Singida Black Stars yawabadilisha Uraia wachezaji wanne wa Kigeni na kuwa raia wa Tanzania ili Kukidhi Kanuni

Malizia naona unasema nusu,robo robo
 
Binafsi huwa nahisi sometimes kwa hizi timu kusajili wachezaji wa kigeni ni kama fashion na ulimbukeni..
Mostly ya hao wachezaji niwakawaida sana.
Wanaweza wakawa a kawaida, ila wakawa na commitment na nidhamu
 
Hii ni hatari kubwa sana kwa Usalama wa Umma.

Je, tangazo la Watu hao kuomba uraia wa Tanzania lilitolewa lini ili kuutaarifu umma? Je, Wananchi wa Tanzania walipewa nafasi ya kuwasilisha Mapingamizi dhidi ya maombi ya uraia ya Watu hao ?
 
Ww mtanzania tafuta passport ya kwenda nje sasa ndo utawajua uhamiaji,,,,lkn kwenye issues za hovyo at mtu anapewa uraia kabisaaa,,,,maajabu hayaishi tz
Na hao jamaa watapewa passport bila usumbufu wowote ule kabla hata ya wazawa walianza kutafuta passport 🛂 tangu mwezi wa 5 mwaka jana.. nchi ya kiseenge sana hii
 
Huyu jamaa kwa sasa nadhani ana nguvu isiyo ya kawaida kwenye hii nchi.
Yeye ndio mtunza kibunda na deals zote lazima zipitie kwake, Abdul mwenyewe akitaka kuchukua Hela lazima apitie kwake...!!

Kwa hiyo lazima awe na nguvu Tena anaitumia bila kuogopa
 
Wana kitu gani special kupewa uraia kwa mwendokasi?
 
Tanzania kuna wachezaji wengi wazuri, tumekosa mfumo wa kuwatambua na kuwaendeleza.
Hatuna uhaba na hili la kuwapa uraia ni kuthibitisha ubutu wetu.
Tanzania ili utoboe ni juhudi zako mwenyewe siyo kupitia mifumo
 
Simba nayo imethibithisha kuwa wachezaji wake 9 wa kigeni wameomba uraia wa Tanzania
 
Unasomaga magazeti?
 
Kuna harufu ya Rushwa hapa. Maana sioni kama vigezo vilitimia:

Kwa mujibu wa Sheria ya Uraia ya Na. 6 ya Mwaka 1995, mtu yeyote anayefuzu kuwa raia wa Tanzania kwa kuzaliwa ni yule aliyezaliwa nchini Tanzania na ambaye wakati wa kuzaliwa kwake mmoja wa mzazi wake alikuwa raia wa Tanzania.
Uraia wa Tanzania kwa Kurithi

Mtu yeyote aliyezaliwa nje ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania siku ya Muungano au baada ya Muungano anahesabika kuwa raia wa Tanzania kwa kurithi kuanzia tarehe ya kuzaliwa kwake kama siku ya kuzaliwa kwake mama au baba yake ni raia wa Jamhuri ya Muungano kwa kuzaliwa au tajnisi. Hii ina maana kuwa kama wazazi wake walikuwa ni raia wa Tanzania kwa kurithi wakati wa kuzaliwa kwake mtu huyo hawezi kuwa raia wa Tanzania kwa kurithi.
Uraia wa Tanzania kwa Tajinisi:

Mtu yeyote ambaye siyo raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuzaliwa au kurithi anaweza kuomba uraia wa Tanzania kwa tajnisi kwa mujibu wa vifungu Na.8 na 9(1) vya Sheria ya Uraia ya 1995. Kwa mujibu wa Sheria hiyo, Mhe. Waziri mwenye dhamana ya kusimamia masuala ya uraia nchini (kwa sasa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi) ndiye mwenye mamlaka ya mwisho kutoa au kutotoa uraia wa Tanzania kwa wageni walioomba uraia.
Sifa za Kuomba uraia wa Tajnisi:

Mgeni anayetaka kuomba uraia wa Tanzania anapaswa kuwa na sifa zifuatazo:-

i. Mwombaji awe na umri wa miaka 18 au zaidi na awe na uwezo wa kufanya maamuzi yanayokubalika kwa mujibu wa sheria za nchi

ii. Awe ameishi ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa muda wa miezi 12 mfululizo kabla ya kutuma maombi

iii. Katika muda wa miaka kumi kabla ya miezi kumi na mbili hiyo awe ameishi ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa muda usiopungua miaka saba

iv. Awe anaelewa vizuri lugha ya Kiswahili au Kiingereza

v. Awe na tabia nzuri

vi. Awe alichangia na ataendelea kuchangia katika ukuzaji wa uchumi, Sayansi na teknolojia na utamaduni wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

vii. Awe anakusudia kuishi moja kwa moja ndani ya Jamhuri ya Muungano ikiwa ombi lake la uraia litakubaliwa

Taratibu za kuomba uraia wa Tajnisi

Zifuatazo ni taratibu za kuomba uraia wa tajnisi kwa mgeni ambaye ana umri wa miaka 18 na kuendelea:-

i. Mwombaji anatakiwa kujaza fomu za maombi ya uraia ambazo zinapatikana katika ofisi zote za Uhamiaji za Wilaya, Mikoa na Makao Makuu

ii. Mwombaji anatakiwa kutoa matangazo ya nia yake yakuomba Uraiya mara mbili mfululizo kwenye gazeti lililosajiliwa Tanzania
Tanzania Bara na Zanzibar.

Mchakato wa kushughulikia maombi ya uraia

Ili kuhakikisha kuwa wageni wanaopewa uraia ni wale wenye manufaa kwa Taifa, maombi yote yanapaswa kupitia na kujadiliwa katika vikao vya Kamati za Ulinzi na Usalama vya:-
Ngazi ya Kata au Shehia (kwa upande wa Zanzibar)

Katika ngazi ya Kata au Shehia anayoishi mwombaji atahojiwa na maombi yake kujadiliwa na kikao hicho na hatimaye ombi kupelelekwa kwa Mkuu wa Wilaya kwa hatua zaidi.
Ngazi ya Wilaya

Kikao cha Ulinzi na Usalama cha Wilaya hujadili maombi ya uraia na hatimaye kutoa maoni na mapendekezo yake
Ngazi ya Mkoa

Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa hujadili maombi yaliyowasilishwa na kutoa maoni na mapendekezo yake kuhusiana na ombi husika na hatimaye hutumwa kwa Kamishna Mkuu wa Uhamiaji au kwa Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, ambaye naye hutoa ushauri na mapendekezo kwa Waziri wa Mambo ya Ndani. Waziri wa Mambo ya Ndani ndiye mwenye mamlaka kisheria kutoa Uraia wa Tanzania
 

Attachments

  • 1737696184458.gif
    42 bytes · Views: 1
Kupewa uraia wa nchi maskini hakuna shida yoyote, waafrika ni ndugu ni jamii moja, ni mipaka ya wazungu ilitutenganisha tu.

Shida itakuja pale wakishuka viwango na kuachwa na timu hiyo wataenda wapi kula ugali na sukari maana hawana ukoo bongo!! Au kwa Shem yule mrembo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…