Sipendezwi na wanachama wa Simba wanaotoa taarifa za klabu kabla ya klabu yenyewe

Sipendezwi na wanachama wa Simba wanaotoa taarifa za klabu kabla ya klabu yenyewe

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975
Hili nitalielezea kwa ufupi sana ila naomba ujumbe uwafikie wahusika na wawajibike.

Kuna haka kamtindo na katabia ka baadhi ya wanachama wa Simba, nimewahesabu wawili mpaka sasa ambao wana mtindo wa kujitokeza na kutoa taarifa za klabu ya Simba kabla ya taarifa rasmi kutolewa na klabu yenyewe.

Wa kwanza ni huyu anajiita "Aggysimba". Huyu nilishawahi kumsema kwa kucopy content zooote zinazotoka katika account ya Simba na kuziweka katika account yake. Jana niliposikia tetesi za kufungiwa kwa Simba nilipoanza kuangalia online kujidhihiridha kuhusu taarifa hizo nikakuta yeye ameripoti kabla hata ya klabu kutoa taarifa. Hili halijanifurahisha kabisa. Najua atakuwa alipewa za ndani labda na kiongozi lakini sijajua kiherehere cha kukimbilia kupost kilitokea wapi. Na mpaka sasa amelivalia njuga suala hilo utadhani ana maslahi nalo.

Wa pili ni huyu anajiita "Dr. Mohammed". Huyu huwa anaripoti taarifa za Simba hasa za usajili kwa mamlaka kabisa kama vile yeye ndiye msemaji mkuu wa Simba akitaja hadi gharama za usajili na mishahara ya wachezaji. Kajipachika msemaji wa tawi lake basi anajiona anaweza kuzungumzia habari za ndani za timu. Na huyu naye huwa anajipambanua kuwa na ukaribu na viongozi na sijawahi kuona wala kusikia akikemewa kwa tabia hiyo.

Naomba uongozi wa Simba uliangalie hili. Tusiwe kama klabu ya kihuni ambayo inajiendeshea mambo hovyo hovyo. Wanaokiuka taratibu au kuvujisha taarifa za klabu tuone wakichukuliwa hatua.

Ubaya Ubwela.
 
Umewaonea tu,hizo taarifa zilivuja mapema sana, waandishi baadhi waliripoti suala hilo.....changia timu yako maana Rage alishasema mashabiki wengi wa Simba ni mbux3....... umewahi kuona wapi timu iliyoshinda ndiyo inavunja viti kama siyo kuprove kauli ya Rage
 
Huyo anayejiita Dr Mohamed anatabia ya hovyo ya ujivuni na kujifanya mjuaji.

Kwanza most of taarifa zake sio data sahihi na mara kibao ameandika habari za uongo ila tangu mwanzo nilishachagua kumpuuza.

Kuna tabia fulani hivi ya kujifanya mtu wa kupata habari za mapema kabla umma haujazifikia.

Utaskia "jana nimeongea na Fadlu amenihakikishia leo Mpanzu anaanza kwenye kikosi cha leo" Camon man who the fck are you??

Mara "Nimeongea na viongozi wa Simba tayari wamemaliza dili la Feisal na sasa tusubirie utambulisho tu" Shensiiiii!!

We uongee na Fadlu kama nani? Hiyo access unaipatia wapi? Ahmed Ally mwenyewe ana mipaka yake hawezi kuwa na direct access kwa kila mtu ndio awe huyu Muha?

Kisa tu umepata title na hivyo vi followers vya Insta na kiblog chako ambacho unakipambania kupata visitors ndio uje na taarifa potoshi uvimbe uonekane nawe ni mtu wa kitengo??

Yani anajiona ni mtu fulani hivi non regular ambaye ana access ya taarifa nyeti za nje na ndani ya vilabu. Yani mchizi anajionaga ni Fabrizio wa Kigoma.
 
Huyo anayejiita Dr Mohamed anatabia ya hovyo ya ujivuni na kujifanya mjuaji.
Mkuu umenena vyema sana, haka kashamba ka Buzebazeba huko kanajiona kana Title simba. Ile siku ya Simba day tulikua tumepanga foleni ya kuingia uwanjani kajamaa kakapita na koti la suti na jua kali lile eti kanatupungia mkono funny enough hakuna mtu alikapa attention.
 
Umewaonea tu,hizo taarifa zilivuja mapema sana, waandishi baadhi waliripoti suala hilo.....changia timu yako maana Rage alishasema mashabiki wengi wa Simba ni mbux3....... umewahi kuona wapi timu iliyoshinda ndiyo inavunja viti kama siyo kuprove kauli ya Rage
Nitajie hao waandishi waliopost na muda. Suala siyo kujua mapema, yeye kwa nafasi yake ilibidi ajiulize ulazima wa kupost haraka ukichukulia ni habari mbaya na ambayo haina faida kwa timu.

Kuna mtu mwenye uwezo wa kupata taarifa mapema kama MickyJnr? Mbona yeye hakukimbilia kupost?
 
Huyo anayejiita Dr Mohamed anatabia ya hovyo ya ujivuni na kujifanya mjuaji.

Kwanza most of taarifa zake sio data sahihi na mara kibao ameandika habari za uongo ila tangu mwanzo nilishachagua kumpuuza.

Kuna tabia fulani hivi ya kujifanya mtu wa kupata habari za mapema kabla umma haujazifikia.

Utaskia "jana nimeongea na Fadlu amenihakikishia leo Mpanzu anaanza kwenye kikosi cha leo" Camon man who the fck are you??

Mara "Nimeongea na viongozi wa Simba tayari wamemaliza dili la Feisal na sasa tusubirie utambulisho tu" Shensiiiii!!

We uongee na Fadlu kama nani? Hiyo access unaipatia wapi? Ahmed Ally mwenyewe ana mipaka yake hawezi kuwa na direct access kwa kila mtu ndio awe huyu Muha?

Kisa tu umepata title na hivyo vi followers vya Insta na kiblog chako ambacho unakipambania kupata visitors ndio uje na taarifa potoshi uvimbe uonekane nawe ni mtu wa kitengo??

Yani anajiona ni mtu fulani hivi non regular ambaye ana access ya taarifa nyeti za nje na ndani ya vilabu. Yani mchizi anajionaga ni Fabrizio wa Kigoma.

Mkuu umenena vyema sana, haka kashamba ka Buzebazeba huko kanajiona kana Title simba. Ile siku ya Simba day tulikua tumepanga foleni ya kuingia uwanjani kajamaa kakapita na koti la suti na jua kali lile eti kanatupungia mkono funny enough hakuna mtu alikapa attention.
Nilishaacha kumsikiliza. Ila access ya timu alikuwa nayo labda kama watakuwa wameikata. Ni kama Kisugu pia naye sipotezi bando langu kumsikiliza na mambo yake ya kuingiza siasa kwenye mpira.
 
Mkuu kwa watu kama kina Micky Jr mtasemaje,yule jamaa ndo anakuwaga na habari kabla ya waandishi wa habari wa ndani na taarifa ambazo hazijatangazwa,ni mwandishi wa CAF na ana-assess za ndani kila sehemu, kila mtu anajifanya Fabrizo Romano siku hizi.
 
Sio hao Kuna watu wanajifanya mashabiki kindakindaki na Wana uchungu na timu lakini hata tiketi hawanunui.
Hao wako Simba kimaslahi na ndio wanaongoza kuanzisha majungu kwenye timu, viongozi lazima wawawekee mipaka Kuna watu Wana mchango mkubwa kuliko hao machawa.
 
Mkuu kwa watu kama kina Micky Jr mtasemaje,yule jamaa ndo anakuwaga na habari kabla ya waandishi wa habari wa ndani na taarifa ambazo hazijatangazwa,ni mwandishi wa CAF na ana-assess za ndani kila sehemu, kila mtu anajifanya Fabrizo Romano siku hizi.
Jana Micky hakukimbilia kupost ile taarifa, kuna kitu hapo cha kujifunza.
 
Nilishaacha kumsikiliza. Ila access ya timu alikuwa nayo labda kama watakuwa wameikata. Ni kama Kisugu pia naye sipotezi bando langu kumsikiliza na mambo yake ya kuingiza siasa kwenye mpira.
Mzee Masatu je?

Huyu dingi ndio komesha sasa

Kaulizwa swali na mwandishi ni mazingira gani ambayo Simba unaweza kuiona ikivuka kwenda robo fainali?

Majibu yake "aaaah kwanza nimshukuru Mungu kwa kuniamsha salama lakini pia nimshukuru jemedari wetu na raisi wetu mpendwa mama Samia Suluhu Hasan kwa upendo wake kwa watanzania" aah unajia Japhet"

Niliacha kufuatilia story za michezo zinazohusu kilinge cha pale Station.
 
Huyo anayejiita Dr Mohamed anatabia ya hovyo ya ujivuni na kujifanya mjuaji.

Kwanza most of taarifa zake sio data sahihi na mara kibao ameandika habari za uongo ila tangu mwanzo nilishachagua kumpuuza.

Kuna tabia fulani hivi ya kujifanya mtu wa kupata habari za mapema kabla umma haujazifikia.

Utaskia "jana nimeongea na Fadlu amenihakikishia leo Mpanzu anaanza kwenye kikosi cha leo" Camon man who the fck are you??

Mara "Nimeongea na viongozi wa Simba tayari wamemaliza dili la Feisal na sasa tusubirie utambulisho tu" Shensiiiii!!

We uongee na Fadlu kama nani? Hiyo access unaipatia wapi? Ahmed Ally mwenyewe ana mipaka yake hawezi kuwa na direct access kwa kila mtu ndio awe huyu Muha?

Kisa tu umepata title na hivyo vi followers vya Insta na kiblog chako ambacho unakipambania kupata visitors ndio uje na taarifa potoshi uvimbe uonekane nawe ni mtu wa kitengo??

Yani anajiona ni mtu fulani hivi non regular ambaye ana access ya taarifa nyeti za nje na ndani ya vilabu. Yani mchizi anajionaga ni Fabrizio wa Kigoma.
Nimemuona huyu mlimani kwenye duka la kampuni moja ya simu akiulizia simu ya mkopo.😀😀 na panki lake
 
Mzee Masatu je?

Huyu dingi ndio komesha sasa

Kaulizwa swali na mwandishi ni mazingira gani ambayo Simba unaweza kuiona ikivuka kwenda robo fainali?

Majibu yake "aaaah kwanza nimshukuru Mungu kwa kuniamsha salama lakini pia nimshukuru jemedari wetu na raisi wetu mpendwa mama Samia Suluhu Hasan kwa upendo wake kwa watanzania" aah unajia Japhet"

Niliacha kufuatilia story za michezo zinazohusu kilinge cha pale Station.
Yees. Huyo mwingine naye nilimweka pembeni, daah. Ila uchawa ni noma, sijui watanzania tumekuwaje aisee inasikitisha kwa kweli.

Juzi nilikuwa naangalia interview ya Azim Dewji timu ilipoenda Algeria, alisema kitu kuhusu Mama, mwandishi akamuuliza mama yupi akajibu "kuna mama mmoja tu kwenye nchi yetu, hakuna mwingine" nikasema wooow!
 
Duh ya kwenu mnapenda yafichike ila ya kwa jirani kutwa kiranga mpaka mnakuja kuanzisha nyuzi za mechi kabla ya siku husika
 
Duh ya kwenu mnapenda yafichike ila ya kwa jirani kutwa kiranga mpaka mnakuja kuanzisha nyuzi za mechi kabla ya siku husika
Usiwe serious sana. Ule uzi ulikuwa wa kuchangamsha genge tu nilijua hautadumu.

Halafu siyo suala la kuficha, ni suala la kuheshimu taasisi unayousapoti ili taarifa zake zitoke kwa usahihi. Si unaona taarifa yake ilivyoishia kuwa na mapungufu?
 
Nitajie hao waandishi waliopost na muda. Suala siyo kujua mapema, yeye kwa nafasi yake ilibidi ajiulize ulazima wa kupost haraka ukichukulia ni habari mbaya na ambayo haina faida kwa timu.

Kuna mtu mwenye uwezo wa kupata taarifa mapema kama MickyJnr? Mbona yeye hakukimbilia kupost?
Mick Jr naye ni kanjanja tu na Mwandishi yenu na shabiki yenu hawezi tweet taarifa mbaya kwa watu wanaompa kula ndiyo maana alikausha......hiyo taarifa ingekuwa ni Yanga ungeona makala kibao,sina haja ya kuhangaika kukupa,nenda Instagram utaona mapema tu ilipostiwa
 
Mick Jr naye ni kanjanja tu na Mwandishi yenu na shabiki yenu hawezi tweet taarifa mbaya kwa watu wanaompa kula ndiyo maana alikausha......hiyo taarifa ingekuwa ni Yanga ungeona makala kibao,sina haja ya kuhangaika kukupa,nenda Instagram utaona mapema tu ilipostiwa
Bado haujajibu swali. Unaposema ilipostiwa mapema, nitajie wapi na muda gani. Pia kama umeona Micky ni shabiki wa Simba kwa hiyo anakaushia habari mbaya, je huyo mwingine ambaye naye anajitanabaisha kama shabiki wa Simba kwa nini hakusubiri kama mwenzake? Hiyo ndiyo hoja yangu ya msingi.
 
Back
Top Bottom