Sipendi kuomba wala kuombwa vitu. Je, nina roho mbaya au ni kawaida?

Sipendi kuomba wala kuombwa vitu. Je, nina roho mbaya au ni kawaida?

Johnny Sack

JF-Expert Member
Joined
Jan 21, 2017
Posts
8,984
Reaction score
19,288
Habari wadau,

Kuna jambo moja linakera ila naona wengine kama wanaona ni vizuri kwao, sasa inanifanya nijiulize nina matatizo au vipi. Ni kuhusu kupeana vitu na watu, hasa nyumbani na majirani. Sitaki Jirani anipe vitu vyake wala sitaki aniombe vya kwangu, labda awe ametokewa na shida ya kweli. Vitu vyenyewe ni kama vyakula, vifaa vya ndani, n.k

Aisee kuna nyumba za kota tumehamia mimi na wife hapa, kuna majirani wana roho nzuri lakini naona hii ni too much, wanapenda sana ku-share vitu, yaani kuna siku moja atamuita wife wakapike chakula cha pamoja, siku nyingine mwingine atapika chakula kisha atuletee wakati sisi tumeshapika, siku nyingine atawaambia mumpakulie kwa kuwa yeye hajisikii kupika siku hiyo, wakati mmepika cha size yenu pekee.

Kuna mmoja juzi katoka mkoani kaleta mazagazaga mengi kampa wife, sasa siku hiyo ndio natoka kunununa vyakula vya wiki nzima nakuta friji imeshajaa, sasa na wao unakuta siku wanakuambia gesi imeisha tunaomba tutumie jiko lenu.

Wife nishampiga marufuku kuomba ama kuchukua vitu kutoka kwa majirani lakini imekuwa mtihani kukataa na yeye akiwapa vitu kesho naye atakuja kuomba kwenu, hii inaharibu ratiba na bajeti kwani mimi ni mtu ninayependa kupangilia kila kitu changu kwa usahihi.

Naona ni kama tunalazimishana kuishi kijamaa wakati haya maisha sijayaozea kabisa, japokuwa nimekulia kijijini tulikuwa hatuombani vitu hovyohovyo, labda iwe imetokea shida ya kweli.

Sasa watu wengine niliowakuta hapa naona wanaiona ni lifestyle nzuri, najiuliza pengine mimi ndio nina roho mbaya ama hili linawakera pia baadhi yenu?
 
Tatizo wife kazoeana sana na hio familia.

binafsi sijalelewa kwenye mazingira ya kuzoeana kuingiliana vyumbani/kuombana vyakula tabia ya ajabu sana.

-Sina uchoyo natoa kadiri ya uwezo wangu kwa wahitaji nikiona mtu ananizoea zoea namkwepa kwakweli.

-Napenda privacy na familia yangu aisee [emoji849][emoji849] mazoea ya kuombana mchuzi ni uswahili uliopitiliza,inakwaza hata kama sio mchoyo

Halafu tabia ya kupika pamoja ni mbaya kuliko hamtachelewa kukwaruzana na kujualiana siri za familia maana hampiki tu bila kupepesa macho na mdomo mkigombana "Ndo mana kwako kupo hivi,ndo mana mumeo hivi /mwanamke utakua wewe vijiko vyako vimepinda)
 
Hali hiyo inatokana na athari ya siasa ya UJAMAA na KUJITEGEMEA. Watz tunaishi kindugu, ni jambo zuri maana huchochea upendo kwenye jumuiya ya watu ingawa kwa ulimwengu wa leo tabia hiyo huwa ni kero. Siku hizi wanadamu wengi tumekuwa wabinafsi na wachoyo.
 
😀😀 pole sana mkuu huna tatizo wala huna roho mbaya, ni kwakuwa unapenda ratiba yako iende kulingana na vile unapanga pia kuazimisha si kilamtu anapenda maana maswala yakwenda kuomba kitu ambacho umeazimisha nayo si nzuri. kiufupi misaada inakufanya unaisha maisha ambayo si yako kiuhalisia maana ukipewa kitu tayari unajiona mdaiwa kwahiyo inakufanya huna uamuzi pingi mtu ajapo kwako
 
Wewe ni mbinafsi uliekomaa mkuu sifa kuu ya wabinafsi hawapendi kupewa ili na wao wasitoe hii tabia ya kupeana misosi wanayo sana wazungu mida ya dinner unagongewa mlango unakutana na plate ya wali nazi au wajuba wanakuja na chupa zao za gambe mnaishi nazo kiroho safi tu hili suala nililiona tabora vijijini na nikalikua states ndio nkajua kwanini wamarekan wanaitwa wanyamwèzi so kwakifupi wewe ndio mbinafsi na mswahili.
 
Chief, wala hiyo siyo roho mbaya kwa maana hata maandiko yanasema "uchunge mguu wako usiingie sana kwa jirani asije akakukinai", hivyo kila mmoja lazima awe na ratiba ya mipango na namna ya kuishi katika maisha haya. Misaada isiyokuwa na kichwa wala miguu inalemaza akili na kukufanya kuwa tegemezi, hivyo kutana na wakuu wenzio wa familia uwaeleze mtizamo wako inawezekana na wao inawakera ila wanashindwa kusema kwa kuogopa kama wewe unavyoogopa.

Kusaidiana kupo ila ni kwa kiasi siyo kwa kila jambo. Yapo mambo ambayo lazima msaidiane mfano sherehe, misiba, ugonjwa nk. Hakikisha yale yaliyondani ya uwezo wako unayafanya bila kuomba msaada.

Akina Mama wakiwa karibu kupitiliza hawakawiii kugombana na kutoleana siri za ndani na kuwaaibisha ninyi waume zao hivyo chukua hatua kwa kumueleza mkeo kuwa ushirikiano huo huupendi kisha mueleze madhara ya mbeleni na umsikie yeye anasemaje (maoni yake) muulize kwa umakini maana busara pia inahitajika.
 
Wewe ni mbinafsi uliekomaa mkuu sifa kuu ya wabinafsi hawapendi kupewa ili na wao wasitoe hii tabia ya kupeana misosi wanayo sana wazungu mida ya dinner unagongewa mlango unakutana na plate ya wali nazi au wajuba wanakuja na chupa zao za gambe mnaishi nazo kiroho safi tu hili suala nililiona tabora vijijini na nikalikua states ndio nkajua kwanini wamarekan wanaitwa wanyamwèzi so kwakifupi wewe ndio mbinafsi na mswahili

Sikuungi mkono kwa kumuita mtoa mada mbinafsi (japo simjui). Kusaidiana kupo lakini kuna mipaka yake. Jambo lolote lizikidi kiasi (kupindukia) huwa ni baya. Binafsi huwa nakaribisha watu nyumbani siku za siku kuu za kidini na wao huwa wananikabirisha na nikiingia bar huwa natoa ofa (kama nipo vizuri) na hata mimi huwa napewa ofa na marafiki.

Lakini hii anayoisemea jamaa ni ya kila siku na imevuka mipaka hadi kila mmoja kutumia jiko la mwenzake. Sasa kwa sisi tuliooa tunazijua saikolojia za akina mama, wakizinguana kidogo tu lazima watagombana, ugomvi huo utaambatana na kutoleana siri za ndani walizoelezana pindi walipokuwa na mahusiano mema jambo litakalopelekea fadhaa kwa waume zao na mleta mada akiwa mmoja wao.

USHIRIKIANO NI MZURI ILA HAUTAKIWI KUZIDI SANA.
 
Hiyo ni roho mbaya wala usitake kusingizia eti unapangilia mambo yako, mambo yanayohusu msosi mara sijui jiko la gesi muachie mkeo ashughulike bro, acha ujinga

Chief, Mume ni kiongozi wa nyumba/familia lazima kufuatilia mambo, ikiwa unaona hayaendi sawa ni vema ukamuelekeza mwenzio namna ya kuyapeleka. Kumuchie mke mambo ya vyakula/misosi wakati unaona kuwa anakwenda ndivyo sivyo huko ni kukwepa majukumu na lawama. Kumbuka ni HERI LAWAMA KULIKO FEDHEHA. KIONGOZI WAJIBIKA MAMA AISHI.
 
Mkuu ninavyofikiria mimi ni kwamba maeneo ya jikoni hiyo ni idara inayomuhusu yeye moja kwa moja, majukumu yako yanaingia pale ambapo umepokea bajeti ya manunuzi ya vifaa vya jikoni.
Chief, Mume ni kiongozi wa nyumba/familia lazima kufuatilia mambo, ikiwa unaona hayaendi sawa ni vema ukamuelekeza mwenzio namna ya kuyapeleka. Kumuchie mke mambo ya vyakula/misosi wakati unaona kuwa anakwenda ndivyo sivyo huko ni kukwepa majukumu na lawama. Kumbuka ni HERI LAWAMA KULIKO FEDHEHA. KIONGOZI WAJIBIKA MAMA AISHI.
 
Back
Top Bottom