Simulizi ya kweli: Niliishi kuzimu siku saba

Simulizi ya kweli: Niliishi kuzimu siku saba

ILIPOISHIA:

Maneno yake yalinipa nguvu sana, akaniambia kwamba aliwalaza usingizi mzito kwa makusudi wale wengine ili tukamalizie kazi ya kumzindua Shenaiza lakini akanipa taarifa ambazo zilinishtua mno. Aliniambia baba yake Shenaiza amejizatiti vilivyo kwa nguvu za nje na ndani na ili tufanikishe azma yetu, ilikuwa ni lazima mtu mmoja kati yetu afe.

“Afe?”

“Ndiyo, lazima afe mtu kwenye kafara.”

SASA ENDELEA...

“Sasa mambo ya makafara yanaingiaje tena hapa? Kama ni hivyo basi mimi najitoa.”

“Ukijitoa maana yake wewe ndiyo utakufa. Wasiwasi wa nini na wewe ni mwanaume? Hebu acha woga, nitakufundisha cha kufanya wala usiwe na wasiwasi,” alisema Junaitha lakini kiukweli alikuwa amenichanganya mno.

Mmoja kati yetu lazima afe? Nani sasa! Kama siyo mimi ni nani? Raya? Haiwezekani. Shenaiza? Hapana. Shamila? Noo! Au Firyaal? Nilijiuliza maswali mengi ambayo yote hayakuwa na majibu. Nilichokifanya ilikuwa ni kujaribu kupambana na hofu ambayo sasa ilikuwa inanitafuna ndani kwa ndani.


Hakuna kitu ambacho binadamu hawezi kukizoea kama kifo! Miaka yote watu wanakufa lakini kwa nini kila mtu anapokufa kunakuwa na msiba mzito kwa watu wanaomzunguka? Ni dhahiri kwamba kifo hakizoeleki.

“Mbona kama umepoteza umakini Jamal? Kwani wewe unaelewa nini kuhusu kifo?” aliniuliza Junaitha, swali ambalo lilinizindua kutoka kwenye lindi la mawazo.

“Kifo? Kifo si ni kufa?”
“Ndiyo ni kufa, unaelewa nini kuhusu kufa?”

“Mtu anakufa na huo ndiyo unakuwa mwisho wa maisha yake,” nilimjibu Junaitha, nikiwa nimemkodolea macho.

“Huna haja ya kuogopa kuhusu kifo kwa sababu kinachotokea inakuwa ni kuhama tu kutoka kwenye ulimwengu mmoja kwenda kwenye ulimwengu mwingine, ni kama hivi tu sisi tunavyofanya lakini tofauti yake ukifa unakuwa huwezi kurudia kwenye mwili wako lakini hakuna tofauti sana.”

“Sijakuelewa.”

“Utanielewa tu wala usiwe na haraka, sitaki kabisa kusikia ukiogopa kuhusu kifo, umenielewa?”

“Nitaachaje kuogopa Junaitha?”

“Sasa unaogopa nini? Mbona huogopi tunavyohama kutoka ulimwengu mmoja kwenda mwingine?” alisema Junaitha lakini bado alichokuwa anakisema hakikuingia kabisa akilini mwangu.

“Hebu tuachane na haya mambo kwanza, tuna kazi kubwa mbele yetu,” alisema, akanibusu mdomoni, nikashusha pumzi ndefu na kuinuka pale tulipokuwa tumelala, naye akainuka, tukatoka na kuelekea kwenye chumba alichokuwa amelala Shenaiza.

“Hebu niambie ukweli, hujawahi kufanya mapenzi na huyu msichana kweli?” Junaitha aliniuliza, akimaanisha Shenaiza, nikamjibu kwa kutingisha tu kichwa.

“Hebu nitazame usoni,” alisema Junaitha lakini sikutaka kumtazama kwa sababu ambazo nazijua mwenyewe.

“Kwa nini tusimalize kazi kwanza halafu hayo mengine yatafuata baadaye?” nilisema huku nikionesha kutofurahishwa na swali lake, ilivoonesha naye hakutaka kuniudhi kwani alibadilisha mada haraka.

“Simama kwa kule,” aliniambia, akinioneshea upande uliokuwa na miguu ya Shenaiza, nikafanya kama alivyoniambia. Yeye alisimama upande wa kichwani kwa msichana huyo, akapiga magoti na kunitaka na mimi nifanye hivyohivyo.

“Katika vidole vyako kumi vya mikono, nataka kila kimoja kiguse kidole cha Shenaiza na ushikilie hivyohivyo, usiachie,” aliniambia, nikafanya kama alivyoniambia. Kweli nilishika vidole vyote vya Shenaiza, nikawa namtazama Junaitha kusubiri maelekezo zaidi.

“Fumba macho,” alisema Junaitha na kusisitiza kwamba nisimuachie vidole wala nisifumbue macho, nikamsikia akianza kuongea maneno ambayo hata sijui ni ya lugha gani au yalikuwa yakimaanisha nini, akaendelea kuyarudiarudia na kadiri alivyokuwa anazidi kuongea ndivyo sauti yake ilivyoanza kuwa ya kutisha, ikawa inasikika kama ile aliyoitoa kule kwenye ulimwengu mwingine ambayo ama kwa hakika ilikuwa ikitisha.

Nilianza kuhisi vitu kama upepo mkali ukivuma mle ndani, sikuelewa umetokea wapi, ukabadilisha na kuanza kuwa kama kimbunga kikali, vitu vikawa vinapeperushwa huku na kule. Upepo ulizidi kuwa mkali, Junaitha naye aliendelea kuyarudiarudia maneno yake kwa ukali, mara ikaanza kusikika miungurumo ya ajabu mle ndani, ikafuatiwa na radi kubwa iliyopiga kwa nguvu kubwa mno, nilijikuta nikipoteza mwelekeo, nikarushwa mpaka ukutani, nikajibamiza na kudondoka chini.

Ninachoshukuru ni kwamba sikufumbua macho kama Junaitha alivyoniambia, nikajikuta nimepoteza fahamu, nikawa sielewi kinachoendelea.

“Wewe ni nani?”

“Na wewe ni nani?” nilijikuta nikirejewa na fahamu lakini nusunusu, jitu kubwa ambalo sikuweza kuona mwisho wake, lilikuwa limesimama mbele yangu, likiniuliza kwa sauti nzito. Cha ajabu, eti wala sikuogopa chochote na badala ya kujibu, na mimi nikaliuliza swali.

“Kwa nini mnaingilia mambo yasiyowahusu? Mnamjua huyu binti? Kwa nini mnataka kumsaidia?”

“Na nyie kwa nini mnamtesa? Si ameshawaambia hataki kushirikiana nanyi?”

“Wewe ndiyo unamsemea? Kwa nini asiseme mwenyewe?”

“Nasema mwenyewe sasa, sitaki kushirikiana na nyie, Jamal nisaidie baba?” sauti ambayo niliitambua vyema kwamba ni ya Shenaiza ilisikika lakini nilipogeuka huku na kule, sikumuona zaidi ya lile jitu.

“Unasemaje wewe?”

“Nimesema sitaki kushirikiana na nyie, niacheni na maisha yangu,” sauti ya Shenaiza ilisikika tena, ghafla ikasikika tena radi kali ambayo safari hii niliona kama imepiga jirani kabisa na pale nilipokuwa.

Fahamu zikanirudia vizuri, nikajikuta nimelala sakafuni, huku Shenaiza akipiga kelele kwa nguvu pale kitandani, Junaitha akikazana kumtuliza.

“Njoo unisaidie Jamal, inuka njoo,” alisema Junaitha, nikainuka pale sakafuni kwa kujikongoja, nikasogea pale nilipokuwa nimesimama awali, Junaitha akaniambia nimshikilie Shenaiza ambaye alikuwa akirusha miguu na kutapatapa.

“Tulia Shenaiza, kila kitu kitakuwa sawa,” alisema Junaitha, msichana huyo ambaye muda wote alikuwa amefumba macho, alifumbua na ghafla akawa ni kama amezinduka, macho yake yakatua kwangu.

“Jamal!”

“Shenaiza.”

“Hapa ni wapi na nimefikaje?”

“Ooh! Ahsante kazi imekamilika,” alisema Junaitha huku akimuachia Shenaiza, akawa anajifuta jasho jingi lililokuwa linamtoka.

“Na huyu ni nani?”

“Tulia Shenaiza, kwanza pole kwa yote yaliyokutokea, pumzika kwanza utajua kila kitu,” nilimwambia, akawa bado ni kama ana mawenge, akawa ananitazama mimi, anamtazama Junaitha, anakitazama kile chumba, anajitazama yeye mwenyewe katika namna ya kushangaa sana.

“Inabidi nikamuogeshee maji ya maiti, amka binti,” alisema Junaitha na kumshika mkono Shenaiza ambaye bado alikuwa ameduwaa. Kiukweli hata mimi nilikuwa na maswali mengi sana lakini ilibidi nijikaze ili Shenaiza atulie. Nilishangaa kwamba iweje ndani ya muda mfupi tu namna hiyo, kutokee mambo ya kutisha kiasi kile mle ndani halafu watu waliopo nje wasijue chochote?

Nini kimefanyika mpaka Shenaiza ambaye kwa siku kadhaa alikuwa amepoteza kabisa fahamu, leo arudiwe na fahamu zake kama hakuna kilichotokea? Wanaosema uchawi haupo, nawapa pole. Uchawi upo na una nguvu kwelikweli.

“Njoo kwanza Jamal,” alisema Shenaiza baada ya kuwa ameshasimama kwa msaada wa Junaitha, mwili wake ukiwa hauna nguvu kabisa. Nilimsogelea, akanikumbatia kwa nguvu na kunibusu mdomoni, tukio ambalo Junaitha alilishuhudia ‘laivu’.

“Nakupenda sana, naamini wewe ndiyo umeyapigania maisha yangu mpaka muda huu,” alisema, nikamuona Junaitha akimshika mkono bila kusema kitu na kuanza kumvuta kuelekea bafuni.

Mate ya Shenaiza yalikuwa machungu kuliko klorokwin, nikawa najikaza tu huku nikijitahidi kuachia tabasamu kwenye uso wangu. Junaitha alimkokota mpaka bafuni na kufunga mlango kwa ndani, nikabaki nimesimama pale koridoni.

Ghafla nikaanza kusikia sauti ya Firyaal akilia kama mtu anayekabwa na kitu, nikakurupuka mpaka kwenye kile chumba walichokuwa wamelala wote, nikafunga breki za ghafla mlangoni, nikiwa siamini kile nilichokuwa nakiona.

Je, nini kitaendelea? Usikose next issue.
 
Jamani inamaana friyaal ndo anakufa badala ya dada yake?
 
Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 60
ILIPOISHIA:
Junaitha alimkokota mpaka bafuni na kufunga mlango kwa ndani, nikabaki nimesimama pale koridoni. Ghafla nikaanza kusikia sauti ya Firyaal akilia kama mtu anayekabwa na kitu, nikakurupuka mpaka kwenye kile chumba walichokuwa wamelala wote, nikafunga breki za ghafla mlangoni, nikiwa siamini kile nilichokuwa nakiona.
SASA ENDELEA...

Firyaal alikuwa amejikaba shingoni kwa kutumia mikono yake miwili, macho yakiwa yamemtoka pima, akikoroma kama mtu anayeelekea kukata roho. Sikuwahi kusikia hata mara moja kama kuna mtu amewahi kufanikiwa kuyakatisha maisha yake kwa kujikaba mwenyewe lakini kwa Firyaal ilionesha kama hilo linaweza kutokea muda wowote.
Kwa kasi ya ajabu nilisukuma mlango na kwenda kumkamata Firyaal, kwa jinsi alivyokuwa na mwili ‘teketeke’, niliamini itakuwa rahisi kwangu kumtoa ile mikono yake shingoni lakini kumbe nilikuwa najidanganya.
Nilishangaa nilipomgusa Firyaal kukuta mwili wake umekakamaa na kuwa mgumu kama mti, nikaanza kuhaha kujaribu kumnasua bila mafanikio, aliendelea kukoroma huku wenzake wakiwa wamelala fofofo.
Ilibidi nitoke na kumkimbilia Junaitha ambaye muda mfupi baadaye naye alikuja na kushuhudia kile kilichokuwa kikiendelea.
“Umemfanya nini?”
“Sijui chochote, mi nimemkuta tu anajikaba,” nilisema, akamsogelea kwa hatua za harakaharaka na katika hali ambayo sikuitegemea, nilishangaa kumuona akimzibua kibao cha nguvu upande wa kushoto, akahamia upande wa kulia, akamzibua kwa nguvu zaidi!
“Utamuumiza?”
“Hapa ndiyo namsaidia, nyamaza?” Junaitha alinifokea, akamuongeza kibao kingine cha upande wa kushoto, nikafumba macho kwani sikutaka kuona jinsi msichana huyo mrembo alivyokuwa akiadhibiwa.
“Eeeh! Hapa ni wapi? Jamal, Jamal,” sauti ya Firyaal iliyokuwa inatoka kwa kukoroma, ndiyo iliyonifanya nifumbue macho, nikashangaa kumuona akiwa amefumbua macho, akijishangaa yeye mwenyewe na kutushangaa sote mle ndani.
“Firyaal,” nilisema huku nikisimama, na yeye akajikongoja na kusimama, tukawa tunataka kwenda kukumbatiana lakini Junaitha alitukataza, akasema Firyaal amevamiwa na pepo wachafu kwa hiyo lazima asafishwe kwanza ndiyo tutakaporuhusiwa kugusana naye.
Maelezo yale yalinishtua sana, nikakumbuka kauli ya Junaitha kwamba lazima kuna mmoja wetu atapoteza maisha kama kafara, nikawa nasali moyoni kwamba asiwe Firyaal kwa sababu nilimuona kama mrembo sana, tena binti mbichi ambaye alikuwa tayari kunipa zawadi ya kuwa mwanaume wake wa kwanza, kama ilivyokuwa kwa Raya.
“Nakuomba msaidie,” nilimwambia Junaitha, akanitazama tu usoni bila kunijibu chochote. Tukiwa tunatazamana, mara tulishtuka kumuona Shenaiza akiingia ndani ya kile chumba akiwa amejifunga taulo tu, naye akapigwa na butwaa kumuona mdogo wake, Firyaal naye akashtuka mno kumuona dada yake akiwa amesimama, wote tukawa tunashangaana, ukimya ukapita kati yetu.
“Naombeni mnisikilize kwa makini, tumefikia hatua nzuri sana lakini kama tusipokuwa makini, tutasababisha matatizo makubwa zaidi, Jamal shughulika na Shenaiza, mimi ngoja nikamalizane na Firyaal, angalizo! Hamtakiwi kugusana kwa sasa,” alisema Junaitha, nikatingisha kichwa kuonesha kukubaliana naye.
“Bado sielewi Jamal, mdogo wangu amefikaje huku halafu mbona kama hayupo sawa?”
“Shenaiza, tulikotoka ni mbali sana kuliko tunakoelekea, amini kila kitu kitakuwa sawa kabisa, twende,” nilisema kwa sauti iliyojaa matumaini makubwa ingawa ukweli hata mimi nilikuwa sijui mwisho wa sarakasi zote zile ungekuwa nini.
Kama alivyosema Junaitha, sikutakiwa kumgusa Shenaiza ingawa mwenyewe alionesha kuwa na shauku kubwa ya kutaka tukumbatiane, tukaongozana mpaka chumbani kwake. Kwa kuwa siku zote hizo hakuwa na fahamu, hata chumba chake kilikuwa kizito mno, tulipoingia tu mwenyewe ndiyo alikuwa wa kwanza kuligundua hilo.
“Mbona humu ndani hewa nzito sana?” alisema, sikumjibu chochote zaidi ya kumsaidia kufungua madirisha na kuwasha feni, yeye akakaa kwenye kiti kilichokuwa pembeni ya kitanda, akiendelea kunitazama kama anayetamani kuzungumza jambo na mimi.
“Unajua bado najihisi kama nipo kwenye ndoto, kumbukumbu zangu zinarudi taratibu sana kichwani.”
“Usiwe na wasiwasi, kila kitu kitakuwa sawa.”
“Wewe si ulikuwa unaumwa hoi hospitalini?” aliniuliza, nikatingisha kichwa huku nikifungua vifungo vya shati langu, nikamuonesha jeraha akubwa lililokuwa kifuani ambalo sasa lilikuwa limepona na kubakiza ganda la juu kubanduka ili lipone kabisa na kuacha kovu, akapigwa na butwaa.
“Mh! Kwa hiyo nilipoteza fahamu kwa muda mrefu kiasi hicho mpaka umepona?”
“Ni stori ndefu Shenaiza, hebu tuliza kwanza kichwa chako, nimeshakwambia kila kitu kitakuwa sawa.
“Sasa ulitokaje hospitalini na mimi nilitokaje? Yule daktari aliyekuwa akinichoma sindano za kwenye mishipa alikuwa akichanganya na nini mbona zilikuwa zikiuma sana halafu nikawa nalala sana baada ya kuchomwa?”
“Jamani Shenaiza, si nimekwambia nitakueleza kila kitu? Kuwa mpole,” nilimwambia. Kwa kuwa shuka lililokuwa limetandikwa pale kitandani lilikuwa limechafuka, ilibidi nifungue kabati na kuchukua jingine safi, nikabadilisha na kumwambia apumzike kitandani.
Kweli alifanya hivyo lakini akataka na mimi nilale naye pale kitandani, jambo ambalo sikukubaliana naye, nikamwambia ni lazima tufuate masharti kwa sababu tulikuwa kwenye kipindi kigumu. Kweli alijilaza pale kitandani kihasarahasara, mimi nikakaa pale alipokuwa amekaa yeye.
Bado alikuwa na maswali mengi lakini niliendelea kumkatisha na kumtaka apumzike. Kutokana na jinsi alivyokuwa amechoka, hazikupita dakika tatu, akapitiwa na usingizi mzito.
Muda mfupi baadaye, Junaitha alirejea akiwa na Firyaal ambaye sasa alionesha kurudi kwenye hali yake ya kawaida.
“Kwa nini umemruhusu huyo alale tena wakati hajala chochote? Hebu muamshe, anaweza kupitiliza tena akatupa kazi ya ziada,” alisema Junaitha na hakusubiri mimi nifanye kazi hiyo, alimsogelea mwenyewe pale kitandani na kuanza kumtingisha.
Shenaiza akakurupuka usingizini na kukaa kitako, macho yake yakatua kwa mdogo wake, safari hii Junaitha aliwaruhusu wakumbatiane, wakafanya hivyo na kila mmoja wao akaanza kuangua kilio kwa sauti ya juu mithili ya watu waliopokea taarifa za msiba.
Cha ajabu, walipokumbatiana na kuanza kulia tu, mvua kubwa ilianza kunyesha ghafla, akina Raya na Shamila waliokuwa usingizini nao wakazinduka na kuja mbiombio kwenye kile chumba tulichokuwemo, yule mwanamke wa ajabu aliyekuwa amefungiwa naye akaanza kunguruma kwa sauti kubwa.
Kila kitu kilibadilika kwa kasi kubwa mno, mvua kubwa ikaendelea kumwagika, huku wingu kubwa jeusi likitanda kila kona na kuimeza kabisa nuru iliyokuwepo, ungeweza kudhani tayari ni usiku.
“Kuna kitu kinataka kutokea siyo kizuri, hebu nifuateni haraka,” alisema Junaitha, wote tukakurupuka na kusimama, tukatoka na kuanza kumfuata Junaitha, tukiwa hatuelewi tunaenda wapi.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.
 
Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 61
ILIPOISHIA:
Kila kitu kilibadilika kwa kasi kubwa mno, mvua kubwa ikaendelea kumwagika, huku wingu kubwa jeusi likitanda kila kona na kuimeza kabisa nuru iliyokuwepo, ungeweza kudhani tayari ni usiku.
“Kuna kitu kinataka kutokea siyo kizuri, hebu nifuateni haraka,” alisema Junaitha, wote tukakurupuka na kusimama, tukatoka na kuanza kumfuata Junaitha, tukiwa hatuelewi tunaenda wapi.
SASA ENDELEA...

Kila kitu kilibadilika kwa kasi kubwa mno, mvua kubwa ikaendelea kumwagika, huku wingu kubwa jeusi likitanda kila kona na kuimeza kabisa nuru iliyokuwepo, ungeweza kudhani tayari ni usiku.
“Kuna kitu kinataka kutokea siyo kizuri, hebu nifuateni haraka,” alisema Junaitha, wote tukakurupuka na kusimama, tukatoka na kuanza kumfuata Junaitha, tukiwa hatuelewi tunaenda wapi.
“Asibaki mtu nyuma, kuweni makini,” alisisitiza Junaitha huku akipiga hatua za harakaharaka, tukazidi kuelekea ndani ya nyumba hiyo, tukafika mpaka sehemu kulipokuwa na korido nyembamba, tukaenda mpaka mwisho wa korido ambako hakukuwa na mlango wala sehemu ya kupita, nikawa sielewi lengo la Junaitha.
“Leso trebos replicas nimbus,” alisema Junaitha na kutuambia na sisi tumfuatishe maneno hayo mara saba kwa kasi, tukaanza kurudia maneno hayo ambayo hakuna aliyeyajua maana yake zaidi ya yeye mwenyewe.
Cha ajabu, tuliporudia kwa mara ya saba, lile eneo ambalo tuliona kama ni ukuta, lilibadilika na kuwa mlango, ukajifungua ambapo alituelekeza kwamba tunatakiwa kuingia kinyumenyume, akaanza yeye huku akituhimiza kufanya haraka kuingia.
Tulipoingia wote, alitamka maneno fulani ambayo hakuna aliyeelewa maana yake, pale palipokuwa na mlango pakajifunga, kule ndani giza likatanda kila sehemu. Hakuna ambaye aliweza hata kumuona mwenzake aliyekuwa naye sentimita kadhaa tu pembeni.
Bado tuliweza kusikia ngurumo za radi na upepo mkubwa vilivyokuwa vikiendelea kusikika, kuonesha kwamba mvua ilikuwa ikiendelea kunyesha. Nikasikia vishindo vya Junaitha na muda mfupi baadaye, tukasikia akiwasha swichi ya ukutani, taa ikawaka, kila mtu akawa anageuka huku na kule kutazama vizuri mandhari ya pale tulipokuwepo.
Kilikuwa ni chumba kikubwa ambacho kwa ilivyoonesha, ni kama kilikuwa sebule ambayo haijatumika kwa miaka mingi iliyopita, ‘matandabui’ yalikuwa yametapakaa kila sehemu, mpaka kwenye ile taa ambayo nayo ilikuwa na mwanga hafifu kutokana na kuzingirwa na vumbi pamoja na matandabui.
Pembeni kulikuwa na samani za kale, makochi ya kizamani, meza ya mbao, kabati dogo lililokuwa na vyombo vichache vya udongo. Kila kitu ndani ya sebule hiyo kilikuwa cha kizamani, vumbi na matandabui vikazidi kupafanya pawe na mwonekano wa kutisha sana.
“Kaeni hapo mtulie kimya, asiondoke yeyote kati yenu,” alisema Junaitha na kufumba na kufumbua, tulishangaa tu ameyeyuka, hakuna aliyejua ameenda wapi.
“Kwani kuna nini kinaendelea jamani? Mbona sielewi?”
“Tumeambiwa tutulie,” nilimjibu Raya ambaye alionesha kuwa na shauku kubwa ya kutaka kujua nini kimetokea. Muda mfupi baadaye, ile taa ilizimika, giza likawa nene kuliko hata mwanzo. Hakuna aliyemsemesha mwenzake, kila mmoja alikuwa kimya kabisa.
Ukimya ulikuja kukatishwa na kelele za mlango uliokuwa ukifunguliwa, Junaitha akaingia na kwenda kuwasha tena taa, wote tukashangaa akiwa amelowa chapachapa na mwili wake kubadilika rangi na kuwa mweusi. Hata maji yaliyokuwa yakichuruzika kwenye mwili wake yalikuwa meusi mithili ya mtu aliyeogea maji ya mkaa.
Cha ajabu, zile ngurumo za radi hazikusikika tena, kukawa kimya kabisa.
“Twendeni,” alisema Junaitha huku akitetemeka kutokana na kulowana, harakaharaka wote tukainuka na kuelekea kwenye ule mlango, tukatoka na Junaitha akawa wa mwisho kutoka. Alipotoka tu, ule mlango nao ulipotea, eneo lote likawa kama lilivyokuwa mwanzo, ukuta.
“Washenzi sana hawa, kazi imekwisha sasa,” alisema Junaitha huku akigeuka na kumtazama Shenaiza ambaye muda wote alikuwa kimya kabisa, kama hayupo.
“Vipi unajisikiaje?”
“Najisikia vizuri lakini bado nina maswali mengi.”
“Hayo mambo ya maswali achana nayo. Jamal wewe kuna waandishi wa habari unaofahamiana nao?”
“Waandishi wa habari? Wa nini tena?”
“Hili suala tunaelekea kulimaliza lakini polisi wa nchi hii nawajua, tunaweza kuwapa ushahidi wote lakini bado wakashirikiana na wahalifu kubadilisha ukweli kuwa uongo kwa hiyo nimewaza kwamba ni bora tuwe na mwandishi wa habari mmoja na mwanasheria mmoja, siku chache zijazo nchi yote hii itatingishika,” alisema Junaitha.
Cha ajabu, Firyaal na Shenaiza ambaye mtuhumiwa mkuu tuliyekuwa tukihangaika kuhakikisha anafikishwa mbele ya sheria ambaye ni baba yao mzazi, walionesha kufurahishwa zaidi na taarifa hizo, wakatazamana na kuachia tabasamu kisha wakawa ni kama wanapeana ishara fulani.
Junaitha alituongoza mpaka sebuleni, kila mtu akawa na shauku ya kuchungulia nje kwani hali ya hewa ilikuwa imebadilika na kurudi kama mwanzo, yaani usingeweza kudhani kwamba muda mfupi uliopita hali ilikuwa tete.
Mimi ndiyo nilikuwa wa kwanza kusimama na kwenda mpaka dirishani, nikafungua pazia na kuchungulia nje. Cha ajabu, hakukuwa na dalili zozote za mvua, nikapigwa na butwaa nikiwa ni kama siamini. Nilifikicha macho yangu nikihisi huenda nilikuwa ndotoni lakini haikuwa hivyo; hakukuwa na dalili yoyote ya mvua kunyesha na jua lilikuwa likiwaka.
Niligeuka na kuwatazama Shamila, Raya, Firyaal na Shenaiza ambao ni kama walikuwa wakisubiri nitawajibu nini, nikatingisha tu kichwa, hali iliyowafanya wainuke haraka na kuja pale dirishani, nao wakapigwa na butwaa kwani hakukuwa na dalili zozote za mvua.
“Kwani mama’ako mdogo ni mchawi?” Raya alimuuliza Shamila lakini kabla hajajibu, Junaitha akaingilia kati.
“Ndiyo, mimi ni mchawi, hata wewe ni mchawi ndiyo maana upo hapa, unafikiri umefika kwa bahati mbaya hapa?” alijibu Junaitha ambaye tayari alishabadilisha nguo na kuvua zile zilizokuwa zimelowa ingawa bado mwili wake ulikuwa mweusi sana.
“Haya njooni huku kila mtu aulize maswali yote aliyonayo, nipo tayari kuwajibu kwa sababu kesho ndiyo siku ya kuhitimisha kila kitu kilichokuwa kikiendelea,” alisema Junaitha, wote tukainuka na kuanza kumfuata, mimi ndiyo nilikuwa nyuma kabisa, nikamuona Shamila akipunguza mwendo kwa makusudi, wote wakapita, tukabaki wawili tu nyuma, akageuka na kunitazama usoni, macho yetu yakagongana.
“Nashindwa kujizuia mpenzi wangu.”
“Vipi tena Shamila.”
“Nimekumisi mpenzi wangu.”
“Lakini si tupo pamoja mama?”
“Ndiyo, lakini mambo yenyewe ndiyo kama hivi, hatupati hata dakika chache za kuwa pamoja, mi nimechoka bwana,” alisema Shamila na kunisogelea mwilini, nikawa naiona hatari iliyokuwa mbele yetu endapo Junaitha atageuka na kugundua kwamba tulibaki koridoni tumesimama, tena tukiwa tumesogeleana mithili ya majogoo yanayotaka kupigana.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.
 
Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 62
ILIPOISHIA:
“Ndiyo, lakini mambo yenyewe ndiyo kama hivi, hatupati hata dakika chache za kuwa pamoja, mi nimechoka bwana,” alisema Shamila na kunisogelea mwilini, nikawa naiona hatari iliyokuwa mbele yetu endapo Junaitha atageuka na kugundua kwamba tulibaki koridoni tumesimama, tena tukiwa tumesogeleana mithili ya majogoo yanayotaka kupigana.
SASA ENDELEA...

“Please Shamila, huu siyo muda muafaka, kama inawezekana tutafute muda baadaye,” nilisema kwa sauti ya chini, akashusha pumzi ndefu na kunitazama usoni kwa macho yake mazuri, tukaendelea kutembea lakini alionesha kweli amemaanisha kile alichokisema.
Tuliingia kwenye kile chumba ambacho tulikuwa tukikutania kila panapokuwa na shughuli maalum, Junaitha akatuelekeza kukaa kwa duara kama ilivyokuwa kawaida yetu kisha akatuambia wote tuanze kuvuta hewa kwa wingi kwa kutumia pua na kuitoa kwa kutumia mdomo.
“Inatakiwa wote tufumbe macho na tuendelee kupumua taratibu, vuta pumzi ndefu kwa kutumia tumbo na sio kifua, unajua kuna watu wengi wanaishi lakini hawajui hata namna ya kupumua, badala yake wao wanahema,” alisema Junaitha na kuanza kutufafanulia kile alichokisema.
Alisema kwa kawaida, unapovuta pumzi inatakiwa hewa iende kujaa kwenye mapafu, ambayo kimsingi yanapatikana chini ya mfupa wa chini wa kifua kwa ndani au kwa Kiingereza diaphragm.
“Unapovuta hewa kwa kutumia kifua, maana yake haifiki kwenye mapafu kama inavyotakiwa na unapoitoa, inakuwa imeishia njiani na kama mjuavyo pumzi ndiyo uhai wenyewe kwa hiyo mtu ambaye hapumui vizuri hawezi kuwa na afya nzuri ya mwili au akili.
“Nataka na nyie mjifunze kuanzia leo, unapopumua tumia tumbo, unapovuta hewa hakikisha tumbo limejaa na unapotoa hakikisha linabaki tupu, hapo ndiyo utakuwa na uhakika kwamba pumzi zimefika sehemu husika na hewa imefika kwenye mapafu,” alisema Junaitha, elimu ambayo awali sikuwa naifahamu.
“Unapotulia kwenye hali hii kwa muda, huku ukiizuia akili yako kufikiria kitu kingine chochote zaidi ya pumzi unazovuta na kutoa, utapata utulivu mkubwa mno wa akili na mwili na hiki ndicho wengine wanachokiita tahajudi au meditation, sasa kabla sijaruhusu maswali nataka wote tufanye kwa dakika kadhaa, nataka wote tufumbe macho na tutaendelea kupumua kwa utulivu mpaka nitakapowapa ishara,” alisema Junaitha, wote tukatii alichotuambia.
Kiukweli kwa upande wangu, nilipoanza kutuliza akili tu, nilijisikia hali ambayo haijawahi kutokea maishani mwangu. Akili yangu ilitulia, mwili nao ukatulia, nikawa najihisi kama nipo kwenye ulimwengu mwingine wa tofauti kabisa. Niliendelea kuifurahia hali hiyo, nikajikuta nikisahau kila kitu, ikafika kipindi nikawa hata sijui pale nipo wapi na nafanya nini, nikawa najisikia raha tu.
Ni mpaka Junaitha alipopiga makofi na kutuambia kwamba inatosha ndipo akili zangu ziliporudi mahali pake, nikagundua kumbe nilikuwa nimekaa juu ya zulia, nikawa najishangaa sana.
“Enhee! Mmejisikiaje?” aliuliza Junaitha, mimi ndiyo nikawa wa kwanza kumjibu kwamba nimejisikia vizuri sana, wenzangu wote nao walijibu hivyohivyo, tukamshukuru Junaitha kwa kutufundisha kitu kizuri namna ile.
“Kwa hiyo mmeanza kuona kwamba kumbe kila mmoja wetu ana nguvu fulani ndani ya mwili wake ingawa wengi hawajui namna ya kuzitumia na ukionesha kujua kidogo ndiyo kila mtu anakuona wewe ni mchawi, hata nyie si mnaamini mimi ni mchawi sana si ndiyo?” alisema Junaitha, akaanza kututolea ufafanuzi kama ule alionipa awali.
Akatuambia kwamba baba yake mzazi alikuwa na nguvu za giza na ndiye aliyemrithisha lakini wakati anarithishwa, tayari na yeye alikuwa ameshaanza mafunzo ya elimu ya utambuzi, ambayo yalimfanya awe na uwezo mkubwa wa kutumia nguvu zisizoonekana.
Kwa jinsi alivyokuwa anajua kujieleza, tulijikuta wote tukiishiwa maswali, Shenaiza yeye akataka kujua kuhusu hali yake aliyokuwa nayo na nini kilichotokea mpaka alipojikuta pale ndani.
Kwa kuwa Junaitha alikuwa ametoa mwenyewe ruhusa ya kuulizwa maswali, alimfafanulia kila kitu, akamueleza mpaka jinsi tulivyoenda kumtorosha Shamila hospitalini baada ya kuwa anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kunitorosha mimi na Shenaiza hospitalini, kwa kushirikiana na Raya na Firyaal.
Mazungumzo yalikuwa marefu lakini mwisho wa yote, Junaitha alituhakikishia kwamba kesho yake ndiyo ingekuwa mwisho wa baba yao akina Shenaiza na shirika lake la kishetani la Black Heart.
“Leo mnajiona kama watu wadogo lakini nawahakikishieni kesho kila mtu atawaona mashujaa kwa kuibua sakata hili,” alisema Junaitha na kutusisitiza kwamba inatakiwa tupambane pamoja maana mzee huyo alikuwa na nguvu kubwa ambazo angeweza kuzitumia kutushinda.
“Kinachonifanya niamini kwamba tutamzidi nguvu ni kwa sababu kwanza mchawi wake yupo mikononi mwetu tunamshikilia na huyo ndiyo alikuwa akimpa jeuri kwa kipindi chote kwa hiyo sasa hivi atabaki kuwa na nguvu za nje tu lakini nguvu za giza hakuna kitu,” alisema Junaitha.
Suala la kuwa na mwandishi wa habari mmoja pamoja na mwanasheria tayari lilishatimia kwa sababu nilimuunganisha na mwandishi mahiri wa habari za uchunguzi, Richard Bukos na kwa kuwa yeye alikuwa akifahamiana na mwanasheria, basi kazi haikuwa ngumu.
Baada ya hapo, alituruhusu kila mmoja akapumzike kwa ajili ya kujiandaa kwa shughuli ya kesho, huku akinitaka mimi nibaki mle ndani ya kile chumba kwanza. Nilimuona Shamila ni kama hajaifurahia kauli hiyo kwa sababu tayari alishanionesha kwamba ananihitaji, nikamkonyeza kama ishara ya kumwambia asiwe na wasiwasi, tutapata tu muda wa kuwa pamoja.
“Unajua kazi kubwa tumeshaikamilisha kwa hiyo huu ni muda mzuri wa mimi na wewe kupumzika, natangulia chumbani kwangu nakuomba uje lakini hakikisha hakuna anayekuona ukiingia,” alisema Junaitha, nikatingisha kichwa kumkubalia. Nilikubali tu japokuwa nilikuwa najua anachokihitaji na japokuwa haikuwa sahihi kufanya vile, nilijikuta tu na mimi nikipenda kuwa karibu naye kwani niliamini nitajifunza mambo mengi zaidi nikiwa naye.
Nilisimama na kuelekea kwenye chumba changu, nikawapita Firyaal na Shenaiza ambao wao walikuwa kwenye chumba kimoja, nikawasikia wakizungumza kwa furaha ndani ya chumba chao, wakinitaja jina langu.
Nilipita pia kwenye chumba alichokuwemo Raya, yeye alikuwa kimya kabisa, nikapita kwenye mlango wa chumba cha Shamila kwa sababu cha kwangu kilikuwa mwishomwisho, nikashangaa kumuona Shamila amesimama mlangoni.
Aliponiona tu, alinivamia, akanivutia ndani ya chumba chake na kufunga mlango kwa ndani, akanikumbatia huku akipumua kama mtu aliyetoka kukimbia mbio za marathon.
“Nakupenda sana Jamal, njoo uutibu moyo wangu,” alisema huku akinimwagia mvua ya mabusu. Kwa hali aliyokuwa nayo, hakukuwa na njia ambayo ningeweza kumkwepa tena, hasa ukizingatia kwamba hata mimi nilikuwa nampenda kutokana na jinsi alivyonisaidia, kuanzia kule hospitalini mpaka muda huo na pia kutokana na jinsi alivyokuwa mzuri.
Sikujivunga, na mimi nilimuonesha ushirikiano wa nguvu, muda mfupi baadaye tukagusanisha ndimi na kuanza kuelewa kwenye ulimwengu wa tofauti kabisa. Shamila alionesha kuwa na papara mno, muda mfupi baadaye akawa tayari yupo kama alivyoletwa duniani, akahamia upande wangu na kuanza kufanya kama alivyofanya kwake.
Muda mfupi baadaye, wote tulikuwa ‘saresare maua’, akanisukuma kwa nguvu kwenye uwanja wa fundi seremala, nikaangukia mgongo, akaja juu yangu kwa kasi, maandalizi ya mechi ya kirafiki isiyo na jezi wala refa yakaendelea huku akionesha kunikamia kama Simba na Yanga zinavyokamiana zinapokutana uwanjani.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.
 
Jamani samahanini kwa hicho nilichokifanya hapo juu mi mwenyewe cjakipenda kwa kweli daah!! Yaani uzi mzima kweli sijafanya vizuri kabisa roho imeniuma kwa kweli
 
Jamani samahanini kwa hicho nilichokifanya hapo juu mi mwenyewe cjakipenda kwa kweli daah!! Yaani uzi mzima kweli sijafanya vizuri kabisa roho imeniuma kwa kweli
Bado una nafasi ya kuufuta na kuacha jina la alie post tu.
 
Back
Top Bottom