba kila kitu kitafanikiwa, ni jinsi Firyaal alivyoonesha kuchukizwa na vitendo vya baba yake, akatuhakikishia kwamba japokuwa anajua baba yake anaweza hata kufungwa, yupo tayari kwa chochote mpaka tufanikiwe.
Wazo hilo lilipitishwa, tukakubaliana kwamba usiku ule Shamila anatakiwa kurudi kule hospitalini ili kuhakikisha hakuna anayeshtukia kama mimi na Shenaiza tumetoroshwa hospitalini, na asubuhi na mapema ya siku inayofuatia, mimi nitaongozana na Raya mpaka kituo kikuu cha polisi kwa ajili ya kwenda kutoa taarifa.
Kwa kuwa muda ulikuwa umeshaenda, Shamila alimwambia Firyaal amrudishe mpaka hospitalini kwa kutumia gari lake kisha arudi nyumbani kwao, Kurasini ili asije akashtukiwa lakini msichana huyo alikataa katakata, akasema alishamuaga mama yake kwamba anakwenda kwenye ‘birthday’ ya rafiki yake na kwamba hatarudi mpaka asubuhi na aliruhusiwa.
“Twende nikupeleke wewe kazini mi nitakuja kulala hapahapa na dadaa’ngu Shenaiza,” alisema, Shamila na Raya wakamkubalia bila kujua kwamba kuna kitu alichokuwa anakifuata.
Raya naye alipoulizwa kama atarudi nyumbani kwao, naye alisema atakaa na mimi mpaka asubuhi ya kesho yake. Shamila alikubali ingawa nilimuona kama wivu unamsumbua sana, akainuka na kwenda kuanza kuandaa mazingira ya sisi sote kulala.
Mimi aliniandalia kwenye chumba cha peke yangu, Firyaal akamwambia atalala na dada yake kwenye chumba cha wageni na Raya atalala kwenye chumba chake, wote tukamkubalia kwani kwa wakati huyo yeye ndiye aliyekuwa bosi wetu.
Alienda kuoga na kuanza kujiandaa kisha akatuaga na kututaka tuwe makini, hasa mimi, akatoka na Firyaal kuelekea hospitali huku akiniachia maagizo kwamba Firyaal akirudi, nikamsaidie kufungua geti aingize gari kisha baada ya hapo, nifunge milango yote na kuzima taa zote za ndani na nje, nikamkubalia.
Walipotoka, ndani nilibaki na Raya tu ambaye ilionesha alikuwa na hamu kubwa ya mimi na yeye kubaki wawili tu. Alipohakikisha wameshaingia ndani ya gari na kuondoka, harakaharaka alinifuata na bila kuzungumza chochote, alianza fujo zake akitaka nikamalizane naye fasta kabla Firyaal hajarejea.
Hata hivyo, kwa kuwa tayari nilikuwa na ratiba nyingine kichwani, nilimdanganya kwamba siku hiyo nilikuwa nimechoka sana na jeraha langu lilikuwa likima kwa sababu ya purukushani za kutwa nzima, nikamuomba kama hatajali, tukapumzike kwanza mpaka baadaye.
Nilimuona akikubali kwa shingo upande, akaenda kuoga na kuniacha niko pale sebuleni najifanya niko bize na laptop. Baada ya kumaliza kuoga alinifuata tena, nikaendelea kumsisitizia kwamba hali yangu haikuwa nzuri, akaniomba basi tukalale kitanda kimoja ambapo pia nilimkatalia na kumwambia nitamfuata usiku sana wakati Firyaal ameshalala ili tusije kuonesha picha mbaya.
“Basi naacha mlango wazi,” alisema, nikatingisha kichwa kuonesha kumkubalia, akaondoka kwa shingo upande na kwenda kulala. Kutokana na uchovu aliokuwa nao wa pilikapilika za kutwa nzima, hakuchukua raundi, akapitiwa na usingizi mzito.
Nusu saa baadaye, alikuwa akikoroma, hata niliponyata na kwenda kumchungulia, alionesha ameshalala fofofo, moyoni nikawa nachekelea. Harakaharaka nilienda kwenda chumba nilichopangiwa kulala, nikaingia bafuni na kujimwagia maji kupunguza uchovu kisha nikatoka na kwenda kukaa sebuleni nikimsubiri Firyaal kwa shauku kubwa, nikiwa nimejifunga taulo tu! Shetani wa mahaba alikuwa amenizidi nguvu.
Dakika kadhaa baadaye, nikasikia honi ya gari, harakaharaka nikatoka na kwenda kufungua geti, alikuwa ni Firyaal, aliponiona nimejifunga taulo tu, alijifanya kushtuka kisha nikamuona akitabasamu, akaingiza gari na kulipaki, nikafunga mageti kama Shamila alivyoniagiza, tukaingia ndani na kwenda mpaka sebuleni.
“Dada Raya yuko wapi?” aliuliza Firyaal kwa sauti ya chini, nikamwambia ameshalala na sasa anakoroma, nikamuona akishusha pumzi ndefu na kunitazama usoni, tukawa tunatazamana.
“Nataka nikalale na dada Shenaiza,” alisema kwa sauti ya kudeka huku akinisogelea na kujilaza kifuani kwangu, nikapitisha mkono wangu na kumshika kiunoni, nikamuona akiruka kama aliyepigwa na shoti ya umeme.
Je, nini kitafuatia?
 
SEHEMU YA 47


ILIPOISHIA:
“Nataka nikalale na dada Shenaiza,” alisema kwa sauti ya kudeka huku akinisogelea na kujilaza kifuani kwangu, nikapitisha mkono wangu na kumshika kiunoni, nikamuona akiruka kama aliyepigwa na shoti ya umeme.
SASA ENDELEA...
“No! Usifanye hivyo,” alisema Firyaal huku akinitoa mkono kwa staili ya ‘sitaki nataka’, nikamvutia kwangu na kusababisha tuwe tunatazamana katika umbali usiozidi nchi tano, kiasi cha kila mmoja kuwa anazisikia pumzi za mwenzake.
“This is not the right time,” (Huu siyo muda muafaka) alisema huku akiipitisha mikono yake na kunishika shingoni, kwa mara nyingine nikamshika kiunoni, akashtuka tena, safari hii kwa nguvu zaidi na kufumba macho yake mazuri, tukagusanisha ndimi zetu na kuanza kuwaiga njiwa wanavyoyalisha makinda yao.
Jambo la ajabu lilitokea kwenye hisia zangu, nikawa nahisi kama nipo kwenye ulimwengu mwingine wa tofauti kabisa, tuliendelea kugandana kama ruba kwa sekunde chache, kelele za kitasa cha chumba alichokuwa amelala Raya ndizo zilizotushtua.
Harakaharaka nikamuachia Firyaal na kumuonesha kwa ishara kwamba aende chumbani alikokuwa amelala dada yake, kweli alifanya hivyo, akakimbia kwa kunyata wakati mimi nikienda kumfungulia Raya.
“Vipi?” nilimuuliza baada ya kumfungulia mlango ambao ni mimi ndiye niliyemfungia kwa nje ili nipate nafasi nzuri ya kuwa na Firyaal.
“Wewe ndiyo ulinifungia mlango kwa nje?”
“Mh! Saa ngapi tena mpenzi wangu? Itakuwa labda mlango ulijiloki,” nilimwambia.
“Kwani ulikuwa hujalala mpaka saa hizi?”
“Nilikuwa namsubiri Firyaal arudi ndiyo nifunge geti, amesharudi na nafikiri muda huu ameshalala na dada yake na mimi nilikuwa najiandaa kulala,” nilijenga mazingira ya kujitetea. Nikampachika swali jingine:
“Mbona umeamka wakati ndiyo kwanza ulikuwa unaanza kulala?”
“Nimeota ndoto mbaya sana mpaka nimeshtuka,” alisema Raya huku akijinyoosha.
“Ndoto gani tena?”
“Inatisha sana, please Jamal mi siwezi kulala peke yangu, nakuomba tukalale wote,” alisema Raya huku akinikumbatia, nikashusha pumzi ndefu kwani niliona ananiharibia sana ‘taiming’ zangu. Hata hivyo sikuwa na namna zaidi ya kukubaliana naye, nikamshika mkono na kuelekea naye kwenye kile chumba ambacho Shamila alinipa mimi nilale.
Hata hivyo, moyoni nilishajiapiza kwamba sitafanya chochote na Raya hasa ukizingatia kwamba tayari nilishampa udhuru mapema kwamba hali yangu haikuwa nzuri. Baada ya kuingia chumbani, kwa sababu muda ulikuwa tayari umeenda sana, hatukuwa na cha ziada zaidi ya kupanda kitandani na kulala.
Japokuwa Raya alikuwa pembeni yangu, akili zangu zote zilikuwa kwa Firyaal, ni kama nilikuwa nimepandwa na pepo ndani ya kichwa changu. Nilikumbuka kila kitu kilichofanyika muda mfupi uliopita, nikawa nazilaumu ndoto za Raya kwani kama asingeota na kushtuka kama mwenyewe alivyosema, huenda tayari ningeshakuwa naelea kwenye ulimwengu mwingine tofauti kabisa.
Wasiwasi wangu mkubwa ulikuwa ni je, Firyaal akija kunigongea usiku huo itakuwaje? Sikupata majibu. Kwa kuwa Raya alikuwa amechoka sana, nilipomkumbatia tu, hakuchukua muda, akaanza kukoroma tena, akiwa amelala fofofo. Niliendelea kutafakari mambo mengi na hatimaye usingizi ukanipitia.
Mlio wa simu ya mezani ndiyo ulionishtua kutoka kwenye usingizi mzito, nikamsogeza Raya pembeni na kuamka, nikatoka mpaka sebuleni na kwenda kuipokea simu hiyo.
“Haloo!”
“Haloo Jamal, umeamkaje mpenzi wangu?”
“Ooh! Shamila, ni wewe? Nimeamka salama, vipi wewe huko?”
“Huku kuna matatizo mpenzi wangu, nimekupigia kukwambia kwamba inawezekana nikawa sipatikani hewani, ishu imeshtukiwa huku na imebainika kwamba nimehusika kuwatorosha wagonjwa wawili, wewe na Shenaiza, hIvi ninavyoongea na wewe tunaingia kwenye mkutano wa dharura na viongozi wetu pamoja na polisi.”
“Mungu wangu, kwa hiyo itakuwaje?”
“Nimekupigia simu kukutaarifu kwamba hapo nyumbani kwangu hapafai tena, kuna uwezekano mkubwa polisi wakaja kufanya upekuzi kwa hiyo nakuomba muondoke haraka iwezekanavyo. Chukua kalamu na karatasi, andika namba hii nitakayokutajia,” alisema Shamila na kunifanya mapigo ya moyo wangu yawe yananienda mbio kuliko kawaida.
Nikachukua kalamu na karatasi.
‘Tayari nimeshachukua,” nilimwambia Shamila baada ya kuuinua tena mkonga wa simu, akanitajia namba hiyo ya simu na kuniambia kwamba ni ya mama yake mdogo anayeishi Kimara Temboni.
“Nimeshampigia na kumwambia kila kitu, yupo tayari kuwasaidia, mpigie sasa hivi,” alisema Shamila kisha akakata simu. Nilipoweka mkonga wa simu chini, nilitazama saa ya ukutani iliyokuwa inaonesha kwamba ilikuwa ni tayari saa kumi na mbili asubuhi, harakaharaka nikaelekea kwenye chumba alichokuwa amelala Firyaal na Shenaiza ambaye bado hakuwa amerejewa na fahamu zake.
“Firyaal, Firyaal,” nilisema huku nikigonga mlango wa chumba hicho, nilipoona kimya nikanyonga kitasa, kumbe hata hakuwa amefunga mlango, nadhani alijua kwa vyovyote usiku ule nitamfuata tena.
Nikaingia na kutupa macho kitandani, Firyaal alikuwa amelala kihasarahasara, akiwa amejifunga khanga moja tu huku dada yake, Shenaiza akiwa amelala kwenye kitanda kingine maana ndani ya chumba hicho kulikuwa na vitanda viwili.
Nilishusha pumzi ndefu kwani nikiri kwamba Firyaal alikuwa akiyafanya mapigo ya moyo wangu yaniende mbio sana, hasa kutokana na hali niliyomkuta nayo, mwenyewe akiwa hana habari ameuchapa usingizi.
Taratibu nilimsogelea, nikainama pale kitandani na kumbusu kwenye paji la uso wake, akafumbua macho na kunitazama, akaachia tabasamu hafifu na kunishika mkono wangu, joto la kikekike likazidi kunifanya nisisimke mno.
“Mbona umechelewa kuja Jamal wangu, hata mlango sikufunga kwa ajili yako,” alisema huku akinivutia pale kitandani ili na mimi nilale.
“Kuna tatizo Firyaal,” nilimwambia, kauli yangu ikamfanya ayakodoe macho yake mazuri ambayo yalikuwa yamelegea sana kwa sababu ya usingizi.
“Tatizo gani tena mpenzi?” aliniuliza kwa sauti iliyojaa shauku.
“Shamila amepiga simu anasema huko kazini kwao kimenuka, wamemshtukia kwamba yeye ndiye aliyetutorosha na hivi tunavyoongea wameingia kwenye kikao cha dharura, anasema inabidi tuondoke hapa haraka iwezekanavyo,” nilimwambia.
“Mungu wangu,” alisema huku akikurupuka pale kitandani, akasimama huku akinitazama kwa wasiwasi, mkono mmoja akautumia kuirudisha ile khanga yake ambayo alipoinuka ilifunuka upande na kusababisha niyaone tena maungo yake ambayo ama kwa hakika yalikuwa yakimuamsha shetani wangu wa mahaba.
“Kwa hiyo itakuwaje?”
“Inabidi tujiandae tuondoke, oga fastafasta kisha muandae mgonjwa, ngoja na mimi nikamuamshe Raya,” nilisema, akatingisha kichwa huku akiendelea kunitazama kwa macho yake mazuri, nikageuka na kutaka kutoka, akanishika mkono huku akiliita jina langu.
“Nambie,” nilijibu kwa upole, akanisogelea hadi mwilini na kunikumbatia kwa nguvu.
“Nakupenda Jamal,” alisema kisha akanibusu kwenye shavu langu la upande wa kushoto, mwili wote ukasisimka tena, nikakosa hata cha kujibu zaidi ya mimi kumkumbatia pia na kumbusu, uvuguvugu wa joto la mwili wake ukanifanya nitamani niendelee kumkumbatia lakini nilipokumbuka mtihani mzito uliokuwa mbele yangu, nilimuachia, nikatoka haraka na kwenda kumuamsha Raya, harakaharaka tukaanza kujiandaa.
Je, nini kitafuatia?
 
Asante.hadithi Nzuri. Ila jamaa amebadilika kawa mtu Wa kupenda wanawake.watakuja kumponza
 
SEHEMU YA 48

ILIPOISHIA:
“Nakupenda Jamal,” alisema kisha akanibusu kwenye shavu langu la upande wa kushoto, mwili wote ukasisimka tena, nikakosa hata cha kujibu zaidi ya mimi kumkumbatia pia na kumbusu, uvuguvugu wa joto la mwili wake ukanifanya nitamani niendelee kumkumbatia lakini nilipokumbuka mtihani mzito uliokuwa mbele yangu, nilimuachia, nikatoka haraka na kwenda kumuamsha Raya, harakaharaka tukaanza kujiandaa.
SASA ENDELEA…
Muda mfupi baadaye, tayari tulikuwa tumeshamaliza kujiandaa, mimi na Raya tukasaidiana kumbeba Shenaiza ambaye bado alikuwa haelewi chochote kinachoendelea, Firyaal akaenda kuwasha gari. Ilibidi kila kitu kifanyike harakaharaka kama Shamila alivyotuambia.
Kwa bahati nzuri tulifanikiwa kutoka salama, tukafunga milango yote na kuiacha funguo mahali alipokuwa ametuelekeza Shamila. Kwa kuwa bado ilikuwa ni asubuhi, hakukuwa na foleni sana barabarani, safari ya kuelekea Kimara Temboni ikaanza.
Ilibidi nimuombe Raya simu yake kwa ajili ya kumpigia yule mtu ambaye Shamila aliniambia kwamba ni ndugu yake ambaye ndiye angeenda kutupokea na kutupa hifadhi. Namshukuru Mungu kwamba nilivyopiga mara moja tu, alipokea, tukazungumza na kuelewana.
Nikawa namuelekeza Firyaal kama na mimi nilivyoelekezwa na yule mwenyeji wetu, kwa bahati nzuri tulipofika Kimara Temboni tu, mwanamke wa makamo, mweupe na mnene kiasi, alitupokea. Yeye alikuwa amepanda bodaboda, akatonesha ishara kwamba tumfuate, Firyaal ambaye alikuwa na uzoefu wa kutosha wa kuendesha gari, akawa anamfuata.
Tulishuka makorongo mpaka tulipotokea ng’ambo ya pili, akasimama mbele ya geti kubwa jeusi na kumlipa yule dereva wa bodaboda, akasubiri mpaka aondoke kisha ndiyo akatufuata. Kwa kuwa kiumri alikua mkubwa kwetu, sote tulimuamkia kwa heshima, akamwambia Firyaal inabidi aliingize gari ndani ya geti kwa usalama zaidi.
Akatufungulia geti na muda mfupi baadaye, tayari tulikuwa ndani, tukasaidiana kumshusha Shenaiza mpaka ndani, akatukaribisha na kututaka kuwa makini kwa muda wote ambao tutakuwa pale nyumbani kwake.
“Inaonesha mambo siyo mazuri kwa Shamila, nimetoka kuongea naye sasa hivi na yeye ndiye mtuhumiwa namba moja, lazima atapewa kashikashi kubwa na polisi kwa hiyo inabidi sote tutulie tusije tukasababisha matatizo mengine, kuweni makini sana na simu zenu,” alisema, wote tukatingisha vichwa kama ishara ya kumuelewa.
Kwa kuwa nyumba ilikuwa kubwa, alitupangia kila mmoja chumba chake na kutuambia tutakaa hapo mpaka mambo yatakapotulia. Ilionesha kwamba mwanamke yule anajimudu sana kimaisha kwa jinsi mazingira ya pale nyumbani kwake yalivyokuwa.
Muda ulizidi kuyoyoma huku nikiwa na shauku kubwa ya kutaka kujua nini kitatokea kwa Shamila kwani kama ni matatizo, basi tulikuwa tumemsababishia makubwa sana.
“Kuna anayejua kufanya ‘meditation’ kati yenu?” aliuliza mwanamke huyo ambaye baadaye alituambia kuwa tuwe tunamuita mama wawili, wote tukatazamana.
“Shamila yupo kwenye matatizo makubwa, inatakiwa tufanye kitu kumuokoa vinginevyo mambo yatakuwa mabaya sana kwake,” alisema, nikashindwa kuelewa uhusiano uliokuwepo kati ya kufanya meditation na kila alichokuwa anakizungumza.
“Kwani meditation ni nini?” nilimuuliza nikiwa na shauku kubwa, akanitazama bila kunijibu chochote kwa sekunde kadhaa kisha atatuambia mimi, Raya na Firyaal tumfuate, tukaingia ndani ya chumba kimoja kilichokuwa kimetandikwa zulia jekundu la bei mbaya.
“Hata kama hamjui ni lazima tushirikiane kumsaidia Shamila, mimi peke yangu siwezi, nitawafundisha nini cha kufanya,” alisema, sote tukashusha pumzi ndefu na kuanza kumsikiliza. Akatuambia kwamba kwa kawaida, binadamu tuna nguvu kubwa zisizoonekaa kwa macho, ambazo kama zikitumiwa vizuri zinaweza kutoa matokeo makubwa.
Akasema jukumu la kwanza ambalo tulitakiwa kulifanya kwa muda huo, ilikuwa ni kumkomboa Shamila kutoka kwenye mkono wa sheria, sikumuelewa kabisa alichokuwa anamaanisha, ikabidi nimuulize.
Akaniambia kwamba tunatakiwa wote tukae na kutulia katika mkao ambao kila mmoja wetu ataruhusu nguvu aliyonayo itumike kwa ajili ya kazi iliyokuwa mbele yetu, bado sikumuelewa zaidi ya kuona kama ananichanganya kichwa.
“Kuna kitu kinaitwa out of body experience au kwa kifupi OBE, yaani mwili wako unakuwa upo hapa lakini kwa wakati huohuo unakuwa sehemu nyingine tofauti ukifanya kitu kingine tofauti kabisa,” alizidi kutueleza lakini bado kwangu ulikuwa ni sawa na usiku wa giza.
Hamjawahi kusikia au kuona mtu anajitazama mwili wake mwenyewe akiwa nje ya mwili huo?” alisema kitu ambacho kiliushtua sana moyo wangu, mapigo ya moyo yakaanza kunienda mbio. Kilichofanya nishtuke ni kwamba kile alichokuwa akikizungumza, mimi kilishawahi kunitokea lakini nilikuwa sijui ni nini na inakuwaje.
Nilikumbuka vizuri siku nilipovamiwa na wale watu ambao walinishambulia vibaya na kutaka kuyakatisha maisha yangu, muda huohuo nikaanza kuhisi kama napaa halafu nikawa nauona mwili wangu ukiwa umelala chini, damu nyingi zikitoka kwenye jeraha la kifuani.
Nilikumbuka kila kitu ambacho kiliendelea kutokea na maruweruwe yote mpaka siku nilipokuja kuzinduka na kurejewa na fahamu zangu.
“Mbona kama uko mbali kimawazo? Tunaenda pamoja kweli?” alihoji mama wawili huku akiwa amenikodolea macho, nikawa namtazama lakini akili zangu zipo kwenye ulimwengu mwingine kabisa, ni kama alijua kwani alinishika na kusababisha nishtuke sana, wote wakawa wananishangaa.
“Ili hiki tunachoenda kukifanya kitimie lazima kila mmoja akili zake ziwe hapa, umenisikia kaka?” alisema mama wawili akinilenga mimi, nikashusha pumzi ndefu na kukaa vizuri. Akaendelea:
“Sasa kwa kuwa kati yenu hakuna anayejua tunachoenda kukifanya, nawaomba kila mmoja atulie tukiwa tumeshikana kisha mimi nitazitumia nguvu zenu kufanikisha hili linalotukabili, mambo mengine tutaendelea kuelekezana taratibu, tumeelewana?” alisema, wote tukaitikia kwamba tumemuelewa.
Akatuelekeza namna ya kukaa, wote tukakunja miguu na kuzunguka kama duara, akatuambia kila mmoja anatakiwa afumbe macho, ainue shingo yake na kupumua kwa uhuru kabisa huku akitutaka kutuliza akili zetu sehemu moja.
“Unatulizaje akili sehemu moja?”
“Nyie wote si mnaijua vizuri hospitali anayofanya kazi Shamila si ndiyo?”
“Ndiyo.”
“Basi nataka mkifumba macho, kila mmoja avute picha na kuanza kujiona kama yupo pale hospitalini na mtulize akili hapohapo, tumeelewana?” alisema mama wawili, wote tukatii alichotuambia, tukaweka duara na kushikana mikono, kila mmoja akawa anavuta hewa na kuitolea mdomoni kama alivyotufundisha.
Ndani ya dakika mbili tangu tukae mkao huo, kuna mambo ya ajabu yalianza kunitokea, mapigo ya moyo yakawa yanazidi kwenda mbio kuliko kawaida kutokana na kile nilichokuwa nakishuhudia.
Je, nini kitafuatia?
 
Mkuu haka ka story kanaenda polepole Sana aisee mpaka kanatia uvivu japo kanahamasisha kujua nini mwisho wake
 
SEHEMU YA 49


ILIPOISHIA:
Ndani ya dakika mbili tangu tukae mkao huo, kuna mambo ya ajabu yalianza kunitokea, mapigo ya moyo yakawa yanazidi kwenda mbio kuliko kawaida kutokana na kile nilichokuwa nakishuhudia.
SASA ENDELEA…
Nilianza kuona ile hali kama ambayo ilinitokea siku ile nilipovamiwa barabarani na kujeruhiwa vibaya na baadaye kuingia kwenye ulimwengu wa tofauti, nikawa najihisi kwamba japokuwa nilikuwa nimekaa pale chini na wenzangu, taswira nyingine ya mwili wangu ilikuwa ikianza kupaa juu na kuelea angani, nikawa sielewi nini kinachotaka kutokea.
Cha ajabu ni kwamba, yule aliyekuwa akianza kupaa ndiyo alikuwa mimi kwa sababu nilikuwa najitambua kabisa, nikainamisha kichwa na kutazama chini, nikajiona nikiwa nimekaa pale juu ya zulia, nikiwa nimeshikana mikono na yule mwenyeji wetu, Raya na Firyaal, jambo ambalo lilisababisha hofu kubwa ndani ya moyo wangu.
“Noo! Sitaki kufa tena, sitakiii,” nilisema kwa sauti ya juu, nikashtukia nikiporomoka kutoka pale juu nilipokuwa nikielea, nikaanguka chini kama furushi na kujibamiza sakafuni kwa kishindo.
Nilipofumbua macho, kila mtu alikuwa amepigwa na butwaa akiwa ni kama haamini kilichotokea, nikawa nahema kwa nguvu huku nikiwa nimelala sakafuni, sikukumbuka hata niliwaachia wenzangu mikono saa ngapi, wote wakabaki kunishangaa.
“Hutaki kufa tena? Unamaanisha nini?” aliniuliza yule mwenyeji wetu, nikainuka pale nilipokuwa nimeanguka na kukaa, nikawa nawatazama mmoja baada ya mwingine huku nikijihisi aibu kubwa usoni.
“Naongea na wewe kijana, vipi mbona sikuelewi?” yule mwenyeji wetu alizidi kunibana kwa maswali lakini sikuwa na cha kujibu, Raya na Firyaal wote wakawa wanaendelea kunitazama kwa macho ya mshangao, kila mmoja akionesha kuwa na shauku kubwa ya kutaka kusikia nitajibu nini.
“Hata sielewi kilichotokea,” nilisema, wote wakashusha pumzi ndefu na kutazamana.
“Hebu naombeni mtupishe mara moja mimi na Jamal, alisema yule mwanamke ambaye kiumri alikuwa mtu mzima, Raya na Firyaal wakasimama na kutoka mle chumbani, wakaenda kukaa sebuleni, nikawa nawasikia wanazungumza lakini sikuelewa walikuwa wakizungumzia nini ingawa nilijua kwamba walikuwa wakiniongelea.
“Hebu niambie ukweli, umeona nini au kipi kilichokutokea?” aliniuliza mwanamke huyo wa makamo, mweupe na mnene kiasi, niligeuka huku na kule na nilipohakikisha tupo wawili tu, nilimuuliza swali juu ya swali.
“Umesema OBE ni nini?”
“Mbona nakuuliza swali unaacha kunijibu na wewe unaniuliza? Tupo nyuma ya muda na tunatakiwa kufanya haraka kumsaidia Shamila, niambie nini kimetokea?”
“Ninachotaka kukwambia kinahusiana na hiyo OBE na nahisi hii si mara ya kwanza kutokewa na hiki kilichonitokea,” nilimwambia, kwa mara nyingine akashusha pumzi ndefu na kunitazama. Nadhani alihisi kwamba sikuwa huru kuzungumza kwa sababu mara kwa mara nilikuwa nikigeuka na kutazama mlangoni.
Ikabidi ainuke na kwenda mpaka mlangoni, akaufunga na kurudi pale nilipokuwa nimekaa, safari hii akanisogelea karibu huku akinitazama kwa macho ya udadisi.
“Shamila si ni rafiki yako?”
“Ndiyo.”
“Unamuamini?”
“Ndiyo. Vipi kwani?”
“Kama unamuamini Shamila basi nakuomba uniamini na mimi, your secrets are safe with me (siri zako zitakuwa salama ukiwa na mimi) aliongea kwa kuchanganya na Kiingereza kuonesha kwamba alikuwa ameenda shule. Kabla sijamjibu, akaendelea:
“Nikikutazama kuna kitu nakiona lakini siwezi kukielezea mpaka mwenyewe uniambie. Halafu inaonekana kuna jambo halipo sawa kwenye mwili wako, una wapenzi wangapi?” aliniuliza swali ambalo lilinishtua sana, nikashindwa kumuelewa alikuwa ameona nini kwangu na swali lile lilikuwa na uhusiano gani na nilichomuuliza.
Nikashindwa cha kumjibu zaidi ya kubaki nikimkodolea macho usoni, akanishika mkono na kunifanya nizinduke. Sijui kwa nini hali ya mawazo kutengana na mwili wangu ilikuwa ikinitokeatokea sana safari hii. Yaani ilikuwa unaweza kuniona nakutazama ukahisi akili zangu zipo pale lakini kumbe nikawa nawaza kitu kingine tofauti kabisa.
“Shamila ni mwanangu, mimi ni mama yake mdogo kwa hiyo nakuomba tena usiwe na wasiwasi unapokuwa na mimi, hebu nijibu maswali yote niliyokuuliza, sawa baba,” aliongea kwa lugha ya upole na kubembeleza, nikashusha pumzi ndefu na kidogo nikaanza kuhisi amani ndani ya moyo wangu.
“Nina mpenzi mmoja tu, kwa nini umeniuliza?”
“Unajua kwa mtu mwenye utaalamu wa elimu ya nguvu zisizoonekana kama mimi, nikikutazama tu naweza nikajua wewe ni mtu wa namna gani. Nikikuangalia naona kama kwa siku za hivi karibuni umekutana kimwili na zaidi ya mwanamke mmoja na inaonesha pia upo kwenye mipango ya kufanya hivyo kwa wanawake wengine zaidi, kama nimekosea naomba unisamehe,” alisema yule mwanamke, kauli iliyozidi kunishangaza mno.
Alichokisema kilikuwa kweli, nilikuwa nimekutana kimwili na Raya na Shamila kwa kuwachanganya ingawa wenyewe hawakuwa wakijua chochote na kama hiyo haitoshi, nilikuwa kwenye mipango ya kufanya hivyo kwa Firyaal pia ambaye yeye ndiye aliyeonesha kunipenda mimi zaidi na kujikuta nikishindwa kuendelea kuvunga.
“Anyway, najua hayo ni mambo ya ujana tuachane nayo lakini kubwa nahisi kama umewahi kutokewa na jambo kubwa sana linalokufanya uwe tofauti na binadamu wengine na ndiyo maana hapa umekwamisha tulichokuwa tunataka kukifanya. Inaonesha una nguvu kubwa sana ambazo pengine hata wewe mwenyewe hujui na ndizo zinazokutesa,” alisema na kuzidi kunichanganya kichwa.
“Unamaanisha nini unaposema nguvu zisizoonekana?”
“Kwani wewe uliposema hutaki kufa tena na ukavuruga kazi tuliyokuwa tunaifanya ulimaanisha nini?” mfumo wa swali juu ya swali uliendelea kutawala katika mazungmzo yetu.
“Umewahi kufika kuzimu?” aliniuliza swali lingine, nikatingisha kichwa harakaharaka kukataa lakini alinigundua kwamba kuna jambo namficha.
“Hapo kifuani umefanya nini?” aliniuliza, eti na mimi nikawa najitazama kama najishangaa, akajua kwamba nilikuwa na mambo mengi ninayoyaficha, akazungumza kwa sauti yenye mamlaka sasa”
“Sikia, kama bado huniamini huwezi kuwa na msaada wowote katika hili tunalotaka kulifanya, itabidi wewe ukakae sebuleni utusubiri mimi na hao wenzako tufanye kinachowezekana kumuokoa Shamila, haupo tayari kushirikiana na sisi, yaani ni kama nakulazimisha hivi.”
“Hapana, siyo hivyo.”
“Siyo hivyo nini? Muda unazidi kuyoyoma, Shamila yupo kwenye matatizo, kila nachokuuliza unanichenga sasa unataka nifikirie nini?” alisema huku akisimama, akionesha kuchukia.
Siyo kwamba sikuwa tayari kumjibu maswali yake lakini alichonichanganya alikuwa akitaka kujua vitu vingi kwa wakati mmoja, wakati mambo yenyewe hayakuwa mepesi kuyafafanua mpaka mtu akaelewa.
“Nataka kumsaidia Shamila,” nilisema.
“Nijibu maswali yote niliyokuuliza.”
“Nitakujibu lakini itakuwa ni baada ya kumaliza kazi ya kumsaidia Shamila.”
“Hapana, wewe una nguvu kubwa sana ambazo mwenyewe hujui namna ya kuzitumia, unaweza kufanya tena kama hiki ulichokifanya hapa ukasababisha tudhalilike huko nje tunakokwenda.”
“Hapana, nitajitahidi naomba uniamini.”
“Unaniahidi?”
“Ndiyo,” nilisema kwa kujiamini, akanitazama usoni kisha akaenda mlangoni na kufungua, akawaita Raya na Firyaal, wakaingia ndani na tukakaa tena kama tulivyokuwa tumekaa mwanzo, kazi ikaanza upya huku akinisisitiza kuwa makini na kuishinda hofu ndani ya moyo wangu, nikatingisha kichwa kama ishara ya kukubaliana naye.
Je, nini kitafuatia?
 
SEHEMU YA 50


ILIPOISHIA:
Sijisifii lakini ukweli ni kwamba katika suala la mbio, nilikuwa na uwezo mkubwa sana, dakika chache baadaye nikawa nimeshatokomea kwenye mashamba ya mikorosho na minazi, kelele za wale watu waliokuwa wakinifukuza zikiwa bado zinaendelea kusikika, sauti ya baba ikasikika tena masikioni mwangu lakini safari hii, ilikuwa na maelezo ambayo yalinimaliza kabisa nguvu, nikajua mwisho wangu umewadia. Niliujutia sana uamuzi wangu wa kujipeleka mwenyewe kwenye mdomo wa mamba.
SASA ENDELEA...
“Inabidi uvue nguo zote na kukimbia kuelekea upande wa Magharibi mpaka uvuke barabara ya lami kisha kimbia mpaka utakapoukuta mti mkubwa wa mbuyu, uzunguke mara saba kisha fumba macho, usifumbue mpaka nitakapokwambia,” sauti ya baba ilisikika masikioni mwangu.
Yaani nivue nguo zote na kuanza kukimbia nikiwa mtupu? Kibaya zaidi, upande huo wa Magharibi aliokuwa anausema ilikuwa ni kulekule nilikokuwa nakimbia. Kwa lugha nyepesi nilitakiwa kuanza upya kukimbia kurudi kule nilikotoka, safari hii nikiwa mtupu! Ilikuwa ni zaidi ya mtihani.
Kitu pekee nilichokuwa nakihitaji, ilikuwa ni kuokoa na balaa hilo kwani kwa jinsi wale wazee waliokuwa wakinikimbiza walivyokuwa na hasira, kama wangenitia mikononi mwao sijui nini kingetokea. Ilibidi nipige moyo konde, harakaharaka nikavua nguo zote na viatu, nikavikunja na kuvitia kwapani.
Mpaka namaliza, lile kundi lilikuwa limenikaribia sana, kitu pekee ambacho nilikuwa nacho makini, ilikuwa ni kuifunga vizuri ile hirizi yangu mkononi, nikaanza kukimbia kulifuata lile kundi huku nikiwa na hofu kubwa mno moyoni.
Cha ajabu, japokuwa nilikuwa nikikimbia kuelekea kule walikokuwa wanatokea, tena nikiwa mtupu kabisa, ilionesha dhahiri kwamba hakuna aliyekuwa akiniona kwani waliendelea kuangaza macho huku na kule huku wakiendelea kukimbia. Nikawafikia na kupishana nao katika namna ambayo nilikuwa makini kuhakikisha simgusi yeyote wala wao hawanigusi kama baba alivyonieleza.
“Hebu simameni kwanza, mbona nywele zinanisisimka hivi?” mmoja kati ya wale wazee. Nadhani yeye alihisi uwepo wangu mahali hapo, wote wakafunga breki na kusimama, wakawa wanatazama huku na kule lakini walishachelewa kwani nilizidi kutimua mbio kama kiberenge.
Nikakwepa kidogo pale kwenye msiba na kupita pembenipembeni kwa kasi kubwa, kizaazaa kikawa kuvuka barabara ya lami. Ikumbukwe kwamba kote huko nilikokuwa napita, japokuwa ilikuwani asubuhi na kulikuwa na watu, ilionesha dhahiri kwamba hakuna aliyekuwa akiniona ingawa mimi nilikuwa nawaona vizuri.
Nilipofika barabarani, kuna pikipiki ilikuwa ikitokea upande wa Morogoro, sikuiona mapema, ile nimeshaingia barabarani ndiyo nikaishtukia ikiwa inakuja kwa kasi kubwa, nikajua kama nisipokuwa makini, inaweza kunigonga na kwa kasi iliyokuwa nayo, sijui nini kingetokea.
Nilichokifanya, nilijirusha juu, nikashangaa mwili umekuwa mwepesi sana, nikamruka yule dereva na bodaboda yake lakini kwa bahati mbaya, mguu mmoja nilimgonga kichwani, nikaenda kuangukia ng’ambo ya pili ya barabara na kuinuka haraka, nikataka niendelee kutimua mbio lakini ghafla nilishtushwa na kishindo kizito barabarani.
Ilibidi nijiibe na kugeuza kidogo shingo kwa sababu miongoni mwa masharti niliyoelekezwa na baba, ni mwiko kugeuka nyumaunapokuwa kwenye shughuli zinazotumia nguvu za giza. Nilimshuhudia yule dereva wa bodaboda akiwa ameanguka katikati ya barabara na kujibamiza kwa nguvu.
Nilishtuka sana, nikajua kwa vyovyote mimi ndiyo nimesababisha kwa sababu hata kama yeye hakuwa ameniona, mimi nilimuona na ndiyo maana nilimkwepa lakini kwa bahati mbaya, nikamgonga kichwani. Kilichonitisha zaidi, ni kasi aliyokuwa nayo na uzito wa kishindo chenyewe, nikajua tayari mambo yameshaharibika.
“Mungu wangui, hawezi kupona yule,” nilisikia sauti za mmoja kati ya waombolezaji waliokuwa pale kwenye msiba kwa sababu tukio hilo lilikuwa limetokea mita chache tu pembeni, hasa ukizingatia nilishaeleza kwamba nyumba yenye msiba ilikuwa karibu na barabarani.
Waombolezaji wengi walikimbilia eneo la tukio kujaribu kutoa msaada lakini wengi walisikika wakisema kwa jinsi alivyokula mzinga hawezi kupona. Nilitamani kwenda kushuhudia kilichotokea lakini kwa sababu na mimi nilikuwa na majanga yangu, niliendelea kukimbia. Nilikimbia sana, miba mikali ikinichoma miguuni lakini sikujali.
Mbele kabisa nikauona mbuyu mkubwa kama baba alivyonielekeza, nikaendelea kukimbia mpaka nilipoufikia, nikaanza kukimbia kuuzunguka kutokea upande wa kushoto kuelekea kulia. Nilipofikisha raundi ya saba, nilisikia kizunguzungu kikali, nikadondoka chini kisha nikaona kama giza nene likitanda kwenye upeo wa macho yangu, sikuelewa tena kilichoendelea.
“Wewe Togo, hebu amka,” sauti ya chini ya baba iliyoambatana na teke zito ubavuni ndiyo iliyonizindua kwenye usingizi wa kifo, nikafumbua macho na kushtuka nikiwa nyuma ya nyuma ya akina Rahma, tena nikiwa uchi wa mnyama.
“Vaa nguo haraka, unajifanya mjuaji sana wewe, siku nyingine sikusaidii, pumbavu,” alisema baba huku akiniongezea teke lingine la ubavuni lililosababisha nijisikie maumivu makali.
Niliijizoazoa huku nikijiziba sehemu za mbele kwa mikono yangu, nikaokota nguo zangu zilizokuwa pembeni na kuanza kuvaa huku nikijiuliza nimefikaje nyumbani bila kupata majibu.
“Sijui kwa nini nimeenda kukuandikisha mtu mjinga kama wewe,” alisema baba kwa hasira huku akinishika masikio yangu mawili na kuyavuta kwa nguvu, akiwa ni kama anataka kuninyanyua juu, akanisindikizia na kofi zito lililosababisha nishindwe kujizua, machozi yakawa yananitoka.
Zilikuwa zimepita siku nyingi sana bila baba kunipiga lakini naona siku hiyo nilikuwa nimemuudhi sana, nikawa nahisi kama masikio yangu yananyofoka kwa jinsi alivyoyavuta kwa nguvu, na ule upande alionizabua kofi nao nikawa nahisi kama unawaka moto.
“Chumbani moja kwa moja na ole wako utoke,” alisema baba kwa hasira, nikatembea harakaharaka huku machozi yakinitoka, uso wangu nikiwa nimeuinamisha. Ile naingia tu mlangoni niligongana na Rahma lakini kwa kuwa nilikuwa nalia na akili ilikuwa na mawenge, sikukumbuka hata kumsalimu, nikatembea harakaharaka huku nikichechemea kwani miguu ilikuwa na miba ya kutosha na sikuwa nimepata hata muda wa kuitoa.
Niliingia chumbani na kujilaza kitandani nikiwa bado najiuliza nimefikaje eneo hilo, nikalia kwanza kupunguza hasira zangu kisha nikaanza kutafakari kwa kina mlolongo wa kila kitu kilichotokea. Yaani ndani ya saa chache tu kulikuwa kumetokea matukio mengi mno ya kutisha, ya kuhuzunisha, ya kushangaza na kuchanganya kichwa.
Bado moyo wangu ulikuwa na huzuni kubwa kutokana na hali niliyoiona kule msibani, na japokuwa malengo yangu ya kwenda Hospitali ya Tumbi kuona hiyo maiti ya yule mtoto hayakuwa yamekamilika, bado nilikuwana shauku kubwa ya kutaka kujua kilichotokea. Lakini ni hapo pia nilipokumbuka ile ajali nyingine ya bodaboda niliyoisababisha na pia nikakumbuka kisanga cha dereva wa Bajaj aliyekuwa akipaki jirani na hapo kwa akina Rahma na jinsi nilivyomkomesha asubuhi hiyo. Sikujua kama amesharudi au la na sikujua siku atakaponiona tena atasema nini.
Nikiwa nimezama kwenye dimbwi la mawazo, nilisikia mlango ukifunguliwa, Rahma akaingiza kichwa na kuchungulia ndani, macho yangu na yake yakagongana.
Je, nini kitafuatia?
Umechanganya Madawa!!!
 
Anaboa sana huyu jamaaaaa
Mpaka namiss story za The Bold hana uswahili huuu
 
Back
Top Bottom