MIXOLOGIST
JF-Expert Member
- Mar 1, 2016
- 14,311
- 36,056
Nikiwa nimejawa na jazba nawakemea watoto wa kiume na wavulana wote wanaodhihaki na kuwa kebehi single mothers.
Ieleweke kwamba, single mother ni mama yake mtu, ni kama alivyo mama yako. Aidha, wanawake hawa ni majasiri, wameamua kutunza uhai , kinyume chake wangetoa mimba na kuwa kama hayo majanamke mengine mauaji (slay queens) ambayo yanaua watoto kwa kutoa mimba na mnayashobokea.
Single mothers, wamefanya kazi ya Mungu, wamelea uhai miezi tisa tumboni na kuleta kiumbe duniani. Kwa kudra za Mwenye-Enzi- Mungu, kiumbe hicho kinaweza kuwa mtu muhimu na kutoa mchango mkubwa kwenye ujenzi wa taifa letu.
Kudhihaki single mothers ni sawa na kuchochea utoaji wa mimba, jambo hili likome mara moja. Waache wakina mama wanaopata mimba walete viumbe duniani. Mungu amesema nendeni duniani mkaijaze dunia, hongereni akina mama mlioamua kulea watoto wenu
Pamoja na hayo niliyoandika hapo juu, single mother ni reflection ya udhaifu wetu wanaume, yaani kuna mpuuzi mmoja ambaye anashindwa au anakataa kutimiza wajibu wake. Uwepo wa single mothers ni aibu kubwa kwetu wanaume, yaani hatufanyi wajibu wetu
Kwa kumalizia, single mothers wanapitia madhila mengi, haswa wale wasio na kipato cha kutosha na cha uhakika,. Hivyo ni rai yangu, kwa wale wababa wenye uwezo tuwatunze single mothers kwa manufaa mapana ya watoto na jamii nzima.
Kwa wale wenye changamoto za afya ya akili, uwanja ni wenu kuja kubisha na kupinga madini haya
Nimetoa uzi huu kama nilivyomuahaidi Demi
Ieleweke kwamba, single mother ni mama yake mtu, ni kama alivyo mama yako. Aidha, wanawake hawa ni majasiri, wameamua kutunza uhai , kinyume chake wangetoa mimba na kuwa kama hayo majanamke mengine mauaji (slay queens) ambayo yanaua watoto kwa kutoa mimba na mnayashobokea.
Single mothers, wamefanya kazi ya Mungu, wamelea uhai miezi tisa tumboni na kuleta kiumbe duniani. Kwa kudra za Mwenye-Enzi- Mungu, kiumbe hicho kinaweza kuwa mtu muhimu na kutoa mchango mkubwa kwenye ujenzi wa taifa letu.
Kudhihaki single mothers ni sawa na kuchochea utoaji wa mimba, jambo hili likome mara moja. Waache wakina mama wanaopata mimba walete viumbe duniani. Mungu amesema nendeni duniani mkaijaze dunia, hongereni akina mama mlioamua kulea watoto wenu
Pamoja na hayo niliyoandika hapo juu, single mother ni reflection ya udhaifu wetu wanaume, yaani kuna mpuuzi mmoja ambaye anashindwa au anakataa kutimiza wajibu wake. Uwepo wa single mothers ni aibu kubwa kwetu wanaume, yaani hatufanyi wajibu wetu
Kwa kumalizia, single mothers wanapitia madhila mengi, haswa wale wasio na kipato cha kutosha na cha uhakika,. Hivyo ni rai yangu, kwa wale wababa wenye uwezo tuwatunze single mothers kwa manufaa mapana ya watoto na jamii nzima.
Kwa wale wenye changamoto za afya ya akili, uwanja ni wenu kuja kubisha na kupinga madini haya
Nimetoa uzi huu kama nilivyomuahaidi Demi