Tetesi: SIRI IMEVUJA: CHADEMA mikononi mwa kampuni ya BELG Sea International



Rubbish
 
Nyuzi kama hizi huwa zinatushtua hata ambao tulikua tunaunga mkono uwekezaji kuanza kua na wasiwasi
 
Hata wakilipwa poa tu.... Dadeki miaka 100 ufala huo bora pavurugike tu
 
Hii imekaa kisiasa kuliko kitaalamu
 
Sawa tu bora iwe IVO
 
UONGO..
Njoo na mpango mzuri..huu umebuma!!..
 

Ngoja tufanye utafiti tutakuja kujibu.

Mimi naunga mkono bandari wapewe mkataba wa kuiendesha DP World lakini hii taarifa yako haijanikalia sawa. Bado sijaikubali.
 
Huu ni ujinga. Toa ushahidi. CHADEMA wamehongwa na jaji Warioba je nae, vipi prof. Shivji, mama prof Tibaijuka! Makamu mwenyekiti CCM mzee Kinana amesikika akisema mkataba uangaliwe ili kurekebisha mapungufu nae amehongwa na nani? Chama cha wanasheria kimetoa hoja na mapendekezo mbona hazijajibiwa au nao wamehongwa! Dr. Rugemereza nae katoa mapungufu mbona hazijajibiwa. Tumemsikia pia Kibajaj kada kindakindaki wa CCM akishauri mapungufu yarekebishwe nae kahongwa na nani. Mzee Butiku ameshauri hoja za wanaopinga ziangaliwe nae kahongwa na nani? Ushabiki na ukada wa vyama tuuache pale inakuja suala la kupigania maslahi ya nchi. Toa maelezo kwa vipengele vinavyolalamikiwa.
 
Kumbe DP World walishindanishwa na Belg Sea International?

Sasa mbona hilo Swali la Kuhusu Zabuni ya Kumpata huyo DP world alishindanishwa na nani halijawahi kupatiwa majibu hadi leo hii?

Si mumpe Majibu Bwana Chongolo awe anajibu badala ya kujiuma uma?
 
Nimetafuta kwenye mtandao sijaiona kampuni inayoitwa "BELG SEA INTERNATIONAL".

Tupatie website yake, au umekuja kujaza watu ujinga kijinga jinga hapa?

Tumpe 1 hour huyu atupatie website ya hiyo kampuni, akishindwa napendekeza apigwe ban.

Watu tupo kwenye maslahi ya taifa, kila mmoja kwa muono wake wewe unaleta ujinga kama hawa chadema?
 
 
Mashudu matupu
 
Hivi huwa mnalipwa kiasi gani hadi mnaweza kujitoa ufahamu kiasi hiki? Ni vyema mkajipanga kwa hoja kuliko kuwarushia matope watu ili mchafuke wote
 
Okay na wengine ambao sio CHADEMA tupo mikononi mwa nani ?

Yaani Kama ni Mkataba / Makubaliano ya Hovyo; hata kama ni shetani ndio atayatetea nitaungana nae.....
 
Kachume bakora Bi Mkubwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…