Sintosahau nilichokishuhudia kwa macho yangu nchini Rwanda wakati wa vita vya kikabila 1994 hadi naingia kaburini

Sio kweli aliyeharibu ni mbelgiji soma historia yako vizuri
 
Hata uombe vipi mkuu,bila kujisahihisha hakuna kitu. KG hajafanya juhudi zozote za kuliweka hilo Taifa pamoja. Badala yake amekweza wa kabila lake kwenye madaraka makubwa ya nchi,hawa wengine wamepewa mifupa ya nchi wana kinyongo.

Kuliponya hilo Taifa ilitakiwa kg awaite pamoja mpaka waasi akae nao wapange namna ya kuliweka pamoja hilo taifa. Kitendo cha kuwafuatilia huko waliko wapinzani na kuwafutilia mbali ni uoga wa kike wa muda tu. Maana hapo unazidi kuchochea moto,yeye anafikiri atadumu milele. Naamini hawa wanaonyanyaswa hawako kimya,lazima nao wana mipango hata iwe ya muda mrefu hawezi kuvumilia kuendelea kuwa chini. Hatuombei ila muda utaongea

Sent using Jamii Forums mobile app
 
[emoji857][emoji857][emoji857] Bado naiona pesa kwenye hii thread.. Mkuu Mungu akijalia uzima .. Na mipango ikampendeza, na mwisho kama wewe hautojali siku moja nitakutafuta.. Unless uwe haupo interested.. Tu make hii kitu iende Amazon.. Naamini kabisa pesa ipo hapa.. Trust me or not [emoji857][emoji857][emoji857]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Shkamoo kwako mkuu...
 
Asee nakumbuka miaka hiyo mimi na familia yangu tulikuwa tunaishi lusumo magereza mama yangu alikuwa ananipa maandazi najwenda kuuza benako na nikiuza nilikuwa nabeba dagaa wale wa mwanza ni maisha ambayo niliyazieya,hiyo vita imepiganwa nimeshuhudia miili ikipita mtoni pale darajani, kiukweli nina mshukuru sana Mama yangu mzangu Mungu amjaalie huko alipo RIP MUM., sahv na watoto na maisha ya naendelea

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ahaa, nashkuru mzee wangu. Basi mm nakwambia haitofika 2050 bomu hilo la rwanda halijalipuka.
Wahutu walio wengi ni wanatanga tanga nchi jirani wakikimbia mkono wa PK, ukiachilia mbali dhana ya wengi kuongozwa na wachache.
Sioni sababu ya kuweka "ni" katikati ya sentensi, inatia kichefuchefu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimesoma hii story nikapitiwa na usingizi nimeota naswakwa mtaani kisa nakata watu mapanga... mimi mwenyewe sikumbuki tukio la kukata mtu ila nimeona damu nyingi sana na jinsi watu wanavyoniogopa na kunisimulia navyotisha hata mimi mwenyewe namejiona adui.

Sasa kuna majamaa wakawa wananilia mingo wanikate na mimi nashukuru ndoto imeisha na usingizi umekata sasa niko hapa kusubiria toleo jingine. Ila sitasoma tena hii nightmare muda mchache kabla ya kulala
 
wewe nae unapumbazwa unaonekana zuzu unakubali tu.
hivi na akili zako timamu (japo zipo robo kilo) unaamini kwamba eti commando mmoja ni sawa na wanajeshi 100!!!

kwamba risasi ikimpiga kichwani hafi?
kwamba gari lao likitupiwa grumeti halilipuki?
Ni grenade mama sio grumeti. Grumeti ni mto upo Serengeti.
 
Uzi umenifikirisha sana!!upande wa mama yangu asili yao ni wanyankole wa uganda!!Kwa sasa ni Wanyambo wa kule kaisho karagwe!!!Kuna vitabia fulani vya Roho ngumu huwa naviona na kujisikia na maringo kwa hawa ndugu zangu wa upande wa mama!!!naona sasa nimeridhika kiuchunguzi kuhusu kabila lao!!!
 
Mkuu nilielezwa na chazo cha uhakika kwamba hata kupanda ndege moja kwa Marais wa Burundi na Rwanda walishawishiwa na mtu unaeza kumuita "EXTREMELY INFLUENTIAL". Mtu mwenyewe ni Mtanzania ambae mpaka sasa hivi hakuna anaemzungumzia kua alikua na mkono kwenye machafuko yale na hatimaye kuingia madarakani RPF, ngoja niishie hapa
 
Huyo kiumbe mbongo bado yupo bongo?!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…