DOKEZO Singida: Barabara ya Unyakumi yaanza kurekebishwa baada ya malalamiko kuwa inawatesa watumiaji

DOKEZO Singida: Barabara ya Unyakumi yaanza kurekebishwa baada ya malalamiko kuwa inawatesa watumiaji

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
WhatsApp Image 2025-02-02 at 17.17.08_5376825e.jpg

WhatsApp Image 2025-02-02 at 17.17.08_4be49443.jpg

WhatsApp Image 2025-02-02 at 17.17.09_d77fb01b.jpg
Siku chache baada ya Mwanachama wa JamiiForums.com kueleza kuwa Wakazi wa Mtaa wa Ginery maeneo ya Singida Sekondari wamekuwa wakiteseka kwa kuwa na Barabara mbovu, Barabara hiyo imeanza kufanyiwa maboresho.

Januari 30, 2025, Mwanachama huyo alisema hali ni mbaya sana hasa msimu huu wa mvua ambapo Watoto wanaenda shule kwa tabu kutokana na maji na matope ya kutosha huku mabasi ya Shule na magari ya binafsi yakipata changamoto kupita.

Alisema kuwa ahadi zimekuwa nyingi bila utekelezaji hivyo akaomba Mamlaka zinazohusika kushughulikia changamoto hiyo.

Jana Februari 2, 2025 Greda lilionekana likipita na kukwangua Barabara hiyo, likafukia mashimo, kunyoosha sehemu zilizokuwa na changamoto na kuondoa visiki kadhaa.

Ilivyokuwa awali, soma hapa ~ Singida: Wakazi wa Unyakumi tunateseka na ubovu wa barabara. Ahadi zimekuwa nyingi bila utekelezaji




 
Back
Top Bottom