Sintosahau nilichokishuhudia kwa macho yangu nchini Rwanda wakati wa vita vya kikabila 1994 hadi naingia kaburini

Yaani East Africa iwe chini ya tutsi?mbona hilo suala ni gumu sana

Sent using Jamii Forums mobile app
Ndugu, hivi vidude huwa ni vya kupuuza tu mara zote. Huwa vinajiona ni extremely special. Rejea ishu ya Mkwere na PK miaka ya mwishon mwa utawala wa Mkwere unajua kwa nini ulinzi wake uliimarishwa!? Hiki kijamaa kilitaka kuleta upuuzi wake, akapewa onyo kidogo tu akaufyata. Na alijua akishaitwaa Tz bas East Africa yote inakuwa chini yake. Anajua kilichompata mtutsi yule
 
Bossless Wakati RPF wanaichukua nchi kwa mtutu wahutu waliokuwepo ni kwamba walijisalimisha baada ya mziki kuwa mnene au niaje?

Na vipi kuhusu idadi yao wakati huo ilikua bado ni significant figure?
RPF walivoingia wakaanza kuua nao wahutu lakini wakawa wamechelewa dunia ikawa imeshajua na kuanza kufuatilia kwa karibu , ikumbukwe hata hapa mkuu wa majeshi Kama sijakosea General Mboma alitishia kuingiza majeshi Rwanda kuzima hii kitu akawa anasubiri final say atoe oda tu .kwa hiyo watusi wakaamua kudeal na wahutu kupitia mahakama za kihuni walizoziita AGACHACHA na hizi ndo zilinifanya nisimuone Tena mpenzi wangu yule niliporudi Rwanda.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Labda alikimbilia hapo nyumbani, mi nilikua na Tumusiime miaka yote hiyo toka 94 tukaachana 2006,mpenzi si mpenzi kishkaji tu miaka yote hiyo.
Demu refu pande la kitu,nyama za kutosha, zurii, jeupee ila bana likipiga bia 2 balaa😂😂😂
 
Bossless naomba msaada wako wa kitu ambacho ni critical. Unasema ulikuwa unafanya kazi ubalozini. Unamaanisha Rais Mwinyi hakutuma kikosi cha kuwarejesha nyumbani raia wake?
Soma vizuri kwanza stori ,mauaji haya yalifungwa kwenye box kwa siku 70 ,huku propoganda kali zikiendelea so viongozi wengi wa Rwanda walikuwa wana Kuja huku Tanzania kwenye mikitano ya upatanishi na waaasi watangaza Kuna amani tele ,kwanza Ilikuwa kutoka ndani ya Rwanda.

Ni ishu utapita wapi.kipindi hakuna social media wala nini waandishi wote kimyaa tangaza uone Cha mtema kuni hata hao bbc walikuwa wanatoa taarifa ambazo zilikuwa zakusadikika tu yani yalifichwa Sanaa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hizo mahakama zilichangia vipi wewe kutokumwona mpenzi wako? Alifungwa? Alikuwa ni mhutu au hao tunaowaita "moderate tutsi" hivyo akajikuta yeye na familia yake wanakuwa victim wa utawala mpya wa RPF?
 
Weka nyama mkuu, vp ilikuaje
 
Mkwere ndo mana alicheka tu, km ukisoma andiko la hii vita utaona kulikua na vichwa saba kule mpakani mchezo wote usikute vinaujua. Vinacheza kama kamari, twende uku sawa,rudisha majeshi poa,skilizia hapo wanakuja hao sawa, twende tukaliwashe huku ili wasumbue huku poa yaani mradi kadance linaendelea
 
Hizo mahakama zilichangia vipi wewe kutokumwona mpenzi wako? Alifungwa? Alikuwa ni mhutu au hao tunaowaita "moderate tutsi" hivyo akajikuta yeye na familia yake wanakuwa victim wa utawala mpya wa RPF?
Ilikuwa hivi yani kutokana hukumu za kihuni ,yani Ilikuwa ukimtaja mtu ndani ya mtaa /Kijiji chenu Kama amewasaidia wahutu kutoroka au kujificha hata Kama mna visasi vya zamani ukaamua kumsingizia mtu tu awe Mtusi au Mhutu Ilikuwa gachacha Haina Tena mjadala ni hukumu tu ,Sasa watu wengi walichokifanya ni kubadili makazi yani mtu anahama na familia yake kutoka eneo moja kwenda eneo jingine la mbali .Sasa nilivyorudi kwenda kuwaangalia kwenye makazi yao pale kwanza nilikuta nyumba imebadilisbwa imekuwa shule ya awali kuuliza wakawa wanasema hata wao hawawajui basiii.....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole sana mkuu maana inauma. Sijui wakati huo ulipokwenda huko na kumtafuta tayari huku nyumbani ulikuwa umeshampata shemeji yetu au ulikuwa bado? Ulitaka ukajikumbushie kidogo kwa mtoto wa kitutsi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…