Siri kubwa kuliko zote kuhusu dunia yetu tambarare

Siri kubwa kuliko zote kuhusu dunia yetu tambarare

JE Dunia ina umbo gani?


  • Total voters
    710
Hiyo bangi unayovuta ni hatari, ko jua kuchomoza na kuzama ndiyo kitu cha kukuonesha kwamba dunia ina move? Ko wewe ukichukua kitabu ukakining'iniza hewani halafu sisimizi ukamuweka juu ya hicho kitabu, baadaye ukaanza kuzunguka hicho kitabu katika nyuzi 360°, huyo sisimizi atajitungia kwamba kitabu kina move, sio? 😂😂😂😂
Sijui hata huo mfano wako unamaana Gani, ila kama wewe unakataa kuwa sunrise na sunset sio uthibitisho tosha kwako basi tuambie ni nini kinafanya sunset na sunrise kutokea?
 
Nilikupa mfano hukujibu;
Imagine upo kwenye basi wewe upo seat ya nyuma kabisa na dereva yupo mbele anaendesha gari, je ukimuamgalia dereva atakuwa anamove away "from the point uliyopo? " Kama unajua maana ya FRAME OF REFERENCE utaelewa kwann nimetumia neno "from the point uliyopo".
hateeb10 hapa hujajibu, unaogopa nini? Na nimekupa task record Jua nioneshe linamove.
 
hateeb10

Angalia hii clip nambie gari inamove au camera ndio inamove?



Halafu angalia na hii nambie je hiyo miti inamove backward au ni nini?

 
1. Kama unasema Kuna milima na mabonde hiyo ni tambarare Gani unayoongelea? Na Hilo Duara tambarare umelithibitisha vipi? Uliona wapi? Picha yake hata CGI tu, ukifika mwisho wake? Au kama umeambiwa au kusoma unauthibiitisho Gani?

2. We umejuaje Jua ndio linamove na sio Dunia ndio inamove? Kama unaona Jua linamove naomba record video leta hapa tuone Jua linamove.

Mfano angalia hii video alafu nambie je hayo majengo yanamove au ni camera ndio inamove? Na kwann?👇👇 hateeb10 pia ajibu hapa.

Chosen Rich Mayu

View attachment 2966325
Asante..!! Nikianza na swali lako la mwisho ulilolisapoti kwa video... hapo kinachoonekana ni majengo yanamove... lakini kiuhalisia ni camera ndiyo inayotembea, na hilo mtu yeyote anaweza kulithibitisha kwakujaribu yeye mwenyewe kufanya hivyo.

Isipokua kwa kesi ya Jua, wewe binafsi unalionaje? je lina utoffauti na Mwezi katika muonekano wa mtembeo wake? Je mwezi nao usingekua unatembea ukabaki sehemu moja tungeendelea kuuona kama tuuonavyo?

Swali lako la kwanza limenithibitishia unapingana na usichokielewa. kama kweli umeshangaa dhana ya Dunia tambarare kua na mito milima na mabonde, basi amini unatumia muda wako bure katika uzi huu labda uamua kweli kutaka kujua.

Kwa vile tupo katika kujifunza na kufunzana naomba nikuweke sawa kwanza. Kwanza elewa kua, maumbo yote ya dunia Mviringo na tambarare, yote ni ya DUARA.

Unaposikia Flat Earth maana yake ni Dunia isiyokua ya Mviringo kama Mpira bali ina Umbo kama DISC. Je Disc ni ya tambarare au mviringo. So hiyo milima na mabonde ni vitu vinavyopatikana katika utambarare huo.. Kama siko sawa utanisapoti na picha yoyote ya tambarare uijuayo nione kama haitakua na vilima au mabonde ili tuwekane sawa katka hili.

Mwisho kabisa mimi kama mimi ninajua Jua ndio lina move kwasababu naliona kama ninavyouona mwezi ukimove bila kufeel hali yoyote tofauti katika mwili wangu iwe wakati naliona jua linatembea au wakati nauona mwezi ukitembea.

SWALI LANGU KWAKO.!
Unadhani nikwanini kabla haujafundishwa kua jua limesimama Ulikua unaamini linatembea?
 
hateeb10

Angalia hii clip nambie gari inamove au camera ndio inamove?

View attachment 2966897

Halafu angalia na hii nambie je hiyo miti inamove backward au ni nini?

View attachment 2966898
Mifano sijui ya ukiwa katika usafiri utaona kama miti inarudi nyuma na blablabla nyinginezo, lakini mbona hamuulizi je wakati unaona miti inarudi nyuma unapokua katika hilo gari, mwili wako unakua unafeel vipi? Je kwenye kuona jua linatembea kumbe ni Dunia, Je Miili inapata hisia yeyote yakuwamo katika kitu kinachotembea kama ambavyo inakua katika gari?

Naomba na mfano mwingine wa Kipi kingine ambacho Tunavyokiona kifanyavyo ni tofauti na uhalisia wa macho yetu kama tunavyoona jua linatembea lakini tunaambiwa limesimama.
 
Hivi Ili ubongo ufikrie si unahitaji taarifa? Hapo sasa Kuna aina tofauti tofauti za taarifa, Kuna taarifa Kwa njia ya kuambiwa, kusoma na kutazama.

Kwahy Kwa vyovyote vile nimehusisha akili yangu vyema. We hujiulizi kama ningekuwa napokea navyoambiwa bila kufikiri si ningeshakubaliana na Hekaya zako humu?
Sorry, Hivi umetumia miaka mingapi kufundishwa tuu Umbo la Dunia? Na je Una Miaka mingapi tangu uanze kukataa Umbo la Dunia Tambarare.?
 
Na hana haki ya kusema ni Jua ama lah!

Maana hii clip umeileta wewe ili kuwapa wao mifano,

La sivyo yeye atuletee mifano yake kuhusu Jua kuzunguka Dunia ( Najua hili hawezi hataa kwa kujaribu )
Mfano wa Jua kuzunguka Dunia unaupata hata katika saa ya Mshale, na Ujue tuu wazee wa zamani kutumia Jua kujua masaa ndio kulileta idea yakutengeneza saa ya mshale kwa kufuata hesabu za mzunguko wa Jua linapoizunguka dunia Masaa 24.

Na katika hili nikugusie kidogo sababu ya wewe Kudanganya mengi, Nikuulize hivi kati ya Jua na Saa kipi kinatoa Muda wa Ukweli, ikiwa wazee waliamini kwa mfano kivuli cha mti kikiwa pale ni saa flan, lakini wewe ni mara ngapi unaamka jua linaonesha ni saa mbili ila saa inaonesha ni saa 12 au kinyume chake..

Nijibu ukiweza... Hivi ni kwanini Kama Jua linazunguka masaa 24 net, lakini masaa ya kuchomoza na kuzama kwake hubadilika? je kwa kutumia jua kuna mabadiliko ambayo yangekua yanatokea kama hayo? mfano mkisema muwe mnaenda shambani jua linapoanza kutoka na mwingine aseme linaanzaga kutoka saa 12, nani atakua kupuyanga?

Sasa chukulia duara la saa ya Mshale ni kubwa kama lile la katikati ya Dimba la mpira, then Chini ya point ya mshalewa saa tuweke taa inayomulika namba. Je huo mwanga utalimulika Duara zima? kama sivyo basi patakapokua na mwanga ndio panaitwa mchana na patakapoukosa mwanga pataitwa usiku.

Si hivyo tuu kama wewe ni Muumini wa imani ya Dini, katika uumbaji Mungu aliumba Jua, Mwezi na Nyota ili tuweze kujua Saa na Majira.
 
Wewe nadhani huitumii akili yako vzr kufikiria, wewe hiyo video umeiona kupitia nini kama sio camera? Na ndio kama sisi tunaliona Jua tukiwa duniani, yaani observer yupo karibu na camera, tumia akili yako
Ndiyo maana nasema mfano wako ni irrelevant......

Kwenye uhalisia Jua tunaliona.....Je, kwenye Video yako Camera tunaiona?

Huoni kama mfano wako unakosa mantiki?


Unasema video nimeiona Kwa kutumia camera,...Je,.Jua tunaliona Kwa kutumia nini?
camera pia?

NB:- Kimsingi mfano wako haueleweki hasa ukiuleta kwenye uhalisia.
 
Halafu nimeshakupa task, record video uoneshe Jua linamove. Simple tu kama Jua ni local na lipo km chache kutoka tulipo na ni dogo kulinganisha na Dunia ni rahisi kuona mjongeo wake, so wewe record video uje utuoneshe Jua linamove.
Hoja yako hasa ni nini?

Mbona wewe umesema Jua lina move na hujaleta video kutuonyesha Jua Lina move?

Au sio wewe uliyesema Jua Lina move?

Hakikisha unakua na kumbukumbu nzuri.


NB:- Mimi ninaposema Jua lina move ni Kwasababu Jua utaliona kwenye point/ position tofauti tofauti kadri ya muda,....na kitu hicho kipo pia Kwa Mwezi au unataka uletewe picha ya mwezi pia?......sijui kwanini unashindwa kuelewa vitu simple hivi ambavyo ni uhalisia kabisa yaani kimsingi ni kwamba Dunia ipo stationary kama vile unavyoiona na kuhisi kwamba ipo fixed,..
 
hateeb10

Angalia hii clip nambie gari inamove au camera ndio inamove?

View attachment 2966897

Halafu angalia na hii nambie je hiyo miti inamove backward au ni nini?

View attachment 2966898
Kwa kukusaidia ngoja nitolee maelezo hiyo video ya pili hapo.....

Ipo hivi 👉🏼 ukitazama hiyo video ndiyo itakupa uhalisia sasa wa Dunia ilivyo.....miti ipo attached na Dunia So miti ipo Stationary na let's say Camera iliyotumika kurekodi ndiyo inafanya movement kiasi ambacho kadri camera inavyosogea inaacha miti ikiwa kwenye position Ile Ile..... So,..jibu ni kwamba kwenye video hapo miti ipo Stationary na Camera ndiyo inapita na kuiacha miti(iliyo attached na Dunia) backward.
 
hateeb10 hapa hujajibu, unaogopa nini? Na nimekupa task record Jua nioneshe linamove.
Sasa hapo kuna kipi cha kufanya niogope....au umesahau kama huo mfano tushaudiscuss humu., Nikijibu swali lako...."Dereva hato move away from the point uliyopo"

Sasa huo mfano unauhusianisha vipi na Dunia, Jua na Mwezi?
 
Mfano wa Jua kuzunguka Dunia unaupata hata katika saa ya Mshale, na Ujue tuu wazee wa zamani kutumia Jua kujua masaa ndio kulileta idea yakutengeneza saa ya mshale kwa kufuata hesabu za mzunguko wa Jua linapoizunguka dunia Masaa 24.

Na katika hili nikugusie kidogo sababu ya wewe Kudanganya mengi, Nikuulize hivi kati ya Jua na Saa kipi kinatoa Muda wa Ukweli, ikiwa wazee waliamini kwa mfano kivuli cha mti kikiwa pale ni saa flan, lakini wewe ni mara ngapi unaamka jua linaonesha ni saa mbili ila saa inaonesha ni saa 12 au kinyume chake..

Nijibu ukiweza... Hivi ni kwanini Kama Jua linazunguka masaa 24 net, lakini masaa ya kuchomoza na kuzama kwake hubadilika? je kwa kutumia jua kuna mabadiliko ambayo yangekua yanatokea kama hayo? mfano mkisema muwe mnaenda shambani jua linapoanza kutoka na mwingine aseme linaanzaga kutoka saa 12, nani atakua kupuyanga?

Sasa chukulia duara la saa ya Mshale ni kubwa kama lile la katikati ya Dimba la mpira, then Chini ya point ya mshalewa saa tuweke taa inayomulika namba. Je huo mwanga utalimulika Duara zima? kama sivyo basi patakapokua na mwanga ndio panaitwa mchana na patakapoukosa mwanga pataitwa usiku.

Si hivyo tuu kama wewe ni Muumini wa imani ya Dini, katika uumbaji Mungu aliumba Jua, Mwezi na Nyota ili tuweze kujua Saa na Majira.

Umeandika maelezo mengi ambayo naweza nkasema sijakuelewa,

Ila hapo mwenye mfano wako nataka nikuulize swali,

Tukiweka taa kwenye hilo duara , vipi hata hiyo sehemu ambayo mwanga haufiki vizuri...Je ( kwamba mbali ) taa itaonekana au haitaonekana ?
 
Hoja yako hasa ni nini?

Mbona wewe umesema Jua lina move na hujaleta video kutuonyesha Jua Lina move?

Au sio wewe uliyesema Jua Lina move?

Hakikisha unakua na kumbukumbu nzuri.


NB:- Mimi ninaposema Jua lina move ni Kwasababu Jua utaliona kwenye point/ position tofauti tofauti kadri ya muda,....na kitu hicho kipo pia Kwa Mwezi au unataka uletewe picha ya mwezi pia?......sijui kwanini unashindwa kuelewa vitu simple hivi ambavyo ni uhalisia kabisa yaani kimsingi ni kwamba Dunia ipo stationary kama vile unavyoiona na kuhisi kwamba ipo fixed,..
Tunaomba uthibitisho kuwa Jua inazunguka Dunia


( Tafadhali usije na maelezo matupu, Unahitajika uthibitisho bila maneno wala maelezo kibao )
 
Nimepita comments za watu humu na leo nikasema ngoja nijaribu hizi nadharia, sijafanya kwenye perfect condition sababu za ukubwa wa space niliyonayo na fact kuwa nimeshindwa kufanya kuwe giza sana sababu ya uwepo wa taa zingine zilizo nje ya uweza wangu.

1. Nime taa fixed, nifanyazoezi lakuzunguka nimeshika camera inarekodi video katika uelekeo wa taa.
2a. Nikaweka camera chini, kisha nianza kuizunguka camera huku nimeshikilia tochi inaangalia camera katika mizunguko yenye kipenyo tofauti tofauti kutoka kipenyo kikubwa niwezavyo hadi kidogo.
2b. Kama 2a ila camera inaangalia chini.
2c, Kama 2a, ila badala ya kuzunguka camera nikawa naenda across kutoka kushoto kwenda kulia, kwanza kutembea kwenye mstari unaopita straight juu ya camera then mistari mbali mbali ambayo ipo parallel na huu mstari.

Sita share video zangu, naombeni ambao hamjawahi fikiria kwa umakini hizi nadharia kama ni za kweli jaribu kutengeneza experiment ya kutest fikira zako utajifunza kitu kipya kama nimivyotoka kujifunza mimi leo.
Katika hizo senarios 4 hapo juu ni video moja tu inayotoa picha inayofanana na kile nachokiaona kila asubuhi na jioni.
 
Nimepita comments za watu humu na leo nikasema ngoja nijaribu hizi nadharia, sijafanya kwenye perfect condition sababu za ukubwa wa space niliyonayo na fact kuwa nimeshindwa kufanya kuwe giza sana sababu ya uwepo wa taa zingine zilizo nje ya uweza wangu.

1. Nime taa fixed, nifanyazoezi lakuzunguka nimeshika camera inarekodi video katika uelekeo wa taa.
2a. Nikaweka camera chini, kisha nianza kuizunguka camera huku nimeshikilia tochi inaangalia camera katika mizunguko yenye kipenyo tofauti tofauti kutoka kipenyo kikubwa niwezavyo hadi kidogo.
2b. Kama 2a ila camera inaangalia chini.
2c, Kama 2a, ila badala ya kuzunguka camera nikawa naenda across kutoka kushoto kwenda kulia, kwanza kutembea kwenye mstari unaopita straight juu ya camera then mistari mbali mbali ambayo ipo parallel na huu mstari.

Sita share video zangu, naombeni ambao hamjawahi fikiria kwa umakini hizi nadharia kama ni za kweli jaribu kutengeneza experiment ya kutest fikira zako utajifunza kitu kipya kama nimivyotoka kujifunza mimi leo.
Katika hizo senarios 4 hapo juu ni video moja tu inayotoa picha inayofanana na kile nachokiaona kila asubuhi na jioni.
Usiteseke mkuu,... unapaswa kuzingatia kwamba milango yako ya fahamu ipo sahihi.
1. Dunia sio tufe
2. Dunia haiifanyi movement yoyote.
3. Mwezi na Jua hufanya movement kwenye anga la Dunia.
 
Usiteseke mkuu,... unapaswa kuzingatia kwamba milango yako ya fahamu ipo sahihi.
1. Dunia sio tufe
2. Dunia haiifanyi movement yoyote.
3. Mwezi na Jua hufanya movement kwenye anga la Dunia.
Kama hatuwezi kujaribu mawazo yetu na mawazo ya watu hatuwezi kufikia sehemu ambayo wote tunakubali wazo fulani linakaribia ukweli.

Watu kupishana mawazo ni sawa na vema, kwa sababu inatengeneza nafasi ya kurekebisha fikara ambazo sio sahihi na pia kugundua vitu vipya.
 
Kama hatuwezi kujaribu mawazo yetu na mawazo ya watu hatuwezi kufikia sehemu ambayo wote tunakubali wazo fulani linakaribia ukweli.

Watu kupishana mawazo ni sawa na vema, kwa sababu inatengeneza nafasi ya kurekebisha fikara ambazo sio sahihi na pia kugundua vitu vipya.
Yes, upo sahihi ni muhimu kuzingatia fikra za watu wengine ili kuja na fikra ya pamoja kama Jamii,...lakini ikitokea fikra za watu wengine zinaenda against uhalisia ni jukumu letu kusimama kwenye njia ya uhalisia bila kujali number yetu.
 
Usiteseke mkuu,... unapaswa kuzingatia kwamba milango yako ya fahamu ipo sahihi.
1. Dunia sio tufe
2. Dunia haiifanyi movement yoyote.
3. Mwezi na Jua hufanya movement kwenye anga la Dunia.
Milango yako ya fahamu ina ukomo wa kufanya kazi,


Prove Jua linazunguka Dunia.
 
Nimepita comments za watu humu na leo nikasema ngoja nijaribu hizi nadharia, sijafanya kwenye perfect condition sababu za ukubwa wa space niliyonayo na fact kuwa nimeshindwa kufanya kuwe giza sana sababu ya uwepo wa taa zingine zilizo nje ya uweza wangu.

1. Nime taa fixed, nifanyazoezi lakuzunguka nimeshika camera inarekodi video katika uelekeo wa taa.
2a. Nikaweka camera chini, kisha nianza kuizunguka camera huku nimeshikilia tochi inaangalia camera katika mizunguko yenye kipenyo tofauti tofauti kutoka kipenyo kikubwa niwezavyo hadi kidogo.
2b. Kama 2a ila camera inaangalia chini.
2c, Kama 2a, ila badala ya kuzunguka camera nikawa naenda across kutoka kushoto kwenda kulia, kwanza kutembea kwenye mstari unaopita straight juu ya camera then mistari mbali mbali ambayo ipo parallel na huu mstari.

Sita share video zangu, naombeni ambao hamjawahi fikiria kwa umakini hizi nadharia kama ni za kweli jaribu kutengeneza experiment ya kutest fikira zako utajifunza kitu kipya kama nimivyotoka kujifunza mimi leo.
Katika hizo senarios 4 hapo juu ni video moja tu inayotoa picha inayofanana na kile nachokiaona kila asubuhi na jioni.
Vizuri, Endelea kufanya tafiti zaidi na zaidi

Natoa na pendekezo lingine ambalo ningependa ukalifanyie tafiti ukipata muda,


Sijajua unaishi wapi ila kama upo Dar es salaam nenda Bagamoyo au Ferry ( Muda: Majira ya usiku )

Angalia uelekeo wa Zanzibar uangalie kama kuna taa zozote ambazo zinaweza kuonekana kutokea Zanzibar, Usipoona tafuta jengo la ghorofa yoyote ndefu angalia tena,
Ukimaliza hiyo tafiti usisite kutuletea mrejesho hapa jukwaani tujadili kwa pamoja
 
Back
Top Bottom