Sipendi kuomba wala kuombwa vitu. Je, nina roho mbaya au ni kawaida?

Sipendi kuomba wala kuombwa vitu. Je, nina roho mbaya au ni kawaida?

Mkuu ninavyofikiria mimi ni kwamba maeneo ya jikoni hiyo ni idara inayomuhusu yeye moja kwa moja, majukumu yako yanaingia pale ambapo umepokea bajeti ya manunuzi ya vifaa vya jikoni....

Najua wajua lakini siyo mbaya kukumbushana. Kimsingi majukumu yote ya nyumbani ni ya Baba (Kiongozi mkuu katika familia) ila kwa kuwa Baba hawezi tekeleza yote peke yake ndiyo anatafuta msaidizi wa karibu ambaye ni mama na kumkasimia baadhi ya majukumu. Hivyo basi kumkabidhi jiko mke wako haina maana kwamba wewe hutakiwi kujua kinachoendelea huko jikoni. Ukiwa kama kiongozi unatakiwa kufanya ukaguzi wa mara kwa mara ikiwa ni pamoja na kupata maoni na kutoa mapendekezo yako na kuchukua hatua pale unapoona mambo hayaendi sawa.

Siku zote mambo yanapoharibika sehemu yoyote wa kulaumiwa huwa ni kiongozi mkuu wa eneo hilo.
 
Najua wajua lakini siyo mbaya kukumbushana. Kimsingi majukumu yote ya nyumbani ni ya Baba (Kiongozi mkuu katika familia) ila kwa kuwa Baba hawezi tekeleza yote peke yake ndiyo anatafuta msaidizi wa karibu ambaye ni mama na kumkasimia baadhi ya majukumu. Hivyo basi kumkabidhi jiko mke wako haina maana kwamba wewe hutakiwi kujua kinachoendelea huko jikoni. Ukiwa kama kiongozi unatakiwa kufanya ukaguzi wa mara kwa mara ikiwa ni pamoja na kupata maoni na kutoa mapendekezo yako na kuchukua hatua pale unapoona mambo hayaendi sawa.

Siku zote mambo yanapoharibika sehemu yoyote wa kulaumiwa huwa ni kiongozi mkuu wa eneo hilo.
Sikubaliani na wewe, lakin pia sitaki kukuhamisha kwenye unachokiamini
 
Habari wadau,

Kuna jambo moja linakera ila naona wengine kama wanaona ni vizuri kwao, sasa inanifanya nijiulize nina matatizo au vipi. Ni kuhusu kupeana vitu na watu, hasa nyumbani na majirani. Sitaki Jirani anipe vitu vyake wala sitaki aniombe vya kwangu, labda awe ametokewa na shida ya kweli. Vitu vyenyewe ni kama vyakula, vifaa vya ndani, n.k

Aisee kuna nyumba za kota tumehamia mimi na wife hapa, kuna majirani wana roho nzuri lakini naona hii ni too much, wanapenda sana ku-share vitu, yaani kuna siku moja atamuita wife wakapike chakula cha pamoja, siku nyingine mwingine atapika chakula kisha atuletee wakati sisi tumeshapika, siku nyingine atawaambia mumpakulie kwa kuwa yeye hajisikii kupika siku hiyo, wakati mmepika cha size yenu pekee.

Kuna mmoja juzi katoka mkoani kaleta mazagazaga mengi kampa wife, sasa siku hiyo ndio natoka kunununa vyakula vya wiki nzima nakuta friji imeshajaa, sasa na wao unakuta siku wanakuambia gesi imeisha tunaomba tutumie jiko lenu.

Wife nishampiga marufuku kuomba ama kuchukua vitu kutoka kwa majirani lakini imekuwa mtihani kukataa na yeye akiwapa vitu kesho naye atakuja kuomba kwenu, hii inaharibu ratiba na bajeti kwani mimi ni mtu ninayependa kupangilia kila kitu changu kwa usahihi.

Naona ni kama tunalazimishana kuishi kijamaa wakati haya maisha sijayaozea kabisa, japokuwa nimekulia kijijini tulikuwa hatuombani vitu hovyohovyo, labda iwe imetokea shida ya kweli.

Sasa watu wengine niliowakuta hapa naona wanaiona ni lifestyle nzuri, najiuliza pengine mimi ndio nina roho mbaya ama hili linawakera pia baadhi yenu?
Kitabia utakuwa mtu mchoyo na mnoko.
 
nikiwa form 3 kuna jirani yetu alihamia kwenye jumba lake pale mtaani,alikuwa anafanya kazi BOT nadhani,alikuwa akitoka kazini akifika getini anabonyeza tu rimoti geti linafunguka anaingia kwake hana habari na watu,haongei na watu wala hajishughulishi na shda za mtaa,ila kwenye michngo mkienda kuomba michango anatoa vizuri ila hashiriki,siku ya siku mkewe alipata ajali na mtoto ote wakafariki,msibani hakwenda mtu hata mmoja sema mtaa mzima tulimchangia around 1.8m,ambzo alipeleka mjumbe toka siku hyo alibadilika na kwenda kuomba radhi kwa kila nyumba na tinted alitowaga.Ishi na watu vizuri hasa mtaani kwako haijalishi unauwezo gani au mamlaka gani kwani siku yakikukuta hao ndo wakwanza kukusaidia
 
Woooi [emoji849] sasa vitu kama vyakula muachie wife adeal navyo ili usiendelee kuumiza kichwa au hama ukakae mtaa ambao kila mtu na geti lake , ukitoka kwenye mishe zako ni ndani huna muda wa kuonana na majirani
Hiyo ni roho mbaya wala usitake kusingizia eti unapangilia mambo yako, mambo yanayohusu msosi mara sijui jiko la gesi muachie mkeo ashughulike bro, acha ujinga
Sasa Mzee si unakuta umetoka kazini unamkuta jirani jikoni, unauliza kulikoni? Wife anajibu ameomba atumie gesi yake imeisha, siku nyingine unauliza mbona chakula leo umepika kidogo? Anajibu jirani akitaka nimchotee yeye hajapika

Nanunua vitu niweke nakuta friji imejaa, kuuliza naambiwa tumepewa na Fulani

Sasa huo Ni uvamizi, siwezi kukaa kimya, Ni nyumbani kwangu, Ni territory yangu siwezi kuwa passive hivyo

Binafsi sioni tabu kuombwa nimsadie mtu Kama akiwa na shida kweli, Kuna kipindi mtoto aliumwa hapa nikawasaidia, Kuna kipindi mwingine mshahara unachelewa nawakopesha, huko ndio kusaidiana kwenye umuhimu
 
nikiwa form 3 kuna jirani yetu alihamia kwenye jumba lake pale mtaani,alikuwa anafanya kazi BOT nadhani,alikuwa akitoka kazini akifika getini anabonyeza tu rimoti geti linafunguka anaingia kwake hana habari na watu,haongei na watu wala hajishughulishi na shda za mtaa,ila kwenye michngo mkienda kuomba michango anatoa vizuri ila hashiriki,siku ya siku mkewe alipata ajali na mtoto ote wakafariki,msibani hakwenda mtu hata mmoja sema mtaa mzima tulimchangia around 1.8m,ambzo alipeleka mjumbe toka siku hyo alibadilika na kwenda kuomba radhi kwa kila nyumba na tinted alitowaga.Ishi na watu vizuri hasa mtaani kwako haijalishi unauwezo gani au mamlaka gani kwani siku yakikukuta hao ndo wakwanza kukusaidia
Ulichoandika hakihusiani na nilichosema, Mimi nazungumzia mtu kuomba vitu vya ndani hovyo wewe unazungumzia kushiriki shughuli za kijamii, hizo nashiriki Sana,
 
Chief, Angekuwa mchoyo majirani wasingeenda kula kwake. Na kwa taarifa yako bila kuwa mnoko mambo yako hayawezi kwenda mbele!!
Wala hata sio unoko, huwa kuna mambo nasaidia Sana Yale ya muhimu

Mfano mfanyakazi wao ameumwa na hawana hela ndani, naagiza wife ampe anakuja kurudisha

Au umeme umeisha na hawana credit kwenye simu, nawasaidia tu kuwanunulia
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Sasa Mzee si unakuta umetoka kazini unamkuta jirani jikoni, unauliza kulikoni? Wife anajibu ameomba atumie gesi yake imeisha, siku nyingine unauliza mbona chakula leo umepika kidogo? Anajibu jirani akitaka nimchotee yeye hajapika

Nanunua vitu niweke nakuta friji imejaa, kuuliza naambiwa tumepewa na Fulani

Sasa huo Ni uvamizi, siwezi kukaa kimya, Ni nyumbani kwangu, Ni territory yangu siwezi kuwa passive hivyo

Binafsi sioni tabu kuombwa nimsadie mtu Kama akiwa na shida kweli, Kuna kipindi mtoto aliumwa hapa nikawasaidia, Kuna kipindi mwingine mshahara unachelewa nawakopesha, huko ndio kusaidiana kwenye umuhimu

Mazoea lazima yawe na mipaka, kuzoeana kupita kiasi siyo kuzuri hasa kwa baadae. Binafsi mimi hata ndugu yangu hawezi kuzoea kwangu namna hiyo halafu nikamuacha. HERI LAWAMA KULIKO FEDHEHA.
 
Wala hata sio unoko, huwa kuna mambo nasaidia Sana Yale ya muhimu

Mfano mfanyakazi wao ameumwa na hawana hela ndani, naagiza wife ampe anakuja kurudisha

Au umeme umeisha na hawana credit kwenye simu, nawasaidia tu kuwanunulia

Chief, Unoko ni ile hali ya kusimamia unachokiamini katika kuhakikisha taratibu na sheria bila kusahau kanuni zinafuatwa kama zilivyopangwa. Neno hili "Mnoko" hutumika hasa kwa wale Polisi wanaotekeleza majukumu yao bila kupindisha. Hivyo usijisikie vibaya kuitwa mnoko.

Binafsi napenda aina yako ya maisha maana ni nzuri hasa katika suala la kutunza usalama (Security), maana linapotokea tatizo hapo kwako ni rahisi kufuatilia na kujua limeanzia wapi tofauti na tabia ya ingia toka ya majirani maana ukiwauliza watakuona unawachimba na hata kama ni mmoja wao ndio amesababisha wataruka futi 100 juu.
 
Wewe ni mbinafsi uliekomaa mkuu sifa kuu ya wabinafsi hawapendi kupewa ili na wao wasitoe hii tabia ya kupeana misosi wanayo sana wazungu mida ya dinner unagongewa mlango unakutana na plate ya wali nazi au wajuba wanakuja na chupa zao za gambe mnaishi nazo kiroho safi tu hili suala nililiona tabora vijijini na nikalikua states ndio nkajua kwanini wamarekan wanaitwa wanyamwèzi so kwakifupi wewe ndio mbinafsi na mswahili
Basi huo unyamwezi mi sina, kila mtu na culture yake
Kuitana Mara moja moja kula pamoja sio mbaya, Ila ikiwa inafanyika randomly Mzee hiyo sio
 
Back
Top Bottom