Sioni haja ya kujenga uzio

Boss la DP World

JF-Expert Member
Joined
Dec 12, 2021
Posts
2,318
Reaction score
8,464
Habari wakuu, kwa mara ya kwanza nilijenga nyumba 2 in 1 mkoa wa Morogoro, kwakuwa lengo ilikuwa kuzipangisha maana sikuwa nimetulia kimaisha nilizizungushia uzio wa matofali na kuziwekea mageti ili kila mpangaji atoke na kuingia kwa geti lake.

Baada ya mwaka na nusu nilihamishwa mkoa mwingine nikakaa kwa muda badae nikarudi Morogoro, sasa nimeona huu mkoa unanipenda kwa hiyo nimejenga nyumba ya kuishi nashukuru imekamilika.

Sasa kuna vihela nimevifuma sehemu wazo la kwanza lilikuwa kuizungushia uzio, ila leo nimepata wazo la kutumia hivyo vihela kuanza ujenzi kwenye kiwanja kingine maana nikipiga hesabu za gharama nilizotumia kujenga uzio wa matofali ya block+ urembo wa vyuma + mageti kwenye nyumba za wapangaji ni kama zinafanana na gharama za kuinua boma la nyumba nzuri tu.

Sijapanga kufuga wala kuwa na biashara nyumbani, nimeona nipande miti ya matunda na kivuli, ukoka na nitengeneze vi bustani vya kuvutia ila uzio naona ni kama ushamba fulani hivi.

Naombeni uzoefu wenu, je nimefikiri kwa usahihi au kuna ulazima wa kujenga uzio?
 
Nikukumbushe tu kuwa, kazi ya kwanza ya uzio ni usalama WAKO na mali hivyo uzio huweza kuwa kipaumbele au la kutokana na usalama wa eneo unaloishi. Sasa wewe kuja kutuomba ushauri wakati hata hatujui unakoishi, huwezi kupata ushauri sahihi......
 
Uko kwenye mstari sahihi.
Panda fence ya mchingoma for privacy.
Unajenga uzio kwa mil 25 kulinda wezi wasiibe TV ya laki saba!
 
weka fensi ya boganvillear itengenezee futi 5 kutoka chini alafu ikate inyooke utakuja kunishukuru
 
Uko kwenye mstari sahihi.
Panda fence ya mchingoma for privacy.
Unajenga uzio kwa mil 25 kulinda wezi wasiibe TV ya laki saba!
Narudia tena, sababu ya msingi ya kujenga uzio au la, inategemea usalama wa eneo ulilopo;
Mwandishi keshasema anamiliki nyumba sijui tatu inamaana hakosi gari nk wewe unaongelea habari ya TV ya laki saba?
 
Narudia tena, sababu ya msingi ya kujenga uzio au la, inategemea usalama wa eneo ulilopo;
Mwandishi keshasema anamiliki nyumba sijui tatu inamaana hakosi gari nk wewe unaongelea habari ya TV ya laki saba?
Gari namiliki miaka kadhaa sasa haliwezi kuibiwa wala kuchezewa kisa sijaweka uzio mkuu, kuna aina za magari zinapendwa na wahalifu ila ukitaka kuwakomesha wewe nunua magari ya mjerumani au mmarekani hakuna atakaye sogelea ila jiandae kwa gharama kubwa ya vipuri.
 
Jenga uzio wa tofali tatu kutoka msingi, lengo ni kuzuia wapita njia kufanya eneo lako ni njia ya mkato.
 
Umejenga sehemu gani nije kupanga nmehamia moro alafu ni mgeni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…