Sio Tanzania pekee yenye Capital City ndogo kuliko Jiji la Biashara

Sio Tanzania pekee yenye Capital City ndogo kuliko Jiji la Biashara

Dodoma haitakaa iifikie mwanza jiji kwa ukubwa hizo ni ndoto za mchana, mkoa wa mwanza una wakazi million 4 na eneo lake ni dogo dodoma ni jiji lenye kmsq zaidi ya 2500 ina population ya watu laki 7 mwanza ukiihesabu kwa hizo kmsq inawatu zaidi ya 2m lakini pia mwanza imezungukwa na kanda ya ziwa yenye watu wengi zaidi nchini kwahio mingiliano ni mkubwa lakini dodoma ilipokaa ni eneo lisilo na watu ukienda km zaidi ya 120 mashariki ndio unakutana na kibaigwa nao ni mji mdogo ukienda magharibi ni mbali hadi uje ukutane na bahi au manyoni nayo ni miji midogo ukienda kaskazini hadi uje ukutane na kondoa karibu km 200 nao ni mji mdogo kwenya upande wa iringa mji mkubwa kule ni iringa km zaidi ya 250 iringa nao si mji wenye watu wengi unazidiwa hata na geita iringa kwa watu ni kama bunda tu kuja kwenye maendeleo mwanza ni ya 4 nyuma ya arusha na zanzibar na dodoma kuzifikia arusha na zanzibar pia ni ndoto imagine arusha kuna ghorofa 7000 dodoma zipo 2000 ghorofa zinaonyesha uwezo wa kiuchumi wa wakazi huwez kua maskini ukajenga ghorofa sasa kufikia huko sio leo ukumbuke dar es salaam kilichoifanya kuwa kubwa ni bandari mwingiliano wa biashara na wala sio kua makao makuu hata sasa hivi mji umeamia dodoma lakini foleni ni vile vile lakini kingine uboreshwaji wa miundominu kila kanda sasa hivi inhospitali kubwa miundominu sasa hivi sgr mtu ataweza kwenda mwanza na dar kwa haraka hata huduma kama interview sasa hivi watu wanafanya online sio lazima wawepo physically huduma makao makuu huduma kama mailing n.k sasa hivi zinafanywa kwa delivery sasa dodoma nje ya kua makao makuu haina pulling factors za kuchochea uchumi mbeya kuna madini na kilimo, mwanza kuna uvuvi, arusha & zanzibar kuna utalii dar kuna bandari dodoma kuna nini ambacho kipo competitive usinitajie kilimo tena kwavile kwenye ile big4 ya chakula dodoma haipo na ndio maana fika dodoma watu wanalalamika maisha ni magumu kwa mtu ambaye sio mwajiriwa au mtumishi wa serikali au mfanyabiashara mkubwa bado dodoma ni mji wa boom la udom na msimu wa bunge au mkutano wa ccm
Labda serikali iache mpango wake wa kukuza utalii ila kama lengo ni lile lile la watalii 5mi hadi hiyo 2039 arusha na zanzibar zitakua mbali sana
Kw hio msimamo kwa maendeleo utabaki kua Dar, zanzibar, arusha, mwanza na dodoma mtachuana hiyo namba 4😀
Ila ambalo hakuna mtu atapinga ni kuwa dodoma ndio utakua mji namba mbili kwa miundombinu bora zaidi nchini ila kwa uchumi sahau chief naiona mbeya iko na bright future kuliko dodoma sio kwa hali ya hewa, vivutio vya utalii, kilimo na resources wanachokosa ni plan tu maskini kwa vile hata mbeya ingehesabiwa kwa ukubwa wa kmsq 2500 ingekua na watu 700k kama dodoma au zaidi kwa sababu kwa kmsq 200 tu mbeya jiji inawatu zaidi ya laki5 ngoja tu serikali iamke kuutilize resources zote za huo mkoa dodoma ni majengo ya serikali tu yakamilike kwisha 😀 irudi kwenye nafasi yake ya 6
NB: Mimi ni mmoja wa watu nnaosapoti sana mpango wa dodoma kua makao makuu kwa vile imeongeza mpangilio mzuri kwenye eneo tabarare la dodoma ambalo ni katikati mwa nchi kuliko
Dar 👏 Ni mafanikio makubwa ya kujivunia kama nchi kwamba hadi 2039 tutakua na la kujivunia kwamba tunamji mmoja smart na uliopangika kisawasawa wa dodoma bila kuathiri ukuwaji wa miji mama ya mbeya, mwanza ,zanzibar, arusha na Daresalaam
Umeandika vitu vingi bila mpangilio😆😆😆labda kwa kukusaidia "population kubwa" wala sio kigezo cha maendeleo ya mji. Unaweza kuwa na population kubwa lakini mipangomiji+miundombinu na huduma za kijamii hazina ubora kama ilivyo kwa Mwanza barabara za lami ni tatizo kubwa.

Nakupa mfano Jiji la Windhoek Namibia lina population ya watu lakitano tu lakini ubora wake na mpangilio wa jiji umezidi Dar yenye watu milioni 5😂😂.
Kuna Jiji Ulaya la Luxembourg City lina population ya watu laki mbili tu lakini ubora wake na maendeleo yake huwezi kulinganisha na baadhi ya majiji yenye population ya mamilioni ya watu.
 
Umeandika vitu vingi bila mpangilio😆😆😆labda kwa kukusaidia "population kubwa" wala sio kigezo cha maendeleo ya mji. Unaweza kuwa na population kubwa lakini mipangomiji+miundombinu na huduma za kijamii hazina ubora kama ilivyo kwa Mwanza barabara za lami ni tatizo kubwa.

Nakupa mfano Jiji la Windhoek Namibia lina population ya watu lakitano tu lakini ubora wake na mpangilio wa jiji umezidi Dar yenye watu milioni 5😂😂.
Kuna Jiji Ulaya la Luxembourg City lina population ya watu laki mbili tu lakini ubora wake na maendeleo yake huwezi kulinganisha na baadhi ya majiji yenye population ya mamilioni ya watu.
Uyo mtu nliemjibu ndio kasema dodoma itakua second largest city sio mimi😀😀 wewe umekurupuka tu sijui ndio umeamka mi nmejaribu tu kumuelewesha kama anaijua mwanza lakin
 
Kwa wale wasiotaka au wasiopenda Dodoma kuwa makao makuu ya nchi kwa sababu eti mji mdogo kuliko Dar es Salaam au Arusha, basi kwa taarifa yenu kuna nchi nyingi tena nchi kubwa na maarufu katika kundi hili. Nchi hizo zina makao makuu ya nchi madogo kuliko jiji au majiji ya Biashara. Nitatoa mifano michache maarufu.

1. United States of America.
Makao makuu: Washington DC
Jiji kubwa la kibiashara: New York City.

2. Peoples Republic of China.
Makao Makuu: Beijing
Jiji kubwa : Shanghai

3. Federal Republic of Brazil
Makao makuu: Brasilia
Jiji kubwa: Sao Paulo

4. Federal Republic of Nigeria
Makao Makuu: Abuja
Jiji Kubwa: Lagos

5. Republic of South Africa
Makao Makuu: Pretoria(ilipo executive)
Jiji Kubwa: Johannesburg.

6. The Kingdom of Morocco
Makao Makuu: Rabat
Jiji kubwa: Casablanca.

7. Scotland
Makao makuu: Edinburgh.
Jiji Kubwa: Glasgow

8. Canada
Makao makuu: Ottawa
Jiji kubwa: Toronto

Kwa hiyo hoja ya Dodoma kuwa ndogo haina mashiko, haina miguu ya kusimamia. Miji yote hujengwa na wananchi na serikali yao kwa mipango na vipaumbele. Viongozi waendelee kuipa Dodoma umuhimu wake kama makao makuu ya nchi.

Mashirika binafsi, mashirika ya dini na mashirika ya umma pia yaipe Dodoma umuhimu kama makao makuu ya nchi.

Tutatengeneza jiji la pili muhimu litakalochangia mapato ya serikali na hivyo maendeleo ya nchi na watu wake.
Sasa unatengenezaje kwa kukusanya mapato jiji la pili kisa tu utashi wako kwanini usiendeleze ambayo tayari inakusanya mapato ikusanye mapato zaidi?
Dodoma iendelezwe bila kuiua miji mingine ili ionekane maamuz waliyofanya ni sahihi
Miji yenye mchango mkubwa kama mwanza mbeya na hata arusha nayo iboreshwe hakuna haja ya kujenga mabarabara dodoma ambayo hata hayatumiki kisa tu ni makao makuu wakat sehemu nyingine hakuna mabarabara tujenge kwa uwiano tukifanikiwa kama nchi dodoma itapendeza tu
 
Back
Top Bottom