Sipendi kuomba wala kuombwa vitu. Je, nina roho mbaya au ni kawaida?

Ngoja na mi nijiseti mapema nikioa tu niwe na ka utaratibu kangu [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 

We Mwanamke una akili ya maisha, safi sana maelezo yako nimeyaelewa. Hivi umeolewa?
 
kweli aisee hii inanihusu mimi maana ni kauzu kweli kweli + sipendi mazoea na watu
 
mazoea yana tabu......itafikia hatua mnaanza kuazimanana wake na nguo za ndani kiroho safi tu mkuu,mimi sina roho mbaya ya kumnyima mtu kitu ninachokimudu ila sipendagi tabia za mtu kuyajua maisha yangu kiundani hasa mtu asiyekuwa ndugu wa karibu.una roho nzuri sana kama mh.
 
Brother, utakuja kufanya kitu ambayo itarefulekiti balaa, hama nenda mitaa ya Kishimba achana na kota.
 
Anyway haka katabia nyumban kapo na majiran ndo wamenilazimsha niwe naishi nao hvyo ingawaje sikapendi ngoja nikipige stop rasmi....ukauzu tu sahivi!
 
mzee wa chai kama kawaida yako!
 

Mkuu ili wasikushtukie una roho mbaya hama hapo tafuta self apartment ambayo kila mtu na mambo yake, hata mimi sipendi kuomba wala kuombwa ombwa, ila nna huruma na wenye shida tena nimsaidie freely sipendi aje aniombe, sio vitu tu hata kuomba lift ya gari au pikipiki sipendi na mimi sipendi kuomba lift, hata mtu akiniona njiani na kujipendekeza kunipanlift namwambia nafika hapo mbele tu nshafika kumbe sipendi mavyombo ya watu hayo. Anaweza kupata shida njiani akakuomba umsaidie kutatua, tayari kisha kupotezea gape
 
Dah... umenikumbusha back in the days!! Sister angu wa ma'mkubwa kaachika wakati alikuwa anaishi na mdogo wake aliyekuwa anasoma day! Wakapiga hesabu huyo msichana akaishi wapi wakati anamalizia shule, wakaona aje kuishi home kwetu ambako by the time nilibaki peke yangu!!

Akaja kuanza maisha mapya!!

Wiki haijapita... sijui ilikuwaje kuwaje, nikatoka mlango wa nyuma ambako nilikutana nae tit-for-tat anatoka nyumba ya jirani, tena kupitia mlango wa nyuma! Nikashangaa kuona mtu ambae hata wiki hajamaliza, anatoka nyumba za watu! Ile kumuuliza, with confidence ananiambia eti alienda kuomba chumvi!!

Alinikera balaa!!!
 
Mimi naona sawa tu mwanaume siku akija anipe support huongeza upendo na urafiki, sisi kwetu wanaume wanajua kupika Tena chakula kitamu Sana ndio tulivolelewa so Mimi sioni shida ukiwa mwanaume siku moja ukapika kwa familia yako.
I can do anything with that lakini kukuna nazi, hapana aisee!! Hivi unapokuna nazi na zile mbuzi zetu za Uswahilini si lazima ujilegeze hivi huku unanesa nesa kwa madaha ya twiga anaetembea, au?! Au ni mbwembwe tu zile za akina dada wakuna nazi?!

Yaani hakuna ukombozi alionifanyia Bakhresa kama zile nazi zake... been asking myself what if kusingekuwa na zile nazi!!!
 
Mi kuombwa sina tatizo, tena huwa nafurahia kutoa kama ninacho lakini kuomba siwezi na sitaki!!!

Hata hivyo, kwa vitu vidogo vidogo kama vile vya jikoni, ukiniomba na kama ni kitu cha kuhitaji kurudisha basi nirudishie mara utakavyomalizia shughuli zako vinginevyo nitakususia jumla kwa sababu sina desturi ya kupiga hodi nyumba au milango ya watu!!

Kwa mfano mtu unaenda kuomba kisu, na unajua kabisa mtu hawezi kuwa na kisu zaidi ya kimoja; halafu unaomba lakini kurudisha hadi mwenyewe akifuate tena... wtf?!

Trust me, kama nitafuata mara ya kwanza, halafu ukachukua tena na ukabaki nacho, kitakachofuata hapo ni mimi kwenda kununua kingine ili nikuachie "kisu chako"!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…