Sintosahau nilichokishuhudia kwa macho yangu nchini Rwanda wakati wa vita vya kikabila 1994 hadi naingia kaburini

Anaitwa Nyandwi means wa Saba...from Nkole district..pure Tutsi.
 
Mkuu wale watu saba wenye Vumbi mpaka machoni kazi yao hasa unahisi ni nini?
Safisha safisha njia.kwa maelezo baadae inadaiwa hata lile tukio pale tulipozuia na interahamwe walikuwepo wanashudia wakuwa wanasubiri Tanzanian waanze kuiliwa waingilie Kati rasmi , ni dhahiri tulivyowakuta pale walivyokuwa na lile gari lilivyokuwa Kuna mapambano makali yaliyokuwa yanaendelea hatua kwa hatua njia walizokuwa wanapita Sasa hozo njia ndo mtihani kuzielezea,respect soldiers

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wale ni wazee wa kazi, hawanaga mbwembwe, Jichanganye sasa kwa anga zao. Ila naamini hawakuwa saba tu kumaliza mziki ambao ungetokea kwa dharula.

Yote kwa yote Mzee wangu pole sana. Thanks for sharing.
 
Upo sahihi kwa maoni yako, nayaheshimu mkuu. Ila binafsi naamini binadamu hatuko sawa kwa kila kitu, ndio maana kuna mataifa yanaitwa "teule", they're gifted.
 
Ni kweli...sijui ujinga huu huwa wanapata wapi...maana wana asili yao..si Rwanda wala Urundi..ila husikii kusema...

Kuna aina flani ya watu hapa tz..nao wana ujinga huo huo..
ndio maana kule huwa kuna mvutano usioisha!...
Wanakosana kidogo tu..kuingiana maungoni...

Wanafiki mno...utaishi na kufanya kazi nao ..lakini huwezi kuwa mwenzao!
Wanaamini wao ni bora na wanatakiwa kuwa juu!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hatimaye nimecheka kwenye huu uzi,nimefikiria tukio kubwa la kusisimua kwa mujibu wa mtiririko wa hii simulizi, kwa kubashiri unafikiri angeweka tukio gani labda ?😀😀
 
ooh okay.
poleni na Hongera zao
 
Nakumbuka mwaka 1994 baba yangu alikuwa na wenzie wakipeleka bidhaa Rwanda, alichelewa sana kurudi, ila siku aliporudi hakuwa na raha hata kidogo ila alirudi na pesa nyingi sana.

Huwa hataki kusikia mtu akisimulia tukio hili, yaani ilikuwa tukimuuliza ilikuwaje, mnamuona kainuka anaenda kulala, ila kuna siku alisema "Vita isikieni tu kwa wenzenu". Akainuka kwenda kulala.
 
Mkuu nashukuru kwa simulizi hii na najua angalau kuna watu tumepata mwanga kwa version yenu ya ubalozini, nasema version maana kuna mwingine labda alikwama katikati ya Kigali labda hotelini nae atakuja na namna yake alivyookoka. Ila naona kama umeamua makusudi kuifupisha na kuikatisha ila nmekuelewa. Kuna matukio ambayo najua ndo yanakujia moja moja ukiwa umetulia na hujatueleza naomba utupe pia kwa mfano najua au nahisi ulijaribu kumtafuta yule demu wako je uliambiwaje, matukio labda ya magari kuishiwa mafuta au wale wadandiaji wa njiani. Wale watu saba je ushawai waona tena au ndo akina kamanda Mwakibolwa(Jocking) na mengineyo
 
Ujinga wa hivi sisomi nimescroll hadi chini nashangaa kuona part 2 bofya link hii nikaachana nayo
Ndio Watanzania mlivyo, mnatafuta sehemu ya kusaini tu lakini Maelezo hamsomi.

Ndio maana Kila siku Mawaziri wanasaini mikataba yenye masharti ya ajabu sababu hasomi masharti.. wanaishia kusaini tu.

Hivyo sioni ajabu kwa hiki ulichokiandika.
 
Mkuu asante sana kwa kumalizia kisa hiki mpaka mwisho kwa yale yote ambayo jicho lako limeyashuhudia. Pamoja na kukatishwa tamaa na baadhi ya members lakini mwisho wa siku tumejua yale mengine ambayo hatukuwahi kusikia wala kusoma mahali.

kuna sehemu umesema wakati mmefika mpakani mwa Rwanda na Burundi kwenye ule mto unaotenganisha hizo nchi mliona maiti zilizotungishwa kwenye miti zikitokea upande wa Burundi zikiletwa na maji tokea upande wa Burundi, inamaana kilichokuwa kikiendelea Rwanda na Burundi pia ndicho kilichokuwa kikitokea? Na je uliweza kugundua au kujua ni kikundi gani au kina nani hasa waliokuwa wakifanya hayo mauaji kwa upande wa Burundi?
 
Kwamba itakua wahutu ndio wanaleta hali ya wasiwasi ? I'm so curious to know the cause of that tension to citizens whilst there is Peace.
Hutu wamebinywa,na kabisa km wanataka amani ni kukiri makosa tu,yaani mpaka mtoto akizaliwa ni kukiri kwamba sisi ni wauaji vinginevyo jela zipo.
Sasa hao waskie tu, Pk anajitahidi kuwapurura ila siku wakikurupuka wale sijui
 
Wakiwa Tanzania ni Wahangaza (Watusi + Wahutu wa Rwanda) na Waha (Watusi + Wahutu wa Burundi)
Japo pia kuna waha Asili.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni miaka mingi imepita tangia hiyo kasia itokee Rwanda na Burundi. Hao walioko ndani ya mipaka ya Tanzania wameshakuwa ndugu zetu na wanashare historia pamoja nasi kwamaana wameshaoa/olewa na kuzaa ndani ya mipaka yetu.
 
Hatimaye nimecheka kwenye huu uzi,nimefikiria tukio kubwa la kusisimua kwa mujibu wa mtiririko wa hii simulizi, kwa kubashiri unafikiri angeweka tukio gani labda ?😀😀
Labda baada ya kujifanya kwamba hajui chochote kuhusu matumizi ya silaha za kivita baadae angeibuka ghafla na kushirikiana na wale makomandoo saba na hatimaye yeye kuwaua mainterahamwe kadhaa ikiwemo kiongozi wao aliyekuwa anakaribia kufyatua kombora la RPG kwa kiongozi wa makomandoo wetu.

Baada ya hapo kwa kitendo hicho cha ujasiri kilichomfurahisha sana balozi wangekumbatiana, kubusiana nae balozi shavuni kisha kuagana kwa kupungiana mikono na wale watoto ili yeye aendelee na safari yake kurejea Dar huku balozi na wale watoto wawili wakibaki Burundi.
 
Miaka hiyo 94 kuna dogo walipanga mtaani jirani ikatokea tukawa friends, basi vile ye mgeni ikawa siku naenda nae viwanja Siku coco Beach Pale mara ghafla kapagawa kaanza kuongea kilugha naona kafuata bonge la jiwe amtupie Jamaa (muhutu)

Yaani mpk namnyanganya namuuliza vp ww unamdai au,mnajuana?ndio anajibu interahamwe hawa ataniua nikimuacha.
Mi nikaona we acha mambo yenu huko huko uko hapa no hate.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…